Академический Документы
Профессиональный Документы
Культура Документы
com
Sauti ya Waislamu
Waislamu, Wakristo
wamkosa Idrisa
Mimbar zitumike
vyema kutoa ujumbe
ANNUUR NEW.indd 1
3/30/2016 1:12:21 PM
Fethullah-Gulen
MWENYEZI Mungu
ndiye mjuzi zaidi wa
mahali atakapouweka
ujumbe wake. [Al AnAam 124]
Kuzaliwa kwa Uislamu
na ujumbe wake, katika
mji wa Makkah kisha
kuenea kwake katika
pande mbalimbali za
ulimwengu, baada ya
hapo kumejengwa juu
ya hekma nyingi sana
na kama ambavyo
kunawezekana
kuifanyia tathmini aya
tukufu:Mwenyezi
Mungu ndiye mjuzi zaidi
wa kupajuwa mahali pa
kuuweka ujumbe wake.
Katika mtizamo na
uelewa huu vile vile
kunawezekana kufanyia
tathmini kwa upande
wa elimu inayotafiti
asili ya binadamu na
maendeleo yake na
mazoea yake na itikadi
zake . Anthropology na
jiografia na Historian
na Ubinadamu na kwa
upande wa lugha na
mahali na baki ya vipeo
vyengine vya masuala
haya. Ndiyo hakika
Mwenyezi Mungu
mtukufu yeye ndiye mjuzi
sana wa yule ambaye
anamchagua kwa ajili ya
utume wake na kwa ajili
ya ujumbe wake na katika
jamii gani utadhihirika
ujumbe wake, na katika
ujumla wa mazingira
gani ya mapambano ya
kimataifa, na ya kidini
na kibinadamu na baada
ya kufikia mapambano
haya, kiwango gani ndipo
humpeleka Mwenyezi
Mungu mjumbe mpya
na dini mpya. Na sasa
tutayapekua mambo
hayo:
1. Upeo wa
ubinadamu kwa ajili
ya ujumbe: Aya hii
inaashiria kwenye
kwamba Mwenyezi
Mungu mtukufu
ndiye anayemjuwa
sana mjumbe ambaye
anamchagua na ataweka
kwake amana ya
kuufikisha ujumbe huu
ANNUUR NEW.indd 2
AN-NUUR
wa Mwenyezi Mungu na
yule ambaye kunafanyika
kuuelekeza ujumbe
huu. Na katika zama za
Mtume kulikuwa kuna
watu ambao wanadhani
kwamba Walid bin
Mughera na Urwa bin
Masoud A-Thaafi, ni
wabora sana kwa kupewa
ujumbe na wanafaa mno.
Na kwa hakika Quran
imetaja rai ya watu hawa
kwa hawa watu wawili
katika aya nyingine kwa
kusema: Na wamesema:
Kwanini isingeteremshwa
hii Quran juu ya mtu
kutoka miji miwili
ambayo ni mtukufu.
[A-Zukhruf 31] Quran
ikawa jibu kwa kusema:
Sisi tumegawa kati yao
maisha yao katika uhai
wa dunia. [Al-Zukhruf
32]. Na hapana shaka
kwamba masuala yote, na
jambo kubwa mno mfano
wa jambo la utume,
hakuwezekani kuliacha
kwa maoni ya huyu au
yule. Akiwa Mwenyezi
Mungu mtukufu anajuwa
na yeye anajuwa hapana
shaka yoyote siri za
binadamu ambazo
zimo katika raha ya
binadamu na moyo wake
na analenga kwenye
kuzihusisha siri hizo, kwa
huyo binadamu, yeye
ndiye anayejuwa sana
pasi na shaka yoyote, mtu
ambaye anafaa sana kwa
kusimama na jukumu
hili. Kwa msingi huu,
mtu ambaye anamtukuza
yeye Mwenyezi Mungu
mtukufu kwa ujumbe,
ndiye mtu anayefaa sana.
Kwa hakika kusimama
kwa Al-Walid Bin AlMughira na wengine
kwa kumdogosha
Mtume wetu (S.A.W.)
na kumwangalia kwa
kumzingatia kuwa hafai
kwa utume kitendo
hicho kinahesabiwa
kuwa ni kuchuma
madhambi makubwa na
wao kwa mtazamo huu
wameporomoka katika
mtazamo wa Mwenyezi
Mungu mtukufu.
Wameshuka kwenye
daraja la chini sana na
kwenye cheo duni sana.
Na Mwenyezi Mungu
mtukufu anatueleza
unyonge na uduni
ambao utawapata watu
hawa katika mtiririko
wa aya hiyo hiyo
(Utawapata wale ambao
wamefanya maovu
uduni kutoka mbele
za Mwenyezi Mungu,
adhabu ngumu kwa
sababu ya yaliyokuwa
wanayatenda [Al-Annam
124].
Na Mwenyezi Mungu
mtukufu anasema:
Mwenyezi Mungu
anawateuwa kutokana
na malaika wajumbe na
kutokana na watu. [AlHajj 75]. Hapana juu yetu,
isipokuwa kumheshimu
na kumtukuza Yule
ambaye ameteuliwa
na Mwenyezi Mungu
mtukufu. Na kama
haikuwa hivyo, kuonesha
kutoridhika kwa namna
yoyote ile dhidi ya yule
ambaye ameteuliwa
na Mwenyezi Mungu,
kuna kiporomosha
cheo cha mtu huyo na
kunamfanya awe duni
mwenye kudhalilishwa
na anakuwa ni mwenye
kunyimwa msaada
na Baraka ambazo
wanafaidika nazo Mitume
na Mawalii na wateule na
wenye kukurubishwa.
Ndiyo mfano wa
mtu huyu vyovyote
kitakavyo kuwa cheo
chake, atafungamanishwa
na unyonge na uduni na
atanyimwa misaada yote
ya Mwenyezi Mungu.
Kisha kwa hakika
utukufu wa Mtume wetu
(s.a.w.) na kufaa kwake
na kukubalika kwake
hayo yanajulikana na
yanakubaliwa katika
zama zote na nyakati
zote na kwa watu wote.
Na umoja na kuwa
vitabu vya mbinguni vya
zamani vimepotoshwa
kwa hakika wanawazuia
watukufu mifano ya
mjuzi sana Rahmatullah
Al-Hindi na mjuzi sana
Al-Jisri wamekuta katika
vitabu hivi bishara mia
moja na kumi na nne
na misemo kuhusu
kuja kwa Mtume huyu
mtukufu. Ndiyo kwa
hakika wamekubaliana
Manabii wote kwa
kuzingatia tokea Dawoud
na Sulayman na Mussa
(a.s.) na kukomelea kwa
Yahya na Zakaria na Issa
(a.s) juu ya bishara ya
kuja kwa mjumbe huyu
mtukufu na waliwaeleza
watu wao kwamba
Mtume huyo atakuwa
ni mwenye kukusanya
ubora wote wa Mitume
(a.s.). Na kwa mazingatio
haya, Mtume (s.a.w.)
ndiyo mwenye daraja kwa
wote. (Itaendelea)
al
211 :30
7 :19
20 :12
8 :9
6:6
20 :7
3 :15
4 :1
MASUALA
1.Enyi watu! Mcheni Mola wenu Mlezi aliye kuumbeni kutokana
na nafsi moja, na akamuumba mkewe kutoka nafsi ile ile. Na akaeneza
kutokana na wawili hao wanaume na wanawake wengi. Na tahadharini
na Mwenyezi Mungu ambaye kwaye mnaombana, na jamaa zenu. Hakika
Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuwaangalieni Suara ipi na aya gani?
