Вы находитесь на странице: 1из 20

TANGAZO LA SEMINA ZA HIJJA

Sauti ya Waislamu

TAASISI YA AHLU SUNNA WAL JAMAA

Inawaalika Waislam wote hasa wanaotarajia kwenda


Hijja kwa mwaka huu wa 2015 wahudhurie katika
Semina za Hijja zitakazoanza kufanyika Jumapili
tarehe 2/8/2015 na kuendelea kila Jumamosi na
Jumapili mpaka Septemba 6/2015, kuanzia saa 4:00
asubuhi hadi saa saa 6:30 mchana kwenye ofisi
ya HIJJA YA AHLU SUNNA WAL JAMAA, mtaa wa
Lumumba jingo la Saba General ghorofa ya tatu,
karibu na PBZ Bank.

ISSN 0856 - 3861 Na. 1188 SHAWWAL 1436, IJUMAA , JULAI 31-AGOSTI 6, 2015 BEI TShs 800/=, Kshs 50/=

Kwa maelezo zaidi wasiliana na namba zifuatazo:


0717 224437 0782 804480 0765 462022

Kuelekea Uchaguzi Mkuu...

Bakora ya Nyerere yaisubiri CCM!

HUENDA Chama cha kupuuza usia wa muasisi


Mapinduzi kikakabiliwa wa chama hicho Mwalimu
na wakati mgumu kwa
Inaendelea Uk. 2

Alionya, Chama kisidharau maoni ya watu.


Wasidhani kuwa wao ni Manna na Salwa
Wandishi wa Habari.
Wapime kwa matendo yao sio ahadi na Ilani
Lowassa achukua fomu kupitia CHADEMA

Mchezo wenu
ni mauti kwetu!
Siri ya Sitakishari haijasemwa bado
Tuambiwe mamluki wanatoka wapi
Kawaingiza nani nchini na kuwalinda

WAZIRI Mkuu wa zamani Mhe. Edward Lowassa alipokuwa akitangaza


kujiunga na kambi ya UKAWA kupitia CHADEMA wiki iliyopita.
Kushoto ni Freeman Mbowe na kulia ni Prof. Ibrahim Lipumba.

IGP Ernest Mangu.

JEN. Davis Mwamunyange

Hofu yatanda,
ni huzuni tupu!
MGOMBEA Urais kwa tiketi ya CCM, Dkt. John Magufuli (kushoto),
kulia ni mgombea mwenza Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Mtuhumiwa wa ugaidi hajulikani alipo


Mmoja aliponzwa na mlio wa simu yake
Ilikuwa ikitoa mlio wa bunduki, akakamatwa

Tahariri/Makala

2
AN-NUUR
S.L.P. 55105, Simu: +022 2400786

Cel: 0784 370 208, 0713 110 148, 0755 260 087 , DSM.
E-mail: annuurpapers@yahoo.co.uk
Ofisi zetu zipo: Manzese Tip Top
Usangi House, barabara ya Morogoro, D'Salaam

www.annuurpapers.co.tz

Tujiulize, maisha
yetu yana thamani?
Do Black Lives Matter
in Africa? Ndivyo
anavyouliza David
Swanson baada ya
kusoma yaliyo katika
kitabu: Tomorrow's
Battlefield: U.S. Proxy
Wars and Secret Ops
in Africa.
Kinachoelezwa
katika kitabu hicho na
uchambuzi wa David
kama ulivyotumwa katika
mtandao Aprili 29, 2015,
ni jinsi mabeberu katika
mikakati yao ya kutimiza
haja na malengo yao
wanavyosababisha
maafa makubwa ikiwa
ni pamoja na mauwaji
ya kikatili kwa Waafrika
(na nchi yoyote lengwa).
Kinachojitokeza ni kuwa
ule ukoloni uliofanywa
n a Wa j e r u m a n i n a
Wa i n g e r e z a k a t i k a
karne ya 18, 19 na 20,
sio fasheni tena. Huu
ni wakati wa Ukoloni
Mambo Leo, ambao kilele
chake ni Utandawazi
na Udhibiti wa Dunia
ukiwa na mbabe mmoja
(hegemony). Na njia
maar ufu ya kupita,
ni kuendesha vita na
mauwaji lakini huku
ukionekana kuwa
wewe ndio msamaria
mwema wa dunia. Ndio
kinachofanyika katika
proxy war na vita dhidi
ya ugaidi.
Ni katika kutizama
j i n s i Wa a f r i k a s i s i
tunavyobamizwa na
kuuliwa kinyama katika
hizi proxy war na vita
dhidi ya ugaidi, watu
wanauliza, maisha ya
Muafrika yana thamani

kweli?
La kusikitisha ni
j i n s i Wa a f r i k a s i s i ,
tunavyogeuzwa kuwa
vibaraka na wasaliti wa
kujisaliti sisi wenyewe,
watu wetu na nchi zetu,
ama kwa ujinga tu au kwa
kugeuka Judas Iscariot
mwana wa Simon.
Wiki iliyopita,
tulisherehekea siku ya
mashujaa. Hii ni siku
adhimu ya kuwakumbuka
wazee wetu waliojitoa
muhang a kupig ania
na kutetea hadhi yetu
na nchi yetu mbele ya
wakoloni. Katika kipindi
kimoja cha televisheni
ikichambuliwa namna
wazee hawa walivyojitoa
muhanga, kilielezwa
kisa cha Mkwawa
alivyopambana na
Wajer umani na hata
alipoona anazidiwa
nguvu, akaona itakuwa
ni fedheha kubwa
kukamatwa na wavamizi
hao akiwa hai, akaamua
kujiua mwenyewe.
Labda tujiulize, kuna
lolote tunalojifunza
kutoka kwa wazee hawa?
Je, tunawaenzi kikweli au
tunawadhihaki? Ikiwa
wao walimwaga damu
kuwazuiya wakoloni
kutawala na kupora
mali zetu, tutasemaje
tunawaenzi ikiwa leo
wa ko l o n i wa l e wa l e
tunawakaribisha kupitia
mlango wa nyuma?
K a ma alivyo sema
aliyekuwa Waziri wa
M a m b o y a N j e wa
U i n g e r e z a , Ro b e r t
F i n l a y s o n " Ro b i n "
Cook, kwamba hakuna
afisa yeyote wa Idara

ya Usalama duniani,
a s i y e j u a k u wa h i k i
kinachoitwa ugaidi na
magaidi wa Al Qaidah
(na wenye majina
mengine) ni pseudo
gangs wanaotumiwa
na mabeberu. Leo
tunavyopigia debe
ugaidi na kukaribisha
propaganda za magaidi
waliojificha katika misitu
ya Pwani badala ya
kulikamata kambaku
kwa mapembe yake,
huu sio usaliti na dhihaka
kwa mashujaa wetu
tunaojidai kuwaenzi?
Do Black Lives Matter
in Africa? Ukitizama
dhihaka ya Westgate,
dhihaka ya Garissa na
matukio kama hayo,
pamoja na msururu wa
watu ambao wamekuwa
wakiuliwa kwa tuhuma za
ugaidi Kenya; ukitizama
dhihaka ya Boko Haram
na mamia ya maelfu
ya watu waliouliwa
kinyama na jinsi vyombo
vyetu vya habari
vinavyoshabikia habari
hizo, lakini zaidi jinsi
serikali zetu na vyombo
vyake zinavyolipeleka
jambo hili, pengine
badala ya watu wengine
kuuliza Do Black Lives
Matter in Africa?,
tujiulize sisi wenyewe:
Je, tunathamini maisha
yetu? Tunajithamini
kuwa sisi ni binadamu
wenye damu, akili
na utu sawa na hao
wanaotuletea proxy war
na fraud zao za War on
Terror?
To ka tuan ze ser a
ya kubinafsisha na
kugenisha rasilimali
zetu, na hasa katika
madini, kumekuwa na
kilio kwamba tumekuwa
tukipunjwa na kwamba
tumezidiwa ujanja
katika kuweka mikataba.
Kilio kipo mitaani
kwa watu wa kawaida
mpaka ndani ya Bunge
hadi kufikia mahali
serikali kusema kuwa
inarekebisha mikataba
hiyo na kuja na sera

AN-NUUR

SHAWWAL 1436, IJUMAA JULAI 31-AGOSTI 6, 2015

mpya itakayohakikisha amani yetu na usalama wetu?


kuwa angalau na sisi wenye
madini yetu tunaambulia
chochote.
Hata hivyo, pamoja na
kilio hicho, na pamoja
na umasikini wao na
shida zao, watu wetu bado

wanafurahiya maisha. Wapo


salama. Hakuna mauwaji
na umwagaji damu kama
inavyotokea katika kila nchi
iliyotumbukizwa katika
mzaha huu wa magaidi.
Ni kwa kunzingatia hili,
tungependa kuuliza, kwa nini
mabeberu hawa wasituache
na amani yetu wakatafuta
njia za amani za kibiashara,
misaada na ushirikiano kama
inavyofanya China, na bado
wakapata mradi wao?
Yawezekana katika siasa
hizi za world hegemony na
ubabe wa mabeberu, huenda
ikawa kitanzi kimetukaba
barabara, hatuwezi
kufurukuta katika kutekeleza
matakwa ya mabeber u.
Lakini tumekosa hata kauli
na uwezo wa kuwashauri
namna bora ya kutimiza yao
wakatuacha na uhai wetu,

Si tunasema ni marafiki
zetu? Sasa watakuwa
marafiki gani wasiotusikiliza
hata tukitoa maoni juu ya
namna bora ya kutuchinja?
Kwamba wanoe kisu kiwe
kikali ili wasitutese?
Kwetu, hilo wanalolitaka,
kama ibebidi, ni bora
walipate kupitia mikataba ya
sisi kupoteza wapate wao,
kuliko kupitia njia hizi za
kutuundia pseudo gangs na
kutuchagiza kuingia katika
mchezo wa kifimbocheza
wa kupambana na magaidi

wanaofadhiliwa na
kulindwa na mabeberu
hao hao kupitia mlango
wa nyuma.
Taz ama ha l i i l iv yo
Congo DRC, Afrika ya
Kati, Somalia, Nigeria,
Mali na sasa Kenya. Tubaki
na swali hili: Do Black
Lives Matter in Africa?
Je, tunathamini maisha
yetu? Tunajithamini kuwa
sisi ni binadamu wenye
damu, akili na utu sawa na
hao wanaotuletea proxy
war na fraud zao za War
on Terror?

Bakora ya Nyerere yaisubiri CCM!

Inatoka Uk. 1
Nyerere.
Mwalimu aliwahi
kuonya kuwa, chama
kitakachodharau maoni
ya watu, kinaweza kupata
kipigo, kikakosa hata mtu
wa kukisaidia kuomboleza
na kukifuta machozi.
Hali hiyo imejitokeza
kufuatia aliyekuwa kada
maarufu wa chama hicho na
Waziri Mkuu mstaafu, Mhe.
Edward Ngoyayi Lowassa
kukihama chama hicho na
kujiunga na UKAWA kupitia
Chama cha CHADEMA na
hatimaye jana (Alhamisi)
kuchukua fomu ya kuwania
Urais kupitia chama hicho.
Bila shaka Mheshimiwa
huyu kuna dalili ya kuwa
mgombea Urais kupitia
Muungano wa vyama vya
upinzani (UKAWA).
Tukio hili linaashiria
kusadiki onyo alilolitoa
Mwalimu Nyerere wakati wa
uhai wake. kuhusu muelekeo
usioridhisha wananchi wa
CCM na serikali yake.
Hilo tuwaachie wenyewe
CCM, lakini mimi kama
mwananchi, katika hali hii
ya kisiasa iliyopo ya UKAWA

Vs CCM, swali muhimu


kwangu ni hili: Kura yangu
nimpe nani?
Yapo mambo ambayo
yalikuwa ni ahadi ya CCM
na mengine kuingizwa
katika Ilani yao ya uchaguzi.
Yametekelezwa vipi, hilo ni
swali.
Lakini yapo pia yale
ambayo hayakuwa katika
Ilani yao, kama haya ya
kukamatwa masheikh wetu
na kubambikiwa kesi za
ugaidi.
Masheikh ambao
wanadai kupigwa, kuteswa,
kudhalilishwa, na kilio chao
kufika hadi Bungeni.
Mbele ya Spika kutoka
CCM, Kinara wa Serikali ya
CCM, Bungeni, akadai kuwa
hajui kama yupo Sheikh
Msellem, mwanachuoni
mfasiri wa Quran aliyepo
Segerea.
Mheshimiwa huyo wa
CCM akataka apewe taarifa
ili ayafanyie kazi malalamiko
ya Masheikh hao.
M p a k a l e o k i my a a a !
Tulichoona ni yeye kuunga
foleni ya wana-CCM kutaka
kurejea Ikulu kwa kura za
Waislamu! (Soma Uk. 6)

Makala

AN-NUUR

SHAWWAL 1436, IJUMAA JULAI 31-AGOSTI 6, 2015

Historia ya skuli na Madrasa visiwani Zanzibar


Na Ben Rijal

MAKALA mbili zitaangalia


skuli na madrasa mbalimbali
k u a n z i s h wa v i s i wa n i .
Madhumuni makubwa ni
sehemu ya kumbukumbu
na kuelewa kuwa, visiwani
watu wake walishughulika
na elimu za akhera na za
duniya.
Historia ni kioo thabiti
kitakachokuonyesha sura yako
katika zama mbalimbali na
kukusaidia kujua uendako kama
ndipo au sipo? Tunaposoma
h i s t o r i a n i wa j i b u we t u
kuyakubali yale yaliyotokea,
kwani historia sio mara zote
itakuwa katika upande wa
kukufurahisha, kuna nyakati
utaiona historia inakuudhi kwa
kuwa inaelezea yale yaliotokea
usioyawafiki.
Tu n a p o s e m a h i s t o r i a
ni kueleza juu ya yale
yaliyokwisha pita, ambayo
ni matokeo tuliyoyatenda na
kusababisha kutokea. Ndugu
z e t u Wa m e r e k a n i we u s i
wanasema kuwa, siku hizi
kuna history and his story,
ikimanisha kuwa ni historia na
hekaya zako. Yanayoandikwa
kwa wingi na wanahistoria wa
zama hizi huwa ni hekaya zao
na zaidi, mwandishi kutaka
kuwaridhisha watawala.
Utakapoichambua historia
ya Zanzibar utaikuta imepita
katika makataa mbalimbali na
kuelezewa na wana historia kwa
kina, kushinda nchi nyingi za
Kiafrika. Zanzibar imekuwa na
uhusiano na nchi za Mashariki
ya mbali katika kipindi kabla
kuzaliwa Mtume Issa (AS).
Zanzibar ilianzia na kuwa
chini ya himaya ya Mreno karne
ya 16-17, kisha Wa-Oman
1698-1856, kisha kuingilia kati
kwa Muingereza 1856-1885
na kuwa chini ya moja kwa
moja ya Uingereza 1890-1963.
Katika mikondo mbalimbali
ya utawala ndio imewezesha
Zanzibar kutambulika zaidi nje
ya mipaka yake.
Uanzishwaji na skuli
mbalimbali visiwani
Waanzilishi wa skuli kwa
visiwa vya Zanzibar walikuwa
ni Misheni za Kikristo, huku
vyuo vikishamiri watoto wa
Kiislamu kusomeshwa Quran
na kuwafanya wengi wa watoto
wa Kiislamu kujua kuandika
kwa herufi za Kiarabu. Vyuo
vingi vya Quran vikifundishwa
kusoma na kuandika, matokeo
yake kwa muda mrefu watu

Walimu na wanafunzi wa
Aboud Jumbe Mwinyi.
wa visiwani wakiwasiliana kwa
kuandika barua kwa kutumia
harufu za kiarabu.
Wa i s l a m u w a l i o g o p a
k u wa p e l e k a wa t o t o wa o

maskuli kwa kuhofia kuwa


watanasirishwa kwa kufanywa
k u wa Wa k r i s t o. M f a l m e
Sayyid Ali Bin Hamoud,
alivunja mwiko huo Kwa
Waislamu kugomea skuli za
kawaida na kuwalazimisha
kuwapeleka watoto wao katika
skuli za kawaida na hili kama
asingelifanya, Waswahili wa
Zanzibar wangechelewa kupata
elimu ya dunia kwa kipindi
kirefu.
Skuli ya mwanzo kufunguliwa
Zanzibar ilifunguliwa mwaka
wa 1860, ikijulikana kama
Roman Catholic ikafwatiwa
na UMCA iliyofunguliwa na
Bishop William Tozer na Dr.

Mwanzo mwanzo skuli hii


ikichukua wanafunzi wa jamii
ya Wahindi tu, na baadaye
ikawa kwa wote na mara tu
baada ya Mapinduzi ya mwaka
wa 1964, skuli hii ikabadilishwa
jina na kuwa Haile Selassie.
Skuli nyingi ambazo zilikuwa
za makabila zilikuja kugeuzwa
majina na kupewa majina ya
viongozi wa Kiafrika kama
Lumumba, Nkur umah,
Benbela n.k.
Jamii ya Aga Khan ina tarehe
refu na visiwa vya Zanzibar na
inaendelea hadi sasa kuimarisha
miradi ya maendeleo kwa
visiwa vya Zanzibar. Katika
mwaka wa 1925 ilifunguliwa
skuli iliyojulikana kwa jina la
Aga Khan Boys na kufuatiwa
na Madressa Muhammadieh ya
Government School waliokaa wa tatu kushoto ni Maalim jamii ya Mabohora, iliyokuwa
na mchanganyiko wa kike
Edward Steere. Bishop Tozer
Katika miaka hiyo ya 1800 na kiume. Mwaka wa 1931
alikuwa mweledi wa Kiarabu kulianzishwa skuli za makabila ikafunguliwa skuli ya Aga Khan
na vile vile alikuwa ameisoma na nyingi zilikuwa za Wahindi, ya wanawake tu, ikiitwa Aga
Quran kwa undani kabisa.
kwani Wahindi waliwekeza Khan Girls.
Aidha mwaka huo huo wa
Bi sh o p To z er a l i kuwa zaidi maisha yao kwenye elimu
1931, ikafunguliwa skuli ya
Maithnashir katika mwaka wa
1931 iliyokuwa ikiitwa Datu
Hemeani Ithnasheri, mwaka wa
1936 ikafwatia skuli ya Hindi
Sunni Madressa na mwaka
wa 1943 ikaanzishwa skuli ya
Hindoo Free Kanyavidyala
Girls na kwa Pemba mwaka
wa 1947 ikafunguliwa Skuli ya
Indian Mixed mjini Wete.
Ja m i i y a w a t u w e n y e
asili ya Ng azija walipata
shida watoto wao kusoma
Kiarabu na wao wakiamini
kuwa Kiarabu ni lugha ya dini
yao, kwa ari wakajikusanya
na kuchangishana na kuweza
kuanzisha skuli yao katika
mwaka wa 1930. Alikuwa
gwiji wa lugha ya Kiarabu
Walimu wa King George the VI
ambaye ni Mgazija, Sheikh
Burhan Mkele, ndiye aliyekuwa
akipenda kushindana na na biashara. Katika mwaka wa mwalimu wa Kiarabu na kutia
Masheikhe wa Kiislamu na 1891 ilifunguliwa skuli ya Sir msingi mkubwa kwa watu
hoja zake zilikuwa nzito Euan Smith Madressa, ikiwa ni wenye asili hiyo. Aidha skuli
mno, katika makala zengine skuli ya mwanzo ya watu wenye hiyo ilifundisha na Kifaransa
nitamzungumzia Padri Toza makabila. Alikuwa Sir Chalerle na wanafunzi wake wa mwanzo
kama wenyewe Waislamu Euan smith, aliyekuwa na cheo waliofuzu hapo walipelekwa
walivyokuwa wakimwita.
cha kama Balozi wa Kiingereza katika visiwa vya Madagascar,
Baada ya kufunguliwa skuli (British Diplomatic Agent and mmoja kati ya wanafunzi hao
hizo hapo mjini Unguja, kwa Consul General), aliwapendelea ni mwana diplomasia maarufu
upande wa Pemba ilifunguliwa Wahindi waanzishe skuli zao ili Sheikh Ahmed Maulidi.
skuli iliyojulikana kama Freinds wapate kudumisha lugha yao,
Hapo juu nilijaribu
Industrial Mission katika mila zao na thaqafa zao.
kuzielezea skuli za binafsi
mwaka wa 1890, ambayo skuli
K w a n z a s k u l i h i y o ambazo mara tu, baada ya
hiyo ikifunza kazi za mikono ilikuwa katika maeneo ya Mapinduzi ya 1964 zilitaifishwa
zikiwa ni kushona, useremala Mchambawima na baadae na kufanywa kuwa skuli za
n.k. Bahati njema skuli hiyo ikahamia Forodhani na mwisho Serikali.
ilichukua wanafunzi wengi wa ikajengwa katika maeneo ya
Skuli za Serikali zilianza
Kiislamu baada ya kupatikana Mnazi Moja na mwishowe
mwamko.
kufanywa Skuli ya Serikali.
Inaendelea Uk. 4

Makala

AN-NUUR

SHAWWAL 1436, IJUMAA JULAI 31-AGOSTI 6, 2015

Historia ya skuli na Madrasa visiwani Zanzibar

Inatoka Uk. 3
miaka mingi katika visiwa vya
Zanzibar, hapa nitaziorodhesha
skuli za Serikali visiwani
Zanzibar.
Skuli ya mwanzo ya
Serikali ilianzishwa mwaka
1905, mwanzilishi wake
akiwa Sultani Sayyid Ali bin
Hamoud, aliyepata elimu ya
kizungu Afrika Kusini na
Harrow huko Uiengereza.
Skuli hii ilikuwa ndani ya kasri
ya kifalme na kuwekwa hapo,
ilikuwa kutoa agizo kuwa elimu
ya kizungu sio ukafiri. Walimu
waliokuwa wakisomesha hapo
walikuwa kutoka nje, wengi
wao wakiwa wazungu. Mbali ya
walimu hao wazungu, aliletwa
mwalimu kutoka Oman,
Sheikh Abdurahman Al-Kindi,
aliyekuwa akisomesha dini na
kizungu.
Aidha akaletwa mwalimu
mwingine akijulikana kwa jina
la Sheikh Abdyul Barri AlAjizy na mwalimu mwengine
kutoka Uingereza akiitwa Mr.
Rivers- Smith. Mwalimu huyu
alikuwa akisomesha lugha ya
Kingereza na kufanywa kuwa
mwalimu mkuu kutokana na
ujuzi wake aliokuwa nao katika
utawala.
Baada ya kipindi kifupi, skuli
hii ikapata wanafunzi wengi
baada ya kupatikana mwamko
na wazee walikuwa wakipigana
vikumbo kupeleka watoto wao
katika skuli hii. Kutokana na
wingi wa wanafunzi, skuli hii
ikahamishwa kutoka kwenye
kasri ya mfalme na kuhamia
karibu na Msikiti wa Ijumaa
wa Forodhani. Baadaye katika
mwaka wa 1925 ikahamia
katika eneo la Mnazi Mmoja na
kuitwa kwa jina la Government
Central School.
S k u l i y a G ove r n m e n t
School ilitoa wanafunzi wengi
waliokuja kushika nafasi
katika Serikali. Skuli nyengine
iliyokuwa na sifa ilikuwa ni
Darajani Primary School,
iliyoanzishwa katika maeneo
ya Darajani. Mwandishi wa
makala hii alisoma skuli hiyo.
Serikali ya kikoloni ilibidisha
kufunguliwa skuli mbalimbali
kwa Unguja na Pemba.
Wakati huo hakukuwa na
mchanganyiko wa watoto wa
kiume na wa kike, kwa hiyo
jengo lililohamwa la Forodhani,
liligeuzwa na kuwa skuli ya
msingi ya watoto wa kike katika
mwaka wa 1925, mwiko wa
kuzitenga skuli za kike mbali

Wanafunzi wa Darajani Skuli, aliyekaa na aliyevaa miwani ni Maalim Abdalla Kassim


Hanga.

