(Shab'ha-ye Peshawar)
Kupangwa katika Kompyuta na: Ukhti Pili Rajab. Toleo la kwanza: Augasti,2008 Nakala: 2000
Kimetolewa na kuchapishwa na: Alitrah Foundation S.L.P. 19701 Dar es Salaam, Tanzania Simu: +255 22 2110640 Simu/Nukushi: +255 22 2127555 Barua Pepe: alitrah@raha.com Tovuti: www.alitrah.org Katika mtandao: www.alitrah.info
YALIYOMO
Peshawar {Mikesha ya peshawar}............................................................................2
Mkutano wa Kwanza.
Uhusiano na Mtukufu Mtume...................................................................................4 Nyongeza ya ushahidi kuthibitisha kwa kizazi cha Fatma ni dhuria wa Mtukufu Mtume.......................................................................................................................6 Kwa nini Shia wanachanganya swala zao...............................................................8 Jinsi wazazi wa Allama walivyohama kutoka Hijazi kwenda Iran.........................12 Jinsi kaburi la Amirul -Muminin Ali (a.s) lilivyogunduliwa.................................12 Bani Umayya na utiaji Najisi wa Makaburi............................................................13 Matendo maovu ya ufalme huu kugunduliwa kwa kaburi tukufu la Ali.......................................................................................................................... 14 Khitilafu kuhusu sehemu aliyozikwa Amir ul-Muminin........................................15
Watu wa Yasin inawahusu watu wa Muhammad..................................................31 Salawat juu ya Muhammad na Aali-Muhammad ni Sunna (iliyokokotezwa), na katika swala za Faradhi ni wajibu..........................................................................32
Kwa nini Mitume walitafuta misaada kutoka kwa watu?.......................................49 Dhuria watukufu wa Muhammad ni njia (Wasyla-visababisho) neema za Mungu.50 Hadithi Ath-Thaqalaini (Hadith ya vizito viwili)....................................................51 Bukhari na Muslim wameandika Hadithi nyingi zilizosimuliwa na wazushi........53 Je, Yazid anapaswa kulaaniwa?..............................................................................70 Kuvunjwa heshima ya makaburi.............................................................................71 Dhuria wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w) ni mashahidi katika njia ya Allah na wako hai.......................................................................................................................... 72 Daraja ya Maimamu Masumin..............................................................................73
Sifa za Ali...............................................................................................................87 Umuhimu wa cheo cha Ali......................................................................................88 Wakati akiwa kwenye rukuu katika sala ali alitoa pete kumpa masikini...............92 Cheo cha Harun kama Mtume kadhalika kama Khalifa........................................92
Mtukufu Mtume (s.a.w.w) alimpendelea Ali kuliko watu wengine wote..............120 Hadith ya ndege aliyebanikwa..............................................................................121 Watu wenye kumbukumbu ni Ahli Muhammad dhuria wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w)................................................................................................................124 Aya za Quran Tukufu kuhusu kuchaguliwa kwa Makhalifa wanne, na majibu..124 Hoja kutokana na Aya ya Pango na majibu yake..............................................126 Kuteremshwa kwa utulivu kulikuwa kwa ajili ya Mtume wa Allah.....................131
Uthman aliwapiga masahaba wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w) Bila huruma.........159 Ammar alipigwa kwa amri ya Uthman.................................................................160 Hadith, Masahaba wote ni kama nyota namhusu na Abu Dharr vile vile............163 Upole na Ukarimu wa Ali bin Abu Talib ..............................................................164 Upole wa Ali kwa Marwan na Abdullah bin Zaubair..........................................165 Upole wa Ali kwa Aisha........................................................................................166 Mashaka na utata kuhusu Aya ya walii na ufafanuzi wake................................168
Ali aliburuzwa kutoka nyumbani kwake na nyumba yake ikachomwa moto.....200 Hoja kumi na mbili zinazounga mkono ukweli kwamba Ali alichukuliwa kupelekwa msikitini kwa ncha ya upanga........................................................................201 Fatma aliwaambia Abu Bakr na Umar kwamba anawalaani hao wote katika kila Salat......................................................................................................................203 Riwaya kuhusu kuharibika mimba ya Fatma........................................................205 Imamu Husein kamwe hakutamani nguvu ya kisiasa...........................................206 Imamu Husein alikataa ushauri wa kuuacha ujumbe wake..................................208 Maana halisi ya Bidaa (uzushi)...........................................................................212 Faida za kuzuru makaburi ya maimam watukufu.................................................213
Baba na Mama zake Mtukufu Mtume hawakuwa washirikina bali wlaikuw awote ni waumini........................................................................................................... 350 Wahenga wa Ali vivyo hivyo waliepukana na ushirikina.....................................352 Kutoeleweka kuhusu imani ya Abu Talib kwa fafanuliwa...................................352 Ijma ya Shia kuhusiana na Imani ya Abu Talib...................................................353 Ushahidi juu ya Imani ya Abu Talib ....................................................................354 Beti za Abil-Hadid katika kumtukuza Abu Talib.................................................355 Beti za Abiu Talib huthibitisha Uislamu wake.....................................................356 kukubali kwa Abu Talib imani yake juu ya Allah wakti wa kifo chake...............358 Mazungumzo ya Mtukufu Mtume na Abu Talib wakati wa Tangazo la Utume wake......................................................................................................................359 Tangazo la Ibrahim la utume na mazungumzo yake na Azar...............................359 Au Talib amhakikishia Mtukufu Mtume msaada kamili na pia asome mashairi katika kuusifu Uislamu.............................................................................................. 359 Abu Talib alikuwa msaidizi na mlezi wa Mtukufu Mtume ................................ 360 Sio sahihi kumwita Muawiya Khalul-Muminin ............................................. 361 Muawiya alitamka Takbir wakati wa kifo cha kishahidi cha Imam Hasan....... 362 Muhammad bin Abi Bakr aliuawa akiwa na kiu na kuchomwa hadi majivu kwa ajili ya mapenzi ya Ahlul-l-Bayt..........................................................................362 Muawiya hakuwa mwandishi wa wahyi bali wa barua tu...................................363 Ushahidi wa ukafiri wa Muawiya........................................................................363 Ushahidi kutoka sura za Qurani tukufu na Hadith-Muawiya na Yazid wamelaaniwa......................................................................................................................... 363 Mauaji ya waumini mashuhuri kama Imam Hasan, Ammar, Hajar bin Adi Malik Ashtar, Muhammad bin Abi Bakr, n.k. kwa Amri ya Muawiya..........................365 Mauji waumini 30,000 waliouawa na Busr bin Artat kwa amri ya Muawiya.....366 Muawiya alitoa Amri kwamba Ali alaaniwe........................................................367 Masahaba wa Mtume walikuwa katika viwango tofauti za uwelewa..................368 Quran tukufu inawasifia masahaba wema lakini pia inawalaani masahaba waovu................................................................................................................... 371 Abu Talib alikuwa muumini imara ..................................................................... 372 Ushahidi wa nyongeza juu ya imani ya Abu Talib...............................................372
Jafar Tayyar amekubali Uislamu kwa amri ya Baba yake..................................372 Nauha za Ali kwa ajili ya baba yake, Abu Talib.................................................374 Abu Talib alificha imani yake ambapo Abbas na Hamza walitangaza za kwao..374 Kwa nini Abu Talib ilikuwa ikijulikana kwa kawaida wakati wa uhai wa mtukufu Mtume...................................................................................................................375 Sunni kwa kweli ndio marafidhi na Mashia ndio Sunni hasa.............................376 Hoja za uhalali wa Muta.....................................................................................377 Ahli Sunna wazingatia uhalali wa Muta..............................................................379 Amri ya inayoruhusu Muta haikufutwa.............................................................. 380 Masahaba maarufu na Imam Malik wanasisitiza kwamba amri ya Muta haijafutwa........................................................................................................................ 381 Masharti yote ya ndoa yanatimizwa katika ndoa ya muta................................. 382 Je, amri ya Quran juu ya muta ilifutwa na mtukufu Mtume?............................383 Hoja zinazohusu kufutwa kwake wakati wa uhai wa Mtume..............................383 Je, Khalifa Umar angeweza kuifuta muta...........................................................384 Amri ya Allah au ya Mtukufu Mtume haiwezi kufutwa na Khalifa ...................386 Manufaa sio misingi kwa ajili ya ufutaji .............................................................387 Imani ya Abu Talib ilikuwa inajulikana sana wakati wa Mtukufu Mtume...........388 Mahali alipozaliwa Ali ilikuwa ni ndani ya Kaaba.............................................388 Asili ya jina la Ali ilikuw ani ulimwengu usionekana.......................................... 389 Baada ya majina ya Allah na Mtukufu Mtume jina la Ali limeandikwa juu ya Arsh..................................................................................................................... 390 Maneno yaliyotumiwa na Adam kwa ajili ya kukubaliwa kwa Toba yake yalikuwa ni majina ya watoharifu watano............................................................................392 Wahyi na Uham vilivyotolewa kwa watu wengine mbali na mitume, hata kwa wanyama...............................................................................................................392 Ufunuo wa Lawh (Uba) kwa Abu Talib................................................................394 Jina la Ali sio sehemu ya Adhana au Iqama.........................................................395 Uchamungu wa Ali...............................................................................................395 Riwaya ya Abdullah bin Rafii ............................................................................395 Riwaya ya Suwaid bin Ghafla..............................................................................396 Ali alijizui kula Halwa..........................................................................................396
Mavazi ya Ali........................................................................................................397 Mazungumzo ya Zubar na Muawiya kuhusu Ali.................................................398 Utambuzi wa Mtume juu ya Uchamungu wa Ali.................................................398 Allah na Mtukufu Mtume walimuita Ali Imamul-Muttaqin (Kiongozi wa wachamungu).......................................................................................................399 Kama Imaml-Muttaqin Ali hakuwa na mapenzi ya kujingiza kwenye anasa au Mamlaka.............................................................................................................. 400 Ukimya wa Mitume watukufu............................................................................ 403 Hali ya Ali inafanana na ya Harun.......................................................................404 Kunyamaza kwa Mitume......................................................................................404 Maelezo ya Ali juu ya kufaa kwa kimya chake baada ya kifo cha Mtukufu Mtume...................................................................................................................406 Barua ya Amirull-Muminin kwa watu wa Misr kuelezea ukimya wake wakati aliponyimwa Ukhalifa..........................................................................................407 Khutba ya Amirul-Muminin baada ya kuuawa shahidi kwa Muhammad bin Abu Bakr.......................................................................................................................408 Khutba ya Shaqshiqayya vile vile na elezea ukimya wa Ali................................409 Seyyid Razi...........................................................................................................409
Amri ya Mtume ya kumtii Ali...............................................................................426 Ulamaa wa Kisunni hawataki Ushirikiano na sisi................................................427 Tofauti ya madhehebu manne zinapuuzwa bali Shia hawavumiliwi...................429 Fatwa za wanachuoni wa Sunni zinakwenda kinyume na maelekezo ya Qurani............................................................................................................... .429 Kuosha miguuu katika udhu ni kinyume na sheria ya Qurani........................... 432 Kupaka juu ya soksi ni kinyume na sheria ya wazi ya Quran Tukufu................433 Kupaka juu ya kilemba ni kinyume na sheria ya Qurani....................................434 Shia pekee wanaolaumiw akwa tofauti kama hizo..............................................434 Kwa mujibu wa ulamaa wa Kisuni kusujudu juu ya kinyesi kikavu na kinyesi cha mnyama ni halali.................................................................................................. 435 Kwa mujibu wa ulamaa wa Kisunni kusujudu juu ya kinyesi kikavu na kinyesi cha mnyama ni halali..................................................................................................435 Shia hawachukulii kusujudu juu ya udongo wa karbala kuwa ni wajibu............436 Kwa nini tunasujudu juu ya ule udongo wa Karbala............................................437 Sifa za Hali ya udongo wa Karbala ....................................................................437 Umri mkubwa sio kigezo cha Ukhalifa................................................................439 Sababu ya kuteuliwa Ali.......................................................................................441 Hadithi ya kufuatana na Abu Bakr .......................................................................441 Mtukufu Mtume alimtuma Ali kwenda Yemen.....................................................442 Njama za maadui ..................................................................................................443 Ali alichukia siasa ya dhulma chafu.....................................................................443 Vurugu wakati wa Ukhalifa wa Amirul-Muminin zilitokana na uadui dhidi yake.......................................................................................................................444 Vita vya Ali vya Jamal, Siffin na Nahrwan vilikuwa kama vita vya Mtukufu Mtume dhidi ya makafiri...................................................................................................445 Baada ya mtukufu Mtume Ali alikuwa ndiye bingwa zaidi ya mambo ya utawala..................................................................................................................446 Ali alikuwa na Elimu ya ulimwengu wa Ghaib....................................................446 Je Elimu ya Ghaibu imetengwa kwa Allah tu?.................................................... 447 Elimu ni ya namna mbili, ya dhati (ya asili) na Arzi( ya kutafuta).................... .450 Ushahidi wa Quran kwamba Mitume walikuwa na elimu ya Ghaib..................451 Madai yakuwa na elimu ya ghaib kupitia njia nyinginezo ni ya uongo.............. 452 Waandamizi wa mitume pia walikuwa na Elimu ya ghaib................................. 453 Maimamu watukufu walikuwa ndio makhalifa wa kweli na walikuwa na Elimu ya ghaib................................................................................................................... 455 Lango la Elimu.................................................................................................... 456 Ulamaa wa Sunni ambao wamesimulia ile Hadithi ya Jiji la Elimu................457
Kusimulia sifa za Ali ni ibada..............................................................................459 Ufafanuzi wa Hadith ya Lango la Elimu...........................................................461 Ali alijua maana ya dhahiri na ya ndani ya Qurani tukufu.................................461 Kuikabidhi Elimu ya Mtume kwa Ali...................................................................464 Jafr-e-Jamia na asili yake....................................................................................465 Imam Ridhaa alitabiri kifo chake .........................................................................467 Jibril alileta kitabu kilichofungwa sili (sealed) kwa ajili ya wasii wa Mtukufu Mtume...................................................................................................................468 Tangazo la Ali la niulizeni mimi na Riwaya za Masunni...................................471 Elimu ya Ali kuhusu watu wanaongoza au wanaopotosha.................................473 Kuutabiri ule ushika bendera wa Habib bin Amamar.......................................... 474 Kutabiri ukandamizaji wa Muawiya.................................................................. 475 Kwa mujibu wa Mtukufu Mtume Ali aliwazidi wengine wote katika Elim....... 479 Ali alizimudu Sayansi zote.................................................................................. 482 Kuzaliwa kwa Imam Husain na pongezi za Malaika...........................................483 Kukubali Ushiah kwa Nawab-Sahib ..................................................................484
NENO LA MCHAPISHAJI
Kitabu kilichoko mikononi mwako ni tarjuma ya kitabu cha Kiingereza kiitwacho, Peshawar Nights. Asili ya kitabu hiki ni cha lugha ya Kifarsi kwa jina la, Shabha-ye Peshawar. Sisi tumekiita, Mikesha ya Peshawar. Mikesha ya Peshawar ni nakala ya mjadala kati ya wanavyuoni mbalimbali wa Kisunni na mwanachuoni mmoja wa Kishia mzaliwa wa Shiraz (Iran) aitwaye Sayyid Abdu l-Fani Muhammad al-Musawi Sultanu l-Waidhiin, ambaye wakati huo alikuwa na umri wa miaka 31 tu. Mjadala huu ulifanyika katika mji wa Peshawar ambao wakati huo ilikuwa ni sehemu ya Bara Hindi na hivi sasa ni sehemu ya Pakistan. Ulifanyika kuanzia tarehe 27 Januari 1927 na kuundelea kwa mikesha kumi ndani ya msikiti ambako watu zaidi 200 walihudhuria kila usiku. Mjadala huu ulifanywa kwa muundo mzuri wa kuheshimiana pande zote bila ya kuvunjiana heshima. Mwandishi mwenyewe amejiita katika kitabu hiki kama Dai yaani mtu anayewaombea mema watu wengine, sisi tumelitafsiri neno hilo kama Muombezi. Masharti ya mjadala yalikuwa kwamba ni vianzo vile tu vinavyokubaliwa na madhehebu zote ndivyo vitakavyorejelewa. Mjadala huu uliandikwa na kuripotiwa na waandishi wanne katika magazeti ya kila siku, na baadaye ukachapishwa kama kitabu huko Tehran, Iran. Huu ulikuwa ni mjadala uliopangwa vizuri, wa kielimu na utumiaji wa vipawa vya akili ambapo kila hoja iliyotolewa ilitumika elimu na akili kuiwasilisha mpaka pande zote zikaridhika. Katika kuwasilisha hoja zake, mwanachuoni huyu mkubwa wa Kishia alitumia rejea za vitabu vingi maarufu vya Kisunni na ambavyo si maarufu sana lakini vyenye kuaminika. Rejea na vitabu hivyo vimeorodheshwa kwa wingi sana ndani ya kitabu hiki ili msomaji aweze kuvirejelea. Lakini kwa bahati mbaya sana, mengi ya matoleo mapya ya vitabu hivyo yamefanyiwa mabadiliko na baadhi ya sehemu kuondolewa, hususan zile zinazounga mkono madai ya Shia. Ufuatao hapa chini ni mfano mdogo tu wa yanayofanywa katika vitabu hivyo: Katika ukurasa wa 301 wa juzuu ya 3 ya Tafsir al-Kashshaaf iliyokusanywa chini ya maelekezo ya Sheikh Mustafa al-Halabi (toleo la pili, 1319 A.H. liliochapishwa na Main Government Printing House ya Amiriah Bulaq ya Misir), kuna beti zinazojitokeza ambazo kwazo Jarullah Zamakhshari, mfasiri wa al-Kashshaaf, alitangaza wazi imani yake katika uhalali wa Ushia. Lakini katika chapisho la 1373 A.H. lililochapishwa na Printing House Istiqamah bil-Qahara, shairi lililotajwa halionekani tena.
Marehemu Allamah Sayyid S. Akhtar Rizvi katika kitabu chake Uimamu uk. 37, anaandika kushangazwa kwake kutokana na maneno yaliyoondolewa katika kitabu cha at-Tarikh cha at-Tabari, chapa ya Leiden (ya mwaka 1879 Masihia) ambayo imeyanakili maneno ya Mtukufu Mtume (s.a.w.) aliyoyatumia wakati wa karamu maarufu ya ndugu wa karibu aliyoitayarisha mwenyewe. Maneno ya mwisho aliyoyasema Mtukufu Mtume (s.a.w.) katika karamu hiyo yalikuwa haya: Enyi watu wangu! Huyu Ali ni ndugu yangu, wasii wangu na khalifa wangu miongoni mwenu; msikilizeni na mtiini. Lakini katika chapa ya Misri (ya mwaka 1963 Masihia) - chapa ambayo inayodaiwa kuwa imechekiwa na ile ya Leiden - maneno haya muhimu: wasii wangu na khalifa wangu yamebadilishwa na kuwa kadha wa kadha na kusomeka hivi: Huyu Ali ni ndugu yangu na kadha wa kadha. Huu ni msiba mkubwa. Sultanu l-Waidhiin, mwandishi wa kitabu hiki, amedondoa rejea nyingi kutoka katika matoleo ya zamani, hivyo, msomaji asishangae kutokuona rejea hizo katika matoleo mapya. Huu ni mchezo umefanywa na unaendelea kufanywa mpaka leo. Na lengo ni kuficha ukweli. Hata hivyo, ukweli siku zote unaelea; matoleo ya zamani yapo mengi na yamehifadhiwa kwenye maktaba zetu. Ni muhimu kufikia kila aina ya maoni katika kujaribu kuamua ukweli. Uislamu kimsingi uko dhidi ya kufuata kibubusa. Mjadala huu umefanywa ili kuwaelemisha Waislamu kwa ujumla juu ya madhehebu za Kiislamu ili kujenga maoni yao kuhusu mtazamo mzuri wa mtu mwenyewe. Ni muhimu mtu kuelewa hoja za wale ambao hakubaliani nao. Inawezekana kusemwa kwamba wale ambao hawaelewi kabisa mtazamo wa maoni tofauti, hawaelewi kwa ukamilifu (mtazamo) wa kwao wenyewe. Hili tena ni jaribio letu kubwa la kutoa kitabu kikubwa kinachohusu mjadala juu ya madhehebu za Kiislamu. Tumekiona kitabu hiki ni chenye manufaa sana, hususan wakati huu wa maendeleo makubwa ya elimu katika nyanja zote, ambapo uwongo, ngano za kale na upotoshaji wa historia ni mambo ambayo hayana nafasi tena katika akili za watu. Kutokana na ukweli huo, Taasisi yetu ya Al-Itrah Foundation imeona bora kukichapisha kitabu hiki kwa lugha ya Kiswahili, kwa madhumuni yake yaleyale ya kuwahudumia Waislamu, hususan wazungumzaji wa Kiswahili. Tunamshukuru ndugu yetu, Dr. M. S. Kanju kwa kukubali jukumu hili la kukitarjumi kitabu hiki. Vilevile tunawashukuru wale wote walioshiriki kwa njia moja au nyingine hadi kufanikisha kuchapishwa kwa kitabu hiki. Mchapishaji:
Mikesha ya Peshawar
PESHAWAR
(MIKESHA YA PESHAWAR)
Sultanul-Waizin Shirazi, mwanachuo mkubwa wa Iran, alitembelea India mwaka wa 1927 (1345 A.H.) wakati akiwa na umri wa miaka 30. Alipata makaribisho makubwa popote alipokwenda. Watu walinufaika kutokana na ujuzi wake wa hadithi, historia, na tafsiri juu ya Qurani Tukufu. Alishauriwa kuingia katika mjadala wa kidini tarehe 23 Rajab, 1345 A.H., na watu wa imani nyingine katika eneo la Peshawar, eneo ambalo lilikuwa ni katika India na ambalo leo ni eneo la Pakistan. Mjadala ulifanyika kwa muda wa mikesha kumi mfulululizo. Washiriki wakubwa wawili kutoka upande mwingine walikuwa ni wanachuoni maarufu wa Kabul, Hafidh Muhammad Rashid na Sheikh Abduls-Salam. Waandishi wanne waliandika taarifa za mjadala huo mbele ya watu takirban 200 (Shia na Sunni). Magazeti ya sehemu hiyo yaliandika taarifa za mjadala huo kila siku asubuhi iliyofuatia. Sultanul-Waidhin alikusanya maelezo ya magazeti kuhusu mjadala huo katika kitabu nchini Iran, na kuchapishwa Tehran kama Shabhaye-Peshawar, au Peshawar Nights ifuatayo ni tarjuma ya kitabu hicho:
Mikesha ya Peshawar
Mkutano wa kwanza
(Usiku wa Alhamisi, 23 Rajab, 1345 A.H.) Hafidh Muhammad Rashid, Sheikh Abdus-Salam, Sayyid Abdul-Hayy, na wanachuoni wengine wa eneo hilo walihudhuria. Mjadala ulianza mbele ya mkusanyiko mkubwa. Katika majarida na magazeti, walimuita mwandishi kama Qibla-o-Kaba, lakini katika kurasa hizi nimejiita mwenyewe kama Muombezi na Hafidh Muhammad Rashid kama Hafidh. Hafidh: Tumefurahishwa sana kupata fursa hii ili kujadili nukta za msingi ambazo kwazo tunahitilafiana. Kwanza lazima tuamue jinsi tutakavyo endesha mjadala huu. Muombezi: Niko tayari kushiriki katika mjadala huu kwa masharti kwamba tunaweka kando mawazo yote tuliyokuwa nayo kabla (juu ya imani zetu), na kujadili masuala kwa mantiki, kama ndugu. Hafidh: Mimi pia niruhusiwe kutoa sharti moja: kwamba mjadala wetu uwe chini ya msingi wa maamrisho ya Qurani Tukufu. Muombezi: Sharti hili halikubaliki kwa vile Qurani Tukufu ni yenye habari nyingi katika maelezo machache ambayo maana zake za ndani lazima zitafsiriwe kwa kurejea kwenye matukio mengine na hadithi. Hafidh: Sawa, hili ni wazo la maana, lakini vile vile ni muhimu kwamba rejea zote zifanywe kwenye hadithi na matukio ambayo chimbuko lake ni juu ya ushahidi usiopingika. Lazima tujizuie kutokana na kurejea kwenye vyanzo vyenye mashaka. Muomezi: Imekubalika. Kwa mtu kama mimi, ambaye ana fahari ya kutosha kudai uhusiano na Mtume, sio haki kwenda kinyume na mifano iliyowekwa na jadi wangu, Mtume wa Uislamu. Ametambulishwa katika Qurani kama ifuatavyo:
Na hakika una tabia njema kabisa. (Qurani; 68:4) Vile vile sio vizuri kutenda dhidi ya maamrisho ya Qurani Tukufu ambayo inasema:
Mikesha ya Peshawar
Waite watu katika njia ya Mola wako kwa hikima na mauidha mema, na ujadiliane nao kwa nama iliyo bora (16:125)
Mikesha ya Peshawar
Muombezi: Kuna ushahidi imara, kutoka katika Qurani na kutoka katika hadithi, kuthibitisha nukta yangu. Hafidh: Tafadhali usimulie ili tupata kuelewa. Muombezi: Wakati ulipokuwa unaongea sasa hivi, nimekumbuka mazungumzo kati ya Harun ar-Rashid, Khalifa wa Kibani Abbas, na Imamu wetu Musa Kadhim juu ya suala hili. Imamu alitoa jibu la kuridhisha kiasi kwamba Khalifa mwenyewe alilikubali. Hafidh: Ningependa kusikia kuhusu mazungumzo hayo. Muombezi: Abu Jafar Muhammad Bin Ali, mwenye lakabu ya Sheikh Saduq, katika karne ya nne A. H., katika kitabu chake Uyun-e-Akbar ar-Ridha (vyanzo vikubwa vya Ridha), na Abu Mansur Bin Ali Tabarsi, katika kitabu chake Ihtijajj, anatoa maelezo kinaganaga ya mazungumzo ambayo yalifanyika kati ya Harun ar-Rashid na Imamu Musa Jafar katika baraza ya Khalifa. Khalifa alimuuliza Imamu: Unawezaje kudai kwamba wewe ni dhuria wa Mtukufu Mtume? Mtume hana dhuria. Inakubaliwa kwamba dhuria ni kutoka upande wa kiume na sio upande wa kike. Wewe ni kizazi cha bint yake. Imamu akasoma Aya ya 84-85 kutoka Sura ya 6 ya Qurani Tukufu:
Na tukampa (Ibrahim) Ishaqa na Yakuub, wote tukawaongoa. Na Nuh tulimuongoa zamani, na katika kizazi chake Daudi na Suleimani na Ayub na Yunus na Musa na Harun. Na hivi ndivyo tuwalipavyo wafanyao mema. Na Zakaria na Yahya na Isa na Ilyasa, wote walikuwa miongoni mwa watu wema. (6:84-85) Imamu akamuuliza Khalifa: Ni nani aliyekuwa baba wa Isa? Harun akajibu kwamba Isa alikuwa hana baba. Imamu akasema: Kulikuwa hakuna yeyote aliyekuwa baba yake, na bado Allah alimjumuisha Isa katika dhuria wa mitume kupitia Mariamu. Hivyo hivyo ametujumuisha sisi katika dhuria wa Mtume kupitia kwa jadi wetu Bibi Fatima. Aidha, Imamu Fakhurd-Din Razi, katika kitabu chake Tafsir-e-Kabir, juzuu ya 4, uk. 124, anasema kuhusiana na aya hii kwamba, inathibitisha kwamba Hasan na Husein ni watoto wa Mtume wa Uislamu. Kwa vile katika aya hii Mungu amemdhihirisha Isa kama kizazi cha Ibrahim, na
Mikesha ya Peshawar
Isa hana baba, uhusiano huu ni kutoka upande wa mama. Katika hali hiyo hiyo, Hasan na Husein ni dhuria wa kweli wa Mtume. Imamu Musa alimuuliza Harun kama anataka uthibitisho zaidi. Khalifa akamuambia Imamu aendelee. Imamu akasoma Aya ya 61 kutoka Sura ya 3 ya Qurani Tukufu: Watakao kuhoji katika haya baada ya kukufikia ilmu, waambie: Njooni tuwaite watoto wetu na watoto wenu, na wanawake wetu na wanawake wenu, na sisi na ninyi, kisha tuombe kwa unyenyekevu tutake laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie waongo, Aliendelea, akisema kwamba hakuna mtu hata mmoja ambaye amewahi kudai kwamba katika tukio hilo la maapizano (Mubahila) dhidi ya Wakiristo wa Najran kwamba Mtume alimchukuwa pamoja na yeye mtu yeyote isipokuwa Ali Bin Abi Talib, Fatima, Hasan na Husein. Kwa hiyo hufuatia kwamba sisi (anfusana) maana yake ni Ali Bin Abi Talib. Wanawake (nisaana) maana yake Fatima na Watoto (abnaana) maana yake Hasan na Husein, ambao Allah amewatambulisha kama watoto wa Mtume mwenyewe. Kwa kusikia hoja hii, Harun aliguta, Hongera, Ewe Abul-Hasan. Kwa uwazi mantiki hii huthibitisha kwamba Hasan na Husein (watoto wa Bibi Fatima) ni watoto wa Mtukufu Mtume.
NYONGEZA YA USHAHIDI KUTHIBITISHA KWAMBA KIZAZI CHA FATIMA NI DHURIA WA MTUKUFU MTUME.
Ibn Abil-Hadid Mutazali, mmoja wa wanachuoni wenu wakubwa, katika kitabu chake Sharhl-Nahjul-Balagha, na Abu Bakr Razi katika tafsir yake, wameionesha aya hiyo hiyo wakithibitisha kwamba Hasan na Husein wanatoka upande wa mama yao, ni watoto wa Mtukufu Mtume katika njia ile ile ambayo Allah katika Qurani Tukufu amemjumuisha Isa katika kizazi cha Ibrahim kutoka upande wa mama yake, Mariamu. Muhammad Bin Yusuf Ganji Shafii, katika kitabu chake Kifayatut-Talib; Ibn Hajar Makki katika ukurasa wa 74 na 93 wa Sawaiq Muhiriqa, kutoka kwa Tabrani na Jabir Bin Abdullah Ansari, na Khatib Khawarizmi katika Manaqib kutoka kwa Ibn Abbas - wote wanasimulia kwamba Mtume alisema: Allah ameumba dhuria wa kila Mtume kutokana na kizazi chake mwenyewe, lakini dhuria wangu waliumbwa katika kizazi cha Ali. Vile vile Khatib-e-Khawarizmi katika Manaqib; Mir Seyyid Ali Hamadani Shafii katika Mawaddatul-Qubra; Imamu Ahmad Bin Hanbal, katika Musnad, na Sulayman Hanafi Balkhi katika Yanabiul-Mawadda wanasimulia katika maneno hayohayo kwa zaidi au pungufu, kwamba Mtukufu Mtume amesema: Watoto wangu hawa wawili, ni maua mawili ya ulimwengu huu, na wote wawili ni Maimamu, imma wawe ni Maimamu kwa wazi au kimya kimya wakiwa wamekaa nyumbani. Na Sheikh Sulayman Hanafi, katika Yanabiul-Mawadda, ameitoa sura ya 57 kwenye suala hili na akaonesha hadithi nyingi
Mikesha ya Peshawar
kutoka kwa wanachuoni wake mwenyewe, kama Tabrani, Hafidh Abdul-Aziz Ibn Abi Shaiba, Khatib-e-Baghdadi Hakim, Baihaqi, na Tabari - wote wanasimulia katika maneno yanayohitalifiana kidogo kwamba Hasan na Husein ni watoto wa Mtume. Kuelekea mwisho wa sura hiyo hiyo, Abu Salih anaandika: Hafidh Abdul-Aziz Bin AlAkhzar, Abu Nuaim, Tabari Ibn Hajar Makki katika ukurasa wa 112 wa Sawaiq Muhriqa, kutoka kwa Muhammad Bin Yusuf Ganji Shafii mwishoni mwa jalada la 1, baada ya sura 100 za Kifayatut-Talib, na Tabari katika simulizi ya Imamu Hasan anasimulia kwamba Khalifa wa pili, Umar Bin Khattab, alisema: Nilimsikia Mtume akisema kwamba katika Siku ya Hukumu kila ukoo utatenganishwa isipokuwa kizazi changu. Kila kizazi cha binti ni kutoka upande wa baba isipokuwa kizazi cha Fatima, ambacho kimeunganishwa na mimi. Mimi ni baba yao na jadi wao. Sheikh Abdullah Bin Muhammad Bin Amir Shabrawi Shafii, katika kitabu chake Kitabul-Ittihaf bi Hubbil-Ashraf, alinukuu hadithi hii kutoka kwa Baihaqi na Darqutni kutoka kwa Abdullah Bin Umar, na yeye kutoka kwa baba yake, kwenye harusi ya Ummu Kulthum. Na Jalalud-Din Suyuti akinukuu kutoka kwa Tabrani katika kitabu chake Ausat, amesimulia kutoka kwa Khalifa Umar na Sayyid Abu Bakr Bin Shahabud-Din Alawi katika ukurasa wa 39-40 wa sura ya 3 ya RishfatusSadi min bahra Fadhail Bani Nabiul-Hadi (iliyopigwa chapa katika Maktabi Alamiyya, Misr 1303 A.H.) huthibitisha kwamba dhuria wa Fatima ni kizazi cha Mtume wa Uislamu. Kwa hiyo, ubeti ambao umeunukuu hauna nguvu mbele ya ushahidi wote huu wa kinyume chake. Muhammad Bin Yusuf Ganji Shafii, katika kitabu chake Kifayatut-Talib, anathibitisha kwamba watoto wa binti wa Mtume ni watoto wa Mtukufu Mtume. Halikadhalika, kuna hadithi nyingine nyingi ambazo huthibitisha kwamba watoto wa Bibi Fatima ni watoto wa Mtume. Safu yetu ya jadi huenda mpaka kwa Imamu Husein; kwa hiyo, sisi ni dhuria wa Mtume. Hafidh: Hoja yako ni ya mantiki na kuridhisha. Watu walitawanyika kwa ajili ya Swala ya Isha. Wakati wa mapumziko Nawab AbdulQayum Khan, ambaye anatokana na familia sharifu ya Kisunni, alitaka ruhusa kumuuliza Muombezi maswali fulani.
Mikesha ya Peshawar
Mikesha ya Peshawar
kumuuliza kuhusu maneno hayo. Alithibitisha kile alichokisema Ibn Abbas. Kupitia sanad nyingine ya wasimuliaji, Abdullah Bin Shaqiq alisimulia kutoka kwa Aqil kwamba siku moja Abdullah Ibn Abbas aliwahutubia watu juu ya mimbari. Alibaki pale kwa muda mrefu mpaka giza likaingia. Wakati mtu mmoja alipopiga kelele mara tatu, Swala, Swala, Swala, Abdullah Ibn Abbas alikasirika na akasema: Ulaaniwe wewe. Unathubutu kunikumbusha mimi kuhusu Swala, ingawaje wakati wa Mtukufu Mtume tulizoea kukusanya Swala za Adhuhr na Alasir na halikadhalika Magharib pamja na Isha. Zarqani katika Sharhe Mawatta cha Imamu Malik, jalada la 1, katika sura ya Jamaa Bainas-Salatain, ukurasa wa 263, anaeleza, Nisai alisimulia kutoka kwa Amru Bin Haram kutoka kwa Abi Shaatha kwamba Ibn Abbas aliswali Dhuhr na Alasir na halikadhalika Magharib na Isha kwa pamoja mjini Basra bila kukawia au kitendo chochote kati yao. Alisema kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) aliswali katika njia hii hii. Vile vile Muslim katika Sahih yake na Malik katika Mawatta, sura ya Jama BainasSalatain, na Imamu Hanbal katika Musnad wanamnukuu Ibn Abbas kutoka kwa Said Bin Jabir kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) aliswali Swala zake za Dhuhr na Alasir pamoja mjini Madina bila kulazimishwa kufanya hivyo kwa hofu au hali mbaya ya hewa. Abu Zubair akasema alimuuliza Abu Said kwa nini Mtume alikusanya Swala hizo mbili. Said akasema yeye vile vile alimuuliza Ibn Abbas swali kama hilo hilo. Ibn Abbas alijibu kwamba alikusanya Swala hizo mbili ili kwamba wafuasi wake wasije wakawekwa katika uzito na shida zisizo na sababu. Vile vile, katika hadithi nyingine nyingi, Ibn Abbas inasimuliwa kwamba alisema Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) wa Uislamu alikusanya Swala za Dhur na Alasir halikadhalika na Magharib na Isha bila kulazimishwa kufanya hivyo. Hadith hizi katika Sahihi zenu na vitabu vyingine sahihi huthibitisha kuruhusiwa ukusanyaji wa Swala mbili, nyumbani au safarini. Hafidh: Hakuna nukuu kama hiyo ya hadithi katika Sahih Bukhari. Muombezi: Kwa sababu waandishi wote wa Sahih, kama vile Muslim, na Nisai, Ahmad Bin Hanbal, na wafasir wa Sahih mbili, ya Muslim, Bukhari, na wanachuoni wengine wakubwa wa ki-Sunni wamenukuu mambo haya, hii inatosha kwetu kuishindisha nukta yetu. Lakini kwa kweli Bukhari vile vile ameziandika hadithi hizi katika Sahih yake, lakini kwa hila ameziweka mbali na sehemu zao husika, ile sehemu inayohusika na ukusanyaji wa Salat mbili. Kama utaipitia ile milango ya Bab-e-Taakhirudh-Dhuhur lil-Asr Min Kitabe Mawaqtus-Salat na Bab-e-Dhikrul-Isha wal-Atma na Bab-e-WaqitulMaghrib, utaziona hadithi zote hizi humo. Hadithi hizi kuandikwa chini ya kichwa cha habari: Ruhusa na Mamlaka ya Kisheria ya kukusanya Salat mbili huthibitisha kwamba ni imani ya kawaida ya wanachuoni wa madhehebu hizi mbili. Usahihi wa hadithi hizi umekwisha kubaliwa katika vitabu vya Sahih. Kwa sababu hiyo, Allama Nuri katika Sharhe Sahih Muslim, Asqalani, Qastalani, Zakariyya-e-Razi katika sharhe ambayo ime-
Mikesha ya Peshawar
andikwa juu ya Sahih Bukhari, Zarqani katika Sharhe yake juu ya Muwatta - kitabu cha Imamu Malik, na wengine wamesimulia hadithi hizi. Baada ya kunukuu hadithi ya Ibn Abbas, walikubali usahihi wake na wakakiri kwamba hadithi hizi ni uthibitisho wa kukubalika kwa kukusanya Salat mbili. Nawab: Imewezekanaje kwamba hadithi hizi zimekuwa katika matumizi tangia wakati wa uhai wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), lakini wanachuoni wamechukuwa njia nyingine? Muombezi: Hali hii haikomei kwenye nukta hii peke yake. Utaona mifano mingi kama hii baadae. Katika suala hili, Mafaqih wa ki-Sunni, kwa wazi bila ya kufikiria kwa makini, au kwa sababu nyingine ambazo mimi sizielewi, wametoa maelezo yasiyoleweka kukinzana na hadithi hizi. Kwa mfano, wanasema kwamba huenda hadithi hizi huzungumzia hali zinazohusiana na hofu, hatari, mvua, au upepo mkali. Baadhi ya wanachuoni wenu wa zamani, kama Imamu Malik, Imamu Shafii, na baadhi ya wanachuo wa Madina wametoa maelezo kama hayo hayo. Namna hii, pamoja na ukweli kwamba hadithi ya Ibn Abbas kwa uwazi kabisa inasema kwamba ukusanyaji wa Swala mbili ulikuwa unafanywa bila kikwazo cha hofu au uwezekano wa kunyesha mvua. Wengine wamesema kwamba huenda mawingu yalikuwa yametanda angani, na wale waliokuwa wakisali hawakujua ni saa ngapi. Pengine walipomaliza kusali Swala yao ya Adhuhur, mawingu yalitawanyika, na wakaona kwamba ilikuwa ni wakati wa Swala ya Alasir. Hivyo wakalazimika kusali Adhuhuri na Alasiri kwa pamoja. Sidhani maelezo zaidi yasiyo yamkinika yanaweza kupatikana. Pengine wafasiri hawa hawakujali kufikiria kwamba mtu aliyekuwa akisali Swala hizo ni Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) wa Uislamu. Mawingu hayakumaanisha kwake kile ambacho kingemaanishwa kwa wengine. Anajua sababu zote na matokeo. Mbali na ukweli kwamba maelezo haya hayaridhishi, ukusanyaji wa Swala za Mahgarib na Isha unakataa maelezo yao. Katika wakati huo mawingu hayana uhusiano na suala hili. Kama tulivyosema, hadithi ya Ibn Abbas kwa uwazi inaeleza kwamba khutuba yake iliendelea kwa muda mrefu mpaka wasikilizaji wakapiga kelele, Swala, Swala. Walimkumbusha kwamba nyota zimetokea na kwamba ilikuwa ni wakati wa Swala. Lakini aliichelewesha Swala ya Magharibi kwa makusudi ili aje kuswali zote, Magharib na Isha kwa pamoja. Abu Huraira vilevle alithibitisha kitendo hiki, akisema kwamba Mtume vile vile aliswali kwa nama hiyo hiyo. Maelezo ya uwongo kama hayo, katika mwanga wa mwongozo wa dhahiri, husikitisha. Wanachouni wenu wenyewe wameyapuuza hayo. Sheikhul-Islam Ansari, katika kitabu chake, Tuhfatul-Bari fi Sharhe Sahihul-Bukhari katika sura ya Salatuz-Dhuhr mal-Asr wal-Magharib mal- Isha ukurasa wa 292, jalada la 2, na halikadhalika Allama Qastalani, katika ukurasa wa 93 jalada la 2 la Irshadus-Sari fi Sharhe Sahihul-Bukhari, na hivyo hivyo na washereheshaji wengine wa Bukhari wanakiri kwamba aina hii ya maelezo ni kinyume na maana ya wazi ya hadithi na kwam-
10
Mikesha ya Peshawar
ba kusisitiza kwamba kila Swala iswaliwe peke yake ni mashrti yasiyo na msingi. Nawab: Basi mgogoro huu umejitokeza vipi mpaka madhehebu mbili za Waislamu kila moja inataka kumwaga damu ya mwenzake, na kulaumu kitendo cha mwenzake? Muombezi: Unasema kwamba madhehebu hizi mbili ni adui kwa kila mmoja, lakini sikubaliani na wewe. Sisi Mashia hatumdharau mwanachuoni yeyote au mtu wa kawaida katika ndugu zetu Masunni. Tunasikitika kwamba propoganda za Makhariji, Manasibi na Bani Umayyah zimeathiri nyoyo za baadhi ya watu. Kwa bahati mbaya sana, baadhi ya Masunni wanawachukulia ndugu zao Mashia, ambao wako pamoja nao kwa kuhusiana na Qibla (Kaaba), Kitabu Kitukufu (Qurani), Mtume, utekelezaji wa matendo ya dini, na kujiepusha kutokana na madhambi, kuwa kama Marafidhi (watofautishaji), waabudu masanamu, na makafiri. Amma kwa swali lako kuhusu vipi tofauti hizi zilivyojitokeza, labda hili tunaweza kulijadili katika mikutano yetu ya baadae. Kuhusu kusali Swala kwa kutenganisha au kwa pamoja, wanachuoni wa sheria wa ki-Sunni wenye kutegemewa wamenukuu hadithi ambazo huruhusu kusali Adhuhuri na Alasiri na Magharibi na Isha kama jambo la wepesi, wasaa au usalama. Sijui kwa nini baadhi ya watu hawaoni kwamba inaruhusika kusali Swala mbili pamoja pasi na kuwa na udhuru wowote. Baadhi ya wanachuo, kama Abu Hanifa na wafuasi wake wameikataza katika hali yoyote, iwe kuna udhuru au la, au Swala iwe inasaliwa wakati mtu akiwa safarini au nyumbani. Shafii, Maliki, na Hanbali, pamoja na hitilafu zao zote katika kanuni za msingi na zisizo za msingi, wameruhusu ukusanyaji wa Swala wakati wa safari ya halali. Lakini Maulamaa wa ki-Shia, wakiwa katika utii wa Imamu na kizazi cha Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) wameruhusu bila masharti yoyote ukusanyaji wa Swala mbili kwa pamoja. Hakika kusali Swala katika wakati ulioanishwa kwa kila Swala ni bora kuliko kuzisali kwa wakati mmoja, kama ambavyo imeelezwa kwa uwazi katika vitabu vya tafsir vinavyoshughulika na matatizo ya utekelezaji wa masuala ya dini vilivyoandikwa na Maulamaa wa ki-Shiah. Kwa vile watu mara nyingi wanakuwa na shughuli nyingi katika mambo yao wenyewe na wasi wasi, wanaogopa huenda wakazikosa Swala zao. Kwa hiyo, kwa nafasi zao na kuepuka uzito na shida, Mashia wanasali Swala zao mbili katika wakati mmoja, mapema au kwa kuahirisha, katika wakati ule ule uliotengwa kwa ajili ya Swala. Sasa nafikiri kiasi hiki kinatosha kuwapa mwanga ndugu zetu Masunni ambao hutuangalia kwa hasira. Bila shaka tunaweza kurudi kwenye majadiliano yetu kuhusu misingi, ambapo baadae masuala yanayohusu ibada yatatatuliwa.
11
Mikesha ya Peshawar
12
Mikesha ya Peshawar
jinai zao nyingi. Allama Maqrizi Abul-Abbas Ahmad bin Ali Shafii ameandika maovu ya Banu Umayya yanayoumiza moyo kabisa katika kitabu chake Annaza Wat-takhasum fima baina Bani Hashim wa Bani Umayya.
13
Mikesha ya Peshawar
14
Mikesha ya Peshawar
15
Mikesha ya Peshawar
16
Mikesha ya Peshawar
kusingekuwa na neno kama Shia katika Uislamu. Babu yako, Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alilichukia neno hilo. Kusema kweli madhehebu ya Shia ni sehemu ya imani ya Kiyahudi. Nashangaa kwa nini umeacha njia za haki za jadi wako na ukafuata njia ya waliokutangu lia, ambao wamefuata njia za Kiyahudi. Ilikupasa ufuate Qurani Tukufu na mfano wa babu yako, Mtume (s.a.w.w.).
17
Mikesha ya Peshawar
Wala hasemi kwa matamanio (ya nafsi yake). Hayakuwa haya ila ni Wahyi uliofunuliwa. (53: 3-4) Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) aliwaita wafuasi wa Ali Shia, waliokombolewa na waliookolewa. Hafidh: Kiko wapi kitu kama hicho? Sisi hatujakiona kamwe. Muombezi: Sisi tumekiona na hatufikirii kuwa ni sawa kuficha ukweli. Allah (s.w.t.) Amewalaani wafichaji na hao akawaita ni watu wa motoni. Allah (s.w.t.) Anasema: Hakika wale wanaficha hoja zilizo wazi na uongozi ambao tumeuteremsha baada ya kuzibainisha kwa watu kitabuni, hao anawalaani Allah na wanawalaani wenye kulaani. (2:159) Hakika wale wafichao aliyoyateremsha Allah katika Kitabu wakafadhilisha thamani ndogo, hao hawali matumboni mwao isipokuwa moto, wala Allah hatawasemeza Siku ya Kiyama wala hatawatakasa, na watapata adhabu iliyo kali. Hafidh: Kama tunaijua kweli na tukaificha nakubali kwamba tunastahili laana kama ilivyofunuliwa katika aya hizi tukufu. Muombezi: Natumaini utaziweka akilini Aya hizi mbili ili kwamba usije ukashindwa nguvu na tabia au kutovumilia. Hafidh Abu Nuaim Isfahani ni moja wa watu wenu maarufu sana katika wasimuliaji wa hadith. Ibn Khallikan amemsifu katika kitabu chake Wafayatul Aayan kama Huffadh mkubwa (Mtu wa hikma) na mmoja kati ya wasimuliaji wa hadith aliyeelimika sana. Vile vile anaelezea kwamba jalida kumi za kitabu chake HilyatulAulya ni miongoni mwa vitabu vizuri mno vya kufundishia. Salahud-din Khalil bin Aibak Safdi anaandika katika Wafiy bil-Wafiyat kuhusu yeye: Mfalme wa wasimuliaji wa hadith, Hafidh Abu Nuaim, alikuwa wa mbele sana katika ilmu, uchamungu, na uaminifu. Alikuwa na nafasi ya hali ya juu katika usimuliaji na uelewaji wa hadhith. Kitabu chake kilicho bora sana ni Hiliyatul-Auliya katika jalida kumi, zikiwa na chimbuko kutoka Sahih mbili (Bukhari na Muslim). Muhammad bin Abdullah alKhatab amemsifu katika Rijalil-Mishkatil-Masabin. akisema kwamba ni miongoni mwa wasimuliaji hadith wa mbele ambaye simulizi zake ni za kuaminika kabisa. Kwa ufupi, Mwanachuo na Muhadithina huyu mwenye kuheshimika na fahari ya Maulamaa wenu, anasimulia kutoka kwa Abdullah ibn Abbas kupitia nyororo yake mwenyewe ya wasimuliaji katika Kitabu chake Hilyatul-Auliya kama ifuatavyo: Wakati aya ifuatayo ya Qurani Tukufu ilipoteremshwa:
18
Mikesha ya Peshawar
(Na kwa) wale ambao wanaamini na kufanya mema, hakika hao ndio wabora wa viumbe. Malipo yao kwa Mola wao ni bustani zipitazo mito chini yake, watakaa humo milele. Allah yuko radhi nao na wao wako radhi Naye, na hayo ni kwa yule amchae Mola. (98: 7 8) Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), akizungumza na Ali, alisema: Ewe Ali, wabora wa viumbe (khairil-Bariyya) katika Aya hii tukufu inakuashiria wewe na wafuasi (Shia) wako. Katika siku ya ufufuo, wewe na wafuasi (Shia) wako mtapita daraja ambayo kwamba Allah atakuwa radhi nanyi na ninyi mtakuwa radhi Naye.
Jalalud-Din Suyuti katika Durrul-Mansur anamnukuu Abul-Qasim Ali Bin Hasan (anayejulikana zaidi kama Ibn Asakir Damishqi) ambaye anamnukuu Jabir Bin Abdullah Ansari, mmoja wa masahaba wakubwa wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), akisema kwamba yeye na watu wengine walikuwa wamekaa pamoja na Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) wakati
19
Mikesha ya Peshawar
Ali Bin Abi Talib alipoingia ndani. Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akasema: Naapa kwa Yule ambaye anamiliki uhai wangu kwamba mtu huyu (Ali) na wafuasi wake watapata wokovu katika Siku ya Ufufuo. Wakati huo huo aya hiyo hapo juu ilishushwa. Katika sharhe hiyo hiyo, Ibn Adi anamnukuu Ibn Abbas akisema kwamba wakati aya hiyo hapo juu iliposhuka, Mtume akasema kumuambia Amirul-Muminin, Ali: Wewe na waafuasi wako mtakuja Siku ya Ufufuo katika hali ambayo kwamba wote mtaridhia juu ya Allah, na Allah ataridhika nanyi. Katika Manaqib ya Khawrizmi, ifuatayo ilisimuliwa kutoka kwa Jabir Bin Abdullah Ansari: Nilikuwa kwenye hadhara ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) wakati Ali alipoungana nasi, na wakati ule Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akasema: Huyu ambaye amekujieni ni ndugu yangu. Kisha, akaelekea Kaba, Mtume akachukua mkono wa Ali na akasema: Naapa kwa Yule ambaye anamiliki uhai wangu, huyu Ali na wafuasi wake watakuwa wamepata wokovu katika Siku ya Hukumu. Kisha akasema: Ali ndiye wa mbele zaidi yenu wote katika imani, mwenye kuzingatia mno kuhusu dhamana za Allah, mwadilifu kupita wote katika kuamua mambo ya watu, na mwadilifu kupita wote katika kugawa masurufu miongoni mwa watu, na aliye juu zaidi ya wote kwa cheo mbele ya Allah. Katika wakati huo aya hiyo hapo juu ilishushwa. Katika Sura ya 11 ya Kitabu chake Sawaiq Ibn Hajar anamnukuu Hafidh Jamalud-Din Muhammad Bin Yusuf Zarandi Madani (Mwanachuo mkubwa wa madhehebu yenu) akisema kwamba: Wakati Aya hiyo hapo juu ilipoteremshwa, Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alisema: Ewe Ali, Wewe na Shia wako ndio wabora wa viumbe walioumbwa. Wewe na Mashia wako mtakuja Siku ya Hukumu katika hali ambayo nyote mkiwa mmeridhia kwa Allah, na Allah atakuwa radhi nanyi. Maadui zako watakuwa wamechukizwa mno, na mikono yao itakuwa imefugwa kuzunguuka shingo zao. Kisha Ali akauliza, ni nani maadui zangu. Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akajibu, Yule ambaye ana uadui kwako na ambaye anakutukana. Allama Samhudi, katika Jawahirul-Iqdain, kwa idhini ya Hafidh Jamalud-Din Zarandi Madani na Nurud-Din Ali bin Muhammad bin Ahmad Maliki Makki, ajulikanaye kama Ibn Sabbagh, ambaye anaheshimiwa kama mmoja wa Wanachuo wenu Mashuhuri na mnadharia mkubwa wa mambo ya dini, katika kitabu chake Fusulul-Muhimma anasimulia kutoka kwa Abdullah bin Abbas, kwamba wakati Aya hii iliyo kwenye mjadala ilipoteremshwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alisema kumuambia Ali; Ni wewe na Mashia wako. Wewe na wao mtakuja Siku ya Hukumu mkiwa mmefurahi mno na mmeridhia, ambapo maadui zako watakuja na huzuni kubwa na mikono iliyofungwa. Mir Seyyed Ali Hamadani Shafii, mmoja wa wanachuo wenu mashuhuri katika kitabu chake Mawaddatull-Qurba na mwanachuo anayejulikana vizuri sana kwa upinzani wake juu ya Shia, Ibn Hajar katika kitabu chake Sawaiq-e-Muhriqa, anasimulia kutoka Ummul-Muminina Umm Salma, mke wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), kwamba Mtume
20
Mikesha ya Peshawar
alisema: Ewe Ali, wewe na Mashia wako mtaishi Peponi; wewe na Mashia wako mtaishi katika Pepo. Mwanachuo anayejulikana sana wa Khawarizm, Muwaffaq bin Ahmad, katika kitabu chake Manaqib Sura ya 19, anasimulia kutoka rejea zinazoaminika kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alisema kumuambia Ali: Katika umma wangu wewe ni kama Masihi Isa Mwana wa Mariamu. Taarifa hii inaonyesha kwamba, kama vile wafuasi wa Mtume Isa (A.S.) walivyogawanyika katika makundi: Waumini wa kweli wajulikanao kama Hawariin, Mayahudi, na wapiga chuku (wenye kutia maneno chumvi) ambao wanamshirikisha yeye na Allah; katika njia hiyo hiyo Waislamu watakuja kugawanyika katika makundi matatu. Mojawapo litakuwa Shia, waumini wa kweli. Kundi lingine litakuwa la maadui wa Ali, na kundi la tatu litakuwa la wenye kukuza cheo chake.
21
Mikesha ya Peshawar
wakati wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) Masahaba kadhaa maarufu wenye kutajika walikuwa wakiitwa Mashia. Hafidh Abu Hatim Razi katika kitabu chake Az-Zainat ambacho amekiandika kwa ajili ya kufafanua maana ya maneno fulani na Semi zinazotumika miongoni mwa Wanachuo, anasema kwamba neno la kwanza jipya ambalo lilikuja kukubaliwa na wote katika Uislamu wakati wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) lilikuwa ni Shia. Neno hili lilitumika kwa masahaba maarufu wanne: Abu Dharr Ghifar, Salman Farsi, Mikdadi bin Aswad Kindi, na Ammar Yasir. Hadith nyingi zaidi zilinukuliwa katika kuunga mkono nukta hii hii. Sasa ni juu yenu kufikiria vipi iliwezekana kwamba wakati wa Mtume (s.a.w.w.) Wanne kati ya masahaba wake wakubwa waliitwa Shia. Kama Mtume (s.a.w.w.) alifikiria kuwa neno hilo ni la uzushi (bidaa), kwanini hakuwakataza watu kulitumia? Ukweli ni kwamba watu walisikia kutoka kwa Mtume (s.a.w.w) mwenyewe kwamba wafuasi (Mashia) wa Ali walikuwa ni wakazi wa Peponi. Walikuwa na fahari nalo na kwa uwazi wakajiita wenyewe Mashia.
22
Mikesha ya Peshawar
inashauku juu ya watu watatu, Ali, Ammar, na Salman. Je, vitendo vya Sahaba hawa Mashuhuri wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) sio vya mfano wa kuigwa na Waislamu wengine? Je, sio aibu kwamba kwa maoni yenu Sahaba wamewekewa mpaka kwa wale tu waliocheza mchezo wa Saqifa, au ambao wameukubali mpango wake bila kupinga, ambapo wengine ambao wamepinga hila za Saqifa wanaonekana kama wasiokuwa waaminifu? Na ikiwa ni hivyo, basi hadith uliyoinukuu ingekuwa na maneno haya: Hakika wachache kati ya Sahaba wangu ni kama nyota .
23
Mikesha ya Peshawar
zao. Walihoji ni kwanini Khalifa awanyime haki za Uislamu kinyume na amri zilizowekwa na Mtukufu Mtume (s.a.w.w.).
24
Mikesha ya Peshawar
25
Mikesha ya Peshawar
Hapa kuna baadhi ya beti kutoka kwa washairi wa Kiiran wakiashiria hoja hii, ambapo Ali mwenyewe alilaani imani kama hizi. Mwisho wa beti hizi unaonyesha Ali akisema: Nani anasaidia wakati wa matatizo! Ni mimi ambaye ni Mungu! Ni mimi. Ubeti wa mshairi mwengine unasema: Kulingana na iman ya wale ambao wana akili na wanamtambua Mungu, Mungu ni Ali na Ali ni Mungu. Muombezi: Nashangaa kwanini, bila kufanya uchunguzi, uweze kuwatuhumu Wairani wote kuwa wanamchukulia Ali kama Mungu. Wanachuo wenu wenyewe wamefanya madai ya kishabiki kama haya. Wamesema kwamba Mashia wanamwabudu Ali na kwa ajili hiyo wao ni Makafiri. Kwa hiyo kuwaua wao ni wajib. Matokeo yake Waislamu wa Uzbekistan na Turkistan kwa ukatili mkubwa wakamwaga damu za Waislamu wa Iran. Watu wa kawaida miongoni mwa Masunni mara kwa mara wanapotoshwa na baadhi ya Ulamaa wenu, na watu wenu wanawachukulia Wairani kuwa ni Makafiri. Katika wakati uliopita, watu wenu Wa-Turkomania wameshambulia msafara wa Wairani karibu na Khorasan, wakawanyanganya na kuwaua watu, na kusema kwamba, yeyote atakayeua marafidh saba (yaani Shia) atakuwa na uhakika wa kwenda peponi. Yakupasa uweke akilini kwamba lawama za kuhusika na mauaji haya zinakuwa moja kwa moja juu ya viongozi wenu, ambao huwaambia Masunni wasio na elimu kwamba Mashia wanamuabudu Ali.
Enyi watu! Hakika tumekuumbeni ninyi mume na mke; na tumekufanyeni mataifa na makabila ili kwamba mpate kujuana; hakika aliye mbora sana miongoni mwenu mbele ya Allah ni yule amchae Allah zaidi (49:13).
26
Mikesha ya Peshawar
Vile vile katika Sura hiyo hiyo ndani ya Qurani Anasema:
Kwa hakika Waumini wote ni ndugu, basi patanisheni baina ya ndugu zenu na mcheni Allah ili mrehemiwe. (49:10). Kwa hiyo, watu wote, Waasia, Waafrika, Wazungu, Waamerika weupe, weusi, wekundu au manjano, makabila yote ambayo ni Waislamu ni ndugu, na hakuna hata mmoja anayeweza kudai ubora juu ya mwingine. Kiongozi mkubwa wa Waislamu, Mwisho wa Mitume, alitenda juu ya msingi huu. Alionyesha mapenzi yake makhususi kwa Salman Farsi wa Iran, Suhaib wa Asia ndogo, na Bilal wa Abysinia (Uhabeshi Ethiopia ya sasa). Na kwa upande mwingine alimpuuza Abu Lahab (ambaye jina lake lina maana ya Baba wa Miali ya Moto), ami yake mwenyewe ambaye amelaaniwa katika Sura ya Qurani Tukufu ambayo inasema:
27
Mikesha ya Peshawar
28
Mikesha ya Peshawar
wisha potea toka zamani, na wakapoteza wengi, na wenyewe wakapotea njia iliyosawa. (al-Maidah; 5:77). Allama Majlisi katika Kitabu chake Baharul-Anwar Juz. 3 ambacho ni ensaklopidia (kitabu cha maarifa yote) ya itiqad ya Shia, ameandika hadith nyingi kuwalaumu Ghullat. Imam Jafar Sadiq (a.s.) ananukuliwa akisema, Sisi ni waja wa Allah, ambaye ametuumba na akatufanya sisi kuwa bora kwa viumbe wake wengine. Hakika sisi tutakufa na tutasimama mbele ya Allah kwa ajili ya hesabu. Yule ambaye ni rafiki ya Ghullat ni adui yetu; na yule ambaye ni adui yao huyo ni rafiki yetu. Maghullat ni makafir na Washirikina; laana naiwe juu yao. Kiongozi mkubwa wa dini wa Mashia vilevile amemnukuu Imam huyu huyu akisema: Laana ya Allah iwe juu ya wale ambao wanadai Utukufu na Umungu kwa Ali. Kwa jina la Allah, Ali alikuwa ni mja mtiifu wa Allah. Laana iwe juu ya wale waliotukashifu sisi; baadhi ya watu wanasema mambo kuhusu sisi ambavyo sisi wenyewe hatuyasemi. Tunasema wazi kwamba hatuna uhusiano nao. Sheikh Saduq (Abu Jafar Muhammad bin Ali) Faqih mwenye kuheshimiwa sana (Mwanachuo Shariah) wa Mashia, anamnukuu Zarara bin Ayun, mwandishi wakuaminika wa Kishia, ambaye alikuwa Hafidh na Sahaba wa Imam Muhammad Baqir na Imam Jafar Sadiq, akisema: Nilimueleza Imam Jafar Sadiq kwamba mmoja kati ya watu anayejulikana kwake, huamini katika Tufiidh (uwakilishi wa mamlaka ya Mungu). Imam akasema: Ina maanishwa nini kwa Tufwidh?, Nikajibu. Yule mtu anasema kwamba, Allah alimuumba Muhammad na Ali na kisha akakabidhi Mamlaka yake kwao juu ya mambo ya watu. Hivyo wao ndio waumbaji, watoaji wa chakula, wao wahuishaji na wao ndio wenye kufisha. Mtukufu Imam akasema: Adui huyo wa Allah, anaongopa. Wakati utakaporudi kwake, msomee Aya hii kutoka katika Qurani Tukufu au wamemfanyia Allah washirika ambao wameumba kama alivyoumba Yeye, kwa hiyo alivyoviumba vikawababaisha (akili)? Sema Allah ndiye Muumbaji wa kila kitu na ni mmoja tu, Mwenye Enzi Kuu . (13:16).
29
Mikesha ya Peshawar
Hakika Allah na Malaika wake wanamtakia Rehema Mtume. Enyi ambao mmeamini mtakieni rehema juu yake na Msalimuni kwa (uzuri) wa Salamu. (33:56). Mwendo wako huo unakiuka kiwazi kabisa hukumu ya Qurani. Neno lako hilo ni Uzushi (bidaa). Muombezi: Aya hii haitukatazi kumuombea rehema mtu wengine yoyote. Tunaamrishwa kumuombea Rehema Mtume. Katika Aya nyingine ya Qurani Tukufu, Allah anasema. Amani na iwe juu ya watu wa Ya Sin (Ahl Ya Sin), yenye maana ya kizazi cha Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Ama kwa Mitume wengine wa Allah, kuombea rehema hakukutolewa pamoja na vizazi vyao popote katika Qurani. Kuombea rehema kumetolewa tu kwa Mitume wa Allah.
30
Mikesha ya Peshawar
Sema: kama mnampenda Allah, basi nifuateni mimi, Allah atakupendeni ninyi(3:31) Na kuhusu Ahlul Bait Allah Anasema:
Sema: Sikuombeni malipo yoyote kwa haya bali Mapenzi kwa Ndugu wangu wa karibu (42:23).
31
Mikesha ya Peshawar
SALAWAT JUU YA MUHAMMAD NA AALI - MUHAMMAD NI SUNNA (ILIYOKOKOTEZWA), NA KATIKA SWALA ZA FARADHI NI WAJIBU.
Wengi wa wasimuliaji wa Hadith hususan Bukhari katika Sahih yake Juz. 3, na Muslim katika Sahih yake Juz. 1 Sulayman Balkhi katika Kitabu chake Yanabiul-Mawadda, na hata Ibn Hajar katika Kitabu chake Sawaiqi wanamnukuu Kab bin Ajza akisema: Wakati Aya: Hakika, Allah na Malaika wake wanamtakia rehema (wanamswalia) Mtume (33:56) ilipoteremshwa, tulimuuliza Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), namna gani tutaomba rehema kwa ajili yako, Ewe Mtume wa Allah,? Mtume akajibu, Ombeni juu ya rehema (Swalawat) zenu kwa namna hii. Ee Allah teremsha rehema kwa (Mtume) Muhammad na Aali Muhammad. Imam Fakhrud-Din Razi, katika Juzuu ya 6, ya Kitabu chake Tafsir-e-Kabir pia anasimulia hadithi kama hiyo. Ibn Hajar, akisherhesha juu ya hadith hiyo, anaonyesha kwamba, ni wazi kutoka katika Hadithi hii kwamba kuomba rehema kwa ajili ya Mtume ni sawa sawa na kuomba rehema kwa kizazi chake pia. Vilevile anamnukuu Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akisema: Msiniswalie (Msiniombee) Swalawat kigutu. Alipoulizwa anamaanisha nini kwa Swalawat kigutu; akasema: Msiseme, Allahumma swali Ala Muhammad, (Ewe Allah Mrehemu Muhammad) bali semeni, Allahumma swali Ala Muhammad wa Ala Aali Muhammad. Dailami anaandikwa kwamba, Mtume alisema: Sala zetu hubakia zimezuiliwa mpaka tuombe Swalawat juu ya Mtume na Ahlul (watu) wake Imam Shafii anasema: Enyi Ahlul Bait (watu wa Nyumba ya Mtume) Allah Amefanya mapenzi kwenu kuwa ni wajib (lazima) kwetu sisi katika Qurani Tukufu. Kwa mintarafu ya ubora wenu, Cheo na Sifa zenu, inatosha kujua kwamba kama mtu hakuomba Swalawat (rehema) kwa ajili yenu, Sala yake haikubaliwi. Kama Swalawat kwa ajili ya Mtume na Dhuria (kizazi) wake inaachwa kwa makusudi, basi swala hiyo ya wajib inakataliwa. Na Mtukufu Mtume amesema: Sala ya wajib ni nguzo ya iman; kama Sala ikikubaliwa, matendo mengine yote (ya ibada) yanakubaliwa; kama imekataliwa, matendo yote mengine yanakataliwa. Kuomba Swalawat kwa ajili ya Ahlul-Bait ni Sunna iliyokokotezwa na ni namna ya ibada ambayo ilikuwa ikifanywa na Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) mwenyewe. Tunaona fahari kufanya kile ambacho Qurani Tukufu na Mtume (s.a.w.w.) wametuarimsha sisi kufanya.
32
Mikesha ya Peshawar
ZAIDIYYA
Zaidiyya wanamfuata Zaid bin Ali bin Husein. Wanamchukulia mtoto wa Imam ZainulAbidin, aitwaye Zaid kuwa ndiye Mrithi wake. Kwa wakati huu watu hawa wanapatikana kwa idadi kubwa nchini Yemen na majirani waizungukao. Wanaamini kwamba miongoni mwa Dhuria wa Ali na Fatima, Yeye ndiye Imam ambaye ni mwanachuo, mcha Mungu, na shujaa. Anachomoa upanga na kusimama dhidi ya maadui, Katika wakati wa Khalifa dhalimu wa Kibani Umayya, Hisham ibn Abdul-Malik, Hadhrat Zaid alisimama dhidi ya wale waliokuwa katika mamlaka na akauwawa Shahidi na kwa ajili hiyo akakubaliwa na Zaidiyya kama Imam. Ukweli ni kwamba Zaid alikuwa na cheo cha juu zaidi kuliko hicho ambacho Zaidiyya wanakidai kwa ajili yake. Alikuwa ni Sayyid mashuhuri wa ukoo wa Bani Hashim, na alikuwa akijulikana kwa ucha Mungu wake, hekima, Sala, na ushujaa. Alipitisha mikesha mingi bila usingizi akikesha kusali na alifunga mara kwa mara. Mtume (s.a.w.w.) alitabiri Shahada yake (kifo cha kishahidi), kama ilivyosimuliwa na Imam Husein: Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akaweka mkono wake Mtakatifu kwenye mgongo wangu na akasema: Ewe Husein haitachukuwa muda mrefu atazaliwa mtu miongoni mwa Dhuria wako. Atakuwa anaitwa Zaid; atauwawa kama Shahid. Katika siku ya ufufuo, yeye na Masahaba
33
Mikesha ya Peshawar
zake wataingia Peponi, wakiweka miguu yao juu ya shingo za watu. Lakini Zaid mwenyewe hakudai kamwe kuwa yeye ni Imam. Ni masingizio yasiyo na msingi kwa watu kusema kwamba alidai. Kusema kweli, yeye alitambua Imam Muhammad Baqir kama Imam na alitoa utii wake kiukamilifu kwake. Ilikuwa ni baada tu ya kufariki kwa Imam Muhammad Baqir ndipo watu wajinga wakatwaa itiqad ya kwamba: Siye Imam yule akaaye nyumbani na kujificha machoni mwa watu; Imam ni yule ambaye ni Dhuria wa Hadharat Fatima, ambaye ni mwenye elimu, na ambaye anachomoa upanga na kusimama dhidi ya adui, na kulingania (kuwaita) watu upande wake. Zaidiyya wamegawanyika katika faraka Tano: Mughairiyya; Jarudiyya; Zakariyya; Khashbiyya; na Khaliqiyya.
34
Mikesha ya Peshawar
35
Mikesha ya Peshawar
36
Mikesha ya Peshawar
37
Mikesha ya Peshawar
38
Mikesha ya Peshawar
Pengine bila shaka umeona maelezo ya Ibn Hajar Makki mwanzoni mwa kitabu chake Sawaiq al-Muhriqa, sura ya Matukio (Matukio ya ukhalifa wa Abu Bakar) kama ilivyoandikwa na Bukhar na Muslim katika Sahih zao mbili, ambavyo ndio vitabu sahihi zaidi na vya kutegemewa baada ya Qurani Tukufu kwa mujibu wa makubaliano ya pamoja ya wafuasi (yaani, Ummah). Anasema kwamba maadam ummah wote uko pamoja katika kuzikubali hadith za vitabu hivyo, chochote ummah wanachokubaliana kwa shauri moja hakiwezi kutiliwa mashaka. Juu ya msingi wa makubaliano haya, hadith zote zilizomo katika vitabu hivi zinakubalika bila kutiliwa mashaka. Kwa hiyo, hakuna mtu anayeweza kujasiri kudai kwamba vitabu hivi vina mambo ya ajabu na ya kuchekesha.
39
Mikesha ya Peshawar
40
Mikesha ya Peshawar
Sasa ni juu yenu ninyi kuamua iwapo maelezo namna hii ni sawa na ukafiri au hapana, kwamba Allah atajitokeza kiumbo mbele za watu na atafunua mguu Wake! Na nukta kubwa sana yenye kuunga mkono hoja yangu ni kwamba Muslim bin Hajjaj anaanza kuandika sura katika Sahih yake kuhusu uhakika wa kuonekana Allah (s.w.t.), na amenukuu simulizi za kubuni kutoka kwa Abu Huraira, Zaid bin Aslam; Suwaid bin Said, na wengine. Na baadhi ya maulamaa wakubwa wa madhehebu yenu wenyewe kama Dhahabi katika Mizanul-Itidal na Suyuti katika kitabu chake Kitabul-Lu-ualialMasnua fi hadithal-Muzua, na Sibt ibn Jauzi katika Al-Muzua; wamethibitisha juu ya hoja za Msingi kwamba simulizi (Hadith) hizi ni za kubuni.
Macho hayamfikii, bali yeye anayafikia macho (6:103) Tena, wakati Nabii Musa alipolazimishwa na wana Israel kwenda sehemu yake ya Sala na amuombe Allah Ajidhihirishe kwake, Qurani Tukufu inaandika tukio hili kama ifuatavyo:
(Musa) akasema: Mola wangu nionyehse (nafsi Yako) ili nikuone, Akasema: Huwezi (Ukathubutu) kuniona (7:143). Seyyid Abdul-Hayy (Imam wa wa jamaat ya Ahli Sunna): Je! Hii sio kweli kwamba Ali Alisema: Siwezi kumuabudu Mungu ambaye simuoni? Wakati Ali anasema kitu cha namna hiyo, ina maana kwamba Allah anaweza kuonekana.
