Вы находитесь на странице: 1из 12

www.annuurpapers.co.

tz

Sauti ya Waislamu

(14) WASITIRI WAZAZI WAKO!


Masahaba waliwahijia wazee wao waliokufa bila kuhijji na waliokutwa wamezeeka ilipofaradhishwa Hijja. Hivi sasa waislamu wengi wanakufa bila kuhijj na kuacha mali zaidi ya malipo ya Hijja. Uislamu hauwatambui wazee hao mpaka wahijiwe! Umeshawaokoa wazazi wako na kuwarudisha katika Uislamu? KaribuAhlu Sunna wal Jamaa. Gharama zote ni Dola 4,300. Tafadhaliwasiliana nasi ifuatavyo: Tanzania Bara: 0717224437; 0777462022;Unguja: 0777458075;Pemba: 0776357117.

Tuambiwe ukweli FFU wamsindikiza nani kalipua bomu Wapo wapi Uamsho waliotua Dar kuchoma Makanisa

ISSN 0856 - 3861 Na. 1070 JAMADUL THAN 1434, IJUMAA - MEI 10-16, 2013 BEI TShs 500/=, Kshs 50/=

Ponda Mtambani
Kivumo cha Takbiira chatikisa Kisutu Yathibitishwa kiwanja kimeporwa Ponda akitetee Mahakama ya Ardhi

Wabunge wasicharuke tu, wahoji mambo ya msingi Kasema kweli Samia Suluhu, tuwe na yakini kwanza

Mh. Pinda, Namanga walipita Waarabu tu?


Siku hiyo hawakusari Wazungu? Au ndiyo yale ya Dowans Vs Symbion!

MH. Waziri Dkt. Nchimbi

MH. Waziri Samia Suluhu

Mkutano wa OIC kufanyika Zanzibar


Na Al ghaithiyyah, Zanzibar

Uk. 6

SHEIKH Ponda Issa Ponda.

CHUO Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA), kinatarajiwa kuwa mwenyeji wa Mkutano Mkuu wa Kimataifa

wa Umoja wa Nchi za Kiislamu (OIC). Mkutano huo kwa mwaka huu unatarajiwa kufanyika Septemba 2 kwa mashirikiano ya nchi ya Oman, Umoja wa OIC na
Inaendelea Uk. 2

2
www.annuurpapers.co.tz

Tahariri/Makala
Cel: 0784 370 208, 0713 110 148, 0755 260 087 , DSM. E-mail: annuurpapers@yahoo.co.uk Osi zetu zipo: Manzese Tip Top Usangi House (Jengo dogo), barabara ya Morogoro, D'Salaam

JAMADUL THAN 1434, IJUMAA MEI 10-16, 2013 Kumekuwa na mlolongo wa kukamatwa Waislamu wanaokutwa na kanda zenye mawaidha ambapo ndani yake kuna ujumbe wa Quran kuwa Yesu si Mungu. Lakini kwa upande mwingine, hatujawahi kuona wauza kanda za kutukuza uungu wa Yesu, wakibughudhiwa. Sasa hapa ni lazima isemwe wazi, je kinachokusudiwa hapa ni kupiga marufuku Waislamu kusema kuwa Yesu sio Mungu? Kusema Yesu si Mungu, ni jambo lisilokubalika kwa Mkristo kwa sababu ni sawa na kupinga uungu wa mungu wake Yesu. Lakini pia ni kufru kubwa kwa Muislamu akisikia mtu akisema kuwa Yesu ni mungu. Katika hali hii, ufumbuzi ni nini? Je, ni kuwapiga marufuku Waislamu wasihubiri kuwa Mungu si Yesu ambayo ni sawa na kuwazuiya wasisome baadhi ya aya za Quran? Je, wakatazwe w o t e , Wa i s l a m u n a Wa k r i s t o ? M u i s l a m u asiseme kuwa Yesu si Mungu na Mkristo asiseme kuwa Yesu ni Mungu? Yo t e h a y a i n a p a s a yafafanuliwe, vingine itabaki kuwa ni utata mtupu na katika utata huu ndio tunaona Serikali inaungana na Wakristo kuwashambulia Waislamu kuwa ndio wanaotukana na kuwakashifu Wakristo. Wale wanaopiga vijembe vya kuwaombea wenye majini na mapepo hawaonekani. Imekuwa sawa na ile agenda ya ugaidi. Haisemwi kwamba ni kuwapiga vita Waislamu, lakini kila tukio, anayekamatwa ni Muislamu/Muarabu. Ndio maana hata Arusha tumekimbilia kuwakamata Waarabu wakati Arusha wapo raia wengi wa kigeni. Kwa mtindo huu wasiwasi wetu ni kuwa tutazidi kuivuruga amani ya nchi badala ya kuitengeneza.

AN-NUUR

AN-NUUR S.L.P. 55105, Simu: +022 2400786


MAONI YETU

Aliyosema Zitto yazingatiwe


AKIFAFANUA Azimio la Bunge juu ya kadhia ya Arusha, Mheshimiwa Anna Abdallah aliitaka Serikali kufuta vikundi vya Kiislamu vyenye dhamira mbaya. Katika kutoa mfano akahoji, inakuwaje Serikali kuandikisha vikundi vya Kiislamu ambavyo lengo lake ni kupinga Bakwata. Kwanza tuseme kuwa hakuna taasisi ya Kiislamu iliyowahi kuanzishwa kwa lengo la kupinga Bakwata. Pili, kama ilivyo kwa taasisi za dini nyingine, ikiwemo Ukristo anaofuata Mheshimiwa Anna, kila taasisi ya Kiislamu inayoanzishwa ni kwa kuzingatia mambo mawili makubwa: Kwanza kutimiza wajibu wa wahusika kwa Mola wao. Kwamba kwa kupitia taasisi hiyo watafanya Dawah, watahubiri na kuwaletea maendeleo waumini wao na Watanzania kwa ujumla. Pili, wanafanya hivyo kwa kutumia haki yao ya uhuru wa kidini wa kuabudu na kujihusisha na vikundi vya kijamii kama inavyotolewa na Katiba ya Nchi. Labda swali ni je, kwa nini Anna Abdallah hakuzungumzia utitiri wa taasisi za Kikristo na makanisa yanayochipuka hivi leo ambayo baadhi yao ndiyo yametuletea mgogoro huu wa kuchinja? Kwa nini hakuzungumzia utitiri wa makanisa yanayokera watu mitaani kwa kuimba na kupiga muziki usiku kucha na wananchi wakilalamika ndio kwanza wanaongeza vinanda na magitaa kwa madai kuwa hiyo ni dalili kuwa shetani anakereka kwa hiyo wazidi kumkera? Anna hakugusa hayo na badala yake kuihami Bakwata, sio kuwa anampenda sana Sheikh Al Had Mussa, Mufti Shaaban Simba na Bakwata yao, bali ni kwa sababu fikira inayomwongoza ni ile ile ya Serikali ya kuwabana na kuwadhibiti Waislamu huku Wakristo wao wakitanua watakavyo na taasisi zao. Na haya ndiyo aliyotahadharisha Mheshimiwa Zitto Kabwe

Mtizamo wa akina Anna Abdallah utatuvuruga

bungeni. Akichangia tarehe 6 Mei katika kikao kinachoendelea Dodoma, Mheshimiwa Zitto Kabwe alitaka Watanzania wasome kutoka yaliyowakuta Ivory Coast na Liberia. Katika uchambuzi wake akasema kuwa kuna lawama ya muda mrefu sana ya Waislamu kuhusu BAKWATA. Kwamba Waislamu miaka mingi toka mwaka 1969 wakati Serikali imeunda BAKWATA wanalalamika. Wanalalamika kuwa wakati Serikali imewapa Wakristo uhuru wa kuwa na taasisi zao huru na haiziingilii, inapokuwa kwa Waislamu, inataka kuwadhibiti Waislamu wote chini ya Bakwata ambayo haina uhalali wowote (legitimacy) ya kuwasemea Waislamu. Mtizamo huu, msimamo na mkakati huu wa kuwanyima u h u r u Wa i s l a m u , n d i o uliomfanya Anna Abdallah atoe mfano wa wapinga Bakwata. Anachotaka kuona ni kuwa Waislamu wanarejeshwa katika ile miaka ya Mwalimu Nyerere ambapo Muislamu hakuruhusiwa kufanya jambo lolote la Kiislamu mpaka apate kibali cha Bakwata, na ukienda Bakwata hupati kwa sababu ilishapewa maelekezo. Hivi tunavyoandika maoni haya kuna Waislamu wanakabiliwa na kesi ya kuchoma makanisa, wengine wapo nje kwa dhamana na wengine kwa zaidi ya miezi sita sasa dhamana zao zimezuiliwa. Makanisa haya ni yale yaliyodaiwa kuchomwa siku ya vurugu za maandamano kupinga hatua ya Polisi kusita kumchukulia hatua kijana aliyekojokolea Quran. Mara nyingi panapotokea matukio kama haya, ndipo hupatikana fursa kwa wahalifu nao kufanya yao kama tunavyoona wakivamia na kupora maduka. Lakini wakati Waislamu wakisubiri hukumu kufuatia kesi hiyo, watu waliochochea waumni wa Kikristo Tunduma wakaandamana na kufanya fujo na kuchoma moto msikiti, taarifa tulizo nazo ni kuwa hakuna mashitaka yoyote waliyokwisha somewa. Labda

swali ni je, ujumbe gani wanapewa Waislamu? Kama mtu anaweza kungoa dirisha la msikiti na asichukuliwe hatua yoyote na vyombo vya dola, salamu gani anapewa mtu huyu? Je, kesho na keshokutwa kwa ujumbe huu aliopewa kuwa yeye haguswi, atashindwa kufanya jingine kubwa? Lakini kwa upande, mwingine, katika hali hii, Waislamu waliovunjiwa msikiti wao ambao wanategenea kuwa kuna Serikali yenye kujali usalama wa wnaanchi wote, wanapewa ujumbe gani? Wa k a t i Wa z i r i w a Mambo ya Ndani ya Nchi, Mheshimiwa Dkt. Emannuel Nchimbi akifunga mkutano wa viongozi wa kidini, jijini Dar es Salaam alisisitiza kauli ya Serikali ya kukataza mihadhra ya kashfa na kauli za kujenga chuki. Ambalo tungependa lifafanuliwe zaidi, ni hili la mihadhara ya kashfa. Je, kinachokusudiwa nini?

Mkutano wa OIC kufanyika Zanzibar


Inatoka Uk. 1

SUZA. Taarifa hiyo imekuja kufuatia ziara ya siku nne ya maafisa wa nchi ya Oman walioambatana na maafisa wa OIC iliyonza mapema wiki hii mjini Zanzibar. Mwenyekiti wa Mamlaka ya kumbumbuku na nyaraka ya nchi ya Oman Dkt. Hamed Mohammed al Dhawiyaniy amesema Zanzibar imepata nafasi hiyo kutokana na kuwa na mahusiano mema na nchi nyingi ulimwenguni na hasa katika nchi za Kiarabu. Amesema, historia na utamaduni wa Kiislamu wa Zanzibar na namna ulivyotumika katika kusambaza Uislamu nchi nyingine, umekuwa kigezo muhimu cha Zanzibar kupata nafasi hiyo. Kwa vile Zanzibar ina historia nzuri katika kusambaza Uislamu nchi nyingine, tunaimani kuwa hata malengo ya mkutano wetu huo yatakiwa kwa kiasi kikubwa , alisema Dkt. al Dhawiyaniy ambaye pia ni mkuu wa msafara huo. Kwa upende wake Mkurugenzi Mkuu wa OIC

katika kitengo cha utati na utamaduni Dkt. Halit Eren amesema mkutano huo utakuwa fursa adhimu kwa Zanzibar kujitangaza katika mataifa mbalimbali na kuendelea kujiongezea umaarufu kimataifa. Amesema, kwa vile watakuja washiriki kutoka mataifa mbalimbali kutoka nchi wanachama wa OIC, Zanzibar itakuwa ni nafasi yake muhimu kufahamika kimataifa na kujipatia nafasi za masomo duniani. Amefahamisha kuwa watoa mada 164 kutoka nchi mbalimbali tayari wameshapeleka maombi yao ili kuwasilisha katika mkutano huo na kuwataka Wazanzibari nao kupeleka maombi yao. Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Chuo cha SUZA Dkt. Haji Mwevura Haji amesema vyuo mbalimbali kutoka nchi tofauti viliomba kuwa mwenyeji wa mkutano huo, lakini SUZA kimeamuliwa kuwa mwenyeji kutokana na historia ya Zanzibar. Amefahamisha kuwa licha ya Zanzibar kutokuwa mwanachama wa jumuiya ya OIC, lakini kigezo hicho hakiizuii Zanzibar kuwa mwenyeji wa mkutano huo

wa kimataifa. Amegusia kuwa mkutano huo unaweza kuwa fursa adhimu kwa Zanzibar kunufaika kupitia jumuiya hiyo kama ambavyo nchi ya Uganda ilifaidika kwa kujengewa Chuo Kikuu cha Mbale. We n z e t u U g a n d a walifaidika na OIC kwa kujengewa Mbale University, nasi pia tuna matarajio mengi ilikwemo kuitangaza SUZA na kupata scholarships duniani, alisema Dkt. Haji D k t . H a j i amewahakikishia maosa hao ushirikiano wa kutosha ili mkutano huo uweze kutimiza malengo yaliyopangwa. Umoja wa Nchi za Kiislam Duniani, OIC, unajishughulisha na mambo mbalimbali ya kimaendeleo ikiwemo kusaidia nchi wanachama wa umoja huo katika huduma za kijamii ikiwemo ujenzi wa taasisi za kielimu, afya na miundombinu. Mkutano Mkuu ndio unaojadili na kupitisha miradi na misaada mbalimbali ambapo mkutano uliopita ulifanyika nchini Omani.

3
Na Bakari Mwakangwale WANAODAIWA kuwa ni vinara wa vurugu za kuchinja zilizoibuka hivi karibuni katika mji wa Tunduru na kusababisha kuvunjwa na kuchomwa moto Msikiti, wahawajafikishwa katika vyombo vya sheria. Kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari kutoka katika mji huo mdogo wa Tunduma, watu hao wametajwa kuwa ni Diwani wa Chadema na Mchungaji mmoja, ambao kabla ya tukio walikuwa ni chachu ya kuibuka kwa vurugu hizo. Sambamba na watuhumiwa hao, chanzo hicho kimedai pia kuwa watuhumiwa wa vurugu hizo na kusabisha kuchomwa moto na kuvunjwa Msikiti, mpaka sasa hawajafunguliwa mashitaka yoyote. Walikishwa mahakamani na kuambiwa warudi nyumbani bila ya kusomewa mashitaka. Watuhumiwa karibia wote wapo nje kwa dhamana, lakini hawajasomewa shitaka lolote, walipelekwa Mahakamani kisha walitajwa majina yao

Habari

JAMADUL THAN 1434, IJUMAA MEI 10-16, 2013


na kuchoma moto Makanisa, na zaidi alidai kwa wale walioko mahabusu ni kuwa wanatuhumiwa kufanya ujambazi wa kutumia silaha kosa ambalo kisheria shitaka hilo halina dhamana. Hawa kumi mpaka sasa wapo mahabusu, huku kesi yao ikiendelea kwa kasi kubwa, na huenda ikachukua muda kwa sababu upande wa Serikali inaorodha ya mashahidi wengi. Alisema Wakili Njama. A l i s e m a , Wa i s l a m u wengine wanakabiliwa na kosa la katika kesi 241, inawahusu takribani washitakiwa nane, ambao wao wapo nje kwa dhamana na kesi yao ishaanza kusikilizwa. Bw. Njama alisema, kuna kesi namba 242, inayowakabili Waislamu pia waliokuwepo katika madai hayo ya uchomwaji wa Makanisa ambayo kesi yao haijaanza kusikilizwa kabisa, kutokana na sababu mbalimbali. Wa i s l a m u w o t e h a o walikamatwa katika sakata la uchomwaji wa Makanisa Mbagala, na kugawanywa katika mashitaka hayo katika kesi tatu tofau. Alisema Wakili Njama.

