Вы находитесь на странице: 1из 12

HABARI

HABARIZA
ZA
NISHATI
NISHATI&MADINI
&MADINI

NewsBulletin
http://www.mem.go.tz

Ni
Rasmi
Wabunge
Toleo
No.117
51
Toleo No.

Limesambazwa
kwa Taasisi
naTaasisi
Idarana
zote
MEM
Limesambazwa
kwa
Idara
zote MEM Tarehe - 23-29 Januari , 2015
Aprili 28 - Mei 4, 2016

WAZIRI WA NISHATI NA MADINI AZINDUA RASMI BODI YA TANESCO -Uk2

Bomba la Mafuta n
kupita Tanzania

Reli, Barabara, Usalama


vyachangia ushindi

Waimwagia sifa MEM, TANESCO, REA

>>SOMA UK. 2

Somahabari Uk.2

Prof. Sospeter Muhongo


Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati) akipunga mkono mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege
wa wa
Kimataifa
akitokea nchini Uganda ambapo ilitangazwa BombaMkurugenzi
la mafuta litajengwa
Hoima nchini
Uganda
Mtend- kutoka
Mkurugenzi
Mkuu wa
Waziri
Nishatiwa Julius Nyerere
NaibuniWaziri
waMkuu
Nishati
Naibu
Wazirina
waMadini,
NishatiProfesa
na
hadi Bandari
ya Tanga. Kulia
Katibu
wana
Wizara
ya Nishati
Justin
Ntalikwa aliyeambatana
na Waziri
nchini
aji
wa TANESCO,
REA,
Dk.
Lutengano
na Madini,
Profesa
Madini,
anayeshughulikia
Madini
anayeshughulikia
MhandisiJuliana
Felchesmi
Uganda.
Kushoto ni Naibu
Katibu
Mkuu anayeshughulikia
masuala
ya Nishati, Dkt. Mhandisi
Pallangyo,Mwakahesya
nyuma kutoka kushoto
Sospeter
Muhongo
Madini
Stephen
Masele
Nishati,
Charles
Kitwanga
Mramba
ni Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Madini, Profesa James Mdoe, Kamishna Msaidizi wa Nishati anayeshughulikia Maendeleo ya
Nishati, James Andilile na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Dkt. James Mataragio.

JWTZ wapongezwa kunusuru mtambo wa Msimbati-Uk4

Ofisi ya M awasiliano Serik alini inapokea habari za matukio mbalimbali


kwa ajili ya News Bullettin hii ya Wizar a ya Nishati na Madini
Ofisi ya Mawasiliano Serik alini inapokea habari za matukio mbalimbali
Wasiliana nasi Kitengo cha Mawasiliano kwa simu Namba +255 22 2110490 Fax 2110389 Mob: +255 732 999263
kwa
ajili ya News Bullettin
Jarida laGhorofa
Wizarya
a Tano
ya Nishati
au Fika hii
Ofisina
ya Mawasiliano
(MEM) na Madini
Wasiliana nasi Kitengo cha Mawasiliano kwa simu Namba +255 22 2110490 Fax 2110389 Mob: +255 732 999263
au Fika Ofisi ya Mawasiliano Ghorofa ya Tano (MEM) Barua pepe: badra77@yahoo.com

HABARI ZA NISHATI/MADINI

NewsBulletin
http://www.mem.go.tz

Bomba la Mafuta
kupita Tanzania
Na Asteria Muhozya, DSM

aziri wa Nishati na
Madini, Profesa
Sospeter Muhongo
amesema kuwa,
bomba la kusafirisha
mafuta ghafi kutoka Hoima Ziwa
Albert nchini Uganda litapita nchini
baada ya hoja za Tanzania kupitisha
bomba hilo nchini kukubaliwa na
Uganda.
Profesa Muhongo aliyasema hayo
mwishoni mwa wiki, mara tu baada
ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege
wa Kimataifa wa Mwalimu Julius
Nyerere (JNIA), akitokea nchini
Uganda, ambapo pia aliambatana na
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati
na Madini, Profesa Justin Ntalikwa
na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika
la Maendeleo ya Petroli Tanzania
(TPDC), Dkt. James Mataragio.
Kauli ya Profesa Muhongo inakuja
baada ya Rais wa Uganda Yoweri
Museveni kutangaza hivi karibuni
wakati wa Mkutano wa 13 wa
Ushoroba wa Kaskazini kuwa, bomba
hilo la mafuta ghafi kutoka Hoima,
Ziwa Albert nchini Uganda litapita
katika ardhi ya Tanzania kwenda
Bandari ya Tanga.
Akieleza kuhusu siri ya ushindi
wa Tanzania, Prof. Muhongo
alisema kuwa, zipo sababu kadhaa
zilizochangia ushindi huo ikiwemo
kina kirefu cha maji katika bandari

ya Tanga ukilinganisha na bandari


ya Lamu nchini Kenya, na kuongeza
kuwa, bandari ya Tanga ina kina cha
futi 25 kwenda chini jambo ambalo
litawezesha shughuli za kupakia
mafuta hayo kuwa rahisi, na kuongeza
kuwa, bandari hiyo ina uwezo wa
kufanya kazi kwa kipindi cha mwaka
mzima.
Vilevile, Prof. Muhongo aliitaja
miunganiko ya njia ya reli ya Tanga
hadi reli ya Kati kuwa ni sababu
nyingine
iliyochangia
Tanzania
kushinda, ambapo alimsifu Rais John
Pombe Magufuli kwa kusimamia vema
masuala ya ujenzi wa barabara nchini
wakati alipokuwa Waziri wa Ujenzi
na kusema kuwa, miundombinu ya
barabara imechangia katika ushindi wa
Tanzania.
Kwa kweli ninampongeza sana
Rais Magufuli kwa kusimamia vema
ujenzi wa miundombinu ya barabara
wakati akiwa Waziri wa Ujenzi.
Uwepo wa barabara nyingi ilikuwa
nafasi nyingine kwa Tanzania kushinda
kwa sababu miundombinu kama hiyo
haipo kaskazini mwa Kenya. Magufuli
asingesimamia vema suala hili,
tusingepata sifa hizi, alisisitiza Prof.
Muhongo.
Mbali na sifa hizo, Prof. Muhongo
pia aliitaja sababu nyingine kuwa
ni usalama na uzoefu wa Tanzania
katika ujenzi wa mabomba na kuyataja
mabomba ambayo tayari yamejengwa
nchini kuwa ni pamoja na bomba la
kusafirisha mafuta kutoka Tanzania

Mmiliki wa Blogu ya Michuzi na Mwandishi wa habari Mwandamizi wa


Magazeti ya Serikali, Issa Michuzi (kulia) akiongea na Waziri wa Nishati
na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati). Kushoto ni Naibu
Katibu Mkuu anayeshughulikia masuala ya Nishati, Dkt. Mhandisi Juliana
Pallangyo , Nyuma ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini,
Profesa Justin Ntalikwa.
hadi nchini Zambia la (TAZAMA),
bomba la gesi la kutoka Kisiwa cha
Songosongo mpaka Ubungo, Dar es
Salaam na bomba la Gesi la
Uzoefu wetu katika ujenzi wa
mabomba mbalimbali nayo ni sababu
iliyochangia ushindi wetu pamoja na
usalama. Tunataka kujenga bomba
hili haraka sana mpango ni kukamilika
ifikapo Juni, 2020, alisema Prof.
Muhongo.
Akizungumzia gharama za mradi
huo, alisema kuwa utagharimu kiasi cha

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati), akiwaonesha waandishi wa habari ramani
ya mahali litakapopita bomba la mafuta kutoka Hoima nchini Uganda hadi Bandari ya Tanga nchini.

Dola za Marekani Bilioni 4 na kuutaja


kuwa ni mradi mwingine mkubwa wa
kihistoria, ambapo kukamilika kwake
kutawezesha kusafirisha jumla ya
mapipa ya mafuta Laki mbili (200,000)
kwa siku, ikiwemo kutoa ajira rasmi na
zisizo rasmi.
Nje ya matumizi ya mafuta, Prof.
Muhongo alisema kuwa, bomba hilo
pia litatumika kwa ajili ya matumizi
ya kupitisha gesi asilia kwenda katika
mikoa ya Kaskazini.
Watanzania tujiamini, tunaweza,
wazazi wasaidieni vijana wasome
masomo ya sayansi. Bado tunahitaji
wataalam wana sayansi. Lakini mbali
na hilo, bomba hili ni fursa ya ajira.
Wafanyabiashara na watanzania
mjitayarishe kuchangamkia fursa
zitakazotokana na ujenzi wa bomba
hili, alisema Prof. Muhongo.
Kuhusu watumiaji wengine wa
bomba hilo nje ya Tanzania, alizitaja
nchi za Burundi, Sudan na Kongo na
kueleza kuwa, kwa miaka ijayo nchi
hizo pia zitatumia bomba hilo.
Ili kuanza utekelezaji wa ujenzi
wa bomba hilo, Prof. Muhongo
alisema kuwa, Aprili 29, 2016, Waziri
anayeshughulikia masuala ya Mafuta
wa Uganda pamoja na kampuni
zitakazojenga bomba hilo za Total
E&P ya Ufaransa, Tullow Oil ya
Uingereza, China National Offshore
Oil Corporation (CNOOC) na
Mamlaka zinazohusika na masuala ya
mafuta za Tanzania watakutana jijini
Dar es Saalam ili kuweka mpango kazi
wa utekelezaji wa mradi huo.
Tanzania ilikuwa ikishindana
na nchi ya Kenya kupata nafasi ya
mradi wa bomba hilo wenye kilomita
zipatazo 1,403 kutoka Hoima
Uganda hadi bandari ya Tanga. Bomba
hilo linatarajiwa kupita katika mikoa
kadhaa nchini, ikiwemo ya Kagera,
Geita, Tabora, Shinyanga, Dodoma na
Tanga.

NewsBulletin

HABARI ZA NISHATI/MADINI

http://www.mem.go.tz

TAHARIRI

Bomba la Mafuta kupita


Tanzania, watanzania
tuchangamkie fursa

Tarehe 24 April, 2016, Viongozi wa Wizara ya Nishati na


Madini wakiongozwa na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa
Sospeter Muhongo walitua kwa ushujaa katika Uwanja wa
Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere
wakitokea nchini Uganda katika Mkutano wa 13 wa Ushoroba
wa Kaskazini ambapo Rais wa Uganda, Yoweri Museveni
alitangaza kuwa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima, Ziwa
Albert nchini Uganda litapita Tanzania badala ya bandari ya
Lamu nchini Kenya.
Mara baada ya kuwasili katika Uwanja huo akiwa ameambata
na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa Justin
Ntalikwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo
ya Petroli Tanzania (TPDC), Dkt. James Mataragio, Profesa
Muhongo alisema kuwa bomba hilo litapita Tanzania baada ya
sababu za kupitisha bomba hilo nchini zilizotolewa na wataalam
wa Tanzania, kukubalika na nchi ya Uganda.
Akieleza kuhusu siri ya ushindi wa Tanzania, Prof. Muhongo
alisema kuwa, zipo sababu kadhaa zilizochangia ushindi
huo ikiwemo kina kirefu cha maji katika bandari ya Tanga
ukilinganisha na bandari ya Lamu nchini Kenya.
Alisema kuwa bandari ya Tanga ina kina cha futi 25 kwenda
chini jambo ambalo litawezesha shughuli za kupakia mafuta
hayo kuwa rahisi, na kuongeza kuwa, bandari hiyo ina uwezo wa
kufanya kazi kwa kipindi cha mwaka mzima.
Vilevile, Prof. Muhongo aliitaja miunganiko ya njia ya reli
ya Tanga hadi reli ya Kati kuwa ni sababu nyingine iliyochangia
Tanzania kushinda, ambapo alimsifu Rais John Pombe Magufuli
kwakusimamiavemamasualayaujenziwabarabaranchiniwakati
alipokuwa Waziri wa Ujenzi na kusema kuwa, miundombinu ya
barabara imechangia katika ushindi wa Tanzania kwani itakuwa
rahisi kwa usafirishaji ikiwemo wa mizigo kama mabomba.
Ili kuanza utekelezaji wa ujenzi wa bomba hilo, Prof. Muhongo
alisema kuwa, Aprili 29, 2016, Waziri anayeshughulikia masuala
ya Mafuta wa Uganda pamoja na kampuni zitakazojenga bomba
hilo za Total E&P ya Ufaransa, Tullow Oil ya Uingereza, China
National Offshore Oil Corporation (CNOOC) na Mamlaka
zinazohusika na masuala ya mafuta za Tanzania watakutana
jijini Dar es Saalam ili kuweka mpango kazi wa utekelezaji wa
mradi huo.
Hizi ni habari njema kwa nchi yetu kwani mradi huo
unakuja na fursa mbalimbali ambazo watanzania sasa inabidi
tuzichangamkie ili kuona manufaa ya mradi huo.
Baadhi ya fursa zitakazopatikana mara baada ya kuanza
kwa utekelezaji wa mradi huo ni pamoja na kufanya huduma
ya Tathmini za ulipaji fidia, Huduma za magreda/makatapila,
Huduma za kunyanyua vitu vizito, Usanifu/michoro, Huduma
za usafirishaji, Uchimbaji visima vya maji, Ukodishaji wa ndege
na helikopta na huduma za kihasibu na ukaguzi wa mahesabu.
Huduma nyingine ni Ujenzi wa kambi za ujenzi, Majengo
ya kuhifadhia vifaa mbali mbali vya ujenzi, Huduma za vyakula
na malazi kwenye kambi za ujenzi , Huduma za uuzaji mafuta,
Karakana za ukarabati wa mashine mbali mbali na magari,
Huduma za sheria, Huduma za Mawasiliano, Kandarasi za
kusamba vifaa vya ujenzi, Huduma za ulinzi wakati wa ujenzi na
pia mradi utakapokamilika.
Hima hima watanzania, tujiandae ili mara fursa hizo
zitakapotangazwa kuanza rasmi, tujitokeze na hivyo kuleta faida
kwa Taifa letu na mwananchi mmoja mmoja.

Makamishna wa Madini
kukutana Morogoro
Na Greyson Mwase,
Dar es Salaam

akamishna Wasaidizi wa
Madini kutoka Makao
Makuu ya Wizara ya
Nishati na Madini pamoja
na Kanda zake, na Maafisa
Madini Wakaazi nchini wanatarajia kufanya
kikao kazi chenye lengo la kujadili shughuli
zinazotekelezwa na Mradi wa Usimamizi
Endelevu wa Rasilimali Madini (SMMRP)
pamoja na Sekta ya Madini kwa ujumla.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka Wizara
ya Nishati na Madini iliyotolewa hivi
karibuni jijini Dar es Salaam imeeleza kuwa
kikao hicho cha siku mbili kitakutanisha
Makamishna wasaidizi wa Madini walioko
Makao Makuu ya Wizara, Makamishna
Wasaidizi wa Madini wa Kanda, Maafisa
Madini Wakaazi na Katibu Mkuu wa
Wizara Prof. Justin Ntalikwa lengo likiwa ni
kujadili maendeleo ya utekelezaji wa miradi
inayosimamiwa na SMMRP na Sekta ya

Madini kwa ujumla.


Taarifa hiyo ilieleza kuwa katika
kikao hicho na Katibu Mkuu wa Wizara
ya Nishati na Madini Prof. Ntalikwa,
Makamishna Wasaidizi na Maafisa Madini
hao kutoka katika ofisi zote za madini
nchini, watatakiwa kuwasilisha changamoto
wanazokabiliana nazo wakati wa utendaji
wa kazi zao ili kuangalia njia bora za
kutatua.
Aidha, kikao hicho kitajadili jinsi ya
kutekeleza Awamu ya Pili ya Mradi wa
Usimamizi Endelevu wa Rasilimali Madini
(SMMRP) hususan uanzishwaji wa senta
bora za mfano kwa ajili ya wachimbaji
wadogo.
Taarifa hiyo iliendelea kueleza kuwa
timu ya Mradi itawasilisha utekelezaji
wa shughuli za mradi na kujadiliwa na
wataalam kama mwongozo wa utekelezaji
wa mradi unavyotaka ambapo sehemu ya
uchimbaji mdogo itawasilisha mafanikio na
changamoto zilizojitokeza wakati wa utoaji
wa ruzuku ya Awamu ya Pili.

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA),


Mhandisi Dominic Rwekaza (kushoto) akiwa na Meneja Mradi wa Usimamizi
Endelevu wa Rasilimali Madini (SMMRP), Mhandisi Idrisa Yahaya na Kiongozi
wa Mradi wa SMMRP wa Benki ya Dunia, Mamadou Barry, wakizungumza
mara baada ya kuhudhuria Semina ya Mafunzo kutoka Chuo cha Jemolojia
cha Madagascar iliyotolewa wakati wa Maonesho ya Tano ya Kimataifa ya
Vito Arusha, yaliyofanyika jijini Arusha tarehe 19 hadi 21 Aprili, 2016.
KWA HABARI PIGA SIMU
KITENGO CHA MAWASILIANO

TEL-2110490
FAX-2110389
MOB-0732999263
BODI YA UHARIRI
MSANIFU: Lucas Gordon
WAANDISHI: Veronica Simba, Asteria Muhozya, Greyson
Mwase, Teresia Mhagama, Mohamed Saif, Rhoda James ,
Nuru Mwasampeta na Zuena Msuya

FIVE
PILLARS OF
REFORMS
INCREASE EFFICIENCY
QUALITY DELIVERY
OF GOODS/SERVICE
SATISFACTION OF
THE CLIENT
SATISFACTION OF
BUSINESS PARTNERS
SATISFACTION OF
SHAREHOLDERS

HABARI ZA NISHATI/MADINI

NewsBulletin
http://www.mem.go.tz

Mnada wa Madini waiingizia


Serikali Bilioni 1.6
Teresia Mhagama na
Asteria Muhozya, Arusha

erikali imepata jumla ya


shilingi bilioni 1.6 ikiwa ni
mapato yaliyopatikana katika
mnada wa madini uliofanyika
wakati wa Maonesho ya Tano
ya Kimataifa ya Vito yaliyofanyika
jijini Arusha katika Hoteli ya Mt.Meru
kuanzia tarehe 19 hadi 21, Aprili
mwaka huu.
Hayo yameelezwa hivi karibuni jijini
Arusha na Mkurugenzi wa Kitengo
cha Uthaminishaji Madini ya Almasi
na Vito (TANSORT) katika Wizara ya
Nishati na Madini, Archard Kalugendo,
wakati akitangaza matokeo ya mnada
huo.
Katika maonesho hayo, kulikuwa
na Tenda Tatu; Tenda ya Kwanza
ilikuwa ya Serikali ikihusisha madini
mbalimbali yaliyokuwa yakishikiliwa
na Kamishna wa Madini ambapo
jumla ya shilingi za kitanzania bilioni
1.3 zilipatikana kutokana na mauzo ya
madini hayo.
Tenda ya pili ilikuwa ni madini
ya Tanzanite ghafi yaliyozalishwa na
mgodi wa TanzaniteOne unaomilikiwa
kwa ubia kati ya kampuni ya Sky
Associates na Shirika la Madini la Taifa
(STAMICO).
Napenda kushukuru mgodi wa
TanzaniteOne kwani wametuletea
madini ya Tanzanite ambayo ni ghafi
yenye thamani kubwa ambapo madini

yote kutoka mgodi huu yamenunuliwa


kwa thamani ya shilingi za Kitanzania
Bilioni Tano (5), alisema Kalugendo.
Kalugendo alisema kuwa tenda
ya tatu ya mnada huo ilikuwa ya
kampuni ya El-Hilal inayochimba
madini ya Almas nchini. Alifafanua
kuwa, kampuni mbili zilizojitokeza
katika tenda hiyo hazikufikia kiwango
cha chini cha bei iliyowekwa na
Serikali hivyo kupelekea madini hayo
kutokuuzwa katika mnada huo.
Hii ni kusema kwamba madini yote
ya Tanzanite yaliyoletwa na mgodi wa
TanzaniteOne na Tanzanite iliyoletwa
na Serikali katika kifurushi cha kwanza
pamoja na dhahabu yote iliyokuwa
katika kifurushi hicho yameuzwa,
alisema Kalugendo.
Aliongeza kuwa, fedha yote
iliyopatikana kutokana na mauzo ya
madini yaliyokuwa yakishikiliwa na
KamishnawaMadini,inaingizwakatika
mfuko wa Serikali na kwamba madini
ghafi yaliyouzwa kutoka TanzaniteOne
yatalipiwa mrabaha serikalini wa
shilingi milioni 245,686,000 ili madini
hayo yaweze kusafirishwa popote.
Aidha, Kalugendo alisisitiza kuwa
mapato hayo ni ya mnada tu hivyo
mauzo ya jumla ya maonesho hayo
yatatangazwa baada ya kujumuisha
matokeo ya mauzo yote yaliyofanyika
katika Maonesho husika.
Pia, Mkurugenzi wa Uthamini wa
Madini na Huduma za Kimaabara
kutoka Wakala wa Ukaguzi wa

Mkurugenzi wa Kitengo cha Uthaminishaji Madini ya Almas na Vito,


katika Wizara ya Nishati na Madini, Archard Kalugendo akiangalia
maombi ya ahadi za bei ya madini yaliyopigwa mnada katika Maonesho
ya Tano ya Kimataifa ya Vito yaliyofanyika jijini Arusha kuanzia tarehe
19 hadi 21, Aprili, 2016. Wanaoshuhudia ni Kamishna Msaidizi wa
Madini, Uchumi na Biashara, Salim Salim (Wa Pili kushoto), Wa Pili
kulia ni Mkurugenzi wa Uthamini wa Madini na Huduma za Kimaabara
katika Wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA), Mhandisi Gilay
Shamika na wa kwanza kulia ni Mthamini Almas wa Serikali, Edward
Rweyemamu.

Madini Tanzania (TMAA), Mhandisi


Gilay Shamika, akiwa katika
Mnada wa Madini yaliyo chini ya
Kamishna wa Madini, alitoa wito
kwa wafanyabiashara kufuata sheria,
taratibu na kanuni za biashara ya
Madini ili kutotaifishiwa Madini yao
mara wanapokamatwa bila kuwa na
vibali husika.
Madini
haya
unayoyaona
yakipigwa mnada, yalikamatwa na
kutaifishwa pindi yakitoroshwa nje ya

nchi bila wahusika kuwa na vibali vya


usafirishaji. Ni vema wafanyabiashara
kufuata taratibu kwa mujibu wa Sheria
ya Madini ya mwaka 2010, Alisema
Shamika.
Naye kamishna Msaidizi wa Madini
anayeshughulikia Uchumi na Biashara,
Salim Salim aliwashukuru wadau wote
walioshiriki na kudhamini maonesho
hayo ambayo ni muhimu katika
uendelezaji wa Sekta ya Madini nchini.

Wadau mbalimbali wakishuhudia, Mkurugenzi wa Kitengo cha


Uthaminishaji Madini ya Almas na Vito, katika Wizara ya Nishati na
Madini, Archard Kalugendo akifungua masanduku yenye bahasha za
ahadi ya bei za madini yaliyopigwa mnada katika Maonesho ya Tano ya
Kimataifa ya Vito yaliyofanyika jijini Arusha kuanzia tarehe 19 hadi 21,
Aprili, 2016.

Wadau mbalimbali walioshiriki Maonesho ya Tano ya Kimataifa ya


Vito yaliyofanyika jijini Arusha kuanzia tarehe 19 hadi 21 wakimsikiliza
Mkurugenzi wa Kitengo cha Uthaminishaji Madini ya Almas na Vito,
katika Wizara ya Nishati na Madini, Archard Kalugendo (hayupo
pichani) wakati akitangaza matokeo ya mnada wa madini uliofanyika
katika Maonesho hayo.

NewsBulletin
http://www.mem.go.tz

Na Teresia Mhagama,
Arusha

meelezwa kuwa Maabara ya


Madini ya Wakala wa Ukaguzi
wa Madini Tanzania (TMAA)
mbali na kupima ubora wa
Sampuli za Madini kutoka katika
Migodi mikubwa, Kati na Midogo
kwa ajili ya Serikali kupata Mapato
kulingana na ubora wa Madini husika
pia inatoa elimu kwa wananchi ili
waweze kutumia maabara hiyo
kutambua aina na thamani ya Madini
ya Vito pamoja na Madini ya Metali.
Hayo yalisemwa na Mkurugenzi wa
Uthamini wa Madini na Huduma za
Maabara kutoka Wakala wa Ukaguzi
wa Madini (TMAA), Mhandisi Gilay
Shamika katika Maonesho ya Tano ya
Kimataifa ya Vito yaliyofanyika jijini
Arusha hivi karibuni.
Alisema kuwa TMAA imeamua
kutumia maonesho hayo kutoa Elimu
hiyo ya kupima ubora wa sampuli za
madini kwa wananchi kwa kuwa watu
wengi hawafahamu aina za Madini
hayo na hivyo kuyauza au kununua
kwa bei isiyo halali.
Mfano, Watu wengi wamekuwa
wakitapeliwa Madini ya Rubi
wanapopeleka sokoni kuyauza na
kuambiwa kuwa siyo Rubi bali ni
Garnert nyekundu. Hali kadhalika
watu huuziwa Iolite kwa kuambiwa
kuwa ni Tanzanite kwa sababu
zinafanana rangi, alisema Mhandisi
Shamika
Pia kwa upande wa dhahabu,
alieleza kuwa kuna wimbi la watu
kuuziwa Madini ya shaba badala ya
dhahabu kwani Dhahabu kidogo
huwekwa juu ya shaba na kuuzwa
kama dhahabu halisi.
Ili kuondokana na utata wote huo
wa kutapeliwa, Mhandisi Shamika
alitumia Maonesho hayo kuwaasa
wananchi kutumia maabara ya
TMAA iliyopo katika Makao Makuu

HABARI ZA NISHATI/MADINI

Wananchi waelimishwa kuhusu


Maabara ya Madini ya TMAA

Meneja wa Maabara ya Wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA), Mhandisi Mvunilwa Mwarabu
akionesha mashine ya kupima kiwango cha madini inayoitwa Atomic Absorption Spectroscopy (AAS).
ya Wakala huo, Barabara ya Chole jijini
Dar es Salaam, Capripoint Mwanza,
Mafao House Arusha na Uhindini
Mbeya.
Alisema kuwa Maabara ya Wakala
wa Ukaguzi wa Madini Tanzania ina
ubora wa kimataifa yaani ISO 17025,
ikimaanisha kuwa huduma zake
zinatambulika na kukubalika ndani na
nje ya nchi.
Kwa upande wa Madini ya

Mkemia kutoka Wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA),


Alfred Aloyce akionesha sampuli ya dhahabu iliyotayarishwa kwa ajili
ya kufanyiwa uchunguzi wa kimaabara ili kubaini kiasi cha madini ya
dhahabu na fedha.

Metali kama dhahabu,shaba, fedha


na chuma, Maabara ya TMAA ina
uwezo wa kutambua aina na asilimia
za Madini zilizopo katika miamba (
rocks) na udongo (soil), pia kupima
ubora wa Madini kwa kuainisha kiasi
cha asilimia za Madini kwa kutumia
AAS Machine, XRF Machine, Fire
assay na njia nyingine.
Aidha kwa Madini ya Vito,
Maabara ya Wakala ina uwezo wa

kutambua aina ya Madini ya Vito


pamoja na kupanga ubora wa hayo na
Huduma nyingine muambata.
Kuhusu Mawasiliano, Mhandisi
Shamika alisema kuwa, tovuti ya
Wakala ambayo ni www.tmaa.go.tz
inaonesha Mawasiliano ya Maabara
zote za Wakala zilizopo katika Ofisi
Kuu na Ofisi za Kanda za Wakala.
Mawasiliano ya Makao Makuu ni
+255-22- 2601819

Mashine ya kuyeyusha sampuli za madini (fusion and cupellation


furnaces) inayotumika kwenye Maabara ya Wakala wa Ukaguzi wa
Madini Tanzania (TMAA).

HABARI ZA NISHATI/MADINI

NewsBulletin
http://www.mem.go.tz

TPDC YASAIDIA MADAWATI


KINYEREZI DAR ES SALAAM
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi (kulia)
akipokea mfano wa hundi ya Shilingi milioni 7,440,000
kwa ajili ya kununulia Madawati katika Shule ya Msingi
Zimbili, Kinyerezi kutoka kwa Meneja Mawasiliano wa
Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Marie
Msellemu (Kushoto) kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji
wa TPDC.

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi (mwenye nguo


nyeupe) akiwa na wafanyakazi wa TPDC katika hafla
fupi ya kukabidhi hundi ya Shilingi milioni 7,440,000 kwa
ajili ya kununulia Madawati ya Shule ya Msingi Zimbili,
Kinyerezi Jijini Dar es Salaam.

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi akionesha


hundi ya Shilingi milioni 7,440,000 iliyotolewa na Shirika
la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kwa ajili ya
ununuzi wa Madawati kwa Shule ya Msingi Zimbili
Kinyerezi jijini Dar es Salaam mbele ya waandishi wa
habari.
Meneja Mawasiliano TPDC, Marie
Msellemu akizungumza katika hafla fupi
ya kukabidhi hundi ya Shilingi milioni
7,440,000 kwa ajili ya kununulia Madawati
ya Shule ya Msingi Zimbili, Kinyerezi Jijini
Dar es Salaam hivi karibuni, wengine ni
Mkuu wa Wilaya ya Ilala,. Raymond Mushi
(wa pili kulia) na Diwani wa Kinyerezi,
Greyson Selestine (kushoto).

NewsBulletin

HABARI ZA NISHATI/MADINI

http://www.mem.go.tz

Profesa Muhongo asaini


kibali cha kuhamisha leseni

Na Zuena Msuya, DSM

W
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, (katikati)
akiwa na ujumbe kutoka Ubalozi wa China ukiongozwa na Kansela
Gou Haodong (kulia kwa Waziri) pamoja na watendaji wa Wizara
wakiwa katika kikao cha pamoja kabla ya kusainiwa kwa kibali cha
kuhamisha leseni ya uchimbaji wa kati wa madini kutoka Kampuni
ya uchimbaji wa madini ya China ya Henan AfroAsia GeoEngeneering (Tanzania) kwenda Kampuni ya uchimbaji wa Dhahabu
EM Tanzania Limited.

aziri wa Nishati
na Madini Profesa
Sospeter Muhongo
amesaini kibali cha
kuhamisha leseni ya
uchimbaji wa kati wa madini kutoka
ampuni ya uchimbaji wa madini ya
China ya Henan AfroAsia GeoEngeneering (Tanzania) kwenda
Kampuni ya uchimbaji wa Dhahabu
ZEM Tanzania Limited.
Akizungumza mara baada ya
kusaini kibali hicho hivi karibuni,
jijini Dar es salaam,Profesa Muhongo
alisema kampuni hiyo itaanza
shughuli za uchimbaji mwanzoni
mwa mwezi Desemba mwaka huu,
katika kijiji cha Nyasirori wilayani
Butiama Mkoani Mara.
Alifafanua kuwa kusaini kibali
hicho kunatoa fursa kwa kampuni
ya China ya uchimbaji wa madini ya
ZEM, ambayo iliingia makubalianao
ya kufanya kazi na kampuni ya
Henan AfroAsia Geo- Engeneering
(Tanzania) mwezi Desemba mwaka
2015. Gharama za mradi huo
zinakadiriwa kufikia kiasi cha dola za
Marekani mlioni43.3.
Aidha Profesa Muhongo alisema
kuwa kampuni za China kuendelea
kuwekeza katika miradi mikubwa ya
maendeleo ni kuendelea kuimarisha
ushirikiano kati ya nchi hizo mbili
Tanzania na china ulioanzishwa na
Mwasisi Baba wa Taifa Mwalimu

Julius Nyerere.
Kwa upande wake Naibu Katibu
Mkuu wa Wizara ya Nishati na
Madini anayeshughulikia Madini
Profesa James Mdoe aliisisitiza
kampuni hiyo kutekeleza masharti
katika leseni za uchimbaji wa madini
ili kuweza kufanya kazi kwa ufanisi
mkubwa.
Vilevile aliwataka wawekezaji hao
kutekeleza mradi huo katika muda
walioahidi ili kuondoa usumbufu
na dhana ya kutokuwa na imani na
Kampuni hiyo.
Aliongeza kuwa, mradi huo
umepokelewa vyema na wakazi
pamoja na wachimbaji wadogo wa
eneo hilo kwani hakuna malalamiko
yoyote yaliyojitokeza hadi kufikia
hatua ya kuanza uchimbaji. Naye
Kansela wa ubalozi wa China nchini
Tanzania, Gou Haodong aliwataka
wawekezaji hao kujenga mahusiano
mazuri kati yao na wakazi wa vijiji
vinavyozunguka mgodi huo kwa
kuwawekea huduma za kijamii.
Haodong alitaja miradi hiyo kuwa
ni pamoja na kujenga visima vya
maji safi na salama karibu na makazi
ya watu kwani wanavijiji wengi
wamekuwa wakitembea umbali
mrefu kwenda kufuata huduma ya
maji. Sambamba na hilo alieleza kuwa
kampuni hiyo ya uchimbaji inatakiwa
kutoa huduma ya afya kwa wananchi
wa maeneo hayo kwa kuwajengea
zahanati na kuwezesha upatikani wa
huduma za dawa na madaktari.
Kansela huyo wa Ubalozi wa
China nchini, alisisita kuhusu suala la
elimu ambalo alisema kuwa ni vyema
kampuni za uchimbaji wa madini
zikaweka mazingira mazuri ya elimu
bora kwa jamii zinazowazunguka ili
kuunga mkono Serikali ya Tanzania
ya kutoa elimu bora kwa kila
mtanzania.

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, akisaini


kibali cha kuhamisha leseni ya uchimbaji wa kati wa madini kutoka
Kampuni ya uchimbaji Madini ya China ya Henan AfroAsia
Geo- Engeneering (Tanzania) kwenda Kampuni ya uchimbaji wa
Dhahabu ZEM Tanzania Limited. Tukio lilifanyika katika Ukumbi
wa Mikutano wa Wizara ya Nishati na Madini.

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, (kulia)


akibadilishana mawazo na Kansela wa Ubalozi wa China, Gou
Haodong (wa pili kushoto) katika Ofisi ya Waziri wa Nishati na
Madini baada ya kumaliza kusaini kibali cha kuhamisha leseni ya
Uchimbaji Madini katika Kijiji cha Nyasirori wilayani Butiama
utakaoanza mwezi Desemba mwaka huu. Kulia ni Meneja wa
Kampuni ya uchimbaji madini ya Henan AfroAsia Zhang Jiangbo.

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, (wa


pili kulia) Kansela wa Ubalozi wa China nchini, Gou Haodong
(wa pili kushoto) na Maneja wa Kampuni ya Uchimbaji Madini
ya Henan AfroAsia Zhang Jiangbo kwa pamoja wakionesha kibali
cha kuhamisha leseni ya uchimbaji wa kati wa madini kutoka
Kampuni ya uchimbaji Madini ya China ya Henan AfroAsia GeoEngeneering (Tanzania) kwenda Kampuni ya uchimbaji wa Dhahabu
ZEM Tanzania Limited, uchimbaji wa madini hayo utafanyika katika
kijiji cha Nyasirori Wilayani Butiama Mkoani Mara kuanzia mwezi
Desemba mwaka 2016.

HABARI ZA NISHATI/MADINI

NewsBulletin
http://www.mem.go.tz

BOMBA LA MAFUTA KUTOKA UGANDA...

Viongozi wakipokelewa JNIA

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter


Muhongo akipongezwa na Madereva wa Taxi wa
Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere kufuatia
ushindi wa Tanzania wa kupitisha bomba la mafuta
nchini. Wengine wanaofuatilia ni baadhi ya watendaji
wa Wizara waliofika uwanjani hapo kumpokea na
baadhi ya wananchi waliokuwa uwanjani hapo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania


(TPDC), Dkt. James Mataragio (kushoto) akipongezwa na baadhi ya
watumishi kutoka Idara ya Mawasiliano wa shirika hilo mara baada
ya kuwasili kutoka nchini Uganda.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia


Madini, Profesa James Mdoe (wa kwanza kulia) akizungumza jambo
na baadhi ya watendaji kutoka Wizara ya Nishati na Madini wakati
wakisubiri kuwasili kwa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa
Sospeter Muhongo. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa
Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Dkt. James
Mataragio, Kamishna Msaidizi wa Nishati anayeshughulikia
Maendeleo ya Nishati, James Andilile, Naibu Katibu Mkuu
anayeshughulikia masuala ya Nishati, Dkt. Mhandisi Juliana
Pallangyo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini,
Profesa Justin Ntalikwa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la
Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Dkt. James Mataragio
(kulia) akiongea jambo na baadhi ya watendaji wakuu wa Wizara
ya Nishati na Madini wakati wakisubiri kuwasili kwa Waziri wa
Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo. Kutoka kushoto
ni Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia masuala ya Nishati,
Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo, Katibu Mkuu wa Wizara ya
Nishati na Madini, Profesa Justin Ntalikwa, Kamishna Msaidizi
wa Nishati anayeshughulikia Maendeleo ya Nishati, James
Andilile na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini
anayeshughulikia Madini , Profesa James Mdoe.

NewsBulletin
http://www.mem.go.tz

HABARI ZA NISHATI/MADINI

Madini ya shilingi Bilioni 3.2 yaokolewa na TMAA


Na Teresia Mhagama,
Arusha

meelezwa kuwa katika kipindi


cha Julai 2015 hadi Januari 2016,
Wakala wa Ukaguzi wa Madini
Tanzania (TMAA) umewezesha
madini yenye thamani ya shilingi
bilioni 3.2 kukamatwa yakitaka
kutoroshwa nje ya nchi bila kuwa na
vibali katika matukio 16.
Hayo yameelezwa na Mhandisi
Gilay Shamika wakati wa Maonesho
ya Kimataifa ya Vito ya Arusha
yaliyofanyika jijini humo kuanzia
tarehe 19 hadi 21, Aprili mwaka huu.
Mhandisi Shamika alisema kuwa
madini hayo yalikamatwa kufuatia
ukaguzi uliofanyika kupitia madawati
maalum yaliyopo katika Viwanja vya
Ndege vya Mwl.Julius Nyerere (Dar
es Salaam), Kilimanjaro, Mwanza,
Songwe (Mbeya) na Arusha.
Aliongeza kuwa watoroshaji
hao wa madini walikamatwa kwa
ushirikiano wa Jeshi la Polisi, Mamlaka
ya Mapato Tanzania (TRA), Mamlaka

ya Viwanja vya Ndege (TAA), Idara ya


Madini na Usalama wa Taifa.
Mhandisi Shamika alisema kuwa,
ili kudhibiti hali hiyo ya utoroshaji
madini, TMAA imekuwa ikifanya
jitihada mbalimbali ikiwemo kutoa
elimu kwa umma kuhusu sheria na
taratibu za kuingiza na kusafirisha
madini nje ya nchi, kuimarisha
ushirikiano na vyombo vingine vya
Serikali na kuchukua hatua za kisheria
kwa
kuwafikisha
watuhumiwa
mahakamani ambapo hupewa adhabu
ya kulipa faini na madini kutaifishwa.
Aidha Mhandisi Shamika alieleza
kuwa madini hayo yanayotaifishwa
huuzwa katika mnada wa madini
unaofanyika katika Maonesho ya
Kimataifa ya Vito ya Arusha ambapo
katika Maonesho ya Tano ya Vito
yaliyomalizika hivi karibuni, Serikali
ilipata jumla ya shilingi za kitanzania
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA),
Bilioni 1.3.
Mbali na kutoa wito kwa wadau Mhandisi Dominic Rwekaza
wa madini kufuata sheria na kanuni
zinazoongoza Sekta ya Madini nchini, hayo ya Vito kutoa elimu kwa wadau vinavyohitajika katika usafirishaji wa
Mhandisi Shamika alieleza kuwa wa ndani na nje ya nchi kuhusu madini yaliyokuwa yakiuzwa katika
Wakala huo umetumia Maonesho umuhimu wa kuwa na vibali vyote maonesho hayo.

MAONESHO YA 5 YA VITO - ARUSHA


APRILI 19 - 21, 2016

Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Maonesho ya Vito Arusha (AGF),


Peter Pereira (Wa kwanza kushoto) na Mwenyekiti wa Chama cha
Wafanyabiashara wa Madini (TAMIDA), Sammy Mollel wakiwakaribisha
Washiriki wa Maonesho ya Tano ya Kimataifa ya Vito ya Arusha.

Vijana wa Kitanzania
wakiwa wamevaa
madini ya aina
mbalimbali ya Vito
yaliyokatwa na
kunakshiwa nchini
Tanzania.
Madini hayo ya Vito
vilivyonakshiwa
pamoja na ghafi
ikiwemo Tanzanite
yanayopatikana nchini
Tanzania yalikuwa
yakiuzwa wakati wa
Maonesho ya Tano
ya Kimataifa ya Vito
yaliyofanyika Jijini
Arusha kuanzia tarehe
19-21 Aprili, 2016.

10

HABARI ZA NISHATI/MADINI

NewsBulletin
http://www.mem.go.tz

MAKALA

Hivi ndivyo Tanzania


inavyonufaika na
Madini ya Graphite
Mradi huo unaendelezwa na
Kampuni ya Uranex Tanzania
Limited ambayo inamilikiwa
na kuendeshwa na Kampuni
Mama ya Magnis Resources
iliyopo nchini Australia.

Na Veronica Simba

Madini
ya
Graphite
yanatumika kwenye betri za
simu zote ambazo ni smart
phones; kwenye betri za
magari yanayotumia umeme
na pia kutengeneza Penseli ambazo
zamani waliziita za risasi. Ukweli hiyo
siyo risasi bali ni Graphite.
Hivyo ndivyo Kamishna Msaidizi
wa Madini Kanda ya Kusini, Mhandisi
Benjamin Mchwampaka alivyoanza
kunieleza kuhusu maendeleo ya
shughuli za Mradi wa Nachu wa
kuchimba madini ya Graphite, huko
wilayani Ruangwa, Mkoani Lindi.
Mhandisi Mchwampaka anaeleza
kuwa, Mradi huo unaendelezwa
na Kampuni ya Uranex Tanzania

Limited ambayo inamilikiwa na


kuendeshwa na Kampuni Mama
ya Magnis Resources iliyopo nchini
Australia.
Kutokana na umuhimu wa Mradi
husika kwa nchi yetu, kama ilivyo
kwa miradi mingine mbalimbali
nchini, yenye lengo la kuinua uchumi
wa nchi yetu, Makala hii inaangazia
maendeleo ya Mradi huo ikiwemo
kazi iliyofanyika mpaka sasa, manufaa
yanayotarajiwa kwa Taifa pamoja na
changamoto zilizopo.
Maelezo yaliyo katika Makala
hii yanatokana na mazungumzo Madini ya Graphite
niliyofanya
na
Kamishna
Mchwampaka pamoja na Taarifa kunatokana na kubaini kuwa yapo
iliyoandaliwa na Kampuni ya Uranex. mashapo ya kutosha ya madini
Graphite ambayo yanaweza
Mradi wa kuchimba Graphite wa ya
kuchimbwa
kwa faida. Uthibitisho
Nachu
huo
unatokana
shughuli za
Inaelezwa kuwa Serikali ya utafutaji wa madininahusika
Wilayani
Tanzania ni Mbia wa Mradi wa Ruangwa uliofanywa na Kampuni
ya
Nachu unaohusika na kuchimba Uranex tangu mwaka 2013 kwa leseni
madini ya Graphite. Hii inatokana na ya utafutaji Namba PL 9076/2013.
Serikali kumiliki hisa asilimia Tano Baadaye, mwaka 2015, Serikali kupitia
(5). Hata hivyo, inaelezwa kuwa, upo Wizara ya Nishati na Madini, ilitoa
uwezekano wa hisa za Serikali kufikia leseni kubwa ya uchimbaji wa madini
asilimia 15.
yenye Namba SML 550/2015
Kuanzishwa kwa Mradi huo hayo,
kwa ajili ya ujenzi wa Mgodi.
Kazi iliyofanyika
Pamoja na shughuli za utafutaji
wa madini katika Wilaya ya Ruangwa
zilizoanza mwaka 2013, Kampuni
ya Uranex pia imetayarisha taarifa ya
Upembuzi Yakinifu ya awali kuhusu
Mradi.
Mpaka
sasa,
mashapo
yaliyogunduliwa ni takriban tani
milioni 156, ambapo madini ya
graphite yaliyomo kwenye mashapo
hayo yanafikia zaidi ya tani milioni
Nane (8). Aidha, inaelezwa kuwa,
kiwango hicho kipo katika eneo dogo
tu la leseni husika ya utafutaji, hivyo
inamaanisha kuwa mashapo ambayo
hayajagunduliwa ni mengi zaidi ya
kiasi kilizhogunduliwa hadi sasa.
Vilevile, inaelezwa kuwa, kutokana
na ubora wa madini ya Graphite
kutoka mgodi huo, Kampuni ya
SINOMA kutoka China imesaini
mkataba wa kutoa mkopo wa kujenga
mgodi wenye thamani ya Dola za
Kimarekani milioni 150, ambazo
ni sawa na asilimia 90 ya fedha zote
zinazohitajika kuanza uzalishaji.

Kamishna Msaidizi wa Madini Kanda ya Kusini, Mhandisi Benjamin


Mchwampaka

Manufaa yanayotarajiwa
Manufaa kadhaa yanatajwa
kuwa yatapatikana na kuwanufaisha
wananchi wa Wilaya ya Ruangwa na
Taifa zima kwa ujumla, kutokana na
Mradi wa Nachu wa kuchimba madini
ya Graphite. Baadhi ya manufaa
yanayoelezwa kuwa yataletwa na
Mradi huo ni ajira kwa Watanzania,
malipo ya kodi na manufaa mengine
yanayotokana na kuongezeka kwa

shughuli za kiuchumi.
Kwa mujibu wa taarifa ya Uranex,
Kampuni hiyo imeandaa mpango wa
Ajira na Mafunzo kwa Watanzania
ambapo kipaumbele kitakuwa ni ajira
kwa Watanzania wenye sifa kwanza
kabla ya kuajiri wataalam kutoka
nje. Watanzania wengi zaidi ya 800
wataajiriwa wakati wa ujenzi wa
mgodi, lakini idadi itapungua hadi
kufikia wastani wa 360 wakati wa
uzalishaji.
Aidha, inatarajiwa kuwa mradi
wa kuchimba Graphite utakapoanza,
utakuwa ndiyo Mgodi mkubwa wa
kuzalisha madini hayo duniani. Kwa
sasa Mgodi mkubwa wa Graphite uko
China na unazalisha tani 150,000 za
Graphite kwa mwaka.
Vilevile,
imeelezwa
kuwa,
Kampuni haijaweka msamaha wa
kodi wa aina yoyote, hivyo kodi
zote zinazostahili kulipwa zitalipwa.
Uzalishaji unatarajiwa kufikia kiwango
cha tani 250,000 baada ya mwaka wa
pili wa kuanza uzalishaji.
Pia, imeelezwa kuwa Mgodi
umepanga
kununua
bidhaa
zipatikanazo hapa nchini na kama
zitakosekana ndipo zitaagizwa nje.
Aidha, huduma nyingi zitakazohitajika
mgodini zitatolewa na Kampuni za
hapa nchini.
Fidia kwa watakaopitiwa na Mradi
Kwa mujibu wa Kamishna
Mchwampaka, hatua iliyofikiwa
kwa sasa ni uthamini wa mali za
watu ambao wanatakiwa kupisha
eneo ambapo mgodi utafunguliwa
na tayari kazi ya uthamini kwa mali
yaani mazao, nyumba na ardhi tupu
lilikamilika mwishoni mwa mwezi
Februari, 2016 na hatua itakayofuata
ni kuanza kuwalipa wahusika kwa
mujibu wa taratibu za nchi.
Ni jambo la fahari kwa Watanzania
kuwa na wingi wa rasilimali za madini
ya aina mbalimbali. Ili madini ya
Graphite yalinufaishe Taifa ipasavyo,
wananchi wa Ruangwa hawana budi
kutoa ushirikiano pale inapotakiwa
pamoja na kuchangamkia fursa
mbalimbali zinakuja sambamba na
uwekezaji huo.

NewsBulletin
http://www.mem.go.tz

HABARI ZA NISHATI/MADINI

11

TEITI yazindua ripoti ya 5 na 6 ya Mapato ya Serikali

n Mapato ya Madini, Mafuta,


Gesi Asilia yaongezeka
Zuena Msuya na
Godwin Masabala DSM

pango wa Uhamasishaji
Uwazi katika mapato
ya madini, gesi asilia
na mafuta( TEITI)
umezindua ripoti ya 5
na 6 ya Mapato ya Serikali kwa mwaka
2012/2013 na 2013/2014 kutoka katika
uchimbaji wa madini,mafuta na gesi
asilia.
Akizindua Ripoti hiyo jijini Dar
es salaam, aliyekuwa Mkaguzi Mkuu
na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali,
Ludovock Utouh pamoja na mambo
mengine alisema ripoti ya TEITI
imeongeza uwazi wa mapato ya Serikali
yatokanayo na Madini, Mafuta pamoja
na Gesi Asilia.
Alisema Ripoti hiyo itawarahisishia
wananchi kufahamu matumizi na
mapato yatokanayo na rasilimali hizo na
kuondoa dhana iliyojengeka kwa jamii
juu ya upotevu wa mapato yatokanayo
na madini, mafuta na gesi asilia katika
shughuli za utafutaji na uchimbaji wa
madini,mafuta na gesi asilia nchini.
Alifafanua kuwa, matokeo ya Ripoti
ya Tano ya TEITI mwaka 2012/2013
imeonesha kuwa Serikali ilipata mapato
ya shilingi bilioni 956 kutokana na
kampuni 46 za madini na kampuni 19
za mafuta na gesi asilia.
Aidha, matokeo ya ripoti ya ya Sita
TEITI ya mwaka 2013/2014 imeonesha
kuwa Serikali imepata mapato ya shilingi
bilioni 1,221 kutokana na kampuni 38 za
madini na kampuni 21 za mafuta na gesi
asilia katika shughuli za uchimbaji na
utafutaji wa mafuta na gesi asilia nchini.
Alisisitiza kuwa baada ya kuundwa

kwa taasisi hiyo, hivi sasa taarifa sahihi


za malipo na mapato ya Serikali
inayopokea kutoka katika makampuni
ya tasnia ya uziduaji inafahamika wazi.
Aidha, Utouh aliishauri TEITI
kuongeza kasi katika ufanisi wa kazi
zake ili kila mtanzania aweze kupata
taarifa za mapato ya Serikali kuhusu
uchimbaji wa madini, mafuta na gesi
asilia na kuondoa maswali yaliyojengeka
miongoni mwa jamii.
Sambamba na hilo alivitaka vyombo
vya habari kuchambua kwa kina ripoti
na kutoa taarifa sahihi kwa wananchi
ili waweze kuelewa kwa undani
kinachofanywa na Serikali katika sekta
ya madini,mafuta na gesi asilia.
Kwa upande wake, Mwenyekiti
wa Kamati ya TEITI, Jaji Mark
Bomani ambaye anamaliza muda
wake, alisema kuwa kwa mujibu wa
ripoti hizo mbili mapato ya Serikali
kutokana na uchimbaji pamoja na
utafutaji wa madini, mafuta na gesi asilia
yameongezeka kutoka shilingi ya zaidi
ya shilingi bilioni mia moja na ishirini
hadi kufikia zaidi ya shilingi bilioni elfu
moja na mia mbili na ishirini ongezeko
la takribani mara kumi ya makusanyo.
Hata hivyo, ameshauri kuwa masuala
ya mauzo ya asilimia 60 ya kampuni za
madini na kwenye mikataba maalum
yazidi kufikiriwa zaidi ili kuongeza
mapato kwa kuzingatia kuwa ni asilimia
20 tu ya madini yaliyogunduliwa nchini
ndio yanayochimbwa hadi leo huku
asilimia 80 zikiwa bado hazijaguswa
kabisa.
Vilevile, aliongeza kuwa bado Sekta
ya Madini inakabiliwa na changamoto
nyingi ikiwamo kutanua wigo wa
wachimbaji madini wa kati ili na wao

Akiyekuwa Mkaguzi Mkuu na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali Ludovick


Utouh (wa pili kulia) akikata utepe, ikiwa ni uzinduzi wa Ripoti za TEITI
ya Mapato ya Serikali yatokanayo na Utafutaji na Uchimbaji wa Mafuta
Gesi na Madini ya mwaka 2012/2013 na 2013/2014. Wa pili kushoto
ni Mwenyekiti wa kamati ya TEITI anayemaliza muda wake, Jaji Mark
Bomani na Katibu Mtendaji wa TEITI Mhandisi Benedick Mushingwe (wa
kwanza kulia)

wachangie katika pato la Serikali kwani


mpaka sasa kampuni kubwa pekee ndio
zimekuwa zikihusika.
Jaji Mark Bomani alitumia uzinduzi
wa ripoti hizo kuwaaga rasmi wajumbe
wa Kamati Elekelezi ya TEITI

iliyoundwa mwaka 2008 iliyopewa


jukumu la kuingalia Sekta ya Madini,
Mafuta na Gesi Asilia kwa undani na
kutoa mapendekezo ya kuiboresha
baada ya kutumikia nafasi ya Uenyekiti
kwa miaka 7.

Mwenyekiti wa kamati ya TEITI anayemaliza muda wake, Jaji Mark


Bomani (kushoto) na aliyekuwa Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za
Serikali, Ludovick Utouh (kulia) wakizungumza wakati wa uzinduzi
wa ripoti ya TEITI ya mapato ya Serikali yatokanayo na uchimbaji na
utafutaji wa Mafuta na Gesi Asilia.

Baadhi ya washiriki wakifuatilia uzinduzi wa ripoti ya TEITI ya mapato ya


Serikali yatokanayo na Utafutaji na Uchimbaji wa Madini, Mafuta na gesi
Asilia za mwaka 2012-2014 uliofanyika jijini Dar es salaam.

Katibu Mtendaji wa TEITI, Mhandisi Benedict Mushingwe (kushoto) na


baadhi ya watendaji wa TEITI (kulia) wakifuatilia taarifa ya Uzinduzi wa
Ripoti za TEITI za mapato ya Serikali kutokana na Uchimbaji na Utafutaji
wa Madini, Mafuta na Gesi Asilia kuanzia 2012-2014.

12

HABARI ZA NISHATI/MADINI

NewsBulletin
http://www.mem.go.tz

Urusi yaalikwa kuwekeza kwenye umeme


Na Greyson Mwase,
Dar es Salaam

African Forum, 2016.


Masuala yaliyojadiliwa katika
jukwaa hilo kwa siku mbili ni pamoja
na Miundombinu, Kilimo, fursa
meelezwa kuwa Tanzania ina
za uwekezaji na Nishati. Katika
vyanzo mbalimbali vya kutosha Jukwaa linalojadili Sekta ya Nishati
kwa ajili ya kuzalisha umeme wa wataalam na wawekezaji katika nchi
uhakika utakaochangia katika
za Tanzania na Urusi walipata fursa
ukuaji wa uchumi wa nchi.
ya kubadilishana uzoefu wa jinsi ya
Hayo yalielezwa na Kamishna
kuboresha sekta ya nishati.
Msaidizi wa Nishati anayeshughulikia
Akizungumza katika jukwaa
Nishati Mbadala Mhandisi
hilo kwa niaba ya Naibu Katibu
Edward Ishengoma katika jukwaa
Mkuu wa Wizara ya Nishati na
linalokutanisha wataalam na
Madini anayeshughulikia Nishati
wawekezaji kutoka Urusi na
Mhandisi Juliana Pallangyo,
Tanzania lijulikanalo kama Russian- Kamishna Msaidizi wa Nishati

Wajumbe wa jukwaa linalowakutanisha wataalam kutoka Tanzania


na Urusi lijulikanalo kama Russian African Forum 2016 wakifuatilia
hotuba iliyokuwa inatolewa na Waziri wa Viwanda na Biashara wa
Urusi, Denis Manturov (hayupo pichani).

Wajumbe wa jukwaa kwa ajili ya kujadili Sekta za Nishati na Madini


kati ya nchi ya Tanzania na Urusi wakiendelea na majadiliano katika
mkutano ujulikanao kama Russian-African Forum 2016 uliofanyika
jijini Dar es Salaam hivi karibuni.

Waziri wa Viwanda na Biashara kutoka Urusi, Denis Manturov


akisoma hotuba ya ufunguzi wa jukwaa linalowakutanisha wataalam
kutoka Tanzania na Urusi lijulikanalo kama Russian African Forum
2016 lililofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.

Kamishna Msaidizi wa Nishati anayeshughulikia Nishati Mbadala,


Mhandisi Edward Ishengoma kutoka Wizara ya Nishati na Madini,
akifafanua jambo katika jukwaa hilo.

anayeshughulikia Nishati Mbadala,


Mhandisi Edward Ishengoma
alisema kuwa Tanzania ina vyanzo
vya kutosha kwa ajili ya uzalishaji
wa umeme na hivyo inawaalika
wawekezaji kutoka Urusi wenye
uwezo katika uwekezaji huo ili
kuwezesha Tanzania kupata umeme
wa uhakika.
Alifafanua kuwa Tanzania ina
vyanzo mbalimbali vya umeme
kama vile Makaa ya Mawe, Upepo,
Umeme Jua, Jotoardhi, Gesi na
Maji na kuyataka makampuni yenye
uwezo kwenye uzalishaji wa umeme
kujitokeza na kuwekeza.
Alisisitiza kuwa vyanzo hivi
vinahitaji kuendelezwa ili kuhakikisha
mpango wa kuzalisha umeme

wa kutosha kwa ajili ya matumizi


ya majumbani na viwandani
unafanikiwa.
Tanzania ina mpango wa
kuwekeza kwenye viwanda,
kwa kutambua umuhimu
wa nishati katika viwanda,
tunakaribisha wawekezaji wenye
uzoefu ili kuzalisha umeme
utakaokidhi mahitaji ya viwanda
vitakavyochangia katika ukuaji wa
uchumi wa nchi kupitia ajira na
kuuza bidhaa nyingine nje ya nchi,
alisisitiza Mhandisi Ishengoma.
Urusi ni nchi inayoongoza
duniani kwa uuzaji wa gesi nje ya
nchi huku ikiwa ni nchi ya nne katika
uzalishaji wa umeme duniani baada
ya Marekani, China na Japan.

Вам также может понравиться