41
Mikesha ya Peshawar
Sheik Saduq katika kitabu chake juu ya Tawhid, Sura ya Ibtal Aqida Ruyatullah. Imam Jafar as-Sadiq ananukuliwa akisema, mwanachuo mmoja wa Kiyahudi alimuuliza AmirlMuminin, Ali (A.S.) iwapo amemuona Allah katika wakati wa Sala. Imam akajibu: Hawezi kuonekana kwa macho haya ya kiumbo. Ni moyo ndio unaomuona Yeye, kwa mwanga wa uhalisi wa kuamini na kusadiki. Kutokana na majibu ya Ali ni kwamba yeye anachomaanisha kwa kumuona Allah, sio kumuona kwa macho, bali kwa mwanga wa imani ya kweli. Kuna ushahidi mwingine mwingi uliotegemezwa juu ya hoja na mambo yaliyoandikwa ya kuthibitisha maoni yetu juu ya nukta hii. Zaidi ya hayo, mbali na wanachuo wa Kishia, maulana wenu wenyewe, kama Qadhi Baidhawi na Jarullah Zamakhshari, wamethibitisha katika Sharhe zao kwamba haiwezekani kwa Allah kuonekana. Yeyote ambaye anaamini juu ya kuonekana kwa Allah, katika ulimwengu huu au ulimwengu ujao, anaamini kwamba ni kiumbe mwenye mwili. Kuamini hivyo ni ukafiri.
REJEA ZAIDI YA HADITH ZA AJABU AJABU KATIKA VITABU VIWILI VYA HADITH
Mnafikiria vitabu vyenu sita vya Hadith, khususan vile vya Bukhari na Muslim, kama vitabu vya Ufunuo. Natamani kwamba mngeviangalia kwa busara na msivuke mipaka katika kuvisifu kwenu. Bukhari, katika Sura ya Kitab-e-Ghusl, na Muslim katika Sehemu ya 2 ya Sahih yake (Sura ya fadhil za Mtume Musa), na Imam Ahmad bin Hanbal katika Musnad yake, Sehemu ya 2 uk. 315, na maulamaa wenu wengine wamemnukuu Abu Huraira akisema: Miongoni mwa wana wa Israel ilikuwa ni desturi yao kuoga pamoja bila nguo, hivyo kwamba kila mmoja aliangalia utupu wa mwenziwe. Hawakufikiria kama kuna kizuizi katika hilo. Mtume Musa ndiye aliyekuwa akiingia kwenye maji peke yake, hivyo kwamba hakuna aliyeweza kuona sehemu zake za siri. Wana wa Israeli walizoea kusema kwamba Mtume Musa alikuwa na hitilafu katika sehemu zake za siri, hivyo alijiepusha kuoga nao. Siku moja Mtume Musa alikwenda mtoni kuoga. Alivua nguo zake, akaziweka juu ya jiwe na akaingia mtoni. Lile jiwe likakimbia na nguo zake. Musa akalikimbiza lile jiwe akiwa uchi, akipiga makelele: Nguo zangu! Ewe jiwe nguo zangu. Wana wa Israel wakamuona Musa akiwa uchi na wakasema: Kwa jina la Allah Musa hana hitilafu katika tupu zake. Kisha lile jiwe likasimama, na Musa akarudishiwa nguo zake. Kisha Musa akalipiga lile jiwe kwa nguvu sana kiasi kwamba lile jiwe likalia kwa sauti kubwa mara sita au mara saba kwa maumivu. Kweli mnaamini kitu kama hicho kinawezekana kwa Nabii Musa (A.S.), au kwamba jiwe, kitu kisicho na uhai, lingeweza kuchukua nguo zake? Kwa hakika itakuwa haiwezekani kwa Mtume kukimbia uchi mbele za watu.
42
Mikesha ya Peshawar
Nitasimulia Hadith nyingine iliyoandikwa katika Sahih ambayo ni ya kichekesho zaidi. Bukhari anamnukuu Abu Huraira katika Sahih yake (Juz. 1, uk. 158 na Juz. 2, uk. 153), na tena katika Sura ya Kifo cha Mtume Musa, na Muslim vilevile anamnukuu huyo huyo (Abu Huraira) katika Sahih yake Juz. 2, uk. 309 katika Sura ya Fadhila za Musa akisema: Malaika wa Mauti alikuja kwa Mtume Musa na akamtaka akubali mwito wa Mola wake. Aliposikia hivi, Musa alimchapa kofi kali la uso kiasi kwamba jicho lake moja lilingoka. Hivyo alirudi kwa Allah na akalalamika kwamba amemtuma kwa mtu ambaye hataki kufa, na ambaye amemngoa jicho lake moja. Allah akaponya jicho lake na akamuamuru arudi tena kwa Musa na amuambie kwamba, kama anataka maisha marefu, yapasa aweke mkono wake juu ya mgongo wa fahali wa ngombe. Ataishi miaka mingi kama idadi ya nywele zitakazofunikwa na mkono wake. Imam Ahmad bin Hanbal katika Musnad yake, Juz. 2 uk. 315, na Muhammad bin Jarir Tabari, katika kitabu chake chaTarikh, Juz. 1, chini ya kichwa cha habari, Kifo cha Mtume Musa, ametoa maelezo haya haya kutoka kwa Abu Hurira pamoja na nyongeza kwamba kufikia wakati wa Musa, Malaika wa mauti alikuwa akitoa roho (za watu) katika mwili kiwaziwazi. Lakini baada ya Musa kumchapa kofi la uso, alikuja bila kuonekana. Sasa ni juu yenu kuamua ni kichekesho gani hiki ambacho kimewekwa katika vitabu hivi viwili vya hadith, ambavyo mnaviita kuwa ni vya usahihi zaidi kuliko vitabu vyote baada ya Qurani Tukufu. Riwaya nilizoelezea hakika zinadhalilisha heshima za Mitume wa Allah. Ama kwa Abu Huraira, sizishangai simulizi zake. Maulamaa wenu wenyewe wanakiri kwamba, ili apate kujaza tumbo lake kwa vyakula vyenye ladha vilivyotolewa na Muawiya, alibuni hadithi za uongo. Kwa sababu ya uzushi wake, Khalifa Umar alimpiga viboko. Ni jambo la kushangaza kwamba watu wenye akili wanaamini ngano kama hizi za kuchekesha. Sasa ngoja turudi kwenye majadiliano yetu kuhusu hadith uliyonukuu. Ni dhahiri, mtu mkweli akiona hadith pekee (iliyosimuliwa na mtu mmoja) atailinganisha na hadith nyingine sahihi. Imma ataisahihisha au ataikataa moja kwa moja kuliko kuitumia kama msingi wa kuwashambulia ndugu zake wa madhehebu nyingine na kuwaita makafir. Kwa vile kitabu Tafsiri-e-Safi hatunacho hapa, hatuwezi kusema chochote kuhusu usahihi wa hadith hii. Hata kama ni kweli, yatupasa kutegemea juu ya kanuni kwamba, kama tunajua athari, tunaweza kujua sababu. Yaani, kama tunamjua Imam kama Imam, kwa hakika tunajua utambulisho wa Allah, katika njia ileile, ambayo kama mtu anamjua Waziri Mkuu, anamjua Mfalme. Ni kwa kuhusu kanuni hii kwamba Sura ya Tawhid na Aya nyingine za Qurani Tukufu zilishuka. Zaidi ya hayo, kuna Hadith nyingi kuhusu upweke wa Allah zilizosimuliwa na Imam Husain mwenyewe na Maimamu wengine. Kumjua Imam wetu ni namna kubwa ya Ibada ya Allah. Maana hiyo hiyo imetolewa katika Ziarat-e-Jamia, ambayo imefika kwetu kutoka kwa Mtukufu Imam. Tunaweza kuitafsiri pia kwa njia nyingine, kama wanachuo
43
Mikesha ya Peshawar
walivyofanya katika mambo kama haya. Mtekelezaji yoyote wa kitendo anaweza kueleweka kwa asili ya kitendo chake. Kwa vile Mtume na kizazi chake walifikia daraja ya juu kabisa katika uwezo wa kibinadamu, hakuna wengine wenye fadhila au ubora kama wao. Kwa kuwa hawa ndio njia dhahiri zaidi ya kumjua Allah, yeyote awajuaye hawa, anamjua Allah. Kama walivyosema wenyewe: Ni kwa kupitia kwetu sisi, kwamba Allah anaweza kutumikiwa. Tunaamini kwamba Ahlul Bait wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) wametufundisha elimu kuhusu Allah na njia zinazostahili za kumuabudu Yeye. Wale ambao hawakuwafuata wamepotea njia.
44
Mikesha ya Peshawar
Kwa hakika wamekufuru wale waliosema: Hakika Allah ni Mmoja katika watatu; hali hakuna mungu ila Allah Mmoja. (al-Maida; 5: 73). Kushirikisha vitu na sifa za Uungu, maana yake ni kuamini kwamba sifa Zake, kama elimu Yake au nguvu ziko tofauti na, au ni nyongeza katika Nafsi Yake Kamilifu. Ashariyya wa Abul-Hasani Ali bin Ismail Ashari Basari, wanaelezewa na Maulamaa wenu wakubwa, kama Ali bin Ahmad katika kitabu chake Al-Kashf na Minhajul-Adilla fi Aqaidil-Mila, Uk. 57 kuwa wanaamini kwamba Sifa za Allah ni nyongeza katika Nafsi Yake kamilifu, na kwamba ni za milele. Hivyo yeyote mwenye kuamini kwa njia yeyote ile kwamba tabia au sifa yeyote ya Allah ni nyongeza katika Nafsi yake kamilifu, huyo ni mshirikina. Kila sifa Yake ni yenye asili kwake. Ushirikina katika matendo ya mtu, ina maana kumshirikisha mtu mwingine katika Dhati Yake Yenye kujitosheleza Daima dumu. Mayahudi wanaamini kwamba Allah aliumba viumbe na kisha akajiweka mbali na viumbe Wake. Katika kuwalaumu watu hawa, aya ifuatayuo iliteremshwa:
Na Mayahudi wanasema: Mkono wa Allah umefungwa! Mikono yao itafungwa (kwa pingu) na watalaaniwa kwa yale wanayoyasema. Bali, mikono yake yote iwazi; Hutoa apendavyo (5:64). Ghullat wanaunda kundi lingine la washirikina. Pia wao wanaitwa Mufawwiza. Wanaamini kwamba, Allah ameweka au kuaminisha Mamlaka ya mambo yote kwa Maimam watukufu. Kwa mujibu wao, Maimam ni waumbaji na pia hutupatia sisi riziki. Kwa uwazi, wale wanaomuona mtu kuwa mshirika katika Mamlaka ya Uungu ni mshirikina.
Anayetarajia kukutana na Mola Wake, naafanye vitendo vizuri, na asimshirikishe yeyote katika ibada ya Mola wake. (18:110).
45
Mikesha ya Peshawar
Aya hii inaonyesha kwamba sharti la msingi wa imani ni kwamba mtu lazima afanye lolote lile ambalo ni zuri na asije kumshirikisha yeyote pamoja na Allah katika kutoa utii na ibada Kwake. Kwa maneno mengine, yule ambaye anasali au kutekeleza Hija, au kufanya kitendo chochote kizuri kwa ajili tu ya kujionyesha kwa watu uzuri wake, ni mshirikina. Amewashirikisha wengine pamoja na Allah katika jambo la kutekeleza vitendo vyake. Kuonyesha kujikinai kwa matendo mazuri ni ushirikina mdogo, ambao hutangua vitendo vyetu vizuri. Imepata kuelezwa kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alisema: Jiepusheni na ushirikina mdogo. Watu wakamuuliza, Ewe, Mtume wa Allah, ni nini ushirikina mdogo? Akajibu: Al-riya was-sama (yaani, kuonyesha watu au kuwafanya wasikie juu ya ibada yako kwa Allah). Vile vile Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alisema: Kitu kibaya mno ninachokuhofieni kwenu ni ushirikina uliofichika; hivyo kuweni na hadhi ya juu yake kwa kuwa miongoni mwa wafuasi wangu ushirikina ni wa siri mno kuliko kutambaa kwa mdudu chungu juu ya jiwe gumu katika usiku wa giza. Tena alisema: Mtu ambaye anatekeleza ibada ya Sala kwa njia ya majivuno, ni mshirikina. Mtu ambaye anafunga au kutoa sadaka au kutekeleza Hija au kumuachia mtumwa huru ili kuonyesha kwa watu uadilifu wake au kujipatia jina zuri, ni mshirikina. Na kwa vile mistari hii ya mwisho inaelekeza kwenye mambo ya roho, umechanganywa katika ushirikina uliojificha. Hafidh: Tunaona katika maelezo yako mwenyewe kwamba kama mtu atafanya maombi kwa kiumbe yeyote aliyeumbwa ni mshirikina. Hivyo Mashia nao ni washirikina, kwa vile wanafanya maombi kwa Maimamu watukufu na watoto wao.
46
Mikesha ya Peshawar
nia ya moyo lazima iwe kwa ajili ya Allah. Sharti la Pili hukamilisha sharti la kwanza; mtu ambaye anafanya Nadhiri lazima aseme kwa maneno kwamba, ni kwa ajili ya Allah. Kwa mfano, kama anaahidi kufunga au kuacha kunywa (ulevi), lazima aweke nia kwa kutumia maelezo ya maneno ambayo yana neno lillah (kwa ajili ya Allah) bila ya hivyo nadhiri itakuwa batili.
Sema: Mtiini Allah na mtiini Mtume, na kama mkigueka basi juu yake kinabakia kile alichobebeshwa juu yake na juu yenu hubakia kile mlichobebeshwa juu yenu (24:54). Ni wajibu wa watu kusikiliza kile anachokisema Mtume wa Allah na kukitekeleza. Walakini, kama mtu hajali kufuata mafundisho ya Kimungu na hayatekelezi, haiwezi kudhuru imani au kanuni ambazo ndani yake imani imesimamishwa.
47
Mikesha ya Peshawar
48
Mikesha ya Peshawar
Kwa msingi wa maelezo ya ushirikina ya hapo juu, ni upi katika mifano iliyoelezwa hapo ambao unafikiri unatumika kwa Mashia? Ni kwa namna gani kutokana na mtazamo wa Sala, imani au hadithi za Shia ambayo umeiona, inayoweza kuwafanya washambuliwe kwa ushirikina? Hafidh: Nakiri kwamba yote uliyosema ni sawasawa, lakini kama utachukua taabu ya kufikiri kidogo, utakubali kwamba kutegemea juu ya Maimam ni ushirikina. Kwa kuwa haitupasi kutafuta njia yoyote ya kibinadamu kumfikia Allah, yatupasa kumwomba Allah moja kwa moja kwa ajili ya kutaka msaada.
49
Mikesha ya Peshawar
(Nafsi) Yake, hakika yeye ni mshirikina. Utakuwa umewasikia Mashia wakiwa katika shida wakilia, Ya Ali, nisaidie! Ya Husain, nisaidie! Lakini ukweli ni kwamba, kwa kuwa ulimwengu ni nyumba ya visababisho vya pili, tunawafikiria wao kama njia ya kutolewa katika shida. Tunaomba msaada wa Allah kupitia kwao. Hafidh: Badala ya kumuomba Allah moja kwa moja, kwa nini muombe visababisho? Muombezi: Matarajio yetu ya kudumu kuhusu haja zetu, dhiki, na hofu yamewekwa juu ya Allah, Mkamilifu. Lakini Qurani Tukufu inasema yatupasa kumfikia Allah, kupitia baadhi ya njia (visababisho) za kupelekea.
Enyi ambao mmeamini! Mcheni Allah na tafuteni njia ya kumfikia Yeye (5:35).
50
Mikesha ya Peshawar
ardhini hutafuta njia ya kumfika Yeye. Miongoni mwa viumbe Wake sisi ni njia (Wasilat) ya kumfikia Yeye.
51
Mikesha ya Peshawar
imuliwa kiujumla na maulamaa wakubwa wa madhehebu yenu, pamoja na Muslim bin Hajjaj na waandishi wengine wa vitabu sita vya hadith, ambao wameziandika katika vitabu vyao kwa ukamilifu sana, na hawategemei ukusanyaji wa Bukhari tu peke yake. Kama unakubali uadilifu wa Maulamaa wako wote mwenyewe, ambao wote walitambuliwa na Masunni waliopita, yapasa ukubali hadithi hii kwamba ni ya kweli, ambayo kwa sababu fulani haikuandikwa na Bukhari. Hafidh: Hakuna sababu ya kuunga mkono kutokuiandika hadith hii. Bukhari alikuwa makini sana katika suala la kusimulia hadithi. Alikuwa ni mwanachuo mwangalifu sana, na kama aliona hadith, kwa mtazamo wa maudhui au chanzo chake, kuwa yenye madhara au kutokubalika na akili za kawaida, yeye hiyo hakuiandika. Muombezi: Kama mithali inavyosema: Kupenda sana kitu humfanya mtu kuwa kipofu na kiziwi. Waheshimiwa Masuni wamekosea hapa, una shauku kubwa katika upendo wako kwa Imam Bukhari. Unasema alikuwa mchunguzi sana wa mambo, na kwamba simulizi zilizomo katika Sahih yake ni za kuaminika na kustahiki sifa ya Wahayi (Ufunuo). Lakini ukweli ni kinyume chake. Nyororo ya riwaya zilizotajwa na Bukhari zina watu ambao mara kwa mara wameshutumiwa kama waongo. Hafidh: Madai yako sio ya kweli. Unashusha elimu na uwezo wa Bukhar, ambavyo ni tusi kwa madhehebu yote ya Sunni. Muombezi: Kama uchunguzi ulioko juu ya msingi wa elimu ni matusi, basi wengi wa Maulamaa wenu maarufu ni watu ambao wamekebehi ile nafasi ya juu ya elimu na maarifa. Ningependa kukushauri uvichunguze mwenyewe vitabu vilivyoandikwa na waandishi wakubwa na maulamaa wa madhehebu yenu ambao wameandika Sherhe juu ya Sahih Bukhari, k.m. Al-Lualil- Masnua fi hadithl-Mazua ya Suyuti, Mizanul-ibtidal na Talkhisul-Mustadraka ya Dhahabi; Tandhkiratul-Mazua ya Ibn Jauzi, Tarikh Baghdad kilichokusanywa na Abu Bakar Ahmad bin Ali Khatib Baghadad, na vitabu vingine vya Ilm Rijal (vinavyoitwa, makala juu ya sifa za wasimuliaji) vilivyoandikwa na maulamaa wenu wengi wakubwa. Kama utasoma vitabu hivi, hutathubutu kusema kwamba nimemkebehi Imam Bukhari.
52
Mikesha ya Peshawar
53
Mikesha ya Peshawar
54
Mikesha ya Peshawar
Samani na Ibn Maghazili Shafii katika Manaqib; Muhammad bin Yusufu Ganji Shafii katika Kifayatul-Talib, Sura ya 1, katika maelezo ya usahihi wa Khutuba ya Ghadir Khum na vilevile katika Sura 62, uk. 130; Muhammad bin Saad Khatib katika Tabaqat, Juz. 4, uk. 8; Fakhrud-Din Razi katika Tafsir Kabir Juz. 3, chini ya Aya Itisma (3:103), uk. 18; Ibn Kathir Damishqi katika Tasfir Juz. 4 chini ya aya ya Mawadda (42:23), uk. 113, Ibn Hajar Makki katika Sawaiq-e-Muhriqah uk. 75, 87, 90, 99 na 136 pamoja na tofauti ya maneno. Kuna wanachuo wengine kadhaa wa madhehebu yenu ambao majina yao siwezi kuyataja katika mkutano huu kutokana na uhaba wa muda. Wengi wa wanachuo wenu wameisimulia hadith hii muhimu kutoka kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) kwa wingi sana na kwa mfuatano usiokatika wa usimuliaji kutoka kwa mmoja hadi mwingine kiasi kwamba imepata hadhi ya hadith inayosimuliwa mara kwa mara. Kwa mujibu wa hadith hii, Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alisema yafuatayo: Ninaacha kati yenu vitu viwili vizito; Kitabu cha Mwenyezi Mungu na Ahlul-Bait wangu. Kama mtaambatana na viwili hivi, kamwe, kamwe hamtapotea. Viwili hivi havitatengana mpaka vije vinifikie kwenye Haudhi ya Kauthar. Kwa msingi wa hadith hii Sahihi, tunaona kwamba yatupasa kutafuta mshikamano kwenye Qurani Tukufu na Ahlul-Bait wa Muhammad (s.a.w.w.). Sheikh: Hadith hii ya Mtume imesimuiliwa na Salih bin Musa bin Abdullah bin Ishaq, kupitia nyororo yake ya wasimuliaji waaminifu, akisema kwamba Abu Huraira ameisimulia katika njia hii: Ninakuachieni vitu viwili vizito: Kitabu cha Allah (Qurani Tukufu) na Sunna zangu (Mwenendo). Muombezi: Unanukuu tena hadith kutoka kwa mkorofi yule yule ambaye amepuuzwa na wakosoaji wa Shia (Kama Dhahabi, Yahaya, Imam Nisai, Bukhari na Ibn Adi, n.k.). Je, hutosheki na rejea za kuaminika ambazo nimezifanya kutoka Maulamaa wenu wenyewe wakubwa kuhusu hadith hii? Unanukuu maneno yasiyokubalika ya Hadith japokuwa Mashia na Masunni wote kwa pamoja wamekubali kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) ametumia maneno, Kitabu cha Allah na kizazi changu, na sio Sunna zangu. Kusema kweli Kitabu (Qurani) na Sunna (mwenendo) vyote vinahitaji tafsir. Kwa hiyo Sunna haiwezi kuelezea Qurani Tukufu. Hivyo kizazi cha Mtume ambao ndio sawa na Qurani Tukufu ndio Wafasir halisi wa Qurani Tukufu na Sunna za Mtume (s.a.w.w.) vilevile.
HADITH YA SAFINA.
Sababu nyingine inayotufanya tutafute kushikamana na kizazi cha Mtume ni hadith sahih, Hadith ya Safina, ambayo imesimuliwa na Maulamaa wenu wote wakubwa, takriban bila kuacha hata mmoja, na mlolongo usiovunjika.
55
Mikesha ya Peshawar
Zaidi ya Wanachuo wenu mia moja wenyewe wameisimulia hadith hii: Muslim bin Hajjaj katika Sahih yake, Imam Ahmad bin Hanbal katika Musnad, Hafidh Abu Nuaim katika Hilyatul-Auliya. Ibn Abdil-Birr katika Istiab. Abu Bakar Khatib Baghdadi katika Tarikh Baghdad; Mohammed bin Talha, Shafii katika Matalibus-Suul; Ibn Athir katika Nihaya Sibti Ibn Jauzi katika Tadhkira; Ibn Sabbagh Makki katika FusululMuhimma; Allama Nurud-Din Samhudi katika Tarikhul-Madina Sayyid Mumin Shablanji katika Nurul-Absar; Imam Fakhnid-Din Razi katika Tafsir MafatihulGhaib, Jalalud-Din Sayuti katika Durrul-Manthur; Imam Thalabi katika Tafsir Kasful-Bayan, Tabrani katika Ausat; Hakim katika Mustadrak Juz. 3, uk, 151; Sulayman Balkhi Hanafi katika Yanabiul-Mawadda, Sura ya 4, Mir Seyyid Ali Hamadani katika Mawaddatul-Kurba Mawadda ya 2; Ibn Hajar Makki katika Sawaiqul-Muhrikah chini ya Aya 8; Tabari katika Tafsir yake, na vilevile katika Tarikh yake; Muhammad bin Yusufu Ganji Shafii katika Kifayatul-Talib. Sura ya 100, uk. 233. Maulamaa wengine wengi wa madhehebu yenu wamesimulia kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alisema: Mfano wa Ahlul-Bait wangu ni ule wa Safina ya Nuh. Ambaye ataipanda ataokolewa; ambaye anaipa mgongo atazama na kuangamia. Imam Muhammad bin Idris Shafii amerejea kwenye Hadith hii Sahih katika beti zake za mashairi ambazo Allama Fazil Ajib ameziandika katika Dhakhiratul-Maal. Imam Shafii, ambaye anatambuliwa kama mmoja wa wanachuo maarufu wa madhehebu ya Suni, anakiri kwamba, kushikamana kwetu na familia iliyotoharishwa ya Mtume ni njia ya wokovu wetu kwa sababu, kati ya Madhehebu sabini za Uislam, ile madhehebu ambayo inafuata kizazi cha Mtume ndiyo peke yake itakayopata wokovu.
56
Mikesha ya Peshawar
kwamba angesali kwa ajili ya mvua siku ifuatayo kupitia njia ya kumfikia Allah. Asubuhui yake alikwenda kwa Abbas, ami yake Mtume na akasema: Toka nje ili tuweze kumuomba Allah kupitia kwako kwa ajili ya mvua. Abbas alimuomba Umar akae kidogo ili kwamba hio njia ya kufikia kwa Allah ipatikane. Basi, Bani Hashim (Ahlul-Bait) walijulishwa. Kisha Abbas akatoka nje pamoja na Ali, Imam Hassan na Imam Husein. Bani Hashim wengine walikuwa nyuma yao. Abbas akamwambia Umar kwamba mtu yoyote mwingine asiongezwe kwenye kundi lao. Kisha walikwenda sehemu ya kuombea ambapo Abbas alinyanyua mikono yake kwa ajili ya maombi na akasema: Ya Allah! Wewe ndio umetuumba sisi, na unajua kuhusu vitendo vyetu. Ya Allah! Kama ulivyokuwa Mwema kwetu mwanzoni, hivyo kuwa Mwema kwetu mwishoni. Jabir anasema kwamba dua yao ilikuwa bado haijakwisha wakati mawingu yalipojitokeza na ikaanza kunyesha. Kabla hawajafika nyumbani kwao, walikwishalowa. Bukhari pia anasimulia kwamba, siku moja wakati wa ukame Umar bin Khatib alimuomba Allah kupitia kwa Abbas bin Abdul-Muttalib na akasema: Tunatuma maombi sisi wenyewe kupitia kwa ami yake Mtume wetu; hivyo, Mwenyezi Mungu tunyeshee mvua. Kisha ilianza kunyesha. Ibn Abil-Hadid Mutazili katika Sherhe Nahjul-Balaghah (Chapa ya Misri), uk. 256, anaandika kwamba Khalifa Umar alikwenda pamoja na Abbas, ami yake Mtume, kumuomba Allah kwa ajili ya mvua. Katika maombi yake kwa ajili ya mvua, Khalifa Umar alisema: Ya Allah! Tunaleta maombi wenyewe kupitia kwa ami yake Mtume Wako, na kwa jadi yake na kwa watu wao maarufu waliobakia. Hivyo linda cheo cha Mtume wako kupitia kwa Ami yake. Tulikuwa tumeongozwa Kwako kupitia kwa Mtume, ili kwamba tutafute msaada wao na kufanya toba. Kama kuwatafuta kizazi cha Mtume na kuwaendea kwa ajili ya haja zetu katika njia ya Allah ni ushirikina, basi Khalifa Umar alikuwa mshirikina wa kwanza. Kizazi cha Muhammad (s.a.w.w.), kutoka wakati wa Mtume mpaka leo hii, wamekuwa ndio njia ya kupitia (Wasilat) katika dua na maombi yetu kwa Allah. Tunawachukulia tu kama watu wacha-Mungu sana na walio karibu mno na Allah. Kwa hiyo tunawaona wao ni njia ya kutufikisha kwa Allah. Na uthibitisho mzuri wa hili ni vitabu vyetu vya Dua zilizoelezwa na Maimam wetu Maasum. Tunakubali maelekezo ya Maimam wetu. Hapa ninavyo vitabu viwili: Zadul-Maad cha Allama Majlisi na Hidayatuz-Zairin cha Sheikh Abbas Qummi, ambavyo ninavitoa kwako ili uvichunguze. (Wote wawili Hafidh na Sheikh walichunguza vitabu vile). Waliisoma Dua ya Tawassul, na waliona kwamba Ahlul-Bait wa Mtume walikuwa ni sehemu ya dua. Kila mahali walikuwa wametajwa kama njia ya kufikia kwa Allah. Katika muda ule Mulla Abdul-Hayy alisoma Dua yote ya Tawassul, iliyoelezwa na Maimam watoharifu na kunukuliwa na Muhammad bin Babawayh Qummi.
57
Mikesha ya Peshawar
DUA YA TAWASSUL.
Haya ni maombi kwa Allah. Kama Ali ambavyo ametajwa hapa, na Maimam wote wametajwa kwa hali hiyo hiyo. Athari ya Ahlul-Bait wa Mtume inatafutwa kutufikisha kwa Allah. Wanatajwa namna hii: Ewe Bwana wetu na kiongozi wetu! Tunatafuta msaada wako wa kutufikisha kwa Allah. Ewe unayeheshimika zaidi mbele ya Allah: Tuombee sisi Kwake. Ahli Bait wote wa Mtume wametajwa katika hali hiyo hiyo.
58
Mikesha ya Peshawar
Hafidh: Hutendi haki. Unachochea chuki bure. Toa mfano mmoja tu wa mwanachuo wa Kishia aliyeuwawa kwa hukumu ya maulamaa wetu! Nani katika Mualamaa wetu aliyetoa maneno ya laana juu ya Shia? Muombezi: Kama ingekuwa nielezee kirefu matendo ya Maulamaa wenu au ya watu wenu wa kawaida, mkutano mmoja usingekuwa mrefu wa kutosha. Nitarejea tu kwenye mifano michache yenye kuhusiana na matendo yao ili ujue kwamba mimi sichochei chuki, bali naonyesha ukweli. Kama utavichunguza vitabu vya Maulamaa wenu mashabiki, utaona sehemu ambazo wamelaani Mashia. Kwa mfano, angalia vitabu vya Tafsiri vya Imam Fakhrud-Din Razi. Wakati anapopata wasaa tu, kwa mfano kuhusiana na Aya za Wilayat, huandika kwa kurudia rudia: Laana iwe juu ya Marafidhi, laana iwe juu ya Marafidhi, lakini maulamaa wetu hata mara moja hawajaandika mambo kama hayo juu ya ndugu zetu Masunni. Mfano wa vitendo vya kikatili vya maulamaa wenu kuhusu maulamaa wa Kishia ni zile hukumu ya Makadhi wakubwa wawili wa Syria (Burhanud-Din Maliki na Ibad bin Jamaat Shafii) dhidi ya mmoja wa Mwanasheria (Faqih) mkubwa, Abu Abdullah Muhammad bin Jamalud-bin Makki Amili. Mwanachuo yule mkubwa alikuwa akijulikana katika wakati wake kwa ucha Mungu wake na elimu ya Sheria. Mfano wa uwanachuo wake ni kitabu chake, Luma, ambacho alikiandika kwa muda wa siku saba bila kuwa na kitabu chochote mkononi mwake juu ya Sheria (Fiqih) isipokuwa Mukhtasar Nafi. Zaidi ya hayo, wanachuo wa madhehebu haya manne (Hanafi, Maliki, Shafii na Hanbal) walikuwa miongoni mwa wanafunzi wake. Kwa sababu ya maonevu ya Massuni, mara kwa mara alifanya Taqiyya (kujigeuza na kuficha mwelekeo wakati wa hatari), na hakutangaza Ushia wake waziwazi. Kadhi Mkuu wa Syria, Ibad bin Jamaat, ambaye ameweka uhusuda dhidi yake, alimzungumza vibaya kwa mtawala wa Syria (Baidmar) na akamshutumu kuwa yeye ni Rafidhi na Shia. Mwanachuo huyu maarufu akatiwa nguvuni. Baada ya kutaabikia ufungwa na mateso ya mwaka mmoja, kwa fatwa ya Makadhi hawa wawili (Ibnul-Jamaat na Burhanud-Din) yeye akauawa na mwili wake ukatundikwa kwenye kiunzi. Kwa vile walitangaza kwamba kuna Rafidh ni Kafiri yuko juu ya miti ya kunyongea, watu wa kawaida waliupiga mawe mwili ule. Baadae, mwili ule ulichomwa na jivu lake likasambazwa. Miongoni mwa maulamaa na wanasheria wa Kishia wa kujivunia wa Syria katika karne ya 10 Hijriya, alikuwa Sheikh Zainud-Din bin Nurud-bin Ali bin Ahmad Amili. Alikuwa akijulikana sana miongoni mwa marafiki na maadui kwa elimu yake na uadilifu. Akiwa mtunzi wa vitabu vingi, alijiweka mbali na ulimwengu na akaandika vitabu 200 juu ya masuala mbalimbali. Ingawa aliishi maisha ya kujitenga, bado maulamaa wa Kisunni walijenga chuki juu yake, na wivu juu ya umaarufu wake miongoni mwa watu. Mkubwa katika wapinzani wake alikuwa Kadhi Saida, ambaye aliandika kwa Mfalme Sultan Salim
59
Mikesha ya Peshawar
malalamiko yafuatayo: Hakika kuna mtu anaishi katika jimbo la Syria ambaye ni mzushi, mtu ambaye hahusiki na mojawapo ya madhehebu manne. Sultani Salim aliamrisha kwamba mwanasharia huyo aletwe mbele ya mahakama huko Istanbul (Uturuki). Alitiwa nguvuni ndani ya Msikiti Mtukufu wa Makka na alifanywa mfungwa siku arubaini mjini Makka. Katika safari ya baharini kuelekea Istanbul, alikatwa kichwa na mwili wake ukatupwa baharini. Ni kichwa chake tu ndicho kilichopelekwa kwa mfalme Waheshimiwa Mabwana! Nakuulizeni kwa shauku moyoni, kwa jina la Allah mseme iwapo mlipata kusikia tabia ya namna hiyo kwa upande wa Maulmaa wa Kishia dhidi ya Sunni kwa sababu ya kutofauta madhehebu ya Shia. Ni hoja gani mtakayoleta kuthibitisha kwamba iwapo mtu akiacha kufuata yoyote katika madhehebu manne, yeye anakuwa ni kafiri na kwamba kuuawa kwake yeye ni wajib? Je, ni mantiki kufuata madhehebu ambayo yamekuja kuweko karne kadhaa baada ya Mtume, ambapo wale wanaofuata kanuni iliyokuwepo tangu wakati wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) wanaamriwa wauawe?
60
Mikesha ya Peshawar
kubakia tumeungana (yaani kulinda umoja wetu). Kwa upande mwingine mara kwa mara maulamaa wa Kisunni wamekuwa wakiwachochea watu wao, wakisema kwamba Mashia ni wazushi, Marafidhi,Ghullat, au Mayahudi. Wanasema kwamba, kwa kuwa hawa Shia hawafuati mmoja katika Maimam wanne wa Kisunni (Abu Hanifa, Malikki, Shafii na Hanbali), basi ni makafiri. Ukweli ni kwamba wale wanaowafuata Ahlul-Bait wa Mtume (s.a.w.w.) wameongozwa sawasawa.
61
Mikesha ya Peshawar
Hafidh: Kila siku maelfu ya watu wanasimama mbele za makaburi ya waliokufa na kuwaomba msaada. Je, kitendo hiki sio mfano wa kuabudu wafu? Kwa nini Maulamaa wasikataze wakati mamilioni ya watu hao wakiweka mapaji yao ya nyuso zao kwenye ardhi wakisujudu katika kuwaabudu wafu? Nashangaa ni kwa vipi bado unayaita mambo haya kuwa sio shirki. Wakati majadiliano na Mawalana Hafidh yakiendelea, faqihi wa Kihanafi, Agha Sheikh Abdus-Salam alikuwa anakichunguza Hidayatuz-Zairin. Akasema kwa msisitizo mzito, Tazama hapa! (akikionyesha kile kitabu). Ulamaa wako anasema kwamba wakati mahujaji wanapomaliza Ziarat katika Makuba ya Maimam, wanapaswa kuswali rakaa mbili za Sala ya Ziarat. Huenda hawaikusudii Sala hii kwa jina la Allah; vinginevyo, nini maana ya Sala ya Ziarat? Huu sio ushirikina kufanya ibada ya Sala kwa ajili ya Imam? Mahujaji wanaosimama na kuelekeza nyuso zao kwenye makaburi na kusali ni ushahidi mzuri wa ushirikina. Hiki ni kitabu chenu Sahihi. Unaweza ukatetea hali yenu hii? Muombezi: Mbona unajiingiza katika mazungumzo ya kitoto! Hivi umewahi kuwako kwenye Ziarat hizo na kuwaona Mahujaji hao ana kwa ana? Sheikh: Hapana. Muombezi: Sasa ni vipi ukaweza kusema kwamba mahujaji hao wanaswali wakiwa wameelekeza nyuso zao kwenye kaburi, na kusema kwamba swala hii ya Ziarat ni dalili ya ushirikina? Sheikh: Kitabu hiki kinasema kwamba waswali Swala ya Ziarat kwa ajili ya Imam. Muombezi: Hebu lete hicho kitabu nikiangalie. Ngoja nisome maelekezo kuhusu Ziarat, mpaka tufikie kipengele cha Sala ambacho ndio hoja ya kukataa kwako. Wakati wowote ukiona dalili ya ushirikina, tafadhali ionyeshe. Na iwapo utaona alama za kuamini na kuabudu Mungu Mmoja kuanzia juu mpaka chini usije ukajisikia vibaya kwa hilo, bali sema kwamba ulikuwa umeelewa vibaya. Kitabu kiko hapa mbele yenu.
62
Mikesha ya Peshawar
asingetuongoza. Wakati akifika lango la Uwanja wa Mtukufu yampasa asome, baada ya kumtukuza Allah: Nashuhudia kwamba hakuna Mungu isipokuwa Allah, aliye Mmoja. Yeye hana mshirika. Na pia ninashuhudia kwamba, Muhammad ni mja na Mtume Wake. Ametuletea kweli kutoka kwa Allah. Na pia nashuhudia kwamba Ali ni mja wa Allah na ndugu yake Mtume wa Allah. Allah ni mkubwa mno, Allah ni mkubwa mno, Allah ni Mkubwa mno. Hakuna Mungu isipokuwa Allah, na Allah ni Mkubwa mno. Shukrani zote ni Zake kwa mwongozo na msaada Wake kuitikia kile alichofunua juu ya njia kuelekea Kwake. Wakati Mwenye kufanya Ziarat akifika kwenye lango la Quba, yampasa asome: Ninashuhudia kwamba hakuna Mungu isipokuwa Allah, aliye Mmoja. Yeye hana Mshirika pamoja Naye mpaka mwisho. Wakati, baada ya kwisha kuomba ruhusa ya Allah, ya Mtume, na ya Maimam, mwenye kufanya Ziarat hufika ndani ya Quba, husoma Ziarat mbalimbali ambazo zina maamkuzi kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) na kwa Amirl-Muminin. Baada ya Ziarat, husali rakaa sita (za Sunna), rakaa mbili kwa ajili ya Amirl-Muminin na rakaa mbili kwa ajili ya Nabii Adam na mbili kwa ajili ya Nabii Nuh ambao wamezikwa katika eneo hilo hilo.
63
Mikesha ya Peshawar
mbili hizi za Sala kutoka kwangu na unijazi, kama ambavyo ungewajazi watendaji wa matendo mema. Ewe Allah! Nimeitoa Sala hii (kama Sadaka) kwa ajili Yako, na nimerukuu na kusujudu mbele yako Wewe kwa kunyenyekea Kwako. Wewe ni Mmoja ambaye huna mshirika. Hairuhusiwi kusali, kurukuu au kusujudia chochote isipokuwa Wewe. Wewe ni Allah, uliye Mkuu na hakuna mungu isipokuwa Wewe. Mabwana waheshimiwa! Kwa jina la Allah, kuweni waadilifu. Kuanzia muda ule mwenye kuzuru anapoweka mguu wake juu ardhi ya Najaf, mpaka baada ya kusali sala yake ya Ziarat, yeye anajishugulisha katika kumkumbuka Allah swt. Sheikh: Inashangaza kwamba huoni yalioandikwa hapa: Busu kizingiti cha mlango na kisha ingia ndani ya haram ya Kuba. Tumesikia kwamba wakati wenye kufanya Ziarat wakifika kwenye mlango wa kuba la Maimam wao, wanakwenda Sijida kwa heshima. Je kusujudu huku sio kwa ajili ya Ali? Je, sio ushirikina wakati tunasujudia mwingine asiyekuwa Allah? Muombezi: Kama mimi ndio ningekuwa ni wewe, nisingelisema neno. Ningenyamaza kimya mpaka mkutano wa mwisho wa mjadala huu na kusikiliza mantiki ya majibu yangu. Lakini nitakuambia kwa ufupi mara nyingine tena kwamba, kubusu kizingiti au sakafu ya makuba ya Maimam sio ushirikina. Umelitafsiri vibaya neno kubusu na kuliona kuwa ni sawa na kusujudu. Wakati unasoma kitabu hicho mbele yetu unadiriki kufanya mabadiliko ya ugeuzaji maana ya maneno kama huu, sijui ni jinsi gani utatusingizia wakati utakapokuwa peke yako ukiwahutubia watu wasio na elimu. Maelekezo yaliyomo katika kitabu hiki na vitabu vinavyohusu Dua na sehemu za Ziarat ni kwamba mwenye kufanya Ziarat, kama namna ya kuonyesha heshima, inampasa kubusu kizingiti sio kusujudu. Vipi unafikiria kubusu na kusujudu kuwa ni kitu kimoja? Na, ni wapi umeona ima katika Qurani tukufu au katika hadith yoyote kwamba kubusu kizingiti cha Kuba la Mtume au Imam kumekatazwa? Hivyo kama huna jibu la maana kwa swali hili, usipoteze wakati wetu. Na, kama unavyosema umesikia kwamba wafanyao Ziarat husujudu kwa heshima. Kwa uhakika hukuwaona kwa macho yako wakifanya hivi. Qurani tukufu inasema, Enyi ambao kwamba mmeamini! Akikujieni fasiki na habari, ichunguzeni, msije mkadhuru watu kwa ujinga, kisha mkawa ni wenye kusikitika kwa yale muliyoyafanya. (49:6). Kwa mujibu wa amri hii ya Qurani Tukufu, hatupasi kutegemea maelezo ya watu waovu. Yatupasa kufanya juhudi kubwa kujua ukweli, hata ikiwezekana kufanya safari ili kupata habari ya kweli moja kwa moja. Wakati nilipokuwa Baghdadi, nilikwenda kwenye makaburi ya Abu Hanifa na Sheikh AbdulKadir Jilani na nikaona watu walivyofanya. Ilikuwa vibaya zaidi kuliko ulivyoelezea kuhusu Mashia wanavyofanya, lakini kamwe sijalizungumza hili. Nilipofika kwenye kaburi la Abu Hanifa hapo Muazzam, niliona kundi
64
Mikesha ya Peshawar
la Masunni wakirudia rudia kubusu Sakafu, badala ya kizingiti, na kujigaragaza kwenye sakafu. Lakini kwa kuwa hawakuonekana kwa mahabithi, na kwa sababu sikuwa na sababu za kuwalaumu, kwamwe sikuitaja habari hii kwa mtu yoyote. Nilielewa kwamba walikuwa wakifanya hivyo kwa ajili ya mahaba sio kama ibada. Ewe bwana mheshimiwa! Hakika hakuna Shia mcha-Mungu ambaye amediriki kusujudu kwa yeyote isipokuwa Allah. Kama, kwa vyovyote vile iwavyo, kama tunaanguka chini ya ardhi katika hali kama ya kusujudu na kusugua mabapa ya nyuso zetu juu yake (bila kuwa na nia ya kuabudu), hiki ni kitu kidogo sana. Kuinama mbele ya mtu mtukufu bila kumfikiria kuwa yeye ni Allah, au kuanguka chini juu ya ardhi na mtu kusugua uso wake juu yake, sio ushirikina. Ni matokeo ya mahaba makubwa. Sheikh: Inakuwaje kwamba tunaposhuka chini juu ya ardhi na kuweka paji letu la uso juu yake, kwamba kitendo hiki kisiweze kuwa sawa na kusujudu? Muombezi: Kusujudu kunategemea juu ya nia, na nia ni jambo la moyo. Ni Allah peke yake ndiye anayejua nia zetu za moyoni. Kwa mfano tunaweza kuona watu wamelala chini juu ya ardhi kwa hali kama ya kusujudu. Ni kweli kwamba kusujudia yeyote asiyekuwa Allah sio sawasawa, hata ikiwa bila nia yoyote. Walakini, kwa kuwa hatujui nia za mioyo yao, hatuwezi kuiita hiyo kuwa ni Sijida ya Ibada.
Na aliwainua wazazi wake na kuwaweka katika kiti cha Ufalme, na wote wakaporomoka kumsujudia, na akasema; Ewe Baba yangu, hii ndiyo hakika ya ndoto yangu ya zamani; bila shaka Mola wangu ameithibitisha .. (12:100). Aidha, Qurani Tukufu inasema katika sehemu nyingi kwamba Malaika walifanya Sajida mbele ya Mtume Adam. Hivyo kama kusujudu namna hiyo ni ushirikina, basi nduguze Mtume Yusufu na Malaika wa Allah walikuwa washirikina. Ni Iblis aliyelaaniwa peke yake ndiye ambaye hakuwa mshirikina!
65
Mikesha ya Peshawar
Hakuna ila maisha yetu haya ya dunia, tunakufa na kuishi, basi, wala sisi si wenye kufufuliwa. (23:37). Kama mjuavyo nyote, wale wanaoamini katika Allah wanajua kwamba kuna maisha baada ya kifo. Wakati mwanadamu akifa, mwili wake unakuwa hauna uhai, lakini, tofauti na wanyama, roho na hisia ya kusema hubakia katika viwiliwili vilivyo sawa na hivi, lakini halisi zaidi na watarehemiwa au kuadhibiwa katika hali ya mpito (barzakh) au mahali pa mateso. Mashahidi na wale waliouawa katika njia ya Allah watafurahia neema maalum. Hii imesimuliwa katika Qurani Tukufu: Na usiwadhanie wale waliouawa katika njia ya Allah kuwa ni wafu; bali wahai na wanaruzukiwa kwa Mola wao, wanafurahia aliyowapa Allah kwa fadhila zake, na wanafurahia kwa hilo hilo wale ambao wameachwa nyuma yao, bado hajajiunga nao; ya kwamba haitakuwa hofu juu yao wala hawatahuzunika. (3: 169-170). Ninatafakari juu ya maneno haya: Wahai (na) wanaruzukiwa kwa Mola wao (3: 169) Wao wanatujibu, lakini kwa vile kusikia kwetu kumefunga kwa mapazia ya ulimwengu wa kimaada hatusikii sauti zao. Kwa ajili hiyo katika salaam (ziarat) kwa Imam Husein, tunasema; Ninashuhudia kwamba unasikia ninayosema na kwamba unajibu. Je, umesoma Khutuba na 85 katika Nahjul-Balagha? Kizazi cha Mtume wametambulishwa kama ifuatavyo: Enyi watu huu ni usemi wa Mtume: Yeyote anayekufa miongoni mwetu sio mfu, na yeyote ambaye anaoza (baada ya kufa) kutoka miongoni mwetu kwa hakika haozi. (Nahjul-Balaghah Tarjuma ya Kiingereza, Juz. 1, uk. 130 iliyochapishwa na Peer Muhammad Ebrahim Trust, Karachi.) Hivyo ni kwamba, katika uwanja wa mwanga na mambo ya Kiroho, Ahlul-Bait wanaishi na wanabakia wenye kudumu milele. Kwa ajili hiyo, Ibn Abil-Hadid Mutazali na Sheikh Muhammad Abdul, Mufti mashuhuri wa Misri, wakisherehesha hadith hiyo hapo juu, wanasema kwamba, dhuria wa Mtume
66
Mikesha ya Peshawar
(s.a.w.w.) hawakufa kwa namna walivyokufa wengine. Hivyo tunaposimama mbele ya makaburi ya Maimam, hatusimami mbele za wafu, na hatuzugumzi wafu. Tunasimama mbele za walio hai na kuzungumza na wanaoishi. Kwa ajili hiyo sisi sio waabuduo wafu. Tunamuabudu Allah. Je huamini kwamba Imam Ali, Imam Husain, na mashahidi wa Badr, Hunain, Uhud na Karbala walitoa muhanga maisha yao katika njia ya Allah kwa ajili ya haki? Je, hawakuwakabili madhalimu wa Kiquraishi, Bani Umayya, Yazid na wafuasi wake, ambao lengo lao lilikuwa ni kuifulitia mbali Dini. Kama vile ule uimara wa masahaba wa Mtume na mihanga ya mashahidi wa Badri, Hunain, na Uhud ulivyopelekea kushindwa kwa ukafiri, kwa njia hiyo hiyo uamuzi imara wa Imam Husain kutoa mhanga maisha yake, uliimarisha Uislamu. Kama Imam asingesimama imara dhidi ya nguvu za uovu, mwana kulaaniwa Yazid angeuharibu Uislamu na angeweza kupenyeza ukafiri wake katika Umma wa Kiislamu. Sheikh: Inashangaza kwamba, unamwita Khalifa wa Waislamu Yazid bin Muawiya kuwa ni kafir. Yakupasa uelewe kwamba Muawiya bin Abu Sufyan alimchagua yeye kuwa Khalifa. Khalifa wa Pili Umar bin Khattab na Khalifa wa tatu Uthman aliyedhulimiwa, walimchagua Muawiya kuwa Amir (Gavana) wa Syria. Kwa sababu ya uwezo na vipaji vyao, watu waliwakubali kuwa Makhalifa kwa uaminifu kabisa. Hivyo uhusishaji wako wa makhalifa wa Uislamu kuwa ni makafiri una maana kwamba hukuwatukana tu Waislamu wote ambao wamewakubali kama makhalifa, bali vile vile umewatukana Makhalifa waliopita ambao wamewaidhinisha wao kuwa makhalifa au magavana. Kwa kweli walifanya makosa, ambayo yalitokea wakati wa ukhalifa wao. Mjukuu wa Mtume, Imam Husain, aliuwawa, lakini hili lilisamehewa. Kwa vile walitubia, Allah Mwingi wa rehema, aliwasamehe. Imam Ghazali na Damiri wameshughulika na nukta hii kwa uangalifu kabisa katika vitabu vyao na wamethibitisha usafi wa khalifa Yazid. Muombezi: Kamwe sikutaraji kwamba ushabiki wako utakwenda mbali kiasi hicho mpaka kutetea kusudi la mlaaniwa Yazid. Unasema kwamba kwa vile wakubwa wao waliowatangulia waliona inafaa kuwafanya ma-Amir au watawala, basi Waislam wote iliwapasa wawakubali. Kauli hii haileti maana yoyote. Tunasema kwamba Khalifa yapasa awe safi (aliyeepukana kabisa na madhambi yote) na kuteuliwa ki-Ungu ili kwamba tusije tukadumu katika ukandamizwaji. Unasema kwamba Ghazali na Damiri wametetea nafasi ya Yazid. Lakini walikuwa mashabiki kama ulivyo wewe. Hakuna mtu mwenye akili timamu ambaye atathubutu kamwe kujaribu kutetea matendo ya mlaaniwa Yazid. Unasema kwamba Yazid alifanya kosa katika kumuua Imam Husain. Lakini kumuuwa mtoto kipenzi mno wa Mtume, kuchanganya pamoja na watu 72, wakiwemo watoto wadogo na wazee, na kuwachukua mateka mabinti wacha-Mungu wa Mtume vichwa wazi na nyuso wazi, haikuwa kosa la hivi hivi tu. Ulikuwa ni ukatili usiosemeka. Aidha, jinai zake hazikuishia kwenye chinja chinja hii ya kutisha peke yake. Kuna mifano mingi mingine ya ukafiri wake.
67
Mikesha ya Peshawar
UKAFIRI WA YAZID.
Miongoni mwa mambo yanayothibitisha ukafir wa Yazid ni beti zake mwenyewe za kishairi. Kwa mfano anaandika hivi: Kama kunywa (pombe) kunakatazwa katika dini ya Muhammad, basi na iwe hivyo; mimi nitaukubali Ukristo. Ni ulimwengu huu tu, kwa ajili yetu. Hakuna ulimwengu mwingine. Haipasi sisi kuzuiliwa starehe za ulimwengu huu. Beti hizi zinajitokeza katika mkusanyiko wa kazi zake za kishairi, na Abul-Faraj bin Jauzi ameyaandika katika kitabu chake Radd Alal-Mutaasibul-Anid. Anasema tena: Mwenye kututishia na hekaya za siku ya mwisho, muache afanye hivyo. Haya ni mambo ya uongo, yanayotunyima sisi starehe zote za sauti na muziki. Sibt Ibn Jauzi anaandika katika kitabu chake Tadhkira, uk. 748 kwamba, wakati dhuria wa Mtume walipoletwa Syria kama mateka, Yazidi alikuwa amekaa katika ghorofa ya pili ya kasri yake. Yeye alisoma beti mbili zifuatazo: Wakati machela za ngamia zilizobeba wafungwa zilipotokea, kunguru alilia (ndege mbaya katika Uarabu). Nilisema: Ewe Kunguru, kama ulie au usilie, nimelipa kisasi juu ya Mtume. Kisasi huelekeza kwenye ukweli kwamba, wazee wake na jamaa zake wa karibu waliuawa katika vita vya Badr, Uhud, na Hunain. Aliwachukulia kisasi cha vifo vyao kwa kuwaua watoto wa Mtume. Ushahidi mwingine wa Ukafir wake ni kwamba alipofanya hafla ya kusherehekea Shahada ya Husain, alisoma beti za Kikafir za Abdullah bin Uzza Bari. Sibt Ibn Jauzi, Abu Raihan, na wengine wameandika kwamba Yazid alitamani wazee wake wangekuwepo, ambao wote walikuwa makafir, na waliuawa katika vita vya Badr kwa amri ya Mtume. Yazid alisema: Natamani watu wa ukoo wangu ambao waliuawa huko Badr, na wale ambao wamewaona watu wa ukoo wa Khazraj wakilia ( katika vita ya Uhud) kwa ajili ya majeraha ya michomo mikali (ya panga, mikuki na mishale), wangekuwa hapa. Wangelinishangilia kwa sauti na kusema: Ewe Yazid mikono yako kamwe isipooze, kwa sababu nimewauwa wakuu wa ukoo wake( yaani ukoo wa Mtume). Nimefanya hivyo kama kisasi cha Badr, ambacho sasa kimekamilika. Bani Hashim walicheza mchezo tu na serikali. Hakukuja ujumbe kutoka kwa Allah, wala ufunuo wowote. Nisingekuwa wa familia ya Khandaq
68
Mikesha ya Peshawar
kama nisingechukua kisasi juu ya dhuria wa Mtume. Tumeyalipa kisasi mauaji yaliyofanywa na Ali kwa kumuuwa mtoto wake, mpanda farasi na simba mwerevu.
69
Mikesha ya Peshawar
kifungu kimoja tu katika Tadhkira, ya Sibti Ibn Jauzi uk. 163, kilichosimuliwa na AbulHasan Madaan: Baada ya mauwaji ya halaiki ya watu wa Madina, wanawake 1000 wasiolewa walizaa watoto.
70
Mikesha ya Peshawar
Ibn Jauzi, Abu Yala na Salih bin Ahmad, wakihoji kutoka kwenye Aya za Qurani wanaandika kwamba: Imethibitika kwamba imeruhusiwa kumlaani Yazid. Ni wajibu wa Waislamu wote kwamba yawapasa kujua haki alizonazo Imam Husein juu yao. Na ni vipi, kwa nguvu ya kupatwa kwake na mateso ya udhalimu na uonevu, yeye alivyounyweshea mti wa Uislamu kwa damu yake mwenyewe na damu ya familia yake. Vinginevyo, mti ule uliobarikiwa ungekufa kwa sababu ya udhalimu wa Bani Umayyah. Alikuwa ni Husain ambaye aliupatia Uislamu uhai mpya. Nasikitika kwamba badala ya kuitambua huduma hii ambayo watu hawa watukufu wameitoa kwa Uislamu, mnazua makinzano kuhusu wafanya ziara ambao wanazuru makaburi yao na kuwaita wenye kuabudu wafu. Mara nyingi tunasoma kwamba katika sehemu muhimu za nchi, kama Paris, London, Berlin, na Washington kuna makaburi ya kumheshimu Askari asiyejulikana. Inasemekana kwamba, kuteseka kwa uonevu wa adui na kwa kuihami nchi yake, alijitoa muhanga maisha yake. Lakini hakukuwa na alama juu ya mwili wake au nguo kuonyesha utambulisho wa familia yake au mji anakotoka. Kwa sababu alitoa maisha yake kwa ajili ya kuitetea nchi yake, ingawaje alikuwa hajulikani, alistahiki heshima. Wakati mfalme au mtu yeyote mashuhuri anapotembelea miji hii, huzuru hilo kaburi la Askari asiyejulikana na kuweka mashada ya maua juu yake. Askari asiyejulikana anapata heshima zaidi, lakini nasikitika kwamba, badala ya kuwaheshimu wafanya Ziara wanaozuru makaburi ya wanachuoni Waislamu wacha-Mungu sisi tunawashutumu. Baadhi yao waliijua Qurani yote kwa moyo. Walitoa mhanga maisha yao kuutetea Uislamu. Watu hawa ni pamoja na mawakala (wadhamini) wa Allah, Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) na dhuria wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) .
71
Mikesha ya Peshawar
Masikitiko yalioje kwamba katika nchi zote zilizostarabika, makaburi ya wafalme, wanachuo, na hata askari wasiojulikana yanaheshimiwa, lakini Waislamu ambao wanategemewa kuonyesha hisia nzuri za umuhimu wa kuhifadhi makaburi, ya wale ambao ni fahari yao, huyapora na kuyabomoa kama washenzi. Katika mji wa Makka na Madina, Wahhabi walibomoa makaburi ya mashahidi wa Uhud, pamoja na la Hamza, na jadi zake Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), kama Abdul-Muttalib, Abdullah, na wengineo. Vile vile walibomoa makaburi ya familia ya Mtume, watoto wake, kama Imam Hasani, Imam Zainul- Abidin, Imam Muhammad Baqir, Imam Jafar Sadiq, Bibi Fatima binti ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), na wengi wengine wa ukoo wa Bani Hashim na Maulamaa watukufu. Bado wanajiita wao ni waislamu. Hakika wao wanajenga ma-Quba makubwa kwa ajili ya watu wao mashuhuri na wafalme. Ukweli ni kwamba, Maulmaa wa madhehebu zote wamenukuu hadithi nyingi zikitutaka tuzuru makaburi ya waumini ili kwamba yasalimike kutokana na kuharibika. Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) mwenyewe alizuru makaburi ya waumini na akamuomba Allah kwa ajili ya wokovu wao.
DHURIA WA MTUKUFU MTUME (s.a.w.w.) NI MASHAHIDI KATIKA NJIA YA ALLAH NA WAKO HAI
Je, Unafikiri familia ya Mtume iliyotukuka ambao walitoa maisha yao katika njia ya dini ni mashahidi? Kama utasema sio mashahidi, ni nini hoja yako? Kama ni mashahidi, vipi utawaita kuwa wao, ni Wafu? Qurani Tukufu inaeleza kwamba;
Wako hai ( na) wanaruzukiwa na Mola wao. (3:169). Hivyo kwa mujibu wa Qurani na hadith, watu wale watukufu wako hai, Hivyo, sisi sio waabudu wafu. Hatuwasalimii wafu, tunawatukuza walio hai. Na hakuna Shia yoyote, msomi au asiye msomi, ambaye anawafanya wao kama waondoaji wa matatizo moja kwa moja. Huwachukulia kama waja wacha Mungu na njia ya kufikisha kwa Allah. Tunaweka mahitaji yetu mbele za Maimam wanyofu ili kwamba wamuombe Allah atuhurumie waja wake. Wakati tukisema, Ewe Ali, nisaidie, Ewe Husain, nisaidie ni kama tu, mtu ambaye anataka kumfikia Mfalme. Anaweza kwenda kwa waziri Mkuu na kuomba amsaidie. Hakika hamfanyi waziri mkuu huyo wa kama kimbilio la mwisho kwa kuondoa matatizo yake. Kusudio lake pekee ni kumfikia mfalme kupitia kwake, kwa vile kwa kutokana na cheo chake, anaweza kuonana na mfalme kwa urahisi sana. Shia hawawachukuli dhuria wa Mtume kama washirika katika vitendo vitukufu; wanawachukulia wao kama waja Wake wacha-Mungu.
72
Mikesha ya Peshawar
MKUTANO WA NNE JUMAPILI USIKU 26 RAJAB; 1345 A.H Mjadala kuhusu Uimamu:
Muombezi: Ninyi watu wema mnayo habari kwamba neno Imam lina maana nyingi. Kilugha lina maana ya Kiongozi. Imam al-Jamaat maana yake ni yule mwenye kuongoza Sala za Jamaa. Anaweza pia kuwa kiongozi wa watu katika mambo ya siasa au ya kiroho. Imam al-Juma maana yake ni yule mtu mwenye kuongoza sala ya Ijumaa. Kwa hiyo, Sunni wafuasi wa madhehebu nne na sheria, wanawaita viongozi wao Maimam kama vile Imam Abu Harifa, Imam Maliki, Imam Shafii, na Imam Hanbal. Wana-itiqadi na mafaqihi hawa ni viongozi wao katika mambo ya dini na wameweka Sheria za dini kwa mujibu wa utafiti wao au kwa mujibu wa kukisia kwao kuhusu uhalali wa matendo. Kwa hiyo wakati tunapovichunguza vitabu vya Fiqih vya Maimamu hawa wanne, tunakuta tofauti nyingi miongoni mwao zinazohusu misingi ya imani na Kanuni za utekelezaji wa imani. Halikadhalika Madhehebu yote yana viongozi kama hao, na miongoni mwa Mashia, maulamaa na mafuqahaa wanashikilia nafasi kama hizo hizo. Kwa kutoweka kwa Imam wetu wa zama aliye hai, wao wanatoa matamko ya kisheria kwa kutegemea elimu yao ya Qurani Tukufu, Hadithi sahihi za Mtume, na Maimamu wa kitume. Lakini hatuwaiti Maimamu kwa sababu Uimam ni wa washika makamu (wa Mtume) kumi na wawili peke yao - dhuria wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Kuna tofauti nyingine, Sunni baadae walifunga mlango wa ijtihad (juhudi ya kutafsiri sheria). Kuanzia karne ya tano A.H wakati ambapo, kwa amri ya Mfalme, maoni yaliyoelezewa na Maulamaa na Mafuqhaa yalikusanywa, huu uitwao uimamu uliishilizwa kwa maimamu wanne. Na madhehebu manne
73
Mikesha ya Peshawar
(Hanafi, Maliki, Shafii, na Hanbali) yakaanzishwa. Watu walilazimishwa kufuata kati ya moja ya hiyo, kama ilivyo desturi kwa wakati huu wa sasa. Haijulikani ni kwa misingi ipi kumfuata Imam mmoja kunapendekezwa. Sifa gani Imam wa Mahanafi alizonazo ambazo Imam wa Maliki hanazo? Ni sifa gani alizonazo Imam wa Shafii alizonazo ambazo Imam wa Hanbal hana.Na kama ulimwengu wa Kiislamu utalazimishwa wenyewe kufungwa kwenye kufuata moja ya Madhehebu manne, basi maendeleo ya Jumuiya ya Kiislamu yatakuwa yamefungwa kabisa, ingawaje kwamba Uislamu hutufundisha kwamba yatupasa kusonga mbele pamoja na nyakati. Iufanya hivi, tunahitaji uongozi wa Maulamaa. Kuna mambo mengi ambayo haitupasi kufuata hukumu ya Mujtahidi aliyekufa. (Kuanzia Jihad, kujitahidi, humaanisha katika hali hii, mtu anayejitahidi kutafsiri na kuunda taratibu na Sheria, kwa vile Ijtihad inahusika kwenye njia ya kujitahidi), bali inapasa kumgeukia mujtahid aliye hai kwa ajili ya kupata mwongozo. Mujitahidi wengi wamezaliwa baadae miongoni mwenu, ambao walikuwa na cheo cha juu katika elimu kuliko wale Maimam wanne. Sijui kwa nini upendeleo unatolewa kwa wale waliopita ili kwamba si wengine ila wao tu waweze kufuatwa na haki za wengine kupuuzwa. Katika fiqih ya Shia, Mujtahid katika kila zama, mpaka wakati wa kujitokeza kwa Mtukufu Imam wa zama zetu, wao wanayo haki ya kufanya jitihada. Katika kuhusu matatizo mapya, hatuwezi kufuata hukumu ya Mujtahid aliyekufa.
74
Mikesha ya Peshawar
Muombezi: Hatulazimiki na mantiki kujifunga sisi wenyewe kuwafuata wao peke yao. Wengi wa Maulamaa wenu wengine walikuwanazo sifa sawa kama hizi. Mpaka wa kuwafuata wao peke yao ni kebehi kwa Maulamaa wengine wenye sifa sawa na zao. Hatuwezi kulazimishwa kufuata mtu mmoja yeyote au watu wengine bila maelekezo ya kimamlaka kutoka kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Hakuna ruhusa kama hiyo kutoka kwa Mtume kuhusu Maimamu wenu wanne. Basi vipi muiwekee dini mpaka (kizuizi) kwenye madhehebu haya manne tu?
75
Mikesha ya Peshawar
hadithi kutoka kwa Mtume isemayo kwamba: Qurani na dhuria wangu ni dhamana zangu; kama mtashikamana wenyewe kwenye viwili hivi, kamwe hamtapotea. Kwa kuliunga mkono hili, Ibn Hajar ananukuu hadithi nyingine kutoka kwa Mtume kuhusu Qurani Tukufu na dhuria wake watoharifu: Msivuke mipaka ya Qurani na dhuria wangu; wala msiwapuuze. Vinginevyo mtaangamizwa. Na msiwafundishe dhuria wangu kwa vile wao wanajua zaidi kuliko mlivyo ninyi. Baada ya hivi, Ibn Hajar akatoa maelezo kwamba, hadithi hizo hapa juu huthibitisha kwamba dhuria wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) ni bora kuliko wengine wote katika elimu na katika kutekeleza wajibati za kidini.
76
Mikesha ya Peshawar
Hawa walikuwa watu aina gani Imam Shafii, Abu Hamid bin Muhammad Ghazali, na Jarullah Zamakhshari? Hafidh: Walikuwa Mafuqaha wakubwa, wanachuo wasomi, watu wachamungu, na Maimamu wetu.
77
Mikesha ya Peshawar
yalikuwa siku zote tofauti na hadith za kweli. Maulamaa wenu wenyewe wemewalaumu Maimamu wenu. Maulamaa wa Kishia hawakuwahusisha na chochote, isipokuwa kile Maulamaa wenu wenyewe walichosema kuhusu wao. Kwa upande mwingine, hakuna tofauti ya maoni miongoni mwa Ulamaa wa Kishia kuhusiana na nafasi za hao Maimamu kumi na mbili. Tunawaona Maimamu watukufu kama wanafunzi wa fundisho moja. Maimamu hawa - wote walitenda kwa mujibu wa sheria za Ki-Mungu ambazo yule mwisho wa Mitume aliwapa. Kamwe hawakutenda kwa kukisia au kuafiki uzushi. Walichosema au kufanya kilikubaliana na maneno ya Mtume. Hivyo, hakukuwa na tofauti miongoni mwao.
78
Mikesha ya Peshawar
Hii imenukuliwa na Maulamaa wenu maarufu, kama Hamidi katika Jami-BainusSahihain na Mulla Sad Taftazani katika Sharhe Aqaid-e-Nasafi. Kutoelewa sharti hata moja la utekelezaji wa imani hakuwezi kuwa sawa na ujinga ulioelezwa na Baidhawi kuhusu kutokujua misingi, yaani kwamba ujinga wake ni sababu ya ukafir. Kwa hiyo Uimamu ni moja ya misingi ya imani na ni hatua ikamilishayo Utume. Kwa ajili ya hiyo, kuna tofauti kubwa kati ya dhana ya Uimamu wetu na ile inayotafsiriwa na ninyi. Mnawaita Maulamaa wenu Maimamu, kama vile Imam Adhma, na Imam Maliki. Lakini hii ni maana ya mdomo. Sisi pia tunatumia neno Imam-e-Jumaa, Imam-e-Ja-maat. Hivyo wanaweza wakawepo mamia ya Maimamu kwa wakati mmoja, lakini katika maana ya kitaalamu (kiistilahi) ambayo kwayo tunatumia neno Imam, ina maana muwakilishi wa Allah. Katika maana hii kuna Imam mmoja tu kwa wakati mmoja. Sifa bora za elimu, Maadili, ushujaa, upenzi kwa Allah, na uchamungu zimekamilishwa ndani yake. Anawashinda binadamu wote katika tabia zote na hushikilia hali ya kutofanya makosa. Dunia haitakuwa bila Imam wa aina hiyo mpaka siku ya malipo. Imam wa ubora kama huo anakuwa katika kiwango cha juu kabisa cha mafanikio ya kiroho. Imam kama huyo anaidhinishwa na Allah na anateuliwa na Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Hushinda viumbe wote pamoja na Mitume waliopita. Hafidh: Kwa upande mmoja unawashutumu Maghulat, na kwa upande mwingine wewe mwenyewe kiububusa unawasifu Maimamu na kuiona nafasi yao ya juu zaidi kuliko ile ya Mitume. Akili ya kawaida inalikataa hili, na Qurani Tukufu vilevile imeeleza kwamba Mitume wamewekwa katika nafasi ya juu zaidi. Nafasi yao iko baina ya uhuru wa ki-ungu na lile lenye kuwezekana. Kwa vile maelezo yako hayaungwi mkono na akili, hayawezi kukubaliwa.
79
Mikesha ya Peshawar
Hakika nitakufanya Imam wa watu. Ibrahimu akasema: Akasema ahadi yangu haiwafikii madhalimu. (2:124).
Na dhuria wangu?
Aya hii ambayo inaonyesha nafasi ya Uimamu, pia inathibitisha kwamba cheo cha Uimamu ni cha juu kuliko cha Utume. Kwa vile nafasi ya Mtume Ibrahimu ilinyanyuliwa kutoka Utume kwenda Uimamu. Hafidh: Hii ina maana, kwa mujibu wa maelezo yako, ni kwamba nafasi ya Ali ilikuwa ya juu kuliko ile ya Mtume wa Mwisho. Hivi ndivyo Maghulat walivyoamini, kama wewe mwenyewe ulivyokiri.
80
Mikesha ya Peshawar
hawako sawa. Kila mmoja yuko tofauti na mwingine kwa mujibu wa kisomo, uwezo, na mafanikio yake. Kwa mtazamo wa lengo la Utume, Mitume wote wa Allah wako sawa sawa. Walakini, kwa sababu ya tofauti katika daraja na elimu, wako tofauti. Qurani Tukufu inasema:
Tumewafanya baadhi ya Mitume kuwazidi wengine; Miongoni mwao wako ambao Allah amesema nao, na baadhi yao Amewatukuza kwa (vyeo vingi) daraja. (2: 253). Mwanachuo wenu wenyewe Jarullah Zamakshari anasema katika kitabu chake, Tafsir-ekush-Shaf kwamba, Aya hiyo hapo juu ina maana Mtume wetu alikuwa bora katika daraja kwa wengine wote kwa sababu ya sifa zake maalumu, muhimu zaidi ni ambayo kwamba alikuwa wa mwisho wa Mitume. Nawab: Nimefurahi umelitatua tatizo hili, lakini nina swali lingine, ingawa kwa namna nyingine halihusiki hapa. Tafadhali tueleze kwa ufupi sifa makhususi za Utume maalumu. Muombezi: Kuna sifa nyingi za pekee kwa Utume Maalumu, na kuna sababu nyingi mno zinazothibitisha vipi Mtume mmoja kati yao wote ndiye Mtume maalum wa Allah. Kwa hakika hatua hiyo huishiliza duru la Utume. Lakini mikutano hii haikupangwa kuthibitisha Utume wa Allah kwa Waislamu. Kama ingekuwa tuijadili nukta hii kikamilifu, tungetoka nje ya nukta yetu ya Uimamu. Walakini kwa ufupi hata hivyo, nitajadili nukta hii.
81
Mikesha ya Peshawar
ambaye huruka juu angani kutokana na nguvu za mbawa zake. Hivyo hivyo kiwango cha mtu cha mafanikio ya ubinadamu hupanda kutokana na elimu yake na matendo sahihi. Kuvuka mipaka ya hali ya kinyama na kufikia nyanja ya matendo ya kibinadamu hutegemea juu ya ukamilifu wa nafsi. Mtu ambaye hukusanya ndani yake stadi za elimu na matendo sahihi na akafikia thuluthi ya tabaka tatu za watu (watu wa kawaida, watu bora na watu bora zaidi), hufikia daraja la chini kabisa la Utume. Wakati mtu kama huyo anapokuwa shabaha ya hisani maalumu za Allah, anakuwa Mtume. Naam, kwa kweli Utume vilevile una daraja tofauti. Mtume anaweza kufikia daraja ya juu zaidi katika tabaka hizi tatu. Cheo hiki ni cha juu sana katika nyanja ya uwezekano, ambayo wenye busara (wataalamu) huiita Hekima ya Kwanza, na ambayo ni Athari ya Kwanza au Matokeo ya Mwanzo. Hakuna cheo cha juu kama hiki katika miliki ya viumbe. Nafasi hii imeshikwa na wa mwisho wa Mitume, ambaye ni wa kwanza, hakuna kama yeye isipokuwa kile Chanzo cha Awali. Wakati Mtume alipopandishwa kwenye daraja hii ya juu zaidi, Utume ulikomelezwa. Uimamu ni daraja la chini kuliko daraja ya juu zaidi ya utume, lakini ni hatua ya juu kuliko daraja zote nyingine za Utume. Kwa vile Ali alipandishwa kwenye hatua ya juu kuliko ya Utume na alikuwa mmoja katika nafsi pamoja na Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), aliaminishwa kazi ya Uimamu na hivyo kuwa mbora kwa Mitume wote waliopita. Hafidh: Sehemu ya mwisho ya maneno yako inachanganya. Kwanza, unasema Ali alikuwa katika ngazi ya Utume, pili, kwamba alikuwa nafsi moja na Mtume Muhammad, tatu, kwamba alikuwa bora kwa Mitume mingine. Nini hoja zako kuthibitisha ukweli wa maneno yako?
HOJA ZA CHEO CHA UTUME KWA AJILI YA ALI KUTOKA KWENYE HADITH MANZILA.
Muombezi: Kwamba Ali amepata cheo cha Utume yaweza kuthibitishwa kwa kurejea kwenye hadith ya Manzila (Hadith inayohusu vyeo), ambayo imesimuliwa kwa kauli moja kwa kadri ya maneno yanayofanana. Wa mwisho wa Mitume watukufu amerudia mara nyingi na katika mikusanyiko tofauti. Je, huridhiki kwamba kwangu wewe ni kama Harun alivyokuwa kwa Musa, isipokuwa tu kwamba hakutakuwa na Mtume baada yangu? Na wakati mwingine aliwaambia wafuasi wake. Ali kwangu mimi ni kama alivyokuwa Hauna kwa Musa. Hafidh: Usahihi wa hadith hii haukuthibitishwa. Hata kama ingethibitishwa kuwa ni kweli itakuwa ni simulizi pekee na kwa hiyo haikubaliki.
82
Mikesha ya Peshawar
83
Mikesha ya Peshawar
Maulamaa wenu wengi wengine wakubwa wameisimuliwa hadith hii muhimu pamoja na tofauti kidogo ya maneno kutoka kwa Masahaba wengi wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) kama vile: (1) Umar bin Khattab, (2) Sad bin Ali Waqqas (3) Abdullah bin Abbas; (4) Abdulllah bin Masud; (5) Jabir bin Abdullah Ansari, (6) Abu Huraira; (7) Abu Said Khurdri; (8) Jabir bin Sumra; (9) Maliki bin Huwairis, (10) Baraa bin Azib; (11) Zaid bin Arqam; (12) Abu Rafi; (13) Abdullah bin Ubai; (14) Abu Suraiha, (15) Hudhaifa bin Assad, (16) Anas bin Malik, (17) Abu Huraira Aslami, (18) Abu Ayyub Ansari, (19) Said bin Musayyab (20) Habib bin Abi Thabit, (21) Sharhbil bin Sad; (22) Ummi Salma (Mke wa Mtume); (23) Asma bint Umais, (Mke wa Abu Bakar); (24) Aqil bin Abi Talib (25) Muawiyya bin Abu Sufyan, na wengi wa Sahaba wengine. Kwa ufupi wote hawa wameisimuliwa pamoja na tofauti kidogo ya maneno kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) amesema: Ewe Ali, wewe uko kwangu mimi kama Harun alivyokuwa kwa Musa, isipokuwa kwamba hakutakuwa na Mtume baada yangu. Je, Maulamaa wote hawa wakubwa na kuna wengi sikuwataja hawatoshi kuthibitisha kwamba hadithi hii imekubaliwa kwa pamoja kuwa ya kweli? Je, utathibitisha sasa kwamba ulikuwa katika kutokuelewa? Kwa vile unachukua mwelekeo wa wasiwasi kuhusu ukweli wa hadith hii, yakupasa uangalie katika Kitabu Kifayatut-Talib fi Manaqib-e-Ali Bin Abu Talib, Sura ya 7, kilichoandikwa na Muhammad bin Yusuf Ganji Shafii, ambaye ni mmoja wa Maulamaa wenu Maarufu mno wa madhehebu yenu. Baada ya kunukuu hadith sita zenye kumtukuza Ali, mwandishi huyu akaisherehesha (uk. 149) hadith hii kama ifuatavyo: Hii ni hadithi ambayo usahihi wake umekubaliwa na wote. Imesimuliwa na Maimamu wenye elimu zaidi na Huffadh (wajuao Qurani Tukufu kwa moyo), kama vile Abu Abdullah Bukhari katika Sahih yake, Muslim bin Hajjaj katika Sahih yake, Abu Dawud katika Sunan yake, Abu Isa Tirmidhi katika Jami yake, Abu Abdur-Rahman katika Sunan yake, Ibn Maja Qazwini katika Sunan yake. Wote hawa kwa pamoja wamekubali usahihi wake. Hakim Nishapuri amesema kwamba hadith hii imeingia katika hatua ya Mutawatir. Nina hakika kwamba sihitaji kutoa ushahidi zaidi kuonyesha kwamba hadith hii ni Sahihi. Hafidh: Mimi sikukosa maadili ya kidini, hivyo siwezi kukataa mantiki yako ya kiakili, lakini hebu vuta mazingatio kwenye kauli ya mwanachuo na mwana itikadi mkubwa, Abul-Hasan Amadi, ambaye ameikataa hadith hii. Muombezi: Nashangaa kwa nini mtu mwenye elimu kama wewe, baada ya kusikia maoni ya Maulamaa wako mashuhuri, utaamini taarifa ya mtu muovu ambaye alikuwa hata kuswali haswali.
84
Mikesha ya Peshawar
Sheikh: Mtu yuko huru kuelezea imani yake. Kama mtu akielezea maoni yake, haitupasi sisi kumkashifu. Haipendezi kwa wewe kumzulia uongo badala ya kutoa majibu yenye mantiki kwenye maelezo yake. Muombezi: Umenielewa vibaya. Simlaumu mtu yeyote kinyume cha haki. Si kuwa ninaishi katika wakati wa uhai wa Amadi. Maulamaa wenu wenyewe wameelezea kwamba alikuwa ni mtu aliyekuwa hana dini. Sheikh: Ni wapi ambapo Ulamaa wetu wamesema kwamba alikuwa ni mtu asiyekuwa na dini?
85
Mikesha ya Peshawar
86
Mikesha ya Peshawar
SIFA ZA ALI.
Muombezi: Hadith hii inathibitisha kwamba Ali anazo sifa tatu: (1) Cheo cha Utume. (2) Cheo cha Mrithi wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.); na (3) Nafasi yake ya juu miongoni mwa Sahaba wote wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Kama alivyo Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), wafuasi wa Ali walimfananisha na Harun, ambaye alikuwa Mtume, aliwekwa kuwa Khalifa wa Musa, na alikuwa mbora juu ya Bani Israel wote. Nawab: Harun alikuwa Mtume? Muombezi: Ndiyo. Nawab: Unaweza kuonyesha Aya kutoka kwenye Qurani yenye kuunga mkono nukta hii? Muombezi: Allah ameutaja Utume wake katika Aya nyingi. Anasema: Hakika tumekuletea wahyi kama tulivyompelekea wahyi Nuh na manabii baada yake. Na tulimpelekea Ibrahim na Ismail na Ishaq na Yakub na makabila; na Isa na Ayub na Yunus na Harun na Suleiman na Daud tukampa Zaburi. (4:163) Na halafu tena Anasema: Na mtaje Musa katika Kitabu, hakika yeye alikuwa mwenye kusafishwa, na alikuwa Mtume, Nabii. Na tukamwita upande wa kulia wa mlima, na tukamsongeza kuzungumza naye kwa siri. Nasi tukampa katika rehema zetu nduguye Harun, Nabii. (19:51-53) Hafidh: Hivyo kwa mujibu wa hoja yako, Muhammad na Ali wote walikuwa Mitume. Muombezi: Mimi sikuelezea katika njia unayoelezea wewe. Kwa kweli wewe mwenyewe unajua kwamba kuna tofauti kubwa ya maoni kuhusu ni Mitume wangapi walikuwepo. Baadhi wanadai kwamba walikuwepo 120,000 - au hata zaidi. Lakini wote hao katika nyakati zao husika walikuwa wamegawanyika katika makundi na walikuwa (daraja ya) chini kwa Mtume mkuu ambaye kwake kilifunuliwa kitabu kitukufu kikiwa na sheria mpya za dini. Watano miongoni mwao walikuwa ni Mitume wakuu: Nuh, Ibrahim, Musa, Isa, na mwisho wa Mitume wote, Muhammad, ambaye cheo chake kilikuwa ndio cha juu zaidi. Harun alikuwa mmoja wa wale Mitume ambao hawakuwa wa kudumu au wa kujitegemea. Alikuwa chini ya Sharia (mfumo wa kidini) ya ndugu yake Musa. Ali alifikia cheo cha Utume lakini hakupandishwa kwenye cheo hicho cha Mtume kwa asili yake yenyewe kwa vile alikuwa chini ya Sharia ya Muhammad. Katika hadith hii ya Manzila, madhumuni ya Mtume yalikuwa ni kuwaambia watu kwamba, kama vile ambavyo Harun amefikia Cheo cha Utume lakini alikuwa chini ya Musa, Ali alifikia cheo cha Utume. Uimamu ulipasishwa kwake, lakini alikuwa chini ya Muhammad (s.a.w.w.).
87
Mikesha ya Peshawar
88
Mikesha ya Peshawar
Mitume wote, akanichagua mimi kwa ubora, na akanifanyia mimi wasii, binamu yangu Ali. Kupitia kwake yeye akaimarisha mabega yangu, kama vile mabega ya Musa yalivyoimarishwa na Harun. Yeye (Ali) ni makamu wangu na msaidizi wangu. Kama kungelikuwepo na Mtume yoyote baada yangu, angelikuwa ni Ali, lakini hakutakuwa na Mtume baada yangu. Hivyo unaona kwamba siko peke yangu katika kudai cheo cha Utume kwa Ali. Mtume na Maulamaa wenu wamelikubali hilo. Kwa vile alikuwa na cheo cha Harun na kwa vile muda wa Utume ulikuwa umefikia kikomo Ali alikuwa mwenye kufaa zaidi kwa Ukhalifa. Moja ya dalili za utukufu wa cheo cha Ali ilikuwa kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) aliruhusu mlango wa nyumba ya Ali kubakia kufunguka kuelekea Msikitini. Maneno haya yalisababisha mshangao na bumbuazi miongoni mwa Masunni. Muombezi akauliza kwa nini inakuwa hivyo. Nawab: Ijumaa iliyopita tulikwenda Msikitini kusali. Hafidh Sahib akatueleza kuhusu ubora wa khalifa Abu Bakar. Alisema kwamba yeye aliruhusiwa kuweka mlango wa nyumba yake kuelekea Msikitini. Tunashangaa kusikia wewe ukisema kwamba ruhusa hii ilikuwa kwa Ali pekee. Tafadhali hebu ifafanue nukta hii. Muombezi: (Akimgeukia kwa Hafidh Sahib) Ulitoa kauli hii? Hafidh: Ndio Imesimuliwa kwenye hadith Sahih zetu, kama iliyoelezwa na Sahaba mchamungu na mwadilifu wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), Abu Huraira. Mtume aliagiza kwamba: Milango yote ifunguliwayo kuelekea Msikitini ifungwe isipokuwa mlango wa nyumba ya Abu Bakr, kwani Abu Bakr anatokana na mimi na mimi ninatokana na Abu Bakr. Muombezi: Hakika unajua kwamba kwa sababu ya ubora wa Amirul-Muminina, Ali, Bani Ummaya walifanya juhudi endelevu kwa kupitia njia za siri na hususani kupitia kwa watu wenye kujipendekeza na kumsifu sifu mno Muawiya, kama Abu Huraira na Mughira ili kubuni hadith kama hizo. Aidha, wafuasi wa Abu Bakr, kwa sababu ya kumuunga mkono kwao yeye, waliziimarisha hadith hizi za kughushi. Ibn Abil-Hadid, katika Sherhe yake ya Nahjul-Balagha Jz. 1, na tena katika Jz. 3, uk. 17, anaeleza kwa urefu kwamba miongoni mwa hadith nyingi za kughushi ni hii ielezeayo kuhusu kufungwa kwa milango ya nyumba zote inayoelekea Msikitini isipokuwa ule wa Abu Bakr. Kinyume na hadith hii ya kughushi, ziko hadith nyingi sahihi, ambazo zimesimuliwa sio tu katika vitabu Sahih vya Shia, lakini vilevile katika vitabu vya kutegemewa vya Mualamaa wenu wenyewe, kama Sahih. Nawab: Kwa vile ni suala la ubishani, huku Hafidh Sahib akisema ni pekee kwa Abu Bakr, na wewe ukisema ni pekee kwa Ali, tungefurahia kama ungenukuu kutoka vitabu vyetu ili kwamba tuweze kulinganisha rejea zako na zile za Hafidh Sahib.
89
Mikesha ya Peshawar
HADITH AMBAYO KWA AMRI YA MTUME MILANGO YA NYUMBA INAYOELEKEA MSIKITINI ILIFUNGWA ISIPOKUWA MLANGO WA NYUMBA YA ALI.
Muombezi: Vyanzo vifuatavyo vimesimulia kwamba, Mtume aliamrisha kwamba ile milango ya nyumba zote inayofunguka kuelekea Msikitini ifungwe isipokuwa mlango wa nyumba ya Ali: Ahmad bin Hanbal katika Musnad. Jz. 1 uk. 175, Jz. 2 uk. 26 na Jz. 4, uk. 369; Imam Abu Abdur-Rahman Nisai katika Sunan na katika Khasaisil-Alawi uk. 13 14; Hakim Nishapuri katika Mustadrak, Jz. 3, uk. 117- 125 na Sibt Ibn Jauzi katika Tadhkira uk. 24 25 wameshuhudia usahihi wa Hadithi hii juu ya msingi wa Sanad za wasimuliaji wa Tirmidhi na Ahmad. Halafu, Ibn Athri Jazri katika Athnal-Matalib, uk, 12, Ibn Hajar Makki, katika Sawaiq Muhriqa, uk. 76; Ibn Hajar Asqalani katika Fathul-Bari Jz. 7, uk. 12, Tibrani katika Ausat, Khatib Baghdadi katika kitabu chake cha Tarikh Jz. 7, uk. 205, Ibn Kathir katika Tarikh Jz. 7, uk. 342, Muttaqi Hindi katika Kanzul-Ummal, Jz. 6, uk. 408; Haithami katika Majimauz-Zawaid, Jz. 9, uk. 65; Muhibud-Din Tabari katika Riyadh Jz. 2, uk, 451; Hafidh Abu Nuaim katika Fadhailus-Sahaba na katika Hilyatul-Auliya Jz. 4, uk. 183; Jalalud-Din Suyuti katika Tarikhul-Khulafaa, uk. 116, katika Jamul-Jawami, katika Khasaisul-Kubra na katika Laaliul-Masunua Jz. 1, uk, 181; Khatib Khawarizmi katika Manaqib, Hamwaini katika Faraid, Ibn Maghazili katika Manaqib, Munawi Misri katika Kunuzud-Daqaiq, Sulayman Balkh Hanafi katika Yanabiul-Mawadda, uk. 87, alitumia sura yote nzima ya 17 kwa suala hili hasa peke yake, Shahabud-Din Qastalani katika Irshad Bari, Jz. 6, uk. 81, Halabi katika Siratul-Halabiyya Jz. 3, uk. 374 na Muhammad bin Talha Shafii katika MatalibusSuul na wengine wengi, hususan kutoka miongoni mwa masahaba mashuhuri wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) wamesimulia kitu hicho hicho. Kwa mfano Khalifa Umar bin Khattab, Abdulla Ibn Abbas, Abdullah bin Umar, Zaid bin Arqam, na Jabir bin Abdullah Ansari wamethibitisha usahihi wa hadith hii. Baadhi ya maulamaa wenu mashuhuri, kwa ajili ya kuepusha watu kutokana na kupotezwa na Bani Umayya wamesisitiza ukweli wa hadith hii. Muhammad bin Yusufu Ganji Shafii, katika kitabu chake Kifayatut-Talib Sura ya 50, ameshughulika na hadith hii chini ya kichwa cha habari maalum. Akinukuu kutoka vyanzo sahihi anasema kwamba, kwa vile idadi ya milango ya masahaba wa Mtume ilifunguka kuelekea Msikitini, na kwa vile Mtume amepiga marufuku watu wote kuingia Msikitini na hali ya janaba au haidh, aliagiza kwamba milango yote ya nyumba ifungwe isipokuwa mlango wa nyumba ya Hadhrat Ali. Yeye alisema: Fungeni milango yote bali acheni mlango wa nyumba ya Ali ubakie
90
Mikesha ya Peshawar
wazi. Muhammad bin Yusuph Shafii anasema kwamba ni Ali pekee yake ambaye kwamba aliruhusiwa kuingia na kukaa ndani ya Msikiti katika hali ya janaba. Aliendelea kusema: Kwa ufupi, Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) kwa kuufanya upendeleo huu wa kipekee juu ya Ali ilikuwa ni heshima kubwa mno. Inaonyesha kwamba Mtume alijua kwamba Ali, Fatima, na dhuria wao walikuwa huru kabisa kutokana na uchafu kama inavyoonyeshwa wazi na aya ya tohara katika Qurani Tukufu. Maneno haya ya mwanachuo wa Ki-Shafii yanaweza kulinganishwa na hadith iliyotajwa na Hafidh Sahib. Tukiachilia mbali vyanzo vyote Sahihi tulivyonukuu, kama mnao uthibitisho wowote wa utohara wa Abu Bakr, tafadhali utoeni. Ukweli ni kwamba hata Bukhari na Muslim katika ukusanyaji wao wa hadithi wameonyesha ukweli huu kwamba mtu aliyanajisika hawezi kukaa ndani ya Msikiti. Mtume alisema: Hairuhusiwi kwa mtu yeyote ambaye sitohara kukaa ndani ya Msikiti isipokuwa kwa mimi na Ali. Labda ningeruhusiwa hapa kunukuu hadith kutoka kwa Khalifa wa pili Umar bin Khattab, ambayo imeandikwa na Hakim katika Mustadrak, uk. 125, na Sulaiman Balkhi katika. Yanabinl-Mawadda Sura ya 56, uk. 210, na wengineo, kama Imam Ahmad bin Hanbal, Khatib Khawarizmi, Ibn Hajar, Suyuti, na Ibn Athir Jazri. Yeye alisema: Hakika Ali bin Abi Talib alikuwa nazo sifa tatu za pekee, kama ningekuwa na mojawapo kati ya hizo, ingelikuwa ni bora zaidi kwangu mimi kuliko ngamia wa manyoya mekundu:- (1) Mtume alimuozesha binti yake kwake, (2) Mtume aliagiza kwamba milango ya nyumba zote inayofunguka kuelekea msikitini ifungwe, isipokuwa mlango wa nyumba ya Ali; (3) Mtume alimpa bendera (ya Uislamu) siku ya vita ya Khaibar. Kutokana na maelezo haya, ni wazi sasa kwamba Ali alikuwa sawa kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) katika sifa zote, kama vile tu Harun alivyokuwa kwa Musa. Hivyo wakati Musa alipomuona anafaa kwa kazi hii, alimuomba Allah kumfanya mshirika katika ujumbe wake, ili kwamba aweze kuwa Waziri wake. Vivyo hivyo, wakati Mtume alipoona kwamba hakuna yoyote miongoni mwa wafuasi wake wote mwenye kustahiki kama Ali, alimuomba Allah amfanye Ali kuwa Waziri na mshirika wake. Nawab: Kuna hadith zaidi zinazohusu suala hili? Muombezi: Ndio, nyingi zinapatikana kuhusiana na suala hili katika vitabu vyenu wenyewe. Nawab: Niko tayari kuzisikiliza mradi ninyi pia (akionyesha upande wa Maulamaa wa upande mwingine) mtataka kusikiliza. Hafidh: Hakuna ubaya. Kusikiliza Hadith ni tendo la ibada kama simulizi yenyewe hiyo.
91
Mikesha ya Peshawar
WAKATI AKIWA KWENYE RUKUU KATIKA SALA ALI ALITOA PETE KUMPA MASIKINI.
Muombezi: Ibn Maghazili faqih Shafii katika Manaqib yake, Jalalud-Din Suyuti katika Durrul-Manthur mwana theolojia mashuhuri, Ahmad Thalabi katika KashfulBayan, Sibt Ibn Jauzi katika Tadhkiratul-Khawasul-Umma, kuhusiana na Aya ya Wilayat wananukuu kutoka kwa Abu Dharr Ghifari na Asma bint Umais (mke wa Abu Bakr) kwamba, wamesema kwamba siku moja walikuwa wanasali Sala ya Adhuhuri msikitini wakati Mtume alikuwepo. Akaja masikini akaomba sadaka. Hakuna aliyempa chochote. Ali alikuwa anarukuu (katika Sala). Wakati alipoonyesha kidole chake, masikini alitoa ile pete kutoka kwenye kidole chake. Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) aliyaona yaliyotokea, akanyanyua kichwa chake kuelekea mbinguni akasema: Ya! Allah, Ndugu yangu Musa alikuomba: Ya! Allah, nifungulie kifua changu na nifanyie wepesi kazi yangu. Chagua kwa ajili yangu msaidizi kutoka kwenye familia yangu, Harun ndugu yangu. Ilifunuliwa Aya kumuambia Musa kwamba dua yake imekubaliwa. Allah akachagua kwa ajili yake msaidizi na akaimarisha mikono yake na akawapa uwezo na mamlaka kiasi kwamba hakuna hata mmoja aliyeweza kuwashinda nguvu. ..na Musa akasema kumwambia ndugu yake Harun: Chukua mahala pangu miongoni mwa watu, na utendee wema wala usifuate njia ya waharibivu (7: 142)
92
Mikesha ya Peshawar
Vivyo hivyo, Ali alikuwa mmoja ambaye mbali na kuwa daraja ya Utume alikuwa ni mshirika wa Mtume katika hatua zote na sifa maalum. Hafidh: Nimeshangazwa kukusikia unavyoitia chumvi nafasi ya Ali. Wote tumeshitushwa. Umesema hivi punde tu kwamba Ali alikuwanazo sifa zote za Mtume. Muombezi: Maelezo haya sio ya kutia chumvi. Ni ya ukweli. Makamu wa Mtume, kutokana na akili ya kuwaida, yapasa awe mfano wa Mtume. Hata Maulamaa wenu wakubwa wameelezea itiqad kama hii hii. Imam Thalabi, katika Sherhe yake, aliithibitisha nukta hii. Na yule mwanachuo mkubwa wa Kisunni, Alim Fadhili Seyyed Ahmad Shahabud-Din, katika Kitabu chake Tauzihud-Dalail amerejea kwenye nukta hii kama ifuatavyo: Sio siri kwamba Amirul-Muminin alifanana na Mtume wa Allah, katika nyingi ya sifa nzuri, matendo yasiyo ya kibinafsi, tabia, maombi kwa Allah, na njia zote tukufu za maisha. Hii imethibitishwa na riwaya sahihi na vianzo vya kutegemea, na haihitaji uthibitisho wowote au hoja. Baadhi ya Maulamaa wamezihisabu kuwa ni sawa sifa zile ambazo Ali na Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) walikuwa nazo. Miongoni mwa sifa walizoshirikiana wote ni nasaba yao safi. Na tukihoji kutokana na aya ya tohara, tunaona kwamba Ali ni sawa na Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) katika utohara (Aya hii iliteremshwa kwa ajili ya watu watano: Muhammad, Ali, Fatima Hasan na Husain). Ali, kama Mtume alikuwa Mwakilishi wa Allah. Kwa mujibu wa madhehebu zote, aya ifuatayo iliteremshwa kwa ajili ya Ali. Hakika rafiki yenu mlinzi ni Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na walioamini; ambao hushika Swala na hutoa Zaka nao wakiwa wamerukuu. Ali alikuwa sawa na Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) katika utendaji kazi za Utume na kuhubiri, kama suala la Suratul-Baraat linavyoonyesha. Mtume alimpa Abu Bakr baadhi ya aya za Sura hii na akamwagiza akazisome kwa watu wakati wa Hija. Mara Malaika Jibril alitokea mbele ya Mtume na akamwambia kwamba ni mapenzi ya Allah kwamba jambo la Qurani tukufu linapaswa kupelekwa ama na Mtume mwenyewe, au mtu ambaye anatokana naye. Ali alikuwa anafanana na Mtume katika wajibu wake kama Muakala wa Allah. Mtume Mwenyewe alisema: Nimeamrishwa na Allah nitangaze hivi kwenu. Kisha akakamata mkono wa Ali na kusema: Jueni nyote, yule ambaye ni mimi ni Maula kwake (yaani, ambaye mimi ni mwenye kutawalia mambo yake). Ali vilevile ni Maula (Bwana) wake. Aidha, nafsi ya Ali imetangazwa kuwa ni nafsi ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Aya ya kuapizana (Mubahila) inasema:
Watakaokuhoji katika haya baada yakukufikia ilmu hii waambie: Njooni tuwaite
93
Mikesha ya Peshawar
watoto wetu na watoto wenu, na wanawake zenu na wanawake zetu, na nafsi zetu na nafsi zenu, kisha tuombe kwa unyenyekevu tutake laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie waongo. (Al-Imran; 3: 61) Tukirudi kwenye wakati ule ndani ya Msikiti, wakati Ali alipompa masikini pete yake na Mtume akamuomba Allah, akimuomba Yeye amfanye Ali kuwa mshirika wake katika Utume wake. Kisha Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akaomba: Ya Allah! Mimi ni Muhammad, mchaguliwa Wako na Mtume Wako. Kifungulie kifua changu. Na nifanyie wepesi kazi yangu na unichagulie msaidizi kutoka kwenye familia yangu, Ali. Imarisha mgongo wangu kupitia kwake. Abu Dharr amesimulia: Kwa jina la Allah! Dua ya Mtume ilikuwa haijafikia mwisho, Malaika Jibril akatokea na kumfunulia Aya hii: Hakika rafiki yenu mlinzi ni Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na walioamini, ambao wanadumisha Swala na kutoa Zaka huku wakiwa wamerukuu. (5: 55) Dua ya Mtume ilikubaliwa, na Ali aliteuliwa kama waziri wake. Muhammed bin Talha Shafii, katika Matalibus-Suul, uk. 19, amelishughulikia suala hili kwa urefu. Juu ya hayo, Hafidh Abu Nuaim Isfahan katika Manaqatul-Mutaharin, Sheik Ali Jafar katika Kanzul-Barahin, Imam Ahmad Bin Hanbal katika Musnad, Seyyed ShahabudDin katika Tauzihud-Dalail, Jalalud-Din Suyuti katika Durrul-Mansur, na wanachuo wenu wengine mashuhuri wa madhehebu yenu wameisimulia hii katika vitabu vyao. Baadhi yao wamesimulia kutoka kwa Asma bint Umais (Mke wa Abu Bakr), na baadhi kutoka kwa masahaba wengine. Ifuatayo imesimuliwa na Abdullah Ibn Abbas. Mtume alitushika mikono mimi na Ali. Alisali rakaa nne, na akiwa amenyoosha mikono yake Mbinguni, akasema: Ya Allah! Musa mtoto wa Imran, alikuomba umteulie msaidizi na kuifanya nyepesi kazi yake. Mimi ni Muhammad. Nakuomba ufungulie kifua changu na uifanye nyepesi kazi yangu. Ufanye ulimi wangu kuwa fasaha ili watu wapate kuelewa maneno yangu. Niteulilie msaidizi kutoka kwa familia yangu, Ali. Niimarishe mgongo wangu kupitia kwake, na mshirikishe pamoja nami katika kazi yangu! Nilisikia sauti ikisema: Ewe Muhammad! Nimelikubali ombi lako. Kisha Mtume akamshika Ali mkono na akasema: Nyanyua mikono yako kuelekea juu mbinguni na umuombe Allah ili kwamba ajaalie kitu juu yako. Ndipo Ali akanyanyua mikono yake juu na kusema: Ya Allah! Niahidi mimi kwa upande wako kwamba utanichukuwa mimi katika upendo Wako. Mara Malaika Jibril akatokea na kuleta Aya ifuatayo katika Suratul-Mariam:Hakika wale waliomini na wakatenda mema, Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehma atawajaalia mapenzi Yake juu yao. 19: 96 Wakati masahaba wa Mtume waliposhangazwa na hili, Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akasema: Kwa nini mnashangaa? Qurani Tukufu ina vigawanyo vinne: Robo moja inatuhusu
94
Mikesha ya Peshawar
sisi Ahlul-Baiti, robo moja inahusiana na mambo ya halali; robo moja ni kwa ajili ya mambo ya haramu; na robo moja inahusu maagizo na Sheria. Naapa kwa jina la Allah kwamba, kuna Aya nyingi katika Qurani ambazo zimeshushwa kwa kumsifu Ali. Sheikh: Hata kama hadith hii itachukuliwa kama ni Sahih, haiashirii cheo maalum kwa Ali. Hadith hiyo hiyo imesimuliwa kuwahusu Khalifa Abu Bakr na Khalifa Umar. Qaza bin Suwaid amesimulia kutoka Ibn Malika ambaye anamnukuu Ibn Abbas akisema kwamba, Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alisema; Abu Bakr na Umar wako kwangu mimi kama alivyokuwa Harun kwa Musa. Muombezi: Yakupasa uangalie tabia za baadhi ya wasimuliaji wenu (wa hadith). Wakati mwingine unahoji kutokana na similizi za Amadi na wakati mwingine kutoka kwenye zile za yule mwongo mwenye sifa mbaya na mzushaji; Qaza bin Suwaid, pamoja na kwamba mualamaa wenu mashuhuhuri wamempuuza. Allama Dhahabi, katika Mizanul-ltidal, katika maelezo ya habari za Qaza bin Suwaid na Ammar bin Harun, wanaipuuza hadith hii na kusema kimkato tu: Huu ni uwongo. Wakati Maulamaa wenu wanampuuza Qaza, hadith anazosimulia inapasa zipuuzwe. Linganisha Hadith hii ya Qaza bin Suwaid na Sanad ya Hadith ambayo nimenukuu kutoka kwa maulamaa wenu mashuhuri mno wa madhehebu yenu na uamue mwenyewe ni hadith ipi unaikubali.
95
Mikesha ya Peshawar
Khalifa wake na mrithi. Vivyo hivyo, Mtume wa mwisho, ambaye dini yake ni kamili zaidi, alikuwa na sababu kubwa zaidi za kuwalinda watu wake kutokana na machafuko ya dhamira zao huru. Alihifadhi Sheria ya dini ili kwamba isije ikapitia katika mikono ya watu wasio na ujuzi, wale ambao wangeweza kuigeuza kwa mujibu wa matamanio yao. Watu wasio na ujuzi wangetegemea juu ya kukisia kwao na kusababisha migawanyiko katika mambo ya Sheria. Hivyo, katika hadith hii tukufu Mtume anasema Ali yuko kwangu mimi kama alivyokuwa Harun kwa Musa, akithibitisha kwamba Ali alishikilia viwango vile vile vya daraja na mamlaka, sawa kama Harun alivyokuwa. Ali alikuwa bora kwa Umma wote na kwa ajili hiyo Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akamchagua kuwa msaidizi wake na mrithi wake. Hafidh: Uliyosema kuhusu Hadith hii hayana ubishani. Lakini kama utaangalia jambo hili kwa uangalifu, utakubali kwamba hadith hii haina maana ya jumla. Maana yake imekomea kwenye Vita vya Tabuk wakati Mtume alipomteua Ali kuwa Khalifa wake kwa muda maalum.
96
Mikesha ya Peshawar
(Makka na Madina kati ya Masahaba) imesimuliwa pia katika sehemu nyingine nyingi. Kwa hiyo, hadith hii sio ya kutafsiriwa katika maana ya kukomea yenye mipaka au kwa tukio moja makhususi tu. Maana yake ya jumla ni jambo lililothubutu. Ni kupitia Hadithi hii ambapo Mtukufu Mtume alitangaza katika matukio yanayostahili umakamu wa Ali baada yake. Moja ya matukio hayo lilikuwa lile la vita ya Tabuk. Hafidh: Inawezekana vipi Masahaba wa Mtume waliisikia Hadith hii katika maana yake ya jumla, wakijua kwamba ilikuwa na maana ya kwamba umakamu wa Ali uliridhiwa na Mtume na bado baada ya kifo cha Mtume, wakawa maadui na wakamkubali mtu mwingine kuwa Khalifa? Muombezi: Nina marejeo mengi ya kuunga mkono jibu langu kwa swali lako, lakini majibu mazuri zaidi kwa wakati huu ni kuiangalia mitihani ya Harun katika hali inayqfanana kama hii hii. Qurani inaeleza kwamba, wakati Musa alipomteua Harun kuwa makamu wake, aliwakusanya mbele yake Bani-Israil (kwa mujibu wa baadhi ya taarifa watu 70,000 walikusanyika). Musa alisisitiza kwamba, wakati wa kutokuwepo kwake yawapasa kumtii Harun, Khalifa na makamu wake. Kisha Musa alikwenda juu mlimani kuwa peke yake na Allah. Kabla ya mwezi kupita, Samiri alichochea fitna miongoni mwa Bani Israil. Alitengeneza ndama (wa ngombe) wa dhahabu na Bani Israil wakiwa wamemuacha Harun, walikusanyika mbele ya msaliti Samiri katika idadi kubwa. Ilikuwa ni muda mfupi tu umepita kabla ya tukio hili, Bani Israil, hawa hawa walimsikia Musa akisema kwamba wakati wa kutokuwepo kwake Harun atakuwa Khalifa wake na kwamba yawapasa kumtii. Hata hivyo watu 70,000 walimfuata Samiri. Nabii Harun kwa nguvu sana alipinga kitendo hiki na kuwakataza wasijiingize katika matendo hayo ya dhambi, lakini hakuna hata mmoja aliyemsikiliza. Aya ya Sura ya Araf inaeleza kwamba, wakati Musa aliporudi, Harun alimwambia: Ewe mtoto wa mama yangu! Hakika watu hawa wameniona mimi mnyonge na walikuwa karibu waniuwe. (7: 150)
97
Mikesha ya Peshawar
Yeye (Harun) akasema: Ewe Mtoto wa Mama yangu! Hakika watu hawa waliniona mimi mnyonge na walikuwa karibu waniuwe (7: 150). Nawab: Wakati Umakamu wa Ali ulikuwa umethibitishwa, kwanini Mtume atumie maneno ambayo yalidokezea hiyo maana tu? Kwa nini hakutangaza wazi kwamba Ali alikuwa ndiye makamu wake, ili kwamba kusiweze kuja kutokea pingamizi lolote baada yake? Muombezi: Nilikuambieni kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alielezea ukweli katika njia zote. Hili liko dhahiri kutoka vitabu vyenu, ambavyo vimeandika hadith nyingi mno kuhusiana na suala hili. Watu wasomi wanaelewa kwamba kidokezo ni chenye nguvu sana kuliko maelezo ya vivi hivi tu, hususan pale kidokezo hicho kikiwa chenye mzizi wa kina mno kiasi kwamba kina maana nyingi sana ndani yake Nawab: Umesema kwamba kuna Hadith nyingi za wazi zilizoandikwa na Maulamaa wenu zinazohusu umakamu wa Ali. Tafadhali, je unaweza kutuelezea zaidi kuhusu hili? Tunaambiwa kwamba hakuna hadith ambayo inathibitisha Umakamu wa Ali. Muombezi: Ziko hadith nyingi zinazohusu Ukhalifa katika vitabu vyenu wenyewe vya uhakika.
98
Mikesha ya Peshawar
99
Mikesha ya Peshawar
Carlyle katika kitabu chake Heroes and Hero-worship ametoa maelezo ya kina juu ya karamu iliyofanyika nyumbani kwa Abu Talib. Baada ya maelezo ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), Ali alisimama na akabainisha imani yake kwa Mtume. Kwa ajili hiyo Ukhalifa uliwekwa juu yake. Waandishi wengine wa Ulaya wamethibitisha jambo hili, wakiwa ni pamoja na George Sale wa Uingereza na Hashim, Mkristo wa Syria katika kitabu chake Maqalatul-Islam, na Bw. John Davenport katika kitabu chake Muhammad and the Quran. Wote wanakubali kwamba mara tu baada ya tangazo la Utume wake, alimuita Ali Ndugu yake, Msaidizi, Makamu na Khalifa wake. Aidha, Hadith nyingi zinathibitisha kwamba Mtume alisisitiza jambo hili katika matukio mengine mengi.
100
Mikesha ya Peshawar
(5) Katika Mawadda hiyo hiyo, ananukuu hadith kutoka kwa Anas bin Malik, ambayo nimeitaja mapema. Kuelekea mwisho wake anasema kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) amesema; Yeye (Ali) ni Makamu wangu na Msaidizi. (6) Muhammad bin Ganji Shafii ananukuu Hadith kutoka kwa Abu Dharr Ghifari katika Kitabu chake, Kifayatut-Talib kwamba Mtume amesema: Bendera ya Ali, Kiongozi wa Waumini, Kiongozi wa watu wenye nyuso zenye kungara, na Makamu wangu, itakuja kwangu katika chemchem ya Kauthari. (7) Baihaqi, Khatib Khawarizmi, na Ibn Maghazili Shafii wanaandika katika Manaqib zao kwamba alisema kumuambia Ali: Sio sawasawa kwamba mimi niondoke kuwaacha watu bila ya wewe kuwa Makamu wangu kwa vile wewe ndiye bora zaidi wa Waumini baada yangu. (8) Imam Abu Abdur-Rahman Nisai mmoja wa Maimam wa vitabu sita (Siha) vya hadith, anasimulia kwa urefu kutoka kwa Ibn Abbas fadhila za Ali kuhusiana na hadith Na. 23 katika Khasaisul-Alawi. Baada ya kuelezea cheo cha Mtume Harun, Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akasema kumwambia Ali: Wewe ni Makamu wangu baada yangu kwa kila Muumini. Hadith hii na nyingine ambazo Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) ametumia maneno baada yangu zinathibitisha wazi kwamba Ali alikuwa ndiye mrithi wa mara tu. (9) Kuna Hadith ya Uumbwaji, ambayo imesimuliwa katika njia mbalimbali. Imam Ahmad Ibn Hanbal katika Musnad yake, Mir Seyyed Ali Hamadani katika Mawadda-tul-Qurba, Ibn Maghazili Shafii katika Manaqib, na Dailami katika Firdaus wamemnukuu Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akisema: Mimi na Ali tumeumbwa kwa Nuru Takatifu moja miaka 14,000 kabla Nabii Adam hajaumbwa. Kutoka kwenye mgongo wa Adam na kupitia kizazi chake kitukufu, Nuru hiyo ilirithiwa na Abdul-Muttalib, na kutoka kwake iligawanywa na kurithiwa na Abdullah (baba yake Mtume) na Abu Talib (baba yake Ali). Mimi nilipewa Utume, na Ali alipewa Ukhalifa. (10) Hafiz Abu Jafar Muhammad bin Jarir Tabari (amekufa 310 A.H.) anaandika katika kitabu chake Kitabul-Wilaya kwamba Mtume amesema mwanzoni mwa khutuba yake maarufu pale Ghadir Khum; Malaika Jibril amenifikishia amri ya Allah kunitaka kwamba nisimame sehemu hii na kuwajulisha watu kwamba Ali bin Abu Talib ni ndugu yangu, wasii wangu, na Khalifa wangu baada yangu. Enyi watu! Allah amemfanya Ali kuwa Walii (mlezi) wenu, na Imam (kiongozi). Utii kwake ni wajibu juu ya kila mmoja wenu; amri yake ni yenye mamlaka ya juu; maneno yake ni kweli tupu; laana iwe juu yake yule ambaye anampinga, rehma ya Allah iwe juu ya yule ambaye amemfanya rafiki.
101
Mikesha ya Peshawar
(11) Sheikh Suleyman Balkhi katika Yanabiul-Mawadda anaelezea kutoka katika kitabu cha Manaqib cha Ahmad, na yeye kutoka kwa Ibn Abbas, hadith inayoelezea fadhila nyingi za Ali. Ninainukuu yote hapa. Ibn Abbas anasimulia kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) amesema: Ewe Ali! Wewe ni Mchukuzi wa Elimu yangu, Walii na rafiki yangu, Wasii wangu, Mrithi wa elimu yangu na khalifa wangu. Wewe ndiye mdhamini wa urithi wa Mitume wote waliotangulia. Wewe ni msiri wa Allah katika ardhi hii na hoja ya Allah kwa viumbe wote. Wewe ni nguzo ya Iman na mlezi wa Uislam. Wewe ni taa katika giza; nuru ya muongozo, na kwa ajili ya watu wa ulimwengu wewe ni bendera iliyonyanyuliwa juu kabisa. Ewe Ali! Yeyote akufuatae wewe atakuwa ameokolewa; yule ambaye hakutii wewe ataangamia; wewe ni njia ingaayo, na iliyonyooka; wewe ni Kiongozi wa watu wasafi, na Kiongozi wa Waumini; kwa yeyote yule ambaye mimi ni mwenye kutawaliwa mambo (Maula) wake wewe pia ni maula (bwana) kwake; na mimi ndiye Maula (Bwana) wa kila muumini; (Mwanaume na Mwanamke). Ni rafiki yako tu yule aliyezaliwa katika ndoa halali. Allah hakunipeleka mbinguni kuzungumza Naye bila kuniambia, Ewe Muhammad! fikisha salamu zangu kwa Ali na muambie kwamba ni Imam wa rafiki zangu na nuru ya waabuduo! Hongera Ewe Ali, juu ya ubora huu wa ajabu. (12). Abu Muayyid Muwafiqud-Din, msemaji mzuri wa Khawarizm, katika kitabu chake Fadhaill-Amirul-Muminin, kilichochapishwa mwaka 1313 A.H., Sura ya 19 uk. 240, ananukuu nyanzo ambavyo vimesimulia kwamba Mtume amesema: Wakati nilipofika Sidratul-Muntaha (Kituo cha juu sana wakati wa Mirraji) nilisemeshwa hivi: Ewe Muhammad! Wakati ulipowajaribu watu, ni yupi uliyemuona mtiifu zaidi. Nikasema Ali! Kisha Allah akasema: Umesema kweli Muhammad! Tena akaendelea kusema: Umechagua Makamu ambaye atafikisha elimu yako kwa watu, na kuwafundisha waja wangu kutoka Kitabu Changu yale mambo ambayo hawayajui? Nikasema, Ewe Allah! Yoyote utakayemchagua Wewe, nami nitamchagua. Yeye akasema: nimekuchagulia Ali juu yako. Ninamfanya yeye Makamu na Wasii wako. Na akampamba Ali na elimu Yake na uvumilivu. Yeye ni Kiongozi wa Waumini ambaye hakuna hata mmoja anayeweza kuwa sawa naye katika cheo miongoni mwa watangulizi wake au warithi wake. Kuna hadith nyingi kama hizi katika vitabu vyenu Sahih. Baadhi ya Maulamaa wenu waadilifu, kama Nizzam Basri, wameukubali ukweli huu. Salahud-Din Safdi katika kitabu chake Wafa-Bil-Wafiyya, kuhusiana na maelezo ya Ibrahim bin Sayyar bin Hani Basri, ajulikanae kama Nizzam Mutazali, anasema: Mtukufu Mtume wa Allah (s.a.w.w.) alithibitisha Uimama wa Ali na akamchagua kuwa Imam. Masahaba wa Mtume walikuwa na habari kamili juu ya hili, lakini Umar kwa ajili ya Abu Bakr, aliufunika Uimamu wa Ali kwa pazia.
102
Mikesha ya Peshawar
Ni wazi kutoka katika vitabu vyenu, hadith na tafsiri za Qurani kwamba Ali alishika nafasi ya juu sana ya ubora. Khatib Khawarizmi anasimulia kutoka kwa Ibn Abbas katika Manaqib, Muhammad bin Yusufu Ganji Shafii katika kitabu chake Kifayatut-Talib, Sibt Ibn Jauzi katika Tadhkira yake, Ibn Sabbagh Maliki katika Fusulul-Mawadda, Suleiman Balkhi Hanafi katika Yanabiul-Mawadda na Mir Seyyed Ali Hamadani katika Mawaddatul-Qurba, Mawadda ya 5, nakala kutoka kwa Khalifa wa Pili, Umar bin Khattab wote wakithibitisha pamoja na tofauti kidogo tu ya maneno kwamba Mtume alisema: Kama miti yote ingelikuwa ni kalamu, kama bahari ingelikuwa ni wino, kama majini wote na watu wangekuwa waandishi - hata hivyo sifa za Ali bin Abu Talib zisingeweza kuorodheshwa zote.
TABIA ZA MASAHABA.
Sheikh Abdus-Salam: (Akimgeukia Hafidh Muhammad Rashid Sahib). Niruhusu niseme kitu kwa ufupi. (Akigeuka kumwangalia Muombezi). Kamwe hatuzikatai sifa za hali ya juu za Ali, lakini kuweka mipaka ya utukufu kwake peke yake sio sawa, kwa vile Masahaba wakubwa wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) walikuwa kila mmoja, ni watu wa uadilifu. Unajiingiza katika mazungumzo ya upande mmoja, ambayo yanawapoteza watu. Niruhusu kunukuu hadith moja juu ya sifa zao ili ukweli juu ya jambo hili uweze kudhihirishwa. Muombezi: Mimi sijishughulishi na mambo na watu, Aya za Qurani tukufu na hadith sahihi zinatuelekeza katika muelekeo mmoja. Ninaapa kwa Jina la Allah kwamba mimi simpendi au kumchukia yeyote kimbumbumbu. Ninawaomba wasikilizaji kunisimamisha kama wakati wowote nitakimbilia njia yoyote ambayo ni kinyume na hoja au busara. Hadithi zinazokubaliwa na madhehebu zote ziwe ndio za kutegemewa. Sizikatai sifa nzuri za masahaba waadilifu wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), lakini yatupasa kutafuta miongoni mwao mmoja ambaye ni bora juu ya umma wote. Mjadala wetu sio wa kuhusu watu wema kwa kuwa wema ni wengi. Yatupasa kutafuta ni yupi aliyekuwa na sifa bora zaidi baada ya Mtume ili kwamba tuweze kumfuata yeye. Sheikh: Unaleta vikwazo visivyo muhimu. Katika vitabu vyenu hakuna hata hadith moja yenye kuwasifu makhalifa. Tutahojiana vipi juu ya msingi huo? Muombezi: Katika usiku wa kwanza wa majadiliano yetu, utakumbuka kwamba Hafidh Sahib mwenyewe aliukubali mjadala juu ya masharti kwamba hoja zetu zitegemee juu ya Aya za Qurani na juu ya Hadith zinazokubaliwa na Madhehebu zote. Kwa vile ninavyo vitabu vyenu Sahih, mimi nilikubali sharti hili. Kama ambavyo nyote mtathibitisha, sijatoka katika msimamo huo. Katika kuunga mkono hoja zangu nimesoma Aya za Qurani tu na Hadith zilizoandikwa katika vitabu Sahih vya Maulamaa wenu mashuhuri. Wakati
103
Mikesha ya Peshawar
mlipoweka sharti hili, hamkujua kwamba mtakuja kunaswa baadae. Hata hivyo, bado sitaki sharti hili lichukuliwe kikamilifu moja kwa moja. Niko tayari kusikiliza hadith zenu za upande mmoja kama ni Sahih. Kisha tutaweza kuyaamua mambo kwa haki. Mimi sina kusita katika kuukubali ukweli kwenye kulinganisha fadhail za Ali. Sheikh: Umetaja hadith inayohusu umakamu wa Ali lakini ukasahau ukweli kwamba kuna hadith nyingi kuhusu Abu Bakr. Muombezi: Kwa kuzingatia akilini kwamba Maulamaa wenu wakubwa, kama vile Dhahabi, Suyuti na Ibn Abil-Hadid wameelezea kwamba Amawi - wafuasi wa Muawiyya na wa Abu Bakr wamebuni hadith nyingi katika kumtukuza Abu Bakr, unaweza kutaja hadithi moja kutoka miongoni mwa nyingi ya hizo ili kwamba mtu muadilifu aweze kuamua juu ya usahihi wake.
104
Mikesha ya Peshawar
motoni. Wakati hadithi inaposimuliwa kwenu kwa niaba yangu ni lazima muipime na Qurani. Hadith nyingine inayokubaliwa na Madhehebu zote, imesimuliwa na Imam Fakhrud-Din Radhi katika Tafsir Kabir Jz. 2, uk. 271 anasimulia kwamba Mtume amesema: Wakati hadith kutoka kwangu inapoelezewa kwenu, iwekeni mbele ya Kitabu cha Allah kama ikikubaliwa na Qurani Tukufu, ikubalini. Vinginevyo, ikataeni. Vitabu vya maulamaa wenu wenyewe mashuhuri vinaeleza kwamba mmoja wa wale ambao walighushi hadith kwa jina la Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), alikuwa huyu mtu aliyekataliwa, Abu Huraira, ambaye umemuita mchamungu. Sheikh: Sikutarajia mtu wa kiwango chako kusema maneno ya kuzua kuhusu masahaba wa Mtume. Muombezi: Unataka mimi nitishwe na neno Sahaba, lakini umekosea kama unafikiri neno Sahaba lazima libebe heshima. Kweli usahaba na Mtume unaongezea fadhila za mtu, lakini hili hutegemea juu ya sharti kwamba Sahaba huyo ni mtiifu kwa Mtume. Kama anakwenda kinyume na maelekezo ya Mtume, basi kwa hakika atakataliwa. Je, Munafiqina (wanafiki) hawakuwa miongoni mwa Masahaba wa Mtume? Ndiyo, walikuwemo, na wote walilaaniwa. Sheikh: Haikuthibishwa kwamba walikataliwa. Kama walikataliwa ni uthibitisho gani kwamba watakwenda motoni? Je, kila mtu aliyekataliwa au kulaaniwa atakwenda motoni? Mtu aliyelaaniwa ni yule ambaye kwa mujibu wa Sheria ya wazi ya Qurani Tukufu, au Hadith ya Mtume ametangazwa hivyo (kuwa atakwenda motoni).
105
Mikesha ya Peshawar
kubembeleza hisani za Muawiya, hakuwa wa kulaaniwa. Kama mtu si tu hanyamazi aonapo matendo maovu ya Muawiya, bali hushirikiana naye hasa na humsaidia ili kuendeleza nafasi yake mwenyewe ya kilimwengu na kujaza tumbo lake, hivi huyo sio mtu wa kulaaniwa? Abu Huraira huyo huyo mwenyewe anasimulia (kama ilivyoandikwa na Maulamaa wenu mashuhuri, kama Hakim Nishapuri katika Mustadrak, Jz. 2, uk. 124, Imam Ahmad bin Hanbali, Tibrani, na wengine), kwamba Mtume amesema: Ali yu pamoja na Qurani na Qurani iko pamoja na Ali. Viwili hivi havitatengana mpaka vinifikie katika Chemchem ya Kauthar. Ali anatokana na mimi na mimi ninatokana na Ali. Yule ambaye anamtweza Ali, hunitweza mimi. Yule ambaye hunitweza mimi, anamtweza Allah. Muawiya katika hutuba zake za Sala ya Ijumaa alimlaani Ali, Hasan, na Husein. Aliagiza kwamba katika mikusanyiko yote, watu hawa watukufu sharti walaaniwe. Hivyo kama mtu kiukamilifu amejishirikisha na watu walaanifu kama hawa na yu aridhia matendo yao, huyu si wa kulaaniwa? Na wakati anashirikiana na watu hawa, kama huwasaidia kwa kughushi hadith na kulazimisha watu watoe laana dhidi ya watu watukufu, huyu si wa kulaaniwa? Sheikh: Je, ni busara kwetu sisi kukubali masingizio haya, kwamba masahaba waaminifu wa Mtume, wanaghushi hadith na waweze kuwalazimisha watu wamlaani Ali? Muombezi: Kwa kweli ni vigumu kuamini kwamba sahaba mwaminifu angeweza kufanya kitu kama hicho. Kama yeyote katika Masahaba amefanya kitu kama hicho, ina maana kwamba hakuwa muaminifu. Kuna Hadithi nyingi zilizosimuliwa na Maulamaa wenu wenyewe kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) amesema: Yule ambaye anamtweza Ali, hunitweza mimi na Allah. Sheikh: Kwa kuwa mkweli, wakati unawasingizia masahaba wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), kusema kwamba, walighushi hadith, vipi tunaweza kutumaini kwamba hutahusisha maarubu mabovu kwa Maulamaa wa vyeo vya juu wa Kisunni? Ninyi Mashia mna tabia inayofahamika ya kuwakashifu watu maarufu. Muombezi: Huna haki katika kuhusisha vitu kama hivyo kwetu. Historia ya Uislamu ya miaka 1400 iliyopita inathibitisha kinyume chake. Kuanzia mwanzo wa karne ya kwanza ya Uislamu, Bani Umayya wamewatukana Maimam Maasum, dhuria wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), na wafuasi wao Mashia. Hata leo, maulamaa wenu mashuhuri wanasimulia hadith za kashfa dhidi ya Mashia katika vitabu vyao ili kuwapoteza watu. Sheikh: Ni ulamaa gani wa Sunni aliyewakashifu Mashia?
106
Mikesha ya Peshawar
107
Mikesha ya Peshawar
sababu hii kwamba waandishi wa vitabu vya Sahih (Sihah Sita) hawakuingiza katika vitabu vyao Hadith zilizosimuliwa na wao. Katika Juz. ya 10, uk. 23 anasema kwamba, Mashia wanaamini katika misingi minne ya dini - Tauhidi, Adili, Nubuwat na Uimam. Kwa kweli katika vitabu vya itiqad vya Shia, vinavyopatikana kila mahali, imeandikwa kwamba itiqad ya Shia ina misingi mitatu: Tauhid, Nubuwat, na Maad (Siku ya malipo); Adil ni sehemu ya Tauhid na Uimam ni sehemu ya Nubuwat. Katika juzuu ya 1, Uk. 131, anaeleza kwamba Mashia hawakusanyiki misikitini. Hawasali Sala ya Ijumaa au Sala za jamaa. Kama wakisali wanasali kila mtu peke yake. (kicheko miongoni mwa Mashia). Lakini kwa hakika tunaweka mkazo mkubwa katika Sala za jamaa. Katika miji mingi ya Iraq na Iran, ambayo ni vituo vya Mashia, misikiti yetu inajaa watu wanaoabudu wakisali sala za Jamaa. Katika ukurasa huohuo, anaandika kwamba Mashia hawafanyi Hijja kwenye Al-Kaaba. Hija yao ni ya kuzuru makaburi tu, ambayo wanaiona ni bora kuliko kwenda kuhiji Makka. Wanawalaani wale ambao hawafanyi Ziara kwenye makaburi. (kicheko). Vitabu vya dua vya Shia vina Sura maalum kwa ajili ya dua za hijja unaoitwa Kitabul-Hajj. Wanatheolojia wa Kishia, wameandika vitabu vingi wakielezea kanuni kwa ajili ya Hijja, ambamo maelekezo maalum yametolewa kutekeleza taratibu za Hijja. Hadithi nyingi kutoka kwa Maimamu wetu zinasisitiza kwamba, kama Muislamu (Shia au Sunni) anao uwezo na bado akashindwa kutekeleza Hija anatengwa katika Uislamu. Wakati akifa anaambiwa: Kufa kifo chochote unachoweza, kiwe kifo cha kiyahudi, Kikristo, au cha muabudu moto. Unaweza kuamini kwamba mbele ya maelekezo kama hayo Mashia wangejiepusha na kutekeleza Hija? Kwa nyongeza juu ya tafsiri hizi potovu, mtu huyu muovu amesema kwamba mwanachuo mkubwa wa Kishia, Muhammad bin Muhammad bin Numan (Sheikh Mufid) ameandika Manasikhul-Hajj lil-Mashahid. Jina sahihi la kitabu hicho ni Mansikhuz-Ziarat, ambacho kinapatikana kila mahali na ambacho kina maelekezo kuhusu kuzuru sehemu za Ziarat, pamoja na Ma-Kuba matukufu ya wastahiki Maimamu. Kama utaviangalia vitabu hivi vya Ziarat, utaona kwamba kutembelea kwenye makaburi ya Mtukufu Mtume na Maimamu kunapendekezwa, sio wajibu. Uthibitisho mzuri dhidi ya tuhuma za mtu huyu mtovu wa dini ni mwendo unaofuatwa na Mashia, ambao huenda kuhiji kwa maelfu kila mwaka. Shutuma nyingine bandia ya muongo huyu, yaweza kupatikana katika juzuu ya 1, uk. 11, ambako anasema kwamba Mashia wanaita mbwa wao kwa majina ya Abu Bakr na Umar na kila siku wanawalaani (hao Abu Bakr na Umar). (Kicheko miongoni mwa Mashia). Hiki ni kichekesho. Kwa mujibu wa itiqad ya Shia, mbwa ni najisi kabisa. Nyumba ya Muislam yenye mbwa hukosa baraka za Allah. Kwa hiyo, Waislamu Mashia wanakatazwa kabisa kufuga mbwa
108
Mikesha ya Peshawar
isipokuwa kwa masharti makhususi (kuwinda, kuilinda nyumba, au kuchunga mbuzi). Moja ya sababu nyingi za kutopatana kati ya Yazid na mjukuu wa Mtume, Imam Husain, ilikuwa kwamba Yazid alikuwa mpenzi wa mbwa na akiwafuga bila kuwa na sababu nzuri. Ibn Taimiyya vilevile anaandika kwamba, kwa vile Mashia wanangojea kutokeza kwa yule wa mwisho wa Maimam wao, katika sehemu nyingi, hususan katika Sardab (Sakafu chini ya nyumba) ya Samara (ambako Mtukufu Imam alitoweka), ameandaliwa farasi kwa ajili yake. Wanamuita Imam wao ajitokeze, wakisema kwamba wamejiandaa kikamilifu kumtumikia Yeye. Vilevile anaandika kwamba Mashia hugeuka kuelekea upande wa mashariki wakati wa siku za mwisho wa Ramadhani na kumwita Imamu ajitokeze. Baadhi yao huacha hata Sala zao za faradhi; wakifikiri kwamba kama watajishughulisha na kusali Sala zao na Imam akajitokeza wangeweza kukosa kumtumikia kwao. (Kicheko kwa Sunni na Mashia). Hatushangazwi sana na Hadith za kuchekesha za mtu huyu muovu. Bali tunashangazwa na tabia za maulamaa wa sasa wa Misri na Damaskas ambao, bila kuwauliza Mashia ambao wanaishi nao, wanafuata upumbavu wa mtu kama Ibn Taimiyya. Itakuwa inachosha sana kutoa orodha ndefu ya riwaya zisizo sahihi za Ibn Hajar Makki, Hafidh, na Kadhi Ruzbahan. Vitabu yao vinajulikana, ingawa katika mtazamo wa usahihi, hivyo havina thamani. Kwa mfano Milal Wan-Nihal cha Muhamma Ibn Abdul-Karim Shahrastani (amekufa 548 A.H.), katika macho ya wanachuoni, hakina thamani hata kidogo. Mtu hataweza kuona chochote ndani yake isipokuwa itiqad bandia kabisa zilizohusishwa kwa Mashia, kama kumuabudu Ali na imani ya kuhama kwa roho (baada ya kufa kuingia katika mwili mwingine). Ni wazi hakuwa mtu mwenye elimu. Akiandika kuhusu Shia Ithnashariyya, yeye anasema kwamba, kaburi la Ali Ibn Hadi Muhamma Naqi, ambaye amekuja baada ya Imam Muhammad Taqi, liko Qum. Lakini hata watoto wadogo wanajua kwamba Kuba Tukufu la Imam Ali Naqi liko ubavuni mwa kuba la Mtoto wake, Imam Hasan Askari huko Samarra. Sidhani kwamba rejea nyingine zaidi za namna hii ni muhimu kuthibitisha kwamba ulamaa wa Kisunni wamebuni riwaya za uongo kuhusu Mashia. Na siko peke yangu katika kulenga shutuma dhidi ya uaminifu wa Abu Huraira. Maulamaa wa Kisunni wamefichua tabia zake mbaya katika vitabu vyao wenyewe.
109
Mikesha ya Peshawar
waliobuni hadith chafu dhidi ya Ali walikuwa Abu Huraira, Amr bin Aas, na Mughira Ibn Shaba. Akitoa maelezo juu ya ngano hizi, Ibn Abil-Hadid anasimulia kwamba, wakati mmoja Abu Huraira aliingia Msikiti wa Kufa na kuona kundi kubwa la watu ambao walikuja kumpokea Muawiya. Alipaza sauti yake kwenye lile kundi la watu: Enyi watu wa Iraq. Mnafikiri kwamba nitasema uongo katika kumpinga Allah na Mtume Wake na kujinunulia moto wa Jahanam? Sikieni kutoka kwangu nilivyosikia kutoka kwa Mtume. Kila Mtume ana Haram (Sehemu takatifu ya kuishi) na Haram yangu ni Madina. Mtu ambaye anahusika na uzushi katika mji wa Madina analaaniwa na Allah, na Malaika Wake, na pamoja na wanadamu wote! Naapa kwa jina la Allah, kwamba Ali alihusika na uzushi. (Yaani, Ali alichochea mfarakano miongoni mwa watu, hivyo, kwa mujibu wa Mtume, anapaswa kulaaniwa). Wakati Muawiya alipolifahamu hili (kwamba Abu Huraira amefanya kitu kama hicho kwa ajili yake na amekifanya katika makao makuu ya Ali, Kufa), alimuita, akampa zawadi, na akamfanya Gavana wa Madina. Je, matendo yake mabaya hayatoshi kuthibitisha kwamba anastahili laana? Je, ni sahihi kwamba mtu ambaye amemfanyia ubaya mbora zaidi wa Makhalifa achukuliwe kama mchamungu kwa sababu tu amewahi kuwa sahaba wa Mtume? Sheikh: Ni katika sababu zipi ambazo Mashia wanamuona kuwa kalaaniwa? Muombezi: Kuna hoja nyingi katika kuunga mkono maoni yetu. Mojawapo ya hizo ni kwamba, mwenye kumtukana Mtume, kwa mujibu wa madhehebu zote amelaaniwa. Kwa mujibu wa Hadith ambayo nimeitaja mapema, Mtukufu Mtume amesema: Mwenye kumtukana Ali, hunitukana mimi, Mwenye kunitukana mimi humtukana Allah. Ni dhahiri kwamba Abu Huraira alikuwa mmoja wa wale ambao, sio tu amemtukana Ali bin Abu Talib, bali ambaye alighushi hadith kuwachochea wengine kumtukana yeye.
110
Mikesha ya Peshawar
ya dhalimu huyu. Bani Umayya na wafuasi wao walitenda ukatili huu wa kiwendawazimu. Mpendwa wenu Abu Huraira alishuhudia unyama huu na hakuwa kimya tu, bali pia aliuunga mkono kikamilifu. Watu wasio na hatia kama Jabir bin Abdulla Ansari, na Abu Ayyub Ansari walitafuta pa kukimbilia. Hata nyumba ya Abu Ayyub Ansari ambaye alikuwa mmoja wa masahaba wakubwa wa Mtume, ilichomwa moto. Wakati Jeshi hili lilipoelekea Makka, Abu Huraira alibakia Madina. Sasa naomba mtueleze, kwa jina la Allah, iwapo mtu huyu mlaghai ambaye alikuwa katika usahibu wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) kwa miaka mitatu, na ambaye amesimulia zaidi ya Hadith 5,000 kutoka kwa Mtume, hakusikia hadithi zile mashuhuri zinazohusu mji wa Madina? Maulamaa wa madhehebu zote (kama Allama Samhudi katika Tarikhul-Madina, Ahmad bin Hanbal katika Musnad Sibt Ibn Jauzi katika Tadhkira uk. 163) wamenukuu kutoka Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) ambaye amesema mara kwa mara: Yule ambaye atawatishia watu wa Madina na mateso, atatishwa na Allah na atalaaniwa na Allah, Malaika Wake, na wanadamu wote. Allah hatakubali kitu chochote kutoka kwake. Na alaaniwe yule mwenye kuwatisha watu wa Madina. Kama mtu yeyote atawadhuru watu wa Madina, Allah atamyeyusha kama risasi katika moto. Sasa ni kwa nini Abu Huraira alijiunga na jeshi lile ambalo liliiangamiza Madina? Kwa nini alibuni hadith zenye upinzani kwa makamu sahihi wa Mtume? Na kwa nini aliwachochea watu kumtukana yule mtu ambaye kuhusu yeye Mtume amesema: Kumtukana yeye ni kunitukana mimi? Wewe amua iwapo kama mtu ambaye amebuni hadith kwa jina la Mtume hakuwa mwenye kulaaniwa? Sheikh: Umekosa huruma, sio vyema kwako kumwita Sahaba muaminifu mno wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) mtovu wa dini na mzushi.
111
Mikesha ya Peshawar
Tabaqat Jz. 4, uk. 90, Ibn Hajar Asqalani katika Isaba, na Ibn Abdi-e-Rabbih katika Iqdul-Farid Jz. 1, wanaandika kwamba Khalifa alisema: Wakati nilipokufanya Gavana wa Bahrain, ulikuwa huna hata kiatu katika miguu yako, lakini sasa nimesikia kwamba umenunua farasi kwa dinari 1,600. umeipataje mali hii. Alijibu, Hizi ni zawadi za watu ambazo faida yake imekuwa marudufu zaidi. Uso wa Khalifa uligeuka kuwa mwekundu kwa hasira, na alimpiga viboko kwa nguvu sana kiasi kwamba mgongo wake ulivuja damu. Kisha akaamuru zile dinari 10,000 ambazo Abu Huraira alizikusanya huko Bahrain zichukuliwa kutoka kwake na ziwekwe kwenye mfuko wa Baitul-Mal. Hii haikuwa mara ya kwanza kwa Umar kumchapa Abu Huraira. Muslim anaandika katika Sahih yake Jz. 1, uk. 34, kwamba wakati wa uhai wa Mtume, Umar bin Khattab alimpiga Abu Huraira kwa nguvu sana mpaka akaanguka chini. Ibn Abil-Hadid anaandika katika Sherhe yake ya Nahjull-Balagha Jz. 1, uk. 360: Abu Jafar Asqalani amesema: Kwa mujibu wa watu wetu mashuhuri (Yaani Wanachuoni), Abu Huraira alikuwa mtu muovu. Hadith zilizosimuliwa na yeye hazikukubaliwa. Umar alimchapa na kiboko na akamwambia kwamba alikuwa amebadilisha hadith na alihusisha maneno ya uongo kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Ibn Asakir katika kitabu chake Tarikh Kabir, na Muttaqi katika Kanzul-Umma wanasimulia kwamba Khalifa Umar alimchapa viboko, alimkemea na akamkataza kusimulia hadith kutoka kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Umar alisema: Kwa sababu unasimulia hadithi nyingi kutoka kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) una uwezo tu wa kuhusisha uongo kwake. - Yaani mtu anatazamia mtu muovu kama wewe kutoa uongo tu kuhusu Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Hivyo ni lazima uache kusimulia Hadith kutoka kwa Mtume; vinginevyo nitakupeleka katika nchi ya Dus. (Kabila katika Yemen ambalo kwamba Abu Huraira anatokana nalo). Ibn Abil-Hadid, katika Sherhe yake ya Nahjul-Balagha, Jz. 1, uk. 360 (iliyochapishwa Misri) anasimulia kutoka kwa mwalimu wake, Imam Abu Jafar Asqalini, kwamba Ali alisema: Jihadharini na muongo mkubwa miongoni mwa watu, Abu Huraira Dusi. Ibn Qutayba, katika Tawil-e-Mukhtaliful-Hadith, na Hakim katika Mustadrak Jz. 3, na Dhahabi katika Talkhisul-Mustadrak na Muslim katika Sahih yake, Jz. 2, wakielezea kuhusu tabia za Abu Huraira, wote wanasema kwamba Aisha alikuwa alipingana naye mara kwa mara na kusema: Abu Huraira ni muongo mkubwa ambaye hughushi hadith na kuzihusisha na Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Kwa ufupi sio sisi peke yetu ambao tumemkataa Abu Huraira. Kwa mujibu wa Khalifa Umar, Amirull-Muuminiina Ali, Ummul-Muuminina Aisha, na Masahaba wengine na wafuasi wa Mtume, wamesema kwamba alikuwa sio muaminifu kabisa. Kwa ajili hiyo, Masheikh wa madhehebu ya Mutazila na Maimam wao, na ulamaa wa Kihanafia kwa kawaida wanakataa hadith zilizosimuliwa na Abu Huraira. Aidha, katika Sherhe yake ya Sahih Muslim, Jz. 4, Nadwi anasisitiza nukta hii: Imam Abu
112
Mikesha ya Peshawar
Hanifa amesema: Masahaba wa Mtukufu Mtume kwa ujumla walikuwa ni wacha-Mungu na wanyofu. Ninaikubali kila hadith yenye ushahidi iliyosimuliwa na wao, lakini sizikubali hadith ambazo chanzo chake ni Abu Huraira, Anas Ibn Malik, au Samara bin Jundab. Tunamkataa Abu Huraira yule yule, ambaye Khalifa Umar alimchapa viboko na kumuita mwizi na muongo. Alikataliwa na Ummul-Muminina Aisha, Imam Abu Hanifa, na masahaba wengi na wafuasi wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Tunamkataa Abu Huraira huyo huyo ambaye alikataliwa na kuitwa muongo na Bwana wetu, kiongozi wa wenye kuabudu Mungu mmoja, Ali, na akakataliwa na Maimamu watukufu na dhuria wa Mtume. Tunamkataa Abu Huraira ambaye alikuwa muabudu tumbo, ambaye pamoja na kujua ubora wa Ali, alimpuuza. Alimpendelea mfadhili wake, mlaaniwa Muawiya, alikaa kwenye meza yake ya chakula na kula vyakula vitamu naye, na akatunga hadithi za kumpinga Ali. Kwa mtazamo wa mjadala wetu mpaka sasa, ninyi na mimi tunawajibika kuangalia kwamba wakati hadithi kutoka kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) ikiwa kwenye mjadala, yatupasa kwanza kuirejesha kwenye Qurani Tukufu. Kama hadith inakubaliana na Qurani, yatupasa kuikubali, vinginevyo la.
MAJIBU KWA HADITH IDHANIWAYO KWAMBA ALLAH ALISEMA, NIMERIDHISHWA NA ABU BAKR - JE NA YEYE AMERIDHIKA NA MIMI?
Hadithi ambayo umeisimulia mapema (ingawa ni ya upande mmoja) yaweza kurejeshwa kwenye Qurani Tukufu. Kama hakuna pingamizi, hapana shaka tutaikubalia. Hata hivyo, aya moja ya Qurani inasema: Na hakika tumemuumba mwanadamu, nasi tunajua yanayopita katika nafsi yake; nasi tukaribu naye zaidi kuliko mshipa wake wa shingo. (50:16) Mnatambua kwamba Hablul-Warid (mshipa wa shingo) ni usemi wa kawaida utumiwao kuelezea ukaribu uliozidi mno. Maana ya Aya hii ni kwamba, Allah ni Mjuzi wa yote. Hakuna kinachofichika kwake, hata kiwe ndani kiasi gani katika moyo wa mtu. Allah anajua siri za nyoyo zetu. Na katika Sura ya Yunus Anasema: Na hushughuliki katika kazi yoyote, wala hasomi humo (kitu chochote) katika Qurani, wala hamfanyi kitendo chochote, isipokuwa sisi tunakuwa mashahidi juu yenu mnaposhughulika nayo. Hakifichikani kwa Mola wako kitu chochote (hata) kilicho sawa na uzito wa mdudu chungu, la katika ardhi wala katika mbingu. Wala (hapana) kidogo kuliko hicho wala kikubwa, isipokuwa kimo katika kitabu (cha Allah) kielezacho (kila kitu). (10:61). Kwa mujibu wa Aya hizi, na kwa mujibu wa akili ya kuzaliwa, hakuna kinachofichikana kwa Allah. Anajua mtu anachofanya au kufikiri. Sasa linganisha hadithi hii na Aya hizi mbili na uone kama zinaweza kupatanishwa. Itawezekana vipi kwamba Allah Mwenye Nguvu zote asijue furaha ya Abu Bakr, kiasi kwamba Yeye mwenyewe awajibike kumuuliza kama ameridhishwa
113
Mikesha ya Peshawar
Naye au la? Akili ya kuzaliwa na Qurani Tukufu vinaonyesha kwamba Hadith hii ni ya uwongo.
114
Mikesha ya Peshawar
Muombezi: Kama utaichunguza kwa karibu zaidi Hadith hii inayotarajiwa, unaweza ukaona kwamba, mbali na ukweli kwamba ulamaa wenu wenyewe wameikataa, hadithi hii haiwezekani kuwa inatoka kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Kila mtu anajua kwamba pepo haitaingiwa na wazee. Hakuna mabadiliko ya kidogo kidogo huko. Kuna riwaya nyingi zinazokubaliwa na madhehebu zote zinazohusiana na jambo hili. Moja ya hizo ni suala la Ashjaiyya, mwanamke mzee ambaye alikuja kwa Mtume. Katika maongezi yake, Mtume alisema: Wanawake wazee hawataingia Peponi. Yule mwanamke alihuzunika sana na akasema, huku akilia: Ewe Mtume wa Allah, hii ina maana mimi sitaingia Peponi. Alipokwisha kusema hivi, akaondoka. Mtume akasema: Muambieni kwamba siku hiyo atakuwa kijana na ataingia Peponi. Kisha akasoma Aya ifuatayo kutoka kwenye Qurani Tukufu:
Hakika tumewafanya wakuwe katika umbo (jipya), na tumewafanya vijana kama kwamba ndiyo kwanza wanaolewa, wanapendana na waume zao (walio) hirimu moja na wao, kwa ajili ya watu wa kheri. (56: 35 38). Katika Hadithi nyingine inayokubaliwa na wote ninyi na sisi, Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alisema: Wakati wakazi wa Peponi watakapoingia Mbinguni, watakuwa vijana na nyuso safi halisi, nywele za kipilipili, macho ya haiba, umri wa miaka 33. Sheikh: Maelezo yako ni kweli kama yalivyo, lakini hii ni hadithi Makhususi (yaani maalumu kwa ajili ya Abu Bakr na Umar). Muombezi: Sielewi. Una maana gani kwa kusema Hadith Makhususi. Una maana kwamba Allah atapeleka kikundi cha wazee Peponi ili kwamba Abu Bakr na Umar waweze kuwa mabwana zao? Isitoshe, ulamaa wenu mashuhuri wanaiona Hadith hii kuwa ni ya kutungwa. Mtume ametupa utaratibu kwa ajili ya kuthibitisha Hadithi. Nilisema mapema kwamba Hadithi yoyote ambayo haipatani na Qurani ni ya kupuuzwa. Wanachuoni wetu sisi wanakataa Hadithi nyingi zinazodaiwa kutokana na Mtume na Maimamu Watukufu katika misingi ya kanuni iliyotamkwa na Mtukufu Mtume (s.a.w.w.): Wakati wowote itakapoelezwa Hadith kwamba inatoka kwangu, irejesheni kwenye Qurani Tukufu; kama inakubaliana nayo, ikubalini, vinginevyo, ikataeni. Kwa ajili hiyo, wanachuoni wetu hawakubali hadith ambazo hazikubaliani na Qurani Tukufu. Nilieleza mapema kwamba Maulamaa wenu wameandika vitabu juu ya kukataa Hadithi za kutungwa. Kwa mfano Sheikh Majdud-Din Muhammad bin Yaqub Firuzabadi katika SafarusSaada (uk. 142), Jalalud-Din Suyuti katika Kitabul-Luali, Ibn Jauzi katika Muzua, Muqaddasi katika Tadhkiratul-Muzua, na Sheikh Muhammad bin Darwish (Mashuhuli kwa jina la Hul-e-Beiruti) katika Asnal-Talib - wote wamesema kwamba nyororo ya wasimuliaji wa hadith isemayo kwamba Abu Bakr na Umar ni mabwana wa
115
Mikesha ya Peshawar
wazee wa peponi humchanganya Yahya bin Anbasa. Dhahabi anasema kwamba, huyu Yahya ni msimuliaji asiyeaminika, na Ibn Jan anashikilia kwamba Yahya alikuwa akitunga hadithi. Hivyo, mbali na hoja zangu zilizopita, hata Maulamaa wenu wanaiona kuwa ni hadithi ya uwongo. Kwa kweli, inawezekana kwamba ilitungwa na wafuasi wa Abu Bakr, familia ya Umayya. Ili kuwadhalilisha Bani Hashim na kizazi cha Mtume, walikuwa wakitunga Hadith sambamba na zile sahihi zilizosimuliwa kwa kuitukuza familia ya Mtume. Mtu kama Abu Huraira, ili kupata mwanya wa kuingia kwenye kundi maalum la kiutawala la Bani Umayya, mara kwa mara alighushi hadithi. Kwa sababu ya uadui wao kwa kizazi cha Mtume, walitunga hadithi sambamba na zile zinazokubaliwa na Maulamaa wote wa Shia na Sunni. Nawab: Ni Hadithi ipi inayokubaliwa katika suala hili?
116
Mikesha ya Peshawar
Sheikh: Lakini hebu angalia hadith hii, ambayo usahihi wake hakuna atakayeukataa. Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) amesema: Katika taifa lolote atakaloishi Abu Bakr, sio sahihi kwa mtu yoyote kufadhilishwa kuliko yeye. Hadithi hii inathibitisha kwamba Abu Bakr ni bora kwa Umma wote. Muombezi: Nasikitika kwamba unakubali hadith bila udadisi hata kidogo. Hadith hii ingelikuwa imesimuliwa na Mtume, yeye mwenyewe angetenda kwa mujibu wake. Lakini alitoa kipaumbele kwa Ali mbele ya macho ya Abu Bakr. Je, Abu Bakr hakuwepo wakati wa Mubahila pale ambapo Ali alichaguliwa kama nafsi ya Mtume? Katika vita vya Tabuk, wakati Abu Bakr mtu mzima na mzoefu zaidi alikuwepo, kwa nini Mtume akamfanya Hadhrat Ali naibu na Khalifa wake? Kwa nini Abu Bakr aliondolewa kwa amri ya Mungu na kupendelewa Ali, wakati mtu mzima huyu alipotumwa kwenda Makka kulingania Uislamu na kuzisoma Aya kutoka Sura ya tisa ya Qurani Baraat (Tawba)? Wakati Abu Bakr alikuwepo kwa nini Mtume alimchukua Ali kwenda pamoja naye Makka kuvunja Masanamu, akamfanya apande juu ya mabega yake, akimuamrisha avunje sanamu la Hubal? Kwa nini wakati Abu Bakr alikuwepo Mtume akamtuma Ali kwenda kuhubiri miongoni mwa watu wa Yemen? Mwisho, kwa nini Mtume akamfanya Ali kuwa Mrithi na Makamu wake badala ya Abu Bakr? Sheikh: Kuna hadithi yenye nguvu sana kutoka kwa Mtume ambayo haiwezi kupingwa. Imesimuliwa na Amr bin Aas ambaye amesema: Siku moja nilimuuliza Mtume. Ewe Mtume wa Allah! Ni nani unayempenda sana miongoni mwa wanawake? Akajibu: Aisha. Nikasema: Nani unayempenda sana miongoni mwa wanaume? Akajibu, Baba yake Aisha, Abu Bakr. Kwa vile Mtume amempendelea Abu Bakr juu ya watu wote, basi alikuwa mbora kwa umma wote. Ukweli huu wenyewe, peke yake ni uthibitisho wenye kuvutia zaidi wa kuonyesha uhalali wa ukhalifa wa Abu Bakr.
MAJIBU KWA HADITH INAYODHANIWA KWAMBA ABU BAKR NA AISHA WALIPENDELEWA ZAIDI NA MTUME.
Muombezi: Mbali na ukweli kwamba hadithi hii imetungwa na wafuasi wa Abu Bakr, haipatani na Hadith Sahihi ambazo zinakubaliwa na Madhehebu zote. Hadith hii inapasa kuangaliwa kwa mitazamo miwilii. Kutoka upande wa Ummul-Muminina Aisha na kutoka upande wa Abu Bakr. Mtume asingeweza kusema kwamba kati ya wanawake wote alimpenda Aisha zaidi. Nimekwisha sema tangu mwanzo kwamba hii inakinzana na Hadithi nyingi Sahihi zilizomo kwenye vitabu vyote vya Sunni na Shia. Sheikh: Ni hadithi zipi zinazopingana na riwaya hii?
117
Mikesha ya Peshawar
Muombezi: Kuna hadithi nyingi kuhusu Mama wa Maimamu; Fatima Zahra, zilizosimuliwa na Maulamaa wenu wenyewe, ambazo zinapingana na maelezo yako. Hafidh Abu Bakr Baihaqi katika Kitabu chake cha Tarikh, Hafidh Ibn Abdul-Bar katika Istiab, Mir Seyyid Ali Hamadani katika Mawaddatul-Qurba, na wengine miongoni mwa Maulamaa wenu, wamesimulia kwamba Mtume mara kwa mara amesema: Fatima ni mbora wa wanawake wote na wa umma wangu.. Imam Ahmad bin Hanbal katika Musnad, na Hafidh Abu Bakr Shirazi katika NuzululQurani Fi Ali anasimulia kutoka kwa Muhammad bin Hanafiyya, na yeye kutoka kwa Amirul-Muminina Ali, Ibn Abdul-Bar katika Istiab, katika maelezo juu ya Fatima, yaliyosimuliwa katoka kwa Ummul-Muminina Khadija, kutoka kwa Abdul-Warith Bin Sufyani na kutoka kwa Abu Dawud na Anas Bin Malik, Sheikh Sulaimani Balkhi Hanafi katika Sura ya 55 ya Yanabiul-Mawadda, Mir Seyyid Ali Hamadani katika Mawaddatul-Qurba, Mawadda ya 13 - hawa na wasimuliaji wengine wa Hadith wameelezea kutoka kwa Anas Bin Malik kwamba, Mtume alisema: Kuna wanawake wanne walioshinda wote wa ulimwengu: Mariam, bint wa Imran; Asiya, bint wa Mazahim; Khadija, bint wa Khalid; na Fatima, binti wa Muhammad. Khatib katika Tarikh Baghdad; anasimulia kwamba Mtume aliwatangaza wanawake hawa wanne kuwa ni wabora wa wanawake wote wa ulimwengu. Kisha akamtangaza Fatuma kuwa ni mbora wao wote ulimwenguni na Akhera. Muhammad bin Ismaili Bukhari katika Sahihi yake, na Imam Ahmad bin Hanbal katika Musnad yake wanasimulia kutoka kwa Aisha bint Abu Bakr kwamba Mtume alisema kumwambia Fatima: Ewe Fatima, ninakupa habari njema kwamba Allah amekufanya mbora wa wanawake wote duniani na amekufanya wewe kuwa ndiye mtakatifu zaidi wanawake wote wa Uislamu.. Vilevile Bukhari katika Sahihi yake, sehemu ya 4, uk. 64 Muslim katika Sahih yake Jz. 2, katika Mlango wa Fadhail za Fatima, Hamidi katika Jama Bainus-Sahihain yake, Abdi katika Jama Bainus-Sihahu-s-Sitta hawa na wengine wengi wamesimulia kutoka kwa Ummul-Muminiina Aisha kwamba Mtume alisema: Ewe Fatima! hufurahi kwamba wewe ni Bibi wa wanawake wote wa ulimwengu? Ibn Hajar Asqalani amenukuu maneno hayo hayo katika kitabu chake Isaba kuhusiana na maisha ya Fatima pamoja na maelezo: Wewe ni mbora wa wanawake wote wa ulimwengu. Vilevile, Bukhari, Muslim, Imam Ahmad Bin Hanbal, Tibrani na Sulaiman Balkhi Hanafi - wote wameiandika hadith hii.
118
Mikesha ya Peshawar
Sulaimani Balkh Hanafi katika Yanabiul-Mawadda, Sura ya 32 kutoka kwenye Tafsir ya Ibn Abi Hatim, Manaqib ya Hakim, Wasit na Wahidi, Hilyatul-Auliya cha Hafidh Abu Nuaim Isfahani na Faraid ya Hamwaini, Ibn Hajar Makki katika Sawaiq, Muhriqa chini ya Aya ya 14 kwa idhini ya Ahmad, Muhammad bin Talha Shafii katika Mutalibus-Suul uk. 8, Tabari katika Tafsir, Wahidi katika Asbabun-Nuzul, Ibn Maghazil katika Manaqib, Muhibud-Din Tabari katika Riyazun-Nuzra, Mumin Shablanji katika Nurul-Absar, Zamakhshari katika Tafsir, Imam Fakhrud-Din Razi katika Tafsir Kabir, Sayyid Abu Bakr Shahabud-Din Alawi katika Rishfatus-Sadi min Bahr-eFazail-e-Baniul-Nabiil-Hadi Sura ya 1 uk. 22 23 kutoka Tafsir ya Baghawi, Tafsir ya Thalabi, Manaqib ya Ahmad, Tafsir Kabir na Ausat vya Tibrani na Sadi, Sheikh Abdullah bin Muhammad bin Amir Shabrawi Shafii katika Al-Ittihaf uk.5 kutoka kwa Hakim, Tibrani na Ahmad, Jalalud-Din Suyuti katika Ihyau-l-Mayyit kutoka Tafsir za Ibn Mudhir, Ibn Abi Hatim, Ibn Mardawaih, na Mujamul-Kabir cha Tibrani; na Ibn Abi Hatim na Hakim - kwa ufupi, wengi wa maulamaa wenu mashuhuri (ukiondoa wafusi wachache wa Bani Umayya na maadui wa Ahlul Bait), wamesimulia kutoka kwa Abdullah bin Abbas na wengine, kwamba wakati Aya ifuatayo ya Qurani Tukufu ilipoteremshwa: Sema: Siombi malipo yoyote kwa haya bali mapenzi kwa jamaa zangu; na anayefanya wema tutamzidishia wema (42:23). Kikundi cha Masahaba wakauliza, Ewe Mtume wa Allah! ni nani hao jamaa zako ambao mapenzi kwao yamefanywa wajibu juu yetu na Allah? Mtume Akajibu, Ni Ali, Fatima, Hasan na Husein. Baadhi ya Hadith zina maneno, na watoto wao yaani watoto wa Hasan na Husein.
119
Mikesha ya Peshawar
120
Mikesha ya Peshawar
yeye kutoka kwa Maazatul-Ghifariyya kwamba alisema: Nilikwenda kuonana na Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) kwenye nyumba ya Aisha ambapo Ali alikuwa nje ya nyumba hiyo. Mtume akamuambia Aisha, Huyu (Ali) ndiye kipenzi mno kwangu na mwenye kuheshimika zaidi miongoni mwa wanaume wote, Tambua haki yake na mpe heshima kwa cheo chake. Sheikh Abdullah bin Muhammad bin Amir Shabrawi Shafii ambaye ni mmoja wa Maulamaa wenu mashuhuri, ameandika katika Kitabul-Ittihaf bi Hubbil-Ashraf, uk. 9, Sulaiman Balkhi katika Yanabiul-Mawadda na Muhammad bin Talha Shafii katika Matalibus-Suul, uk. 6, kutoka kwa Tirmidhi, na yeye kutoka kwa Jami bin Umar - wote wamesimulia ifuatavyo: Nilikwenda kwa Ummul-Muminina Aisha pamoja na shangazi yangu (dada yake baba), na tulimuuliza, ni nani ambaye alikuwa akipendwa zaidi na Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Yeye alijibu, Miongoni mwa wanawake alikuwa ni Fatima na miongoni mwa wanaume, ni mumewe Ali bin Abi Talib. Hadithi hii hii imesimuliwa na Mir Sayyid Ali Hamadani Shafii katika Mawaddatul-Kurba Mawadda ya 2, pamoja na tofauti kidogo kwamba Jami bin Umar alisema kwamba alipokea jibu hili kutoka kwa shangazi yake. Halikadhalika, Khatib Khawarizmi amesimulia hadithi hii kutoka kwa Jami bin Umar, na yeye kutoka kwa Aisha mwishoni mwa sura ya 4 ya Manaqib yake, Ibn Hajar Makki, katika Sawaiq Muhriqa, kuelekea mwishoni mwa sura ya 2, baada ya kuandika hadithi 40 juu ya fadhila za Ali, anasimulia hadith ifuatayo kutoka kwa Aisha: Miongoni mwa wanawake, Fatima alikuwa ndiye mwanamke aliyependwa zaidi na Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), na miongoni mwa wanaume ni mume wake. Muhammad bin Talha Shafii, katika Matalib-us-Suul, uk. 7, baada ya ya kuandika Hadith mahususi mbali mbali juu ya suala hili, anaelezea hitimisho lake mwenyewe katika maneno yafuatayo: Hadith hizi sahihi na zisizokifani huthibitisha kwamba Fatima alikuwa mwenye kupendwa zaidi na Mtume kuliko wanawake wote. Ni mwenye cheo cha juu zaidi ya wanawake wote wa Peponi na pia wa mbele zaidi juu ya wanawake wa Madina. Hadithi hizi za kuaminika, kwa uwazi zinathibitisha kwamba katika viumbe wote, Ali na Fatima walikuwa ndio wenye kupendwa zaidi na Mtume. Uthibitisho mwingine wa Mtume kumpendekeza zaidi Ali kuliko wanaume wengine ni ile Hadith ya Ndege (Hadith-e-Tair). Hadithi hii inajulikana sana na kukubaliwa sana kiasi kwamba hatuhitaji kutaja vyanzo vyake vyote. Nitataja tu baadhi ya hivyo.
121
Mikesha ya Peshawar
kwamba hadithi hii ilielezewa na wasimuliaji wa Hadith 24, kutoka kwa Anas bin Maliki. Ibn Sabbagh Maliki katika Fusulul-Muhimma anaandika kuhusu hadith hii katika maneno haya: Katika vitabu vya Hadith Sahihi na riwaya za kuaminika, Hadith-e-Tair, kutoka kwa Anas bin Malik ni haipingiki. Sibt Ibn Jauzi, katika uk. wa 23 wa kitabu chake Tadhkira na Sunan ya Tirmidhi na Masudi katika uk. wa 49 juzuu ya 2 ya Murujudh-Dhahab, wameangalia hususan katika sehemu ya mwisho ya hadithi hii ambayo ina dua ya Mtume na kukubaliwa kwake na Allah. Imam Abdur-Rahman Nisai katika hadith ya tisa katika kitabu chake Khasaisul-Alawi na Hafidh Bin Iqda na Muhammad bin Jarir Tabari, wote wamerejea kwenye nyororo isiyokatika ya wasimuliaji na kwenye vyanzo sahihi vya hadith hii, wakisema kwamba ilisimuliwa na masahaba 35 wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) kutoka kwa Anas bin Malik. Kwa ufupi, Maulamaa wenu wote mashuhuri wamethibitisha usahihi wa hadith hii na wameijumuisha kwenye vitabu vyao. Allama Sayyid Hamid Husain ameweka juzuu nzima ya kitabu chake Abaqatul-Anwar kwa ajili ya Hadithi hii tu. Alikusanya vyanzo vyote vya kuaminika kutoka kwa Maulamaa wenu mashuhuri na kwa wazi kabisa akathibitisha usahihi wa hadith hii. Kwa mujibu wa Hadith hii, siku moja mwanamke mmoja alileta zawadi ya ndege aliyebanikwa kwa Mtume. Kabla ya kumla, Mtume akiwa amenyoosha mikono yake juu, akamuomba Allah hivi: Ee Allah! Kati ya viumbe wako wote, mlete mtu ambaye ni mpenzi zaidi kwako na kwangu, ili kwamba ale pamoja nami ndege huyu wa kubanikwa. Ndipo Ali akaingia ndani akala ndege yule wa kubanikwa pamoja na Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Baadhi ya vitabu vyenu, kama vile Fusulul-Muhimma cha Malik, Tarikh cha Hafidh Nishapuri, Kifayatut-Talib cha Ganji Shafii na Musnad ya Ahmad Bin Hanbal, n.k. ambamo Hadith hii imesimuliwa kutoka kwa Anas bin Malik, vimeandikwa kwamba Anas bin Malik alisema Mtume alikuwa bado hajamaliza dua yake wakati Ali alipoingia nyumbani pale, lakini nikamficha jambo lile. Wakati Ali alipoingiza mguu wake mara ya tatu, Mtume akiniamrisha nimuache aingie ndani. Wakati Ali alipoingia Mtume akasema: Baraka za Allah ziwe juu yako; ni kitu gani kimekuleta kuja kwangu? Ali akamueleza kwamba alikuja kwake mara tatu lakini aliruhusiwa kuingia safari hii tu. Mtume akaniuliza ni kitu gani kimenifanya niwe hivyo, na nikajibu: Ukweli ni kwamba, niliposikia dua yako, nilitamani kwamba heshima hii ingekwenda kwa mmoja wa kabila langu. Sasa nakuulizeni enyi waungwana iwapo dua ya Mtukufu Mtume ilikubaliwa au kukataliwa na Allah. Sheikh: Ni wazi Allah aliikubali kwa vile aliahidi katika Qurani tukufu kwamba angekubali dua ya Mtume. Aidha, Allah alijua kwamba Mtume asingeweza kuomba dua isiyofaa. Hivyo Allah aliyakubali maombi yake kila wakati. Muombezi: Allah alimpeleka Ali, mtu anayestahiki zaidi katika viumbe Wake, kwa
122
Mikesha ya Peshawar
Mtume. Wanachuoni wenu wenyewe wamethibitisha tukio hili. Muhammad bin Talha Shafii katika Kitabu chake Matalib-Us-Sulu, Sura ya 1, sehemu ya 5, uk. wa 15, amethibitisha cheo cha juu cha Ali kama mwenye kupendwa zaidi na Allah na Mtume juu ya msingi wa Hadith ya Bendera (Riyat) na Hadith ya Ndege. Katika kuhusiana na hilo anasema: Nia ya Mtume ilikuwa kwamba watu waelewe cheocha kipekee na cha hali ya juu cha Ali, ambaye alifikia upeo wa juu zaidi wa kuweza kufikiwa na wacha Mungu. Vilevile Hafidh na Muhammad bin Yusufu Ganji Shafii (aliyekufa 658 A.H.) anaandika katika kitabu chake, Kifayatut-Talib Sura ya 33, akizungumzia fadhila za Ali ibn Abi Talib, kwamba hadith hii kwa uwazi kabisa inathibitisha kwamba Ali alikuwa kipenzi sana katika viumbe kwa Allah. Baadae anasema kwamba Hakim Abu Abdullah Hafidh Nishapuri ameisimulia hii Hadith-e-Tair ya Anas kutoka wasimuliaji 86 na vile vile akaandika na majina ya wasimuliaji wote 86 (Tazama Kifayatut-Talib, Sura ya 32). Ile hadith ambayo umenukuu wewe, ukiilinganisha na Hadith zilizosimuliwa na Maulamaa wenu wa daraja za juu (isipokuwa washupavu wakorofi wachache), haiwezi kutegemewa na ingekataliwa na watu wenye elimu. Sheikh: Nina wasiwasi kwamba umeamua kwa akili yako kutokubali tunayo yasema. Muombezi: Unawezaje kuhusisha chuki kama hizo kwangu? Unaweza ukatoa mfano mmoja tu ambapo umetoa hoja yenye nguvu na mimi bila sababu nikaikataa? Ninaapa kwamba katika mijadala ya kidini na Mayahudi, Wakristo, Wahindu na Wabrahmin na Mabahai wasio na elimu wa Iran, Makadian wa India na wayakinifu (wenye kuamini vitu vyenye kuonekana, kugusika na kuhisiwa tu) katika hali zote hizi mimi sijawahi kufanya ukaidi katika hoja zangu. Kamwe sijawahi kuwa mbishi kwa makafir hawa vipi nitaweza kufanya hivyo kwenu ninyi, ndugu zangu katika Uislamu? Sheikh: Tumesoma maelezo ya mjadala wako na Wahindu na Wabrahmin wa Lahore katika magazeti. Tulivutiwa mno na maelezo hayo. Ingawa tulikuwa hatujakutana na wewe, tulijisikia tumeungana na wewe kimaadili. Natumaini kwamba Allah atakuongoza wewe na sisi kwenye njia iliyonyooka. Tunaamini kwamba kama kuna wasiwasi wowote kuhusu Hadith fulani, inatupasa, kwa mujibu wa ushauri wako, kuirejesha kwenye Qurani Tukufu. Hata hivyo, kama unahoji ubora wa khalifa Abu Bakr na muundo wa ukhalifa wa makhalifa wakubwa, na kama utaziona hadith kuwa ni zenye mashaka, je, utasita vilevile kuamini hoja ambayo imetegemea juu ya Qurani Tukufu? Muombezi: Allah asitujaalie siku tutakayotilia shaka ukweli uliotegemea juu ya Qurani Tukufu au Hadith Sahihi. Walakini, wakati tutakapokuwa tumeingia kwenye mjadala wa kidini na Taifa lolote au Jumuiyya, wao vilevile wanahoji kutoka kwenye Aya za Qurani Tukufu kuthibitisha mtazamo wao. Kwa vile Aya za Qurani zina daraja mbalimbali za maana, Mtume wa mwisho, ili kuwalinda watu dhidi ya kutoelewana, hakuiacha Qurani kama chanzo pekee tu cha mwongozo. Kama inavyokubaliwa na madhehebu zote (Shia na
123
Mikesha ya Peshawar
Sunni), yeye mwenyewe (Mtume) alisema: Nawaachieni vitu viwili vizito: Kitabu cha Allah (Qurani) na kizazi changu. Kama mtashikamana na viwili hivi, kamwe, hamtapotea baada yangu. Hakika viwili hivi kamwe havitatengana mpaka vinifikie kwenye chemchem ya Kauthar. Kwa sababu hii, maana ya ufunuo wa Qurani Tukufu yapasa itafutwe ama kutoka kwa Mtume, fasir mkuu wa Qurani Tukufu, au baada yake, kutoka kwa wale walio sawa na Qurani Tukufu, dhuria watukufu wa Mtume. Qurani Tukufu inasema: Basi waulizeni wenye kumbukumbu ikiwa ninyi hamjui. (21:7).
124
Mikesha ya Peshawar
Muhammad ni Mtume wa Allah, na walio pamoja naye ni wenye nyoyo thabiti mbele ya makafiri, na wenye kuhurumiana wao kwa wao, utawaona wakiinama kwa kurukuu na kusujudu (katika Sala), wakitafuta fadhila za Allah na radhi (yake). Alama zao ni katika nyuso zao kwa taathira (athari) ya kusujudu (48:29). Kwanza Aya hii huthibitisha ubora wa Abu Bakr. Pili huonyesha nafasi za makhailfa wanne kinyume na inavyodaiwa na madhehebu ya Shia kwamba Ali alikuwa Khalifa wa kwanza. Aya hii bila ubishani inaelezea kwamba Ali alikuwa Khalifa wa nne. Muombezi: Hakika Aya hii haitoi dalili yoyote ya wazi kuhusu namna ya kuchaguliwa makhalifa au kuhusu ubora wa Abu Bakr. Kwa hiyo, lazima uonyeshe ni sehemu ipi katika Aya hii ambapo maana hiyo imefichwa. Sheikh: Mwanzoni mwa Aya hii, usemi (usemao) na walio pamoja naye huashiria kwa yule mtu maarufu ambaye alikuwa na Mtume usiku wa pango. Utaratibu wa kupokezana nafasi ya ukhalifa pia iko wazi katika aya hii. Walio pamoja naye ina maana ya Abu Bakr, ambaye alifuatana na Mtume kwenye Pango la Thawr katika usiku wa Hijra. Usemi, wenye nyoyo thabiti mbele ya makafir maana yake ni Umar Bin Khattab, ambaye alikuwa mkali sana kwa makafir. Usemi, wenye kuhurumiana wao kwa wao huashiria kwa Uthman bin Affan, ambaye alikuwa mpole sana. Usemi, alama zao ni katika nyuso zao kwa athari ya kusujudu huashiria kwa Ali. Ni wazi kwamba Ali ni Khalifa wa nne, sio wa kwanza, kwa vile Allah amemtaja katika sehemu ya nne. Muombezi: Nashangaa vipi nitaweza kujibu ili kwamba nisije nikalaumiwa kwa kujipendelea mwenyewe. Hakuna tafsir za Qurani, ukichukua pamoja na zile za maulamaa wenu wakubwa, ambazo zimetafsiri maneno haya kama ulivyofasili wewe. Aya hii ingekuwa inahusu utaratibu wa Ukhalifa, siku ya kwanza baada ya kifo cha Mtume, wakati Ali, Bani Hashim, na masahaba mashuhuri wa Mtume walipoweka vipingamizi na wakakataa kula kiapo cha utii kwa Khalifa, basi hoja zisizo za msingi zisingetolewa pale. Wangeweza kutoa jibu la kunyamazisha kwa kusoma aya hii tukufu pale pale. Kwa hiyo, ni wazi kwamba tafsiri yako ni mawazo yaliyokuja baadaye. Hakuna yeyote katika wafasiri wakubwa wa madhehebu yenu, kama Tabari, Imam Thalabi, Fadhil Nishapuri, JalaludDin Suyuti, Qadhi Baihawi, Jarullah Zamakhshari, Imam Fakhrud-Din Radhi, au wengine ambao wameitafsir hivyo. Nashindwa kuelewa jinsi unavyoipata maana hii. Wapi na kutoka kwa nani maana hii ilitolewa? Aya hii, kielimu na mtazamo wa kifundi, vilevile vinakwenda kinyuma na unavyosema. Sheikh: Sikutarajia kwamba utakuwa mpinzani hivyo kwenye aya iliyo na maana ya wazi kiasi hicho. Hakika kama una lolote la kusema dhidi ya hivi unaweza ukatueleza tujue ili
125
Mikesha ya Peshawar
kwamba ukweli halisi uweze kuthibitishwa. Muombezi: Ukichukulia ujenzi wa kinahau wa aya hii, kama tutaitafsiri maana yake kama ulivyofanya wewe, itakuwa na maana kwamba ama Muhammad ni Abu Bakr, Umar, Uthman na Ali au kwamba Abu Bakr, Umar, Uthman na Ali ni Muhammad! Hata wanafunzi wanaoanza wanajua kwamba aina hii ya tafsir ya kinahau sio sahihi. Mbali na hayo, kama aya hii inaashiria kwa Makhalifa wanne, kungekuwa na kiungo na kupatanisha maneno ili kupata hiyo maana yako, lakini haiko hivyo. Wafasiri wote wa madhehebu yenu wenyewe wanasema kwamba aya hii inaashiria kwa waumini wote. Aidha, sifa zilizotajwa katika aya hii kwa wazi kabisa zinaashiria kwa mtu mmoja tu, ambaye alikaa na Mtume kuazia mwanzo kabisa na sio watu wanne. Na kama tukisema mtu huyu mmoja alikuwa Amirl-Muminina Ali, itakuwa sawasawa zaidi kulingana na akili za kuzaliwa na hadith kuliko kutaja wengine wowote.
126
Mikesha ya Peshawar
Mombezi: Ningekuomba uliache suala hili kwa muda huu kwa sababu maneno huzaa maneno. Baadhi ya watu wenye chuki wanaweza wakafasiri maoni yetu kwa nia mbaya. Sitaki kuchochea chuki. Mtu anaweza akasema tunataka kuwavunjia heshima makhalifa, ingawa cheo cha kila mmoja kimewekwa, na sio muhimu kufanya tafsir zisizo na maana. Sheikh: Unakuwa mkwepaji. Elewa kwamba hoja yenye maana haizai chuki; huondoa kutokuelewana. Muombezi: Kwa vile umetumia neno Mkwepaji, ninalazimika kujibu, ili uweze kujua kwamba silikwepi suala hili. Nilitaka kudumisha utaratibu wa mjadala wetu. Natumaini kwamba hutaona makosa kwa upande wangu. Umetoa utetezi wa kizembe sana kwamba Mtume alijua kwamba Abu Bakr atakuwa Khalifa wake baada yake. Kwahiyo, ilikuwa muhimu kwake kuokoa maisha yake, na hivyo akamchukuwa ili awe pamoja naye.
127
Mikesha ya Peshawar
kitanda chake, na kwa kuogopa kwamba Abu Bakr angetoa siri hii kwa makafiri, Mtume akamchukua awe pamoja naye. Mwisho, ingelikuwa vizuri kama ungeonyesha ni ushahidi gani uliopo katika Aya hii, unaoonyesha ubora wa Abu Bakr au iwapo kufuatana na Mtume katika safari ni uthibitisho kwamba mtu anayo sifa ya Ukhalifa. Sheikh: Ushahidi upo. Kwanza, usuhuba wa Mtume na kwamba, Allah amemuita sahaba wa Mtume, yenyewe ni sifa tosha. Pili, Mtume mwenyewe amesema: Hakika Allah yu pamoja nasi. Tatu, uteremshwaji wa utulivu juu yake kutoka kwa Allah, kama ilivyotajwa katika Aya hii, ni uthibitisho wa kuvutia zaidi wa ubora wa Abu Bakr. Kwa hiyo, nukta zote hizi zikiwekwa pamoja huonyesha ubora wake kwa wengine kuhusiana na ukhalifa. Muombezi: Hakuna anayesita kuikubali nafasi ya Abu Bakr, Mwislam mtu mzima, mmoja wa masahaba mashuhuri na baba wa mke wa Mtume. Hata hivyo, sababu hizi hazithibitishi ubora wake katika ukhalifa. Kama utajaribu kuthibitisha nukta yako hii kwa maelezo haya mbele ya watu waadilifu wasio na upendeleo, utakuwa unavutia lawama nzito. Watasema kwamba usuhuba na watu wema sio uthibitisho wa sifa au ubora. Kwa mfano, mara kwa mara tunaona kwamba watu wabaya hufuatana na watu wema, na kundi la makafiri hufuatana na Waislamu katika safari. Pengine umesahau Qurani Tukufu inavyosema kuhusu Mtume Yusufu ambaye amesema: Enyi wafungwa sahibu wenzangu wawili! Je! waungu wengi wanaofarikiana ndio bora au Mwenyezi Mungu, Mmoja Mwenye nguvu? (12:39). Kuhusu Aya hii, wafasiri wamesema kwamba wakati Yusufu alipopelekwa jela, siku hiyo hiyo mpishi wa Mfalme na mtunza mvinyo ambao wote walikuwa makafiri, vilevile walitiwa jela pamoja naye. Kwa muda wa miaka mitano watu hawa watatu (waumini na makafiri kwa pamoja ) waliishi pamoja kama maswahiba. Wakati akiwahubiria, Yusufu aliwaita sahiba zangu. Je, usuhuba huu wa Mtume Yusufu ulifanya hata mara moja hali ya kuwaona makafiri hawa wawili kama watu bora au wenye heshima? Je, usuhuba wao na Mtume Yusufu ulileta mabadiliko katika Iman zao? Maandishi ya Wafasiri na wanahistoria yanatuambia kwamba, baada ya miaka mitano ya usahaba, waliachana kila mmoja katika hali ile ile.Aya nyingine ya Qurani Tukufu inasema:
Sahiba wake akamuambia na hali ya kuwa anajibishana naye: Je! Unamkufuru, Yule aliyekuumba kwa udongo, kisha kwa tone la manii, kisha akakufanya mtu
128
Mikesha ya Peshawar
kamili? (18:37) Wafasiri wanakubaliana kwamba aya hii inazungumzia ndugu wawili, mmoja alikuwa muumini, ambaye jina lake lilikuwa Yahuda. Mwingine alikuwa kafir jina lake lilikuwa Baratus. Jambo hili limeelezewa vilevile katika Tafsir-e-Kabir na Imam Fakhrud-Din Razi, ambaye ni mmoja katika Maulamaa wenu. Ndugu hawa wawili walizungumza pamoja, maelezo ambayo hayataweza kutolewa hapa. Hata hivyo Allah amewaita wote wawili (Muumin na Kafiri). Masahibu. Je, yule kafiri alipata faida kutokana na usuhuba wake na Muumini? Kwa hakika hapana. Hivyo usuhuba peke yake sio msingi wa mtu kudaiwa kuwa ni bora. Kuna mifano mingi yenye kuunga mkono maoni haya.
MANENO YA MTUKUFU MTUME (S.A.W.W.) ALLAH YUKO PAMOJA NASI SIO UTHIBITISHO WA UBORA WA ABU BAKR.
Umesema pia kwamba kwa vile Mtume alimuambia Abu Bakr, Allah yuko pamoja nasi. kwamba huo ni uthibitisho wa ubora wa Abu Bakr na haki yake ya Ukhalifa! Waweza ukayafikiria tena maoni yako. Watu wanaweza wakakuuliza, kwa mfano, Je, Allah anakuwa na waumini na mawalii tu, na sio na makafir? Unajua sehemu yoyote ambayo Allah hayupo? Je, hivi Allah hayupo na kila mtu? Chukulia kwamba muumini na kafiri wako pamoja katika mkusanyiko. Qurani inasema:
Je! Huoni kwamba Allah anajua vilivyomo mbinguni na vilivyomo ardhini? Haupatikani mnongono wa watu watatu ila yeye huwa ni wanne wao, wala watano ila yeye huwa ni wa Sita wao, wala wachache kuliko hao wala zaidi ila Yeye huwa pamoja nao, popote walipo(58:7). Kwa mujibu aya hii na wa akili ya kawaida, Allah yupo na kila mtu. Sheikh: Maelezo Allah yupo pamoja nasi Yana maana kwamba walikuwa wapenzi mno wa Allah kwa sababu wamesafiri katika njia ya Allah kwa madhumuni ya kuhifadhi dini yake. Baraka za Allah zilikuwa pamoja nao. Muombezi: Lakini hakika maelezo haya hayathibitishi kwamba mtu anazo baraka za
129
Mikesha ya Peshawar
milele. Allah Mwenye nguvu hutizama matendo ya watu. Imetokea mara kwa mara kwamba wakati fulani, watu walifanya matendo mema na wakawa ni wenye kupokea rehema kutoka kwa Allah. Baadae wakamuasi Allah na ikawapata adhabu ya Mungu. Ibilis kama unavyojua, alimuabudu Allah kwa maelfu ya miaka na akapata upole kutoka Kwake. Hata hivyo mara tu alipoasi amri yake, akalaaniwa. Qurani Tukufu inasema:
Akasema: Basi toka humo, na hali ya kuwa wewe ni mwenye kufukuzwa Na kwa yakini itakuwa laana juu yako mpaka Siku ya Malipo. (15:34-35). Kumradhi, hakuna madhara katika kutoa mifano, madhumuni yangu ni kufafanua hii nukta. Historia imejaa mifano mingi ya wale ambao walikuwa karibu na Allah, lakini ambao baada ya kujaribiwa, walilaaniwa. Balam Bin Baur, kwa mfano, wa hirimu moja na Musa, alitokea kuwa karibu sana na Allah kiasi kwamba Allah alimfunulia lile Ism-eAdhim (jina tukufu la Allah, ambalo kupitia hilo chochote kinachoombwa kinakubaliwa upesi sana na Allah). Alimuomba Allah kwa njia ya Ism-e-Adhim na akasababisha shida ikampata Musa katika Bonde la Tia! Lakini wakati wa majaribio, Balam alizidiwa nguvu na mahaba ya vitu vya ulimwengu. Alimfuata Ibilis na akalaaniwa. Wafasiri wametoa maelezo kamili ya tukio hili. Imam Fakhrud-Din Razi katika Tafsir yake sehemu ya 4, uk. 463, ameelezea habari hii kutoka kwa Ibn Abbas, Ibn Masud, na Mujahid. Allah katika Qurani Tukufu anatueleza hivi: Na wasomee habari za yule tuliyempa Aya zetu kisha akajivuna nazo. Na shetani akamuandama na akawa miongoni mwa waliopotea.
BARSISA ABID.
Au angalia la Barsisa Abid, ambaye mwanzoni alimwabudu Allah kiasi kwamba akakuwa Mustajabud-dawa (mtu ambaye maombi yake hukubaliwa). Hata hivyo, wakati muda wa majaribio ulipofika, alishindwa. Akipotezwa na Shetani, akafanya zinaa na msichana, akanyongwa, na akafa kafiri, Qurani inamzungumzia katika maneno haya:
Ni kama shetani, anapomwambia mtu: kufuru; na anapokufuru akamwambia: Mimi si pamoja na wewe, hakika namuogopa Allah, Mola wa walimwengu. Basi mwisho wa wote wawili hao ikawa waingie motoni wakae humo, na hiyo ndiyo jaza ya madhalimu. (59:16-17).
130
Mikesha ya Peshawar
Hivyo kama mtu aliwahi kufanya matendo mema wakati fulani, haina maana kwamba mwisho wake utakuwa mzuri. Ni kwa sababu hii kwamba tunaelekezwa kusema katika maombi yetu: Matendo yetu na yawe na mwisho mwema. Sheikh: Kwa hakika sikutarajia mtu mwenye heshima kama wewe kutoa mfano wa shetani, Balam Baur na Barsisa. Muombezi: Samahani, nimekwishaeleza kwamba hakuna madhara katika kutoka mifano. Kwa kweli ni lazima tuitoe katika mijadala ya kielimu ili kuthibitisha ukweli. Allah awe shahidi yangu: Kamwe sikukusudia kumtweza yeyote kwa kutoa mifano hii. Madhumuni yangu ni kuthibitisha hoja yangu tu. Sheikh: Aya hii kwa wazi kabisa huthibitisha ubora wa Abu Bakr kwa sababu inasema: Hivyo Allah akamteremshia utulivu juu yake. (9:40). Kijina hapa humuashiria Abu Bakr, ambacho huthibitisha ubora wake. Muombezi: Umeielewa vibaya, kijina kilichotumiwa baada ya Sakina (utulivu) huashiria kwa Mtume. Utulivu uliteremshwa kwake na sio kwa Abu Bakr, kama ilivyo dhahiri katika sentensi inayofuatilia ambapo Allah anasema: na akamnusuru kwa majeshi msiyoyaona (9:40) ukweli ni kwamba majeshi ya Malaika wasioonekana yalikuwa kwa ajili ya kumsaidia Mtume, sio Abu Bakr. Sheikh: Nakubali kwamba msaada wa Mungu ulikuwa kwa ajili ya Mtume, lakini Abu Bakr akiwa pamoja na Mtume, hakuwa bila rehma.
131
Mikesha ya Peshawar
Muombezi: Kwa misingi gani wewe unasema kwamba Mtume alikuwa hategemei upewaji wa rehma za Mungu? Hakuna mtu - awe Mtume Imam au Walii ambaye anajitegemea kwa (upewaji wa) rehma za Mungu. Pengine umesahau Qurani Tukufu inasema nini kuhusu tukio la Hunain. Kisha Allah akateremsha utulivu wake juu ya Mtume wake na juu ya waliomini (9:26). Kitu hicho hicho kimesemwa katika Sura ya 48 (Fath) aya ya 26, ya Qurani Tukufu. Waumini wamejumuishwa baada ya Mtume katika aya hii, kama vile katika aya ya Pango. Kama Abu Bakr angekuwa mwenye kustahiki kupewa utulivu, ima kijina kwa ajili ya watu wawili kingetumika, au jina lake lingetajwa mbalimbali. Jambo hili liko wazi kabisa kiasi kwamba Maulamaa wenu wenyewe wanakiri kwamba kijina kilichofungamanishwa na utulivu hakiashirii kwa Abu Bakr. Unaweza kuitazama Naqzul-Uthmaniyya kilichoandikwa na Sheikh Abu Jafar Muhammad bin Abdullah Iskafi, ambaye ni mmoja wa Maulamaa mashuhuri na masheikh wa Mutazil. Mwanachuo huyu anaukana moja kwa moja uongo wa Abu Uthman Jahiz. Ibn Abil-Hadid vilevile ameandika baadhi ya majibu hayo katika Sharh yake ya Nahjul-Balagha Jz. 3, uk. 253281. Kwa nyongeza, kuna usemi katika Aya hii, ambao maana yake halisi ni kinyume na hoja yako. Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alimuambia Abu Bakr: Usihuzunike. Usemi huu unaonyesha Abu Bakr alikuwa muoga. Je, woga huu ulikuwa unafaa kusifiwa au hapana? Kama ingelikuwa hivyo, Mtume asingemzuia yeyote kufanya tendo jema. Mwakilishi wa Allah ana sifa makhususi. Muhimu zaidi ya hizo, kama ilivyotajwa katika Qurani Tukufu, ni kwamba haogopi kubadilika kwa maisha. Anafanya uvumilivu na ushujaa. Qurani Tukufu inasema: Sikilizeni (eleweni)! Hakika vipenzi vya Allah hawatakuwa na khofu wala hawatahuzunika. (10:62).
132
Mikesha ya Peshawar
haikukamilika. Muombezi: (Akiangalia upande wa Maulamaa wa Kisunni). Mradi na nyie mliruhusu hilo. Hafidh: (Kwa hasira kidogo). Hakuna madhara. Kama kuna kitu kimebakia kusemwa, tuko tayari kukisikiliza. Muombezi: Usiku uliopita nilithibitisha kwa mtazamo wa kinahau kwamba maelezo ya baadhi ya wafasiri wanaosema kwamba aya hii huonyesha namna ya kuamua ukhalifa yalikuwa hayakubaliki. Sasa nitaelezea kutokana na mtazamo mwingine. Sheikh Abdus-Salam Sahib alisema usiku uliopita kwamba kuna sifa nne zilizotajwa katika aya hii. Sifa hizi, alisema, zinaonyesha kwamba aya hii iliteremshwa kwa habari ya Makhalifa wanne wa kwanza na kwamba aya hii inaonyesha mpango wa ukhalifa. Majibu yangu kwa hoja hii ni: kwanza, wafasir wenye kuaminika hawajawahi kutoa maelezo kama hayo kuhusu maana halisi ya aya hii. Pili, nyote mnajua kwamba wakati sifa inapohusishwa na mtu inaenda sawasawa na tabia yake, hapo ndipo (sifa hiyo) itakuwa na maana. Kama tutayaangalia mambo kwa busara zaidi, tunaona kwamba ni Ali tu ambaye alikuwa na sifa hizo zilizoelezewa katika aya hii. Sifa hizi kwa njia yoyote haziafikiani na hizo zilizotajwa na Sheikh Sahib. Hafidh: Aya zote hizo ulizokwishasimulia kuhusu Ali hazikutosha? Unataka sasa kwa ujanja wako wa ufasaha wa kusema kuthibitisha kwamba aya hii tukufu vilevile iliteremshwa kwa kumtukuza Ali? Kama ni hivyo, hebu tujulishe ni vipi haikubaliani na ukhalifa wa makhalfa wanne wa kwanza.
133
Mikesha ya Peshawar
mu ya 62, anasimulia kutoka kwa Ibn Abbas, na Muhadith wa Syria katika kitabu chake Tarikh-e-Kabir, na wengine wameandika Aya nyingi kiasi kama mia tatu za Qurani Tukufu zenye kumtukuza Ali. Je, watu hawa walikuwa Mashia au wanatokana na maulamaa wenu wakubwa? Hatuhitaji kuhusisha kwa uongo aya ya Qurani tukufu kwa ajili ya kuthibitisha cheo cha Amirl-Muminina Ali. Maadui zake (Bani Umayya, Nawasib na Khawarij) wamezuia fadhila zake zisitajwe na marafiki zake wakasita kusimulia ubora wake kwa kuogopa matokeo yake. Bado, vitabu vimejaa fadhila zake na vinatoa mwanga juu ya mambo yote ya kufanikiwa kwake. Kwa vyovyote inavyohusika aya hii, sikujitia katika ujanja wa ufanisi wa kusema. Nimefichua ukweli, nikitoa hoja kutoka katika vitabu vyenu. Mmeona mpaka hapo kwamba sikutoa hoja kutoka kwenye riwaya za waandishi wa Kishia. Hata kama vitabu vya Shia viwekwe kando, bado nitathibitisha ubora wa kipekee wa Ali. Niliyosema kuhusu Aya hii yanakubaliana na maoni ya Maulamaa wenu wenyewe. Muhammad bin Yusufu Ganji Shafii amenukuu Hadith ya kufanana katika kitabu chake Kifayatut-Talib Sura ya 23, kutoka kwa Mtume yenye maana kwamba Ali alikuwa anafanana na Mitume. Anasema kwamba sababu ya Ali kuitwa kwamba anafanana na Mtume Nuh katika hekima ni kwamba Ali alikuwa mkali dhidi ya makafiri na mpole kwa waumini. Allah amezitaja sifa hizi katika Qurani Tukufu. Ali ambaye siku zote alikuwa pamoja na Mtume, alikuwa mkali dhidi ya makafiri na mwenye huruma kwa waumini. Na ukichukulia, kama Sheikh Sahib anavyosema: kwamba usemi Na wale ambao wako pamoja naye unamuashiria Abu Bakr kwa sababu kwa muda wa siku chache alikuwa na Mtume ndani ya Pango, Hivi mtu kama huyo anaweza kuwa sawa na yule aliyekuwa na Mtume tangu utotoni na kupata maelekezo kutoka kwake?
134
Mikesha ya Peshawar
ka kwa Anas bin Malik na wengine kwamba: Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alipewa Utume wa Allah siku ya Jumatatu, na Ali akatangaza imani yake kwake siku ya Jumanne. Vilevile imesimuliwa tena kwamba: Utume wa Allah ulitangazwa siku ya Jumatatu na Ali akasali na Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) siku ya Jumanne. Na halafu tena, Ali alikuwa mtu wa kwanza kutangaza imani yake kwa Mtume. Vilevile Tabari, Ibn Abi-Hadid, Tirmidhi, na wengine wanasimulia kutoka kwa Ibn Abbas kwamba Ali alikuwa wa kwanza kusali.
135
Mikesha ya Peshawar
ni majibu ya barua ya Muawiya aliyomuandikia Ali ambayo kwayo alijigamba kwamba baba yake alikuwa kiongozi wa kabila lake wakati wa zama za ujinga na kwamba katika Uislamu Yeye (Muamiya) alikuwa ni Mfalme. Muawiya vilevile alisema kwamba yeye alikuwa mjomba wa waumini mwandishi wa wahayi (ufunuo), na mtu sifa njema. Baada ya kusoma barua hii, Ali akasema: Mtu wa tabia hii mtoto wa mwanamke ambaye alitafuna maini - anajigamba mbele yangu! (kuhusu mama yake Muawiyya Hindi ambaye baada ya Vita vya Uhud akiwa na hasira kali alichana maiti ya Hamza, akakata ini lake, na akalitafuna). Hata hivyo, Muawiyya ingawa alikuwa mpinzani mkali wa Ali, hakuweza kuzikataa sifa hizi. Aidha, Hakim Abul-Qasim Haskani, mmoja wa Maulamaa wenu, anasimulia kutoka kwa Abdur-Rahman Bin Auf, kuhusu aya hiyo hapo juu ya Makuraishi kumi waliokubali Uislamu, kwamba Ali alikuwa wa mbele zaidi miongoni mwao. Ahmad Bin Hanbal, Khatib Khawarizmi, na Sulayman Balkhi Hanafi, wanasimulia kutoka Anas bin Malik kwamba Mtume alisema: Malaika walinitakia rehma mimi na Ali kwa muda wa miaka saba, kwani kwa muda huo hakuna sauti iliyotamka Upweke wa Allah isipokuwa yangu na ya Ali. Ibn Abil-Hadid Mutazali katika Sherh-e-Nahjul-Balagha, Jz. 1, uk. 373-5, ameandika Hadith nyingi mbalimbali zilizosimuliwa kupitia wanachuoni wenu zenye maana kwamba Ali alikuwa wa mbele zaidi katika jambo la Uislamu. Baada ya kuandika vifungu mbalimbali vya maneno na simulizi anahitimisha kwa kusema: Hivyo mukhtasari wa yote tuliyoeleza ni kwamba Ali ni wa kwanza miongoni mwa watu kuhusu Uislamu. Maoni kinyume na haya ni mara chache kuyasikia, na hayana maana kwetu kuyazingatia. Imam Abdur-Rahman Nisai, mwandishi wa moja ya vitabu sita Sahih vya hadith, ameandika katika Khasaisul-Alawi hadith sita za mwanzo juu ya suala hili na amethibitisha kwamba mtu wa mbele zaidi katika Uislamu na wa kwanza kusali na Mtume alikuwa Ali. Kwa nyongeza, Sheikh Sulayman Balkh Hanafi katika Yanabiul-Mawadda. Sura 12, ameandika hadith 31 kutoka kwa Tirmidhi, Hamwaini, Ibn Maja, Ahmad Bin Hanbal, Hafidh Abu Nuami, Imam Thalabi, Ibn Maghazili, Abul-Muwayyid Khawarizmi, na Dailami, ambayo hitimisho lake ni kwamba Ali alikuwa wa kwanza katika umma wote wa Kiislamu kukubali Uislamu. Hata shupavu mchungu Ibn Hajar Makki ameandika katika Sawaiq-Muhirika, Sura ya 2 Hadith juu ya Suala hili hili, ambazo baadhi ya hizo zimekubaliwa na Sulayman Balkhi Hanaf katika kitabu chake Yanabiul-Mawadda kuelekea mwisho wa kufunga Sura ya 2, amesimuluia hadith juu ya suala hilo hilo, baadhi yake ambazo zimekubaliwa na Suleiman Balkhi Hanafi ndani ya YanabiulMawadda yake. Zaidi ya hayo, ndani ya YanabiulMawadda, kuelekea mwisho wa Sura ya 12, amesimulia kutoka Ibn Zubair, Makki na yeye kutoka kwa Jabir Ibn Abdullah Ansari, Hadith kuhusu
136
Mikesha ya Peshawar
sifa za Ali, ambayo ningependa kuitoa hapa kwa ruhusa yenu ili kuhitimisha hoja yangu. Mtume alisema: Mwenyezi Mungu alinichagua mimi kuwa Mtume na akanifunulia maandiko matakatifu. Mimi nikamwambia, Ee Allah, Mola Wangu, ulimtuma Musa kwa Firauni, Musa akakuomba umfanye ndugu yake, Harun, Waziri wake ambaye angeweza kuimarisha mkono wake, ili maneno yake yapate kushuhudiwa. Sasa nakuomba, Ee Allah, uchague kwa ajili yangu kutoka miongoni mwa familia yangu Waziri ambaye ataimarisha mkono wangu. Mfanye Ali kuwa Waziri wangu na ndugu yangu, ingiza ushujaa kwenye moyo wake, na mpe nguvu juu ya maadui. Ali alikuwa mtu wa kwanza kuniamini na kushuhudia Utume wangu na mtu wa kwanza kutamka Upweke wa Allah sambamba pamoja na mimi. Baadae niliendelea kumuomba Allah. Kwa hiyo Ali ni kiongozi wa warithi (wangu). Kumfuata yeye ni rehma; kufa ukiwa na utii kwake ni Shahada. Jina lake huonekana katika Taurat pamoja na jina langu; mke wake, mwaminifu zaidi, ni binti yangu; watoto wake wawili wa kiume, ambao ni mabwana wa vijana wa Peponi, ni watoto wangu. Baada yao, Maimam wote ni wawakilishi wa Allah juu ya viumbe baada ya Mitume; na ni milango ya elimu miongoni mwa watu wangu. Yeyote ambaye atawafuata ameokolewa kutokana na moto wa Jahanam; yeyote ambaye atawafuata ameongozwa katika njia iliyonyooka; yeyote ambaye amejaaliwa na Allah kuwa na mapenzi kwao hakika atapelekwa Peponi. Hivyo, watu wenye akili, chukueni tahadhari. Ningeweza kunukuu hadith za namna hiyo usiku wote, ambazo zote zimeandikwa na Maulamaa wenu. Lakini nafikiri hii inatosha. Ni Ali peke yake aliyefuatana na Mtume tangu utotoni, na kwa hiyo ni sawa kwamba tunamuona ni mtu aliyeashiriwa katika maneno, Wale ambao wako pamoja naye, na sio mtu ambaye alifuatana na Mtume kwa safari ya siku chache tu.
137
Mikesha ya Peshawar
Muombezi: Mazungumzo kama hayo kutoka kwa mtu msomi kama wewe kwa hakika yanashangaza. Nashangaa jinsi gani nitaivunja hoja kama hiyo. Kama ningekuwa niseme kwamba umechukuwa msimamo kama huo kwa ukorofi tu, ingekuwa dhidi ya tabia yangu kuhusisha sababu kama hiyo kwa mtu msomi. Ngoja nikuulize Swali: je, kuukubali Uislamu kwa Ali kulitegemea juu ya kupenda kwake mwenyewe binafsi au kwa kulinganiwa ya Mtume? Hafidhi: Kwa nini unachukuwa mtizamo mkali kama huu juu ya namna tunavyoongea, kwani tunapokuwa na mashaka ni lazima tuyajadili. Kwa kujibu swali lako, nakiri kwamba Ali aliukubali Uislamu kwa ulinganio wa Mtume. Muombezi: Wakati Mtume alipomlingania Ali akubali Uislamu, yeye hakujua kwamba mtoto hafungwi na majukumu ya kidini? Kama ukisema kwamba alikuwa hajui utakuwa unahusisha na ujinga na kama alijua na akamhubiria Ali hata hivyo, basi kitendo chake kilikuwa cha upuuzi. Ni dhahiri kwamba, kuhusiha upuuzi kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) ni ukafir kwa vile Mtume ni Masum (hakosei wala hatendi dhambi). Allah anasema kuhusu yeye katika Qurani Tukufu: Wala hasemi kwa matamanio (ya nafsi yake). Hayakuwa haya ila ni Wahyi uliofunuliwa (kwake) (53:3-4). Mtume alimuona Ali ni mtu wa kufaa kulinganiwa kuukubali Uislamu. Mbali na hili, ujana si lazima kutanguliwa na hekima. Utu uzima huchukuliwa maanani kuhusiana na utekelezaji wa wajbat za kidini, lakini sio mambo yanayohusiana na hekima. Imani inahusiana na mambo yanayo endana na hekima na sio sheria za kidini. Hivyo Imani ya Ali wakati wa utoto ni sifa kwa ajili yake kama vile Allah anavyotuambia katika Qurani Tukufu kuhusu Isa katika maneno haya: Hakika mimi ni Mtumishi wa Allah: Allah amenipa kitabu na amenifanya Nabii. (19:30). Vilevile katika Sura hiyo anasema kuhusu Mtume Yahaya: Na tulimpa hekima angali mtoto. (19:12). Seyyed Ali Humairi Yamani, (alikufa 179 A.H.) anaonyesha ukweli huu katika mashairi yake. Ansema: Kama vile Yahaya alivyofikia cheo cha Utume katika utoto wake, Ali ambaye alikuwa mrithi wa Mtume na baba wa watoto wake, vilevile alifanywa mwakilishi wa Allah na mlezi wa watu akingali mtoto. Sifa na heshima inayotolewa na Allah haitegemei juu ya umri. Hekima na akili hutegemea juu ya hali ya kuzaliwa. Nashangazwa na maelezo yako kwa vile hoja kama hizo zilitolewa na Manasibi na Makhariji kwa kuchochewa na Bani Umayya. Waliishusha imani ya Ali kwamba ilikuwa ya utii wa kibubusa kwa yale aliyofundishwa. Hata wanachuo wenu wameikubali sifa ya Ali kwa namna hii. Muhammad bin Talha Shafii, Ibn Sabbagh Maliki, Ibn Abil-Hadid na wengine wamenukuu mashairi ya Ali. Katika moja ya mashari yake anasema: Nilikuwa wa kwanza na wa mbele zaidi miongoni mwenu katika kuukubali Uislamu wakati nilipokuwa mtoto mdogo tu. Kama imani ya Ali katika umri mdogo kama huo haikua bora, Mtume asingeielezea namna hiyo. Sulayman Balkhi Hanafi katika Yanabiul-Mawadda, Sura ya 55, uk. 202, anasimulia kutoka kwa Ahman Bin Abdullah
138
Mikesha ya Peshawar
Shafii akinukuu kutoka kwa Khalifa wa pili, Umar Bin Khattab, ambaye alisema: Abu Bakr, Abu Ubaida Jarra na Kundi la watu waliokuwepo pamoja na Mtume wa Allah aliposhika bega la Ali na kusema: Ewe Ali! Wewe ni wa kwanza na wa mbele zaidi miongoni mwa waumini wote na Waislamu katika kuukubali Uislamu, Wewe kwangu mimi ni kama alivyokuwa Harun kwa Musa. Vilevile Imam Ahmad Bin Hanbal anasimulia kutoka kwa Ibn Abbas, ambaye amesema yeye, Abu Bakr, Abu Ubaida Bin Jarra, na wengine walikuwa pamoja na Mtume wakati alipoweka mkono wake katika bega la Ali na akasema: Wewe uko mbele zaidi katika imani ya Uislamu miongoni mwa Waislamu wote, na uko kwangu Mimi kama Harun alivyokuwa kwa Musa, Ewe Ali! Anayefikiria kwamba mimi ni rafiki yake ambapo ni adui yako, huyo ni muongo. Ibn Sabbagh Maliki ameandika hadith kama hiyo katika Fusulul-Muhimma, uk. 125, kutoka Khasa-isul-Alawi kama simulizi ya Abdullah bin Abbas, na Imam Abu AbdurRahman Nisai anaeleza katika Khasaisul-Alawi kwamba alisema: Nimemsikia Umar bin Khattab akisema, Litajeni jina la Ali kwa heshima kwa sababu nimemsikia Mtume akisema kwamba Ali anazo sifa tatu. Mimi (Umar) natamani kwamba ningelikuwa na moja tu kati ya hizo kwa sababu kila moja ya sifa hizo ni yenye thamani kubwa sana kwangu kuliko kitu chochote katika ulimwengu huu. Ibn Sabbagh amesimulia kama ifuatavyo kwa nyongeza ya walivyoandika wengine. Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alisema kuhusu Ali, Yeye ambaye anakupenda wewe hunipenda mimi, na ambaye ananipenda mimi, Allah Humpenda, na yeyote apendwaye na Allah, humuingiza Peponi. Lakini yule ambaye ni adui kwako ni adui kwangu, na ambaye ni adui kwangu, Allah ni adui kwake na humhukumu kwenda Motoni. Kujitangaza kwa Ali kuwa Mwislamu hata ambapo alikuwa bado mdogo huthibitisha ubora wa hekima na sifa yake, ambayo hakuna Mwislamu mwingine anayeweza kuipata. Tabari katika kitabu chake cha Tarikh ananukuu kutoka Muhammad Bin Saad Bin Abi Waqqas, ambaye alisema: Nilimuuliza Baba yangu iwapo Abu Bakr alikuwa wa kwanza wa Waislamu. Yeye akasema, Hapana, zaidi ya watu hamsini waliingia Uislam kabla ya Abu Bakr; bali alikuwa mbora kwetu kama Mwislam. Vilevile anaandika kwamba Umar Bin Khattab aliingia Uislamu baada ya wanaume arobaini na tano na wanawake ishirini na moja. Ama kwa aliyekuwa mbele zaidi katika Uislamu na Imani, alikuwa ni Ali Bin Abi Talib.
139
Mikesha ya Peshawar
140
Mikesha ya Peshawar
141
Mikesha ya Peshawar
Baba yake akajibu, Yeye ni katika dhuria watukufu wa Mtume. Hatuwezi kutaja jina lake (kwa jinsi alivyo maarufu) sambamba pamoja na watu wale. Tunaona katika Qurani Tukufu kwamba katika aya ya Mubahila, Ali anatajwa kama nafsi ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Kuna hadithi yenye kuunga mkono habari hii, ambayo imeandikwa katika Mawadda ya 7 hiyohiyo, iliyosimuliwa kutoka kwa Abdullah Bin Umar Bin Khattab. Alisema kwamba siku moja walipokuwa wakihesabu majina ya masahaba, yeye alimtaja Abu Bakr, Umar, na Uthman. Mtu mmoja akasema, Ee Abdur-AbdurRahman! Kwa nini umeliacha jina la Ali? Yeye alijibu Ali ni mmoja wa dhuria wa Mtume. Hawezi kuchanganywa na mtu yoyote yule. Yuko katika kundi namna moja na Mtume wa Allah. Ngoja nisimulie hadith nyingine kutoka katika Mawadda hiyo hiyo. Imesimuliwa kutoka kwa Jabir Bin Abdullah Ansari kwamba siku moja wakiwepo mbele ya Muhajirina na Ansari, Mtume alimwambia Ali: Ewe Ali! Kama mtu atatekeleza Sala zake kamili kwa Allah, na kisha akatia shaka kwamba wewe na familia yako ni bora kwa viumbe wengine wote, makazi yake yatakuwa Jahanam. (Baada ya kusikia hadith hii, wale wote waliokuwepo pale, hususan Bw. Hafidhi, walionyesha kutubu, isije wakawa miongoni mwa wenye kutia mashaka). Nimerejea hadith chache tu. Chaguo lenu linaelekea kuwa ni kuzikataa hadith zote hizi sahihi, ambazo zimeandikwa kwenye vitabu vyenu, au kukubali kwamba imani ya Ali ilikuwa bora kuliko ile ya masahaba wote, pamoja na ya Abu Bakr na Umar. Vilevile naomba muiangalie hadith hii (inayokubaliwa na madhehebu zote) ambamo Mtume alisema wakati wa Ghazawa-e-Ahzab (hujulikana vilevile kama vita vya Handaq), wakati Ali alipomuua Amru Ibn Abdu-e-Wudd kwa pigo moja la upanga wake: Pigo moja la Ali katika vita vya Khandaq limempatia fadhila zaidi kuliko malipo ya matendo mema ya umma wote (majini na watu) mpaka Siku ya Hukumu. Kama pigo moja la upanga wake lilikuwa bora katika fadhila kuliko Sala za majini na watu zikichanganywa zote pamoja hakika ubora wake hauwezi kuhojiwa na yeyote isipokuwa na mashupavu waovu.
142
Mikesha ya Peshawar
Ama kwa nini Ali hakufuatana na Mtume katika usiku wa kuhama kutoka Makka, ni wazi kwamba Mtume alimkabidhi Ali majukumu muhimu zaidi. Hakuna aliyekuwa muaminifu kama Ali. Aliachwa nyuma kurudisha kwa wenyewe mali zilizowekwa amana kwa Mtume. (Jukumu la pili la Ali lilikuwa ni kuipeleka familia ya Mtume na Waislamu wengine Madina. Na hata ingawa Ali hakuwa pamoja na Mtume katika pango usiku ule, alitekeleza jukumu muhimu zaidi kwa vile alilala katika kitanda cha Mtume).
AYA YA QURANI YENYE KUMSIFU ALI KWA KULALA KWAKE KATIKA KITANDA CHA MTUME KATIKA USIKU WA HIJRA.
Wanachuoni wenu wenyewe wametaja sifa za Ali katika tafsir zao (za Qurani). Kwa mfano, Ibn Sabi Maghribi katika Shifaus-Sudur, Tibrani katika Ausat na Kabir, Ibn Athir katika Usudul-Ghaiba, Jz. 4, uk. 25, Nurud-Din Sabbagh Maliki katika FusulilMuhimma Fi Marifatil-aimma, uk. 33, Abu Ishaq Thalabi, Fazil Nishapuri, FakhrudDin Radhi na Jalalud-Dini Suyuti, kila mmoja katika Tafsir yake, Hafidh Abu Nuaim Isphahani, muhadithina maarufu wa Ki-Shafii katika Ma-Nazalal-Quran fi Ali, Khatib Khawarizmi katika Manaqib Sheikhul-Islam Ibrahim bin Muhammad Hamwaini katika Faraid, Muhammad bin Yusuf Ganji Shafii katika Kifayatut-Talib, Sura ya 62, Imam Ahmad bin Hanbal katika Musnad, Muhammad bin Jarir kupitia vyanzo mbalimbali, Ibn Hisham katika Siratun-Nabi, Hafidh Muhadith wa Damascus katika Arbain Tiwal, Imam Ghazali, katika Ihyaul-Ulum, Jz. 3, uk. 223, Abus-Saadat katika Fadhailul-Iratit-Tahira, Ibn Abil-Hadid katika Sharhe Nahjul-Balagha, Sibt Ibn Jauzi katika Tadhikira na wengine katika maulamaa wenu mashuhuri, wanasimulia kwamba wakati Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alipokusudia, kwa amri ya Allah, kuondoka Makka na kwenda Madina, alimtaka Ali ajifunike shuka lake la kijani na alale katika kitanda chake. Kwa hiyo, Ali akalala pahali pa Mtume kisha Mwenyezi Mungu akawaambia Malaika Jibril na Mikael kwamba amewafanya wao kuwa ndugu, na kwamba mmoja wao ataishi muda mrefu kuliko mwingine. Aliwauliza ni nani alikuwa tayari kumpa ndugu yake maisha yake ya ziada, ambayo kadiri yake hakuna mmoja wao aliyejua. Walimuuliza (Allah) iwapo chaguo hilo ni wajibu. Walielezwa kwamba sio wajibu. Hakuna hata mmoja wao aliyechagua kuachana na maisha yake ya ziada. Kisha yakafuata maneno haya matukufu: Mimi nimeumba undugu kati ya mwakilishi wangu Ali na Mtume wangu Muhammad. Ali amejitolea kutoa mhanga maisha yake kwa ajili ya maisha ya Mtume. Kwa kulala katika kitanda cha Mtume, anayalinda maisha ya Mtume. Sasa ninyi wote mnaagizwa kwenda duniani kumuokoa kutokana na mbinu za uovu wa maadui.
143
Mikesha ya Peshawar
Kwa hiyo, wote wakaja duniani. Jibril akakaa kichwani kwa Ali na Mikaeli miguuni kwake. Jibril akasema, Hongera, Ewe mwana wa Abu Talib! ambaye kwako Mwenyezi Mungu anajivunia mbele ya Malaika Zake. Baada ya haya, Aya ifuatayo ikateremshwa kwa Mtume. Na kuna aina ya watu ambao hutoa maisha yao kuzitafuta radhi ya Allah; na Allah ni mwingi wa upole kwa waja (wake). (2:207). Sasa nakusihini waheshimiwa, kuingalia aya hii kwa uangalifu wakati mtakaporudi nyumbani usiku na kutoa uamuzi wenu wenyewe. Je, ubora kwa haki ni wa yule ambaye alibakia pamoja na Mtume katika safari ya siku chache, akionyesha woga na huzuni, au kwa yule ambaye alihatarisha maisha yake usiku ule kishujaa na kwa furaha, kwa ajili ya usalama wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Imam Jafar Askafi, mmoja wa maulamaa wakubwa na viongozi wa Mutazil, anathibitisha, (kama ilivyosimuliwa katika Sharhe ya Nahajul-Balagha na Abil-Hadid Jz. 3, uk. 269-281), kwamba kulala kwa Ali katika kitanda cha Mtume kulikuwa bora zaidi kuliko muda mfupi wa Abu Bakr aliokaa pamoja na Mtume. Anasema: Maulamaa wa Kiislamu kwa pamoja wanashikilia kwamba, kwa ukweli halisi, ubora wa Ali katika usiku ule ulitukuka mno kiasi kwamba hakuna mtu angeweza kuufikia isipokuwa Ishaka na Ibrahimu wakati walipokuwa tayari kutoa maisha yao mhanga katika kutii mapenzi ya Allah. (Wafasiri wengi, maulamaa na wanahistoria wanaamini kwamba alikuwa ni Ismail ambaye alijitoa mhanga na sio Ishaka). Katika ukurasa wa 271 wa Sharhe ya Nahajul-Balagha, maelezo ya Abu Jafar Askafi katika kumjibu Abu Athman Jahiz Nasib yameandikwa. Anasema: Nilikwisha kuthibitisha mapema kwamba kulala kwa Ali katika kitanda cha Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) katika usiku wa kuhama kulikuwa bora zaidi kuliko kule kwa Abu Bakr kubakia pamoja na Mtume katika Pango. Ili kusisitiza hoja yangu, nitaithibitisha katika mitazamo mingine miwili: Kwanza, Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) wa Allah akiwa na mkuruba wa karibu na wa siku nyingi na Ali, alimpenda mno. Kwa hiyo alihisi kupotea kwa upendo wakati walipotengana. Kwa upande mwingine, Abu Bakr alipata fursa ya kwenda pamoja na Mtume. Kwa vili Ali alikuwa na uchungu wa kutengana kwao, malipo yake yaliongezeka kwa sababu jinsi maumivu yanavyokuwa makali zaidi katika utumushi, ndivyo yanavyopata malipo makubwa zaidi. Pili, kwa vile Ali alikusudia kuondoka Makka na hata aliwahi mara moja kuondoka peke yake, hali yake kama raia kule iliongezeka kuwa ngumu. Hivyo wakati akiondoka Makka pamoja na Mtume, hamu yake ya kuondoka ilitimia. Kwa ajili hiyo hakuna ubora wa kimaadili kama huo kwa ajili yake kama ulivyo kwa Ali, ambaye alivumilia machungu makali katika kuhatarisha maisha yake mbele ya panga zilizochomolewa za maadui. Ibn Saba Maghrib anasema katika kitabu chake Shifaus-Sudur kuhusu ushujaa wa Ali: Kuna umoja kamili (wa makubaliano) miongoni mwa maulamaa wa Kiarabu kwamba katika usiku wa Hijra, kulala kwa Ali katika kitanda cha Mtume kulikuwa bora zaidi ya kutoka pamoja naye. Ali alijifanya mwenyewe mwakilishi wa Mtume na akahatarisha
144
Mikesha ya Peshawar
maisha yake kwa ajili ya Mtume. Hoja hii ni wazi mno kiasi kwamba kamwe hakuna hata mtu mmoja aliyeikataa isipokuwa wale waliopatwa na uwenda wazimu au ushabiki. Nitakomeshea hapa na kurudi kwenye nukta yangu muhimu. Umesema kwamba, maneno ya Qurani Wakali dhidi ya makafir (48:29) yanamuashiria Khalifa wa pili, Umar Bin Khattab. Lakini dai hili haliwezi kukubaliwa kwa sababu tu kwamba umesema hivyo. Ni lazima tuamue iwapo sifa hii ni katika tabia yake au laa. Kama ndivyo, niko radhi kuikubali. Kwa hakika ukali unaweza kuonyeshwa katika njia mbili: Katika majadiliano ya kidini ambayo kwayo kwa nguvu ya hoja, maulamaa wa upande mwingine wananyamazishwa. Pili, unaweza kuonyeshwa katika uwanja wa vita. Kwa kadiri mijadala ya kielmu ihusikanavyo, hakuna mfano hata mmoja katika historia ambapo Umar ameonyesha ukali wowote. Katika kiwango chochote, sijaona taarifa yoyote ya kihistoria yenye kuonyesha kwamba Umar alionyesha ukali katika majadiliano ya kielimu. Nitawashukuruni kama mtanionyesha mfano wowote. Kwa kweli, maulamaa wenu, wamekubali kwamba alikuwa ni Ali ambaye aliyatatua yale matatizo ngumu ya kisheria na kufutu masala ya kidini wakati wa kipindi cha Makhalifa watatu. Ingawaje Bani Umayya na wafuasi mbumbumbu wa Abu Bakr walibuni hadithi zisizo na idadi kwa niaba yao, hawakuweza kuficha ukweli kwamba wakati watu wa imani nyingine walipokuja kwa Abu Bakar, Umar, au Uthman, kutatua matatizo magumu, makhalifa hawa waliyapeleka matatizo hayo kwa Ali. Ali aliwapa majibu ya kuvutia kiasi kwamba watu wengi wasiokuwa Waislamu waliingia Uislamu. Ukweli kwamba Abu Bakr, Umar na Uthman walikubali ubora wa Ali unatosha kuthibitisha hoja yangu. Wanachuoni wenu wameandika kwamba Khalifa Abu Bakr alisema: Niondoeni, niondoeni, kwa vile mimi sio bora kuliko ninyi alimuradi Ali yuko kati yenu. Kwa uchache kabisa, takriban mara sabini, khalifa Umar alikiri: Kama Ali asingekuepo Umar angeangamia. Mazingira mengi yenye hatari yametajwa kwenye vitabu, lakini mimi sitaki kueleza sana juu ya nukta hii. Kunaweza kuwa na mambo mengi muhimu ya kujadili. Nawab: Ni habari gani zaweza kuwa za muhimu zaidi kuliko hii? Je, mambo haya yametajwa katika vitabu vyetu? Kama yametajwa tafadhali tueleze tupate kujua. Muombezi: Maulamaa waadilifu wa madhehebu yenu wanakubali kwamba, mara kwa mara Umar alikiri kwamba Ali alikuja kumuokoa.
145
Mikesha ya Peshawar
146
Mikesha ya Peshawar
hivyo. Umar akamueleza (maneno ya Hudhaifa) na Ali akasema: Hakuna ubaya wowote kuhusu maneno haya. Alichosema Hudhaifa ni sawa sawa: Haki maana yake kifo, ambacho anakichukia; fitna maana yake mali na watoto ambavyo anavitaka; na anaposema kwamba anashuhudia ambavyo hakuviona, hii ina maana kwamba anashuhudia upweke wa Allah, kifo, siku ya malipo, Pepo, Moto, daraja juu yake inayoitwa Sirat, ambavyo hakuna hata kimoja kati ya hivyo alichokiona. Anaposema anajifundisha kwa moyo ambacho hakikuumbwa, hii huashiria kwenye Qurani. Anaposema kwamba anasali bila wuudhu, hii huashiria katika kumswalia Mtume wa Allah (kumtakia rehema na amani) ambako kuna ruhusiwa bila wuudhu; wakati akisema anacho kitu duniani ambacho si kwa ajili ya Allah Mbinguni, hii huashiria kwa mke wake, kwa vile Allah hana mke au watoto. Kisha Umar akasema: Umar angepotea kama Ali asingetokea. Ganji Shafii anasema kwamba maelezo ya Umar yanathibitika kwa mujibu wa riwaya za wasimuliaji wengi wa hadith. Mwandishi wa Manaqib anasema kwamba Khalifa Umar, mara kwa mara alisema: Ewe Abul-Hasan! (Ali). Sitakuwa sehemu ya jamii bila wewe. Vilevile alisema: Wanawake hawana uwezo wa kuzaa mtoto kama Ali. Muhammad bin Talha Shafii katika Matalibus-Su-ul na Sheikh Sulayman Balkh Hanafi katika Yanabiul-Mawadda, Sura ya 14, akisimulia kutoka kwa Tirmidhi, ameandika riwaya yenye kinaganaga kutoka kwa Ibn Abbas ambapo mwisho wa riwaya hiyo anasema: Masahaba wa Mtume walikuwa wakitafuta hukumu za kidini kutoka kwa Ali, na walikubali maamuzi yake. Hivyo, Umar Bin Khattab alisema katika nyakati mbalimbali, Kama isingekuwa ni Ali, Umar angeangamia. Katika mambo ya kidini na mijadala ya kielimu Umar hakuonyesha ukali wowote. Kinyume chake, alikiri udhaifu wake mwenyewe na kumkubali Ali kama kimbilio lake. Hata Ibn Hajar Makki katika sura ya 3 ya Sawaiq-Muhriqa, akielezea kutoka kwa Ibn Sad anamnukuu Umar akisema: Naomba msaada wa Allah katika kuamua yale matatizo magumu ambayo kwamba Abul-Hasan (Ali) hayupo.
147
Mikesha ya Peshawar
ushindi mkubwa. Kwa sababu ya Umar, jeshi la Waislamu lilishinda vita vyao. Unamuita muoga na kusema kwamba alikimbia kutoka uwanja wa vita na kwamba kushindwa kwa jeshi la Kiislamu kulikuwa ni kwa sababu yake! Je, ni sahihi mtu wa hadhi kama yako kumsingizia Khalifa Umar? Muombezi: Nina wasiwasi kwamba umekosea. Ingawa umekuwa na mimi kwa mikesha mingi, hujanielewa bado. Pengine unafikiria ni kwa sababu ya chuki kwamba ndio ninalaumu au kusifu watu. Sio hivyo. Kuna kuwiwa kukubwa katika mijadala ya kidini, ambako kumekuwa ni chanzo cha upinzani miongoni mwa Waislamu kwa karne nyingi. Mijadala kama hiyo mara kwa mara uchochea hali ya uovu, ambayo haipatani na maamrisho ya Qurani. Qurani kwa uwazi inasema: Enyi ambao mmeamini! Jiepusheni sana na dhana (kama iwezekanavyo) kwani baadhi ya dhana katika hali nyingine ni dhambi. (49:12). Unafikiria kwamba maelezo yangu yamechochewa na uovu. Ukweli ni kinyume chake. Sijatamka neno kinyume cha ambavyo maulamaa wenu wameandika. Umesema hivi punde tu kwamba nimemtukana Khalifa Umar. Lakini kulikuwa hakuna hata chembe ya dalili ya matusi. Niliyosema yanaoana na kumbukumbu za Historia. Sasa nalazimika kutoa mtazamo ulio wazi ili kunyamazisha upinzani huu.
148
Mikesha ya Peshawar
Namna ya pili ya ushindi inahusiana na vile vita ambavyo vilipiganwa baada ya kifo cha Mtume. Ushindi huu ulikuwa ni kutokana na ushujaa wa maaskari mashuhuri wa Kiislamu na ubingwa wao wa kupanga. Lakini hapa hatuhusiki na ushindi wa Kiislamu wa wakati wa Ukhalifa wa Umar. Maudhui yetu ni kuhusu ujasiri wa Umar mwenyewe. Hauthibitishwi na ushahidi wowote wa kihistoria. Hafidh: Ni matusi kudai kwamba Umar alikimbia kutoka uwanja wa mapambano, na kwamba hii ilipelekea kushindwa kwa Waislamu. Muombezi: Kama kuonyesha ukweli wa kihistoria kuhusu mtu ni matusi, basi matusi haya yameandikwa na maulamaa wenu. Hafidh: Ni wapi maulamaa wetu walipoandika kwamba Khalifa Umar alikimbia kutoka Uwanja wa mapambano? Ni wakati gani alisababisha kushindwa kwa Waislamu?
149
Mikesha ya Peshawar
kumsifu Ali. Kuhusu lango la Khaibar, anasema: Je, umesikia hadithi ya ushindi wa Khaibar? Miujiza mingi imefunganishwa pamoja ambayo huchanganya hata akili zenyes busara! Hawa wawili (Abu Bakr na Umar) walikuwa hawana mapenzi kwayo, au maarifa, ya kubeba bendera (kuongoza jeshi). Hawakujua siri za kutunza heshima ya bendera, waliifunika na twezo na wakakimbia ingawa walijua kwamba kukimbia kutoka kwenye uwanja wa mapambano ni sawa sawa na ukafiri. Walifanya hivyo kwa sababu ya mmoja wa wanajeshi shujaa wa Kiyahudi, kijana mrefu na upanga wa wazi mkononi, akiwa amepanda juu ya farasi mwenye umbo refu, akiwashambulia kama mbuni dume aliyesisimuliwa, ambaye amepata nguvu kutokana na hewa ya msimu wa kuchipua na uoto wake wa mimea. Alikuwa kama ndege mkubwa ambaye amejipamba kwa rangi za kupendeza na aliyekuwa akienda kuelekea kwa mpenzi wake. Mngaro wa moto wa kifo kutoka kwenye upanga wake na mkuki uliangaza na kuwatishia watu wawili hawa. Ibn Abil-Hadid akizungumza nao (Abu Bakr na Umar) anaendelea kusema: Nakuombeeni msamaha juu yenu, kwa kule kushindwa na kukimbia kwenu, kwa vile kila mtu anachukia kifo na kupenda uhai. Kama wengine wote, ninyi pia hamkukipenda kifo ingawa hakuna kinga kutokana na kifo. Lakini hamkuweza kujihatarisha na kifo. Lengo langu sio kumkashifu mtu yeyote, ninasimulia ukweli wa kihistoria kuonyesha kwamba Khalifa hakuwa na ushujaa kama huo ambao angestahiki sifa ya Mkali dhidi ya Makafir. Ukweli ni kwamba yeye alikimbia kutoka uwanja wa mapambano. Sifa hii katika mjadala inamhusu Ali peke yake, ambaye katika kila vita alikuwa mkali dhidi ya makafiri. Ukweli huu umethibitishwa na Allah kwenye Qurani Tukufu. Yeye Anasema: Enyi mlioamini! atakayeiacha dini yake miongoni mwenu, basi hivi karibuni Mwenyezi Mungu ataleta watu wengine ambao atawapenda, nao watampenda, wanyenyekevu kwa waumini, na wenye nguvu kwa makafiri. Watapiganaia dini ya Mwenyezi Mungu, wala hawataogopa lawama ya wenye kulaumu. Hiyo ndiyo fadhila ya Mwenyezi Mungu, humpa amtakaye, na Mwenyezi Mungu ni Mweny wasaa, Mwenye kujua. (5:54-56). Hafidh: Inashangaza kwamba unajaribu kuhusisha aya hii na Ali. Hii inazungumzia waumini ambao wanazo sifa hizi na vipenzi wa Allah. Muombezi: Ingekuwa vizuri kama ungeniuliza ni hoja gani ningeweza kutoa kuunga mkono maneno yangu. Jibu langu ni kwamba kama aya hii ingeteremshwa katika kuwasifu waumini, wasingekimbia kamwe kutoka uwanja wa mapambano. Hafidh: Je, ni haki kuwalaumu waumini na masahaba wa Mtume (lawama) ya kukimbia kutoka kwenye hatari? Watu hawa walipigana kishujaa katika vita. Muombezi: Sio mimi niliyewaita Wakimbiaji. Historia inawaonyesha kama hivyo. Pengine umesahau kwamba katika vita vya Uhud na Hunain waumini wote na masahaba kwa ujumla, pamoja na masahaba wakubwa wa Mtume, walitafuta usalama kwa kukimbia.
150
Mikesha ya Peshawar
Kama ilivyosimuliwa na Tabrini na wengine, wao walimuacha Mtume peke yake kati ya makafiri. Je, inawezekana kwamba wale waliogeuka na kuwapa maadui migongo wakimuacha Mtume peke yake kuwakabili maadui walikuwa wapenzi wa Allah na Mtume Wake? Siko peke yangu katika kudai kwamba Aya hii iko katika kumsifu Ali. Abu Ishaq Imam Ahmad Thalabi, ambaye mnamchukulia kama mkubwa wa wasimuliaji wenu wa Hadith, anaandika katika kitabu chake Kashful-Bayan kwamba aya hii imeteremshwa katika kumsifu Ali kwa sababu hakuna mtu mwingine aliyekuwa na sifa zilizotajwa ndani yake. Hakuna mwanahistoria - wa kwetu au wa nje - ambaye ameandika kwamba katika vita 36 vilivyopiganwa na Mtume, Ali hakuserereka kamwe hata katika moja. Katika vita vya Uhud, wakati masahaba wengine wote walipokimbia, na jeshi la adui lenye askari 5000 likawashambulia Waislamu, mtu pekee aliyebakia kwenye sehemu yake mpaka ushindi ulipopatikana alikuwa ni Ali. Ingawa alijeruhiwa sehemu mbalimbali na kuvuja damu kwa wingi, aliwakusanya wale ambao walikuwa wamekimbia na kuendelea kupigana mpaka ushindi ulipopatikana. Hafidh: Huna aibu kuhusisha kukimbia kwa masahaba wakubwa? Masahaba wote kwa ujumla na hasa Abu Bakr na Umar kwa ushujaa walimzunguuka Mtume na kumlinda. Muombezi: Hukujifunza historia kwa uangalifu. Kwa ujumla, wanahistoria wameandika kwamba, katika vita vya Uhud Hunain na Khaibar masahaba wote walikimbia. Nimekueleza kuhusu Khaibar. Amma kuhusu Hunain, Hamid katika Jam-e-BanusSahihain na Halabi katika Siratul-Halabiyya, Jz. 3, uk. 123, anasema kwamba masahaba wote walikimbia isipokuwa wanne: Ali na Abbas walikuwa mbele ya Mtume, Abu Sufyan Bin Harith alishika hatamu za farasi wa Mtume, na Abdullah Bin Masud alisimama upande wake wa kushoto. Kukimbia kwa Waislamu huko Uhud hakukukataliwa na mtu yeyote. Muhammad bin Yusuf Ganji Shafii katika Kifayatut-Talib Sura ya 27, kwa vyanzo vyake mwenyewe, anamnukuu Abdullah Bin Masud akisema kwamba Mtume amesema: Wakati wowote Ali anapopelekwa peke yake katika pambano, nilimuona Jibril upande wake wa kulia, Mikael upande wake wa kushoto, na wingu likimfunika kutoka juu mpaka Allah Alipomfanya mshindi. Imam Abu Abdur-Rahman Nisai anasimulia hadith 202 katika kitabu chake Khasais-eAlawi kwamba Imam Hasan, akiwa amevaa kilemba cheusi alikuja kwa watu na akasimulia sifa za baba yake, akisema kwamba katika vita vya Khaibar, wakati Ali alipokwenda kuelekea ile ngome, Jibril alikuwa akipigana upande wake wa kulia na Mikael upande wake wa kushoto. Alimkabili adui kwa ushujaa mkubwa mpaka alipopata ushindi na akawa anastahiki mapenzi ya Allah.
151
Mikesha ya Peshawar
152
Mikesha ya Peshawar
andika hadith hii, hivyo kwamba Hakim anasema: Hadith hii imefikia hatua ya makubaliano ya pamoja. Tabrini anasema: Ushindi wa Ali katika Khaibar unathibitishwa na umoja wake. Wakati jeshi la Waislamu lilipoizingira ngome ya Khaibar, lilishindwa mara tatu chini ya uongozi wa Abu Bakr na Umar, na wakakimbia. Masahaba walivunjika moyo sana. Ili kuwatia moyo masahaba Mtume alitamka kwamba Khaibar itatekwa. Alisema: Kwa jina la Allah, kesho nitampa bendera mtu ambaye atarudi na ushindi. Ni mtu ambaye hushambulia kwa kurudia rudia na kamwe haondoki kwenye uwanja wa mapambano na kamwe harudi nyuma mpaka apate ushindi. Yeye anampenda Allah na Mtume Wake, na Allah na Mtume Wake, wanampenda yeye. Usiku ule masahaba hawakuweza kulala, wakifikiria ni nani angepewa upendeleo huu maalum. Asubuhi, kila mmoja alivaa nguo za kijeshi na wakajitokeza mbele ya Mtume. Mtume akauliza: Yuko wapi ndugu yangu na mtoto wa ami yangu, Ali Bin Abu Talib? Walimwambia: Ewe Mtume wa Allah, yeye anaumwa na macho sana kiasi kwamba hawezi hata kusogea. Mtume akamtuma Salman amuite Ali. Salman akamshika Ali mkono akampeleka kwa Mtume. Alimsalimia Mtume na baada ya kumrudishia salaam, Mtume akamuuliza, una hali gani Ewe Abul-Hasan? Akajibu, Yote ni kheri kwa baraka za Allah. Naumwa kichwa na maumivu makali katika macho kiasi kwamba siwezi kuona chochote. Mtume alimuomba aje karibu. Wakati Ali aliposogea karibu, Mtume aliweka mate ya kinywa chake mwenyewe kwenye macho ya Ali na akamuombea. Punde tu macho yake yakawa meupe na maumivu yake yakatoweka kabisa. Akampa Ali bendera ya ushindi. Ali alielekea kwenye ngome za Khaibar, akapigana dhidi ya Mayahudi, akauwa wanajeshi wao mashujaa kama vile Marhab, Harith, Hisham na Alqama, na akazishinda ngome za Khaibar zilizokuwa hazishindiki. Ibn Sabbagh Malik katika Fusulul-Muhimma uk. 21, amenukuu taarifa hii kutoka vitabu sita vya hadith, ambapo Muhammad bin Yusufu Ganji Shafii katika Kifayatul-Talib Sura ya 14, baada ya kuisimulia hadithi hii anasema kwamba mtunga mashairi mkuu wa Mtume, Hassan bin Thabit, alikuwepo wakati wa tukio hili. Alitunga mashairi kumsifu Ali: Ali alikuwa akiumwa macho. Kwa sababu kulikuwa hakuna tabibu, Mtume alimtibia kwa mate yake mwenyewe. Hivyo wote muuguzi na mgonjwa walibarikiwa. Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) amesema: Leo nitampa Bendera mpanda farasi aliye hodari mno, shujaa na muungwana, mwenzi wangu katika mapambano. Anampenda Allah na Allah anampenda; hivyo kupitia kwake Yeye Allah atatufanya tuzishinde ngome. Baada ya hili, akiwaacha wote pembeni, alimchagua Ali na akamfanya mrithi wake. Ibn Sabbagh Maliki anasimulia kutoka Sahih Muslim kwamba Umar bin Khattab amesema: Kamwe sijatamani kuishika bendera lakini siku ile nilikuwa na hamu kubwa nayo.
153
Mikesha ya Peshawar
Nilirudia rudia kujifanya nionekane mbele ya Mtume, nikitamani kwamba huenda pengine akaniita na kwamba nikaweza kubarikiwa heshima hii. Lakini alikuwa ni Ali ambaye aliitwa na Mtume na utukufu ukaenda kwake. Sibt Ibn Jauzi ameandika riwaya hii katika kitabu chake Tadhkira, uk. 15, na Imam Abdur-Rahman Ahmad Bin Ali Nisai katika Khasaisul-Alawi, baada ya kusimulia hadithi kumi na mbili juu ya habari ya Ali kushika bendera kule Khaibar, ananukuu riwaya hiyo katika hadith ya kumi na nane kuhusu matumaini ya Umar kuipata bendera. Vilevile Jalalud-Din Suyuti katika kitabu chake Tarikhul-Khulafa, Ibn Hajar Makki, katika Sawaiq na Ibn Shirwaini katika kitabu chake Firdausul-Akbar anasimulia kwamba Umar Bin Khattab amesema: Ali amejaaliwa mambo matatu na kama ningelikuwa na moja tu ningelipendelea kuliko ngamia wote walioko katika miliki yangu:Ndoa ya Ali na Fatima; kukaa kwake msikitini katika hali yoyote na hii haikuruhusiwa kwa yeyote isipokuwa Ali, na kushika kwake bendera katika vita vya Khaibar. Hoja yangu, kutegemea juu ya riwaya za Muhadithina wenu, inathibitisha kwamba maneno katika Aya - Yeye (Allah) anawapenda na wao vilevile wanampenda Yeye yanahumhusu Ali. Muhammad Bin Yusufu Ganji Shafii katika Kifayatut-Talib, Sura ya 13, anasimulia kwamba Mtume amesema: Kama mtu anataka kumtazama Adam, Nuh na Ibrahim, na amtazame Ali. Anasema kwamba, Ali ndiye yule anayesemwa na Allah katika Qurani Tukufu: Na wale ambao wako pamoja naye ni wakali dhidi ya makafiri, (na) wenye kuhurumiana wenyewe kwa wenyewe. (48:29). Ama kwa kauli yako kwamba kifungu cha maneno katika aya hii kuhurumiana wenyewe kwa wenyewe kinamhusu Uthman na huonyesha nafasi yake kama Khalifa wa tatu, hii haiungwi mkono na ushahidi wa kihistoria. Kwa kweli, tabia yake ilikuwa ni kinyume chake kabisa. Kuna hoja nyingi zenye kuthibitisha jambo hili, lakini nitasimama hapa. Mambo ambayo yangesemwa yanaweza kuchochea uhasama. Hafidh: Kama utaishia kwenye rejea sahihi tu, hakuna sababu kwa nini tuchukizwe. Muombezi: Nitataja tu baadhi ya hizo.
154
Mikesha ya Peshawar
Mtume (s.a.w.w.) na vilevile dhidi ya mwendo wa Abu Bakr na Umar. Madhehebu zote zinakubaliana kwamba katika Kamati ya Ushauri (Shura) ambayo kwayo alichaguliwa kuwa Khalifa, Abdur-Rahman Bin Auf alimlisha kiapo cha kutegemea juu ya kitabu cha Allah, Suna ya Mtume, na mwendo wa Abu Bakr na Umar. Moja ya masharti ya kiapo chake ilikuwa kwamba Uthman hatawaacha Bani Umayya kuingilia (mambo ya uongozi) wala hangewapa mamlaka yoyote. Lakini nafasi yake (ya uongozi) ilipoimarika aliyavunja masharti haya. Kwa mujibu wa Qurani Tukufu na hadith za kuaminika, kuvunja makubaliano (Mkataba) ni dhambi kubwa. Maulamaa wenu wenyewe wanasema kwamba Khalifa Uthman alivunja ahadi yake. Katika Ukhalifa wake wote alitenda kinyume na mwendo wa Abu Bakr na Umar. Aliwapa Bani Ummaya Mamlaka kamili juu ya maisha ya watu na mali zao.
155
Mikesha ya Peshawar
Alimwambia mwanae kwamba wamekuwa wafujaji. Kama utalinganisha mwendo wa ulaji mdogo wa Umar na matumizi ya kifujaji ya Uthman, utakubali kwamba mwendo wa maisha ya Uthman ulikuwa kinyume na kiapo chake katika ile Kamati ya Ushauri.
KHALIFA UTHUMAN ALIWAPA MOYO WATENDA MAOVU MIONGONI MWA BANI UMAYYA.
Uthmani vilevile aliwapa Bani Umayya mamlaka juu ya maisha na heshima za watu. Hatimaye, machafuko yalijitokeza katika ardhi za Waislamu. Aliwachagua watu wake anao wapendelea katika nafasi za juu kinyume na matakwa ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), Abu Bakr na Umar. Kwa mfano alimpa nafasi za juu ami yake, Hakam Bin Aas, mtoto wake, Marwan ambao wote walihamishwa na kulaaniwa na Mtume. Hafidh: Unaweza ukathibitisha kwamba walilaaniwa? Muombezi: Kuna njia mbili za kuthibitisha kwamba walilaaniwa. Allah aliwaita Bani Umayya Mti uliolaaniwa katika Qurani Tukufu (17:60). Imam Fakhurud-Din Razi, Tabari, Qartabi, Nishapuri, Suyuti, Shawkani, Alusi, Ibn Abi Hatim, Khatib Baghdad, Ibn Mardawaih, Hakim, Maqrizi, Baihaqi na wengine katika maulamaa wenu wanasimulia kutoka Ibn Abbas kwamba Mti uliolaaniwa katika Quan unahusu kabila la Umayya. Katika ndoto, Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) aliona nyani wakipanda na kushuka katika mimbari yake (na kufukuza watu kutoka Msikitini). Alipoamka, Malaika Jibril akateremsha Aya hii na kumueleza Mtume kwamba nyani wale walikuwa Bani Umayya, ambao watanyanganya Ukhalifa wake baada yake. Sehemu yake ya kusalia na mimbari vitabakia katika mamlaka yao kwa miezi elfu. Imam Fakhnid-Din Razi anasimulia kutoka Ibn Abbas kwamba Mtume alitaja jina la Hakam Bin Aas. Kwa hiyo amelaaniwa kwa vile anatokana na Mti uliolaaniwa. Kuna Hadith nyingi kutoka vyanzo vya Sunni kuhusu kulaaniwa kwao. Hakim Nishapuri, katika Mustadrak Jz. 4, Uk. 437 na Ibn Hajar Makki katika Sawaiq-e-Muhriqa, ananukuu kutoka kwa Hakim hadith ifuatayo kutoka kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Hakika muda mfupi tu familiya yangu itatawanyishwa na kuuawa na Umma wangu. Bani Umayya, Bani Mughira, na Bani Makhzum ni makatili zaidi katika maadui zetu. Mtume Akasema kuhusu Marwan, akiwa mtoto wakati huo, Huyu ni mjusi, mtoto wa mjusi, mwenye kulaaniwa, mtoto wa aliyelaaniwa. Ibn Hajar anaelezea kutoka kwa Umar bin Murratul-Jihni, Halabi katika SiratulHalabiyya, Jz. 1, uk. 337; Baladhuri katika Ansab, Jz. 5, uk. 126; Sulayman Balkhi katika Yanabiul-Mawadda; Hakim katika Mustadrak, Jz. 4, uk. 481; Damiri katika Hayatul-Haiwan, J. 2, uk. 291; Ibn Asakir katika kitabu chake cha Tarikh; Imamul-
156
Mikesha ya Peshawar
Haram Muhyid-Din Tabari katika Dhakhairul-Uqba na wengine wamesimulia kutoka kwa Umar bin Murratul-Jihni kwamba Hakam Bin Aas alitaka mazungumzo na Mtume. Mtume alipoitambua sauti yake, akasema: Muacheni aingie ndani. Laana iwe juu yake na juu ya kizazi chake, isipokuwa wale ambao wanaamini, na watakuwa wachache. Imam Fakhrid-Din Razi, katika kitabu chake Tafsir-e-Kabir, Jz. 5, akiandika kuhusu Aya ya Mti uliolaaniwa....... na namna yake, anarejea kwenye kauli ya Aisha ambaye alisema kumuambia Marwan: Allah alimlaani baba yako wakati upo kwenye mbegu zake za uzazi; hivyo na wewe vilevile ni sehemu yake yule ambaye amelaaniwa na Allah. Allama Masud, anasema katika kitabu chake Murujudh-Dhahab, Jz. 1, uk. 435, kwamba Marwan bin Hakam alilaaniwa na kuhamishwa na Mtume. Alihamishwa kutoka Madina. Hakuruhusiwa kuingia Madina wakati wa Ukhalifa wa Abu Bakr na Umar, lakini Uthman alipokuwa Khalifa, alitenda kinyume cha mafundisho ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), Abu Bakr, na Umar na akamruhusu kuingia Madina. Alimuweka karibu sana naye mwenyewe pamoja na Bani Umayya wote na akawafanyia upendeleo. Nawab: Hakam Bin Abil-Aas alikuwa ni nani, na kwanini alihamishwa na Mtukufu Mtume (s.a.w.w.)? Muombezi: Hakam Bin Aas alikuwa ni ami yake Khalifa Uthman. Kwa mujibu wa Tabari, Ibn Athir, na Baladhuri, ambaye anaandika katika Ansab, Jz. 5, uk. 17, yeye alikuwa ni jirani yake Mtume Zama za Jahiliyya. Alimtukana Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), hususan baada ya tangazo lake la Utume. Alitembea nyuma ya Mtume na kumdhihaki kwa kumuigiza miondoko ya utembeaji wake. Hata wakati wa Sala, alikuwa akimyooshea kidole kwa dharau. Baada ya kulaaniwa na Mtume, alibakia katika hali ya kupooza wakati wote na hatimaye akapoteza hali ya utimamu akili. Baada ya kutekwa Makka, alikuja Madina na inavyoonekana aliingia Uislamu, lakini mara kwa mara alimtukana Mtume. Wakati alipokwenda nyumbani kwa Mtume, Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) mara moja alitoka nje ya nyumba yake na akasema Mtu yeyote asiombe msamaha kwa niaba yake. Sasa yeye na watoto wake, Marwan na wengine wanapaswa waondoke Madina. Kwa hiyo, mara moja Waislamu wakamtoa na kumfukuzia Taif. Wakati wa kipindi cha Abu Bakr na Umar, Uthman alimsaidia, akisema kwamba alikuwa ni ami yake na kwamba inapaswa aruhusiwe kurudi Madina. Lakini hawa wengine hawakulikubali shauri hili, wakisema kwamba kwa vile alilaaniwa na kuhamishwa na Mtume hawatamruhusu kurudi. Wakati Uthman alipokuwa Khalifa, aliwarudisha wote. Ingawa watu wengi walilipinga shauri hili; Uthman alionyesha upendeleo maalum kwa jamaa zake na wengine anaowapenda. Alimfanya Marwan kuwa msaidizi wake na Afisa Mkuu wa Baraza lake. Alijikusanyia karibu yake waovu wengi wa kabila la Umayya na akawateua kushika nafasi za juu (katika serikali). Matokea yake ni kwamba, kwa mujibu wa utabiri wa Umar, wao
157
Mikesha ya Peshawar
ndio walihusika na janga lililompata Uthman. Miongoni mwa watu walioteuliwa na Uthman alikuwa Walid bin Aqaba bin Abi Muith ambaye alipelekwa Kufa kuwa Gavana. Kwa mujibu wa riwaya ya Masud katika Murujudh-Dhahab, Jz. 1, Mtume alisema kuhusu Walid: Hakika yeye ni mmoja wa wale watakaokwenda motoni. Alijitumbukiza waziwazi kabisa katika matendo maovu. Kwa mujibu wa maelezo ya Masud katika MurujudhDhahab, Abdul-Fida katika Tarikh yake, Suyuti katika Tarikhul-Khulafa, uk. 104, Abul-Faraj katika Aghani Jz. 4, uk. 128, Imam Ahmad bin Hanbal katika Musnad, Jz. 1, uk. 42 Yaqubi katika Tarikh yake Jz. 2, uk. 142; Ibn Athir vilevile katika UsudulUqba, Jz. 5, uk. 91 na wengine walisema kwamba, wakati wa ugavana wake huko Kufa, Walid alipitisha usiku mzima akifanya ufuska. Alikuja msikitini kwa ajili ya Sala ya Alfajiri akiwa amelewa na akasalisha rakaa nne za Sala ya asubuhi (badala ya mbili) kisha akawageukia watu na kusema Uzuri ulioje wa asubuhi hii! Ningetaka kuendeleza Sala hii kama mutaridhia. Baadhi wanasema kwamba alitapika kwenye kibla ya msikiti kitendo ambacho kilileta maudhi makubwa kwa watu ambao walilalamika kwa Khalifa Uthman. Mmoja wa watu hawa wanaojulikana sana ni Muawiya, ambaye alifanywa kuwa Gavana wa Syria. Walid aliondolewa na badala yake akateuliwa Said Bin Aas kama Gavana wa Kufa. Wakati watu walizipogundua sera za Uthman, sera zilizo kinyume na mafunzo ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), walighadhibika. Walichukuwa hatua ambazo hatimae zilisabisha matokeo yake mabaya kama hayo. Uthman alihusika na kifo chake mwenyewe kwa sababu hakufikiria athari za matendo yake. Alipuuza ushauri wa Ali na akawa amepotezwa na wadanganyifu wenye kujipendekeza. Ibn Abil-Hadid ananukuu mazungumzo kati ya Umar na Ibn Abbas katika Sherhe ya Nahjul-Balagha, Jz. 3, uk. 106. Khalifa Umar alisema kitu kuhusu kila mmoja wa wajumbe sita wa Kamati ya Ushauri na akaonyesha udhaifu wao. Wakati jina la Uthmani lilipotajwa, baada ya kushusha pumzi mara tatu, Umar akasema kwamba, Kama Ukhalifa utamfikia Uthman atawaweka watoto wa Abi Muit (Bani Umayya) juu ya watu. Kisha Waarabu watasimama na kuasi dhidi yake na kumuua. Ibn Abil-Hadid anakubaliana na uchambuzi wa Umar. Wakati Uthman alipokuwa Khalifa aliwakusanya karibu yake Bani Umayya. Aliwateuwa kuwa magavana na wakati walipoyachezea vibaya mamlaka yao, alifumba macho. Khalifa Uthman hakutaka hata kujinasua mwenyewe kutokana na Marwan. Watu wakichemka kwa kutoridhika, waliasi dhidi yake na mwishowe wakamuua.
158
Mikesha ya Peshawar
MTUKUFU MTUME (S.A.W.W.) ALIWALAANI ABU SUFYAN, MUAWIYA NA MTOTO WAKE YAZID.
Itasaidia sana kama utasoma kitabu maarufu cha Historia cha Jarir Tabari, mmoja wa maulamaa wenu wakubwa, ambaye ameandika: Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alimuona Abu Sufyani akiwa amepanda punda. Muawiya alikuwa anaivuta kwa mbele, na mtoto wake Yazid, alikuwa anaisukuma kwa nyuma. Mtume akasema: Laana iwe juu ya mpandaji, mvutaji na msukumaji. Maulamaa wenu mashuhuri, kama Tabari na Ibn Asam Kufi wamemuona Khalifa Uthman kuwa ni mwenye makosa kwa kutomuua Abu Sufyan wakati alipoukana Uislamu, Wahyi (ufunuo), na kuwepo kwa Jibril. Baada ya kumkemea Abu Sufyan kidogo, Uthman akalitupa kando suala hili. Nitawaomba vilevile muangalie Khutba ya 163 ya Nahjul-Balagha na simulizi ambayo Ibn Abil-Hadid katika Sherhe yake ya Nahjul-Balagha Jz. 2, (iliyochapishwa Misr) uk. 582, ananukuu kutoka Tarrikh-e-Kabir, ya Tabari kwamba baadhi ya masahaba katika majimbo mbalimbali waliandika barua wakishawishi watu kutangaza vita vya Jihad, ili kujilinda kutokana na uonevu wa kikatili wa Uthman. Katika mwaka 34 A.H. watu wenye malalamiko dhidi ya maofisa walioteuliwa na Uthman walikuja Madina kwa Ali na wakamuomba aingilie kati.
159
Mikesha ya Peshawar
ameeleza kwamba, Khalifa Umar alisisitiza kwamba Abdullah abakie naye kwa sababu alikuwa na elimu kamili ya Qurani Tukufu na kwa sababu Mtume alimsifia sana. Ibn Abil-Hadid na wengine wameandika jambo hilo hilo. Maulamaa wenu wanakubali kwamba wakati Uthman alipokusudia kukusanya Qurani Tukufu, alichukuwa nakala zote kutoka kwa waandishi. Alidai vilevile nakala ya Qurani Tukufu kutoka kwa Abdullah bin Masud. Abdullah hakumpa nakala yake hiyo. Uthman alikwenda mwenyewe nyumbani kwake na akaichukuwa hiyo nakala ya Qurani Tukufu kutoka kwake kwa nguvu. Baadae wakati Abdullah alipogudua kwamba, kama ilivyofanywa kwa nakala nyingine za Qurani Tukufu, na nakala yake pia imechomwa moto, alihuzunika mno. Katika mikusanyiko ya kijamii na kidini alisimulia hadith za shutuma ambazo alizijua kuhusu Uthman. Wakati habari hizi zilipomfikia Uthman, aliamrisha watumwa wake, wakampiga sana kiasi kwamba meno yake yalivunjika na alibakia kitandani. Baada ya siku tatu alikufa kwa majeraha yake. Ibn Abil-Hadid anaandika kwa kina kuhusu ukweli huu kutoka Jz. 1, uk. 67 na 226 wa Sharh Nahjul-Balagha (iliyochapishwa Misir) chini ya Tan VI na akaendelea kusema kwamba Uthman alikwenda kumuangalia Abdullah aliyekuwa anaumwa. Walizungumza pamoja kwa muda. Uthman akasema, Ewe Abdur-Rahman! Niombee msamaha kwa Allah. Abdullah akasema, Namuomba Allah achukue haki yangu kutoka kwako. (yaani haki ifanyike). Wakati Abu Dharr, sahaba wa karibu wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), alipohamishiwa Rabza, Abdullah alikwenda kumuaga. Kwa sababu hii, Abdullah alipigwa viboko arubaini. Hivyo Abdullah akamsisitizia Ammar Yasir kwamba Uthman asikubaliwe kumsalia Abdulla Sala ya jeneza. Ammar Yasir alikubali, na baada ya kifo cha Abdullah, alisali Sala ya jeneza pamoja na kikundi cha masahaba. Uthman alipogundua mpango huu wa mazishi, alikuja kwenye kaburi la Abdullah na akamuuliza Ammar kwanini alisali Sala ya jeneza. Akajibu kwamba alilazimika kufanya hivyo kwa sababu Abdullah aliusia hivyo.
160
Mikesha ya Peshawar
wako. Wameyatuma kwako kupitia kwangu. Baada ya kusoma misitari michache, Uthman akaitupa ile barua chini. Ammar akasema: Ilikuwa sio vizuri kwako wewe kufanya hivyo. Barua kutoka kwa masahaba wa Mtukufu Mtume wa Allah (s.a.w.w.) inastahiki heshima. Kwa nini umeitupa chini? Ingelikuwa vizuri kwako wewe kuisoma na kuijibu. Unaongopa Uthman alisema kwa sauti kali. Kisha akaamuru watumwa wake kumpiga, na Uthman mwenyewe akampiga teke la tumbo. Alianguka chini, akazimia; jamaa zake wakaja wakamchukua, wakampeleka kwenye nyumba ya Ummul-MuMinin Umm Salma (mmoja wa wake za Mtume). Kuanzia adhuhuri mpaka usiku wa manane alikuwa bado amezimia. Makabila ya Hudhail na Bani Makhzun waligeuka dhidi ya Uthman kwa sababu ya ukatili wake kwa Abdullah Bin Masud na Ammar Yasir. Uthman alikuwa katili vilevile kwa Jandab Bin Junada, anayejulikana kama Abu Dhar Ghifari, mmoja wa masahaba karibu mno wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) na mtu mwenye elimu. Muhadithina wakubwa na wanahistoria wa madhehebu zote wamesimulia kwamba mzee huyu wa miaka tisini alihamishwa isivyo halali kutoka sehemu hii kwenda sehemu nyingine kwa fedheha kubwa - kutoka Madina kwenda Syria, kutoka Syria kwenda Madina tena, kisha kutoka Madina kwenda kwenye Jangwa la Rabza. Alipanda ngamia asiye na matandiko akifuatana na binti yake tu. Alikufa katika (jangwa) la Rabza katika hali ya umasikini na ya kutelekezwa. sMaulamaa na wanahistoria wenu wakubwa, pamoja na Ibn Sad katika Tabaqat, Jz. 4, uk. 168, Bukhari katika Sahih yake, mlango wa Kitab-e-Zaka; Ibn Abil-Hadid katika Sherhe yake ya Nahjul-Balagha, Jz. 1, uk. 240 na Jz. 2, uk. 375 87, Yaqubi katika kitabu chake cha Tarikh Jz. 2, uk. 148; Abul-Hasan Ali Bin Husain Masud, muhadithina na mwanahistoria mashuhuri wa Karne ya Nne katika kitabu chake MurujudhDhahab, 1, uk. 438; na wengine wengi wamesimulia ukatili wa Uthman. Imeelezwa kwa mapana jinsi gani alivyomfanyia ubaya Abu Dharr mtu mwenye moyo safi, mtu aliyependwa na Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), na vilevile jinsi gani Abdullah Bin Masud, Hafidh na mwandishi wa Wahyi, alivyopigwa viboko arobaini kwa sababu alikwenda kumuaga Abu Dharr Ghifari. Hali ya ufidhuli wa aina hiyo hiyo ulionyeshwa kwa Ali kwa sababu hizo hizo. Hafidh: Kama Abu Dharr alipatishwa mateso, ni kwa sababu ya maofisa wakorofi. Khalifa Uthman, ambaye alikuwa mpole sana na mwenye moyo laini, alikuwa hana habari na matukio haya. Muombezi: Utetezi wako kwa Khalifa Uthman ni kinyume na ukweli. Mateso aliyopata Abu Dharr ilikuwa ni kwa ajili ya amri za wazi za Uthman mwenyewe. Kuthibitisha ukweli huu, anachohitaji mtu ni kurejea kwa Maulamaa wenu tu. Kwa mfano unaweza
161
Mikesha ya Peshawar
ukaangalia Nihaya kitabu cha Ibn Athir, Jz.1, na kitabu chake, Tarikh-e-Yaqubi na hususan uk. 241 wa Jz. 1, ya Sharhe Nahjul-Balagha cha Ibn Abil-Hadid. Wanachuoni hawa wameinakili barua ya Uthman iendayo kwa Muawiyya. Wakati Muawiyya alipopeleka taarida yenye uovu dhidi ya Abu Dharr kutoka Syria, Uthman alimuandikia hivi: Mlete Jundab (Abu Dharr) kwangu juu ya ngamia asiye na matandiko, peke yake, na mtu katili atakayemswaga ngamia huyo mchana na usiku. Wakati alipofika Madina, miguu yake Abu Dharr ilikuwa imechubuka na kutoa damu. Na bado Maulamaa wenu wamesimulia hadith isemayo kwamba Abu Dharr alitajwa makhususi kabisa na Mtume kama mtu ambaye kila mwanadamu lazima ampende. Hafidh Abu Nuaim Isfahani katika Hilyatul-Auliya, Jz. 1, uk. 172; Ibn Maja Qazwini katika Sunan yake Jz. 1, uk. 66; Sheikh Sulayman Balkhi Shafii katika YanabiulMawadda, Sura ya 59, akisimulia hadithi ya tano kati ya hadith arobaini zilizoandikwa katika Sawaiq-Muhriqa na Ibn Hajar Makki kama sahihi, zikiwa zimechukuliwa kutoka kwa Tirmidhi na Hakim, kama ilivyosimuliwa na Buraida, na yeye kutoka kwa baba yake; Ibn Hajar Asqalani katika Isaba, Jz. 3, uk. 455; Tirmidh katika Sahihi yake, Jz. 2, uk. 213; Ibn Abdil-Birr katika Istiab, Jz. 2, uk. 557; Hakim katika Mustadrak, Jz. 3 uk. 130; na Suyuti, katika Jamus-Saghir wamesimulia kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) amesema: Allah ameniamrisha mimi kuwapenda watu wanne; na amenijulisha kwamba Yeye pia anawapenda. Watu wakasema Ewe Mtume wa Allah tueleze majina yao. Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akasema Ni Ali, Abu Dharr, Miqdad, na Salman. Je, haki itaruhusu kwamba watu kama hao wapendwao na Allah kutendewa ukatili hivyo na kuyaita matendo hayo kuwa ni huruma? Hafidh: Historia imesimulia kwamba Abu Dharr alikuwa mtu mvurugaji. Aliendesha propaganda kali huko Syria yenye kumpendelea Ali, akawatanabahisha watu wa Syria juu ya cheo cha Ali, na akasema kwamba alikuwa amemsikia Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akisema kwamba Ali alikuwa ndiye mrithi wake. Kwa sababu aliwaita wengine wanyanganyi na akasema kwamba Ali alikuwa Khalifa wa haki aliyeteuliwa na Allah, Khalifa Uthman, ili kulinda umoja na kuepusha matatizo, alilazimika kumuita kutoka Syria (arudi Madina). Kama mtu anajaribu kusababisha fitna miongoni mwa watu, ni jukumu la Khalifa kumuondoa kutoka sehemu hiyo. Muombezi: Kama mtu anasema kweli, ni haki kumhamisha na kumtesa kwa sababu anafanya hivyo? Je, Uislamu unaturuhusu kumlazimisha mtu mzee kupanda ngamia aliyekonda, asiye na matandiko, ikiswagwa kwa nguvu na mtumwa mwenye harara, bila kusimama kwa ajili ya kupumzika, hivyo kwamba anawasili mashukio yake akiwa amechubuka na kuvuja damu? Je, hii inaonyesha upole na moyo wa wema? Mbali na hilo kama Uthman alitaka kudumisha umoja na kuepusha matatizo kwa nini asiwaondoe Bani Umayya wahalifu, kama Marwan, ambaye alilaaniwa na kuhamishwa na Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) na Walid mpotovu na fuska wa dhahiri (afanyaye maovu bila kuficha) ambaye alisalisha akiwa amelewa na ambaye alitapika kwenye kibla ya msikiti? Kwa nini asi-
162
Mikesha ya Peshawar
waondoe wanasiasa madhalimu kutoka kwenye serikali yake, watu ambao wamewaonea watu, ambao mwishowe wakaasi na kumuuwa Uthman. Hafidh: Unawezaje kusema kwamba Abu Dharr alisema kweli? Unajuaje kwamba aliyosema yako katika misingi ya elimu iliyo sawa na kwamba hakubuni hadithi kwa jina la Mtukufu Mtume (s.a.w.w.)? Muombezi: Tunasema hivyo kwa sababu Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) mwenyewe alithibitisha ukweli wa Abu Dharr. Maulamaa wenu wenyewe wameandika kwamba Mtume alisema: Abu Dharr miongoni mwa watu wangu ni kama Isa miongoni mwa Bani Israil katika ukweli, utii na Ucha Mungu. Muhammad Bin Sad mmoja wa Maulamaa wa cheo cha juu na muhadithina wa madhehebu yenu, ndani ya Tabaqat, Jz. 4, uk. 167168; Ibn Abdul-Birr katika Istiab, Jz. 1, Sura ya Jundab, uk. 84; Tirmidh katika Sahih yake Jz. 2, uk. 221; Hakim katika Mustadrak, Jz. 3, uk. 342; Ibn Hajar katika Isaba Jz. 3, uk. 662; Muttaqi Hindi katika Kanzul-Ummal, Jz. 6, uk. 169; Imam Ahmad Bin Hanbal katika Musnad Jz. 2 uk.163 na 175; Ibn Abil-Hadid katika Sherhe NahjulBalagha Jz. 1, uk. 241; kutoka kwa Mahidi; Hafidh Abu Nuaim Isfahani katika Hilyatul-Auliya na mwandishi wa Lisanul-Arab, juu ya vyanzo mbali mbali vya kutegemewa wamesimulia kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alisema: Ardhi haikuzaa wala mbingu haikufunika mtu muaminifu zaidi kuliko Abu Dharr. Kama Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) anathibitisha uaminifu wa mtu, tunaweza kuwa na uhakika kwamba mtu yule alisema kweli. Wala Allah hamuiti mtu mpenzi wake, yule ambaye ni muongo. Kama kungalikuwa na mfano mdogo tu wa Abu Dharr kusema uwongo, Maulamaa wa mwanzo wa madhehebu yenu wangeuandika kama walivyoandika kuhusu Abu Huraira na wengine. Mtume alithibitisha uaminifu wake na vilevile akatabiri mateso yake. Hafidh Abu Nuaim Isfahani katika Hilyatul Auliya, Jz. 1 uk. 162, anasimulia kutoka vyanzo vyake mwenyewe kwamba Abu Dharr alisema kwamba alikuwa amesimama mbele ya Mtume wakati alipomuambia: Wewe ni mcha-Mungu, mara tu baada yangu utapatwa na shida. Nikauliza: Katika njia ya Allah? Akasema: Ndio, katika njia ya Allah! Nikasema: naikaribisha (naikubali) amri ya Allah! Hakika shida aliyopata sahaba mtukufu Abu Dharr katika jangwa kwa amri ya Muawiyya, Uthman na jamaa zao Bani Umayya ilikuwa ni shida ile ile aliyotabiri Mtukufu Mtume (s.a.w.w.).
163
Mikesha ya Peshawar
huzuni, wewe unamtetea mkosaji! Yakupasa ama upuuze maelezo ya maulamaa wenu, au ukubali sifa zilizotajwa katika aya iliyo katika mjadala kwamba hazihusiani na wale waliowatesa masahaba watukufu wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Hafidh: Abu Dharr alichagua kwenda Rebza kwa hiari yake mwenyewe. Muombezi: Maelezo kama hayo yanaakisi majaribio ya maulamaa wenu mashabiki kuficha matendo mabaya ya viongozi wao. Kuhamishwa Abu Dharr kwa nguvu kwenda Rabza kunajulikana wazi sana. Kama mfano, nitaishia kunukuu riwaya moja, ambayo imesimuliwa na Imam Ahmad Bin Hanbal katika Musnad Jz. 5, uk. 156, Ibn Abil-Hadid katika Sharhe Nahjul-Balagha Jz. 1, uk. 241, na Waqid katika kitabu chake cha Tarikh kutoka kwa Abul-Aswad Duili. Abu Dharr aliulizwa kuhusu Safari yake ya Rabza. Abu Dharr akasema kwamba, alihamishwa kwa nguvu na kupelekwa kuishi porini. Akaendelea: Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alinijulisha kuhusu hili. Siku moja nililala Msikitini. Mtume akaja na akaniuliza kwa nini nimelala msikitini. Nikasema kwamba usinginzi umenipitia tu. Akaniuliza nitafanya nini kama nitahamishwa kutoka Madina. Nikasema ningekwenda kwenye nchi takatifu ya Syria. Akaniuliza nitafanya nini kama nitahamishwa huko pia. Nikasema nitarudi msikitini. Aliniuliza tena ningefanya nini kama ningefukuzwa kutoka hapa pia. Nikasema: Nitachomoa upanga na kupigana. Aliniuliza kama ningependa aniambie kitu ambacho kingekuwa kwa manufaa kwangu. Niliposema Ndio yeye akaniambia: Nenda sehemu yoyote watakayokupeleka! Hivyo nikasikiliza alivyoniambia na nikamtii. Baada ya hivi Abu Dharr akasema, kwa Jina la Allah, wakati Uthman atakapokwenda mbele ya Allah atasimama akiwa ni mwenye dhambi kuhusiana na suala langu.
164
Mikesha ya Peshawar
Uondoaji wa maofisa uliofanywa na Ali ulipelekea uhasama kwa watu wenye uchu wa madaraka, kama Muawiyya, na wakaitayarisha njia ya vita vya Jamal na Siffin. Kama Talha na Zubair wangechaguliwa kama magavana, wasingelichochea ghasia kule Basra na kuacha vita vya Jamal kutokea. Upole na ukarimu wake ulienea sawasawa kwa marafiki na maadui. Uthman alikuwa katili sana kwake (zaidi kuliko alivyokuwa Abu Bakr na Umar), lakini waasi walipolazimisha kizuizi kwenye Ikulu ya Uthman, wakizuia maji na chakula, aliomba msaada kwa Ali. Ali aliwatuma watoto wake, Hasan na Husein, wakiwa na mikate na maji. Ibn Abil-Hadid anaelezea tukio hili kwa kina katika Sharhe NahjulBalagha. Khalifa Uthman alikuwa na sifa ya kutoa Sadaka na kusaidia wengine, lakini ilikuwa kwa jamaa zake tu, kama Abu Sufyani, Hakam Bin Abil-As na Murwan Bin Hakam. Aliwamwagia pesa na zawadi kutoka hazina ya Umma bila kibali cha kidini. Lakini Amirul-Muminina Ali kamwe hakutoa zaidi ya kilichostahiki, hata kwa jamaa zake wa karibu. Kaka yake mkubwa, Aqil, alikuja kwake na kutaka pesa zaidi kuliko kawaida ya alivyokuwa akipewa. Ali hakusikiliza ombi lake. Aqil alisisitiza na akasema kwamba kwa vile Ali alikuwa Khalifa na alikuwa na mamlaka kamiki juu ya mambo inapasa haja zake zitekelezwe. Kama onyo kwa kaka yake, Ali akapasha moto kipande cha chuma kwa siri na akakiweka karibu na mwili wa Aqil. Alipiga kelele kama mtu aliye katika maumivu makali, akiogopa kuwa ataungua. Ali akasema: Wacha waombolezaji waomboleze kifo chako, ewe Aqil! Ulinywea wakati chuma kilichopashwa moto na mwanadamu kiliposogazwa karibu yako, na bado unanisogeza mimi kunielekeza kwenye moto ambao Allah ameumba kwa ghadhabu yake. Je, ni sawa wewe utafute hifadhi kutokana na maumivu haya ya kawaida, na kwamba mimi nisijihifadhi mwenyewe na Moto wa Jehanamu?
165
Mikesha ya Peshawar
166
Mikesha ya Peshawar
Sheikh: Kuna majibu mengi kwa maelezo yako, lakini umetafsri tu visivyo aya hii. Usemi na wale ambao wako pamoja naye ni wa wingi na hauwezi kuonyesha mtu mmoja tu. Kama sifa zilizotajwa katika aya zinamuonyesha mtu mmoja tu, kwanini vijina vikawa kwa wingi? Muombezi: Kwanza, unasema kwamba kuna majibu mengi kwa maelezo yangu. Kama hiyo ilikuwa kweli, basi kwa nini usiyataje? Kunyamaza kwako ni uthibitisho kwamba hakuna mjibu mengi kwa maelezo yangu. Pili, ulichosema hivi punde tu ni hoja potofu. Unajua kwamba katika luhga zote ikiwemo Kiarabu utumiaji wa wingi kwa ajili ya mmoja ni kitu cha kawaida kama dalili ya heshima. Kuna mifano mingi ya utumiaji huu katika Qurani Tukufu kama aya hii: Hakika walii wenu ni Allah na Mtume wake na walio amini ambao husimamisha Salat na hutoa zaka na huku wamerukuu. (5:55) Inakubaliwa na wote kwamba aya hii imeshuka kwa ajili ya Ali. Wafasiri na muhadithina, kam vile Imamu Fakhrud-Din Razi katika Tafsir Kabir, juzuu ya 3, uk. 431; Imamu Abu Ishaq Thalabi katika kitabu chake Kashfu l-Bayan; Jarullah Zamakhshari katika Tafsir Kashshaf, juzuu ya 1, uk. 422; Tabari katika Tafsir yake, juzuu 6, uk. 186; Abul-Hasan Rammani katika Tafsir yake; Ibn Hawazin Nishapuri katika Tafsir yake; Ibn Sadun Qartabi katika Tafsir yake, juzuu ya 6, uk. 221; Nasafi Hafiz katika Tafsir yake, uk.496 (kwa njia ya ufafanuzi kwenye Tafsir ya Khazin Bahgdadi); Fazil Nishapuri katika GharibulQurani, juzuu ya 1, uk.461; Abul-Hasan Wahidi katika Asbabun-Nuzul, uk. 148; Hafiz Jassas katika Tafsir Ahkamul-Qurani, uk. 542; Hafiz Abu Bakr Shirazi katika Fima Nazala Minal-Qurani Fi Amirul-muminin; Abu Yusuf Abdus-Salam Qazwini katika Tafsir Kabir; Kadhi Baidhawi katika Anwart-Tanzil, juzuu ya 1, uk. 345; Jalalud-Din Suyiti katika Durrl-Mansur, juzuu ya 2, uk. 239; Kadhi Shukani Sanai katika Tafsir Fathul-Qadir; Sayyid Muhammad Alusi katika Tafsir yake, juzuu ya 2, uk. 329; Hafiz Ibn Abi Shaiba Kufi katika Tafsir yake; Abul-Baraka katika Tafsir yake, juzuu ya 1, uk. 496; Hafiz Baghawi katika katika Maalimut-Tanzil; Imamu Abu Abdur-Rahman Nisai katika Sahih yake. Muhammad bin Talha Shafii katika Matalibus-Suul, uk. 31; Ibn Abil-Hadid katika Sharhe Nahjul-Balagha, juzuu ya 3, uk. 375; Khazin Alaud-Din Baghdadi katika Tafsir yake, juzuu ya 1, uk. 496; Suleimani Hanafi katika Yanabiul-Mawadda, uk. 212; Hafiz Abu Bakr Baihaqi katika Kitab Musnnaf; Razin Abdari katika JamBainusSiha Sitta; Ibn Asakir Damishiq katika Tarikh Sham; Sibt Ibn Jauzi katika Tadhkira, uk. 9; Kadhi Azudaili katika Mawaqif; uk.276; Sayyid Sharif Jurjani katika Sharhe Mawaqif; Ibn Sabbagh Malik katika Fusul-Muhimma, uk. 123; Hafiz Abu Sad Samani katika Fadhails-Sahaba; Abu Jafar Askafi katika Nagzil-Uthmaniyya; Tibrani katika Ausat; Ibn Maghazili Faqih Shafii katika Manaqib; Muhammad bin Yusuf Ganji Shafii katika Kifayatut-Talib; Mulla Ali Qushachi katika Sharhe Tajrid; Sayyid Muhammad Mumin Shablanji katika Nurul-Absar, uk. 77; Muhibud-Din Tabari katika Riyazun-Nuzra, juzuu ya 2, uk. 247, halikadhalika na wengine wengi
167
Mikesha ya Peshawar
miongoni mwa wanachuoni wenu maarufu, wote wamesimesimulia kutoka kwa Said, Mujahid Hasan Basri, Amash, Atba Bin Hakim, Ghalib Ibn Abdullah, Qais Bin Rabia, Abaya Bin Rabi , Abdullah Ibn Abbas, Abu Dharr Ghifari, Jabir Ibn Abdullah Ansari, Ammar, Abu Rafi, na Abdullah Bin Salam, na wengine wanakiri kwamba aya hii iliteremshwa katika kumsifia Ali. Aya hii inaashiria kwenye wakati ambao Ali alitoa pete yake kumpa muombaji wakati akiwa kwenye rukuu. Hapa vile vile maneno yapo katika wingi kwa staha na heshima juu ya cheo cha Wilaya (walii), na kuthibitisha kwamba Ali alikuwa Imamu na mrithi wa Mtume (s.a.a.w.). Msisitizo wa neno Innama, hutoa maana ya uamuzi wa Allah wa mwisho na uliopangwa, yaani, uamuzi wa Allah kwamba Walii wa waumini lazima awe ni Allah, Mtume Wake (Muhammad), na waumini ambao hutoa sadaka huku wakiwa wanasali, huyu wa mwisho akiashiriwa bayana kuwa ni Ali. Sheihk: Hakika utakubali kwamba tafsiri yako haikuthubutu kwa vile kuna maoni tofauti kuhusu hilo. Baadhi wanasema huashiria kwa Ansar, baadhi wanasema ni katika kumsifia Ibadat Bin Samit, na baadhi wanasema kwamba inaashiria kwa Abdullah Bin Salam. Muombezi: Kwa hakika inashangaza kwamba mwanachuo kama wewe unaweza kupingana na ulamaa wako mwenyewe. Unachukua maoni ya wajinga wachache na wasioaminika ambao riwaya zao zinakataliwa. Wanachuoni wenu wakubwa kwa pamoja wametamka kwa dhati kuthibitisha juu ya nukta hii, watu kama Fazil Taftazani na Mulla Ali Qushachi, ambaye anasema katika kitabu chake, Sharhe Tajrid: Kwa mujibu wa maoni ya pamoja ya wafasiri, aya hii iliteremshwa katika kumsifia Ali, ambaye wakati akiwa kwenye rukuu katika Sala, alitoa pete yake kumpa muombaji.
168
Mikesha ya Peshawar
Muombezi: Umeulewa vibaya msemo Walii wenu Wali ni (sarufi ya) umoja, kum (wenu) ni wingi ambao huashiria kwa watu na haioneshi umoja. Naam hakika, Wali ni kwa ajili ya mtu ambaye ni mlezi kwa jamii nzima katika zama zote. Pili, katika aya ambayo iko kwenye mjadala, pale ambapo wingi umetumika, baadhi ya mashabiki wamesema kwamba haiwezi kutafsiriwa kama umoja kama katika aya wale ambao wanasimamisha Sala pingamizi hili nililijibu mapema. Nilisema kwamba, waandishi wakubwa mara nyingi wametumia umoja kumaanisha wingi. Vile vile umedai kwamba muundo wa (sarufi ya) umoja katika aya hii huashiria watu kwa ujumla. Tunasema kwamba, kwa mujibu wa msisitizo wa neno hakika, anayeashiriwa ni Ali, lakini hatukusema kwamba kuhusika huko ni kwa aina ya pekee tu kwake. Wengine kutoka nyumba ya Mtume wanakuwemo pia. Kwa mujibu wa hadithi zilizo sahihi, Maimamu wote wa kizazi cha Mtume wamejumuishwa katika aya hii. Jarullah Zamakhshari anaandika katika Kashshaf kwamba aya hii iliteremshwa makhususi katika kumsifia Ali, lakini ule wingi uliotumika ndani yake, unamaanisha kwamba wengine lazima wamfuate. Sheikh: Katika aya hii neno Wali haswa lina maana ya msaidizi. Kama lingekuwa na maana ya mlezi ambayo hujumuisha na cheo cha mrithi, basi angeliteuliwa wakati wa uhai wa Mtume (s.a.w.w.). Muombezi: Cheo cha Ali ni cha kudumu. Ujengaji wa sentensi kisarufi na neno Wali uliotumika kama sifa, huthibitisha cheo cha kudumu cha Ali. Ukweli huu unaungwa mkono zaidi na Mtume kwa kumtangaza Ali kama makamu wake wakati wa safari ya Tabuk na kamwe hakulifuta tangazo hilo. Mtazamo wetu unaimarishwa zaidi na Hadith-eManzila (Hadithi ya cheo) ambayo Mtukufu Mtume amerudia mara nyingi kuisimulia: Ali kwangu mimi ni kama Harun alivyokuwa kwa Musa, ambayo nimeilezea katika mikesha iliyopita. Hii yenyewe ni uthibitisho mwingine kwa Ali wa kuwa kwake Walii au Makamu wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) wakati wa uhai wa Mtume na baada ya kufa kwake. Sheikh: Kama ingekuwa tulipe suala hili mazingatio yanayostahili, tungelikiri kwamba aya hii haimzungumzii Ali. Cheo chake ni kikubwa kuliko kile tunavyotaka kukithibitsha kutoka kwenye aya hii. Haithibitishi ubora wowote juu yake, bali hukiangusha chini cheo chake. Muombezi: Sio wewe wala mimi si yeyote katika Umma pamoja na wale masahaba wakubwa wa Mtume, ambaye ana haki yoyote ya kuingilia tafsiri halisi za aya hizi. Aya za Qurani hazikuteremshwa kwa mujibu wa matakwa yetu. Kama baadhi ya watu wakitafsiri maana zao kwa kuegemeza juu ya maoni yao au wakataja tukio au habari ambayo imeteremshiwa, basi kwa hakika hao sio watu wa dini. Kwa mfano, wafuasi wa Abu Bakr wanasema kwamba kwa mujibu wa hadithi iliyosimuliwa na mghushaji mkorofi Akrama, aya hii iliteremshwa kwa ajili ya Abu Bakr. Unaweza ukatueleza ni jinsi gani aya hii inavyoangusha cheo cha Ali?
169
Mikesha ya Peshawar
Sheikh: Moja ya tabia za murwa wa cheo cha Ali ni kwamba, wakati anaposali kamwe hageuzi hadhari yake kwenye kitu kingine. Wakati fulani Ali alijeruhiwa katika vita. Kiwembe cha mshale kilibakia mwilini, na ilikuwa haiwezikani kukiondoa bila kusababisha maumivu makali. Lakini aliposimama kwa ajili sala, kiwembe cha mshale kiliondolewa, na kwa sababu ya kuzama katika ibada yake kwa Allah, hakusikia maumivu. Kama wakati wa kusali alitoa pete yake kumpa muombaji, kulikuwa na dosari kubwa katika Sala yake. Itaezakana vipi mtu ambaye amezama katika rehema ya Allah na wakati huo huo andoe hadhari yake kutoka kwa Allah kwa ajili ya kuitikia sauti ya omba omba? Aidha, katika kutenda kila jambo jema na kutoa sadaka kuweka nia ni kitu cha lazima. Wakati wa kusali hadhari ya mtu lazima iwe imeelekea kwa Allah peke Yake. Inawezekana vipi kwamba nia yake imegeuka kutoka kwenye Sala na kugeuka kumuelekea kiumbe? Kwa vile tunakiona cheo cha Ali kuwa ni cha juu sana, hatukubali tafsiri yako. Na kama alitoa chochote kwa omba omba, basi kwa hakika haikuwa wakati wa Sala, kwa vile rukuu maana yake ni kunyenyekea mbele ya Allah. Muombezi: Umejifunza vizuri jinsi ya kusoma, lakini umeikosa njia ya kuendea kwenye maombi. Pingamizi hili ni dhaifu kuliko hata utando wa buibui. Kwanza, kitendo cha Ali kwa njia yoyote hakiangushi chini cheo chake. Kwa hakika kumsikiliza omba omba ili kumpa sadaka, ni chanzo cha ubora. Katika hali hii, alikusanya sala yake ya kimwili na ya kiroho pamoja na sala ya kiyakinifu. Sala zote zilikuwa katika njia ya Allah. Ndugu wapenzi! Uharibifu ambao unanyongesha Sala ni ule ambao unatokana na fikra binafsi. Kuzingatia sala nyingine, wakati ambapo unasali Sala mahususi, ni dalili ya ubora. Kwa mfano, kama wakati wa ibada ya Sala, mtu akalia kwa mapenzi makubwa ya jamaa zake, Sala yake itakuwa batili. Lakini kama akilia kwa mapenzi makubwa ya Allah, au kwa kumuogopa Yeye, basi hiyo ni dalili ya ubora. Umesema kurukuu maana yake ni kunyenyekea kwa unyofu kwa Allah. Maana hii inaweza ikatumika kwa matukio mengine. Lakini kama ukisema kwamba kurukuu katika Sala, ambako ni hakika na lazima, kunabeba maana hiyo hiyo ya kilugha, watu wasomi watakudharau. Vile vile umejaribu kuondoa au kupuuza maana ya wazi ya aya. Umeitolea maana ya kistiari, ingawa unajua kwamba neno hilo huelezea kitendo kinachohitajika cha ibada ya Sala, ambacho ni kuinama mpaka viganja kufikia magoti. Na ukweli huu umekubaliwa na maulamaa wenu wakubwa, kama nilivyoelezea mapema. Fadhil Qushachi, katika Sharhe Tjrid, anaelezea maoni ya wafasiri kwa ujumla kwamba Ali, wakati anarukuu katika Sala, alitoa pete yake kumpa omba omba. Tukiweka kila kitu pembeni, tafadhali tueleze iwapo aya hii ilitaremshwa kwa kusifu au kwa kulaumu? Sheikh: Ni wazi ilikuwa kwa kusifia. Muombezi: Hivyo wakati maulamaa wa madhehebu zote wamesema kwamba aya hii iliteremshwa kwa kumsifia Ali, na kwamba ina ridhaa ya Allah (swt), kwa nini ulete ukin-
170
Mikesha ya Peshawar
zani usio na maana, ukubaliane na Makhawariji washabiki, ambao maoni yao yamedukizwa kwenye akili yako safi tangu utotoni? Kwa nini hukubali ukweli huu? Sheikh: Samahani! Kwa vile wewe ni mzungumzaji fasaha, mara nyingi unatumia vidokezo na rejea ambazo zinaweza kujenga mawazo ambayo yanaweza kuleta matokeo yasiyofurahisha katika akili za watu ambao hawana elimu ya kutosha juu ya masuala haya. Ingekuwa vyema kama ungejizuia kutokana na lugha kama hizo. Muombezi: Katika mazungumzo yangu hakuna chochote ila ukweli. Allah awe shahidi wangu, kamwe sijakusudia kutumia madokezo au rejea zisizo za moja kwa moja. Hakuna haja ya kufanya hilo. Chochote ninachotaka kusema, nakisema kwa wazi. Tafadhali nieleze ni vidokezo gani unavyomaanisha. Sheikh: Muda mfupi uliopita wakati wa mazungumzo yako kuhusiana na aya iliyoko kwenye mjadala, ulisema kwamba sifa zilizotajwa ndani yake ni za kipekee kwa Ali Bin Abu Talib ambaye kuanzia mwanzo mpaka mwisho wa uhai wake, kamwe hajawa na shaka katika imani yake. Kwa namna hii unaonesha kwamba wengine walikuwa na hatia ya ukana mungu. Je, wale makhalifa wakubwa au masahaba kuna yeyote aliyekuwa na shaka katika imani zao? Bila shaka hao masahaba, kama alivyokuwa Ali, kamwe hawajautilia shaka ukweli wa Uislamu. Hata mara moja hawajakengeuka katika mafindisho ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Muombezi: Kwanza, kamwe sijatumia maneno ambayo wewe umeyatumia sasa hivi. Pili, unaelewa kwamba kuthibitisha kitu kwa mtu fulani haina maana ya kutothibitisha kitu hicho kwa watu wengine. Tatu, ingawa unajaribu kunikosoa, nafikiri wengine hawana kitu kama hicho katika akili zao. Allah awe shahidi wangu, sikufanya rejea yoyote isiyo ya moja kwa moja kwa kitu chochote, wala sijafikiria kufanya hivyo. Na kama kitu chochote kilitokea kwenye akili yako, ungeweza kuniuliza kuhusu kitu hicho kwa faragha. Sheikh: Namna ya uzungumzaji wako huonyesha kwamba kuna nukta fulani ambazo unazinyamazia. Nakuomba utufahamishe kilichoko akilini mwako na kutupa rejea sahihi kwa unachosema. Muombezi: Ni wewe uliyejenga kitu hicho akilini mwetu; unasisitiza kwamba suala hili lijadiliwe. Nakuomba tena, liache suala hili na uache kusisitiza juu yake. Sheikh: Kama kulikuwa na kitu chochote cha usafihi, imekwisha. Sasa huna jinsi ila kujibu. Kama hutatoa jibu la wazi, ima la kukubali au kukataa, basi nitawajibika kuamua kwamba uliyoyasema yalikuwa hayana msingi wowote. Muombezi: Hakuna chochote cha usafihi katika maelezo yangu, lakini kwa vile unasisiti-
171
Mikesha ya Peshawar
za, sina jinsi isipokuwa kuufichua ukweli. Ulamaa wenu wakubwa wanakubali kwamba masahaba wa Mtume ambao imani yao ilikuwa bado haijakamilika, mara kwa mara walionyesha kuwa na mashaka. Baadhi yao walilea shaka hiyo na uasi wa kidini. Baadhi ya aya ziliteremshwa kwa ajili ya kuwalaumu. Kwa mfano, walikuwepo munafiqin (wanafiki) ambao katika kulaumiwa kwao Sura nzima ya Qurani Tukufu iliteremshwa. Lakini masuala kama hayo hayapaswi kujadiliwa waziwazi. Nakuomba tena ujizuiye kuindama nukta hii. Sheikh: Una maana kwamba wale makhalifa wakubwa walikuwa ni miongoni mwa wale waliokuwa na mashaka. Muombezi: Kama majibu yangu yatasababisha hisia mbaya miogoni mwa watu wasio na elimu, wewe ndiye utakayebeba lawama. Umesema sasa hivi, Useme hivi au umesema kwamba. Lakini tena, ni maulamaa wenu wenyewe ndio ambao wamesimulia mambo haya. Sheikh: Wameandika kuhusu suala gani, na ni katika tukio gani makhalifa wameonesha shaka yao, na ni watu gani ambao walitia shaka? Tafadhali tujulishe. Muombezi: Watu wengi walikuwa na shaka kubwa sana, lakini wakarudi kwenye imani yao ya asili. Baadhi yao wakangangania katika shaka zao. Ibn Maghazili Shafii, katika kitabu chake Manaqib, na Hafidh Abu Abdullah Muhammad Bin Abi Nasir Hamidi katika JamBainus-Sahihain-e-Bukhari, na Muslim wanaandika: Umar Bin Khattab alisema, Sijapata kuutilia mashaka utume wa Muhammad kama nilivyofanya siku ya Hudaibiyya. Maelezo haya yanaonyesha kwamba aliutilia shaka utume wa Muhammad zaidi ya mara moja. Nawab: Samahani. Ni tukio gani katika Hudaibiyya ambalo lilimfanya awe na shaka kuhusu Mtume? Muombezi: Mtume aliona usiku mmoja kwenye ndoto kwamba alikwenda Makka pamoja na mashaba zake kufanya Umra. Asubuhi yake, aliposimulia ndoto hii kwa masahaba zake, walimuomba aitafsiri ndoto hiyo. Mtume akasema, Mwenyezi Mungu akipenda tutakwenda Makka kuitekeleza ibada hii Inshaallah. Lakini hakuainisha ni wakati gani itafanyika. Akiwa na nia ya kuizuru Nyumba ya Allah, Mtume aliondoka na masahaba zake kuelekea Makka katika mwaka ule ule. Wakati walipofika Hudaibiyya (kisima kilicho karibu na Makka), Maquraishi walikuja pale na kuwazuia wasiendelee mbele. Kwa vile Mtume hakuenda kule akiwa amejiandaa kupigana, alijitolea kufanya amani nao. Mkataba ulisainiwa na Mtume akarudi Madina. Katika tukio hili, Umar alikuwa na mashaka. Alikwedna kwa Mtume na akasema: Je, wewe sio Mtume wa Allah na mtu mkweli? Je, wewe hukutuambia kwamba utakwenda Makka na kufanya Umra kisha unyoe kichwa
172
Mikesha ya Peshawar
chako na upunguza ndevu zako? Kwa nini sasa umeshindwa kufanya hivi? Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alimuuliza iwapo yeye aliweka muda kwa ajili ya hilo au kama aliwaambia kwamba atakwenda kule katika mwaka ule ule. Umar akakiri kwamba Mtume hakuainisha wakati. Mtume akasema kwamba alichowaambia ni sahihi, na Mungu akipenda watakwenda Makka siku zijazo na ndoto yake itatimizwa. Hakika wakati kwa ajili ya utekelezaji wa tafsiri ya ndoto, uwe mapema au baadae utetagemea juu ya utashi wa Allah (swt). Kisha kwa uthibitisho wa maelezo ya Mtume, Jibril alijitokeza na kuteremsha aya ifuatayo ya Qurn Tukufu: Hakika Allah amemtimizia Mtume Wake ndoto kwa haki. Bila shaka ninyi mtauingia Msikiti Mtukufu, insha-Allah kwa amani, na hali mmenyoa vichwa vyenu na (baadhi) mmepunguza nywele. Hamtakuwa na hofu. Yeye anajua msiyoyajua. Basi atakupeni kabla ya haya ushindi karibuni. 48:27. Ushindi hapa una maana ya ushindi wa Khaibar. Hii ilikuwa kwa ufupi tukio la Hudaibiyya ambalo kwa kweli lilikuwa ni mtihani kwa waumini na kwa watu wanaoyumba. Kufikia hapa ulifuatia mjadala wa iwapo tuendelee na mjadala au la, kwa ajili ya ratiba ya wageni wa ki-Sunni kutoka Afghanistan na halikadhalika na Muombezi, matokeo yake ambayo ilikuwa ni uamuzi wa kuendelea.