AN-NUUR

Waliochoma, kubomoa Msikiti Bado hawajasomewa shitaka


Walikishwa mahakamani wakaachiwa Wanaodaiwa kuchochea hawakuguswa Waislamu Mbagala wanasota rumande Wengine wamesomewa kesi za ujambazi
na kupewa dhamana bila kusomewa mashitaka, na walitakiwa kurudi kuripoti Mahakamani Mei 18, 2013. Kilisema chanzo hicho. Chanzo hicho kilisema kuwa cha kushangaza ni kwamba wale ambao walikuwa vinara na wahamasishaji wa vurugu zile, ambao ni Mchungaji mmoja na Diwani wa Chadema, waliitwa Polisi wakahojiwa kisha wakaachiwa, wala hawajajumuishwa na watuhumiwa wengine. Hatuelewi ni kwa nini hawajahusishwa na wafuasi wao waliofanya vurugu kubwa mjini hapa na kusababisha hofu na hasara kubwa sambamba na kubomoa Msikiti na kuchoma moto, jamaa waliohojiwa tu na kuachiwa. Kilibainisha chanzo hicho. Wakati huo huo Waislamu kumi katika sakata la kuchoma moto Makanisa Mbagala, wanasota rumande hadi sasa. Wa t u h u m i w a h a o , n i miongoni mwa Waislamu waliokamatwa kwa madai ya kuchoma moto Makanisa, na kufanya uharibifu, ambapo katika kufunguliwa mashitaka, baada ya kufikishwa Mahakamani, walifunguliwa kesi tatu tofauti tofauti. Kwa mujibu wa wakili anayesimamia kesi hizo, Bw. Yahaya Njama, alisema watuhumiwa wa kwanza wanashitakiwa kwa kosa la kuvamia Kanisa. Alisema, katika kuvamia huko wanadaiwa kuharibu mali, kujeruhi watu, kuiba

FFU wamsindikiza Ponda Mtambani


Na Shaaban Rajab
JANA Kikosi cha Polisi cha Kutuliza Ghasia, FFU, kilikuwa na wakati mgumu kilipolazimika kumsindikiza Sheikh Ponda hadi Msikiti wa Mtambani. Ilikuwa heka heka katika Mahakama ya Kisutu baada ya kurindima kivumo cha Takbiira wakati Hakimu aliposoma hukumu kuwa washitakiwa wote hawana kosa na kuachiwa huru ila Sheikh Ponda aliyepewa kifungo cha nje cha mwaka mmoja. M a m i a y a Wa i s l a m u waliofika Mahakamani hapo, walianza kuondoka kwa lengo la kusindikiza gari iliyomchukua Ponda kuelekea Msikiti wa Mtambani na hapo ndipo gari nne za FFU zikajitokeza kuongoza msafara huo. Katika msafara huo, gari moja ya FFU ilikaa mbele ikiongoza gari aina ya Prado aliyopanda Ponda, kisha gari moja pembeni mwa gari hiyo ya Ponda huku nyingine mbili zikifuatia nyuma. Pamoja na msafara huo kupelekwa kasi ambapo mara kadhaa FFU katika gari ya mbele walilazimika kushuka kuziondoa gari zisizuiye msafara huo, bado Waislamu nao walipiga mbio kufuata msafara huo hadi Mtambani. Katika hukumu ya jana, ilimchukua Hakimu Victoria Nongwa, zaidi ya saa mbili na nusu, kusoma hukumu hiyo ambapo washitakiwa 49 waliachwa huru huku Sheikh Ponda akitakiwa atumikie miezi 12 kwa amani bila kutenda kosa na kuendelea kuhubiri amani na kuonyesha tabia njema, yaani (Conditional discharge). Awali akisoma mtiririko wa mashahidi upande wa mashitaka, Hakim Nongwa alianza kwa kufafanua kila kosa waliloshitakiwa watuhumiwa, kuanzia na kosa la kula njama ya kutenda kosa. Katika kipengele hicho, Hakimu Nongwa alisema katika hati ya mashitaka, haielezwi ni kosa gani watuhumiwa walikula njama miongoni mwa makosa waliyoshitakiwa kwayo. Aidha, aliongeza kuwa mashahidi hawajaonyesha ushahidi juu ya kosa hilo la kula njama ya kutenda kosa. kwa mujibu wa ushahidi uliotolewa, upande wa mashitaka umeshindwa kuthibitisha au kudhihirisha namna washitakiwa walivyokula njama za kutenda kosa. Hivyo aliutaka upande wa mashitaka kuwa makini wakati wa kuwasilisha ushahidi wa kosa la kula njama kwa kuwa njama siku zote ni jambo la siri na vigumu kulithibitisha. Akitoa ufafanuzi juu ya kosa jingine la kuingia kwa nguvu kwa kuzingatia ushahidi uliotolewa, Hakimu Nongwa alisema hakuna mahali ambapo kunadhihirishwa kwamba kuna nguvu iliyotumiwa na watuhumiwa kuingia katika kiwanja hicho. Aidha alisema, mahakama inaona ushahidi wa upande wa mashitaka hauko wazi dhidi ya waliokuwepo katika kiwanja hicho isipokuwa kwa mtuhumiwa namba moja ambaye ni Sheikh Ponda. Alisema, suala la kuingia kwa nguvu ni lazima lithibitishwe kwa nguvu iliyotumika. Hata hivyo kipengele hiki kilimwangukia Sheikh Ponda, kuwa aliingia kwa nguvu katika kiwanja hicho, hasa ikizingatiwa kuwa baadhi ya mashahidi wa upande wa mashitaka walishabainisha mahakamani hapo kwamba Sheikh Ponda aliwahi kufika eneo hilo na kuwataka kusitisha ujenzi wa uzio wa eneo hilo. Katika kosa la wizi, Mahakama iliona kwamba ushahidi wa upande wa mashitaka haukuweza kuwasilisha kielelezo chochote kinachoweza kuthibitisha wizi huo. Hakimu Nongwa alifafanua zaidi kwamba, hata huo Msikiti wa muda uliojengwa, hauonyeshi kutumia vifaa vya thamani ya milioni 56 kama ulivyodai upande wa mashitaka kuwa vifaa vilivyoibwa ni vya thamani ya kiasi hicho. Alisema, baadhi ya vifaa vilivyotajwa katika ushahidi, vilishatumika kujengea sehemu ya uzio wa kiwanja hicho. Pia alisema baadhi ya mashahidi wa upande wa utetezi nao walithibitisha kwamba Msikiti wa muda ulijengwa kwa mabati na mbao, vifaa walivyoshuhudia vikiteremshwa katika eneo la Markaz. Aidha, usahidi wa Sheikh ponda unathibitisha hilo pale alipotoa ushahidi wake kuwa Msikiti huo wa muda ulijengwa baada ya michango ya waumini iliyofikia kiasi cha laki sita, ukiwemo mchango wa Bw. Suleiman Nassor Mohammed, mmoja wa wakurugenzi wa Agritanza. Kuhusu kosa la kufanya ushawishi wa kutenda kosa, lililokuwa likiwakabili Sheikh Ponda na Ustadh Saleh Mukadam, mahakama iliona kuwa kadhalika katika kosa hilo upande wa mashitaka ulishindwa kubainisha katika ushahidi kutendwa kosa hilo. Haikuelezwa ni kosa gani waliloshawishi Ponda na Mukadam. Wala haikuthibishwa ni namna gani Ponda na Mukadam walishawishi kutenda kosa na kosa lenyewe ni kosa gani. Hata hivyo Hakimu Victoria Nongwa, alisema ni wazi kwamba kiwanja cha Markaz Changombe, ikiwa ni pamoja na eneo lenye kesi hiyo, ni kwa ajili ya Maendeleo ya Waislamu. Aidha alisema ni wazi kwamba eneo hilo lilikuwa kubwa, zaidi ya ekari 27 lakini limekuwa likimegwa kinyume na utaratibu kama walivyobainisha mashahidi wa upande wa mashitaka, ambao walisema waliohusika na vitendo hivyo walishaondolewa Bakwata. Aidha alisema kulingana na ushahidi uliotolewa na pande zote mbili, ni wazi kuwa Bakwata walibadilishana kiwanja katika eneo hilo bila ridhaa ya

Waislamu. Hata hivyo alisema mashitaka yaliyowasilishwa mahakamani ni ya jinai na kwamba, Mahakama haizungumzii tarataibu za Bakwata kubadilishana ardhi na Agritanza. Hata hivyo alisema Sheikh Ponda ana haki ya kutetea mali za Waislamu, hivyo alishauri angefungua kesi hiyo katika mahakama ya Ardhi. Baada ya kutoa maelezo yote juu ya kesi hiyo, Hakim Nongwa alimtaka Sheikh Ponda kutoa utetezi wake kabla ya kuhumu kutolewa. Wakili wake, Bw. Yahya Njama, alisimama na kutoa utetezi kwa mteja wake ambapo alieleza kuwa Sheikh tayari ameshakaa rumande kwa muda mrefu, pia aliieleza mahakama kuwa Sheikh Ponda hajawahi kutenda kosa lolote na ikizingatiwa kwamba yeye ni kiongozi anayetegemewa na watu anaowaongoza. Baada ya hapo Hakim Victoria Nongwa alitoa hukumu ya kesi ambapo watuhumiwa wote 49 waliachiwa huru na Sheikh Ponda kupewa kifungo cha nje cha masharti ya kutotenda kosa kwa mujibu wa kifungu cha 25 (g) cha sheria ya adhabu za makosa ya jinai. Mara baada ya kutolea hukumu hiyo, mara moja vivumo vya takbir vilisikika nje ya mahakama hiyo kutoka kwa umati mkubwa wa Waislamu waliokuja kushuhudia hukumu hiyo.

4
Na Ibn e Abdul Haq
April 30, 2013 Mtandao wa kupashana habari PTV - Baada ya miaka 12 na vifo vya watu milioni baadaye, Marekani na washirika wake wa NATO wameelezea wazi nia yao ya kuondoa majeshi kutoka Afghanistan mwakani. Vita ya Afghanistan imekuwa mkwamo mtupu, mkiwa kijeshi na katika mahusiano ya kiraia, wakati uharibifu wa maisha, mali na miundombinu ikiwa kubwa sana. Muhimu zaidi, tofauti na madai ya awali, vita ya duniani kote dhidi ya ugaidi haijafanya dunia iwe mahali salama zaidi. Matukio ya ugaidi yamekuwa yakiongezeka, yakizingira nchi moja baada ya nyingine zinazoizunguka Afghanistan. Ili tusisahau, takriban vita vyote vilivyotokea baadaye vinavyopiganwa na Marekani na NATO vimeanzia katika vita iliyoingizwa Afghanistan baada ya 9/11. Sehemu kubwa ya siasa ya nje ya Marekani kuanzia 9/11 imewekwa katika mtazamo kuwa ilishambuliwa na Waislamu siku ile. Mtazamo huu ulitumika, zaidi ya kwingine, kuhalalisha vita nchini Afghanistan na Irak. Ni wazi kuwa kila vita iliyopiganwa na Marekani na washirika wake katika muongo wa kwanza wa karne mpya imejikika katika dhana iliyofuatia 9/11 ya kushambulia kujihami kwanza. Inakubalika kwa kiwango kikubwa sasa kuwa kutumia 9/11 kama msingi wa kushambulia Irak ilikuwa si halali; wateka nyara ndege hakuna aliyekuwa raia wa Irak, hapakuwa na uhusiano wowote wa kikazi kati ya Saddam Hussein na Osama bin Laden, na Irak haikuhusika na mashambulio ya vimelea vya anthrax (kimeta). Lakini bado inaaminika kwa kiasi kikubwa kuwa shambulio la Marekani kwa Irak lilikuwa sawa. Kwa zaidi ya muongo mmoja sasa, mashirika hodhi ya habari duniani yamekuwa yakichomekea riwaya hii ya kutunga kama tukio lisilo na ubishi. Inaelekea kuwa itikadi hii itaingia katika ngazi za juu zaidi wakati warembeshaji wa wanasiasa Marekani wakijaribu kuhalalisha mpango wa kujiondoa Afghanistan na kudhihirisha kuwa vita dhidi ya ugaidi imekuwa ni mafanikio makubwa yasiyo na mfano wake katika historia ya binadamu. Jukwaa limeshaandaliwa kwa mpambano mkali wa kisaikolojia na vyombo vya habari utakaofumuliwa katika hisia za watu wasiojua linaloendelea. Kwa mfano, majuzi tu mwaka 2011, gazeti la New York Times likizungumzia mashambulio ya Marekani dhidi ya Irak kama vita ya kujiamulia, iliita mapambano ya Afghanistan vita ya lazima. Jarida la Time liliviita vita sahihi. Na mwaka 2009, Barack Obama aliripotiwa kusema moja ya sababu za kumaliza ushiriki wetu nchini Irak ni kuwa na askari na raslimali za kuwafuata watu

Makala

JAMADUL THAN 1434, IJUMAA MEI 10-16, 2013


na visumeno vya kukata bodi laini. Ingawa simu hizi zilitaariwa, kama zilivyojumuishwa na Ted Oslon, hazikuwaeleza wateka nyara kuwa walikuwa wanachama wa Al Qaeda, maelezo kuhusu watu hao yalitolewa katika simu za safari nyingine (za ndege zilizotekwa) zilizosema kuwa watekaji ni watu wanaoonekana kama ni wa Mashariki ya Kati na wana sura za Kiislamu. Kutoka simu hizo, kwa hiyo, watu walifahamishwa kuwa wateka nyara walikuwa wanafanana na watu wa Mashariki ya Kati na hata Waislamu. Hata hivyo kulikuwa na tatizo kubwa na simu hizi zilizoripotiwa. Ukizingatia teknolojia iliyokuwepo mwaka 2001, miito ya simu kutoka ndege zikiwa angani zaidi ya futi mia kadhaa, na hasa zinazodumu zaidi ya sekunde chache zilikuwa bado haziwezekani. Na bado simu hizo, baadhi zikiwa zinasemekana zilidumu kwa dakika moja au zaidi, zinasemekana zilipigwa wakati ndege zikiwa juu futi 30,000 au futi 40,000 kutoka ardhini. Tatizo hili lilielezwa na watu kadhaa wanaoaminika, akiwemo mwanasayansi A.K. Dewdney, ambaye kwa miaka mingi aliandika safu katika jarida la Scientic American. 4. Kuwepo kwa watekaji kulithibitishwa na tangazo la redio kutoka American 11? Inaweza kupingwa, kama majibu, kuwa hii siyo kweli, kwa sababu tunajua kuwa ndege ya shirika la American Airways safari ya 11, kwa kuanzia, ilitekwa, hasa kutokana na urushaji wa maelezo hewani ambako sauti ya mmoja wa watekaji inasikika. Kwa mujibu wa Ripoti ya Tume ya 9/11, mwongozaji ndege ardhini wa safari hii alisikia tangazo la redio ambako mtu mmoja anawaambia Inaendelea Uk. 11

AN-NUUR

Je, ni kweli Waislamu waliishambulia Marekani mnamo Septemba 11?


walioko Afghanistan ambao walitushambulia mnamo 9/11. Mwaka jana, baada ya kushinda tena uchaguzi, Barack Obama aliripotiwa kusema vita dhidi ya ugaidi imeshinda, na wahusika wakuu, ikiwa ni pamoja na Osama bin Laden, kukisha mbele ya sheria. Tutaendelea kupigana na Al Qaeda na kuunga mkono harakati za uhuru na haki za binadamu kote duniani, aliongeza, akitoa picha ya kile ambacho Marekani na washirika wake wa NATO wameweka kibindoni kwa dunia kwa jumla na hasa Mashariki ya Kati, katika muda ujao. Mtazamo kuwa Marekani ilishambuliwa na Waislamu mnamo 9/11 imekuwa msingi wa hisia iliyosambaa kote kuwa Uislamu ni dini ambayo imejichimbia katika umwagaji damu na hivyo Waislamu wote wana hatia hadi ithibitishwe vinginevyo. Mtazamo huu kwa hakika ulichangia juhudi za kumwonyesha Obama kama Muislamu, ambazo zilipigwa dongo na katuni iliyoleta zogo katika gamba la jarida la New Yorker la Julai 21. 2008. Pia kumekuwa na ongezeko lililoripotiwa la matukio ya kuuchukia Uislamu, kuanzia matamshi ya chuki dhidi ya jamii za Kiislamu hadi kuitukana Qurani na mtume wa Uislamu. K a m a a m b a v y o ingedhihirishwa na maelezo kuhusu kilichotokea baada ya 9/11, ikiwa ni pamoja na ujasusi, utesaji, urudishaji nchi zenye sifa ya kutesa, majopo ya kijeshi ya kusikiliza kesi, dhana mpya ya Marekani ya vita ya kujihami, na ongezeko lake kubwa la matumizi ya kijeshi, mtazamo kuwa minara pacha ya Kituo cha Biashara cha Kimataifa na Pentagon, makao makuu ya jeshi la Marekani vilishambuliwa na wateka nyara wa Kiislamu umekuwa na athari kubwa sana katika masuala ya kimataifa na ndani ya Marekani. Kwa mwanga wa matukio yaliyofuata inakuwa lazima kukumbushia uhalisi wa tukio la 9/11, ambalo limekuwa kisingizio cha kampeni kubwa inayoitwa vita dhidi ya ugaidi. 1. Mohamed Atta na wateka nyara wengine walikuwa Waislamu wa kweli? Picha ya wateka nyara inayoonyeshwa na Ripoti ya Tume kuhusu shambulio la 9/11 ni kuwa walikuwa waumini wa dhati wa Uislamu. Lakini mchoro huu unapingwa na maelezo kadhaa ya taarifa za magazeti. Gazeti la San Fransisco Chronicle lilisema kuwa Atta na wateka nyara wengine walifanya safari angalau sita kwenda Las Vegas, ambako walishiriki katika mchanganyiko wa raha ambazo zinakatazwa katika Uislamu. Shughuli hizi zilikuwa kinyume na Uislamu kwani, kama anavyoeleza Mkuu wa Mfuko wa Kiislamu wa Nevada, Waislamu wa kweli hawanywi pombe, hawachezi kamari na hawaendi katika klabu za usiku za wanawake kuvua nguo jukwaani. 2. Watawala wana ushahidi halisi wa kuhusika kwa Osama bin Laden kwa 9/11? Wiki mbili baada ya 9/11, Waziri wa Mambo ya Nje Colin Powell, akihojiwa na Tim Russert katika kipindi cha Kutana na Wanahabari, alisema anatarajia katika muda mfupi ujao .... kutoa.... taarifa inayoonyesha kwa uwazi ushahidi tulio nao unaomhusisha (bin Laden) na shambulio hili. Lakini katika mkutano na waandishi wa habari pamoja na Rais Bush kesho yake asubuhi, Powell aligeuza maelezo yake, akisema licha ya kuwa serikali ina habari zinazohakikisha kabisa uhusika wa bin Laden, sehemu yake kubwa ni siri. Kwa mujibu wa Seymour Hersh, akinunuu maofisa wa CIA na Idara ya Sheria, sababu halisi ya kugeuza usemi ilikuwa ni kutokuwepo kwa ushahidi wenye nguvu. Inadaiwa mara kadhaa kuwa uhusika wa bin Laden unathibitishwa na mkanda wa video unaosemekana ulikuwa na maofisa wa kijasusi wa Marekani nchini Afghanistan mwezi Novemba 2001, ambako bin Laden anaonekana kukiri kuhusika katika kupanga mashambulio hayo. Lakini wakinzani, wakionyesha matatizo mengi kuhusu kukiri kwa mkanda wa video wamesema ni feki. Jenerali