Jawabu: 4:1 (An-Nisaa)
2.Kibla cha mwanzo kilikuwa wapi? Jawabu Bayt al Maqdis
3.Kuba lijulikanalo kwa Kiengereza Dome of the rock liliopo Jerusalem
linaitwaje kwa Kiarabu? Jawabu Qubatt as Sakhrah
4.Siku gani inakaririwa sana katika Quran? Jawabu Qiyama
5.Sehemu gani katika Quran imetajwa kuwa maji ndio chimbuko la
maisha? Jawabu 21 :30
6.Mwanamke gani wa pekee jina lake linasomeka kwenye Quran?
Jawabu Maryam
7.Kushuka kwa wahyi wakawanza na wapili kilipita kipindi cha muda
gani? Jawabu Miaka 2 miezi 6
8.Sura ipi inaanza bila Bismillahi? Jawabu Tawba
9.Sura ipi Bismillahi inajitokeza mara mbili? Jawabu Suratul Naml
10.T'alaka ni mara mbili. Kisha ni kukaa kwa wema au kuachana kwa
vizuri. Wala si halali kwenu kuchukua chochote mlicho wapa wake zenu,
ila ikiwa wote wawili wakiogopa ya kwamba hawataweza kushikamana
na mipaka ya Mwenyezi Mungu. Basi mkiogopa kuwa hawataweza
kushikamana na mipaka ya Mwenyezi Mungu hapo itakuwa hapana
lawama ikiwa mwanamke atajikomboa. Hii ndiyo mipaka ya Mwenyezi
Mungu; basi msiikiuke. Na watakao ikiuka mipaka ya Mwenyezi Mungu,
hao ndio madhaalimu. Aya hii ni yangapi katika Sura ipi? Jawabu 2:229
CHEMSHA BONGO: 45
Weka duara kwenye jawabu ilio sawa. Jawabu kamili wiki ijayo.
A
77 :19
KJ
57 :26
14
86
49 :7
ER
28
47 :1
45 :5
MASUALA
1.Sura gani na aya ya ngapi? Na kupishana usiku na mchana, na riziki anayo iteremsha
Mwenyezi Mungu kutoka mbinguni, na kwayo akaifufua ardhi baada ya kufa kwake,
na mabadiliko ya upepo, ni Ishara kwa watu wenye akili.
2.Sura gani na aya ya ngapi? Walio kufuru na wakazuilia njia ya Mwenyezi Mungu,
Yeye atavipotoa vitendo vyao.
3.Sura gani na aya ya ngapi?Na jueni kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu yuko nanyi.
Lau angeli kut'iini katika mambo mengi, bila ya shaka mngeli taabika. Lakini Mwenyezi
Mungu amekupendezeeni Imani, na akaipamba katika nyoyo zenu, na amekufanyeni
muuchukie ukafiri, na upotovu, na uasi. Hao ndio walio ongoka
4.Sura gani na aya ya ngapi? Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
5.Sura gani na aya ya ngapi? Na bila ya shaka tulimtuma Nuhu na Ibrahim, na
tukaweka katika dhuriya zao Unabii na Kitabu. Basi wapo miongoni mwao walio
ongoka, na wengi katika wao ni wapotovu.
6.Kuna aya ngapi za Sajda katika Quran?
7.Jamaa yupi wa Mtume aliotajwa katika Quran?
8.Sura za Makka ni ngapi?
9.Sura za Madina ni ngapi?
10.Siku ya Qiyama hali ya watu itakuwaje?
Jee Unajua?
3/30/2016 1:12:26 PM
3
Na Bakari Mwakangwale
SHEIKH mpya wa BAKWATA
Mkoa wa Morogoro
Abdallah Salim Mkangambe
amesema kazi yake ya
kwanza atakayoanza nayo
ni kuhakikisha vijana wa
Kiislamu wanaosoma katika
shule za sekondari mkoani
humo wanapata elimu ya dini.
Hayo ameyasema mwishoni
mwa juma lililopita mjini
Morogoro muda mfupi mara
baada ya kumalizika kwa
uchaguzi Mkuu uliomweka
madarakani kwa kura 34 dhidi
ya kura mbili za mshindani wake
Sheikh Idd Hussein Nyagongo.
Akifafanua zaidi kuhusu azma
yake hiyo, sheikh Mkangambe
alisema hadhani kama kwa
kushirikiana na Waumini wa
dini ya Kiislamu mkoani humo
watashindwa kusambaza vitabu
vya Elimu ya Dini ya Kiislamu
walau 20 kwa kila shule iliyopo
mkoani humo.
Habari
AN-NUUR
Kielimu.
Uchumi, Ardhi na Elimu
ni vitu muhimu sana kwetu
Waislamu na hasa katika
ulimwengu huu wa Sayansi na
Teknolojia ambao maendeleo
yoyote yanategemea iwapo una
Elimu, Ardhi ama Uchumi kwa
kiasi gani, aliongeza.
Mbali na hayo Sheikh
Mkangambe ameahidi kutatua
changamoto mbalimbali mkoani
humo ikiwemo hitilafu za
makundi ya kidini na kijamii
ili kurejesha heshima na
ustawi mzuri wa maendeleo ya
Waislamu mkoani Morogoro.
ANNUUR NEW.indd 3
asilimia 2 tu.
Hata hivyo, Msikiti mkuu
wa nchi hiyo, maarufu, The
Mosque of Rome (Kitaliano:
3/30/2016 1:12:28 PM
Tahariri/Makala
AN-NUUR
ANNUUR NEW.indd 4
AN-NUUR
WAZANZIBARI
tulichagua maridhiano
na kukataa mfarakano.
Tulichagua umoja na
kukataa mgawanyiko.
Tulichagua upendo
na kukataa chuki.
Tulichagua matumaini
na kukataa khofu.
Tulichagua amani na
kukataa fujo.
Tarehe 5 Novemba
2009 daima itakumbukwa
kuwa ni siku ambayo
nchi yetu iliandika
historia mpya pale
viongozi wawili
wazalendo na mashujaa,
Dk. Amani Abeid
Karume na Maalim
Seif Sharif Hamad,
walipowaongoza
Wazanzibari kufikia
MARIDHIANO.
Haikuwa kazi rahisi
lakini kwa kuongozwa
na hisia za uzalendo na
mapenzi kwa nchi yao
na wananchi wenzao,
Dk. Karume na Maalim
Seif waliamua kujitolea
kuongoza enzi mpya za
siasa. Walijua kwamba
katika vyama vyao viwili,
CUF na CCM, wapo watu
ambao wasingewaunga
mkono na pengine
wangeyatumia
MARIDHIANO yale
kutaka kuwahujumu
kisiasa. Na kweli,
walikuwapo watu wa
aina hiyo na wapo hadi
leo.
Kwa kutambua
kuwa watu waovu
wasiopendelea umoja na
masikilizano miongoni
mwa Wazanzibari
watakuja kusema kuwa
MARIDHIANO hayo
yalikuwa ni maamuzi
ya watu wawili tu, na
hayawakilishi matakwa
ya watu, Dk. Karume
alipendekeza kwa
Maalim Seif kukubali rai
ya kufanya kura ya maoni
ili kupata ridhaa ya
Wazanzibari kuhusiana
na mwelekeo huo mpya
wa siasa na hasa kuhusu
haja ya kuanzisha
muundo wa Serikali ya
Umoja wa Kitaifa.
