Академический Документы
Профессиональный Документы
Культура Документы
tz
Uk. 12
Kushambuliwa Ponda:
Adaiwa kuwamwagia tindi kali Wazungu Anataka Sheria Kali za Kiislamu Unguja! Ni kuchonganisha Waislamu na Wakristo
Uchochezi wakolea
Kosa la Ponda nini hadi kupigwa risasi?
Ahoji Sheikh Mussa Kundecha Isije kuwa la kuuliwa Sheikh Unguja Ataka madai ya Waislamu yasikilizwe
Na Bakari Mwakangwale
SHEIKH Ponda Issa Ponda akiwa amelazwa katika Wodi ya MOI Hospitali ya Taifa Muhimbili.
SHEIKH Azzan
SERIKALI imetakiwa kubainisha kosa la Sheikh Ponda Issa Ponda ni lipi ambalo likawa hukumu yake ni kupigwa risasi. Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu (T), kupitia Amir wake
Mkuu Alhaj Mussa Yusuph Kundecha, limeitaka Serikali kutoa majibu hayo baada ya kuunda Tume huru ya uchunguza kuchunguza kadhia ya k u p i g wa r i s a s i Sheikh Ponda Issa Ponda, akiwa Mkoani
Inaendelea Uk. 3
2
www.annuurpapers.co.tz
Tahariri/Makala
Cel: 0784 370 208, 0713 110 148, 0755 260 087 , DSM. E-mail: annuurpapers@yahoo.co.uk Osi zetu zipo: Manzese Tip Top Usangi House (Jengo dogo), barabara ya Morogoro, D'Salaam
AN-NUUR
a j i l i ya M a r e k a n i , yote hiyo imeelezewa k i n a g a u b a g a mahali pengi. Kama m wa n d i s h i k i j a n a wa habari za kivita nchini Vietnam, ilinia kutambua kuwa Marekani inahamisha hisia zake za mauaji nchi nyingine na kuita ni vita, kuwa ni harakati adilifu. Kama shambulio hilo la Apache, mauaji yaliyotingisha dunia mwaka 1968 ya My Lai hayakuwa tukio tofauti na mengine. Katika jimbo hilo la Quang N g a i , n i l i k u s a n ya ushahidi wa mauaji ya watu wengi: maelfu ya wanaume, wanawake na watoto, waliouawa kwa makusudi na bila kutangazwa katika maeneo ya kuachwa mapigano. Huko Irak, nilipiga picha za video za mchunga wanyama ambaye ndugu yake na familia yake waliuawa kwa bomu lililoteremshwa na ndege ya Marekani, katika eneo la wazi. Hii ilikuwa ni mzaha, mchezo tu wa kawaida. Nchini Afghanistan, nilipiga picha za video kwa ajili ya mwanamke mmoja ambaye nyumba yake ya tope, na familia, viliteketezwa na bomu la ratili 500 (kilo 220). Hapakuwa na adui. Vikapu vyangu vya lamu za video vimejaa ushahidi kama huo. Katika kesi ya Bradley Manning, serikali ya Marekani haipingi anayosema m t u h u m i w a , lakini kosa ni kuwa kwanini kafichua unyama, ukatili na mauwaji ya kinyama wanayofanyiwa Waislamu. Ndio pale shahidi wa serikali katika kesi hiyo anasema, The militant
group used Mannings releases to claim that the United States does not value human life, particularly among Muslims. Kwamba Al Qaeda walitumia nyaraka na video za Manning kuonyesha jinsi Marekani isivyojali uhai wa watu wengine, hasa Waislamu na hivyo kuzidisha chuki ya Waislamu dhidi ya Marekani. K w a h i y o kinachoonekana hapa sio, ule uhalifu na ukatili wanaofanyiwa Waislamu, lakini kosa ni kwa nini unyama huo uanikwe hadharani na kwa namna n y i n g i n e i t a k u wa kwa nini Waislamu wanaofanyiwa unyama huo walalamike na kupinga kuhujumiwa! Hayo anayofanyiwa askari kachero Manning, ndiyo yanayowakuta Wa i s l a m u k a t i k a nchi hii. Kwa miaka mingi sasa, Waislamu wamekuwa wakilalamika kuwa kuna ubaguzi, uonevu na dhulma inayofanywa na v y o m b o v ya d o l a dhidi yao. Kwa upande mwingine, wamekuwa wa k i o n ye s h a j i n s i ambavyo, Wakristo walivyokuwa na wanavyoendelea kupata upendeleo katika maeneo mbalimbali kinyume na katiba, sheria, sera na kanuni za nchi. Hata hivyo, badala ya madai hayo kuchunguzwa ili kubaini ukweli na kuchukua hatua, utaratibu umekuwa kwamba kila anayelalamika na kutaja dhulma hizo, hushutumiwa kuwa analeta udini na uchochezi na hivyo kudaiwa kuhatarisha amani ya nchi.
Kwa vile Serikali inachotizama sio malalamiko na madai ya Wa i s l a m u , b a l i kupuuza na kutafuta njia ya kuyakwepa kwa kuwarushia shutuma wanaolalamika, yamekuwa yakiibuka makundi ya Waislamu na taasisi mbalimbali kuzungumzia masuala hayo kwa namna tofauti tofauti. Anachofanya S h e i k h Po n d a n a Masheikh wengine, waliojaaliwa ujasiri wa kusema hadharani ya l e wa n a yo a m i n i k u wa n i s a wa , n i katika mlolongo huo wa k u z i d i k u p a z a sauti, asaa Serikali ipate kusikia kilio cha Waislamu. Sasa inawezekana kuwa kwa kukosekana mawasiliano yenye kuratibiwa vizuri baina ya Serikali na Waislamu juu ya madai haya, basi ikatokea watu wakakosea katika njia ya kupita. Ikitokea hivyo, kwa bahati mbaya, inachukuliwa kuwa hilo ndio tatizo, na yake madai ya msingi kuachwa pembeni. N d i o h a p o yatazuliwa maneno kwamba hawa siasa kali, al Qaida, al Shabab na haya ya magazeti ya Uingereza kuwa Ponda amewamwagia tindi kali wasichana wa Kizungu. Katika hali hii, sisi tunasema kuwa, h a k u n a n a m n a ya kuleta salama ya kweli katika nchi hii, zaidi ya kuukabili ukweli na kusikiliza madai ya wananchi (Waislamu). Njia nyingine zitakuwa za mkato za kukwepa tatizo na hatimaye kulifanya kuwa saratani isiyotibika. Tu n a c h o h o f i a tusije tukafika hapo i k a wa m c h e z o wa kukamatana uchawi tukitafuta mlango wa kutokea tusiuone.
Habari
AN-NUUR
sheria. Alisema Amir Kundecha. Amir Kundecha, alisema Umma wa Kiislamu unaamini kabisa kwa matumizi ya silaha ya moto dhidi ya Sheikh Ponda, lengo lilikuwa kumuua na sio kumpa jeraha alilolipata. Alisema, kwa bahati mbaya matukio kama hayo yakitokea kwa Waislamu, kwa Serikali huwa ni suala dogo, kwani Mjini Zanzibar, kuna Sheikh aliuliwa na Polisi kwa risasi akitoka Msikitini, kwa madai ya kudhibiti maandanao ya chama cha siasa kwa siku inayofuata. S e r i k a l i haikuchukua hatua yoyote juu ya kifo cha Sheikh huyo na ilihali alipigwa risasi na Polisi, hakuna tume iliyoundwa na jambo hilo likapita hivi hivi utadhani aliyeuwawa si binaadam. Alisema Amir Kundecha. Alisema, kwa upande mwingine hivi karibuni alipigwa risasi Padri Visiwani Zanzibar, nchi yote ilitikisika kuanzia ngazi ya viongozi wa Serikali na kuamuru kuundwa kwa tume haraka kuchunguza shambulio hilo. Amir Kundecha alisema, tukio la kushambuliwa Sheikh Ponda na Polisi kwa risasi ya moto kitendo hicho huenda kikatafsiriwa na Waislamu ikawa n i n j i a ya k u t a k a kuwanyamazisha Waislamu washindwe k u w a s i l i s h a malalamiko yao hadharani.