Hamid Gul, mkuu wa zamani wa shirika la ujasusi la majeshi ya Pakistan (ISI) alisema nadhani kuna mfananisho na Osama bin Laden. Kusema kweli, mtu huyo katika mkanda wa video hata si mfananisho halisi, kwani ni mzito zaidi na maji ya kunde zaidi ya bin Laden, ana pua pana zaidi, amevaa vito vya thamani, na anaandikia mkono wa kulia. Shirika la upelelezi la FBI, hata hivyo, kwa hali yoyote haliuoni mkanda huu wa video kuwa ushahidi kwa nguvu wa uhusika wa bin Laden kwa 9/11. Hivyo, Ikulu ya Marekani, serikali ya Uingereza, FBI au Ripoti ya Tume ya 9/11 hawajatoa ushahidi kamili kuwa Osama bin Laden alihusika na 9/11. 3. Kulikuwa na ushahidi wa wateka nyara Waislamu kutokana na simu kwenye ndege? Wasomaji wengi wanadhani hapawezi kuwa na shaka kuwa ndege zote zilitekwa na wafuasi wa Al Qaeda, kwa sababu kuwepo kwao na yaliyotokea kwenye denge ziliripotiwa katika simu za abiria na wahudumu wa ndege, na simu za mkononi zikiwa na nafasi muhimu. Simu iliyopata sifa sana ilikuwa ni ya mchambuzi wa habari wa CNN, Barbara Olson kwa mumewe, mwanasheria mkuu Ted Olson. Kwa mujibu wa CNN, aliripoti kuwa mkewe alimwita mara mbili kwenye simu ya mkononi kutoka ndege ya American Airlines safari ya 77 akisema kuwa abiria wote na wahudumu wa ndege walikuwa wamekusanywa nyuma ya ndege na ...wateka nyara wenye visu

SHINDANO LA KIELIMU
Kwa kusherehekea kumbukumbu ya kutimiza miaka kumi na tatu tangu kuanzishwa kwa Darasa la Hadithi za Bwana Mtume (s.a.w.) katika msikiti wa Kipata. Wadhamini wa Darasa hilo wameandaa shindano la kielimu katika somo la Hadithi. Mwanafunzi/msomi yeyote nchini anakaribishwa kushiriki. Zawadi nzuri imetayariishwa kwa mshindi, Inshallah. MAMBO MUHIMU YANAYO MUHUSU MSHIRIKI: 1. Vitabu vya rejea ni; Nukhbah, Bulughul-Maraam na Sunan Abi Daawoud. 2. Waraka wa maswali unapatikana Msikiti wa Kipata kwa Ustaadh Maneno; Naibu wa Imamu. Aidha dukani kwa Ibnu Hazm (jirani ya Msikiti wa Mtoro) kwa Ustaadh Jamali. 3. Waraka huo unatakikana kurejeshwa mapema kabla ya tarehe 8, JUNI, 2013. 4. Washindi wote watatangazwa siku ya Jumamosi ya tarehe 29, JUNI, 2013 katika haa maalumu itakayo fanyika katika Msikiti wa Kipata, Inshallah. Wabillah Tauq

Makala

JAMADUL THAN 1434, IJUMAA MEI 10-16, 2013


wa Iraq. This is the story of James Steele, the veteran of Americas Dirty War in El Salvador. He was in charge of the U.S. advisers who trained notorious Salvadoran paramilitary units to ght left-wing guerrillas. In the course of that civil war, 75,000 people died and over 1 million people became refugees. Steele was chosen by the Bush administration to work with General David Petraeus to organize these paramilitary police commandos. The thousands of commandos that Steele let loose came to be mostly made up of Shia militias, like the Badr Brigades, hungry to take revenge on the Sunni supporters of Saddam Hussein. Inasema taarifa moja ikitoa ufafanuzi juu ya Documentary hiyo inayoelezea hali ya Iraq. (Tazama: Documentary Exposes US Role in Iraq Sectarian Conflict, Executive Producer Maggie OKane) Ninachotaka kusema hapa ni kuwa tukio la Arusha likiwa la Waislamu, Wakristo na wenye dini nyingine lakini wote wakiwa ni Watanzania, jepesi sana kulimaliza kama watu wa Iraq walivyofanikiwa kutulizana kutokana na kulipuliwa msikiti wao mtakatifu. Hata hivyo maadhali palikuwa na watu wa nje wenye agenda zao, na bahati mbaya walikuwa wameikalia nchi hiyo, Iraq haikusalimika. Waliovamia Iraq na kufanya mauwaji ya kutisha walikuwa na agenda zao kubwa ikiwa kudhibiti rasilimali kuu ya nchi hiyo, mafuta. Sisi hapa tuna rasilimali nyingi yakiwemo madini na sasa gesi na mafuta yanayoaminika kuwa yapo. Lakini pia ukirejea nyuma toka Septemba 11, 2001, kumekuwa na jitihada kubwa za kutangaza na kuwaaminisha Watanzania na walimwengu kuwa Tanzania kuna ugaidi. Taarifa kama ile porojo na usanii wa mtoto wa shule ya msingi kufanikiwa kupenya ngome ya ulinzi ya ubalozi mmoja jijini Dar es Salaam akiwa na kigaloni chake cha mafuta ya taa kwa ajili ya kulipua ubalozi huo, zile taarifa za kuingia nchini gaidi wa Kijerumani lakini picha zinatolewa za kwenye internet (sio mhusika kupigwa picha akiwa kakamatwa na Polisi), za akina Fazul kuwa wamezingirwa Dar es Salaam pamoja na zile za kumpakazia ugaidi Profesa Jahazi huku Polisi wakitawanywa kulinda Makanisa; ni ushahidi tosha wa kuwepo kwa juhudi hizi za kutaka kuisajili Tanzania kuwa ni nchi yenye magaidi. Lililo la kweli kama tutataka kusema kweli kama alivyohimiza Kadinali Pengo, agenda hii si yetu maana sioni Tanzania itakavyonufaika kwa kujitangazia ugaidi yenyewe. Sasa tumeambiwa kuwa FBI wapo Arusha kusaidia kuchunguza tukio hili, wasiwasi ni kuwa isije ikawa tukio hili ni katika mkakati ule ule wa kukamilisha mpango wa kuitangazia ugaidi Tanzania. Na hapa ndipo tunapotarajia kuwa vyombo vyetu vya usalama

AN-NUUR

Mapadri wapongezwe Usalama wawe makini


Na Omar Msangi
KAULI za Maaskofu hasa wa Kanisa Katoliki kuwatuliza waumini wao ni za kupongezwa na kuthaminiwa kwa dhati kabisa. Toka matukio yale ya Zanzibar ambapo Padri Ambrose Mkenda alijeruhiwa kwa risasi na lile la kuuliwa Padiri Evaristi Mushi, viongozi hao wa Kanisa Katoliki nchini wamekuwa wakiwatuliza waumini wao, wakiwataka wasichukue hatua za kulipiza kisasi bali wamwelekee Mungu kuwaombea waliofanya uovu huo. Kwa upande mwingine, wamekuwa wakivitaka vyombo vya dola kufanya kazi zao ili kuhakikisha kuwa wahusika wanakamatwa na kuchukuliwa hatua. Akizungumzia suala hili Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycap Kadinali Pengo amesema kuwa tukio hili na lingine lolote lile, liwe kwa nia mbaya au nzuriisiwe sababu ya kuanza mapambano na kuwa chimbuko la ukosefu wa amani katika nchi yetu. Akifafanua zaidi akatoa tahadhari akiwataka waumini wake na Watanzania kwa ujumla, kuwa wasikimbile kujenga dhana kwani dhana haitaleta amani, bali kupatikana kwa amani kutategemea sana ukweli na ukweli kabisa bila kujaribu kupotosha ukweli kwa namna yoyote. Tusipojua kusema ukweli ulivyo hatutaweza kufaulu kuleta amani katika taifa letu. Kwa hiyo pamoja na kuendelea kuwaomba waumini wa Kikatoliki pamoja na watu wenye mapenzi mema kuendelea kumwomba Mwenyezi Mungu arehemu taifa letu. Tuendeleze nia yetu njema ya kusema ukweli, haidhuru ukweli huu unamgusa nani amani ya taifa letu ni jambo la msingi na amani itajengwa tu iwapo kila mtu anayehusika atakuwa tayari kusema ukweli kama ulivyo. Alihitimisha Kadinali Pengo. Niseme kuwa msimamo huu wa kuwatuliza wananchi, umekuwa pia ndio msimamo wa viongozi wa Serikali. Kwamba, watu wajizuiye kunyosheana vidole, bali waviache vyombo vya dola kufanya kazi yao. Hii ni kauli stahiki kabisa. Matukio kama haya, hayahitaji kuhemkwa wala kwenda kasi katika kupitisha maamuzi, bali kufanya uchunguzi wa kina na wa uhakika kujua hasa nini kilitokea, nani alihusika na kwa lengo gani. Nasaha hizi za Kadinali Pengo kwa hakika ni za kuzingatiwa sana, na hasa watu wanaotakiwa kuzichukua kwa uzito zaidi ni vyombo vya usalama vyenye jukumu la kuchunguza jambo hili. Wa pili ni vyombo vya habari. Gazeti la NIPASHE (Mwanga wa Jamii) la Jumatano Mei 8, likiripoti nasaha hizi za Askofu Mkuu Kadinali Pengo, lilisema kuwa kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki amewataka Watanzania kuacha kuwanyoshea kidole Waislamu kuwa ndio wahusika kwa sababu katika watuhumiwa wanaoshikiliwa wamo Wakristo. Watuhumiwa hao wanaoshikiliwa ni Victor Ambrose, Joseph na David. Hata hivyo, gazeti baada ya kueleza kwa ufupi juu ya kauli ya Kadinali Pengo, likarejea taarifa ya kukamatwa Wasaudia. Likasema kwamba Uchunguzi wa NIPASHE umebaini kuwa watuhumiwa hao (Waarabu) waliingia nchini kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) Mei 4, mwaka huu, na baada ya tukio la mlipuko wa bomu hilo walianza safari ya kutoroka nchini kupitia mpaka wa Tanzania na Kenya wa Namanga. KUTOROKA. Ukisema AKITOROKA baada ya mlipuko wa bomu, unachosema ni kuwa anatoroka baada ya kulipua bomu hilo. Anahusika! Mpaka sasa vyombo vya usalama havijasema lolote juu ya uchunguzi wao wala watuhumiwa waliokamatwa hawajakishwa mahakamani na ushahidi wa kuwahusisha na tukio hilo, ukawasilishwa. Sasa habari hizi kwamba wanatoroka baada ya shambulio, lengo lake nini? Je, kwa mtindo huu, ukweli utajulikana kama alivyosema na kusisitiza Kadinalin Pengo? Kama tunaanza na kujiaminisha akili zetu kuwa wahusika ni akina fulani, je, uchunguzi ukionyesha vinginevyo, tutakuwa tayari kusema ukweli huo bila kujali unamgusa nani? Muadhama Polycap Pengo anasema kuwa amani ya taifa letu ni jambo la msingi na amani itajengwa tu iwapo kila mtu anayehusika atakuwa tayari kusema ukweli kama ulivyo. Februari 22, 2006 Msikiti wa Kale uliopo Samarra, wenye historia takatifu, hasa kwa Madhehebu ya Shia kule Iraq (alAskari Mosque-wenye kaburi la Imam Ali al-Hadi, aliyefariki mwaka 868 AD, ulilipuliwa kwa bomu na sehemu ya Msikiti huo ukaharibiwa kabisa. Muda mfupi tu baada ya tukio hilo, viongozi mbalimbali wa Kiislamu duniani, Shia na Sunni, walitoa kuli za kuwatuliza Waislamu, wasije kulipizana kisasi ikawa vita baina ya Waislamu (Sunni) kwa Waislamu (Shia). Kwa

Bomu Kanisani Arusha:

upande mwingine, vyombo mbalimbali vya habari hasa vya Ulaya, vilitabiri kuwa tukio hilo ilikuwa ndio mwanzo wa vita ya wenyewe kwa wenyewe Iraq. Kiongozi na Ulamaa mashuhuri wa Shia Ali alHusayn Al-Sistani katika jambo lisilo la kawaida kwake, alitokea katika Televisheni akiwataka waumini na wafuasi wake kutulia. Naye Sheikh Muqtada Al-Sadri, alikatiza ziara yake Lebanon na kurejea Iraq ambapo aliwataka wafuasi wake, na hasa kikosi chenye silaha cha Washia kuhakikisha kuwa kinalinda Misikiti ya Wasuni isije ikashambuliwa na mtu yeyote (Washia wenye hasira). Kwa upande mwingine, Masheikh wa Kisuni baada ya kulani shambulio hilo, waliendesha kampeni kubwa ya kutuliza hali ikiwa ni pamoja na kufanya mazungumzo ya mara kwa mara na Masheikh wa Kishia. Kwa hakika vitabu vya historia vimeweka kumbukumbu hii wazi kabisa kwamba viongozi wa kidini wa Iraqi walifanikiwa kuwaongoza wananchi wa Iraq wakafanikiwa kuzuiya kulipuka kwa matendo ya kulipizana visasi ambayo yangeleta vita ya wenyewe kwa wenyewe. Lakini swali ni, je, baada ya Masheikh kufanikiwa kutuliza waumini wao na wananchi kwa ujumla katika tukio hilo la kulipuliwa Msikiti wa al-Askari, Iraq ilitulia? Jibu ni kuwa haikutulia. Ingawa Masheikh walifanikiwa kutuliza waumini wao katika tukio hilo, lakini masiku yaliyofuatia yalishuhudia umwagaji damu wa kutisha ambapo Misikiti ilikuwa ikilipuliwa, waumini wa pande zote mbili wakiuliwa, ikawa hasa ni umwagaji damu baina ya Washia na Wasuni. Ingekuwa Tanzania ingekuwa ni ulipuaji Misikiti na Makanisa huku damu ikimwagika na roho zikiangamia kwa maelfu. Taarifa mbalimbali zinaonyesha kuwa watu waliouliwa katika mashambulizi haya yaliyoacha Iraq ikiwa nchi iliyogawika mapande mawili, zinasema kuwa watu zaidi ya 3,000 walikuwa wakiuliwa kila mwezi. Documentary moja iliyotolewa hivi karibuni, imefichua jinsi wavamizi wa Iraq walivyochochea mgogoro baina ya Washia na Wasuni, baada ya kuona kuwa wananchi wameshika silaha wamekuja juu kupinga uvamizi. Vilianzishwa vikosi vya Washia vya kufanya mashambulizi na mauwaji dhidi ya Wasuni. Vikosi na makundi ya kihalifu yakapewa silaha, mafunzo na fedha. Matokeo yake ni janga kwa wananchi

Polycap Kadinali Pengo vifanye kazi yao kwa umakini mkubwa na viseme kweli bila kujali nani anahusika. Katika kitabu A Plan to Divide and Destroy the Theology cha Dr. Michael Brant anaelezwa jinsi mabeberu walivyopatana kuweka mradi kabambe wa kuwagawa Waislamu na kupandikiza chuki miongoni mwao (Sunni na Shia) katika zile nchi zenye Waislamu wengi kama Pakistan. Baada ya kikao cha makachero wa nchi za kibeberu kilichofanyika mwaka 1983, Uingereza ikiwa kinara kwa sababu ina uozefu kwa sababu ilitawala nchi nyingi za Kiislamu, Dr. Brant anasema kuwa ulianzishwa mradi wa kuwashughulikia Waislamu katika nchi za Kiislamu uliotengewa kiasi cha Dola milioni 4 kila mwaka. Inaelezwa kuwa lengo ni kuhakikisha kuwa Waislamu hawawi kipingamizi mahali popote ambapo mabeberu watataka kuingia kuvuna rasilimali na masilahi yake mengine. It was calculated that by 2010 the situation between Shias and Sunnis would be so bad that USA would be able to capitalize upon it to its maximum benet. Also, with its stooges in already in place at the top theocratic positions in Sunni factions and the new breed of Shia scholars reaching the top positions (nurtured by the CIA from the start), US wouldnt have to sacrice a lot. Huo ni muhutasari wa yaliyotarajiwa kuwa manufaa watakayopata mabeberu kutokana na mradi huo. Hapana shaka hali tunayoiona na kuisikia Pakistan, Iraq na kwingineko, ni matokeo ya mkakati huu uliowekwa mwaka 1983. La kuzingatia hapa ni kuwa kama kutakuwa na watu wa nje ambao wanadhani watanufaika kwa namna yoyote iwapo Watanzania watachukiana na kupambana wenyewe kwa wenyewe, hawataingia kwa gia ya Wasuni na Washia wala Wasukuma na Wachaga. Uchochoro mwepesi ni wa Waislamu Vs Wakristo. Kwa hiyo, tunapochunguza suala hili, ni lazima tuzame kwa mapana na marefu. Kama ni mtu kawehuka tu tujue, lakini tujue kwa uhakika. Kama ni mtu mwenye masilahi ya kisiasa au aliyetumiwa na watu wengine wa ndani kwa masilahi Fulani, tujue na tujue pia kwa uhakika. Lakini pia kama kuna uhusiano na watu wa nje tujue na tujue kwa uhakika pia.