Tarehe 31 Julai 2010
ikafanyika kura ya maoni
ya kwanza katika historia
ya Zanzibar. Asilimia
66.4 ya Wazanzibari
wakapiga kura ya
NDIYO kuchagua
MARIDHIANO na
muundo wa Serikali
ya Umoja wa Kitaifa.
Baada ya maamuzi hayo
ya Wazanzibari, ndipo
Baraza la Wawakilishi
ambayo tukiyakataa
kupitia kura ya maoni ya
tarehe 31 Julai, 2010.
Nawapa NASAHA
ndugu zangu tukatae
kuingia katika mtego
huo. Tuoneshe kama SISI
NI TOFAUTI NA WAO.
Tusijibu lugha zao za
matusi, chuki na ubaguzi
na sisi tukaandika lugha
za matusi, chuki na
ubaguzi. Haitoonekana
tofauti kati yetu.
Tuithamini na kuilinda
kazi kubwa iliyofanywa
na Dk. Amani Karume
na Maalim Seif Sharif
Hamad.
TUNAYOPITIA
SASA NI MAJARIBU
TU. TUSIKUBALI
KUSHINDWA
TUKARUDISHWA
TULIKOTOKA.
TUWAONESHE
WAOVU KWAMBA
SISI NI WEMA. NA
WEMA SIKU ZOTE
HUUSHINDA UOVU.
3/30/2016 1:12:29 PM
HABARI ZA KIMATAIFA
AN-NUUR
Mashindano
kuhifadhi Quran
kufanyika
Singapore
MASHINDANO ya kitaifa
ya kuhifadhi Quran nchini
Singapore yanatarajiwa
kufanyika wiki ijayo siku ya
Jumamosi na Jumapili Aprili
2-3.
Makundi matatu yanatarajiwa
kushiriki ambayo ni ni ya umri
wa miaka 7 mpaka 12, miaka 13
mpaka 18 na miaka 19 mpaka 25.
Washiriki hao
watashindanishwa
kwa kuzingatia namna
walivyohifadhi (hifz).
Matamshi,(Tajweed) na ufasaha
(fasahah).
Imeelezwa kuwa lengo la
mashindano hayo ni kuibua
vipaji vipya katika uwanja
wa usomaji wa Quran na
kuhamasisha kuhifadhi Quran.
Lengo jingine ni kuifanya
jamii kuwa na utamaduni wa
kuhifadhi Quran na pia kupata
vijana watakaoiwakilisha
Singapore katika mashindano ya
Kimataifa.
Mashindano hayo yatafanyika
katika Msikiti wa Darul Aman
na washindi watapata vyeti na
pesa taslim. Ahbaabur.blogspot.
ANNUUR NEW.indd 5
3/30/2016 1:12:30 PM
AN-NUUR
ANNUUR NEW.indd 6
Mafuta ya mbegu
seli kwenda inavyotakiwa.
Aidha kila seli ndani ni kama
bahari yenye visiwa vingi. Vitu
vinavyoitwa organele, ambavyo
ni maumbile kadhaa wa kadhaa
yenye majukumu tofauti
huelea kama visiwa kwenye
majimaji yaliyomo ndani ya
seli. Majimaji yaliyomo ndani
ya seli yana vitu vingi ndani
yake, ikiwa ni pamoja na viini
lishe vilivyoingizwa humo
kwa minajili ya kuchakatwa
ili kuzalisha nishati, kufanya
ukarabati, kuzimua mazao hatari
ya pembeni ya mchakato wa
kuzalisha nishati; na kuunda
maumbo mengine ambayo ni
muhimu kwa utendaji sawa
wa mwili. Majimaji haya pia
hupokea kwa ajili ya kutoa nje
ya seli, na hatimaye nje ya mwili,
uchafu au taka zinazozalishwa
na organele katika michakato
mbalimbali.
Katika ngozi ya kila seli
(cell membrane) kuna vipokezi
(receptors) ambavyo hufanya
kazi ya kuingiza ndani ya seli
vile vilivyomo kwenye majimaji
ya nje ya seli vinavyotakiwa
kungia ndani, na kutoa nje ya
seli vile vilivyomo kwenye
majimaji ya ndani ya seli
vinavyotakiwa kutolewa nje.
Mwili unapokumbwa na mfuro
utendaji kazi wa hivi vipokezi
kwenye ngozi ya seli huathirika.
Hii ina maana kuwa kazi ya
kuingiza na kutoa nje ya seli
vitu mbalimbali haifanyiki kwa
wepesi na ufanisi unaotakiwa,
jambo ambalo huvuruga uwiano
wa vitu hivyo.
Hali ikiwa hivyo ni rahisi
3/30/2016 1:12:30 PM
Makala
AN-NUUR
WIKI iliyomalizia 20
Machi 2016 Ulimwengu
umeshuhudia chaguzi siku
hiyo katika bara la Afrika.
Macho na masikio ya
ulimwengu yaliangaza zaidi
Zanzibar si kwa uangalizi
bali kuhabarisha kile
kitakacho tokea.
Kwa nini Zanzibar?
Uchaguzi wa marejeo
umevuta hisia na mvuto wa
waandishi na wachambuzi
mbalimbali kwa vile
kususiwa na waangalizi wote
wa ndani na nje, uliosusiwa
na vyama takriban 10 kati ya
14,umegubikwa na mzozo
wa kisheria juu ya ufutwaji
na ufanyikaji wa Uchaguzi
mpya ni miongoni mwa
maswali mengi na ambayo
huwa kama kitendawili
kisicho na mteguzi.
Mazingira na mtiririko wa
matukio tokea Oktoba 28
ulipofutwa uchaguzi wa
Oktoba 25 uliupa uchaguzi
wa Machi 20 picha ya aina
yake kutizamwa kiuandishi
(Reporter) zaidi kuliko
kiuangalizi (Observer).
Kuelekea siku ya Uchaguzi
Wiki moja kuelekea Machi
20 tulishuhudia matukio
kadhaa ya Miripuko katika
maskani ya CCM Kisonge
na nyumba ya Kamishna
wa Polisi, Uchomwaji moto
wa Nyumba za wananchi,
Uchomwaji moto wa Maskani
za CUF, pia tumeshuhudia
ukamatwaji wa wafuasi
na viongozi wa CUF
kuhusishwa kwao na matukio
kadhaa yaliyotokea. Kubwa
zaidi lililoibua mjadala
mkubwa ni kutekwa kwa
Mwandishi mahiri wa Radio
DW na Mwananchi Bi. Salma
Said. Mtiririko wa hayo yote
pamoja na Uimarishwaji
mkubwa wa Ulinzi kwenye
viunga vya Zanzibar kulizidi
kuleta taswira ya kipekee
kwa Uchaguzi wa Machi 20.
Siku ya Uchaguzi
Machi 20 iliwadia
siku ya upigaji kura kwa
Uchaguzi ambao uliokuwa
hauna Kampeni na ambao
ulifuatiwa na mtiririko
kadhaa wa kadhaa. Vyombo
takriban vingi vilijikita
kuhabarisha hasa upande
wa Pemba kutokana na
kuwa na wafuasi wengi wa
CUF. Taarifa za awali kabisa
zilianza kutoka kujulisha
ANNUUR NEW.indd 7
kuhitimishwa kutangazwa.