Amir Kundecha, alisema kama Serikali inadhani hiyo ndiyo njia sahihi, aliitanabaisha kuwa hivyo sio sahihi, kwani kumzuia mtu kwa nguvu asiseme, huwa hasaidii kwani tatizo huendelea kuwepo daima. Kunyamazisha mwenye madai yake ya msingi huwa sio ufumbuzi wa tatizo, bali ni kuliongeza tatizo kuwa kubwa zaidi, lakini kuchukua hatua isiyofaa ni hatua mbaya zaidi. Alisema Amir, Kundecha. Alisema, Waislamu wamekuwa na malalamiko mengi kwa Serikali yao na malalamiko yao sio siri, aliyataja baadhi yake kuwa ni juu ya MoU, ambayo ni ya muda mrefu kama ambavyo Serikali haina dini, Waislamu wasingetegemea Serikaki kuegemea upande mmoja wa Dini. Alisema, Waislamu wamekuwa pia na malalamiko juu ya Baraza la Mitihani (NECTA) kuwa dhidi ya Shule zao na dhidi ya wanafunzi wa Kiislamu, lakini hakuna hatua zinazochukuliwa. Akahoji, vipi suala likisemwa na Waislamu haliwi ni tatizo ila likisemwa na mwingine huwa lina maana zaidi? Alisema, Waislamu wameitaka Serikali kwa muda mrefu ichuke hatua za makusudi kushughulikia malalamiko yao bila mafaniko, badala yake huonekana ni Inaendelea Uk. 11
SISI, Umoja wa Wa n a z u o n i w a Kiislamu Tanzania (Hay atul Ulamaa), t u m e p o k e a kwa masikitiko makubwa habari za kushambuliwa na kujeruhiwa kwa silaha za moto, Sheikh Ponda Isa Ponda, huko Morogoro, Jumamosi Agosti 10, 2013. Hay-atul Ulamaa, imesitushwa na tukio hili linalo uma na linaloumiza na kuleta mshtuko na fazaa katika jamii kama ilivyoshtushwa na matukio mengine kama hili hapa nchini. Hili ni tukio ambalo linaashiria kuwa walio litenda hawaitakii mema na amani nchi yetu. Tunalaani vikali kitendo hicho na tunaitaka Serikali ya Jamhuri ya Muungano
PRESS RELEASE
wa Tanzania kuchukua hatua kali na za haraka dhidi ya wale wote walio husika katika tukio hili lenye kuumiza nyoyo za wengi. Aidha tunawasihi Waislamu na jamii kwa ujumla kuwa watulivu, wenye subira na wenye kunyenyekea kwa Mola wao katika jambo hili zito, wakati tunasubiri vyombo vya dola vichukue hatua zinazo stahiki dhidi ya wahusika wa tukio hili. Tu n a m u o m b e a S h e i k h Po n d a I s a Ponda Allah Amponye haraka na Ampe baraka katika umri wake. Amin Sheikh Suleiman Amran Kilemile Mwenyekiti U m o j a w a Wa n a z u o n i w a Kiislamu Tanzania. 11/August/2013
Makala
AN-NUUR
Agosti 8, 2013 Mtandao wa kupelekeana habari H AT U A m u h i m u katika kesi ya kisiasa ya karne ilikuwa Februari 28 wakati Bradley Manning (aliyekuwa askari katika jeshi la Marekani) aliposimama na kueleza kwanini alihatarisha maisha yake kuvujisha makumi ya maelfu ya mafaili ya serikali. Ilikuwa ni taarifa ya maadili, dhamira na ukweli: sifa ambazo zinamtambulisha binadamu. Hii haikuonekana kuwa ni habari muhimu nchini Marekani, na isingekuwa kwa ajili ya Alexa OBrien, mwandishi wa habari wa kujitegemea, sauti ya Manning ingekuwa imezimwa. Akifanya kazi usiku kucha, aliandika ushuhuda huo wote uliorekodiwa na kuutoa kama ulivyo. Ni taarifa ndefu yenye kuchua mengi. Akielezea shambulio la helikopta ya kivita ya A p a c h e , wa p i g a picha walioeleza jinsi raia walivyouawa na kujeruhiwa mjini Baghdad mwaka 2007, Manning alisema: Kilichonishtua zaidi katika video hiyo ilikuwa ni muonekano wa kufurahia kumwaga damu waliokuwa nao. Walikuwa wanaonekana kutothamini maisha ya binadamu na kuwaita dead bastards na kupongezana kwa uwezo wa kuua kwa idadi kubwa. Wakati mmoja katika video kuna mtu ardhini akijisogeza kufika mahali salama zaidi aliyekuwa amejeruhiwa vibaya. Kwangu mimi hii ilikuwa ni kama mtoto anayetesa mchwa kwa kifaa cha kunasa mwanga kuwa moto. Alikuwa anatumaini
The Courage Of Bradley Manning Will spire Others To Seize Their Moment of Truth
By John Pilger
AUGUST 08, 2013 Information Clearing House - The critical moment in the political trial of the century was on 28 February when Bradley Manning stood and explained why he had risked his life to leak tens of thousands of official les. It was a statement of morality, conscience and truth: the very qualities that distinguish human beings. This was not deemed mainstream news in America; and were it not for Alexa OBrien, an independent freelance journalist, Mannings voice would have been s i l e n c e d . Wo r k i n g through the night, she transcribed and released his every word. It is a rare, revealing document. Describing the attack by an Apache helicopter crew who lmed civilians as they murdered and wounded them in Baghdad
in 2007, Manning said: The most alarming aspect of the video to me was the seemingly delightful bloodlust they appeared to have. They seemed not to value human life by referring to them as dead bastards and congratulating each other on the ability to kill in large numbers. At one point in the video there is an individual on the ground attempting to crawl to safety [who] is seriously wounded... For me, this seems similar to a child torturing ants with a magnifying glass. He hoped the public would be as alarmed as me about a crime which, as his subsequent leaks revealed, was not an aberration. Bradley Manning is a principled whistleblower and truth-teller who has been vilied and tortured and Amnesty International needs to explain to the world why it has not adopted him as a prisoner of conscience; or is
Amnesty, unlike Manning, intimidated by criminal power? It is a funeral here at Fort Meade, Alexa OBrien told me. The US government wants to bury Manning alive. He is a genuinely earnest young man with not an ounce of mendacity. The mainstream media nally came on the day of the verdict. They showed up for a gladiator match to watch the gauntlet go down, thumbs pointed down. The criminal nature of the American military is beyond dispute. The decades of lawless bombing, the use of poisonous weapons on civilian populations, the renditions and the torture at Abu Graib, Guantanamo and elsewhere, are all documented. As a young war reporter in Indochina, it dawned on me that America exported its homicidal neuroses and Cont. Pg. 10
adilifu. Kama shambulio hilo la Apache, mauaji yaliyotingisha dunia mwaka 1968 ya My Lai hayakuwa tukio tofauti na mengine. Katika jimbo hilo la Quang Ngai, nilikusanya ushahidi wa mauaji ya watu wengi: maelfu ya wanaume, wanawake na watoto, waliouawa kwa makusudi na bila k u t a n g a z wa k a t i k a maeneo ya kuachwa mapigano. Huko Irak, nilipiga picha za video za m c h u n g a wa n ya m a ambaye ndugu yake na familia yake waliuawa kwa bomu l i l i l o t e r e m s h wa n a ndege ya Marekani, katika eneo la wazi. Hii ilikuwa ni mzaha, mchezo tu wa kawaida. Nchini Afghanistan, nilipiga picha za video kwa ajili ya mwanamke mmoja ambaye nyumba yake ya tope, na familia, viliteketezwa na bomu la ratili 500 (kilo 220). Hapakuwa na adui. Vikapu vyangu vya lamu za video vimejaa ushahidi kama huo.