6
Na Omar Msangi
NI lazima wawe Waarabu. Isingekuwa jambo la kueleweka iw a p o w a t u wa nje waliokamatwa wakituhumiwa kuhusika na shambulio la bomu Kanisani Arusha, ingesemwa kuwa ni Wajerumani, Wataliano au Wamarekani! Akitoa taarifa fupi ya awali Bungeni Jumanne wiki hii, Waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda alisema kuwa Waarabu wanaoshikiliwa walikamatwa tu katika utaratibu wa kawaida wa kutaka kujiridhisha kuwa hawahusiki kwa namna yoyote. Akifafanua akasema kuwa Wa a r a b u h a o w a l i k u w a wakisafiri kwenda Nairobi kwa njia ya barabara, lakini kwa vile mipaka ilikuwa imefungwa, haikuwa rahisi kwao kupita. Walikamatwa ili wahojiwe. Labda swali hapa laweza kuwa, kama mipaka ilikuwa imefungwa ili kuwachunguza watu wote wanaopita, Jumapili siku ya tukio hilo hawakuwahi kupita Wazungu? Kwa nini wakamatwe Waarabu peke yao? Kabla ya kutokea vurugu wilayani Geita zilizosababisha kuuliwa kiongozi mmoja wa kidini, palifanyika mhadhara mkubwa wa Kikristo ambapo Wakristo walihamasishwa juu ya suala la kuchinja. Mhadhara ule ndio uliozua balaa kwa sababu Wakristo walipotoka pale walikwenda kutekeleza waliyoambiwa jambo lililoleta vurugu. Iliwahi kuarifiwa katika baadhi ya vyombo vya habari kuwa katika mhadhara ule palikuwa na Wazungu, watu kutoka nje. Serikali mpaka leo haikuwahi kusema lolote juu ya uwezekano wa Wazungu wale kuhusika kuwachochea Wakristo wa Geita. Swali ni je, mhadhara ule ungekuwa ni wa Waislamu na wangekuwepo Waarabu, hali ingekuwaje? Je, Serikali ingekuwa kimya mpaka leo? Isingesema lolote kuhusiana na wageni wale? Mwezi Februari mwaka huu 2013 kundi kubwa la Wazungu lilikuwa limesambaa katika Wilaya ya Same. Wa k i w a k a t i k a v i k u n d i vidogo vidogo walikuwa na Kamera za Video wakipiga picha maeneo mbalimbali kuanzia kule Kiwanja, Stesheni, Kavambughu, Majevu, Mwembe, Same mjini na maeneo mengine. Japo wananchi walikuwa wakijiuliza, Wazungu wale walikuwa na lengo gani, hasa walivyokuwa wakichukua tahadhari wakigundua kuwa kuna mtu anawafuatilia, lakini hapakuwa na namna yoyote ilionekana Serikali ikishughulishwa na Wazungu hao. Inawezekana walikuwa washajieleza kwa mamlaka husika na serikali ilishajua nini wanafanya na iliridhika. Hatujui. Lakini ni mara nyingi tumeona Masheikh wa

MAKALA

JAMADUL THAN 1434, IJUMAA MEI 10-16, 2013


akachaguliwa kuwa ndiye gaidi wa leo. Propaganda imepigwa ikakolea kwa mtindo ule ule wa ki- Operation Northwoods, walimwengu wanaaminishwa kuwa ukimuona Muarabu mahali popote ni gaidi. Ndio maana katika tukio hili haikushangaza kuwa watu wa nje waliokamatwa ni Waarabu. Na ni kwa sababu ya propaganda hizi za kumezeshwa na mabeberu, tulipiga sana kelele kukataa mitambo ya Dowans tukisema kuwa ni mibovu, tukahiyari kukaa kizani. Lakini walipokuja Wa z u n g u w a S y m b i o n , wamechukua mitambo ile ile ya Dowans na kuisia kuwa ni mizuri. Sasa wanatuuzia umeme. Kimyaa, hakuna mbunge wala mwandishi anayesema kitu. Kwa chuki za kulishwa, tumekataa kununua mitambo ya Dowans kutoka mkononi mwa Muarabu Brigedia Jenerali Mstaafu Mohammed Yahya Al Adawi ambapo tungekuwa tunazalisha umeme wenyewe na kudhibiti bei ya umeme. Tu k a p i g a k e l el e k u w a n i mitambo chakavu. Tukaizima tukakaa kizani. Kinyume chake alipoinunua Mzungu Paul Hinks, sisi hao hao tukaisifia kuwa ni mitambo safi na aliyekuwa Ka tibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, David Jairo, akatangaza kuwa Serikali itawapa kila msaada akina Paul na kampuni yao ya Symbion kuhakikisha kuwa wanazalisha umeme kwa kutumia mitambo ya Dowans na kutuuzia. Na hawa kwa vile ni watu wa nje, tena kutoka kule anakotokea Economic Hit Man, John Perkins, wakitaka kutuhujumu wanaweza kutishia kuizima kama shinikizo la kuwatekelezea jambo fulani. Lakini pili, watapandisha bei watakavyo wakisingizia gharama za uzalishaji na hatutakuwa na la kusema. Hii ndiyo gaharama ya kufanya mambo kwa kutumia akili iliyoathiriwa na propaganda za mabebebru. Hoja hapa sio kuhoji kwa nini vyombo vya usalama vimewatuhumu Waarabu au visikamate Muarabu anapohisiwa kuwa muhalifu. Lakini mtizamo unaoonekana kujengeka nchini, kwa wananchi na kwa viongozi, ni ule unaowaona Waarabu/ Waislamu kuwa ni wahalifu kwa hiyo wanachotakiwa kufanya ni kuthibitisha kuwa wao sio magaidi. Kwa upande mwingine, Mzungu anaonekana mtu mwema, mstaarabu na anayewatakia mema Watanzania. Na hii inawezekana kuwa ndio sababu hata wanapotujia na mikataba ya kutupunja katika uchimbaji madini hatuhoji. Tunakubali tu. Tukiwa na mtizamo hasi juu ya Waarabu, hata pale watakapo patikana wawekezaji makini katika miradi mbalimbali ambayo ina manufaa makubwa kwa wananchi, tutaikwamisha. Au hata tukipata misaada isiyo na riba kama ile ya Benki ya Kiislamu (IDB) na OIC, tutaikataa na kukimbilia kujitia katika kitanzi wanachotusokotea Economic Hit Men.

AN-NUUR

Mh. Pinda, Namanga walipita Waarabu tu?


Siku hiyo hawakusari Wazungu? Au ndiyo yale ya Dowans Vs Symbion!
kuwa: the purpose of U.S. low intensity warfare was to sustain United States control over much of the worlds resources against the efforts of the have-nots who are attempting to overturn the established political and economic order. (Tazama The Legitimate Claims of National Security Foreign Affairs, April 1974Taylor warns that As the leading have power, we may expect to have to ght to protect our national valuables against envious have nots.) Akimaanisha kuwa ilikuwa lazima Marekani kuingia vitani kwa gharama yoyote kuhakikisha kuwa inalinda fursa yake ya kupora mali katika nchi mbalimbali duniani. Hata hivyo, ili kupata kuungwa mkono na wananchi wake, Marekani ilihitaji kupiga propaganda kuwatisha wananchi kuwa Makomunisti ni maadui wakubwa na kwamba wasipovamiwa na kupigwa huko huko kwao, wangeweza kuvamia Marekani na kufanya vitendo vya kigaidi. I think the most critical special operations mission we have today is to persuade the American public that the Communists are out to get us. The task is mind-boggling. If we win the war of ideas, we will win everything else. (Tazama:Special operations in US strategy National Defense University, National Strategy Information Center, 1984) Alisema mmoja wa Makamanda wa Kijeshi (Deputy Assistant Secretary of the Air Force), J. Michael Kelly akionyesha kuwa kwanza ilikuwa ikihitajika propaganda kubwa kuwafanya wananchi wa Marekani (na kisha walimwengu) waone kuwa Marekani ina haki ya kuingia Amerika ya Kusini kijeshi. Ukisikia Operation Northwoods au Operation Mongoose, ni katika mbinu chafu zilizoandaliwa kupiga propaganga mpaka Wamarekani wakaaminishwa kuwa Wakomunsiti ni magaidi hatari kwa Marekani. Baada ya ukomunisti kuanguka, limetafutwa jinamizi jingine, lakini lengo likiwa lile lile: to sustain United States control over much of the worlds resources against the efforts of the have-nots who are attempting to overturn the established political and economic order. Muarabu/Muislamu

Waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda


Kiislamu kutoka nchi za nje wakibughudhiwa na mamlaka za nchi japo waliingia nchini kihalali, wana viza na wameandamana na wenyeji wanaotambulika. Zahama hii imewakuta sana watu wa Tabligh kutoka nchi za Kiarabu na Asia. Taarifa hii ya Waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda japo yeye mwenyewe alisisitiza wakati akitoa taarifa hiyo kwamba watu waache chuki za kidini, lakini taarifa yake mwenyewe ina harufu fulani inayoashiria mtizamo hasi wa Serikali juu ya Waarabu. Na ndiyo tunayoyaona kwa baadhi ya Wakuu wa Mikoa/Wilaya na Makamanda wa Polisi. Yupo Polisi mmoja mwaka 2008 aliwahi kumtia nguvuni na kumtimua mtu mmoja aliyekuwa katika mkutano wa hadhara uliokuwa ukihutubiwa na Makamu wa Rais kwa sababu mtu huyo alikuwa amevaa kanzu, koa na kanzu. Ilielezwa kuwa Polisi huyo alimtuhumu mtu huyo kuwa ni gaidi. Lililo wazi kabisa ni kuwa hii sio akili yetu. Hii kukimbilia kukamata Waarabu na kuwatilia shaka wananchi wenzetu waliovaa kanzu na koa, sio akili yetu kabisa. Ni akili ya kupewa. Kanzu na kofia hizi ndio zilizokuwa zimejazana katika mikutano ya TANU wakati wa kupigania uhuru. Imekuwaje leo kanzu hizi zimekuwa alama ya ugaidi? Kanzu na koa hizi ndio zilizompokea Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam na kumkaribisha katika harakati za kupigania uhuru. Akashonewa suruali, akapewa nyumba, gari na mshahara. Vipi leo Polisi anamtimua mwananchi aliyevaa kanzu katika mkutano wa kisiasa kwa kumdhania kuwa ni gaidi? Kwa hakika hii sio akili yetu kabisa. Wakati rais Ronald Reagan anaingia madarakani aliweka mpango kabambe kuhakikisha kuwa siasa za ukombozi katika Amerika ya Kati na Kusini, hazifanikiwi kwa sababu zilionekana kuwa hatari kwa masilahi ya Marekani. Siasa hizo za ukombozi zilikuwa zikilenga kungoa tawala za kidikiteta zilizokuwa vibaraka wa Marekani walioachia rasilimali za nchi hizo zikiporwa huku wananchi wakibaki masikini. Harakati hizo kwa wakati ule zilichukua itikadi za ki-Maxisti (Ukomunisti) kama ilivyokuwa Cuba. Kama alivyosema Mhariri wa jarida la Boston Globe, Randolph Ryan, Serikali ya Marekani iliona kuwa harakati na moyo wa ukombozi, ulikuwa kama kirusi , virus, ambacho ni lazima kipigwe stop kisisambae. Kwa sababu hiyo ikapangwa mikakati ya kijeshi kuhakikisha kuwa vikundi vya ukombozi na wanasiasa wenye mawazo ya kizalendo wanashughulikiwa. Generali Maxwell Taylor (Chairman of the Joint Chiefs of Staff), akieleza lengo la kuhakikisha kuwa wazalendo wanaopinga ubeberu wa Marekani wanashughulikiwa, alisema

Makala

JAMADUL THAN 1434, IJUMAA MEI 10-16, 2013

AN-NUUR

8
Na Omar Msangi
NCHI yetu inapita katika kipindi tete na lau hatutakuwa makini, tutatumbukia katika janga ambalo huenda tukaona tu mlango wa kuingilia, lakini itakuwa tabu kuona wa kutokea hata kama tutataka kutoka. Lakini kabla ya kwenda mbele niungane kwanza na Watanzania wote kulani tukio lililotokea Arusha ambapo inatuhumiwa kuwa mtu mmoja alirusha bomu kanisani lililoua mpaka sasa watu watatu na wengine wengi kujeruhiwa. Shambulio hilo lilifanyika katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi, Parokia ya Olasiti, jijini Arusha. Taarifa za awali ambazo zishatolewa na Serikali zinafahamisha kuwa kijana mmoja anayejulikana kwa jina la Victor Ambrose anashikiliwa na Polisi akituhumiwa kurusha bomu hilo. Vijana wengine wa Kitanzania waliotajwa (kwa jina moja tu) kukamatwa ni Joseph na David. Aidha wanashikiliwa pia raia wanne kutoka nchi za Kiarabu. Tunaambiwa kuwa watu hao wa Kiarabu waliingia nchini Jumamosi usiku kwa ndege kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), na kwamba walitaka kuondoka Jumapili kwa gari kuelekea Kenya kwa njia ya barabara kupitia Namanga. Hadi sasa taarifa ya Polisi haijafafanua ni kwa nini Waarabu hao wamekamatwa kwa maana kuwa ni sababu gani zilizopelekea watuhumiwe kuhusika na tukio hilo. Hata hivyo taarifa ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulugo inasema kuwa, Victor Ambrose ndiye aliyewataja watuhumiwa hao Waarabu na kuelekeza walipo. Mulugo alisema raia hao wa Saudi Arabia waliingia nchini kupitia kiwanja cha Kimataifa cha Kilimanjaro (KIA) Mei 4, na Mei 6, walikuwa wakitoroka nchini kupitia mpaka wa Namanga wakielekea nchini Kenya. Liliripoti gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, Mei 7, 2013. Pengine swali la kuuliza hapa ni je, Waarabu hao walikuwa WAKITOROKA au wakienda Kenya (Nairobi) kwa njia ya barabara? Na kama Victor Ambrose ndiye aliyewataja, huyu Victor ni nani na nini uhusiano wake na Waarabu hao? Awali gazeti la Mwananchi likiripoti habari hizi, likimnukuu msemaji wa wa Kanisa Katoliki, Jimbo Kuu la Arusha, Padri Festus Mangwangi, lilisema kuwa mtu aliyerusha bomu hilo alikuwa amevaa Kanzu. Hiyo ilikuwa Jumatatu, Mei 6, 2013. Katika kuripoti taarifa ya Serikali juu ya watuhumiwa likasema, Wasaudia wanne mbaroni, FBI watua. Likimnukuu Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mwananchi likasema kuwa Waarabu hao waliingia nchini Jumamosi na siku iliyofuata ndipo kukatokea ulipuaji huo. Na kwamba lengo la shambulizi hilo lilikuwa kumdhuru Askofu Padilla. Lilisema Mwananchi na kumnukuu Mkuu huyo wa Mkoa akisema kuwa Victor Calisti Ambrose ndie aliyesaidia kuwapata watu hao wa Saudi Arabia.