Mara hii iliichukua Tume
masaa 16 tu kuja na matokeo
ya mwisho na kumtangaza
Dkt Ali Mohammed Shein
ndie mshindi wa kiti cha
Rais wa Zanzibar kwa miaka
mitano mpaka Machi 2021.
Hapana shaka palitarajiwa
nderemo na vifiji kuanzia
Bwawani na kwenye
viunga vyake tokea hapo
alipotangazwa majira ya saa
4 asubuhi kuwa mshindi.
Ila hali ilikuwa tofauti mji
uliendelea kuwa kimya
kizito na kuanzia jioni jioni
ndipo palipoanza kuonekana
makundi machache ya
wafuasi wa CCM wakielekea
Kachorora na Kisonge na
ambao wengi wao ni vijana
na kutumbuizwa na muziki
uliokuwepo hapo. Hali katika
mitaa mingi ilibaki kimya na
yenye simanzi kubwa. Hii
ilizidi kuleta taswira ya safari
refu sana ya miaka mitano
ya Dkt Shein kuongoza
Zanzibar. Naam wingu la
kwanza zito limetanduka
lakini, Je safari ya miaka
mitano na muonekano wa
wananchi wengi kutokupiga
3/30/2016 1:12:31 PM
Makala
AN-NUUR
ANNUUR NEW.indd 8
Mwananyamala B. Sheikh
Haydar umri wake wote
amefanyakazi Kabidhi Wasii
hadi alipostaafu kazi miaka
michache iliyopita.
Msaada wake katika
ofisi hii ndiyo Waislamu
watamkumbuka daima. Kusajili
taasisi yoyote ya Kiislamu
nchini petu, ni kitu kigumu
sana kuanzia mwaka wa 1968
pale BAKWATA ilipoundwa na
kufanywa ndiyo kila kitu kwa
Waislamu. Sheikh Twahir juu
ya matatizo yote yaliyokuwapo,
alijitahidi sana kuwaelekeza
Waislamu nini wafanye ili
waweze kusajili taasisi zao. Hii
haikuwa kazi nyepesi kwake
kwani juu yake walikuwapo
wakubwa zake kimadaraka
ambao walifanya kila juhudi
kuhakikisha kuwa taasisi za
Kiislamu hazipati tasjila.
Mfano wa karibu sana ni
pale mwaka wa 1992 Waislamu
walipotaka kusajili Baraza Kuu.
Ala kuli hali wakati wa Rais Ali
Hassan Mwinyi angalau mambo
yalikuwa mepesi kidogo na
kipindi hiki Waislamu wengi
watamkumbuka Sheikh Twahir
alivyowasaidia kusajili taasisi
zao.
Nilipofanya mazungumzo
naye mwezi Septemba 2012 kwa
ajili ya kipindi cha televisheni
nilimuomba tutoke katika
kazi yake anieleze historia ya
East African Muslim Welfare
Society (EAMWS) baada ya
kupigwa marufuku na serikali
ya Nyerere mwaka wa 1968
na Sheikh Hassan bin Amir
aliyekuwa Mufti wa Tanganyika
kufukuzwa nchini.
Sheikh Twahir alinieleza
mengi kuanzia maisha yao
Kisutu Dar es Salaam yeye
akiwa kijana mdogo akisoma
Al Jamiatul Islamiyya Muslim
School katika miaka ya 1950
na baba yake akiwa mmoja wa
wanachama shupavu wa TANU.
Alinieleza usuhuba mkubwa
uliokuwapo baina ya baba yake
Sheikh Haydar Mwinyimvua,
Sheikh Suleiman Takadir na
Mwalimu Nyerere. Alinieleza
kazi na mafanikio yaliyofikiwa
na EAMWS na pigo Uislamu
uliopata baada ya kupigwa
marufuku.
Picha alonipa Sheikh Twahir
3/30/2016 1:12:31 PM
Tangazo
AN-NUUR
Waislamu kote nchini mnatangaziwa nafasi za Kidato cha Tano kwa shule zifuatazo:
Shule hizi ni za Kiislamu zenye lengo la kuwapa wanafunzi taaluma ya hali ya juu na malezi
bora ya Kiislamu. Shule hizi ni za BWENI za mchanganyiko wa wavulana na wasichana.
Zipo Combinations zote za SAYANSI, ARTS na BIASHARA.
Muombaji awe na ufaulu wa masomo matatu (3) kwa kiwango cha Credit (yaani A, B na C)
Daraja la III (Division three) au zaidi na Grade D kwenye masomo ya Combination.
Mwisho wa kurudisha fomu ni tarehe 02/05/2016.
Fomu za maombi zinapatikana kwa gharama ya Shilingi 10,000= katika Tovuti:www.ipcorg.tz na katika vituo vifuatavyo:
ARUSHA: Ofisi ya Islamic Education Panel, Jambo
Plastic, Ghorofa ya 2 mkabala na Msikiti Mkuu
Bondeni : 0783 438676/0715 438676.
KILIMANJARO: Moshi: Msikiti wa Riadha:07673453
: 0716
544757/0718661992
SINGIDA: Ofisi ya Islamic Education. Panel
karibu na Nuru snack Hotel : 0786
425838/0784 928039.
MANYARA: Ofisi ya Islamic Ed. Panel Masjid
Rahma: 0784491196
KIGOMA: Msikiti wa Mwandiga: 0714717727.
Kibondo Islamic Nursery School:
0766406669. Kasulu: Murubona Isl.SS:
0714710802/0763 298440
LINDI: Wapemba Store: 0784 974041/0783
488444/0653 705627.
MTWARA: Amana Islamic S.S: 0715
465158/0787 231007.
SONGEA: Kwa Kawanga Karibu na Msikiti
wa NURU : 0713249264. Mkuzo Islamic
High School :0654 876317
MBEYA: Ofisi za Islamic Education Panel
Uhindini 0785425319. Rexona Video
mkabala na Mbeya RETICO: 0713
200209/0785425319.
Rukwa: Sumbawanga:Jengo la Haji
Said Shule ya Msingi
Kizwike:
0757090228/0786 313830
TABORA: Kituo cha Kiislamu Isevya: 0784
944566/0718 556355. Nzega - Dk. Mbaga0754 576922/0784576922.
IRINGA: Madrastun Najah: 0714 522 122.
PEMBA: Wete: Wete Islamic School : 0777
432331/0712772326.
UNGUJA: Madrasatul Fallah: 0777125074.
PANDU BOOKSHOP 0777462056 karibu
na uwanja wa Lumumba
MAFIA: Ofisi ya Ust. Yusufu Ally jirani na
msikiti mkuu : 0773580703.
ANNUUR NEW.indd 9
3/21/2016 3:58:37 AM
3/30/2016 1:12:32 PM
10
Makala
Na Nizar Visram
KWA muda wa miezi kadha
sasa habari kutoka Marekani
zimekuwa zikitawaliwa na
kinyanganyiro cha urais.
Wagombea wanaowania
tiketi za chama wamekuwa
wakipambana na kulumbana
huku washabiki wao wakitiana
ngumi na kushikana mashati.
Mgombea mmoja anasema
ukinichafulia mkutano wangu
nami ntamwaga mboga katika
mkutano wako. Alimradi
watazamaji wengi wamekuwa
wakichukulia mchakato mzima
kama burudani ya aina yake.
