Академический Документы
Профессиональный Документы
Культура Документы
UTANGULIZI.
Semina hii ilifanyika tarehe 30/03/2012 ikiwa ni katika kukamilisha mkakati uliopangwa kwa muda
mrefu ili kurahisisha zoezi la utambuzi wa wahamiaji walowezi, pia kuwaandaa viongozi hawa katika
ushiriki wa zoezi zima la utoaji wa vitambulisho vya uraia na kuwahamasisha kushiriki kwa hali na mali
katika mapambano dhidi ya wahamiaji haramu.Semina hii iliratibiwa na ofisi ya uhamiaji wilaya kwa
msaada wa ofisi ya uhamiaji mkoa.
WASHIRIKI.
Idadi na vyeo vya washiriki katika semina hiyo ni kama inavyoonyeshwa hapa chini.
SN
1
2
3
CHEO
Makatibu Tarafa
Watendaji wa Kata
Watendaji wa Vijiji
JUMLA
IDADI
2
12
48
62
MADA
Uraia
Madhara ya Rushwa
Ulinzi na Usalama wa
Nchi
Maadili ya Uongozi na
uwajibikaji
MTOA MADA
Afisa wa uhamiaji
Afisa wa TAKUKURU
OCD-Bunda
OFISI/TAASISI
ALIYOTOKA
Uhamiaji-Bunda
TAKUKURU-Musoma
Jeshi la Polisi-Bunda
Halmashauri ya Wilaya ya
Bunda.
Mtoa mada kutoka jeshi la polisi hakuwa na chapisho lolote kwani hakuwa
ameandaa ila aliahidi kuandaa na kuhakikisha washiriki wanapata chapisho hilo.
MATARAJIO.
Ni matarajio yetu kwamba baada ya semmina hiyo tutapata ushirikiano mkubwa kutoka kwa
viongozi hawa hivyo kurahisisha jitihada zetu za kuwatambua wahamiaji walowezi na
kupunguza kama si kukomesha kabisa wimbi la wahamiaji haramu katika wilaya yetu na mkoa
kwa ujumla.
SHUKRANI.
Tunatoa shukrani za dhati kwa kamati ya ulinzi na usalama kwa ushirikiano mkubwa walioutoa
katika kufanikisha semina hii, hasa mgeni rasmi ambaye ni mwenyekiti wa kamati hiyo kwa
kukubali kuacha shughuli zake na kuwa mgeni rasmi katika semina hiyo. Pia tunatoa shukrani
zetu za dhati kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri aliyetusaidia kutoa taarifa kwa
washiriki wote na kutupatia ukumbi mzuri na wakisasa kwa ajili ya semina hiyo.Shukrani za
pekee tunazitoa kwa ofisi ya uhamiaji mkoa kwa kuwezesha kwa kiasi kikubwa semina hii
kufanyika.
OMBI/USHAURI.
Tunaomba ufanyike utaratibu wa kufanya semina nyingine kama hii kwa tarafa zingine
zilizobaki.
Nawasilisha.