Katika Eneo la Adui Kuokolewa na Silaha ya Siri: Swahili
Автор Danny Clifford
()
Об этой электронной книге
Ili kuendelea kuishi nchini Vietnam, ili uweze kurudi nyumbani ukiwa mzima, unahitajika kupitia mafundisho ya hali ya juu, kupata ozoefu wa mwili na akili na kuwa na uhusiano mwema na wenzako. Kama tungeshindwa kuwa makini, kutotii, kupuuza, au kutozingatia nia yetu kuu mahali pale, basi idadi ya kuishi ilipungua kwa kiasi kikubwa.
Niamini nikisema, kuna mambo mengi yalituzuia. Baadhi yetu tulianza kutumia madawa ya kulevya, unywaji wa pombe, kushiriki ngono kihorera, haya yote katika harakati ya kutafuta maisha ya kupendeza, hatari nyingine ilikua inatukondolea macho, hata kabla twende vitani kupigana na makali ya adui zetu, kabla tuwapate nyoka, magonjwa, na wanyama wa pori walioishi katika maeneo haya
Kitabu hiki kinaelezea matukio ya kusisimua ambayo nilipitia mimi mwenyewe, mafunzo niliyopata, nilivyopata uzoefu na kuwa na uhusiano mwema na wenzangu, nikiwa mwanajeshi wa Marekani katika kikosi cha 75 cha wanahewa wa kupiga doria mnamo mwaka wa 1969 na 1970, tukifanya upelelezi katika maeneo ya adui zetu.
Ni mwaka wa 1971, nikihudumu kama mshauri wa washika doria wa kikosi cha pili milimani, ndani ya msitu katika eneo lililopakana na kambi ya sita katika kijiji cha Plei Mrong, Kusini mwa Vietnam kupakana na nchi ya Cambodia. Jukumu langu lilikuwa kufundisha kikosi cha Mountain Yard na wanajeshi wa Vietnam kuhusu mbinu za kivita na jinsi ya kuwahamisha wanakijiji walioathiriwa na vita.
Matukio haya yatakutoa katika vita vya kimwili nchini Vietnam hadi kwenye vita vya kiroho vinavyoendelea kila siku kwa ajili yako. Maswali mengi kuhusu ulimwengu wa kiroho yatapata majibu na imani yako itachukua mwelekeo mpya. Ombi langu ni kwamba, kupitia kitabu hiki, utapata mtazamo mpya kuhusu vita vinavyoendelea kila siku kati ya wema (Mungu) na ubaya (Shetani) kwa ajili ya nafsi yako, wewe binafsi.
Kwa hivyo tulia na ufurahie kisa hiki kifupi, ingawa kina uzito wake. Lengo langu ni kuwa ukimaliza kukisoma kitabu hiki, utakuwa umemfahamu kabisa mshindi wa Medali ya Heshima ambaye ni Mwokozi Yesu Kristo. Yesu anakupenda na anataka kuwa na uhusiano mwema na wewe, uhusiano utakao leta mabadiliko kwa nafsi yako, kutoka kiumbe ulicho sasa hadi kiumbe kipya. Roho yako ndio msingi wa kitabu hiki.
Mwandishi Danny Clifford
Danny Clifford
Thank - you for stopping byI am a Vietnam War Veteran who served as an Army Airborne Recondo Ranger from 1969 to 1971. I performed reconnaissance missions with a sex-man Ranger team and was also an adviser to the Vietnamese Rangers.Today I am a Pastor and multi-published author who teaches the Holy Bible. I am fortunate to have traveled during the past 7 years to Ghana, Kenya, Kosovo, Pakistan, Rwanda, Tanzania, Uganda, and back to Pakistan teaching the Gospel of Jesus Christ.I am blessed to be a father and grandfather who enjoys fishing, hunting, and spending time with family and doing God's work.I am also a retired Master Instructor, 4th Degree Black Belt in the Martial Art of Taekwondo, certified by the World Taekwondo Federation in Seoul, Korea. I was the coach of the State of Maine’s Junior Olympic Taekwondo Teams that attended the United States Nation Championship competitions each year from 1993 to 2002. competingI hope you read, enjoy, and are blessed, by my books; Lost Behind Enemy Lines - Who Do You Say I Am - and - Enter Thru the Narrow Gate.You may contact me by email at the ministry email: danny@ziongarden.orgGod Bless you,Author and EvangelistDanny Clifford
Отзывы о Katika Eneo la Adui Kuokolewa na Silaha ya Siri
0 оценок0 отзывов
Предварительный просмотр книги
Katika Eneo la Adui Kuokolewa na Silaha ya Siri - Danny Clifford
Katika Eneo la Adui
Kuokolewa na Silaha ya Siri
Mwandishi
Danny Clifford
Mchapishaji
Heart and Soul Ministry
Imechapishwa katika Smashwords
Hati Miliki © 2014 na Danny Clifford
* * *
Katika Eneo la Adui
Kuokolewa na Silaha ya Siri
Na Danny Clifford
Imechapishwa nchini Marekani
Book ISBN
Haki zote zimehifadhiwa na mwandishi. Mwandishi amehakikisha maandishi yote ni asili na haivunji kisheria kazi ya mtu mwingine yeyote.