Kinachofanyika kwa sasa ni
uchaguzi wa awali (primaries)
utakaopelekea kufanyika
kwa uchaguzi wa urais nchini
Marekani tarehe 8 Novemba
2016. Wao hufanya uchaguzi
wa rais kila baada ya miaka
minne. Katiba yao imeweka
kikomo cha mihula miwili,
hivyo Rais Obama analazimika
kungatuka na kumpisha
mwengine atakayechaguliwa
Hivyo, huu uchaguzi wa awali ni
mchakato wa kumteua mgombea
wa urais kutoka kila chama.
Vyama vikuu vinavyojulikana
zaidi ni Democratic na
Republican. Utaratibu wao wa
kuteua wagombea na hata wa
kumchagua rais ni tofauti na
wa hapa Tanzania. Kwa kweli si
wote wanaoelewa utaratibu huu.
Sitashangaa hata Wamarekani
wenyewe wasipoelewa. Wao
wanadai kuwa wanaongoza
dunia katika demokrasi. Lakini
cha ajabu ni kuwa mgombea wa
chama hateuliwi na wanachama,
na rais hachaguliwi na wananchi
moja kwa moja kama tufanyavyo
sisi hapa kwetu. Ndio maana
wanapofanya uchaguzi basi
ubalozi wao hapa jijini huwaita
waandishi ili kuwaelimisha na
wengine hata hupewa fursa ya
kwenda Marekani ili waandike
makala za kuusifu mfumo wao.
Huko Marekani wananchi
watawachagua watu
watakaomchagua rais kwa niaba
yao. Watachagua kikundi cha
wapiga kura (electoral college)
ambao ndio watakaopiga kura
ya kumchagua rais. Hivi sasa
kinachofanyika ni mchakato
wa kuwateua wagombea urais
ulioanza tarehe 1 Februari
ANNUUR NEW.indd 10
na utakaomalizikia tarehe
14 Juni mwaka huu. Uteuzi
huu unahusu majimbo 50
nchini kote. Watu watapiga
kura kuwachagua wajumbe
watakaohudhuria mkutano
mkuu wa chama (nominating
convention) ambao ndio
utamchagua mgombea wa urais
atakayepeperusha bendera
ya chama. Katika hatua hii ya
kichama hata Wamarekani walio
ughaibuni nao wanashirikishwa.
Kwa mfano, chama cha
Republican kitawachagua
wajumbe 2,472 watakaohudhuria
mkutano mkuu (convention)
ambako mgombea urais wa
chama atateuliwa. Chama hiki
kilianza na wanachama 17
waliotangaza nia ya kugombea
tangu Machi mwaka jana. Hii ni
idadi kubwa ya watia nia ambao
haijapata kutokea huko. Wengi
wao ni watu wenye nyadhifa
wakiwa magavana wa mikoa au
maseneta (wabunge). Ila mmoja
ni tofauti. Huyu ni Donald
Trump ambaye si gavana wala
seneta bali ni bilionea kutoka
New York ambaye amewekeza
hata katika Mashariki ya Kati.
Hiyo ndio sifa yake ambayo
imewavutia Wamarekani wengi.
Trump si mwanasiasa
kama wagombea wengine.
Yeye ni bilionea anayefanya
biashara ya kujenga na kuuza
majengo, pamoja na kuendesha
mahoteli na vituo vya kamari
(casino). Anadai kuwa kwa
vile amefanikiwa kutajirika,
basi akiwa rais atahakikisha
wananchi nao wanatajirika.
Lakini kisichosemwa ni kuwa
kampuni zake zimewahi
kufilisika mara nne. Huo si
mfano mzuri wa kuigwa. Wengi
wanamuona kama ndumila
kuwili, kwa vile aliwahi
kujiunga na Democrat. Aliwahi
hata kumuwezesha kifedha Bi
Hillary Clinton katika kampeni
zake mnamo 2008. Trump pia
amewahi kuwaunga mkono
wanawake waliokuwa wakidai
haki ya kutoa mimba. Sasa
anapinga jambo hilo na hata
kuishambulia serikali kwa
kuziwezesha asasi za uzazi wa
mpango (family planning).
Mwaka 2000 alikuwa akiunga
mkono mfumo wa bima ya
matibabu kwa wananchi wote
ukisimamiwa na serikali. Leo
anadai eti huko ni kuingilia
uhuru wa raia kujichagulia
bima. Yaani anataka makampuni
ya bima yaruhusiwe kushindana
katika soko huria na kila
mmoja ajiamulie kujiunga au
kutojiunga bila ya kuingiliwa
na serikali. Aidha, Trump
amekuwa akichochea chuki
na ubaguzi wa kidini dhidi ya
Waislamu wanaoishi Marekani
kwa kuwaita wakuja wasio
na haki ya kuishi nchini.
Anasahau kuwa Waislamu
walianza kuingia Marekani
kabla ya babu yake kuhamia
huko kutoka Ujerumani. Halafu
anasema akiwa rais, Waislamu
AN-NUUR
hawataruhusiwa kuingia
Marekani.
Anazishambulia pia
China, Mexico na Japan kwa
kuyalaumu makampuni
yanayowekeza huko badala ya
kuwekeza nyumbani. Hawa
anawaita wasaliti waliokosa
uzalendo. Anasahau kuwa
kufanya biashara na nchi hizo na
kuwekeza huko ni muendelezo
wa sera ya utandawazi, sera ya
kibeberu ambayo ina manufaa
kwa mabepari wa kimataifa.
Trump anasema akiwa rais
atawaua watuhumiwa wa
ugaidi bila ya kuwafikisha
mahakamani. Anasema ataua
hata familia zao. Huyu ndie rais
mtarajiwa wa Marekani na sera
zake za kifashisti.
Mpinzani mkuu wa Trump
katika chama cha Republican
ni seneta Ted Cruz. Huyu
huwa anaelezwa kuwa ni
mwenye siasa za wastani.
Kinachosahauliwa ni kuwa
Cruz naye anaunga mkono
mashambulizi zaidi katika
Mashariki ya Kati, pamoja
na upunguzaji wa kodi kwa
matajiri.
Kwa upande wa Democrat
mgombea seneta Bernie Sanders
amewavutia watu wengi,
hasa vijana, kutokana na sera
yake anayoiita usoshalisti
wa kidemocrasia. Yeye
anazungumzia mapinduzi
ya kisiasa lakini tukiangalia
zaidi tunaona kuwa msimamo
kama huo hauwezi kukubaliwa
asilani na chama cha Democratic
ambacho siku zote kimekuwa
kikitumikia maslahi ya
kibepari kikishrikiana na
Republican, kwa muda wa
miaka 150. Ni kweli vyama
hivyo vinatofautiana, lakini si
kimsingi. Democratic ni cha
mrengo wa kulia na Republican
ni cha mrengo wa kulia zaidi.
Ndio maana hata Sanders
akishinda urais itamuwia
vigumu kutekeleza ahadi zake.
Ni sawa na rais Obama ambaye
kabla ya kuchaguliwa aliahidi
kufunga gereza la Guantanamo,
lakini jitihada zake zimegonga
ukuta. Hivi sasa tunaambiwa
Obama anashindwa kutekeleza
ahadi zake kwa sababu bunge
(Congress) linatawaliwa na
chama cha Republican. Lakini
ukweli ni kuwa mwaka 2009 na
2010 bunge lilikuwa na wingi
wa Democratic, kina Sanders
na wenzake pamoja na rais
wao katika ikulu ya White
House. Hata hivyo hakuna
hatua walizochukua tofauti na
Republican. Wakati huo uvamizi
wa kijeshi katika Mashariki ya
Kati uliongezeka.
