Академический Документы
Профессиональный Документы
Культура Документы
www.annuurpapers.co.tz au facebook:annuurpapers@yahoo.com
Sauti ya Waislamu
ISSN 0856 - 3861 Na. 1214 RABBIUTH THAN 1437, IJUMAA , JAN 29-FEB. 4, 2016 BEI TShs 800/=, Kshs 50/=
Karume Shujaa
Aliepusha balaa la Aus na Khazraj
Dua zetu, Shein atuvushe salama
Yale ya Micheweni 2001 yasirejee
Soma Uk. 13
CUF haitashiriki
Uchaguzi Machi
DK. Ali Mohamed Shein.
Tatizo ni majipu ya
Kamati ya Kutunuku
CHAMA cha
Wananchi,
CUF, kimesema
hakitashiriki
uchaguzi
wa marudio
uliopangwa
kufanyika Machi
20, 2016.
CUF imesema,
haitashiriki
kwa sababu
uchaguzi huo sio
halali kwa vile
uchaguzi halali
ulishafanyika.
CUF inatoa
wito kwa
Wazanzibari
wote
wanaoipenda
nchi yao
na ambao
wanaamini
katika utawala
wa sheria,
demokrasia
na kuheshimu
Katiba na Sheria
za nchi yetu
kutoshiriki
katika uchaguzi
huo usio halali.
(Soma Tamko la
CUF uk.5)
An nisaa: 29
Fethullah-Gulen
ENYI wale ambao
mmeamini msile mali
zenu kati yenu kwa batili,
isipokuwa zitakapokuwa
ni biashara yenye kutokana
na maridhiano kati yenu
na msiziuwe nafsi zenu
hakika Mwenyezi Mungu
hakuacha kuwa kwenu ni
mwenye huruma sana.
[AN-NISAA 29]
Wakati Quran inaposema:
Msile mali zenu kati yenu
kwa batili inatumia msemo
wenye kukusanya. Quran
inayaelekeza macho kwenye
uharamu wa kula mali
za umma ubavuni mwa
mali za jamaa na wenye
udugu au kutumia vitu
vyao, pasi na radhi yao,
kama unavyoingia katika
maelezo hayo, uporaji, na
wizi na matumizi mabaya
na ujinga katika kutumia
mali na kupata mali kwa njia
AN-NUUR
zisizokubaliwa na sheria.
Ama faida yenye
kupatikana kutokana
na kubadilishana mali
kutokana na kuridhiana
pande zote zinazohusika,
na faida yenye kutokana
na biashara (hiyo sio kosa)
na Ndiyo iliyotajwa hapa,
kwa sababu biashara ni
njia muhimu na nyenzo ya
kupata faida. Hiyo ni faida
inayotosha kwa ajili ya
maisha, hakuna haja wala
ulazima wa kutumbukia
katika njia za haramu, wala
kwenye njia ambazo uhalali
wake na uharamu wake
hauko bayana.
Kunawezekana
kulifahamu angalizo la
maneno haya na msiziue
nafsi zenu angalizo ambalo
limekuja katika aya hii juu
ya maana mbili:
1. Hakika yule ambaye
anatenda madhambi ya
kuteleza katika riba au
kamari au rushwa na
kadhalika katika njia za
haramu, hakika mtu huyo
kwa kufanya hivyo, atakuwa
ameiua nafsi yake kihali na
ameimaliza.
2. Hakika watu
watakapoingia katika
muamala wowote katika
miamala iliyoharamishwa na
iliyobatili na yenye dhulma
katika kuchuma mali na
kuzitoa, na kila matumizi
yoyote yaliyo katika namna
hii, na kuukubali msingi
wowote wenye kutegemea
kwenye utaratibu huo
384,400 Km
980,00Km
111,111,000Km
788
88,888
12,345,679
4.5
4.57 bilioni
888,999 Km
25
75
35
MASUALA
1.Sayari ipi ilio na baridki kali kabisa? Jawabu: Neptune
2.Sayari ipi ilio na uzito mkubwa kuliko zote? Jawabu: Jupiter
3.Jua lina asilimia ngapi ya Hydrogen na Helium? Jawabu: 25, 35
4.Umri wa Jua miaka mingapi? Jawabu: 4.57 bilioni
5.Masafa ya kutoka duniani hadi mwezini. Jawabu: 384,400km
6.Kwenye Mwezi kuna maisha? Ndio, Sio. Jawabu: Sio
7.Mwezi wa Kiislamu hufwata mzunguko wa
Jawabu: Mwezi
8.Mwezi wa Kizungu hufwata mzunguko wa
Jawabu: Jua
9.Matumaini ya maji kupatikana yapo katika Sayari ipi? Jawabu: Mars
10.Jua likitoka Magharibi itakuwa nini? Jawabu: Mwisho wa dunia.
CHEMSHA BONGO: 37
Weka duara kwenye jawabu ilio sawa. Jawabu kamili wiki ijayo.
M L
B T U
A A T
D I
M G
O J
A Z
G A
D A U
M A
M B N K
O S
D O U I
H R
M X
M U
D M U E
U E
K N A
M A
W I
A Y
O M E
N U
A S
T K O A
W D
A I
M R
MASUALA
1.Asili ya mto Amazon unatokea wapi? Peru, Brazil Kenya.
2.Mto gani unaigawa Urusi na China? Amur, Missisipi.
3.Azerbhajan mji mkuu wake ni Baku ipo katika sehemu ya ziwa gani? Lake
Balghash, Caspian Sea, Zambezi
4.Ziwa gani kubwa nchini Ulaya?
5.Nchi gani ya Afrika ina jina la ziwa na ndio jina la nchi? Zambia, Tanzania,
Malawi
6.Muislamu yupi nchini Marekani akijinasibisha na Utume?
7.Muislamu gani nchini Marekani aliopinga watu kujinasibisha rangi yao
na Uislamu?
8.Jina la asili la mwanzo la Msumbiji lilikuwa ni :
9.Nchi ya Ureno ikijulikana awali kama :
10.Kisiwa cha Comoro kinajulikana kwa jina gani kwa Kiarabu?:
Jee Unajua?
1.Ujerumani ndio nchi yenye watu wake wenye kuzaa kwa idadi ndogo,
katika kila watu 1,000 huzaliwa watoto 8.2: http://www.bbc.com/news/
world-europe-32929962
2.Nchi za Kiafrika zinaongoza kwa uzazi nchi ya Niger katika kila watu 1,000
huzaliwa watoto 45, Mali 44, Uganda 43, Zambia 42, Burundi na Malawi
42, Somali 40: https://www.cia.gov/library/publications/the-world-factbook/
rankorder/2054rank.html
3.Nchi ya Lesotho inaongoza kwa watu kufariki kwa idadi kubwa, katika
kila watu 1,000 hufariki watu 14: https://www.cia.gov/library/publications/
the-world-factbook/rankorder/2066rank.html
4.Kati ya nchi zenye wanawake wengi kuliko wanaume ni Estonia, Latvia,
Russia, Ukraine, Belarus, Armania, Lithuania: http://www.aneki.com/
women_men.html
5.Nchi zinaongoza miji yake kuwa na usafi wa hali ya juu ni Finland
ikifwatiwa na Norway, Sweden, Iceland, Canada, Switzerland: http://
www.aneki.com/cleanest.html?&order=desc&orderby=table_cleanest.
value&number=10&cntdn=asc
6.Kati ya nchi zinazozalisha nishati mbadala kwa wingi ni Zambia, Nepal,
Congo DRC, Albania, Tajiksatn, Norway: http://www.aneki.com/highest_
renewable_electricity.html
7.Miji ilio na maisha magumu na matumizi ya chini ni: Brazzaville iliopo
Congo, Bangui Afrika ya Kati, Baghdad huko Iraq : http://www.aneki.com/
worst_cities.html
8.Kati ya nchi ambayo Matetemeko ya ardhi ndio kwao ni Afghanistan,
Algeria: http://www.aneki.com/list_countries.php?t=Earthquake_Prone_
Countries&slide=3
9.Nchi zinaongoza viogozi wao kula rushwa ni Indonesia, Philippines,
Congo DRC, Nigeria, Serbia na Montenegro, Haiti, Peru, Ukraine: http://
www.aneki.com/corruption_leaders.html
10.Nchi ya Sweden inaongoza katika usawa wa jinsia ikifwatiwa na Norway,
Iceland, Denmark, Finland, New Zealand, Denmark: http://www.aneki.com/
best_gender_equality.html
Habari
Karume Shujaa
Salma Said, Zanzibar
Bismillahir Rahmanir Rahim.
NA KUMBUKENI neema ya
Mwenyezi Mungu iliyo juu yenu.
(Zamani) mlikuwa maadui, Naye
akaziunganisha nyoyo zenu,
hivyo, kwa neema yake mkawa
ndugu. Na mlikuwa ukingoni mwa
shimo la moto (wa Jahannam),
Naye akakuokoeni nalo.
Namna hivi Mwenyezi Mungu
anakubainishieni aya zake ili
mpate kuongoka. (3:103)
Nimeanza na kumtanguliza
Mwenyeenzi Mungu kwa kuwa
ninachokiandika ni kitu kizito na
hakijawahi kuandikwa popote kwa
ukamilifu wake zaidi ya kwenye
kitabu kile kilichotayarishwa na
Chama Cha Wananchi (CUF) na
kwenye ripoti za Shirika la Human
Rights Watch ya mwaka 2012.
Ni mambo ambayo yanahitaji
mazingatio makubwa kwetu sote
kama wananchi kwa kila mmoja na
nafsi yake kuwa ana dhima kubwa
ya kuhakikisha usalama wake na
usalama wa mwenzake. Lakini pia
kwa viongozi ambao nao wamebeba
dhima na jukumu kubwa zaidi
mbele ya Mwenyeenzi Mungu na
wanaowaongoza.
Naamini maandishi yangu
yatawaathiri wengi pamoja na mimi
mwenyewe kwa kila hali kiusalama,
kiafya, na hata kisaikolojia. Ni
kwa sababu najaribu kuvuta hisia
za miaka 15 iliyopita ambapo
makubwa yalitokea katika nchi yetu
ya majonzi na huzuni ya unyama
uliokithiri. Ni maumivu yasiopona.
Ni uonevu usiosahaulika. Na ukatili
usiosameheka. Lakini tafakari
isiyofikirika kutokea katika nchi
ambayo inajivunia kuwa na asilimia
99% ya Waislamu ambao ni ndugu.
Nimekuwa nikitumia mfano
mmoja kila mara panapotokea
masuala ya kuzungumzia umuhimu
wa kudumisha amani na maelezo
haya ninayoyandika leo ni kama
hadithi au simulizi lakini ni simulizi
ya ukweli ambao imetokea Januari
27 mwaka 2001 wakati ambao nchi
iligubikwa na harufu ya damu
ya Wazanzibari iliyomwagika.
Maumivu makali yaliokosa tiba.
Majonzi na masikitiko makubwa
yaliojaa ndani ya nyoyo za wengi.
Nchi iligubikwa kiza kinene
ambayo yaliokuwa hayajawahi
kushuhudiwa yakashuhudiwa.
Yaliokuwa hayajaonekana na
kusikika, yakaonekana na kusikika
katika aridhi hii ya Tanzania
kwenye Visiwa vya Zanzibar.
AN-NUUR
Inaendelea Uk. 6
Tahariri/Makala
AN-NUUR
TAYARI Mwenyekiti
wa Tume ya Uchaguzi
ya Zanzibar Bw. Jecha
Salum Jecha, ametangaza
tarehe ya uchaguzi wa
marudio Zanzibar kuwa
ni 20 machi 2016 siku ya
Jumapili.
Bw. Jecha alisema
watakaopigiwa kura hizo
za marudio watakuwa
ni wagombea walewale
waliogombea nafasi
ya Urais wa Zanzibar,
Wawakilishi na
Madiwani na kwamba
hakutakuwa na kampeni
za uchaguzi.
Tangazo hilo la Jecha
limekuja baada ya awali
kufuta uchaguzi wa
Zanzibar Oktoba 28,
2015 na hatma ya kisiasa
Zanzibar kubakia katika
sintofahamu.
Kwa kipindi chote
cha karibu miezi mitatu
cha kufutwa uchaguzi
huo, hakuna suluhu
iliyopatikana kati ya
pande mbili zilizokuwa
zinachuana katika
uchaguzi huo, yaani
vyama vya CCM na
CUF licha ya kufanyika
mazungumzo pogo ya
kusaka suluhu.
Mpaka Jecha
analitangazia Taifa
kuhusu tarehe ya
marudio ya uchaguzi,
msimamo wa CUF na
mgombea wake Maalim
Seif Sharif Hamad ni
kutokubali kushiriki
uchaguzi wa marudio.
Ila Tume kumtangaza
mshindi halali wa
uchaguzi uliofutwa.
CCM na mgombea
wake Dk. Ali Mohammed
Shein, wamesimamia
kurudiwa uchaguzi kama
ilivyotangazwa na Tume
huku wakiwashadidia
wafuasi wao kuwa
wawape ushindi wa
kishindo!
Hata hivyo, pamoja
na Bw. Jecha kutangaza
tarehe ya kurejewa
uchaguzi Zanzibar ili
kutanzua mkwamo
uliopo na kumaliza
AN-NUUR
MAKALA YA MTANGAZAJI
AN-NUUR
haki itendeke.
Baraza Kuu linazihakikishia
t a a s i s i n a j u m u i ya h i z o
zote na pia kuwahakikishia
Wazanzibari na Watanzania
wote kwamba CUF itaendelea
kusimama kidete katika
kulinda na kutetea Katiba
na Sheria za nchi yetu na
p i a k u t e t e a m a a m u z i ya
Wazanzibari waliyoyafanya
tarehe 25 Oktoba, 2015.
7. KWAMBA limesikitishwa
na kushangazwa na kitendo
cha Msajili wa Vyama vya
Siasa, Jaji Francis Mutungi,
kuandika barua na kutoa
t a a r i f a k wa v y o m b o v ya
habari kutaka vyama vya siasa
vishiriki uchaguzi wa marudio
uliopangwa kufanyika tarehe
20 Machi, 2016 bila ya kujali
kwamba uchaguzi huo ni
haramu na unakiuka matakwa
ya Katiba ya Zanzibar na Sheria
ya Uchaguzi ya Zanzibar Nam.
11 ya 1984.
Baraza Kuu halikutarajia mtu
mwenye hadhi ya Ujaji kufanya
kazi ya kutumikia maslahi ya
watawala ambao wameamua
kuvunja Katiba na Sheria za
nchi yetu na kukanyanga
misingi ya haki na demokrasia
huku akishindwa kukemea
uhuni mkubwa uliofanywa wa
kubaka demokrasia na haki za
watu.
8. KWAMBA limesikitishwa
na kitendo cha Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania,
Mheshimiwa Dk. John Pombe
Magufuli, kukwepa dhamana
na wajibu wake kama Mkuu wa
Nchi na Amiri Jeshi Mkuu kwa
kuiacha njiani kazi aliyoianza
ya kutafuta ufumbuzi
wa mkwamo wa uchaguzi
Zanzibar.
Baraza Kuu linamtaka
Rais Magufuli kujitathmini
na kujiuliza anajiweka vipi
na kutoa taswira gani mbele
ya macho ya Watanzania na
jumuiya ya kimataifa kutokana
na kutosimamia ahadi yake
aliyoitoa mbele ya Watanzania
wakati akilizindua Bunge
jipya kwamba atafanya kazi
na vyama vya CUF na CCM ili
kuupatia ufumbuzi mkwamo
huu.
9 . K WA M B A l i n a l a a n i
matumizi ya nguvu kubwa ya
vyombo vya ulinzi na usalama
vya Jamhuri ya Muungano
na Vikosi vya SMZ dhidi ya
wananchi wasio na hatia na
ambao wamekuwa watulivu
licha ya vitendo vingi vya
AN-NUUR
Karume Shujaa
kama hiyo itokee ili wawapate tena.
(Allah atuepushie mbali kwa fadhila
zake na huruma yake).
Kwa kweli sitawacha
kuyakumbuka yaliomkuta Mama
mmoja wa Micheweni akielezea
habari zake huku nikiwa mkono
wangu ukishikilia shavu langu
na kuona michirizi ya machozi
ikichuruzika. Mama anasema
alifukuzwa na majeshi na kuanguka
chini na kisha kuingilia kinyume
na maumbile kwa kuwa alikuwa
na mtoto mchanga na aliwaeleza
kwamba yeye ndio kwanza
amejifungua yupo kwenye nifasi,
lakini wakamwambia hivyo hivyo
tukutie adabu.
Baada ya kumfanyia kitendo
hicho akawa hawezi kutembea
kwa maumivu aliokuwa akiyapata
akaanza kukimbia kidogo kidogo
na kupita kwenye bonde bahati
mbaya huku akipepesuka akaja
akakanyaga kama utelezi mtoto
wake akadondoka kwenye matope.
Inaendelea Uk. 14
Habari
AN-NUUR
BARAZA la Wakuu wa
Shule za Kiislamu Tanzania,
limeonyesha hofu katika
uharaka wa mabadiliko ya
kurejesha viwango vya ufaulu
vya zamani uliofanywa na
Waziri wa Elimu, Dk. Joyce
Ndalichako.
Baraza hilo limesema kuwa,
tatizo sio mfumo wa GPA wala
Divisheni, bali utaratibu wa
kutunuku usio na vigezo vilivyo
wazi uliokuwepo wakati wa Dr.
Joyce Ndalichako akiwa Katibu
Mtendaji Baraza la Mitihani.
Wamesema, wakati huo
kulikuwa na kitu kinaitwa
Kamati ya Kutunuku, ambao
ndio walikuwa na mamlaka ya
kutoa viwango vya ufauli kwa
vigezo ambavyo walivijua wao
wenyewe.
Wakafafanua kuwa alama za
ufaulu zilikuwa ni siri kubwa
ya Baraza la Mitihani na zenye
kubadilikabadilika somo hadi
somo na mwaka hadi mwaka.
Wasiwasi huo wa Wakuu wa
Shule za Kiislamu, umekuja
kufuatia hatua ya hivi karibuni
ya Waziri Ndalichako kutangaza
kurejesha mfumo wa zamani wa
kukokotoa matokeo ya Mitihani
ya Taifa chini ya Baraza la
Mitihani la Taifa, na kuachana na
mfumo mpya wa GPA.
Katika barua yao kwenda
kwa Waziri Mkuu, Mh.
Kassim Majaliwa, Baraza hilo
(BAWAKITA), limeonyesha
wasiwasi wao huo baada ya
Waziri wa Elimu, kusikiliza
madai ya Chama cha Wamiliki
na Mameneja wa Shule na Vyuo
Visivyo vya Serikali (Tangmosco)
wakidai kuwa mabadiliko hayo
kwenda katika mfumo wa GPA
yameingia pasi ya kushirikishwa.
Barua hiyo iliyosainiwa na
Mwenyekiti wake Mwalim
Hamisi Togwa, imesema hatua
ya Waziri Ndalichako, kumtaka
Katibu Mtendaji wa sasa Dr.
Charles Msonde, aeleze kuhusu
matumizi ya mfumo wa GPA
kunaifanya jamii ione na
kuelewa kwamba mfumo huo
kaunzisha yeye.
BAWAKITA, imebainisha
kuwa mfumo wa GPA,
ulianza kutumika katika
kutangaza matokeo kabla ya
Katibu Mtendaji wa sasa, kwa
watahiniwa wa Ualimu ngazi ya
cheti na Diploma.
Kwa maana hiyo, Baraza
hilo limemweleza Waziri Mkuu
kwamba wana wasiwasi na
uharaka wa Waziri wa Elimu,
Mheshimiwa Dk. Ndalichako
kurejesha mfumo wa zamani
ambao ulibadilishwa baada ya
kubainika kuwa na matatizo
makubwa.
Ikifafanua hoja ya
ushirikishwaji wa Tamongsco,
katika maamuzi ya kutumia
mfumo huo wa GPA, Baraza hilo
limesema, walishirikishwa katika
Tume iliyoongozwa na Profesa
Sifuni Mchome, ambayo ilitoa
ripoti yake Juni 15, 2015.
Imeeleza kuwa Tume hiyo
ilikuwa na ushiriki mkubwa
wa wadau mbalimbali wa
Elimu ambapo mambo mengi
yaliibuliwa na kuwa chachu
ya mabadiliko katika sekta ya
Elimu, ukilinganisha na tume
tatu zilizo tangulia kati ya
mwaka 2011 na 2013.
Ikifafanua zaidi barua
hiyo, imesema kuwa kabala
ya mabadiliko hayo kwa
muda mrefu wadau wa elimu
walikuwa hawafahamu mfumo
sahihi wa ukokotoaji wa matokeo
ya mitihani ya Taifa katika
ngazi mbalimbali kama ilivyo
bainishwa na ripoti ya Prof.
Sifuni Mchome.
Mh. Waziri Mkuu, ni Tume
hiyo ndiyo iliyopendekeza
ushirikishwaji wa wadau wa
elimu katika kuboresha mfumo
wa ukokotoaji wa matokeo,
ambapo ilisambaza dodoso juu
ya mapendekezo ya alama na
madaraja ya ufaulu katika shule
za Sekondari. Imesema sehemu
ya barua hiyo.
Ikaeleza kwamba kuuatia
hatua hiyo, Baraza lilimuandikia
barua Waziri wa Elimu na
Mafunzo ya Ufundi, aliyepita
wakiipongeza Serikali kwa
hatua iliyochukua katika
kuwashirikisha wadau katika
kuboresha mfumo wa ukokotoaji
na kuondoa mfumo wa usiri
chini ya Kamati ya Kutunuku,
ambapo sasa kila mwalimu
anajua wazi madaraja ya ufaulu
na namna yanavyopatikana.
Baraza hilo, limeweka wazi
kuwa kabla ya kuanza kutumika
Inatoka Uk. 4
sana na watu mbali mbali,
viongozi wa dini na wanasiasa
ambao wana khofu ya kuzuka
machafuko kutokana na maneno
yanayoandikwa katika ubao
huo.
Wakati wa kampeni, jeshi la
polisi lilipiga marufuku ubao
huo kuandika ujumbe wowote
ambao utachochea hamasa na
kusababisha uvunjifu wa amani
nchini.
Juzi Kamanda wa polisi wa
Mkoa wa Mjini Magharibi,
Mkadam Khamis Mkadam
alisema kuwa ujumbe
unaoandikwa pale Kisonge ni
mkali lakini hilo ni jukumu la
vyama vya siasa na sio jeshi la
polisi.
Kamanda Mkadam aliwataka
wanasiasa kuwakataza vijana
wao ili kuibakisha nchi katika
hali ya amani kwani maneno
yanaweza kuamsha hisia kali na
hatimae kuzusha mapigano ya
wenyewe kwa wenyewe.
Bakari amezikwa juzi katika
Makala
AN-NUUR
Na Nizar Visram
HABARI za hivi majuzi
zinasema suala la Burundi
litajadiliwa na kamati
maalum ya Bunge la
Afrika Mashariki (EALA)
linaloshughulikia utatuzi
wa migogoro. Mwenyekiti
wa kamati hiyo, Abdullah
Mwinyi amesema ujumbe
wa Rais Pierre Nkurunziza
umekubali kuhudhuria
mkutano huo utakaofanyika
mjini Arusha wiki hii.
Kamati hiyo pia itatoa
fursa kwa raia na asasi
za kiraia kutoa maoni
yao kuhusu mgogoro wa
Burundi ambao umepelekea
mamia ya watu kupoteza
maisha yao. Moja ya asasi
iliyosambaza risala yake
ni jumuiya ya wanasheria
wa Afrika (PALU) ambao
wamependekeza kuwa
Nkurunziza asiruhusiwe
kushika uwenyekiti wa
Jumuiya ya Afrika Mashariki
(EAC) mpaka akubali
kushiriki mikutano ya
usuluhishi.
Kwa mujibu wa katiba ya
EAC, uwenyekiti unatakiwa
ushikwe na Nkurunziza
baada ya Rais Magufuli
kumaliza muda wake.
Wengine wamediriki hata
kusema kuwa Burundi
ifukuzwe kutoka EAC
Wakati kamati ya EALA
inapanga mkutano wa
usuluhishi, tarehe 6 mwezi
huu mawaziri wa mambo
ya nje wa Tanzania, Uganda,
na Angola walihitimisha
kikao cha faragha kuhusu
Burundi uliofanyika mjini
Arusha. Hii ni baada ya
mazungumzo ya amani
yaliyopangwa kufanyika
Arusha kuahirishwa kwa
vile ujumbe wa Nkurunziza
ulikataa kuhudhuria
wakisema hawatakaa meza
moja na wale wanaochochea
vurugu nchini Burundi.
Wakati huo huo, Rais
Museveni ameteuliwa na
marais wenzake wa EAC
kuwa msuluhishi katika
mgogoro wa Burundi. Yeye
MWENYEKITI wa kamati
maalum ya Bunge la Afrika
Mashariki (EALA) , Abdullah
Mwinyi.
aliahidi kungatuka baada
ya mihula miwili lakini sasa
anaendelea na muhula wa
tano akiwa ametawala nchi
kwa muda wa miaka 30.
Sasa anatarajia kugombea
urais mwezi ujao baada ya
kubadili katiba iliyoweka
kikomo. Alifanya mabadiliko
hayo mnamo 2005 na tangu
wakati huo amekuwa
akisema shamba ambalo
nimelisafisha, kulipalilia
na kulilima mwenywe sasa
iweje niwaachie wengine
walivune? Kwa maneno
mengine nchi imegeuzwa
shamba lake.
Hata hivyo EAC imemteua
kuwa msuluhishi wa Burundi
, jambo ambalo limekubaliwa
na AU, UN na wafadhili.
Kwa muda huu Rais
Magufuli ni mwenyekiti wa
EAC na ndio maana huwa
anamtumia waziri wake wa
mambo ya nje, Augustine
Mahiga kushughulikia
mgogoro wa Burundi.
Mpaka sasa hajasafiri nje ya
nchi na haieleweki iwapo
atahudhuria mkutano mkuu
wa EAC au wa Umoja wa
Afrika (AU) unaotarajiwa
kufanyika mjini Addis Ababa
ili kuzungumzia mgogoro
wa Burundi. Tanzania ina
nafasi nzuri kwa vile Burundi
imekuwa na uhusiano wa
karibu na Tanzania. Wengi
tutakumbuka wakati ule
marais wa EAC walipokuwa
wakikutana Tanzania na
Burundi zilitengwa kwa
sababu ilionekana sisi
hatukuwa tayari kujiunga
na miradi ya EAC. Wenzetu
walijihesabu kama nchi
zilizokuwa zinakubaliana
(Coalition of the Willing CoW).
Mgogoro wa Burundi
ulianza pale mahakama
za magharibi zikielekezwa
kwa marais wa Rwanda,
Uganda na DRC (Congo)
ambao pia wameongeza
mihula yao. Kagame
na Kabila nao, sawa na
Nkurunziza, waliteuliwa
kushika muhula wa kwanza
na kwa hiyo wanadai
hauhesabiki.
Kagame aliteuliwa
kuwa rais mwaka 2000,
kisha akachaguliwa kwa
kishindo mwaka 2003 na
2010. Sasa awamu yake
ijayo itakuwa ya nne lakini
yeye anasema ni ya tatu. Pia
anakusudia kuondoa kikomo
ili aendelee kuchaguliwa
bila kikomo. Kama ni kosa
kwa Nkurunziza, kwanini
isiwe kosa kwa Kagame na
wengine?
Baraza la Usalama la
Umoja wa Mataifa (UN)
lilipiga kura tarehe 12
Novemba mwaka jana na
kupitisha azimio likilaani kile
ilichokiita mauaji, utesaji
na ukandamizaji wa haki za
binadamu nchini Burundi.
Ufaransa ndio ilitayarisha
muswada wa azimio hilo
na kuzihimiza nchi 15
wanachama wa baraza hilo
kuunga mkono. Hapa inabidi
tujiulize iweje azimio kuhusu
nchi ya Kiafrika lipigiwe debe
na nchi ya Ulaya badala ya
Waafrika wenyewe?
Hata hivyo nchi za Kiafrika
zikisaidiwa na Urusi zilipinga
kipengele kinachotaka
Burundi iwekewe vikwazo.
Mwishowe azimio
likapitishwa bila ya kipengele
cha kikwazo. Sasa baada
ya kupitishwa kwa azimio
hilo, ikatangazwa kuwa
UN itafanya mipango ya
kuhamisha baadhi ya askari
wake kutoka DRC (Monusco)
hadi Burundi. Wazo mbadala
likatolewa kuwa badala ya
UN kutuma majeshi yake,
ni vizuri Umoja wa Afrika
(AU) ikafanya kazi hiyo.
Ikapendekezwa kuwa majeshi
ya Monusco yanaweza
yakaunganishwa na majeshi
ya AU. Rais Obama wa
Marekani akampigia simu
Rais Jacob Zuma wa Afrika
Kusini na wakazungumzia
hali ya Burundi.
AU ina sera ya kuwa na
vikosi kila kanda barani
Afrika. Hivyo, kwa upande
wa Afrika Mashariki kuna
kile kinachoitwa kikosi cha
akiba cha Afrika Mashariki
(East African Standby Force).
Ni kikosi hiki ndicho
kinachofikiriwa kupelekwa
Burundi. Uamuzi wa
Inaendelea Uk. 18
Makala
Na Omar Msangi
AN-NUUR
Na Andre Vitchek
Januari 22, 2016 'Mtandao
wa Kupashana Habari,' na
'Counterpunch'
UGAIDI una mifumo tofauti
na sura nyingi, lakini baya
zaidi kati yake ni ukatili.
Tunaambiwa tuamini
kuwa magaidi ni wehu na
wakora, wanaozunguka na
mabomu, bunduki nzito
na mikanda ya milipuko.
Ndiyo tunavyoambiwa
tuwafikirie. Wengi wao
Inaendelea Uk. 10
10
Inatoka Uk. 9
mateso ya kutisha wakati
hawajahukumiwa kwa
kosa lolote. Na wote hao ni
Waislamu au watu kutoka
Mashariki ya Kati na Asia.
Wiki iliyopita gazeti
hili lilichapisha kisa cha
kijana Saidi Michael Danieli
alivyoteswa akiwa mikononi
mwa vyombo vya dola, yote
kutaka akiri kuwa yeye ni
gaidi/mshiriki wa jinai ya
Sitakishari. Hata baada ya
kuthibitisha kuwa hana hatia,
bado polisi wakambambika
tuhuma ya kukutwa na
sare walizodai ni za Al
Shabaab. Katika kusimulia
yaliyomsibu, Saidi Michael
Danieli aligusia pia majaaliwa
ya mwezake, marehemu sasa,
aliyemtaja kwa jina moja la
Khalfan ambaye aliteswa na
kufariki.
Aliponiona tu, alieleza
kuwa amenitaja ili nifike
nimuone katika hali
aliyokuwa nayo, hata akifa
ifahamike kuwa amekufa
akiwa mikononi mwa Polisi.
Kweli jamaa alifariki usiku
wa saa nane, siku ile ile
niliyoingia mimi.
Anaelezea Saidi Michael
Makala
AN-NUUR
Danieli, akisimulia
yaliyomkuta kijana Khalfan
hadi mauti kumfika akiwa
mikononi mwa polisi.
Haya anayosimulia Saidi,
yaliyomkuta Khalfan na
yale ya Joseph "Jihad Jack"
Terrence Thomas, ndiyo
majaaliwa ya Waislamu dunia
nzima hivi sasa.
Andre Vltchek ameandika
Makala aliyoipa jina
How the West Creates
Terrorism. Humo anaeleza
na kuchambua jinsi nchi
za Marekani na Ulaya
zilivyounda zimwi hili ugaidi,
zinavyotengeneza magaidi
kila uchao na kuwatumia
katika kufanikisha agenda
zao za kibeberu. Andre
Vltchek anasema, mabeberu
wa Marekani na Ulaya,
ndio magaidi wa kweli na
wabaya wasio na mfanowe.
Ni waharibifu, wanyonyaji,
Inatoka Uk. 9
ushindani wa malengo ya
usawa na maadili kimataifa.
Hivyo nchi za
Magharibi (zikabuni na)
zikaambatanisha ugaidi na
Uislamu. Uislamu ambao
ni moja ya tamaduni kubwa
zaidi duniani, kwa lengo
la kuwatisha mama wa
nyumbani wa matabaka
ya wenye fedha mitaa ya
miji mikubwa ya nchi za
Magharibi! Na zaidi ya hapo
ilibidi Uislamu uzungukwe
udhibitiwe kwani Uislamu
ulikuwa na mwelekeo wa
wazi mno wa Ujamaa na
ulikuwa na amani kupita
kiasi (kwa hiyo uvurugwe
kuondoa Amani katika nchi
za Waislamu na badala yake
kupandikiza machafuko na
mauwaji).
Wakati huo katika historia,
viongozi wote muhimu wa
mwelekeo wa siasa usio
wa kidini na wa Kijamaa
katika nchi za Kiislamu,
kama Iran, Indonesia na
Misri, walipinduliwa na
nchi za Magharibi, urithi
usiopingika kitamaduni na
kimaadili. (Kwa maana kuwa
ukishaupaka matope Uislamu
kuwa ni dini ya kigaidi na
magaidi, unaacha Umagharibi
(Ukristo?) kuwa ndio
utamaduni bora na ustaarabu
wenye maadili yanayofaa.)
Hivi ndivyo inavyofanya kazi
11
Inatoka Uk. 10
(ya Marekani) ilibidi kwanza
ielekeze hisia katika siasa kali
na kuharibu asasi na taasisi
za Kiislamu zisizohesabika.
Halafu kuunda hizo mpya,
hivyo kuzipatia mafunzo,
kutoa silaha na fedha, ili
ziweze kuonekana zinatisha
vya kutosha.
Kuna mambo kadhaa ya
kuchanganua hapa kutokana
na maneno haya ya Andre
Vltchek. Moja ni kuwa
magaidi na ugaidi kama
ulivyo katika sura yake ya
sasa, ni jambo lililobuniwa
na mabeberu. Ni mkakati
na program inayoratibiwa
na mabeberu wa Ulaya na
Marekani katika kufanikisha
malengo yao. Nitafafanua
zaidi mbele. Pili, serikali yetu
na serikali zote duniani, kadiri
zitakavyojitahidi kutumia
nguvu na mbinu mbalimbali
kupambana na magaidi,
magaidi wataendelea
kuwepo na kunona zaidi.
Ugaidi utakoma pale tu
ambapo waliouanzisha
watakapoutema kama
walivyoacha ukoloni wa
kuvamia na kukalia nchi
Makala
AN-NUUR
Inatoka Uk. 10
12
Makala
AN-NUUR
Inatoka Uk. 11
ya wakoloni, au kupeleka
watu kujiunga na vikosi vya
maangamizi.
Mfalme Leopold II na
mawakala wake waliua
takriban watu milioni 10
katika eneo la Afrika ya
Kati na Magharibi, ambayo
sasa inajulikana kama
Congo. Alikuwa akiwinda
watu kama wanyama,
akiwalazimisha kufanya
kazi katika mashamba yake
ya mpira. Kama alidhani
hawajazi mapipa yake
kwa haraka inavyotakiwa,
hakusita kuwakata mikono,
au kuwachoma moto wakazi
wote wa vijiji katika vibanda
vyao, wakiwa hai.
Wahanga milioni 10
walipotea. Milioni 10! Na
hiyo haikutokea katika
wakati wa mbali uliopita,
katika "zama za giza," lakini
katika karne ya 20 chini
ya utawala unaoitwa ni
ufalme wa kikatiba, na pia
hujitangaza kuwa ni wa
kidemokrasia. Inafananaje
na ugaidi ambao unatawala
katika maeneo yanayokaliwa
na ISIS? Tulinganishe idadi
na kiwango cha ukatili!
Na Jamhuri ya
Kidemokrasi ya Congo tangu
1995 imepoteza tena kiasi
cha watu milioni 10 katika
mzunguko wa kikatili wa
vita na mauaji, ulioanzishwa
Inatoka Uk. 11
Jihad, Al Shabaab, Makafiri
Vs Waislamu, na mambo
kama hayo, kupitia Wasapu,
Facebook na vitu kama hivyo,
na wengine kufikia hatua ya
kuhamasishana kufanya jinai
kwa hoja ya kupambana na
makafiri. Ukitafuta mzizi wa
yote haya ni kutumbukizwa
kijinga katika kile alichosema
Andre Vltchek kwamba:
In order to make Islam a
worthy enemy, the Empire had
to first radicalize and pervert
countless Muslim movements
and organizations, then create
the new ones, consequently
training, arming and financing
them, so they could really look
frightening enough.
Anachotufahamisha Andre
Vltchek ni baada ya mabeberu
kumaliza vita baridi na Mrusi
na baada ya kufanikisha
mikakati ya Mongoose na
na mawakala wa nchi za
Magharibi, Rwanda na
Uganda (ona kiongezeo cha
filamu ya mwandishi huyu ya
Kamari ya Rwanda).
Wajerumani walifanya
mauaji ya kimbari katika eneo
la kusini magharibi ya Afrika,
iitwayo sasa Namibia. Kabila
la wa-Herero liliteketezwa, au
kufikia kiasi cha asilimia 90
13
Na Mwandishi Maalum,
Zanzibar
ANAYEMFUATIA kwa ujasiri
na msimamo alikuwa Salmin
Awadh Salmini.
Kwa hakika CCM
imeondokewa na majemadari,
ambao kama kuna kuonana,
hivi sasa wanaulizana ya
mitaa ya Barzakh, sio tena ya
Kisiwandui!
Na hapo ndipo yalipo
mazingatio kwa kila Muislamu.
Kwamba, tunaweza kukataa
kutoa serikali kwa staili ya
Jecha Salim Jecha, lakini hatuna
ubavu wa kukataa kutolewa
roho zetu na kuchukuliwa uhai
wetu muda unapofika.
Ni majira ya saa 11 Alfajiri
nafungua simu yangu napata
ujumbe ulioanza na:
Innaa Lillahi Wainnaa Ilayhi
Rajiuun. Asha Bakari hatunaye
tena. Ameshatangulia mbele
ya haki. Waarifu na wengine.
Ujumbe huo ukitokea Dubai.
Naam Alhamdulillah
Mwenyeenzi Mungu ampokee
na amsamehe mja wake huyo.
Amin.
Asubuhi ilipofika
kila unapopita, taarifa
zimeshasambaa na kauli
unayoisikia katika vinywa vya
watu ni hii Nakwambieni nchi
hii haipatikani kwa karatasi
sisi tumepindua labda na nyie
mpindue.hatutoi hatutoi
hatutoi, wenye madaraka ni sie.
Ni kauli ya Bi Asha Bakari
wakati wa uhai wake ni kauli
iliyompa umaarufu mkubwa
katika siasa za Zanzibar ambayo
imemalizia maisha yake.
Sisi ndio wenye madaraka.
Nawaambia tena jamaa
zangu, wallaahi, wallaahi,
wameshindwa kutawala
1995 hawatawali tena maisha
yao yote na narudia tena
na siogopi kusema. Serikali
hii ni ya kimapinduzi si ya
mchezo, hawawezi, hawawezi
kutupinduahatuwezi
kukabidhi serikali kwa njia ya
vikaratasi (kura).
Nchi haitolewi kwa kura,
haya kuitisha uchaguzi
kusumbua watu na kupoteza
gharama zote hizo ya nini?
Hata hivyo, mtu unaweza
kusema, hiyo ni kauli ya Asha
Bakari si ya CCM wala Serikali
ya Mapinduzi Zanziar. Lakini
ukweli ulio wazi ni kwamba
aliyofanya Jecha ni kutafsiri
kivitendo aliyosema Asha
Bakari! Lakini maadhali CCM
imemuunga mkono Jecha, ina
maana kuwa huo ndio msimamo
wa CCM na SMZ yake. Na kwa
maana hiyo, hata tangazo la
kurudia uchaguzi halina maana
yoyote.
Vyovyote iwavyo, hayo ndiyo
matamshi yaliompa umaarufu
mkubwa Asha Bakari Makame
na kuonekana jasiri hapa
Zanzibar akijulikana zaidi kwa
jina la Mtama ambalo alipewa
Makala
Safari ni nzito!
Tumkumbuke Asha kwa Dua
Aungana na Awadh Barzakh
Jecha anakazia tu kauli zao
AN-NUUR
Inaendelea Uk. 14
14
MAKALA/MASHAIRI
Karume Shujaa
AN-NUUR
Safari ni nzito!
Inatoka Uk. 7
kuwa sekretari wa Baraza
la Wawakilishi ambapo
aliitumikia mwaka 1983
hadi 1985.
Baadae akateuliwa
kuwa mjumbe wa Baraza
la Wawakilishi kuanzia
mwaka 1985 hadi mwaka
1990 wakati huo akiwa
Naibu Waziri wa Usafiri
na Mawasiliano mnamo
mwaka 1990 hadi mwaka
1995 na baadae kuwa
Naibu Waziri wa Habari,
Utamaduni, Utalii, Vijana
na Wanawake, mnamo
mwaka 1995 hadi mwaka
2000 alikuwa Waziri wa
Wanawake na Watoto
na Mjumbe wa Baraza
la Wawakilishi akitokea
kwenye jumuiya za
wanawake wa CCM
Zanzibar.
Mbali na nafasi hizo
za serikali, lakini Bi Asha
alikuwa mstari wa mbele
katika kukiendeleza Chama
ambapo mnamo mwaka
1964 alikuwa ni Mjumbe wa
Vijana wa Paunia kupitia
Chama Cha ASP na baadae
mwaka 1972 alijiunga na
Afro Shirazi Youth League
hadi hapo mwaka 1977
vyama vya TANU na ASP
vilipoungana na kuzaliwa
Chama Cha Mapinduzi
(CCM) yeye akawa
miongoni mwa wajumbe wa
mwanzo wa chama hicho.
Tokea hapo mwaka
1978 kwenye jumuiya ya
wanawake wa CCM kisha
kuwa mjumbe wa JUWATA
na baadae kuwa mjumbe
wa Wazazi wa chama hicho
cha CCM mwaka 1980 na
akaanza kukamata nyadhifa
nyengine mbali mbali ndani
ya chama ikiwemo Mjumbe
wa Kamati Kuu ya CCM na
1992 hadi 2010 Mjumbe wa
Halmashauri Kuu ya CCM
(NEC) mwaka 2007 hadi
anamaliza uhai wake yeye
ni Makamo Mwenyekiti
wa Umoja wa Wanawake
Tanzania (UWT).
Katika uhai wake Bi
Asha amaekabiliwa na
changamoto mbali mbali
lakini zaidi kwa wapinzani
wake wa Chama Cha
Wananchi (CUF) ambao
alikuwa ni mpinzani wao
mkubwa katika siasa. Bi
Asha ambaye maarufu
anajulikana kwa msimamo
wake wa maneno alitokuwa
akiyatoa mara kadhaa
kuhusiana na Maalim
Seif kushika dola yeye ni
miongoni mwa wahafidhina
wachache waliokuwa
wakipinga na kusema
kwamba Hii ni nchi ya
kimapinduzi na haitoki kwa
karatasi.
Matamshi yake hayo
yakimaanisha hata mkipiga
kura hamuwezi kushinda
P.O. Box 90042, +255 713 586 186 au 713 455 255
Dar es Salaam, Tanzania
15
Inatoka Uk. 11
dola na kisha kufuatia
msururu wa kukamatwa
kwa kila aliyekuwa katika
mtandao huo. Hao ndio
tunasema kuwa wamenaswa
kwa ujinga kwa sababu,
kwanza wanayojadili
ukiyaweka katika mizani,
yanakwenda kinyume
kabisa na mafundisho
yenyewe ya Uislamu. Pili,
hayawezi kutatua matatizo
ya Waisamu yaliyopo na
tatu ni kuwa wanajadili
mambo ya hatari bila hata ya
kujua kuwa kwa utaalamu
uliopo, wanayoandika si
siri, kila wanachoandika
kinasomwa na wengine bila
wao kujua, wakiwepo polisi,
wanausalama wa ndani na
nje.
Ugaidi unavyowasaidia
mbeberu
Mfalme Leopold II na
wenzake, waliangamiza
takribani Waafrika milioni
10 wa Congo hivi sasa, watu
wakisakwa kama wanyama
wa porini ili wakafanye kazi
katika mashamba ya mpira
(rubber plantations) ya
mabeberu. Ndiyo yaliyojiri
pia Namibia ambapo
Wajerumani waliangamiza
kabila la Herero kwa
mauwaji ya halaiki (mass
killing) ambapo manusura
walitimuliwa katika majumba
yao na mashamba yao
wakakimbilia jangwani
kuwapisha Wazungu.
Mpaka leo mashamba yao
yanatumiwa na Wazungu.
Hawa walikuwa raia
wasio na hatia ambao kama
ni kosa, basi kosa lao lilikuwa
kutokuwa Wazungu, halafu
wakazaliwa katika ardhi safi
kwa kilimo na yenye madini.
Watu wa makabila ya
Herero na Namaqua,
Namibia, wakati huo
German South-West Africa,
walipinga ukoloni na ubeberu
wa Ujerumani katika nchi
yao. Kutokana na hilo
wakatangaziwa ugaidi na
uasi. Adhabu yao ikawa
kuteswa na kuuliwa kwa
kunyongwa, kupigwa risasi,
kufanywa panya wa majaribio
na kufukuzwa katika miji
na vijiji vyao, wengi wakafa
jangwani kwa kiu na njaa.
Zaidi ya kuwafanyisha
kazi kitumwa, huku
wakiwa wamewafunga
minyororo, serikali ya
Wazungu wa Ujerumani,
haikutosheka, lakini ikawa
inaleta wataalamu wake
wa vyuo vikuu na hospitali
Makala
AN-NUUR
WAJERUMANI waliwafunga minyororo kabila la Herero nchini Namibia kipindi cha ukoloni.
16
AN-NUUR
17
MAKALA/TANGAZ0
AN-NUUR
Inatoka Uk. 16
ya kurejewa ikiwa imeshatangazwa,
kumeibua sintofahamu kubwa
katika nchi kwa sababu uchaguzi
uliopita Tanzania ilipata sifa, kwa
uchaguzi kufanyika kwa amani na
utulivu. Lakini sasa bado suala hili
halieleweki.
Hata hivyo Dk. Salim, alisema
hadhani suala la kufutwa uchaguzi
lilikuwa ni la mtu mmoja, kwamba
hadhani ni la Jecha peke yake na
kusema huo sio mustakabali mzuri
visiwani humo.
Alisema, Zanzibar ni nchi ndogo
lakini ina historia kubwa kisiasa,
hivyo juhudi za pamoja zinahitajika
kufanyika kutatua mgogoro uliopo
kwa maslahi ya Watanzania kwa
ujumla.
Aliwataka Viongozi katika suala
la Zanzibar haki itendeke na waache
ushabiki wa vyama na kwamba,
wote waweke ushabiki pembeni
na watatue mgogoro huo kwa
mustakabali wa Wazanzibari na
Watanzania kwa ujumla.
Alishauri pande zote ziendelee
kukutana hadi suluhu ya pamoja
ipatikane, japo viongozi kadhaa
wameshakutana na kufanya
mazungumzo bila kupata suluhu.
Dk. Salim alitoa tahadhari
kwamba nchi ipo katika hali
mbaya na Watanzania hatujazoea
na kwamba, suala la Zanzibar
likiendelea linaweza kuzaa matatizo
makubwa katika Taifa.
Akizungumzia kuhusu vitendo
vya ubaguzi yakiwamo mabango
yaliyokuwa yameandikwa ujumbe
wa kibaguzi kwa maandishi
makubwa katika sherehe za miaka
52 ya Mapinduzi ya Zanzibar,
zilizoadhimishwa Januari 12, Dk.
Salim alisema ameshangazwa na
hali hiyo.
Alisema kitendo cha baadhi ya
wanachama wa CCM kubeba bango
hilo hadharani kimeitia doa na ni
aibu kwa Zanzibar na Tanzania
wakati inafahamika kuwa suala la
ubaguzi lilimalizika tangu mwaka
1964.
Aliongeza kuwa, kitendo kile ni
jambo la kufedhehesha na halistahili
kupewa nafasi hata kidogo.
Alisema wakianza kubagua,
watakaoathirika wengi ni watoto wa
viongozi na kwamba, ubaguzi huo
ni ujinga na unaudhi.
Alisema kitendo cha wana-CCM
kubeba bango hilo kinaonyesha
wazi kuwa wameishiwa hoja kwa
sababu suala la Hizbu lilikufa tangu
mwaka 1964.
Hata hivyo, Dk. Salim alihoji
kuwa iweje wanachama wabebe
mabango yanayochochea ubaguzi
katika sherehe za Mapinduzi na
waliachwaje kufanya hivyo, hali
ya kuwa viongozi walikuwapo na
waliona.
Alisema, kama kuna mtu yeyote
anaona hilo ni sawa, basi huyo ni
sawa na kusema kafilisika kabisa.
Itakumbukwa kuwa mwaka 2005
katika harakati za kuwania nafasi
ya Urais ndani ya CCM kuelekea
Uchaguzi Mkuu, Dk. Salim alidaiwa
waziwazi na baadhi ya wana kambi
wa CCM kuwa hakustahili kuwania
kiti hicho kwa kuwa yeye alikuwa
ni mwanachama wa Hizbu, chama
kutilia mkazo.
Tayari Katibu huyo Mkuu wa
CUF ameshatangaza kujitoa kwenye
mazungumzo hayo.
Membe alifafanua zaidi
kwamba, kilichotokea Zanzibar
kimeihuzunisha dunia na kwamba,
kilichoishitua dunia ni kule kufuta
matokeo kwa ujumla wake.
Kwamba imeshangaza katika
majimbo yote, hakuna hata moja
lililofanya vizuri na hapo ndipo
wengi wanapopata wasiwasi.
Aidha alisema haridhishwi
na jinsi mgogoro huo wa kisiasa
unavyotafutiwa ufumbuzi kutokana
na kuwahusisha zaidi Dk. Shein na
Maalim Seif.
Alisema kama kuna mwanasiasa
wanaodhani tatizo la Zanzibar
litamalizwa na sehemu moja ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
wanafanya makosa makubwa kwani
umoja uliopo Bara na Zanzibar ni
umoja wa kusaidiana wakati wa
raha na matatizo.
Kwamba tatizo ambalo linaweza
kuhatarisha usalama Zanzibar,
18
MAKALA
AN-NUUR
Inatoka Uk. 8
kupeleka wanajeshi 5,000
huko Burundi ulichukuliwa
mnamo Disemba 2015 na
Baraza la Amani na Usalama
la AU. Nkurunziza alipewa
muda wa kukubaliana na
uamuzi huu, lakini akaupinga
na kusema majeshi yake
yatapambana na kikosi cha
uvamizi cha AU.
Aghlabu tunapoongelea
majeshi ya UN au ya AU,
kisichotajwa ni kuwa majeshi
hayo huwa yanafadhiliwa
na mataifa makubwa kama
Marekani. Bendera ni ya UN
au AU na askari ni Waafrika,
lakini Marekani na Ulaya
wanatoa kila kitu kuanzia
silaha hadi sare na posho.
Wakati AU imechachamaa
kupeleka majeshi ya kulinda
amani ili kuzuia mauaji
nchini Burundi, wachunguzi
wanahoji iweje AU hiyo hiyo
ilikaa kimya wakati majeshi
ya Ufaransa yalipoishambulia
Ivory Coast mwaka 2010.
Halafu kuna uvamizi wa
Libya (2011), Mali (2012) na
CAR (2013) uliofanywa na
majeshi ya kigeni. Je yalikuwa
wapi hayo majeshi ya AU ya
Inatoka Uk. 20
zaidi.
Hata hivyo wakazi
wengi wa jiji la Dar es
Salaam wamesikitishwa na
kutofurahishwa na hatua hiyo
tofauti na alivyodai Nape, kwani
walisema kitendo cha serikali
kuingilia chombo cha habari
na kuweka maamuzi yake ni
kuingilia uhuru wa vyombo vya
habari kwa mujibu wa sheria
na vile vile kuzuia uhuru wa
wananchi kupata habari.
Kurwa mkazi wa Mbagala
alisema kutorushwa mijada ya
Bunge moja kwa moja, kunatoa
fursa kwa watendaji wa TBC
kuhariri sehemu kubwa ya
mijadala hiyo, hasa sehemu
ambazo haiifurahishi serikali
na kuruhusu ile ambayo kwao
wanaona inawafaa, jambo
ambalo ni sawa na kuwakatili
wananchi.
Maide Omar, mkazi wa
Manzese yeye alikwenda mbali
zaidi na kuhoji kama TBC ni
mali ya viongozi, ni mali ya
serikali au mali ni ya umma wa
Watanzania?.
Alihoji inakuwaje televisheni
ya Taifa iwe na wasaa mrefu wa
kurusha moja kwa moja hewani
harusi ya mtu kwa maslahi ya
familia Fulani, lakini ikose muda
19
MAKALA
AN-NUUR
Inatoka Uk. 20
AN-NUUR
20
MAKALA
20
Soma gazeti la
AN-NUUR
KWA TSH 800/=
kila Ijumaa
AN-NUUR
Na BakariMwakangwale
WAKATI Kamanda
Suleiman Kova akitangaza
kustaafu utumishi
katika Jeshi la Polisi,
ametajwa kuingia katika
kumbukumbu mbaya
dhidi ya umma wa
Kiislamu nchini wakati
wa utumishi wake.
Imeelezwa kuwa, hiyo
ni kutokana na miaka ya
hivi karibuni Waislamu
kuwa wahanga wa tuhuma
za ugaidi. Afande Kova
amestaafu baada ya
kufikia ukomo wa umri
wa utumishi wa umma
Serikalini, akiwa katika
nafasi ya Kamanda wa
Kanda Maalum Jijini Dar
es Salaam tangu mwezi
Juni 2008.
Kabla ya hapo amekuwa
katika nyadhifa mbalimbali
katika Jeshi la Polisi nchini.
Akitangaza kustaafu
kwake, mapema hivi
karibuni katika viwanja
vya Chuo Cha Maafisa wa
Polisi Kurasini, Jijini Dar
es Salaam, na kutambulisha
Kamanda Simon Siro,
kukaimu nafasi yake,
aliyataja baadhi ya matukio
kuwa kwake yatabaki kuwa
ni kumbukumbu kichwani
mwake. Kufuatia kauli hiyo
ikawasukuma Waislamu
nao kutoa maoni yao juu
ya utumishi wake hususan
kwa umma wa Kiislamu,
kwamba ameondoka huku
akiacha maumivu makali
katika familia za Kiislamu
na hawezi kusahaulika
kutokana na madhila aliyo
wasababishia.
Ustadhi Said Awadhi,
alisema chini ya Kamanda
Kova, baadhi ya Waislamu
wamekuwa ni wahanga
Inaendelea Uk. 19
miaka 10 ameshuhudia
polisi wakitinga
nyumbani kwake
kumhoji na kuangalia
kompyuta inayotumiwa
Inaendelea Uk. 19
SERIKALI imeondoa
sehemu ya vipindi vya
matangazo ya moja
kwa moja ya vikao vya
Bunge vilivyokuwa
vikirushwa na
Televisheniya Taifa
TBC kutoka Dodoma.
Uamuzi huo wa
serikali umetangazwa
na Waziri wa Habari,
Utamaduni na Michezo
Nape Nnauye katika
kikao cha pili cha
mkutano wa 11 wa
Bunge la Jamhuri
ya Muungano mjini
Dodoma Jumatano wiki
hii.
Kufuatia kauli hiyo
ya serikali, TBC sasa
itakuwa ikirusha baadhi
tu ya matangazo ya
moja kwa moja ya
vikao na mijadala ya
Bunge, huku sehemu
nyingine ya mijadala
hiyo ikirekodiwa na
kurushwa hewani
katika kipindi maalum,
ambacho Nape alikitaja
kuwa kinaitwa Leo
katika Bunge.
Baadhi ya wananchi
wameonyesha
kuridhishwa na
utaratibu huo na
wameipongeza serikali.
Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na Business Printers Ltd, Dar es Salaam.