Inaendelea Uk. 10
Habari za Kimataifa/Tangazo
AN-NUUR
siri za nchi hiyo. Kwa upande mwingine Lon, amevituhumu vyombo vya usalama na vya sheria vya Marekani akisema haviwezi kumhukumu kwa uadilifu mwanaye. Edward Snowden, yupo nchini Urusi ambako amepata hifadhi, jambo ambalo limezua mvutano mkubwa hivi sasa kati ya Marekani na Urusi.
Refa asimamisha mechi kufuturu Mamia waandamana kuunga mkono jeshi la Syria
DAMUSCUS Mamia ya wananchi wa mkoa wa ArRiqqah Kaskazini mwa Syria, wamefanya maandamano karibu na bustan ya ArRashid, wakilaani vitendo vya kikatili vinavyofanywa na waasi wanaojiita Ahraarus-Sham wanaodhibiti eneo hilo. Wa a n d a m a n a j i waliokuwa na hasira kali, wametaka kuondoka waasi hao katika mji huo na kudhibitiwa na serikali ya Syria. Hata hivyo waasi waliwashambulia waandamanaji kwa risasi za moto. Miji ya ArRiqqah na AlHasakah ina idadi kubwa ya Wakurdi, ambapo kwa kipindi cha wiki kadhaa yameshuhudiwa mapigano makali baina ya wapiganaji wa Kikurdi na waasi wa Jabhatu Nasrah, wa k i s h i r i k i a n a n a kundi la DawlatulIslamiyya lenye uhusiano na mtandao wa Al-Qaida. I d a d i k u b wa ya watu wameuawa na wengine kujeruhiwa katika mapigano hayo. Mauaji hayo yanafanyika baada ya kutolewa fatwa na viongozi wa Kiwahabi ya kuhalalisha mauaji dhidi ya Wakurdi. RAIS wa Syria, Dkt. Bashar -al- Assad
DAKAR R E FA O u s s e y n o u Gueye, amesimamisha mechi ya soka nchini Senegal, ili kupata fursa ya dakika chache kufuturu na wenzake baada ya saumu ya mwezi mtukufu wa Ramadhani. Ripoti zinasema kuwa mechi hiyo kati ya timu za Casa Sport na Yeggo, ilianza dakika 30 kabla ya adhana ya Magharibi, hivyo refa Ousseynou Gueye ambaye ni Muislamu, alilazimika kusimamisha pambano hilo kwa muda ili kutoa fursa fupi ya kufuturu kwa waliofunga. Baada ya mechi, refa huyo alisema anafahamu kuwa kitendo chake kinakiuka kanuni za soka, lakini alichukua uamuzi huo kwa mujibu wa mafundisho ya dini yake ya Kiislamu. Alisema baada ya kufuturu kwa tende na maji, aliweza kuendelea na kazi yake akiwa na nishati zaidi katika mechi hiyo ya Julai 14 iliyomalizika kwa sare bila mabao.
Wakati huo huo, jeshi la Syria limeendelea kuwaangamiza waasi wa Jabhatu Nasra katika eneo la Dir azZur na Daraa. Jeshi hilo pia limemuangamiza kiongozi wa kikundi cha waasi kinachojiita Al-Muhajirina, anayeitwa Abu Hudhaifah At-Tunisi, katika mapigano na jeshi la Syria kwenye viunga vya mji wa Laadhiqiyyah
Makala
AN-NUUR
Kushambuliwa Ponda:
Na Omar Msangi WAKATI Sheikh Ponda Issa Ponda akiendelea kupata matibabu hospitalini, vyombo vya habari vya Uingereza vimeibuka na kudai kuwa Ponda anahusika na tukio la kumwagiwa tindi kali (acid) mabinti wawili wa Uingereza. Katika taarifa za baadhi ya televisheni na magazeti ya juzi na jana, vyombo hivyo vimesema kuwa Ponda alipigwa risasi na polisi wakati polisi wakaribu kumkamata kwa kuhusika na kuwamwagia tindi kali Kirstie Trup na Katie Gee. Mabinti hao wa Uingereza ambao hivi sasa wanapata matibabu huko Uingereza, ilidaiwa uwa walimwagiwa tindi kali hivi karibuni katika mitaa ya Mji Mkongwe Zanzibar. A h a t e p r e a c h e r hunted over the acid attack on two British girls was last night under armed guard in hospital. Ndivyo lilivyoripoti gazeti la- Daily Mirror, jana katika kutoa maelezo ya picha ya Ponda akiwa hospitali. Nao Sky News, wakizungumzia tukio hilo wakasema: A radical Muslim preacher wanted over an acid aack on two British teenagers in Zanzibar has been caught by police, according to reports. It was claimed that Sheikh Issa Ponda Issa was shot in the shoulder with a tear gas canister as he tried to escape from ocers aer being cornered near the Tanzanian coastal city of Dar es Salaam. He was reported to be ghting for his life in hospital. Ufupi wa maneno wakisema kuwa Ponda alipigwa risasi wakati a k i s a k wa n a Po l i s i kwa kuhusika na kuwamwagia tindi kali Wazungu wawili. Gazeti maarufu la The Sun, nalo likawa na taarifa likisema: A RADICAL Muslim preacher wanted over the acid aack on two British teenagers in Zanzibar has been shot while eeing from cops. Sheikh Issa Ponda Issa tried to make a run for it when he
Uchochezi wakolea
ya Udaktari wa Falsafa, akisisitiza ile nadharia kwamba ni taharuki hali si shwari tena, duniani, Afrika, na Tanzania pia. Miongoni mwa hoja zilizosimama hapo ni iweje Dola pamoja na Watawala wake, tena kwa kinywa kipana, wasimame kumnadia raia huru kuwa ni mtu hatari, na kuyafumbia macho yale mengi yanayoweza kuwa ya hatari zaidi na ambayo Serikali zenyewe huenda zilikuwa chanzo. Moja kati ya kampeni chafu za Wamarekani Weupe dhidi ya Rais Barack Obama, ilikuwa ni kumjengea hoja ya kamuhoji angelifanyanje kukabiliana na wahalifu Wamarekani We u s i a m b a o w a o Inaendelea Uk.7