Walimu na wanafunzi wa Muslim Academy


na kiume mbali hapa visiwani,
ulivunjwa katika mwaka wa
1969 na kuwachanganya kuwa
pamoja watoto wa kiume na
kike. Lakini hivi karibuni skuli
iliyokuwa ya Government
School na sasa Ben Bela
Secondary School, imerejea
kuwa ni skuli wanaosoma
wanawake tu.
Pemba nako kwenye mwaka
1930 kulifunguliwa skuli za
msingi katika Wilaya ya ChakeChake na Wete, lakini kuna
maandiko yenye kuonyesha
kuwa Chake-Chake na Wete
kulifunguliwa skuli mapema
zaidi.
Wa p a n g a m i p a n g o y a
taaluma kwa nyakati hizo
wa l i t a m b u a k u wa e l i mu
inahitaji walimu wenye
taaluma ya kusomesha, kwa
hiyo katika mwaka wa 19231935 kilifunguliwa chuo cha
mwanzo cha walimu na L.
W. Hollingsworth kuwa ndio

mwalimu mkuu wa mwanzo,


akisaidiwa na Sheikh Abdulla
Ahmed Seif na kufuatiwa na
Sheikh Muhammad Salim
Barwani (Jinja).
Hollingsworth alifanya
juhudi kubwa ya kusomesha
na alifungua madarasa ya
jioni ambapo alifuatana na
mkewe kusaidia kusomesha.
Hollingsworth ndiye aliyekuja
kuanzisha jarida lililokuwa
likijulikana kama Mazungumzo
ya Walimu, Jarida ambalo
walimu walikuwa wakipata
fursa ya kuandika Insha,
matatizo yao, hadithi fupi na
makala za dini ambazo alikuwa
akiandika Sheikh Abdalla Saleh
Farsy, na zaidi makala za dini
na alifika kuwa Naibu Mhariri
wa Jarida hilo.
Rais mstaafu wa awamu ya
pili wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania, Mhe. Ali Hassan
M w i n y i a l i k u wa k a t i y a
wachangiaji wa Jarida hilo.

Katika juhudi za
kuendelezwa elimu visiwani,
ilifunguliwa Skuli ya Biashara
(Commercial School) baina ya
mwaka wa 1923-1924. Skuli
hii ilitoa wanafunzi ambao
hawakuwa wanafanya kazi za
ukarani visiwani Zanzibar, bali
wengine walifika kufanya kazi
sehemu nyengine za Afrika
Mashariki na kukubalika. Aidha
kulifunguliwa Skuli ya ufundi
ikijulikana kama Industrial
School baina ya mwaka wa
1924-1932, ikiwa inafundisha
ufundi wa mekanika wa magari,
useremala. Nako kwenye
kijiji cha Dole ikaanzishwa
skuli kwa jina la Rural Middle
School katika mwaka wa
1935. Skuli hii ilichukua zaidi
wanafunzi waliokuwa wakikaa
mashambani.
Katika mwaka wa 1935
ikaanzishwa skuli ya mwanzo
ya Sekondari chini ya mwalimu
mahiri Hollingsworth, ambaye

yeye ndiye ambaye aliyeanzisha


chuo cha walimu Zanzibar.
Katika elimu hutajwa sana
mzungu huyu kwa kuwa
aliwajali wanafunzi wake
kama wanawe. Alifika hata
kuwafunga vifungo vya shati
wanafunzi wake waliokuwa
hawafungi vifungo kikamilifu
katika kuwaongoza kuwa na
tabia njema.
Chuo cha kwanza cha
walimu wa kike kilifunguliwa
katika mwaka wa 1942, huku
skuli ya Sekondari ya wanawake
ilikuwa imeanza kuchukua
wanafunzi katika mwaka wa
1947. Kwa upande wa Pemba
ilifunguliwa Dakhalia ya
watoto wa kike katika mwaka
wa 1930.
Mwaka wa 1942 ilianzishwa
Domestic Science School
skuli ya kufunza mafunzo
ya kuendesha mambo ya
nyumbani. Skuli hili ilikuja
kurahisisha shughuli za
wanawake majumbani,
ikiwa kazi za kupika, kulea,
kutunza watoto, kushona,
kufuma, kusuka mikeka,
misala, kutia nakshi kwenye
foronya na kadhalika. Skuli
hii imewanufaisha wanawake
wengi na kustawisha maisha
majumbani. Alikuwa bibi wa
kizungu kwa jina Bibi Johnson,
aliyejizatiti kuwafunza
wanafunzi wa kike mambo ya
nyumbani, ikisemekana kuwa
wakati wake wote wa siku,
alikuwa yupo na wanafunzi na
kutumia wakati wake mchache
nyumbani kwake na mumewe.
Serikali ya kikoloni
ilimtuma Mr. Foster, ambaye
alifungua Teacher Training
Center kikiwa Chuo cha
pili cha kutoa mafunzo kwa
walimu wa mashamba katika
kijiji cha Dole. Bw. Foster
alivunjika moyo sana kuona
kuwa skuli nyingi zinakosa
wanafunzi. Katika utafiti
aliokuja kuufanya, aligundua
kuwa wazee wakiona kuwa
masomo ya dini ya Kiislamu
na Kiarabu hayapewi uzito,
ndipo Mr. Foster alipoanzisha
masomo ya dini pamoja
na Kiarabu na kuwapatiwa
wanafunzi uji asubuhi na
wakati wa mapumziko. Wengi
ya wanafunzi wa chuo hicho
walikuwa wanafunzi waliotoka
m a s h a m b a n i n a Pe m b a .
Baadaye skuli hiyo na ya
Dole ikahamishiwa Bait-Ras,
ambapo chuo hicho kilichukua
wanafunzi hadi kutoka Kenya
Inaendelea Uk. 9

Habari za Kimataifa SHAWWAL 1436,

AN-NUUR

IJUMAA JULAI 31-AGOSTI 6, 2015

Kenyatta agomea ushoga wa Obama


Ampasha bila kupepesa

LICHA ya serikali ya
K e nya n a M a r e k a n i
kutiliana saini katika
mi k atab a k a d h a a ya
maelewano na kuafikiana
kuimarisha uhusiano wa
nchi hizo mbili katika
sekta za kibiashara na
kidiplomasia na katika
mapambano dhidi
ya ugaidi, agenda ya
ushoga aliyokuja nayo
Rais Barack Obama
imekwama.
Pamoja na kwamba Rais
Obama aliingia nchini
Kenya Julai 24 usiku na
kupata mapokezi ya
kihistoria katika nchi hiyo
inayomchukulia kama mtoto
wa nyumbani, aliyerudi na
taji la ukuu wa nchi kubwa
n a yenye nguvu z a i di
duniani, alipogusia suala la
haki za mashoga alielezwa
uso kwa uso kuwa suala hilo
halina nafasi Kenya na wala
haliwezi kuwa mipango ya
Wakenya na haliko katika
fikra za Wakenya.
Akiongea mbele ya
waandishi wa habari katika
Ikulu ya Kenya, Rais Obama
alipinga kwa nguvu ubaguzi
dhidi ya watu wanaojihusisha
na mapenzi ya jinsia moja na
kueleza hadharani kuhusu
haki za mashoga ambapo
aliyataka mataifa ya Afrika

kutowabagua watu kwa


misingi ya hisia za kimapenzi.
Kama mtu ni raia
anayefuata sheria, ambaye
anafanya biashara zake na
kufanya kazi na kufuata
taratibu na kufanya mambo
yote mengine ambayo raia
mwema anastahili kufanya
bila kuleta madhara kwa
yeyoye, wazo kwamba
wanaweza kutendewa tofauti
au kukashifiwa kwa sababu
ya wale wanaowapenda ni
kosa, alisema Rais Obama,
katika mkutano na waandishi
wa habari Ikulu ya Kenya
wakati alipozuru nchini
humo hivi karibuni.
Muda mfupi baadae
ilikuwa ni zamu ya Rais
Kenyatta kuzungumza
ambapo alisema, nchi yake
ya Kenya na Marekani
wa n a s h i r i k i a n a k a t i k a
mambo mengi, lakini suala
la haki za mashoga ni suala
ambalo nchi hizo haziwezi
kuafikiana.
Akiwa sambamba na
Rais Obama, Rais Uhuru
Kenyatta alisimama imara na
kumueleza mgeni wake kuwa
utamaduni huo hauna nafasi
nchini Kenya na kwamba,
ni vigumu kuingiza imani
ambayo watu wa Kenya
kamwe hawaikubali.
"Kuna mambo ambayo

BARAZA Kuu la Haki za


Binadamu la Umoja wa
Mataifa limetoa ripoti,
likieleza wasiwasi wake
kuhusu hali ya haki
za b i n a d amu n ch i n i
Uingereza hususan katika
sheria za kupambana na
ugaidi nchini humo na
kutoa wito wa kutazamwa
upya sheria hizo.
Kifungu nambari 8
cha ripoti ya Baraza Kuu
la Haki za Binadamu la
Umoja wa Mataifa,
kimekosoa ongezeko la
jinai zinazohusiana na
ubaguzi wa kidini na kitaifa
nchini Uingereza na kueleza
wasiwasi wake kuhusu
mwelekeo wa vyombo
vya habari nchini humo
wa kuhubiri chuki dhidi
ya wageni na maneno ya
kibaguzi ambayo yamekuwa

yakisababisha vitendo vya


kibaguzi, uhasama na ukatili
katika jamii ya Uingereza.
Baraza hilo pia limekosoa
sheria mpya ya kupambana
na ugaidi nchini Uingereza,
ambayo inalipa jeshi la
polisi la nchi hiyo mamlaka
makubwa sana, ikiwa ni
pamoja na kufanyia ujasusi
na kudukua mazungumzo ya
watu binafsi kwa kisingizio
cha kulinda amani ya jamii.
Baraza hilo limeitaka
serikali ya Uingereza
kuifanyia marekebisho
sheria hiyo ili iendane na
sheria za kimataifa na kanuni
za haki za binadamu.
Kifungu namba 16 cha
ripoti ya Baraza Kuu la Haki
za Binadamu la Umoja wa
Mataifa kimezungumzia
ongezeko la idadi ya watu
wanaojiua katika jela za
Uingereza na kusisitiza
kuwa, hadi sasa maafisa wa

RAIS Barack Obama wa Marekani (kulia) na Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya.


lazima tukubaliane kuwa ambayo ndio maisha ya kila kosa kubwa na lisiloruhusia
hatuwezi kushirikiana. siku ya wananchi.
kabisa.
Katika utamaduni wetu,
Hivyo mkutano huo
Rais Obama aliendelea na
jamii yetu haiwezi kukubali ulionyesha kuwa Marais ziara yake nchini Ethiopia
mapenzi ya jinsia moja. Hili w a n c h i m b i l i h i z o ambako nako ni kosa la
suala sio lililomo katika wametofautiana vikali jinai kwa watu kujihusisha
fikra za watu wa Kenya na kuhusu haki za mashoga na vitendo vya ngono ya
huo ndio ukweli. Alisema na wasagaji, ambapo kila jinsia moja.
Rais Kenyatta mbele ya mmoja alishikilia msimamo
H U KO U j e r u m a n i ,
mgeni wake na waandishi wake.
Chama cha CDU
wa habari.
Wakati Marekani ikipigia kinachounda serikali ya
Rais Kenyatta alifafanua chapuo haki za ushoga kwa nchi hiyo, nacho kimekataa
kuwa suala la ushoga sio mataifa mengine, hasa baada pendekezo la kuanzishwa
suala muhimu wala la ya Mahakama Kuu nchini ndoa za jinsia moja nchini
kipaumbele kwa watu wa humo kuruhusu ndoa za Ujerumani.
nchini humo na kwamba, jinsia moja, nchi nyingi
Chama cha CDU katika
nchi hiyo inahitaji kujikita za bara la Afrika ikiwemo jimbo muhimu la Berlin
zaidi katika maeneo mengine Kenya, zinaona suala hilo ni nchini ujerumani, kimekataa
kata kata kuanzishwa sheria
za mapenzi ya jinsia moja
nchini Ujerumani.
Shirika la habari la
ABNA limeripoti kuwa
vyombo vya mahakama za kuwa, Canada ina zaidi ya wanachama wote 12,500 wa
Uingereza hawajachukua wazawa na wakazi asilia chama hicho katika mji huo
hatua za kutosha za kuzuia milioni moja na laki mbili, Mkuu, walitakiwa kushiriki
hali hiyo.
ambao wanaishi katika kwenye kura ya maoni juu
Baraza hilo pia limeitaka hali ya kusikitisha. Jamii ya ya pendekezo hilo.
Wakijibu swali la endapo
serikali ya Uingereza kubuni wazawa na Wacanada hao
njia za kisheria za kuzuia asili inatawaliwa na kiwango wapenzi wa jinsia moja
wa z a z i k u wa ch a p a n a cha juu cha umaskini, waruhusiwe kuoana, asilimia
kuwapiga watoto wadogo.
kujinyonga na uraibu wa 45 ya wanachama wa chama
hicho kinachoongozwa na
Hata hivyo suala la dawa za kulevya.
ukiukaji wa haki za binadamu
Takwimu zilizotolewa Kansela Angela Merkel
haliihusu Uingereza pekee, na jumuiya za kimataifa wa Ujerumani, walisema
b a l i n ch i n y i n g i n e z a z a k u t e t e a h a k i z a hapana, kwa mujibu wa
Magharibi nan chi washirika b i n a d a m u k a m a l a Katibu Mkuu wa CDU, Kai
wa London kama Canada, Amnesty Inter national Wegner.
Mjadala wa ama
zimekuwa zikikiuka kwa kuhusu ukiukwaji wa haki
kiwango kikubwa haki za za binadamu, hususan Ujerumani iruhusu ndoa
Wahindu Wekundu ambao za jinsia moja au la kama
binadamu.
Miongoni mwa vipengee ndio wazawa na wakazi asilia yalivyo mataifa mengine ya
vya ukiukwaji mkubwa wa wa Canada, zinaonesha faili Magharibi, umeligawa taifa
haki za binadamu nchini jeusi la ukiukwaji wa haki za hilo lenye nguvu kubwa
Canada ni jinsi ya kuamiliana binadamu.
Miongoni mwa ukiukwaji zaidi kiuchumi barani Ulaya,
na wazawa na wenyeji asili
wa
haki hizo nchini Canada hadi kwenye serikali ya
wa nchi hiyo, ambao ni
ni
pamoja na kubanwa mseto inayoongozwa na
mashuhuri kwa jina la taifa
uhuru
wa raia kwa kisingizio muungano wa CDU/CSU
la kwanza.
pamoja na chama cha SPD.
Takwimu zinaonesha cha kupambana na ugaidi.

UN yakosoa ukiukwaji haki za binadamu Uingereza

6
Na Juma Jumanne
TUKIWA tunaelekea
kwenye uchaguzi mkuu
mwezi Oktoba, mengi
yanasemwa kila kona za
mitaa, vitongoji, vijiji,
ilimradi kila mtu anaonesha
hisia na shauku yake juu ya
jambo hili. Kwenye vijiwe
vya kahawa ndio usiseme.
Wakati watu wanaendelea
na pilika za hapa na pale
za porojo na mengineyo,
serikali nayo katika
kuliendea hilo inafanya
uratibu kwa lengo lile lile la
kufanikisha uchaguzi. Moja
ya mambo ambayo serikali
inayasimamia kidete
ni suala la uandikishaji
wapiga kura ili kuwapata
washiriki halali wa zoezi
hili kwa mujibu wa vigezo
vilivyowekwa vya wapiga
kura.
Kama tunavyojua, nchi yetu
inaendeshwa kwa mfumo wa
kidemokrasia unaotokana
na uwepo wa vyama vingi
vya siasa. Hili hutoa fursa
kwa mpiga kura kumpigia
mg ombea amtakaye kwa
mujibu wa vigezo anavyojua
yeye, kwamba nikimchagua
fulani atafanya hiki na kile
kwa manufaa ya ummah.
Na sisi kama Waislamu, pia
hatukuachwa nyuma kwani
hatuishi hewani, tupo katika
nchi hii hii tukikamuliwa kodi
na TRA.
Mfumo huu wa
k i d e m o k r a s i a u l iv yo n i
kwamba, tunawapigia kura
watu ambao wanaonekana
wana sifa kwa mujibu wa vyama
vyao wanavyoviwakilisha.
Hata kama kuna mtu ambaye
kwa uelewa na ufahamu
wetu tunaona anafaa kuliko
hawa tulioletewa, hakuna
fursa ya kumchagua. Ni
lazima tuwapigie hao hao
walioonekana wanafaa
zaidi kwenye vyama vyao.
Lakini ifahamike kuwa, hawa
wagombea wa nafasi mbali
mbali ni watu ambao kila
mmoja amejipima mwenyewe
na kuona kuwa anafaa na
anaweza kuongoza nchi.

Makala/Tangazo

AN-NUUR

SHAWWAL 1436, IJUMAA JULAI 31-AGOSTI 6, 2015

Kura yangu nimpe nani?

Mhe. Edward Lowassa alipokuwa akitangaza kujiunga na kambi ya UKAWA kupitia


CHADEMA wiki iliyopita.

Dkt. John Magufuli (kushoto), kulia ni mgombea mwenza Mhe. Samia Suluhu Hassan.
Kwa kuwa kuna mfumo kingine kisichokuwa Chama maeneo yanayofikika kufanya
wa vyama vingi, ilitegemewa Cha Mapinduzi. Kwa haraka kampeni. Lengo la kampeni ni
k w a m b a k u t a k u w a n a haraka unaweza kusema pamoja na kukitangaza chama
kupokezana vijiti. Awamu kwamba, pengine kinafanya husika, sera yake na ilani yake.
hii chama hiki kinashinda vizuri sana ndiyo maana kila Dhana yangu ni kwamba,
na awamu nyingine chama awamu kinashinda.
ahadi ambazo chama hutoa
kingine kinashinda. Jambo
Nasema hivyo kwa sababu kwa wananchi ndizo ambazo
la kushangaza ni kwamba, kila chama kina ilani yake, humfanya mwananchi aungane
tangu kuanzishwa mfumo sera na kanuni yake. Inapofika na hicho chama na hatimaye
wa vyama vingi hapa nchini wakati wa uchaguzi, kila chama kukipigia kura inapofika wakati
m wa k a 1 9 9 2 , h a i j awa h i hupata fursa ya kuzunguka wa uchaguzi.
kutokea kushinda kwa chama kila mahali kote nchini kwa
Nchi hii ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, ni
zao la nchi mbili ambazo
ni Tanganyika na Zanzibar.
Kwa upande wa Tanganyika
kuna mchanganyiko wa dini
mbali mbali, kuu zikiwa
Uislamu na Ukristo. Visiwani
n a o n i h iv yo h iv yo, i l a
tofauti na Bara, Waislamu
wamewazidi Wakristo kwa
mbali. Tunaambiwa ni takriban
asilimia zaidi ya 99% wakati
huku Bara Waislamu na
Wakristo hawakuachana sana
kwa idadi (%).
Ikiwa ukweli ndio huo,
m a a n a y a ke n i k wa m b a
Wa i s l a m u n d i o w e n y e

maamuzi ya kusema nani awe


Rais Zanzibar na hata Rais
wa Jamhuri. Tafsiri yake ni
kwamba Waislamu ndio wanaCCM kwa kuwa imeendelea
kukaa madarakani kwa muda
mrefu sasa. Na kukaa huku
madarakani, kunatokana na
ushindi ambao imekuwa
ikiupata katika awamu zote
za chaguzi zilizofanyika kwa
kupata kura nyingi kushinda
vyama pinzani kutoka kwa
Waislamu.
Bila shaka wengi wetu
tumekuwa tukiamini kuwa
sera na Ilani ya chama ndio
vigezo pekee vinavyokipa
chama uwezo wa kushika
hatamu. Lakini pia, kura
katika sanduku la kura, ndiyo
i n ayo t o a m s h i n d i . Kwa
maana na tafsiri hiyo, inaweza
kusemwa kuwa CCM imekuwa
na sera na Ilani nzuri ambazo
zimekuwa zikiwanufaisha
Waislamu wa nchi hii ndio
maana wameendelea kuipa
kura kushika usukani.
Ahadi mbali mbali ambazo
serikali iliyopo madarakani
imekuwa ikizitoa imeweza
kuzitekeleza ipasavyo!!! (?)
Mambo mbali mbali
a m b ayo s e r i k a l i i l i a h i d i
kufanyia kazi ni pamoja na
kuhuishwa kwa Mahakama
ya Kadhi, kujiunga na OIC,
na mengine mfano wa hayo.
Mengine ambayo yalitekelezwa
lakini hayakuwepo kwenye
Ilani ya CCM iliyomwingiza
Mheshimiwa Jakaya Mrisho
Kikwete madarakani, ni
pamoja na haya ya kukamatwa
masheikh wetu na kubambikiwa
kesi za ugaidi. Masheikh ambao
wanadai kupigwa, kuteswa,
kudhalilishwa, na kilio chao
kufika hadi Bungeni ambapo
Kinara wa Serikali ya CCM,
Bungeni Waziri Mkuu alidai
kuwa hajui kama yupo Sheikh
Msellem, mwanachuoni mfasiri
wa Quran aliyepo Segerea
na wenzake na kwamba
wamedhalilishwa mwisho wa
kudhalilishwa.
Mheshimiwa huyo wa
CCM akadai apewe taarifa,
ili ayafanyie kazi malalamiko
ya Masheikh hao. Mpaka leo
kimyaaa! Tulichoona ni yeye
kuunga foleni ya wana-CCM
kutaka kurejea Ikulu kwa kura
za Waislamu!
Huu ni muhtasari wa
mazuri pengine yanayoweza
kutajwa kuwa wamefanyiwa
Waislamu na hivyo kuipigia
kura CCM muda wote wa siasa
za vyama vingi (iwapo kura
ndiyo iliyokuwa ikiwabakiza
CCM Ikulu, Dar es Salaam

Inaendelea Uk. 9

TANGAZO

AN-NUUR

SHAWWAL 1436, IJUMAA JULAI 31-AGOSTI 6, 2015

BISMILLAHI RAHMANI RAHIIM

ISLAMIC PROPAGATION CENTRE

KIRINJIKO ISLAMIC TEACHERS COLLEGE


(NA.YA USAJILI WA NACTE-REG/TLF/078

P.O. Box 62, Same Kilimanjaro, Mob: 0657 705 878

NAFASI ZA DIPLOMA YA UALIMU WA SHULE ZA MSINGI


2015/2016

Waislamu Kote NchiniWaislamu


Mnatangaziwa
Nafasi za
Mafunzo ya Diploma
na NACTE
au VETA
ufaulu
Kote Nchini
Mnatangaziwa
Nafasi zakinachotambulika
Mafunzo ya Diploma
ya Ualimu
wana
Shule
zawa D nne katika mtihani
ya Ualimu wa Shule za Msingi katika Chuo cha Ualimu Kirinjiko Islamic
wa kidato cha nne (CSEE).
kilichopo Same Mkoani Kilimanjaro.
B: NAMNA
YA KUOMBA:
Msingi katika Chuo cha Ualimu Kirinjiko Islamic kilichopo
Same
Mkoani Kilimanjaro.
Chuo kimepata usajili kamili wa NACTE na kinaendeshwa kwa misingi
1. Mwombaji anatakiwa kujaza fomu ya maombi AU
na maadili
ya Kiislamu.
na maadili ya Kiislamu. Chuo kimepata usajili kamili wa NACTE na kinaendeshwa
2. Kuombakwa
kwamisingi
njia ya mtandao
(Online
Application) kupitia Tovuti ya
NACTE(www.nacte.go.tz).
A: SIFA ZA MWOMBAJI:
TANBIHI: Atakayeomba kwa njia ya fomu, hatatakiwa kuomba kupitia
1. Awe Muislamu na; A: SIFA ZA MWOMBAJI:
njia ya mtandao wa NACTE.
2. Amehitimu kidato cha nne (CSEE) na kufaulu kwa kiwango cha Division
1. Awe Muislamu na;
I-III au GPA.1.6, AU
D: ADA YA MAOMBI:
3. Mwenye cheti cha Grade IIIA, AU
Ada ya maombi ya NACTE ni shilingi elfu ishirini (20,000/=) tu.
2. level
Amehitimu
cha nne
(CSEE)
na chuo
kufaulu kwa
kiwango
Division
I-III au GPA.1.6,
4. Mwenye cheti (NVA
4) cha kidato
kozi yoyote
kutoka
katika
C: MWISHO
WAcha
KURUDISHA
FOMU:
Mwisho wa kurudisha fomu za maombi ni tarehe 15/08/2015.