Kuhusu gharama za kampeni,
michango mingi ya Hillary ni
kutoka makampuni makubwa
wakati Sanders anategemea
wachangiaji wadogo. Wakati
mmoja Hillary alikuwa
amekusanya dola milioni 29.4
na Sandera dola milioni 26.2.
Fedha za Hillary zilitoka kwa
3/30/2016 1:12:33 PM
11
Makala
AN-NUUR
Na Bakari Mwakangwale
ANNUUR NEW.indd 11
3/30/2016 1:12:34 PM
12
Tangazo
AN-NUUR
298440
LINDI: Wapemba Store: 0784 974041/0783
488444/0653 705627.
MTWARA: Amana Islamic S.S: 0715 465158/0787
231007.
SONGEA: Kwa Kawanga Karibu na Msikiti wa NURU
: 0713249264. Mkuzo Islamic High School :0654
876317
MBEYA: Ofisi za Islamic Education Panel Uhindini
0785425319. Rexona Video mkabala na Mbeya
RETICO: 0713 200209/0785425319.
Rukwa: Sumbawanga:Jengo la Haji Said
Shule ya Msingi Kizwike: 0757090228/0786
313830
TABORA: Kituo cha Kiislamu Isevya:
0784
944566/0718 556355. Nzega - Dk. Mbaga-0754
576922/0784576922.
IRINGA: Madrastun Najah: 0714 522 122.
PEMBA: Wete: Wete Islamic School : 0777
432331/0712772326.
UNGUJA: Madrasatul Fallah: 0777125074.
PANDU BOOKSHOP 0777462056 karibu na
uwanja wa Lumumba
MAFIA: Ofisi ya Ust. Yusufu Ally jirani na msikiti
mkuu : 0773580703.
Kwa maelezo zaidi piga simu: 0787 188964, 0784 267762 na 0654 613080
ARABIC CHETI.indd 1
ANNUUR NEW.indd 12
3/21/2016 3:59:12 AM
3/30/2016 1:12:35 PM
13
AN-NUUR
ANNUUR NEW.indd 13
ya wapiganaji ya kutaka
ulinzi kutoka kwa miungu.
Kitambaa kilichotengenezwa
kwa sufi kilichotoka Ulaya,
kilitiwa rangi ambayo ilikuwa
ghali na huenda kiliwasili
nchini Japani kupitia ufanyaji
biashara na Wareno. Utumiaji
wa vitambaa vyenye thamani
kama hivyo pia ulikuwa
ishara ya kuonyesha nguvu.
Pia utagundua hisia ya kutaka
kutambulika ya wapiganaji
wanapokuwa vitani katika
enzi za vita vikali. Hakika
nguo za sufi ndio nguo
ambazo zimetawala duniani
na wazalishaji wa sufi wengi
wao hawafaidi mapato
yatokanayo na sufi.
Msufi hutoa pamba na ni
mmoja kati ya mti maarufu
duniani katika mti ambao sio
wa chakula. Msufi ni maarufu
tunaweza kusema kuliko
ya aina yoyote ile ya miti
mengineo. Nusu ya viwanda
vilivyo vya kutengenezea
nguo duniani hutumia
pamba katika matengenezaji
wa nguo. Aidha pamba
hutumiwa katika utengenezaji
wa miripuko, mafuta, chakula
kwa ngombe na dawa za
kupigia meno.
Misufi ya kutengenezwa
viwandani imeanzishwa
duniani lakini juu ya hayo
bado sufi itokanayo katika
miti ya asili huwa na thamni
kubwa inagwa mara nyingi
huhujumiwa na wadudu
na kutumiwa kwa dawa
za kupambana na hao
wadudu. Pamba ina pambana
kujiweka katika soko na
matumizi ya nailoni, na aina
nyenginezo. Biashara ya
Pamba imekuwa ni moja ya
kutumiwa Watumwa katika
kazi ya kuuhisha Misufi,
katika nchi ya Marekani
Watumwa waliotokea Afrika
walikuwa kwenye mashamba
ya miti iliopandwa Misufi
wakiimarisha na Mapinduzi
ya viwanda yalitokana na
kushamiri kutokana na
kukuwepo kwa Pamba.
Katika karne ya 18 na 19
Waengereza walikuwa ndio
wenye viwanda vingi vya
kutengeneza nguo zitokanazo
na Pamba. Mwana taaluma
wa Kimerekani Ely Whitney
katika mwaka wa 1793 ndio
alioasisi mashine ya kwanza
ya kukamulia mbegu za
Pamba na kupunguza kazi ya
mwanadamu kufanya hayo
3/30/2016 1:12:35 PM
14
MAKALA/MASHAIRI
ANNUUR NEW.indd 14
AN-NUUR
Na Sheikh Kamal
Ahmed Hassan
AMESEMA Mwenyezi
Mungu mtukufu Ita
watu katika dini ya
Mola wako mlezi kwa
hekima na mawaidha
mazuri na jadiliana
nao kwa yale yaliyo
mema Zaidi.
Amesema Imamu
Kurtubi katika
tafsiri Mawaidha
na maneno mazuri
ambayo ameyaweka
Mwenyezi Mungu
kuwa ni hoja kwao
katika kitabu chake.
Na amesema Ibnu
Kayim /mawaidha
mazuri ni kuamrisha
mema na kukataza
mabaya kwa matumaini
na kwa utisho na
kwa umuhimu wa
mawaidha mazuri .
Ameweka mlango
mzima Imamu Bukhari
katika sahihi yake
akasema, hakua Mtume
(s.a.w) akiwavamia
watu au kuwarefushia
mawaidha ili
wasikimbie na
kuondoka.
Juu ya mawaidha
ya Mtume (s.a.w)
kwa masahaba ili
kubadilisha mwenendo,
imeelezwa kutoka kwa
Abdilahi Bin Masud
amesema, amesema
mtu mmoja ewe
Mtume wa Mwenyezi
Mungu mimi siachi,
kuwa ninaiwahi
swala kwa namna
anavyorefusha fulani
sijapatapo kumuona
Mtume (s.a.w) akitoa
mawaidha makali kwa
hasira kuliko siku hiyo,
na akasema enyi Watu
hakika mnakimbiza
watu misikitini, basi
anayeswalisha watu,
basi na afifishe kwani
wapo miongoni mwao
wagonjwa na madhaifu
na wenye haja.
Hekima, mjadala
kwa njia nzuri ni
miongoni mwa
vitu vya lazima. Ni
lazima pia kuwa
mpole, kutumia kauli
laini na kuwapenda
watu. Hebu tazama
mfano huu ulio hai
katika kubadilishwa
mwenendo. Kuna
kijana mmoja alikuja
kwa Mtume (s.a.w)
akasema ewe Mtume
wa Mwenyezi Mungu
niruhusu mimi
kuzini, watu wakapiga
mayoe.
Mtume (s.a.w)
akasema nisogezeeni
kwangu, wakamsogeza
3/30/2016 1:12:37 PM
15
SHUKRANI zote zinamstahikia
Allah (sw). Sala na salamu
zimfikie mtukufu wa daraja,
Masahaba wake na wote
wanaofuata mwenendo wake
mpaka siku ya malipo.
Somo la nne katika mfululizo
wa masomo haya ya Tawhiid,
ni taratibu za kukufurishana,
yaani ni wakati gani Muislamu
ataitikadiwa kuwa ni kafiri.
Somo hili ni muhimu sana kwani
makundi yote yaliyochupa
mipaka na kuanza kugeuka
kuwa ni makundi ya kihalifu
kupitia jina la Kiislamu, yalianza
kupotea katika suala la kumjua
ni nani kafiri na inakuwaje
mpaka unamuitakidi mtu kuwa
ni kafiri.
Kipengele nambari sitini
na saba katika kitabu cha
Imam Tahawy kinasema
hatumuitakidi yeyote katika
watu wa kibla,(yaani wafuasi
wa Muhammad (saw)) kuwa ni
kafiri kwa kufanya madhambi
makubwa, mpaka aitakidi kuwa
hiyo dhambi kubwa ni halali,
pia hatusemi kuwa dhambi
haimdhuru mtu madhali
ameamini.
Huu ndio mtizamo sahihi
wa Kiislamu tofauti na ile ya
makundi mawili, moja likiitwa
Khawarij ambalo lilikuwa na
itikadi kuwa kila Muislamu
anayefanya dhambi kubwa ni
kafiri. Ametoka kabisa katika
Uislamu, na akhera atakaa
milele motoni . Hilo ni Kundi
lililochupa mipaka katika
suala la kukufurishana, wao
waliitakidi kuwa Ali (ra) na
Muawiyya(ra ) na wafuasi wao
wote ni makafiri na waliamini
kila mtu ambaye si Khawarij ni
kafiri. Waliwakataza wafuasi
wao kusema na watu ambao
si Khawarij, kutowaozesha na
kutoolewa na wasio Khawarij.
Baya Zaidi, walihalalisha
kumwaga damu ya kila
asiyekuwa Khawarij kwa vile
waliwaona ni makafiri (lakini
tambua pia kuwa katika
Uislamu hakuna amri wala
hukumu ya kuua makafiri. Mtu
atauliwa kutokana na hukumu
ya kimahakama kutokana na
kosa kulingana na shera ya
Kiislamu.).
Kundi la Muutazila wao
waliamini kuwa dhambi
kubwa inamuweka mfanyaji
baina ya Uislamu na Ukafiri,
haimfanyi awe kafiri kikamilifu
lakini akhera atadumu motoni
milele. Muutazila na Khawarij
walihitilafiana kuhusu mwenye
kufanya dhambi kubwa, duniani
namna yake iko vipi, lakini
walikubaliana kuwa akhera
watadumu milele motoni.
Kundi la Murjia liliamini
kuwa Muislamu hata afanye
dhambi kubwa kiasi gani,
haitomdhuru madhali
ameamini yaani kule kuamini
tu kunamtosha, na imani
haidhuriwi na madhambi hata
ANNUUR NEW.indd 15
Makala
Tawhiid -4
AN-NUUR
3/30/2016 1:12:37 PM
16
Makala
AN-NUUR
ANNUUR NEW.indd 16
3/30/2016 1:12:38 PM
17
Na Abuu Nyamkomogi
HAWAKUNIPIGA kisu wala
fimbo. Walinipiga kwa mabuti,
mateke. Wakanipiga sana
vibao (makofi), kwa hiyo uso
wangu ulikuwa umevimba.
Walinipiga ngumi, mateke,
popote pale wananipiga. Tarehe
18 Machi, Ijumaa mwaka 2016,
ni miongoni mwa siku ambazo
sitazisahau za mateso kutokana
na uandishi wa habari na
utetezi wa haki za binadamu.
Maneno hayo, yaliyotamkwa
na mwandishi wa habari na
ripota jasiri na mahiri Bi.
Salma Said wakati akihojiwa
na Idhaa ya Kiswahili ya
Sauti ya Ujerumani-DW kama
yalivyonukuliwa katika toleo
la gazeti hili la juma lililopita
chini ya habari kuu iliyobeba
anwani 'Sitaisahau tarehe
18-Salma', ndio yaliyonisukuma
kuteua anuwani ya makala
haya kama isomekavyo hapo
juu. Nitafafanua sababu ya
msukumo wa uteuzi huo kadri
tunavyoendelea na upembuzi
wetu katika makala haya huko
mbele inshaallah.
Nimetumia ibara ya 'Pole
na Hongera' katika anuwani
ya makala yangu haya kwa
wakati mmoja, si kwa bahati
mbaya bali kwa makusudi, kwa
malengo makuu mawili. Mosi,
nimetumia neno 'Pole' kwa
lengo la kumfariji mwandishi
husika kutokana na mazonge
au masaibu yaliyomsibu baada
ya kutekwa nyara kwa siku
mbili mtawalia, kadhia ambayo
ilijiri katika majuma mawili
yaliyopita. Pili, nimetumia neno
'Hongera' kwa madhumuni ya
kumshajiisha au kumtia moyo
mwandishi asikate tamaa na
badala yake aendelee na harakati
zake za mapambano ya kutetea
haki na uadilifu pamoja na
kupinga dhulma na uonevu,
vinavyoonekana kukithiri na
kuzidi kukita mizizi katika jamii,
kwa kutumia kalamu yake isiyo
na woga wala hofu dhidi ya
madhalimu wasiopenda kuona
haki na uadilifu vikitamalaki
katika jamii.
Aidha, sababu zilizonisukuma
kuteua anwani ya makala
haya ni mbili. Mosi, ni kipigo
kikali, alichokumbana nacho
mwandishi husika kipindi
alipokuwa ametekwa nyara
kama alivyosimulia katika
mahojiano yake na Idhaa ya
Kiswahili ya Sauti ya Ujerumani;
kipigo ambacho kiliziathiri
baadhi ya sehemu za viungo
vyake vya mwili ikiwemo uso
ambao ulivimba kutokana na
kipigo hicho, na hapa ndipo
nalazimika kusema ''Pole dada
Salma''.
Pili, ni utambuzi wa
mwandishi husika juu sababu
inayoonekana kupelekea hali
hiyo ambayo, si nyingine
isipokuwa, ni uandishi wake wa
ANNUUR NEW.indd 17
MAKALA
AN-NUUR
3/30/2016 1:12:40 PM
18
Makala
AN-NUUR
NAAAM Uchaguzi wa
marejeo wa Zanzibar Machi
20 umemaliza kwa amani
na woga. Mungu ni mwema
sana kwa kuwapa watu wake
Wazanzibari moyo wa subra
wa kuelewa kuwa Zanzibar
na amani yao ni jambo la
kwanza kuliko chochote.
Wazanzibari walioshiriki
Uchaguzi wametimiza haki
yao ya Kidemokrasia na wale
waliokuwa hawakushiriki,
pia wametimiza haki yao ya
Kidemokrasia pia.
Kwa mujibu wa sheria ya
sasa ya Zanzibar, masuala
ya kupiga au kutopiga kura
yanabaki ni hiari na maamuzi
ya mtu binafsi. Nawapongeza
wote wale ambao walibaki
majumbani kwao kwa Amani
na Utulivu mkubwa na wale
waliokwenda kupiga kura
kwa Amani na Woga mkubwa.
Nasema woga kwa mazingira
yaliyotokea kuelekea uchaguzi
wenyewe wa visa kadhaa
vyenye sura ya uvunjifu wa
amani yetu adhimu. Waliotoka
kupiga kura wamechukua
ujasiri mkubwa zaidi kuliko
wale ambao hawakwenda na
wale ambao hawakwenda
wamechukua busara kubwa
kubaki majumbani kwa usalama
na hivyo kupelekea kutokuwa
na tukio lolote la uvunjifu wa
amani siku ya Uchaguzi Machi
20.
Makundi haya yote imani na
matarajio yao kubwa ni kutimia
matakwa yao na kuondokana
na hali duni ya maisha katika
Nyanja zote Elimu, Afya,
Uchumi, na Michezo. Dkt
Shein ametangazwa mshindi
na kuapishwa Machi 24 kuwa
Rasi wa Zanzibar kwa miaka
mitano ijayo. Ingawa Uchaguzi
haukuwa na Kampeni lakini
kwa vile ni merejeo, basi
wananchi waliopiga kura
na kumchagua Dkt Shein
walikuwa wanaingia vituo
vya kupigia kura na mwangwi
wa sauti ya ahadi zake za
kuboresha maisha na kubwa
haswa kugeuza Zanzibar
kuwa Dubai ya Afrika na
wale waliobaki majumbani
waliitamani Zanzibar kuwa
Singapore.
Yupo alieshinda na kubeba
dhamana ya kuongoza nchi
nae si mwengine ni Dkt Shein.
Mantiki ya kuwa Zanzibar
kuwa Dubai ya Afrika
wananchi wanaikimbuka na
wanahitaji iwekwe kwenye
vitendo na ionekane.
Baada ya kutangazwa kwa
matokeo na kumpa Dkt Shein
dhamana ya uongozi kwa mara
ANNUUR NEW.indd 18
MJI wa Dubai
ya pili tumeshuhudia na kusikia
Marekani na washirika wote wa
Jumuiya ya Ulaya wakitoa tamko
ambalo linaashiria kutokuwa
tayari kutoa ushirikiano na
Serikali mpya ya awamu ya
pili ya Dkt Shein. Na wao
kuhimiza tena majadiliano baina
ya pande zote katika kuleta
demokrasia inayoshirikisha
pande zote. Kilichonishtusha
ni kusikia kauli mbili kutoka
kwa mawaziri waandamizi wa
serikali na ambao kwa kiasi
kikubwa wanatarajiwa kurudi
tena kwenye uongozi. Mh
Mohammed Aboud Zanzibar
ni nchi huru na itaendelea kuwa
huru. Tuko tayari kupokea
misaada inayozingatia utu
na heshima kwa Zanzibar na
wananchi wake kinyume cha
hivyo tuko tayari kufa njaa .
Na Mh Omar Yussuf kwa
upande wake amesema Zanzibar
inategemea 20% mpaka 28%
kama msaada wa kibajeti na pia
mikopo kutoka Mabenki ya Nje
na ya kimataifa ili kuikamilisha
kila mwaka katika utekelezaji
wa miradi mbalimbali ya
maendeleo. Mh Omar Yusuf
ambae aliwahi kuwa Naibu
Waziri wa Fedha amesema
wanategemea kuongezeka
watalii kwa mwaka unaofuata
na pia kuweza kupunguza safari
za nje kama afanyavyo Rais
Magufuli na pia wagonjwa wote
kutibiwa hapa kwa kuweka
program maalum ya kuleta
madaktari.
Kwa kauli hizi za kuwa tuko
tayari kufa njaa nimeshtushwa
sana na kuanza kuhisi
Serikali hii mpya ya Dkt Shein
imeanza kuwasaliti wananchi
wake na hususan wafuasi
wake waliotegemea Dubai
ya Afrika. Matumaini yao
yameanza kwenda harijojo.
Kwani mipango ya kutengeneza
Zanzibar kuwa Dubai ya
Afrika ilitegemea mfadhili
gani?. Kwa kiwango gani na Je
Dubai yetu tulotaka kuijenga
3/30/2016 1:12:41 PM
19
Ukurasa wa Watoto
AN-NUUR
Kuku
WIKI iliyopita
tulimalizia darasa
letu kwa kusema
kuwa:
1. Aliyeumba ardhi
na kuitandaza ni Allah
(SW)
2. Aliyeumba
milima na kuikalisha
juu ya ardhi ni Allah
(SW)
3. Anayeshusha
mvua kutoka
mawinguni ni Allah
(SW).
4. Aliyeotesha
mimea ya aina
mbalimbali katika
ardhi ni Allah (SW).
5. Allah (SW)
ametukuka kweli
kweli.
6. Allah (SW)
ni fundi, muweza
mwenye ujuzi kuliko
wajuzi wote.
Katika darsa la leo,
tutaangalia, ni nani
fundi wa watu na
wanyama.
Hebu tujaribu kujibu
maswali yafuatayo:
Kuku ametoka wapi?
Kuku ametokana na
yai.
ANNUUR NEW.indd 19
Ngombe amezaliwa
na mama yake.
Mama yake ngombe
ametoka wapi?
Mama yake ngombe
amezaliwa na mama
yake.
Ngombe wa kwanza
ametoka wapi?
Nani aliyemuumba
ngombe wa kwanza?
Yai
Ng'ombe
Maziwa
3/30/2016 1:12:43 PM
AN-NUUR
20
MAKALA
20
Soma gazeti la
AN-NUUR
KWA TSH 800/=
kila Ijumaa
AN-NUUR
BWENI la Shule ya
Kiislamu ya Ilala, Jijini
Dar es Salaam, limeteketea
kwa moto na kusababisha
hasara ya zaidi ya Shilingi
Milioni 45.
Moto huo uliozuka
majira ya saa saba usiku
wa Ijumaa kuamkia
Jumamosi ya wiki iliyopita,
umeunguza bweni lote la
wavulana la shule hiyo na
hakuna mali iliyookolewa.
Akielezea tukio hilo,
Meneja msaidizi wa
Shule hiyo (Ilala Islamic)
Mwalim Ramadhan Fadhil
Shaaban, alisema katika
ajali hiyo wanafunzi wote
wamenusurika na kwamba
hakuna mwanafunzi aliye
pata madhara pamoja
na wafanyakazi wengine
waliokuwepo wakati huo.
Hata hivyo, Mwl.
Ramadhani, alisema
pamoja na kusalimika
huko lakini hawakuweza
kunusuru mali ya aina yoyote
na kupelekea moto huo
kuteketeza karibia magodoro
SHINIKIZO LA DAMU
(HYPERTENSION/HIGH BLOOD PRESSURE)
UGONJWA WA MOYO
KIHARUSI
JONGO (GOUT)
MAUMIVU YA VIUNGO (RHEUMATISM)
MAUMIVU SUGU YA KICHWA
BAWASIR (PILES/HEMORRHOIDS)
MAGONJWA YA INI
SARATANI MBALIMBALI
UOTO/UVIMBE MBALIMBALI KATIKA
VIUNGO VYA UZAZI VYA MWANAMKE
(FIBROIDS, POLYPS NA CYSTS)
KUSHINDWA KUZUIA MKOJO (URINARY
INCONTINENCE)
ATHARI ZA KISUKARI CHA UKUBWANI
PUMU
UPUNGUFU WA KINGA ZA MWILI
KASI YA KUZEEKA
MATATIZO YA MFUMO WA MZUNGUKO
WA DAMU
MKAKAMO WA NGOZI;
UDHAIFU WA MACHO
KUPOTEZA KUMBUKUMBU
KASI NDOGO YA KUPONA MAJERAHA
MAKOVU KWENYE MAPAFU
UGONJWA WA NGOZI KUCHUJA RANGI,
YAANI, VITILIGO
Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na Business Printers Ltd, Dar es Salaam.
ANNUUR NEW.indd 20
3/30/2016 1:12:45 PM