Dar es Salaam. The Times likafuata mkondo huo huo liliposema: A radical Muslim preacher wanted in connection with an acid attack on two British teenagers in Zanzibar has been shot by police, it was reported. Sheikh Issa Ponda Issa was hit in the shoulder with a tear gas canister as he tried to escape from ocers aer being cornered near Tanzanias capital Dar es Salaam. H a t a h i v y o likawabebesha lawama The Sunday Mirror kwamba walinukuu kutoka kwao. L a k i n i t a a r i f a ya the Mirror haisemi moja kwa moja kuwa Ponda anatafutwa kwa kuhusika na shambulio la tindi kali, ila inasema anadaiwa kuchochea watu kufanya shambulio hilo. Linasema: An extremist Islamic preacher who allegedly inspired the acid attack on two British volunteer teachers was shot and captured in Tanzania earlier today. Police hit Sheikh Issa Ponda Issa in the shoulder with a teargas canister aer cornering him near the capital Dar es Salaam. A manhunt was launched aer it was claimed he provoked the aack on Kirstie Trup and Katie Gee, both 18. Sheikh Ponda was taken to hospital where he was ghting for his life under armed police guard. It has been claimed that he provoked the ambush to raise the prole of his campaign to rid Zanzibar of foreigners and impose hardline Islamic law. Hapa the Mirror wameongeza kitu kingine wakisema kuwa, Ponda anafanya yote hayo kwa sababu anataka kusimamisha Sheria Kali za Kiislamu (hardline Islamic law) Zanzibar na kuendesha kampeni za kupiga marufuku Wazungu ( Wa k r i s t o ) k u i n g i a visiwani humo. Gazeti la The Telegraph likinukuu taarifa ya Polisi Dar es Salaam lenyewe likasema: A radical Muslim
Inaendelea Uk.7
7
Inatoka Uk. 7 preacher wanted for questioning over the acid attack on two British tourists in Zanzibar was shot on Saturday night as he ed police trying to arrest him. Sheikh Issa Ponda is understood to have survived the raid and was on the run but injured, police sources told The Daily Telegraph. He narrowly escaped from the police in Morogoro, he was shot by our ocers, but we are pursuing him, said Faustine Shilogile, a senior police commander in Morogoro, the town 110 miles west of Tanzanias commercial capital, Dar es Salaam, where Ponda was shot. Nalo gazeti la Daily Mail likiwa na uhakika na linachokisema likaandika kama ifuatavyo: Muslim preacher wanted for acid attack on British teenagers in Zanzibar shot by police as he tried to escape Sheikh Issa Ponda Issa shot in shoulder with tear gas canister Shot as he was cornered by police near Tanzanias capital Dar es Salaam Accused of acid attack on Katie Gee and Kirstie Trup. Mchambuzi mmoja akiandika kutoka Uingereza anasema kuwa kinachojitokeza katika ripoti za vyombo vya habari vya Uingereza, ni kampeni ile ile ya kupandikiza ugaidi na uhalifu miongoni m w a Wa i s l a m u i l i ipatikane sababu ya kuwahujumu. A n a s e m a , kinachoonekana ni kuwa hii ni kampeni ya kimataifa kwa sababu wakati taarifa rasmi za Polisi Tanzania hazijasema kuwa Ponda anahusika na kuwamwagia tindi kali Wazungu, wao huko nje wanapiga propagada hiyo wakiamini kuwa nchi za Kiafrika zinategemea sana na kuamini habari za BBC, CNN, Sky News na vyombo vya habari kama hivyo vya kimataifa. Anasema, kumsema Sheikh Ponda kama Sheikh mwenye siasa kali asiyetaka Wazungu na anayetaka kusimamisha siasa kali za Kiislamu Zanzibar,
Uchochezi wakolea
MAKALA
AN-NUUR
SHEIKH Ponda Issa Ponda (kulia) na Ustadh Mkadamu inalenga kule kule katika kupandikiza kitisho cha ugaidi, kuchonganisha Waislamu na Wakristo kama ilivyowahi kufanya hivyo kwa Masheikh wa Uamsho. J i n g i n e n i kuwachonganisha Waislamu na Serikali yao ambapo badala ya Serikali kusikiliza madai
Wazungu waliwajengea taswira wakaisambaza ulimwenguni kote kuwa ati jamaa zake hao Obama ni hatari kwa Taifa hilo kubwa. H a p a Wa m a r e k a n i We u p e wa l i c h o j a r i b u kuchongea ni kusahau matatizo na hatari waliyoijenga wenyewe kwa akina Obama hao karne hadi karne, kutokana n a a d h a ya d h u l m a , idhilali, ubaguzi, fitna, chuki, uonevu na kusahau matatizo ya Wamarekani We u s i t a n g u a s i l i n a zama. Kwa sababu Obama amejifunza siasa, mwenye washauri wanaoona mbali duniani, na pia anayejua alifanyalo, hakutafuna maneno akababaisha. Alipoingia tu madarakani aliuma jongoo kwa meno, akaandaa Mswada wa Bima ya Afya, ambapo Sheria hiyo pamoja na vizingiti vikubwa ilivyokabiliana navyo, hatimaye imeelekea kuwa mkombozi wa Wamarekani, hasa wale wahanga Weusi, ambao
wanaendelea kubaguliwa na kunyimwa baadhi ya haki zao kutokana na msingi uliokwishajengeka huko nyuma, dawa sio kuwapuuza na k u wa t a n g a z i a u a d u i . Madai yao yatizamwe na yajengewe utaratibu wa kupata ufumbuzi. Hii itaepusha watu kujitafutia n a m n a z a o we n ye we ambazo zaweza kuleta balaa katika nchi. Wapo waliohoji kwa n i n i R a i s wa Awa m u ya Kwanza na Awamu ya Tatu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Mwalimu Julius Nyerere na Mhe Benjamin Mkapa, wao waliyaona wanayohitaji Wakristo na wakayakazania kwa nguvu zote, pasi na kumuonea muhali yeyote, jee, Mzee Mwinyi, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, wanamuonea aibu nani? Kwa nini kama Waislamu wanalalamika, malalamiko yao yasitazamwe kisayansi, kufanyiwa uchunguzi na kubaini ukweli wake? Inaendelea Uk. 8
ya Waislamu kama raia wengine, inawatizama kama maadui na watu wakoro. Huko nyuma kuliwahi kufanyika vurugu Zanzibar ikadaiwa kuwa makanisa yamechomwa moto na osi za CCM, lawama wakatupiwa Masheikh wa Uamsho. Pamoja na kuwepo ushahidi wa kuonekana magari ya watu wanaofahamika wakisomba vijana na matairi kufanya zogo hilo, lakini propaganda kubwa ilipigwa kuwapaka matope Masheikh kuwa ndio waliofanya uhalifu huo. Katika makala yake Taharuki, mwandishi mmoja anasema kuwa upo ushahidi kutoka Maafisa wa Kibalozi k u p i t i a Ta a s i s i y a Demokrasia ya Nchi za Ulaya, (unaoonyesha) namna watu wao walivyonasa baadhi ya gari zinazomilikiwa na baadhi wakubwa wenye mamlaka serikalini zikibeba janjaweed na matairi na kuchoma moto maeneo ya Mwanakwerekwe na Kisonge Zanzibar usoni mwa vyombo vya dola halafu wakasingizia Uamsho. Pia lipo lile tukio pale vilipounguzwa m o t o v i b a n d a v ya biashara katika Mkoa wa Kaskazini Unguja, ambapo vyombo vyote vya habari vya Tanzania Bara na Nje ya Nchi, vilipakazia kuwa Waislamu wenye msimamo mkali Zanzibar wamechoma maduka ya Wabara na Wageni na kuwataka ati wahame, kama kwamba mtego ulikuwa umetegewa hapo. Akasema, Ni mengi yaliyojiri hapo kabla na hata kuhusishwa na Uamsho usoni mwa Vyombo vya Habari vya ndani na vya Nje ya N c h i , l i k i wa m o t u k i o l a k u c h o m wa moto nyasi za kibanda cha Kanisani Tunguu, ambapo hatimaye Polisi walibaini ni hujuma za waumini wa kanisa hilo wenyewe kwa wenyewe kutokana na mgogoro uliotokota hapo kwa muda mrefu (Na kwamba) licha ya kuwa ni Waislamu wa Unguja waliowapa
