Академический Документы
Профессиональный Документы
Культура Документы
Polisi
yanacheleweshwa
www.annuurpapers.co.tz au facebook:annuurpapers@yahoo.com
Sauti ya Waislamu
ISSN 0856 - 3861 Na. 1218 JAMADUL AWWAL 1437, IJUMAA , FEB. 26-MACHI 3, 2016 BEI TShs 800/=, Kshs 50/=
Soma Uk.4
Gogu wa
Magogu!
Tatizo Makahaba wa habari
Kosa la Sheikh Msellem nini?
USTADH Salum
An nisaa: 118
Fethullah-Gulen
SHETANI ambaye
amemlaani yeye
Mwenyezi Mungu
alisema: kwa
hakika nitafanya
katika waja wako,
fungu maalumu.
[An-Nisaa 118]
Maneno haya
yaliyotuka ambayo
aliyazungumza
shetani pamoja na
Mwenyezi Mungu
mtukufu, na
ambayo yamekuja
katika aya hii na
katika aya nyingine
nyingi. Ama ni
kwamba Mwenyezi
Mungu mtukufu
aliyasikia na
akamruhusu, kwa
kusema maneno
haya. Na ama ni
kwamba kufuatana
na maelezo ya
wafasiri wengi,
haya ni maneno
yaliyopita katika
fikra na mawazo
yake na yale
yaliyohukumiliwa
na maumbile
yake, na kwamba
Mwenyezi Mungu
mtukufu ametueleza
maneno hayo.
Ni sawa sawa
haya yalikuwa ni
maelezo ya ulimi
wa hali ya shetani,
au ni ghadhabu
ya maumbile yake
kwani yeye anaweka
wazi azma yake ya
kuwatesa waja wa
Mwenyezi Mungu
ambao hawakufikia
kwenye ngazi ya
Ikhlasi. Na kwa
hakika mchezo wa
shetani wa kwanza
ambao ulipita
pamoja naye juu
ya mgongo wa
ardhi hii, mchezo
huo unaendelea
leo. Kutoka
upande wake na
kutoka upande
wa wafuasi wake
wao wanaendelea
katika mbinu za
kuwafitini watu na
kuwahadaa kwa
matumaini ya batili
na kufanya mbinu
za kumsukuma
binadamu ili
kubadilisha
maumbile yake
na maumbile ya
viumbe wengine na
kuharibu uwiano.
Waliomfuata, kwa
hakika wamo
katika hasara
iliyowazi na ni
katika watu wenye
bahati mbaya.
Ama wale ambao
wamewezeshwa
kukaa mbali na
shetani na njia yake,
hao ndiyo wenye
bahati nzuri na hao
ni kwa ajili ya kukaa
kwao karibu na
Mwenyezi Mungu
mtukufu.
AN-NUUR
11
365
128
357
65
30
354
29 na 31
20 na 30
25
10 na 30
43
45
31
55
50
30
80
1965
29 na 30
33
1969
1437
42
MASUALA
1.Kabla ya mwezi wa Ramadhani, huwa ni mwezi gani? Shaaban
2.Huu ni mwaka gani wa Kiislamu? 1437
3.Mwezi wa Kiislamu una siku ngapi? 29 na 30
4.Idadi ya siku katika mwaka wa Kiislamu ni siku ngapi? 354
5.Kuna siku ngapi pungufu baina ya mwezi wa Kiislamu na mwezi wa
Kizungu?11
6.Msikiti wa mwanzo nchini Marekani ulijengwa katika mji gani? Detroit
TMI
7.Mwaka wa 1964 alisilimu bingwa wa masumbwi Mohammed Ali ilikuwa
mwezi gani? Aidha mwaka huo huo alisilimu mwana harakati wa kudai
haki za watu Weusi Marekani, ilikuwa mwezi gani? Februari na April
8.Malcolm X aliuwawa mwaka gani? 1965
9.Yarrow Mamount baada ya kuachiwa huru kuwa mtumwa alifika kuwa
ni mbia (Sahareholder) wa Bank ya Colombia, Jee unajua aliishi miaka
mingapi? 128
10. Quran ndio imemfanya mtu Mweusi kujivua katika minyororo ya
utumwa na kujihisi huru, hakuna dini yoyote ile iliowatetea watu huru
kuondokana na ubeberu wa watu wa Ulaya na Marekani . Maneno haya
yalisemwa katika mwaka wa 1889 na Edward Blyden.
CHEMSHA BONGO: 40
Weka duara kwenye jawabu ilio sawa. Jawabu kamili wiki ijayo.
J
22
23
24
25
23
629AD
628 AD
630AD
MASUALA
1.Asiokula, kunywa, kulala ni nani?
2.Unapokwenda Chafya unatakiwa useme kalima gani?
3.Jina jengine la Mfalme wa Abysynia (thiopia) ambae aliwapokea Waislamu
akiitwa nani?
4.Sahaba gani alisoma ujumbe wa Mtume (SAW) mbele ya Mfalme Najash?
5.Khutba ya mwisho alioitoa Mtume (SAW) ikiwa ni wasia mkubwa kwa
Waislamu ilikuwa tarehe ngapi katika mfungo tatu?
6.Mkataba wa Hudaybiyah Mtume Mohammed (SAW) aliwekeana mwaka
gani na Makafiri?
7.Utume wa Mtume Mohammed (SAW) umedumu kwa miaka mingapi?
8.Mtoto yupi wa kike wa Mtume Muhamad (SAW) alikuwa ndio mkubwa
wao?
9.Mtoto yupi wa kike wa Mtume Mohammed (SAW) aliye wa mwanzo
kufariki?
10.Nani alikuwa Mhandisi wa Firauni?
Jee Unajua?