Makala

JAMADUL THAN 1434, IJUMAA MEI 10-16, 2013


kama ile iliyojitokeza katika fujo za Mbagala watashindwa kutia moto kanisa ili wasingiziwe Waislamu? Kwa bahati nzuri pengine kwa wenye mradi huu, na kwa upande mwingine kwa bahati mbaya kwa taifa na nchi, badala ya Serikali kukomesha habari hizi za uzushi za kuwasingizia Waislamu, viongozi takribani wote na wanasiasa, nao wamejiunga na akina Askofu David Mwasota wakiimba wimbo huu kuwa makanisa yanachomwa! Serikali inasema kuwa imeanza kuwachukulia hatua watu wanaosambaza taarifa za chuki na za kuwagawa Watanzania kwa misingi ya kidini. Ni kweli wapo vijana na Sheikh aliyekamatwa Tanga kwa kudaiwa kuwa anasambaza kanda za chuki akawekwa ndani na kunyimwa dhamana. Je, ni hatua gani zilizochukuliwa juu ya hawa wanaosambaza habari za urongo kuwa Waislamu wamechoma makanisa Yombo na wakawataka Wakristo wajihami kwa visu, mapanga, mishale na mikuki? Au kuwataka watu washike mapanga, visu, mikuki na mishale dhidi ya Waislamu, sio uchochezi? Kama ni uchochezi, je, unakoma kuwa uchochezi unapokuwa umetamkwa na Askofu? Siku ya Ijumaa Oktoba 19, 2013, gazeti moja liliibuka na kichwa cha habari katika ukurasa wake wa mbele kikisema: Uamsho watua Dar kumuunga mkono Ponda. Kisha katika vichwa vidogo vya habari likasema: Wawasili kinyemela kwa boti za kukodi. Wapania kuongeza nguvu kuchoma makanisa. Polisi wasema wanatikisa kiberiti, watawakabili. Katika ufunguzi wa habari hiyo gazeti likasema kuwa: Wafuasi 150 wa taasisi ya Uamsho wamekodi boti tatu kutoka Zanzibar kuelekea Dar es Salaam na zimepangiwa (kukia) Bagamoyo na Mbweni kwa siku tofauti. Kisha gazeti hilo likasema kuwa watu hao wamepewa maelekezo na viongozi wao (majina tunayahifadhai) ya kuhakikisha wanaendeleza falsafa za kuteketeza makanisa na majumba ya Wakristo huku Tanzania Bara bila kuacha vielelezo wala ushahidi. Likiendelea gazeti hilo la kila wiki likasema kuwa, ufuatiliaji wa nyendo za kundi hili umebaini kwamba baadhi yao wametua Dar siku ya Alhamisi kwa jahazi maalum (jina tunalihifadhi) huko Mbweni na kukodi daladala ili waanze shughuli waliyotumwa. Likinukuu chanzo chake cha habari liliyemuita msiri wao ambaye ni katika hao walioandaliwa kuchoma makanisa likasema: Tumefika watu 45 wakiwemo wanawake 12 waliopewa mafunzo maalum ya judo, karate, miereka na kujichanganya mitaani bila kutiliwa shaka, na kituo cha kwanza tutatia kambi eneo la Tandika Yombo. Katika kumalizia habari yake gazeti hilo likasema: Habari tulizozipata jana wakati gazeti hili linaenda mitamboni zimedai kuwa baadhi ya watu wenye sampuli ya wafuasi wa Uamsho wanaonekana huko Tandika wakivinjari karibu na makanisa na vilabu vya kuuzia pombe. Likaongeza kuwa Jeshi la Polisi limewatoa wasiwasi Inaendelea Uk. 9

AN-NUUR

Tuambiwe ukweli nani kalipua bomu


Wakati Mkuu wa Mkoa wa Arusha Bwana Mulugo anatoa taarifa hii, vyombo vya usalama vilikuwa havijafanya uchunguzi na kutoa taarifa. Yeye alijuaje kuwa mrusha bomu alikuwa na lengo la kumdhuru Balozi wa Papa, Askofu Francisco Padilla. Taarifa hii ya Mkuu wa Mkoa Bwana Magesa Mulugo, ni tofauti kabisa na alichosema Mheshimiwa Waziri Mkuu, Mheshimiwa Mizengo Pinda ambaye alisema kuwa wageni hao wenye asili ya Kiarabu walikuwa wakienda Nairobi kwa njia ya barabara na hawakuweza kupita kwa urahisi kwa sababu barabara zilikuwa zishafungwa kwa hiyo walikamatwa kwa nia ya kutaka kujiridhisha na kwamba wanaendelea kuhojiwa (ila hadi sasa hakuna Mzungu aliyekamatwa katika Wazungu ambao wanavuka kila uchao kwenda Kenya kupitia Namanga). Kufuatia tukio hilo, Waziri wa Mambo ya Ndani, Mheshimiwa Dr. Emannuel Nchimbi amesema kuwa, Serikali itachukua hatua kali kwa wote watakaobainika kuhusika na tukio hilo. Lakini akawaonya pia baadhi ya wanasiasa na viongozi ambao amesema kuwa wanatumia nafasi zao kufanya uchochezi wa kidini. Serikali isilaumiwe kwa hatua kali za kisheria itakayochukua dhidi ya viongozi wa aina hii ambao masilahi yao ni muhimu kuliko maisha ya Watanzania. Amesema Mheshimiwa Dkt. Nchimbi. Amesema kweli Dkt. Nchimbi kwamba Serikali haina budi kuwachukulia hatua kali wanasiasa au mtu yeyote anayechochea chuki za kidini nchini. Hata hivyo, tunachotakiwa kuzingati ni kama alivyosema Mheshimiwa Waziri Samia Suluhu, ni lazima hatua hizo zitanguliwe na uchunguzi wa kina na kweli katika kubaini ukweli. Ni lazima tuwe na yakini, nini kimetokea, nani anahusika na kwa lengo gani. Tahadhari na angalizo hili la Mheshimiwa Suluhu ni la muhimu sana maana kama hatutakuwa makini, tunaweza kuchukua hatua ambazo badala ya kuleta ufumbuzi tutajikuta tukilitumbukiza Taifa katika maafa zaidi. Katika nchi ambazo zimepitia katika historia chungu ya vita ya wenyewe kwa wenyewe iliyoleta maafa makubwa ikiwa ni pamoja na mauwaji ya watu wasiopungua 75, 000, ni pamoja na El Salvador. Katika jumla ya mauwaji yaliyotikisa nchi hiyo, kuchochea mgogoro, vita na mauwaji zaidi, ni mauwaji ya wanakijiji 200 pale El Mozote wengi wao wakiwa wanawake na watoto mwaka 1980. Mauwaji mengine ni yale ya askofu Mkuu Oscar Arnulfo Romero pamoja na Wachungaji 6 wa ki-Jesuit na watumishi wao. Katika matukio yote haya ilipigwa propaganda kuwa wahusika ni wapinzani wa

Wapo wapi Uamsho waliotua Dar kuchoma Makanisa Wabunge wasicharuke tu, wahoji mambo ya msingi Kasema kweli Samia Suluhu, tuwe na yakini kwanza
Serikali ambapo katika baadhi ya matukio zilikuwa zikiachwa alama na vidhibiti ambavyo kwa namna yoyote vitaonyesha kuwa wahusika ni waasi wa kundi la Farabundo Mart National Liberation Front (FMLN). Hata hivyo uchunguzi uliokuja kufanywa kiasi miaka 31 baadae ulikuja kubaini kuwa waliohusika na mauwaji hayo walikuwa maosa wa Jeshi la Serikali na kwamba walitumiwa na mataifa ya nje ambao walikuwa wakitaka kuzima sauti za wananchi wazalendo ambao walikuwa wakipinga ubeberu wa mataifa hayo. Mataifa hayo ya kibeberu yanatajwa pia kwamba pamoja na kuwatumia wanajeshi wa Serikali kuzima harakati za wananchi wazalendo, walikuwa pia wakitumia vikundi vya kigaidi (armed rebels) kuuwa viongozi wa dini na wa Serikali. Kwa upande mwingine taarifa hiyo inataja pia jinsi Mahakama Kuu (Supreme Court) ya El Salvador ilivyotumiwa kuhakikisha kuwa watuhumniwa wakuu, ambao walikuwa makamanda wa jeshi, waliokimbilia nchi za nje, hawakamatwi na kurejeshwa nchini El Salvador kushitakiwa. Learn from History, 31st Anniversary of the Assassination of Archbishop Oscar Romero, ni taarifa iliyochapishwa kutokana na yaliyonukuliwa kutoka National Security Archive Electronic Briefing Book No. 339. Taarifa hiyo kama ilivyoandikwa na kuwekwa katika mtandao na Kate Doyle na Emily Willard (March 23, 2011), inafafanua jinsi maosa kadhaa wa kijeshi (Captains) Alvaro Rafael Saravia, Eduardo Avila, na Fernando (El Negro) Sagrera, walivyohusika katika kumuuwa Askofu Mkuu Romero. H o w We K i l l e d t h e Archbishop, ni taarifa ndefu iliyonukuliwa ikinukuu mahojiano ya Alvaro Saravia akielezea walivyohusika kumuuwa Askofu Mkuu huyo. Mauwaji ambayo ni kama yalitia Petroli katika mgogoro wa El Salvador. Watu wakazidi kuuwana. Lakini muhimu kufahamu hapa ni kuwa waliohusika kumuuwa Askofu Mkuu Romero ni maofisa katika jeshi na walitumiwa na mabeberu waliotaka kulinda masilahi yao katika Amerika ya Kusini. Kama alivyosema Mheshimiwa Mnyaa (MB), katika suala hili tusiangalie tu Waislamu na Wakristo, kwa maana kuwa tusitizame ndani tu. Akasema kuwa tutizame isije ikawa kuna chokochoko za kutoka nje. Tukumbuke kuwa kuna Balozi mmoja aliwahi kusimama katika jukwaa la kidini na kuwataka Wakristo wawe macho na Waislamu. Kwa maana nyingine alikuwa akiwaambia Wakristo wa Tanzania wawatizame Waislamu kama maadui zao. Yupo Bwana mmoja karejea

hivi majuzi kutoka safari yake ya kikazi Kilwa. Nilipokuwa nazungumza naye Jumatatu wiki hii akasema kuwa alikutana na mama mmoja akiwa anahadithia jinsi walivyotahadharishwa na Padiri wao Kanisani kuwa (eti) wawe macho maana wale watu wanaochoma Makanisa wameingia Kilwa. Hapa lazima tujiulize, hizi taarifa kuwa kuna kikosi cha Waislamu waliodhamiria kuchoma makanisa zimetoka wapi? Je, nini lengo la viongozi wa makanisa kusambaza habari hizi? Je, vyombo vya usalama vina taarifa hizi na hatua gani zimechukuliwa? Ukiacha taarifa za mama huyu wa Kilwa, lakini upo waraka maalum wa Makanisa ambapo ilidaiwa kuwa kuna kikosi cha Waislamu kimeingia Mbeya kwa ajili ya kuchoma makanisa. Akitoa taarifa hiyo kwa vyombo vya habari Desemba mwaka jana, Katibu Mkuu wa Baraza la Makanisa ya Kipentekoste Tanzania (PCT), Askofu David Mwasota aliwataka Wakristo kujitayarisha kupambana na Waislamu aliodai kuwa wameunda vikosi vya kuchoma makanisa. Akawataka kujihami kwa visu, mikuki na mishale. Likielekea mitamboni, bado uchomaji moto makanisa jijini Dar es Salaam ulikuwa ukiendelea ambapo Kanisa la Kipentekoste la Faraja International Yombo Dovya lilikuwa likiteketea huku jingine la KKKT Yombo Dovya nalo likinusurika kuteketezwa na watu wanaojiita wanaharakati wa Kiislamu. Mlinzi wa Kanisa hilo aliripotiwa kujeruhiwa. Hivi ndivyo lilivyoripoti gazeti la Msema Kweli likisherehesha taarifa ya Katibu Mkuu wa PCT, Askofu David Mwasota. Lililo la uhakika ni kuwa vyombo vya usalama vina habari na barua hiyo ya wachungaji. Swali ni je, madai hayo kuwa kuna kikosi cha Waislamu wachoma makanisa kilichoingia Mbeya zilikuwa za kweli? Kama jibu ni ndio, serikali ilichukua hatua gani dhidi ya watu hao? Mbona mpaka sasa hatujasikia kuwa kuna watu walikamatwa wakienda Mbeya kuchoma makanisa? Kama taarifa hazikuwa sahihi, serikali ilichukua hatua gani dhidi ya wanaosambaza uzushi na taarifa hizo za kichochezi? Makanisa yaliyodaiwa kuchomwa Yombo, ulikuwa ni uzushi mtupu. Hakukuwa na Kanisa lililochomwa moto. Swali ni je, hatua gani zilichukuliwa kwa waliosambaza habari hizo za uwongo? Je, hatudhani kuwa kwa kutokukemea taarifa kama hizo na kuwachukulia hatua wahusika, tunasababisha ziaminike na hivyo kuwafanya Wakristo kuwachukia Waislamu? Inaonyesha kuwa kuna watu wamekamia kuona kuwa Waislamu wanasajiliwa kama wahalifu wachoma makanisa na Serikali inakuwa upande wao kwa huruma. Je, katika mazingira haya, watu hawa wakipata fursa

9
kwenye madrasa juu ya heshima na adabu yako pale pale. Hayo ni matakwa ya Quran na Hadith. Ingawa kweli Waislamu wa leo wameamua kuwa w amechoka kuonewa, ile khulka yao ya adabu bado imo na hujitokeza hata pale ambapo wao wameamua kuchukua hatua za kujaribu kukomesha kuonewa huko. Itakumbukwa kwamba katika kadhia ile ya kuvunja mabucha ya nyama ya nguruwe Waislamu hawakuzuka tu kuanza kuyavunja na kubomoa, maduka yale. Kwa heshima kubw a kabisa walipeleka malalamiko yao kwa viongozi wanaohusika ili wachukue hatua zinazostahili. Sheria za nchi mpaka leo haziruhusu uuzaji wa nyama ya nguruwe katika makazi ya watu mijini. Hilo walikuwa wakilifahamu ndipo kwa heshima waliyofundishwa madrasa na nyumbani walipeleka malalamiko yao panapostahili. Ushahidi unaofahamika ni kuwa ilikuwa ni baada ya kuonyesha heshima hiyo, walilopewa ni dharau na kubezwa tu. Inasemekana kuwa hata dini yao ilidharauliwa. Bahati mbaya Sheikh Jongo hakuzungumzia huyu Muislamu anayedharauliwa na dini yake pia kubezwa afanyeje kuhifadhi heshima yake, ya Waislamu wenziwe na dini ile ya Uislamu, dini ya Allah. Nilibahatika kuhudhuria Swalat-il-Jumaa ya tarehe 3 May, 2013 kule msikiti maarufu wa Wa-Manyema Khutba akiwa Sheikh Hamid Masoud Jongo. AlhamduliLlahi huyu Sheikh amekuwa Imam kiongozi wa msikiti huo kwa takriban miaka

TANGAZO

JAMADUL THAN 1434, IJUMAA MEI 10-16, 2013

AN-NUUR

Heshima na adabu wajibu wa Muislam


ishirini sasa na amekubalika miongoni mwa Wa-Manyema. Akiwa ndiye Kadhi wa Mkoa wa Dar es Salaam ilikuwa ni sahihi kabisa Khutba yake aliilenga kuwafundisha waumini sio tu umuhimu wa heshima na adabu lakini alisisitiza umuhimu wake kutokana na maagizo yaliyomo katika Quran na Hadith. Katika kusisitiza ukweli kuwa kila mtu anastahili heshima aliyakosoa yale yanayosisitizwa na baadhi ya vyombo vya kimataifa kama vile kutaka tu kuwe na Heshima kwa wanawake ilihali hakuna linalozungumziwa juu ya heshima kwa wanaume. Hivyo kwa mfano kiko chama Umoja wa Wanawake wa Tanzania (UWT) ilihali wanaume hawana chombo kama hicho cha kuwatetea. Wakati huo huo inafahamika kiasi gani haki za wanaume zinapondwa hata katika sheria za nchi. Hayo hata yameambukizwa ama wao ndio wameambukiza vyombo vya Serekali hata na serekali za nchi nyingi kukazania haki za wanawake na watoto na kusahu haki za wanaume. Hivyo hivyo haki za wazazi wanazostahili kupata kutoka kwa watoto wao. Hapa alitoa mfano, mzuri sana kufuatia sheria za nchi hii ambazo zinambana mwanamume kwa mfano katika mambo ya mirathi na ndoa. Alitoa mfano wa mke ambaye kufuatana na sheria anaweza kurithishwa kila kitu alichoacha marehemu mume wake na kabisa kuwasahau wazazi wa marehemu. Uonevu huu unajitokeza pale ikikumbukwa kuwa ni yule marehemu ndiye aliyechuma ile mali; na aliweza kuichuma hiyo Mali tu kwa sababu ya malezi aliyopata kutoka kwa wazazi wake. Hasa ikiwa kwa mfano yule marehemu alikuwa ni mtu aliyepata cheo kikubwa serekalini. Ni baba na mama wa huyo marehemu ndio waliomlea mpaka kupata ile elimu iliyomuwezesha kupata cheo kikubwa na kuweza kuchuma mali aliyoicha. Ni jambo lisiloingia akilini alisema kuwa sasa hawa wazazi wanakuwa si watu wa maana tena. Mke achukue kila kitu. Lakini alisisitiza kuwa hayo ni kinyume kabisa na sheria za mirathi za Kiislamu ambapo mke ana haki yake ya thumni tu. Aliwasisitizia Waumini siku ile kuwa ni adabu na heshima kuwakiria wazazi kama Quran inavyoagiza. Kuwa kwamba wazazi wana nafasi maalum haina mbadala alisisitiza. Lazima waheshimiwe kiasi kwamba hata kama mtoto kaona kuwa mzazi wake kateleza kidogo, si pahali pa mtoto kumkemea mzazi wake. Analoweza kulifanya huyo mtoto ni kutafuta msaada kutoka kwa wazee ambao wanaweza kumkabili mzazi wake na kuzungumza naye kumuonya kuwa mwenendo wake si mzuri au kitu kama hicho. Alitoa mfano wa Swahaba mmoja ambaye hakuacha ulevi licha ya kukatazwa na kuonywa kila siku na Rasul-ulu-Llah Muhammad SAW. Ilika wakati maswahaba wenzake walichoka naye kutokana na vitendo vyake hivyo na waliamua kumlaani na kumtenga kabisa. Lakini walistaajabu kuwa Rasu-ul-Llah Muhammad SAW aliwakataza