AU

Fomu za Maombi zinapatikana chuoni Kirinjiko Islamic Teachers college na katika vituo vilivyoorodheshwa hapa chini.
3. Mwenye cheti cha Grade IIIA, AU
705627.
Karume,Nyumba Na. 05 :
Arusha: Ofisi ya Islamic
4. Mwenye
(NVAJambo
level 4) cha 0765024623
kozi yoyote kutoka katika chuo
kinachotambulika
NACTE
Mtwara:
Amana Islamic S.S:na
0715
Educationcheti
Panel,
465158/
231007.
Msikiti mtihani
wa Majengo
Plastic,au Ghorofa
2 waShinyanga
VETA naya
ufaulu
D nne katika
wa kidato cha
nne0787
(CSEE).
Songea: Kwa Kawanga Karibu na
karibu na Manispaa ya
mkabala na msikiti Mkuu
B: NAMNA
Shinyanga
Mjini
Bondeni YA KUOMBA::
Msikiti
wa
NURU
:
:0752180426
Kahama
ofisi
ya
0783552414/0762817640
0713249264/0683670772.
1. Mwombaji anatakiwa kujaza fomu ya maombi AU
AN NUUR Karibu na msikiti
Kilimanjaro: Moshi: Msikiti wa
Mkuzo Islamic High School
2. Kuomba
kwa njia
ya mtandao (Online
Application)
kupitia Tovuti
ya 348375.
wa
Ibadhi
: 0753
Riadha :712
216490Same
:0717
993930/0688794040
Juhudi Studio mkabala na
Mbeya: Ofisi za Islamic Education
NACTE(www.nacte.go.tz).
Dar es Salaam: Ubungo Islamic
Benki ya NMB Same: 0757
Panel
Uhindini

High
School
:
013344.
0785425319.
Rexona
Video
TANBIHI: Atakayeomba kwa njia ya fomu, hatatakiwa kuomba kupitia njia ya mtandao wa
0756584625/ 0657350172
Same: Kirinjiko Islamic Secondry
mkabala na Mbeya RETICO:
NACTE.
School: 0784 296424/0655 Ofisi ya Islamic Ed. Panel
0713 200209/0785425319.
697 075, Usangi- Falhum Temeke -Msikiti wa Nurul Ya
Rukwa :Sumbawanga:Jengo la
kin :
Kibakaya : 0787 142054.
Haji Said Shule ya Msingi
D: ADA
YA MAOMBI:
Ugweno
Kifula Shopping 0655144474/0787119531
Kizwike 0717082 072.
Morogoro
Wasiliana
na
Centre- Yusuph Shanga :
Tabora: Kituo cha Kiislamu
Ramadhani
Chale
:
078458776.
Isevya:
0784
0715704380.
Tanga: Twalut Islamic Centre
944566/0787237342
Dodoma Hijra Islamic Primary
Mabovu Darajani : 0715
Nzega:
Dk
Mbaga-0754
School
:
0716
544757/071
894111 Uongofu Bookshop:
576922/0784576922.
Singida: Ofisi ya Islamic
0784 982525, Korogwe:
Iringa: Madrastun Najah: 0714
Education. Panel karibu na
SHEMEA SHOP : 0754
522 122.
Nuru snack Hotel : 0786
690007/071569008. Mandia
Pemba: Wete: Wete Islamic
425838/0784 928039.
Shop - Lushoto: 0782257533.
School
:
0777
Manyara:
Ofisi ya Islamic Ed.
Handeni Mafiga -0782
432331/0712772326.
Panel Masjid Rahma:
105735/0657093983
Unguja : Madrasatul Fallah:
0784491196
Mwanza
Nyasaka
Islamic
0777125074.
PANDU
Kigoma: Msikiti wa Mwandiga:
Secondary School : 0717
BOOKSHOP
0777462056
0714717727 Kibondo
417685/0786 417685.Ofisi ya
karibu na uwanja wa
Islamic Nursery School:
Islamic Education Panel
Lumumba
0766406669.
Kasulu:
Mtaa wa Rufiji mkabala na
Mafia: Ofisi ya Ust. Yusufu Ally
Murubona
Isl.SS:
Msikiti Al-Amin 0785 086
jirani na msikiti mkuu :
0714710802.
770/0714097362
0773580703.
Lindi Wapemba Store: 0784
Musoma Ofisi ya Islamic Ed
974041/0783 488444/0653
Panel
-Mtaa
wa
Kwa maelezo zaidi piga simu: 0787 188964, 0784 267762 na 0654 613080

Makala

8
Na Shaba Rajab
SUALA la kuanzishwa
Mahakama ya Kadhi kwa
Waislamu nchini, ni suala
ambalo kamwe haliwezi
kutoka katika fikra za
Waislamu. Waislamu
kuwa na Mahakama
ya Kadhi, ni muhimu
kwa kuwa kungewapa
uhakika wa kusimamia
kwa usahihi wa mambo
yao ya kiibada na kiimani.
Suala hili lilishika kasi
zaidi, hasa pale Chama
cha Mapinduzi (CCM)
kilipoamua kuliingiza suala
hilo katika Ilani yake ya
uchaguzi ya mwaka 2005.
Hapo Waislamu wakawa
na matumaini kwamba,
sasa umefika wakati wa
kuwahudumia Waislamu
kwa haki na kwa yakini
katika Sheria za Ndoa,
Talaka, Mirathi na Wakfu.
Hata hivyo baada ya suala
hilo kuonekana kuridhiwa
na serikali na mchakato
wa k u l i we k a k i s h e r i a
kuanza, kuliibuka shinikizo
kali kutoka kwa Wakristo
wakiitaka serikali kuachana
na suala hilo.
Licha ya serikali
kuunda timu kuchunguza
uendeshaji wa mahakama
hiyo katika nchi nyingine
zenye Mahakam hiyo ili
kujiridhisha na hatimaye
kukiri kuwa haikuwa na
tatizo, bado wasiopenda
uwepo wake walishinikilia
kuikataa. Hata pale ofisi
ya Waziri Mkuu ilipounda
kamati ya kufanikisha
mchakato huo, bado jambo
hilo lilisuasua huku muda
nao ukizidi kuyoyoma.
Shinikizo la Wakristo
kuikataa Mahakama hiyo
lilikolea na wao ndio
walisikilizwa, hoja za
Waislamu zikatupiliwa kwa
mbali.
Hata katika Bunge la
katiba, Tume ya Katiba nayo
haikutaka kusikia haja hiyo
ya Waislamu. Walitupilia
mbali maoni yao ya kuhitaji
chombo chao hicho.
Serikali ilisitisha
uwasilishwaji wa muswada
wa Mahakama ya Kadhi
katika Mkutano wa 19 wa
Bunge uliohitimishwa mjini
Dodoma April mwaka huu
na ukawa ndio mwisho wa
matumaini ya kuanzishwa
mahakama hiyo kwa
Waislamu.
K atibu wa Bunge,
Dk. Thomas K ashilila

AN-NUUR

SHAWWAL 1436, IJUMAA JULAI 31-AGOSTI 6, 2015

Tuingie uchaguzi tukitafakari


hali ya Masheikh wetu Segerea
Ponda alipigwa risasi, akatupwa Sero
Amekuwa mfungwa ambaye hajahukumiwa
Lipo pia la kuzimwa Mahakama ya Kadhi, OIC

SHEIKH Ponda Issa Ponda (kushoto) akiongea na mmoja wa mawakili


wake akiwa mahakamani.
alithibitisha kuwa muswada
wa Mahakama ya Kadhi
hautakuwapo katika
mkutano huo.
Dk. Kashilila alisema
haijulikani ni lini
utawasilishwa bungeni kwa
sababu Mkutano wa Bunge
uliofanyika Mei mwaka huu,
ulipangwa mahsusi kwa ajili
ya bajeti.
Waziri Mkuu alivyosema
wataangalia na kushauriana
kimsingi, alitoa maneno ya
busara tu au ilikuwa kauli
ya mtu mzima, lakini huu
muswada hautakuwapo,
alisema Dk. Kashilila.
Awali hali iliyojitokeza
wakati wa semina ya
wabunge haikuwa nzuri
kutokana na mvutano mkali
miongoni mwa wabunge.
Kulikuwa na mvutano
mkubwa baina ya viongozi
wa dini kuu mbili, Waislamu
na Wakristo kundi moja
likitaka uwasilishwe huku
kundi lingine likipinga. Kwa

mujibu wa taarifa ambazo


zipo, Waislamu walidai kuwa
waliahidiwa na viongozi
ambao wako madarakani
kwamba watapatiwa
Mahakama ya Kadhi. Hiyo
ilikuwa wakati wa kampeni
kabla ya uchaguzi mkuu
2010.
Pia wakati wa Bunge la
Katiba ilipotokea mvutano
kuhusu hatma ya mahakama
hiyo hadi kusababisha
baadhi ya wajumbe
Waislamu wa lililokuwa
Bunge la Katiba kutamka
bayana kuwa wangeipigia
kura ya hapana rasimu
ya tatu ya katiba, Serikali
ikaahidi kupeleka muswada
bungeni ili kutunga sheria
itakayo ruhusu uundwaji
wa Mahakama ya Kadhi,
muswada ambao kama
tulivyoona, ulikataliwa
kufika Bungeni kama
alivyobainisha Dk Kashilila
hapo awali.
Kimsingi kinachoonekana

hapa, Serikali na hata CCM,


wa m e k u wa wa k i t u m i a
mbinu za aina mbalimbali
ili kuhakikisha mambo yao
yanafanikiwa kwa mgongo
wa umma wa Kiislamu. Suala
la uhakika wa kutekelezwa
jambo lenyewe halitizamwi.
Kwa kuwa jambo lenyewe
ni ahadi, basi jamii kama
ya Waislamu huahidiwa
na kubakia na matumiani.
Wa n a p o t i m i z a wa j i b u
wao kulingana na ahadi
walizopewa, na kwa kuwa
iliyotolewa ilikuwa ni ahadi
tu, basi huachwa njia panda.
Unapokaribia uchaguzi
mwingine hutengenezwa
hadaa nyingine kwa
staili nyingine, alimradi
wanaohadiwa waendelee
kuishi kwa matumaini
bila kutimiziwa yale
wanayoahidiwa.
Sasa ni wazi suala hili
la Mahakama ya Kadhi
halipo tena. Uchaguzi Mkuu
ndio huo umeingia tena.

Tunahoji, jamii ya Kiislamu


imejitambua na kujitathimi
namna ya kuuendea
uchaguzi huo, pamoja na
mambo mengine, lakini kwa
kuweka mbele zaidi maslahi
mapana ya jamii?
Ukweli unaothibitika
hapa ni kwamba, hakuna
nia ya dhati ya serikali wala
chama tawala kuwaruhusu
Waislamu kuwa na chombo
hicho kisheria zaidi ya hadaa
kwa maslahi ya kisiasa.
Tutakumbuka kuwa Rais
Jakaya Kikwete, aliwahi
kuzungumzia hadharani
kuhusu suala la Mahakama
ya Kadhi wakati suala hilo
lilipozidi kushamiri katika
mijadala ya kijamii. Ilifika
mahali kwa kauli yake
kueleza kuwa hakuhusika
kuliweka suala hilo katika
Ilani ya Uchaguzi ya Chama
Cha Mapinduzi (CCM).
Ndugu zangu napenda
mtambue kuwa, mgombea
urais hahusiki na uandaaji
wa Ilani, wala hahusishwi
nawasihi tu tuwe watulivu
na tuiache kamati ifanye
kazi yake, ni watu wenye
busara, naamini hawatafanya
maamuzi mabaya, hayo
ni maneno ya Rais Jakaya
Kikwete aliponukuliwa
na vyombo vya habari
Novemba 11 mwaka huu.
Rais Kikwete alitoa kauli
hiyo wakati alipokuwa
akizungumza katika Ibada ya
kumsimika Askofu Mkuu wa
Kanisa la Kiinjili la Kilutheri
Tanzania (KKKT), Alex
Malasusa, katika Kanisa
Kuu la Azania Front, Dar
es Salaam.
Katika hotuba yake, Rais
Kikwete alisema ameamua
kulizungumza suala hilo
kwa sababu ameziona
dalili zinazoashiria kuwa
kusipokuwa na uangalifu,
upendo na mshikamano
baina ya Waislamu na
Wa k r i s t o h a p a n ch i n i
utaharibika kutokana na
mjadala kuhusu Mahakama
ya Kadhi.
Lakini aliwasihi
Wa t a n z a n i a k u w a n a
subira kwa sababu suala
hilo, ambalo mjadala wake
unashika kasi, hatma
yake itajulikana Februari
mwakani (2015), Tume
ya Kurekebisha Sheria,
itakapotoa ripoti yake.
Hata hivyo, Rais Kikwete
a l i o n e k a n a k u wa t u p i a
lawama wanasiasa kuwa
ndio wanaochochea suala
Inaendelea Uk. 13

9
Inatoka Uk. 6

na Zanzibar. Kama zipo njia


nyingine, hayo ni mengine.
Mimi siyajui).

K i n a c h o z i d i
kunichanganya zaidi
ni kwamba, kila mmoja
anasema vizuri kuhusu
msimamo wa chama
chake, kwamba wakiingia
watadhibiti maovu yote.
Lakini pamoja na ushawishi
huo, binafsi nimeshindwa
kushawishika kwa nukta
moja tu, ambayo ni
uaminifu. Nafsi inashindwa
kukubali kuwaamini watu
ambao hawana elimu ya
muongozo, watu ambao
wako mbali na mafundisho
ya dini, watu ambao wako
mbali na Mungu!!
M g o m b e a U r a i s wa
CCM, kwa awamu hii ni
Dk. John Pombe Magufuli.
Ni katika viongozi ambao
wanadaiwa kufanya vyema
katika nyadhifa mbali mbali
alizowahi kushika, na hasa
aliposhiriki zoezi la kuuza
nyumba za serikali.
Ni muhimu sana
kufahamishana juu ya
mambo nyeti kama haya kwa
kuwa, aghalabu tumekuwa
tukishiriki uchaguzi lakini
mp a ka leo hii hatuna
lolote la kujivunia kwamba
limetekelezwa na serikali

Makala

AN-NUUR

SHAWWAL 1436, IJUMAA JULAI 31-AGOSTI 6, 2015

Kura yangu nimpe nani?

SHEIKH Farid Hadd

SHEIKH Msellem.

tuliyoichagua.
Kumbuka uchaguzi
haupo mbali. Kura yangu
nimpe nani ambaye
atanihakikishia usalama wa
dini yangu, wazazi wangu,
m a s h e i k h z a n g u, m ke
wangu, wanangu, ndugu
zangu, rasilimali za taifa na

mengineyo?
Ila kuna mambo mawili,
matatu inafaa tuyafahamu
uzuri tusije jichanganya.
Kuna matatizo yetu ya
msingi kama Waislamu,
ambayo hayawezi kutatuliwa
na yeyote atakayeingia
madarakani kama sisi

Pemba nayo ikaanzishwa


Sayyid Abdalla Secondary
School katika mwaka wa 19621963. Madhumuni ya kujengwa
skuli hii ilikuwa imalizike kuwa
ni College, Maalim Zubeir
Rijal, alikuwa ndiye mwalimu
mkuu wake wa kwanza na
kufuatiwa na rafiki yake
Maalim Ahmed Abdulrahman.
Baadaye skuli hii ikabadilishwa
jina na kuitwa Fidel Castro
Secondary School.
MIOME (Mombasa
Institute of Muslima
Education), Chuo hiki
kilikuwa Kenya katika mji
wa Mombasa, ikiwa zaidi ya
asilimia 50 ya wanafunzi wake
wakitokea Zanzibar. Chuo
hicho mfadhili wake mkubwa
alikuwa Mfalme Sayyid Khalifa
bin Harub, pamoja na Aga
Khan. Mzalendo wa Mombasa
Khamis Muhamadi, alitoa eka
30 za ardhi yake kujengwa
chuo hicho. MIOME na
East Africa Muslim Welfare
Society nitaielezea katika
makala za siku za mbele na
pigo walilolipata Waislamu wa
Afrika ya Mashariki.
Mwaka wa 1952 kilifunguliwa
Chuo cha Kiislamu kwa jina la
Muslim Academy na wengi
waliosoma hapa walimalizia
katika vyuo vya Hadhramout

na Al-Azhar. Aliyepata kuwa


Balozi wa Tanzania Uingereza
na Naibu Waziri wa Mambo ya
nchi za Nje Dk. Abdulkadeer
Shareef ni matunda ya Muslim
Academy. Muslim Academy
ilikuwa chimbuko la kutoa
wanafunzi mahiri katika lugha
ya Kiarabu na dini ya Kiislamu.
Mwaka uliofwatia wa 1953
ilianzishwa skuli iliyokuwa
ikijulikana Arabic Speaking
School, ambayo ikiwaandaa
wanafunzi kukimudu kiarabu,
lugha ya dini ya Kiislamu
na baadhi ya wanafunzi
waliosoma hapo waliendelea
na masomo yao huko Misri,
ukiwa kama mpango maalumu
baina ya Serikali ya Misri chini
ya Jamedari Gamal Abdul
Naseer na serikali ya Zanzibar.

wenyewe hatujakuwa na
mtaji wa kutosha. Mtaji
utakaomfanya yeyote
anaiyeingia madarakani
kututizama kama Mwalimu
Nyerere alivyowatizama
wazee wetu wakati wa
kupigania uhuru na miaka
ya mwanzo ya Uhuru hata
akawa anavaa kofia na
kufunga swaumu ya sunna
akiwa na Sheikh Ramia na
wazee wa Kiislamu. Pili,
yapo mambo yanatuhusu
kama Watanzania, tunaoishi
na wenzetu wa dini nyingine
katika nchi hii Tanzania,
ambao tunalazimika kuwa
chini ya serikali yoyote
itakayokuwa madarakani
kwa mujibu wa Katiba na
Sheria za nchi. Hapa ndipo
ninapojadili mimi, kura
yangu nimpe nani Oktoba.
Tatu, kipo kisa cha Wayahudi
kupewa manna na salwa
wao wakasema wamechoka
chakula kimoja miaka
nenda miaka rudi, wakataka
wa b a d i l i s h i we wa p a t e
mchicha, kabichi, matango,
vitunguu, ngano, kunde na
kama hayo. Wakakemewa
kuwa wanataka kubadili
vizuri kwa vilivyo vibaya.

Quran inasema:
Na (kumbukeni habari
hii kadhalika) Mliposema:
Ewe Mussa! Hatuwezi
kusubiri kwa chakula cha
namna moja tu (Manna
na Salwa), basi tuombee
kwa Mola wako atutolee
vile vinavyooteshwa na
ardhi, kama mboga zake na
matango yake na ngano yake
na adesi zake na vitunguu
vyake. Akasema (Mwenyezi
Mungu), mnabadili vitu
d u n i k wa v i l e v i l iv yo
bora?.(2:61)
Katika agenda yetu hii
ya Uchaguzi Mkuu na
wagombea wake, katika
kupima Sera, Ilani na ahadi
za vyama vilivyoingia
katika kinyanganyiro hiki,
ka tika ku wa tiza m a n a
kuwapima wagombea, la
kuzingatia hapa ni kwamba
hatuzungumzii habari ya
Manna na Salwa.
Jamani nisaidieni; Kura
Yangu Nimpe Nani Mwezi
Oktoba Mwaka 2015?
Mkamilifu ni Allah pekee.
Wabillah Tawfiiq!
(Juma Jumanne-Simu:
+255 659 789 468/ +255
752 527 833, Kateshi,
Manyara)

Historia ya skuli na Madrasa visiwani Zanzibar


Inatoka Uk. 4
sehemu za Mombasa.
Mwaka wa 1955
ikafunguliwa Skuli ya ufundi,
Trade School katika maeneo
ya Mikunguni, chuo hicho cha
ufundi kilisaidia sana katika
ufanisi wa kuzitengeneza
samania za maskuli pamoja na
ofisi za Serikali na majumba
yaliyokuwa yakimilikiwa na
Wakfu.
Sekondari ya Ufundi
( S e c o n d a r y Te c h n i c a l )
ilifunguliwa Baiti Ras mwaka
wa 1949 na skuli hii ikatoa
mwanafunzi wa mwanzo
Afrika Mashariki aliyebobea
juu ya somo la Nuclear
Physics Sheikh Mohammed
Abubakar.
Bada ya Chuo hicho cha
ufundi ikafwatia kujengwa skuli
ya Sekondari ya King George
the VI ambayo walimu wake
wote walikuwa ni wageni na
walimu wachache waliokuwa
ni wazalendo, wakiwemo
Maalim Aboud Jumbe Mwinyi,
Khakoo, Maalim Zubeir Rijal,
Maalim Ahmed Abdulrahman,
Maalim Abdallah Farhan.
Skuli hii ya King George the
VI ilijengwa kwa michango ya
wananchi na Serikali kusaidia.

Wahitimu kuelekea
Makerere College
Mara tu Chuo cha
Makerere kilipoanza kuchukua
wanafunzi kutoka nchi za
Afrika Mashariki, Zanzibar
ilipeleka wanafunzi na wengi
wa wanafunzi wa mwanzo wa
Makerere College walikuwa ni
watu muhimu katika sehemu
ya serikali na utawala.
Wanafunzi wa mwanzo

waliopelekwa walikuwa
Othman Shariff, aliyekuja kuwa
mwanaharakati wa kutetea
Zanzibar kupata Uhuru na
bingwa wa kutibu wanyama,
Ali Khamis bingwa wa kilimo
akaja kuwa Spika wa mwanzo
wa Baraza la Wakilishi, Ahmed
Rashid alikuwa ni kati ya
wataalamu wa mwanzo katika
Afrika Mashariki katika fani ya
mifugo, Ali Muhsin Barwany
kiongozi wa ZNP mpiganiaji
wa Uhuru wa Zanzibar, alikuwa
kati ya mawaziri wa Serikali ya
mwanzo ya Zanzibar kabla ya
Mapinduzi.
Wanafunzi hao wanne
waliokwenda Makerere
College wakafwatiwa baada
ya miaka miwili na Sheikh
Mohd Nassor Habsi, Sheikh
Omar Abdalla ndio aliyekuwa
mwanafunzi wa kwanza kwa
Zanzibar kufuzu kwa somo la
Uhai (Biology) na kufwatiwa
na Maalim Zubeir Rijal ambaye
yeye akatakhasusi juu ya somo
la wanyama (Zoology) kisha
kuwa ni mwanafunzi wa
mwanzo kuchukua shahada
ya kwanza (BSc Honours)
ya Zoolog y katika chuo
cha Queen Marry College
cha Uingereza, Abdulrasul

Khakoo, mtaalamu mkubwa


wa hisabati aliyemalizikia kuwa
ni Profesa wa hesabu nchini
Uieng ereza, Muhammad
Ghasani (Bingwa) mtaalamu
huyu alipata umri mrefu
na kuweza kutoa mchango
mkubwa katika taaluma ya
kilimo visiwani na Mohammad
Ali Awadh.
Baada ya kundi hili la
wanafunzi likafuatia kundi
lililoong ozwa na Maalim
Aboud Jumbe Mwinyi, bingwa
mwengine huyu wa elimu
ya uhai (Biology) baada ya
kujiunga na siasa na kuwacha
uwalimu anakuwa Rais wa
pili wa Serikali ya Mapinduzi
Zanzibar. Daktari Ahmed
Idarus Baalawi, bingwa wa
meno aliyekuwa katika mwezi
anatumai nusu ya mwezi
hospitali ya Manazi Mmoja na
nusu mwezi kuwashughulikia
wanafunzi.
Ta k r i b a n h a o wo t e
n i l i owa t a j a wa l i o h i t i mu
Makerere College, walikuwa ni
sehemu muhimu ya maendeleo
ya Zanzibar.
Makala ijayo itaelezea
namna vyuo na Madrasa
vilivyoanzishwa Zanzibar na
maendeleo yake.

10
Na Omar Msangi
JUMAMOSI ya wiki
iliyopita Julai 25, 2015 gazeti
la JamboLeo lilitufahamisha
k u wa wa t u h u m i wa wa
uvamizi wa kituo cha Polisi
Sitakishari wametoa siri
nzito. Siri yenyewe ni kuwa
watuhumiwa hao wamesema
kuwa wanakusanya silaha
kwa ajili ya kusimika dola ya
itikadi ya imani yao.
Habari zilizopatikana
kutoka ndani ya askari
waliopo kwenye operesheni
inayofanywa katika kijiji
cha Mandikongo, Bupe na
Chamanzi Wilaya ya Mkuranga
mkoani Pwani zinaeleza
kuwa baadhi ya watuhumiwa
wamesema kwamba wanavamia
vituo vya polisi ili kukusanya
silaha ambazo zitawapa nguvu
ya kugeuza utawala nchini ili
uwe wa itikadi ya dini yao.
Limeandika gazeti hilo.
Gazeti hilo limedai kuwa kwa
mujibu wa taarifa zilizotolewa
na vijana hao wa Afande
Mangu, pamoja na kuteka vituo
ili kupata silaha, watuhumiwa
hao huwa wanapewa mafunzo
(ya kijeshi?) na wakufunzi wa
ndani na nje.
Tu n a p a t a wa k u f u n z i
kutoka ndani na nje, lakini
suala kubwa linalotukwamisha
ni jinsi ya kuingiza silaha, hivyo
kutokana na kuwezeshwa na
wahisani wetu ndio maana
tunakusanya bunduki za
ndani.
Anadaiwa kusema
a s k a r i m m o j a a k i nu k u u
maneno ya mtuhumiwa
wa tukio la Sitakishari na
kuongeza akisisitiza kuwa
polisi watapambana vikali
kuhakikisha kuwa vikundi
kama hivyo vinachakazwa
kokote viliko ndani ya nchi.
Kule Upareni, ukisikia
m s e m o, N d a m a y a e t e
mikono, maana yake ni kuwa
kama kuna jambo mlikuwa
mkilisubiri kwa hamu, basi
muda wake umetimia.
Kama lilivyosema gazeti
tunalolisherehesha hapa,
Sitakishari kuna siri nzito.
Haihitaji kuwa mtaalamu
bingwa wa masuala ya uhalifu
(criminolog y), kugundua
mashimo katika taarifa hizi
tunazopewa juu ya suala la
Sitakishari na hata yale
matukio yanayodaiwa kutokea
Morogoro watu wakikamatwa
na bendera zenye maandishi
ya Kiarabu!
Gazeti linatuambia kuwa
waliokamatwa wamesema
kuwa wanateka vituo vya polisi
ili kupata silaha za kusimamisha
dola inayoongozwa na dini yao.
Tuanze kusema kuwa kama ni
siri, haya maneno sio mara ya
kwanza kusemwa. Bila shaka
tutakumbuka kuwa baada ya
lile tukio la Songea la mtu

Makala

AN-NUUR

SHAWWAL 1436, IJUMAA JULAI 31-AGOSTI 6, 2015

Wandishi wa Habari.

Mchezo wenu ni mauti kwetu!


Siri ya Sitakishari haijasemwa bado
Tuambiwe mamluki wanatoka wapi
Kawaingiza nani nchini na kuwalinda

MKUU wa Jeshi la Polisi IGP Ernest


Mangu.

MKUU wa Majeshi Jenerali Davis


Mwamunyange.

aliyekuwa akipita misikitini


kukusanya pesa za kununulia
bunduki na tasbihi (risasi),
tulihoji, inakuwaje mtu apite

msikiti wa kwanza wa pili wa


tatu na ujumbe huo lakini
hakamatwi? Na mpaka leo,
hakuna taarifa kuwa mtu

yule aliyetambuliwa kwa jina


la Abdallah Kesi, aliwahi
kukamatwa na kufikishwa
mahakamani. Aliwahi kusimulia

Na Shaban Rajab

jina moja la Ustadh Ahmad


wa Mikumi na fundi cherehani
aliyetajwa kwa jina la Muya
pamoja na mfanyabiashara
aliyetajwa kwa jina moja la
Mushi.
Taarifa zinaeleza kuwa
chanzo cha kukamatwa Bw.
Muya ni simu yake ya mkononi
kukutwa na milio ya bunduki
huku kwenye kioo cha simu
yake hiyo (screen wallpaper)
kuonyesha picha ya wapiganaji
wa al Shaabab.
Aidha, imedaiwa kuwa
hadi sasa kuna baadhi ya
wakazi wa Kidatu Kilombero
wa m e l a z i m i k a k u k i m b i a
makazi yao kutokana na hofu
ya kukamatwa na polisi, baada
ya kuzagaa fununu kwamba
majina yao yapo katika orodha
ya watu wanaotafutwa na
polisi, ambao wanatakiwa
kuunganishwa na wenzao
walioko rumande katika ya kesi
hiyo hiyo ya ugaidi.
Kundi la kwanza la
Waislamu wanaoshikiliwa
rumande kwa tuhuma za ugaidi
mkoani Morogoro ni Majaliwa
Mohammed Ngarama, Muhudi
Omar Jambia, Ramadhani
Mohammed Athuman, Juma
Ismail salum, Nassir Abdallah
Mussa, Ally Shaban Athumani,

Ramadhani Hamisi Wawa,


Juma Ramadhani Ibrahim,
Hassan Ally Hamis, Hamis
Hassan Ntuko na Maulid
Hassan Sultan.
Hawa wote wamefunguliwa
kesi ya ugaidi namba 16 ya
mwaka 2015.
Kundi la pili linawajumuisha
Bw. Khalid Omary Jumbe,
John Wales, Fredrick Evarist
Chamnungu, Ridhiwani Issa
Mwiru, Yusuf john Juma
Bakihayo, Juma Salum Abdalla,
Shomary Rajabu Singo, Ally
A b d a l l a E n z i M n g i n d o,
Khamis Fadhili Nahoda,
Hamis Islam, Rahibu Salimu
Msuya, Dawali Ramadhani
Msuya na Athumani Omary
Jumbe.
Kundi hili limefunguliwa
kesi ya ugaidi namba 17,
2015 ambapo kesi yao
ilitajwa Jumatatui wiki hii
katika makahama ya mkoa
w a M o r o g o r o, a m b a p o
iliahirishwa na watuhumiwa
kurejeshwa rumande hadi
Agosti 8 kesi yao itakapotajwa
tena.
Pamoja na kwamba
kesi za watuhumiwa hao
zimekuwa zikitajwa tu tangu

Hofu yatanda, ni huzuni tupu!


HOFU imetanda miongoni
mwa Waislamu baada ya
kupatikana kwa taarifa kuwa
baadhi ya watuhumiwa
katika kesi ya ugaidi,
hawajulikani walipo.
Taarifa zilizopo ni kwamba
kuna baadhi ya watuhumiwa
hawajukani walipo na wala
hawaonekani mahamakani siku
za kutajwa kesi zao.
Aidha, hakuna taarifa zozote
zilizotolewa mahakamani
kueleza wapo wapi na kwa nini
hawaletwi mahakamani, jambo
ambalo limezua wasiwasi kwa
Waislamu wa Morogoro.
Mmoja wa watuhumiwa
hao ametajwa kwa jina moja la
Amini, ambaye ni mfanyakazi
wa Shirika la Usambazaji
Umeme nchini TANESCO.
Taarifa zaidi zinabainisha
kuwa baadhi ya watuhumiwa
waliachiwa lakini hali zao kiafya
zikielezwa kudhoofu sana
tofauti na walivyokamatwa.
Inaaminiwa kuwa hali hiyo
imetokana na mateso makali
waliyopata watuhumiwa hao
baada ya kukamatwa.
Baadhi ya walioachiwa ni
mtuhumiwa aliyetajwa kwa

Inaendelea Uk. 11

kijana mmoja katika vijana


waliowahi kukamatwa Songea
wakituhumiwa kwa ugaidi
na baadae kuachiwa, kuwa
wakati akihojiwa, aliuliza juu
ya yule jamaa Kesi, waliokuwa
wakimuhoji wakamkatiza kwa
kumwambia, huyo tunajua
habari zake! Habari gani?
Kwa nini mtu apite akichagiza
watu kununua silaha kihalifu
na kinyume na sheria, lakini
husikii akikamatwa? Basi
kama ni siri, watakuwa nayo
hawa akina Kesi na hao
waliosema kuwa wana taarifa
zake. Ni kama inavyotokea
kule Mwanza, anakamatwa
Mkuu wa Kitengo katika
msikiti fulani unaohimiza
Jihad Feki ya kuuwa makafiri,
lakini kiteng o kinaachwa
kinaendelea na mahubiri ni
yale yale na kila baada ya muda
watu wanatoweka, unaambiwa
wamekwenda shamba! Je,
tutakuwa tumekosea tukiingiwa
na wasiwasi kuwa huenda hawa
ndio mtaji wa kutuundia
pseudo gangs tunaoambiwa
wapo msituni Lindi, Pwani na
Morogoro?
Pili, baada ya muda mfupi,
katika masiku yaliyoendana
na lile tukio la Amboni,
zilisambazwa taarifa katika
CD na picha za mtu
aliyejifunika nyuso, akisema
hayo tunaoambiwa leo kuwa
ni siri nzito. Mtu yule aliyejitaja
kwa jina la Kaisi, alisema kuwa
yeye ndio kiongozi wa kundi
linaloteka vituo vya polisi
kukusanya silaha za kufanyia
Jihad.
Sisi baada ya tukio
lile tulisema kuwa katika
ulimwengu wa leo, hakuna
namna vyombo vyetu vya
usalama vinavyoweza kudai
kuwa havijui nani alitoa
ujumbe ule. Lakini zaidi ya
hapo ni kuwa iliripotiwa katika
gazeti moja kuwa gazeti hilo
lilipewa CD na muhusika na
wao wakaenda kutaka maoni
ya Mkuu wa Jeshi la Polisi.
Kwa hiyo, tulitarajia kuwa
waliopewa CD Hizo, ndio
wangekuwa mashahidi namba
moja. Lakini kimya!!!
Sasa kama ni siri nzito,
siri hiyo haijasemwa bado.
Wananchi wanahitaji kujua,
nani yule alikuwa akipita
misikitini kukusanya pesa za
kununulia tasbihi. Nani yule
aliyetengeneza CD na kudai
kuwa ndiye kiongozi wa kuteka
vituo vya Polisi.
Kwa mujibu wa gazeti, polisi
mmoja anaripoti kuwa watu
wanaowashikiliwa wamesema
k u wa wa n a wa k u f u n z i
kutoka ndani na nje ya nchi.
Wakufunzi hao ni akina
nani? Wameingiaje nchini na
kujichimbia katika misitu hiyo
bila serikali kujua?
Kama polisi wetu wameweza
kuwahoji watuhumiwa mpaka

Inaendelea Uk. 11

11
Inatoka Uk. 10

wakakiri kuwa ndio waliovamia


na kuuwa Sitakishari na
kupora silaha, kama askari
wetu wameweza kuwahoji
wakaweza kusema kuwa lengo
la kupora silaha hizo ni nini,
kama wameweza kuwahoji
wakafichua kuwa wana
wakufunzi kutoka ndani na
nje wa kuwapa mafunzo ya
kijeshi, bila shaka polisi pia
watakuwa wanajua, wakufunzi
hao ni akina nani. Na kama ni
siri nzito, ipo hapa.
Kama kuna watu, wawe
wa dini yoyote, Watanzania
wenzetu, ambo sio pseudo
wenye kuundwa na kutumiwa na
maaduni wa nchi hii au tuseme
mabeberu wenye malengo yao
ya kutuletea machafuko na
kupandikiza ugaidi, hawa sio
wa kutisha. Kama alivyosema
yule polisi aliyenukuliwa
na JamboLeo kuwa polisi
wanapambana kuhakikisha
kuwa wanavitokomeza vikundi
vyenye kuteka vituo, wala
haichukui muda, wanamalizwa
kweli.
Katika toleo la wiki iliyopita
la gazeti hili, tulielezea mbinu
chafu za wakoloni/mabeberu
kuunda, kufadhili na kuendesha
makundi haramu, maarufu
kama pseudo gangs ambayo
hufanya matukio ya kihalifu,
kuuwa na kufanya hujuma
mbalimbali, kisha husingiziwa
watu au vikundi fulani. Na
tukasema, hiyo hutumika sana
katika hii inayoitwa vita dhidi
ya ugaidi. Kwa hiyo, kama
kuna Al Shabaab wa kweli kule
Somalia, basi wapo na pseudo
al Shabaab. Na kwamba
hawa pseudo al Shabaab
huwezi kupambana nao na
kuwashinda kwa sababu,
kama lilivyo neno pseudo, ni
kitu cha uwongo. Na ukitaka
kujua uwongo wake, fikiria
utakavyofikiria kuwafikiria
vijana wa Kitanzania, fikiria
utakavyofikiria, unaoweza
kuwaita vijana siasa kali au
mujahidina wa Tanzania (bila
ya kuwa na bias), hutamuona
mwenye jeuri na uwezo wa
kufanya tukio la Sitakishari.
Kwa hiyo, kama ni siri nzito,
basi siri yenyewe ni kuwa
tushaingiliwa na pseudo
kundi la watu wanaotaka
kusimamisha dola kwa mujibu
wa dini yao kupitia kupora
silaha katika vituo vya polisi.
Na kama ni kufichua siri,
basi siri ya kufichuliwa ni
hii kwa sababu hii ndiyo
itakayotuangamiza.
Kule Nigeria, kulikuwa na
watu wakijiita Jam'at Ahl asSunnah lid-Da'wah wa'l-Jihd'.
Hawa walikuwa na mtizamo
tofauti juu ya elimu waliyoiita ya
Magharibi kwamba inapotosha
maadili ya Kiislamu. Mara
kimzahamzaha, ukaanza
mtindo kama huu wa kuteka
Sitakishari zetu. Kila likitokea
tukio kama hilo, hudaiwa kuwa
ni Jam'at Ahl as-Sunnah lidDa'wah wa'l-Jihd' (Boko
Haram). Na taarifa kama
hizi za JamboLeo, zikawa

Makala

AN-NUUR

SHAWWAL 1436, IJUMAA JULAI 31-AGOSTI 6, 2015

Mchezo wenu ni mauti kwetu!

KAMANDA wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, Kamishna Suleiman Kova.


zinasambazwa kuwa wanateka
silaha ili kusimamisha Dola ya
Kiislamu. Leo Boko Haram
kutoka silaha za kuteka kituo
cha polisi mithili ya Ushirombo,
wana mpaka vifaru, na kila
aima ya silaha nzito unayoijua
ya kivita. Wanafikia kudaiwa
kuteka kambi za kijeshi!

Wanateka wasichana 200,


mwaka wa pili sasa, si polisi,
si jeshi la Nigeria wala usaidizi
kutoka Marekani, Ulaya na
Israel, uliweza kuwakomboa!
Hawa hawawezi kuwa wale
Boko Haram-Jam'at Ahl
as-Sunnah lid-Da'wah wa'lJihd'. Watakuwa pseudo Boko

Haram.
Yapo mambo matatu hapa
ya kuzingatia. Kwa muda sasa
kumekuwa kukiendeshwa
harakati za kuwakamata watu
ikidaiwa kuwa ni operasheni
ya kuwasaka magaidi. Hili
likichanganywa na haya ya
Sitakishari, inapandikizwa

Inatoka Uk. 10

a k i o n g e a n a m wa n d i s h i
mapema wiki hii jijini Dar es
Salaam.
Alisema kuwa hivi sasa wapo
katika mawasiliano na familia
na ndugu za watuhumiwa,
ili kukamilisha mipango ya
kupata mawakili.
Alisema ujumbe wa
Waislamu wa Morog oro
wamelazimika kuja jijini
Dar es Salaam kukutana
na K amati ya Kutetea
Waislamu, inayowahudhumia
watuhumiwa wa ugaidi na
uchochezi katika Gereza la
Segerea, wakiwemo Sheikh

ya Muung ano wa Tanzania


walipanga njama za kufanya
vitendo vya kigaidi, ambavyo
vinavyojumuisha kushambulia
watu na hata kusababisha vifo.
Katika mashitaka hayo, baadhi
ya watuhumiwa wamedaiwa
kuandaa shambulio dhidi ya
maofisa wa polisi huko Udzungwa,
wengine wakidaiwa kujaribu kuua
watu.
Baadhi ya watu waliotajwa
kutaka kuuliwa walitajwa kuwa
ni Anna Tendwa Pius, Amosi
Alphonce Msopole, Thomas
Fransis Manjole, Azama
Namiyuya na Novatus Osmond
Ngupe.
Hata hivyo, tangu wakati huo,
kesi za watuhumiwa hao zimekuwa
zikipangiwa tarehe za kutajwa tu
katika mahakama ya Mkoa wa
Morogoro bila kusikilizwa, huku
watuhumiwa wakiendelea kusota
rumande bila kuwekewa dhamana
wala kuwa na mawakili.
Kundi la pili la watuhumiwa,
wamejumishwa watuhumiwa 12
akiwem o Imamu wa Msikiti

Hofu yatanda, ni huzuni tupu!

waliposhitakiwa, baadhi ya
Waislamu wanaofuatilia kesi
za wenzoa hao, wamelalamikia
kitendo cha kuzuiwa na polisi
kuingia mahakamani kila
zinapotajwa kesi za wenzao
hao.
Wakati huo huo, wakati
sakata la ug aidi likizidi
kuwaandamana baadhi ya
Waislamu na viongozi wao nchini,
Waislamu mkoani Morogoro
wameutaka umma wa Kiislamu
nchini kuwaunga mkono katika

kuwasaidia watuhumiwa hao.


Waislamu hao wa Morogoro
wamesema kwa jinsi kesi
inavyopelekwa, juhudi za
makusudi za kuwawekea
watuhumiwa hao mawakili
zinahitajika haraka kwa
k u wa h a d i s a s a h a k u n a
wa kuwatetea na kesi zao
zimekuwa zikipangiwa terehe za

kutajwa tu na si kusikilizwa tangu


waliposhitakiwa mahakani hapo.
Wenzetu waliokamatwa hadi
sasa wanasota korokoni kwa
kukosa dhamana, kesi zimekuwa

za kutajwa tu, mawakili hatuna,


hawana msaada wowote, kesi
yao haionekani katika vyombo
vya habari, wengi hawaijui
wala hawajui kinachoendelea,
sasa tumeamua kuutangazia
umma wa Kiislamu kwamba
watuunge mkono kuwasaidia
na kuwatafutia mawakili,
alisema Ust. Juma Kitunga
kutoka Morogoro, wakati

Ponda Issa Ponda, Sheikh Farid


Hadd, Sheikh Msellem Ali
Msellem na wenzao, ili kuangalia
namna ya kushirikiana katika
kazi hiyo.
Ju m l a y a Wa i s l a m u 2 5
walikamatwa na polisi huko
Kidatu na Ruaha Wilayani
Kilombero mkoani Morogoro
tangu Februari mwaka huu na
kuwekwa rumande wakidaiwa
kupanga njama za kufanya ugaidi.
Kwa mujibu wa hati ya
mashitaka katika kesi namba
17, 2015 iliyofunguliwa katika
mahakama ya mkoa Morogoro,
imeonyesha kuwa kundi la kwanza
lenye watuhumiwa 13 akiwemo
Imamu wa Msikiti wa Sunna
Kidatu, Juma Salum Abdalla,
walikamatwa wakidaiwa kuwa
kati ya Febriari 4, 2015 na Mei 1
mwaka huu katika Kata za Kidatu
na Sanje Wilaya ya Kilombero
mkoani Morogoro na katika
maeneo mengine ya Jamhuri

wa Kilombero, wakidaiwa
kukutwa na maguruneti mawili
ya kutupa kwa mkono na sare
zisizoruhusiwa.
Walidaiwa kuwa walikutwa
na viatu jozi mbili, kofia, koti
ambavyo vinafanana na sare za
jeshi la wananchi.
Baadhi yao walifunguliwa
mashitaka ya kukutwa na vitu
vya milipuko na mafuta ya
mlipuko (water jelly Explosives
Vol IV.)

jambo la kuzikubalisha akili


zetu kuwa miongoni mwetu
wapo magaidi au watu wenye
nia ya kusimamisha Dola ya
Kiislamu kupitia njia za kigaidi,
kwa maana nyingine tunao
akina Jihad John wa IS.
Pili, hili likishakubalika,
inakuwa ni hatua muhimu
ya kupandikiza pseudo
gangs, kama mutawaita Al
Shabaab, Boko Haram au IS
au vyinginevyo.
Ta t u , p s e u d o g a n g s
zikishapandikizwa, hakuna
mtakachoweza kufanya
kujisalimisha. Mkipigwa
Sitakishari Ukonga, mnatuma
vikosi kuwatafuta Kisarawe,
wakati pseudo g angs,
w a m e e l e k e a B a g a m oy o,
Zanzibar au hata je ya nchi
kusubiri maelekezo ya kuja
kupiga shabaha nyingine.
Kama ni kufichuka siri nzito,
basi itafichuka tukiwajua
wanaounda hizi pseudo gangs
walio nje na ndani ya nchi,
wanaowalinda waweze kudumu
kufanya yale yanayoendelea
Nigeria utadhani nchi haina
serikali, polisi wala jeshi.
Nne, ambalo linaweza
kutusaidia kwa sasa, ni kukataa
kuaminishwa uwongo utakao
athiri akili zetu, uoni wetu
na saikolojia yetu tukafikia
mahali pa kuona kuwa
tuna IS miongoni mwetu.
Tukishindwa kufanya hilo,
t u k i s h i n d wa k u l i k a m a t a
kambaku kwa mapembe
yake, mengine yatakuwa ni
porojo tupu. Hakuna ahadi ya
kamanda yoyote iwe wa polisi
au jeshi kwamba tutapambana
na wauwaji wa Sitakishari au
magaidi, itakayotusaidia.
Itakuwa ni yale yale ya mzaha
wa Boko Haram. Mwaka wa
pili sasa, kauli mbiu iliyoanzia
Washington DC ya hoax ya
Bring Back Our Girls, bado
haijawaokoa wasichana 200 wa
Chibok.
Ni magaidi wa aina gani
ambao kwa mfano wanaweza
kuteka wasichana 200,
watawaficha wapi, katika
msitu gani Tanzania ambapo
kwa zaidi ya miaka miwili,
polisi, makachero na JWTZ,
wanashindwa kuwafikia na
kuwakomboa kama si mambo
ya mzaha (hoax, fraud na
jokes).
Maadhali tuna akili, tuna
hiyari: kujiuza wenyewe
katika fraud hii au kusimama
madhubuti kama wahenga
wetu Suleiman Mamba katika
Majimaji na akina Mkwawa.
Hawa walikuwa wazalendo
kweli, walio hiyari kujiuwa
kuliko kunajisi nchi yao kwa
kuwa vibaraka wa wakoloni.
Wakoloni ambao ndio hao
hao wanaotujia leo na ukoloni
mpya wa world hegemony
wakitumia njia hii ya kuleta
vurugu na machafuko kupitia
wanachoita ugaidi badala ya ile
ya kuja kuvamia kijeshi.

12

MAKALA

UTUNZI U MASHANI

Narejea Mhariri, niweke japo pembeni


Niutowe ushauri, tungo zetu gazetini
Siri kuwa hadharani, kwetu sisi mtihani
Tuziunde tungo zetu.

Tuziunde tungo zetu, Bara hata Visiwani


Tungo zitukuze utu, waja siyo hayawani
Tusiwatukuze watu, mbele yetu mtihani
Faragha tena hakuna

Atukuzwaye manani, akhera na duniani


Kutukuzwa ikhiwani, wapi aya nambieni
Mtukufu Jailani, n Rasuli Ikhiwani
Kulikoni Ikhiwani?.
Kiigizo ni Shaban, Robert wa Ngamiani
Aliitukuza fani, leowanatoa shani
Faragha zatiwa ndani, warithi wapate nini
Haki zetu mtihani.

Ela bila ushairi, lugha zote mtihani


Shake Spear mahiri, wamsifu kulikoni
Tena waona fahari, mtukuzapo wageni
Tungo zetu bure kwani?
Nchi yetu Tanzaniya, Tanzania kulikoni
Ni fasaha yenye riya, manufaa kwa wageni
Lugha waliyovamiya, tukawaweka jikoni
Tungo zetu bure kwani?
Mrambowa-0713 616 313

MILA ZAO DINI YETU

Ibada kwetu ni dhima, ela walioamini


Qalima ikisimama, ya Mola wetu Manani
Aula waloamini, Duniya ni mtihani
Wapi Aya na Hadithi.
Kongole kwa Ikhiwani, jahidi Afghani
Kwa Farao gerezani, kosa lao kuamini
Mkono wa Marekani, demo mtego wa nyani
Wapi Aya na Hadithi.
Wale wasioamini, huishi kwa kutamani
Mapito ni mtihani, Akhera na duniani
Wakosapo hulaani, lawama kwa ikhiwani
Wapi Aya na Hadithi.
Wao vyote hutamani, waviweke kibindoni
Dhahabu yote madini, wamiliki na Urani
Watawala kulikoni, rejeo la wakoloni
Wapi Aya na Hadithi.
Iwapi Palestina, Burma cello visiwani
Wauliwa kwa mapana, wale walioamini
Mauaji yafanana, kuuliwa waumini
Wapi Aya na Hadithi.
Kinara ni Mareni, Ulaya na Duniani
Kila aliyeamini, hupewa jina kwanini
Siasa kali ni nani, kama sio waumini
Wapia Aya na Hadithi.
Kadhi wamekomaliya, asiwepo kulikoni
Uganda, Zenj na Kenya, yupo tangu ukoloni
Wakomaa waso haya, alibaini Manani
Wapi Aya na Hadithi.
Tamati naweka nanga, tukaishi nchi gani
Semeni sisi wapanga, nchi tuitafuteni
Muone tabu ya unga, ugali apate nani
Wapi Aya na Hadithi.
Masare SR (Mrambowa)
071361633

SHAWWAL 1436, IJUMAA JULAI 31-AGOSTI 6, 2015

Dini ni Mwenendo unaokusanya watu


pamoja na wala hautenganishi

Na ziamrishe mema, tungo zetu ikhiwani


Tusitete na kusema, hizi nazo tungo gani
Ajifunzaye kusema, hivi kwake kosa gani
Leo twatukuza waja.

Watunzi wa ushairi, sisi tumekosa nini


Twalaumu wahariri, malipo hatuyaoni
Katuni mwazihariri, na mapeni mfukoni
Bure tungo zetu kwani?.

AN-NUUR

Na Dr. Akili Mohamed


Akili

HUKURANI
zote anastahiki
mwenyezi
mungu mola mlezi
wa ulimwengu na
rehema na amani
zimfikie mbora wa
viumbe bwana wetu
muhamad na jamaa
zake na sahaba zake
wote: ama baada
ya utangulizi huu
mfupi:Kwa hakika
dini ya kiislamu
ambayo ni nyepesi
inaling ania umoja
daima na kuzoeana
kati ya watu wote na
inakataza kutengana
na kusambaratika
kwani miongoni mwa
msiba mkubwa ambao
umeukumba umma
huu ni kuonjwa kwa
kudhoofika kwa nguvu
yake ni kutokana
na kutengena na
na kusambaratika.
amesema mwenyezi
mungu "enyi mlioamini
mnapokutana na
kundi la maadui basi
liangamizeni na mumtaje
mwenyezi mungu kwa
wingi ili mpate kkufaulu
na mumtii mwenyez i
mungu na mtume wake
na wala msigombane
mtagawanyika na
kuharibikiwa na
kuondoka nguvu zenu na
subirini hakika mwenyezi
mungu yupo pamoja na
wenye kusubiri. hanfali
miongoi mwa upendeleo
pekee wa umma huu ni
uma mmoja. amesema
mwenyezi mungu ((na

hakika umma wenu ni


umma mmoja na mimi
ni mola wenu mlez i
niogopeni" (51) AlM u u m i nu n a . k wa
hakika zimekuja aya
na hadithi kwa aina
mbalimbali juu ya dalili
za qur-ani na suna
zinazoamrisha umoja.
wakati mwingine
huja kwa mari ya
uwazi kama katika
neno lake mwenyezi
mungu mtukufu
((shikamaneni katika
dini ya mwenyezi
mungu nyote na
wala msifarakane na
kumbukeni neema
za mwenyezi mungu
kwenu pale mlipluwa
maadaui akazizoesha
nafsi zenu mukawa kwa
neema za mwenyezi
mu n g u n d u g u n a
mlikuwa pembezoni
mwa shimo la moto
na tukakuokoeni ,
hivyo hivyo ndivyo
anavyobainisha
m we n y e z i mu n g u
aya zake ili mpate
kuongoka)) 103 AlImrani.
Amesema Kurtubi
((Mungu amrehemu))
hapa mwenyezi mungu
mtukufu anaamrisha
kuzoeana na
anakataza kutengana
kwani kuteng ana
ni kuangamia na
kushikamana ni
kuokoka) na katika
sahihi ya muslim toka
kwa abii hurarata
amesema, amesema
mtume (saw) ((hakika
m we n y e z i mu n g u
anaridhia kwenu
mambo matatu.
anaridhia kwenu
mumuabudu yeye na
wala msimshirikishe
na chochote na
mshikamane katika
dini ya mwenyezi
mungu nyote na
wala msifarakane na
anachukia kwene,
pamesemwa na
amesema, na wingi wa
maswali na kupoteza
mali (kufuja) na wakati

mwingine huja amri


ya kupatikana jambo
ambalo halipatikani
isipokuwa kwa umoja.
amesema mwenyezi
mungu ((kwa hakika
waumini ni ndugu, basi
utengenezeeni udugu
wenu na muogopeni
m we n y e z i mu n g u
i l i mu r e h e m i we ) )
(1) anfali na kutoka
kwa anasi bin maliki
(ra) kwamba mtume
(saw) amesema
((msibughudhiane
wala msihusudiane
na wala msilipishane,
na kuweni waumini
wote ni ndugu, si
halali kwa muislamu
kununiana na nduguye
zaidi ya siku tatu (3).
ameipokea imamu
ahmad, hii ni dalili
inaamrisha waislamu
kufanya mambo
yanayozidisha mapenzi
kati yao. na kukatazwa
na kila jambo
linalozlaishamaudhi
k wa wa i s l a mu n a
kuamrisha kwa
uwazi kabisa kuwa
wawe ndugu, na
wala haiwezekani
kwa waislamu wae
ndugu isipokuwa
wawe ni wenye
k u p e n d a n a k wa n i
udugu ni kinyume
cha kuteng ana na
miongoni mwa
sampuli za qur-ani
na suna katika dalili
zawajibu wa udugu na
umoja kati ya waislamu
ni katazo la wazi juu
ya kufarikiana na
kuhitilafiana ambao ni
kinyume na umoja na
kukusanyika. amesema
m we n y e z i mu n g u
mtukufu ((na mtiini
m we n y e z i mu n g u
na mtume wake na
wala msig ombane
mkadhoofika na
zikaondoka nguvu
zenu, subirini
h a k i k a m we n y e z i
mungu yu pamoja
na wanaosubiri))

(45) anfali amesema


a twa b a ri ((a n a s ea
m we n y e z i mu n g u
ametaja kwa waumini
tiini enyi waumini
mola wenu, na
mtume wake kwa
yale aliyowaamrisha
na yaacheni yale
aliyowakataza na wala
m s i g o m b a n e k wa
lolote msikorofishane
mtaharibikiwa
akasema wala
msihitilafiane
mtatengana na nyoyo
zenu kukosana na
kuharibikiwa. akasema
wala msihitilafiane
mtatengana na nyoyo
zenu kukosana
na kuharibikiwa
akasema mkadhoofika
mkaingia woga na
kuondoka nguvu
zenu. ameitoa toka
barani toka kwa bin
abbas, katika neno lake
mwenyezi mungu (( na
wala musiwe kama
wale waliofarikiana na
wakagombana baada
ya wale waliokuja na
katika ubainifu hapo
wao wana adhabu
kubwa 9105) al-imrani
amesema katika hili na
nyinginezo ndani ya
qur-ani ameamrisha
m we n y e z i mu n g u
juu ya kuwasifu
waumini kuungana na
amekataza kutengana
na kug ombana na
akawaambia kuwa
waliangamia waliopita
kabla yao kwa sababu
ya kujionyesha na
na kug ombana na
kukosana katika dini
ya mwenyezi mungu
inatakikana kwa wote
tuwe mkono mmoja
ch i n i y a b e n d e r a
ya uislamu ambayo
imaamrisha kuzoeana
na kushikamana
na tunakatazwa
juu ya kuteng ana
na kug ombana na
m we n y e z i mu n g u
ndiye anayesema
kweli na yeye ndiye
anayeokoa njia.

13

MAKALA

Tuingie uchaguzi tukitafakari


hali ya Masheikh wetu Segerea

RAIS Jakaya Kikwete (katikati), kulia kwake ni Kaimu Muft Sheikh Zuber na
Mhe. Bernard Membe.
Inatoka Uk. 8
hilo kutokana na manufaa
yao binafsi. Kitendo cha
Rais Kikwete kupenda
kuzungumzia suala la
Waislamu Makanisani,
kilidhihirisha kwamba hofu
aliyo nayo kuwa mkwamo
m k u u wa k u a n z i s h wa
mahakama hiyo ulikuwa
Kanisa.
Kama
Kanisa
wangeridhia, basi moja
kwa moja na serikali nayo
ingeliharakisha suala hili la
Waislamu bila mizwengwe
yeyote.
Lakini Rais Kikwete
alisema pia kuwa kiini cha
mjadala kuhusu Mahakama
ya Kadhi ni wanasiasa na
akajivua kuhusika. Balala
yake akatupa mzigo kwa
awamu ya Rais Mstaafu
Benjamin Mkapa, Philip
Mangula na Mzee Kingunge
Ngombale Mwiru.
Chimbuko
la
kinachosemwa sasa kuhusu
Mahakama ya Kadhi ni
bungeni, na muasisi wa
hoja hii ni Mheshimiwa
Augustino Lyatonga Mrema
alipokuwa Mbunge wa
Temeke.
Bwana Mrema alikuja
na hoja binafsi bungeni
ya kutaka kuundwa kwa

Mahakama ya Kadhi
n ch i n i , a l i s e m a R a i s
Kikwete na kubainisha kuwa
hoja hiyo iliungwa mkono
na aliyekuwa Mbunge wa
Bagamoyo wakati huo,
marehemu Baruti Rajabu.
Alisema kuwa baadaye
ikafuatiwa kwa nguvu na
hoja binafsi ya aliyekuwa
Mbunge wa Moshi Vijijini
k u p i t i a T L P, T h o m a s
Ngawaiya.
Aliongeza Rais Kikwete
kusema kuwa kwa busara za
Spika wa kipindi hicho, Mzee
Pius Msekwa, akisaidiwa
na kiongozi wa shughuli
za serikali bungeni wakati
huo, Waziri Mkuu mstaafu
Frederick Sumaye, alikataa
hoja hiyo kujadiliwa bungeni
moja kwa moja kutokana
na kile alichokitaja kuwa
ni unyeti wake, na kuamua
kuipeleka katika Kamati
ya Bunge ya Katiba na
Sheria, ambako kamati hiyo
iliyoongozwa na wenyeviti
wawili tofauti, Arcado
Ntagazwa. Alipoteuliwa
kuwa waziri, nafasi hiyo
ilishikwa na Athumani
Janguo.
Alisema baada ya kamati
hiyo kukamilisha utafiti na
kukabidhi ripoti kwa Spika,
aliikabidhi serikalini ambako

inafanyiwa kazi ili kutoa


ushauri upasao.
Serikali imekabidhi
Tume ya Kurekebisha Sheria
kulifanyia kazi jambo hilo na
kushauri ipasavyo. Tume
inaendelea na kazi yake
ya utafiti wa kina na kwa
taarifa nilizonazo, huenda
mwezi Februari mwakani
watamaliza kazi yao ya
utafiti na kuwa na lolote la
kushauri, alisema Kikwete.
Aliwahakikishia
Watanzania kuwa serikali
haitafanya uamuzi ambao
hauna maslahi kwa nchi
na wala jambo hilo
halitaamuliwa kinyemela.
Alisema suala la
Mahakama ya Kadhi si lake
binafsi, na kuwa lilikuwepo
kabla yake na mchakato
wake ameukuta.
Alisema mchakato wa
suala hilo haukuanza na
Ilani ya Uchaguzi ya CCM
ya mwaka 2005, kama
wengi wanavyodai na kuwa
Ilani hiyo ya uchaguzi
imeutambua mchakato
huo kujipa dhima ya
kuuendeleza ili kujaribu
kutafuta ufumbuzi.
Akikanusha kuhusika
kwake kuliweka suala hilo
katika Ilani, akisema kuwa
mchakato wa kuandika Ilani

AN-NUUR

SHAWWAL 1436, IJUMAA JULAI 31-AGOSTI 6, 2015

huanza kabla ya uteuzi wa


mgombea urais.
Alinukuliwa Rais
Kikwete akisema kuwa
Ilani ilitayarishwa chini ya
uongozi wa Mwenyekiti,
Mheshimiwa Benjamin
Mkapa (ambaye naye
alikuwepo kwenye ibada
hiyo), Katibu Mkuu, Philip
Mangula na Mwenyekiti
wa Kamati, Mheshimiwa
Kingunge Ngombale
Mwiru.
Tu n a k u m b u k a k u wa
baada ya kukwama ahadi ya
Mahakam ya Kadhi, Baraza
la Jumuiya na Taasisi za
Kiislam Tanzania, kupitia
vyombo vya habari lilitoa
tamko juu ya Muswada
wa Marekebisho ya Sheria
Mbalimbali Na. 02, wa
mwaka 2014 , hasa kuhusu
marekebisho kwenye sheria
ya tamko la Sheria za
Kiislamu.
Baraza hilo lilieleza kuwa
Waislamu wanafahamu
kuwa kuanzia tarehe 13
hadi 23 Mwezi huu wadau
mbalimbali wataitwa mbele
ya Kamati ya Bunge ya
Sheria na Katiba kwa ajili ya
kuwasilisha mapendekezo
yao, hivyo Jumuiya na Taasisi
za Kiislamu Tanzania wakiwa
sehemu ya wadau muhimu,
wanaona mtiririko wa
mchakato wa marekebisho
ya sheria kwa mujibu wa
muswada huo unaokusudia
kutambua Mahakama za
Kadhi Tanzania bara una
kasoro kubwa.
Kwamba unaonesha wazi
kuwa serikali haina nia ya
kweli ya kuunda Mahakama
ya K adhi yenye hadhi
kamili ya kimahakama na
uthabiti wa kuwepo kwake
na kuwa, muswada huo ni
hadaa nyingine ya serikali
ya CCM kwa Waislamu
kwa sababu malalamiko juu
ya mahitaji ya Mahakama
ya Kadhi yana historia ya
kupindishwa pindishwa
na serikali inayoundwa na
CCM.
Hata mchakato wa Katiba
mpya ulipokuja, asilimia
kubwa ya maoni ya Waislamu
yaliyohitaji Mahakama ya
Kadhi kuingizwa ndani ya
Katiba, mapendekezo hayo
yalikataliwa na Tume ya Jaji
Warioba kwa hoja kuwa
katiba inayotengenezwa ni

ya Muungano na suala la
Mahakama ya Kadhi si la
Muungano, hivyo lisubiri
wakati wa kuandaa Katiba
ya Tanganyika.
Lakini Bunge Maalum la
Katiba likaikataa Katiba ya
Warioba na kutunga Katiba
Mpya Pendekezwa yenye
mambo yote ya Muungano
na yasiyo ya Muungano bila
ya kuingiza Mahakama ya

Kadhi kama ilivyoahidiwa


na Tume ya Jaji Warioba.
Bunge la Katiba
lililokuwa linaundwa na
wajumbe wengi wa CCM
hawakuona umuhimu
wa kutimiza ahadi yao
ya kuweka Mahakama
ya Kadhi katika katiba
pendekezwa. Kwa
makusudi Mahakama
ya K adhi ikakataliwa
na wajumbe wengi wa
CCM walishangilia
jambo hilo hali wanajua
dhahiri kuwa Waislamu
hawakufurahishwa
na uamuzi wao na pia
kukiuka Ilani yao na ahadi
kwa Waislamu.
Hili ni somo tosha kwa
Waislamu kujifunza na
kufanya maamuzi sahihi
kila wanapokuwa katika
uchaguzi Mkuu.
Lakini pia wakati huu,
jamii ya Waislamu imekuwa
ndio waathirika wakubwa
wa sheria ya ugaidi, hata
pale ambao masuala
yenyewe hayahusiani na
uovu wa kigaidi, lakini
yakiwahusisha Muislamu
au Kiongozi wa Kiislamu,
basi ugaidi utaoteshwa.
Leo Masheikh wengi
wa p o r u m a n d e k wa
sababu ya kuadhibiwa kwa
mambo ya kisiasa lakini
yakafanywa kuwa tuhuma
za ugaidi. Hili linawauma
na linawakera Waislamu.
Tabia haina dawa, aliyezoa
kudhulumu, ni vigumu
kuacha dhulma.

Is ita r a jiwe a h a d i ya
kuondoa dhulma ndani
ya mfumo ulioasisi
dhulma kwamba itakuja
kutekelezwa. Uchaguzi
mkuu ujao Waislamu wakae
kitako na kutafakari kwa
kina. Nini hatma yao katika
nchi hii.

14

MAKALA

AN-NUUR

SHAWWAL 1436, IJUMAA JULAI 31-AGOSTI 6, 2015

Matokeo ya mwezi wa Shawal - 2


Na Ben Rijal

Na Ben Rijal

ATIKA makala
ya wiki iliopita
niliweza kuelezea
matokeo mawili ambayo
yalitokea katika mwezi
wa S h awa l wa k a t i wa
Mtume (SAW), nayo ni
tokeo la Banu Kaynukaa
na vita vya Uhud. Katika
muendelezo huo katika wiki
hii nitazungumzia ju ya vita
vya Uhud
Vita hivi vilikuwa katika
mwezi wa Shawal, ilikuwa
mwaka wa tano tokea Mtume
(SAW) kuhamia Madina.
K atika mwezi kama huu
kwenye kalenda ya Kiislamu
kulitokea nusra kubwa kwa
Waislamu juu ya makafiri wa
Kikuraishi wa Makka ,vilitokea
vita vikubwa vilivyoitwa vita
vya Khandaq au kwa jina
jengine vita vya Ahzaab.
Kuitwa kwa vita vya vita
vya khandaq ni kutokana na
kuchimbwa khandaki kubwa
na Waislamu kutokana na fikra
ya Sahaba Suleimna bin Farsy .
M a t o ke o y a k i l a k i t u
hutokea kutokana na sababu
i n ayo s a b a b i s h a k u t o ke a
tokeo na sababu ya vita vya
Uhud ni pale Mayahudi
wa kabila la Bani Nadhiri,
walivyotaka kumkengeuka
Mtume Muhammad (S.A.W)
kwa kumuendea kinyume na
kutaka kumtoa katika mji wa
Madina kwa dhana zao kuwa,
Mtume Muhammad (SAW)
kafika Madina kuwatawala na
kuwawekea sheria kali.
Kutokana na hayo likatoka
kundi la Bani Nadhiri,
walikwenda Makka kwa
Makuraishi na baadhi ya
makabila mengine ya Kiarabu
yakiwemo makabila ya Atfaan,
Bani Fuzara na Murrah kwa
kuwataka msaada wa kumpiga
vita Mtume (SAW) kwa
kuwaeleza yafuatayo, Sisi
tuko pamoja na nyie kwa
kumtoa Muhammad, na dini
yenu ni bora kuliko dini ya
Muhammad. Mayahudi ni
watu wa mbinu na siku zote
huwa na hila na kuhakikisha
kuwa utulivu unakosekana.
Zilipomfika habari hizo
Mtume (SAW) za Mayahudi
na makafiri wa Makka kuwa

tayari washaondoka Makka


kuwakabili Waislamu, akawaita
Masahaba zake na kuwapa
habari ya Makuraishi juu ya
njama na hujuma walioipanga
na kuwataka fikra Masahaba
juu ya ya kukabiliana na shari
hiyo, iliyopangwa na Mayahudi
wakishirikiana na Makureishi.
Masahaba waliemewa na
kuona kizungumkuti kutojua
lakufanya, hapo akachomoza
Sahaba mmoja ambaye tarehe
ya Kiislamu haitomsahau kwa
mchango wake mkubwa katika
kufaulu Waislamu katika vita
hivi. Alikuwa Sahaba Salmaan
Al-Farisy, pale alipotoa fikra ya
kuchimbwa khandaki ambalo
huko kwa kwenye maeneo ya
Farsy, ilikuwa ndio mbinu kuu
ya kivita. Kwa kutoa fikra hii
Waislamu wakashangaa kwa
kuwa kitu hicho kilikuwa ni
kigeni nao. Aidha hata neno
khandak lilikuwa halitumiki.
Fikra hiyo iliungwa mkono
na Mtume Muhamd (SAW)
na Masahaba wote kwa jumla,
baada ya hapo wakatoka
Waislamu nje kidog o ya
mji wa Madina na kufunga
kambi baina majabali mawili,
hapo ndipo palipochimbwa
mahandaki baina ya majabali
mawili. Wakati kazi inaendelea
ya uchimbaji handaki,
alijitokeza Sahaba mmoja na
kumtaka Mtume (SAW) yeye
na watu wake wawili au watatu
kwenda kupata chakula kidogo
kilichoandaliwa na mkewe.
Mtume (SAW) baada ya
kupewa mualiko huo akanadi
kwa umma wote uliokuwepo
pale kuwa, fulani anakualikeni
chakula kwake.
Kwa furaha likatoka jeshi
zima mpaka kwa yule Sahaba na
ilikuwa idadi ya jeshi linakaribia
wapiganaji alfu tatu, hapo
Bwana Mtume alitoa sharti
kuwa chungu kilichopikiwa
kisiepuliwe jikoni na wala
isichomwe mikate mpaka
Mtume afike. Alipofika Mtume
Muhammad (SAW) akaingia
moja kwa moja mpaka jikoni
na kuanza kukata mikate na
kuwagaiya jeshi lake, chakula
hicho kidogo kiliweza kuliwa
na jeshi lote la wapiganaji alfu
tatu na kubakia.
Ama ndani ya Madina
mambo yalishtadi na Mayahudi
wa Banii Nadhiri hawakusita
kutafuta msaada nje ya
Madina, bali wakawasiliana
na Mayahudi wenzi wao
kuwataka kuvunja mkataba na
Mtume Muhammad (SAW)
walioutia katika masuala ya
kivita wakati alipofika Mtume
(SAW) katika mji wa Madina.
Aidha likatoka kundi ndani
ya Waarabu wa Madina kwa
kujiengua na ndugu zao kwa

kutakaka nusra ya Allah kwa


kurudi majumbani mwao,
nao Mayahudi wakishikilia
msimamo wa mapambano.
Zilipomfika habari za
kuvunjwa ahadi na kujitenga
kwa wanafiki wa Madina,
Mtume Muhammad (SAW)
akamtuma Sahaba Saad Ibn
Muaadh, kwenda kuhakikisha
habari hizo na matokeo yake.
Alipopata uhakika wake,
Mtume (SAW) alitoa tamko
la Allah Akbar nakubashirieni
mambo ya kheri enyi
Waislamu.
Inafahamika kuwa habari
zilivowafikia Waislamu kuwa
munafikina wa Madina
wamer udi majumbani na
Mayahudi wamevunja ahadi,
hapo Waislamu wakahisi
kuwa wameelemewa kwa
kila upande, kinyume na
walivotaraji kuwa adui atakuwa
mbele yao na baina yao kuna
hilo khandaki, lakini sasa adui
kawazunguka kila upande huku
munafikina wakizidi kuwatia
sumu waumini kwa kuwambia
Muhammad alikuwa akiahidi
kuwa watakula katika hazina
za wafalme wa Fursy na Masri,
lakini sasa imefikia hadi mtu
hajiaminishi kwenda kufanya
haja nje ya Madina.
Zilipomfika habari hizi
Mtume Muhammad (SAW)
na kuona kuwa balaa lishakuwa
kubwa na fitna zinaongezeka,
aliwaita baadhi ya Masahaba
kutaka ushauri akiwemo Saad
bin Muaadh na Saad bin
Ubaada kwenda kufanya sulhu
na kabila la Ghatfaan kuwa
wajitoe katika vita na wakifanya
hivyo na kurudi, watawapa robo
tatu ya mitende ya Madina.
Saad bin Muaadh na Saad
bin Ubaada wakamwambia
Mtume Muhammad (SAW)
kwa kusema Ewe mjumbe
wa Allah, je hizi ni fikra zako
tu ambazo umezipendekeza
au ni amri kutoka kwa Allah
au unatuonea huruma sisi
Waislamu? Akasema mjumbe
wa Allah, huruma juu yenu
ili kuvunja nguvu za maadui
zenu, akala kiapo Saad bin
Muadh kwa kuapa Naapa
kwa jina la Allah hatuna haja
ya suluhu kwa kuwapa mali
zetu, bali hatutowapa chochote
isipokuwa upanga mpaka Allah
atuhukumie baina yetu juu ya
hili. Akafurahi Mtume (SAW)
kwa kusikia msimamo wa
Masahaba.
Kwa upande wao
Mushrikina wa Makka
walipofika Madina wakalikuta
khandaki limechimbwa
walishangazwa na kupigwa
b u t w a a k w a n i Wa a r a b u
hawakuwa na ada kuchimba
mahandaki katika vita mpaka

Mchoro wa sehemu ya mapambano ya Khandak


baadhi yao wakasema hivi
ni vitimbi vya Wafursy na sio
watu wa Madina. Hapo tena
Makafiri wakabaki kulizunguka
khandaki na kujaribu kilipenya
kwa kuliruka na miongoni
mwa waliojaribu kufanya hivyo
na kuweza kuliruka ni kafiri
mmoja wa Makka, Amru
bin Wudi, ambaye aliuawa
katika mikono ya Sayidna Ali

bin Abi Talib (RA). Makafiri


walijizatiti kutaka kulivuka
khandaki na hakulivuka yoyote
yule ila aliuawa. Kutokana na
kushindwa kulivuka khandaki,
baadhi ya Makuraishi na
Makafiri wakaweka kambi nje
kidogo ya eneo la khandaki
kwa siku kumi takriban kwa
ajili ya kuwadhikisha kwa
Inaendelea Uk. 16

MAJIBU YA CHEMSHA BONGO NAMBA: 16


F

114

260

103

Masuala:
1.Wataje wanawake 4 ambao watakuwa ni wanawake wa Peponi
waliojulikana wakiwa bado wahai. Jawabu: Maryam, Asya, Khadija,
Fatma
2.Majina mengine ya Quran. Jawabu: Furqan, Kitaab, Noor, Huda
3.Sura ngapi katika Quran. Jawabu: 114
4.Mtume yupi katajwa sana katika Quran? Jawabu: Mussa
5.Sahaba yupi aliomshauri Khalifa Syd Abubakar aikusanye Quran,
iwe katika kitabu kimoja? Jawabu: Umar
6.Sahaba yupi alikusanya Quraan katika mfumo huu tuliokuwa nao
Sasa? Jawabu: Uthman
7.Ukifunga mwezi wa Ramadhani na ukafwatisha siku sita za Shawal
utakuwa sawa umefunga? Jawabu: Mwaka.
8.Msikiti ulikokuwa mkongwe kuliko yote. Jawabu: Alqaaba
9.Ameangamia pamoja na mikono yake miwili, ni nani huyo? Jawabu:
Abulahab
10. Tafsiri zinazojulikana za Quran kwa lugha kutoka Kiarabu
kwenda lugha mbalimbali ni ngapi? 103, 250, 1,000 Jawabu: 103

Fatilia kuandama kwa Mwezi

Leo Ijumaa ni tarehe 15 Shawal 1436 AH,


sawa na tarehe 31 Julai 2015.
Mwezi unategemewa kuandama kwa
Mfungo Pili tarehe 16 August. Kutokea leo
hadi kufikia Mfungo Pili tumebakisha siku 15.

15

MAKALA

SHAWWAL 1436, IJUMAA JULAI 31-AGOSTI 6, 2015

Mawingu na faida zake


M
Na Ben Rijal

AKALA ya
wiki iliopita
ilielezea juu
ya mawingu katika
kitabu kitukufu cha
Quran na makala ya
wiki hii yatamurika
mawingu na faida
zake.
Tu n a p o a n g a l i a
angani huona mawingu,
lakini mawingu
huwa yanatembea na
kusogea na kutoweka
saa nyengine mawingu
huja kwa maumbile
tafauti, nikujuliza
haya mawingu ni kitu
gani? Akiniuliza mtoto
wa skuli ya msingi
nitamwambia kama
ifwatavyo, Mawingu ni
mkusanyiko wa matone
ya maji yaliojikusanya
juu ya anga, mawingu
hufanyika pale maji
yanapoyayuka ardhini
na kuwa mvuke na
kwenda ang ani na
kukamuliwa na
kupozwa kisha ndio
huona mawingu.
Kuna tabaka ya anga
yetu ijulikanayo:
troposphere ikiwa
sehemu ya chini ya
mawingu na kuna
tabaka nyengine
mbili zijulikanazo
kama stratosphere
au mesosphere. Haya
mawingu tunayaona
hubeba tani milioni
za matone ya maji,
huyaona mawingu
kuwa ni meupe
kutokana na jua kupika
na mwanga unaporudi
huyafanya tuyaone
mawingu kuwa ni
meupe.
Stratus, Cumulus
na Cirus ni aina ya
mawingu na maumbo
yake, Stratus huwa
na umbo la bapa na

huwa kama busati


hivi, Cumulus huwa na
umbo kama la pamba
na huwa yanatembea
na Cirus yapo kwa
umbo jembamba na
mara huparaganyika,
mawingu hujitengeneza
kwa kipindi cha
dakika hadi saa na
ndio mara utayaona
sehemu fulani na mara
hutoweka. Kemikali
nazo huchangia
kutengenezwa kwa
mawingu mfano sayari
ya Venus imejengeka
n a s u l f u r- d i ox i d e
wakati sayari ya Jupiter
na Saturn zikiwa na
Ammonia.
Kutoakana na
masafa kutoka
ardhini kwenye
masafa ya feet 18,000
hupatikana Cirrus
kwenye masafa baina
ya feet 6,500 mapka
18,000 hupatikana
yale yaitwayo Alto
katika masafa ya chini
kabisa ya feet 6,500
hupatikana aina ya
mawingu yajulikanayo
Stratus. Mawingu
yanayojengeka wima
huitwa Cumulus yale
ya aina yake huitwa
Mammatus, Lenticular,
na Contrails.
Kuna faida yoyote
ile kukuweko kwa
mawingu? Mawingu
ni muhimu kwa maisha
yetu kwasababu
mbalimbali kwanza
hujalia kufanya kivuli
kutokana na mianga
ya jua, huweka na
kubakisha maji ya
duniani, ing ekuwa
hakuna mawingu maji
yangebakia duniani na
kuwa sehemu yote ya
dunia imezungukwa
na maji, ilipokuwa
mawingu hunyonyoa
joto basi mawingu

Mawingu yakione kana meupe

husaidia kuifanya
sayari yetu hii ya dunia
kupozwa na kuweza
kukalika.
Maisha ya viumbe
hutegemea maji na maji
ndio maisha na pale
maji yatapomalizika
duniani ni kusema
uhai utasita kukuweko,
mvua zinaponyesha
kwa kukuza kilimo ni
kutokana kwa kuweko
kwa mawingu na ile
duru itwayo duru ya
maji kufanyika mvua
inategemea zaidi
mawingu.
Mvua inavyokuwa
Mzunguko wa maji
katika dunia ni safari
ambayo hatuihisi lakini
ni safari muhimu sana
katika maisha yetu
ya kila siku. Dunia
yetu imezungukwa na
bahari, mito, maziwa,
chemchemu n.k.
Kwahio safari huanzia
duniani yaani nchi kavu
nakuelekea mawinguni
mvua zinaponyesha
kisha maji yakarudi
ardhini, baadhi yakawa

AN-NUUR

kwenye bahari, baadhi


yakenda chini ya ardhi
nakubaki huko na
mengine husukumwa
na kurudi baharini na
kuwa ya sehemu ya
chumvi.
Safari hii huanza
na kuchangiwa na
jua, kukuweko kwa
jua ndio maisha yetu
y a n a p owe z a k u wa
endelevu, jua hutoa
joto na joto hili
huyachemsha maji
yaliomo baharini na
maeneo mengine
kisha yakapanada
hewani ikiwa matone
madogo ya mvuke,
matone haya hubanwa
na kukamuliwa
yanapokuwa kwenye
m aw i n g u , m b i n yo
huo na mkamulio
huo hujaalia tena maji
kuteremka ardhini
kama ni mvua, kisha
yakabakia na kurudi
kwa njia hio hio
niliokwisha kuieleza,
lau inegekuwa safari
hii haipo maisha
yangekuwa hayapo na
kama yangeanza basi
yangedumu kwa muda
mfupi kabisa.
Mawingu ni sehemu
kubwa ya maisha
kama nilivyokwisha
kuieleza na namna
yanavyochangia
maisha yetu. Makala
itakayofwata
yatakwenda ndani
zaidi juu ya faida za
mawingu, InshaAllah.

UWANJA WA VIJANA - JIONGEZEE MAARIFA

CHEMSHA BONGO NAMBA: 17


Weka duara kwenye jawabulio sawa. Jawabu
kamili wiki ijayo.
Y
A
T
H
R
I
B
14
15
Z

D
N
I
K
A
H
I
70
A

A
Y
U
S
U
F
F
S
25
K

M
E
T
I
C
A
L
R
Z
K

A
M
P
R
I
H
R
A
A
A

S
A
A
E
N
O
E
M
T

C
L
P
D
D
L
C
L
B
A

U
A
U
S
I
A
H
P
I
N

S
W
A
E
A
N
I
P
A
Z

Y
I
G
A
N
D
N
O
T
A

K
B
I
A
L
M
A
K
U
N

P
A
C
I
F
I
C
U
G
C

1. Jina jengine la mji wa Madina


2. Idadi ya Waislamu waliouawa kwenye vita vya
Badr?
3. Zakka, Nikah, Shahada, Sawm, ipi iliyokuwa sio
katika nguzo za Kiislamu?
4. Uongozi wa Bani Ummaya waliweka makao
makuu wapi?
5. Mtume aliyetafsiri ndoto ya Mfalme Misri?
6. Bendera ya nchi gani yenye nyota ya Daud? (Star
of the David)
7. Inakadiriwa Tembo huishi umri wa maiaka 60,
70, 25.
8. Pesa ya Msumbiji inajulikana kwa jina la .
Peso, Metical, Shilling.
9. Nchi gani ikijulikana kama ni Nyasaland?
Zambia, Malawi, Zimbabwe, Namibia.
10. Bahari ipi inaigawa baina ya Saudi Arabia na
Misri?

Jee Unajua?

1. Liberia ilikuwa huru 26 Julai 1847. http://


africanhistor y.about.com/librar y/timelines/
blIndependenceTime.htm
2. Mataifa ya Liberia na Ethopia hayajapata
kutawaliwa http://africanhistory.about.com/od/
eracolonialism/tp/AfricaNotColon.htm
3. Mji mkuu wa Algeria unaitwa Algiers,
Tunisia, Tunis? http://africanhistory.about.com/
od/eraindependence/fl/Alphabetical-List-of-AllAfrican-Countries.htm?utm_source=exp_nl&utm_
medium=email&utm_term=list_africanhistory&utm_
campaign=list_africanhistory&utm_content=20150726
4. Mabibi wanne Wakiafrika waliojijengea
umaarufu wao wenyewe, akiwemo Ngozi OkonjoIweala? http://africanhistory.about.com/od/biography/
ss/Four-African-Women-who-are-Changing-the-Worldin-2015.htm
5. Wa-Africa maarufu, Kenyatta, Sir Seretse
Khama, Nyerere: http://africanhistory.about.com/od/
biography/
6. Hisne Habre aliyeitawala nchi ya Chad kwa
mkono wa chuma alifikia kupata shahada ya Phd. http://
africanhistory.about.com/od/chad/fl/HissegraveneH a b r e a c u t e. h t m ? u t m _ s o u r c e = e x p _ n l & u t m _
medium=email&utm_term=list_africanhistory&utm_
campaign=list_africanhistory&utm_content=20150726
7.
Tafiti ni ufunguo wa maendeleo, tabaka za
utafiti katika elimu za jamii. http://sociology.about.com/
od/Research/
8.
Siasa za kibaguzi zilimgeuza Malcolm X alivyo
kwenda Kuhijji Makka. http://middleeast.about.com/
od/religionsectarianism/a/me080220b.htm
9. Hotuba ya Martin Luthr King, I have
Dream? maneno yake. http://grammar.about.com/
od/classicessays/a/dreamspeech.htm
10. Malcolm X alitoa hotuba Message to the
grassroots akiwa maneno yanamtoka pasi kuangalia
mahali, hutuba hiyo ikatoa mwamko mkubwa kwa
Wamerekani weusi: https://www.youtube.com/
watch?v=Ku2JzolPt50 /

16

AN-NUUR

MAKALA

Inatoka Uk. 14
njaa Waislamu, mbinu hiyo
haikufaulu na wala hakujatokea
vita, Allah akapitisha nusra
yake kuyatawanya makundi
hayo kwa njia mbili kuu, njia
ya kwanza kwa kumtumia
mtu mmoja ambaye alisilimu
kipindi si kirefu, naye ni
Naaim bin Masoud na kuanza
kuwagongesha makafiri na
Mayahudi kwa kutoka mpaka
kwa Mayahudi wa kabila la
Banii Kuraidha, hali ya kuwa
wanadhani kuwa bado Naaim
bin Masoud hajasilimu kwa
kuwambia msikubali kushiriki
katika vita na Makuraish
mpaka wakupeni rehani ya
watu wao, tena katika viongozi
ili wasiweze kuondoka mpaka
mkubaliane, pindi hamkufanya
hivyo, watakuwacheni peke
y e nu m k awa h a m n a wa
kukunusuruni Madina.
Mayahudi wakawafik fikra
yake hiyo, akatoka tena Sahaba
Naaim bin Masoud mpaka
kwa Makuraishi wakiwa pia
wana dhana kuwa bado yupo
katika ukafiri nao, akawapa
ushauri kwa kuwambia kuwa
Bani Nadhiri wanajilaumu
kwa walioyoyafanya

SHAWWAL 1436, IJUMAA JULAI 31-AGOSTI 6, 2015

Matokeo ya mwezi wa Shawal - 2

kwa Muahammad na
wamekubaliana kuwa waje
wachukuwe watukufu
miongoni mwenu na
wawasalimishe kwa
Muhammad, ili awauwe na
watakuja tu Mayahudi kutaka
hilo na ole wenu mkiwapa watu
wenu.
Baada ya kumwaga
propaganda hiyo kali, kisha
akatoka mpaka katika kabila
la Atfaan, akawambia kama
alivyowambia Makurashi, hapo
ndipo kila mmoja alipotoa
uaminifu juu ya mweziwe na
wakaamini waliyoambiwa na
Naaim bin Masoud na hikma
na propaganda ya Sahaba
ikiwafan ya kug awa n yika
kutokana na hikma kubwa
iliyotumiwa na Sahaba Naaim
bin Masoud.
Ama njia ya pili ni pale
Allah alipowaletea upepo mkali
wenye kutisha katika usiku wa
giza lenye baridi ndani yake,
kila mmja hamjuwi alokuwepo
pembeni yake kutokana na

tokeo hilo, wakaamua viongozi


wa Makafiri na Mayahudi
kuwatangazia watu kuondoka
na Abuu Sufian kabla ya
kusilimu ndio alikuwa mstari
wa m b e l e k u wa t a n g a z i a
kuondoka na kurudi walikotoka
na kulipopambazuka
siku ya pili, makafiri wote
walikwisha ondoka na hapo

tena pakapatikana nusra kwa


Waislamu juu ya makafiri.
Tokeo hili lilitokea kwenye
mwezi wa Shawal kama
nilivyotangulia kueleza na
funzo kubwa linalopatikana ni
kuwa, mkubwa achukue fikra
za wadogo na ndivyo Mtume
Muhammad (SAW) alivyofanya

wenye misimamo mikali


nchini Marekani.
Waziri Mkuu wa Israel,
Benjamin Netanyahu na
kundi la Mashinikizo la
Mayahudi nchini Marekani
IPAC, kwa muda mrefu kabla
ya kufikiwa makubaliano
ya nyuklia kati ya Iran na
kundi la 5+1, walikuwa

tayari wameshachukua
uamuzi kwamba njia yoyote
ya kidiplomasia kuhusu
miradi ya nyuklia ya Iran
zinapaswa kufungwa.
Kundi hilo la wanasiasa
b a d o l i n a a m i n i k u wa ,
linaweza kuilazimisha Iran
kulegeza misimamo yake
kwa kuzidisha mashinikizo

ya kiuchumi.
Hata hivyo katika kipindi
cha miaka 10 iliyopita ya
vikwazo vikubwa dhidi
ya Iran, uwezo wake wa
nyuklia ulipanda kiasi cha
kuweza kuzalisha nishati
iliyorutubishwa kwa asilimia
20 kwa ajili ya kuzalisha
nishati ya kituo cha utafiti

Mchoro unaonyesha khandak lilipokuweko na Waislamu na Makafiri


na funzo jengine linalopatikana
ni kule Waislamu kuwa kitu
kimoja na katika spirit hiyo,
sio tu Waislamu walishinda
katika vita vya Khandak, bali
walipata mafanikio makubwa
katika nyakati mbalimbali,
pale Waislamu walipoiondosha
spirit hiyo ndio wamefika

Nyuklia ya Iran yazua vita Marekani

Inatoka Uk. 20

katika mazingira hayo vita


litakuwa chaguo lisiloweza
kuepukwa.
Pa m o j a n a h ayo,
inaonekana kuwa hoja za
Mawaziri hao watatu wa
serikali ya Barack Obama,
hazitaweza kubadili
mtazamo wa wanasiasa

KINGDOM OF SAUDI ARABIA


COMMITTEE OF DA-AWAH IN AFRICA
MAJINA YA WASHINDI WA MASHINDANO YA FAMILIA YA MTUME (S.A.W.) NA MA SWAHABA 1436H/2015M.

Yafuatayo ni majina ya washindi wa mashindano ya Familia ya Mtume na Swahaba yaliyo fanyika kati ya mwezi wa tano na
wasita 2015.:( TANZANIA BARA NA VISIWANI)
N
a.