Isipokuwa imeonyeshwa vinginevyo, Nukuu za Biblia zimetolewa kutoka kwa Toleo la New Intenation Version. Hati Miliki © 2008. Mchapishaji: Zondervan
Muundo: Heart and Soul Ministry Inc.
Translated By: Karunguru Mwangi
* * *
Utangulizi wa Mwandishi
Ili kuendelea kuishi nchini Vietnam, ili uweze kurudi nyumbani ukiwa mzima, unahitajika kupitia mafundisho ya hali ya juu, kupata ozoefu wa mwili na akili na kuwa na uhusiano mwema na wenzako. Kama tungeshindwa kuwa makini, kutotii, kupuuza, au kutozingatia nia yetu kuu mahali pale, basi idadi ya kuishi ilipungua kwa kiasi kikubwa.
Niamini nikisema, kuna mambo mengi yalituzuia. Baadhi yetu tulianza kutumia madawa ya kulevya, unywaji wa pombe, kushiriki ngono kihorera, haya yote katika harakati ya kutafuta maisha ya kupendeza, hatari nyingine ilikua inatukondolea macho, hata kabla twende vitani kupigana na makali ya adui zetu, kabla tuwapate nyoka, magonjwa, na wanyama wa pori walioishi katika maeneo haya
Kitabu hiki kinaelezea matukio ya kusisimua ambayo nilipitia mimi mwenyewe, mafunzo niliyopata, nilivyopata uzoefu na kuwa na uhusiano mwema na wenzangu, nikiwa mwanajeshi wa Marekani katika kikosi cha 75 cha wanahewa wa kupiga doria mnamo mwaka wa 1969 na 1970, tukifanya upelelezi katika maeneo ya adui zetu.
Ni mwaka wa 1971, nikihudumu kama mshauri wa washika doria wa kikosi cha pili milimani, ndani ya msitu katika eneo lililopakana na kambi ya sita katika kijiji cha Plei Mrong, Kusini mwa Vietnam kupakana na nchi ya Cambodia. Jukumu langu lilikuwa kufundisha kikosi cha Mountain Yard na wanajeshi wa Vietnam kuhusu mbinu za kivita na jinsi ya kuwahamisha wanakijiji walioathiriwa na vita.
Matukio haya yatakutoa katika vita vya kimwili nchini Vietnam hadi kwenye vita vya kiroho vinavyoendelea kila siku kwa ajili yako. Maswali mengi kuhusu ulimwengu wa kiroho yatapata majibu na imani yako itachukua mwelekeo mpya. Ombi langu ni kwamba, kupitia kitabu hiki, utapata mtazamo mpya kuhusu vita vinavyoendelea kila siku kati ya wema (Mungu) na ubaya (Shetani) kwa ajili ya nafsi yako, wewe binafsi.
Kwa hivyo tulia na ufurahie kisa hiki kifupi, ingawa kina uzito wake. Lengo langu ni kuwa ukimaliza kukisoma kitabu hiki, utakuwa umemfahamu kabisa mshindi wa Medali ya Heshima ambaye ni Mwokozi Yesu Kristo. Yesu anakupenda na anataka kuwa na uhusiano mwema na wewe, uhusiano utakao leta mabadiliko kwa nafsi yako, kutoka kiumbe ulicho sasa hadi kiumbe kipya. Roho yako ndio msingi wa kitabu hiki.
Mwandishi Danny Clifford
* * *
Tathmini
Katika Eneo la Adui: Kuokolewa na Silaha ya Siri; ni kisa chenye uhakika na cha kuvutia sana. Napenda vile ulivyohusisha ulimwengu wa vita nchini Vietnam na ulimwengu tunaoishi kila siku tukikabiliana na adui na umuhimu wa kumtegemea Roho wa