Na Khalid S Mtwangi IMEKUWA inafahamika kwa muda mrefu sana kuwa ile elimu inayotolewa katika madrasa za Kiislamu sifa kubwa ni ile ya kuwafundisha wanafunzi umuhimu wa kuwa na heshima na adabu kwa kila mtu. Waliopata elimu yao huko wana sifa hiyo sana kila wanapokuwepo. Lakini pia ni khulka hiyo ndiyo imetumiwa na maadui wa Uislamu kuwakandamiza Waislamu kwa sababu ya kuwaheshimu wakubwa kazini na katika maisha ya kawaida. Tukumbukle ule msemo unaofahamika miongoni mwa Waislamu kuwa HEWALLAH SI UTUMWA. Kweli hivi sasa mambo yamebadilika kidogo kuhusu msemo huo na hapo ndipo pameanza matatizo na kuleta yale yasio na maana yeyote ya kuitwa ati kuna Waislamu wenye msimamo mkali . Hawa vijana wameamua tu kwamba sasa kuonewa kwa sababu ya itikadi yao basi. Lakini kwa kiasi kikubwa yale wanayofundishwa nyumbani na Inatoka Uk. 8 (Wakristo) kwa kuwathibitishia kuwa nyendo na njama za mashabiki wa makundi hayo zinajulikana na wanafuatiliwa tangu unyayo hadi kivuli kabla hawajaleta madhara. Habari kama hii inathibitisha jambo moja tu: kuwa kuna jitihada za makusudi za kuchochea chuki na uhasama baina ya Waislamu na Wakristo. Kabla ya viongozi wetu, na hasa Wabunge kucharuka, labda waulize vyombo vyetu vya usalama: Je, walikuwa na taarifa ya boti tatu za kukodiwa zilizoleta Waislamu 150 kutoka Zanzibar kwa lengo la kuchoma makanisa? Je, waliwaona walipotua Mbweni na kuchukua daladala hadi Tandika ambapo inaelezwa kuwa haikuwa tabu kuwagundua kwani inasemwa kuwa walikuwa na alama za kuwatambulisha kuwa ni Uamsho (Waislamu)? Je, vyombo vya usalama vilichukua hatua gani, maana tumeambiwa kuwa waliwatoa wasiwasi Wakristo kuwa watulie na wawe na amani kwa sababu Polisi wanafuatilia nyendo za Waislamu hao wachoma makanisa tangu unyayo hadi kivuli. Kama taarifa zote hizi zilizoelezwa katika gazeti tulilolinukuu hazikuwa sahihi, maana yake ni kuwa lilikuwa linapandikiza chuki, uhasama na uchochezi. Je, vyombo vya dola vilichukua hatua gani? Kwa Serikali kukaa kimya, maana

wasifanye hivyo kwa kuwa na wao watakuwa kama vile wameungana na Iblis ambaye ndiye aliyekuwa akimpoteza hivyo yule Swahaba. Mtume alipendekeza tu nasaha ziendelee. Kufuatana na mfano huu kama alivyonasihi Rasu-ul-Llah ni wazi kuwa kweli mtoto hana haki ya kuweza kumlaani ama hata kumkemea mzazi wake kwa matendo mabaya anayoyatenda huyu mzazi wake. Hiyo si heshima kabisa kufuatana na maadali ya Kiislamu, alisisitiza Sheikh Hamid Masoud Jongo. Alisistiza kwa mkazo kabisa kuwa ni muhimu kwa wazazi wa Kiislamu kuwafundisha watoto wao heshima na adabu kufuatana na mafundisho ya Quran na Hadith. Hapo alipendekeza kuwa Madrasa ziwe ndio kitovu cha mafundisho hayo. Hakika kwa muda mrefu sana Madrasa hata kama ni yale ya pembeni, mwa nyuumba yamekuwa ndio kiini cha maadili ya Kiislamu na msingi wa utekelezaji wa yale Muislamu anatakikana ayatekeleze iwe FARDHI ama SUNNA. Kwa siku hizi pia ni muhimu kuisisitiza kwa hawa vijana kuwa ni lazima waihami dini ya Sub-hana Wa Taala. Kwa muda mrefu Waislamu wamekuwa wakinyanyaswa kwa vile wamefundishwa heshima na adabu ya hali ya juu kabisa. Kumekuwa wale adui wa Uislamu wamekiona hicho kama Waislamu wanyonge wanaoweza kusukumwa huku na kule. Ingawa kweli Sheikh Hamid Masoud Jongo hakulitaja hili, lakini bila shaka atakubaliana na hoja ya kuwataka Waislamu

Tuambiwe ni nani Victor Ambrose


yake ni kuwa inabariki uchochezi huu. Je, haioni kwa kufanya hivyo inawafanya Wakristo waamini yale aliyosema Askofu David na kwa upande mwingine inabariki pia agizo alilowapa Wakristo kuwa waandae visu, mikuki na mishale kwa ajili ya kupambana na Waislamu? Je, ingekuwa taarifa inawasingizia Wakristo kutoka Mbeya au Peramiho kuwa wameingia Zanzibar kuchoma Misikiti, Serikali ingekaa kimya? Ukitizama hapa hili sio tatizo la mihadhara wala Masheikh na Mapadiri. Na kwa hiyo hakuna ufumbuzi utakaopataikana kwa kuwakutanisha Masheikh wa Bakwata na Maaskofu. Kama ni kukutana, wakutane Serikali (Vyombo vya Dola) na akina Askofu David na vyombo vya habari vinavyotumika kusambaza urongo kama huu wa boti za Uamsho kuja Dar kuchoma makanisa, waambizane kuwa mchezo wao mbaya. Utaliangamiza taifa. Wa t u w a n a o s a m b a z a habari hizi za urongo, hapana shaka wanachotaka kuona ni Serikali ikichukua hatua kali za kuwabamiza Waislamu na wakati huo huo kuwakumbatia Wakristo kwa huruma, kuwalea na kuwalinda. Na tumesikia jinsi Serikali inavyojitahidi kuwatuliza na kuwahakikishia usalama wao baada ya tukio hili la Arusha. Lakini kama hilo ndio lengo, je, hatuoni kuwa iwapo watu hawa wataona kuwa uwongo wao kama ule wa kudai kuwa kuna Waislamu wameingia Mbeya kuchoma Makanisa, haikufanyiwa kazi na Serikali, wanaweza kubuni, kutekeleza na kuleta kitisho cha kweli kama hiki cha bomu Kanisani? Awali nimetaja kuwa gazeti la Mwananchi likiripoti habari hizi, likimnukuu msemaji wa wa Kanisa Katoliki, Jimbo Kuu la Arusha, Padri Festus Mangwangi, lilisema kuwa mtu aliyerusha bomu hilo alikuwa amevaa Kanzu. Ukisema kuwa mtuhumiwa kavaa kanzu au baraghashia, unachosema bila kutamka ni kuwa mtuhumiwa ni Muislamu. Lakini hii ni sawa na kusema kuwa majambazi wameenda kuiba na kamera ya video. Wakati wengine wakiweka watu chini ya ulinzi huku wengine wakikusanya fedha na vitu vinavyofaa kuibwa, mmoja anarekodi tukio lote, halafu wakimaliza wanaiacha kamera hapo ili Polisi wasipate tabu kuwatambua. Hakuna jambazi au muhalifu yoyote anayeweza kufanya jambo kama hili. Sasa hizi kauli kuwa mtuhumiwa alikuwa kavaa kanzu, zinazidi kutia wasiwasi. Kwa hiyo, yote haya ni lazima tuyazingatie na kama alivyosema Mheshimiwa James

Mbatia kwamba katika kufanya kazi zake, vyombo vya dola viwe na uadilifu wa hali ya juu.

Omar Bakar Almas Video Production wanakutangazia kuwa katika maduka yao ya mtaa wa Livingstone na Mahiwa mkabala na Kariakoo Bazar na lile la mtaa wa Mafia jirani na Msikiti wa Manyema Kariakoo jijini Dar es Salaam zinapatikana DVD, CD Original na mawaidha ya Kiislamu kutoka kwa Masheikh wetu maarufu. Pia CD mpya za Sheikh Nurdin Kishki za kila wiki zinapatikana pamoja na Hija ya mwaka 2012 aliyeiongoza yeye, Njoo ujipatie DVD bora zenye kiwango cha kimataifa. Kwa mawasiliano zaidi piga simu kwa namba zifuatazo: 0754 805 528, 0785 793 395 au 0716 888 358 NYOTE MNAKARIBISHWA

Tangazo

Visiegemee upande wa dini yoyote. Na kama alivyosema pia Muadhama Polycap Kadinali Pengo, katika kuchunguza tukio hili, ni lazima ukweli uanikwe hadharani bila kujali unamgusa nani.

10
Na Said Rajab JUMATATU ya April 15 mwaka huu, jiji la Boston, Massachusetts nchini Marekani, lilishambuliwa kwa mabomu mazito mawili wakati wa mashindano ya mbio za Marathon za Boston. Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa, watu watatu walipoteza maisha na wengine 171 kujeruhiwa vibaya. Kwa takriban wiki yote ile, tulishuhudia vyombo vya habari vya nchi za Magharibi vikiripoti tukio lile kama habari ya kwanza yenye uzito mkubwa. Licha ya hatari ya kuhukumu kabla ya uchunguzi kufanyika, hisia za watu wote duniani zikaelekezwa na vyombo hivyo kwamba waliolipua mabomu yale ni Waislamu. Wakati mtuhumiwa mmoja alipouawa kwa risasi, na msako wa mwingine ulipoanza, ambao wote ni ndugu, na raia wa Marekani wenye asili ya Chechnya, tulishuhudia maneno ya chuki dhidi ya Uislamu yakihusishwa na tukio hilo. Walikuwa wakijaribu kuhusisha uhalifu ule na Uislamu wa Watuhumiwa. Gazeti la An nuur liliandika kwa kirefu sana kuhusu habari ile na miye siyo lengo langu hasa kuwachosha wasomaji. Bali ningependa tu kuchambua kidogo baadhi ya mambo, ili iwe changamoto ya kra kwa wasomaji wanaofuatilia masuala ya dunia. Matukio kama hayo yanapotokea, basi fursa pia hupatikana ya kuwekana sawa kimtazamo. Kwa masikitiko makubwa, kelele hizi za vyombo vya habari, zikiungwa mkono na maoni ya wanasiasa wenye chuki dhidi ya Uislamu, zikajenga mtazamo kwamba, ingawa Waislamu wote siyo magaidi, lakini magaidi wengi hakika ni Waislamu. Hata hivyo, mtazamo kama huo unakosa mashiko, pale unapoulinganisha na idadi halisi ya mashambulizi ya kigaidi. Gazeti la Europol lilichapisha tak w imu zin azo o n y es h a kwamba kati ya mwaka 2006 mpaka 2008, asilimia 99.6 ya shughuli zote za kigaidi barani Ulaya, zilifanywa na wasio Waislamu. Na rekodi rasmi za FBI zinaonyesha kwamba asilimia 94 ya mashambulizi ya kigaidi katika ardhi ya Marekani kuanzia mwaka 1980 mpaka 2005 yalifanywa na wasio Waislamu. Kinachokera zaidi ni kwamba taarifa potofu za vyombo vya habari ndizo zinazoaminika na kujenga mitazamo hasi dhidi ya Waislamu, lakini zile halisi hazipewi nafasi, kwa hiyo hazijulikani kwa watu wengi. Tatizo lingine kubwa la vyombo vya habari ni kutoa tuhuma za jumla jumla. Yaani Muislamu mmoja akituhumiwa kufanya uhalifu, basi jamii nzima ya Waislamu inalaumiwa kwa hilo. Kimsingi, Uislamu unakataza vitendo vya ukatili na kumwaga damu za watu wasio na hatia, kama tulivyoona katika mabomu ya Boston. Lakini kwanini Waislamu wote wanaoishi Marekani walaumiwe, wasumbuliwe na watishiwe kwa sababu ya mabomu ya Boston? S i y o Wa k a t o l i k i w o t e wanaohusishwa na kashfa ya kulawiti watoto, kwa sababu tu baadhi ya mapadri wamekuwa wakifanya uchafu huo! Siyo

Makala

JAMADUL THAN 1434, IJUMAA MEI 10-16, 2013


tukio la Boston, yatakuwa ndiyo vichuguu vya Serikali ya Marekani kusimamia, na kurusha makombora mazito dhidi ya wale inayowaona maadui, huku ikitumia vibaya hisia na huruma ya wananchi wao kwa watu hao. Kwa bahati mbaya, matukio haya ya Boston yanasaidia sana kujenga taswira ya Marekani, kama taifa lililo tayari kujihami kwa vita wakati wote, kwa sababu linatishiwa na magaidi wakati wote! Na watu wengine duniani wasiojua vizuri mambo haya, wanaweza kudhani Marekani ina haki ya kufanya vile inavyofanya katika nchi nyingine. Wanakiri inajihami kwa kupambana na magaidi. Lakini ukweli ni kwamba Marekani haikuwa na tishio lolote la kiusalama wakati ilipoivamia Afghanistan, kufuatia shambulio la kupanga la Septemba 11, au ilipoivamia Iraq baada ya kubuni uongo wa silaha za maangamizi. Huzuni, huruma, simanzi na hasira za wananchi wa Marekani zitatumiwa kisanii na Serikali yao, ili kukamilisha malengo maovu yaliyopangwa muda mrefu. Hatujui safari hii mabomu ya Boston yataleta gharika gani! Maana, historia inatupa muongozo sahihi, kiasi cha kuweza kufahamu uhalifu unaofanywa na Marekani kupitia visingizio. Kwa kumalizia, hatua zozote zitakazochukuliwa na Marekani au Serikali za Magharibi kupanga mashambulizi dhidi ya Waislamu kwa kisingizio cha kupambana na ugaidi, ikitumia huruma iliyopatikana kufuatia uhalifu uliofanyika Boston, lazima zipingwe kwa nguvu zote.

AN-NUUR

Mashambulizi ya Boston, nani alaumiwe?


Waingereza wote ni waongo, kwa sababu tu Serikali ya nchi hiyo, iliudanganya ulimwengu kuhusu Iraq kumiliki silaha za maangamizi mwaka 2003! Vilevile kuhusika kwa Muislamu mmoja katika uhalifu au tuhuma, haiwafanyi Waislamu wote katika jamii husika kuwa wahalifu wa tuhuma hizo! Vyombo vya habari vya Magharibi vimewazoesha watu wake kuwaangalia Waislamu kama Wao na wenyewe kujiona Sisi ingawa wote ni raia wa nchi moja. Mara nyingi utakuta vyombo hivyo vinaripoti matukio kama ya Boston katika misingi ya Wao, Sisi, Yao na Yetu. Huwa wanasema Wao hawapendi maadili Yetu. Wameshaweka kizingiti katika akili za watu wao na Waislamu. Wamejenga mazingira Waislamu waangaliwe kwa mashaka kila uhalifu kama wa Boston unapotokea. Lakini mtu anahitaji kuelewa msingi hasa wa mashambulizi kama haya ni nini? Kwa bahati mbaya sana, mjadala kama huu unapuuzwa kwa makusudi kwa sababu utatoa taswira sahihi na kuzikamata Serikali za Magharibi kuwa ndizo zinazojenga mazingira ya chuki na hasira za kiasi hicho. Muongo mmoja tu uliopita, kufuatia kile kilichoitwa mashambulizi ya Septemba 11, Marekani na washirika wake walifanya uhalifu wa kutisha dhidi ya Waislamu. Ukiangalia mateso ya AbuGhraib, Guantanamo Bay, vifo vya Wairaq, uharibifu wa Afghanistan mwaka 2002, mashambulizi ya drones nchini Pakistan, Yemen na Somalia, kuingilia kijeshi Mali, kuunga mkono uhalifu wa Israeli dhidi ya Palestina, kuwaunga mkono madikteta katili katika nchi za Waislamu, unaweza kuona sababu halisi za huzuni, hasira na hisia za wale wanaonyanyaswa. Haya ndiyo masuala mazito ambayo ulimwengu wa Magharibi hautaki kuyaangalia kwa ukweli wake. Uvamizi wa mataifa ya Magharibi katika nchi zingine na kudhibiti mambo umesababisha amani kutoweka sehemu kubwa ya dunia na uharibifu kutawala, jambo ambalo linazalisha chuki kwa viwango vikubwa na vidogo. Ni jambo la upuuzi sana kujaribu kukwepa hisia zinazoendana na ukweli huu na kuhamishia lawama kwa Uislamu kama Itikadi. Bila shaka, kujibu mapigo kwa kuwashambulia wasio na hatia inakatazwa katika Sheria ya Kiislamu, na hakuna kisingizio chochote cha kuhalalisha hilo, lakini muktadha nyuma ya vurugu za kisiasa, ambazo Waislamu wanahusishwa, mara nyingi hupuuzwa. Tu k i e n d a m b a l i z a i d i , hebu tufanye tathmini ndogo tu jinsi shambulizi la Boston lilivyoripotiwa kwa mapana na vyombo vya habari vya Magharibi kama unyama, halafu tulinganishe na unyama unaofanywa na Marekani dhidi ya mataifa mengine. Siku chache tu, kabla ya mabomu ya Boston, mashambulizi ya anga ya NATO, yaliua watoto 11 na mwanamke mmoja Mashariki mwa Afghanistan. Vifo vya watoto 11, kwa vipimo vyote, ni hali ngumu zaidi kuliko vifo vya watu watatu. Kwanini vyombo vya habari na huruma ya ulimwengu hailekezwi dhidi ya unyama unaofanywa Afghanistan, badala yake tunalazimishwa kuamini kwamba kilichofanyika Boston ndiyo unyama zaidi? Au vifo vya watoto wa Afghanistan ndiyo collateral damage? (uharibifu mdogo). Hisia hii ya huruma na huzuni iliyoonyeshwa kwenye shambulio la Boston huwa inakwenda wapi wakati Israeli inapoangusha mabomu mahospitalini na kuua raia kule Palestina? Maneno makali ya kulaani mashambulizi dhidi ya watu wasio na hatia na upotevu wa maisha ya binadamu huwa yanakuwa wapi, wakati wananchi wa Libya, Mali, Iraq, Afghanistan, Pakistan, Chechnya na kwengineko wanapoangamizwa? Hao wanaoomboleza uhalifu uliofanyika Boston, wajitathmini kama wanaweza kutaja hata jina moja tu la muathirika wa mabomu yanayoangushwa na jeshi la nchi yao, dhidi ya watu wasio na hatia katika baadhi ya nchi hizo! Wajiulize, wanathamini uhai wa binadamu wenzao kwa sababu ni binadamu, au kwa sababu ni Wazungu wenzao wanaotoka kwenye nchi zao? Kama jibu ni binadamu wenzao, kama mtu yeyote mwenye akili atakavyojibu, sasa kwanini tunafanya upendeleo katika kutoa huruma, mapenzi

na simanzi zetu? Lazima tuumizwe na kukasirishwa na vitendo vyote vya ukiukaji haki na mauaji ya binadamu wasio na hatia duniani kote. Tunaona upendeleo waziwazi. Vifo vinavyotokea ulimwengu wa Magharibi vinaripotiwa kwa kina na kugeuzwa ajenda ya dunia, lakini vifo na madhila yanayotokea katika ulimwengu wa Waislamu vinaripotiwa kidogo sana! Mbaya zaidi madhila hayo huletwa na Serikali za Magharibi, hususan Marekani. Ukichimba zaidi, utaona ulimwengu wa Magharibi umetumia shambulio la Boston kukamilisha ajenda zake za kisiasa. Jinsi vyombo vya habari vilivyoripoti kwa kina tukio hilo, msukosuko waliopata Waislamu kabla ya kutambuliwa mtuhumiwa, kukamatwa kwa mwanafunzi mmoja wa Saudi Arabia, aliyekuwepo kwenye eneo la tukio na jitihada kubwa za kuwatupia lawama Waislamu, kabla ya ukweli kufahamika ni sehemu tu ya picha pana zaidi. Inafahamika vizuri kwamba shambulio hili la Boston litageuzwa geuzwa ili kukamilisha malengo fulani ya sera ya nje ya Marekani, ikiwa ni pamoja na kuhalalisha matumizi ya kijeshi, na kuhuisha propaganda inayovia kwamba Marekani inakabiliwa na tishio la magaidi. Makaburi ya wale waliokufa kwenye