Inaendelea Uk. 8
8
Inatoka Uk. 7 kiwanja, na sio kuwauzia Wakristo, kwa hiyari yao, lakini hatimaye ikatangazwa kwa kishindo na vyombo vya habari vya Tanzania Bara, kuwa waliotenda hujuma hiyo ni Waislamu ati Uamsho, tena kabla ya kusubiri uchunguzi wa Jeshi la Polisi. Kadhia hii i n a y o e n d e l e a kumuhusisha Sheikh Ponda na uhalifu wa kuwamwagia tindi kali wasichana wawili wa Kizungu, labda itasaidia kuwafanya Waislamu kufungua macho na b o n g o z a o k u f a n ya kazi kujua hatari inayowakabili na jinsi wasio watakia mema walivyounganisha nguvu za kimataifa kuwapiga vita. Anasema Ustadh
Uchochezi wakolea
Makala
SHAWWAL 1434, IJUMAA AGOSTI 9 - 15, 2013 mmoja na kuongeza kuwa pamoja na Waislamu kujitambua na kutambua hatari inayowakabili, muhimu zaidi ni kwa Watanzania kujua jinsi watu wa nje wanavyowachochea na kujenga fitna baina ya Waislamu na Wakristo. Na kwa hiyo, wasiwe ni wenye kuzipokea na kuzikubali kibubusa taarifa za watu wanaokuja na madai k u wa Wa i s l a m u wanachoma makanisa au kushambulia na kuuwa Maaskofu. K a m a wa n a we z a kusema uwongo mchana kweupe kwamba Ponda anahusika na tukio la kumwagiwa a s i d i Wa z u n g u Wakristo, watashindwa kusambaza uwongo k u wa Wa i s l a m u wanachoma makanisa na kuuwa Mapadiri? Alihoji.
AN-NUUR
MAALIM Ally Bassaleh (wa pili kushoto) akiwa na Sheikh Ponda Issa Ponda katika moja ya haa za Kiislamu nchini.
lakini pakasahaulishwa ule ufedhuli wa makusudi wa kupanga wa kuikashifu Q u r a n Tu k u f u k w a kuikojolea na wale walioichoma moto kule Kanda ya Ziwa. Wa p e m b u z i wa mambo wakiwamo Wanadiplomasia Wazungu wameshangazwa na namna mfululizo Magazeti makubwa kama vile Daily Mirror na The Independence ya Uingereza, yalivyopania k u k a z i a U k u r a s a wa mbele, kila siku habari za Mabinti wawili kumwagiwa tindi kali, Sh. Ponda kupigwa risassi, t e n a wa k i m u h u s i s h a moja kwa moja na tukio la kujeruhiwa kwa watu hao, na zaidi hata bila ya kuripoti mtiririko sahihi wa mambo yalivyokwenda, bali ni propaganda na upotoshaji wa makusudi wa habari, huenda kwa lengo maalumu. Wamehoji yapo mambo mengi ya msingi kwa wakati huu, lakini la kushangaza Vyombo hivyo vya habari mashuhuri duniani vilivyolenga kupakazia matukio hayo pasi na uchunguzi makini wala kufuatilia kwa undani. Mmoja wa Wachunguzi na wafuatiliaji wa Siasa za Tanzania aliwasilisha Inaendelea Uk. 9
9
Inatoka Uk. 8
Polisi. Hapo ipo namna. W a n a c h o h o j i wapembuzi wa mambo ya kisiasa na kijamii ni jee, haya ya kupigwa risasi kwa Padri, Muhasibu wa Kanisa, Moto wa Kanisa la Mpendae, Moto wa Kanisa la Kijangwani, Moto wa Uamsho, Umwagiaji ovyo wa tindikali kwa baadhi ya watu wakiwamo Mabinti Wawili wa Kiingereza, na mengi mengineyo, pia ipo namna? Kwa ujumla maswali haya ya kukuna vichwa, wakati ambao hajulikani n a n i wa k u l a u m i wa , Jeshi la Polisi linajibari upande wake kutohusika, uchunguzi ukiendelea, watawala wakiendelea k u s h a n g a z wa , u m m a ukiwepowepo tu, kinachoonekana sasa ni kama kuwa taharuki hali si shwari tena.
Makala
AN-NUUR
KATIKA safu yako ya gazeti la Mzalendo la Agosti 11,2013 katika mada ya Unguja Njema? umeeleza kuwa Zanzibar ile ya zamani ya utawala wa wakoloni wa Uingereza na Usultani wa Kiarabu walijenga jamii ya uvumilivu na ustaarabu....na ukaendelea Naam kweli wakati huo kisiwa cha Unguja kilikuwa njema na neema. Maneno yako haya yanakinzana sana na kauli zilizomo kwenye makala zako nyingi zilizopita ambazo mara kwa mara hutuelimisha na kutukumbusha kuwa utawala wa Sultan wa Mwarabu ulikuwa ukiwadhalilisha na kuwakandamiza Wa a f r i k a w e u s i wa Unguja yaani Waswahili ambao kwa mujibu wa maandishi yako ni Wahadimu, Watumbatu na Wapemba Weusi. Kila mara umekuwa ukitisisitizia kuwa jazaa na khatima ya watu hawa Waafrika Weusi ndani ya jamii ya Zanzibar chini ya utawala wa Mwarabu ilikuwa ni aidha kuwa wajakazi na mayaya kwa upande wa wanawake ama kubaki kuwa wapagazi, maboy wa
majumbani, wachukuzi na wakwezi kwa upande wa wanaume yaani kwa ujumla watwana. Sasa mimi napagawa mwalimu wangu! Sijui n i s h i k e l i p i k a t i ya mafundisho yako ya kila wiki ya kuwaumbua na kuwashutumu Waarabu na hili jipya la sasa kwenye Mzalendo wa leo kuwa utawala wa Wamanga (Waarabu) ulenga jamii njema ya ustaarabu na uvumilivu! Nina yakini hutonibu kunifafanulia na kuniondosha katika hii hali yangu ya kuchanganyikiwa kwa maelelezo yako (narration) ya aina mbili kinzani kuhusu shauri la Waarabu Zanzibar. Vile vile gazeti letu la Mzalendo huwa pia kwa kawaida halichapishi maoni ya wasomaji yanayohoji au kujibu makala zako. Inawezekana wahariri wa gazeti wanaogopa kuchapisha labda kwa vile wewe Dr. Khatib ni bosi wao ukiwa ni mjumbe wa Sekretariat na NEC ya CCM. Mimi najaribu kudadisi na naona napata dhana
Unguja njema?