173
Mikesha ya Peshawar
kuchanganya akili zenu. Kama utaangalia kwa makini utaelewa kwamba sijasema kitu chochote cha kupotosha, lakini ma-Mulla hawa wasomi waliuliza maswali ambayo nililazimika kuyajibu. Sasa kama una swali lolote la kuuliza, unaweza kufanya hivyo, na kwa msaada wa Allah, nitalijibu. Sayyid: Tunataka kujua vipi inawezekanaje kwamba watu wawili wanaweza kuungana kiasi kwamba muungano wao unawafanya kuwa mtu mmoja na yule yule.
174
Mikesha ya Peshawar
Tumewatukuza baadhi yao juu ya wengine (2:253). Na kikamilifu zaidi katika cheo kwa Mitume wote ni cheo maalumu cha Muhammad, kama Allah alivyosema: Muhammad sio baba wa yeyote katika wanaume wenu, bali ni Mtume wa Allah na mwisho wa Manabii, na Allah ni mjuzi wa kila kitu (33:40). Ni kwa ukamilifu huo wa utume ambao umepelekea kwenye ukomo wa utume. Hivyo katika sifa hii ya ukamilifu, hakuna mtu yeyote anayeweza kujumuishwa humo. Katika mambo mengine yote ya ubora, kuna ushirikiano na usawa, ambao kwamba kuna uthibitisho mwingi. Sayyid: Unaweza ukaleta hoja yoyote kutoka kwenye Quan kuthibitisha madai haya?
AYA YA MAAPIZANO (MUBAHILA) INATHIBITISHA UMOJA WA NAFSI YA ALI NA YA MTUKUFU MTUME (S.A.W.W.)
Muombezi: Hakika, hoja yetu ya kwanza ni kutoka Qurani Tukufu, ambayo ni ushahidi wa ki-Mungu wenye nguvu sana, yaani aya ya maapizano (Ayatul-Mubahila) ambayo kwayo Allah anasema:
Watakao kuhoji katika haya baada ya kukufikia elimu hii waambie: Njooni tuwaite watoto wetu na watoto wenu, na wanawake zetu na wanawake zenu, na nafsi zetu na nafsi zenu, kisha tuombe kwa unyenyekevu tutake laana ya Allah iwashukie waongo. (3:61) Maulamaa wenu wakubwa, kama vile Imamu Fakhurud-Din Razi, Imamu Abu Ishaq Thalabi, Jalalud-Din Suyuti, Qadhi Baidhawi, Jarullah Zamakhshari, Muslim bin Hujjaj, na wengine wengi, wameandika kwamba aya hii tukufu iliteremshwa siku ya maapizano, ambayo ilikuwa mwezi 24 au 25 Dhul-Hijja katika mwaka wa 9 A.H. Wakati Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alipowalingania Uislamu Wakristo wa Najran, wao waliwateua watu wao wenye elimu sana kama vile Seyyed, Aqib, Jasiq, Alqama na kadhalika, idadi yao ikiwa ni zaidi ya watu sabini na wakawatuma kwenda Madina pamoja na watu 300 kati ya wafuasi wao, ili kukutana na Mtukufu Mume na kujifunza Uislamu ulikuwa ni nini. Waliingia katika mjadala wa kielimu na Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) na walishangazwa na hoja zake nzito. Alithibitisha ukweli wa ujumbe wake kutoka kwenye vyanzo vyao vyenye kuaminika na akasema kwamba, Isa mwenyewe alitabiri kuwasili kwake (Muhammad) kwa ishara mbali mbali, na Wakristo walikuwa wanangojea kutimia kwa
175
Mikesha ya Peshawar
utabiri wa Isa ambao kwa mujibu wake, mtu huyo atatokea akiwa amepanda ngamia kutokea milima ya Faran (katika Makka) na atahamia kwenye sehemu iliyopo kati ya Ayr na Uhud (ambayo ilikuwa ni Madina). Hoja hzi ziliwavutia sana Wakristo, lakini mapenzi yao ya heshima za kidunia yaliwazuia kuukubali ukweli. Basi Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) aliwaeleza amri ya Allah, ambayo walikubaliana nayo kama njia ya kumaliza mjadala na kwa ajili ya kubainisha kati ya wakweli na waongo.
176
Mikesha ya Peshawar
ninyi na mimi tunajua kwamba huyu Muhammad ni Mtume yule yule wa Mungu ambaye alikuwa akitazamiwa, na chochote anachosema kinatoka kwa Mungu. Naapa kwa jina la Mungu kwamba yeyote aliyeshindana na Mtume wa Mungu aliangamia, na hakuna katika vijana wao na wazee wao aliyebakia hai. Kwa hakika kama tungeshindana nao, wote sisi tungeliuawa na asingebakia hai Mkristo yeyote ulimwenguni. Kwa jina la Mungu, wakati nilipowaangalia niliziona nyuso ambazo kama zingemuomba Mungu, wangeweza kusogeza milima. Hafidh: Ulichosema ni kweli kabisa na kinakubaliwa na Waislamu wote, lakini hakina uhusiano na suala tunalojadili, yaani, kwamba Ali alikuwa ameungana kiroho na Mtukufu Mtume (s.a.w.w.).
177
Mikesha ya Peshawar
na Husein ndio walikuwepo pamoja na Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) katika maapizano, usemi katika aya hii tukufu, watoto wetu na watoto wenu, wanawake wetu na wanawake wenu huashiria Hasan na Husein na Fatima kwa mpangilio huo, na mtu mwingine angeweza kutambuliwa kama nafsi zetu katika kundi hili tukufu alikuwa ni Amirul-Muminin, Ali. Kwa hiyo, maneno haya nafsi zetu huthibitisha muungano wa nafsi kati ya Mtume Muhammad na Ali. Kwa vile mungano halisi wa nafsi mbili hauwezikani, Allah kumuita Ali nafsi ya Mtume Muhammad maana yake ni muungano wa kutwaliwa wa nafsi mbili. Unajua vizuri sana kwamba kimsingi ni bora kulitambua neno kwa dhana ya karibu kuliko na ile ya mbali, na dhana ya karibu sana maana yake kuhusiana katika fadhila zote isipokuwa zile ambazo zimeondolewa kwa sababu fulani. Na tayari tumekuambieni kwamba ni utume maalumu wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) na upewaji wa Wahyi juu yake, ambavyo ni vitu vya kipekee kwake tu. Kwa hiyo, hatumchukulii Ali kama mshirika wake kuhusiana na sifa hizi mbili. Lakini kwa mujibu wa aya hii tukufu, Ali anashirikiana pamoja na Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) katika fadhila nyingine zote, na kwa uhakika Allah (swt) amemjaalia Ali kupitia kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) kwa baraka Zake zote. Hii peke yake inathibitisha muungano wa nafsi zao, ambao tulitaka kuuthibitisha. Hafidh: Kwa nini unasisitiza kwamba aya hii haimaanishi kuita nafsi yake mwenyewe? Kwa nini dhana hii isiwe bora kuliko dhana nyingine? Muombezi: Ni matumaini yangu kwanba hutapoteza muda katika mazungumzo yasiyo na mantiki na kutoka nje ya njia ya uadilifu. Kwa kweli uadilifu huhitaji kwamba kama tumekubaliana juu ya nukta fulani, lazima tuendelee mbele. Sikutegemea mtu wa cheo chako na elimu yako kujiingiza katika mjadala bandia. Kama ujuavyo wewe mwenyewe na kwa mujibu wa wanachuoni wote, nafsi moja inafananishwa na nafsi nyingine kwa njia ya dhana. Miogoni mwa watu wasomi ni kawaida kudai muungano wa dhana, kama nilivyoeleza mwanzo. Mara kwa mara inaonekana kwamba mtu mmoja anamuambia mwingine: Wewe ni maisha yangu na nafsi yangu mwenyewe. Hususan katika lugha ya hadith na simulizi, uhusiano huu mara kwa mara umekuwa ukielezewa kuhusu Amirul-Muminin, Ali, na kila simulizi kama hiyo ikuchukuliwa kwa peke yake ni uthibitisho wa kuonesha ukweli wa msimamo wangu.
178
Mikesha ya Peshawar
SIMULIZI ZAIDI NA HADITH KAMA USHAHIDI WA UMOJA WA MSINGI WA MTUKUFU MTUME (S.A.W.W.) NA ALI
Imamu Ahmad bin Hanbal, katika Musnad yake, Ibn Maghazili, mwanachuoni wa kiShafii katika Manaqib yake, na Muwafiq Ibn Ahmad Khawarizmi katika Manaqib yake, wanasimulia kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alisema: Ali anatokana na mimi na mimi natokana na Ali; yeyote anayempenda yeye, amenipenda mimi; na ambaye ananipenda mimi, amempenda Allah. Vile vile Ibn Maja katika Sunan yake, sehemu ya 1, uk. 92; Tirmidhi katika Sahih yake; Ibn Hajar katika kitabu cha Hadithi cha 5 cha Hadithi Arobaini zinazohusu fadhaila za Amirul-Muminin zilizosimuliwa katika Sawaiq kutoka kwa Imamu Ahmad Bin Hanbal, Tirmidhi, Imamu Abu Abdur-Rahman Nisai, na Ibn Maja; Imamu Ahmad Bin Hanbal katika Musnad, juzuu ya 4, uk. 164; Muhamad Ibn Yusuf Ganji Shafii katika sura ya 67 ya Kifayatut-Talib kutoka Musnad ya Ibn Samak, juzuu ya 4, na Mujim Kabir cha Tibrani; na Imamu Abudur-Rahman Nisai katika Khasais, na Sulaiman Balkhi Hanafi katika Yanabiul-Mawadda kutoka kwenye Mishkat wote wamesimulia kutoka kwa Jash Bin Junada as-Saluni kwamba wakati wa hijja ya muago, Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alisema kule Arafa: Ali anatokana na mimi, na mimi natokana na Ali. Hakuna mtu anayenifidia mimi (yaani, hakuna awezaye kufanya kazi ya ujumbe wangu) isipokuwa mimi na Ali. Sulaimani Balkhi Hanafi katika Yanabiul-Mawaddat, sura ya 7, anasimulia kutoka Zawaid-e-Musnad cha Abdullah Bin Ahmad Bin Hanbal kutoka kwa Ibn Abbas kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alisema kumuambia Ummul-Muminin Salma: Ali anatokana na mimi na mimi natokana na Ali. Nyama yake na damu yake inatokana na nyama yangu na damu yangu. Yuko kwangu mimi kama alivyokuwa Harun kwa Musa. Ewe Umm Salma! Sikiliza, na uwe shahidi kwamba huyu Ali ni bwana na mkuu wa Waislamu. Hamidi katika kitabu chake JamBainus-Sahihain na Ibn Abil-Hadid katika SharheNahjul-Balagha wanasimulia kwamba, Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) amesema: Ali anatokana na mimi na mimi natokana na Ali. Ali kwangu mimi ni kama kichwa kilivyo kwa mwili; mtu anayemtii yeye, ananitii mimi; na mtu anayenitii mimi, anamtii Allah. Muhammad Bin Jarir Tabari katika Tafsir yake na Mir Sayyid Ali Hamdani, mwanachuoni wa ki-Shafii, katika Muwadda ya 8 cha Muwaddatul-Qurba, wanasimulia kutoka kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) ambaye alisema: Hakika Allah (swt) aliisaidia imani hii ya kiIslamu kupitia Ali, kwa vile yeye anatokana na mimi, na mimi natokana na yeye, na aya hii tukufu imeteremshwa kwa ajili yake. Basi je, yeye ni kama mtu ambaye ana dalili
179
Mikesha ya Peshawar
za wazi kutoka kwa Mola wake na kufuata ushahidi kutoka Kwake? (11:17) Sheikh Sulaimani Balkhi Hanafi ameainisha katika sura ya 17 ya kitabu chake YanbiulMawdda kuhusu suala hili hili chini ya maelezo mafupi: Kuhusu Ali kuwa kama nafsi ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) na hadithi kwamba Ali anatokana na mimi, na mimi natokana na Ali. Katika sura hii amesimulia hadithi 24 katika njia tofauti na kwa maneno tofauti kutoka kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), ambaye alisema Ali alikuwa kama nafsi yake mwenyewe. Kuelekea mwishoni mwa sura hii, alisimulia hadithi kutoka kwenye Manaqib kama ilivyosimuliwa na Jabir, ambaye alisema kwamba, alimsikia Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akisema kwamba, Hadhrat Ali anazo sifa ambazo kwamba kama mtu anakuwa na moja kati ya hizo, ingelitosha kuthibitisha murwa wa mtu huyo na ubora wake. Na kwa sifa hizo ilimaanishwa hadithi za Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) kuhusiana na yeye kama vile: Yeyote yule ambaye mimi ni mwenye kumtawalia mambo yake basi huyu Ali ni mwenye kutawalia mambo yake, au Ali yuko kwangu mimi kama alivyokuwa Harun kwa Musa, au Ali anatokana na mimi na mimi natokana na Ali au Ali yuko kwangu mimi kama nafsi yangu ilivyokuwa kwangu, utii kwake ni utii kwangu, au Kupigana dhidi ya Ali ni kupigana dhidi ya Allah, na kufanya amani na Ali ni kufanya amani Allah, au Rafiki wa Ali ni rafiki wa Allah, na adui wa Ali ni adui wa Allah, au Ali ni Hujjat (udhihirisho) wa Allah juu ya viumbe Wake, au Mapenzi kwa Ali ni imani, na uadui dhidi yake ni ukafiri, au Kundi la Ali ni kundi la Allah, nakundi la maadui wa Ali ni kundi la Shetani; au Ali yuko pamoja na haki, na haki pamoja naye, (na hivyo) havitengani, au Ali ndiye mgawaji wa Pepo na Moto, au Mtu anayejitenga na Ali, amejitenga na mimi, na anayejitenga na mimi, anajitenga na Allah, au Wafuasi wa Ali wataokolewa Siku ya Hukumu. Mwishowe, alinukuu hadithi nyingine yenye maelezo marefu kutoka kwenye Manaqib ambayo mwishoni mwake Mtume anasema: Naapa kwa jina la Allah ambaye ameweka utume juu yangu, na kunifanya mimi mbora wa viumbe Wake: Ewe Ali! Hakika wewe ni Hujjat (udhihirisho) wa Allah kwa ajili ya watu, mdhamini Wake, mjuzi wa siri Zake, na Khalifa juu ya waja Wake. Kuna hadithi nyingi kama hizo kwenye vitabu vyenu. Maneno nafsi zetu kwa uwazi huonesha ushirikiano wa karibu kati ya Mtume na Ali katika masuala yote ya ubora. Nafikiri kwamba aya hii ni ushahidi tosha wa msimamo wangu. Aidha, swali lako la pili linajibiwa na aya hiyo hiyo. Tumethibisha kwamba, ukiondoa utume na Wahyi, ambavyo vinamhusu Mtume tu peke yake, Ali alishirikishwa pamoja naye katika masuala yote ya ubora. Vile vile ina maana kwamba katika sifa za hali ya juu za ubora Ali alikuwa mbora zaidi ya Masahaba na kwa mtu yeyote katika umma huu. Kwa hakika aya hii inathibitisha kwamba anawapita Mitume wote wengine waliopita, kama vile ambavyo Mtume anawapita Mitume wote wengine.
180
Mikesha ya Peshawar
KWA VILE MTUKUFU MTUME ALIKUWA MBORA KWA MITUME WOTE WENGINE NA ALI PIA ALIKUWA MBORA KWAO
Katika Ihyaul-Ulum ya Imam Ghazali, Sharhe Nahjul-Balaghah ya Ibn Abil-Hadid Mutazil, Tafsir ya Imam Fakhrud-Din Razi, na Tafsir za Jarullah Zamakhshari, Baidhawi, Nishapuri na kadhalika, utaikuta hadith hii ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.): Wanachuoni wa umma wangu ni kama mitume wa Bani-Israili. Katika hadith nyingine amesema: Ulamaa wa umma wa Mtukufu Mtume walikuwa sawa au bora kuliko mitume wa Bani-Israil kwa sababu tu kwamba chanzo chao cha elimu kilikuwa ndio kiini hasa cha elimu, Mtukufu Mtume Muhammad (s.a.w.w.). Kwa hiyo, Ali ibn Abi Talib bila shaka alikuwa mbora kwa mitume, kwa vile Mtukufu Mtume amesema: Mimi ni Jiji la elimu na Ali ni lango lake. Vile vile amesema: Mimi ni nyumba ya hekima na Ali ni lango lake. Wakati Ali mwenyewe alipoulizwa kuhusu jambo hili, yeye alieleza baadhi ya vipengele vya ubora wake kwa mitume wa Bani-Israil. Mnamo mwezi 20 ya Ramadhan, wakati Ali alipokuwa katika kitanda chake cha umauti kufuatia lile shambulizi la Abdul-Rahman Ibn Muljim Muradi, alimtuma Imam Hasan kuwaita wale Mashia waliokuwa wamejikusanya kwenye mlango wa nyumba yake. Walipoingia ndani, walikuzunguka kitanda chake huku wakilia kimya kimya. Ali akasema: Mnaweza kuuliza swali lolote mnalolitaka kabla sijakuacheni, lakini maswali yenu yawe mafupi. Mmoja wa wale waliokuwepo pale alikuwa ni Sasaa bin Suwhan. Wanachuoni wenu maarufu kabisa kama Ibn Abdul-Birr na Ibn Saad, wameandika kuhusu maisha na tabia yake, wamemtegemea yeye Sasaa, wakithibitisha kwamba yeye alikuwa ni mtu mwenye elimu kubwa. Sasaa alimwambia Ali: Naomba unifahamishe ni nani mbora, ni wewe au Adam. Imam Mtukufu akasema: Haifai kwa mtu kujisifia mwenyewe, lakini kulingana na kauli adilifu: Na neema za Mola Wako alizokujaalia zisimulie, ninakwambia kwamba mimi ni bora kuliko Adam. Alipoulizwa ni kwa nini imekuwa hivyo, Ali alieleza kwamba Adam alikuwa na kila namna ya huruma, starehe na neema kwa ajili yake ndani ya Pepo. Alitakiwa tu kujizuia kutokana na chakula kile kilichokatazwa. Lakini hakuweza kujizuia na akala kutoka kwenye mti ule. Matokeo yake yeye alifukuzwa kutoka peponi. Mwenyezi Mungu hakumkataza yeye Ali kutokana na kula ngano (ambayo, kwa mujibu wa imani ya Kiislam ndio mti uliokatazwa). Lakini kwa kuwa yeye hakuwa na mwelekeo kwenye dunia ya mpito, yeye alijizuia kwa hiari yake mwenyewe kula ngano. (Hoja ya kauli hii ya Ali ilikuwa kwamba ubora wa mtu mbele ya Mwenyezi Mungu ulitegemea kwenye uchamungu na utii, na kwamba kilele cha uchamungu kinaegemea katika kujizuia hata kwa kile ambacho kinaruhusiwa kihalali).
181
Mikesha ya Peshawar
Sasaa akauliza: Ni nani mbora, wewe ama Nuh? Ali akajibu: Mimi ndiye mbora. Nuh aliwalingania watu wake kumuabudu Mwenyezi Mungu lakini hawakutii. Kitendo chao cha aibu kilikuwa ni kumtesa yeye. Yeye aliwalaani na akamuomba Mwenyezi Mungu: Ewe Mola Wangu! usiabakishe hata mtu mmoja juu ya ardhi miongoni mwa madhalimu hawa. Baada ya kifo cha Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), ingawaje watu walinisababishia matatizo makubwa, mimi sikuwalaani kamwe. niliyabeba mateso yao kwa subira kubwa. Sasaa akauliza: Ni nani aliye mbora, wewe ama Ibrahim? Ali alijibu: Mimi na mbora, kwani Ibrahim alisema: Mola Wangu! nionyeshe jinsi unavyofufua wafu. (Mungu) Akasema: Kwani huamini? Akasema: Hasha! bali ili moyo wangu utue ..... (2:260) Imani yangu ilikuwa kiasi kwamba nilisema: Hata kama pazia la yale yaliyo ghaibu lingefunuliwa, imani yangu isingeongezeka. Sasaa akauliza: Ni nani mbora, wewe au Musa? Imam Mtukufu akajibu: Mimi ndiye mbora, kwani wakati Mwenyezi Mungu Mtukufu alipomtuma Musa kwenda Misri kumlingania Firauni kwenye haki, Musa alisema: Mola Wangu! Kwa hakika niliuwa mmoja wao, kwa hiyo naogopa wataniuwa. Na ndugu yangu Harun ni fasihi zaidi ulimi wake kuliko mimi. Basi mtume aende pamoja nami kunisaidia, ili anisadikishe. Hakika mimi na hofu watanikadhibisha. (28: 33-34) Mtukufu Mtume aliniagiza mimi, kwa amri ya Allah kwenda Makka kuzisoma aya za Sura ya Al-Baraa kutoka juu ya Kaaba kwa makafiri wa Quraishia. Mimi sikuwa na hofu, ingawaje kulikuwa na watu wachache ambao walikuwa hawajapoteza ndugu yao wa karibu kwa upanga wangu. Kwa kuitii amri yake, niliitekeleza kazi hiyo peke yangu. Nilizisoma aya za al-Baraat na nikarejea. Sasaa akauliza tena: Ni nani mbora, wewe au Isa (ibn Mariam)? Ali akasema: Mimi ni mbora, kwani wakati Mariam alipokuwa mjamzito kwa Rehma za Mwenyezi Mungu, na wakati wake wa kujifungua ukakaribia, ulishushwa wahyi kwake: Ondoka katika Nyumba hii tukufu, kwani Nyumba hii ni nyumba ya ibada, sio mahali pa kuzalia watoto. Matokeo yake aliondoka kwenye Nyumba tukufu hiyo na akaenda kwenya kichaka ambako alijifungua mtoto Isa. Lakini wakati mama yangu mimi, Fatima binti al-Asad, alipojisikia uchungu wa uzazi ndani ya eneo la Kaaba tukufu, alingangania kwenye ukuta na akamuomba Mwenyezi Mungu kwa jina la Nyumba ile na mjenzi wa Nyumba ile, ili apunguziwe maumivu yake. Mara ufa ukajitokeza katika ukuta huo, na mama yangu akasikia sauti ya kimuujiza ikimwambia, Ewe Fatima! Ingia kwenye Nyumba ya Kaaba. Yeye akaingia ndani na mimi nikazaliwa ndani ya Kaaba tukufu.
182
Mikesha ya Peshawar
183
Mikesha ya Peshawar
Ali alikuwa na sifa zote ambazo Mitume wengine walikuwa nazo mmoja mmoja. Hadithi hii inayokubaliwa na wote huthibitisha kwamba Ali alikuwa na fadhail za hali ya juu sana, ambazo kila moja ya hizo ilikuwa sawa na sifa za juu sana za Mitume. Ni wazi kwamba, mtu ambaye alikuwa na fadhaila za juu sana za mitume wote, basi aliwapita wote kwa cheo. Sheikh Sulayman Balkhi Hanafi katika Yanabiul-Mawadda, Sura ya 40, ananukuu kutoka kwenye Manaqib ya Khawarizmi kutoka kwa Muhammad Bin Mansur, ambaye alisema kwamba alimsikia Ahmad Ibn Hanbal akisema: Kulikuwa hakuna sifa kama hizo kwa Sahaba yeyote wa Mtume, kama zilivyokuwa kwa Ali Bin Abu Talib. Muhammad Bin Yusuf Ganji Shafii vile vile anasimulia maneno yenye maana hiyo hiyo. Ibn Abil-Hadid Mutazali katika Sharhe-Nahjul-Balagha, juzuu ya 1, uk. 46, anasema: Ali alikuwa ndiye mtu mwenye kufaa sana katika nafasi ya Wilaya (Ulinzi) kwa fadhaili za ubora wake. Ukimuondoa tu Mtume wa Allah, alikuwa ni mtu mwenye kustahiki sana kwa cheo cha Khalifa. Ali kwa hakika alikuwa mwenye kustahiki zaidi kwa Ukhalifa, lakini aliwekwa kando kwa mbinu za kisiasa za watu duni. Angalau wangelimjulisha Ali kwamba walikuwa wakifanya mkutano huko Saqifa Bani Sada kuangalia juu ya suala muhimu la kumchangua Khalifa. Hawakufanya hivyo ili kumnyima haki yake ya urithi.
184
Mikesha ya Peshawar
kijana kuyaweka pembeni madai ya masahaba watu wazima. Na hatuchukilii kuachwa huku kwa Ali kama ni kushindwa kwake, kwani ubora wake kwa upande mwingine hukubaliwa na wote. Vile vile kuna hadithi iliyosimuliwa na Khalifa Umar kutoka kwa Mtume, ambaye alisema: Utume na uongozi haviwekwi pamoja katika familia moja. Kwa hiyo, Ali alinyimwa ukhalifa kwa sababu anatokana na familia ya Mtume. Alikuwa hafai kwa ajili ya cheo hicho.
185
Mikesha ya Peshawar
Muombezi: Je, Mtume, mtu anayefaa zaidi kuongoza ummah, aliitoa haki yake kwa upande wa ummah wake? Je, alitoa haki yake ili kwamba watu wa ukoo wa Aus, ambao walikuwa maadui kwa ukoo wa Khazraj, wale kiapo cha utii kwa ajili ya hofu ya maadui wao kushika madaraka? Je, aliacha haki yake ili kwamba watu wake waunde serikali kwa misingi ya hofu na ulafi? Je, unaweza kuita kikundi hiki kidogo cha watu kuwa ndio ummah? Je, Waislamu wa Makka, Yemen, Jeddah na miji mingine hawakuwa sehemu ya ummah? Je, hawakuwa na haki ya kutoa maoni yao kuhusiana na ukhalifa? Kama kulikuwa hakuna hila, kwa nini wasingojee na kupata msimamo wa Waislamu wote katika suala muhimu kama hili la Ukhalifa? Katika njia hii, Ijmai kwa maana yake halisi ingewza kupatikana. Hata leo, ili kusimamisha serikali ya kidemokrasi au kuchagua kiongozi wa taifa, hufanyika uchaguzi mkuu. Wananchi wanapiga kura zao, na kiongozi anachaguliwa kwa wingi wa kura. Viongozi wa nchi zilizostaarabika na watu wote wastaarabu wataucheka utaratibu wenu huu wa Ijmai usio na mpangilio mzuri. Hafidh: Kwa nini unajiigiza katika mazungumzo yasiyopendeza? Ijmai ina maana kwamba kulikuwa na mkusanyiko wa watu wenye akili na masahaba wakubwa ambao walikutana ndani ya Saqifa. Muombezi: Unasema kwamba Ijmai ilimaanisha kwamba kulikuwa na mkusanyiko wa watu wenye akili na masahaba wakubwa wa Mtume, lakini huna msingi wowote kwa maelezo haya isipokuwa hadithi uliyoitaja. Ni wapi hadithi imetaja watu wenye akili au masahaba wakubwa? Narudia kwamba neno umma maana yake ni umma wote, sio idadi ndogo ya Masahaba, hata kama wakiwa wana elimu. Hata kama unayosema yakiwa ni kweli, kwamba Ijmai maana yake mkusanyiko wa watu wenye akili na masahaba wakubwa, je, watu wenye akili na masahaba wakubwa wa Mtume walikomea kuwa ni hao watu wachache tu ambao walikusanyika chini ya paa dogo la Saqifa siku hiyo? Je, kulikuwa hakuna watu wengine wenye akili na masahaba wakubwa katika ulimwengu wa ki-Islamu? Na je, wote kwa pamoja walipiga kura kwa ajili ya Khalifa? Hafidh: Kwa vile suala la Khalifa lilikuwa ni jambo nyeti, watu walikuwa wanahofia kwamba huenda kukatokea machafuko. Ilikuwa haiwezekani kuwaarifu Waislamu katika sehumu nyingine. Wakati Abu Bakr na Umar waliposikia kwamba baadhi ya Ansar wamekusanyika kule, na wao vile vile walikwenda kule kuzungumza. Kwa sababu Umar alikuwa mwanasiasa mweledi, aliona kwamba inafaa kwa ummah kula kiapo cha utii kwa Abu Bakr. Wengine walimfuata na kula kiapo cha utii kwa Abu Bakr, lakini kikundi cha Ansar na watu wa ukoo wa Khazraj wanaomuunga mkono Sad Bin Ubaida, hawakula kiapo cha utii na wakaondoka Saqifa. Hiyo ndio ilikuwa sababuya kwa nini walifanya haraka. Muombezi: Hivyo na wewe unakubali, kama wanahistoria na maulamaa wenu walivyokubali, kwamba katika siku ya Saqifa, wakati mashauri ya msingi yalipokuwa
186
Mikesha ya Peshawar
yanafanyika kulikuwa hakuna Ijmai. Kwa ajili ya maslahi ya kisiasa, Abu Bakr alimpendekeza Umar na Abu Ubaida Bin Jarra, na wao pia, kwa kulirudisha pendekezo hilo, walitaja jina la Abu Bakr, wakimuambia kwamba yeye anastahiki zaidi kwa nafasi hiyo. Wao mara moja tu wakala kiapo cha utii kwake. Baadhi ya watu wa ukoo wa Aus waliokuwa pale vile vile walikula kiapo cha utii kwa Abu Bakr kwa msimamo wao wa uadui dhidi ya ukoo wa Khazraj, na vile vile walihofia kwamba Sad bin Ubaida angeweza vinginevyo kuwa Amir. Kwa njia hii uungaji mkono ulipanuka na kuwa mkubwa. Hata hivyo, kama Ijmai ingekuwa ni hoja yenye nguvu kuweza kutegemewa, wangelisubiri mpaka umma wote au, kama ulivyosema: watu wenye akili wakusanyike pale kupata idhini ya umma wote. Hafidh: Nimekuambia kwamba hofu ya machafuko ililazimisha kundi hili kutenda kama walivyofanya. Watu wa ukoo wa Aus na Khazraj wamekusanyika katika Saqifa na walikuwa wakigombana wenyewe kwa wenyewe. Kila mmoja wao anataka kuamua uhuru wa dola ya ki-Islamu kwa ajili yao wenyewe. Muombezi: Nakubaliana na unayoyasema. Muhammad Bin Jarir Tabari (tazama Tarikh yake, Jz. 2, uk. 457) na wengine wameandika kwamba, Waislamu hawakukusanyika chini ya Saqifa kumchagua Khalifa wao. Koo za Aus na Khazraj zilitaka kujichagulia Amir wao wenyewe. Abu Bakr na Umar wakanufaika kutokana na tofauti zao. Kama kweli walikusanyika kujadili Ukhalifa, kwa kweli wangeliwaita Waislamu wote kutoa maoni yao juu ya suala hilo. Kama ulivyosema: Hawakuwa katika hali ya kuweza kuwajulisha Waislamu wote, na muda ulikuwa unakimbia. Ilikuwa kweli kwamba walikuwa hawana mawasiliano ya mara moja na Makka, Yemen, Taif, au miji mingine ya mbali ya Waislamu. Lakini je, walikuwa hawana hata njia ya kuwasiliana hata na Jeshi la Usama Bin Zaid, ambalo lilikuwa limepiga kambi nje kidogo ya Madina? Hivi wasingeweza kuwaarifu masahaba wakubwa wa Mtume ambao walikuwa kule? Mmoja wao alikuwa mtu maarufu, Kamanda wa jeshi la Waislamu, aliyechguliwa na Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) mwenyewe. Abu Bakr na Umar walikuwa chini yake. Wakati Usama aliposikia kwamba, kwa hila watu watatu wamemchagua Khalifa bila kuwashauri watu wengine, au hata kuwajulisha, na kwamba walikuwa wamekula kiapo cha utii kwa mtu moja, alipanda farasi wake mpaka kwenye mlango wa Msikiti na akesema kwa sauti kubwa: Vurugu yote hii ni ya nini? Kwa amri ya nani mmemchagua Khalifa? Kulikuwa na umuhimu gani, wa watu wachache ambao bila kuwashauri masahaba, wamemchagua Khalifa? Umar akajitokeza mbele kumtuliza na kusema: Usama! Kazi hiyo imekwisha. Kiapo cha utii kimekwishatolewa. Usisababishe vurugu sasa miongoni mwa watu. Na wewe mwenyewe pia ule kiapo cha utii. Usama akakasirika, na kusema: Mtume amenifanya mimi Amir wenu, akasema. Inawezekana vipi Amir aliyeteuliwa na Mtume atoe heshima ya utii kwa watu wa chini ambao waliwekwa chini ya amri yake? Ingawa mengi zaidi yalitokea, kiasi hiki kidogo kinatosha kuthibitisha hoja yangu.
187
Mikesha ya Peshawar
188
Mikesha ya Peshawar
Je, Ijma yenu hii kwa haki inaundwa na watu watatu? Ni wapi katika sehemu yoyote ya ulimwengu ambako utaratibu kama huu unakubalika? Tuchukulie kwamba watu watatu au kikundi chochote cha watu, wakakusanyika katika mji na wakaunda Ijma na kisha wakamchagua kiongozi wa nchi. Je, ni wajibu juu ya Maulamaa na wasomi wa miji mingine yote kuwatii? Au hata kama baadhi ya watu wenye ujuzi na wasomi ambao hawakuchaguliwa na wengine kutoa mawazo, je, ni lazima kwamba wasomi na maulamaa wote waliobakia wawafuate wao? Je, ni sahihi kukandamiza hisia za umma wote kwa tabia ya vitisho vya kundi moja la watu? Kama kwa upande mwingine, katika mijadala ya kielimu, kundi la watu wakafichua kwamba Ukhalifa haukithibitshwa na sheri za dini au za asili, ni haki kuwaita Rafidhi? Unasema kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) aliliacha suala la Ukhalifa juu ya umma au kwa wasomi wa Umma, kama unavyoita. Je, wasomi wa Umma wanaundwa na Abu Bakr, Umar na Abu Ubaida Jarra? Kila mmoja akipendekeza jina la mwingine, na kisha wawili kati yao wakamkubali wa tatu. Na hiyo ikawa mwisho. Je, ni wajibu kwa Waislamu wote kuwafuata wao? Wachache, wengi, na Ijma humaanisha vitu tofauti kabisa. Kama mkutano wa kushauriana unafanywa kwa ajili ya kuangalia tatizo fulani, na idadi ndogo ya watu ikatoa wazo moja, ambapo ile idadi kubwa ya watu ikatoa wazo jingine, kisha inasemwa kwamba, moja ni maoni ya wachache. Maoni ya idadi kubwa ya watu yanaitwa maoni ya wengi, na kama wote (bila tofauti yoyote) wakatoa kauli moja, inaitwa Ijmai. Je Ijmai ilifikiwa ndani ya Saqifa au baadae Msikitini, au baada ya hapo katika mji wa Madina? Kama, hata hivyo, kwa kustahi matakwa yako, tukiondolea mbali haki za umma wote na kusema kwamba maoni ya wasomi na masahaba wa Mtume yalikuwa yanatosha kwa ajili ya Ijmai, nauliza je! Kulikuwa na Ijmai amabayo kwamba wasomi wote na masahaba mashuhuri wa Mtume walishiriki? Je, kikundi kidogo kile kule Saqifa kilikubaliana wote katika maoni yao? Jawabu lake lazima litakuwa ni hapana. Mwandishi wa Mawaqif mwenyewe amekiri kwamba kulikuwa hakuna Ijmai wakati wa Ukhalifa wa Abu Bakr, na kwa yakini vile vile kulikuwa hakuna maoni ya wote miongoni mwa wanachuoni wa Madina. Sad Bin Ubaida Ansari, kizazi chake, masahaba mashuhuri wa Mtume, Bani Hashim wote, rafiki zao, na Ali Bin Abu Talib, - wote walimpinga Abu Bakr kwa muda wa miezi sita. Watu hawa katu hawakula kiapo cha utii kwake. Mjini Madina, makazi ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), hakuna Ijmai iliyofikiwa ambayo kwayo wasomi na masahaba walimuunga mkono Abu Bakr kama Khalifa. Wanahistoria wenu mashuhuri wenyewe, kama Imamu Fakhrud-Din Razi, Jalalud-Din Suyuti, Ibn Abil-Hadid Mutazali. Tabari, Bukhari na Muslim, wameandika kwamba Ijma kamwe haikutokea hapo Madina. Bani Hashim, Bani Umayya, na masahaba kwa ujumla isipokuwa hao watu watatu waliotaja hapo juu hawakuwepo Saqifa ili kupiga kura zao. Aidha, wengi waliupinga uamuzi huo kwa nguvu sana. Kusema kweli, baadhi ya masahaba wakubwa ambao walikataa kula kiapo cha utii kule Saqifa, walikwenda msikitini na kulalamika kwa Abu Bakr. Miongoni
189
Mikesha ya Peshawar
mwa muhajirina walikuwa ni; Salman Farsi, Abu Dharr Ghifari, Mikidadi bin Aswad Kindi, Ammar-e-Yasir, Buraida Aslami, na Khalid Bin Said Bin Aas Amawi. Miongoni mwa Ansari walikuwa; Abul-Hathama bin Tihan, Khuzaima Bin Thabit DhushShahadatain, Abu Ayyub Ansari, Ubai bin Kab, Sahl Bin Hunaif, Uthman Bin Hunaif, ambao walipingana na Abu Bakr ndani ya Msikiti. Nimetoa tu kwa mukhtasari mfupi juu ya matukio haya. Hakuna Ijmai ya aina yoyote iliyofikiwa. Ijma inayosemwa ya wasomi na masahaba mashuhuri wa Madina ni uwongo mtupu. Kwa kutegemea juu ya vyanzo vyenu wenyewe, nitakupa ordha ya majina ya wale ambao walipinga Ukhalifa. Ibn Hajar Asqalani na Baladhuri, kila mmoja katika Tarikh yake, Muhammad Bin Khawind Shah katika kitabu Rauzatus-Safa, Ibn Abdul-Birr katika Istiab na wengine wanasema kwamba , Sad Bin Ubaida na sehemu ya Makhawarij na kikundi cha Makuraishi hawakula kiapo cha utii kwa Abu Bakr. Aidha, watu kumi na nane ambao walikuwa Masahaba wakubwa na mashuhuri wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) hawakula kiapo cha utii kwa Abu Bakr. Walikuwa ni Mashia wa Ali Bin Abu Talib. Majina ya watu hao kumi na nane ni haya yafuatayo: 1. Salman Farsi 2. Abu Dharr Ghifari 3. Mikidadi Bin Aswad-e-Kindi 4. Ammar Yasir 5. Khalid Bin Saidbin al-Aas 6. Buraida Aslami 7. Ubaid Bin Kab 8. Khuzaima Bin Thabit Dhush-Shahadatain 9. Abul-Hathama Bin Tihan 10. Sahl Bin Hunaif 11. Uthmani Bin Hunaif Dhush-Shahadatain 12. Abu Ayyub Ansari 13. Jabir Ibn Abdullah Ansari 14. Hudhaifa bin Yaman 15. Sad Bin Ubaida 16. Qais Bin Sad 17. Abdullah Bin Abbas 18. Zaid Bin Arkam Na Yakubi anaandika katika Tarikh yake: Kikundi cha Muhajirina na Ansari kilijitenga bila kula kiapo cha utii kwa Abu Bakr, na walikuwa ni wafuasi wa Hadhrat Ali. Miongoni mwao walikuwa ni Abbas Bin Abul-Muttalib, Fazl Bin Abbas, Zubair Ibnul-Awwam Bin As, Khalid Bin Said, Miqdadi Bin Umar, Salman Farsi, Abu Dharr Ghifari, Ammar Yasir, Baraa Bin Azib, na Ubai Bin Kab.
190
Mikesha ya Peshawar
Je, watu hawa hawakuwa wasomi wa Umma? Ali, Abbas, ami yake Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) na watu wengine mashuhuri wa ukoo wa Bani Hashim je, watu hawa hawakuwa ni wenye busara na waaminifu? Ilikuwa Ijma ya aina gani hiyo, ambayo ilifanyika bila ushauri wa watu hawa? Wakati Abu Bakr anachaguliwa kwa siri siri, na Masahaba wengine mashuhuri hawakujulishwa, je, hii inakuwa ni Ijma? Au ni njama za kisiasa?
191
Mikesha ya Peshawar
Sasa hiyo ilikuwa ni Ijmai ya aina ngani? Masahaba wakubwa, wasomi, na kizazi cha Mtume walikuwepo hapo Madina wakati wa Saqifa. Hivyo hakuna shaka kwamba suala hili halikuamuliwa kwa wingi wa kura, wachilia mbali Ijma. Ibn Abdul-Birr Qartabi, mwanacuoni mkubwa wa madhehebu yenu, katika kitabu chake Istiab, Ibn Hajar katika Isaba, na Maulamaa wengine wanaandika kwamba, Sad Bin Ubaida, ambaye alikuwa ni mgombea wa Ukhalifa, kwa msimamo mkali kabisa alikataa kula kiapo cha utii kwa Abu Bakr na Umar. Hakutaka kusababisha vurugu, hivyo aliondoka na kwenda Syria. Kwa mujibu wa riwaya katika Rauzatus-Safa, kwa uchochezi wa mtu maarufu, yeye aliuawa. Kwa mujibu wa wanahistoria, mtu ambaye alitenda jinai hiyo ni Khalid Bin Walid. Baada ya kumuua Malik Bin Buwaira na kumuoa mke wake, wakati wa mwanzo wa Ukhalifa wa Abu Bakr, Umar akawa ni mwenye kumchukia sana, wakati Umar alipokuwa khalifa, Khalid akamuua Sad Bin Ubaida kwa ajili ya kutaka kupata upendeleo wa Umar. Hafidh: Kwa vile kulikuwa na hatari ya vurugu, na hawakuweza kupata mawasiliano kwa umma wote, walilazimika kutegemea juu ya hao watu wachache waliokuwepo Saqifa ambako kiapo cha utii kilichukuliwa. Baadaye Umma waliuridhia (Ukhalifa huo). Muombezi: Kama kulikuwa hakuna njia za kuwasiliana na Masahaba mashuhuri wa Mtume (saw), na wasomi wa Umma ambao walikuwa nje ya Madina, tafadhali tuambie kwa ikhlasi: Kama kulikuwa hakuna njama katika suala hili, kwa nini wasiwaite wale walio kuwepo mjini Madina kwenye mkutano wa Saqifa? Je, haikuwa ni muhimu kwao kupata ushauri wa Abbas, Ali ibn Abu Talib, na Bani Hashim? Je, maoni ya Umar na Abu Ubaida Bin Jarra yalitosha kwa ulimwengu wote wa ki-Islam? Hoja yako iliyotegemea juu ya Ijma, iwe ya jumla au makhususi, haikubaliki. Wasomi na Masahaba wakubwa hawakushiriki kwayo, badala yake waliipinga. Kama nilivyosema: Ijmai maana yake ni kwamba asiwepo hata na mtu mmoja ambaye hakubaliani na wengine. Katika Ijma hii umekiri kwamba wasomi kwa ujumla hawakushiriki. Imamu Fakhrud-Din Razi katika Nihayatul-Usul anasema kwamba, kulikuwa hakuna Ijmai ya makubaliano katika Ukhalifa wa Abu Bakr na Umar, mpaka baada ya kuuawa kwa Sad Bin Ubaida. Nashindwa kuelewa vipi unaiita Ijmai hii ya kuwazika kuwa ni uthibitisho kwa ajili ya uhalali wa Ukhalifa. Dai lako la pili, kwamba Abu Bakr alikuwa mtu mzima kuliko Ali na kwa hiyo alikuwa anafaa zaidi kwa ajili ya Ukhalifa ni dhaifu kuliko hoja ya kwanza. Kama umri ulikuwa sharti juu ya Ukhalifa, basi walikuwepo watu wazima wengi kuliko Abu Bakr na Umar. Kwa hakika Abu Qahafa, baba yake Abu Bakr alikuwa mkubwa kuliko mtoto wake, na alikuwa yu hai wakati ule. Kwa nini asichaguliwe kuwa Khalifa? Hafidh: Umri wa Abu Bakr ukiungana na uwezo wake, ulimfanya kuwa chaguo la sawa sawa. Wakati kulikuwa kuna mzee, mwenye ujuzi, mtu anayependwa na Mtume katika Umma, kijana mdogo asiye na uzoefu hawezi kupewa amana ya uongozi.
192
Mikesha ya Peshawar
Muombezi: Kama hiyo ingekuwa ni kweli, basi shabaha ya upinzani wako ni Mtume mwenyewe. Wakati alipoondoka kwenda kwenye vita vya Tabuk,wanafiki kwa siri walipanga kufanya maasi mjini Madina wakati akiwa hayupo. Kwa hiyo aliteua mtu mzoefu kushika nafasi yake ili aweze kudhibiti hali mjini Madina na kuivunja ile mipango ya wanafiki. Nakuomba utueleze, Mtume alimuacha nani katika nafasi yake mjini Madina kama mrithi na Khalifa wake? Hafidh: Inajulikana sana kwamba alimfanya Ali khalifa na mrithi wake. Muombezi: Je, Abu Bakr, Umar na masahaba wengine wazee zaidi hawakuwepo Madina wakati huo? Ndio. Na bado Mtume akamfanya kijana mdogo, Ali, kuwa Khalifa na mrithi wake. Kwa ajili ya kusoma baadhi ya aya za Sura ya Al-Baraa, ya Qurani Tukufu kwa watu Makka, mtu pengine angefikiri kwamba, mtu mzoefu lazima angekuwa anafaa kwa kazi hiyo. Lakini Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alimurudisha mzee Abu Bakr kutoka kwenye nusu ya safari yake, na akamuamuru yule kijana mdogo, Ali kutekeleza jukumu hili muhimu. Mtukufu Mtume akasema kwamba Allah amemwambia kwamba mtu wa kuwasilisha hiyo Qurani tukufu lazima awe ni yeye mwenyewe Mtume au mtu ambaye anatokana naye. Halikadhalika, kwa ajili ya kuwaongoza watu wa Yemen, kwa nini Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alimtuma Kiongozi wa Waumini Ali badala ya mzoefu zaidi Abu Bakr, Umar, au wengine waliokuwepo pale? Na katika matukio mengi kama haya, wakati wakiwepo Abu Bakr, Umar na wengine, alimteua Ali kutekeleza majukumu makubwa. Hivyo ina maana kwamba ukhalifa unaousisitiza ni ustahili. Imenijia hivi punde tu kwamba uthibitisho wa nguvu wa kukataliwa kwa ukhalifa wa watu hawa ni upinzani wa ile inayoitwa ijmai kwa Ali, ambaye kwa mujibu wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), alikuwa ni mwenye kubainisha kati ya haki na batili. Maulamaa wenu mashuhuri wamesimulia hadithi nyingi kuhusiana na suala hili. Sheikh Suleimani Balhki Hanafi katika kitabu chake Yanabiul-Mawadda, Sura ya 16 akinukuu kutoka Kitabus-Sabiin-Fi-Fadhail-e-Amirul-Muminin, Imamul-Haram Abu Jafar Ahmad bin Abdullah Shafii, katika hadithi ya 12 iliyosimuliwa kutoka Firdaus ya Dailami ya hadithi ya sabini, Mir Sayyid Ali Hamadani Shafii katika Mawaddatul-Qurba, Mawadda ya 6, Hafidh katika kitabu chake Amali, Muhammad bin Yusuf Ganji Shafii katika kitabu chake Kifayatut-Talib, Sura 44 anasimulia pamoja na hitilafu ndogo katika maneno, kutoka kwa Ibn Abbas, Abi Laila Ghifari, na Abu Dharr Ghifari kwamba, Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alisema (kifungu cha mwisho kikiwa sawa katika kila hadithi): Punde tu baada ya kuondoka kwangu kwenye ulimwengu huu, yatatokea machafuko. Wakati yakitokea, lazima mumfuate Ali Bin Abi Talib kwa vile atakuwa mtu wa kwanza kukutana na mimi na kupeana mikono na mimi katika Siku ya Hukumu. Yeye ametukuka kwa daraja na ni mwenye kubainisha kati ya haki na batili. Wakati Mtume alipofariki, machafuko makubwa yalitokea. Muhajirina na Ansar walitaka
193
Mikesha ya Peshawar
kupata Khalifa kutoka upande wao. Kwa mujibu wa maelekezo ya Mtume, Umma ulipaswa kumleta Ali ili kwamba aweze kubainisha kati ya haki na batili. Hafidh: Hadith hii ina simulizi pekee (Hadith Ahad) na kwa hiyo si ya kutegemewa. Muombezi: Nilikwisha jibu pingamizi lako kuhusu hadithi pekee. Maulamaa wa ki-Sunni huchukulia hadithi kama hiyo kama hoja ya msingi, hivyo huwezi kuikataa katika misingi hiyo. Mbali na hilo, sio hadithi hiyo pekee katika jambo hili. Kuna riwaya nyingi kama hizo zilizosimuliwa na Maulamaa wenu wenyewe ambazo zinaelekeza kwenye maana hiyo hiyo, ambzo baadhi yake nimezitaja katika mikesha iliyopita. Kwa kuzingatia kikwazo cha muda wetu kuwa mfupi, nitakomea katika kutaja tu hapa baadhi ya majina ya waandishi. Moja ya riwaya hizi inasimuliwa na Muhammad Bin Talha Shafii katika kitabu chake Matalibus-Suul, Tabari katika Tafsir Kabir, Baihaqi katika Sunan yake, Nurd-Din Maliki katika kitabu chake Fusull-Muhima, Hakim katika kitabu chake Mustadrak, Hafidh Abu Naim katika kitabu chake Hilya, Ibn Asakir katika kitabu chake Tarikh Ibn Asakir, Ibn Abil-Hadid katika Sharhe yake ya Nahjul-Balagha, Tabrani katika kitabu chake Ausat, Muhibud-Din katika kitabu chake Riyaz Hamwaini katika kitabu chake Faraid, Suyuti katika kitabu chake Durr-e-Mansur, kutoka kwa Ibn Abbas, Salman, Abu Dharr na Hudhifa wote wanasimulia kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), akinyoosha mkono wake kuelekea kwa Ali Bin Abi Talib, alisema: Hakika huyu Ali ndiye mtu wa kwanza ambaye alitangaza imani yake kwangu na wa kwanza ambaye atakayepeana mikono na mimi katika Siku ya Hukumu. Yeye ni Siddiq-e-Akbar (mkweli mkubwa) na Faruq wa Umma huu (mtambuzi wa Umma huu). Atabainisha kati ya haki na batili.
194
Mikesha ya Peshawar
hivyo vile vile kuna hadith nyingine iliyosimuliwa na Sheikh Sulemani Qunduzi Hanafi, katika Sura ya 20 ya Yanabiul-Mawadda, kutoka kwa Hamwaini kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alisema: Ali yuko pamoja na haki na haki iko pamoja na Ali. Hafidh Abi Naiim Ahmad ibn Abdullah Ispahani katika kitabu chake Hiyatul-Auliya Jz. 1, uk. 63, anasimulia kwamba, Mtume alisema: Enyi kundi la Ansar! Je, nikuelekezeni kwa mtu ambaye kama mkishikamana naye kamwe hamtapotea? Wote wakasema: Ndio, Ewe Mtume wa Allah. Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akasema: Mtu huyo ni Ali. Mpendeni kama mnavyonipenda mimi, na mheshimuni kama mnavyoniheshimu mimi, yale niliyokuambieni yalikuwa ni amri ya Allah iliyosimuliwa kwangu na Jibril. Lengo la ujumla la hadithi hizi ni kuonyesha dalili za upendeleo wa Mtume kuhusiana na mrithi wake. Mtume aliamrisha Umma wake kugeukia kwa Ali baada yake na kumfuata yeye. Kwa mwanga wa hadithi kama hizi, tueleze upinzani wa Ali kwa Abu Bakr una maanisha nini kwako. Kwa hakika inasikitisha sana na kushangaza kwamba haraka kubwa mno ilifanywa katika siku ya Saqifa. Kila mtu mwenye akili ambaye anajua yaliyotokea katika siku hiyo amefadhaika mno. Kama kulikuwa hakuna njama, kwa nini wasingoje (angalau kwa saa chache) ili kwamba Ali Bin Abi Talib, Bani Hashim, na Abbas waweze kuelezea maoni yao juu ya Ukhalifa? Hafidh: Kulikuwa hakuna njama. Kwa vile walihofia vurugu, walifanya haraka kuamua suala la Ukhalifa kwa ajili ya usalama wa Uislamu. Muombezi: Una maana kwamba Abu Ubaida Jarra, mchimba kaburi wa zamani wa Makka, na wengine walikuwa na wasiwasi zaidi na usalama wa Uislamu kuliko Abbas, ami yake Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) anayeheshimiwa, na Ali Bin Abi Talib? Una maana kwamba kama wangelingojea kwa muda kidogo, au kama Abu Bakr na Umar, wakiwashughulisha watu, wangemtuma Abu Ubaida kumjulisha Abbas na Ali juu ya hali hii mbaya, hilo lingefanya Uislamu uangamie? Tafadhali jaribu kuwa mkweli. Kama wangewakaribisha watu wanaostahili huko Saqifa, nafasi yao ingelikuwa salama zaidi. Kusingelikuwa na hitilafu katika Uislamu kama ilivyo leo. Baada ya miaka 1335, sisi ndugu wa ki-Islamu tusingezozana wenyewe kwa wenyewe kama tulivyo usiku huu, bali tungekuwa tumeungana katika kumpinga adui yetu wa pamoja. Sehemu kubwa ya msingi wa jengo hili lenye kasoro la Uislamu uliwekwa siku hiyo. Ilikuwa ni kwa ajili ya haraka za watu wale watatu za kutaka kukamilisha mipango yao ya siri. Nawab: Bwana mheshimiwa, tafadhali tueleze kwa nini walifanya haraka. Kwa nini wasiwajulishe hata watu waliokuwa Msikitini au katika nyumba ya Mtume? Muombezi: Sababu sio za kutafuta mbali. Walifanya haraka kwa sababu walijua kwamba kama wakingojea Waislamu wote waje, au angalau hata watu mashuhuri wa jeshi la Usama Bin Zaid, masahaba mashuhuri wa Mtume waliokuwepo mjini Madina, au Bani Hashim, jina la Ali, miongoni mwa mwa mengine, lingependekezwa. Uwezekano wa kisiasa wa
195
Mikesha ya Peshawar
Abu Bakr na Umar ungelipunguzwa sana. Hivyo basi waliharakisha mipango yao ili kwamba, wakati ambapo Bani Hashim na masahaba mashuhuri wakiwa wanajishughulisha na taratibu za mazishi ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), wao walifanikiwa katika kumteua Abu Bakr kuwa Khalifa juu ya msingi wa kura za watu wawili! Waliucheza mchezo huo, na usiku huu hapa ninyi watu wazuri mnaupa jina la ijmai! Hata ulamaa wenu wakubwa, kama Tabari, Ibn Abil-Hadid na wengine wameandika kwamba Umar alisema: Ukhalifa wa Abu Bakr ulisimamishwa kwa haraka sana. Allah atusaidie! Amma kwa madai yenu mengine, ambayo mnayatoa kutoka kwa khalifa Umar, kwamba utume na utawala haviwezi kuchanganywa kwenye familia moja, vile vile yanakataliwa kwa mujibu wa Qurani Tukufu:
Au wanawahusudu watu kwa yale aliyowapa Allah kutokana fadhila Zake? Basi tuliwapa ukoo wa Ibrahim Kitabu na hikma na tukawapa mamlaka makubwa. (4:54) Hadithi hii ambayo inahusishwa na Khalifa Umar, ni ya kubuniwa. Mtume kamwe hajasema neno lenye kukinzana na amri ya Qurani Tukufu. Aidha, ukhalifa hauwezi kutenganishwa na utume kwa sababu Khalifa wa kweli ni mfano wa sheria ya Mungu inayofanya kazi ulimwenguni. Kuuchukulia ukhalifa kama kazi ya kisiasa tu iliyotenganishwa na utume ndio kosa lenyewe hasa lililofanywa na Abu Bakr na Umar. Kama Harun, ndugu yake Mtume Musa, angeweza kuondolewa kwenye ukhalifa wa Musa, Ali vile vile angeweza kunyimwa ukhalifa wa Mtume. Na kwa vile utume na ukhalifa, kwa mujibu wa Qurani, vilichanganywa juu ya Musa na Harun, hapana shaka ulichanganywa juu ya Muhmmad na Ali. Hadithi yenu hii ilibuniwa na Bani Umayya. Kama utume na ukhalifa usingeweza kuchanganywa katika familia moja, basi kwa nini katika Majilis-eShura (Kamati ya ushauri) Khalifa Umar alimpendekeza Ali kwenye ukhalifa? Hata hivyo, ninyi vile vile mnamkubali kuwa ni Khalifa wenu wa nne! Ni ukinzano wenye kushangaza kwamba kwa kumetegemea juu ya hadithi ya Umar, mnakataa kuchanganywa utume na ukhalifa, lakini wakati Umar mwenyewe alipoidhinisha hali hii miaka michache baadae, mkaiunga mkono! Je, mnaweza kupinga na kuunga mkono pendekezo lile lile moja? Mnasema kwamba utume na utawala havichanganywi katika familia moja, ingawa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) amefanya kuwa ni wajibu kwa Umma wake kufuata kizazi chake. Alisema kwamba kuwa na uadui nao ni kupotea njia. Amesema katika mara nyingi, Ninakuachieni vitu viwili vizito: Kitabu cha Allah (Qurani Tukufu) na Ahulul-Bayt wangu. Kama mkifungamana na viwili hivi, kamwe hatapotea baada yangu. Hadithi hii sahihi imekubaliwa na madhehebu zote. Nimeitaja katika mikesha iliyopita pamoja na vyanzo vyake.
196
Mikesha ya Peshawar
197
Mikesha ya Peshawar
198
Mikesha ya Peshawar
nyingine, itakupasa kumfuata Ali. Ewe Ammar! Ali hatakuruhusu wewe kupotea kutoka kwenye njia ya mwongozo na hatakuongoza kwenye upotovu; Ewe Ammar! Utii kwa Ali ni utii kwangu, na utii kwangu ni utii kwa Allah. Katika mwanga wa Maamrisho haya, na katika mwanga wa upinzani wa Ali kwa Abu Bakr, je, watu siwangemfuata Ali? Hata kama Bani Hashim, Bani Umayya, Masahaba mashuhuri, watu wajuzi wenye elimu wa umma, Muhajirina, na Ansari wasingekuwepo pamoja naye (na walikuwa pamoja naye) watu wangelimfuata Ali. Hafidh: Wakati wa mjadala wetu, umesema vitu viwili vya ajabu. Kwanza, umerudia rudia kumuita Abu Ubaida mchimba kaburi. Unaweza kuthibitisha kwamba hii ilikuwa taaluma ya bwana mkubwa huyu? Pili, umesema kwamba Ali, Bani Hashim, na masahaba hawakula kiapo cha utii kwa Abu Bakr, walimpinga. Lakini wanahistoria na wanahadithiwote wameandika kwamba Ali, Bani Hashim na masahaba wa Mtume walikula kiapo cha utii kwa Abu Bakr. Muombezi: Sio sisi peke yetu tunaodai kwamba Abu Ubaida alikuwa mchimba kaburi. Imo katika vitabu vyenu wenyewe. Unawza kurejea kwenye Al-Bidayya wan-Nihaya, Jz. 5, uk. 266-267 (kitabu) kilichokusanywa na Ibn Kathir Shami, ambaye anasema kwamba, kwa vile Abu Ubaida amezoea kuchimba kaburi za watu Makka, Abbas alimtuma mtu kumtafuta Abu Talha, mchimba kaburi wa Madina, na mtu mwingine kumtafuta Abu Ubaida, ili kwamba wote wawili waweze kuchimba kaburi la Mtume.
KULAZIMISHWA KWA ALI NA BANI HASHIM KULA KIAPO BAADA YA MIEZI SITA
Unasema kwamba Ali, Bani Hashim, na masahaba wa Mtume walikula kiapo cha utii kwa Abu Bakr. Umesoma maneno walikula kiapo cha utii, lakini hukuelewa ni kwa nani na vipi walivyokula kiapo. Wanachuoni wenu wote wa hadithi na wanahistoria wakubwa wameandika kwamba Ali na Bani Hashim walikula kiapo cha utii (kwa nje), lakini hilo limefanywa baada ya miezi sita, na hata hivyo chini ya vitisho vikubwa. Hafidh: Sio vyema kwa mtu mtukufu kama wewe kutumia maneno ambayo hutumiwa na Mashia wa kawaida kwamba, Ali aliburuzwa kutoka kwenye nyumba yake na alitishiwa kuuawa kama asingekula kiapo cha utii. Ukweli ni kwamba katika siku chache za mwanzo za ukhalifa kwa utashi na kwa furaha alikubali ukhalifa wa Abu Bakr. Muombezi: Ali na Bani Hashim hawakula kiapo cha utii kwa mara moja. Wanahistoria wenu wameandika kwamba Ali alikula kiapo cha utiibaada ya kifo cha Hadhrat Fatima. Bukhari katika katika Sahih yake, Jz. 3, Sura ya Ghazawa Khaibar, uk. 37, na Muslim Bin Hujjaj, katika Sahih yake, Jz. 5, uk. 154, wameandika kwamba Ali alikula kiapo cha utii
199
Mikesha ya Peshawar
baada ya kifo cha Fatima. Baadhi ya maulamaa wenu wanaamini kwamba Fatima alikufa siku 75 baada ya kifo cha Mtume. Ibn Qutayba vile vile anashikilia maoni hayo hayo, lakini wanahistoria wenu wengi wanadai kwamba alikufa miezi sita baada ya kufariki kwa Mtume. Kwa hiyo ina maana kwamba kiapo cha Ali kilikuja wakati fulani baada ya miezi 3 au 6 baada ya kufariki kwa Mtume. Masudi katika kitabu chake Murujus-Sahab, Jz. 1, uk. 414, anasema: Hakuna mtu kutoka Bani Hashim aliyekula kiapo cha utii kwa Abu Bakr mpaka baada ya kifo cha Bibi Fatima. Ibrahim Bin Saqafi anasimulia kutoka kwa Zuhri kwamba Ali hakula kiapo cha utii kwa Abu Bakr mpaka miezi sita baada ya alipofariki Mtume, na watu hawakuwa na ujasiri wa kumshawishi isipokuwa baada ya kifo cha Bibi Fatima. Ibn Abil-Hadid katika Sharhe Nahjul-Balagha anasimulia jambo hilo hilo. Kwa hali yoyote, maulamaa wenu wenyewe wanasisitiza kwamba kiapo cha Ali hakikuwa cha haraka bali kilikuja tu baada ya muda fulani kupita na hata hivyo ni wakati mazingira yalipomlazimisha kufanya hivyo. Ibn Abil-Hadid, katika Sharhe Nahjul-Balagha, Jz. 2, uk. 18, anasimulia kutoka kwa Zuhri, kutoka kwa Aisha, ambaye amesema: Ali hakula kiapo cha utii kwa Abu Bakr kwa muda wa miezi sita, na hakuna mtu kutoka Bani Hashim aliyekula kiapo mpaka Ali alipofanya hivyo. Ahmad Bin Asam-e-Kufi Shafii katika Futuh na Abu Nasr Hamidi, katika Jama Bainus-Sahihain anasimulia kutoka kwa Nafiy, akinukuu kutoka Zuhri, ambaye alisema: Ali hakula kiapo cha utii mpaka baada ya miezi ya kufariki kwa Mtume (s.a.w.w.).
200
Mikesha ya Peshawar
HOJA KUMI NA MBILI ZINAZOUNGA MKONO UKWELI KWAMBA ALI ALICHUKULIWA KUPELEKWA MSIKITINI KWA NCHA YA UPANGA
Muombezi: (1) Abu Jafar Baladhuri Ahmad Bin Yahya Bin Jabir Baghdadi, mmoja wa wanahadithi na wanahistoria wenu wa kutengemewa, anaandika katika kitabu chake cha Tarikh - Historia kwamba, wakati Abu Bakr alipomuita Ali ili kula kiapo cha utii, Ali alikataa. Abu Bakr alimtuma Umar akiwa na kijinga kwenda kuchoma moto nyumba ya Ali. Fatima akaja mlangoni na kusema: Ewe mtoto wa Khattab! Umekuja kuichoma nyumba yangu? Akasaema: Ndio, hili lina athari zaidi kuliko kitu chochote alichokifanya baba yako. (2) Izzud-Din Ibn Abil-Hadid Mutazili, na Muhammad Bin Jarir Tabari, wanasimulia kwamba Umar alikwenda kwenye mlango wa nyumba ya Ali pamoja na Usay Bin Khuzai, Salama Bin Aslam na kikundi cha watu. Kisha Umar akaita, Tokeni nje! Vinginevyo nitaichoma nyumba yenu! (3) Ibn Khaziba anataarifu katika kitabu chake Kitab-e-Gharrar kutoka kwa Zaid Bin Aslam, ambaye alisema: Nilikuwa mmoja wa wale waliokwenda pamoja na Umar tukiwa na vijinga vya moto mpaka kwenye mlango wa nyumba ya Fatima. Wakati Ali na watu wake alipokataa kula kiapo cha utii, Umar alimuambia Fatima: Yeyote yule aliyeko ndani ya nyumba atoke nje. Vinginevyo nitaichoma nyumba na yeyote aliyemo ndani.Ali, Hasani, Husein, Fatima, na kikundi cha Masahaba wa Mtume, na Bani Hashim walikuwemo ndani. Fatima akasema: Utaichoma nyumba yangu moto pamoja na mimi mwenyewe na watoto wangu? Akasema: Ndio, Wallahi, kama hawatoki nje na kula kiapo cha utii kwa Khalifa wa Mtume. (4) Ibn Abd Rabbih, mmoja wa maulamaa wenu mashuhuri, anaandika katika kitabu chake Iqdul-Farid, Jz. 3, uk. 63, kwamba Ali na Abbas walikuwa wamekaa nyumbani kwa Fatima. Abu Bakr akamuambia Umar: Nenda ukawalete watu hawa. Kama wakikataa kuja, pigana nao. Hivyo Umar akaenda nyumbani kwa Fatima na vijinga vya moto. Fatuma akaja mlangoni na akasema: Umekuja kuchoma nyumba yetu? Akasema: Ndio na kadhalika. (5) Ibn Abil-Hadid Mutazili katika sharhe yake ya Nahjul-Balagha, Jz. 1, uk. 134, akinukuu kutoka kitabu cha Jauhari, Kitab-e-Saqifa ameandika kwa kinaganaga
201
Mikesha ya Peshawar
kuhusu suala la Saqifa-e-Bani Saad: Bani hashim na Ali walikuwa wamekusanyika nyumbani kwa Ali. Zubair pia alikuwemo kwa vile naye alijiona kama ni mmoja wa Bani Hashim. Ali alizoea kusema, Zubair alikuwa siku zote pamoja nasi mpaka watoto wake walipokuwa wakubwa. Wao wakamgeuza dhidi yetu. Umar akaenda nyumbani kwa Fatima na kikundi cha watu. Usayd na Salma vile vile walikuwa pamoja naye. Umar akawataka watoke nje wachukue kiapo cha utii. Wao wakakataa. Zubair akachomoa upanga wake na akatoka nje. Umar akasema: Mkamateni mbwa huyu. Salma Bin Aslam akamnyanganya upanga huo na akautupa kiambazani. Kisha wakambururuza Ali kumpeleka kwa Abu Bakr. Bani Hashim wengine wakamfuata na walikuwa wanangojea kuona Ali atafanya nini. Ali alikuwa akisema kwamba yeye ni mtumishi wa Allah na ndugu yake Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Hakuna aliyemsikiliza. Walimpeleka kwa Abu Bakr, ambaye alimtaka kula kiapo cha utii kwake. Ali akasema: Mimi ndiye ninayestashiki zaidi katika nafasi hii, na sitakula kiapo cha utii kwako. Ni wajibu juu yako kula kiapo cha utii kwangu. Umeichukuwa haki hii kutoka kwa Ansar kwa kutegemea uhusiano wako na Mtume (s.a.w.w.). Na mimi vile vile, kwa msingi huo huo, nalalamika dhidi yako. Hivyo kuwa muadilifu. Kama unamuogopa Allah, kubali haki yangu, kama Ansar walivyofanya kwa yako. Vinginevyo, itakupasa ukubali kwamba unanidhulumu kwa makusudi. Umar akasema: Hatutakuacha mpaka ule kiapo cha utii. Ali akasema: Mmekula njama wote vizuri sana. Leo unamuunga mkono, ili kwamba kesho aweze kuurudsha ukhalifa kwako. Naapa Wallahi kwamba sitakubaliana na maombi yenu na sitakula kiapo cha utii (kwa Abu Bakr). Yeye anapaswa atoe kiapo cha utii kwangu. Kisha aliwageukia watu na akasema: Enyi Muhajirina! Muogopeni Allah. Msipore haki ya mamlaka ya familia ya Muhammad. Haki hiyo imeamriwa na Allah. Msimuondoe mtu anayestahiki kutoka katika nafasi yake. Kwa jina la Allah sisi Ahlul-Bayt tuna mamlaka makubwa katika suala hili kuliko mlivyo ninyi. Kuna mtu miongoni mwenu ambaye ana ujuzi juu ya Kitabu cha Allah (Qurani), Sunna ya Mtume, na sheria za dini yenu. Ninaapa Wallahi sisi tunavyo vitu vyote hivi. Hivyo msifuate nafsi zenu mkaja mkapotea kutoka kwenye ukweli. Ali alirudi nyumbani bila kula kiapo cha utii na akajitawisha mwenyewe nyumbani kwake mpaka Fatima alipofariki. Hapo tena, alilazimishwa kula kiapo cha utii. (6) Abu Muhammad Abudullah Bin Muslim bin Qutayba Bin Umar Al-Bahili Dinawari, ambaye alikuwa mmoja wa maulamaa na Kadhi rasmi wa mji wa Dinawari, anaandika katika kitabu chake mashuhuri Tarikhul-Khulafati Raghibin wa Daulati Bani Umayya, kijulikanacho kama Al-Imama was-Siyasa, Jz. 1, uk. 13: Wakati Abu Bakr alipofahamu kwamba kundi la watu walio na uadui kwake wamekusanyika katika nyumba ya Ali, alimtuma Umar kwao. Wakati Umar alipompigia kelele Ali atoke nje na kula kiapo cha utii kwa Abu Bakr, wote walikataa kutoka nje. Umar alikusanya kuni na kusema Naapa kwa jina la Allah, ambaye ana uhai wangu katika miliki Yake,
202
Mikesha ya Peshawar
amma mtatoka nje, au nitaichoma nyumba pamoja na wote waliomo ndani. Watu wakasema: Ewe Abu Hafsa! Fatima vile vile yumo ndani. Akasema: Hata akiwemo, nyumba nitaichoma moto tu. Hivyo wote wakatoka nje na kula kiapo cha utii, isipokuwa Ali, ambaye alisema: Nimeweka nadhiri kwamba, mpaka nitakapomaliza kuikusanya Qurani, sitatoka nje ya nyumba wala kuvaa nguo kiukamilifu. Umar hakulikubali hili, lakini malalamiko ya huzuni ya Fatima na kubezwa na wengine, kulimlazimisha kurudi kwa Abu Bakr. Umar alimhimiza kumlazimisha Ali atoe kiapo cha utii. Abu Bakr alimtuma Qanfaz mara kadhaa kumuita Ali, lakini safari zote alikatishwa tamaa. Mwishowe Umar, na kundi la watu walikwenda kwenye mlango wa nyumba ya Fatima. Wakati Fatima aliposikia sauti zao, alipiga kelele: Ewe baba yangu, Mtume wa Allah! Ni mateso gani haya tunayopata kutoka kwa mtoto wa Khattab na mtoto wa Abi Quhafa! Wakati watu hao walipoyasikia malalamiko ya Fatima, baadhi yao walirudi nyuma mioyo yao ikiwa imevunjika, lakini Umar alibaki pale na baadhi ya watu wengine mpaka mwishowe wakamburuza Ali kutoka nje ya nyumba. Walimchukuwa Ali na kumpeleka kwa Abu Bakr, na akamuambia achukue kiapo cha utii kwake. Ali alisema: Kama sikula kiapo cha utii kwako utanifanya nini? Wakasema: Tuna apa kwa jina la Allah kwamba tutaivunja shingo yako.Ali akasema: Mtamuuwa mtumishi wa Allah na ndugu wa Mtume? Umar akasema: Wewe sio ndugu wa Mtume wa Allah. Wakati haya yakijiri, Abu Bakr alinyamaza kimya. Kisha Umar akamuuliza Abu Bakr iwapo yeye (Umar) alikuwa hafuati amri yake katika suala hili. Abu Bakr akasema kwamba muda Fatima yuko hai hatamlazimisha Ali kula kiapo cha utii kwake. Kisha Ali aliweza kufikia kaburi la Mtume, ambako akiomboleza na kulia, alimueleza Mtume kile ambacho Harun alimueleza ndugu yake (Mtume Musa), kama ilivyoandikwa katika Qurani Tukufu:
..Ewe mtoto wa mama yangu! Hakika watu hawa wamenidharau, na wakakaribia kuniuwa( 7:150)
FATIMA ALIWAAMBIA ABU BAKR NA UMAR KWAMBA ANAWALAANI HAO WOTE KATIKA KILA SALA
Baada ya kuelezea Suala hili kwa urefu, Abu Muhammad Abdullah Bin Qutayba anasema kwamba Ali hakula kiapo cha utii na akarudi nyumbani. Baadae Abu Bakr na Umar walikwenda nyumbani kwa Fatima kumbembeleza na kuomba msamaha wake. Fatima akasema: Allah awe ni shahidi wangu kwamba ninyi wawili mmenikosea. Ninawalaani katika kila Salat, na nitaendelea kuwalaani mpaka nitakapomuona baba yangu na kumlalamikia dhidi yenu.
203
Mikesha ya Peshawar
(7) Ahmad Bin Abdul-Aziz ni mmoja wa maulamaa wenu. Ibn Abil-Hadid anaandika kuhusu yeye katika maneno yafuatayo: Alikuwa mtu msomi, mwanahadithi na mwandishi mkubwa. Yeye anaandika katika kitabu chake, Kitab-e-Saqifa, na Ibn AbilHadid Mutazili vile vile anamnukuu katika Sharhe Nahjul-Balagha, Jz. 1, uk. 9, kutoka kwa Abil-Aswad, ambaye amesema: Kundi la Masahaba na Muhajirina mashuhuri walielezea kuhusu kuudhiwa kwao na ukhalifa wa Abu Bakr na wakauliza ni kwa nini wao hawakushauriwa. Vile vile Ali na Zubair walionyesha hasira zao, wakakataa kula kiapo cha utii na wakarudi nyumbani kwa Fatima. Fatima alilia kwa nguvu na akawasihi kwa taadhima sana, lakini bila mafanikio yoyote. Walichukuwa upanga wa Ali na wa Zubair wakazirusha kwenye ukuta na kuzivunjilia mbali. Kisha wakawaburuza mpaka Msikitini na kuwalazimisha kula kiapo cha utii. (8) Jauhari anasimulia kutoka kwa Salma bin Abdur-Rahman kwamba wakati Abu Bakr aliposikia kwamba Ali, Zubair, na kundi la Bani Hashim walikuwa wamekusanyika nyumbani kwa Fatima, alimtuma Umar kwao. Umar alikwenda mpaka mlangoni mwa nyumba ya Fatima na akaita kwa sauti kubwa: Tokeni nje, vinginevyo, naapa nitaichoma nyumba yenu! (9) Jauhari, kwa mujibu wa Ibn Abil-Hadid katika sharhe ya Nahajul-Balagha, Jz. 2, uk. 19, anasimulia kutoka kwa Shabi: Wakati Abu Bakr aliposikia kuhusu mkusanyiko wa Bani Hashim katika nyumba ya Ali, alimuambia Umar: Wewe na Khalid nendeni mkamlete Ali na Zubair waje wale kiapo cha utii. Hivyo Umar aliingia nyumbani kwa Fatima na Khalid akabakia nje. Umar akamuambia Zubair Upanga huu ni wa nini? Akajibu, Nimeupata kwa ajili ya kula kiapo kwa Ali. Umar akaunyakua upanga ule na kuutupa kwenye jiwe ndani ya nyumba na kuuvunja. Kisha akamtoa nje kwa Khalid. Alirudi tena ndani ya nyumba ambako kulikuwa na watu wengi, akiwemo Miqdadi, na Bani Hashim wote. Akimsemesha Ali, alisema: Nyanyuka! Ninakupeleka kwa Abu Bakr. Lazima ule kiapo cha utii kwake. Ali akakataa. Umar akamburuza mpaka kwa Khalid. Khalid na Umar wakamlazimisha katika barabara ambayo ilikuwa imejaa watu ambao walishuhudia kitendo hiki. Wakati Fatima alipoona tabia hii ya Umar, yeye pamoja na wanawake wengi wa Bani Hashim (ambao walikuja kumliwaza), walitoka nje. Walikuwa wakiomboleza na kulia kwa vilio vya sauti ya juu. Fatima alikwenda msikitini ambako alimuambia Abu Bakr: Mapema ilioje umewafukuza Ahlul Bayt wa Mtume wa Allah. Naapa kwa jina la Allah, sitazungumza na Umar mpaka nitakapomuona Allah (yaani Siku ya Hukumu). Fatima alionesha kuchukizwa kwake mno na Abu Bakr na hakuzungumza naye kwa muda wote uliokuwa umebakia wa maisha yake. (Tazama Sahih Bukhari, sehemu ya 5 na 7). (10) Abu Walid Muhibud-Din Muhammad bin Muhammad Bin Ash-Shahna Al-Hanafi (amekufa 815 A.H.), mmoja wa maulamaa wenu wakubwa anaandika katika katika kitabu chake, Raudhatul-Manazir Fi Khabarul-Awail wal-Awakhir kuhusiana na
204
Mikesha ya Peshawar
suala la Saqifa: Umar alikwenda nyumbani kwa Ali akiwa amejiandaa kuichoma nyumba moto pamoja na wote waliokuwemo ndani yake. Umar alisema: Ingieni kwenye kile ambacho umma umeingia. Tabari, katika kitabu chake Tarikh Jz. 2, uk. 443, anasimulia kutoka kwa Ziyad Bin Kalbi kwamba, Talha, Zubair, na baadhi ya Muhajirin walikuwa nyumbani kwa Ali. Umar bin Khattab alikwenda huko na kuwataka watoke nje. Kama hawakutoka, alisema, angeichoma nyumba moto. (12) Ibn Shahna, katika Hashiyya-e-Kamil ya Ibn Kathir, Jz. 11, uk. 112, anaandika kuhusiana na suala la Saqifa kwamba: Baadhi ya Masahaba wa Mtume, na Bani Hashim, Zubair, Atba Bin Abi Lahab, Khalid Bin Said Bin As, Mikidadi Bin Aswad Kindi, Salman Farsi, Abu Dharr Ghifari, Ammar Bin Yasir, Baraa Bin Azib, na Ubai Bin Kab walikataa kula kiapo cha utii kwa Abu Bakr. Walijikusanya katika nyumba ya Ali. Umar Bin Khattab alikwenda kule kwa nia ya kuichoma nyumba. Fatima akamlalamika. Umar akasema: Ingia kule ambako wengine wameingia. Hizi ni sampuli tu za ukweli mwingi wa kihistoria ulioandikwa na wanahistoria wenu. Suala hili lilikuwa linajulikana sana kiasi kwamba washairi wa zamani wamelitaja. Mmoja wa washairi wenu, Hafidh Ibrahim wa Misr, anasema katika shairi la kumsifu Umar: Hakuna mtu mwingine bali Abu Hafsa (Umar) ambaye angelikuwa na ujasiri wa kumuambia mkuu wa ukoo wa Adnan (Ali) na jamaa zake, akisema: Kama mkishindwa kula kiapo cha utii, nitaichoma nyumba yenu, hata Fatima mwenyewe. Hafidhi: Hadithi hizi zinaonyesha tu kwamba walichukuwa vijinga vya moto kuwatisha na kuwatawanyisha wapinzani wa ukhalifa. Kusema kwamba nyumba ya Ali ilichomwa moto na matokeo yake Fatima kuharibu mimba yake, ni maneno yaliyobuniwa na Mashia.
205
Mikesha ya Peshawar
alipoelezwa kwamba Hubbar Bin Aswad amevipiga vitoto vya binti yake (vikiwa tumboni bado) kwa mkuki, ambapo kwa sababu hiyo Zainab akaharibu mimba yake, Mtume aliruhusu yeye auwawe. Abu Jafar akasema: Lau Mtume wa Allah angelikuwa hai bado, kwa hakika angeamuru adhabu ya kifo vile vile kwa yule ambaye amemtisha Fatima kiasi kwamba mtoto wake Muhsin, alikufa kwa mimba yake kuharibika. Hafidhi: Sielewi inasaidia lengo gani la manufaa kwa kusimulia visa hivi. Mambo ya aina hii husababisha kutokuelewana kwa pande hizi mbili. Muombezi: Unakataa kusimulia kwangu mambo haya. Lakini ninafanya hivi kukana shutuma za waandishi waovu wanaowapoteza ndungu zetu ambao hawana ujuzi, na kuwaita Mashia makafir na kusema kwamba mambo haya yalikuwa ni ubunifu wa Mashia. Hatusemi kitu chochote kuhusu Ali mbali na kile ambacho Mtume amesema kuhusu yeye. Tuliwaeleza katika mikesha iliyopita kwamba tunamchukulia Ali kama mja mtiifu wa Allah, makamu na mrithi wa Mtume aliyeteuliwa kwa utaratibu wa Mungu. Unadai kwamba hakuna maana ya kusimulia mambo haya. Kama msingezileta nukta hizi, tusingezijadili. Kama msingesema usiku huu kwamba hizi ni imani za Shia bila hoja ya msingi kwazo, nisingelazimika kuiambia hadhara hii kwamba hizi ni imani za maulamaa wa ki-Sunni wasio na upendeleo. Nawab: Mheshimiwa, tunaamini kwamba Husein, ash-Shahid, alikuwa ameongoka sawasawa na kwamba aliuawa kwa dhulma na maofisa wa Bani Umayya. Lakini kuna baadhi ya watu, hususan miongoni mwa vijana wetu, ambao wanasema kwamba vita vya Karbala vilikuwa ni vya kijeshi (kisiasa), na sio kadhia ya kidini. Inasemekana kwamba Husein Bin Ali alielekea Kufa kutafuta mamlaka, na ni jukumu la kila serikali kuzima hatari kama hizo. Kwa hiyo, Yazid alizuia tishio hili. Walimtaka Mtukufu Imamu kula kiapo cha utii bila masharti kwa Khalifa Yazid, ambaye kwamba utii kwake ilikuwa ni wajibu. Walimtaka aende Syria akaishi kule na Khalifa kwa heshima au arudi mjini kwake (Madina). Lakini hakufuata ushauri wao, na hatimaye aliuawa. Wanahitimisha kwamba maombolezo yoyote kwa ajili ya mtu wa kidunia kama huyu, ambaye aliuawa kwa ajili ya mapenzi yake ya mamlaka, sio tu hayana maana, bali pia ni bida. Je, una jibu kwenye nukta hii? Unakanusha vipi wazo la kwamba vita vya Karbala havikuwa kilele cha harakati za kisiasa?
206
Mikesha ya Peshawar
ushahidi wa usafi wa Husein katika Qurani Tukufu. Anasema: Allah anapenda kuwaondoleeni uchafu, Enyi watu wa nyumba (Ahlul-Bayt)! Na kuwatakaseni kwa utakaso ulio safi kabisa (Qurani; 33:33). Maulamaa wenu wengi, kama Muslim, Tirmidhi, Thalabi, Sijistani, Abu Nuaim Isfahani, Abu Bakr Shirazi, Suyuti, Hamwani, Ahmad Bin Hanbal, Zamakhshari, Baidhawi, Ibn Athir, na wengine wameshikilia kwamba aya hii iliteremshwa kwa kuwatukuza wale watukufu watano, Ahlul-Bayt (watu wa Nyumba): Muhammad, Ali, Fatima, Hasan na Husein. Aya hii ndio uthibitisho mkubwa wa kutokukosea (Masum) na usafi wa watu hawa watukufu. Uchafu mkubwa sana ni mapenzi ya mamlaka ya kidunia. Kuna hadithi nyingi kutoka kwa Mtume na Maimamu zinazolaumu hamu ya mamalaka ya kidunia na utekelezaji wa matamanio yetu maovu. Mtume alisema: Mapenzi na urafiki na dunia ni mzizi wa maovu yote. Abu Abdillah Husein hakuwa na mapenzi na mamlaka ya kidunia. Kwa kweli hakuhatarisha maisha yake na maisha ya familia yake kwa ajili ya kupata utawala wa mpito katika dunia hii. Kama kusimama kwa Husein dhidi ya Yazid kulikuwa kwa ajili ya mamlaka ya kilimwengu tu, Mtume asingeamuru watu kumsaidia. Maulamaa wenu wenyewe wanathibitisha nukta hii. Sheikh Suleimani Balkhi Hanafi katika Yanabiul-Mawadda kutoka katika vitabu vya historia vya Bukhari, Baghawi, na Ibnus-Sikkin kutoka Dhakhairul-Uqba ya Imamul-Haram Shafii, na Sirat-e-Mulla wanasimulia kutoka kwa Anas Bin Harith Bin Bayya, ambaye amesema kwamba alimsikia Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akisema: Hakika, mtoto wangu Husein atauawa katika ardhi ya Karbala. Kila mtu kati yenu ambaye atakuwepo wakati huo lazima amsaidie. Taarifa inaendelea: Anas Bin Harith alifika Karbala na kwa kutii amri ya Mtume, aliuawa shahidi pamoja na Imamu Husein. Kwa hiyo ina maana kwamba kule Karbala Imamu Husein alisimama kwa ajili ya haki na sio kwa mapenzi ya dunia hii. Kuandaa safari kwa Imamu Husein akiwa na kundi dogo, wakiwemo wanawake na watoto wadogo, ni ishara nyingine kuonesha kwamba alitoka nyumbani kwake sio kwa madhumuni ya kupata mamlaka. Kama hiyo ingekuwa ndio nia yake, angelikwenda Yemen, ambako anaungwa mkono na wengi. Yemen ingelikuwa ni kituo cha kimantiki cha kuanzishia shughuli za kijeshi. Kwa hakika rafiki zake mara nyingi wamemshawishi kwenda Yemen, lakini walikuwa hawatambui madhumuni yake. Lakini Imamu Husein alijua kwamba hakuna njia ya kupata mafanikio ya dhahiri. Safari yake ilianza na watu 84, wakiwemo wanawake na watoto, akilenga kwenye msingi mzuri. Ule mti mtukufu la ilaha illallah (hakuna mungu isipokuwa Allah) ulipandwa na babu yake, ukarutubishwa na damu yake na damu ya mashahidi wa Badir, Uhud, na Hunain. Mti huo uliaminishwa kwa mtunza bustani mzuri, Ali Bin Abu Talib, ambaye alizuiwa kwa vitisho vya mauaji na uchomaji moto mali wa makusudi. Matokeo yake ilikuwa kwamba ile chemchem ya Tawhid (upweke wa Mungu) na utume ukakumbwa na mbadiliko ya kipupwe. Taratibu utawala wa bustani ukaangukia
207
Mikesha ya Peshawar
mikononi mwa Bani Umayya waovu. Kuanzia ukhalifa wa Uthman Bin Affan, Bani Umayya wakahodhi utawala wa dola. Abu Sufyan, mzee na kipofu, lakini daima hamu yake ya mamlaka ilikuwa kali, alipiga kelele kwenye baraza ya Bani Umayya: Enyi Bani Umayya! Uzuieni ukhalifa kwenye familia yenu wenyewe. Pepo na moto ni ngano za watu wa kale. Enyi Bani Umayya! Ukamateni ukhalifa kama mpira. Naapa kwa kile ambacho nakiapia, kwamba kila siku nimetamani utawala huu kwa ajili yenu. Uchungeni ili kwamba uwe ni urithi wa vizazi vyenu. Makafiri hawa waliwaondoa watunza bustani sahihi kutoka kwenye bustani. Maji ya uhai yalisimamishwa na mti mtukufu ulisinyaa mpaka wakati wa utawala wa Yazid, wakati ulipoonekana kuelekea kufa. Imamu Huseini akasafiri kwenda Karbala kuinyweshea ile bustani ya utume na kuimarisha ule mti mtukufu wa la ilha illAllah. Baadhi ya watu wanahoji kwa nini Imamu Husein asipandishe bendera ya upinzani mjini Madina. Hawajui kwamba angebakia Madina malengo yake yangelibakia bila kueleweka. Imamu Husein alikwenda Makka katika mwezi wa Rajabu alihutubia maelfu ya watu, akiwambia kwamba Yazid alikuwa anaungoa mti wa Tawhid. Alisema kwamba Yazid ambaye alidai kuwa Khalifa wa Waslamu, alikuwa anauharibu msngi wa Uislamu. Akiwa ametawaliwa na ulevi wa pombe na kamari, Yazid alijiburudisha kwa kucheza na mbwa na manyani. Imamu Husein aliona kutoa mhanga maisha yake ni muhimu kwa ajili ya kuuhifadhi Uislamu.
208
Mikesha ya Peshawar
kuwaona wao wakiwa mateka. Hivyo, kutokana na amri ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), ninawachukuwa na kwenda nao. Kutekwa kwa wanawake kutakuwa ndio sehemu ya maamuzi ya kuuliwa kwake shahidi. Watauonesha ulimwengu ukatili wa Bani Umayya kwa kizazi cha Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Bibi Zainabu binti wa Ali na Fatima, alitoa hotuba fasaha ya malalamiko katika baraza ya Yazid iliyojaa watu, ambapo mamia ya watu, wakiwemo watu maarufu, watu wakubwa kutoka Bani Umayya, na mabalozi wa nje, walisheherekea ushindi wao. Imamu wa nne, Zainul-Abidin Ali Ibn Husein, naye vile vile alitoa hotuba ya madai fasaha juu ya haki na uadilifu katika mimbari ya Msikiti wa Bani Umayya, mbele ya Yazid. Baada ya kumtukuza Allah (swt) Zainul-Abidin alisema: Enye watu! Sisi kizazi cha Mtume Muhammad, tumejaaliwa na Allah sifa sita na tumefanywa wabora kwa viumbe wote kwa kupewa fadhila saba. Tumepewa elimu, uvumilivu, ujasiri, haiba yenye kupendeza, ufasaha, ushujaa, na tunapendwa na waumini. Sisi ni bora juu ya kila mtu kwa sababu Mtume Muhammad anatokana na sisi; Siddiq Ali Bin Abu Talib anatoka kwetu; Jafar-eTayyar anatoka kwetu; Hamza anatoka kwetu, wajukuu wawili wa Mtume, Hasan na Husein, wanatoka kwetu; na Mahdi wa uma huu (Imam-e-Hujjat Bin Hasan) anatokana na sisi. Mtu ambaye hanijui mimi anapaswa ajue kuhusu familia yangu na hadhi yake; mimi ni mtoto wa Mtume wa Allah aliyetukuka mno na mbora, Muhammad Mustafa! Kisha kutoka kwenye mimbari ileile ambayo Muawiya na Yazid waliitumia kumtukana Ali, Imamu alimtukuza babu yake mashuhuri wa kupigiwa mfano, Ali Bin Abu Talib, mbele ya Yazid na wakuu wa Bani Umayya. Watu wengi wa Syria hawajawahi kusikia sifa za Ali na fadhila zake. Imamu akasema: Mimi ni mtoto wa mtu yule ambaye alipigana mbele ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.); ambaye awalipiga makafiri kule Badir na Hunain; ambaye katu hakupoteza imani yake kwa Allah japo kwa sekunde. Mimi ni mtoto wa mtu mchamungu mno zaidi wa waumini wote, mrithi wa mitume, muuaji wa makafir, mtawala wa Waislamu, rehema ya waabuduo, mfalme wa wale ambao wanalia kwa hofu juu ya Allah, mvumilivu mno wa wavumilivu, mbora wa wanaotekeleza Salat. Mimi ni mtoto wa mtu ambaye alisaidiwa na Jibril na Mikail. Mimi ni mtoto wa mtu yule ambaye alikuwa mlinzi wa heshima ya Waislamu na mkataji vichwa vya makafir. Ni mtoto wa mtu yule ambaye alipigana vita takatifu dhidi ya maadui, ayelikuwa fahari ya Makuraishi, mtangulizi wa wale walioukubali ujumbe wa Allah na Mtume Wake, wa kwanza kati ya wale walioukubali Uislamu, ulimi wa hekima ya Allah, msaidizi wa dini ya Allah, mlinzi wa amri za Allah, bustani ya hekima ya Allah, hazina ya elimu Yake. Mimi ni mtoto wa mkuu wa wenye subira, mvunjaji wa vizuizi, ambaye moyo wake ulikuwa imara zaidi, ambaye maamuzi yake yalikuwa imara zaidi, ambaye tabia yake ilikuwa imara sana kuliko mtu yeyote. Alikuwa simba mkali kwenye uwanja wa vita, ambaye aliwakata maadui na kuwaangusha chini kwa upanga wake na kuwatawanya kama upepo mkali unavyotawanya majani makavu. Alikuwa ndiye shujaa zaidi miongoni mwa watu wa Hijaz, jasiri zaidi miongoni mwa watu wa Iraq, Mwislamu safi zaidi, yeye ambaye
209
Mikesha ya Peshawar
alikula kiapo cha utii kule Aqaba, shujaa wa Badir na Hunain, mtu jasiri zaidi wakati wa kiapo cha utii chini ya mti, mtoa kafara wa aina yake, ya kipekee wakati wa kuhama kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), mkuu wa ulimwengu wa ki-Arabu, mlinzi wa Kaba Tukufu, baba wa wajukuu wawili wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Hizi ni sifa za babu yangu, Ali Bin Abu Talib. Mimi vile vile ni mtoto wa Khadijatul-Kubra; mimi ni mtoto wa Fatima Zahra; mimi ni mtoto wa yule ambaye ameuawa kwa dharuba nyuma ya shingo; mimi ni mtoto wa yule ambaye aliutoka ulimwengu huu akiwa na kiu; mimi ni mtoto wa yule ambaye alinyimwa maji wakati ambapo maji yaliruhusiwa kwa viumbe waliobakia. Mimi ni mtoto wa yule ambaye mwili wake haukuoshwa wala kuvishwa sanda; mimi ni mtoto wa yule ambaye kichwa chake kitukufu kilinyanyuliwa katika ncha ya upanga; mimi ni mtoto wa yule ambaye wanawake wake walikashifiwa na kunyanyaswa waziwazi katika ardhi ya Karbala na kuchukuliwa mateka. Mimi ni mtoto wa yule ambaye wanawake wake waliletwa Syria kama mateka. Kisha Imamu alilia kwa sauti kubwa, na kuendelea: Mimi niMimi ni yaani, aliendelea kueleza fadhila za wahenga zake waliomtangulia na mateso ya mtukufu baba yake na Ahlul-Bayt. Kama matokeo ya hotuba yake hii, watu walilia sana. Baada ya kuliwa shahidi kwa Imamu Husein, majlis ya kwanza (kikao cha maombolezo) kwa ajili ya mateso ya kikatili aliyoyapata Imamu Husein ilifanyika katika Msikiti huu mkuu wa Bani Umayya. Imamu Zainul-Abidin, baada ya kusimulia sifa za Ali mbele ya maadui, alitoa maelezo yenye kugusa nyoyo juu ya mateso aliyopata mtukufu baba yake ambayo yalisababisha kilio kikubwa cha kuumiza kutoka kwa watu wa Syria mbele ya Yazid. Alitishika sana na kuondoka Msikitini pale. Ilikuwa ni kutoka Msikitini hapa, kutokana na hotuba ya Imamu, ndipo watu wakasimama dhidi ya Yazid. Kwa sababu ya kelele za upinzani mkubwa wa watu, Yazid alilazimika kumlaani Ubaidullah Bin Marjana kwa kitendo chake kiovu. Hatimaye, ngome ya dhulma ya Bani Umayya iliteketezwa. Leo hatuoni katika Syria yote kaburi hata moja la Bani Umayya. Tukirudi kwenye swali lako, Imamu Husein mara kwa mara alitabiri kuuawa kwake shahidi. Wakati mmoja aliwahi kusimulia mjini Makka, mnamo siku ya Tarwia (siku ya 8 ya Dhul-Hijja 60 A.H.), akisema: Kifo kimeambatanishwa kwa kila mmoja wa kizazi cha Adamu kama mkufu ulivyoambatanishwa kwenye shingo ya msichana. Nina shauku ya kukutana na wahenga wangu kama vile Yaqub alivyokuwa kwa ajili ya kukutana na Yusuf. Sehemu ambayo nitafia imekwishateuliwa kwa ajili yangu, na lazima niende kwenye sehemu hiyo. Ninawaona chui mwitu wakiniuwa, wakichana vipande vipande mwili wangu kati ya Nawawis na Karbala. Imamu Husein alijua kwamba hatafika Kufa, makao makuu ya Iraqi (zama hizo). Alijua
210
Mikesha ya Peshawar
kwamba atauawa na watu ambao walikuwa kama wanyama wakali, wakikata mwili wake vipande vipande. Alifanya safari hiyo kwa madhumuni ya kufa shahidi na sio kwa sababu za kisiasa. Njiani humo aliwambia watu juu ya kifo chake kinachomngojea. Aliwaeleza marafiki zake na jamaa zake kwamba mfano mmoja ulikuwa unatosha kuthibitihsa jinsi ulimwengu huu usivyokuwa na thamani. Alisema kwamba baada ya Nabii Yahya kukatwa kichwa chake, kichwa hicho kiliwasishwa kwa mzinifu. Alisema kwamba kichwa chake yeye hivi punde kitachukuliwa kupelekwa kwa mlevi, Yazid. Fikiria suala hili kwa muda. Hur Bin Riyahi pamoja na kikosi cha farasi cha askari 1000 waliizuia njia ya Husein. Kufa ilikuwa umbali wa maili thalathini tu. Hurr alikuwa ameteuliwa na Ubaidullah Ibn Ziyad kumzuia Imamu Husein. Hurr alikuwa asimuachie andelee kwenda Kufa wala kuachana naye bila kupata maelekezo zaidi. Kwa nini Imamu alijisalimisha kwa Hurr? Kama Husein alikuwa akitafuta mamlaka ya kisiasa, kwa hakika asingeweza kuzuiwa na Hurr, ambaye alikuwa hana zaidi ya askari 1000. Imamu alikuwa na askari 1300. Hali ya kuwa angewashinda, Imamu angelifika Kufa, ambako ana watu wengi wanaomuunga mkono. Kutoka huko hali ya kuwa jeshi limeongezeka nguvu, angeweza kukabiliana na adui na kupata umiliki. Lakini alikubali amri ya Hurr, alisimama pale katika jangwa akizunguukwa na adui. Baada ya siku nne majeshi ya nyongeza ya adui yaliwasili pale, na mtoto wa Mtume akalazimika kustahamili mateso ya ukatili. Ushahidi mzuri katika kuunga mkono maoni yangu ni hotuba ya Imamu katika usiku wa kuamkia Siku ya Ashura. Mpaka usiku ule askari 1300 walikuwa wako tayari kupigana kwa ajili yake. Husein aliwakusanya watu hao pamoja na akawaambia: Wale ambao wamekuja kwa ajili ya kupata faida ya kidunia, basi wajue kwamba yeyote atakayebakia hapa kesho katika ardhi hii atauawa. Adui ana haja na mimi peke yangu; naondoa nguvu ya kifungo cha utii kutoka katika shingo zenu. Huu sasa ni usiku, na mnaweza kuondoka katika giza hili la usiku. Wengi walikubali pendekezo lake na wakaondoka. Watu 42 tu walibakia, 18 Bani Hashim na 24 Masahaba. Baada ya usiku wa manane, askari 30 wa adui walielekea kwenye kambi ya Imamu kwa ajili ya mashambulizi ya usiku, lakini walipomsikia Husein akisoma Qurani Tukufu, walijawa na jazba na wakaungana na Imamu. Hawa ndio wale watu 72 waliojitolea mhanga maisha yao Siku ya Ashura. Wengi wao walikuwa wachamungu, na wengi walikuwa ni wasomaji wa Qurani Tukufu. Leo mhanga mtukufu wa Husein unakubaliwa na marafiki na maadui kwa pamoja. Hata wale ambao ni wageni katika dini yetu wamevutia na ushujaa wake. Katika DairatulMarif ya Kifaransa, kuna makala ndefu yenye anwani ya Mashahidi watatu iliyoandikwa na mwanachuo mwanamke wa Kiingereza. Dhamira yake ni kwamba katika historia yote kumekuwa na mashahidi watatu, ambao kwa kujitolea kwao mhanga maisha yao, wamekuwa kivutio kikubwa katika kuendeleza njia ya haki. Wa kwanza alikuwa ni Socrates, na wa pili alikuwa ni Yesu - Isa Masihi (mwandishi alikuwa ni Mkristo). Sisi Waislamu, kwa hakika tunaamini kwamba Isa hakusulubiwa. Qurani Tukufu kwa uwazi inasema:
211
Mikesha ya Peshawar
Na hawakumuuwa wala hawakumsulubisha, bali walifananishwa kwao (mtu mwingine, kama Isa), na kwa hakika wale ambao wanatofautiana kwalo wana shaka juu ya hilo. Hawana elimu kuhusiana nalo, bali hufuata dhana tu. Kwa yakini hawakumuuawa. Hasha! Allah alimchukuwa juu Kwake. (Qurani 4:157-158) Shahidi wa tatu, anaandika mwanamke huyu, alikuwa ni Husein, mjukuu wa Muhammad. Anaandika: Wakati tunapokusanya matukio ya kihistoria na kuyaangalia yale mazingira ambamo watu hawa watatu walitoa maisha yao, tunakubali kwamba mhanga wa Husein uliipita ile mingine miwili. Ukweli ulikuwa kwamba, Socrates na Yesu walitoa tu maisha yao wenyewe kwa kafara katika njia ya Mungu, lakini Husein alitoka nyumbani kwake kwenda nchi ya mbali ya jangwa kwenda kuzunguukwa na adui. Yeye na familia yake yote waliuawa mashahidi kwa ajili ya kutetea njia ya haki. Aliwapeleka rafiki na jamaa zake kumkabili adui na kutoa mhanga maisha yao kwa ajili ya dini ya Allah. Hii kwa hakika ilikuwa ni ngumu mno kuliko kutoa maisha yake mwenyewe. Mfano wa dhahiri zaidi wa mateso ya udhalimu aliyopata Husein ulikuwa ni yale mauaji ya kikatili ya mtoto wake mdogo wa miezi sita. Alimbeba mtoto mikononi mwake akiomba maji kwa ajili yake (ambayo yalikuwa mengi), lakini maadui wakatili wale, badala ya kumpa maji, walimuuwa mtoto yule kwa mshale. Ushenzi huu wa maadui unathibitisha kwamba Imamu Husein alikuwa ni muathiriwa wa udhalimu. Uvumilivu wake wa kushangaza ulivunjilia mbali kabisa nguvu za Bani Umayya na uliwashutumumbele ya ulimwengu. Ilikuwa ni kwa ajili ya mihanga yake na Ahlul-Bayt wake watukufu ambapo dini ya Muhammad ilipata uhai mpya. Nawab: Kwa hakika tunawiwa mno na wewe. Tumevutiwa sana na maelezo yako ya mambo yanayomhusu Imamu Husein. Mpaka sasa tulikuwa tunafuata watu wengine na tulikuwa tunazikosa fadhila za ziarat (kuzuru kaburi tukufu la Imamu). Tumeambiwa kwamba kuzuru kaburi la Imamu Husein ni bidaa uzushi. Ama kwa hakika ni bidaa nzuri iliyoje hiyo, kwa vile humfanya mtu awe na ari na kumsaidia aelewe ukweli kuhusu kizazi cha Mtume.
212
Mikesha ya Peshawar
AhlulBayt wake, ambalo halikuamriwa na Allah. Hata hivyo, kuhusu suala la kuzuru kaburi la Husein, kuna hadithi nyingi katika vitabu vya maulamaa wenu wenyewe. Nitakomea kwenye hadithi moja mashuhuri iliyoandikwa katika vitabu vyote vya maqatil na hadith mukhtar. Siku moja Mtume alikuwa nyumbani kwa Aisha wakati Husein alipoingia ndani. Mtume alimchukuwa mikononi mwake, akambusu na kumnusa. Aisha akasema: Maisha ya baba yangu na mama yangu yawe mhanga kwa ajili yako! Kiasi gani unampenda Husein! Mtume akasema: Hujui kwamba mtoto huyu ni sehemu ya ini langu na ua langu? Baada ya hapo Mtume akaanza kulia. Aisha akauliza sababu ya kulia kwake. Mtume akajibu kwamba alibusu mahali ambako Bani Umayya watakuja kumjeruhi Husein. Aisha akauliza kama watamuuwa. Akasema, Ndio atauawa. Hawatapata usaidizi wangu (kesho akhera). Aliyebarikiwa ni yule anayekwenda kuzuru kaburi lake baada ya shahada yake.Aisha akamuuliza Mtume, ni malipo gani yatakuwa kwa ajili ya ziarat hiyo. Mtume akasema: Itakuwa ni sawa na hijja yangu moja. Aisha akasema, Hijja moja ya kwako! Akasema, Hapana, mbili, Aisha alipoonesha mshangao tena, akasema, Hapana, Hijja nne. Jinsi alivyozidi kuonesha mshangao ndivyo malipo yalivyozidi kuongezeka, mpaka mwishowe akasema, Aisha! Kama mtu atakwenda kuzuru kabutri la Husein, Allah atampa malipo sawa na Hijja 90 na Umra 90 zilizofanywa na mimi. Kisha Aisha akanyamaza. Sasa nakuulizeni, Ziarat kama hiyo ni uzushi (bidaa)?
213
Mikesha ya Peshawar
malipo ya thawabu. Kila mwaka watu wengi miongoni mwa madhehebu ya Sunni huzuru sehemu hizi ingawa Mtume kamwe hajalipendekeza hilo. Inawezekana vipi kwamba ziarat kwenye kaburi la Shahidi mkuu, mjukuu wa Mtume, ambayo Mtume ameipendekeza, iambiwe kuwa ni bidaa? Naamua kwa dhati kabisa kwamba, Allah akipenda, mwaka huu nitakwenda kuzuru kaburi la mjukuu kipenzi cha Mtume, Husein. Nitamuomba Allah anisamehe makosa yangu yaliyopita.
214
Mikesha ya Peshawar
tumenyenyekea (tumesilimu); lakini imani bado haijaingia nyoyoni mwenu. (Qurani; 49:14) Kwa hakika lazima uelewe kwamba aya hii iliteremshwa katika kuwalaumu lile kabila la jangwani la Bani Asad, ambao walikuwa Waislamu kwa majina tu. Wakati wa mwaka wa ukame, walijazana mjini Madina, na ili kupata msaada walidai kwamba wao ni waumini. Lakin nyoyoni mwao walikuwa si waumini kwa Allah na Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Aya hii inathibitisha kwamba kuna makundi mawili ya Waislamu. Waislamu waaminifu, ambao wamekubali uhalisi wa Imani, na wale ambao wanatamka imani maneno kwa mdomo tu. Katika nyanja yetu ya kijamii kundi la mwisho wanapasika na usalama na manufaa ya sheria zilizokusudiwa kwa Waislamu wote. Lakini, kwa mujibu wa amri za Qurani Tukufu, hawapasiki na malipo yoyote katika akhera. Kutamka kwao kwamba hakuna mungu ispokuwa Allah na Muhammad ni Mjumbe Wake, na kujionyesha kwao katika jambo la kwamba wao ni Waislamu, hakuna maana ya kweli. Sayyid: Umesema sawa, lakini Uislamu bila Imani hauna maana, kama vile ambavyo Imani bila Uislamu haina ubora. Allah anasema katika Qurani Tukufu: Na msimwambie anayekutoleeni salamu: Wewe sio muumini...... (Qurani; 4:94). Aya hii inathibitisha kwamba lazima tumtendee mtu kwa mujibu wa mtu anavyoonekana kwa nje. Kama mtu yeyote atasema, Hakuna mungu isipokuwa Allah na Muhammad ni Mjumbe wa Allah, lazima tukubali imani yake. Hii yenyewe ni ushahidi mzuri kwamba Uislamu na Imani ni maneno yanayofanana. Muombezi: Aya hii iliteremshwa kuhusiana na mtu mahususi, imma Usama Bin Zaid au Muhallam Bin Jasama-e-Laisi, ambaye inasemekana aliuwa mtu katika vita, mtu ambaye ametamka, Hakuna mungu isipokuwa Allah. Aliuawa kwa dhana kwamba alitamka maneno haya kwa woga. Lakini kwa vile unafikiri kwamba iko katika hali ya ujumla, sisi vile vile tunawaona Waislamu wote kuwa ni safi. Labda kwa kweli pale tunapowaona wakikiuka ile misingi ya dini. Lakini kuna tofauti kati ya Uislamu na Imani kwa sababu kuna daraja mbali mbali za Imani. Imam Jafar Bin Muhammad As-Sadiq anasema katika hadithi ya Umar na Zubair: Amma kuhusu Imani kuna masharti, daraja, na hatua. Baadhi ya hizo ni dhaifu na udhaifu wao uko wazi; baadhi ni nzuri zenye uzito; baadhi zimetimia na zimefikia ukamilifu. Imani dhaifu ni hatua ya kwanza kabisa ambayo kwamba mtu hupita kuingia katika Uislamu kutoka kwenye ukafiri. Daraja za juu za Imani zinawezekana. Rejea zake zimetajwa katika baadhi ya hadithi. Miongoni mwao ni hadithi katika Usul Kafi na NahjulBalagha kutoka kwa Amir wa Waumini (Ali) na Jafar Bin Muhammad As-Sadiq ambaye amesema: Allah ameigawanya Imani katika daraja saba ambazo ni wema, ukweli, kusadikisha kwa moyo, kujisalimisha kwenye utashi wa Allah, utii, elimu, na uvumilivu.
215
Mikesha ya Peshawar
Sifa hizi saba zimegawanywa bila ulingano miongoni mwa wanadamu. Mtu ambaye anazo sifa zote hizi ni muumini kamili. Kwa hiyo, Uislamu uko katika kundi la kwanza la Imani, ambamo kuna tamko la mdomo la imani katika utume wa Muhammad na Upweke wa Allah. Imani haijaingia katika moyo wa mtu kama huyo. Mtume wa Allah alikiambia kikundi cha watu: Enyi watu! Ninyi ni miongoni mwa wale ambao mmekubali Uislamu kwa ndimi zenu, lakini bado kwa nyoyo zenu. Ni dhahiri kwamba Uislamu na Imani viko tofauti. Lakini hatutakiwi kupekuwa nyoyo za watu wengine. Nilisema usiku uliopita kwamba dalili ya muumini ni vitendo vyake. Lakini hatuna haki ya kuchunguza kuhusu vitendo vya Waislamu. Hata hivyo tunalazimika kuonyesha tabia za Imani, ili kwamba wale ambao wamezama katika usingizi waweze kutiwa moyo wa kutekeleza wajibu wao. Hivyo wataelewa ukweli wa Imani na watajua kwamba wokovu katika akhera utakuja tu kwa kufanya matendo mema, kama hadithi inavyosema: Imani maana yake kukiri kwa ulimi, kusadikisha katika moyo, na kutenda kwa viungo vyetu. Kukiri kwa ulimi na kusadikisha moyoni ni vitangulizi vya vitendo. Naam tunajua kwamba ulimwengu huu mbaya ni utangulizi tu wa ulimwengu ujao. Njia ya wokovu kwa ajili ya mtu huyo imefungwa katika akhera mpaka awe ni mtu mwenye kufanya matendo mema hapa duniani. Allah (swt) anasema katika Qurani Tukufu:
Naapa kwa Zama! Hakika mwanadamu yumo katika hasara, isipokuwa wale walioamini na wakatenda matendo mema (103:1-3) Kwa ufupi, kwa mujibu wa Qurani Tukufu, uchamungu ndio msingi wa Imani. Na kama mtu hana matendo mema katika sifa yake, kukubali kwake kwa mdomo au kusadikisha kwenye moyo bado kutamuacha mbali na Imani. Kama ni kweli kwamba inatupasa kumchukulia kila mtu kuwa ni Mwislamu, yule ambaye anasema , Hakuna mungu isipokuwa Allah na Muhammad ni Mjumbe wa Allah, kwa nini mnawachukilia Mashia kama makafiri? Hakika Mashia wanaamini katika upweke wa Allah, utume wa Muhammad, Kibla moja, Kitabu kimoja. Wanatekeleza matendo yote ya wajibu, wanatekeleza saumu kama ilivyoelekezwa, wanakwenda kuhiji, wanatoa khums na zakat (kodi za kidini), wanaamini kufufuliwa katika mwili, na Siku ya Hukumu. Je, ninyi sio ndio mnaosababisha utengano miongoni mwa Waislamu? Mnawatenga mamilioni ya Waislamu na kuwaita makafiri ingawa hamna hata chembe ya ushahidi kuunga mkono madai yenu. Hamtambui kwamba hizi ni mbinu za maadui ambao wanataka kusababisha migogoro miongoni mwa Waislamu kwa njia za uwongo kama huu. Ukweli ni
216
Mikesha ya Peshawar
kwamba hatuna tofauti katika misingi ya imani isipokuwa katika Uimamu na ukhalifa. Na vipi ingekuwa kama kungekuwa na tofauti katika matendo ya imani? Hitilafu kama hizo zipo miongoni mwa madhehebu zenu nne, nazo ni mbaya zaidi kuliko zile zilizoko kati yetu na ninyi. (haitakuwa sahihi sasa kuonyesha tofauti kati ya madhehebu za Hanafia na Maliki au kati ya Shafii na Hanbal.). Kwa maoni yangu mimi, ninyi hamna hata chembe ya ushahidi kuthibitisha ushirikina au ukafiri wa Mashia. Kosa pekee la Mashia lisilosameheka, kwa mujibu wa kile walichoeneza Khawariji na Manasibi, kwa njia ya Bani Umayyah ni kwamba Shia hawapotoshi katika kutafsir hadithi. Hawawapi nafasi watu kama Abu Huraira, Anas, na Samura kuwa kati ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) na sisi. Hata maulamaa wenu wenyewe na makhalifa wenu wakubwa waliwashutumu kama waongo. Kosa kubwa wanalohusihswa nalo Mashia ni kwamba wanafuata kizazi cha Mtume, Ali na Maimamu kumi na mbili, na sio hao Maimamu wanne. Lakini ninyi hamna ushahidi kutoka kwa Mtume unaoonyesha kwamba ni lazima Waislamu wawafuate Ashari, au Mutazali katika misingi ya imani na Maliki, Hanafi, Hanbal nau Shafii katika matendo ya ibada. Kwa upande mwingine kuna maelekezo mengi kutoka kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) yanayotuambia kwamba kizazi na Ahlull-Bayt wa Mtume wanalingana na Qurani Tukufu, na kwamba umma lazima ushikamane nao. Miongoni mwa hadithi hizo ni Hadith Thaqalain, Hadth-e-Safina, Hadith-e-Bab-e-Hitta. Je, unaweza kunukuu hadthi moja tu ambayo kwayo Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) amesema kwmba baada yake yeye watu wake lazima wamfuate Abul-Hasan Ashari na Wasil Bin Ata, na kadhalika, katika misingi ya imani na mmojawapo wa Maimamu wanne Malik Bin Anas, Ahmad Bin Hanbal, Abu Hanifa, au Muhammad Bin Idris Shafii katika matendo ya ibada? Sheikh Suleiman Balkhi Hanafi katika kitabu chake Yanabiul-Mawadda, Sura ya 4, anasimulia kutoka kwa Faraid Hamwaini akinukuu kutoka kwa Ibn Abbas kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alimuambia Amirul-Muminin (Ali): Ewe Ali! Mimi ni Jiji la elimu na wewe ni Lango lake. Hakuna mtu awezaye kuingia katika jiji bila kwanza kuingia katika lango. Ni mwongo yule anayedai kunipenda mimi ambapo akiwa ni adui yako, kwa sababu wewe watokana na mimi na mimi natokana na wewe. Nyama yako ni nyama yangu, damu yako ni damu yangu, nafsi yako ni nafsi yangu, haiba yako ndio haiba yangu mimi. Amebarikiwa yule mtu ambaye anakutii wewe, ole wake yule ambaye anakuasi wewe. Rafiki yako ni mwenye kunufaika, na adui yako yuko kwenye hasara. Mtu ambaye yuko pamoja na wewe amefuzu, na mtu ambaye yuko mbali na wewe amepotea. Baada yangu mimi, wewe na Maimamu wote katika kizazi chako ni kama Safina ya Nuh: ambaye atapanda humo ataokolewa, na yeyote yule ambaye atakataa kupanda humo ataangamia. Mfano wao (Maimamu) ni kama nyota: wakati nyota moja inapozama, nyingine hutokeza. Mpangilio huu utaendelea mpaka Siku ya Kiyama.
217
Mikesha ya Peshawar
Imeelezewa wazi kabisa katika Hadith-e-Thaqalain (inayokubaliwa na madhehebu zote) kwamba Kama mtashikamana na Ahlul-Bayt, kamwe hamtapotea. Hata shupavu Ibn Hajar Makki anaandika katika matokeo ya utafiti wake katika Sawaiq Muhriqa, Sura ya 2 sura ndogo,1, uk. 92, kuhusiana na aya ya Qurani Tukufu:
Na wasimamisheni hakika hao wataulizwa. (37:24) Na Sheikh Suleiman Balkhi Hanafi vie vile amenukuu kutoka kwenye Sawaiq katika kitabu chake Yanabiul-Mawadda, Sura ya 95, uk. 296, (kilichochapishwa Istanbul) akisema kwamba hadithi hii imesimuliwa katika njia tofauti. Ibn Hajar anasema: Hakika, hadithi ya kushikamana na Vitu Viwili Vizito (Thaqalain) imesimuliwa katika njia tofauti, imesimuliwa na Masahaba zaidi ya 25 wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Ibn Hajar anasema kuhusiana na aya hiyo hapo juu ya Qurani kwamba Siku ya Hukumu, watu watauliza kuhusu Wilayat ya Ali na kizazi cha Mtume. Anaandika kwamba kwa mujibu wa baadhi ya vyanzo, hadithi hii ilisimuliwa katika siku ya Arafa, na baadhi wanasema ilisimuliwa wakati Mtume yuko katika kitanda cha mauti na nyumba yake ikiwa imejaa Masahaba wake. Wengine wanasema ilikuwemo ndani ya hotuba yake ya mwisho baada ya Hija ya muago. Ibn Hajar anatoa maoni yake kuhusiana na sehemu mbalimbali ilikosimuliwa hadithi hii: Hakuna kutokulingana katika uwezekano kwamba Mtume katika kupenda kwake kuonesha Utukufu wa Qurani na kizazi chake kitukufu, alirudia rudia hadithi hii katika sehemu hizi na nyingine tofauti. Imesimuliwa kwa usahihi kabisa kwamba Mtume alisema: Ninakuachieni miongoni mwenu vitu viwili vizito: kama mkivifuata, kamwe hamtapotea. Na viwili hivyo ni Kitabu cha Allah (Qurani) na Ahlul-Bayt wangu. Tabrani ameisimulia hadithi hii na nyongeza hii: Angalieni jinsi mtakavyojihusisha na viwili hivi: Qurani na Ahlull-Bayt, hivyo msijaribu kuwatangulia, vinginevyo mtaangamia. Msiwapuuze, vinginevyo mtaharibikiwa. Msijaribu kuwafundisha, kwani wao wanajua zaidi kuliko ninyi. Hata Ibn Hajar mshupavu, baada ya kunukuu kutoka kwa Tabrani na wengine, anaandika: Mtume aliita Qurani na kizazi chake, Vizito Viwili kwa sababu viwili hivi ni vizito mno na vitukufu katika kila kipengele. Mtume vile vile alisema: Namshukuru Allah ambaye ameijaza mioyo ya Ahlull-Bayt wangu kwa hekima. Na Mtume vile vile alisema katika hadithi iliyotajwa huko mwanzoni: .....Na kamwe msijaribu kuwafundisha (kizazi changu) kitu chochote kwa vile ni wenye elimu zaidi ya ninyi wote. Muwaone ni bora kwa maulamaa wenu wote kwa sababu Allah amewaumba safi (watoharifu) na amewatambul-
218
Mikesha ya Peshawar
isha kwenye umma kuwa na uwezo za kimiujiza na sifa nyingi nyingine zisizo na idadi. Kuna nukta moja katika hadithi hii ambayo inasisitiza kushikamana kwa Ahlull-Bayt: yaani, kwamba mfuatano wa vizazi vya Ahlull-Bayt, hautakatika mpaka Siku ya Hukumu. Inashangaza kwamba baadhi ya watu wanakiri kwamba watu wa Ahlull-Bayt wana elimu kubwa lakini wanakiuka amri za Mtume na kuwafanya kama viongozi wao; wale watu wengine ambao hawana haki ya kutangulizwa. Je, mnaweza ninyi au sisi kubadisha Qurani Tukufu? Je, tunaweza kuchangua kitabu kingine chochote? Sayyid: Hapana, haiwezekani kamwe. Hii ni amana ya Mtukufu Mtume, ujumbe mtukufu, na chanzo kikuu kabisa cha mwongozo. Muombezi: Mwenyezi Mungu akubariki! Umezungumza kweli kabisa. Wakati tukiwa hatuwezi kuibadili Qurani tukufu na kuiwekea kitabu kingine badala yake, kanuni hiyo hiyo ni lazima ifuatwe kuhusiana na wale ambao wanalingana na hiyo Qurani tukufu. Hivyo, ni kwa mujibu wa kanuni gani ambayo kwamba wale ambao hawatokani na kizazi cha Mtume walikubaliwa kuwapita wale wa kizazi chake? Nataka jibu rahisi kwa swali hili ili tuweze kujua iwapo kwamba wale makhalifa watatu - Abu Bakr, Umar, na Uthman walitokana na Ahlul-Bayt wa Mtume (s.a.w.w.), na kwamba walijumuishwa katika hadith zile tulizozitaja (ya Thaqalain, Safina na Bab-e-Hitta). Kama wameingizwa, basi lazima tuwafuate, kwa mujibu wa maagizo ya Mtume. Seyyed: Hakuna anayeamini kwamba yeyote kati ya makhalifa hao, mbali na Ali, walikuwa wameingizwa kwenye Ahlul-Bayt wa Mtume. Kama ilivyo, makhalifa hao watatu waliotajwa walikuwa ni masahaba wazuri wa Mtume (s.a.w.w.) Muombezi: Je, Mtume alituambia tufuate mtu maalum au kikundi cha watu? Ikiwa kundi moja linasema kwamba ni jambo lenye manufaa kufuata watu wengine, hivi tumtii Mtume ama tufuate uangalifu kama ulivyoamuliwa na umma? Seyyed: Ni dhahiri kwamba utiifu kwa Mtume ni wajibu wa lazima. Muombezi: Baada ya kwamba Mtume ametuelekeza tufuate Qurani tukufu na kizazi chake, kwa nini wamependelewa kufuatwa wengineo? Je, Abul-Hasan Ali bin Ismail Ashari, Wasil bin Ata, Malik bin Anas, Abu Hanifa, Muhammad Idris Shafii na Ahmad Hanbal walitokana na kizazi cha Mtume au Amirul-Muminin Ali na wale kumi na moja toka kwenye kizazi chake? Seyyed: Ni wazi kabisa, hakuna ambaye amewahi kamwe kusema kwamba watu hawa wanatokana na kizazi cha Mtume, lakini walikuwa mafaqihi maarufu na watu wachamungu wa umma.
219
Mikesha ya Peshawar
Muombezi: Lakini kwa mujibu wa makubaliano ya pamoja ya umma, maimamu hawa kumi na mbili ni kizazi cha moja kwa moja cha Mtukufu Mtume. Ulamaa wenu wenyewe wanakubali kwamba wao wanalingana na Qurani tukufu, na kwamba utii kwao unaongoza kwenye uongofu. Zaidi ya hayo, Mtukufu Mtume alisema kwamba wao ndio wenye elimu zaidi kati ya watu. Kwa kuzingatia kanuni hizi mbili zenye nguvu, ni majibu gani watakayotoa wakati Mtume atakapowauliza ni kwa nini walikiuka miongozo yake yeye, na wakawaachia watu wengine kukitangulia kizazi chake? Kuna maagizo yoyote kutoka kwa Mtume kwamba hawa Ashari na Mutazila wawafuate viongozi wao au kwamba Maliki, Hanbali, Hanafi na Shafii wawafuate viongozi wao katika matendo ya ibada? Hakuna yoyote kiasi kwamba aliyataja majina yao kwa miaka 300 baada ya kifo cha Mtume. Ni baada ya hapo tu, kwa sababu za kisiasa au nyinginezo ambazo mimi sizitambui, wao ndipo wakatokea uwanjani. Lakini hawa Maimam na kizazi cha Mtukufu Mtume walikuwa wakijulikana vema wakati wa uhai wa Mtume mwenyewe. Ali, Hasan, Husein na Fatima walikuwa wakijulikana kama Ahlul-Kisaa, yaani watu wa chini ya shuka. Walikuwa ni wao ambao kwa sifa zao ile Aya ya Utakaso - Ayat-Tathiira - ilishuka kwa ajili yao. Hivi inafaa kweli, kuwaita wale wanaowafuata Ali, Hasan, Husein na wale Maimam wengine kuwa ni makafiri? Mmewafadhilisha wale ambao hawatokani na kizazi cha Mtume juu ya wale ambao walikuwa mafaqihi wakamilifu, wa kupigiwa mfano. Ni majibu gani mtakayotoa kwenye mahakama tukufu ya haki mtakapoulizwa ni kwa nini mliwapotosha watu, kwa nini mliwaita wafuasi wa Ahlul-Bayt makafiri na wazushi? Mnatutia makosani kwa sababu sisi sio wafuasi wa kanuni za kiimani za wa-Hanafi, Maliki, Hanbali au Shafii. Na bado hamumfuati Ali, licha ya maagizo ya wazi na ya dhahiri kabisa kutoka kwa Allah na Mtume wake kwamba mnapaswa kufanya hivyo. Bila ya sababu nzuri za maana, mnafuata moja ya madhehebu nne hizi na mmeifunga milango elimu ya sharia - fiqh. Sayyed: Tunategemea juu ya Maimam hawa wanne kwa namna ileile kama ninyi mnavyotegemea kwa Maimam kumi na mbili. Muombezi: Vizuri sana! ni jambo zuri kiasi gani hilo ulilosema! Idadi ya Maimam kumi na mbili haikuainishwa na Mashia au ulamaa wao karne nyingi baada ya kifo cha Mtume. Hadithi nyingi zilizosimuliwa na kutoka kwenye vyanzo vya wote, Shia na Sunni, zinathibitisha kwamba Mtume mwenyewe aliiainisha idadi hiyo ya Maimam kuwa ni kumi na mbili. Miongoni mwa ulamaa wenu ambao wamesimulia jambo hili ni Sheikh Sulayman Qanduzi Hanafi, ambaye anaandika katika Yanabiul-Mawadda yake, Sura ya 77, kuhusiana na tamko hili: Watakuwepo makhalifa kumi na mbili baada yangu.
220
Mikesha ya Peshawar
Yahya bin Hasan katika Kitabul-Umma amesimulia kwa njia ishirini kwamba Mtukufu Mtume amesema kwamba warithi wake watakuwa ni kumi na mbili kwa idadi, na wote watatokana na Quraishi. Imesimuliwa kwa njia tatu ndani ya Sahih Bukhari, katika njia tisa ndani ya Sahih Muslim, kwa njia tatu ndani ya Sunnan Abu Dawuud, kwa nji moja ndani ya Sunnan-Tirmidhi, na kwa njia tatu ndani ya Jam-e-Bainas-Sahihain ya Hamidi. Wako ulamaa wenu wengi, kama vile Hamwaini katika Faraid, Khawarizmi na ibn Maghazili kila mmoja katika Manaqib yake, Imam Thalabi katika Tafsiir yake na ibn Abil-Hadid ndani ya Sharh Nahajul-Balaghah, na Sayyid Ali Hamadani Shafii katika Mawaddatul-Qubra, Mawadda 10. Wote wamesimulia hadithi kumi na mbili zilizosimuliwa na Abdullah ibn Abbas, Ubaya bin Rabii, Zaid bin Haritha, Abu Huraira na AmirulMuminin Ali. Wote hawa wanasimulia kwa njia tofauti, lakini maneno yale yale kwamba Mtume amesema kwamba idadi ya warithi wake na Maimam watakuwa w12 na kwamba wote watatokana na Maquraishi. Baadhi ya hadith zinasema kwamba wao watatokana na Bani Hashim. Katika baadhi ya riwaya yale majina mahususi ya warithi kumi na mbili hao pia yametajwa. Wengine wao wanatoa idadi tu. Nimetoa kati ya hadith nyingi za ulamaa wenu. Sasa je, mnaweza kutaja hadith moja tu ambayo inaashiria kwamba idadi ya warithi wake watakuwa wanne tu? Hata kama ingekuwepo hadith moja tu kama hiyo, sisi tutaikubali kuliko ile ya kwetu wenyewe. Bila kuzingatia ukweli kwamba hamuwezi kunukuu hadith hata moja kuhusu maimam wenu wanne, kuna tofauti kubwa sana kati ya Maimam wa Shia na hao Maimam wenu. Maimam wetu kumi na mbili ni warithi walioteuliwa ki-mbinguni. Kuhusu maimam wenu, ni kiasi hiki tu kinachoweza kukubalika: walikuwa na elimu ya fiqhi (sharia za kiislam) na waliweza kutafsiri Qurani tukufu na hadith. Baadhi yao, kama Abu Hanifa, kulingana na kukiri kwa ulamaa wenu wenyewe, walikuwa hawakujuishwa miongoni mwa wasimuliaji wa hadith, mafaqih, au mujtahidi, bali walikuwa ni watu waliotegemea juu ya rai zao wenyewe. Hii peke yake ni ushahidi wa kukosa kwao kuwa na elimu. Kwa upande mwingine, Maimam wa Shia ni waongozaji walioteuliwa ki-mbinguni, warithi walioagizwa, wa Mtukufu Mtume. Kwa kweli katika kila zama wanakuwepo baadhi ya mafaqihi wenye elimu ya hali ya juu na wanachuoni miongoni mwa Mashia ambao wanazitafsiri amri za Allah, wakizingatia Qurani tukufu, hadith na makubaliano ya maoni. Tunafuata fatwa za ulamaa kama hao. Ingawa mafaqihi wenu walikuwa wanafunzi wa, na walipata nyingi ya elimu yao, kutoka kwa Maimam wa Shia, ninyi mnawafuata wahenga wenu ki-kichwakicha tu, wale kati ya wanafunzi wao, ambao walikengeuka kutoka kwenye misingi ya elimu na wakategemea kukisia kwao. Sayyed: Unawezaji kudai kwamba Maimam wetu walipata manufaa ya elimu yao kutoka kwa Maimam wenu? Muombezi: Ni ukweli wa kihistoria kwamba Imam Jafar as-Sadiq aliwazidi wengine
221
Mikesha ya Peshawar
wote katika elimu. Yule Aalim mashuhuri, Nurud-Din bin Sabbagh Maliki anakiri ndani ya kitabu chake, Fusulul-Muhimma kwamba Mtukufu Imam alikuwa akijulikana na kuonekana wazi kwa elimu yake. Yeye anaandika: Watu walipata elimu ya nyanja mbali mbali kutoka kwake. Watu walikuja kutoka nchi za mbali kupata maelekezo. Akajulikana sana katika nchi zote na ulamaa walisimulia hadith nyingi kutoka kwake kuliko kwa mtu mwingine wa Ahlul-Bayt ..... Kundi kubwa la watu mashuhuri wa umma, kama Yahya bin Said ibn Jarih, Malik bin Anas, Sufyan Thawri, Abu Ainiyya, Abu Ayyub Sijistani, Abu Hanifa, na Saba - wote wamesimulia hadith zake. Kamalud-Din Abi Talha pia anaandika katika Manaqib yake kwamba maulamaa maarufu na viongozi wa kidini wamenukuu hadith kutoka kwa mtukufu Imam na wamepata elimu kutoka kwake. Miongoni mwao anataja majina ya wale waliotajwa kwenye FusululMuhimma. Hata maadui walikiri fadhaili za mtukufu Imam. Kwa mfano, Maliki katika Fusulul-Muhimma na hususan Sheikh Abu Abdur-Rahman Salmi katika TabaqatulMashaikh yake anaandika: Hakika, Imam Jafar as-Sadiq aliwapita wenzie wote wa wakati wake. Alikuwa na elimu ya kisilika na ujuzi katika dini, uchamungu kamilifu katika ulimwengu, kujizuia kutokana na matamanio yote ya kidunia, na hekima ya kina kikubwa. Na Muhammad bin Talha Shafii ameziandika sifa hizi zote za mtukufu Imam katika Matalibus-Suul yake, Sura ya 6, uk. 81: Mtu huyu mwenye elimu kubwa alitokana na viongozi mashuhuri wa Ahlul-Bayt. Alijaaliwa na elimu nzito na alikuwa wakati wote katika hali ya kumkumbuka Allah. Alisoma Qurani tukufu mara kwa mara na alitoa tafsiri yake. Wafuasi wake walijikusanyia lulu kutoka kwenye bahari ya elimu yake. Aligawanya muda wake wakati wa mchana na usiku katika miundo mbalimbali ya ibada. Kumtembelea yeye kulikuwa kama ukumbusho wa akhera. Kuisikiliza hotuba yake kulimuongoza mtu kupata uchamungu, na kufuata maelekezo kulimuongozea mtu kwenye kupata pepo. Uso wake mngaavu ulijulisha kwamba alitokana na familia ya Mtukufu Mtume. Usafi wa vitendo vyake pia ulionyesha kwamba anatokana na Ahlul-Bayt wa Mtume. Wengi wa ulamaa wamepokea hadith na kupata elimu kutoka kwake. Miongoni mwao walikuwa ni Yahya bin Said Ansari, ibn Jarih, Malik bin Anas, Sufyan Thawri, Ibn Ainiyya, Shaba na Ayyub Sijistani. Wote walishukuru kwa bahati njema na fursa ya kusoma kutoka kwake.
222
Mikesha ya Peshawar
223
Mikesha ya Peshawar
uliwekwa wazi na sifa za Ahlull-Bayt wa Muhammad zilitangazwa na Imamu Jafar Sadiq. Kwa hiyo, madhehebu hii ikaja kujulikana kama Jafaria, lakini hakuna tofauti kati ya Imamu Jafar na yeyote katika Maimamu wanne miongoni mwa wahenga zake waliomtangulia au Maimamu sita waliokuja baada yake. Wote walikuwa viongozi wa kiroho waliowekwa na Mungu. Ingawa marafiki na maadui wote kwa pamoja walitambua ubora wake katika elimu na ukamilifu wake katika sifa zote, viongozi wenu waliopita walikataa kumfanya kama mwanachuoni mkubwa wa dini na mtu mkamilifu wa zama zake. Walikataa kutambua madhehebu yake sambamba na madhehebu nyingine nne ingawa yeye alishikilia daraja la juu zaidi katika elimu uchaji kama ilivyokubaliwa na maulamaa wenu wenyewe. Kwa vile alitokana na Ahlull-Bayt wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), alikuwa na haki ya kupata kipaumbele juu ya wengine. Pamoja na mambo yote haya, maulamaa wenu washupavu wameonesha dharau sugu kama hii kwa kizazi cha Mtume wao kiasi kwamba wanachuoni wenu wa daraja za juu kama Bukhari na Muslim, hawakuweza kuandika hata hadithi moja kutoka kwa faqih huyu au Ahlul-Bayt. Aidha, hawakunukuu hadithi yoyote kutoka kwa Imam yoyote au Sadat (mabibi) wa kizazi kitukufu: Alawi, Husaini, Abidi, Musawi, Ridhawi, au kutoka kwa maulamaa kama hawa na mafuqahaa kama, Zaid Bin Ali Bin Husein, yule Shahid, Yahaya Bin Zaid, Muhammad Bin Abdullah, Husein Bin Ali, Yahya Bin Abdullah bin Hasan na kaka yake Idris, Muhammad Bin Jafar Sadiq, Muhmmad Bin Ibrahim, Muhammad Bin Zaid, Abdullah Bin Hasan, Ali Bin Jafar (Arizi) na wengine, wote hao ambao walikuwa maulamaa na mafaqih wakubwa na ambao walitokana na familia ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Kwa upande mwingine, wamenukuu hadithi kutoka kwa watu kama Abu Huraira, ambaye tabia yake mnaijua ninyi wote, na kutoka kwa yule mwongo mkubwa na mzushi, Akrama, yule Khawariji. Maulamaa wenu wenyewe wamethibitisha kwamba watu hawa walikuwa waongo na bado wanakubali hadithi zao kwa mioyo yao yote. Ibn Bayyit anaandika kwamba Bukhari amenukuu hadithi nyingi kufikia kiasi cha hadithi 12,000 kutoka kwa Khawariji na Nasibiyya, kama Imamu bin Hattan, mwenye kuvutiwa na Ibn Muljim, muuwaji wa Amir wa Waumini. Wafuasi wa Imam-e-Adhma (Abu Hanifa), Imamu Malik, Imamu Shafii na Imamu Hanbal huwaona hawa kama Waislamu safi ingawa hakuna hata mmoja aliyetokana na Ahlul-Bayt wa Mtume, na kila mmoja wa madhehebu zile iko huru kuchukuwa njia zake mwenyewe ingawa kuna tofauti kubwa katika misingi na halikadhalika katika matendo ya ibada miongoni mwao. Ni masikitiko makubwa kiasi gani kwamba wanawaita wafuasi wa Jafar Bin Muhammad As-Sadiq makafiri! Na katika sehemum zote zinazotawaliwa na Masunni, ikiwemo Makka, ambayo kwa kuihusu Allah anasema: Yeyote anaingia humo yuko huru, hawako huru kuelezea imani yao au kutekeleza Sala zao. Hivyo ninyi watu
224
Mikesha ya Peshawar
wema mnapaswa muelewe kwamba sisi Shia sio chanzo cha hitilafu zilizoko katika Uislamu; hatukuleta mtengano miongoni mwa Waislamu. Kusema kweli, migogano mingi hutokea upande wenu. Ni niyni mnaowaita Waislamu milioni 100 makafiri, ingawa ni waumini waaminifu sambamba na ninyi. Hafidh: Ni kweli, kama ulivyosema, kwamba mimi sio mtu dhalimu. Nakubali kwamba kumekuwepo na vitendo viovu kwa sababu ya ushupavu. Ningependa kusema bila kujidai au kumpendeza yeyote kwamba nimenufaika sana kutokana na mazungumzo yako na nimejifundisha vya kutosha. Lakini kwa idhini yako, niruhusu niseme kitu kimoja, ambacho ni malalamiko, na halikadhalika ni utetezi wa madhehebu stahiki ya Sunni. Unaweza kuniambia ni kwa nini wahubiri na maulamaa wa ki-Shia kama wewe hamchungi watu wenu wa kawaida kutokana na kutoa maneno ambayo hupelekea kwenye ukafiri? Matokeo yake ni kwamba wengine hupata nafasi ya kutumia neno kafiri dhidi yao. Mtu anaweza kuwa shabaha ya mashambulizi kwa sababu ametoa maelezo yasiyo sahihi. Hivyo ninyi watu vile vile msiwafanye Masunni kuwa shabaha ya mashambulizi yenu. Mashia husema mambo ambayo huathiri nyoyo za Masunni, ambao kwa kulipiza huhusisha ukafiri kwa Mashia. Muombezi: Naomba unieleze ni maelezo gani au vitendo gani hupelekea kwenye ukafiri vinavyofanywa na Mashia? Hafidh: Mashia kuwakosoa Masahaba wakubwa na baadhi ya wake safi wa Mtume, ni dhahiri hicho ni kitendo cha ukafiri. Kwa vile Masahaba wamepigana kwa miaka mingi pamoja na Mtume dhidi ya makafiri, ni wazi kwamba huduma yao ilikuwa safi kabisa kutokana na maadili yasiyokamilika. Kwa hakika wanastahiki Pepo, hususan wale ambao walipata baraka za Mungu. Kwa muijibu wa Qurani Tukufu : Hakika Allah aliridhishwa sana na waumini wakati walipokula kiapo cha utii kwako chini ya mti (Qurani 48;18) Hakuna shaka kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) aliwaheshimu. Mtu ambaye anakataa ubora wao hakika amepotea. Qurani inasema: Wala hazungumzi kwa matamanio yake. Hayakuwa haya ila ni ufunuo uliofunuliwa. (Qurani; 53:3-4) Mtu kama huyo anamkataa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) na Qurani Tukufu, na mtu ambaye anamkataa Mtume na Qurani Tukufu hapana shaka yoyote ni kafiri. Muombezi: Nilitegemea kwamba nukta kama hizo zisingeletwa katika mkutano huu wa hadhara. Majibu yangu yanaweza kuwafikia watu wasio na elimu na wanaweza wakaeneza propaganda potovu. Ingekuwa vizuri kama tungejadili masuala haya kwa faragha. Nitakuja kwako siku moja na tutalitatua tatizo hili kwa faragha. Hafidh: Nasikitika, lakini watu wetu wengi katika mikesha kadhaa iliyopita wamesisitiza kwamba nukta hii ijadiliwe. Majadiliano yako siku zote ni yenye busara. Kama utatoa majibu mazuri yenye mvuto, hakutakuwa na matokeo mabaya. Vinginevyo ukubali kushindwa na hoja yetu.
225
Mikesha ya Peshawar
Nawab: Ni sawa sawa. Wote tunataka suala hili litatuliwe hapa hapa na sasa hivi. Muombezi: Nakubaliana tu matakwa yenu. Si kutarajia mtu mwenye uwezo kama wewe, baada ya maelezo kamili ambayo nimeyatoa katika usiku wa masiku yaliyopita juu ya suala la ukafiri ungeihusisha madhehebu ya Shia na ukafiri. Tayari nimewasilisha kwa ukamilifu uthibitisho kwamba Shia Ithna Ashari ni wafuasi wa Muhammad na kizazi chake kitukufu. Umeleta masuala mbalimbali. Nitajibu kila moja ya hayo kwa kuyatenganisha.
226
Mikesha ya Peshawar
Mulla Sad Taftazani anaandika katika Sharhe Aqaid-e-Nasi kwamba, baadhi ya watu wasio na uvumilivu wanasema kwamba wale ambao wanawatukana Masahaba ni makafiri. Ni vigumu kukubali mtazamo huo. Ukafiri wao hauthibitishwi kwa sababu baadhi ya maulamaa wamewapendelea, wakapuuza matendo yao maovu, na kutoa utetezi wa kipumbavu katika kuwaunga mkono. Wamesema kwamba Masahaba wa Mtume walikuwa hawana dhambi yoyote, ingawa maelezo haya yalikuwa kinyume na ukweli wa mambo. Wakati mwingine walipigana wenyewe kwa wenyewe. Husda na kupenda madaraka mara kwa mara kuliwasababishia kufanya matendo maovu. Hata baadhi ya Masahaba wakubwa hawakuwa huru kutokana na vitedno viovu. Hivyo, kama kwa msingi wa ushahidi fulani mtu akawakosoa, hapaswi kulaumiwa kwa hilo. Baadhi ya watu, kwa sababu waliwapendelea Masahaba walificha maovu yao, lakini baadhi wameandika matendo yao maovu na kuwalaumu. Mbali na hili, Ibn Athir Jazari, mwandishi wa Jamul-Usul, amewajumuisha Mashia katika madhehebu ya ki-Islamu, basi mnawezaje kuwaita makafiri? Wakati wa kipindi cha Makhalifa wa kwanza, baadhi ya watu waliwalaani Masahaba kwa ajili ya matendo yao maovu. Hata hivyo, Makhalifa hawakuamuru wauawe kwa ukafiri wao. Kwa hiyo, Hakim Nishapuri katika kitabu chake Mustadrak, sehemu ya 4, uk. 335, 354, Imamu Ahmad Hanbal katika Musnad, sehemu ya 1, uk. 9, Dhahabi katika Talkhise Mustadrak, Kadhi Ayaz katika Kitab-e-Shifa, sehemu ya 4, sura ya 1, na Imamu Ghazali katika IhyaulUlum, Jz. 2, anataarifu kwamba wakati wa Ukhalifa wa Abu Bakr, mtu mmoja alikuja kwake na akatoa lugha chafu na laana dhidi yake kiasi kwamba wale waliokuwepo pale walishikwa na hasira. Abu Barza Salmi alimuomba Khalifa kama angemruhusu ili amuuwe yule mtu kwa sababu amekuwa kafiri. Abu Bakr alisema kwamba haiwezekani kufanya hivyo kwa vile hakuna mtu yeyote isipokuwa Mtume anayeweza kupitisha hukumu kama hiyo.
227
Mikesha ya Peshawar
akimtukana Khalifa Uthman na kwa uwazi akatangaza: Muuwenu mzee huyu mpumbavu, kwani hakika amekuwa kafiri. Hata hivyo, kama Shia atasema kwamba ilikuwa vema kwamba Uthman aliuawa kwa sababu alikuwa kafiri, mara moja mtasimama dhidi yake. Lakini wakati Aisha alipomuambia Uthman mbele yake kwamba yeye ni Nathal na kafiri, Khalifa hakumkataza kufanya hivyo wala Masahaba hawakumkemea. Wala ninyi hamuoni kwamba alifanya kosa. Nawab: Mheshimiwa, unamaanisha nini kwa neno Nathal? Muombezi: Firuzabadi, ambaye ni mmoja wa maulamaa wenu mwenye daraja ya juu, anatoa maana yake katika Qamusul-Lughat kama mzee mjinga. Vile vile kulikuwa Myahudi aliyekuwa na ndevu ndefu mjini Madina aliyekuwa akiitwa kwa jina hilo, ambaye alifananishwa na Uthman. Mfafanuzi juu ya Qamus, Allama Qazwini, vile vile anatoa maana hiyo hiyo, anasema kwamba Ibn Hajar katika kitabu chake Tabsiratul-Muntaha, anaandika, Nathal Myahudi mwenye ndevu ndefu aliyeishi Madina; alifanana sana na Uthman.
228
Mikesha ya Peshawar
KWA MUJIBU WA ABUL-HASAN ASHARI HATA KUMUITA ALLAH AU MTUKUFU MTUME (S.A.W.W.) KWA MAJINA MABAYA SIO UKAFIRI
Baadhi ya maulamaa wenu wakubwa, kama, Abul-Hasan Ashari na wafuasi wake, wanaamini kwamba kama mtu ana imani katika moyo wake na bado akaonyesha ukafiri (km. Kwa kuabudu kiyahudi au kikristo, kwa mfano) au akasimama na kupigana dhidi ya Mtume, au akamuita Allah au Mtume kwa majina mabaya, hata hivyo sio kafiri. Imani maana yake kuamini ndani ya moyo na kwa vile hakuna mtu anayeweza kuujua moyo wa mtu mwingine, haiwezi kusemwa iwapo ule ukafiri wa dhahiri unatoka moyoni au la. Maulamaa wa ki-Ashari vile vile wamejadili masuala haya katika vitabu vyao. Ibn Hazm Andalusi ameandika kwa urefu kuhusu nukta hizi katika kitabu chake Kitabul-Fazl (sehemu ya 4, uk. 204, 206). Kwa kuzingatia ukweli huu, ninyi mna haki gani ya kuwashutumu Mashia kwa ukafiri?
MASAHABA WENGI WALITUKANANA WENYEWE KWA WENYEWE LAKINI HAWAKUCHUKULIWA KAMA MAKAFIRI
Katika vitabu vyenu sahihi, kama Musnad cha Imamu Ahmad Bin Hanbal, Jz. 2, uk. 236; Siratul-Halabiyya, Jz. 2, uk. 107, Sahih Bukhari, Jz. 2, uk. 74, Sahih Muslim, Kitab-e-Jihad wa Asbabun-Nuzul Wahid, uk. 118, kuna hadithi nyingi zinzoonesha kwamba Masahaba wengi walitukanana wenyewe kwa wenyewe mbele ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Lakini Mtume hakuwaita watu hawa makafiri. Aliwaonya. (hadithi za kuhusu mizozo hii na uadui
229
Mikesha ya Peshawar
wa wao kwa wao zimeandikwa katika vitabu vya Sunni tu, sio katika vitabu vya Shia). kwa mtazamo wa maneno haya, natumaini kwamba mmetosheka kwamba kulaani au kumtukana Sahaba yeyote hakumfanyi mtu kuwa kafiri. Kama tunamlaani mtu fulani bila sababu, tutakuwa ni watenda dhambi, sio makafiri. Na kila dhambi inaweza kusamehewa.
230
Mikesha ya Peshawar
wabakia motoni milele? Kwa hiyo ina maana kwamba ile ridhaa ya Mungu hakuwa kwa ajili ya Baiat-e-Shajara (kiapo cha utii chini ya mti) peke yake, bali ilitegemea juu ya imani nyofu na matendo mema. Wale ambao wameamini katika upweke wa Mungu (Tawhid) na Utumme (Nubwat) na wakala kiapo cha utii walistahiki radhi za Mungu. Walitangazwa kuwa watu wa Peponi. Lakini wale waliokula kiapo cha utii bila imani, au ambao hawakula kiapo, wanastahili ghadhabu Yake. Hakika, Masahaba walifanya matendo mazuri, na kwa ajili ya matendo yao mazuri (kama kula kiapo chini ya mti) lazima wasifiwe. Na hata kama muumini, awe yeye ni Sahaba au la, akifanya kosa, anaweza kukosolewa.
231
Mikesha ya Peshawar
wanawafahamu vizuri sana. Hili linaweza kuthibitishwa vizuri na ile Sura ya Munafiqun (wanafiki) na aya za sura nyingine, kama Tawba ambayo vile vile inajulikana kama AlBaraa (Kinga) na Ahzab (koo), ambazo ziliteremshwa kwa ajili ya kuwalaumu Masahaba ambao walikuwa wanafiki na waovu. Maulamaa wenu mashuhuri wenyewe wameandika katika baadhi ya makosa na matendo mabaya ya Masahaba katika vitabu vyao sahihi. Hisham Bin Muhammad Sayib Kalbi, mmoja wa ulamaa mashuhuri wa madhehebu yenu ameandika kitabu juu ya makosa na kasoro za Masahaba. Wanafiki ambao wamelaumiwa na Allah (swt) na Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) walikuwa ndumila kuwili, ambao walikuwa Waislamu kwa nje tu. Nyoyo zao zilikuwa imechafuliwa na dhulma na upotofu; na wote hao walijumuishwa katikakundi la Masahaba. Hivyo tutawezaje kuwa na nia njema kwa Masahaba wote? Na vipi tutakuwa na hakika kwamba kumfuata yeyote kati yao kutahakikisha uwongofu? Je, sio ukweli kwamba katika suala la Aqaba kulikuwa na Masahaba ambao walionekana kuwa waaminifu lakini walikusudia kumuua Mtukufu Mtume (s.a.w.w.)?
232
Mikesha ya Peshawar
wenyewe pamoja, aliwatambua wote. Saba miongoni mwao wanatokana na Bani Umayya. Hudhaifa alirudi kwa Mtume na kuwataja wote. Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akamuamuru kuiweka siri njama hiyo, na akasema Allah ndiye mlizi wao. Katika sehemu ya kwanza ya usiku Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alianza safari, akifuatiwa na jeshi lake. Ammar-e-Yasr alimwongoza ngamia kwa mbele na Hudhaifa alikuwa akimswaga kwa nyuma. Wakati walipofikia kile kichochoro chembamba, wale wanafiki walimtupia ngamia mifuko yao ya ngozi iliyojaa mchanga (au makopo ya mafuta), ikatoa sauti kubwa, wakidhania kwamba mnyama yule aliyetishika atamtupa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) chini ya ule mporomoko mkali. Lakini Allah (swt) alimkinga na wahaini wakakimbia na kutokomea katika kundi. Je, watu hawa hawakuwemo mwiongoni mwa Masahaba? Je, ni kweli kwamba kuwafuata wao maana yake ni njia ya wokovu? Wakati tunapozungumza kuhusu Masahaba wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) wa Allah kwa nini tufumbie macho makosa yao?
233
Mikesha ya Peshawar
234
Mikesha ya Peshawar
Zubair, ambao vile vile walipigana dhidi ya khalifa wa haki. Kwa hakika wamepigana dhidi ya mtu ambaye kuhusu yeye Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alisema: Ewe Ali, kupigana dhidi yako ni kupigana dhidi yangu. Je, hii si sawa na kupingana dhidi ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.)? Basi vipi unasema kwamba neno Ashab au kuwepo chini ya mti wa kiapo ni uthibitisho wa wokovu?
235
Mikesha ya Peshawar
Miongoni mwa vyanzo vya hadithi hii ni Harith Bin Ghazin, ambaye tabia yake inajulikana, na Hamza Ibn Abi Hamza Nussairi, ambaye alishutumiwa kwa kuongopa. Udhaifu wa hadithi hii uko wazi. Ibn Hazm vile vile anasema kwamba hadthi hii ni ya kubuni na ni yenye kukataliwa. Hivyo katika majadiliano yetu hatuwezi kutengemea juu ya hadithi kama hii yenye nyororo (asnad) dhaifu ya vyanzo. Hata tukichukulia kwamba hadithi hii ilikuwa sahihi, isingeweza kutumika katika maana ya ujumla; ingeashiria tu kwa wale Masahaba watiifu na wachamungu ambao kwa mujibu wa amri ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) wamefuata Kitabu cha Allah na kizazi kitukufu cha Mtume.
236
Mikesha ya Peshawar
Nawab: Kama kulikuwa na hafla kama hiyo, majina ya huyo mwenyeji na wageni vilevile yatakuwa yametajwa. Unaweza kuelezea nukta hiyo? Muombezi: Ndio, maulamaa wenu wenyewe wameielezea hiyo.
237
Mikesha ya Peshawar
Sheikh: Pengine mambo haya yalitokea kabla pombe haijafanywa haramu. Muombezi: Tunayoyapata kutoka kwenye vitabu vya Tafsir na historia yanaonesha kwamba hata baada ya aya za kuharamisha pombe baadhi ya Waislamu na Masahaba waliendelea kunywa pombe iliyokatazwa. Muhammad Bin Jarir Tabari anasimulia katika Tafsir-e-Kabir, Jz. 2, uk. 203, kutoka kwa Abil Qamus Zaid Bin Ali, ambaye alisema Allah ameteremsha mara tatu aya zinazokataza pombe. Katika aya ya kwanza anasema:
Wanakuuliza kuhusu ulevi na kamari. Sema: katika hivyo mna dhambi kubwa na manufaa kwa watu, lakini dhambi zake ni kubwa kuliko manufaa yake (2:219) Lakini Waislamu hawakuacha pombe mara moja. Wakati mmoja watu wawili, wakiwa wamelewa, walisali Swala zao na kuzungumza mambo yasio kuwa na maana, aya nyingine iliteremshwa, isemayo:
Enyi ambao mmeamini! msikaribie Sala hali mmelewa, mpaka myajue mnayo yasema (4:43) Hata baada ya aya hii, unywaji wa pombe uliendelea, lakini watu hawakusali wakiwa wamelewa. Siku moja mtu mmoja alikunywa pombe (kwa mujibu wa taarifa ya Bazar, Ibn Hajar na Ibn Mardawiyya mtu huyo alikuwa ni Abu Bakr) na akatunga shairi kwa ajili ya makafiri ambao waliuawa katika vita ya Badir. Wakati Mtume aliposikia hili alikasirika sana. Alikwenda kule inakofanyika hafla hiyo na akataka kumpiga. Yule mtu akasema, Naomba kinga ya Allah kutokana na ghadhabu ya Allah na Mtume Wake. Allah awe shahidi yangu, sitakunywa pombe tena. Kisha aya ifuatayo ikateremshwa:
Enyi ambao mmeamini! Bila shaka ulevi, na kamari na kuabudu masanamu na kupiga ramli, ni uchafu katika kazi ya shetani. Basi jiepusheni navyo, ili mpate kufanikiwa. (5:90).
238
Mikesha ya Peshawar
Miongoni mwa Masahaba wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) walikuwepo wazuri na wabaya kama ambavyo wapo miongoni mwa Waumini na Waislamu wengine. Wale miongoni mwao ambao walijaribu kumtii Allah na Mtume Wake walifikia daraja ya juu. Wale ambao walifuata tamaa za kidunia walikuwa wakidharauliwa na wengine. Hivyo wale ambao wanakosoa Masahaba wa kidunia, wanafanya hivyo kwa sababu fulani. Yale matendo maovu ya baadhi ya masahaba, ambayo yameandikwa katika vitabu sahihi vya maulamaa wenu wenyewe, vile vile yanafaa kulaumiwa kwa mujibu wa ushahidi wa Qurani Tukufu. Mashia wanawalaumu katika misingi hiyo. Kama kuna majibu ya mantiki kwenye hoja hii, tuko tayari kuikubali.
239
Mikesha ya Peshawar
(9:119)
Wakweli maana yake Muhammad na Ali. Hivyo wafuasi wa familia hii tukufu hawawezi kuwa waongo au waghushaji kwa sababu ni yule mtu tu ambaye hana sababu za kweli na na zenye nguvu ndiye anaweza kusema uwongo au kughushi visa vya uwongo na kupata kitu cha kutegemea juu ya njia hii. Wanachosema Mashia kimeandikwa na maulamaa wenu wenyewe. Kwanza mnapaswa kuwakataa maulamaa wenu, ambao wameandika mambo haya. Lau maulamaa wenu wasingeandika kuhusu uvunjaji wa kiapo wa Masahaba katika vitabu vyao sahihi, nisingelitaja hilo katika mkutano huu. Hafidh: Ni nani katika maulamaa wa ki-Sunni ambaye ameandika kwamba Masahaba walivunja kiapo cha utii. Maneno matupu hayawezi kusaidia. Muombezi: Mimi sio ninazungumza tu. Hoja yangu ni yenye mantiki kamili. Masahaba walivunja kiapo chao cha utii mara nyingi. Walivunja kiapo cha utii ambacho kwacho Mtume wa Allah aliwaamuru wao, cha muhimu zaidi ni kiapo cha utii kule Ghadir-eKhum.
240
Mikesha ya Peshawar
241
Mikesha ya Peshawar
kumbukumbu na maulamaa wenu wote wachamungu katika vitabu vyao sahihi. Ningependa kutaja hapa baadhi ya majina ya waandishi na vitabu vyao ili uelewe kwamba maulamaa wenu wote maarufu walitegemea hadithi hii. 1. Imam Fakhrud-Din Razi Tafsir-e-Kabir Mafatihul-Ghaib. 2. Imam Ahmad Thaalabi Tafsir-e-Kashful-Bayan. 3. Jalalud-Din Suyuti Tafsir-e-Durrul-Manthur. 4. Abul-Hasan Ali Bin Ahmad Wahidi Nishapuri Asbabun-Nuzul. 5. Muhammad Bin Jarir Tabari Tafsirul-Kabir. 6. Hafidh Abu Nuaim Ispahani Ma Nazal Minal-Qurani fi Ali na Hilyatul-Auliya. 7. Muhammad Bin Ismail Bukhari Tarikh, Jz. 1, uk. 375. 8. Muslim Bin Hajjaj Nishapuri Sahih, Jz. 2, uk. 325. 9. Abu Dawud Sijistani Sunan. 10. Hafidh Ibnul-Iqda Kitabul-Wilaya. 11. Ibn Kathir Shafii Damishqi Tarikh. 12. Imam Ahmad Ibn Hanbal Musnad Jz. 4, uk. 281&371. 13. Abu Hamid Muhammad Bin Muhammad Al-Ghazali Sirrul-Alamin. 14. Ibn Abdul-Birr Istiab. 15. Muhammad Bin Talha Shafii Matalibus-Suul, uk. 16. 16. Ibn Maghazili Faqih Shafii Manaqib. 17. Nurud-Din Bin Sabbagh Maliki Fusulul-Muhimma. 18. Husain Bin Masud Baghawi Masabihus-Sunna. 19. Abul-Muayyid Muwafiq Bin Ahmad Khatib Khawarizmi Manaqib. 20. Majdud-Din Bin Athir Muhammad Bin Muhammad Shaibani Amul-Usul. 21. Hafidh Abu Abdur-Rahman Ahmad Bin Ali Nisai Khasaisul-Alawi na Sunan. 22. Sulaiman Balkhi Hanafi Yanabiul-Mawadda, Sura ya 4. 23. Shahabud-Din Ahmad Bin Hajar Makki Sawaiq Muhriqa na Kitabul-ManhulMalakiyya, hususan Sawaiq, sehemu ya 1, uk. 25. pamoja na ushupavu wake mkubwa, anasema: Hii ni hadithi ya kweli; ukweli wake hauwezi kutiliwa shaka. Hakika imesimuliwa na Tirmidhi, Nisai na Ahmad, na kama ikichunguzwa, vyanzo vyake ni vizuri vya kutosha. 24. Muhammad Bin Yazid Hafiz Ibn Maja Qazwini Sunan. 25. Hafidh Abu Abdullah Muhammad Bin Abdullah Hakim Nishapuri Mustadrak. 26. Hafidh Sulaiman Ibn Ahmad Tabrani Aust. 27. Ibn Athir Jazari Usudul-Ghaiba. 28. Yusuf Sibt Ibn Jauzi Tadhkiratul-Khasaisul-Umma, uk. 17. 29. Abu Umar Ahmad Bin Abi Abd Rabbih Iqdul-Farid. 30Allama Samhudi Jawahirul-Iqdain. 31. Ibn Taimiyya Ahmad Bin Abdul-Halim Minhajus-Sunna. 32. Ibn Hajar Asqalani Fathul-Bari na Tahdhibut-Tahdhib. 33. Abdul-Qasim Muhammad Bin Umar Jarrullah Zamakhshari Rabiul-Abrar.
242
Mikesha ya Peshawar
34. Abu Said Sijistani Kitabud-Darayab Fi Hadithil-Wilaya. 35. Ubaidullah Bin Abdullah Haskani Duatul-Huda ila Ada Haqqil-Muwala. 36. Razin Bin Muawiya Al-Abdari Jam Bainus-Sahihis-Sitta. 37. Imam Fakhrud-Din Razi anasema katika Ktabul-Arbain kwamba jumuiya yote kwa pamoja wanathibitisha hadithi hii. 38. Muqibili hadithul-Mutawatira. 39. Suyut Tarikhul-Khulafa. 40. Mir Sayyid Ali Hamadani Mawaddatul-Qurba. 41. Abu Fath Nazari Khasaisul-Alawi 42. Khwaja Parsa Bukhari Faslul-Khitab. 43. Jamaluddin Shirazi Kitabul-Arbain. 44. Abdul Rauful-Manawi Faizul-Qadir fi Sharh-i-Jamius-Saghir. 45. Muhammad Bin Yusuf Ganji Shafii Kifayatut-Talib, sehemu ya 1. 46. Yahya Bin Sharf-Nauwi Tahzibul-Asma wal-Lughat. 47. Ibrahim Bin Muhammad Hamwaini Faraidus-Simtain. 48. Kadhi Fadhlullah Bin Ruzhahan Ibtalul-Batil. 49. Shamsuddin Muhammad Bin Ahmad Sharbini Sirajul-Munir. 50. Abul Fath Shahristani Shafii Milal wan-Nihal. 51. Hafidh Abu Bakr Khatib Baghdadi Tarikh. 52. Hafidh Ibn Asakir Abul-Qasim Damishqi Tarikh-i-Kabir. 53. Ibn Abil-Hadid Mutazali Sharhe Nahjul-Balagha 56. Alauddin Samnani Urwatul-Wuthqah. 57. Ibn Khaldun Muqaddima. 58. Mawlana Ali Muttaqi Hindi Kanzul-Ummal. 59. Shamsuddin Abul Khair Damishiqi Asanu Matalib. 60. Sayyid Sharif Hanafi Jurjani Sharh-i-Mawaqit 61. Nizamuddin Nishapuri Tafsir-I-Gharaibul-Qurani.
243
Mikesha ya Peshawar
Baadhi ya Maulamaa wenu wakubwa wameandika vitabu juu ya suala hili. Kwa mfano, mufasir mashuhuri na mwanahistoria wa karne ya nne hijiriya, Abu Jafar Muhammad Bin Jarir Tabari (amekufa 310 A.H.), anatoa maelezo kamili ya hadithi ya Ghadir katika kitabu chake Kitabul-Wilaya na ameisimulia kupitia sanad sabini na tano za wapokezi. Hafidh Abul-Abbas Ahmad Bin Said Abdur-Rahman Al-Kufi, mashuhuri kwa jina la Ibn Iqda (amekufa 333 A.H.), amesimulia hadithi hii sharif katika kitabu chake KitabulWilaya kupitia sanad 125 za wapokezi kutoka kwa Masahaba 125 wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Ibn Haddad Hafidh Abu l-Qasim Haskani (amekufa 492 A.H.), katika kitabu chake Kitabul-Wilaya, amesimulia kwa urefu hadithi ya Ghadir sambamba na kushuka kwa aya za Qurani. Kwa ufupi, wanachuoni wenu wote wateule na maulamaa wa daraja za juu (isipokuwa idadi ndogo ya wapinzani washupavu - wakaidi), wamenukuu asili ya hadithi hii kutoka kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.),ambaye alimtangaza Ali kama makamu wake siku ya mwezi 18 Dhul-Hijja katika mwaka wa hija yake ya mwisho. Vile vili ni ukweli kwamba Khalifa Umar alikuwa wa kwanza miongoni mwa Masahaba kuonesha furaha yake juu ya tukio hili. Huku akiwa ameushika mkono wa Ali, alisema: Hongera ewe Ali! Asubuhi hii imeleta neema kubwa kwako. Umekuwa maula wangu na maula wa waumini wote wanaume na waumini wanawake.
244
Mikesha ya Peshawar
Sasa nataka kutafuta haki kutoka kwenu, je, ilikuwa sahihi kwa wao kuvunja angano imara na Mtume wa Allah ndani ya miezi miwili, kuenda kinyume na kiapo chao kitakatifu cha utii kwa Ali, kuchoma moto nyumba yake, kuchomoa panga dhidi yake, kumfedhehesha, kumburuza mpaka msikitini kumlazimisha kula kiapo cha utii? Hafidhi: Sikutengemea kwamba mwanachuoni wa kuheshimiwa na Sayyid mstaarabu kama wewe ungelihusisha mambo ya kidunia kwa Masahaba wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) aliwatangaza wao kwamba ni chanzo cha uongofu kwa ajili ya umma wakati aliposema: Masahaba wangu ni kama nyota; kama mkimfuata yeyote kati yao, mtaongoka.
245
Mikesha ya Peshawar
kwenye macho yetu. Hivyo, enyi wapenda haki, je, mnathibitisha kwamba hadithi nyingi kwenye vitabu vyenu sahihi zinazohusu kupigana dhidi ya Amirul-Muminin Ali, kama vile asemavyo Mtukufu Mtume (s.a.w.w.): Kupigana dhidi ya Ali ni kupigana dhidi yangu, zote hizi ni za uwongo? Au mnakiri kwamba hadithi hizi ni za kweli kikamilifu hasa? Je, hazikuandikwa pamoja na vyanzo vya kuaminika katika vitabu vyenu vya maulamaa wenu wenyewe wa mashuhuri? Hatuhitaji kutaja kwamba hadithi hizi zimeandikwa na maulamaa wa ki-Shia pamoja na maoni kamili ya wote pamoja katika vitabu vyao vyote. Kama mnakubali hadithi hizi, lazima mkubali kwamba Masahaba wengi walikuwa wachupa mipaka na wenye dhambi kama Muawiya. Umar Ibn As, Abu Huraira, Samra Bin Jundab, Talha, Zubair wote hawa ambao waliasi na wakipigana dhidi ya Ali, kwa kweli waliasi dhidi ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) mwenyewe. Na kwa vile wamepigana dhidi ya Mtume, kwa hakika walipotea kutoka kwenye njia iliyo nyooka. Hivyo, kama tunasema kwamba baadhi ya Masahaba walikuwa watumwa wa tamaa zao, hatukuwa tumekosea, kwa sababu tulichokisema kilikuwa ni kweli. Mbali na hili, hatuko wenyewe tu katika kushikilia kwamba baadhi ya Masahaba walikuwa wenye dhambi, madhalimu na wachupa mipaka. Tunategemeza msimsmo wetu juu ya vitabu vya maulamaa wenu wenyewe wakubwa.
MAONI YA IMAMU GHAZALI KUHUSU MASAHABA KUVUNJA KIAPO KILICHOCHUKULIWA SIKU YA GHADIR-E-KHUM.
Kama utachunguza kitabu cha Sirrul-Alamin kilichokusanywa na Abu Hamid Bin Muhammad Ghazali Tusi, kamwe hutapinga kile ambacho ninasema. Hata hivyo, ninalazimika kunukuu sehemu ya tansifu yake ya nne kwa kuunga mkono maelezo yangu. Anasema: Ushahidi na mantiki vikawa na mwanga, na kuna makubaliano ya wote pamoja miongoni mwa Waislamu kuhusiana na matini (maandiko) ya hotuba ya katika siku ya Ghadir-e-Khum kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alisema: Yule ambaye ni maula kwake (ambaye namtawalia mambo yake), Ali ni maula wake (mwenye kumtawalia mambo yake). Kisha Umar mara moja akasema, Hongera, hongera, Ewe Abul-Hasani! Wewe ni maula wangu na vile vile maula wa waumini wote wanaume na wanawake. Aina hii ya pongezi kwa uwazi inaonesha kukubaliwa kwa amri ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), na kukubaliwa kwa uongozi na ukhalifa wa Ali. Lakini baadae walizidiwa na tamaa zao za kidunia. Kupenda utawala na mamlaka kuliwanyima huruma. Walijichukulia
246
Mikesha ya Peshawar
wenyewe kumchagua Khalifa kule Saqifq-e-Bani Sadat. Walitaka kupandisha bendera ya kizazi chao wenyewe na kuteka nchi ili kwamba majina yao yaweze kuhifadhiwa katika historia. Walilewa tamaa ya madaraka. Walipuuza maamrisho ya Qurani, na maagizo ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Waliuza dini yao kwa ajili ya dunia hii. Biashara mbaya iliyoje waliyofanya na Allah! Wakati Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alipokuwa katika kitanda chake alichofia aliomba apewe kalamu na wino ili kwamba aweze kufafanua suala mrithi. (Allah anisamehe kwa kulisema hili), Lakini Umar alisema: Muacheni mtu huyu. Anaweweseka. Hivyo wakati ambapo Qurani Tukufu na hadithi hazikuweza kuwasaidia, walitegemea juu ya Ijma (makubaliano ya wote pamoja). Lakini hii vile vile ni batili kwa sababu Abbas, kizazi chake, Ali, mke wake na watoto wao hawakujihusisha na wale ambao wamekula kiapo cha utii kwa Abu Bakr. Halikadhalika, watu wa Saqifa vile vile walikataa kula kiapo kwa Khazraji, na Ansar vile vile waliwakataa wao. Enyi watu mnaoheshimiwa! Tafadhali kumbukeni, Mashia hawadai chochote isipokuwa kile ambacho maulamaa wenu wa haki wanacho kidai. Lakini kwa vile mnatuchukia sisi, mnaona makosa katika yale tunayo yasema, hata yawe ya mantiki kiasi gani. Lakini kamwe hamuwalaumu maulamaa wenu ni kwa nini wameandika mambo kama haya ingawa kwa kweli wameufichua ukweli na wakachapisha ukweli huu kwenye kurasa za historia. Sheikh: Sirrul-Alamin haikuandikwa na Imamu Ghazali. Cheo chake kilikuwa cha juu sana kwa yeye kuweza kuandika kitabu kama hicho, na maulamaa wakubwa hawaamini kwamba kitabu hiki kiliandikwa na yeye.
247
Mikesha ya Peshawar
hakikuandikwa na mwandishi huyo, au kwamba ni ubunifu wa Mashia. Au hata wakati mwingine wanakwenda mbali zaidi kufikia kusema kwamba watu hawa waadilifu wote walikuwa wenye dhambi na makafiri.
248
Mikesha ya Peshawar
249
Mikesha ya Peshawar
Muombezi: Nafikiri wakati mwingine bila sababu unachukuwa tabia ya viongozi wako waliokutangulia. Kama utaufikiria ukweli huu kwa makini, ukweli wa suala hili utakuwa wazi. Hafidhi: Ni mambo gani yanayothibitisha maoni yako? Tafadhali tujulishe.
250
Mikesha ya Peshawar
maula (bwana) wake, huyu Ali vile vile ni maula wake. Hata hivyo, inashangaza kwamba Kadhi huyu huyu mpotofu katika Kashf Ghumma anatoa taarifa ya ajabu kutoka kwa Razi Bin Abdullah: Wakati wa uhai wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) tulizoea kusoma aya hii hivi: Ewe Mtume wetu (Muhammad) fikisha yale uliyoteremshiwa kutoka kwa Mola wako, yaani kwamba Ali ni bwana wa waumini. Kama hutafanya, basi utakuwa hukufikisha ujumbe wake. Vile vile Suyuti katika Durrul-Mansur kutoka kwa Ibn Mardawiyya, Ibn Asakir na Ibn Abi Hatim kutoka kwa Abu Said Khudiri, Abdullah Ibn Masud (mmoja wa waandishi wa Wahyi) na Kadhi Shukani katika Tafsir-e-Fathul-Ghadir wanasimulia kwamba wakati wa uhai wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) wao vile vile walisoma aya hiyo katika njia hiyo hiyo. Kwa ufupi hili onyo lililomo katika aya hii linasema: Kama hukufanya basi utakuwa hukufikisha ujumbe (kabisa) huonesha kwamba ujumbe ambao Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) aliamriwa kuutoa ulikuwa wa umuhimu mkubwa sana. Kwa hakika ulikuwa ni muhimu kwa ukamilifu wa utume wenyewe. Kwa hiyo, kwa hakika suala katika mjadala lilikuwa habari ya uimamu, utunukiaji wa mamlaka juu ya mtu ambaye angewaongoza watu kwa mujibu wa mafundisho ya Uislamu baada ya kifo cha Mtukufu Mtume (s.a.w.w.).
KUSHUKA KWA AYA SIKU YA LEO NIMEKUKAMILISHIENI DINI YENU PALE GHADIR-E- KHUM
Mazingira ya pili ambayo yanathibitisha nukta yangu ni kule kushuka kwa aya:
Siku ya leo nimekukamilishieni dini yenu na kukutimizieni neema yangu kwenu na kuwachagulieni Uislamu kuwa ndio dini yenu. (5:3) Hafidh: Lakini ni jambo linalokubalika kwamba aya hii iliteremshwa siku ya Arafa, na hakuna hata mmoja katika maulamaa aliyedai kwamba aya hii iliteremshwa siku ya Ghadir. Muombezi: Nakuomba usifanye haraka isiyo na maana katika kuukataa ukweli huu. Kama mambo yalivyo, nakubali kwamba baadhi ya maulamaa wenu wamesema kwamba aya hii iliteremshwa siku ya Arafa, lakini idadi kubwa ya ulamaa wenu waheshimika vile vile wamesema kwamba iliteremshwa siku ya Ghadir. Vile vile baadhi ya ulamaa wenu wana maoni ya kwamba pengine aya hii iliteremshwa mara mbili, mara ya kwanza pale
251
Mikesha ya Peshawar
mwishoni mwa siku ya Arafa na tena siku ya Ghadir. Kwa hiyo, Sibt Ibn Jauzi anasema katika Khawasul-Umma, uk. 18: Inawezekana kwamba aya hii iliteremshwa mara mbili, mara ya kwanza katika siku ya Arafa na mara nyingine katika siku ya Ghadir-e-Khum, kama vile aya ya: Kwa jina la Allah Mwingi wa rehema Mwenye kurehemu, ilivyoteremshwa mara mbili, mara ya kwanza mjini Makka na mara nyingine tena mjini Madina. Wanachuoni wenu wakuaminika, kama Jalalud-Din Suyuti katika Durrul-Mansur, Jz. 2, uk. 256 na Itqan, Jz. 1, uk. 31; Imamu l-Mufassirin Thalabi katika Kashful-Bayan; Hafidh Abu Nuaim Ispahani katika Ma Nuzala Minal-Qurani Fi Ali; Abul-Fatha Nazari katika Khasaisul-Alawi; Ibn Kathir Shami katika Tafsir Jz. 2, uk. 41 akimfuata Hafidh Ibn Mardawiyya: Muhammad Bin Jarir Tabari, Mwanachuo, mfasiri na mwanahistoria wa karne ya tatu A.H. katika Tafsir-e-Kitabul-Wilaya; Hafidh AbullQasim Haskani katika Shawahid-ut-Tanzil; Sibt Ibn Jauzi katika Tadhkira-e-KhawasulUmma uk. 18; Abu Ishaq Hamwaini katika Faraidus-Simtain sura ya 12; Abu Said Sijistani katika Kitabul-Wilaya; Al-Khatib-e-Baghdadi katika Tarikh-e-Baghdad, Jz. 8, uk. 290; Ibn Maghazili Faqih Shafii katika Manaqib, sura ya 14 na Maqtalul-Husain, sura ya 4, wote wameandika kwamba katika siku ya Ghadir-e-Khum Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alimteuwa Ali kwa amri ya Mungu kwenye cheo cha Wilaya (Makamu). Aliwaeleza watu kila kile ambacho aliamriwa kukisema kuhusu Ali na akainua mikono yake juu kiasi kwamba weupe wa makwapa yake ulionekana. Aliwahutubia watu hivi: Mpongezeni Ali kwa sababu ni Amir wa waumini. Jumuiya yote ilitekeleza amri hii. Walikuwa hawajaachana kila mmoja kuchukua njia yake wakati aya iliyotajwa hapo juu iliposhuka. Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alifurahishwa mno kwa kuteremshwa aya hii. Hivyo, wakati akiwahutubia watu alisema: Allah ni Mkubwa, Ambaye ameikamilisha dini kwa ajili yao na amekamilisha neema Zake kwao na ameridhishwa na Utume wangu na umakamu wa Ali baada yangu. Imamu Haskani na Imamu Ahmad Bin Hanbal wametoa maelezo kamili ya tukio hili. Kama ninyi, waheshimiwa, mngeacha mawazo yenu yaliyojipandikiza juu ya suala hili, mtaweza kuzielewa aya tukufu na hadith, ambazo huonesha kwamba neno Maula maana yake walii (bwana) yaani, mtu aliye na mamlaka juu ya wengine wote. Kama maula au wali haikumaanisha mtu ambaye ana mamlaka makubwa juu ya wengine, neno liliofuatia baada yangu lingekuwa halina maana. Na maneno haya ambayo Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) aliyarudia rudia kuyasema kutoka kwenye ulimi wake mtukufu, yanathibitisha kwamba maula na wali humaanisha mtu ambaye ana mamlaka makub-
252
Mikesha ya Peshawar
wa juu ya wengine wote, kwa sababu alisema kwamba cheo kile haswa kilitolewa kwa Ali baada yake. Tatu, unaweza kuyaangalia yale mazingira. Katika jangwa lile lenye joto, ambako kulikuwa hakuna hifadhi kwa ajili ya wasafiri, Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akakusanya umma wote. Watu walikaa kwenye vivuli vya ngamia, miguu yao ikiwa imefunikwa, katika joto kali linalochoma la jua. Katika hali hii Mtume alitoa hotuba ndefu, ambayo Khawarizmi na Ibn Mardawiyya katika Manaqib zao na Tabari katika Kitabul-Wilaya na wengine wameisimulia. Je, inaleta maana kufikiria kwamba Mtume angetaka maelfu ya wafuasi wake kukaa siku tatu katika jangwa linalochoma kwa ajili ya kula kiapo kwa Ali kuonesha tu kwamba Ali alikuwa rafiki yao? Kwa hakika hakukuwa na mtu hata mmoja katika jumuiya yote ambaye alikuwa bado haujui ule uhusiano wa karibu kati ya Mtume na Ali au hajasikia kuhusu habari zake (kama nilivyokwishaeleza mapema). Kuteremshwa kwa aya ya Qurani iliyoko kwenye mjadala kwa mara ya pili, hususan katika mazingara tofauti pamoja na maelekezo hayo makali kwamba watu wangeweza kuwekwa kwenye takilifu kubwa na mashaka, isingeweza kuwa na maana tu kwamba lazima wao wawe marafiki wa Ali. Itakuwa utekelezaji huu wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) ama ulikusudiwa kuonesha umuhimu mkubwa sana, au ulikuwa ni upuuzi. Na hakika Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) yuko mbali na matendo yote ya kipuuzi. Kwa hiyo ni jambo la busara kuhitimisha kwamba, matayarisho haya hayakufanywa hivi hivi kwa ajili ya kuelekeza tu kwamba watu lazima wafanye urafiki na Ali. Kwa hakika tukio hili linaashiria kukamilika kwa ujumbe wa Mtume: kuthibitishwa kwa Uimamu, chanzo cha mwongozo wa umma baada ya kifo cha Mtukufu Mtume (s.a.w.w.).
253
Mikesha ya Peshawar
mkononi alisema: Yeyote yule ambaye mimi ni bwana (Maula) juu ya nafsi yake, Ali naye pia ni bwana (Maula) juu ya nafsi yake. Sibt ibn Jauzi anasema, Hadith ya Mtukufu Mtume inayosema kwamba Ali anayo mamlaka au ni bwana juu ya nafsi za waumini wengine inathibitisha wazi Uimam au Umakamu wa Ali na kwamba utiifu kwake yeye ni wajibu.
254
Mikesha ya Peshawar
uainishaji huu bila ya lengo maalumu ni batili. Pingamizi ulilofanya linakurudia wewe mwenyewe na sio kwetu kwa sababu maana ambazo tumezibainisha hazikukosa kuwa na lengo maalum lililoainishwa. Aya za Qurani Tukufu, hadith, na maoni ya wanachuoni, vyote vinathibitisha maana hiyo hiyo tuliyoitoa. Miongoni mwa hizi ni zile sababu ambazo maulamaa wenu wakubwa, kama Sibt Ibn Jauzi, Muhammad Ibn Abi Talha Shafii wamezitoa kuhusiana na maana yake. Aidha, imesimuliwa kwa idadi kubwa ya hadithi kutoka kwenye vyanzo vyenu na vyangu kwamba aya hii tukufu ilikuwa inasomwa hivi kimaana: Ewe Mtume wa Allah! Fikisha kile ambacho kimeteremshwa kwako kutoka kwa Mola wako kuhusu wilaya ya Ali (umakamu) na kuwa kwake bwana wa waumini. Jalalud-Din Suyuti, ambaye ni mmoja wa maulamaa wenu mashuhuri amekusanya hadithi hizi kwenye kitabu chake, Durrul-Mansur.
HOJA ALIYOITOA ALI NDANI YA MSIKITI WA KUFA ILIYOKO JUU YA MSINGI WA HADITH YA GHADIR
Kama hadith hii na neno maula havikuwa uthibitisho wa Ali kama Imamu na Khalifa, Amirul-Muminin asingerudia mara kwa mara kuhoji kutokana nayo. Kwa hakika katika mikutano ya kamati za washauri alizirejea kama ushahidi wa Uimamu wake, kama walivyoandika: Khatib Khawarizmi katika Manaqib yake uk. 217; Ibrahim Ibn Muhammad Hamwaini katika Faraid sura ya 58; Hafidh Ibn Iqda katika KitabulWilaya; Ibn Hatim Damishqi katika Durrun-Nazim, na Ibn Abil-Hadid katika Sharhe-e-Nahjul-Balagha, Jz. 2, uk. 61. Cha umuhimu haswa ni ule ushahidi uliotolewa na masahaba thelathini kule Rahba. Maulamaa wenu mashuhuri wamesimulia majadiliano aliyoyafanya Ali pamoja na Waislamu kule Rahba-e-Kufa (yaani, katika uwanja wa msikiti wa Kufa). Ifuatayo ni sehemu ya orodha ya wale ambao wameandika tukio hili: Imam Ahmad Hanbal katika Musnad yake sehmu ya 1, uk. 129; Ibn Athir Jazari katika Asadul-Ghiba, Jz. 3, na Jz. 5, uk. 206 na 276; Ibn Qutayba katika Maarif uk. 194; Muhammad Bin Yusuf Ganji Shafii katika Kifayatul-Talib; Ibn Abil-Hadid katika Sharh-e-Nahjul-Balagha, Jz. 1, uk. 362; Hafidh Abu Nuaim Isfahani katika HilyatulAuliya, Jz. 5, uk. 26; Ibn Hajar Asqalani katika Isaba, Jz. 2, uk. 408; Muhbud-Din Tabari katika Dhakhir-e-Uqba, uk. 67; Imamu Abdur-Rahman Nisai katika Khasaisul-Alawi, uk. 26; Allama Samhudi Katika Jawahirul-Iqdain; Shamsud-Din Jazari katika Asnul-Matalib, uk, 3; Sulaimani Balkhi Hanafi katika YanabiulMawadda, sura 4; Hafidh Ibn Iqda katika Kitabul-Wilaya. Ali alisimama mbele ya watu na akawataka kutoa ushahidi kuhusu kile walichosikia Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akisema kuhusu yeye pale Ghadir-e-Khum. Mashaba thelathini, pamoja na watu wa Badir kumi na
255
Mikesha ya Peshawar
mbili (wale ambao wamepigana katika vita ya Badr), walisimama na wakasema kwamba waliona katika Siku ya Ghadir-e-Khum Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akiushika mkono wa Ali akiwaambia watu: Je, mnajua kwamba ninayo mamlaka makubwa juu ya waumini kuliko waliyonayo katika nasi zao wenyewe? wote wakasema: Ndio. Kisha Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akasema: Kwa yeyote yule ambaye mimi ni maula wake (mwenye kumtawalia mambo yake), basi huyu Ali ni maula wake (mwenye kumtawalia mambo yake).
HOJA YA NNE: JE, MIMI SINA MAMLKA MAKUBWA JUU YENU KULIKO MLIYO NAYO KWENU WENYEWE?
Muombezi: Nne, njia ambayo hadithi hii imesimuliwa yenyewe inaonesha kwamba neno maula maana yake ni bwana. Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) katika hotuba yake kule Ghadir, aliwauliza watu: Je mimi sina mamlaka makubwa juu yenu kuliko mliyonayo kwenu wenyewe? Hii inarejea kwenye yale maneno ya Qurani Tukufu: Mtume ana mamlaka makubwa juu ya waumini kuliko waliyo nayo juu yao wenyewe. (33:6) Aidha, kuna hadithi ya kutengemewa katika vitabu vya madhehebu zote ambayo inansmulia kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) amesema: Hakuna muumini ambaye kwamba sina mamlaka makubwa juu yake katika ulimwengu huu na katika Akhera, kuliko aliyonayo mwenyewe. Wote wakajibu kwa sauti moja kwamba ana mamlaka makubwa juu yao kuliko waliyonayo wao wenyewe. Baada ya hapo Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akasema: Yule ambaye mimi ni mawla (namtawalia mambo yake) huyu Ali ni mawla wake (mwenye kumtawalia mambo yake). Hivyo kutokana na muktadha wa hadithi hii hufuatia kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alimaanisha mamlaka au ubwana juu ya wengine wakati alipotumia neno maula. Hafidh: Katika vitabu vingi hakuna kumbukumbu kama hiyo ya Mtume kuwa amewahi kusema maneno haya: Je, mimi sina mamlaka juu yenu kuliko mliyonayo juu yenu wenyewe?
256
Mikesha ya Peshawar
Muombezi: Katika kusimulia hadithi ya Ghadir, wasimuliaji wametumia maneno tofauti kidogo, lakini kadiri ya hadithi za Shia zinavyohusika, maulamaa wote wa ki-Shia wanasema kwamba matini na muktadha wa hadithi ya Ghadir ni kama ilivyosimuliwa hapo juu. Na katika vitabu sahihi vingi vya Sunni, vilivyoandikwa na maulamaa wenu wakubwa, kama Sibt Ibn Jauzi katika Tadhkira-e-Khawasul-Umma uk. 18; Imamu Ahmad bin Hanbal katika Musnad yake; Nurud-Din Sabagh Maliki katika Fusulul-Muhimma; na kundi la wengi wengine ambao wamesimulia hadithi ya Ghadir, maneno Je, mimi sina mamlaka makubwa juu yenu kuliko mliyonayo wenyewe hupatikana humo. Sasa kwa ajili ya baraka nawasilisha hapa Tarjuma ya hadihti hii ambayo imesimuliwa na Imamu Ahmad Bin Hanbal katika Musnad yake, Jz. 4, uk. 281, kutoka kwa Baraa Bin Azib. Yeye alisema: Nilikuwa nasafiri na Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Tulifika Ghadir. Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akatangaza: Kusanyikeni kwa ajili ya Sala. Ilikuwa ni kawaida kama kulikuwa na kitu muhimu ambacho kilikuwa kitokee punde, Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) aliwaamuru watu kukusanyika kwa ajili ya Sala. Wakati watu wakiwa wamekwishakutanika na Sala imekwisha kutekelezwa, Mtume alizoea kutoa hotuba. Sehemu maalumu ilitayarishwa kwa ajili ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) kati kati ya miti miwili. Baada ya kumalizika kwa Sala Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akiwa amenyanyua mkono wa Ali juu kupita kichwa chake, alizungumza na watu waliokusanyika pale: Je, mnajua kwamba mimi ni bwana wa waumini na nina haki zaidi juu ya kuliko waliyo nayo wao wenyewe juu ya nafsi zao. Wote wakasema, Ndio, tunajua hivyo. Alisema tena, Je, mnajua kwamba nina haki zaidi juu ya klia muumini kuliko aliyo kuwa nayo yeye mwenyewe? Wote wakajibu, Ndio tunalijua hilo. Baada ya hapo Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akasema, Yeyote yule ambaye mimi ni maula wake (mwenye kumtawalia mambo yake) huyu Ali ni maula wake (mwenye kumtawalia mambo yake). Kisha akamuomba Allah: Ewe Allah! Kuwa rafiki kwa yule ambaye ni rafiki kwake (yaani, Ali) na kuwa adui kwa yule ambaye ni adui kwake. Mara tu kufuatia hili, Umar Bin Khattab alikutana na Ali na akasema, Hongera, Ewe mwana wa Abu Talib! Sasa umekuwa maula wa waumini wote wanaume na wanawake. Vile vile Mir Sayyid Ali Hamadani Shafii katika Mawaddatul-Qurba Mawadda ya 5; Sulaimani Balkhi katika Yanabiul-Mawadda na Hafidhi Abu Nuaim katika kitabu chake Hilya wameandika hadithi hii pamoja na tofauti kidogo katika maneno. Hafidhi Abul-Fatha, ambaye kutoka kwake Ibn Sabbagh vile vile amenukuu katika kitabu chake Fusulul-Muhimma, amesimulia hadithi hii katika maneno haya: Enyi watu! Allah Swt ni Maula wangu, nami ninayo mamlaka makubwa juu yenu kuliko mliyonayo juu yenu wenyewe. Inakupaseni mfahamu kwamba yeyote yule ambaye mimi ni maula kwake na huyu Ali vile vile ni maula wake. Ibn Maja Qazwini kaika Sunan yake na Imamu Abu
257
Mikesha ya Peshawar
Abdur-Rahman Nisai katika kitabu chake Ahadith (uk. 81, 83, 93, 24) wameisimulia hadithi hii kwa namna hiyo hiyo. Na Zaid Ibn Arqam anaandika katika hadithi yake Na. 84 kwamba Mtume wa Allah alisema katika hotuba yake: Je, mnajua kwamba ninayo mamlaka makubwa juu ya waumini wote, wanaume na wanawake, kuliko waliyonayo wao wenyewe? Wote wakasema: Tunashuhudia kwamba unayo mamlaka makuu juu ya kila muumini kuliko aliyonayo yeye mwenyewe. Katika wakati huo Mtume akasema: Kwa yeyote yule ambaye mimi ni maula (bwana) kwake huyu Ali vile vile ni maula (bwana) wake. Kisha akaunyoosha mkono wa Ali. Kwa nyongeza Abu Bakr Ahmad Bin Al-Khatib Baghdadi (amekufa 462 A.H.), katika kitabu chake Tarikh-e-Baghdad, Jz,. 8, uk. 289, 290, amesimulia hadithi ndefu kutoka kwa Abu Huraira kwamba kama mtu yeyote atafunga siku ya mwezi 8 Dhul-Hijja (Siku ya Ghadir), atalipwa malipo ya funga ya miezi sita. Kisha hapo akaindika hadithi hiyo hapo juu katika njia hiyo hiyo.
258
Mikesha ya Peshawar
wote lazima muwe watiifu na waminifu katika kumsaidia yeye. Kisha Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akaomba kwa Allah: Ewe Allah! Kuwa rafiki kwa yule ambaye ni rafiki kwake (Ali) na kuwa adui kwa yule ambaye ni adui kwake. Mashairi haya ni ushahidi wa wazi kwamba siku ile masahaba wa Mtume hawakulitafsiri neno maula katika njia nyingine yoyote isipokuwa ya Imamu na kwamba Ali atakuwa Khalifa baada ya Mtume kufariki. Kama neno maula halikuwa na maana ya Imamu au bwana juu ya wengine, basi Mtume mara moja angelimkatiza Hasan wakati anasoma ubeti, Ninaridhika na wewe kuwa Imamu na mlezi baada yangu, na angemuambia kwamba amekosea na kwamba hakuwa na maana kwamba Ali atakuwa Imamu na mrithi baada yangu, na kwamba kwa neno maula alimaanisha rafiki au msadizi. Lakini kwa kweli Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alimuunga mkona kwa kusema, Ruhul-Qudus naye vile vile atakusaidia. Mbali na hili, Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) kwa uwazi alielezea nafasi ya uimamu au wilaya (umakamu) wa Ali katika hotuba yake. Inakubidi uichunguze hotuba ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) aliyoitoa kaita Siku ya Ghadir-e-Khum na ambayo imeandikwa kwa ukamilifu na Abu Jafar Muhammad Ibn Jarir Tabari (amekufa 310 A.H.) katika kitabu chake Kitabul-Wilaya. Anaandika kwamba Mtume alisema: Sikilizeni na mtii. Hakika, Allah swt ni Maula wenu na Ali ni imamu wenu. Mpaka Siku ya Hukumu uimamu utabakia kwenye familia yangu, kizazi cha Ali.
259
Mikesha ya Peshawar
MASHIA WANAWALAUMU MASAHABA WALE TU AMBAO VITENDO VYAO HAVIKUWA VYA HAKI
Sielewi ni kwa nini ninyi watu mmekuwa mkitushambulia kwa karne nyingi. Mnachoandika chochote ninyi kinakubaliwa, lakini kama tukiandika yale ambayo maulamaa wakubwa wa Sunni waliyo andika, tunaitwa makafiri kwa sababu tu tunakosoa dhulma za baadhi ya Masahaba. Hata hivyo, kama ukosoaji wa Masahaba humaanisha Urafidha, basi kwa dhahiri Msahaba wote walikuwa Marafidhi, kwa sababu wote kila mmoja alikosoa vitendo vibaya vya mwenziye. Hata Abu Bakr na Umar walifanya hivyo. Baadhi ya Masahaba wa Mtume walikuwa waumini wachamungu na walikuwa wakiheshimiwa sana. Wengine waliendekeza matamanio yao machafu na walilaumiwa. Kama unataka ushahidi wa kihistoria wa ukweli huu, nashauri kwamba usome Sharh-e-NahjulBalagha ya Abil-Hadid, Jz. 4, uk. 454, 462, na usome majibu ya marefu ya Zaid kwa ukinzani wa Abul-Maali Juwaini, ambayo Abu Jafar Naqib ameyaandika. Hapo ndipo utakapojua ni kiasi cha migogoro ilyokuwepo miongoni mwa Masahaba, ambao kwa hakika walilaaniana wenyewe kwa wenyewe kama waovu na makafiri.
260
Mikesha ya Peshawar
Khattab, walionesha kuchukia kwao kuhusiana na masharti ya mkataba. Walimueleza Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) kwamba walikuwa hawakuridhika na mkataba wa amani na walitaka kupigana. Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akawaambia kama walitaka kupigana walikuwa wako huru kufanya hivyo. Hivyo walishambulia. Lakini Masahaba wakashindwa vibaya na wakakimbia milimani na hawa hata hawakurudi kumlinda Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Ndipo Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alimuambia Ali achomoe upanga na kuwafukuza Makuraishi. Walipomuona Ali mbele yao, Makuraishi walirudi nyuma. Baadae Masahaba waliokimbia walirudi na kuomba msamaha kwa Mtume. Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akawaambia: Kwani mimi sikujueni ninyi! Nyie sio watu wale wale ambao walitetemeka kwa hofu katika vita vya Badir mpaka Allah swt akatuma malaika kwa ajili ya kutusaidia! Ninyi sio Masahaba wangu wale wale ambao katika Siku ya Uhud mlikimbia milimani na mkaniacha bila ulinzi? Ingawa niliendelea kuwaita, lakini ninyi hamkurudi. Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akawahesabia udhaifu wao wote, na waliendelea kuelezea masikitiko yao kwa ajili ya vitendo vyao. Ibn Abil-Hadid anasema mwishoni mwa kazi yake ya kuandika kwamba karipio hili lilielekezwa haswa dhidi ya Umar, ambaye hakuamini ahadi zozote zilizowekwa na Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Kisha anaandika kwamba, kwa mwanga wa maelezo ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), Khalifa Umar lazima alikimbia kutoka kwenye vita ya Uhud kwa sababu katika mazungumzo yake Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alilitaja hilo pia. Sasa mnaweza mkaona wenyewe kwamba kama tukielezea ukweli huu, ambao umeandikwa na maulamaa wenu wakubwa kama Abil-Hadid na wengine, mara moja tunalengwa kushambuliwa (eti) kwa sababu tumemtukana Khalifa, lakini hakuna kikwazo kwa AbilHadid. Kwa kweli hatuna nia ya kumtukana mtu yeyote. Sisi tunasimulia mambo ya kihistoria tu, na mnatuangalia kwa macho ya dharau. Mnayapuuza mambo hayo.
261
Mikesha ya Peshawar
Muombezi: Uonevu na dhulma sio jambo geni leo kwetu sisi. Lakini msingi wake ulijengwa mara tu baada ya kufariki kwa babu yetu, Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Haki ya bibi yetu mdhulumiwa, Fatima Zahra ambayo aliachiwa na baba yake, Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), kwa ajili ya kuwalea watoto wake, iliporwa. Hakuna kujali kokote kulikofanywa kwa ajili ya malalamiko na upingaji wake wa dhati. Hatimaye alifariki katika ujana wake akiwa amevunjika moyo. Hafidh: Tafadhali, unawachochea watu bila sababu yoyote. Tuambie ni haki gani ya Fatima iliyoporwa? Tafadhali kumbuka kwamba kama utashindwa kuthibitisha dai lako, kwa kiasi fulani utashindwa katika Mahakama Tukufu ya Haki. Jione uko katika Mahakama ya Mungu ya Uadilifu na utetee kesi yako. Muombezi: Siku moja tutakuwa mbele ya Mahakama Tukufu. Tunategemea kupata haki. Kama wewe pia unayo hisia ya uadilifu, basi yakupasa kama hakimu muadilifu kusikiliza hoja yangu bila chuki. Naamini utakubali uhalali wa dai letu. Hafidh: Naapa kwamba sina chuki au ukaidi. Hakika umeona katika mikesha hii kwamba sihoji kipumbavu. Wakati niliposikia hoja zenye mantiki nilizikubali. Kunyamaza kwangu kwenyewe kulikuwa kunaonesha kwamba nimekubaliana na mwenendo huu wa haki. Kwa asili mimi sio mtu wa kupenda mizozo. Nakiri kwamba kabla sijakutana na wewe hapa, nilitaka nikushinde. Lakini nimevutiwa mno na usafi wako, upole wako, tabia nzuri, wepesi na hisia ya kweli, kiasi kwamba nimeweka nadhiri mbele ya Allah kwamba nasalimu amri kukubali ukweli wote wenye mantiki ingawa msimamo huu utavunja mioyo juu ya matarajio ya wengine. Niamini mimi, sioyule mtu wa ule usiku wa kwanza. Nakueleza kwa ukweli na uwazi kabisa kwamba hajo zako zimeacha athari ya ndani mno katika moyo wangu. Kwa dhati kabisa natumaini kwamba nitaweza kufa pamoja na mapenzi na upendo kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) na kizazi chake, ili kwamba niweze kusimama kwa furaha na kuridhia mbele ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Muombezi: Naam, hakika msimamo kama huo ulikuwa unategemewa kwa mwanachuoni kama wewe. Hakika mimi pia nimevutiwa sana na maelezo yako, na imejengeka kwangu hisia ya urafiki kwa upande wako. Sasa ningependa kuleta ombi kwako. Natumaini utalikubali. Hafidh: Ndio, tafadhali. Muombezi: Usiku huu ningetaka niwe hakimu na wengine wawe mashahidi, ili kwamba uweze kuamua bila chuki yoyote iwapo dai langu ni haki. Baadhi ya waumini wasio na ujuzi wanasema kwamba hakuna maana kujadili suala ambalo limetokea miaka 1,300 iliyopita. Hawajui kwamba masula yanayohusiana na elimu yanajadiliwa katika kila zama. Majadiliano ya haki hufichua ukweli na madai ya urithi yanaweza kufanywa kisheria na
262
Mikesha ya Peshawar
mwenye kurithi, kwa wakati wowote ule. Kwa vile mimi ni mmoja wa warithi, nataka kukuuliza swali. Tafadhali nakuomba unipe jibu la haki. Hafidh: Ndio, nitapendezewa sana kusikia maelezo yako. Muombezi: Kama kwa amri ya Mungu baba anampa mtoto wake mali, na, baada ya kifo cha baba, kama mali ile inachukuliwa kutoka kwa mtoto ambaye anamiliki mali ile, je, itakuwa ni aina gani ya madai? Hafidh: Kitendo cha mnyanganyi kitakuwa sio cha haki kabisa. Lakini unamkusudia nani wakati unaposema muonevu na muonewa?
263
Mikesha ya Peshawar
Hafidh: Tafadhali fafanua unachosema kuhusu tukio ambalo aya hii tukufu imeteremshwa. Je, imeandikwa kwenye vitabu vya historia na tafsir vya Shia, au vile vile umeiona (habari hii) katika vitabu vyetu vya kutegemewa? Muombezi: Mkuu wa wafasir, Ahmad Thalabi katika kitabu chake Kashful-Bayan; Jalalud-Din Suyuti katika Tafsir yake, Jz. 4, akisimulia kutoka kwa Hafidh Ibn Mardawiyya; yule mufasir mashuhuri Ahmad Bin Musa (aliyekufa 352 A.H.) Akisimulia kutoka kwa Abu Said Khadiri na Hakim Abu l-Qasim Haskani; Ibn Kathir; Imadud-Din Ismail; Ibn Umar Damishqi; Faqih-e-Shafii katika kitabu chake cha Tarikh, na Sheikh Sulaimani Balkhi Hanafi katika Yanabiul-Mawadda, sura ya 39, akisimulia kutoka Tafsir-e-Thalabi, Jamul-Fawaid na Uynul-Akhbar wote wanasimulia kwamba wakati aya, Na mpe jamaa yako wa karibu haki yake, ilipoteremshwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) wa Allah alimuita Fatima na akampa Fatima Fadak kubwa kama zawadi kwake. Kwa hiyo, kadiri Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alivyoishi, Fadak ilibakia katika miliki ya Fatima. Bibi yule mtukufu aliikodisha ardhi ile; mapato yake yalikusanywa katika awamu tatu. Kutoka katika hesabu hii alichukuwa pesa ya kutosha kwa ajili ya chakula chake na cha watoto wake na akagawanya alubaki kwa watu masikini wa Bani Hashim. Baada ya kifo cha Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), maofisa wa Khalifa anayetawala walinyakua mali hii kutoka kwa Fatima. Nakuulizeni enyi waheshimiwa, mnieleze katika jina la uadilifu mtakiitaje kitendo hiki? Hafidh: Hii ndio mara ya kwanza nimesikia kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alimpa Fatima Fadak kwa amri (ya Allah). Muombezi: Inawezekana kwamba hukuweza kusikia kuhusu (suala) hili. Lakini kama ambavyo nimekuambia, wengi wa maulamaa wenu wakubwa wameandika kuhusu suala hili katika vitabu vyao vya kutegemewa. Ili kuthibitisha nukta hii kwa uwazi nakurejeshea kwa Hafidh Ibn Mardawiyya, Waqid na Hakim (Angalia Tafsir na Tarikh zao); JalaludDin Suyut Durrul-Mansur, Jz. 4, uk. 177; Kanzul-Umma ya Mullah Ali Muttaqi na maelezo mafupi ambayo ameandika juu ya Kitabul-Akhlak ya Musnad ya Ahmad Bin Hanbal kuhusu tatizo la Sila-e-rahm; na Sharh-e-Nahjul-Balagha ya Ibn Hadid, Jz. 4. Maulamaa wote hawa wamesimulia katika njia tofauti, isipokuwa maelezo kutoka kwa Abu Said Khudr, kwamba aya hiyo hapo juu ilipoteremshwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) aliitoa Fadaka na kumpa Fatima Zahra.
264
Mikesha ya Peshawar
urithi wowote nyuma yetu; chochote tunachoacha kama urithi ni sadaka (yaani, ni mali ya umma).
Lakini wakati ametumia wingi Sisi Mitume tunawajibika kuchunguza ukweli wa hadithi hii. Sasa kwa msingi wa maelezo yako mwenyewe tunarejea kwenye Qurani Tukufu kwa ajili ya mwongozo. Tunaona kwamba kuna idadi ya aya ambazo zinatueleza kwamba kwa kweli mitume waliacha urithi. Hii inathibisha kwamba hadithi hii ni ya kutupwa moja kwa moja.
265
Mikesha ya Peshawar
Marzabani, yeye kutoka kwa Zaid bin Ali bin Husein; yeye kutoka kwa baba yake, na yeye kutoka kwa baba yake, Imam Husein; na yeye kutoka kwa mama yake maarufu, Fatima Zahra; na maulamaa wengine wengi wa madhehebu yenu wamesimulia hotuba ya Fatima mbele ya mkusanyiko mkubwa wa Waislamu. Wapinzani walifadhaishwa wakati waliposikia hoja zake na hawakuweza kujibu. Kwa vile walikuwa hawana majibu ya kutoa walianzisha ghasia.
Basi nipe mrithi kutoka kwako, ambaye atarithi kutoka kwangu na mrithi (vile vile) wa nyumba ya Yaaqub (19:5-6) Kuhusu maombi ya Zakariya Qurani Tukufu inasema:
Na Zakariya alipomuomba Mola Wake: Mola Wangu, usiniache peke yangu (bila mtoto), na Wewe ndiye Mbora wa wanaorithi. Basi tukamkubalia na tukampa Yahya (21:89-90) Baada ya haya akasema: Ewe mtoto wa Abu Qahafa! Je, imo ndani ya Kitabu cha Allah kwamba wewe ni mrithi wa baba yako na mimi ninanyimwa urithi wa baba yangu? Umefanya kashfa kubwa mno. Enyi watu! Je, mmekiacha kwa mkusudi Kitabu cha Allah (Qurani Tukufu) na kukipuuza moja kwa moja? Je, mimi sio mtoto wa Mtukufu Mtume? Kwa nini unaninyima mimi haki yangu? Kwa nini aya zote hizi za urithi, ambazo zimekusudiwa kwa watu wote kwa ujumla na hususan kwa Mitume zimejumuishwa katika Qurani Tukufu? Je, si kweli kwamba aya za Qurani zitabakia bila kubadilishwa mpaka
266
Mikesha ya Peshawar
Siku ya Hukumu? Je, Qurani haisemi: .....na ndugu wa nasaba wana haki zaidi wao kwa wao katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu..... (8:75) na: Allah anakuusieni juu ya watoto wenu! Mtoto mwanaume atapata vigawanyo viwili vya mwanamke (4:11) na: Mmelazimishwa, mmoja wenu anapofikiwa na umauti, kama ameacha mali, kuwausia wazazi wake wawili na jamaa wa karibu kwa uadilifu. (Huu) ni wajibu kwa wamchao Mwenyezi Mungu (2:180). Basi kwa nini mimi hasa hasa niwe nimenyimwa urithi wa baba yangu? Je Allah ameteremsha aya maalumu kwako, ambazo zinamuondoa baba yangu (kutoka kwenye haki yake hii). Je, wewe unajua maana ya nje na ya ndani ya Qurani Tukufu kuliko baba yangu Muhammad na binamu yake Ali?
267
Mikesha ya Peshawar
wameyakubali mambo haya. Ibn Abil-Hadid Mutazali katika Sharh-e-Nahjul-Balagha Jz. 4, uk. 80, iliyochapishwa Misri, akisimulia kutoka kwa Abu Bakr Ahmad Bin AbdulAziz Jauhari, ameandika kwa urefu kuhusu Abu Bakr kupanda juu ya mimbari baada ya malalamiko ya upinzani wa Ali na Fatimah.
268
Mikesha ya Peshawar
Wallahi Ali anasema kweli. Kwa nini binti ya Mtume afanyiwe fedheha kiasi hicho?
269
Mikesha ya Peshawar
hazikuwa za kupitia. Uhusikaji wake ulikuwa wa wazi. Ibn Hadid akasema: Kama ungekuwa wa wazi, nisingeuliza. Hapo alicheka na akasema: Mambo haya yalisemwa dhidi ya Ali. Ibn Hadid akayarudia maneno haya kwa mshangao: Maneno yote haya yalisemwa dhidi ya Ali? Mwalimu wake akasema: Ndio, Ewe mwanangu! Hivi ndivyo utawala unavyomaanisha.
270
Mikesha ya Peshawar
ma kwamba Ali alikuwa hakimu bora katika Umma mzima. Alisema: Ali ni mbora miongoni mwenu wote katika kuzitafsiri sheria. Hadithi hii imeandikwa katika vitabu vyenu vyote vya sahihi. Hivi Mtukufu Mtume angeweza kutangaza ubora wa ubingwa wa mtu wa sheria kama mtu huyo alikuwa hayaelewi matatizo ya mirathi na haki za watu? Sehemu ya lengo la Mtukufu Mtume lilikuwa ni kuleta mageuzi ya kijamii kwa ajili ya watu katika dunia hii na amani na starehe kwa ajili yao katika akhera. Angeweza vipi basi kumfanya yeye Ali kuwa Amirul-Muminin na kisha bado asimfikishie desturi kama hii ambayo inaathiri utaratibu wote wa kijamii? Sheikh: Hakuna kati ya vitu hivi viwili kilichothibitishwa kwa mujibu wetu. Hadithi ya Jiji la elimu haikubaliwi na maulamaa wetu mashuhuri na masala ya umakamu na urithi (wa nafasi ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.)) pia vile vile yamekataliwa na wale maulamaa wakubwa. Bukhari na Muslim katika kukusanya kwao hadithi na wengine miongoni mwa maulamaa wakubwa, wanasimulia kutoka kwa Ummul-Muminin Aisha kwamba, kichwa cha Mtume wakati wa kifo chake kilikuwa kimelala kifuani mwake mpaka alipokata roho. Alieleza kwamba hakutengeneza wosia. Lau angelitengeneza wosia Ummul-Muminin angesimulia na suala la wosia lingeliweza kutatuliwa.
271
Mikesha ya Peshawar
Nawab: Khalifa wa Mtume pia ni makamu wake, mtu ambaye aliendesha mambo yake ya ndani. Kwa mfano, walilipa posho kwa wake za Mtume. Kwa nini unasema kwamba Ali aliteuliwa kuwa makamu? Muombezi: Unasema kweli. Ni wazi kwamba Khalifa wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alikuwa pia ni makamu wake. Wakati wa mikesha iliyopita nimewasilisha hoja zangu na kauli za kuaminika kuhusiana na ukhalifa. Kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alimteua Ali kuwa Khalifa wake na makamu wake ilikuwa ni sahihi kabisa. Ambapo wengine walikuwa wanajishughisha na mambo yao na njama za kisiasa, huyo makamu wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alishughulika na taratibu za mazishi ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Baadaye alijishughulisha katika kurudisha fedha za amana na vitu vingine vya thamani na kuangalia masuala mengine ambayo Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alikuwa ameyakabidhi kwake. Hili liko wazi mno kiasi kwamba hakuhitajiki uthibitisho wowote. Maulamaa wetu wote wanakubalina kuhusiana na jambo hili.
272
Mikesha ya Peshawar
mrithi wa Salman? Akasema, Yusha Bin Nun. Kisha Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akasema, Makamu wangu na mrithi wangu, ambaye atalipa madeni yangu na atakayekamilisha ahadi zangu, ni Ali Bin Abi Talib. (3) Kila Mtume alikuwa na Mrithi wake, Ali ni Mrithi wangu. Imesimuliwa kutoka kwa Muwaffaq Bin Ahmad, ambaye ananukuu kutoka kwa Buraida kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) amesema: Kila Mtume alikuwa na makamu na mrithi, na kwa hakika, makamu na mrithi wangu ni Ali. Muhammad Bin Yusuf Ganji Shaii katika kitabu chake Kifayatut-Talib, sura ya 62, uk. 131 ananukuu hadithi hiyo hiyo ambayo vile vile imesimuliwa na Muhadith wa Syria katika kitabu chake Tarikh. (4) Ali ni mwisho wa Mawasii. Sheikhul-Islam Hamwaini anasimulia kutoka kwa Abu Dharr Ghifari, ambaye amesema, Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alisema, mimi ni mwisho wa Mitume na wewe, Ewe Ali, ni mwisho wa mawasii mpaka Siku ya Hukumu. (5) Ali ni makamu wangu kutoka kwenye kizazi changu: Imesimuliwa kutoka kwa Khatib Khawarizmi, ambaye anasimulia kutoka kwa Ummul-Muminin Ummi Salama, ambaye amesema; Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) amesema: Allah amechagua mrithi kwa ajili ya kila Mtume na baada yangu mimi makamu wangu kutoka kwenye kizazi changu na Umma wangu ni Ali. (6) Ali alitetea cheo chake katika hotuba. Imesimuliwa kutoka Maghazili Faqih Shafii, ambaye anasimulia kutoka kwa Asbagh Bin Nabuta, mmoja wa Masahaba wakubwa wa Amirul-Muminin, na Muslim na Bukhari vile vile wamenukuu kutoka kwake kwamba bwana wake Amirul-Muminin amesema katika moja ya hotuba zake: Enyi watu! Mimi ni Imam (kiongozi) wa viumbe wote. Ni mrithi wa (makamu) wa mbora mno wa viumbe; mimi ndio baba wa kizazi kilicho takasika kabisa na chenye kuongoza; mimi ni ndugu wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.); mrithi wake, rafiki yake muaminifu na mwenza wake wa karibu. Mimi ni bwana wa waumini; ni kiongozi wa wale ambao wana nyuso angavu, mikono angavu na miguu angavu; mimi ni mkuu wa Mawasii wote. Kupigana dhidi yangu ni kupigana dhidi ya Allah. Kufanya amani na mimi ni kufanya amani na Allah. Utii kwangu ni utii kwa Allah; urafiki na mimi ni urafiki na Allah; wafuasi wangu ni marafiki wa Allah; na wasaidizi wangu ni wasidizi wa Allah. (7) Allah alinifanya mimi Mtume na Ali makamu wangu. Vile vile Ibn Maghazili Shafii katika Manaqib yake anamnukuu Abdullah Bin Masud kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) alisema: Ujumbe wa utume uliishilizwa kwangu mimi na Ali; katu hakuna kati yetu sisi aliyewahi kusujudu mbele ya sanamu; hivyo Allah alinifanya mimi Mtume na Ali kuwa makamu.
273
Mikesha ya Peshawar
(8) Umakamu wa Ali ni sehemu ya kanuni ya kiapo cha utii kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Mir Sayyid Ali Hamadani Shafii anaandika katika kitabu chake Mawaddatul-Qurba Mawadda ya 4, kutoka kwa Atba Bin Amir Jahni, ambaye amesema: Tunatoa kiapo cha utii kwa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.), tukukiri ukweli kwamba hakuna mungu isipokuwa Allah. Ni Mmoja na mshirika na hakika Muhammad ni Mtume Wake na Ali ni makamu Wake. Hivyo kama tunaacha chochote kati ya mambo haya matatu tutakuwa makafiri. (9) Ninawaita watu kwenye haki na Ali anaitia nuru. Katika Mawaddatul-Qurba hiyo hiyo, vile vile imeandikwa kwamba Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) amesema: Hakika Allah ameteua makamu kwa kwa ajili ya kila Mtume: Seth, makamu wa Adamu; Joshua, makamu wa Musa; Simon Petro makamu wa Yesu; na Ali ni makamu wangu; na makamu wangu ni mbora wa makamu wote. Nawaita watu kwenye haki na Ali anaitia nuru.
ALLAH ALIMTEUA ALI KUTOKA MIONGONI MWA WATU WOTE KUWA MAKAMU WANGU
Mwandishi wa Yanabi ananukuu kutoka kwenye Manaqib ya Muwaffaq Bin Ahmad Khawarizmi, ambaye alisimulia kutoka kwa Abu Ayyub Ansari, ambaye amesema kwamba wakati Mtume wa Allah alipokuwa yu mgonjwa kitandani, Fatimah alikuja na kuanza kulia. Kisha Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) akasema: Ewe Fatimah, wewe umebarikiwa makhususi na Allah ambaye amekupa mume ambaye Uislamu wake ni wa mbele zaidi, ambaye elimu yake ni bora kuliko ya mtu yeyote yule, na ambaye uvumilivu wake unapita uvumilivu watu mengine wote. Kwa hakika Allah swt. Amewapa upendeleo maalumu watu wa ulimwengu huu. Kutoka miongoni mwao Alichagua na kuniteua mimi kama Mtume na Mjumbe Wake. Kisha akawapa baraka nyingine maalumu na kutoka miongoni mwa watu akamchagua mume wako. Na amenifunulia kwamba nikuoze wewe kwake na nimfanye makamu wangu.
274
Mikesha ya Peshawar
wengine wote, na ni mume wako. Shahidi (aliyejitolea mhanga) anayewapita mashahidi wengine wote, na ni ami yako, Hamza. Kutoka miongoni mwetu sisi (Ahlul-Bayt) kuna mtu ambaye ana mbawa mbili ambazo kwazo anaruka kwenda popote anapopenda, huko Peponi, na ni binamu yako, Jafar. Kutokana na sisi kuna wajukuu wawili ambao ni mabwana wa vijana wa Peponi, na ni watoto wako. Na ninakuambia, kwa jina la Allah ambaye anamiliki uhai wangu, kwamba Mahdi wa Umma huu, ambaye kwamba Isa Bin Mariamu atasali Salat nyuma yake, atakuwa ni katika kizazi chako.
WAKATI WA KIFO CHAKE, KICHWA CHA MTUKUFU MTUME (S.A.W.W.) KILIKUWA JUU YA KIFUA CHA AMIRUL-MUMININ (A.S.)
Amma kwa madai ya kwamba wakati wa kifo cha Mtume, kichwa chake kilikuwa juu ya kifua cha Ummul-Muminin Aisha, sio kweli. Maulamaa wenu wenyewe wameonesha kwamba wakati wa kifo cha Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) kichwa chake kilikuwa kimeegamia juu ya kifua cha Amirul-Muminin. Sheikh: Ni katika kitabu kipi ambacho ma