Inatoka Uk. 12 waliosalimika kuishi maisha ya hofu, serikali imeshindwa kukomesha hali hiyo. Wakati akitoa taarifa Bungeni baada ya kuzuru eneo la tukio huko Arusha kufuatia tukio hilo, Waziri Mkuu, Mheshimiwa Mizengo Pinda, alisema kuwa watu nane wameshakamatwa, wanne wakiwa ni wa asili ya Uarabuni, wanne Watanzania ambao aliwataja kuwa ni Victor Ambrose, mwenzake ni Joseph na mwingine ambaye hakutajwa. Naye kama ilivyokuwa kwa wabunge wengine, hakusita kuonya kwamba katika tukio la safari hii siasa, dini na kauli za kichochezi zisihusishwe na tukio hili, na badala yake vyombo vya dola viachwe vifanye kazi yake na kutoa majibu. Hata hivyo, baadhi ya vyombo vya habari na baadhi ya wasemaji wa Polisi, bado hawajaona kama kuna haja ya kuacha kutoa habari za matukio ya jinai huku wakidhihirisha chuki zao za kidini. Baada tu ya kutokea mlipuko katika kanisa hilo, gazeti moja la kila siku liliripoti siku ya Jumatatu, kwamba aliyerusha bomu hilo alikuwa amevaa kanzu nyeupe na koti la mvua. Na alikimbia baada ya kurusha bomu hilo na kwamba tukio hilo lilishuhudiwa na mtoto mdogo. Hiyo ni kauli aliyonukuliwa akizungumza msemaji wa kanisa Katoliki Jimbo la Arusha Padri Festus Mangwangi. Iliendelea kuwa aliyerusha bomu huyo wakati wanakimbia huku akiwachanganya watu

Safari hii Vigogo wamejifunza


kwa kupiga kelele za mwizi na kuwazubaisha watu na mtoto huyo alithibitisha kuwa ndiye mhusika. Katika gazeti la Mtanzania la Jumanne Mei 7, lenyewe likimnukuu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dk. Emmanuel Nchimbi, lilieleza kuwa Waarabu sita wamekamatwa kwa kutuhumiwa kulipua kwa bomu Kanisa hilo na kusababisha vifo vya watu watatu na kujeruhi 59. Pia likamnukuu akieleza kuwa miongoni mwa waliokamatwa, ni kijana wa umri wa miaka 20, dereva wa boda boda aliyetajwa kwa jina la Victor Ambrose, ambaye ndiye anayetuhumiwa kurusha bomu hilo. Gazeti hilo liliripoti kuwa kati ya waliokamatwa, watu wanne ni raia wa kigeni ambao hakutaja nchi zao na mmoja ni Mtanzania na wanashikiliwa kwa mahojiano. Katika habari hiyo ya gazeti hilo, ni vigumu kupata idadi ya Waarabu sita waliokamatwa kama kilivyoeleza kichwa cha habari. Hasa kwa kuzingatia kuwa wageni wanaotajwa kukamatwa katika habari yenyewe ni wanne tu, na Mtanzania mmoja ukiacha kijana Ambrose. Waarabu wawili waliosalia watakuwa wapi? Waziri Mkuu Pinda yeye alilieleza Bunge kuwa wageni waliokamatwa ni wanne wenye asili ya Uarabuni, sio sita. Na watanzania ni wanne na kuwataja wawili, yaani Ambrose na Joseph. Tunajiuliza, katika gazeti la Mwananchi la Jumatatu Mei

6, Msemaji wa Kanisa Katoliki Jimbo la Arusha Bw. Padri Festus Mangwangi amenukuliwa akieleza kwamba, aliyerusha bomu kanisani ni mtu aliyekuwa kavaa kanzu. Kwamba hata baada ya kulirusha, alikimbia huku akipiga kelele za mwizi na kutokomea huku watu wakiwa wamezubaa. Katika gazeti la Mtanzania la Jumanne, lilitaarifu kuwa anayetuhumiwa kurusha bomu ni dereva wa bodaboda Victor Ambrose, ambaye inaonekana alirusha bomu na kutoweka na pikipiki. Hapa tunahabarishwa juu ya watu wawili wanaosadikiwa kurusha bomu. Kuna aliyevaa kanzu nyeupe na koti la mvua na Victor Ambrose, dereva wa bodaboda! Je, wananchi washike lipi? Kwa upande mwingine, yapo magazeti kama NIPASHE ambayo yaliripoti kuwa Waarabu walikamatwa WAKITOROKA baada ya shambulizi. Anachosema mwandishi hapa ni kuwa Waarabu hao ndio waliolipua bomu maana kama si wao hawakuwa na sababu ya kutoroka. Swali ni je, walikuwa wakitoroka au wakienda Nairobi? Katika mazingira haya, kuna haja ya vyombo vya habari navyo kuacha kuripoti matukio haya yanayogusa imani za watu, kwa kuegemea hisia za mwandishi au Mhariri, au kwa msukumo wa udini na chuki ili kupoteza uhalisia wa tukio lenyewe.

11

Na Sheikh Abou Bakar Soliman SHUKRANI zote anastihiki Mwenyezi Mungu Mola wa viumbe wote na Rehema na Amani zimfikie yule aliye tumwa kuwa ni Rehema kwa viumbe vyote ambae ni mtume wetu Muhamad. Ama baada ya utangulizi huu umefikia Uislamu msamaha wake ukomo wa ukubwa ambao haujapata kukia hapo kale wale hautokiwa baadae katika sheria. Maisha ya Amani yemeletwa na Uislamu kwa watu wote. Basi mazungumzo yetu ya leo ni juu ya vyanzo vya kra na nadharia juu ya msamaha huu. Sisi waislamu tunaamini tupo katika haki na wengine wapo katika batili. Sisi tupo katika uongofu na wengine wapo katika Upotevu sisi ni waumini na wengine ni makafiri katika mtazamo wetu na vipi tuishi nao makafiri kwa mshamaha huu ambao Uislamu umeuleta. Msamaha huu una shina na msingi wa kikra muhimu.

Je, ni kweli Waislamu wali shambulia Marekani mnamo Septemba 11?


Inatoka Uk. 4 abiria: Tuna ndege kadhaa, Nyie kaeni kimya, na mtakuwa salama tu. Tunarudi uwanja wa ndege. Baada ya kunukuu mrusho huo wa redio, Tume iliandika Mwongozaji ndege alituambia kuwa alifahamu hapo kuwa ilikuwa ni utekaji nyara. Je, mrusho huo wa redio siyo ushahidi wa kutosha kuwa ndege ya Safari ya 11 ilikutwa imetekwa nyara? Ingekuwa imetoa uthibitisho kama huo kama tungekuwa tunafahamu, kama Ripoti ya Tume iliyodai, kuwa mrusho huo ulitoka ndege American (Airlines) safari ya 11. Lakini hatujui. Kwa mujibu wa taarifa ya Mamlaka ya Safari za Ndege Marekani (FAA) katika muhtasari wa matukio ya utekaji nyara ndege iliyochapishwa Septemba 17, 2001, mrusho huo wa redio ulikuwa kutoka kusikojulikana. Dai la Ripoti ya Tume kuwa ulitokea denge ya American 11 ulikuwa ni wa kupachika tu. Mrusho huo unawezekana kuwa umetoka katika chumba kimoja ambako miito ya simu ya abiria ilisikika. Hivyo, taarifa ya mrusho wa redio kutoka Safari ya 11 ( ya shirika la American Airlines), kama simu zinazodaiwa kupigwa kutoka kwenye ndege, haitoi ushahidi kuwa ndege hizo zilitekwa na wafuasi wa Al Qaeda. 5. Hati za kusafiria na kibana kichwa zinatoa ushahidi kuwa washirika wa Al Qaeda walikuwepo katika ndege zilizotekwa? Hata hivyo, ilichosema serikali kuwa watekaji walikuwa washiriki wa Al Qaeda iliegemea kwa upande mmoja madai kuwa hati za kusaria na kibanio cha kichwa vya washirika wa Al Qaeda vilikutwa katika maeneo ya kuanguka ndege hizo. Lakini madai yote mawili yalikuwa upuuzi. Wi k i m o j a b a a d a y a mashambulio hayo, shirika la upelelezi la FBI lilitoa taarifa kuwa msako katika mitaa baada ya kuteketea kwa Kituo cha Kimataifa cha Biashara uligundua hati ya kusaria ya mmoja wa watekaji wa (ndege ya American Airlines) Safari ya 11, Satam al-Suqami. Lakini dai hili halikupita mtihani wa kuguna. Dhana kuwa hati hii ya kusaria ilipona katika moto huo bila kuguswa, aliandika mwandishi wa habari mmoja wa Uingereza, lingesumbua imani ya mtu anayeunga mkono kwa dhati mapambano ya FBI dhidi ya ugaidi. Kilichoonekana pia ardhini, kwa mujibu wa ushahidi wa serikali uliotolewa, ni kibanio kichwa chekundu. Hii ilionekana ni ushahidi kuwa wateka nyara wa Al Qaeda walikuwa katika ndege ya Safari ya 93 kwa sababu walikuwa, kwa mujibu wa baadhi ya simu zilizopokelewa, walikuwa wamevaa vibanio kichwa vyekundu. Licha ya madai haya kuwa ya kipuuzi kwa sababu hizi hizo kama dai hilo kuhusu hati ya kusaria, dai hili kuhusu kibanio kichwa lilikuwa

Mwanzo wa shina hilo ni imani yetu kuwa kutofautiana na watu ni kwa uwezo wa mwenyezi Mungu na yeye ndiye anayetaka haya yote yatokee na hakuna wa kuzuia anayoyataka Mungu na uwezo wa Mwenyezi Mungu umeambatana na hekima zake kwani yeye halifanyi jambo isipokuwa lina hekima. Anaijua atakaejua na ataekosa kuijua na hivyo sio kwa tama za Muislamu hii ni kinyume cha matakwa ya Mwenyezi Mungu Mtukufu. Amesema mwanyezi Mungu Mtukufu. (Lau angetaka Mola wako wangeamini watu wote duniani hivi wewe unawachukia watu hadi wawe waumini Na shina la pili ni kwamba kari na muumini hisabu zao sio hapa duniani na hazitolewi ni kiumbe bali hesabu zao juu ya ukari au Imani inakua ni huko akhera na inatoka kwa mwenyezi Mungu Mtukufu anasema Allah Na wakikujia wambie Mwenyezi mungu anayajua ninayoyafanya. Mwenyezi Mungu atahukumu kazi yenu siku ya kiama kwa yale mnayotofautiana hadi 68 69 hukumu siku ya kiama inatoka kwa Mwenyezi Mungu na sio kutoka kwako wewe. Na pia anasema Mola Mtukufu Mwenyezi Mungu ni Mola wetu na Mola wenu sisi tunamatendo

Mashina ya msamaha katika Uislamu


yetu na kati yenu mwenyezi Munga atatukusanya kati yetu na kwake tutarejea. Na hii hupelekea kupumzisha moyo wa Muislamuu. Mtu huyu ni kari Mwenyezi Mungu ndiye atamlipa juu ya ukafiri wake huyu mtu anastahiki jahanamu Mwenyezi Mungu ndiye anaejua ikiwa alikufuru kwa ujinga au kwa ukaidi basi huu ndio mfano wa pili katika shina la msamaha katika Uislamu. Shina la tatu Imani ya Muislamu juu ya utukufu na Binadamu ni utukufu wa kibinabamu. Anasema Mwenyezi Mungu kwa hakika tumemtukuza binadamu Israi (70) utukufu sio wa Muislamu peke yake bali ni kwa watu wote. Utukuf huu ni wa binadamu wote kila aliye binadamu hauangalii:Rangi yake Mweupe au mweusi Utaifa wake Mwarabu au Mwafrika Bara lake Mmashariki au Mmagharibi Tabaka lake - Masikini au Tajiri Utamaduni wake Msomi au mjinga Binadamu kama binadamu ni Mtukufu kwa Mwenyezi Mungu. Na katika mifano ya kazi juu ya hayo ni kwa yale aliyopokea Imamu bukhari katika sahihi yake toka kwa jabiri Bin Abdillah (R.A) kwamba Mtume (SAW) walipita na jeneza Mtume akasimama wima wakasema ewe Mtume hilo ni jeneza la Myahudi!! Akasema Jee hiyo sio nafsi? Ndiohiyo ni nafsi ya Binadamu na kila nafsi ya binadamu ina utukufu wake na thamani yake. Shina la nne:- Kwamba

Makala/Tangazo

JAMADUL THAN 1434, IJUMAA MEI 10-16, 2013

AN-NUUR

Uislamu unaamrisha uadilifu (usawa) kwa watu wote na usawa sio kwa Waislamu peke yao. Akasema Allah Na mnapo hukumiwa kati ya watu hukumianeni kwa usawa (Uadilifu Nisai 58) Basi uadilifu wa mwenyezi Mungu ni kwa viumbe wake wote kwani zimeteremshwa aya tisa katika Surat nisai 105113 kwa kumtetea myahudi ambaye alituhumiwa wizi na ilikuwa walio iba ni ni Waislamu au katika walio tuhumiwa juu ya unafiki. Walijaribu kumbandikizia hizi tuhuma huyu myahudi na alikusudia mtume kutaka kuwatetea wezi hawa na i k a t e r e m k a Q u r- a n i i l i kumtakasa huyu Myahudi na

Mungu Mtukufu atufundishe yaliyo na manufaa na atunufaishe kwa yale tunayojifunza.