1.Phd ni shahada ya tatu aipatayo mtu kutoka Chuo Kikuuu na huitwa Doctor
anapoipata, kuna wengine huwa na Shahada zaidi ya 3, kwa kujikusanyia
Shahada kutoka vyuo vikuu mbalimbali. Anayeongoza duniani kuwa na
Shada nyingi kutoka vyuo vikuu vilivyokuwa ni vingi ni mzee wa miaka 72
Michael Nicholson wa Kalamazoo huko Marekani akiwa na Shahada kwa
ujumla 29 kuelekea 30 : http://abcnews.go.com/US/michigan-man-29-collegedegrees-stopping/story?id=16597200
2.Rais wa Zimbabwe ndio Rais mwenye Shahada nyingi za vyuo vikuu
Barani-Afrika akiwa na Shahada 7. Shahada zake mbili alizipata akiwa jela na
moja ya Master aliipata akiwa kishakuwa Rais wa Zimbabwe : http://www.
universityworldnews.com/article.php?story=20101029224442993
3.Aliyekuwa kiongozi mkuu wa kampuni ya Armament ya Afrika ya Kusini,
Shamim chippy Shaik alipokonywa Shahada yake ya Phd kutoka Chuo
Kikuu cha Natal ambacho kwasasa kinajulikana kwa jina la KwaZulu Natal
mwaka wa 2008 baada ya kugundulika kuwa katika risala yake zaidi ya
asilimia 75 alidokoa maandishi yake : http://www.usnews.com/education/
best-global-universities/articles/2012/05/02/10-high-profile-people-whosedegrees-were-revoked
4.Ikiwa muamko wa kusoma Vyuo Vikuu unaongezeka Barani Afrika na
kuwa na wafanyakazi wengi waliopitia vyuo vikuu, kinyume chake nchi
ya Uiengereza ina watu kwa idadi ya wastani wasiopita vyuo vikuu wala
kutegemewa kufana hivyo : http://www.theguardian.com/higher-educationnetwork/blog/2013/jun/04/higher-education-participation-data-analysis
5.Inakisiwa kuwa duniani kuna watu wenye Sahahada ya vyuo vikuuu
wafikao asilimia 6.7 tu : http://www.huffingtonpost.com/2010/05/19/percentof-world-with-col_n_581807.html
6.Vyuo vikuu vilio bora duniani vimewekwa na ubora wake Chuo Kikongwe
Tanzania, Chuo cha Dar es Salaam (University of Dar es Salaam) kimewekwa
daraja ya +701 : http://www.huffingtonpost.com/2010/05/19/percent-of-worldwith-col_n_581807.html
7.Chuo Kikuu cha Massachusetts Institute of Technology ndio Chuo Kikuu
namba mmoja duniani : http://www.topuniversities.com/university-rankings/
world-university-rankings/2013#sorting=rank+region=+country=+faculty=+s
tars=false+search=
8.Vijue vyuo Vikuu 10 vinavyoongoza duniani, Chuo cha Stamford
kinashikilia nafasi ya 3, Havard namba 2, Oxford namba 6 n.k.: http://www.
topuniversities.com/student-info/videos/top-10-universities-world-201516
9.Kuna vyuo vikuu visiopungua 23,729 duniani: http://www.webometrics.
info/en/node/54
10.Donald Trump ni mgombea wa Rais wa kupitia chama cha Republican
nchini Marekani aliozusha tafrani za Waislamu wasiruhusiwe kuingia nchi ya
Marekani, katika mmoja ya hotuba zake amesema kuwa wale waliokwenda
Skuli na Rais Obama hawajapata kumuona : http://www.politifact.com/
truth-o-meter/statements/2011/feb/14/donald-trump/donald-trump-sayspeople-who-went-school-obama-nev/
Habari
AN-NUUR
wamegawanywa katika
makundi mawili tofauti
moja linatuhumiwa kwamba
lilikutwa Msikitini, wakidaiwa
kukutwa na milipuko na
kundi la pili ni lile lilohusu
kamatakamata ya Polisi,
akiwemo mwanafunzi Juma
Ismail (13), aliyekamatwa
akiwa Msikitini Kilombero.
Ust. Kitunga, alisema
katika hati zao za mashitaka
zinaonyesha kuainishiwa vitu
walivyo kutwa navyo ikiwa ni
milipuko, sare za Jeshi pamoja
na kuhusishwa na mauaji.
Tahariri
AN-NUUR
Majipu Mahakamani,
Polisi yanacheleweshwa
TANGU Rais wa
awamu ya tano ya
serikali ya Jamhuri
ya Muungano
Rais John Pombe
Magufuli, iingie
madarakani, kazi yake
ya kwanza kabisa
ambayo imeifanya na
inaendelea kuifanya
ni kuboresha utendaji
na uwajibikaji wa
watumishi wa umma,
kupambana na rushwa
na ubadhirifu wa mali
ya umma, kusimamia
na kufuatilia
kukusanya kodi na
kubana matumizi ya
serikali.
Rais Magufuli
na safu yake ya
uongozi wa juu
serikalini wamekuwa
wakiendesha
operesheni hii ya
kudhibiti utendaji kwa
watumishi wa umma
na kuwawajibisha
wale wanaobainika
kwenda kinyume na
maadili ya kazi, kwa
mtindo unaoitwa wa
kutumbua majibu.
Kama uadilifu
unachukua nafasi yake
katika utumbuaji huo
wa majibu, bila shaka
huo utakuwa mwanzo
mzuri kwa Rais
Magufuli na wenzake
kutengeneza serikali
inayowajibika barabara
kwa wananchi, tofauti
na serikali za Marais
wa awamu zilizopita.
Hata hivyo, kuna
Idara mbili muhimu
sana, ambazo kwa
hakika bado Rais
Magufuli hajasikika
kuchukua hatua za
kutumbua majipu,
licha ukweli kwamba
yapo na yanaonekana
dhahiri.
Sote tunatambua
kwamba amani na
usalama wa nchi
ndio kigezo kikubwa
na muhimu katika
AN-NUUR
walihojiwa, asilimia
50 waliitaja polisi
kukithiri kwa rushwa,
TRA (asilimia 37),
Mahakama asilimia
36, Takukuru asilimia
29 wakati maofisa wa
Serikali za mitaa ni
asilimia 25.
Utafiti huo ulibaini
kuwa miongoni mwa
watu watatu ambao
wanaenda kupata
huduma Polisi na
mahakamani, mmoja
kati ya watu hao
anadaiwa rushwa.
Watu wanane
kati ya 10 ambao
walihojiwa ambao
tayari walishatoa
rushwa, walikiri kuwa
hawakutoa taarifa
mahali popote licha ya
kutoa rushwa.