kuwa maelezo yako hayo mawili kinzani yana walengwa wawili tofauti. Kundi moja la walengwa ni Watanzania wa Bara wa k i we m o v i o n g o z i wa Chama ambao kwa b a h a t i m b a ya h u wa hawaelewi undani na uhalisia wa mambo ya Zanzibar ingawa wao wenyewe huamini kuwa wanaelewa. H a wa h u s i s i m k a n a hupenda kusikia na kuamini maelezo yako. Kinachofuata ni kupanda kwa chati ya ukada na umaarufu wako kwa hawa ndugu zetu wa Bara na kuzidi kukupakia siagi kwenye mkate wako. Alhamdulilah! Kundi la walengwa wa pili ni vana wadogo wa hapa Zanzibar hasa wa UVCCM ambao wana hamu kujuwa historia ya visiwa hivi. Wanajikuta wanakuwa wakereketwa waliojazwa itikadi za uhasama bila kutanabahi kuwa pengine hadisi walizonazo vichwani hazina mashiko wala mantiki. Jambo la pili kwenye makala yako vile vile umelaani ipasavyo
hisia za chuki za kidini unazohisi zimeibuka hapa visiwani na kutia doa haiba ya Unguja. Suala linalonia kichwani mwangu kukuuliza kuhusu hili ni: Kwa nini nyie viongozi wetu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar huwa mnapaza sana sauti zenu kulaani UDINI lakini hamfanyi hivyo hivyo kwa upande wa kulaani UBAGUZI WA NASABA na RANGI ZA NGOZI unaoendekezwa hapa Zanzibar? Kwani ni dhahiri majanga mawili ya UDINI na UBAGUZI WA NASABA na RANGI Zanzibar ya n a r u t u b i s h a n a n a mtu huwezi kupambana na kulaani janga moja l a U D I N I n a wa k a t i huo huo ukashajiisha na kuhamasisha janga jengine la UBAGUZI. Hizi ni pande mbili za sarafu ambazo lazima ziangamizwe kwa mpigo mmoja. Ni tutapofanya hivyo tu, ndio Zanzibar yetu itakuwa kweli njema na ya AMANI. Vinginevyo tutajidanganya na kujihadaa. Afwan mwalimu wangu! DOTTO KESI ZANZIBAR
10
Makala
AN-NUUR
Mwaka 2010, askari Manning akiwa ni private tu wa jeshi, alifanya wajibu wake kwa binadamu kwa jumla na kutosha uthibitisho wa jambo hilo kutoka ndani ya mashine ya m a u a j i . H u u n d i yo ushindi wake; na kesi yake ya kimeonyesho isiyo na haki ndani yake inaonyesha tu woga wa dola haramia ya watu kujua ukweli. Inatoa pia mwanga kwa wategemea f a d h i l a k u wa k a b i l i wasema ukweli. Dhamira ya Manning i m e c h a m b u l i wa n a kutumiwa hovyo na wale ambao hawakuwahi kumjua na bado wanadai kumuunga mkono. Sinema iliyotajwa sana, Tunaiba siri: Undani wa WikiLeaks, inambadilisha askari k i j a n a k u wa m t u mpweke, aliye na hitaji muhimu la kihisia kutokana na kuwa na mzozo wa kujitambua kwani yuko katika mwili usiomfaa na anataka k u wa m wa n a m k e . Ndiyo alivyosema Alex Gibney, mkurugenzi wake, ambaye bwabwaja ya k e k u h u s u h i s i a ilipata masikio sikivu katika nyanda za vyombo vya habari vya wavivu wasiojituma vya kutosha au wapumbavu wasioweza kuhoji ubabaishaji huona kuelewa kuwa vivuli vinavyoangukia wapiga filimbi vinaweza pia kuwakia hata wao. Kutoka kichwa chake cha uwongo, filamu ya G i b n e y i l i f a n ya kazi ya kuwakata shoka Manning, Julian Assange na WikiLeaks. Ujumbe wake si mpya wasiofuata mstari unaotakiwa na watawala wana tatizo la kihisia. Taarifa aliyotoa Alexa OBrien kuhusu maadili na ujasiri wa kisiasa wa Manning, unavunjilia mbali upakaji matope huu. K a t i k a f i l a m u ya G i b n e y, w a n a s i a s a
wa Marekani na mwenyekiti wa wakuu wa majeshi ya Marekani wanaletwa kurudia, bila kupingwa, kuwa, kwa kuchapisha uvujishaji wa Manning, mtandao wa WikiLeaks na Assange wanahatarisha maisha ya wanaopeleka habari kwa mashirika ya kasusi ya Marekani, na kuwa wana damu katika mikono yao. Mnamo Agosti 1, gazeti la Guardian liliandika: Hakuna vifo kutokana na uvujishaji WikiLeaks, mahakama yaambiwa. Jenerali wa Pentagon aliyeongoza uchunguzi wa miezi kumi kuhusu athari kote duniani za uvujishaji huo alitaarifu kuwa hakuna hata kifo kimoja kingeweza kuhusishwa na uvujishaji.
The Courage Of Bradley Manning Will spire Others To Seize Their Moment of Truth
From Pg. 4 called it war, even a noble cause. Like the Apache attack, the infamous 1968 massacre at My Lai was not untypical. In the same province, Quang Ngai, I gathered evidence of widespread slaughter: thousands of men, women and children, murdered arbitrarily and anonymously in free re zones. In Iraq, I filmed a shepherd whose brother and his entire family had been cut down by an American plane, in the open. This was sport. In Afghanistan, I filmed to a woman whose dirtwalled home, and family, had been obliterated by a 500lb bomb. There was no enemy. My lm cans burst with such evidence. In 2010, Private Manning did his duty to the rest of humanity and supplied proof from within the murder machine. This is his triumph; and his show trial merely expresses corrupt powers abiding fear of people learning the truth. It also illuminates the parasitic industry around truth-tellers. Mannings character has been dissected and abused by those who never knew him yet claim to support him. The hyped film, We Steal Secrets: the Story of WikiLeaks, mutates a heroic young soldier into an alienated... lonely... very needy psychiatric case with an identity crisis because he was in the wrong body and wa n t e d t o b e c o m e a woman. So spoke Alex Gibney, the director, whose prurient psycho-babble found willing ears across a media too compliant or lazy or stupid to challenge the hype and comprehend that the shadows falling across whistleblowers may reach even them. From its dishonest title, Gibneys lm performed a dutiful hatchet job on Manning, Julian Assange and WikiLeaks. The message was familiar - serious dissenters are freaks. Alexa OBriens meticulous record of Mannings moral and political courage demolishes this smear. In the Gibney film, US politicians and the chairman of the joint chiefs of staff are lined up to repeat, unchallenged, that, in publishing Mannings leaks, WikiLeaks and Assange placed the lives informants at risk and had blood on his hands. On 1 August, the Guardian reported: No record of deaths caused by WikiLeaks revelations, court told. The Pentagon general who led a 10month investigation into the worldwide impact of the leaks reported that not a single death could be aributed to the disclosures. Yet, in the film, the journalist Nick Davies describes a heartless Assange who had no harm minimisation plan. I asked the film-maker Mark Davis about this. A respected broadcaster for SBS Australia, Davis was an eyewitness, accompanying Assange during much of the preparation of the leaked les for publication in the Guardian and the New York Times. His footage appears in the Gibney lm. He told me, Assange was the only one who worked day and night extracting 10,000 names of people who could be targeted by the revelations in the logs. While Manning faces life in prison, Gibney is said to be planning a Hollywood movie. A biopic of Assange is on the way, along with a Hollywood version of David Leighs and Luke Hardings book of sculebu on the fall of WikiLeaks. Proting from the boldness, cleverness and suering of those who refuse to be co-opted and tamed, they all will end up in historys waste bin. For the inspiration of future truth-tellers belongs to Bradley Manning, Julian Assange, Edward Snowden and the remarkable young people of WikiLeaks, whose achievements are unparalleled. Snowdens rescue is largely a WikiLeaks triumph: a thriller too good for Hollywood because its heroes are real. This article rst appeared in the New Statesman Follow John Pilger on twier @johnpilger
Na bado, katika lamu hiyo, mwandishi wa habari Nick Davies anaelezea kuhusu A s s a n g e a s i v yo n a huruma ambaye hakuwa na mpango wa kudhibiti athari za uvujaji huo. Nilimwuliza mtengeneza filamu Mark Davis kuhusu hili. Mtangazaji anayeheshimika wa shirika la utangazaji la SBS Australia, Davis alikuwa shahidi, akifuatana na Assange wakati wa kutayarisha mafaili yaliyovujishwa kwa uchapishaji katika gazeti la Guardian (la Uingereza) na lile la New York Times. Kipande chake kinaonekana katika lamu ya Gibney. Aliniambia, Assange alikuwa ndiye pekee a l i ye k u wa a k i f a n ya
kazi usiku na mchana kuondoa majina 10,000 ya watu ambao wangeweza kulengwa na ufichuaji huo katika mlolongo wa wahusika. Wa k a t i M a n n i n g akiwa hatarini kutumikia kifungo cha maisha, Gibney anasemekana ana mpango wa kutengeneza s i n e m a H o l l y wo o d . Sinema kuhusu maisha ya Assange inaandaliwa, pamoja na kuonyesha kama sinema kitabu cha David Leigh na Luke Harding cha porp cha porojo na uvumi kuhusu kuanguka kwa WikiLeaks. Wakifaidisha kutokana na ujasiri, werevu na taabu za wale wanaokataa kuingizwa katika mfumo na kutawaliwa, wote hao
wataishia katika debe la taka la historia. Kwa kuwatia moyo wa s e m a u k we l i wa huko baadaye wapo |Bradley Manning, Julian Assange, Edward Snowden na vijana shupavu wa WikiLeaks, ambao mafanikio yao hayana mfano wake. Kuokolewa kwa Snowden hasa ni ushindi wa WikiLeaks: hadithi changamfu kupita kiasi kwa Hollywood kwa sababu mashujaa wake ni wa kweli. (Makala hii ilichapishwa kwanza katika jarida la New Statesman. Imetafsiriwa kwa Kiswahili na Anil Ka. Mfuatie John Pilger katika twier@johnpilger)
11
Habari/Matangazo/Shairi
AN-NUUR
MGENI ASINDIKIZWE !
Tumefunga wetu babu, kwa swamu kitimiza, Twamhimidia RABBU, kwa sisi hilo kuweza, Kilosalia hesabu, kwa kwetu kuekeleza, MWENI kumsindikiza, ni wetu sote wajibu. Ramadhani bila tabu, yote tumeitimiza, Kulikoni na ajabu, kwa SITA tukipuuza, Sunna ya wetu MUHIBU, twapasa kuiigiza, MWENI kumsindikiza, ni wetu sote wajibu. Jazaye tumbi thawabu, ja kwamba mwaka timiza, Alonena MAHAUBU, si kwamba ninachombeza, Anza kesho kaka Abu, na wewe dada Aziza, MWENI kumsindikiza, ni wetu sote wajibu. Watu wa zote janibu, aula ni kujikaza, SITA shawali ajibu, RASULI kakokoteza, Tusikubali ghilibu, kwa bidaa kwokoteza, MWENI kumsindikiza, ni wetu sote wajibu. Haya enyi mashababu, mabanati nahimiza, Kadhalika mashaibu, pamoja na maajuza, Aula mjiratibu, SITA msezibeza, MWENI kumsindikiza, ni wetu sote wajibu. Kuzidi sitajaribu, beti SITA ninalaza, Kuacha usaribu, SITA anza dunduiza, Shawali iseghibu, bila SITAZE timiza, MWENI kumsindikiza, ni wetu sote wajibu. ABUU NYAMKOMOGI MWANZA.
Msaada
katika vyombo vya sheria. Alisema Amir Kundecha. Alisema, Umma wa Kiislamu na wapenda amani wamepata mstuko mkubwa kwa Serikali inayojinadi kuwa sikivu inayowasikiliza watu, ikiamini kabisa upo uhuru wa kujieleza na kutoa mawazo. Amir Kundecha, alisema sawa mawazo na maoni hayo yakafurahisha au yanakuchukiza, lakini zipo taratibu za kukosoa mawazo yanayochukiza. Alisema, wanaamini kuwa Sheikh Ponda, alikuwa akiwasilisha mawazo yake lakini pia ni sehemu kubwa ya m a l a l a m i k o ya Umma wa Kiislamu na inawezekana mawazo hayo yakatofautiana na ya mtu yoyote hivyo njia ya kukosoa ilikuwa sio kumlenga risasi. Alisema, Waislamu wanaamini kwamba tukio lilomkuta Sheikh Ponda Issa Ponda, halikufanywa na wahuni mitaani wala halikufanywa na walevi bali limefanywa
na watu wenye akili zao timamu. Lakini Amir Kundecha alisema, la kusikitisha sana ni tukio hilo kufanywa na vyombo vya dola, v yo m b o a m b a v yo vimeapa kufanya kazi kwa mujibu wa sheria katika ulimwengu wa haki na Demokrasia na zama za utawala bora.
Aw a l i a l i s e m a , zilikuwepo na taarifa kupitia vyombo vya h a b a r i z i k i o n ye s h a kuwa Sheikh Ponda, anatafutwa na Jeshi la Polisi, ila alisema anaamini Serikali na vyombo vya Dola, inapomtafuta mtu njia yake si kuagiza vyombo vya habari viandike kumtaarifu mtuhumiwa wake. Utaratibu wa kumtafuta mtu kisheria upo na wanaweza kumpata yeyote wanayemuhitaji bila kuleta madhara yoyote, kama kweli Jeshi l a Po l i s i l i n a m t a k a Ponda, limeshindwa kutumia njia sahihi na badala yake kutumia vyomb o vya hab ari kupika propaganda? Alisema na kuhoji Amir Kundecha.
Alisema, unapoona y u l e a n a ye t a k i wa kusimamia sheria anakuwa wa kwanza kuvunja sheria, basi kuna tatizo kubwa katika nchi.
Watukufu Waislamu nakufahamisheni ya kwamba sasa kunatenda ya Allah. Mtume S.A. W amesema kupitia maneno ya Allah ya kuwa Mja ni mja wangu, mimi na peponi ni wa pepo yangu mimi, basi na wewe mja wangu nunua pepo yangu kwa mali zangu nilizokupeni mimi. Kwa mujibu wa hadithi hii kwa yeyote ambaye yupo tayari Tunaomba Msaada wa hali na mali. Tunahitaji choo chenye matundu 25. Tunahitaji upande juu kama unavyoona. Unahitaji kisima cha maji. Umeme nguzo tayari kama unavyoona. Madrasa ya chuo na nursery school. Msikiti huu upo Kitunda Kibeberu. kwa yeyote ake kituoni hapo bila masharti afanye mwenyewe au awasiliane na Amiri wa Kituo hicho kwa namba 0714 565619 au 0753 673820 Akaunti ya Msikiti jina MASJID SWABIRINA 3300386233 K.C.B. WABILLAH TAWFIQ UST. KHATWIBU YUNUSU
Jipatie vitabu vyenye mafunzo ya Funga ya Ramadhani, vilivyoandaliwa na Sheikh Nurdin Kishki kama vile:- Hadithi 30 kuhusu Funga ya Ramadhan. Hukumu za Funga ya Ramadhan. Ipi Idadi sahihi ya Swala ya Tarawehe. Vingine ni Ndoa Talaka na Eda. Pamoja na Uislamu si Dini ya Ugaidi. Kwa mahitaji ya jumla na reja reja, ka dukani kwa Saimu Gwao, Msikiti wa Mtoro au Ibn Hazim MediaCentre. Simu:-0713 471 090, 0715 825 672, 0773 194 646.