kumtetea. Na kuwaonyesha hawa ambao walijaribu kumpa tuhuma asiyehusika basi usawa haugawanyiki na wala haupimiki kwa mizani bali ni kwa uadilifu na usawa na mwenyezi Mungu anasema:Enyi mlioamini kuweni na msimamo kwa ajili ya mwenyezi Mungu mashahidi wa Usawa (uadilifu) na wala zisikudanganyeni uadui wa watu hadi mkaacha uadilifu (USAWA) fanyeni uadilifu huko ndio karibu na ucha Mungu na mcheni Mwenyezi Mungu Su-rat Maidah. Uadui maana yake sawa ikiwa uadui huo na dharau hizo ni kwenu nyinyi kwao au bughudha yao kwenu isikuchukulieni vitu hivyo mkaacha kufanya uadilifu (usawa) na katika hadithi (Dua ya aliyedhulumiwa hata kama ni kari haina pazia kati yake na mwenyezi Mungu Tunamuomba Mw enyezi

na tatizo kwa sababu nyingine. Mshirika wa CIA wa zamani Milt Bearden, aliyesaidia kutoa mafunzo kwa wapiganaji wa Mujahidina nchini Afghanistan, amekumbushia kuwa ingekuwa jambo la ajabu kuwa wanachama wa Al Qaeda walivaa vibanio kichwa vya aina hiyo. Kibanio kichwa chekundu ni kielelezo maalum cha mavazi ya wafuasi wa madhehebu ya Shia. Kinatokea wakati wa kuanzishwa kwa dhehebu hilo ...Kinawakilisha utayari wa mvaaji wa kibanio kichwa chekundu kutoa maisha yake, kujiua kwa ajili ya harakati. Wa-Sunni, ambao kwa wingi zaidi ndiyo wafuasi wa Osama bin Laden hawafanyi hivi. Tukisikia muda mfupi baada ya kuvamiwa Irak kuwa baadhi ya watu katika serikali ya Marekani hawakuwa wanajua tofauti kati ya Waislamu wa Sunni na Shia. Hivi ni watu kama hawa walioamua kuwa wateka nyara waelezewe kuwa walikuwa wamevaa vibanio kichwa vyekundu? 6. Habari kuhusu mizigo ya Atta kwenye ndege inaonyesha kuhusika kwa washiriki wa Al Qaeda? Ushahidi ambao unasemekana kutoa uthibitisho wa nguvu zaidi kuwa ndege hizo zilitekwa na Mohamed Atta na wanachama wengine wa Al Qaeda ni kuwepo kwa mabegi mawili ya Atta yaliyogunduliwa uwanja wa ndege wa Boston baada

ya mashambulio. Mabegi yalikuwapo, tulielezwa, kwa sababu licha ya Atta kuwepo Boston hapo Septemba 10, yeye na mshirika mwingine wa Al Qaeda, Abdul al-Omari, walikodisha Nissan ya buluu na kuendesha hadi Portland, jimbo la Maine, na kulala huko. Waliingia ndege ya safari fupi kurudi Boston mapema kesho yake tayari kupanda ndege ya Safari ya 11, lakini mabegi ya Atta yalibaki nyuma. Mabegi hayo yanasemekana yalikuwa na ushahidi mwingi wa kuonyesha kuhusika na utekaji nyara, ikiwa ni pamoja na kompyuta ya uendeshaji ndege ya kushika mkononi, mtaala wa kuonyesha jinsi ya kuruka, mikanda miwili ya video kuhusu ndege za Boeing, rula ya hesabu za mruko angani, nakala ya Qurani, na hati ya maelekezo kuhusu akifa nini kifanyike. Vifaa hivi vilichukuliwa kote kama ushahidi kuwa Al Qaeda na hivyo Osama bin Laden walihusika na mashambulio ya 9/11. Yakiangaliwa kwa karibu, hata hivyo, habari hizi za Atta kwenda Portland zinapoteza uthabiti wowote. Tatizo moja ni wazo kuwa Atta alikuwa amepanga kupeleka vitu hivi katika sanduku ambalo lingepelekwa ndege ya Safari ya 11. Nini ambacho kompyuta ya uendeshaji ndege na vifaa vingine vya kuruka angani ndani ya begi katika sehemu ya mizigo ingemsaidia kwa shughuli ya utekaji? Angetaka vipi kuchukua hati yake ya nini kifanyike baada ya kifo chake ndani ya

ndege aliyopanga kuibamiza katika Kituo cha Biashara cha Kimataifa? Tatizo kubwa zaidi la habari hiyo hata hivyo haikutokea hadi Septemba 16, siku tano baada ya 9/11, baada ya kuporomoka kwa habari nyingine ya awali. Kwa mujibu wa taarifa za habari mara baada ya 9/11, vifaa hivyo vinavyoonyesha kuhusika, badala ya kukutwa katika mabegi ya Atta ndani ya uwanja wa ndege, vilikuwa katika Mitsubishi nyeupe, ambayo Atta aliiacha katika uwanja wa ndege wa Boston kunakoegeshwa m a g a r i . Wa t e k a j i w a w i l i waliendesha Nissan ya buluu hadi Portland halafu wakapanda ndege ya safari fupi kurudi Boston asubuji yake, lakini majina yao ni Adnan na Ameer Bukhari. Habari hii iliporomoka mchana wa Septemba 13 wakati ilipogunduliwa kuwa kina Bukhari hao wawili, ambao maosa wa serikali waliripotiwa kuwashuku kutokana na vifaa vilivyokuwa katika Nissan pale uwanja wa ndege ndogo wa Portland, hawakufa katika tukio la 9/11. Adnan alikuwa bado hai na Ameer alikufa mwaka uliotangulia. Ukichukulia habari hii ya Atta kwenda Portland, ni vipi unaweza kukwepa hitimisho kuwa ilikuwa imetungwa? (Makala hii imefasiriwa kutoka Kiingereza na Anil Kija kutoka makalakama ilivyoandikwa na Ibn e Abdul Haq)

12

AN-NUUR
MAKALA

12

JAMADUL THAN 1434, IJUMAA MEI 10-16, 2013

Usikose nakala yako ya AN-NUUR kila Ijumaa


alisema hawakufanya hivyo walifika na mwanaye hivyo walipoka hawekuweza kuuliza kwani wanaamani kuwa mpaka kufikishwa kwake, mwanaye alikuwa ameshajiridhisha kwa hilo. Naye Bi. Mwali, ambaye ni dada wa Sheikh Ponda, aliyekuwapo siku ya tukio hilo, alisema watu hao walipofika walieleza kuwa wameka hapo kutaka kujua kama kweli Ponda, kuzaliwa Tanzania au Burundi. Bi. Mwali, alisema watu hao walitoa maelezo kuwa kuna taarifa wanazo kwamba Sheikh Ponda alizaliwa Burundi, na kwamba aliingia nchini kwa Mzee Issa Ponda, kwa ajili ya kusoma dini akiwa mdogo. Hivyo wana wasiwasi na maneno hayo wanayokishiwa, hivyo wanataka vitu hivyo ili wakalinganishe na vya Sheikh Ponda ili mamlaka husika wajiridhishe. Alisema Bi. Mwali. Bi. Mwali, alisema waliwapa maelezo ya kutosha kukanusha madai hayo. A n n u u r, i l i p o j a r i b u kuwasiliana na watu hao kupitia namba za simu walizokuwa wakitumia kuwasiliana na ndugu wa Sheikh Ponda, ili kuweza pata maelezo yao kuhusu zoezi wanalotaka kulifanya hazikuweza kupatikana muda wote.

Na Bakari Mwakangwale WATU waliodai kuwa ni maasa Uhamiaji na mmoja mkemia wametoka kapa, baada ya Mama Ponda, na wanae kugoma kuchukuliwa damu, mate na nywele, kwa ajili ya kujiridhisha na Uraia wa Sheikh Ponda. Watu hao inadaiwa kwamba walifika nyumbani kwa Bi. Mariamu Ally Kassa (Mama Ponda) mtaa wa Ngamiani, Ujiji Kigoma, mapema wiki hii na kumtaka Mama huyo pamoja na wanae wakubali kuchukuliwa vitu hivyo. Akiongea na An nuur, kwa simu kutoka Kigoma, Bw. Maabadi Issa Ponda, alisema alifuatwa na watu watatu ambapo wawili walidai kuwa ni Maafisa Uhamiaji kutoka Kigoma na mmoja alikuwa amejitambulisha kuwa ni mkemia kutoka Dar es Salaam, akiwa na vifaa vyake kwa ajili ya kuchukua walivyohitaji, kutoka kwao. Wale jamaa walikuja haja yao kubwa walitaka wachukue damu ya mama, mate au nywele pamoja na vitu kama hivyo kutoka kwa ndugu wa kuzaliwa na Sheikh Ponda. Baada ya mjadala mrefu tuligoma kutoa vitu hivyo. Alisema Bw. Maabadi. B w. M a a b a d i , a l i s e m a kwanza walitaka kujua kwamba huyo anayetakiwa kuchunguzwa damu, kwa maana ya Sheikh Ponda Issa Ponda, kama anafahamu suala hili. Alisema, watu hao hawakuwa na majibu yaliyonyooka kwa familia hiyo kwa ujumla kwani alidai walihoji zaidi kutaka kujua uhalali wa majibu ikiwa watachukua hivyo wanavyo hitajia, ikiwa hicho wanachodai kuwa uchunguzi watafanya wao wenyewe. Bw. Maabadi alisema, katika majibu yao jamaa hao walidai, kuwa Sheikh Ponda hana tatizo kwa kuwa yupo chini ya himaya ya Serikali, hivyo hatokuwa na hiyari ya kukataa kuchukuliwa damu kwa ajili ya vipimo. K w a m u j i b u w a B w. Maabadi, alimnukuu mama yao akisema kwamba yeye kama mama Ponda, hatochukuliwa damu, wala nywele kwa ajili wa hayo wanayokusudia kwenda kuyafanya dhidi ya mwanaye. Alisema, Mama Ponda aliwaeleza watu hao kuwa kama yupo mtu ambaye anasema Ponda Issa siyo mtoto wake, ajitokeze na ushahidi lakini siyo kusikia maneno ya uzushi na kusababisha usumbufu. Kwa kifupi mjadala ulikuwa mrefu sana mama na sisi wote tukibaki na msimamo wetu kuwa hatuchukuliwi damu, mate wala nywele, huku wao wakitusihi tukubaliane nao, mwisho waliamua kuondoka. Alisema Bw. Maabadi. Akiongea kufuatia tukio hilo, Bi. Mariamu Kassa (Mama wa Ponda), alitihibitisha kufuatwa na watu hao nyumbani kwake, wakimtaka yeye na mwanae mmoja wachukuliwe damu,

Bado familia ya Ponda inasumbuliwa Kigoma

Uhamiaji wadaiwa kutaka mate ya mama yake


mate na nywele. Walifika hapa wakisema watuchukue damu, nywele au mate yangu na Slei (Kaka wa Ponda) ili waje navyo huko (Dar es Salaam) ili walinganishe na vya Ponda, lakini tulikataa mimi na wanangu. Alisema Bi. Kassa. Alisema, baada ya kuwagomea aliwataka waitwe Masheikh ili isomwe albadir, kama kweli Ponda si mtoto wake au si raia wa Tanzania, ili Mwenyezi Mungu atoe majibu kwani alidai anavyojua yeye suala hili lilishafanyiwa kazi na majibu yalitolewa. Mama Ponda, alisema baada ya kutoa rai hiyo jamaa hao waliamua kuondoka, wakidai hilo ni suala zito huku na kusema kwamba wanapeleka majibu kwa wakuu wao, na ikibidi wanaweza kurejea tena. Alipoulizwa kama watu hao walionyesha vitambulisho kutoka katika mamlaka hizo,

Safari hii Vigogo wamejifunza


Na Shaban Rajab KATIKA tukio la mlipuko wa bomu katika Kanisa Katoliki la Joseph Mfanyakazi huko Olasiti jijini Arusha, safari hii kwa kiasi fulani wanasiasa na viongozi wa serikali wamejitahidi kutoa kauli au lugha za kistaarabu badala ya zile zilizozoeleka za uchochezi na chuki, hususan kwa watu wa imani nyingine. Na mara nyingi, kauli hizi za chuki na ushabiki na uchochezi dhidi ya watu wa imani nyingine pale panapotokea uhalifu, hasa unaohusiana na ugaidi, basi viongozi, vyombo vya habari, wanaharakati, wanasiasa na hata viongozi wa dini, mara moja huharakisha katika kutoa hukumu, shutuma na kulaani watu wa imani inayolengwa kuwa ndio wahusika. Tumeshuhudia kauli za namna hii mara baada ya kutokea tukio la kupigwa risasi Askofu wa Kanisa Katoliki Mpendae Zanzibar Desemba, Padri Ambrose Mkenda. Tumeshuhudia kauli hizi za kichochezi na chuki pale alipouliwa Padri Evarist Mushi wa Kanisa Katoliki Minara Miwili Zanzibar, Tumeshuhudia kauli za namna hii katika tukio la kihalifu la kuchomwa kanisa huko huko Zanzibar. Nadhani sasa viongozi na wanasiasa wamejifunza kutokana na matokeo yanayotokana na kauli zao za kichochezi na za kuhukumu watu kwa misingi ya imani pale yanapotokea matukio yanayohusisha imani za kidini. La msingi ni kumsaka mhalifu, kumkamata na kumchukulia hatua kwa mujibu wa sheria za nchi. Awe ni Sheikh au Askofu, madhali imethibitika kutenda jinai iliyotokea, basi ashughulikiwe kama mhalifu mwingine, badala ya kutoa kauli za kujumuisha tuhuma kwa watu wa imani ya mhalifu husika, kama vile nao ni wahusika wa uhalifu wake. Katika tukio la safari hii, watoa kauli wamejitahidi kufuata njia sahihi katika kuzungumzia matukio haya, hususan yanayohusisha dini. Bila shaka wametambua udhaifu wa kauli zao zilizojaa hisia za kichochezi na chuki. Kila mmoja sasa anatoa kauli ya kutahadharisha kutonyosheana vidole, kuepuka tuhuma zinazoelemea hisia za kidini. Kwa mfano, Sehemu kubwa ya mjadala wa Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, katika kikao cha 20 cha Mkutano wa 11 wa Bunge, ulitawaliwa na hoja juu ya tukio la mlipuko wa bomu katika Kanisa Katoliki la St. Joseph, Olasiti jijini Arusha Jumapili ya Mei 5 mwaka huu. Mhe. James Mbatia, Joseph Selasini na Salum Barwan, ni baadhi tu ya wabunge waliochangia kwa kina juu ya tukio hilo. Kwa upande wake, Mhe. Mbatia alisema umeka wakati sasa wabunge wa vyama vyote, serikali na viongozi wa dini kutatua tatizo hili badala ya kunyoosheana vidole. Alisema wabunge wana dhima ya kushughulikia tatizo hili na kutahadharisha kwamba, tusije shangaa miaka mitano ijayo wabunge wakapelekwa The Hargue kwa makosa ya jinai iwapo maafa yataendelea kutokea kutokana na kauli za wanasiasa. Mhe. Mbatia alitolea mfano

Bi. Mariamu Ally Kassa (Mama mzazi wa Sheikh Ponda)

Wote watahadharisha kunyoshea mtu kidole Waandishi bado wanatuchanganya Mrusha bomu ni Ambrose au mwenye kanzu nyeupe
wa mzozo wa kuchinja, ambapo alisema inafahamika wazi kwamba kuna sheria kamili juu ya suala hilo, ambayo aliitaja kuwa ni sheria ya mwaka iliyopitishwa mwaka Desemba 6, 2008 ya Animal Welfare. Alihoji inakuwaje watu wanavunja sheria hiyo kwa kuanzisha uchochezi wa kuchinja na kusababisha vurugu na serikali kuwafumbia macho huku ikitambua fika uwepo wa sheria hiyo na kwamba walioleta hoja ya kuchinja wameikiuka sheria hiyo? Kwa upande wake Bw. Barwani yeye alisisitiza haja ya kuwepo mjadala wa kitaifa juu ya tatizo la udini nchini. Hata hivyo alishangazwa na juhudi za serikali kukia hatua ya kuazima vikosi vya FBI kutoka Marekani kuchunguza matukio ya mauaji ya Padri na mlipuko wa Olasiti, wakati miaka nenda rudi makumi ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Albino) wamekuwa wakiuliwa, wengine kujeruhiwa vibaya na Inaendelea Uk. 10

Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na Business Printers Limited, S.L.P. 78495 Dar es Salaam.

Вам также может понравиться

  • Rasimu Ya Katiba (Toleo La Pili)
    Rasimu Ya Katiba (Toleo La Pili)
    Документ0 страниц
    Rasimu Ya Katiba (Toleo La Pili)
    Muhidin Issa Michuzi
    0% (1)
  • Annuur 1092
    Annuur 1092
    Документ16 страниц
    Annuur 1092
    annurtanzania
    Оценок пока нет
  • Annuur 1087
    Annuur 1087
    Документ7 страниц
    Annuur 1087
    annurtanzania
    Оценок пока нет
  • Annuur 1082
    Annuur 1082
    Документ16 страниц
    Annuur 1082
    MZALENDO.NET
    100% (1)
  • Annuur 1091
    Annuur 1091
    Документ16 страниц
    Annuur 1091
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Annuur 1078
    Annuur 1078
    Документ12 страниц
    Annuur 1078
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Annuur 1076
    Annuur 1076
    Документ12 страниц
    Annuur 1076
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Annuur 1063
    Annuur 1063
    Документ16 страниц
    Annuur 1063
    Hassan Mussa Khamis
    Оценок пока нет
  • Annuur 1065
    Annuur 1065
    Документ12 страниц
    Annuur 1065
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • An-Nuur 1071
    An-Nuur 1071
    Документ12 страниц
    An-Nuur 1071
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Annuur 1030
    Annuur 1030
    Документ16 страниц
    Annuur 1030
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Annuur 1077
    Annuur 1077
    Документ12 страниц
    Annuur 1077
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Annuur 1072
    Annuur 1072
    Документ12 страниц
    Annuur 1072
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Annuur 1062
    Annuur 1062
    Документ16 страниц
    Annuur 1062
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Annuur 1067
    Annuur 1067
    Документ12 страниц
    Annuur 1067
    annurtanzania
    Оценок пока нет
  • Annuur 1046
    Annuur 1046
    Документ12 страниц
    Annuur 1046
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Annuur 1057
    Annuur 1057
    Документ16 страниц
    Annuur 1057
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Annuur 1060
    Annuur 1060
    Документ16 страниц
    Annuur 1060
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Annuur 1061.
    Annuur 1061.
    Документ16 страниц
    Annuur 1061.
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Annuur 1049
    Annuur 1049
    Документ12 страниц
    Annuur 1049
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Annuur 1031
    Annuur 1031
    Документ16 страниц
    Annuur 1031
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Annuur 1059
    Annuur 1059
    Документ16 страниц
    Annuur 1059
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Annuur 1022
    Annuur 1022
    Документ12 страниц
    Annuur 1022
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Nadharia Ya Meli
    Nadharia Ya Meli
    Документ6 страниц
    Nadharia Ya Meli
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Annuur 1029
    Annuur 1029
    Документ20 страниц
    Annuur 1029
    annurtanzania
    100% (1)
  • Annuur 1028
    Annuur 1028
    Документ16 страниц
    Annuur 1028
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Annuur 117
    Annuur 117
    Документ16 страниц
    Annuur 117
    annurtanzania
    Оценок пока нет
  • Zaka 3
    Zaka 3
    Документ61 страница
    Zaka 3
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Annuur 1027
    Annuur 1027
    Документ16 страниц
    Annuur 1027
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет