Академический Документы
Профессиональный Документы
Культура Документы
com
Sauti ya Waislamu
ISSN 0856 - 3861 Na. 1227 RAJAB 1437, IJUMAA , APRILI 29-MEI 5, 2016 BEI TShs 800/=, Kshs 50/=
Asilimu akibatiza
Katimba hatunaye
IDDI Katimba ni katika
wanaharakati walioshiriki
semina ya kuratibu harakati
za maendeleo ya Waislamu
nchini iliyoandaliwa na
Islamic Propagation Centre
(IPC) Januari 12-18, 1991,
jijini Dar es Salaam.
Hiyo ilikuwa ndiyo
semina iliyozalisha chachu
ya kuratibu harakati
zilizochangia kuanzishwa
shule za Kiislaamu nchini.
Ni semina hiyo pia
iliyopitisha azimio la
kuanzishwa gazeti hili la
Kiislaamu la AN-NUUR.
Kwa taufiki ya Allah
(S.W), gazeti lilifanikiwa
kusajiliwa na kuanza kutoka
rasmi mnamo mwezi Agosti,
1991 pamoja na shule ya
sekondari ya Kiislaamu ya
Ubungo ambayo ilianza
rasmi mnamo Januari, 1992.
(Soma Uk. 9)
Mafia Style:
Baada ya urafiki
msiba juu ya msiba
Soma Uk. 10
ANNUUR NEW.indd 1
4/27/2016 12:27:41 PM
Fethullah-Gulen
(ALIPOWAPA mtoto
mwema walimfanyia
washirika katika kile
alichowapa ametukuka
Mwenyezi Mungu na yale
wanayomshirikisha nayo.
[AL-AARAAF 189-190]
Kuna hakika ambayo
imethibiti nayo ni
kwamba baadhi ya
waumini wanaingia mara
nyingi katika duara ya
kumshirikisha Mwenyezi
Mungu. Je, kutokuwa
kurejea huko ni kwa mkato
wa watu wa Shirki. Na
kama inavyoweka wazi
aya hii tukufu, kwa hakika
mapenzi ambayo yamevuka
mpaka kwa watoto, ni njia
katika njia za kumshirikisha
Mwenyezi Mungu kwani
badala ya kuwaangalia
watoto wetu na wajukuu
wetu kwamba wao ni neema
na msaada na amana kutoka
kwa Mwenyezi Mungu
iliyowekwa katika shingo
zetu; tunawaangalia kana
kwamba sisi tunawamiliki.
Bali baadhi ya watu
wanaacha swala na ibada
kwa sababu yao kana
kwamba mapenzi yao kwa
watoto, ni zaidi kuliko
mapenzi yao kwa Mwenyezi
Mungu mtukufu. Badala ya
kuwapenda kwetu watoto
kwa ajili ya Mwenyezi
Mungu, tunawapenda
watoto pasi na kumfikiria
Mwenyezi Mungu
Iwapo msemo huu
unafaa, na tunahisi
kiwango cha mahusiano na
hisia na mapenzi ambayo
yanapelekea kwenye daraja
la shirki ya ujumla pasi na
kukusudia; kwa sababu
hiyo kunapasa kutenda
kufuatana na kanuni hii:
Moyo mmoja haukunjuki
mapenzi mawili na tuwe
juu ya maandalizi wakati
wote dhidi ya kushirikisha
kitabia. Hakika jambo hili
ni jepesi sana kwa upande
wa kusema na kwa upande
wa kiasi cha kusema tu,
isipokuwa utekelezaji wake
katika maisha ni mgumu
sana kuliko inavyoonekana.
Pamoja na hayo, kunapasa
kufanya yale yote yaliyo
katika uwezo wetu, ili
ANNUUR NEW.indd 2
AN-NUUR
kujisafisha na kushirkisha
na kutoa kila juhudi kwa
ajili ya kutokaribia katika
sehemu ambazo inanuswa
kwa umbali kutoka sehemu
hizo harufu ya kushirikisha.
Tutakapofanya hivi,
yanakuja maombi ya Mtume
(s.a.w.) kama kielelezo
muhimu na cha lazima:
Ee Mola wangu wa haki,
hakika mimi ninajikinga
kwako na kushirikisha na
wewe kitu chochote na hali
ya kuwa mimi ninajuwa na
ninaomba msamaha kwako
kwa lile ambalo silijuwi.
Kunawezekana
kuyaangalia maudhui ya
kuwapenda watoto kwa
mitizamo tofauti: Huenda
mtu asipatilizwe katika
masuala ya hisia. Isipokuwa
yeye analazimishwa
kwa upande wa dini,
kuzirekebisha (kuzidhibiti)
hisia zake za kimaumbile
kwa mfano huenda akawa
mmoja wao ni mroho katika
kula na katika kunywa
na huenda akatamani
kuishi maisha ya juu, na
anaonyesha matakwa na
pupa kubwa katika jambo
hili, kwa hiyo anafanya
mambo pasi na kufanya
hesabu yoyote ya mwisho
wa mwenendo huu. Kwa
sababu binadamu kwa
maumbile yake ameumbwa
hali yakuwa ni dhaifu mbele
ya matakwa yake na bakhili
na mwenye haraka. Mambo
haya yanapatikana katika
maumbile yake. Kama
ambavyo yeye anabeba
katika mbavu zake pamoja
na hisia za mfundo na
chuki na uadui, anabeba
pia hisia za kibinadamu.
Hii kumekuwa ni juu yake
kusimama na kuyaziba
madirisha na milango
iliyo na mambo haya
katika nafasi ya njia mbili,
inazopelekea kwenye shari
na kwenye kheri. Kwa
sababu hiyo, kumekuwa
ni juu yake kusimama na
kuyaziba madirisha na
milango iliyofunguliwa
katika uhakika wake juu
ya shari na kukiunda
juu ya hisia zake na kwa
fikra za hisia zake zaidi.
Kufanya hivi, ndiko
tunakokuita kwa msemo
wa kidini, Kuchuma
maumbile ya pili ili afikie
kwenye ukamilifu ambao
umekadiriwa kwake.
Maana kwamba afanye
kutokana na maumbile
yake ambayo anayafungulia
mlango juu ya kila kitu
ayafanyie mlango mmoja
tu wenye kupelekea kwa
Mwenyezi Mungu mtukufu
na kuimarisha uhusiano
wake na Mwenyezi Mungu
mtukufu.
Kuwapenda watoto kwa
namna hii, huko ndiko
Weka duara kwenye jawabu ilio sawa. Jawabu kamili wiki ijayo.
M
3:154
40
41
42
na Q
43
na S
na N
44
45
na W I
JK B
46
47
H na
48
94:5-6 U
W W 25
55
AN R
W Z
40:68
MASUALA
1.
Sura ipi na aya ya ngapi isemayo Kisha baada ya dhiki
alikuteremshieni utulivu - usingizi ambao ulifunika kundi moja
kati yenu. Na kundi jengine nafsi zao ziliwashughulisha hata
wakamdhania Mwenyezi Mungu dhana isiyo kuwa ya haki,
dhana ya kijinga. Wakisema: Hivyo tuna lolote sisi katika jambo
hili? Sema: Mambo yote ni ya Mwenyezi Mungu. Wanaficha
katika nafsi zao wasiyo kubainishia. Wanasema: Lau ingelikuwa
tuna lolote katika jambo hili tusinge uliwa hapa. Sema: Hata
mngeli kuwa majumbani mwenu, basi wangelitoka walio
andikiwa kufa, wakenda mahali pao pa kuangukia wafe.(Haya ni
hivyo) ili Mwenyezi Mungu ayajaribu yaliyomo vifuani mwenu,
na asafishe yaliyomo nyoyoni mwenu. Na Mwenyezi Mungu
anayajua yaliyomo vifuani.
2. Sura ipi aya hii imerejewa mara 34 Basi ni ipi katika neema
za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha.
3. Zitaje Sura neno Hamim ndio inaanzia.
4. Mitume mingapi wametajwa kwa majina yao katika Quran?
5. Mti gani ambao ni mchungu wenye miiba watu wa motoni
ndio kitakuwa chakula chao?
6. Mtume yupi alikuwa na wajihi wa kupendeza na kuwatia
kiwewe wanawake?
7. Mtume yupi aliiona Nuru ya Mwenye-enz-Mungu?
8. Taja Baba na watoto wakiwa ni Mitume?
9. Allah akitaka jambo liwe huwa? Itaje Sura na Aya.
10. Sura ipi na aya ya ngapi Mwenye-enzi-Mungu
anamhakikishia Mtume (SAW) baada ya dhiki ni faraji?
(Tunaomba radhi kwa makosa yaliotokea wiki iliopita katika
kupangilia kazi hii ya Chemsha Bongo)
Jee Unajua?
4/27/2016 12:27:43 PM
Habari
Na Shabani Kihara
ANNUUR NEW.indd 3
Asilimu akibatiza
AN-NUUR
4/27/2016 12:27:47 PM
Tahariri/Makala
AN-NUUR
ANNUUR NEW.indd 4
AN-NUUR
Na Dk. Mahmud
Hassan Mahmud
SHUKURANI
zote anastahiki
Mwenyezi Mungu
na ninashuhudia
kwamba, hakuna
apasaye kuabudiwa
kwa haki isipokuwa
Mwenyezi Mungu, na
ninashuhudia kwamba
Mtume Muhamad ni
Mjumbe wake.
Mwenyezi Mungu
amekataza kutoa
maana ya maneno
yake bila ya ujuzi wala
elimu. Atakayelifanya
hilo, huyo ana
dhambi kubwa bali
amemuweka kwenye
daraja la juu amesema
Mwenyezi Mungu
mtukufu sema kwa
hakika amekataza
Mola wangu mlezi
mambo machafu,
yale ya wazi na yale
ya siri na madhambi
na ujeuri bila ya haki
na kumshirikisha
Mwenyezi Mungu.
Yule asiyeteremsha
dalili na aya ya
Mwenyezi Mungu
katika mambo
ambayo hamyajui,
akapangilia vitu vya
haram, daraja nne
zinamsubiri. Atalianza
lililo jepesi, nalo ni
mambo machafu,
kisha likafuata lililo
kubwa kwa lile jepesi,
nalo ni la madhambi
na dhulma, kisha la
tatu ni zito kuliko
hayo mawili, nalo
ni kumshirikisha
Mwenyezi Mungu,
la nne ambalo ni zito
zaidi ya yote hayo, nalo
ni kuyasema mambo
ya Mwenyezi Mungu
bila ya elimu. Nako
ni kumsemea mambo
yake Mwenyezi Mungu
bila ya elimu katika
majina yake.
Amesema Allah
(S.w) Wala msiseme
kwa yale yanayosifu
mnamzulia. Basi
vya halali ni vile
alivyovihalalisha
Mwenyezi Mungu
na Mtume wake na
vya haram ni vile
alivyoharamisha
Mwenyezi Mungu na
Mtume wake.
Toka kwa Amr Bin
Shuaib, toka kwa
baba yake, toka kwa
babu yake amesema,
amesikia Mtume (saw)
watu wakibishana kwa
Quran, akasema Kwa
hakika wameangamia
wale waliopita
kabla yenu kwa hili,
wakipigana kwa
kitabu cha Mwenyezi
Mungu wao kwa wao.
Bali kimeteremshwa
kitabu cha Mwenyezi
Mungu, ili wasadikishe
baadhi yao na
baadhi, na wala sio
wakanushane baadhi
yao na baadhi, basi yale
muyajuayo yasemeni
na yale msiyoyajua
basi yapelekeni kwa
wanaoyajua.
Basi amri kwa
wasiojua jambo katika
kitabu cha Mwenyezi
Mungu, yampasa
apeleke kwa anayejua
kwa kuyaegemeza
kwa wanazuoni na
wala usilazimishe
neno usilolijua, ni
bora ukalipeleka kwa
anayejua.
Amesema Mtume
(s.a.w) ni mbingu
gani itakayonifunika
mimi na ardhi gani
inanihifadhi mimi,
ikiwa nitasema kwa lile
nisilolijua.
Na amepokea Ayubu
toka kwa Ubaya
Malikat, amesema
Ni ardhi gani
itanihifadhi na mbingu
gani itanifunika na
nitakwenda wapi na
nitafanya nini, pale
nitakaposema katika
kitabu cha Mwenyezi
Mungu kwa mambo
ambayo hayakutakiwa
na Mwenyezi Mungu.
Na imesihi toka
kwa Bin Masudi na
Ibnu Abbas, Yeyote
mwenye kufutu
(kujibu) katika kila
wanayo muuliza, huyo
ni mwendazimu.
Email : eg_islamic_
center39@yahoo.com
4/27/2016 12:27:49 PM
5
Banki ya Kiislamu ya Dubai
kufunguliwa Kenya
BENKI kubwa ya Kiislamu nchini
Falme za Kiarabu imetangaza
kufungua tawi lake nchini Kenya
kabla ya mwisho wa mwaka 2016.
Benki hiyo ya Dubai itakuwa
benki ya tatu ya Kiislamu
kuendesha huduma kwa mujibu wa
Shariah nchini Kenya.
Licha ya mamlaka ya benki za
Kenya kutoa leseni mpya kwa
benki na kusababisha kufungwa
kwa baadhi ya benki muhimu
nchini humo, Benki ya Kiislamu ya
Dubai inasubiri uamuzi wa mwisho
kutoka Benki Kuu ya Kenya ili
kuanzisha rasmi utoaji wa huduma
zake nchini humo.
Hivi karibuni Mwanasheria
Mkuu wa serikali ya Kenya,
Profesa Githu Muigai, alisema
serikali ya Kenya itaweka sheria
itakayosimamia taasisi za fedha
za Kiislamu kabla ya mwisho wa
mwaka huu.
Profesa Muigai aliliambia
Baraza la Kiislamu la Kenya
mjini Nairobi, kuwa serikali
inawasiliana na wadau mbalimbali
ili kuandaa rasimu ya sheria hiyo.
Alisema rasimu hiyo inatarajiwa
kuwasilishwa bungeni katika miezi
michache ijayo ili iweze kuwa sheria
mwishoni mwa mwaka huu.
Bw Muigai alisema pamoja na
kuwa mwaka 2008 Kenya iliweka
msingi wa kisheria kuruhusu
benki za Kiislamu kufanya kazi,
bado mabadiliko zaidi yanatakiwa
kufanyika ili benki hizo ziweze
kufanya kazi kwa ufanisi zaidi.
Tangu wakati huo benki kadha
za Kiislamu zilianza kutoa huduma
nchini Kenya na benki nyingine za
kawaida zilianza kutoa huduma
zinazotolewa na Benki za Kiislam.
Kuingia katika soko mabenki
ya Gulf African Bank na First
Community Bank kunatarajiwa
kuanzishwa kwa mara ya kwanza
mfumo kamili wa kibenki wa Sheria
kwa silimia 100.
Kuanzishwa kwa mfumo kamili
wa kibenki kwa mujibu wa sharia
kulikuwa kunasubiriwa kwa hamu
kubwa na jamii ya Kiislamu, hasa
ikizingatiwa kuwa miaka miwili
iliyopita kulizinduliwa madirisha
ya huduma za kibenki kwa taratibu
za Kiislamu katika benki kadhaa za
kawaida.
Benki za Barclays Bank (Kenya)
Limited na Kenya Commercial Bank
Limited zimekuwa zikitoa huduma
hizo za kibenki kwa mujibu wa
sheria kupitia dirisha hilo, huduma
ikiitwa, "LARIBA Banking".
Kumekuwa na ongezeko la benki
za Kiislamu katika nchi mbalimbali
duniani, hususani katika
ulimwengu wa Waislamu.
Mtaalamu wa masuala ya
fedha katika mfumo wa fedha
wa Kiislamu Bw. Mohaimin
Chowdhury anaifafanua kuwa
Waislamu husema kuwa Uislamu ni
mfumo kamili wa maisha, na si dini
ya imani tu ya kiroho.
Kwa hali hiyo, vipengele vyote
vya maisha ya mwanadamu
lazima viendane ni misingi ya
Uislamu. Hii ina maana kuwa,
mbali ya kufuata faradhi za ibada
zilizoagizwa kama vile kuswali
Swala tano, kutoa Zaka, kufunga
Mwezi wa Ramadhani na kwenda
Hija, Muislamu pia hana budi
kufuata misingi ambayo Uislamu
umeiweka, kuhusiana na mambo
mengine katika maisha ya kijamii
kwa mfano, mahusiano yake na
wengine kifamilia na kijamii, na
masuala ya kifedha.
ANNUUR NEW.indd 5
HABARI ZA KIMATAIFA
AN-NUUR
Askofu alalamikia
Obama ageuka sasa anapinga mapinduzi Syria maudhi ya ngono
kwa watoto
4/27/2016 12:27:51 PM
AN-NUUR
ANNUUR NEW.indd 6
4/27/2016 12:27:59 PM
Hoja ya Visram
AN-NUUR
Na Nizar Visram
TAREHE 5 Aprili mwaka
huu bunge la Afrika Kusini
(AK) lilijadili na kuipigia
kura hoja ya kutokuwa na
imani na Rais Jacob Zuma
wa nchi hiyo. Kwa vile
wabunge wengi ni kutoka
chama tawala cha ANC,
matokeo yake wabunge
233 waliipinga hoja na
143 waliunga mkono.
Matokeo yake ni kuwa
hoja ilishindwa na Zuma
akasalimika. Kwa mujibu
wa katiba ya AK hoja hiyo
ilihitaji theluthi mbili ya
kura ili kumfanya Zuma
ajiuzulu.
Wakati wa kuwasilisha
hoja bungeni, kiongozi wa
upinzani, Mmusi Maimane
kutoka chama cha Democratic
Alliance (DP) alisema Zuma
anakiaibisha chama chake
cha ANC kilichoongoza
vita vya ukombozi chini
ya viongozi mashuhuri
kama Oliver Tambo, Albert
Luthuli, Walter Sisulu,
Nelson Mandela na Ahmed
Mohammed Kathrada.
Maimane akasema kati ya
vigogo hao ni Kathrada
peke yake aliyebaki, naye
amemtaka Zuma ajiuzulu.
Hii peke yake ingemfanya
Zuma aone aibu na aachie
madaraka, alisema Maimane.
Zuma amebaki madarakani,
lakini utawala wake
umeathirika sana kutokana
na kashfa iliyopelekea bunge
lijadili hoja ya kumtimua
(impeachment).
Hoja hii iliwasilishwa
bungeni baada ya mahakama
ya katiba ya AK kutoa
hukumu kuwa Zuma ana
hatia ya kukiuka katiba kwa
kutumia vibaya fedha za
umma katika kujenga makazi
yake binafsi yaliyo katika
kijiji cha Nkandla. Mahakama
hiyo pia imemuona amevunja
katiba kwa kukataa kurejesha
fedha hizo, akidai kuwa
ujenzi huo ulikuwa ni kwa
lengo la kuimarisha usalama
wake kama rais.
ANNUUR NEW.indd 7
4/27/2016 12:28:02 PM
Kalamu ya Ghassani
AN-NUUR
Na Mohammed Ghassani
NIMETUMIWA ujumbe katika
simu ya mkononi usemao: you
can not eat your cake and have
it, soma e-mail. Nilipofungua
akaunti yangu ya barua-pepe,
nikakuta ufafanuzi wa ujumbe
huo. Kumbe nilikuwa nasutwa
kwa kuandika makala iliyopita
katika safu hii.
Nikumbushe kuwa katika
makala hiyo, nilikuwa nimempa
heshima yake mkereketwa wa
Chama Cha Mapinduzi (CCM)
hapa Zanzibar, Mohammed Raza
Dharamsi, kwa uthubutu wake
wa kuitetea Zanzibar dhidi ya
ukandamizwaji inayofanyiwa
kwa jina la Muungano.
Nimesutwa kwamba nilikwenda
mbali mno katika kuipa maana
hatua ile ya Raza. Kwamba
aidha nilikuwa ninamkuza sana
asivyostahili au nimepotosha
kile hasa alichokikusudia.
Nimehojiwa pia kwamba
nahalalisha bendera ya Zanzibar
hali nikijuwa vyema kwamba
kuwepo kwake ni hatari kwa
Muungano.
Nikaambiwa kuwa mimi na
Raza hatuwezi kuizungumzia
Zanzibar kama nchi baki, huku
tukijuwa kuwa ilijiingiza kwa
hiari yake kwenye Muungano.
Kwamba hatuwezi kuzungumzia
Zanzibar yenye nguvu zaidi au
kwa maneno yake Zanzibar
iliyo Zanzibar zaidi ya hivi
ilivyo sasa halafu wakati
huo huo tukasema tu waumini
wa Muungano. Huko, mbali ya
kuwa ni kwenda kinyume na
katiba, bali pia ni utoto wa kuila
keki yetu, kisha tukataka tubakie
nayo!
Ukweli ni kuwa makala hiyo
inayozungumziwa haikuwa
imejikita hasa katika bendera
ya Zanzibar wala kuonesha
upinzani kwa Muungano.
Nilichojaribu kufanya ni
kuonesha mshikamano wangu
na Mzanzibari mwenzangu
kwa ajili ya Watani wetu,
Mama yetu Zanzibar. Lakini
nachukulia ujumbe ule kama
njia ya kunifanya niseme zaidi
kuhusu kizungumkuti hiki cha
uhusiano wa Tanganyika na
Zanzibar kupitia Muungano
tulionao. Nami hakuna jambo
nisilolionea haya kulisema kama
hilo. Sijawahi kujihisi vibaya
kujitambulisha kwa Uzanzibari
wangu popote pale na, kwa
hivyo, sioni tabu kuutetea dhidi
ya chochote na yeyote. Basi,
ikiwa aliyenitumia ujumbe
ANNUUR NEW.indd 8
panapohusika mambo ya
Muungano. Kwa hivyo, hata lile
agizo lililokuwemo katika Katiba
ya Muda kwamba Tanganyika and
Zanzibar are one United Sovereign
State likabadilika na sasa ikawa
Tanzania is one State and is a
Sovereign United Republic,
ambayo ndiyo iliyomo hadi
sasa, na ndiyo inayotajwa na
hao wanaodai kuwa Zanzibar
kuwa na bendera yake ni
kuvunja katiba. Kumbe tamko
hili lenyewe liko kinyume na
misingi ya Muungano, ambayo
ni sehemu muhimu ya katiba
yenyewe.
Kuanza hapo haikuwa tena
ajabu wala aibu kwa vikao
vya chama na serikali kukaa
Chimwaga kwa jina la Tanzania,
kupitisha maamuzi yoyote
wanayoyapendelea wakubwa wa
Tanganyika, bila ya kuzingatia
upande wa pili wa Muungano.
Lakini ikawa ni dhambi kubwa
kwa Wazanzibari kukaa na
kuizungumzia khatima ya
nchi yao ndani ya Muungano.
Hata viongozi waliowekwa
au kutumwa na Wazanzibari
wenyewe walipothubutu
kufanya jambo ambalo
lingelimaanisha kuitutumua
Zanzibar, basi kifimbo cha
Mwalimu Nyerere kiliwachapa.
Hicho ndicho kifimbo
kilichowachapa akina Aboud
Jumbe, Maalim Seif Sharif na
Salmin Amour.
Hizi ndizo siasa za Muungano
huu, za mkubwa kummeza
mdogo, za mbinu na hila na
vituko na vitimbi. Mambo
haya, bila ya shaka, ndiyo
ambayo yamekuwa yakiwatia
khofu Wazanzibari kuhusiana
na khatima ya nchi yao katika
Muungano. Kuna kauli maarufu
sana ya kumezwa kwa Zanzibar
na kufutwa kabisa. Inasemwa
kuwa hii ndiyo sera ya siri
ya CCM, ingawa wenyewe
wanalikanusha hilo. Lakini
mtiririko kama huo wa matukio
Inaendelea Uk. 14
4/27/2016 12:28:04 PM
9
Na Abuu Nyamkomogi
JUMAMOSI ya tarehe
16.04.2016 nikiwa mkoani
Kagera nilipokea katika simu
yangu ya mkononi ujumbe
mfupi wa maandishi mara
baada ya swala ya alfajiri,
kutoka kwa aliyewahi kuwa
Mudiir wa muda mrefu katika
Kituo cha Kiislamu cha Kulelea
Mayatima (IYF) kilichopo
wilayani Ilemela jijini Mwanza,
Sheikh Nasib Issa, uliosomeka
hivi:
Innaalillaah wainnaa ilayh
rajiuun. IDD MUSSA KATIMBA
amefariki dunia usiku huu
mazishi ni kesho Mabatini,
Mwanza.''
Huo ulikuwa ni ujumbe wa
kwanza kabisa, kati ya jumbe
kadhaa nilizotumiwa kwa
siku hiyo, kunitaarifu kuhusu
msiba wa mmojawapo wa
wanaharakati wa Kiislaamu
wa muda mrefu katika jiji
la Mwanza. Mara baada ya
kupokea ujumbe huo na
kuuhakiki, sikuwa na namna ya
kufanya kwa muda huo zaidi ya
kusema:
Innaa lillaahi wainnaa
ilayhi raajiuun. Kisha nami
nikaanza kuwataarifu, baadhi
ya Waislamu wanaomfahamu
marehemu, kwa kadri
nilivyojaliwa. Hata hivyo,
sikujaaliwa kushiriki si mazishi
wala maziko yake kwa kuwa
katika kipindi hicho sikuwako
jijini Mwanza.
Taazia ya mwanaharakati
huyu ilinifanya niyakumbuke
majina ya wanaharakati
wengine wanne wa jijini humo
ambao aliungana nao mnamo
1991 kuelekea jijini Dar es
Salaam kuhudhuria semina
ya kutathmini maendeleo
ya Uislamu nchini pamoja
na kuratibu harakati za
maendeleo ya Waislamu
nchini iliyoandaliwa na
kuratibiwa na Kituo cha
Kueneza Uislamu nchini-Islamic
Propagation Centre (IPC).
Majina ya wanaharakati hao,
alioshirikiana nao marehemu
Katimba, waliokuwa wajumbe
au wawakilishi wa Waislamu
wa mkoa wa Mwanza katika
semina ile ni pamoja na Mzee
Miraji Mbwana, Ustadh Hussein
Yasin, Ustadh Haruna Cheyo
pamoja na Bw. Abdallah Amin
ambaye ni mtoto wa aliyewahi
kuwa Sheikh wa kwanza wa
mkoa wa Mwanza aliyefahamika
kwa majina ya Sheikh Amin
Abdallah.
Semina hiyo iliyofanyika
kwa juma moja kuanzia Januari
12-18, 1991 na kuhudhuriwa
na marehemu Katimba pamoja
na wanaharakati hao wengine
niliowataja. Kwa wasiofahamu,
hiyo ilikuwa ndiyo semina
iliyozalisha chachu ya kuratibu,
pamoja na mambo mengine,
harakati za maendeleo ya
kielimu ya Waislamu nchini
na ndio iliyochangia kwa kiasi
kikubwa kuibuka kwa baadhi ya
shule za zamani na hata za sasa
za Kiislaamu nchini ikiwemo,
pamoja na shule nyingine,
shule ya msingi ya Kiislaamu ya
Thaqibu na shule ya sekondari
ANNUUR NEW.indd 9
Makala
AN-NUUR
4/27/2016 12:28:09 PM
10
MAKALA
Na Omar Msangi
ANNUUR NEW.indd 10
AN-NUUR
Mafia Style:
Baada ya urafiki
msiba juu ya msiba
kuizuiya Marekani/NATO na
mpango wake na ISIS katika
Syria.
Tukiachana na siasa hizo
za kutunishiana misuli za
wababe, zipo zile za Marekani
na Saudi Arabia. Siasa za
mkubwa kumfanya mdogo
tambara, kichaka, kibaraka
na mtumwa. Mapema wiki
iliyopita Rais Barack Obama
amesema kuwa hivi sasa
maofisa wa ngazi za juu wa
Idara za Usalama, wanapitia
MFALME Salman
inavyotaka. Kinachotakiwa
ni kuwa kurasa hizo ziwekwe
hadharani (declassification).
28 pages ni kurasa
ambazo zinadaiwa
kunyofolewa kutoka ripoti
maalum juu ya Septemba 11,
na inadaiwa kuwa kurasa
hizo zimeondolewa na
kufanywa siri kubwa kwa
sababu zinaihusisha Saudia
Arabia. Kwamba zinafichua
kuwa Saudi Arabia, kama
Serikali, na baadhi ya watu
wa nyumba ya kifalme
(royal family), walihusika
katika shambulio la kigaidi
lililoporomosha majengo
pacha ya-WTC na kuuwa
watu wanaokadiriwa kufikia
4000.
Mbunge wa zamani,
Seneta Robert Graham, ,
ambaye alishiriki uandishi
wa ripoti ya serikali juu ya
Septemba 11, akihojiwa na
CBS (CBS This Morning/CBS
Evening News) hivi karibuni,
anasema kuwa kurasa hizo 28
ambazo zimefichwa zinaweza
kufichua uhusika wa Saudia
katika kuwasaidia magaidi
walioteka ndege wakapiga
World Trade Center, New
York na nyingine kugonga
Pentagon, huku ndege ya tatu
ikianguka kule Pennsylvania
tarehe 11, Septemba 2001.
How US Covered Up Saudi
Role in 9/11, ni Makala na
uchambuzi uliofanywa na
Paul Sperry juu ya hizi kurasa
28. Katika Makala hiyo
mwandishi ananukuu taarifa
za vyombo vya usalama
juu ya uhusika wa Saudi
Arabia kupitia ubalozi wake
Washington na jinsi serikali
ya Marekani ilivyowaziba
mdomo na kuwashika mikono
FBI na CIA kuchunguza
suala hilo. Mwandishi Sperry
anasema kwamba alifanya
mahojiano na kachero wa
kikosi cha kupambana na
ugaidi- Joint Terrorism Task
Forces (JTTF), Washington
na San Diego, ambaye
alimwambia kuwa kulikuwa
na mawasiliano ya karibu
baina ya magaidi waliokuwa
wamepiga kambi San Diego
na Ubalozi wa Saudia,
Washington na kwamba ni
Prince Bandar bin Sultan bin
Abdulaziz Al Saud, ambaye
wakati huo alikuwa Balozi wa
Saudia Arabia, Washington,
ambaye alimpelekea mmoja
wa magaidi aliyekuweko
San Diego kiasi cha Dola
130,000. Na kwa sababu hiyo,
kama alivyosema kachero
wa FBI John Guandolo,
ilikuwa Bandar awe gaidi
mtuhumiwa namba moja wa
9/11. Hata hivyo, kinyume
chake, wakati Wamarekani
bado wakiwa hawajaanua
tanga la msiba wa Septemba
11, Bandar akaonekana
akiwa na Rais Bush tarehe 13
mwezi huo huo wa Septemba
wakivuta cigar pale Truman
Balcony na baada yapo
baadhi ya wanafamilia wa
Bandar na Osama bin Laden,
wakasaidiwa na idara za
Inaendelea Uk. 11
4/27/2016 12:28:14 PM
11
Inatoka Uk. 10
usalama kurejea Saudi Arabia.
Anasema kachero wa FBI
Mark Rossini, kwamba ni
Ikulu ya Marekani iliyozuiya
kukamatwa watuhumiwa
wakuu wa familia ya kifamle,
akiwemo Prince Bandar
Sultan bin Abdulaziz Al Saud.
FBI waliziba kabisa
masikio kila walivyotajwa
Wasaudia. Ilikuwa kaa la
moto kuwagusa. Alisema
Afisa mmoja wa Polisi (Fairfax
County) Lt. Roger Kelly.
Akizungumzia jambo hilo,
mmoja wa makamishna wa
Tume ya 9/11, John Lehman,
anasema kuwa ilikuwa
ni jambo la kushangaza
kwamba magaidi walikuwa
na uhusiano wa karibu
na Balozi Bandar, mkewe
Bandar halikadhalika ofisi
inayohusika na mambo ya
Kiislamu (Islamic affairs office)
katika ubalozi wa Saudia
ndani ya Washington. Hata
hivyo, la kushangaza na
kutisha zaidi ni kuwa serikali
ya Marekani haitaki kurasa
za uchunguzi zinazoihusisha
Saudia, ziwekwe hadharani.
(Soma pia: 9/11, The 28 Pages,
The CIA & The Art of the
Hangout).
Katika ujumla wake,
kinachoelezwa ni kuwa
Saudi Arabia ni mtuhumiwa
namba moja wa shambulio la
kigaidi Septemba 11, lakini
Saudia imekuwa na msuli wa
kuizuiya Marekani kufunua
mdomo!
Gazeti la New York Times
likizungumzia jambo hili
likasema: Saudis Tell U.S. To
Back Off Bill On 9/11 Lawsuits.
Swali hapa ni je, tangu
lini Marekani ikapokea amri
kutoka Saudi Arabia? Au
kama anavyouliza Kristen
Breitweiser, katika Makala
yake, Saudi Arabia Coerces US
Over 9/11:
When did the U.S.
government start taking orders
from foreign nations? Have we
become a foreign territory of the
Kingdom of Saudi Arabia? Did
Saudi Arabia somehow become a
branch of the U.S. government
with sway over the President,
Congress, and the Judiciary?
Ukizungumzia Putin
au Xi Jinping kuitunishia
msuli, Washington, ni jambo
linaloeleweka, lakini sio
Mfalme Salman bin Abdulaziz
Al Saud. Sasa ukilizingatia
hilo, utaona kwamba hapa
kuna mchezo wa namna
mbili na Marekani inanufaika
kwa namna zote. Moja ni
kuwa tafiti na uchambuzi wa
ANNUUR NEW.indd 11
Makala
Baada ya urafiki
msiba juu ya msiba
AN-NUUR
4/27/2016 12:28:15 PM
12
AN-NUUR
Inaendelea Uk. 13
ANNUUR NEW.indd 12
4/27/2016 12:28:15 PM
13
AN-NUUR
Inatoka Uk. 12
ANNUUR NEW.indd 13
(27: 31).
Akasema: Enyi
wahishimiwa! Nipeni shauri
katika jambo langu hili, kwani
mimi sikati shauri yoyote
mpaka mhudhurie. (27:32
),
Wakasema: Sisi ni
wenye nguvu na wakali kwa
vita; na amri iko kwako, basi
tazama ni nini unaamrisha.
(27: 33), Akasema: Hakika
wafalme wanapo uingia
mji wanauharibu, na
wanawafanya wale watukufu
wake kuwa wanyonge. Na
hivyo ndivyo watendavyo.
(27:34), Lakini mimi
nitawapelekea zawadi, nami
nitangoja watakayo rudi nayo
wajumbe. (27: 35).
Basi alipo fika (mjumbe)
kwa Sulaiman, alisema
(Sulaiman): Hivyo ndio
nyinyi mnanisaidia kwa
mali? Aliyo nipa Mwenyezi
Mungu ni bora zaidi kuliko
aliyo kupeni nyinyi. Lakini
nyinyi mnafurahia hii zawadi
yenu. (27:36 ),
Rejea
kwao! Kwa yakini sisi
tutawajia kwa majeshi wasio
yaweza kuyakabili. Na hakika
tutawatoa humo na hali wao
wamekuwa madhalili na
wanyonge. (27:37 ),
4/27/2016 12:28:16 PM
14
MAKALA/MASHAIRI
ANNUUR NEW.indd 14
AN-NUUR
4/27/2016 12:28:17 PM
15
Inatoka Uk. 9
alifanikiwa kupata daraja la
kwanza la pointi/alama kumi na
tano (15) katika matokeo yake ya
masomo yake ya kidato cha nne
na kupata daraja la kwanza la
pointi/alama (6) katika matokeo
ya masomo yake ya kidato
cha sita, halikadhalika ndiye
mwanafunzi aliyeongoza kwa
kanda ya ziwa nzima katika
ufaulu wa somo la lugha ya
Kiarabu kwa matokeo ya kidato
cha sita kwa mwaka 2011. Baada
ya ufaulu wake wa kidato cha
nne alifanikiwa kuchaguliwa
kujiunga na shule ya sekondari
Umbwe ya mkoani Kilimanjaro,
lakini hakwenda kutokana
na mchepuo, wa masomo ya
Historia, Kiswahili na Kiingereza
(HKL) kutokuwepo shuleni
hapo, ambao yeye aliupendelea
zaidi kutokana na utashi pamoja
na utayari wake wa kujikita
zaidi katika masomo ya lugha
hapo baadae kuliko mengineyo.
Kwa mazingira haya na baada
ya kushauriana na baba yake
mlezi, alijiunga na shule ya
sekondari Thaqaafa ambako
mbali na kuchukua mchepuo wa
masomo ya Historia, Kiswahili
na Kiingereza (HKL) aliongeza
pia na somo la lugha ya Kiarabu.
Katika matokeo yake ya masomo
ya kidato cha sita alifanikiwa
kupata alama (B) katika masomo
yote ya Lugha yaani Kiswahili,
Kiingereza na Kiarabu wakati
ambapo alipata ufaulu wa alama
(D) katika somo la Historia
jambo ambalo lilidhihirisha
dhamira yake ya tangu awali
ya kupendelea zaidi masomo
ya lugha kuliko vinginevyo.
Hata hivyo, ndoto zake za
kuendelea zaidi na masomo ya
lugha zilififia baada ya kujikuta
amechaguliwa kujiunga katika
kitivo cha sheria katika Chuo
Kikuu cha Dar es Salaam
ambako alifanikiwa kuhitimu na
kupata Shahada yake ya Sheria
mnamo 2015.
Kutokana na malezi
aliyoyapata na makuzi
aliyoyapitia chini ya marehemu
Katimba, kijana huyu amejifunza
mengi ambayo alisema ni
vigumu kuyaeleza yote ila alitaja
machache ikiwa ni pamoja na
subira na uvumilivu, upendo,
ukarimu, insafu, hekima na
busara pamoja na uchamungu.
Kwa upande wa wasifu wa
marehemu, kijana huyu anaeleza
kwamba:
''Pamoja na sifa mbalimbali
zinazoweza kuelezwa na kila
mmoja wetu kutokana na jinsi
alivyomfahamu mzee (Idd
Katimba), mimi kwa upande
wangu ninaona kwamba mzee
huyu alikuwa ni mzazi, mlezi na
kiongozi.''
Akaongeza kwa kusema,
''Kwa kweli kwangu mimi
alikuwa ni mtu wa kupigiwa
mfano.'' Akahitimisha kwa
kumwombea dua,''Allah
amsamehe pale alipoteleza kama
mwanadamu''.
Aidha, marehemu Katimba
aliwahi kushika nyadhifa
ANNUUR NEW.indd 15
Makala/Tangazo
AN-NUUR
AFRICA MUSLIMS
AGENCY, KUWAIT
TANZANIA OFFICE,
VACANCIES ANNOUNCEMENT
4/27/2016 12:28:21 PM
Makala
16
Na Khatib J Mziray
ENYI mlioamini!
Mmelazimishwa
kufunga (Sumu) kama
walivyolazimishwa waliokuwa
kabla yenu ili mpate kumcha
Mungu. (Quran 2:183.)
Kulingana na aya
hiyo, tunafahamu kuwa,
Mitume waliomtangulia
Nabii Muhammad S.A.W.
Walilazimishwa kufunga; na
kuwa, katika funga ndipo
panapapotikana tija ya Ucha
Mungu.
Lakini kwa wasiokuwa
Waislamu, wanasema kuwa,
Muhammad S.A.W. Ndiye
aliyeleta ibada ya funga, na
wameandika poropoganda
nyingi kuhusu funga.
Moja katika nguzo za imani
katika Uislamu, ni kuamini
mitume wa Mwenyezi Mungu
na vitabu walivyoteremshiwa
(Ufunuo-Wahayi) kutoka kwa
Mwenyezi Mungu.
Vitabu hivyo ni Torati,
aliyopewa Nabii Mussa A.S.
Zaburi, aliyopewa Nabii Daudi
A.S. Injili, aliyopewa Nabii
Isa (Yesu) A.S. Na Quran
Aliyopewa Nabii Muhammad
S.A.W. Kwa maana hiyo,
inatulazimu kuviangalia vitabu
vitatu vilivyoitangulia Quran,
kuwa vinaizungumziaje funga
(saumu)?
Nabii Musa A.S. ndiye
aliyeteremshiwa Torati (Sheria).
Nabii Mussa A.S.
Alikabidhiwa Torati akiwa
amefunga; kwa kuwa funga
ilishamfikisha katika Ucha
Mungu:BWANA akamwambia
Musa, Andika maneno haya;
kwa kuwa mimi nimefanya
agano nawe, na pamoja
na Israeli, kwa mujibu wa
maneno haya. Naye alikuwa
huko pamoja na BWANA
siku arobaini na masiku yake;
hakula, wala kunywa maji. Naye
akaandika katika hizo mbao,
hayo maneno ya maagizo, hizo
amri kumi. (Biblia 34:27-28.)
Kwa bahati mbaya waandishi
hawakueleza hapo kuwa, Nabii
Musa A.S. Alikuwa amefunga,
bali wamesema kuwa hakula
wala kunywa maji, lakini
tutaona baadae. Kwa kuwa
andiko limesema kuwa, Nabii
Mussa A.S. aliandika amri
hizo za Mwenyezi Mungu,
tunahakika kuwa Manabii
waliofuata baada yake
watakuwa wakitekeleza amri
hizo ikiwemo hiyo ya kufunga:Habari za Nehemia,
mwana wa Hakalia.Hata
ikawa niliposikia maneno
hayo, nikalia nikaomboleza
siku kadha wa kadha; kisha
nikafunga, nikaomba mbele za
Mungu wa mbinguni; nikasema,
Nakusihi, Ee BWANA, Mungu
wa mbinguni, Mungu mkuu,
mwenye kuogofya, mwenye
ANNUUR NEW.indd 16
Funga ya Ramadhani
AN-NUUR
4/27/2016 12:28:23 PM
17
MAKALA
Udini-1
Na H. Hashim
ANNUUR NEW.indd 17
AN-NUUR
4/27/2016 12:28:27 PM
18
Makala
Tawhiid -8
Na Mussa Ame
ANNUUR NEW.indd 18
AN-NUUR
4/27/2016 12:28:27 PM
19
M
Ukurasa wa Watoto
AN-NUUR
Nguzo za Uislamu
Wiki iliyopita
tujifunza kuwa
Uislamu ni Dini ya
Allah (SW).
Uislamu ni Dini ya
kumtii Allah (SW)
kwa unyenyekevu.
Uislamu ni Dini
inayofuatwa na
maumbile.
Uislamu ni Dini
iliyofundishwa na
Mitume wote.
Uislamu ni Dini ya
walimwengu wote.
Uislamu ni
Dini ya haki na
inayosimamia haki
katika jamii.
Leo tutajifunza juu
ya nguzo za Uislamu.
Uislamu umejengwa
juu ya nguzo tano:
1. Kutoa shahada
mbili.
2. Kusimamisha
Swala tano.
3. Kutoa Zakat.
4. Kufunga mwezi
wa Ramadhani.
ANNUUR NEW.indd 19
5. Kuhiji katika
nyumba takatifu (AlKaabah) kwa kila
mwenye uwezo.
Nini maana ya
Shahada mbili?
Shahada ya
kwanza ni kusema:
Nashuhudia kuwa
hapana mungu
apasaye kuabudiwa
kwa haki ila Allah.
Shahada ya pili
ni kusema: Na
ninashuhudia kuwa
Muhammad ni
Mtume wa Allah.
Muislamu wa kweli
anashahadia kila
akiswali.
Waislamu
walioshahadia
kikweli, hufuata yale
yote aliyowaamrisha
Allah (SW) na
Mtume wake.
Pia hijiepusha
na vitu vyote
alivyokataza Allah
(SW) na Mtume
wake.
4/27/2016 12:28:33 PM
AN-NUUR
20
MAKALA
20
Soma gazeti la
AN-NUUR
KWA TSH 800/=
kila Ijumaa
AN-NUUR
kusonga mbele.
Taarifa hiyo imesema, maandalizi
mengine yanaweza kufanyika
kwa kuwahimiza Waislamu
kuchangamkia fursa mbalimbali
zinazoanzishwa miongoni mwa
jamii wanamoishi.
Mathalani taarifa hiyo
ikasema fursa za elimu zilizopo
sasa, zitumike kwa Waislamu
kuwapeleka watoto wao Shuleni
sambamba na kuwahimiza elimu
ya dini, kwa kufanya hivyo ikasema
taarifa hiyo wataweza kuwapata
vijana wenye elimu nzuri hapo
baadae ikiwa watasimamiwa vizuri.
Taarifa hiyo ikaeleza lengo la
kuwakusanya Waislamu katika
mkutano wake huo kuwa ni
kuwahamasisha Waislam wa
Dodoma pamoja na Wilaya zake
kujiunga katika Taasisi hiyo
(DGMA).
Tumefanya hivi kuwaita kwa
misingi ya kuleta mapenzi, upendo
na umoja miongoni mwetu ili
tuweze kufaidika kupitia Taasisi
hii. Imesema taarifa hiyo.
Kwa upande wake Mwenyekiti
wa Taasisi hiyo, Sheikh Mohammed
Thabiti, akiongea katika mkutano
huo, alisema kila Muislamu ana
wajibu wa kuwaeleza Waislamu
wenye nia njema na Taasisi hiyo
ili waweze kujiunga kwa lengo la
kuunganisha nguvu.
Maimamu na Viongozi wa
Taasisi nyingine ni Mabalozi wa
kuitangaza kwa waumini Taasisi
hii, pia kuwaeleza au kuwaelekeza
waweze kufika ofisini na kupata
taratibu za namna ya kujiunga.
Amesema Shkh Thabiti.
Alisema, huduma za Kiroho au
https://www.facebook.com/Herbal-Impact-157972014402705/
Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na Business Printers Ltd, Dar es Salaam.
ANNUUR NEW.indd 20
4/27/2016 12:28:35 PM