12
AN-NUUR
MAKALA
12
Tanzania Muslim Hajj Trust Safari ya Hijja 2013 Uandikishaji unaendelea gharama za Hijja ni dola za Kimarekani $ 4200. Safari ni tarehe 5 na 7 Octoba, na Kurudi Tarehe 27 na 28 Octoba, 2013. Wahi kujiandikisha Sasa. Uandikishaji wa Hijja Zijazo 2014, 2015 kwa Kulipia kidogo kidogo, unaendelea. Simu: 0717 000 065, 0784 222 911, 0754 304 518, 0754 498 888 Au kupitia Tovuti yetu. www.hajjtrusttz.org. wametoa maoni yao kwa njia za simu na mitandao, wakiitaka serikali kuchukua hatua kama ilizochukua katika matukio ya kuuliwa Padri Mushi kule Mpendae Zanzibar na tukio la kulipuliwa Kanisa la Katoliki la Joseph Mfanyakazi, Olasiti Arusha. Katika matukio hayo, serikali iliagiza taasisi ya upelelezi ya Marekani FBI kusaidia kufanya chunguzi ili kubaini ukweli. Wengine wanaona kuwa tukio la kupigwa risasi Sheikh Po n d a , n i m a t o k e o ya kibri walichopata polisi kufuatia amri waliyopewa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda, kufuatia tukio la mlipuko wa Risasi katika mkutano wa CHADEMA kule Arusha, pale aliposema bungeni Juni mwaka huu, mimi nasema muwapige tu kwa sababu hakuna namna nyinginemaana tumechoka. Hata hivyo, tukio la kupigwa risasi Sheikh Ponda, limekumbusha wengi juu ya tukio la kitambo kidogo la kujeruhiwa kwa risasi Padri Ambrose Mkenda wa Kanisa Katoliki Za nz ib ar, wa k at i a l i p o k u wa a k i e n d a Kanisani kwa ajili ya misa. Tukio hilo lilifuatiwa na jingine la Februari mwaka huu ambapo safari hii, Padri Evarist Mushi wa Z a n z i b a r a l i p i g wa risasi na kuuliwa na watu wasiojulikana wa l i o k u wa k we n ye pikipipi. Katika tukio hilo lililozua hisia za chuki za udini, mara moja serikali iliagiza msaada wa kiuchunguzi wa shirika la upelelezi la Marekani la FBI kulisaidia jeshi la polisi katika uchunguzi. FBI pia walialikwa katika upelelezi wa tukio jingine la kulipuliwa kanisa Katoliki la Joseph Mfanyakazi la Olasiti Arusha. Tu k i o h i l o p i a lilihusisha hisia z a u g a i d i n a wa t u kadhaa walikamatwa, wakiwemo raia wanne wa nchi za Kiarabu wa l i o k u wa n c h i n i , waliotajwa kwa majina ya Said Abdallah Said, Abdulaziz Mubarak, Foud Saleem Ahmed na Said Mohsen waliokamatwa wakituhumiwa kuhusika na tukio hilo. Hata hivyo baada ya juhudi za ubalozi wa Saudia nchini, baadae raia hao walibainika kuwa hawahusiki na ugaidi huo na kuachiwa huru na kurejea makwao. W e n g i n e waliokamatwa walikuwa ni waendesha bodaboda Joseph Yusuph Lomayani na Victor Ambrose wote wakazi wa Arusha. T u k i o l a kushambuliwa Sheikh Po n d a , a m b a y e n i kiongozi wa dini bado halatangazwa kuwa ni la kigaidi japo lina sifa za ugaidi. K wa k u wa p o l i s i wamekanusha tuhuma zilizozagaa kuwa wa n a h u s i k a k a t i k a shambulizi hilo huku mtuhumiwa halisi akiwa bado hajakamatwa, kuna haja ya mamlaka kama ilivyofanya katika tukio la Padri Mkenda, Mushi, na lile la kulipuliwa Kanisa la Olasiti, serikali ikaazima nguvu za FBI kuchunguza zaidi ili kuondoa utata, hisia za udini na mashaka yaliyopo hivi sasa.
JESHI la polisi nchini Ta n z a n i a , t a y a r i limekanusha kuhusika na kumpiga risasi Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini humo, Sheikh Ponda Issa Ponda, ambaye amelazwa katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili baada ya kujeruhiwa kwa risasi. Sheikh Ponda alijeruhiwa kwenye bega lake la kulia, baada ya kupigwa risasi siku ya J u m a m o s i m j i n i Morogono alikokuwa a m e h u d h u r i a
kongamano la Waislamu. Awali taarifa zilienea kuwa, Sheikh Ponda alipigwa risasi na polisi waliokuwa katika jaribio la kutaka kumkamata. Wakati taarifa za kupigwa risasi Sheikh Ponda zikienea kwa haraka sehemu mbalimbali za nchi, mara moja Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro Bw. Faustine Shilogile, alikanusha madai ya polisi kuhusika kumpiga risasi Sheikh Ponda na kuwataka wa n a n c h i k u p u u z a uvumi huo. Hata hivyo Msemaji wa Polisi, Advera Senso,
alisambaza taarifa kwa vyombo vya habari Jumapili akithibitisha kuwa Sheikh Ponda anaendelea kutibiwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, lakini naye akidai kwamba jeshi la polisi halihusiki na tukio hilo. Kamanda Senso alisema kuwa, jeshi hilo limeamua kuunda Tu m e ya Wa j u m b e kutoka Jukwaa la Haki, kufanya uchunguzi wa tukio hilo. Kufuatia Jeshi la polisi ambalo ndilo linalotuhumiwa na tukio la kupiga risasi Sheikh Ponda kukanusha madai hayo, watu mbalimbali
Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na Business Printers Limited, S.L.P. 78495 Dar es Salaam.
Taasisi ya Khidmat Islamiya inawatanganzia Waislamu wote Safari ya Hijja kwa Gharama ya Dola 4450 tu. unaweza kulipa kwa awamu (Kuhijiwa) ni Dola 1450 tu. Kuondoka ni 5/10/2013 kurudi 27/10/ 2013 Piga Simu 0784 786680, 0713 986 671, 0774 786 680 E-Mail) hajjkhidmat@gmail.com , Tovuti (Website) www.khidmatislamiya.com
Markazi Ummu Suhail ni kituo cha kuhifadhisha Qur aan kwa Mabinti wa Kiislamu. Kituo ni cha bweni kipo mkoani Kilimanjaro wilaya ya hai. Umri: kuanzia miaka 13 na kuendelea. Kituo kitafunguliwa 9/08/2013 Inshaalah. Fomu za kujiunga zinapatikana msikiti wa Riadha, wahi nafasi ni chache Kwa mawasiliano zaidi tupigie simu namba 0754 029 518 Mlete mwanao apate elimu yenye manufaa.
14
AN-NUUR
15
AN-NUUR
16
AN-NUUR