Академический Документы
Профессиональный Документы
Культура Документы
danadana zaendelea
www.annuurpapers.co.tz au facebook:annuurpapers@yahoo.com
Sauti ya Waislamu
ISSN 0856 - 3861 Na. 1211 RABIUL AWWAL 1437, IJUMAA , JANUARI 8 - 14, 2016 BEI TShs 800/=, Kshs 50/=
Soma Uk. 20
Soma Uk. 10
ANNUUR NEW.indd 1
1/7/2016 3:17:00 PM
2
HAKIKA shukrani zote
zinamstahikia Allah.
Tunamhimidi,
tunaomba msaada Kwake,
na tunaomba maghfira.
Tunaomba hifadhi kwake
Allah
kutokana
na
maovu ya nafsi zetu,
na makosa ya matendo
yetu.
Yeyote Allah
Anayemuongoza, hakuna
wa kumpotosha, na yeyote
Allah Anayempotosha,
hakuna wa kumuongoa.
Ninashuhudia
pia
kwamba hakuna yeyote
anayestahiki kuabudiwa
isipokuwa Allah, na
ninashuhudia kwamba
Muhammad (Swalla
Allaahu alayhi wa aalihi
wa sallam) ni mjumbe na
Mtume Wake.
Amesema Allah (SWT):
Enyi
mlioamini!
Mcheni Allaah kama
ipasavyo
kumcha;
wala msife isipokuwa
mmekwishakuwa
Wa i s l a m u
kamili.
(Suratul Al-Imraan: 102).
Enyi watu! Mcheni
Mola wenu Ambaye
amekuumbeni katika
nafsi (asli) moja. Na
Akamuumba
mkewe
katika nafsi ile ile.
Na Akaeneza wanaume
wengi na wanawake
kutoka katika wawili hao.
Na mcheni Allaah ambaye
kwaye mnaombana. Na
(mwatazame) jamaa.
Hakika ni Mlinzi
juu yenu (anayaona kila
mnayoyafanya). (Suratul
An-Nisaa: 1)
Enyi mlioamini!
Muogopeni Allaah
na semeni maneno ya
haki. Atakutengenezeeni
vizuri vitendo vyenu na
Atakusameheni madhambi
yenu; na anayemtii
Allaah na Mtume Wake,
bila shaka amefanikiwa
mafanikio makubwa.
(suratul Al-Ahzaab: 70-71).
Amesema Allah (s.w):
Na uwe kutokana na
nyinyi umma unao
lingania kheri na unao
amrisha
mema
na
unakataza maovu. Na
hao ndio walio fanikiwa.
(Suurat Al 'Imran 3: 104).
Na amesema Allah (s.w):
Na saidianeni katika
wema na uchamungu. Wala
msisaidiane katika dhambi
na uadui. Na mcheni
Mwenyezi
Mungu.
Hakika Mwenyezi Mungu
ni Mkali wa kuadhibu.
(Suurat Al- Maida 5: 2).
Muislamu kama yeye
binafsi hawezi kuibadili
jamii bila kusubiana na
watu wengine wenye lengo
kama lake.
Kazi ya harakati ya
ANNUUR NEW.indd 2
Darsa Duara-1
AN-NUUR
Q A R
M U H A
M A
D R
U R
U L
A L
M U H A
M A
A D U M A
O O D
H A
O N S
H A
O O D
A B A
W A
H H I
H T
A I
N U
H A
H A
M U S
MASUALA
1.Itaje Sura inayotaja juu ya matunda mawili? Jawabu : Attin.
2.Jina kamili la Imam Shafi. Jawabu : Muhama Idrissa.
3.Sura ipi ya Quran inayomalizia kwa majina ya Mitume wawili? Jawabu :
Suratul Al Alaa.
4.Alipohama Mtume Muhammad (SAW) Makka kwenda Madina alimtaka
sahaba yupi alale kwenye kitanda chake? Jawabu : Ali Abi Talib.
5.Suratul Faatiha ina aya ngapi? Jawabu : 7.
6.Ashuraa ipo katika mwezi gani wa Kiislamu? Jawabu : Muharam.
7.Mtume Hud (AS) alitumwa kwa Umma upi? Jawabu : Ad.
8.Mtume Saleh alitumwa kwa Umma upi? Jawabu : Thamood.
9.Mtume Mussa alifwatana na Mtume gani kwenda kukabiliana na Firauni?
Jawabu : Haroon.
10.Jina la ngamia Mtume Muhammad (SAW) alimpanda alipoingia Madina?
Jawabu : Kaswah
CHEMSHA BONGO: 34
Weka duara kwenye jawabu ilio sawa. Jawabu kamili wiki ijayo.
N S
O A
H U A
W A
U L
T U
D A
K D
H S
H I
U M A
M Z
A U
W I
Y D
M H E
D T
H M A
53 A
54 I
M Y
10 E
U
A
H I
H M
M A
H M I
H T
H A
N E
MASUALA
1.Jina la kitabu cha Hadithi kilichokusanywa na Imam Malik kinaitwa:
Muwatta, Bukhari, Riyadh Salihina.
2.Sahaba yupi aliotajwa kwa jina katika Quran?
3.Taja jina la mava ambalo wamezikwa Masahaba na ambalo hadi sasa
wanazikwa watu.
4.Taja jina kati ya wake wa Mtume Muhammad (SAW) aliokuwa na umri
mdogo na alikuwa sio mjane.
5.Mtume Muhammad (SAW) alipohajiri kwenda Madina alikuwa na umri
gani?
6.Mtume Muhammad (SAW) alipohajiri kwenda Madina aliishi Madina
kwa miaka mingapi kabla ya kufariki?
7. Shahidi wa mwanzo kuuwawa katika Uislamu alikuwa ni: Syd Hamza,
Bibi Sumayah au Bilali (RA).
8.Mtumwa wa mwazno kusilimu?
9. Taurat aliteremshiwa Mtume gani?
10.Nimrood aliishi katika zama za Mtume yupi?
Jee Unajua?
1/7/2016 3:17:01 PM
Habari
AN-NUUR
ANNUUR NEW.indd 3
Kama ulivyofanyika
ubabe kufuta uchaguzi chini
ya mtutu wa bunduki kwa
staili ya umafia, wafanye
hivyo hivyo kumtangaza mtu
wao wa CCM wanayemtaka,
wasiharibu kodi za wananchi
na muda wao kuendesha
1/7/2016 3:17:09 PM
Tahariri/Habari
AN-NUUR
Lengolakenininananianafaidika?
MISAMAHA ya
kodi isiyoleta tija
inayotolewa na
serikali kwa taasisi,
makampuni na
wafanyabiashara
wakubwa kwa
ujumla, ni jambo
ambalo limekuwa
likilalamikiwa kwa
muda mrefu na
wananchi, wabunge
na wanahatakati wa
kijamii hapa nchini.
Kila
mwaka
wabunge wa Bunge la
Jamhuri ya Muungano
Ta n z a n i a h u p i t i a
na kuchanganua
kwa makini bajeti
ya Serikali. Lakini
misamaha ya kodi kwa
upande mwingine,
haipati nafasi sawia
ya kupitiwa vizuri
Bungeni, hivyo kuwa
vigumu kufahamika
bayana ni kiwango
gani cha misamaha
k i n a c h o t o l e wa n a
imesababisha hasara
kiasi gani kwa serikali,
au imewasaida vipi
wananchi.
Hata hivyo mwaka
2009/10 peke yake,
ilibainika kuwa
asilimia 2.3 ya pato
la taifa au TZS 695
b i l i o n i z i l i t o l e wa
kama misamaha ya
k o d i . U k u b wa wa
kiwango cha fedha
kinachohusishwa na
misamaha kiliibua
maswali kuhusu
makusudi ya motisha
hizi na iwapo kiwango
kinachotumika kinafaa
kutolewa.
Kwa kuwa misamaha
ya kodi ilionekana
kuwa mikubwa
mno kwa nchi
ambayo inakabiliwa
na changamoto ya
kukusanya fedha za
ANNUUR NEW.indd 4
kutosha kugharamia
bajeti yake, mwaka
2009 Serikali ya
awamu ya nne ya Rais
mstaafu Jakaya Mrisho
Kikwete, ilieleza
Bungeni kwamba
imefuta misamaha ya
kodi kwa mashirika
na taasisi za dini hapa
nchini kama moja ya
hatua ya kuongeza
mapato.
Serikali ilieleza
kwamba hatua yake
hiyo, ilitokana na
kubaini kukithiri kwa
matumizi mabaya ya
misamaha ya kodi
inayotolewa katika
taasisi hizo za kidini.
Tulishuhudia hoja
hiyo ikiibua mvutano
mkubwa kati ya
serikali na viongozi
wa dini ambao ndio
wanaosimamia
mashirika na
taasisi hizo za dini
zinazosamehewa kodi.
Viongozi mbalimbali
wa dini hasa wa
Kikristo, walijitokeza
kupinga kwa nguvu
hatua hiyo ya serikali
ambapo tulishuhudia
wakilazimika kuweka
kambi Dodoma, ili
kushinikiza kuzuiwa
hoja hiyo ya kufutwa
misamaha Bungeni.
Kweli, shinikizo lao
lilifaulu na hatimaye
hoja ile ilikwama.
Serikali ikarejesha
misamaha kwa sharti
la kuwataka viongozi
hao kuwa waadilifu
kwa misamaha
wanayopewa na
serikali.
Tunafamu kwamba
lengo la serikali
kuweka misamaha
ya kodi kwa taasisi
na mashirika ya
dini, lilikuwa ni
kuyawezesha
mashirika na taasisi
hizo kuisaidia serikali
kutoa huduma
nafuu za kijamii kwa
wananchi kama vile
kutumika kugharimia
afya, maji na elimu nk.
Lakini pamoja
na kuwepo kwa
misamaha hiyo, bado
huduma za kijamii
katika taasisi hizo
zimeendelea kuwa
za ghali kama ilivyo
katika taasisi za binafsi.
Hakuna nafuu yeyote
inayopatakina hadi
sasa. Ada katika shule
zao ni sawa au zaidi
ya shule za binafsi na
serikali. Gharama za
huduma za matibabu
katika hospitali zao
hazina tofauti na zile
za binafsi. Ndipo
linapokuja swali, nini
sababu ya misamaha
hii na ni nani anafaidika
na misamaha hii?
Tunaamini kabisa
kwamba, fursa hii
ya s e r i k a l i k u t o a
misamaha ya kodi kwa
taasisi na mashirika ya
dini, ilikuwa ni kwa
lengo la kuisaidia
serikali kufikisha
huduma nafuu kwa
Mtanzania. Kwamba
mashirika hayo
yaweze kupata uwezo
wa kutoa huduma
kwa wananchi kwa
gharama nafuu. Lakini
hali imekuwa sivyo.
Kimsingi, kwa jinsi
hali ilivyo sasa ya
huduma za kijamii
zinazotolewa katika
taasisi hizi za dini,
hakuna tena sababu
ya kuwepo misamaha
ya kodi, maana lengo
limekiukwa.
Wanaofaidika na
misamaha hii bila
shaka ni hao hao
v i o n g o z i wa d i n i
na marafiki zao,
lakini sio waumini
wala wananchi
wanaozunguka taasisi
husika.
Kwa
maana
nyingine, tuna imani
kwamba serikali
inatambua kuwa
fursa waliyoitoa,
AN-NUUR
inawanufaisha
wachache, tena
wenye uwezo badala
ya kunufaisha wengi
ambao ni makabwela.
Ndio maana
walipochunguza,
wakangundua
udhaifu, wakafuta
msamaha huo kwa
kuwa kihalisia ulikuwa
hauna maana kwa
mwananchi na kwa
hivyo hauna madhara
ukiondolewa.
Tukiacha suala la
misamaha ya kodi,
bado kuna nafuuu
nyingine wanayopata
mashirika na taasisi
za kidini hasa katika
sekta ya Afya. Kwa
muda mrefu serikali
imekuwa ikitoa
ruzuku katika vituo
vya afya na hospitali
za taasisi za kidini,
ili kuweza kutoa
huduma ya afya kwa
wananchi.
Pamoja na kutolewa
ruzuku hizo, bado
tunaona hospitali
hizo zikiendeshwa
kibiashara zaidi
huku huduma zake
z i k i e n d e l e a k u wa
za gharama kubwa
i k i l i n g a n i s h wa n a
hospitali za serikali,
ambazo
nazo
huendeshwa kwa
fedha za serikali.
Tunaona kuna haja
ya serikali kufikiri upya
kuhusu misamaha ya
kodi kwa taasisi zetu
za dini.
Tunaona siku hizi
v i o n g o z i wa d i n i
wakiiba sadaka za
waumini. Wakitajirika,
wakijenga mahekalu
yao binafsi kwa
sadaka, wakinunua
magari ya thamani
kwa matumizi yao
binafsi kwa sadaka
na kwa kutumia
fursa za misamaha
ya kodi waliyo
nayo. Wanajenga na
kuendesha shule zao
binafsi kwa mgongo
wa taasisi za kidini,
wakipata misamaha
ya kodi lakini huduma
zikiwa juu zaidi kwa
Mtanzania.
W e
n
g
i
wameshindwa kuwa
waadilifu kiasi cha
kuaminiwa kutumia
fursa ya misamaha wa
kodi kutoka serikalini
ili kuihudumia jamii.
Tunaona hata serikali
inapogusa eneo hilo
la kuondoa misamaha,
viongozi hawa
hungaka na kuwa
wakali kama mbogo,
lakini wanakiri
kwamba kuna udhaifu
j a p o wa o n a d a wa
sio serikali kufuta
misamaha hiyo.
Wengi wanaficha
uhalisia wao,
wakihadaa kwamba
inachotakiwa
kufanya serikali ni
kuwatafuta wakosaji
na kuwachukulia
hatua, lakini si kufuta
misamaha ya kodi!.
L e o t u k i a m b i wa
taasisi za dini ni
miongoni mwa zile
kampuni zinazotakiwa
kuwasilisha nyaraka
kwa ajili ya kuhakiki
kama zinalipa
ushuru wa Bandari
uliosababisha serikali
kupoteza kiasi cha
shilingi bilioni 48
haishangazi.
Ta y a r i t u m e o n a
katika orodha
iliyotolewa na TPA
Jumatano ya Desemba
30, 2015 ambapo taasisi
na mashirika haya ya
dini, tena makubwa
na yanayoaminiwa
yakiwemo.
Dalili kama
hii inadhihirisha
wazi kwamba hata
hiyo misamaha ya
kodi haiwezi kuwa
inatumika vizuri hata
baada ya kutolewa
onyo na serikali 2009.
Ni ushauri wetu kwa
serikali kwamba, kwa
hali tuliyofikia ambapo
mashirik a ya d ini
yamekuwa yakifanya
biashara kama taasisi
au kampuni nyingine
za kibiashara, iangalie
upya kipengele hiki
cha misamaha ya kodi.
Vinginevyo kuwe na
utaratibu madhubuti
wa kuhakikisha kuwa
malengo ya misamaha
hiyo yanafikiwa.
1/7/2016 3:17:09 PM
5
MWIGIZAJI
maarufu wa filamu
za Hollywood nchini
Marekani Samuel
Jackson, amesema
hivi sasa waumini
wa dini ya Kiislamu
nchini humo
wanabaguliwa kama
wanavyobaguliwa
watu Weusi.
Samuel Jackson
aliyasema hayo hivi
karibuni kwamba
waumini wa dini
ya Kiislamu nchini
Marekani kwa sasa
wamekuwa kama watu
Weusi kwa kubaguliwa
na wanaonekana
hivi sasa kuwa ni
Weusi wapya wa
Kimarekani, ambapo
hufanyiwa dhulma
na kudharauliwa na
daima hawapewi haki
zao za msingi.
Aidha mwigizaji
huyo aliashiria
matukio ya kigaidi
ya hivi karibuni
yaliyotokea Paris
Habari za Kimataifa
AN-NUUR
Waislamu wanabaguliwa
kama watu weusi Marekani
na California, kuwa
matukio hayo yalikuwa
ndio ufunguo wa
kushadidia hali
hiyo ya ubaguzi na
kuwanyanyapaa
Waislamu.
Alimalizia maelezo
yake kwa kusema
kuwa baada ya
matukio hayo nchini
Marekani na Ufaransa,
siku hadi siku
kumekuwa kukitokea
suala la kuvamiwa
Misikiti na kuichoma
moto, kuwanyanyapaa
Waislamu katika
mataifa hayo na
mataifa mengine katika
bara la Amerika na
Ulaya. ABNA.
SAMUEL Jackson
KAMATI ya
Uchunguzi ya Baraza
la Wawakilishi la
Marekani imelitaka
Shirika la Usalama
wa Taifa NSA, kutoa
taarifa kuhusu ripoti
kwamba shirika hilo
lilinasa mawasiliano
kati ya maafisa wa
Waisrael na wabunge
wa Marekani.
Katika barua
iliyotumwa kwa
Mkurugenzi wa NSA
Michael Rogers,
Mwenyekiti wa Kamati
ya Usimamizi Jason
Chaffetz na Mwenyekiti
wa Kamati Ndogo Ron
DeSantis, walisema
habari iliyotokea katika
toleo la Jumanne la
jarida la Wall Street,
iliibua maswali kuhusu
utaratibu unaofuatwa
na wafanyakazi wa
NSA katika kuanisha
iwapo mawasiliano
yaliyonaswa
yanawahusisha
wabunge wa Bunge la
Marekani Congress.
Jarida hilo
likiwanukuu maafisa
wa sasa na wa
zamani wa serikali
ya Marekani, lilisema
NSA ilikuwa ikimlenga
Waziri Mkuu wa
Israel Benjamin
ANNUUR NEW.indd 5
MKURUGENZI wa NSA
Michael Rogers.
Netanyahu na maafisa
wengine wa Israel,
baada ya kuanzisha
kampeni yao katika
Bunge la Marekani
kujaribu kukwamisha
makubaliano ya
nyuklia ya Iran.
Sambamba na kunasa
mawasiliano ya maafisa
wa serikali ya Israel,
uchunguzi huo ulinasa
pia taarifa za ndani
kuhusu juhudi zao
za uraghibishi, ikiwa
ni pamoja na baadhi
ya mazungumzo
yao na wabunge wa
Congress na makundi
ya Wayahudi wa
Marekani, liliripoti
jarida hilo.
Barua kutoka kwa
Chaffetz na DeSantis,
wote kutoka chama cha
Republicans, ilimtaka
Rogers kuwapatia
taarifa juu ya utaratibu
wa shirika hilo kuamua
iwapo mawasiliano ya
wabunge yamenaswa
katika udukuzi wa
NSA, na kwa kiasi
gani wafanyakazi wa
shirika hilo wamekuwa
wakitoa taarifa
hizo kwa mashirika
mengine ya Marekani
pamoja na Ikulu (White
House).
Kamati hiyo pia
iliitaka NSA iipe
maelezo mafupi
kuhusu wafanyakazi
wake. Jarida la Wall
Street liliripoti kuwa
NSA ilifuata muongozo
unaozitaka ripoti
zake za uchunguzi
kuondoa majina
yoyote ya Wamarekani,
wakiwemo wabunge
waliotajwa katika
mawasiliano ya
Waisrael yalionaswa.
Ripoti ya Jarida hilo
ilisema hata baada ya
Rais Barack Obama
kutangaza miaka
miwili iliyopita kuwa
angeweka ukomo
kwenye kuyachunguza
mataifa washirika,
NSA iliendelea
kumchunguza Waziri
Mkuu wa Israel
Banjamini Netanyahu,
pamoja na maafisa wa
ngazi za juu nchini
humo.
White House ilikataa
kuzungumzia shughuli
zozote mahususi za
kijasusi zilizofanywa
na Marekani. Lakini
maafisa wa White
House walisema
Marekani haifanyi
uchunguzi nje ya nchi,
mpaka pawepo na
sababu ya usalama wa
taifa inayoisukuma
kufanya hivyo na
kusisitiza kuwa, kanuni
hiyo inatumika kwa
viongozi wa dunia na
raia wa kawaida.
Na katika juhudi
za kuonyesha kuwa
uhusiano wa kiulinzi
kati ya Marekani na
Israel haujaathiriwa
na ripoti hizo, maafisa
walibainisha kuwa
maafisa wa Marekani
walisafiri kwenda Israel
mwezi huu kuanzisha
tena mazungumzo ya
makubaliano mapya
ya miaka 10 kuhusu
msaada wa kijeshi wa
Marekani. DW.
Nkurunziza kurejesha
mchezo wa hatari
Burundi
WAKATI mzozo nchini
Burundi ukiendela
kupanuka zaidi,
tayari kuna harufu ya
kuibuka mzozo mbaya
wa ukabila huku Rais
Pierre Nkurunziza
akiwa ameshatishia
kukabiliana na wanajeshi
wa kusimamia amani wa
Umoja wa Afrika.
Rais Nkurunziza
amesema kikosi cha kulinda
amani cha Umoja wa Afrika
ambacho kimependekezwa
kwenda kulinda amani
nchini humo, kitakiuka
katiba ya Burundi ambayo
inapinga uingiliaji wowote
iwapo kuna serikali
inayofanya kazi na hakuna
vita kati ya pande mbili.
Rais huyo amesema
Burundi itachukulia hatua
hiyo ya kupelekewa vikosi
vuya Afrika nchini kwake
kuwa ya uvamizi na ikiwa
wanajeshi wa kigeni
wataingia nchini humo,
atawakabili.
Tayari kuna taarifa
kwamba Rais Nkurunziza,
ambaye anatoka kabila
la Hutu anaonekana
kuwatenga maafisa kijeshi
wa Kitutsi, ambao utiifu
wao unatiliwa shaka.
Baadhi ya Watusti
wamedaiwa kuanza pia
kuliasi jeshi na tayari Kanali
mmoja ametangaza kuunda
kundi jipya la waasi wiki
iliyopita.
Kuasi kwa Luteni Kanali
Edouard Nshimirima,
kumeeneza uvumi kuwa
wanajeshi wengine Watusti
watamfuata na kusababisha
kuzidi kwa mzozo huo na
umwagikaji mkubwa wa
damu.
Serikali ya Burundi
imeilaumu Rwanda ambayo
ina makabila sawa na
Burundi na inayoongozwa
na Rais Mtutsi Paul
Kagame kwa kusajili na
kutoa mafunzo kwa waasi
wanaompinga Nkurunziza,
madai ambayo serikali ya
Rwanda imeyakanusha.
Bado ulimwengu
unakumbuka kwamba
zaidi ya watu 800,000
kutoka kabila la Watsusi na
Wahutu wenye msimamo
wa wastani waliuawawa
nchini Rwanda wakati wa
mauwaji wa halaiki 1994.
1/7/2016 3:17:11 PM
AN-NUUR
ANNUUR NEW.indd 6
(rosuvastatin); Zocor
(simvastatin) and Vytorin
(simvastatin/ezetimibe).
Kufuatia tafiti kadhaa
zilizohusisha makundi
makubwa ya watumiaji,
hatimaye mnamo mwezi
wa 2, mwaka 2012 taasisi
ya chakula na dawa ya
Marekani, FDA, ilitoa
orodha yenye maonyo
wa kumbukumbu.
Kutopata muda wa
kutosha wa kupumzika,
hususan wakati wa
usiku, ni chanzo
kingine kikubwa cha
kumbukumbu dhaifu.
Kwa baadhi ya viumbe,
mwanadamu akiwemo,
usiku (kwa maana ya
kuingia giza) ni muda
mahsusi kwa ajili ya
kupumzika. Viumbe
hawa ni wale ambao
hawaoni gizani. Ni
dhahiri kuwa tofauti na
mababu zetu, hivi sasa
tumepunguza sana muda
wa kupumzika usiku
kutokana na msaada
wa mataa, hususan yale
yanayotumia umeme.
Kwa viumbe ambao
hawakuumbwa
kuhangaika usiku,
lakini wanafanya
hivyo kwa msaada wa
1/7/2016 3:17:13 PM
7
SHUKRAN zote
njema ni zake Allah
Taala, Mola Mlezi
wa ulimwengu
wote. Rehema na
amani zimwendee
mtume Muhammad
(Swallalahu Alayh
Wassalam), sahaba
zake, aali zake na wote
waliofuata sunnah
yake mpaka siku ya
Qiyaamah.
Ni takriban miaka
thelathini na sita sasa
tangu kutokea kwa
vita ya Tanzania na
Uganda, almaarufu
vita vya Kagera.
Ni vita ambavyo
vilipiganwa kati ya
mwaka 1978-1979.
Kutokana na utata
uliopatikana kufuatia
vita hivyo na ambao
mpaka leo wengi wetu
hawajui vema ni nani
aliyeanzisha vita ile,
nimeamua nieleze
kwa uchache kuhusu
vita hivyo. Tusafiri
pamoja na makala
ya Inocent Kasyate,
ya Julai 26, 2009,
ambayo nimeifanyia
marekebisho kidogo ya
lugha, kwa kuongeza
na kupunguza bila
kuharibu maudhui
yenyewe.
Nani Aliyeanzisha Vita Hivyo?
Je, ni Iddi Amini au Tanzania?
Kila mwaka nchi yetu
imekuwa ikisherehekea
kumbukumbu ya
mashujaa wa vita
ya Kagera. Ni tukio
linalokumbushia juu
ya ushiriki wa nchi
ya Tanzania katika
vita pekee kubwa
iliyoigharimu nchi yetu
kwa kiwango kikubwa
kabisa. Hebu kwanza
tuangalie mtizamo wa
nje ya Tanzania juu ya
chanzo cha vita ile:
Miaka thelathini na
sita iliyopita, serikali
ya kijeshi ya Uganda
ikiongozwa na Iddi
Amin ilipinduliwa
na muungano wa
majeshi ya wakombozi
ambao walikuwa ni
waasi waliokuwa
wakiishi nchini Kenya
na Tanzania katika
miaka ya sabini
ANNUUR NEW.indd 7
Makala
AN-NUUR
ilimuua Makamu wa
Rais wa Amini, ndugu
Mustapha Adrisi;
kutokana na ajali hiyo
watu waliamini kuwa
ajali hiyo ilipangwa na
ilileta hali ya wasiwasi
mkubwa katika jeshi
la Uganda. Hali hii
ilimfanya Amini aamue
kuivamia Tanzania ili
kuhamisha mawazo
ya maafisa wa jeshi
na hata akili za
wananchi wa Uganda.
Hili linathibitishwa
na taarifa iliyowahi
kutolewa na Rais
Milton Obote ambaye
alipinduliwa na Iddi
Amin ambaye alisema
kuwa: Kuna ushahidi
wa kutosha kuwa
uvamizi wa Amini
dhidi ya Tanzania
ulikuwa ni hatua za
makusudi za Amini
kujinasua kutokana na
kushindwa kwa Amini
kulidhibiti jeshi lake.
Tatizo moja kubwa
ambalo limejitokeza
kila tunapojaribu
kuelezea kuhusu
historia ya Uganda
wakati wa utawala
wa Iddi Amini, ni
ile kukosekana kwa
mtizamo wenye
usawa na kuachana
na mitizamo iliyojaa
uzandiki (stereotyping)
wanausalama wa
Iddi Amini na pia
heshima kwa amiri
jeshi mkuu. Kutokana
na uongozi wa Amini
kuwa wa kibabe hasa
ikizingatiwa alikuwa
tayari ana maadui
wengi, vyombo vya
habari vya magharibi
vilikuwa havina
uhusiano mzuri na
Iddi Amini hasa
ikizingatiwa ugonjwa
wa kutu ya kahawa
(frost) kule Brazili
uliwezesha mauzo ya
kahawa ya Uganda
kuleta mafanikio katika
uchumi hivyo hakujali
sana nchi za magharibi.
Tarehe 28/07/2006,
kupitia kituo cha
redio cha STAR FM,
mtangazaji Semwanga
Kisolo alikumbusha
wasikilizaji kuwa
kipindi cha Iddi Amini
alihakikisha mishahara
ya wafanyakazi
wa umma ilikuwa
inalipwa si zaidi ya
tarehe ishirini na tano
na kama ingelichelewa
Iddi Amini mwenyewe
alikuwa akitoa karipio
kali kwa wanaohusika.
Anaeleza kuwa Amini
alikuwa mtu anayejali
muda kuwahi kazini
na katika matukio
muhimu ya kitaifa na
alisisitiza wafanyakazi
pia wajaliwe ili waweze
kuwahi na kutimiza
majukumu yao.
Anasema kuwa wakati
wa serikali ya Iddi
Amini, majeshi yote,
polisi, magereza, jeshi
la anga, na usalama wa
Taifa na hata maafisa
wa kati katika utumishi
wa umma, waliishi
maisha ya kujitosheleza
(comfortable): kama
kumudu kusomesha
watoto katika shule
nzuri, kuendesha
magari mapya katika
idara mbalimbali za
serikali. Magari hayo
yalikuwa kama Fiat
Mirafiori, Honda Civic,
na Honda Accord.
Kwa ufupi kipindi cha
utawala wa Iddi Amini
sarafu ya Uganda
Inaendelea Uk. 16
1/7/2016 3:17:13 PM
Habari
AN-NUUR
Inatoka Uk. 3
Inatoka Uk. 3
la Katibu Mkuu wa Chama
au mgombea pekee, ni la
chama. Lakini kila nikitizama
kinachoitwa mazungumzo,
ni mtu mmoja Vs Sita wa
upande wa pili, ambao
tafsiri yake ni kuwa hao CUF
wenyewe kamwe hawatajua
kinachozungumzwa!
Alisema Mzee mmoja na
kusisitiza kuwa hajawahi
kuona wala kusikia
mahali popote duniani
ambapo mgogoro wa
kisiasa unatatuliwa kwa
kufanywa mazungumzo
ya sura ya jambo binafsi
na bila kuzingatia uwiano
wa ushiriki wa pande mbili
husika katika mgogoro.
Hadi sasa, zaidi ya
habari za kuambiwa, CUF,
hawajui kwa uhakika nini
Maalim aliongea na Rais
M s t a a f u K i k w e t e wa l a
alichoongea na Rais JPM au
anachozungumza na wazee
Marais wastaafu.
CCM ikitangaza kujiandaa
na uchaguzi wa marudio,
kuna wasiwasi kuwa hilo
ndilo ambalo Maalim
amekubaliana na Rais
Magufuli walipokutana Ikulu
jijini Dar es Salaam.
Ukiangalia mfuatano
wa matukio baina ya kikao
cha Rais na Kamati ya CCM,
Zanzibar na kutolewa tamko
la kurudiwa uchaguzi, lakini
pia ukisikiliza msisitizo wa
CCM, Zanzibar kwamba eti
nao hawamkubali Jecha na
Tume yake, kuna wasiwasi
kwamba hapa kuna mchezo.
Alisema mchambuzi
ANNUUR NEW.indd 8
ya wananchi na kuleta
ukoloni wa watu Weusi
dhidi ya watu Weusi jambo
linalowapora Wazanzibari
haki yao ya msingi ya
kumchagua kiongozi
wanayemtaka.
W a k a t i
h u o
huo,
Maimamu
Zanzibar wameelezea
kutokuridhishwa
kwao na yanayodaiwa
kuwa mazungumzo
ya n a y o f a n y i k a I k u l u
Zanzibar kutafuta
muafaka.
Wamesema, kwanza
mazungumzo hayo
yametawaliwa na usiri
m k u b wa n a k wa m b a
mpaka sasa hakijulikani
kinachozungumzwa.
Lakini pia wakasema
kwamba mazungumzo
yamechukua muda mrefu
huku hao hao wa upande
wa CCM wanaoshiriki
mazungumzo hayo,
wakitoka wanatoa kauli
za chuki, uchochezi
na kuwakatisha tamaa
wakitawaliwa na busara,
hekima, uadilifu na
wakiweka mbele maslahi
ya taifa badala ya vyama
vyao, basi muda si mrefu
tungepata ufumbuzi wa
mgogoro huu.
Ilisema taarifa ya
J U M A Z A i l i y o s o m wa
na Katibu wake Sheikh
Muhiddin Zuber na
kuongeza kuwa, bahati
mbaya ni vikao 8 sasa
vimeshafanyika tokea
kikao cha mwanzo cha
tarehe 9 Novemba, 2015
(lakini) hakuonekani kuwa
matumaini yale wananchi
waliyoyajenga kwao kuwa
yatatimia.
Lakini zaidi anasema
kuwa pamoja na vikao
hivo kuchukua muda
mrefu sana na kufanyika
kwa siri kubwa, baadhi
ya wajumbe wanaoshiriki
mazungumzo hayo
wamekuwa wakitoa kauli
zinazoshabikia msimamo
wa upande mmoja
hali inayowatoa imani
wa aliyekuwa mgombea
urais kupitia CUF kupinga
jambo hilo. Alisema.
Katika hali kama hiyo
amesema kuwa hata ile kauli
ya Jussa kwamba CUF ipo
imara na itasimamia kura
za wananchi, inaonekana ni
kupiga porojo tu na danganya
toto.
Taarifa ya chama hicho
iliyotolewa na Ismail Jussa
kufuatia kauli ya viongozi wa
1/7/2016 3:17:14 PM
9
R A I S
J o h n
Pombe Magufuli
( JPM) amejitahidi
kutengeneza mazingira
ya kuaminiwa na
ameaminika.
Kila kona ni slogan za
Rais Magufuli. Kila mtu
anamuunga mkono Mh.
Rais Magufuli.
Kamualika Mufti
Zuber wa BAKWATA
akamsifia sana.
Kipi tena mnataka
Wa i s l a m u z a i d i ya
heshma aliyopewa Mufti
kukaribishwa Ikulu?
AWA L I y a y o t e
naomba nitangulie
kusema na mapema
kuwa yawezekana
wakatokea watakao
tofautiana nami
na pengine hata
kunishambulia. Hii ni
kwasababu kila mmoja
ana haki ya kuwa na
mtazamo wake na hata
ujasiri wa kufumbia
macho dhulma
pale inapofanywa
kwasababu dhulma
hiyo haimgusi yeye
wala familia yake.
Wakati tunaelekea
kupata uhuru mwishoni
mwa miaka ya 1960,
wengi tunakumbuka
k u l i k u wa
n a
mgawanyiko miongoni
mwa wapigania uhuru.
Mgawanyiko huu
ulipelekea kuwa na
vyama viwili, TANU
na AMNUT. Japo
AMNUT haikuwa na
nguvu sana kiasi cha
kuitikisa TANU, bado
ukweli unabaki kuwa
yalikuwepo makundi
mawili tofauti. Moja
katika mtazamo wa
AMNUT ilikuwa
kwamba, ilikuwa
ni mapema kwa
Tanganyika kupewa
uhuru, kwakuwa kwa
hali ilivyokuwa kwa
w a k a t i u l e , TA N U
kupewa uhuru ilikuwa
kuwapa nafasi Wakristo
wanufaike na kufaidika
na uhuru peke yao huku
Waislamu wapigania
uhuru wakiishia kuwa
raia wa daraja la tatu.
Kwa maoni yao, ilikuwa
n i b o r a k u c h e l e wa
kupata uhuru ili kupata
muda wa kusawazisha
tofauti zilizokuwepo,
hasa za kielimu, baina
ya wananchi wa dini
kuu mbili, Uislamu na
Ukristo.
ANNUUR NEW.indd 9
Makala
AN-NUUR
RAIS Dk. John Magufuli (kulia) akiwa na Muft wa BAKWATA Sheikh Abubakar Zuberi.
serikali ya Awamu ya
Kwanza, imebakia kuwa
historia chungu kwa
Umma wa Kiislamu
nchini Tanzania. Kama
alivyojisemea Remmy
Ongala, imekuwa
ni kilio cha samaki,
machozi yamekwenda
na maji. Hakuna hata
anayesikia na kujali kilio
cha Waislamu katika
walioshikilia mpini.
Wakati wa kamapeni,
Mh. John Pombe
Magufuli mara kadhaa
alisisitiza kuwa
hatowabagua watu kwa
rangi zao, kwa makabila
yao wala kwa dini zao.
Hii ilileta faraja kuwa Mh.
Magufuli ataleta usawa
na haki katika serikali
yake. Hata hivyo, Rais
John Pombe Magufuli
(JPM) nae ameingia kwa
gia ileile. Amejitahidi
kutengeneza mazingira
ya kuaminiwa na
ameaminika. Kila
kona ni slogan za Rais
Magufuli. Kila mtu
anamuunga mkono
Mh. Rais Magufuli. Sasa
katika mazingira haya
na katika kuzingatia
historia na uzoefu wa
mambo wakati wa
Mwalimu Nyerere, kuna
haja ya kuwa makini.
Katika mazingira
haya yanayoendelea
kujiumba, iwapo
atatokea wa kulalamika
kwamba kuna hujuma
dhidi ya kundi fulani,
iwe la kidini au kikabila,
watu watamshangaa.
Na ni hivi majuzi tu
kakutana na Mufti Zuber
wa BAKWATA naye
akamsifia sana. Kipi tena
cha kuthibitisha kuwa
Rais ni mtenda haki,
asiye bagua watu zaidi
ya heshma aliyopewa
Mufti kukaribishwa
Ikulu?
Mara baada ya
kuapishwa kuwa
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania,
Mh. Magufuli alianza
kwa hotuba kali sana
wa k a t i a k i l i z i n d u a
Bunge la Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania.
Hotuba ile ilileta hamasa
ya hali ya juu sana na
hata kuamsha ari ya
uungwaji mkono kutoka
kwa Watanzania wa
ngazi ya kati na chini.
Kilichofuatia ni kuanza
na operation aliyoiita
operation ya kutumbua
majipu! Operation hii
ilifanyika kwa kuanzia
bandari na Mamlaka ya
Mapato Tanzania (TRA).
Msisimko na shangwe
za uungwaji mkono
zilisikika kila kona ya
Tanzania. Haikuchukua
muda, akaanza
kuonekana kama mtu
aliyekuja kulikomboa
taifa letu Naam,
mazingira yakawa
wazi kufanya atakalo
n a h a k u n a m t u wa
kulalama wala kudadisi.
Kwanini? Kwasababu
ameaminiwa kuwa yeye
anafanya kwa maslahi
ya taifa. Yeyote atakaye
nyoosha kidole kudadisi
au kuhoji, anaonekana
m t u wa a j a b u t e n a
anataka kukwamisha
harakati za kizalendo.
Ubaya wa mazingira
kama haya ni kuwa
huenda watu wakawa
wazito kumsaidia
Mheshimiwa Rais pale
wanapohisi kwamba
mambo hayaendi sawa.
Wingu la umaarufu
na kuungwa mkono
litawazuiya watu
k u wa wa k we l i k wa
Rais kwa kuhofia
yasije yakawakuta
yaliyomkuta Sheikh
S u l e i m a n Ta k a d i r i .
Lakini kwa Mheshimiwa
Rais naye, kwa kusikia
nyimbo na ngonjera za
sifa tu na kuungwa
mkono, anaweza
asipate fursa ya
kutizama pale penye
dosari ndogo ndogo
ambapo pangehitaji
marekebisho.
Binafsi naamini
kwamba, haitakuwa
t u n a m s a i d i a
Mheshimiwa Rais JPM
iwapo hatutasema pale
tunapoona kuwa mambo
hayaendi sawa kama
ilivyo dhamira njema
ya Rais. Mheshimiwa
Rais JPM ni binadamu
na katika ari na hamasa
ya kulitumikia taifa
anaweza kujikwaa
hapa na pale. Na
hivyo ni wajibu wetu
kumsaidia Rais wetu
kipenzi. Na hapa mimi
nitazungumzia yale
ambayo nadhani hata
katika mazungumzo
yake na Mufti Zuberi
hawakuyagusa.
Uteuzi wa Baraza la
Mawaziri
Uteuzi wa Baraza
la Mawaziri, kwangu
mimi, umeacha maswali
mengi kuliko majibu.
Japo inashangaza
Wa i s l a m u k u p i g wa
Inaendelea Uk. 15
1/7/2016 3:17:18 PM
10
Na Omar Msangi
UKIENDA Zanzibar
ukifika pale bandarini
Dar es Salaam, utakutana
na kijana kashika kipaza
sauti akiwahimiza abiria
kwamba saa zao, simu,
m i k a n d a ya s u r u a l i ,
sarafu na vitu vya chuma,
waweke ndani ya mabegi
yao, tayari kwa ukaguzi.
Kwa nini wanafanya
hivyo? Hofu ya ugaidi
ndiyo imetufikisha
hapo. Baada ya hofu,
watu hawana tena muda
wa kujiuliza, zoezi lile
linamzuiya vipi gaidi?
Kiasi wiki tatu zilizopita
zilisambaa habari katika
vyombo vya habari vya
Kenya na vya kimataifa
juu kilichodaiwa ushujaa
na uzalendo wa akina
mama wa Kiislamu
ambao walichukua
hatua za kuwanusuru
abiria wenzao Wakristo.
Kinachoelezwa ni kuwa
basi lililokuwa likisafiri
kutoka Nairobi kwenda
Mandera, lilivamiwa na
magaidi wa Al-Shabaab
wapatao 15. Wakaingia
ndani ya basi wakiwa
na bunduki nzito AK4 7 . Wa k a a n z a z o e z i
la kuwatenganisha
Waislamu na Wakristo
ili wawauwe Wakristo.
Hata hivyo, akina mama
Waislamu wakavua hijabu
zao na kuwapa Wakristo
wavae, kwa hiyo zoezi la
kuwatambua Wakristo
likakwama Al-Shabaab
wakakimbia.
Ni katika taarifa ya
habari, katika televisheni
zetu, unamkuta mtangazaji
anatangaza habari hizo
kwa mkazo akiwaaminisha
wasikilizaji na watazamaji
kuwa hizo ni habari za
kweli kabisa! Ile akili
ndogo tu ya mtu kujiuliza,
hivi hao akinamama
wakivua hijabu na
kuwapa Wakristo wavae,
Al-Shabaab walikuwa
hawaoni? Kitisho cha
ugaidi kimewaondolea
hata kile kiwango cha
chini kabisa cha kufikiri
na kutumia akili.
Kuna lile tukio la
Paris ambapo ilidaiwa
kuwa magaidi walilipua
mabomu katika uwanja wa
mpira. Unatizama taarifa
ya habari au unasoma
gazeti, imewekwa picha ya
mashabiki wapo uwanjani,
wengine wanaongea na
simu wakicheka, wengine
wamekaa wanasogoa.
Ilimuradi hakuna ishara
yoyote ya taharuki. Lakini
mwandishi anakuambia
kuwa hawa ni mashabiki
wanaosubiri kuokolewa
ANNUUR NEW.indd 10
Makala
AN-NUUR
RAIS Barack Obama wa Marekani (kushoto) akiwa na Rais Vladimir Putin wa Urusi.
na polisi wa uokozi baada
ya magaidi kupiga bomu!
Hivi kweli pale uwanja
wa taifa wakati wa mechi
liripuke bomu, yupo
mtu atasubiri waje polisi
kumuokoa? Lakini yote
hayo, wala watu hawana
tena muda wa kufikiri.
Ngoma ya kitisho cha
ugaidi iliyopigwa kwa
muda mrefu, ishawatia
ujinga uliokusudiwa.
N a m k u m b u k a
m wa l i m u wa n g u wa
inorganic chemistry Chuo
Kikuu cha Dar es Salaam
m wa k a 1 9 8 4 , P r o f e s a
Saxena akisema kuwa
yeye alikuwa hatoi mtihani
mgumu maana akitaka
wanafunzi wake wote
wafaulu. Kwa hiyo mtihani
wake anaokupa unahitajia
kutumia asilimia 10 tu ya
akili yako, kufaulu. Sasa,
ukifeli ujue kuwa sio kosa
lake. Jilaumu mwenyewe
kwa kushindwa kutumia
japo sehemu moja tu
ya kumi ya akili yako.
Inavyoonekana katika
hili la kitisho cha ugaidi,
t u m e f i k i s h wa m b a l i .
Vichwa havifanyi kazi
tena.
Aliwahi kusema Josef
Stalin kuwa-The easiest way
to gain control of a population
is to carry out acts of terror."Akimaanisha kwamba njia
nyepesi ya kuwadhibiti
watu na kuwapelekesha
unavyotaka, ni kuwapa
kipigo cha ugaidi,
kuwaundia ugaidi. Kwa
nini? Kwa sababu, Fear
of Terror Makes People
Stupid ikiwa na maana
kuwa kitisho cha ugaidi
huwatia watu ujinga.
Kinawaondolea kufikiri
na kutumia akili zao. Na
ndio maana Rais Franklin
Roosevelt katika hotuba
ya k e ya k wa n z a k wa
wananchi wa Marekani
alisema kuwa kama kuna
jambo la kuogopa, basi ni
hofu yenyewe.
Kwa bahati mbaya katika
ulimwengu tunaokwenda
nao wa utandawazi na
ubeberu wa ma-neocons,
wanaotengeneza hofu
na kitisho cha ugaidi
ni vyombo vya dola ili
k u k i d h i m a t a k wa n a
agenda za mabeberu.
K a t i k a v i wa n g o v y a
kimataifa, wametegeneza
kitisho cha ugaidi wa
Saddam Hussein na
Al-Qaida wakapata
sababu ya kuzipiga na
kuzisambaratisha Iraq na
Afghanistan. Wakaunda
kitisho cha Gadhafi kuwa
anauwa watu wake, na
sasa cha Bashar Assad.
Libya ishasambaratishwa,
Syria ipo chumba cha
wagonjwa mahututi (ICU).
Ili uone kitisho cha
ugaidi kinavyotia
watu ujinga, tizama IS
wanavyopambwa kwamba
wana nguvu za kutisha
na jeshi lisilowezekana.
Kwa zaidi ya miaka miwili
Marekani na washirika
wake wanajitahidi
kuwaangamiza, lakini
wapi! Bado wana nguvu
na uwezo wa kupenya
h a d i Pa r i s wa k a p i g a
n a wa k a o n d o k a b i l a
kukamatwa! Na watu
wanaamini. Wala mtu
hajiulizi, kama ni kweli
hao IS wana nguvu
kiasi hicho, hizo silaha
wanapata wapi?
Marekani, Uingereza
na washirika wao,
wanadai kupeleka ndege
za kivita kuwapiga IS
kwa miaka miwili sasa,
IS wanadunda tu. Na
watu wanaamini kuwa
Marekani na washirika
wake wamewashindwa
IS. Ukiwaambia kuwa
Marekani inafanya usanii,
haiwapigi IS kwa sababu
ni vijana wake, wanaona
kama unafanya masikhara.
Lakini sasa imefika
mahali, Vladimir Putin
kafanya kweli. Alianza
kwa kutoa kauli kwamba
ule mtindo wa mtu mmoja
(Marekani) kuwaburuza
walimwengu wote na
kuwafanya wengine
wajinga, ufikie mwisho.
1/7/2016 3:17:19 PM
11
Inatoka Uk. 10
na Qatar. Mwandishi
Finian Cunningham,
akizichambua Saudi
Arabia na Qatar katika
mchezo huu wa ugaidi
anasema: Saudi Arabia and
Qatar, serves as a conduit
for American CIA weapons
to the more known terrorist
outlets.
Hili BBC wamekwepa
kulisema badala yake
wanaeleza kana kwamba,
wanaokimbia ni wapinzani
wa kawaida wa Bashar,
Voice of America (VOA)
wakimpa Zahran Alloush,
cheo cha rebel leader.
Ukija katika nchi
zetu, ujinga ni ule ule,
tena wenye maangamizi
makubwa kwa nchi. Hivi
sasa Kenya, vipo vikosi
maalum ambavyo hupokea
amri na maelekezo kutoka
makachero wa nchi za
Ulaya, Marekani na
Israel (Western Security
Agencies), sio kutoka kwa
Amiri Jeshi Mkuu wa
nchi wala kwa wakuu wa
vyombo vya usalama vya
nchi hiyo. (Tazama: Inside
Kenyas Death Squads).
Kwa ujumla kutokana na
propaganda ya kitisho
cha ugaidi, serikali zetu
z i m e f i k i s h wa m a h a l i
p a k u a m i n i k wa m b a
hatupo salama mpaka
tupate ulinzi kutoka kwa
mabeberu. Na kwa sababu
hiyo, tunawaruhusu
kuweka kambi zao za
kijeshi (military bases)
na kuwa na kauli juu
ya majeshi yetu. Zipo
nchi hivi sasa wanajeshi
wao wamekuwa kama
mgambo wa kuwabebea
mikoba makamanda
wa jeshi la Marekani.
Kupitia kitisho cha
ugaidi, tunapumbazwa,
tunapumbazika,
tunafanikisha agenda
ya beberu kusambaza
makucha yake ya kijeshi
duniani (Network of Military
Bases) kufikia lengo lake la
World Hegemony.
Tunachopata nini? Nchi
huru inafikishwa mahali
inakuwa koloni kasorobo.
Haina sauti hata juu ya
rasilimali zake. Haiwezi
kuamua ifanye biashara
na nani katika madini
yake na mafuta/gesi yake.
Na wenyewe hawafichi.
Wanasema wazi kwamba
wa n a c h o l e n g a k a t i k a
kusambaza makucha yao
ya kijeshi ni namna mbili.
Kwanza kudhibiti uchumi
wa dunia na masoko yake
ya fedha. Pili, kudhibiti
na kukomba rasilimali
zote muhimu. Lakini kwa
ujinga tuliokwishatiwa
kutokana na kitisho cha
ANNUUR NEW.indd 11
Makala
AN-NUUR
ugaidi, tunawakaribisha
kwa mikono miwili kwa
hoja kuwa wanatusaidia
kupambana na ugaidi.
Ndio wataalamu wetu
wa kutufundisha na
kutuelekeza namna ya
kukabiliana na Al-Qaida
na Al-Shabaab!
Lakini baya zaidi,
ili ugaidi ukolee,
m t a l e t e wa u g a i d i
ambao utaporomosha
na kuondoa Amani
mliyokuwa nayo.
Matukio kama ya
Westgate, Garrisa na
Mandera, lazima yaje
m a r a k wa m a r a i l i
kukumbushwa kuwa
m a g a i d i wa p o . N a
k wa b a h a t i m b a ya ,
wala hamtajua
n a n i a n a wa p i g a a u
ya pombe, hotelini,
mtaani au majumbani)
wanawafikisha polisi,
lakini hawawasajili,
bali huwapeleka porini
n a k u wa p i g a r i s a s i
(Elimination Programme).
Ndio maana katika
ile documentary ya
Aljazeera wakapewa
jina la Death Squad.
N i n a a n d i k a h a ya
nikizingatia kuwa kuna
Watanzania wenzetu
wamo mikononi mwa
vyombo vya dola
kwa muda mrefu sasa
wakikabiliwa na tuhuma
za ugaidi. Watuhumiwa
hawa unaweza
kuwagawa katika
makundi mawili. Wapo
ambao inawezekana
hawana hatia kabisa.
Ni wahanga ama wa
njama za makusudi
au wameangukia
katika bahati mbaya
ya mtego wa panya.
L a k i n i ya we z e k a n a
wapo ambao kulikuwa
na sababu za msingi
za kuwatilia shaka na
pengine walishafanya
au walikuwa mbioni
k u f a n ya m a m b o ya
hatari. Hawa nao ni
wahanga tu wa mpango
mzima wa maadui.
Wametumbukia kwa
1/7/2016 3:17:20 PM
12
AN-NUUR
KATIKA makala za
nyuma niliandika
juu ya wahubiri wa
Kikristo waliokuwa
wanaletwa katika
ukanda wa Afrika
ya Mashariki ikiwa
wengi wao walikuwa
wajuzi wa kuielewa
Quran na walikuwa
wanakizungumza
Kiarabu kwahio
walikuwa wanaifanya
kazi yao ya uhubiri
kwa kuelewa vipi
kukabiliana na
Waislamu wengi hasa
wale ambao walikuwa
wakazi wa mwambao.
Quran ya mwanzo
kwa lugha ya Kiswahili
iliandikiwa mwaka
wa 1923 na Padri
Dale ambaye alifanya
kazi nzito ya kutafsiri
Quran kwa Kiswahili
ambayo Kiswahili
chake kilikuwa cha
watu wa Pwani.
Tafsiri hiyo ilikuwa na
kurasa 542 na kurasa
zisopungua 142 ikiwa
ni Sharhi (maelezo
ya ufafanuzi) Quran
hii hasa ililengwa
kwa wahubiri wa
Kikiristo walioajiriwa
na University
Mission to Central
Africa (UMCA),
iliyoanzishwa mwaka
1873. Wahubiri
hao wakiitumia na
kuwashtua Masheikhe
namna walivyokuwa
wanaielezea, hio ikawa
ndio Quran iliopo kwa
Kiswahili.
Tafsiri hii ya Padre
Dale ililenga zaidi
kuikingia kifua
Ukiristo na sherhe
yake ilikuwa imezama
sana kuwa nje ya
ukweli wa Kiislamu.
Kutokana na hayo,
ikaonekana kuwa kuna
haja haraka kabisa
kupatikana kwa tafsiri
ANNUUR NEW.indd 12
ya Kiswahili ambayo
imeandikwa na
Waislamu wenyewe.
Hapo ndipo Sheikh
Mubarak bin Ahmed
akiwa kiongozi mkuu
wa Makadiani wa
Afrika ya Mashariki
akaanza kuandaa
matayarisho ya
uandikaji wa Tafsiri
ya Quran kwa
Kiswahili na katika
mwaka wa 1942.
Tafsiri hio ikapelekwa
kwa mchapishaji na
kuhakikiwa katika
kamati ya lugha ya
Kiswahili iliokuwa
ikijulikana kwa jina
la Inter-Territorial
Swahili Language ili
iweze kukubalika na
kusomeka kirahisi na
Waswahili. Kamati
hiyo ilithibitisha kuwa
lugha iliotumika ni
lugha ya Kiswahili
bulbul na inakubalika
kisha tafsiri hiyo
ikapelekwa kwa
viongozi mbalimbali
wa Makadiani wa
Afrika ya Mashariki
na kukubaliwa kuwa
lugha iliyotumika
inakidhi haja.
Sheikh Amri
Abeid malenga wa
lugha ya Kiswahili
maarufu wakati huo
katika Tanganyika na
ukanda wa Afrika ya
Mashariki, aliokuja
kuheshimika na
kupewa jina uwanja
wa mpira wa Arusha
kwa jina lake Sheikh
Amri Abeid Stadium.
Sheikh Amri Abeid
akiwa muumini
wa madhehebu ya
Makadiani alipewa
mafunzo ya dehehebu
hilo ambalo liliasiwa
nchini India,
alifanyiwa mpango
wa kwenda kupata
taaluma ya ndani
ya madhehebu
hio na alikwenda
nchini Pakistan kati
ya mwaka wa 1954
hadi 1956 huko
alipikwa vya kutosha.
Wakati Sheikh Amri
Abeid anakwenda
Pakistan, Makadiyani
walikuwa tayari
wameshatoa nakala ya
Quran ya Kiswahili
ambayo inakingana
na mwenendo
wa kuwa Mtume
Muhammad (SAW)
ndio Khatim yaani
mwisho wa Mitume
wote. Sheikh Amri
Abeid alikuja kuwa
mtetezi mkubwa wa
tafsiri hii na wafuasi
wa madhehebu ya
Suni kuemewa na
kuonekana kuwa kuna
haja ya kutengenezwa
tafsiri ambayo itakidhi
haja ya watu wa
madhehehbu hio ikiwa
idadi yao ni wengi
katika ukanda wa
Afrika Mashariki kama
yalivyokuwa madhebu
ya Malik kuwa na
wafuasi wengi katika
Afrika ya Kaskazini.
Nchini Kenya tafsiri
ya Quran iliyoegemea
madhehebu ya Sunni
ilikuwa inatafsiriwa
kwa khatua na Sheikh
Al-Amin Ali Mazrui,
lakini haikuwa kamili
na ndipo Sheikhe
Abdalla Saleh Farsy
akaanza kuitafsiri
Quran kwa Kiswahili
katika mwaka wa 1956
kwa kuirejeza tafsiri
ya Makadiyani. Mmoja
kati ya wanafunzi
wake Sheikh Abdalla
Saleh Farsy, marehemu
Shariff Abdulwahab
Alawy ambaye nilipata
fursa ya kujadiliyana
naye katika nyakati
mbalimbali, alinambia
kuwa Sheikh Abdalla
Saleh aliwateua
wanafunzi wake
watano akiwa yeye
mmoja kati ya hao
na kuwapa kazi
ya kila baada ya
darsa kutalii nao na
kutafsiri baadhi ya aya
kuzitafsiri naye Sheikh
Abdalla alikuwa kila
aendapo alikuwa
na kitabu chake
maalumu ambacho
alikuwa ananukulu
na kufanya tafsiri.
Alikuwa na mkoba
wake maalumu ambao
humo ulikuwa mfano
wa maktaba, kwani
wakati wote alikuwa
na rejea (references)
mbalimbali
zilizoshikamana na
Uislamu na tarekhe
yake. Kwahivyo
alianza kazi hii kwa
juhudi kubwa sana na
alikuwa akiwasiliana
na watu mbalimbali
ikiwa Kenya,
Pakistan na maeneo
mengineo. Kazi yake
iliweza kukamilika
ilipofika mwaka wa
1961 alikuwa tayari
kishakamilisha
juzuu 12 na kuweza
kuchapishwa. Sheikh
Abdalla alipata moyo
kuona kazi yake kuwa
sasa imo kwenye
mikono ya Waislamu
na kueleweka maelezo
ya kina ya Quran
na kuonyesha yale
mapunguku ya
Makadiyani. Sheikhe
alikuwa na upungufu
wa kifedha lakini
juu ya kuwa na
upungufu wa kifedha
wa kumwezesha
kuichapisha kopi
yake ya kwanza lakini
hayo hayakumsitisha
kuiendeleza kazi yake
hio na ilipofika mwaka
wa 1969 chini ya
udhamini wa Islamic
Foundation ya Kenya
ilitoka tafsiri hio
kwa mara ya kwanza
maarufu ambayo
Sultan wa Qatar
alisaidia pakubwa
kifedha kuweza
kuchapishwa nakala ya
mwanzo (first edition)
na kutolewa nakala
4,000 kugaiwa bure na
nakala 3,000 zikawa
zinauzwa kwa shilling
3,000.
Islamic Foundation
ya Nairobi yenye
kuunga mkono Jamaat
al Islam ya Pakistan,
ndiyo iliyosimamia
upigwaji wa chapa
kwa mara ya mwanzo
Tafsiri ya Sheikh
Abdullah Saleh
Farsy, na kumpatia
tafsiri hiyo gwiji
mwanaharakati wa
Pakistan Sayyid Abdul
Ala Maududi ambaye
baada ya kufanyiwa
tafsiri na kufahamu
yalioandikwa,
akaikubali tafsiri ya
Qurani Takatifu ya
Sheikh Abdalla na kwa
upande wake Sheikh
Abdullah Saleh Farsy
akaitegemea tafsiri ya
Maududi inayoitwa
'Qur'an Fahmi Ke
Bunyadi Usul' (Msingi
wa kuifahamu Quraan), na Syd Maududi
akaombwa utangulizi
wa tafsiri yake hio
Tafhim Al-Qur-aan
itumike kwenye
utangulizi wa Qurani
Takatifu ya Sheikh
Abdalla hapo ikawa
Waswahili wamepata
tafsiri iliokamilika.
Sambamba na tafsiri
hii ipo tafsiri ya
Kiswahili ilioandkiwa
na Mzanzibari
mwengine Sheikh Ali
Muhsin Barwany kwa
jina la Al Muntakhab
Qurani Takatifu
(quranitukufu.net).
1/7/2016 3:17:21 PM
13
SAFARI hii makala hii
itajaribu kuangaza utupwaji
wa taka na mbinu za
kutumika. Taka zinakuwa
mazonge kwetu kutokana na
kushindwa kujuwa namna
ya kuzitupa. Tuzitupe vipi
na tuzitupe wapi?
Jiulize wewe unaosoma
makala hii unazitupaje taka
ulizonazo ikiwa kutoka
unapoishi, kiwandani kazini
au popote pale. Jee, unazitupa
popote pale utapoona kuna
upenyu utakuwezesha
kutupa taka, au unazitupa
katika msingi (mtaro) wa
maji, au unazitupa katika
maeneo ya skuli ambapo
baada ya masomo huwa
hakuna usimamizi au
unazitupa pembeni mwa
jirani yako au unazitupa
palipotengwa taka tuzitupe,
au unazifukia au unazichoma
moto?
Kama ningeweza kupata
watu 100 wakawa wakweli
kunambia wanavyozitupa
taka, naamini jawabu
nitayoipata zaidi ya asilimia
90 watanipa jawabu
isioridhisha. Ukijiuliza
kwanini ikawa hivyo? Moja
kati ya jawabu nikuwa ni
dharau na watu kuona mji,
nchi, makazi yao sio lolote lile
na wao kutokuwa na wajibu
wa usafi kwa kuwa wapo
wahusika wanaowajibika
kusafisha wakiwa wanalipwa
na serikali. Fikra hizi ni
potofu zinahitajika kupatiwa
ufumbuzi kwa haraka kabisa
ili dhana nzima ile ya yale
Yawe Endelevu ipatikane.
Wa t u wa n a f i k r a
mbalimbali fikra walizonazo
zinatafautiana na fikra za
b i n a d a m u k u n a wa k a t i
zinahitajika kutafautiana
na kuna wakati zinahitajika
ziwe za aina mmoja. Kwenye
uvumbuzi hapa ndipo fikra za
mwanadamu zinatafautiana
n a k u t a f a u t i a n a k wa k e
kunapelekea binadamu
kufanya tafiti na kuweza kuja
na mambo yenye manufaa.
Lakini kuna sehemu fikra
za wanadamu hazitakiwi
kutafautiana na ukitaka
kutafautiana na fikra za
pamoja huwa ni majanga.
Kwa mfano kupiga chanjo
ya Polio, jambo hili ni lazima
wala hakuna kutafautiana
na utapo jifanya hutaki ni
janga litakalo kukabili kwa
mtoto atakaye kuja kuzaliwa,
tumeyaona haya Nigeria.
Sasa sisi tukiwa kama ni
wananchi tumo katika taifa
letu kuna haja kabisa fikra
zetu ziwe zenye kukubaliana
kwa yale yalio lazima tuwe
tunakwenda sambamba kwa
uslama na maendeleo yetu.
Tunatupa taka kila kukicha
na tunazlizalisha kila siku
ikiwa kitu hicho kila siku
unakizalisha kisha inabidi
ukitupe itakulazimu uwe na
mbinu yakinifu zilizokuwa
mujarab kufanya hivyo.
Huko nyuma tushasema
namna ya kuzigawa hizo
taka na kuzitupa, sasa
lakujiuliza wahusika
ANNUUR NEW.indd 13
Yawe endelevu-3
taka anazozizalisha.
Ninapoishi mie kulikuwa
na jaa kubwa ambalo taka
zote za Manispaa zikitupwa
hapo, lakini mji ulipotanuka
na kukua imebidi jaa hilo
liondoshwe lisogezwe nje
ya mji kidogo na huko
liliposogezwa kutokana
na kutotumika utaalamu
wa kuzitupa taka, matokeo
yake katika kipindi kifupi
eneo hilo lilijaa kwa kuwa
gari la Manispaa linachukua
hizo taka na kisha kuzitupa
kwenye shimo ambalo lilipata
kuchimbwa mawe, gari la
Manispaa linabeba taka
kisha huja gari la kuzifukia
na kumwagwa mchanga
na nyengine huchomwa
moto. Hapo utajiuliza dunia
ndivyo inavyozidhibiti taka
kwa mtindo huo? Haya
nayazungumzia eneo la
kisiwa cha Unguja lakini
AN-NUUR
1/7/2016 3:17:22 PM
14
Na Shaban Rajab
SIKU hizi matukio ya
watumishi wa majumbani
(yaya) kuwatesa watoto
yameonekana kuwa ni
m e n g i n a k u wa g u s a
watu wengi. Yawezekana
matukio na namna
hii yamekuwepo kwa
kipindi kirefu siku
za nyuma lakini
yalikuwa hayafamiki au
kugundulika. Na hata
yakigundulika taarifa
zake ziliishia eneo
lilipotokea tukio husika.
Lakini kutokana na
kasi ya kukua sayansi na
teknolojia ya mawasiliano,
wingi wa vyombo vya
habari vya kielekroniki
kama mitandao ya kijamii
na televisheni na internet,
siku hizi matukio haya
yamekuwa yakigundulika
mapema na kufahamika
kwa haraka sana. Matukio
haya ya utesaji watoto
mbali na kuzua hisia za
hofu na hasira miongoni
mwa jamii, lakini
yamewafanya wazazi,
hasa kina mama kufikiria
upya ni nani wa kumuajiri
kuwa yaya.
K wa k u wa f a m i l i a
nyingi wazazi hawashindi
nyumbani, yameripotiwa
matukio ya yaya
kuwatwesa watoto katika
madimbwi ya maji, yaya
kumweka mtoto kwenye
jokofu na yeye kutoweka,
wakati mwingine yaya
kumweka mtoto mchanga
hata kwenye jiko la oven.
Ai dha yames h uh udia
matukio mengi ya watoto
kunyimwa chakula,
kupigwa, kutelekezwa
nyumbani bila uangalizi
huku yaya akikata
mitaa. Matukio ya wizi
ndio hayaelezeki. Hayo
ni baadhi tu ya madhila
ambayo hufanywa na
watumishi wa majumbani
kwa watoto wakati wazazi
wao hawapo nyumbani.
Zipo sababu nyingi
ambazo zinaweza kuwa
chanzo cha kuwepo
kwa ufedhuli huu kwa
watoto. Pande zote mbili,
mwajiri na mwajiriwa
z i m e k u wa n a k a s o r o
katika mahusiano yao.
Upande mmoja unaweza
kuwa sahihi na upande
wa pili ukawa na matatizo
kulingana na mazingira ya
pande husika.
Kwa mfano kwa upande
wa Mayaya, mojawapo
ya kasoro au udhaifu
unaoweza kuwa sababu ya
malezo mabaya ya watoto
inaweza kuwa historia ya
maisha pamoja na malezi
aliyopitia yaya katika
makuzi yake.
Yaya wengine wametoka
katika familia zenye malezi
yasiyokuwa na madili.
ANNUUR NEW.indd 14
MAKALA/MASHAIRI
AN-NUUR
wasiyostahili.
Watoto anaweza kuwa
wa t u n d u s a n a , k i a s i
k wa m b a a n a y e wa l e a
anaweza kuwa na kipimo
cha adhabu ya kiungwana
mradi asiwaumize
au kuwadhuru, ili
kuwajengea hofu
wasirudie makosa. Lakini
wengi hawawezi kufanya
hivyo hata kama watoto
watamkosea. Atanyamaza
hadi afikishe ujumbe kwa
mama mwenye nyumba.
Lakini alishuhudia mtoto
a n a ye m l e a a m e f a n ya
kosa na kweli linahitaji
kumchapa kidogo au
kumfinya kama mwana
familia na hata wazazi
wakirudi akawaeleza kisa
chote. Katika mahusiano
mabovu ya namna hii,
ndio maana tunashuhudia
kuna matukio mengi ya
kuteswa watoto, ambao
hawana makosa. Watoto
wanadhulumiwa na
k u k o s a m s a a d a k wa
s a b a b u ya u m r i wa o
mdogo.
I m e f i k a b a a d h i ya
wazazi hasa wale wenye
uwezo, kuanza kutumia
teknolojia ili kuhakikisha
usalama wa watoto wao
wanapokuwa nje ya
nyumba, badala ya kujenga
magusiano ya kiutu baina
ya pande mbili hizo.
" N i k i wa n a u w e z o
nitaweka kamera kwa
n y u m b a ya n g u . K wa
sababu kama umeweka
k a m e r a uk i wa k a z i ni
hautakuwa na wasiwasi.
Anazungumza mzazi
mmoja wa huko Uganda.
L a k i n i m s h a u r i wa
mambo ya jamii Bi. Anne
Nafula anaona kwamba
k u w e k a m i t a m b o ya
kamera sio suluhu la
kutosha kwa masuala
kama haya.
"Lazima mwajiri aelewe
k wa m b a m f a n ya k a z i
nyumbani sio mfanyakazi
tu, anafaa amuweke karibu
kama mmoja wa ukoo au
jamii ili ajione ni sehemuya
familia na amwangalilie
mtoto kwa njia nzuri,
lakini ukimchukulia
kwamba hana thamani
katika nyumba yako, basi
atafanya vile anavyopenda"
Alibainishamtaalam huyo.
Aidha kulingana na
ripoti za vyombo vya
habari ni wazi matukio ya
yaya kuolewa au kupata
watoto na waajiri wao
yameongezeka.
Haya ni matokeo ya
wazazi kuthamini zaidi
kazi na kutumia muda
wote kazini kuliko
mahusiano ya kifamilia. Bi.
Nafula analaumu baadhi
ya wanawake walioolewa
kwa kutelekeza majukumu
yao na kumwaachia yaya
kufanya shughuli zote
za nyumba hata zile
zinazochochea mahusiano
ya mume na mke.
M a j u k u m u
yanayostahili kufanywa
n a m k e wa n y u m b a ,
yanapatiwa msichana
w a k a z i . Wa n a w a k e
we n g i wa m e s h i n d wa
na majukumu yao hata
ya kulea watoto, hata
kuangalia waume zao. Na
wengi kwa kuzoe huduma
z a Ya ya , wa m e k u wa
wavivu kupita kiasi.
Na baadhi ya wanaume
wenye husuda ya mapenzi
na wakayakosa kwa wake
zao, hawaangali sana
urembo linapofika swala
la mapenzi, wanaangalia
yule anayemletea huduma,
kumpelekea maji ya kuoga,
maji ya kunywa nk.
Sote tunakiri kwamba
kitendo cha kumfanyia
mtoto mateso, ni uhalifu na
unyama mkubwa. Adhabu
yake ni jela kisheria iwapo
mtuhumiwa atapatikana
na hatia. Nchi9ni Uganda
mtuhumiwa huadhibiwa
kwa kufungwa hadi miaka
15 gerezani wakati nchini
Kenya adhabu ya kosa hilo
ni zaidi ya miaka kumi.
Lakini ifahamike kuwa
kukinga ni bora kuliko
kuponya. Ni vyema wenye
nyumba kujenga urafiki na
watumishi wao. Hapo hata
wakitokea wale ambao
hawavumiliki, basi ni haki
ya mwajiri kumfukuza
au kumchukulia hatua za
kisheria mtumishi wake.
Kwa kufanya hivyo,
kwa kweli kutapunguza
kwa kiwango kikubwa sio
tu kuteswa kwa watoto,
bali pia kuwa na familia
imara.
1/7/2016 3:17:23 PM
15
Inatoka Uk. 9
ganzi na kushindwa
kupaza sauti, pengine ni
kutokana na mazingira
ya kizalendo
yaliyokwishajijenga.
Ukiangalia Baraza la
Mawaziri alilotangaza
Mh. Magufuli, utaona
kuwa Waislamu katika
Baraza hilo (Japo kwa
majina yao tu) ni 9
(8?) kati ya 34 sawa na
24%! tu. Hii ina maana
Wakristo katika Baraza
la Mawaziri ni 76%!
Tu n a j u a h i i n i
Awamu ya Hapa Kazi
tu, na kigezo cha mtu
kuingia katika Timu
ya Kumsaidia Rais, ni
uchapa kazi. Swali ni
je, hakuna Waislamu
wachapa kazi wenye
sifa za kuwa mawaziri
wa kumudu kasi ya
Mheshimiwa Rais JPM?
Tunajua pia kuwa
Imani ya mtu, haitafsiri
utendaji kazi wake au
uvivu wake au hata
ufisadi wake na hivyo
katika Hapa Kazi Tu,
hoja ya Imani wakati
wa u t e u z i , ya we z a
kuwa haikuzingatiwa.
Lakini pengine tujiulize,
itakuwa halali na sawa
kisiasa, watu wa dini
moja kufanya maamuzi
na kuamua mustakabali
wa nchi hii peke yao? Je,
hii inasaidia vipi kujenga
umoja na mshikamano
w a Wa t a n z a n i a n a
kuondoa ubaguzi? Je,
hii ndiyo tafsiri stahiki
(kivitendo) ya kauli na
ahadi ya Mheshimiwa
Rais Magufuli kwamba
ataongoza kwa haki
bila ya kubagua dini za
watu?
Wa p o M a w a z i r i
waliotolewa kutoka
s e h e mu mb al i mb al i
na hawajawahi kuwa
viongozi wa kisiasa,
haiingii akilini kwangu
k u wa Wa i s l a m u
hawapo!
Ikiwa inadhaniwa
kuwa suala la imani
sio muhimu katika
uteuzi, hii ina maana
inahalalisha watu wengi
wa dini moja kufanya
maamuzi ya nchi peke
yao. Labda tusaidiane
kwa pamoja, tunajua
katika nchi hii zipo Dini
Kuu mbili, Uislamu na
Ukristo. Je, iwapo haya
ya 20 kwa 80 yaliyo kwa
Waislamu yatageuziwa
ANNUUR NEW.indd 15
Makala
AN-NUUR
PROF. Chachage
lilikuwa kwamba inabidi
kwanza ufanyike utafiti
tujue serikalini katika
nafasi zote muhimu,
kuna Waislamu wangapi
na Wakristo wangapi,
ndio tuseme.
Kama huu ndio ukweli
kama alivyoubainisha
Mzee Mtei, na kama hii
ndiyo hali unapogeuza
mambo kwa upande wa
pili, kwa nini idhaniwe
kuwa Waislamu wao
wataridhia kuona Baraza
la Mawaziri na Timu
ya Watendaji Wakuu
Serikalini katika Uwiano
huu wa 20 kwa 80?
Kama Mh. Rais
anaamini kuwa kuna
Waislamu walimpigia
kura na hata kumpigania
hata akashinda, siamini
kuwa walikuwepo tu
Waislamu wa kupiga
kura, lakini wa kushika
nafasi za Mawaziri na
Makatibu Wakuu, tabu
kuwapata.
Katika mambo ambayo
Waislamu wamebaki na
butwaa, ni uteuzi wa
Mh. Ndalichako kuwa
Waziri wa Elimu. Mtu
ambae alisababisha
mpaka maandamano
dhidi yake kutokana
na tuhuma za hujuma
i l i y o k u wa i k i d a i wa
k u f a n y wa d h i d i ya
Waislamu akiwa Katibu
Mtendaji wa Baraza la
Mitihani la Taifa. Mh.
Ndalichako alidiriki
kubadilisha matokeo
ya mtihani yaliyokuwa
tayari yametangazwa
b a a d a ya k u p i g i wa
kelele! Wakati akiwa
1/7/2016 3:17:23 PM
16
Inatoka Uk. 7
ilibadilishwa kwa kati
ya shilingi 7 na 7.50
kuanzia mwaka 1971
1979. Mfumuko wa
bei ulikuwa ni chini
kwa kipindi chote cha
utawala wa Iddi Amini.
Hadi Iddi Amini
anapinduliwa mwaka
1979, hospitali kuu
ya Mulago pamoja
na hospitali zote
za serikali Uganda
zilikuwa na magodoro,
mashuka na mito na
mablanketi na hakuna
mgonjwa aliyelala
chini kama ilivyo leo
hii. Pia kila chumba
cha binafsi hospitalini
hapo kilikuwa na
televisioni ya rangi.
Matibabu yote kwa
Waganda yalikuwa
ni bure. Kwa ujumla
kiuchumi Uganda
ilikuwa haijafikia hali
mbaya hata kidogo na
ndio maana baada ya
Iddi Amini kuingia
madarakani jumuiya
ya kimataifa iliiwekea
vikwazo vya kiuchumi
Uganda, lakini Uganda
iliweza kumudu hali
hiyo bila matatizo.
Baada ya kuvunjika
kwa Jumuiya ya Afrika
Mashariki mwaka 1977,
Uganda iliunda Shirika
la Ndege (Uganda
Airlines) na shirika
la reli kutokana na
masalia ya Jumuiya ya
Afrika Mashariki. Hii
yote ilikuwa ni katika
kuimarisha Hadhi ya
Taifa- National Pride.
Tatizo kubwa kwa
Iddi Amini lilikuwa
ni vikundi vya waasi
waliokuwa katika
nchi za jirani wakipata
misaada mbalimbali
kutoka nchi za
magharibi wakijipanga
kuivamia Uganda
na kumngoa Iddi
Amini wakati wowote.
Ikumbukwe tu kuwa
vikundi vya waasi
vilikuwa vikiongozwa
na watu kama Yoweri
Museveni ambaye
kwa sasa ni raisi wa
Uganda.
Hadi hapa ni wazi
kuwa Iddi Amini
ANNUUR NEW.indd 16
Makala
AN-NUUR
uchokozi wa mwanzo
kabisa ulitokea
Tanzania, kwani
Iddi Amini aliwahi
kulalamika kuwa
Tanzania inatumia
eneo la Mtukula
kuwapenyeza waasi
wa Uganda ambapo
aliweka kikosi
maalumu kujaribu
kuzuia shambulizi
lolote ambalo
alilitarajia.
Je, waganda ambao
walitokea Tanzania ni
akina nani? Na kama
walikuwepo, ni wazi
Iddi Amin alikuwa
sahihi ama alikuwa
anaongopa? Ingawa
hakuna uhakika sana,
lakini kama mtu
atarejea katika kitabu
kiitwacho: Sowing
the Mustard Seed: The
Struggle for Freedom and
Democracy in Uganda
ambacho kimeandikwa
na mwanamapinduzi
wa Uganda, Yoweri
Kaguta Museveni,
tunaweza kuona
uhalali wa madai
ya Amin. Katika
ukurasa wa 62, ni
kuwa katika kipindi
hicho, yeye alikuwa ni
mpigananji wa msituni
akiongoza kikundi
cha wakombozi wa
Uganda waliokuwa
wakiendesha harakati
zao katika eneo la
Kagera, sehemu
iitwayo Kagera
Salient. Kikundi
cha akina Museveni
kilijulikana kama
FRONASA. Je,
si inawezekana
ndio waliokuwa
wakiendesha mauaji
dhidi ya raia wa
Uganda mpakani
Mtukula mwaka 1978
ambapo waliwaua
wakazi wanne wa
Kiganda waliokuwa
wakinywa pombe ya
kienyeji MALWA
mpakani? Mauaji hayo
ndiyo yaliyomchagiza
Amin kuamua
kuiona Tanzania
kama mchokozi. Na
inawezekana kabisa,
FRONASA ilikuwa
inagombanisha nchi
mbili hizi ziingie
vitani huku wakijua
watafaidika na vita
hiyo.
Kwa mfano,
inasemekana Iddi
Amini aliunda kikosi
maalum kuweka
usalama eneo la
Mtukula Malire
Troops baada ya
mauaji ya raia wa
Uganda na watu
wenye asili ya Uganda
ambao waliingia
kutokea Tanzania
na baada ya mauaji,
walikimbilia nchini
Tanzania. Chanzo cha
uvamizi wa Tanzania
inasemekana ilikuwa
katika kujibu mapigo
baada ya jeshi la
Uganda, kupitia
kikosi cha Malire
Troops kuingia Kagera
kuwasaka wauaji
wa raia mmoja wa
Uganda aliyeuawa.
Raia huyo alikuwa ni
shemeji wa Kamanda
Mkuu wa Malire
Troops, Luteni Kanali
Juma Ali. Malire
Troops waliingia
Kagera hadi kilomita
80 ndani ya Kagera.
Kwa mujibu wa
gazeti la Weekly
News, toleo la tarehe
5/11/1978. Majeshi ya
Tanzania yaliivamia
Uganda kuanzia
tarehe 10 31, 1978
na kuteka maili 400
za mraba sehemu
ya Uganda ambapo
mapambano makali
yalifanyika katika
kilima cha Minziro.
Mpaka nukta hii,
bila shaka umepata
picha kwa kiasi
fulani, chanzo cha
vita hii ambayo ilitia
nchi yetu kwenye
lindi kubwa la
umaskini. Kimsingi
zipo sababu zaidi
ya hizi na tutaziona
zaidi Inshaallah.
(Juma Jumanne,
Katesh, Manyara, 0659
789 468.)
1/7/2016 3:17:24 PM
17
MAKALA/TANGAZO
AN-NUUR
SHUKURANI zote
anastahiki Mwenyezi
Mungu, Mola mlezi
wa dunia na rehema na
amani zimfikie mbora wa
Manabii na Mitume wote,
Sayyid na Muhammad
(S.A.W) .
U i sl amu n i din i ya
msamaha na huruma
n a m u o n g o z o , k wa n i
ameamrisha Mwenyezi
Mungu mtukufu kwa waja
Inatoka Uk. 20
ANNUUR NEW.indd 17
Inawatanganzia Waislam wote kuwa imeandaa safari ya Hijja mwaka 2016 sawa
na mwaka 1437 Hijria kwa Dola US$ 3,555
Kutakuwa na punguzo la asilimia 16% kuanzia muda huu mpaka Feb 29/2016.
Itakuwa Dola $2986 tu.
Kuanzia mwezi Machi 01-2016 mpaka Juni 12-2016 kutakuwa na punguzo la
asilimia 6% sawa na Dola $3,341 tu.
MAMBO YATAKAYOGHARAMIWA
1. Semina za Hija, 2. Huduma za afya na kuchinja 3.Airport Charge na ticket
za Ndege 4.Nyumba Makkah na Madina 5.Irham na Kuchinja kwa ajili ya
Tama-tuu 6.Chakula wakati wote 7.Usafiri na ziara Makkah na Madina
8.Mahema Mina na Arafa.
UMRA MWEZI WA RAMADHANI ITAKUWA NI DOLA US $1995
Fomu zinapatikana sehemu zifuatazo:1.Ofisi ya Ahlul Daawa Dar es Salaam Mtaa wa Dosi na Mkadini nyumba
Namba 26 mkabala na Showroom ya magari Tell. 0713 730 444, 0773
804 101 ,0785 930 444 au 0773 930 444.
2. Ofisi ya Ahlu Daawa Zanzibar Rahaleo Tel: 0777 484 982, 0777 413
987.
3. Abubakr Maulana wa Markaz Kiwalani Dar es Salaam, Tel: 0784 453
838
4. Abdallah Salehe Mazrui (Hoko) Dar es Salaam, Tel: 0715 724 444
5. Abdallah Hafidh Mazrui, Wete Pemba Tel: 0777 482 665
6. Mohammed Hafidh Mazrui Mkoani Pemba 0777 456 911
7. Sheikh Daud Khamis Shekha Tel: 0777 679 692
8. Maalim Seif Humoud Hamed (Kijichi Zanzibar) 0777 417 736
WAHI KULIPIA
1. Ofisi ya Ahlul Daawa Dar es salaam Tel: 0713 730444, 0773
804101,0785 930444.
2. Ofisi ya Ahlul Daawa Zanzibar Rahaleo Tel: 0777 484982, 0777 413
987.
Maalim Seif Humoud Hamed (Kijichi Zanzibar) Tel: 0777 417 736
TANBIH
(a) Atakaemaliza taratibu zote mwanzo ndie atakayeshughulikiwa
mwanzo
(b) Ili uwemo katika fungu la kwanza unatakiwa umalize taratibu
zote kabla ya punguzo
(c) Kumbuka kikundi cha Ahlul Daawa kwa bei nafuu kuliko wote
na huduma kuliko wengi.
Wabillah Tawfiq
1/7/2016 3:17:24 PM
18
MAKALA/TANGAZO
AN-NUUR
Jadweli ya Survey
Makala
1.Ukarasa wa mwanzo na wa mwisho (Habari)
2. Tahariri.
3. Uchambuzi wa Omar Msangi.
4. Habari za Kimataifa.
5.Hoja za Juma Kilaghai.
6. Makala kwa Jumla.
7. Safu ya Ben Rijal
8. Masheikhe waliopita.
9. Mashairi.
10. Waandishi
Msangi
Juma Kilaghai
Ben Rijal
Khatib J Mziray na Waalikwa wengine
Chakuongezwa
Chakuondolewa
(SUMAIT University)
(FORMERLY UNIVERSITY COLLEGE OF EDUCATION-ZANZIBAR)
15TH GRADUATION
The Vice Chancellor of SUMAIT University invites all Granduands of the academic year
2013/2014 to the 15th Graduation, which will be held on Tuesday 19th January 2016 at
the SUMAIT University premises- Chukwani.
All Graduands are required to confirm their participation to the Academic Office not later
than Thursday 14th January 2016. Graduands are reminded to pay TZS 10,000/=
(nonrefundable) before Friday 15th January 2016 for graduation gowns.
Please note that travel, meals and boarding expenses will be met by the Graduands
themselves. All Graduands are requested to report at the University by 3.00 pm on
Monday 18th January 2016 for rehearsal and logistical briefings. Graduands who will
not participate in the rehearsal will not be allowed to take part in the event.
For more information please contact SUMAIT University at the following address:
The Academic Office,
SUMAIT University,
P.O.BOX 1933, Zanzibar,
E- mail: info@zitec.org/amacez@zitec.org
Website: www.sumait.ac.tz
Mobile: 0776-463405/ 0773-181786
ANNUUR NEW.indd 18
1/7/2016 3:17:25 PM
19
KUNA imani kuwa
Msalaba ni nembo
ya Ukristo, lakini
inawezekana kuwa watu
hawajui kuwa nini maana
ya neno msalaba. Neno
msalaba linatokana na
neno sulubu, kwa maana
ya tabu, mateso, shida
n.k. Hivyo kama ni kazi,
ni kazi ya mateso, kama
ni maisha, ni maisha ya
mateso, kama ni kipigo,
ni kipigo cha mateso na
kama ni kifo, au kuuawa,
ni kifo au kuuawa kwa
mateso mabaya.
Kuunganishwa kile
kinachoaminika kuwa
Ye s u a l i s u l u b i s h wa
k wa m a a n a ya k u wa
alipigiliwa msalabani,
na kuunganishwa kuwa
msalaba ni nembo ya
ukombozi kwa dini ya
Kikristo, inawezekana
kuwa si sahihi, kwa kuwa,
k u wa s u l u b i s h a wa t u
kulikuwepo hata kabla ya
Yesu kuzaliwa. Na ilikuwa
ni sheria ya ukatili ulio
tendwa na serikali ya
Kirumi kwa enzi hizo.
Ndiyo maana walikuwa
na mahali maalumu
pa kusulubishia watu
palipoitwa Goligotha.
Ya a n i m a h a l i p e n y e
mafuvu ya watu walio
teswa na kufia hapo na
kuozea hapo.
Ndiyo maana sheria
ya Taurati ikatofautisha
unyongwaji wa mtu
aliyestahili kunyongwa na
ile sheria ya Kirumi, pale
ilipoandikwa hivi:
Akiwa mtu ametenda
dhambi ipasayo kufa,
akauwawa, nawe
ukamtundika juu ya mti,
mzoga wake usikae usiku
kucha juu ya mti, lazima
utamzika siku hiyo hiyo,
k wa n i a l i ye t u n d i k wa
amelaaniwa na Mungu,
usije ukatia unajisi katika
nchi yako akupayo Bwana
Mungu wako iwe urithi
wako. (Kumb. 21: 22-23)
Alama ya pande nne,
au jumlisha sio msalaba.
Neno hilo la msalaba,
limeingizwa na mfalme
wa Rumi ili kuchochea
jazba na hasira kwa askari
wake wakati wakipigana
vita kwa kuvamia mataifa
mengine, ili wahakikishe
kuwa wanawasulubu
bila huruma
wale
wote waliowaita
kuwa ni maadui zao.
Kilichozungumziwa hapo
juu, ni kutundikwa mtini
ANNUUR NEW.indd 19
MAKALA/TANGAZO
Vita ya Msalaba
au kunyongwa, iwe ni
kwa kamba au nduano
(ndwana).
Mwaka A.D. 312
Constantine alikwenda
kupigana vita na Maximian
aliyekuwa amejitwalia
kwa hila ufalme wa Italy
na wa Afrika. Constantine
alipokuwa akisafiri
kwenda vitani alisema
kwamba aliona maono ya
ajabu: maana mbinguni
ilitokea dalili au ishara
k a m a ya m s a l a b a wa
mwanga ukizungukwa
n a m a n e n o ya m o t o
ya l i y o n g a a : m a n e n o
yenyewe ni haya: Kwa
ms alaba h u u u ta p a ta
ushindi. Basi Constantine
akaamuru kwamba mfano
wa msalaba ushonwe
katika bendera zote za
majeshi yake. Akaenda
akamshinda Maxsentius
kisha aliporudi Rumi
akasimamisha sanamu
humo mjini mfano wake
yeye mwenyewe, sanamu
aliyechorwa katika jiwe
kuu. Na sanamu huyo
alikuwa na msalaba
mkononi, nao umeandikwa
chini ya anuwani yake ya
kusema kwamba msalaba
huo ulishindia vitani.
(Historia ya Kanisa uk.55,
cha Canon H.J.E. Butcher.)
Ndiyo maana, Peter
the Hermit, alipozusha
poropoganda, za kuwa,
Waislamu wanawauwa
Wakristo kule Yerusalemu,
na akaomba kibali kwa
Pope Urban II; alifanya
kazi hii hii inayofanywa
na Marekani, na mataifa ya
Ulaya; ya kuzunguka nchi
za Ulaya, na kukusanya
mataifa kusulubu
Waislamu.
Wa f u n d i s h a j i
wa
Ukristo, wanatwambia
kuwa, msalaba ni alama
ya ukombozi, na askari
wa Crusades walivaa
m a va z i ya l i y o c h o r wa
misalaba kama alama
ya ukombozi, lakini
kazi waliyofanya ni ya
kuwaokoa Waislamu
kwa kuwakata vichwa
kwa upanga!Sasa katika
vita vinavyoitwa vya
magaidi, wanavyofanyiwa
Wa i s l a m u , n i h a y o
h a y o . K a t i k a v i t a ya
Iraq, Mchungaji Teghua
aliandika kwamba:
mipango ilishapangwa,
na mashirika ya Makanisa
ya dunia yalikuwa
yanasubiri tu Rais George
Bush, awaokoe wa Iraq
na Waislamu kwa risasi
na makombora. Naye
mwandishi wa gazeti
la Kanisa liitwalo
Msemakweli, toleo na.
266 la Jumapili ya April
6-12, 200, aliandika
kuwa: Bustani ya Edeni
kukarabatiwa upya nchini
Iraki baada ya vita, Eneo
h i l o l i m e h a r i b i wa n a
utawala wa Sadam.
Kwa maelezo
ya
mwandishi, ni kuwa vita na
mauwaji waliyofanyiwa,
n a wa n a v y o e n d e l e a
kufanyiwa watu wa Iraq,
ambao ni Waislamu, lengo
kuu ni kuwa Rais Sadam
Husseni alipaharibu kwa
kuwa hakuna misalaba
na anatajwa Allah s.w.
badala ya Kristo.
Zamani miaka ya
sitini kulikuwa na vitabu
wanafundishiwa watoto
wa darasa la pili; vilikuwa
na hadithi zikiwavutia
watoto, kulingana na picha
na maudhui zake. Moja ni
ile iliyochorwa shamba
la mtama, na mtoto aliye
kuwa analinda mtama, na
ndege wanaokula mtama.
Kijana anaye linda
amelala chali, na ndege
wanakula mtama; alafu
maandishi yanasomeka
Baba aliniambia nilinde
mtama,
nimekalia
kichalichali, mtama waliwa
na ndege, mvivu wee.
Sasa tusemeje? Mwenyezi
Mungu ametujaalia mali
asili na akatujaalia kupata
Uhuru. Akatujaalia
kupata viongozi (walinzi
wanchi) na wana nchi,
hivi tuna tofauti gani na
yule mtoto aliyekuwa
akilinda mtama?
Uroho na Ufisadi kwa
maana halisi ya ufisadi, wa
watu wa vita ya msalaba
wa n a t a k a k u i c h u k u a
Edeni, alipoumbiwa
Nabii Adamu, kama
walivyoeleza; ili
waibadilishe Historia
yake, iwe nchi ya Biblia;
lakini wanasingizia
silaha za maangamizi.
Wanataka waichukue Iraq
litengenezwe sanamu
la Adamu na mkewe,
na mungu aliyeshika
upanga akiwa pekupeku
AN-NUUR
1/7/2016 3:17:25 PM
AN-NUUR
20
MAKALA
20
Soma gazeti la
AN-NUUR
KWA TSH 800/=
kila Ijumaa
AN-NUUR
Na Bakari Mwakangwale
SERIKALI ndiyo yenye
dhima ya kukamilisha
upelelezi wa tuhuma za
Ugaidi iliyowapa Sheikh
Mselem Ally na wenzake
23, waliopo mahabusu
katika Gereza la Segerea
Jijini Dar es Salaam.
Hayo yamebainishwa
na Wakili wa upande
wa utetezi akizungumza
na An nuur, Mh. Ubaid
Hamidu, kufuatia
kuendelea kuahirishwa
kwa kesi hiyo, huku wateja
wake wakiendelea kusota
mahabusu kwa miaka
miwili sasa.
Kwa mujibu wa Hakimu
aliyesikiliza kesi hiyo,
Alihamisi ya wiki iliyopita
katika Mahakama ya
Kisutu Jijini Dar es Salaam,
ni kwamba kesi hiyo
imeahirishwa hadi Januari
15, 2016.
Alisema, umma wa
Kiislamu na wapenda
amani unapaswa
kufahamu kuwa katika
Kuu.
Akifafanua zaidi,
Wakili Hamidu, alisema
Mahakama ya Kisutu,
haina uwezo wa kusikiliza
kesi zinazowatuhumu
watu na masuala ya ugaidi
badala yake kesi hiyo
inapaswa kusikilizwa
katika Mahakama Kuu.
Mahakama hii ya
Kisutu, huwa haisikilizi
hizi kesi za Ugaidi, badala
yake huwa inasimamia
mpaka pale upelelezi
utakapo kamilika na
Inaendelea Uk. 17
Na Salma Said
Inaendelea Uk. 18
Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na Business Printers Ltd, Dar es Salaam.
ANNUUR NEW.indd 20
1/7/2016 3:17:27 PM