JINA LA MSHINDI

ZAWADI ALIYOPATA

ALI USSI ALI

SAFARI YA HIJA

HAJI DAUD SULEIMAN

Na.

JINA LA MSHINDI

MUSA RISASI RAJABU

SAFARI YA HIJA

SAFARI YA HIJA

11
12

ATHUMANI RAMADHANI KONDO

SAFARI YA HIJA

JUMA HATIBU THANI

)KOMPYUTA (LAPTOP)

13

AMINA IDRISA KUDEFA

)KOMPYUTA (LAPTOP)

KAZIJA ALLY SHEHA

)KOMPYUTA (LAPTOP)

14

RASHIDI A. KIBIRITI

)KOMPYUTA (LAPTOP)

KAZIJA HAJI AMIRI

KIFAA CHA KUFUNDISHIA QUR'ANI

15

LATIFA SEBASTIAN

KIFAA CHA KUFUNDISHIA QUR'ANI

ASHURA HAMADI ALLY

KIFAA CHA KUFUNDISHIA QUR'ANI

16

UMMU KULTHUM ALLY

KIFAA CHA KUFUNDISHIA QUR'ANI

AISHA HAJI ALLY

KIFAA CHA KUFUNDISHIA QUR'ANI

17

SHAKILAABDULMALIK MOHAMED

KIFAA CHA KUFUNDISHIA QUR'ANI

BATIIMA HAJI AMIRI

SIMU YA MKONONI

18

ATHUMANI AMOUR ALLY

SIMU YA MKONONI

AISHA MUNSAB HAJI

SIMU YA MKONONI

19

JUMANNE ZUBERI SABUNI

SIMU YA MKONONI

1
0

AMINA ABDALLAH HAJI

SIMU YA MKONONI

20

MWANAHAMISI KHATIBU
MKOMBOLAGUHA

SIMU YA MKONONI

WASHINDI WATAFAHAMISHWA KUPITIA NAMBA ZAO ZA SIMU NAMNA WATAKAVYO KABIDHIWA ZAWADI ZAO.
1

cha Tehran.
Hivi sasa baada ya juhudi
za miaka 35 na mazungumzo
ya miaka miwili kuhusu
kadhia ya nyuklia ya Iran,
serikali ya Marekani imekiri
kuwa vikwazo na vitisho vya
kijeshi dhidi ya nchi hiyo
havikuwa na faida yoyote.
Hata hivyo inaonekana
kuwa, wanachama wengi wa
Congress ya Marekani ama
hawajaelewa uhakika huo
au kutokana na kuathiriwa
na mashindano ya kisiasa
baina ya vyama hasimu na
mifungamano yao na lobi za
Wazayuni, wanataka kukariri
njia ile ile iliyoshindwa. Hii
ni pamoja na kuwa kukataa
makubaliano yaliyoungwa
mkono na wanachama
watano wa kudumu wa
Baraza la Usalama la Umoja
wa Mataifa, nchi 28 za Umoja
wa Ulaya na nchi karibu zote
za dunia hakutakuwa na tija
nyingine zaidi ya kuifanya
Marekani itengwe katika uga
wa kimataifa.
Hii ni pamoja na kuwa,
ukiukaji wowote wa
Marekani azimio nambari
2231 la Baraza la Usalama
lililoidhinisha makubaliano
hayo ya nyuklia, utaizuia nchi
hiyo kuiweka tena vikwazo
Jamhuri ya Kiislamu.

17

MAKALA

AN-NUUR

SHAWWAL 1436, IJUMAA JULAI 31-AGOSTI 6, 2015

Waislamu chukueni tahadhari


juu ya madai ya Quran ya kale
Asema Balozi Shareef Abdulkadeer
Inayotambulika ni iliyopo Istanbul

BALOZI Dk. Shareef


Abdulkadeer.

A I B U Wa z i r i
wa zamani wa
Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Kimataifa
nchini, Balozi Dk. Shareef
A b d u l k a d e e r, a m e t o a
thadhari kwa Waislamu
kufuatia kuripotiwa habari
ya kugundulika sehemu
ya nakala ya Quran
inayoelezwa kuwa inaweza
kuwa ndiyo ya kale zaidi
huko Uingereza.
Dk. Abdulkadeer aliandika
katika ukurasa wake wa
face book kuwa, pamoja na
kutolewa habari za ugunduzi
huo na kusambaa katika
mitandao ya kijamii na vyombo
vya habari sehemu mbalimbali
duniani, kwamba yawezekana
kipande hicho cha kale ndio
Qurna ya kale zaidi duniani,
bado kuna haja ya Waislamu
kuipokea habari hiyo kwa
tahadhari.
Alisema kugundulika
kwa Quran hiyo ya kale,
inawezekana kuna matayarisho
ya kugunduliwa vipande
vingine kutoka katika
makusanyo makubwa ya
maandiko (collection) yaliyopo
katika hazina ya Chuo Kikuu
cha Birmingham Uingereza.
Akitoa ufafanuzi, Dk.
Abdulkadeer alisema nakala
ya Quran, tena kamilifu na
ambayo ndiyo ya kale kabisa
duniani ni nakala iliyopo
nchini Uturuki, ambayo ni
Msahafu kamili uliokusanywa
na Sayydna Othman bin
Affan, aliokuwa akiusoma
nyumbani kwake hadi pale
alipouliwa ndani ya nyumba
hiyo akiwa anasoma Msahafu
huo na matone ya damu yake
bado yapo kwenye kurasa za
Msahafu huo.
Alisema kuwa Sayydna
Othman aliposhika ukhalifa
miaka sabab baada ya kifo cha
Mtume Muhammad (saw) na
kukuta watu wanajiandikia au
kuandikwa sehemu mbalimbali
za Quran kwa ajili ya matumizi

binafsi, huku wengine wakiwa


wanaandika sura moja moja
ambazo haziendani na
mpangilio waliourithi kutoka
k wa M t u m e ( s aw ) wa l a
Msahafu kamili, ulioandikwa
wakati wa Mtume mweyewe,
aliona ipo haja ya kutayarisha
Msahafu kwa hati na maandishi
mamoja na mpangilio wa sura
kama ilivyo katika Msahafu
waliourithi kutoka kwa Mtume
(saw).
Hivyo Sayydna Othman
(ra) aliitisha jopo la Hufadh
al Quran na yeye mwenyewe
akiwa mmoja wao na
Maswahaba wengine wakubwa
wakubwa na kutayarisha
Msahafu wa Mtume.
Baada ya kukamilishwa
nakala hiyo, kukatolewa nakala
saba ambazo sita zilipelekwa
kwenye miji mikuu ya Uislamu
wakati huo, ili watu wanakili
kutoka kwenye nalaka hiyo
rasmi peke yake na nakala
zote za zamani zilikusanywa
na kuchomwa moto.
Alisema zoezi hilo lilifanyika
na ndio maana hii leo kuna
Msahafu mmoja tu ambao
ni nakala ya kutoka Msahafu
Othman ambao nakala yake
halisi ipo Uturuki na kwamba,
ina ya visomo vyote saba
vinasomwa kutoka Msahafu
Othman.
Mimi najikita katika hilo
tangazo lililotolewa na kudaiwa
kuwa maandishi hayo ndiyo
ya kale kabisa ya Quran

kuwepo duniani. Maelezo


yangu mafupi na tahadhari
ninayoitoa ni hayo. Alieleza
Balozi Abdulkadeer katika
mtandao wa ahbaabur Rasuul.
Alifafanua zaidi kwamba
kama kuna tofauti yeyote
ni kuhusiana na ishara
zinazowekwa juu ya neno
fulani ndani ya Msahafu huo,
kuonyesha litamkwe vipi
kulingana na qiraa mojawapo
kati ya qiraatal al sab Bas.
Kwa msingi huo, Balozi
Shareef Abdulkadeer
anasema kuwa hicho kipande
ch a m s wa d a wa Q u r a n
kinachoelezwa kuwa ndicho
cha kale kabisa duiniani siyo
kweli.
Kama nilivyosema,
Msahafu wa Sayydna Uthman
umeandikwa miaka saba
baada ya kufa kwa Mtume
Muhammad (saw), yaani
mwaka wa 17 katika kalenda
ya Hijriya.
V i p i m o v i n av yo d a i wa
vya carbon kuhusu hicho
kipande kinachodaiwa kuwa
ndicho cha kale kabisa na
kuwa yawezekana kabisa
kimeandikwa na Swahaba,
inadaiwa kuwa umri wake ni
miaka 1370. Yaani imeandikwa
mwaka wa 30 AH. Ikiwa ni
hivyo basi, hakiwezi kuwa
ndiyo maandishi ya kale kabisa
ya Quran. alibainisha
Alisema yeye kama

Muislamu, hana budi kupokea


taarifa hizo kwa tahadhari, na
siyo kukurupuka na kukubali
anayoambiwa.
Alisisitiza kuwa Mwenyezi
Mungu amewaamrisha
Waislamu kuwa wakiletewa
habari na fasiki (asiye na imani
au mwenye mashaka na imani
yake), basi kwanza waifanyie
uchunguzi kuhakikisha
ukweli wa habari hiyo, ili
wasije wakajuta wenyewe kwa
kujichukulia maamuzi ambayo
hayana mashiko,. (a-Hujurat).
Wiki iliyopita, vyombo
vya habari nchini Uingereza,
ikiwemo BBC, vitang aza
habari ya kugunguliwa nakala
ya maandiko ya Qur'ani katika
Chuo Kikuu cha Birmingham,
Uingereza na kuelezwa kuwa
inawezekana ikawa ni miongoni
mwa nakala za zamani zaidi za
Quran Tukufu duniani.
Gazeti la Times la
Uingereza liliripoti kuwa,
uchunguzi uliofanyika katika
ngozi ambayo Qur'ani hiyo
imeandikwa, umethibitisha
kuwa mnyama wa ngozi hiyo
alikuwa akiishi katika zama za
Mtume Muhammad (saw) au
muda mfupi baadaye.
Prof David Thomas wa
Chuo Kikuu cha Birmingham
nchini Uingereza, ambaye
ni mtaalamu wa Uislamu
na Ukristo alisema kuwa
matokeo ya uchunguzi huo
yanashangaza na kwamba,

nakala hiyo ya Qur'ani ya kale


inafanana na Qur'ani iliyopo
hivi sasa.
Prof. T homas alisema
uchunguzi wa Chuo Kikuu
cha Oxford umebaini kuwa,
kuna uwezekano wa asilimia 95
kwamba nakala hiyo iliandikwa
baina ya mwaka 568 hadi
645 Miladia na kwa msingi
huo, mtu aliyeiandika alikuwa
akiishi katika zama za Mtume
Muhammad (saw).
Imeelezwa kuwa vipimo
v y a k u t a m b u a u m r i wa
vitu mbalimbali vya kale
Radiocarbon dating
vimeonyesha kuwa umri
wa Msahafu huo ni miaka
i s i yo p u n g u a 1 , 3 7 0 , h a l i
inayoyakinisha watafiti hao
kuwa Msahafu huo unaweza
kuwa miongoni mwa Misahafu
kongwe kuwepo duniani katika
asili yake.
Msahafu huo ambao
umehifadhiwa katika
maktaba ya Chuo Kikuu cha
Birmingham kwa karne moja
tangu kama moja ya miswada
ya ukusanyaji wa vitabu na
nyaraka kutoka Mashariki
ya Kati, umekuwepo katika
maktaba hiyo kwa miaka mingi
bila yeyote kufahamu thamani
yake wala kujishughulisha nao.
Msahafu huo uligunduliwa
kuwa mkongwe baada ya
mtafiti wa shahada ya uzamifu
(PhD), Bw. Alba Fedeli,
alipoamua kufanya uchunguzi
wa karibu zaidi katika kurasa
zake na kuzifanyia vipimo kwa
kutumia mionzi yenye kujua au
kukisia asili na umri wa viumbe
mbalimbali (Radiocarbon
Dating) na matokeo yalikuwa
ni ya kushangaza sana.
Mkurugenzi wa Chuo hicho
kuhusu makusanyo ya vitu
maalum, Susan Worrall, alisema
watafiti hao hawakutarajia wala
kuota kuwa Msahafu huo
utakuwa ni wenye umri huo na
kwamba, ni bahati kwao kuwa
na nakala ya asili ya Msahafu
ambao unasadikiwa uliandikwa
kipindi cha Makhalifa.
Imedokezwa kuwa nakala
hiyo ya kale ya Qur'ani ni
miongoni mwa maelfu ya
nyaraka nyingine za kale kutoka
Mashariki ya Kati, ambazo
zilimilikiwa na mwana historia
mzawa wa Iraq, Alphonse
Mingana, aliyekabidhi kwa
C h u o K i k u u h i ch o ch a
Birmingham mwaka 1920.
Habari zinasema kwamba
Qur'ani hiyo ambayo
imeandikwa kwa maandishi
ya Hijazi itaonyeshwa kwa
umma mwezi Oktoba mwaka
huu katika Chuo Kikuu cha
Birmingham.

18
Na Mwinijisti Kamara
Kusupa

WALI ya yote
namshukuru
M h a r i r i
aliyenipa tena fursa
ya kuwasiliana na
wa s o m a j i wa A n n
u u r, n i k i r i u k we l i
wa moyoni kwamba
huko nyuma magazeti
mawili ya Kiislamu
Nasaha na An uur
yalikubali kuchapisha
mada zangu licha ya
kunielewa fika kwamba
mimi ni Mkristo tena
mwinjilisti, nami
sikuona kikwazo
chochote katika
kushirikiana na
Waislamu.
Hata baada ya mimi
kukutwa na zahama ya
kufungwa, mag azeti
hayo mawili yalinisaidia
kwa namna ya kipekee
ambayo hata ndugu
z a n g u wa d a mu n a
ndugu zangu katika imani
(Wakristo wenzangu)
hawakunisaidia kama
walivyonisaidia waandishi
wa Nasaha na Ann uur.
Nimeyaeleza kwa kirefu
ndani ya kitabu changu
cha MAISHA YANGU
GEREZANI SIMULIZI
LA SIKU 1888 ZA
MATESO.
Baada ya kutoka
gerezani kama ilivyo
ada kwa yeyote
anayetoka kifung oni
huwa mgeni ndani ya
nchi yake. Mawasiliano
na waliokuwa karibu
hupotea, hata hivyo
niliendelea kununua
na kusoma An nuur na
A LH U DA kwa kuwa
NASAHA sikuiona tena
mitaani wala sikujua
nimuulize nani.
Kuna jambo la pili
lililoongeza ufa kati
y a n g u n a Wa i s l a mu
waliokuwa karibu nami
hapo awali, baada ya
kumaliza kifungo nilikuta
wanaendesha harakati
tofauti za kuutokomeza
Mfumo Kristo ambao
siuelewi na kwa hiyo
sikuwaelewa. Nikiwa
mwenye kuikubali imani
ya Kikristo, singeweza
kujumuika nao na kukiri
kwa kinywa changu
kwamba Mfumo
Kristo utokomezwe.
Zamani tulipokuwa
karibu tuliimba wimbo
mmoja wa haki sawa

MAKALA

AN-NUUR

SHAWWAL 1436, IJUMAA JULAI 31-AGOSTI 6, 2015

Waislamu wasimame kidete


kulinda Ubinadamu, Uafrika

AMIR wa Baraza Kuu, Sheikh Mussa Kundecha akizungumza na waumini katika


moja ya Misikiti jijini Dar es Salaam.

kwa wote na kupinga


dhuluma kwa sababu
haifai. Kwa hiyo
niliamua kuwaachia hilo
nisilolielewa waendelee
nalo peke yao ila
katika mengine yenye
kutuunganisha katika
haki tuendelee kuwa
pamoja tukiwa kama
Watanzania, Waafrika
na Waja wa Mwenyezi
Mungu tuliowekwa
duniani kwa makusudi
mema ya muumba wetu.
Leo nakuja na
changamoto ya Waislamu
kuulinda Uafrika na
Ubinaadamu kijumla,
kwasababu tayari
nimeyaona mapungufu
k wa Wa k r i s t o.
Mapungufu hayo yako
dhahiri kiasi kwamba ni
mnafiki peke yake ndiye
anayeweza kuyavumilia,
kuyanyamazia ama
kujifanya hayaoni. Awali
ya yote nianze kwa kukiri
maneno yaliyoko kwenye
Injili ya Yesu ambapo
alionya juu ya ukengeufu
na chukizo la uharibifu
ambalo pia lilitabiriwa
na Nabii Danieli. Yesu
alisema tutakapoliona
chukizo limeinuliwa juu
na hatimaye kuwekwa hadi
patakatifu, basi aliyeko
juu ya dari asishuke chini

kuvichukua vyombo
vyake.
Hilo chukizo la
uharibifu limefichwa
yawezekana sehemu ya
maandiko ya unabii wa
Danieli yalifichwa kwa
makusudi ili kuulinda
uovu.
B a a d a
y a
kutahadharisha hilo, Yesu
akasema maneno yenye
changamoto walakini
hapo atakapokuja tena
mwana wa Adamu,
ataikuta imani duniani?
Naye Yuda mdog o
wake tumbo moja
n a Ye s u a l i a n d i k a
walakini katika kutafuta
mambo yote nimeona
niwaandikie juu ya jambo
m o j a t u k u wa o n y a
kwamba muishindanie
imani waliyokabidhiwa
watakatifu mara moja
tu. Maana ya maneno
hayo ni moja kwamba
mwanadamu anapaswa
kuipigania imani awapo
d u n i a n i , k wa s a b a b u
hatapata wasaa mwingine
wa kuitetea ama
kuipigania imani yake
baada ya kufa kwake.
Mtu akiisha kufa hana
tena nafasi ya kuamini
wala kuikiri imani yake,
k wa k u wa m a z i n g i r a
hayaruhusu.

Ipo imani ya awali


ambayo mitume na
manabii wote kuanzia
Nuhu, Ibrahimu hadi
Musa waliikiri, kwa leo
sitaijadili kwa sababu
s i yo l e n g o l a m a d a
yangu. Madhumuni ya
mada yangu kwanza ni
kuyaweka wazi masikitiko
yangu na huzuni yangu
kutokana na jinsi
watu waliotegemewa
wanavyosita kuusimamia
u k wel i k wa k uhof i a
maslahi yao ya kidunia
yataathirika.
Ulaya imeukubali
kidhati ushoga na
machukizo mengine
ambayo wameyapa jina
bandia la ndoa za jinsia
moja. Lililo baya zaidi ni
hili kwamba baada ya wao
kuyaridhia machukizo,
wanashinikiza na
wanadamu wengine
waishio sehemu zingine
za dunia wakubaliane
na chukizo lao. Kwa
Waafrika inatumika silaha
ya misaada kushinikiza
walikubali chukizo na
kwa Waarabu zinatumika
silaha za moto. Uvamizi
k ati ka nchi zote za
Kiarabu una lengo
moja tu la kusimika
utamaduni mpya.
Mabeberu walipoivamia

Afrika kwenye karne ya


18, waliua, walichinja
na kuharibu ili kuimiliki
Afrika, kuufaidi utajiri
wake na kuitamadunisha
upya.
Mabeber u hao leo
wanalivamia bara la
Arab si kwa sababu ya
rasilimali ya mafuta kwa
kuwa tayari mafuta ya
Petroli yapo chini ya
udhibiti wao, kumbe ni
kwa nini wazishambulie
kijeshi nchi za Kiarabu?
Mabeber u wanakijua
wanachopigania ingawa
hawakiweki wazi.
Wazungu wa Ulaya na
Wamarekani wameamua
kidhati kwamba misaada
yao kwa nchi za Afrika
imeambatanishwa
na sharti kwamba
wanaosaidiwa kuukubali
ushoga, kinyume cha
hivyo wakikataa ushoga
wasitarajie hata senti
itakayotoka Ulaya
na Marekani kuingia
Afrika. Waziri Mkuu
wa Uingereza David
Cameroon aliwaambia
bayana viongozi wa Afrika
waliohudhuria mkutano
wa Jumuia ya Madola
kwamba wabadilishe
katiba zao zikubaliane
na haki ya watu wa jinsia
moja kuoana.
Cameroon anataka
katiba za dola za Afrika
zitambue haki ya awali
ya wale waaminio katika
chukizo hili, kwa tafsiri
nyepesi Cameroon
analiinua juu chukizo na
kulisogeza mbele zaidi.
Mwisho watalifikisha
kwenye imani kwamba
dini isiyolikubali suala
la ushoga, ipigwe vita
haiwafai walimwengu.
Cameroon aliwaeleza
hayo ya kubadilisha
katiba zao ili kuutambua
ushoga wakiwa kwenye
mkutano wa wakuu wa
nchi wanachama wa
Commonwealthy
yaani Jumuia ya madola,
asasi ambayo mama
yake Malkia Elizabeth
ndiye mkuu wake na pia
ndiye mkuu wa Kanisa la
Anglican.
Hilo halikuwastua
Wakristo wa dhehebu
hilo na madhehebu
mengine kiujumla
walioko Afrika hususan
Tanzania kwamba Ukristo
unaelekea wapi kama siyo
Inaendelea Uk. 19

19
Inatoka Uk. 18

kulikumbatia chukizo
linaloharibu na hatimaye
kuliweka patakatifu?
Nilitarajia Watanzania
kushikamana na kuutetea
ukweli kwamba kama
tulivyoupinga na kuukataa
ubaguzi wa rangi, sasa
tunaupinga na kuukataa
ushog a kwa vitendo.
N i l i t a r a j i a t u t awe k a
wazi misimamo ya
Taifa hili kwamba ikiwa
Uingereza iliyo kinara
wa Commonwealthy
inasema hivyo na inaamini
hivyo, basi Tanzania si
kwamba tunaikataa tu
misaada iliyoambatana
na shinikizo la kuukubali
ushoga, bali kuonyesha
tumechukizwa na
msimamo wa Uingereza,
Tanzania inajitoa kwenye
Jumuia ya madola.
Kwa s a b a b u n i a s a s i
isiyotusaidia chochote
kimaisha na sasa
imeangia hatua nyingine
ya kupig ana kufa na
kupona ili kutuondoa
kwenye maadili ya utu
na kutupeleka kwenye
ushetani. Maana ushoga
haustahili hata kuitwa
unyama kwani mbwa
pamoja na uumbwa wake,
bado dume la mbwa
halimwingilii kingono
dume mwenzake.
Jambo linalopaswa
kuhojiwa na watu makini
ni hili kwamba ni kitu
g ani kinachowafanya
watu wakubwa kama
Cameroon na Baraka
O b a m a k u wa p i g a n i a
mashoga kwa nguvu zote?
Je, wana huruma sana na
mashoga wa Afrika hadi
wawapiganie kiasi hicho?
Kama wana huruma ni
kwanini wasiwahurumie
watoto wafao kwa utapia
mlo katika nchi maskini
za Kiafrika? Kwanini
wasiwahurumie watoto
wa Iraq, Libya na Yemen
walikovamia bila sababu
za msingi?
Hapa
ndipo
inapojidhirisha wazi
kwamba hawawapiganii
mashoga kama wanadamu,
bali wanapigania
utamaduni wao unaoua
uhuru wa kweli na kuachia
u h u r u wa k i s h e t a n i
binaadamu kuwa mbaya
kwa kiwango chochote
anachotaka yaani uhuru
ambao kimsingi unaasi
maagizo ya Mwenyezi

HABARI

AN-NUUR

SHAWWAL 1436, IJUMAA JULAI 31-AGOSTI 6, 2015

Waislamu wasimame kidete


kulinda Ubinadamu, Uafrika

Mungu. Uhuru wa aina


hiyo hauwezi kusimikwa
duniani kama Uafrika
na Uislamu vikiwa
hai kwakuwa wanajua
Uafrika na Uislamu hauna
compromise.
Mwaka 2001 kabla ya
kufungwa nilikuwa na
mazungumzo na balozi
wa Pakistan hapa nchini,
alinitolea orodha ya nchi
zitakazoshambuliwa
(kuvamiwa) na Marekani
na washirika wake baada
ya Iraq.
Balozi huyo akasema
hata Saudi Arabia
inajidanganya, utafika
wakati itageukwa kama
ilivyogeukwa Iraq na
ilivyogeukwa Iran baada
ya kuondoka kwa Shah
Mohamed Reza Pahlav
mwaka 1978. Kwenye
orodha yao nchi ya mwisho
kuvamiwa itakuwa China
Mabadiliko ya katiba
na kupata katiba mpya
itakayotambua ushoga
maana yake halisi ni
kwamba vitabu vya sheria
k a m a Pe n a l C o d e
Criminal Procedure
Act na Evidence
Act vitabidilishwa ama
vitafutwa na kuandikwa
upya. Vifungu vya
offences against
morality itabidi visomeke
vingine ama visiweko
kabisa ili kukidhi mila
mpya inayopiganiwa na
kina Obama na Cameroon
Kwanini hakuna NGO
za kupinga ushoga na
usagaji kama mila potofu
sambamba na hizi NGOs
zinazopinga ukeketaji
na mitala? Hapa ndipo
in a p o jio ny es h a waz i
kwamba NGOs nyingi
zimeanzishwa ili kunasa
f e d h a k u t o k a U l ay a
mangaribi na Marekani si
kweli kwamba wahusika
wana wito wa kumkomboa
mwanamke. Ni ukombozi
gani huu wa kumwokoa
mwanamke asikekete
wala asikeketwe, lakini
usimwokoe mwanamke
anayekosa haki yake ya
kupata mume kwa vile
wanaume wanaowana
wenyewe kwa wenyewe?