Pia utafiti huo
ulibaini kuwa asilimia
34 ya wahojiwa,
walitoa rushwa
wakati wanatafuta
haki mahakamani na
wengine asilimia 34
walitoa rushwa kwa
kuepuka usumbufu wa
Polisi.
Ni tafiti nyingi
zimethibisha kuoza
kimaadili katika
taasisi zetu hizi nyeti
za kusimamia haki na
usalama wa raia.
Rais JPM na serikali
yake wana kazi
kubwa kumaliza
P.O. Box 90042, +255 713 586 186 au 713 455 255
Dar es Salaam, Tanzania
AN-NUUR
pamoja na watuhumiwa
wengine 114.
Mwanasheria huyo
aliyenukuliwa akizungumza
kwa hasira alisema, Hii
inadhihirisha kuwa Jaji
hakuisoma wala kuitafakari
kesi iliyokuwa mbele yake
na huu ni ushahidi kwamba,
hakuna haki nchini Misri.
Inaelezwa kuwa zaidi
ya wanachama 40,000 wa
upinzani wakiwemo wafuasi
wa Ikhwanul Muslimin,
wanazuiliwa katika
mazingira ya kutisha katika
korokoroni za nchini Misri
bila kuthibitika kufanya kosa
lolote.
Maelfu ya watu
wamewekwa kizuizini nchini
Misri baada ya jeshi la Misri
likiongozwa na Jenerali Abdul
Fattah al-Sisi, Julai mwaka
2013 kuiondoa madarakani
serikali ya Muhammad Morsi,
Rais wa kwanza kuwahi
kuchaguliwa kidemokrasia
katika nchi hiyo ya Kaskazini
mwa Afrika.irib
Makala
AN-NUUR
yanahaitajiwa!
Unakwenda Brazil, huko
Amazonia. Unazungumza na
watu katika mapori na katika
maeneo yaliyokuwa makazi
duni ya kujazana mijini. Watu
wanakwambia kuwa hali sasa ni
nzuri kuliko mwanzoni, ikiwepo
serikali ya kijamaa kwa miaka
mingi sasa. Halafu unafungulia
televisheni ya O'Globo usiku; na ni
uharo tu mara nyingine tena.
Upo Zimbabwe, ambako
ulishaambiwa utazamie uchafu
umezagaa na shida nyingi.
Unatokea Nairobi inayofuata nyayo
za nchi za Magharibi ambako
zaidi ya asilimia 50 ya wananchi
wanaishi katika makazi mjazano
ya kutisha. Jijini Harare, mji mkuu
wa Zimbabwe, ni nadra kuona
makazi duni, ila kuna utamaduni na
ujenzi wa miundombinu, pamoja na
kiwango kikubwa zaidi cha kusoma
na kuandika katika Bara lote la
Afrika. Jiji liko safi. Lakini unasoma
jarida la The Economist na takriban
machapisho mengine makubwa
yote ya Uingereza na unaambiwa
kuwa nchi hiyo inachungulia
kaburi.
Unakwenda China... Kila kitu
kimepinduka ukilinganisha na kile
ulichokuwa unatazamia, ukisoma
magazeti ya nchi za Magharibi.
Katika Jamhuri ya Watu wa China
unaona taifa la Kikomunisti
lenye malengo halisi ya baadaye,
likiwa na uhuru zaidi wa sanaa na
fikra kuliko unavyoweza kukuta
kokote barani Ulaya, na pia nafasi
nyingi zaidi. Lakini unaporudi
Paris au London na kuzungumza
ulichokiona, unachekwa.
Uhalisia bandia umeshinda. Hasa
katika nchi za Magharibi, takriban
kila mmoja amenaswa hapo,
amepigwa na bumbuazi.
Uhalisia rahisi na wa kweli
unatemewa mate, unanyanyaswa,
unabezwa na siyo tu na vyombo vya
habari na vianzio vya propaganda,
kama zamani. Wengi zaidi kati ya
watu wa kawaida nchi za Magharibi
kwa unyenyekevu na kujiamini
katika haki ya wanachofanya
wanajitolea: wanahisi kuwa
inawapasa kudhihirisha utiifu wao
kwa kile serikali zao zinachosema.
Wanafanya hivyo huku wakijisifu
kwa nguvu kuhusu demokrasia,
uhuru binafsi na uhuru wa kisiasa
katika sehemu yao ya dunia.
Cha kushangaza ni kuwa jinsi
wanavyozidi kunyonywa bongo,
Makala
Na Rashid Mtagaluka
AN-NUUR
8
BILA shaka wengi tunakumbuka
sakata la sensa ya watu na makazi
mwaka 2012. Baadhi ya Waislamu
waligoma kuhesabiwa kwa sharti
la kuwekwa kipengele cha dini ili
kuondoa utata uliojitokeza kuhusu
idadi ya watu kwa munasaba wa
dini zao. Serikali yetu ilipinga
sharti hilo.
Mgomo wa baadhi ya Waislamu
HAO ulitokana na taarifa zisizo
rasmi zilizopeperushwa hewani
na TBC. Tulipinga kauli za
madai kwamba, Waislamu tuwachache kwa kurejea takwimu
mbalimbali za sensa zilizotangulia.
Tulikuwa na haki hiyo kwa kuwa
hatujawahi kupewa taarifa za
kutokea maafa yaliyopelekea
Waislamu kupungua. Lakini pia,
hata idadi ya Waislamu kuingia
dini zingine haioneshi kuwa na
athari ya kutosha kufanya idadi ya
Waislamu ipungue. Tulichonyimwa
hapa ni VIGEZO vilivyotumika
kusema kwamba huyu ni Muislam
na yule siye! Na hapa ndipo lilipo
tatizo na utata ambao ulipelekea
Waislamu wengi kuingia matatizoni
kwa kupigwa, kudhalilishwa na
kushitakiwa.
Kila mmoja amepewa akili
na uwezo wa kufikiri tofauti na
mwenzake. Ndiyo maana Allah
Mtukufu amewasifu wale wenye
kufanya mambo yao kwa shura,
kwa kuwa yeye anatufahamu
zaidi kuliko tunavyojifahamu sisi.
Anasema Mwenyezi Mungu.
Katika dodoso la sensa, mtu
huulizwa mambo mengi ambayo
ndiyo msingi wa kupatikana taarifa
itakayokuwa na mchanganuo wa
Makala
Hoja si wingi
AN-NUUR
Inatoka Uk. 7
ubavuni, miguuni na kifuani
kutokana na vipigo nilivyopata.
Sikuweza kulala kwa masiku.
Baadae nikapelekwa kituo cha
polisi cha Shitakishari, Buguruni
na Msimbazi pamoja na wenzangu
niliowakuta shimoni tukiwa
tukihamishwa siku baada ya siku.
Baadae tukarudishwa
shimoni pale tulipotoka Central
Police. Kutoka hapo sasa ndipo
tukapelekwa Oyster Bay kwa
mahojiano na Task Force ambacho
ni kitengo maalum kwa ajili ya
ugaidi.
Walionihoji hapo Task
Force waliniambia kuwa
mateso niliyokwishapata huko
nilikotoka ni madogo, hapo
nitapata mateso makubwa zaidi.
Wakanitahadharisha kuwa itabidi
nionyeshe silaha ziko wapi kabla
hawajanishughulikia zaidi anazidi
kuweka wazi Ustaadh Yassin.
Maswali yakawa ni yale yale na
akaanza kupigwa safari hii miguuni
baada ya kufungwa katika kitu
kama pipa ambacho kinashikilia
miguu. Anasema alipigwa hadi
akawa hawezi kusimama. Kutoka
hapo sasa akapelekwa Mikese,
Morogoro. Wakati anapelekwa
huko alikuwa amefungwa kitambaa
cheusi usoni.
Hapo Mikese ni sehemu ya
wazi hatukuwa ndani ya majengo.
Hapo panaitwa gereji, kwa
kuwa hapo ni sehemu makhsusi ya
kuwashughulikia Waislamu.
Makala
AN-NUUR
Na Nizar Visram
TAREHE 1 Februari mwaka
huu tulitangaziwa kuwa
Rais mstaafu Jakaya Kikwete
ameteuliwa na Umoja wa
Afrika (AU) kuwa mwakilishi
wake katika mchakato wa
kusuluhisha mgogoro wa Libya.
Uteuzi huo ulifanywa mjini
Addis Ababa katika kikao
cha wakuu wa nchi za Afrika,
naye Kikwete amewashukuru
wakuu wa nchi za AU kwa
imani kubwa waliyoonyesha
kwake na pia amewashukuru
wadau wa siasa nchini Libya
kwa kuridhia uteuzi wake. AU
imemueleza Kikwete kuwa
inayo matarajio makubwa juu
yake na iko nyuma yake.
Katika jukumu hili, Kikwete
atakuwa anaongoza jopo la
marais watano walioteuliwa na
AU. Kazi yao kubwa itakuwa
ni kusuluhisha makundi
yanayounda serikali mbili
tofauti nchini Libya moja iliyo
mashariki ambayo inatambuliwa
na Umoja wa Mataifa (UN) na
ya pili iliyo katika mji mkuu wa
Tripoli ambayo inatawala kwa
kutumia majeshi.
Ni vizuri tukajiuliza kama
imani hii ya AU inatosha, kwani
bila shaka Kikwete atakumbwa
na matatizo yanayotokana na
mapigano yanayoendelea tangu
Libya kuvamiwa na majeshi
ya NATO, ikapelekea kuuliwa
kikatili kwa mtawala wa nchi
hiyo Muammar Gaddafi miaka
mitano iliyopita. Kikwete siyo
tu atakumbana na matatizo ya
ndani, bali pia na mataifa ya
NATO ambayo yana nia tofauti
na ile ya AU. Wakati AU inataka
ushuluhishi kwa njia ya amani,
NATO kama kawaida yake
inajiandaa kutumia nguvu zake
za kijeshi. Ili kulielewa hili ni
vizuri tukaangalia chimbuko la
mgogoro huu.
Mnamo mwaka 2011 Gadhafi
alipinduliwa na akauliwa
baada ya uvamizi wa majeshi
ya NATO. Walifanya hivyo
kinyume na azimio la Umoja wa
Mataifa (UN) ambalo halikutoa
idhini ya kuishambulia Libya.
Sasa imetimia karibu miaka
mitano na Marekani na wenzake
wa NATO wanapanga uvamizi
mwengine katika nchi hii
inayoongoza kwa utajiri wa
mafuta barani Afrika. Haya
yamesemwa na Marekani
wenyewe.
mujahidina wenzao
Wanaweza wakaelekea hadi
nchi za Ulaya. Ikumbukwe
kuwa kisiwa cha Italy kiitwacho
Lampedusa ni maili 200 tu
kutoka Libya. Hili ni tishio
kubwa kwa nchi za magharibi.
Hivyo kinachotia hofu na
wasiwasi zaidi kwa mataifa
ya NATO ni kuwa hawa
mujahidina wa Daesh wanaweza
kutumia Libya ili kuvuka bahari
ya Mediterania na kuingia Ulaya
ambako tayari kuna vijana
watakaosaidiana na wenzao
kutoka Libya. Ikumbukwe kuwa
Daesh ni kikosi cha kimataifa
na wala si Waarabu peke yao.
Inasemekana wametoka nchi 60
duniani.
Nchini Libya majeshi
yanadhibiti sehemu kubwa
mashariki mwa nchi, wakati
makundi kadha ya mujahidina
yako magharibi ambako
wameunda Baraza la Vijana wa
Kiislamu (Majlis Shura Shabab
Al Islam - MSSI)
Ni mwezi uliopita tu Daesh
wamefanikiwa kudhibiti
machimbo mawili ya mafuta
maeneo ya mashariki ambayo
yanazalisha asilimia 80 ya
mafuta yote ya Libya. Inakisiwa
kuwa Daesh ina wapiganaji
takriban 3,000 na wanadhibiti
kilometa 300 za mwambao.
Wengi wao ni kutoka nje ya
Libya na wamekuwa wakipigana
nchini Iraq na Syria. Mnamo
Novemba walipouchukua mji
wa Darna walianza kubomoa
maduka ya manukato na
mapambo ya kina mama,
pamoja na saluni. Wengi wao
ni wafuasi wa Gaddafi ambao
waliingia mitini baada ya rais
wao kuuawa mnamo Oktoba
2011. Ni sawa na wafuasi wa
Saddam Hussein (Iraq) ambao
walijiunga na Daesh baada ya
rais wao kukamatwa mnamo
2003 na kunyongwa.
Leo wakati NATO
inajitayarisha kuivamia
Libya kwa mara ya pili, AU
nayo inamteua Kikwete
kusuluhisha kwa njia ya amani.
Inatukumbusha mwaka 2011
wakati AU pia ilijaribu kuzuia
mashambulizi ya NATO lakini
ikashindwa. Tarehe 23 Februari
2011 wakati vurugu zipoanza
nchini Libya, Baraza la Amani
na Usalama la AU (PSC)
lililaani utumiaji wa nguvu
kukandamiza maandamano ya
wananchi dhidi ya utawala wa
Gaddafi. Hata hivyo Baraza hilo
halikukubaliana na msimamo
wa NATO wa kuivamia kijeshi
Libya.
Tarehe 10 Machi 2011 PSC
ikaandaa mpango wa kuzuia
vurugu kwa njia ya maridhiano.
Pande zote zilitakiwa ziache
kutumia silaha na badala yake
zianzishe mazungumzo ya
amani. Kamati ya AU ikateuliwa
ili kufuatilia jambo hili kwa
kuonana na wahasimu.
Kamati hiyo ikaandaa safari
Inaendelea Uk. 16
10
Makala
Na Omar Msangi
AN-NUUR
Gogu wa Magogu!
11
Inatoka Uk. 10
Makala
Gogu wa Magogu!
ulimwengu) kutokana na
jinsi walivyoripoti suala la
IS katika Syria. Ufupi wa
maneno anachosema katika
Makala yake; The Media
are Misleading the Public
on Syria, ni kwamba wale
magaidi IS na wenzao
wengine wanaoungwa
mkono na Marekani na
NATO, ndio wanaoonekana
wakombozi wa Syria,
huku Urusi inayowapiga
kikweli magaidi IS,
inaonekana kuwa ndio
muuwaji. Katika lugha ya
Bush, anachosema Stephen
Kinzer ni kuwa wakati
Marekani na washirika
wake waliowatengeneza
IS na kuwatuma kazi
Syria, wanapaswa
kuonekana kuwa ndio
Gogu na kupigwa vita na
AN-NUUR
12
13
AN-NUUR
14
MAKALA/MASHAIRI
Laata na Ng'uza
AN-NUUR
Gogu wa Magogu!
Inatoka Uk. 11
wanaotenda aibu
hii ya Karne, BBC,
Fox News, New
York Times, CNN,
na wengine, ndio
walimu wetu na
tumekuwa kama
vipaza sauti vyao.
Kwa hiyo tunaingia
katika ukahaba
huu, tena kwa
namna mbaya kabisa
inayotudhuru sisi
wenyewe.
Wanasiasa wetu na
watendaji serikalini
na katika vyombo
vya dola nao ni
hivyo hivyo. Bush,
Obama na Cameroon,
wakisema yule ni
Gogu wa nchi ya
Magogu, mkuu wa
Roshi, Mesheki na
Tubai, apigwe, nasi
tunaimba wimbo huo
huo. Bila kujua kuwa
tukiwapata akina
Gogu wetu bandia,
ndio tunamfungulia
milango Gogu wa
kweli aweke kambi
zake za kijeshi
apate kutudhibiti
kisawasawa na
kupora atakacho na
atakavyo. Agenda
yake ya Hegemony
inatimia.
Dhul-Qarnayn
Katika Quran
Gogu ametajwa
kama Yaajuju na
Maajuju ambapo
ilibidi apatikane Dhul
Qarnayn wa kujenga
ukuta mkubwa na
madhubuti kumzuiya
Yaajuju kuingia
katika miji ya watu
kufanya ufisadi. Ili
kuepuka ufisadi,
uovu na agenda
chafu zilizobebwa
na vita hii feki
dhidi ya ugaidi,
Dhul-Qarnayn
tunayemuhitajia ni
vyombo vya habari
na wanasiasa walio
tayari kusema ukweli
na kufichua uwongo.
Na kwa maana hiyo,
ule ukuta aliojenga
Dhul-Qarnayn,
kama ilivyokuja
katika Surat Kahfi, ni
kusema ukweli.
Mwandishi
Finian Cunningham
amefanya utafiti
na kuandika
alichokiita Pentagon
Mercenaries:
Blackwater, AlQaeda whats in
a name? Humo
anaeleza jinsi
makampuni binafsi
yanavyotumiwa
kutengeneza magaidi
wa kuwafanyia kazi
mabeberu. Anatoa
mfano wa Komandoo
Erik Dean Prince
ambaye zamani
alikuwa katika
kikosi maalum cha
makomandoo wa
jeshi la Marekani
(US Special Forces
commando) ambaye
sasa hivi ameanzisha
kampuni iitwayo
Blackwater (baadae
Xe Services and
Academi), ambayo
imekuwa wakala
mkuu wa Pentagon
katika kuunda
na kutengeneza
wapiganaji binafsi
(rebels). Kampuni
hii imefungua tawi
Mashariki ya Kati
likijulikana kwa jina
la Reflex Responses au
R2. Na kwa mujibu
wa taarifa moja ya
The New York Times,
R2, ndiyo inafanya
kazi ya kutoa
mafunzo na kuunda
vikosi vya magaidi na
wapiganaji waliopo
Yemen na Syria.
Sasa kama
wapo vijana wetu
wa Kitanzania/
Afrika, walionasa
katika chambo
cha makachero
na majasusi wa
mabeberu, tusiwaone
kuwa hao ni Gogu.
Tujue kuwa ni
waathirika tu wa
mbinu chafu za
Gogu na mikakati
ya akina Erik Prince
na R2 zao. Kwa hiyo
tutafute namna ya
kuwatibu. Sio kupigia
zumari u-Gogu wao
bandia. Tutakuwa
tunawafanyia kazi
akina Bush.
Kama tuna
matatizo na Sheikh
Msellem juu ya
msimamo wake
katika siasa zetu,
tuseme lililo la kweli.
Tusiparamie agenda
ya akina Bush ya
kutumia vipengele
vya Biblia kumwita
Saddam Hussein
kuwa ni Gogu wa
Magogu.
15
Habari/Makala
Nasaha
Umuhimu wa kuchunga wakati
KILA sekunde moja
inapoondoka, hairudi na
wakati wako wa maisha
unazidi kupungua. Saa,
siku, wiki, mwezi, mwaka,
muongo na hata karne,
ni vipindi vya muda na
nyakati, ambavyo vikipita
havirudi tena. Kadiri
wakati unavyopita na umri
nao unasogea kuelekea
ukingoni mwa maisha.
Kwa kuwa muda
au nyakati zinapita na
kupunguza umri, basi
kuna haja ya wanadamu
kutafakari juu wa wakati
walinao. Anafanya nini na
kwa maslahi gani.
Wakati ndio unaotoa
fursa ya kupanga ratiba
ya kutenda na kuwa na
mpangilio wa maisha ya
kila siku. Kwa mantiki hiyo,
haliwezi kuwa jambo zuri
kwa wanadamu kupoteza
wakati. Tusipoteze muda
kwa kufanya mambo ya
kipuuzi hali ya kuwa kuna
mambo mengi, ambayo
yanaweza kutushughulisha
na yenye faida hapa
Duniani na huko akhera.
Kwa msingi huo, ni
vyema Waislamu wakawa
mfano wa kutumia wakati
vizuri. Kupanga matumizi
mazuri ya muda kwa kuwa
walishabainishiwa katika
Quran kwamba, kila jambo
la kheri ni ibada.
Mwenyezi Mungu
anasema katika Quran,
Nami sikuwaumba majini
na watu ila waniabudu
Mimi.
Hapa linabainishwa
wazi kuwa lengo kuu la
Mwenyezi Mungu (sw)
kuwaumba wanadamu ni
kumuabudu Yeye pekee.
Wanachuoni wa Kiislamu
wanafafanua zaidi kwamba
maana ya ibada kwa ujumla
wake ni kila anachokipenda
Mwenyezi Mungu na
kukiridhia, hiyo ni ibada
bila shaka.
Kwa maana hiyo
wanadamu wajifunze
kuacha kuishi kwa mazoea
kwa kuwa wanakula,
wanalala na wanapumua.
Kwamba wanaweza
kufanya vyovyote bila
kuathiri muda wao wa
maisha hapa duniani. Inafaa
tuzingatie sana kutumia
muda katika mambo
mema na mazuri, ambayo
yatawakurubisha zaidi kwa
Mola.
Tumia muda kwa
kufanya kazi halali
unayoweza kukupa kipato
cha kusaidia kuendesha
maisha. Tumia muda
kumuabudu na kumuomba
Mwenyezi Mungu, tumia
muda kusoma Quran ili
kujifunza moja au mawili
ambayo yatakusogeza
zaidi kwa Allah (Sw) na
kumjua Mola wako na yale
aliyotuamrisha kutafuata
hapa duniani katika maisha
yako. Furahi na familia
yako, tumia muda wako
kupumzika na kustarehe
katika starehe za halali,
tumia muda katika kutenda
mema katika jamii nk.
Kwa kujali muda, ni
rahisi kuepuka kufanya
mambo ya kipuuzi,
ambayo hayatokusaidia
hapa duniani wala Akhera.
Ni muhimu sana kuacha
kuishi na kutenda kwa
mazoea, kwa kuwa wakati
hautabiriki na kwa kuwa
watu hawajui muda wala
saa ya kuondoka hapa
duniani.
Tukumbashane tu
kwamba, kila Muislamu
hawezi kufika ngazi yeyote
siku ya Kyama hadi pale
atakapojibu maswali manne
ya Allah (sw). Miongoni
mwa maswali hayo ni
lile litakalohoji namna
ulivyotumia muda wako
katika maisha ya duniani.
Yaani muda wako uliutumia
katika kufanya mambo gani.
Uliutumia katika mambo ya
heri au ya shari.
Mwenyezi Mungu
kaumba usiku na mchana
kwa makusudio maalum.
Akashauri wanadamu
watafute riziki mchana
na usiku mpumzike.
Ndio maana usingizi wa
usiku haukwepeki. Hata
ukilazimika kutolala usiku,
mwisho wake ni kupatwa
na maradhi na hutamudu
kuukosa.
Hata vipindi vya swala
vimewekewa wakati wake
maalum. Hii ni ishara tu
kwamba Mwenyezi Mungu
ametaka kutudhihirishia
umuhimu na utukufu wa
wakati. Nakumbusha tu
kwamba, kuna haja ya
kupangilia shughuli zetu
kwa kujali sana wakati.
Ishini kwa kufanya
ibada kwa wakati na hapo
mtakuwa mmeoinyesha
jamii tabia sahihi ya
Kiislamu, nanyi mtakuwa
kiigizo chema kwa
walimwengu.
Inshaallah Mwenyezi
Mungu awajaalie muwe
miongoni mwa wale
wenye kusikia machache
na kuyazingatia. Na
awawezeshe katika umri
wenu uliobaki, muweze
kuutumia muda wenu
vizuri kwa kutenda
yale anayoyapenda na
kuyaridhia.
Na Shaban Rajab
AN-NUUR
Inatoka Uk. 12
170 m/t (metric tones)
ikifwatiwa na Afrika
ya Kusini 970,795 m/t,
Marekani 585, 788 m/t. Misri
454,407 m/t na Morocco 294,
572.
Jambo ambalo ni
tatizo kubwa kwa nchi
zinazoendelea hasa nchi
za Kiafrika nikuwa kilimo
kimekuwa kama wenyewe
tusemavyo ni kazi ya jadi
wala sio kama tumekiweka
kitupeleke mbela na kuja
na mbinu za kila aina juu
ya ukulima. Machungwa
kwetu huwa ni fruti ya
msimu, msimu ukisha
machungwa hayaonekani
na yakipatikana bei yake
hapo utasema unataka
chungwa kwa dawa lazima
ulipate kwahio utajitaarisha
Inatoka Uk. 13
anayokwenda Ulaya,
aliyotumwa akamjibu
yupo pahali sawa, binti
akasema haiwezi kuwa,
akawa anajipanga sasa
kwenda kumtoa yeye
mwenyewe kilichomudhi
hakifahamiki, lkawa
anamuhudumia msafiri
wa Kifaransa ambaye
hajui Kiengereza, ikawa
vuta ni kuvute na wakati
unakwenda Sayyid Omar
akamsogelea yule bibi wa
Kifaransa na kumuamikia
kwa Kifaransa na kutaka
kujua nini shida yake,
akawa Sayyid Omar
sasa anatafsiri kutoka
Kifaransa anapeleka
kwa Kiengereza kwa
mratibu wa Tiketi, binti
wa Kikenya hakuamini,
kuambiwa wanapanga
njama ya kupindua
Serikali, akawekwa
korokoroni kwa mwezi
mmoja badaye ilikuja
kuelekweka kuwa
ilikuwa ni fitna tu,
tena hapo Mzee Abeid
Amani Karume akaamua
kuwachia, afya yake
iliathirika sana kwani
akisumbuliwa na kisukari
na akawa hapati dawa
ya kupiga shindano ya
Insulin. Sayyid Omar
baada ya kutolewa jela
alikuwa akiishi na khofu
akaona asije akafungwa
tena akaamua kuhama
Zanzibar huku tayari
kapatiwa nafasi ya
kurudi Uiengereza lakini
aliona vyema kwenda
kuishi katika visiwa vya
Comoro ambavyo ana
nasaba navyo.
Safari mmoja akiwa
anasafiri kutokea
Kenya anaelekea Ulaya,
amesimama kwenye
foleni, binti wa Kikenya
alio katika kupima
mizigo na kutoa namba
ya viti kwenye ndege
kumuona mzee na
majuba na kashika
bakora akamshika
kumwambia eeh muzee
nenda kwenye foleni
ile ya kwenu Mombasa,
ndege itakukimbia.
Sayyid Omar alikaa
kimya lakini jeuri ya
kitoto ikazidi kwa
kumtaka mmoja ya
wafanyakazi kumtoa
kwenye Foleni, Sayyid
Omar akatoa Pasi ya
kusafiria ikiwa na hadhi
ya kidiplomasia na
mrundo wa tiketi, mpaka
akaiona tiketi yake
alivyoyasuluhisha
binti akataka kujua
wapi aliposoma kujua
Kiengereza na Kifaransa,
16
Makala
AN-NUUR
17
Na Shaban Rajab
NABII Muhammad (saw)
alipotumwa na Mwenyezi
Mungu Mtukufu kuja
ulimwenguni kuuhusisha
Uislamu ulioasisiwa na
Mitume waliomtangulia,
alimkuta mwanamke
akiishi chini ya
mazingira na kivuli cha
ukandamizaji.
Katika ulimwengu
ule, mwanamke hakuwa
na haki yeyote katika
jamii zaidi ya kuonekana
kama bidhaa inayoweza
kuuzwa wakati wowote.
Mwanamke alichukuliwa
kama ni chombo cha
kumstarehesha na kukidhi
matamanio ya kimwili ya
mwanamume. Mwanamke
alihesabika kuwa ni chombo
cha uzalishaji, hakuwa
na uhuru wa kupanga na
kuamua. Kwa ufupi haya
ni sehemu ya mazingira
ambayo Uislamu ulimkuta
mwanamke akiishi hapa
duniani.
Kwa rehema za
Mwenyezi Mungu, Uislamu
kupitia kupitia kwa
Mtume Muhammad (saw),
ukamuondolea mwanamke
unyonge, udhalili, dhulma,
uonevu na unyanyasaji
uliokuwepo. Uislamu
ukamjengea mwanamke
mazingira bora, kanuni na
sheria ambazo zilihakikishia
uhuru, usalama, amani,
haki na usawa katika jamii
yake. Kupitia mafundisho
ya Mtume Muhammad
katika Uislamu, mwanamke
aliwekewa mazingira ya
kujiona kuwa ni binadamu
kamili, mwenye haki
sawa kama mwanamume
na ukamhakikishia
kupata haki zote kama
binadamu, bila ya kuhitaji
upendeleo maalum kama
inavyofanyika sasa.
"Wanawake ni ndugu
baba mmoja, mama
mmoja na wanamume,
wanayo haki kwa sheria
(kufanyiwa na wanamume)
kama ile haki iliyo juu yao
kuwafanyia wanamume"
Abu Dawoud.
Kwa jicho la mfumo
kamili huu wa maisha
(Uislamu) wanamume na
wanawake kiasili ni sawa
sawa bila tofauti yeyote
mbele ya Mola wao.
Ila tofauti na ubora
utajitokeza katika amali
njema anazozifanya kila
mmoja wao. Ni dhahiri
kuwa mzuri na mwingi
wa amali njema hawezi
kulingana sawa na mchache
wa amali njema bila ya
kuangalia ni mwanamume
au mwanamke. Hii ndio
mojawapo wa misingi na
kanuni za Uislamu.
Pamoja na kwamba
wengi hawajui, iwe ni kwa
makusudi au kwa kutotaka
kujifunza, mwanamke ni
kiumbe aliyetoa mchango
mkubwa sana katika kuenea
kwa Uislamu tangu enzi za
Mtume wetu Muhammad
(saw). Mtume Muhammad
alipata msaada mkubwa
sana kwa wanawake katika
kueneza ustaarabu wa
Kiislamu.
Leo nitamzungumzia Bi.
Khadija bint Khuwaylid,
mke wa kwanza wa Mtume
(saw). Yeye aliolewa
MAKALA/TANGAZO
AN-NUUR
akiwa na miaka 40 na
Mtume Muhammad (saw)
akiwa na miaka 25. Kwa
kifupi ni kwamba Mtume
Muhammad alimuoa
Bi. Khadija hata kabla
ya kupewa Utume na
Mwenyezi Mungu.
Bi. Hadija alizaliwa
katika mji wa Makkah
katika familia yenye
heshima. Baba yake alifariki
katika vita. Mama yake ni
Fatima bint Zaidah.
Hata hivyo katika
mtandao wa al-islam.org,
inaelezwa kuwa kabla ya
kuolewa na Mtume (saw),
Bi. Khadija aliwahi kuolewa
mara mbili na Abu Halah
bin Zaraarah na Atiq bin
Aaid. Alijaaliwa watoto
katika ndoa hizi, nao ni
Hind na Haalah (alizaa
na Abu Haalah) na Hind
aliyezaa na Atiq.
"Mwana Khadija kabla ya
kuolewa na Mtume (s.a.w.)
alikwisha olewa na waume
wawili kabla ya Mtume
Muhammad (s.a.w.) na
amepata watoto wawili.
Zimetaja kidogo baadhi
ya hoja zinazosemwa juu
ya Bi. Khadija kuhusu
watoto aliopata kwa waume
wengine kabla ya Mtume
Muhammad (s.a.w.) kama
ifuatavyo:
Wanasema shahidi wa
kwanza katika Uislamu ni
mtoto wa Mwana Khadija
aitwae Harithi bin Abi
Hala, alipata shahada pale
Mtume (s.a.w.) alipotangaza
Uislamu hadharani. Al'
Isaba J. 1 Uk. 293, Al'Awaail
J. 1 Uk. 311-312.
Hata hivyo katika riwaya
ya Qatada inasema kuwa,
shahidi wa kwanza katika
Uislamu ni Sumaiya, mama
yake Ammar bin Yasir. Al'
Isaba J. 4 Uk. 335.
Pia imepokewa kuwa
Bi. Khadija (a.s) alikuwa
na nduguye akiitwa
Hala, aliolewa na mtu
mmoja katika koo ya Al
Makhzumi, akazaa mtoto
wa kike aliyeitwa Hala,
kisha aliachika akaolewa na
mtu mmoja katika koo ya
Tamim aitwaye Abu Hindi,
akamzalia mtoto jina lake
Hind.
Huyo Abu Hindi,
alikuwa na mke mwingine
ambaye alimzalia watoto
wawili Zaynab na Ruqayya.
Hatimaye Abu Hindi na
mkewe wa pili walikufa,
akabakia Bi. Hala ndugu
ya Bi. Khadija, pamoja na
watoto wawili Zaynab
na Ruqayya. Yule mtoto
wake wa kuzaa, Hind,
alikwenda kwa jamaa
za mumewe. Ndipo Bi.
Khadija alipowakusanya
wote akawa nao, Bi. Hala na
watoto wawili walioachwa
na mama yao Zaynab na
Ruqayya.
Bi. Khadija alipoolewa
na Mtume (s.a.w.) Bi. Hala
alifariki, wakabaki Zainab
na Ruqaya wakilelewa na
Mtume (s.a.w.). Katika
mila za Kiarabu, walikuwa
wakiamini kuwa mtoto
18
TANGAZO
AN-NUUR
19
TANGAZO
AN-NUUR
AN-NUUR
20
20
MAKALA
Uchaguzi wa Bunge
Syria kufanyika Aprili
RAIS Bashar al-Assad wa Syria
ametangaza kuwa Aprili 13
mwaka huu wa 2016, kuwa siku
ya uchaguzi wa Bunge nchini
humo.
Taarifa ya Rais Assad,
imetolewa muda mfupi baada
ya Urusi na Marekani kutangaza
kuwa Februari 27 ndiyo tarehe
ya usitishaji vita katika nchi hiyo
ya Kiarabu.
Rais Bashar al-Assad
amebainisha kwamba, Damascus
mara kadhaa imekuwa ikieleza
kuwa, kutangaza tu mpango
wa usitishaji vita hakutoshi,
bali kuna haja ya jambo hilo
kutekelezwa kwa vitendo.
Hata hivyo mpango huo wa
usitishaji vita haujayajumuisha
makundi ya kigaidi na ISIS
na al-Nusra. Hii ni katika hali
ambayo, Rais Bashar al-Assad
ameiomba Jamhuri ya Kiislamu
ya Iran iendeleze misaada yake
kwa serikali ya Damascus katika
njia ya kupambana na magaidi.
Rais Bashar amebainisha
kwamba misaada ya Urusi
na Iran imekuwa na nafasi
muhimu katika kulifanya jeshi
la Syria lisonge mbele na kupata
mafanikio katika vita dhidi ya
waasi.
Hayo yanajiri siku chache
baada ya watu zaidi ya 80
kuuawa katika milipuko ya
mabomu katika mji mkuu
Damascus na mkoa wa Homs
siku ya Jumapili.
Mlipuko mmoja katika siku
hiyo ya Jumapili ulitokea katika
wilaya ya Sayeda Zeinab,
Damascus, karibu na Haram ya
Bibi Zeinab (SA), mjukuu wa
Mtume Mtukufu SAW.
Soma gazeti la
AN-NUUR
KWA TSH 800/=
kila Ijumaa
AN-NUUR
VIJANA wa Kiislamu
wametakiwa kutambua
kuwa wana dhima juu ya
kuisimamia dini yao kwa
kutumia neema ya ujana
wao.
Wito huo umetolewa na
Ustadhi Maulid Haruna
Nkumilwa, akiwahutubia
Waislamu katika ibada
ya Swala ya Ijumaa, wiki
iliyopita katika Msikiti wa
MSAUD, Jijini Dar es Salaam.
Ust. Nkumilwa, alisema
Alisema, kijana wa
Kiislamu anapoona kuna
matatizo katika dini yake,
hana budi kutumia fursa
ya ujana na elimu yake kwa
kuyatatua kwa kuzingatia
mafundisho ya Uislamu,
kupitia Qur an na Sunna na si
vinginevyo.
Alisema, katika usia wake,
Mtume (s a w) anasema,
tumia ujana wako, kabla ya
kufikiwa na utu uzima, na
kwamba hakuna kipindi
ambacho mtu anatakikana
kutafuta elimu kwa nguvu
kama mahala pa ujana.
silaha.
Uuzaji wa silaha duniani
umeongezeka kufuatia ongezeko la
vita na machafuko hususan katika
maeneo ya Mashariki ya Kati na
katika baadhi ya nchi za Afrika
katika miaka ya hivi karibuni.
Ripoti hiyo ya Februari 22,
2016 inaonesha kuwa Marekani
inaongoza katika biashara hiyo,
ambapo asilimia kubwa ya silaha
hizo wamekuwa wakiuziwa
makundi ya magaidi na baadhi ya
nchi za kiarabu.
Afisa mmoja mwandamizi
wa taasisi hiyo, Pieter Wezeman
alisema, muungano wa nchi za
Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na Business Printers Ltd, Dar es Salaam.