WAISLAMU wakiwa katika moja ya mashindano ya usomaji wa Qur'an.

UNODC kuisaidia Zanzibar


Inatoka Uk. 20

wa UNODC pia utajumuisha


kuimarisha mazingira ya vyuo
vya mafunzo, ili kuepusha
maambukizi ya ukimwi na
athari nyengine zinazotokana
na dawa za kulevya.
Wakati huo huo Makamu
wa Kwanza wa Rais wa
Zanzibar, Mhe. Maalim Seif
Sharif Hamad, ametuma
salamu za rambi rambi kwa
wananchi wa India kufuatia
k i f o ch a m wa n a s a y a n s i
aliyewahi kuwa Rais wa nchi
hiyo, Dk. Avul Pakir Abdul
Kalam kilichotokea Jumatatu
iliyopita.
Maalim Seif ametuma
salamu hizo wakati alipofika
kusaini kitabu cha maombolezi
na zungumza na Balozi mdogo
wa India hapa Zanzibar,
Satendar Kumar, katika ofisi
za Ubalozi huo Migombani.
Maalim Seif alisema
Kiongozi huyo msomi alitoa
mchango mkubwa kwa Taifa
la India, hasa katika uvumbuzi
wa vyombo vya anga za juu
kwa ajili ya matumizi ya kiraia
na Kijeshi.
Alisema bila shaka kifo
chake kimeacha pengo na

masikitiko makubwa sio tu kwa


wananchi wa India, bali kwa
jamii ya wasomi Duniani, na
amewataka wananchi wa India
kuwa na subira katika wakati
huu mgumu wa maombolezi.

Abdulkalam (83) ambaye


alipewa jina la umaarufu mtu
wa misaili wa India alishika
nafasi ya Urais wa India mwaka
2002 kwa muda wa miaka
mitano.

VACANCIES

(In the College and Schools of WEC)


Nursing tutor:- Matured with experience
of 5 years.
(Qualification- Degree or Diploma
holder.)
Head Mistress:-Qualification- Degree
holder with 5 years experience
Academic Inspector (Degree or diploma
holder)
Email your CV to - applications.wec@gmail.
com or post to P.O BOX 19711.

AN-NUUR

20

MAKALA

20

Na Khamis Haji (OMKR)


SHIRIKA La Umoja wa
Mataifa la Kupambana na
Dawa za Kulevya na Uhalifu
(UNODC) limesema
litafanya tathmini ya kina
kupata njia muafaka
za kuisaidia Zanzibar
kukabiliana na biashara,
matumizi na athari za dawa
za kulevya kwa jamii.
Hayo ameyasema kiongozi
wa ujumbe kutoka shirika
hilo, Jose Vila Del Castillo,
alipokutana na Makamu
wa Kwanza wa Rais wa
Zanzibar, Mhe. Maalim Seif
Sharif Hamad ofisini kwake
Migombani na kufanya naye
majadiliano.
Del Castillo alisema
kutokana na mazingira
ya nchi za visiwa kama
Zanzibar, mikakati maalum
ya kupambana na dawa na
biashara za dawa za kulevya
haina budi kuchukuliwa, ili
kuwaokoa wananchi wake
kugeuzwa njia za kusafirishia
biashara hiyo haramu.
Alisema msaada huo
utalenga zaidi kuipatia
Zanzibar vifaa vya kisasa,
kukuza utaalamu kwa
watendaji na wadau muhimu
wa kupambana na dawa za
kulevya, ikiwemo wendesha
mashitaka, wapelelezi,
watendaji wa Ofisi ya Mkemia
Mkuu wa Serikali pamoja na
wanasheria.
Alisema UNODC litaanza
kufanya tathmini hiyo mwezi
ujao na ikikamilika, Shirika
hilo litaweza kufahamu ni

SHAWWAL 1436, IJUMAA JULAI 31-AGOSTI 6, 2015

AN-NUUR
(19)
HIJJA
INAZAA
UMOJA
NA
NGUVU.
SHAWWAL 1436, IJUMAA

JULAI 31-AGOSTI 6, 2015


Hijja inatukusanya wakati mmoja waislamu kutoka kila
pembe ya dunia bila kubagua Taifa, kabila, wala itikadi.
Hijja ni zoezi na fundisho kubwa la umoja wa waislamu.
Utukufu, nguvu na ushindi ni vya Allah!Twendeni Allah
Ajisikie! Muda unakwisha! Gharama zote kwa Hijja ni Dola
4,500. Umra ya Ramadhani ni Dola 2,300. Karibuni Ahlu
Sunna Wal Jamaa kwa huduma nzuri na uongozi bora.
Wasiliana nasi: Tanzania Bara: 0765462022;0782804480;
0717224437.
Zanzibar: 0777468018;0777458075;0777845010.

UNODC kuisaidia Zanzibar


kupambana na mihadarati
Maalim Seif atuma rambirambi India

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, akiwa katika
picha ya pamoja na ujumbe wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na Dawa za
Kulevya na Uhalifu (UNODC) Afrika Mashariki, pamoja na baadhi ya watendaji wa Tume
ya Udhibiti wa Dawa za Kulevya Zanzibar. (Picha na Salmin Said, OMKR)
hayo, Makamu wa Kwanza
wa Rais wa Zanzibar Mhe.
Maalim Seif Sharif Hamad,
alisema Serikali inachukua
hatua mbalimbali kuiepusha
Zanzibar kuwa kituo cha

kuingizwa na kusafirishiwa
dawa za kulevya.
Aliongeza kuwa juhudi hizo
pia zinajumuisha kuwasaidia
wananchi wasijiingize
katika vitendo vya kutumia

Ni kati ya White House na Congress

magoti Iran na suala la


kuepuka vita na nchi hiyo.
Waziri wa Mambo ya Nje
wa Marekani John Kerry,
alisisitiza mara kadhaa
katika kikao hicho kwamba
fikra ya kuipigisha magoti
Iran na kuilazimisha itupilie
mbali miradi yake ya nyuklia
ni ndoto tupu na kwamba,
jamii ya kimataifa haitaunga
mkono takwa la Marekani
la kuinyima Iran haki zake
za nyuklia.

hatua gani linapaswa kuanza


kuzichukua kwa kushirikiana
na Serikali ya Zanzibar
kukabiliana na biashara hiyo
na madhara yake.
Katika mazungumzo

au kufanya biashara hiyo,


ikiwemo kutoa miongozo
kwa makundi mbalimbali ya
jamii, na wanafunzi wa skuli
mbalimbali.
Kuhusu wale ambao
tayari wanatumia dawa hizo,
Maalim Seif alisema Serikali
kwa kushirikiana na jumuiya
na watu binafsi, imefungua
vituo maalum kwa ajili ya
kuwasaidia kubadilisha tabia,
ili baadaye wawe raia wema
katika jamii yao.
Makamu huyo wa Kwanza
wa Rais alisema hivi sasa
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar
tayari imeanza ujenzi wa kituo
cha kisasa cha kurekebisha
tabia za wananchi wanaotumia
dawa hizo, ambacho jengo
lake litakuwa na ghorofa tatu
na sehemu zote muhimu kwa
mahitaji yao.
Hata hivyo alisema zipo
baadhi ya chang amoto
zinazojitokeza katika
mapambano dhidi ya dawa za
kulevya Zanzibar, ikiwemo
uhaba wa vifaa vya kisasa
vya uchunguzi na ukaguzi
katika maeneo ya kuingilia na
kutokea nchini.
Changamoto nyengine
alizozitaja ni mazingira ya
visiwa vya Zanzibar kuwa
na bandari nyingi zisizokuwa
rasmi, ambazo hutumiwa na
baadhi ya watu kuingiza vitu
vyenye madhara, zikiwemo
dawa za kulevya.
Katika mazungumzo
hayo, mshauri wa masuala ya
Ukimwi wa Shirika hilo Kanda
ya Afrika Mashariki, Sylvie
Bertrand, alisema msaada huo
Inaendelea Uk. 19

Nyuklia ya Iran yazua vita Marekani


K U M E I B U K A
mpambano mkali kati
ya Ikulu (White House)
na Bunge la Marekani
(Cong r ess) kuhusu
makubaliano ya nyuklia
na Iran yaliyofikiwa hivi
karibuni.
Mpambano huo ulianza
wiki iliyopita katika kikao
cha maswali na majibu
cha K amati ya Seneti,

kilichohudhuriwa na
Mawaziri watatu wa serikali
ya Rais Barack Obama
a m b a p o Jo h n K e r r y,
Ernest Moniz na Jacob
Lew, Mawaziri wa Mambo
ya Nje, Nishati na Fedha
wa Marekani walifanya
jitihada za kuwashawishi
wenzao katika Bunge hilo,
wakijaribu kusisitiza faida

za makubaliano ya nyuklia
ya kundi la 5+1 na Iran
na kujaribu kujibu hoja
za upinzani kutoka kwa
baadhi ya Maseneta dhidi
ya makubaliano hayo.
Matamshi ya muda mrefu
ya mawaziri hao wa serikali
ya Marekani, yalijikita zaidi
katika suala la kushindwa
Washington kuipigisha

Viongozi waandamizi
wa serikali ya Marekani
wanaona kuwa, iwapo
makubaliano yaliyofikiwa
kati ya Iran na kundi la 5+1
yatapingwa na Congress,
Iran itaingia katika mkondo
wa kurutubisha madini ya
urani kwa kiwango kikubwa
bila ya kuwa chini ya udhibiti
wa Wakala wa Kimataifa wa
Nishati ya Atomiki.
Kerry alisisitzia kuwa,
Inaendelea Uk. 16

Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na POA Printing Works LTD, S.L.P. 4605, Dar es Salaam.

Вам также может понравиться

  • Nyuma ya Mapazia
    Nyuma ya Mapazia
    От Everand
    Nyuma ya Mapazia
    Рейтинг: 5 из 5 звезд
    5/5 (1)
  • Dini ya Fedha
    Dini ya Fedha
    От Everand
    Dini ya Fedha
    Оценок пока нет
  • Annuur 1161 PDF
    Annuur 1161 PDF
    Документ16 страниц
    Annuur 1161 PDF
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1173 PDF
    Annuur 1173 PDF
    Документ20 страниц
    Annuur 1173 PDF
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1111
    Annuur 1111
    Документ16 страниц
    Annuur 1111
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1170
    Annuur 1170
    Документ20 страниц
    Annuur 1170
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1096
    Annuur 1096
    Документ12 страниц
    Annuur 1096
    annurtanzania
    Оценок пока нет
  • Annuur 1180 PDF
    Annuur 1180 PDF
    Документ20 страниц
    Annuur 1180 PDF
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1168 PDF
    Annuur 1168 PDF
    Документ20 страниц
    Annuur 1168 PDF
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annur Toleo La Ijumaa
    Annur Toleo La Ijumaa
    Документ16 страниц
    Annur Toleo La Ijumaa
    annurtanzania
    Оценок пока нет
  • ANNUUR 1176b PDF
    ANNUUR 1176b PDF
    Документ20 страниц
    ANNUUR 1176b PDF
    annurtanzania
    Оценок пока нет
  • Annuur 1172 PDF
    Annuur 1172 PDF
    Документ20 страниц
    Annuur 1172 PDF
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • ANNUUR1004
    ANNUUR1004
    Документ16 страниц
    ANNUUR1004
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Annuur 1122
    Annuur 1122
    Документ16 страниц
    Annuur 1122
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Gazeti La Annur
    Gazeti La Annur
    Документ12 страниц
    Gazeti La Annur
    Hassan Mussa Khamis
    Оценок пока нет
  • Annuur 1153 PDF
    Annuur 1153 PDF
    Документ16 страниц
    Annuur 1153 PDF
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1112
    Annuur 1112
    Документ16 страниц
    Annuur 1112
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1064
    Annuur 1064
    Документ12 страниц
    Annuur 1064
    annurtanzania
    Оценок пока нет
  • Annuur 1082
    Annuur 1082
    Документ16 страниц
    Annuur 1082
    MZALENDO.NET
    100% (1)
  • Annuur 1179 PDF
    Annuur 1179 PDF
    Документ20 страниц
    Annuur 1179 PDF
    annurtanzania
    100% (1)
  • Annuur 112
    Annuur 112
    Документ16 страниц
    Annuur 112
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • ANNUUR 1175b PDF
    ANNUUR 1175b PDF
    Документ20 страниц
    ANNUUR 1175b PDF
    annurtanzania
    Оценок пока нет
  • Annuur 1187 PDF
    Annuur 1187 PDF
    Документ20 страниц
    Annuur 1187 PDF
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1062
    Annuur 1062
    Документ16 страниц
    Annuur 1062
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • ANNUUR 1169a PDF
    ANNUUR 1169a PDF
    Документ20 страниц
    ANNUUR 1169a PDF
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1107
    Annuur 1107
    Документ16 страниц
    Annuur 1107
    annurtanzania
    Оценок пока нет
  • Annuur 114
    Annuur 114
    Документ12 страниц
    Annuur 114
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Annuur 1151
    Annuur 1151
    Документ16 страниц
    Annuur 1151
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1056 PDF
    Annuur 1056 PDF
    Документ16 страниц
    Annuur 1056 PDF
    annurtanzania
    Оценок пока нет
  • Annuur 1165
    Annuur 1165
    Документ20 страниц
    Annuur 1165
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1040
    Annuur 1040
    Документ12 страниц
    Annuur 1040
    Hassan Mussa Khamis
    Оценок пока нет
  • Annuur 1109
    Annuur 1109
    Документ16 страниц
    Annuur 1109
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1123
    Annuur 1123
    Документ16 страниц
    Annuur 1123
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1007
    Annuur 1007
    Документ16 страниц
    Annuur 1007
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Annuur 1088 PDF
    Annuur 1088 PDF
    Документ12 страниц
    Annuur 1088 PDF
    annurtanzania
    Оценок пока нет
  • Annuur 1119
    Annuur 1119
    Документ16 страниц
    Annuur 1119
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1102
    Annuur 1102
    Документ12 страниц
    Annuur 1102
    annurtanzania
    Оценок пока нет
  • Annuur 1039
    Annuur 1039
    Документ16 страниц
    Annuur 1039
    Hassan Mussa Khamis
    Оценок пока нет
  • ISSN 0856 - 3861 Na. 986 DHUL-HAJJ 1432, IJUMAA NOV. 25 - DES. 1, 2011 BEI TShs 500/, Kshs 50
    ISSN 0856 - 3861 Na. 986 DHUL-HAJJ 1432, IJUMAA NOV. 25 - DES. 1, 2011 BEI TShs 500/, Kshs 50
    Документ16 страниц
    ISSN 0856 - 3861 Na. 986 DHUL-HAJJ 1432, IJUMAA NOV. 25 - DES. 1, 2011 BEI TShs 500/, Kshs 50
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • ANNUUR1003
    ANNUUR1003
    Документ16 страниц
    ANNUUR1003
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Annuur 1115
    Annuur 1115
    Документ16 страниц
    Annuur 1115
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1217
    Annuur 1217
    Документ20 страниц
    Annuur 1217
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1144
    Annuur 1144
    Документ16 страниц
    Annuur 1144
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1178
    Annuur 1178
    Документ20 страниц
    Annuur 1178
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1077
    Annuur 1077
    Документ12 страниц
    Annuur 1077
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Annuur 1143
    Annuur 1143
    Документ16 страниц
    Annuur 1143
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1195
    Annuur 1195
    Документ20 страниц
    Annuur 1195
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • ANNUUR 1160a PDF
    ANNUUR 1160a PDF
    Документ16 страниц
    ANNUUR 1160a PDF
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Gazeti La ANNUR
    Gazeti La ANNUR
    Документ12 страниц
    Gazeti La ANNUR
    Hassan Mussa Khamis
    Оценок пока нет
  • Hofu
    Hofu
    От Everand
    Hofu
    Рейтинг: 5 из 5 звезд
    5/5 (1)
  • Tishio la Ukombozi: Ubeberu na Mapinduzi Zanzibar
    Tishio la Ukombozi: Ubeberu na Mapinduzi Zanzibar
    От Everand
    Tishio la Ukombozi: Ubeberu na Mapinduzi Zanzibar
    Оценок пока нет
  • HAYAAN, The Long Journey of the Nomad Boy
    HAYAAN, The Long Journey of the Nomad Boy
    От Everand
    HAYAAN, The Long Journey of the Nomad Boy
    Рейтинг: 5 из 5 звезд
    5/5 (2)
  • Mwongozo wa Tumbo Lisiloshiba na Hadithi Nyinginge
    Mwongozo wa Tumbo Lisiloshiba na Hadithi Nyinginge
    От Everand
    Mwongozo wa Tumbo Lisiloshiba na Hadithi Nyinginge
    Рейтинг: 4.5 из 5 звезд
    4.5/5 (3)
  • Miaka Miwili Ya Urais Wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Au Nyota Iliyofifia?
    Miaka Miwili Ya Urais Wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Au Nyota Iliyofifia?
    От Everand
    Miaka Miwili Ya Urais Wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Au Nyota Iliyofifia?
    Рейтинг: 1 из 5 звезд
    1/5 (1)
  • Nyayo Za Obama
    Nyayo Za Obama
    От Everand
    Nyayo Za Obama
    Оценок пока нет
  • Afisa Usalama Wa Taifa Ni Mtu Wa Aina Gani? Na Anafanya Nini?
    Afisa Usalama Wa Taifa Ni Mtu Wa Aina Gani? Na Anafanya Nini?
    От Everand
    Afisa Usalama Wa Taifa Ni Mtu Wa Aina Gani? Na Anafanya Nini?
    Рейтинг: 4 из 5 звезд
    4/5 (24)
  • Peter DM Bwimbo: Mlinzi Mkuu wa Mwalimu Nyerere
    Peter DM Bwimbo: Mlinzi Mkuu wa Mwalimu Nyerere
    От Everand
    Peter DM Bwimbo: Mlinzi Mkuu wa Mwalimu Nyerere
    Рейтинг: 5 из 5 звезд
    5/5 (3)
  • Kufikirika
    Kufikirika
    От Everand
    Kufikirika
    Оценок пока нет
  • Mmoja Wenu Ni Shetani
    Mmoja Wenu Ni Shetani
    От Everand
    Mmoja Wenu Ni Shetani
    Оценок пока нет
  • Waathirika.
    Waathirika.
    От Everand
    Waathirika.
    Оценок пока нет
  • Annuur 1264
    Annuur 1264
    Документ20 страниц
    Annuur 1264
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1227 PDF
    Annuur 1227 PDF
    Документ20 страниц
    Annuur 1227 PDF
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1232 PDF
    Annuur 1232 PDF
    Документ20 страниц
    Annuur 1232 PDF
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1231 PDF
    Annuur 1231 PDF
    Документ20 страниц
    Annuur 1231 PDF
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1262
    Annuur 1262
    Документ20 страниц
    Annuur 1262
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1225
    Annuur 1225
    Документ20 страниц
    Annuur 1225
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • ANNUUR 1228d
    ANNUUR 1228d
    Документ20 страниц
    ANNUUR 1228d
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1230 PDF
    Annuur 1230 PDF
    Документ20 страниц
    Annuur 1230 PDF
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • ANNUUR 1228d
    ANNUUR 1228d
    Документ20 страниц
    ANNUUR 1228d
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1229 PDF
    Annuur 1229 PDF
    Документ20 страниц
    Annuur 1229 PDF
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1213 PDF
    Annuur 1213 PDF
    Документ20 страниц
    Annuur 1213 PDF
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1217
    Annuur 1217
    Документ20 страниц
    Annuur 1217
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1226 PDF
    Annuur 1226 PDF
    Документ20 страниц
    Annuur 1226 PDF
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1224
    Annuur 1224
    Документ20 страниц
    Annuur 1224
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1218 PDF
    Annuur 1218 PDF
    Документ20 страниц
    Annuur 1218 PDF
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1219
    Annuur 1219
    Документ20 страниц
    Annuur 1219
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1220
    Annuur 1220
    Документ20 страниц
    Annuur 1220
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1223
    Annuur 1223
    Документ20 страниц
    Annuur 1223
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1210a
    Annuur 1210a
    Документ20 страниц
    Annuur 1210a
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1214
    Annuur 1214
    Документ20 страниц
    Annuur 1214
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • ANNUUR 1216d
    ANNUUR 1216d
    Документ20 страниц
    ANNUUR 1216d
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • ANNUUR 1209aaa
    ANNUUR 1209aaa
    Документ20 страниц
    ANNUUR 1209aaa
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1202
    Annuur 1202
    Документ20 страниц
    Annuur 1202
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1208
    Annuur 1208
    Документ20 страниц
    Annuur 1208
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1201
    Annuur 1201
    Документ20 страниц
    Annuur 1201
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1204
    Annuur 1204
    Документ20 страниц
    Annuur 1204
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1195
    Annuur 1195
    Документ20 страниц
    Annuur 1195
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1207...
    Annuur 1207...
    Документ20 страниц
    Annuur 1207...
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1200
    Annuur 1200
    Документ20 страниц
    Annuur 1200
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет