Вы находитесь на странице: 1из 16

www.annuurpapers.co.

tz

Sauti ya Waislamu

Age of Deception

Siri ya mafunzo feki ya Al Qaida Mtwara


Tumieni CD za Rambo, Noris, Anold Msikilizeni Elbaradei kama mna akili Hizi ni zama mbaya. Age of Deception

ISSN 0856 - 3861 Na. 1094 DHUL-HIJJA 1434, IJUMAA , OKTOBA 11-17, 2013 BEI TShs 500/=, Kshs

Uk. 6

Sheikh amiminiwa risasi 40


Auliwa kama alivyouliwa Rogo Serikali yarushiwa tuhuma nzito

Waislamu watiwa msukosuko Mtwara


CHUCK Noris (kushoto) na John Rambo. Soma Uk. 6 Na Bakari Mwakangwale za kuzaliwa kulinganisha n a t u h u m a h i z o k wa WAJE wawaone watu kujiuliza kuwa huyu wenyewe maana itasaidia kweli alikuwa na dhamira hata kutumia akili zao tu Inaendelea Uk. 4

Sheikh Ibrahim Omari, maarufu Ibrahim Rogo , ameuliwa kama alivyouliwa Sheikh Aboud Mohammed Rogo.

Ni baada ya taarifa za ugaidi wa magazeti Sheikh atoa tahadhari, nasaha kwa Wahariri

2
AN-NUUR S.L.P. 55105, Simu: +022 2400786
www.annuurpapers.co.tz

Tahariri/Makala/Tangazo
Cel: 0784 370 208, 0713 110 148, 0755 260 087 , DSM. E-mail: annuurpapers@yahoo.co.uk Ofisi zetu zipo: Manzese Tip Top Usangi House (Jengo dogo), barabara ya Morogoro, D'Salaam

DHUL-HIJJA 1434, IJUMAA

OKTOBA 11-17, 2013

AN-NUUR

ZIPO taarifa kuwa kuna kamatakamata ya chini kwa chini inaendelea hasa maeneo ya Ilala na Buguruni ambapo watu kadhaa wamekamatwa na wanashikiliwa na Polisi. Inadaiwa kuwa watu hao, baadhi walikamatwa Misikitini na wengine nyumbani na wote inadaiwa kuwa walikuwa wakiangalia kanda za Al Shabaab. Kwa ambaye amewahi kuona CD hizo kama zilivyozagaa katika mitandao na akawahi kuangalia taarifa ya habari ya TBC1 Jumanne saa mbili usiku, ataridhika kuwa documentary hizo zimeandaliwa na watu maalum kwa lengo la kupiga propaganda ya k u wa t i a k a t i k a h a t i a Waislamu na kuupaka matope Uislamu. Kitu wanachotakiwa k u f a h a m u Wa i s l a m u ni kuwa hizi ni zama za udanganyifu (Age of Deception) kama anavyosema Mohamed Elbaradei. Documentary kama hizo zimetengenezwa nyingi na kuingizwa katika mtandao kwa malengo mawili. Moja ndio hizo vyombo vya habari kama TBC hutumia katika taarifa zao za habari katika jitihada za kuhusisha Waislamu na ugaidi. Pili, kuwatia hatiani Waislamu na kuleta kama kidhibiti kuwa wanajifunza ugaidi. Wanajua wakiziweka katika mtandao au CD Kuna watu watazifanyia biashara na wapo Wa i s l a m u w a t a t a k a kuzitizama. Lakini wanajua pia wapo Polisi waliokwisha andaliwa, wanajua nini cha kumfanya mtu watakayemkuta na CD hizo. Watamtia katika ugaidi. Sasa kuna haja kwa vijana wa Kiislamu na Waislamu kwa ujumla kuwa makini. Tutambue kuwa kwa muda mrefu kumekuwa na jitihada kubwa sana za kujiaminisha sisi wenyewe kuwa hapa Tanzania kuna kitisho cha kweli cha magaidi. Toka tulikuwa tukiambiwa kuwa magaidi hao ni wa kutoka nje

Tutajiangamiza kwa upumbafu

mpaka sasa tumefikia mahali pa kufanya juhudi mpya kwamba sasa magaidi hao wapo ndani ya nchi na wana kambi za kutoa mafunzo hayo kwa Watanzania wenzetu. Juhudi jingine ambayo tumekuwa tukiifanya kwa juhudi kubwa sana ni kuwatambulisha magaidi hao ni akina nani. B a a d a ya k a z i h i y o kubwa na ya muda mrefu ambayo imefanywa kwa juhudi kubwa na vyombo vya habari, mambo makubwa manne sasa yanajidhihirisha kama kielelezo cha mafanikio yaliyofikiwa. Moja, ni kukubalika kuwa nchi inakabiliwa na kitisho cha magaidi. Pili, kuwatambua magaidi hao kuwa ni al Qaida na Al Shabaab walio nje na ndani ya nchi. Tatu, Al Qaida na Al Shabaab hao ni wananchi wenzetu Waislamu. Nne, t u m e j i a m i n i s h a k u wa magaidi hao wana uwezo mkubwa sana usio wa kawaida, hata nchi ikitaka haiwezi kuwazuiya. Tunalotakiwa kutambua hapa ni kuwa kwa yote tuliyokuwa tukifanya, (Mwenyezi Mungu aepushilie mbali), yanaweza kutuletea balaa kubwa na hili likitokea itabidi tujilaumu wenyewe. Nitafafanua. Ifikirie nchi kama Marekani na maguvu yake ki-intelijinsia, kijeshi, kipolisi, Sheria za uhamiaji, u d h i b i t i wa wa s a f i r i kuingia kupitia viwanja vya ndege na bandarini, tekinolojia na umakini wa vyombo vya kusimamia sheria, lakini tunaambiwa kuwa magaidi kutoka nchi duni kwa kila kitu, Afghanistan wameingia na kushambilia sehemu nyeti kama Pentagon na WTC! Haikuishia hapo bado tunaambiwa kuwa kumekuwa na mashambulizi mengine madogo nadogo kama hili la juzi la Boston Marathon Bombing! Kwa waliowahi kufika Marekani baada ya Septemba 11, 2001 wanajua kiwango cha upekuzi na harakati za kiusalama zinazofanyika. Lakini bado tunaambiwa kuwa Al Qaida wameweza kufanya

shambulizi la Boston na kuuwa watu! Mambo mawili hapo yanajitokeza: Moja ni kuwa lazima tukubali kuwa magaidi hao ni hatari sana na uwezo wao ni mkubwa sana na kwamba kama hata baada ya kuuliwa Osama Bin Laden, bado wana uwezo wa kupiga Marekani, basi sisi huku uwezo wa kukabiliana nao utakuwa ni mdogo sana. Pili, kama hilo la kwanza sio sahihi, basi tukubali kuwa tumetiwa upumbafu wa kutisha kuwa likitokea jambo hatuna muda wa kuhoji hakika yake. Tunakwenda tu na ujinga tuliokwishalishwa kuwa hao ni Al Qaida. Hatari iliyopo ni kuwa ukishaaminishwa kuwa wapo Al Qaida wenye uwezo wa kiwango hicho na ukifikishwa mahali kuwa akili yako ishaliwa na virusi vya kulemaza kufikiri na kuhoji, kinachoweza kutokea ni kuwa usiyemdhania kabisa anaweza kutumia fursa hiyo kufanya shambulio akijua wazi kuwa wala hutahangaika kuchunguza nini kimetokea na nani kahusika. Anajua kabla hata Tw i t t e r h a i j a s e m a waliohusika ni Al Qaida/Al Shabaab, tawi la Tanzania, wewe tayari ushajiaminisha kuwa hakuna wa kufanya hilo ila magaidi wa Al Shabaab/Al Qaida. Katika zama hizi za elektroniki na dijitali, ambapo mtu anaweza kuanzisha blog/page, katika mtandao na akaipa jina na anuwani anayotaka, nini na nani mweye Twitter ipi? Lakini anajua kwa upumbafu waliokwishatiwa watu kupitia vyombo vya habari, ikitokea tu Al Jazeera ikasema, Twitter ya Al Qaida/Al Shabaab,

imesema wanahusika, hutakuwa na muda wala akili ya kuhoji na kutafakari. Utaimba hilo hilo la Twitter. Huu ni upumbafu wa kutisha na kwa hakika unaochefua na ndio utakaotuangamiza. Na kwa hali hii ambapo Al Qaida wana nasibishwa na wanaorukuu na kusujudu, basi watakaofanya shambulio ambao wewe wala hutawafikiria, wanajua wazi kuwa watu wa upande mwingine watataka kulipa kisasi. Na hiyo itakuwa njia ya uhakika ya kuitia nchi katika machafuko. Hivi sasa kuna ukaguzi mkubwa unaofanyika kwa watu wanaoingia katika maduka makubwa kama Mlimani City na Quality Plaza. Lakini tujiulize, hivi pale Westgate hapa kuwa na walinzi? Hapa kuwa na camera za security. Awali ikasemwa gaidi mwanamke kaingia na kikosi cha watu 30 na lundo la AK-47. Sasa tunaambiwa ni kama watu saba/nane tu wanaoshikiliwa na kuhojiwa. 23 hawajulikani wameyeyukia wapi. Ndio hii mara wadau wakuu katika kututia ujinga ( wa h a r i r i / wa a n d i s h i ) wa n a s e m a h a o 2 3 n a Kamanda Mkuu Samantha wametoroka kupitia mtaro wa maji machafu. Hebu ichukulie Westgate kama Mlimani City au Quality Plaza. Ndani kuna askari na makachero kwa mamia wanaopambana na magaidi. Nje jengo limezungukwa na mamia ya Polisi na wanajeshi wakiwa na silaha nzito. Mtaro upi wa maji machafu magaidi 23 na kamanda wao watatumia kutoroka? Kama si mtaro huo wa maji machafu, Samantha alipitaje ngome hii ya askari? Labda askari h a o wa t u a m b i e n d i o wa l i o m r u h u s u k u p i t a

na kwa maana hiyo wao watakuwa ndio wa mwanzo kuhojiwa watuambie nini kilitokea. Kama tunaamini kuwa magaidi waliweza kuingiza silaha za kutosha p a l e We s t g a t e M a l l , Nairobi, bila kugundulika na vyombo vya usalama, wakashambulia na kuondoka, hapana shaka magaidi hao kama w a t a i n g i a Ta n z a n i a , itakuwa vigumu kuwadhibiti. Kwa mtindo huu wa kuwa na Boston Marathon Bombing baada ya harakati zote za kiusalama baada ya Septeba 11, pamoja na kumuuwa Osama Bin Laden, ni wazi kuwa hakuna Usalama wa Taifa, Polisi, Mgambo, Polisi Jamii au Jeshi wanaoweza kuzuiya magaidi hawa. We unapekuwa watu Mlimani City, wao watapiga sokoni Kariakoo. Ukizidisha upekuzi Kariakoo watapiga soko la Tandale! Unazidisha ulinzi Dar na Arusha, wanashambulia Kibondo na Kirando! Sisi tunadhani kuwa kubwa la kufanyika hapa ni kufanya utafiti wa kisomi kukitambua kwanza kwa uhakika hiki kirusi Al Qaida/Al Shabaab na ugaidi wake kwa sababu kinavyoonekana kasi yake ya kujibadili (mutation) ni kubwa mno ambao unampa uwezo wa kushambulia usipotarajia, akapita mahali bila wewe kumtambua kama tunavyoaminishwa kuwa walifanya WTC, Pentagon, Boston, Westgate Kenya na kwingineko. H i i m a a n a ya k e n i kuwa dawa ya kupekuwa watu, kutumia mbinu za kipolisi na usalama wa taifa, zinaweza kuishia kuuwa na kutesa tu watu wasio na hatia, lakini bado hatutakuwa salama.

Ubungo Islamic high School


MAANDALIZI YA KUJIUNGA KIDATO CHA I, 2014 (PRE- FORM ONE ORIENTATION COURSE)

P.o. Box 55105 Tel: 2450069, 0712 974428, fax: 2450822 Dar es salaam. E-mail: ipcubungoislamic@gmail.com

UBUNGO ISLAMIC HIGH SCHOOL inatangaza program maalum ya maandalizi ya kujiunga na kidato cha kwanza 2014. Program hii itaanza tarehe 16/09/2013 hadi tarehe 16/12/2013. Jumatatu hadi ijumaa kuanzia saa 2:00 kamili asubuhi hadi saa 9:00 Alasir. Masomo yatakayofundishwa ni:Elimu ya dini ya Kiislamu, English language, Lugha ya kiarabu, basic Mathematics na Computer. ADA: Ni Tshs 60,000/= (Elfu sitini) tu. Inalipwa yote kabla ya kuanza programu. Fomu za Kujiunga zinapatikana shuleni BURE baada ya kulipa ada. Mlete mwanao apate Elimu yenye tija itakayomweze kujiunga na kidato cha kwanza. Kwa mawasiliano zaidi piga simu namba: 0714 888 557/0712 974428 Wabllah tawfiq MKUU WA SHULE

3
MOMBASA J A M I I ya Wa i s l a m u Mombasa nchini Kenya, wamedai kuwa Maofisa wa Kupambana na Ugaidi Kenya ndio waliomuua Sheikh Ibrahim Omar na wenzake watatu. Aidha wamedai kuwa maofisa hao wanaandaa m i p a n g o ya k u m u u a Sheikh mwingine aliyetajwa kwa jina la Abu Bakar Makaburi. Habari kutoka Mombasa Kenya, zimeeleza kuwa Sheikh Ibrahim Omari, maarufu Ibrahim Rogo na wenzake watatu walipigwa risasi na kuuliwa wakiwa ndani ya gari lao katika barabara ya Bamburi mjini Mombasa. Mashuhuda wamedai kuwa Sheikh Ibrahim Omar na wenzake hao walipigwa risasi zaidi ya arobaini, hali iliyoonyesha kuwa maadui hawakutaka kumbakisha hata mtu mmoja kwenye msafara huo, uliokuwa unatoka katika msikiti ambao marhuum Sheikh Aboud Mohammed Rogo, kaka wa marehemu ambaye naye anadaiwa kuuliwa na polisi mwaka jana, na wahusika hajakamatwa hadi sasa. Ta a r i f a z i n a e l e z a kwamba Abu Makaburi na Sheikh Ibrahim Omar, kabla ya kukutwa na mauti walikuwa wakipata v i t i s h o v ya k u u l i wa , ikidaiwa kuwa vitisho hivyo vililenga kuzima vuguvugu la Da'awah ya haki. Kufuatia kushambuliwa Jengo la kibiashara la Westagte ambapo watu zaidi ya 67 waliuliwa, imedaiwa kuwa maofisa wa serikali wamekuwa wakipanga mkakati wa kuwapoteza vijana na Masheikh ambapo katika orodha yao, imebainika kuwemo majina ya Sheikh Ibrahim na Abu Bakar Makaburi. Imeelezwa kwamba siku mbili kabla ya Sheikh Rogo na wenzake kufikwa n a m a u t i , u l i e n e z wa uvumi katika mji wa Mombasa kuwa Abu Bakar M a k a b u r i a m e u l i wa , jambo lililowatia hofu Waislamu wa eneo hilo. Pamoja na kuuliwa Sheikh Ibrahim Rogo na wenzake watatu, habari zinaarifu kwamba mtu a n a y e c h u n g u z wa n a kufuatiliwa kwa karibu zaidi na maofisa hao wa kupambana na Ugaidi, ni Abu Bakar Makaburi na kwamba, mpango uko mezani na utatekelezwa wakati wowote.

Habari

DHUL-HIJJA 1434, IJUMAA

OKTOBA 11-17, 2013

AN-NUUR

Kwa upande wao, Waislam wa Mombasa wameeleza kuwa Serikali ya Kenya imeamua kuwaua baada ya kushindwa vita vyao na Somalia. A wa l i P o l i s i K e n ya ilitangaza kuwa, watu wanne akiwemo Sheikh Ibrahim Ismail Rogo, wa m e u a wa u s i k u wa Alhamisi Octoba 3, baada ya kupigwa risasi na watu wasiojulikana wakiwa ndani ya gari dogo mjini Mombasa. Taarifa ya Polisi ya Kenya imeeleza kuwa, Sheikh Ibrahim Rogo alikuwa mrithi wa Sheikh Aboud Rogo, ambaye naye aliuawa pamoja na familia yake kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana mwezi Agosti 2012. Mauaji ya Sheikh Ibrahim Rogo ambayo yameutikisa mji wa Mombasa, ya m e t o k e a b a a d a ya kupita takriban wiki mbili tangu kutokea uvamizi wa maduka ya Westgate jijini Nairobi, uliodaiwa kufanywa al Shabab au al Qaeda ambapo watu wasiopungua 63 waliuliwa na wengine kujeruhiwa. Polisi wamesema k u wa m u h u b i r i h u y o alikuwa amehubiri katika m s i k i t i u l i o h u s i s h wa na wanamgambo wa Kiisilamu wa Al Shabaab. Baadhi ya wananchi wa Mombasa wanakituhumu kikosi maalumu cha kupambana na ugaidi kuwa ndicho kilichotekeleza mauaji hayo. Sheikh Ibrahim Rogo, ambaye alikuwa akitoa mihadhara kwenye Msikiti wa Musa mjini Mombasa, alituhumiwa na jeshi la polisi kuwa anawachochea vijana wa Kiislamu kujitumbukiza kwenye makundi ya kigaidi. Polisi ya Kenya imesema kuwa, Gaddafi Mohammad, Issa Abdallah na Omar Abu Rumeisa ni miongoni mwa waliouawa, huku Salim Aboud akinusurika katika shambulio hilo. Sheikh Ibrahim Rogo, alikuwa muhubiri katika msikiti aliokuwa akihubiri k a k a ya k e m a r e h e m u Sheikh Aboud Rogo, ambaye pia aliuawa kwa kupigwa risasi mwaka jana. Vyombo vya usalama Kenya vimekuwa vikimshutumu Sheikh Rogo kuwa anatoa mafunzo yanayodaiwa kuwa ni yenye itikadi kali, ambayo yanadaiwa k u wa s h a w i s h i v i j a n a kujiunga na makundi ya kigaidi kama Al Shabaab.

Sheikh amiminiwa risasi 40


Siku ya Jumatatu Agosti 27, 2012, Sheikh Aboud Rogo Mohammed kaka wa maremu Sheikh Ibrahim Rogo aliyeuliwa alhamisi iliyopita, aliuawa akiwa katika gari yake wakati akimpeleka mkewe hospitalini mjini Mombasa. Mauaji hayo yalisababisha ghasia a m b a p o wa t u wa t a t u walipoteza maisha yao, ambapo ilielezwa kuwa polisi waliokuwa wakijaribu kutuliza ghasia za baada ya kifo cha Sheikh Rogo ndio chanzo cha mauaji hayo. Ilielezwa kuwa mauaji ya Sheikh huyo yalitia shaka kama yalikuwa ni alama ya ukatili au ni sura nyengine ya vita dhidi ya ugaidi. Siku moja baada ya mauaji hayo, shirika la kutetea haki za binaadamu, Human Rights Watch, likatoa taarifa ya kutaka uchunguzi wa haraka ufanyike dhidi ya mauaji ya Sheikh Rogo, pamoja na kulaani mauaji hayo na vurugu za baada ya mauaji. "Tunataka uchunguzi wa kina juu ya kile ambacho kimemtokea Sheikh Rogo. Tunadhani ni lazima tukio hili lichunguzwe na hatua zichukuliwe." Alisema Ben Rawlence, Afisa wa Utafiti wa Shirika la kutetea haki za binadamu alipozungumza na DW kwa njia ya simu akiwa jijini Nairobi. Baraza la Usalama l a U m o j a wa M a t a i f a lilimuwekea vikwazo vya kusafiri na kuzuia mali zake mwezi Julai, likidai kuwa alikuwa ametoa "msaada wa kifedha, vitu, mafao au ufundi kwa alShabaab." Kwa mujibu wa Baraza hilo, Sheikh Rogo alikuwa ndiye "kiongozi mkuu wa kiitikadi" wa kundi la Hijra la Kenya, ambalo pia linajulikana kama Kituo cha Vijana wa Kiislamu, na ambalo Umoja wa Mataifa unalichukulia kuwa mshirika wa karibu wa alShabaab kwa Kenya. A wa l i P o l i s i n c h i n i Kenya walimkamata Sheikh Aboud Rogo, kwa tuhuma za kumkuta na silaha kinyume na sheria. Alipelekwa mbele ya mahakama ya Mombasa Agosti 14 kwa mashitaka ya kupanga mashambulizi katika maeneo ya umma. Aliyakana mashitaka dhidi yake na kuachiwa kwa dhamana hadi Oktoba 15, ambapo kesi yake ilikuwa isikilizwe tena. Lakini akauawa takribani wiki tatu kabla ya tarehe hiyo. Kwa mujibu wa vyanzo

mbalimbali vya habari, S h e i k h R o g o a l i k u wa ameliarifu jeshi la polisi nchini Kenya, Julai 24, 2 0 0 2 k wa m b a m a i s h a yake yalikuwa hatarini na kwamba alihitaji ulinzi. Ripoti hiyo aliiwasilisha pia kwenye Kamisheni ya Haki za Binaadamu ya Kenya na pia mahakama ya nchi hiyo. Kwenye taasisi hizo zote, Sheikh Rogo aliripoti kwamba, watu waliojidai kuwa polisi walikuwa wa m e j a r i b u k u m t e k a nyara yeye na mwenzake, Abubakar Sharif Ahmed. Hata hivyo kilisababisha mauaji ya Sheikh Aboud Rogo, hakijajulikana hadi leo wala wahusika kukamatwa. Lakini mashirika ya haki za binadamu ya ndani na nje ya Kenya yaliinyoshea vidole mamlaka za Kenya, kwamba hata kama hazihusiki moja kwa moja, bado zina wajibu wa moja kwa moja wa kuwalinda raia wake, na katika hili kufanya uchunguzi wa kina. Wa z i r i M k u u w a wakati huo, Raila Odinga alilitolea maelezo jambo hilo, akisema kwamba waliofanya mauaji hayo ni maadui wa Kenya ambao wanataka kuiingiza nchi hiyo kwenye mapambano ya kidini. Kufuatia mauaji hayo, Al-Amin Kimathi, Mwenyekiti wa Jukwaa la Waislamu la Haki za Binaadamu nchini Kenya, alisema hana sababu ya kuiamini serikali kwani si mara moja wala mbili mauaji kama haya kutokea na wala hakukuwa na hatua zilizochukuliwa. Kenya ilipeleka wanajeshi wake nchini S o m a l i a m wa k a j a n a , kwa lengo la kupambana na wanamgambo wa alShabaab, ambao Kenya inawatuhumu kwa kufanya mashambulizi ndani ya ardhi yake, ikiwemo pia utekaji nyara wageni na wafanyakazi wa mashirika ya misaada. Lakini Ben Rawlence wa shirika la kutetea haki za binaadamu la Human R i g h t s Wa t c h , h a o n i uhusiano wa moja kwa moja wa sura hizi mbili za kupambana na ugaidi. "Siwezi kusema kwamba Kenya inafuata mtindo huo wa Marekani. Hata Marekani yenyewe haiwezi kumuua raia wake nchini mwake. Na sisi hatuwezi k u j u a k u wa n i k we l i serikali imehusika, lakini mahakama na sheria za Kenya zipo. Mtuhumiwa anapaswa

kupelekwa mahakamani na kuhukumiwa kisheria. Si kuuawa mitaani." Alisema Bw. Rawlence. Kwa mujibu wa taarfa ya Jukwaa la Haki za Binaadamu kwa Waislamu, m n a m o m we z i M a c h i mwaka 2002, mhadhiri mwengine wa Kiislamu, Samir Khan, aliyekuwa pia akikabiliwa na mashitaka ya kuwa na silaha kinyume na sheria na kutoa mafunzo kwa ajili ya al-Shabaab, na rafiki yake Mohammed Qassim, walitolewa kwenye basi mjini Mombasa na watu waliojitambulisha kama polisi. Mwili wa Khan ulikuja kugundulika siku kadhaa baadaye katika mbuga ya Tsavo, ukiwa umekatwakatwa vibaya huku hatima ya Kassim ikiwa hadi sasa haijuilikani. Kwa mujibu wa Human Rights Watch, mwanzoni Polisi ya Kenya ilikuwa imewaambia waandishi wa habari kuwa Khan alikuwa ameshikiliwa na Kikosi Maalum cha Kupambana na Ugaidi, lakini baadaye wakakana kumshikilia. Mara kadhaa, wakili wa Sheikh Rogo, Mbugua Mureithi, alikuwa amesema mteja wake alilalamikia kufuatwafuatwa na polisi, na hata kumtaja afisa mmoja wa polisi ambaye alimtishia kwamba wao, polisi, wangelitafuta njia ya kumalizana naye. Al-Amin Kimathi, ambaye mwenyewe si mgeni wa kutiwa misukosuko na polisi, anasema kwamba hayo hayashangazi. Wakati Wakenya na dunia wakisubiri majibu kwa mauaji dhidi ya Sheikh Aboud Rogo na machafuko ya l i y o t o k e a b a a d a ya hapo, majibu ya kutekwa na hatimaye kutoweka kwa akina Samir Hashim Khan, Mohamed Bakhit Qassim, Sylvester Opiyo, Jacob Musyoka, Jeremiah Onyango Okumu, Stephen Mwanzia Osaka, Omar Shaib na Salim Abubakar ndani ya kipindi hicho cha mwaka mmoja, bado hayajapatikana. Kwa mujibu wa Jukwaa la Haki za Binaadamu la Waislamu nchini Kenya, matukio yote hayo yaliripotiwa kwenye vyombo vya dola. Katika mazingira yale yale, kauliwa kaka yake Aboud Rogo, Sheikh Ibrahim Omar Rogo na wenzake watatu. Mauaji ya Sheikh Ibrahim Rogo na vijana wengine watatu wa Kiislamu, ni i s h a r a t o s h a k wa m b a maisha ya walinganiaji wa Kiislamu yamo hatarini kwa mgongo wa lugha ya ugaidi, al shabab na al Qaeda.

4
Inatoka Uk. 1 hiyo? Au mazingira haya yanalingana na mafunzo ya Al-qaid au kijeshi ? Kuliko kukurupuka bila kupata maelezo ya upande wa pili wa jambo lenyewe, zaidi huishia kuwatisha wananchi tu. Hali imekuwa ya wasiwasi huku polisi wakimwagwa katika baadhi ya vijiji Wilayani N a n y u m b u b a a d a ya kuripotiwa kuwepo kwa magaidi wa Al Qaida. Taarifa zinasema, askari wamekuwa ni wengi na wanawapa tabu wananchi hasa Waislamu. Mashuhuda wanasema kuwa askari wamemwaga kila sehemu, katika mji huo na zaidi wamekuwa wakiwaandama Waislamu haswa wale wenye kajipamba na zile sifa za Kiislamu, huangaliwa ama kudhaniwa ni adui hivyo wanakuwa ni watu wa kupata misukosuko ya ajabu kwa kuwatuhumu ugaidi. Katika hali hiyo, baadhi ya viopngozi wa Dini ya Kiislamu Mkoani Mtwara, wamelaani taarifa ya Jeshi la Polisi na kushabikiwa na vyombo vya habari kuhusiana na vijana 11 kuwa walikuwa mafichoni wakipata mafunzo ya kijeshi. Vyombo mbalimbali vya vya habari mapema wiki hii, viliripoti taarifa ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Zelothe Stephen, kwamba wamewatia mbaroni vijana hao na kudai kuwa walikuwa wakipata mafunzo ya kijeshi ambayo ni hatari na yakutisha. Tukio hilo limeripotiwa kutokea katika milima ya Kijiji cha Nakopi, kilichopo kati ya Wilaya za Masasi, Nanyumbu na Newala, ambapo wanadaiwa kukutwa na CD za AlShabab, mapanga mawili na Visu. Mmoja wa viongozi hao, aliyepo Wilayani Nanyumbu, alilifahamisha gazeti hili kwa njia ya simu akidai kwamba vyombo vya habari vimep ak a matope juu ya suala hili, na kwamba anadiriki kusema kuwa vimekurupuka sana kwa kule kuripoti kuwa wamekamtwa magaidi. Akavitaka vyombo v ya h a b a r i k u t o i s h i a hapo katika kulikuza na kulishabikia suala hilo na kuwatisha wananchi hususani katika eneo la tukio, zaidi akavitaka vyombo hivyo kufika eneo la tukio kufanya uchunguzi wa kina kuliko kulishwa habari na Jeshi la Polisi. Waje wawaone watu wenyewe maana itasaidia

Habari

DHUL-HIJJA 1434, IJUMAA

OKTOBA 11-17, 2013

AN-NUUR

hata kutumia akili zao tu za kuzaliwa kulinganisha n a t u h u m a h i z o k wa kujiuliza kuwa huyu kweli alikuwa na dhamira hiyo (?) au mazingira haya yanalingana na mafunzo ya Al-qaid au kijeshi (?), kuliko kukurupuka bila kupata maelezo ya upande wa pili wa jambo lenyewe, zaidi huishia kuwatisha wananchi tu. Alisema. Kiongozi huyo akielezea tukio hilo alisema, wao baada ya kusikia vijana hao wamekamatwa na taarifa zikihusisha tukio hilo na Uislamu, waliwasiliana na baadhi ya Polisi wa kituo cha Nangaka, kama pia waliwakamata na silaha za moto, lakini akadai kwamba walijibu kuwa hawakuwakuta nazo. N i k a wa h o j i , k a m a silaha za moto hawakuwa nazo, sasa kosa lao ni lipi, ili hali pia ni wakazi wa huko huko Likokona, alinijibu kuwa hayo yote yanaendelea kuchunguzwa, kwa kuwa taarifa zao wamezipata kupitia uongozi wa kijijini kwao. Alisema kiongozi huyo. Alisema, vijana hao wamekuwa na shughuli zao za mazoezi ya mwili kila siku katika utaratibu wao waliojiwekea, lakini alidai taarifa zao zilivyoripotiwa zimegubikwa na propaganada zaidi kuliko uhalisia wa jambo lenyewe na haswa baada ya kunaswa na vyombo vya habari. Alisema, hali hiyo hawajakutwa na silaha za moto zaidi ya kuwa na panga na visu, ambavyo vitu hivyo si kosa kuwa navyo hususani kwa watu wa vijijini, kwani ndiyo vitendea kazi vikubwa katika shughuli zao. K wa u p a n d e wa k e Naibu Amir wa Jumuiya moja ya Kiislamu Mkoani humo, alisema, hajafika eneo la tukio lakini kwa m u j i b u wa m wa l i m u mmoja wa Shule ya msingi aliyeko katika Kijiji hicho, alimueleza kuwa, vijana hao walikamatwa na kufanyiwa mahojiano ya kawaida na Polisi kujiridhisha na ndio maana walipewa dhamana, kulingana na wepesi wa tuhuma zenyewe. Mwalimu huyo, alimueleza Amir huyo kuwa kadhia hiyo, ni ya wiki moja iliyopita wala si ya wiki hii kama umma

Waislamu watiwa msukosuko Mtwara


u l i v y o h a b a r i s h wa n a vyombo vya habari, na ilikuwa ni ya kawaida kwani vijana hao wana kawaida ya kwenda na kurudi katika mazoezi ya viungo na wala si kwa kificho. Tukio hili limetokea siku nane au saba zilizopita, lakini zimeripuka upya, kutokana na namna lilivyoripotiwa na vyombo vya habari na kuwa kama ni suala jipya kabisa na la hatari. Alisema Amir huyo. Kabla ya hapo, alisema tukio hilo la kukamatwa vijana hao lilikuwa ni la kawaida tu, maana walichukuliwa na Polisi wakahojiwa na kupewa dhamana, lakini akadai, baada ya vyombo vya habari kuripoti katika sura ya hatari, sasa vijana hao wamekamatwa tena licha ya kuwa nje kwa dhamana na wamesafirishwa kwa magari ya Polisi zaidi ya mawili. Awali, imeelezwa kuwa wiki moja iliyopita, kabla ya k u r i p o t i wa k a t i k a vyombo vya habari, vijana h a o wa l i p o k a m a t wa walipelekwa katika kituo cha Polisi na kuhojiwa kisha walipelekwa Mkoani Mtwara, na waliporudi walifikishwa Mahakamani. Kadhia hii ilitokea I j u m a a ya w i k i m o j a iliyopita ilitulazimu sisi kufika katika kituo cha Polisi Nangaka, na baada ya kupata fursa ya kuonana nao tuliwahoji ambapo wa l i t u e l e z a k wa m b a walikutwa mlimani, wakifanya mazoezi ya mwili, lakini pia katika r a t i b a ya o wa l i k u wa wa k i e n d e s h a d a r s a . Kilisema chanzo chetu kikinukuu maongezi yao na vijana hao. Imeelezwa kuwa, vijana hao walitolewa kwa dhamana Ijumaa ya wiki iliyopita na kurejea makwao na baada ya hapo zilifatia taarifa katika vyombo vya habari katika sura tofauti kabisa na uhalisia wa tukio hilo lilivyo. Baada ya vijana wale kutolewa ndipo tukasikia taarifa kupitia vyombo vya habari kupitia Televisheni, magazeti na mitandao ya kijamii, kuwa Wilaya ya Nanyumbu wamekamatwa vijana 11, wakijifunza ugaidi. Wakati taarifa hizo zinaripotiwa hivyo vijana hao wapo nje kwa dhamana na wala suala hili halikuwa na ukubwa

kama lilivyoripotiwa. Kilisema chanzo chetu kwa mshangao. Taarifa hizo zilieleza kuwa baada ya taarifa hizo kupitia vyombo vya habari, zilipatikana taarifa kuwa vijana hao wanatakiwa wakamatwe tena, jambo ambalo lilitekelezwa na vijana hao walikamatwa siku hiyo hiyo. Leo asubuhi (Jumatano) nilifika katika kituo hicho cha Polisi, nimekutana na ndugu wa vijana hao ambao walitokea huko Kijijni, ambao walikuwa wanafuatilia ndugu zao na kuthibitisha kweli walikamatwa na kwamba wapo ndani. Niliporudi kuwaandalia chai ili tuwapelekee pale, niliona gari za Polisi, zikiongozana moja likiwa na jamaa zetu wakiondoka nao, huku nyuma wakifuatiwa na gari ya Kamanda wa Polisi Mkoa (RPC). Kilieleza chanzo chetu cha habari. Chanzo hicho kilieza kwamba vijana hao wamechukuliwa ingawa wapo nje kwa dhamana huku sababu za msingi zikiwa hazieleweki kufutia hatua hiyo. Kufutia hatua ya kukamatwa tena vijana hao na Jeshi la Polisi, mpashaji wetu habari alisema kwamba hadhani kuwa watuhumiwa hao walivunja mashariti ya d h a m a n a , p a m o j a na kwamba hajayajua, ndio maana walipoenda kukamatwa waliwakuta katika makazi yao hapo Kijijini. Naye Ustadhi Pwirila, aliye makazi Wi l a ya n i N a n y u m b u , akizungumzia tukio hilo, aliitaka Serikali kuwa makini pindi wanapopata taarifa za aina yoyote, k wa n i a l i d a i e n d a p o watakuwa wanazichukua kwa kukurupuka bila kuzifanyia kazi, wanaweza wakawa wanawatesa watu bila kuwa na hatia yoyote. Alisema, kutokana na Jeshi la Polisi kuwakamata vijana hao kwa mara ya kwanza na kuwahoji kisha kuwafikisha Mahakamani, wa l i s h a r i d h i k a k u wa wa n a st a hi l i dhama na kulingana na tuhuma wanazowatuhumu nazo. Lakini akasema, kitendo cha kuwakamata t e n a b a a d a ya s u a l a hili kuripotiwa kupitia vyombo vya habari na kuonekana kubwa na zito kuliko uhalisia wenyewe,

wamechukua jukumu la kuwakamata tena. Huu ni uonevu wa dhahiri unaofanyika dhidi ya Waislamu, na pengine Serikali yetu inafanya kazi kwa kuongozwa na vyombo vya habari kwani suala hili walivyorilipoti limestua zaidi kuliko ambavyo lilikuwa halijaripotiwa. Alisema. Ama kuhusu Jeshi la Polisi, Ust. Pwirila, alisema linapaswa pia kuwa makini kwa sababu wanapokamata watu kwa tuhuma wawe wepesi kuwafikisha katika m i k o n d o m i n g i n e ya sheria ili waweza kujieleza kwa mujibu wa sheria kuliko kukaa nao kwa muda mrefu. Si sahihi kuendelea k u m n g a n g a n i a mtuhumiwa kwa muda mrefu sana, upande mwingi inaonekana kama ni utesaji na kuwanyima watu haki zao na suala hili limekithiri sana kwa watuhumiwa wanapokuwa ni Waislamu. Alisema. Ust. Huyo alisema, baada ya kadhia hiyo, kuripotiwa na vyombo vya habari, askari wamekuwa ni wengi na wanawapa tabu wananchi hususan Waislamu. Alisema, askari wamemwaga kila sehemu, katika mji huo na zaidi wamekuwa wakiwaandama Waislamu haswa wale wenye kajipamba na zile sifa za Uislamu, huangaliwa ama kudhaniwa ni adui hivyo wanakuwa ni watu wa kupata misukosuko ya ajabu. Mmoja wa viongozi wa M s i k i t i Wi l a ya n i Nanyumbu, aliliambia gazeti hili kuwa, amestushwa na taarifa k u p i t i a v y o m b o v ya habari siku ya Jumanne, wiki hii pamoja na kuwa watuhumiwa hao walikuwa wapo nje kwa dhamana. Sasa inasemekana Mkuu wa Polisi wa Mkoa (RPC), ameamuru vijana wale wakamatwe tena wakati Mahakama iliwaachia kwa dhamana, hivyo mpaka sasa ( Jumatano) wapo mikononi mwa Polisi tena. Alisema kiongozi huyo. Ama kuhusu CD, wanazotuhumiwa nazo, alisema mikanda hiyo ipo kwa watu mbalimbali na pengine na wao walikuwa nayo kwa ajili ya kungalia tu huwezi kusema moja kwa moja malengo yao i l i k u wa n i k u j i f u n z a ugaidi.

Habari za Kimataifa

DHUL-HIJJA 1434, IJUMAA

OKTOBA 11-17, 2013

AN-NUUR

BALI WAZIRI wa Mambo ya Nje wa Marekani, John Kerry, ametetea hatua ya nchi yake ya kufanya operesheni za kijeshi katika nchi za Libya na Somalia. John Kerry ambaye hivi sasa yuko kisiwani Bali, Indonesia kwa ajili ya kushiriki katika kikao cha Jumuiya ya Kiuchumi ya Asia na Pasifiki (APEC), amedai kuwa, Marekani haitaacha kampeni zake za kupambana na makundi ya kigaidi. A i d h a Wa z i r i h u y o wa Mambo ya Nje wa Marekani amejigamba

Marekani kuendeleza mashambulizi Afrika


kuwa, wanachama wa mtandao wa al Qaida na makundi mengine ya kigaidi wanaweza kukimbia, lakini kamwe hawawezi kujificha. Hivi karibuni vikosi vya Marekani vilifanya mashambulizi katika maeneo kadhaa ya Somalia na Libya kwa madai ya kupambana na magaidi. Marekani inadai kuwa Jumamosi ilimtia mbaroni Abu Anas al Liby, kiongozi wa ngazi za juu wa al Qaida kwa madai kuwa alihusika katika operesheni za kushambulia balozi za Marekani katika nchi za Kenya na Tanzania miaka 15 iliyopita. Katika shambulio jengine, vikosi vya Marekani vimeua wanamgambo kadhaa wa al- Shabab nchini Somalia, baada ya vikosi hivyo kuvamia makazi ya kamanda mmoja wa wanamgambo hao katika mji wa Baraawe. Hata hivyo taarifa zinabainisha kuwa wanajeshi wa Marekani walishindwa kumkamata kamanda huyo wa alShabab.(irib.ir)

TEHRAN MKURUGENZI wa Shirika la Atomiki la Iran (AEOI), Dk. Ali Akbar Salehi, amesema kuwa vikosi vya usalama vya Iran vimewatia mbaroni watu wanne wa l i o k u wa wa n a p a n g a njama za kufanya hujuma kwenye taasisi moja ya nyuklia humu nchini. Dk. Saleh ameongeza kuwa, wahujumu hao wanne wametambuliwa. Hata hivyo imeelezwa kuwa Mkurugenzi huyo hakutoa ufafanuzi zaidi kuhusu jambo hilo kwa sababu za kiusalama. Katika miaka ya hivi k a r i b u n i , wa n a s a ya n s i kadhaa wa nyuklia wa Iran waliwahi kuuliwa nchini

Iran yawatia mbaroni wahujumu wa nyuklia

humo kutokana na njama za maadui wa taifa hilo, ukiwemo utawala wa Kizayuni wa Israel kwa kushirikiana na baadhi ya vibaraka wa ndani. Hata hivyo Maafisa usalama nchini Iran wamekuwa macho wakati wote katika kulinda taasisi za nyuklia nchini humo na wamefanikiwa kuvunja njama kadhaa za kuhujumu miradi hiyo. Dk. Salehi amesema kuwa, kuna nchi hazipendi kuona kadhia ya nyuklia ya Iran inatatuliwa kwa njia za amani na hivi sasa wameongeza njama zao, baada ya kuona kuwa kuna muelekeo wa suala hilo kutatuliwa kidiplomasia.

Jumuiya na Taasisi za Kiislamu (T) Inawatangazia Waislamu wote kuwa kutakuwa na Baraza la Idd. Litakalo fanyika:- Masjidi Mtambani, uliopo Kinondoni-DSM. Siku ya Idd Mosi ya Jumatano-Tarehe 16/10/2013. Muda:- 9:00 (Saa Tisa-Alasiri). Mada mbalimbali zitawasilishwa na Masheikh (Viongozi) kuhusiana na mwenendo wa masuala ya Uislamu na Waislamu kwa ujumla. Wahi mapema Kwa niaba ya Katibu

BARAZA LA IDD

Nchi za Mashariki ya Kati na jamii ya kimataifa zina wasiwasi mkubwa kuhusu hatari ya silaha za nyuklia za utawala wa Israel. H a y o ya m e s e m wa n a mkuu wa ujumbe wa Jordan katika Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) kwenye mkutano wa kila m wa k a wa wa k a l a h u o unaoendelea mjini Vienna. Husam al Husseini amesema kuwa silaha za nyuklia za Israel zinatia wasiwasi mkubwa na kwamba utawala huo unalazimika kutia saini mkataba wa kuzuia utumiaji na usambazaji wa silaha za atomiki (NPT). Al Husseini amesisitiza kuwa, maghala ya silaha za nyuklia za Israel yanapaswa kuwekwa chini ya usimamizi wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki na kusema kuwa, kujiunga Israel na mkataba wa NPT kunaweza kuimarisha amani Mashariki ya Kati na kuzihamasisha nchi mbalimbali zielekeze juhudi zao kwenye masuala ya ustawi na maendeleo badala ya k u t u m b u k i a k we n ye mashindano ya silaha. Mkutano wa kila mwaka wa 57 wa wakala wa IAEA ulianza kazi zake Jumatatu iliyopita na utamalizika kesho katika makao ya Umoja wa Mataifa mjini Vienna. Novemba 2011, taarifa ziliripoti juu ya kuongezeka jitihada za Israel za kuzalisha na kujirundikia silaha za kijeshi za nyuklia. Hii ni katika hali ambayo, fikra za walio wengi duniani zinahofia hatua hizo za Israel za kuzalisha kwa wingi silaha za nyuklia na kemikali, silaha ambazo kivitendo z i m e b a d i l i s h a Pa l e s t i n a inayokaliwa kwa mabavu kuwa ghala la silaha za mauaji

Silaha za nyuklia Israel zinatia wasiwasi mkubwa


ya halaiki. Kuhusiana na suala hilo Gazeti la Guardian la Uingereza lilitoa ripoti kuhusiana na kuendelea hatua za Israel za kuzalisha na kuasisi viwanda vipya vya nyuklia. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, Marekani na mataifa mengine ya kibeberu yanakusudia kutumia fedha nyingi kwa ajili ya kukarabati na kupanua viwanda vya nyuklia. Gazeti la Kizayuni la Haaretz pia limewahi kuandika kwamba, hivi karibuni manowari za Israel zitasheheni silaha za atomiki. Vi l e v i l e s i k u k a d h a a zilizopita jarida la kila wiki la Uingereza za Jane's Defence, liliandika kuwa utawala wa Kizayuni unamiliki karibu vichwa vya nyuklia 300. Kwa mujibu wa jarida hilo, wataalamu wa silaha wamepata ushahidi unaonesha kuwa, Israel mbali na vichwa vya nyuklia ilivyonavyo pia inazalisha silaha za nyuklia za aina mbalimbali kama vile mabomu ya ardhini na risasi zenye umbo la mpira. Jarida hilo aidha limeitaja Israel kuwa utawala pekee unaomiliki silaha za atomiki katika eneo la Mashariki ya Kati. Makadirio ya awali yalionyesha kwamba Israel i l i k u wa n a v i c h wa v ya nyuklia 200 lakini makadirio mapya yamedhihirishwa kwamba katika miaka ya hivi karibuni, vichwa vya nyuklia vya utawala wa Kizayuni vimefikia 300. Gazeti la al Wafd la Misri mwaka 2010 lilichapisha ripoti iliyoelezea jitihada zinazofanywa na Israel za kujenga kwa siri viwanda vipya vya nyuklia. Gazeti hilo lilifichua kuwa moja ya viwanda hivyo vya nyuklia vya Tel Aviv, kipo katika mpaka wa Palestina

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, John Kerry.

inayokaliwa kwa mabavu na nchi ya Misri na kwamba, kinajengwa kwa msaada wa madola ya Magharibi. Pia hivi karibuni ilifichuliwa kwamb a Israel imeanza kujenga kiwanda kipya cha atomiki katika eneo la an Naqab. Zaidi ya hayo mwaka huo huo 2010, Israel ilitiliana saini makubaliano mapya na Marekani ya kushirikiana katika masuala ya nyuklia. Misaada ya Marekani na madola mengine yenye silaha za nyuklia ya Magharibi kwa utawala wa Kizayuni kwa ajili ya kutengeneza silaha za nyuklia yanakiuka wazi Mkataba wa Kuzuia Uzalishaji na Usambazaji wa Silaha za Nyuklia NPT. Hii ni katika hali ambayo Israel kwa kuungwa mkono kila upande na nchi za Magharibi imekataa kutia saini mkataba wa NPT na kutoruhusu wakaguzi wa IAEA wakague viwanda vyake vya nyuklia. Hatua za Israel, Marekani na nchi nyinginezo zinazomiliki silaha za nyuklia za kuzidi kuzalisha silaha hizo, zinakiuka Mkataba wa NPT na kupingana na makubaliano ya upokonyaji silaha ya kimataifa. Makubaliano ya upokonyaji silaha yanazitaka nchi zote zenye kumiliki silaha hizo kutekeleza ahadi zao za kutokomeza kikamilifu silaha za atomiki kwa njia za wazi, kutodanganya katika ahadi hizo na kuharakisha mwenendo huo wa kimataifa. Hata hivyo dola hizo zimeendelea kuzalisha silaha za nyuklia huku yakihatarisha amani ya ulimwengu, huku zikipiga propaganda za kuzisakama nchi za Korea Kaskazini, Irani, na sasa Syria.

6
Na Omar Msangi KATIKA taarifa ya habari ya TBC1 saa mbili usiku juzi Jumanne, kulikuwa na taarifa za mambo ya ugaidi na Marekani. Taarifa ilikuwa ikieleza k a u l i y a Wa z i r i w a Mambo ya Nje, John Kerry kwamba ilikuwa halali kwa Marekani kumvizia na kumkamata mtuhumiwa wa ugaidi ndani ya Tripoli, Libya na kutoweka naye. Taarifa hiyo ilihusu lile tukio la Jumamosi iliyopita ambapo Kikosi Maalum cha Marekani kilichopo ndani ya Libya kilimkamata Nazih AbdulHamed al Ruqai, maarufu kwa jina Abu Anas al Libi. Marekani inamtuhumu mtu huyo kuwa ni al Qaida. Lakini wakati Kerry akisema hayo, Serikali ya Libya inasema kuwa huo ni sawa na utekaji nyara na kwamba hiyo ni sawa na kuidhalilisha Libya, kwamba jeshi la nje linaingia na kukamata watu ndani ya nchi huru kana kwamba hakuna Serikali. Katika kusherehesha taarifa hiyo, zilitolewa picha za video zikiwaonyesha Waislamu wakiwa katika s wa l a . Wa m e s i m a m a , wakirukuu na kusujudu huku wengine wakiwa wameshikilia bunduki. Hapana shaka habari na picha zile kilichokusudiwa kuonyeshwa ni kuwa hao wanaorukuu na kusujudu, ndio magaidi. Mtu unajiuliza, habari zinamhusu Abu Anas al Libi, kwa nini haoneshwi huyo Libi ikatosha, wanaonyeshwa na Waislamu wakiswali? Halafu wanaunganishwa na wengine waliofunika nyuso zao wakiwa na bunduki ambao mara nyingi picha hutolewa na kudaiwa kuwa hao ndio Al Shabaab. Kama ni kujenga habari ya Anas al- Libi, basi labda ingeelezwa kuwa hawa Marekani inaodai kuwa ni magaidi, ndio hao iliokuwa ikishirikiana nao na kuwapa silaha na kila aina ya msaada katika kumpiga na kumngoa Gadhafi. Wanajuana! Habari hizo za TBC zinakuja siku ambayo asubuhi yake, takribani magazeti yote yalizungumzia kukamatwa kwa vijana 11 waliodaiwa kuchukua mafunzo ya ugaidi msituni huko mkoani Mtwara.

Makala

DHUL-HIJJA 1434, IJUMAA

OKTOBA 11-17, 2013

AN-NUUR

Siri ya mafunzo feki ya Al Qaida Mtwara


kinahofiwa kutoa mafunzo yenye mwelekeo wa kigaidi. Ta h a r i r i i n a e l e z a mengi, lakini la muhimu inasisitiza kuwa Chuo cha Kiislamu kilichopo Ukerewe (kwa utafiti wa gazeti la Mtanzania), ni

Salam za Elbaradei
MOHAMED Elbaradei ameandika kitabu chake alichokipa jina: The Age Of Deception: Nuclear Diplomacy in Treacherous Times. Katika sehemu moja ya utangulzi wa kitabu hicho anasema, kila mara huwa anapitia ushahidi wao juu ya Silaha za Maangamzi Iraq, na kwamba hazipitii bila ya kutafakari juu ya maelfu ya askari na mamia ya maelfu ya raia wasio na hatia waliouliwa, mamilioni kutiwa vilema, kuharibiwa makazi yao na kuwa wakimbizi na nchi kuvurugwa kabisa. Anasema, anayatafakari haya kwa sababu, vita ya Iraq 2003, haikuwa na

cha kigaidi na mhariri anashangaa ni kwa nini mpaka sasa serikali haijachukua hatua. Kwa hiyo katika kuikumbusha serikali, mhariri wa RAI anasema: Wito wetu kwa Serikali ni kwamba, inapaswa s a s a k u z i n d u k a k wa kuhakikisha inazichukulia kwa uzito unaostahili t a a r i f a z o z o t e z e n ye mwelekeo wa kigaidi au kuhatarisha amani, b a d a l a ya k u z i p u u z a kama ambavyo imekuwa ikitokea.

Nazih Abdul-Hamed al Ruqai, maarufu kwa jina Abu Anas al Libi. Vijana 11 wanaswa wakijifunza ugaidi. Vijana wabambwa wakijinoa kijeshi: Walikuwa na CD za Al-Shabab. Hivyo ni baadhi ya vichwa vya habari magazeti ya Jumanne. Gazeti la Rai lenyewe liliandika: Wafuasi 11 wa Al Qaida watiwa mbaroni Mtwara.Watumia mapanga, video za Osama bin Laden kujifua. Katika para ya kwanza gazeti hilo linasema: Jeshi la Polisi mkoani Mtwara, linawashikilia watu 11 kwa tuhuma za kukutwa msituni wakifanya mazoezi ya kijeshi. Pamoja na mengi yaliyoelezwa, lakini moja muhimu kuliko yote ni kuwa: Vijana hao walikutwa na vitabu vya Kiislamu. RAI likaendeleza habari hiyo kwa tahariri ya gazeti lake la Jumatano ambapo lilisema: Serikali isipuuze taarifa za ugaidi. Katika maelezo yake likasema, Jana vyombo vya habari nchini, vilitawaliwa na habari kubwa iliyokuwa ikieleza kunaswa kwa vijana 11 waliokuwa wanafanya mazoezi ya kivita msituni kwa kutumia video za makundi ya kigaidi. Vijana hao wanatajwa kuwa wakazi wa Nanyumbu, mkoani Mtwara na walikamatwa na polisi wakifanya mazoezi kwa kutumia CD za kundi la kigaidi la Al Shabaab na Al Qaida. Likiendelea Rai l i n a s e m a , : Ta a r i f a hizi ni za kushtusha na zinatusukuma sisi wa RAI Jumatano kuamini kuwa taifa letu sasa linakabiliwa na tishio kubwa la vikundi vya kigaidi. Kisha linasema, Kukamatwa kwa vijana hao kunaturejesha miezi michache nyuma, ambapo gazeti Dada la Mtanzania Jumatano liliripoti habari ya c h u o k i m o j a ( c h a Kiislamu kwa jina la Al Jazeera) kilichoko wilayani Ukerewe ambacho

sababu. Ilikuwa ni uvamizi na uhalifu wa wazi kwa sababu Tume iliyopewa kazi na Umoja wa Mataifa kutizama madai kuwa Iraq ina silaha za maangamizi ilionyesha kuwa hakuna silaha hizo. Lakini Marekani kwa ubabe wake ikavamia tu na kupiga bila hata ya idhini ya Baraza la Usalama la Umoja wa mataifa. Elbaradei alikuwa ndiye Mkurugenzi Mkuu wa International Atomic Energy Agency (IAEA) toka 1997 hadi 2009 na n d i o wa l i o p e wa k a z i ya kutizama madai ya Marekani kuwa Saddam Husein alikuwa na silaha za maangamzi (WMD).

MOHAMED Elbaradei.

Makala
kwenye kiwanda cha silaha zenyewe na kuhakiki. Kwa upande mwingine anasema, taarifa za kuwa Saddam ameagiza madini ya Uranium kutoka Niger, zilipigiwa sana debe na Marekani na Uingereza ambapo Rais George W Bush katika hotuba yake kwa taifa Januari 2003 alisema: The British government has learned that Saddam Hussein recently sought significant quantities of uranium from Africa. Kufuatia madai hayo, Elbaradei anasema walitaka serikali ya Uingereza iwape taarifa zao za ki-intelijensia ili wazifuatilie kuthibitisha jambo hilo. Anasema baada ya kudai sana walipewa nyaraka mbili ambazo hata hivyo waligundua kuwa zote ni za kughushi. Moja ilidaiwa kuwa ni barua ya Rais wa Niger Mamadou Tandja kwenda kwa Saddam. Lakini saini i l i k u wa ya k u g h u s h i na mambo mengine ya uwongo yalikuwa ndani yake. Nyaraka ya pili ilikuwa barua ya Oktoba 2000 kutoka kwa Waziri wa Mambo Nje ya Niger ikiwa na saini ya Allele Habibou. Walioghushi barua hiyo walisahau kuwa Habibou hajawahi kushika nafasi Serikalini toka mwaka 1989. Pennsylvania Ave NW, Wa s h i n g t o n , D . C . n a Downing Street, London, kwamba Saddam ana silaha za maangamzi. Anasema Elbaradei, hata walivyotoa nyaraka za kuonesha jinsi barua za Niger kwenda kwa Saddam juu ya uranium zilivyoghushiwa, vyombo v ya h a b a r i v i l i p u u z a habari hizo. D e s p i te th e on -th e ground knowledge of the UN inspectorate, we were losing the battle of information, in the Western press, and to some extent in the public eye. IAEA and UNMOVIC statements were being discounted, or

DHUL-HIJJA 1434, IJUMAA


quoted selectively, even though we were the ones with the best access to the truth, the eyes of the international community. (THE AGE OF DECEPTION uk.68) Likishikilia bango kuwa Samantha, mwanamke wa Uingereza, alihusika katika shambilo la kigadi Westgate Mall, Nairobi, gazeti moja la kila siku hapa nchini lilisema kuwa limepata habari za uhakika kutoka gazeti linaloheshimika la Daily Mail la Uingereza kuwa huenda Samantha baada ya kufanya shambulio ametoroka na amejificha Tanzania.

OKTOBA 11-17, 2013

AN-NUUR

Ushahidi wa kughushi
KATIKA maelezo yake ndani ya kitabu chake, Ebaradei anasifia wanasayansi ya nyukilia na fisikia kwa ujumla waliokuwa katika Wakala huo wakiwemo kutoka Ufaransa na Marekani kwenyewe na kwamba walifanya kazi kubwa ya kuchunguza sehemu zote ambazo zilikuwa zikidhaniwa kuwa zina silaha ikiwa ni pamoja na zile walizopewa habari zake kupitia mashirika ya kijasusi ya Marekani na NATO. Hata hivyo anasema hawakuona kitu. Lakini pamoja na hayo anasema Marekani ilikuwa ikishikilia kuwa Saddam ana silaha za maangamzi na walipotaka ushahidi wa k a a m b i wa m a m b o mawili: Moja anasema Marekani lidai kuwa vyombo vyake vya kijasusi vina taarifa ya k u p a t i k a n a v i f a a fulani (tubes za bati) zinazoweza kutumika kutengenezea silaha hizo. Na pili ni taarifa kuwa Saddam Hussein alinunua madini ya Uranium kutoka Niger. Mohamed Elbaradei anasema walifuatilia madai hayo na walichogundua ni kuwa tubes zile za bati (aluminium tubes) zilikuwa za kutengenezea roketi za kawaida na walikwenda mpaka

JUZI Jumanne wakati napitia kurasa za kitabu hiki cha Elbaradei nikakumbuka tena kile kisa cha Fake BBC Video. Bado mgogoro wa Syria unazidi kutokota. Na baada ya Marekani kukwama katika namna nyingi, ilikuja na hoja kuwa Serikali ya Syria inatumia silaha za sumu katika kupambana na wapinzani. Moja ya vyombo vya habari ambacho akina

Fake BBC Video


and carnage here, erm weve had a massive influx of what looks like serious burns, er seems like it must be some sort of, Im not really sure, may be napalm, something similar to that.. Amenukuliwa Dr. Rola akisema katika kipindi hicho Panaroma Aleppo ambapo ilidaiwa kuwa jeshi la Syria lilipiga bomu la sumu katika uwanja mmoja wa michezo wa shule (Tazama: http:// www.bbc.co.uk/news/

S a s a k a m a inavyoonyesha timu hii ya wataalamu wa Umoja wa Mataifa juu ya masuala ya nguvu na silaha za nyukilia, IAEA, wanaonyesha hayo magazeti yanayodaiwa kuwa ya kuheshimika kwamba jamani barua inayodaiwa kutoka kwa Waziri wa Mambo ya Nje ya Niger Allele Habibou ya Oktoba 2000 ni ya kughushi kwa sababu huyu Allele si Waziri kutoka mwaka 1989, hawasikilizi, wao wameshikilia lile l i l e wa l i l oa m b i wa na Washington kuwa Saddam kaandikiwa barua na Allele ya kupewa Uranium. Na nani kasema hivyo, Blair!

kwamba ndio jeraha baya na lenye maumivu makali zaidi kuliko jeraha lolote linalotambulika duniani. Kwa hiyo haiwezi kuwa akinamama na watoto wanaodaiwa kuwa wana majeraha ya kuunguzwa na napalm halafu wamekaa wametulizana wakimtizama mpiga picha anavyowarekodi huku wanaongea bila wasiwasi. Footage of genuine napalm victims would likely be far too horrific and

Vyombo vya habari balaa

Samantha KILICHOWASHANGAZA wajumbe wa IAEA ni kuwa pamoja na ushahidi walitoa kuwa nyaraka zote hizo zilikuwa za kughushi, lakini waliokuwa wamepania kufanya vita waliendelea kushikilia msimamo wao. Lakini kilichowatisha z a i d i n i v y o m b o v ya habari. Kadiri IAEA ilivyojitahidi kutoa taarifa za kiuchunguzi zenye ushahidi na uthibitisho wa uhakika, vyombo vya habari viliendelea kupiga tarumbeta kutoka 1600

yahe huku ndio wanasema kuwa ni vya kuheshimika sana, BBC, Agosti 29, 2013 ikaja na mkanda wa Video (documentary) inayoonyesha lililodaiwa shambulio la silaha za s u m u k a t i k a m j i wa Aleppo. I n a o n y e s h wa k u n a z a h a m a k u b wa wa t u wanaoneshwa wana majeraha ya kuungua huku wakipiga kelele. Dakitari naye, ambaye ni Dr. Rola, anapaza sauti akidai kuwa anapokea majeruhi wengi wakionekana kuunguzwa na silaha za sumu. Its just absolute chaos

world-23892594) Hata hivyo, haukupita muda, barua, simu na makala mbalimbali zimeandikwa kuchambua tukio hilo kuonesha kuwa ilikuwa mchezo wa kuigiza (fabrication.) Waliohusika na kuandaa kipindi hicho ambacho sasa kinaonekana kuwa ni igizo, Ian Pannell na D a r r e n C o n wa y ( B B C cameraman), wanaambiwa na wataalamu wa silaha z a s u m u k u wa s u m u ya napalm huunguza na k u t o a j o t o ( m o t o ) unaofikia nyuzi joto 800 mpaka 1,200 (Celsius) na

distressing to broadcast and to describe the alleged injuries depicted in these scenes as napalm-like is an insult to those who have suffered the reality. Anayesema maneno haya amejitambulisha kwa jina la Robert akiwa mmoja wa watu walioiandikia BBC kulalamika kuwa wanaonyesha habari za kutunga na anawaambia kudai kuwa watu walioonyeshwa katika kipindi chao wana majeraha ya napalm, ni sawa na kuwatukana na kuwakejeli watu Inaendelea Uk. 8

Makala
magodoro nao vipi?, Umeporomoshaje jengo? Nani kalipua wakati ilishaambiwa magaidi wameondoka? Na tangu lini moto wa magodoro ukaporomosha jengo kama lililopigwa bomu zito? Hayo hutasikia wakijiuliza waandishi wetu na magazeti yetu. Sana sana utawasikia wakiandika, eti Samantha n a m a g a i d i we n z a k e walitoroka kupitia mtaro wa maji machafu ulio chini ya jengo! Wanaleta stori za yale wanayoona katika picha za Hollywood. Lakini wanaoandika habari hizo huko Marekani na Ulaya sio wajinga. Wanajua wanachokifanya. Kubwa ni kukupumbaza (age of deception) kuwa hawa magaidi al Qaida na al Shabaab, wanaorukuu na kusujudu, ni hatari sana. Ni makomandoo ambao kupambana nao ni kazi kweli! Kwa sisi huku tunaiga na kukariri tu. Zaidi ni ujinga na kuwa na akili ya kushikiwa. MHARIRI wa RAI anahimiza Serikali k u wa c h u k u l i a h a t u a watuhumiwa wa ugaidi ikiwa ni pamoja na vyuo vya Kiislamu anavyodai v i n a t o a m a f u n z o ya kigaidi. Lakini jingine linaloandamana na hilo, ni hii hali inayooekana hivi sasa ambapo ukifika mahali kama pale Mlimani City au kuingia mpirani Uwanja wa Taifa, unakuta upekuzi mkubwa. Wanapekuwa asije akapita Al Shabaab na silaha!!! Kama tunaamini kuwa Samantha na wanaodaiwa kuwa ni magaidi wenzake, waliweza kuingia Kenya wakaingiza lundo la silaha ndani ya Westgate Mall na kuondoka baada ya shambulio, basi ambalo ni la uhakika ni kuwa hakuna Polisi, mgambo, jeshi au Usalama wa Taifa wanaoweza kuzuiya magaidi wa namna hiyo. We ukipekuwa watu Mlimani City na Uwanja wa Taifa, wao wanapiga na kuuwa watu Soko la Tandika. Ukilinda Soko la Kisutu (Soko Mjinga), wao wanapiga Soko Matola Mbeya au huko Newala! Na wakifanya hivyo, utasikia Twitter imesema wanaohusika ni Al Shabaab tawi la Tanzania. Magazeti yetu yatapiga tarumbeta na kwa ujinga, tutaamini. Wala hatutajiuliza, Twitter ni nani katika zama hizi za electronic/digitali. Mtu anakwambia Twitter ya Al Qaida imesema wanahusika unaamini. Sasa katika upumbafu wa kiwango hiki, hatutasalimika. Tu k i o l a v i j a n a kukamatwa Mtwara, lilitokea kiasi wiki moja iliyopita. Vi j a n a wa k a f i k i s h wa mahakamani wakapewa dhamana. Lakini lilivyoripotiwa juzi ni kana kwamba ndio kwanza linatokea. Ndio polisi wakaenda na kuwakamata tena na kuwaweka ndani. Na walikutwa kijijini wakiendelea na shguli zao kama kawaida. Si watu waliojificha kama wahalifu. Labda la kusema hapa kwa Waislamu ni hili: Hizi ni zama za Deception. Jambo la uwongo linapigiwa zumari mpaka linaonekana kuwa kama kweli. Iraq imeangamizwa kwa mtindo huo. Hivi sasa Syria inasukiwa kitanzi. Vyombo vya habari vinatoa taarifa za kutunga. Stand By, Camera

DHUL-HIJJA 1434, IJUMAA

OKTOBA 11-17, 2013

AN-NUUR

Inatoka Uk. 7

Fake BBC Video Funzo kutoka Syria

Hatari ya uwongo
KATIKA Quran ipo aya inasema: Kama fasiki akikujieni na habari (yoyote ile msimkubalie tu), bali pelelezeni (kwanza) msije mkawadhuru watu kwa ujahili na mkawa wenye kujuta juu ya yale mliyoyatenda. (49:6) Ili kuelewa vizuri somo la aya hii, sikiliza habari hii. It turns out we were all wrong. Mohamed Elbaradei anamnukuu David Kay akitoa taarifa yake kwa Kamati ya Kijeshi ya Seneti (U.S. Senate Armed Services Committee), kwamba wote katika Marekani walisema uwongo juu ya Saddam Hussein. Anamnukuu pia Makamo wa Rais Dick C h e n e y a k i h o j i wa n a MSNBC katika kipindi Meet the Press ambapo anasema: We never had any evidence that (Saddam Hussein) had acquired a nuclear weapon. Lakini Elbaradei anasema hiyo ni Septemba 2003 na Januari 2004 wakati huo Iraq ishavamiwa maelfu kwa mamilioni ya watu washauliwa,

waliopatwa na msiba wa kweli wa kushambuliwa na sumu hiyo wakati wa vita ya Vietnam. Sasa kwa watu ambao akili zao na mawazo yao ni kuwa hawa BBC na Daily Mail ndio vyombo vya kuheshimika, haishangazi leo kuona kuwa hakuna wanachojiuliza: Inakuwaje mwanamke Samantha, atoke Mogadishu aingie nchi ya watu na lori la silaha, nchi yenye Usalama wa Taifa, yenye polisi na jeshi mpaka ateke Westgate Mall, lenye walinzi masaa 24 na kamera za ulinzi!. Na akimaliza shambulio atoroke asikamtwe huku jengo zima limezingirwa na Jeshi la Kenya! Wala hatajiuliza, hivi hawa watu wanaodaiwa kupigwa risasi mgongoni, mguuni na tumboni, mbona wanatembea wenyewe? Mbona picha haziwaoneshi hao magaidi wakivamia na kukata watu mikono au kuwapiga risasi? Na ule moto wa

John Rambo rolling, action Watu wanapigwa picha wakiwa na majeraha bandia ikidaiwa ni ya silaha za sumu. Huku kwetu napo inaonekana wana hamu s a n a ya k u p a n d i k i z a kitisho cha ugaidi. Zipo kanda nyingi zimetengenezwa kama zile zilizoonyeshwa na TBC katika taarifa ya habari wakionyeshwa watu wanaswali huku wana bunduki na unaambiwa kuwa hawa ni Al Qaida au Al Shabaab. Wa l i o z i t e n g e z e a na kuziingiza katika mtandao, wanajua wapo vijana watazi-down load, kuzirudufu na kufanya biashara. Wa n a j u a p i a k u wa wapo vijana wa Kiislamu wa t a z i p e n d a . L a k i n i wanajua pia kuwa P o l i s i wa m e a n d a l i wa kutafuta vitu kama h i v y o . Wa k i k a m a t wa nazo, vyombo vya habari vitadaka Vijana 11 wa Al Qaida wakamatwa Mtwara. Vitaandika. Swali ni je, kujifunza kareti, mpaka uwe na kanda hizo zinazodaiwa kuwa za al Shabaab na al Qaida? Kama shida yako ni kujua kareti au kuwa jitu lenye nguvu linalojua kupigana, tumia za John Rambo, Anold Schwarzenegger na Chuck Noris.au hata Jackie Chan. Na kujifunza kareti sio lazima uende porini. Hata nje ya nyumba yako au darasa la shule ya msingi mnafanya. Lakini mjue kuwa kama ilivyo ile Fake BBC Video. Wanaweza kupatikana vijana pia wa k a wa t o s a we n z a o . Watakuja na kuleta hoja k u wa wa o wa m e i va . Wanajiandaa na kitali au kupigana Somalia. Watataka ushiriki darasa

Chuck Noris. lao la harakati. Ujue hao ni washenga wa vita dhidi ya Uislamu. Ni maadui sawa na maadui wengine japo utawaona wanaswali na kusoma aya kali kali. Mohamed Elbaradei baada ya kufanya kazi kama Mkuu wa IAEA na kuona Iraq ilivyozuliwa uwongo, jinsi watu walivyotumika kuweka ushahidi bandia, anasema: This is The Age of Deception. Ni zama za uwongo, hadaa, udanganyifu, ulaghai, propaganda na kila wazimu. Na yote hayo hufanywa kwa sasa kwa lengo la kuwapiga vita Waislamu na kwa upande mwingine kutoa fursa kwa wababe kutawala dunia wakitawanya makucha yao katika kila kona. Vijana wa Kiislamu tumieni akili. Nyie ndio walengwa. Wale waliochezeshwa Fake BBC Video ni vijana na raia wa Syria. Basi mjue na nyinyi m t a c h e z e s h wa F a k e Mafunzo ya Al Qaida Nanyumbu. Sikilizeni, chambueni mjue lipi la kweli. Ipi propaganda. Upi udanganyifu. Muhimu zaidi, msinaswe mkajidhuru kwa mikono yenu wenyewe. Anayekwambia kaiva, mwambie akalime ajitosheleze kwa chakula na kingine atuuzie. Ajenge shule, hospitali na kutuondolea dhiki ya maji. A k i n g a a n g a n i a mazoezi ya kwenye kambi na darasa za ki-Al Shabaab zilizoko katika kanda za CD/DVD, ujue huyo ni kachero au mtu mjinga sana anayetumiwa bila ya kujijua. Na mtu mjinga muepuke. Mjinga wa kiwango hicho, mkimbie, la sivyo atakutosa.

Makamo wa Rais Dick Cheney.

wakionekana kuwa ni collateral damage! Uwongo umeangamiza roho za mamilioni ya watu na inavyoonekana hakuna anayejali-collateral damage. Anasema kilichokuwa k i k i t a f u t wa I r a q s i o silaha za maangamizi, demokrasia, kuondoa udikiteta au usalama wa Marekani na dunia. N i v i t a ya K i i t i k a d i iliyochanganyika na masilahi. Kwa baadhi ya watu usalama wa dunia ni pale wao wanapodhibiti rasilimali za kila mahali na kuwafanya wengine watwana wao.

Makala

DHUL-HIJJA 1434, IJUMAA

OKTOBA 11-17, 2013

AN-NUUR

Na Sheikh Abdallah Ahmad Bawazir


AL-KAABA ni neno la Kiarabu linalo maanisha kitu chenye pande nne. Kila upande una urefu sawa na ule mwingine. Lakini katika Qur-ani kinacho kusudiwa kwa neno AlKaaba ni nyumba ya Allah (s.w.t.) iliyo jengwa na Nabii Ibrahim (a.s.), iliyoko katika mji mtakatifu wa Makka ambayo kuikusudia kwa ibada ni wajibu juu ya Muislamu katika umri mara moja kwa mwenye uwezo. Nabii Ibrahim (a.s.) alizaliwa Iraq katika mji wa Babli (Babylon). Baada ya hapo alihama Iraq akiwa na mke wake pamoja na Lut mtoto wa ndugu yake, kuelekea Sham. Huko walifikia Harran, kijiji ambacho kilikuwa kinatawaliwa na washirikina, walio kuwa wakiabudu sayari na masanamu. Katika kijiji chote hicho hapakuwa na Muislamu ila yeye mwenyewe Nabii Ibrahim (a.s.), mke wake Bibi Sara na Lut mtoto wa ndugu yake. Katika kipindi ambacho nchi ya Sham ilikumbwa na janga kubwa la ukame ulio fuatiwa na njaa kali, Nabii Ibrahim alihama yeye na mke wake kuelekea Misri. Na wakati huo Misri ilikuwa i k i t a wa l i wa n a m f a l m e d h a l i m u j a b a r i a m b a ye alikuwa hamuoni mtu ana m k e m z u r i i s i p o k u wa atafanya hila amnyanganye. Nabii Ibrahim alipofika Misri mfalme huyu kama kawaida yake alitaka kumfanyia dhulma na kumnyanganya mke wake. Hivyo, ghafla mfalme akamuita Nabii Ibrahim na akamuuliza kuhusu mwanamke aliye ambatana nae, ana uhusiano nae gani. Nabii Ibrahim (a.s.) alimjibu mfalme huyo dhalimu, kwamba huyu ni dada yangu. Alisema hivyo kwa kukusudia kwamba ni ndugu yake katika dini na itikadi, ikiwa ni hekima ya kujihifadhi na shari ya mfalme huyu lau kama angejua kwa uhakika kwamba huyo ni mke wake. Mfalme akaagiza mwanamke huyo aletwe kwake ili akae naye faragha na watumishi wake wakaitii na kuitekeleza amri yake, wakamleta mbele yake mke wa Nabii Ibrahim. Wakati hilo likijiri Nabii Ibrahim

(a.s.) alikuwa amesimama kuswali na kunyenyekea kwa Mola wake kwa nguvu zote, akimuomba Allah (s.w.t.) amuhifadhi na kumlinda mke wake na dhulma ya mfalme huyo. Mfalme alivutika sana na uzuri wa Bibi Sara wakati walipo kuwa faragha peke yao wao wawili tu. Ghafla alipo nyoosha mkono wake kutaka kumshika Bibi Sara, mkono wake ulipatwa na kiharusi akawa hawezi hata kuutikisa, akaingiwa na hofu kuu na kutetemeka. Akamuomba mwanamke huyo amuombee dua na papo hapo hali yake ikarejea katika ukawaida wake. Lakini mfalme huyu hakukoma na kwa mara ya pili tena akajaribu, akataka kuunyoosha mkono kwa mara nyingine lakini hali ikawa ni ile ile, hakupoa isipo kuwa baada ya dua ya m wa n a m k e m w e m a yule. Hatimaye alimgeukia mtumishi wake, akamlaumu sana na kudai kwamba huyo mwanamke aliye mleta si mwanadamu bali huyo ni shetani. Mfalme akaamrisha mwanamke huyo arejeshwe kwa mwenyewe na apewe binti katika wajakazi wa mfalme awe ni mtumishi wake. Baada ya mtihani huo, Nabii Ibrahim (a.s.) akarejea Sham akiambatana na mke wake na binti huyo aliyepewa na mfalme ambaye jina lake ni Hajara. Kwa vile Bibi Sara hakuwa amepata ujauzito kwa kipindi kirefu c h a m a i s h a ya o , j a m b o ambalo liliashiria huenda alikuwa tasa, bibi mwema huyu alimtaka mume wake amkubali binti huyo kama mke wake na amuingilie pengine akaruzukiwa mtoto kwake. Nabii Ibrahim na bibi Sara, pamoja na mjakazi wake Hajara akiwa kama mke wake wa pili, waliondoka Misri na kurejea Shamu. Baada ya kitambo kifupi, Nabii Ibrahim (a.s.) alijaaliwa kupata mtoto wa kiume kwa mke huyo wa pili mwenye asili ya Misri, akampa jina la Ismail. Huyo ndiye mtoto wa kwanza wa Nabii Ibrahim (a.s.) ambaye Allah (s.w.t.) alimsifu katika Qur-ani kwamba ni mkweli wa kutimiza ahadi, nabii na mjumbe wa Allah (s.w.t.). Kwa mujibu wa maumbile ya kila mwanamke, Bibi Sara baada ya muda alianza kuhisi tofauti katika nafsi yake. Alihisi upweke na huzuni kwa kujiona ni muda mrefu na yeye hakujaaliwa kupata mtoto, akatawaliwa na ghera hadi akawa anashindwa kumuangalia mtoto huyo na mama yake. Hapo ndipo Bibi Sara alipoamua kumshauri Nabii Ibrahim (a.s.) kumuhamisha mtoto huyo na mama yake, awaweke mbali na macho yake katika sehemu

Al-kaaba na Makka katika historia


nyingine. Nabii Ibrahim (a.s.) akahama yeye, mke wake Hajara na mwanawe Ismail, wakaondoka Shamu katika ardhi ya Phalastin na kuelekea Kusini kwenye milima ya Parani. Qur-ani inasema kwamba Nabii Ibrahim (a.s.) aliwaweka wawili hao katika bonde lililo baina ya milima hiyo na akasema: MOLA WETU! HAKIKA MIMI NIMEWEKA BAADHI YA K I Z A Z I C H A N G U KATIKA BONDE LISILO KUWA NA MMEA MBELE YA N Y U M B A YA K O TUKUFU. MOLA WANGU! ( n i m e f a n ya h i v y o ) I L I WASIMAMISHE SWALA, BASI JAALIA NYOYO Z A WAT U Z I E L E K E E KWAO, NA UWARUZUKU KATIKA MATUNDA ILI WASHUKURU. [14:37] Bibi Hajara yeye na mwanawe Ismail akiwa bado ni mtoto mdogo anaye nyonya, wakabaki peke yao katika bonde hilo baada ya kuondoka kwa Nabii Ibrahim (a.s.) kurejea Sham. Maji waliyo kuja nayo katika kiriba yaliisha yote na kiu kikaanza kumsumbua mama na mwanawe. Bibi Hajara alihangaika sana katika bonde hilo kavu, baina ya jabali la Swafaa na Marwa kutafuta maji. Mara alikuwa akipanda jabali la Swafaa na akishuka kupanda jabali la Marwa, akitafuta maji bila ya kufanikiwa kuyapata. Baada ya kufanya hivyo mara saba, Allah (s.w.t.), alileta rehema yake kwa kumleta Malaika Jibril (a.s.), akaja na kupiga sehemu katika bonde hilo kwa ubawa wake na hapo hapo chemchem ilichimbuka na maji kububujika. Jibril (a.s.) alimbashiria Bibi Hajara kwamba hapo alipo hakupotea, kwani jirani yake kuna eneo takatifu ambalo Allah (s.w.t.) amekwisha andika ya kwamba Al-Kaaba; n y u m b a ya k e ya i b a d a ijengwe hapo. Na atakaye

ijenga ni Nabii Ibrahim na mwanawe huyo Ismail. Wa a r a b u w a k a b i l a la Jurhum walipo kuwa wakipita katika msafara wao wa kibiashara, waliiona sehemu hiyo na namna i l i v y o c h a n g a m k a k wa kuzungukwa na ndege, kwa sababu ya neema ya maji ya chemchem hiyo. Wakaenda mahala hapo na wakaomba ruhusa kwa Bibi Hajara ili na wao waweze kuishi hapo pamoja na wanyama wao. Jurhum waliishi hapo na Ismail akawa pamoja nao, akajifunza lugha yao na akaoa kwao. Baada ya kupita muda fulani, Nabii Ibrahim alikuja na akamkuta mwanawe Ismail tayari amesha kuwa ni kijana mwenye rika la mtu mwenye akili timamu. Akamwambia ya kwamba Allah (s.w.t.) amemuamrisha ajenge nyumba ya ibada, ambayo kwa hivi sasa ndio inayoitwa Al-Kaaba na hapo ilipo ndio Makka. Nabii Ismail (a.s.) akaijenga Al-Kaaba kwa ushirikiano wa mwanawe Ismail, baba anajenga na mtoto akimbebea mawe. Na kwa baraka hiyo Makka ikaanza kuimarika kidogo kidogo. Hii ndio mara ya kwanza nyumba hii kujengwa kama Qur-ani inavyo tueleza. Nabii Ibrahim (a.s.) baada ya kumaliza ujenzi wa nyumba hii, Allah (s.w.t.) akamuamrisha awatangazie watu Hijja kokote waliko duniani. Mara ya pili, Al-Kaaba ilijengwa kabla ya kudhihiri kwa Uislamu katika mji wa Makka, wakati Bwana Mtume (s.a.w.) akiwa bado ana umri wa miaka thelathini na tano. Kufuatia mvua kubwa iliyo nyesha katika mji wa Makka, mafuriko makubwa yaliingia katika eneo lenye AlKaaba na kuta za Al-Kaaba zilidhoofika na kupasuka. Makureishi wakakubaliana kuijenga Al-Kaaba na Bwana Mtume (s.w.a.) pia alipata

fursa ya kushiriki katika ujenzi huo. Mara ya tatu, Al-Kaaba ilijengwa tena katika kipindi cha Yazidu bin Muawiya, aliye kuwa kiongozi mkuu katika awamu ya pili ya dola ya Bani Umayya baada ya kushambuliwa na majeshi yake kutoka Sham. Yeye Ya z i d u n d i ye a l i ye t o a amri jeshi lake kumzingira Abdullah bin Zubeir (r.a.) kutokea nje ya Makka na akaishambulia Al-Kaaba hadi ikavunjika na kuungua. Baada ya mashambulizi hayo, Abdullah bin Zubeir akaijenga tena Al-Kaba n a a k a f a n ya b a a d h i ya mabadiliko humo. Mara ya nne, baada ya Abdullah Zubeir kuuawa kwa dhuluma, Abdul-Malik b i n M a r wa n ; k i o n g o z i wa Dola ya Bani Umayya k a t i k a a wa m u ya t a n o , naye huyu alifanya baadhi ya marekebisho katika AlKaaba. Lakini katika kipindi cha Dola ya Abbasiya, Harun Rashid akachukua uongozi wa dola hiyo katika awamu ya tano, na yeye alitaka kufanya mabadiliko katika ujenzi wa Al-Kaaba. Hasa katika yale marekebisho yaliyo fanywa na Abdul Malik bin Marwan na kuyarejesha katika hali yake ile ile kama yalivyo kuwa wakati wa Bwana huyo Abdul Malik bin Marwan. Lakini Imamu Malik bin Anas akamkataza na akamtaka awe na tahadhari Al-Kaaba isije ikawa ni mchezo wa wafalme baada yake na hatimaye heshima yake ikatoweka katika nyoyo za watu. Kuna kauli nyingine zinazo semwa kwamba Nabii Ibrahim (a.s.) sie wa kwanza aliye ijenga Al-Kaaba, bali Nabii Adam (a.s.) ndiye wa kwanza kuijenga Al-Kaaba. Na wengine wanasema wa kwanza kuijenga ni Shiyth mtoto wa Nabii Adam. Ukweli ni kwamba kauli hizo zipo na zimeandikwa katika baadhi ya vitabu, lakini si kauli sahihi. (abawaziri@hotmail. co.uk +255 767 215 998)

10
Nabtadi kuangaza, halisi yake launi Si mwingine mpendeza, mwalimu Pugu shuleni Isimuye kudokeza, Nyerere si jina geni Sura halisi ni hii, ya Julius Nyerere. Kila kona husifiwa, kwa sifa ziso kifani Na chapuo hupigiwa, ndani na ughaibuni Wa Mungu mteuliwa, yanadiwa hadharani Sura halisi ni hii, ya Julius Nyerere. Ya uasisi kasumba, imewalevya vichwani Huyumba huku wakimba, "mwasisi nambari 'wani' " Waimbaji mnoimba, 'wimbo' huu sikizeni Sura halisi ni hii, ya Julius Nyerere. Nyerere mkaribishwa, hilo nyote ng'amueni Na Bantu katambulishwa, kwa Abdul jijini Kisha akakutanishwa, na wa TAA waumini Sura halisi ni hii, ya Julius Nyerere. Ikawa mara ya kwanza, kutajika siasani Safari akaianza, yu chini ya waumini Nguvu hawakumtenza, kwa tofauti ya dini Sura halisi ni hii, ya Julius Nyerere. Kwa wema wakaamuru, aushike usukani Akajifanya 'jabaru, alipowekwa kitini Wema akaukufuru, kwa kugeuka mdini Sura halisi ni hii, ya Julius Nyerere. Kura tatu ikajiri, Tabora unyamwezini Ikatoka tahadhari, ya dalili za udini Udini ukadhihiri, na umma kuufitini Sura halisi ni hii, ya Julius Nyerere. Sheikh wetu Takadiri, muhanga nambari 'wani' Kisa kutoa indhari, kwa nduguze waumini Wakamsusa dahari, kisa eti yu mdini Sura halisi ni hii, ya Julius Nyerere. Likatimu lake lengo, Nyerere 'Bwana' udini Ukawa wake ulingo, na siriye mtimani Akaja kushika 'bingo', sitina moja mwakani Sura halisi ni hii, ya Julius Nyerere. Masaibu yakaanza, kuwazonga waumini Ni walewale wa kwanza, waanzilishi chamani Kikubwa kilowaponza,si kingine yao dini Sura halisi ni hii, ya Julius Nyerere. Masheikh wakakamatwa, na kutiwa gerezani Mongoni mwalokamatwa, ni Sharifu Adinani Kisha nyuma akafatwa, na Sheikh Komoriani Sura halisi ni hii, ya Julius Nyerere. Kisha Sheikh Nurdini, mwana mwema wa Husseni Akaongezwa kundini, na Sheikh Al-Amini Hata Bilali Rehani, yu hai muulizeni Sura halisi ni hii, ya Julius Nyerere. Mwisho akajakamatwa, Mufti wetu nchini Hassan yeye aitwa, Amir wake ubini, Ikawa mchana kutwa, mazonge kwa waumini Sura halisi ni hii, ya Julius Nyerere. Orodha ni ndefu sana, kuitaja shairini Lengo sio kulumbana, bali haki kubaini Yeyote anayekana, alete hoja mezani Sura halisi ni hii, ya Julius Nyerere. Mwisho nakuusieni, tarekh tuisomeni Iwe yetu ya nchini, au ya Ughaibuni Mengi tutayabaini, ya dhahiri na batini Huyo jama tambueni, n'do mwalimu Nyerere. ABUU NYAMKOMOGI MWANZA.

SHAIRI/HABARI

DHUL-HIJJA 1434, IJUMAA

OKTOBA 11-17, 2013

AN-NUUR

Huyu ndiye Nyerere ! (Kumbukumbu)

Waislamu wachangia Damu Salama lita 286


Na Bakari Mwakangwale
KIASI cha unit 572, sawa na lita 286 za damu zimetolewa na Waislamu wa Jumuiya ya Al-akhlaquul Islam, kwa lengo la kusaidia jamii katika vituo mbalimbali vya Afya nchini. Jumuiya hiyo imefanya zoezi hilo la utoaji wa damu mwishoni mwa wiki iliyopita, na kuwajumuisha Waislamu mbalimbali katika vituo vyao vilivyopo mahospitalini. Kwa mujibu wa Amir wa jumuiya hiyo, Ust. Yahaya Tate Ally, alisema Jumla ya vituo 25, katika mikoa 15, nchini, walishiriki katika zoezi hilo na kufanikiwa kuchangia damu kiasi cha Unit 572, kwa ujumla. Alisema, matarajio na malengo yao ni kuelimisha na kusaidia Waislamu na wasio Waislamu sambamba na kuiongoza jamii katika wema kwa ujumla, mbali na shughuli zingine za kihuduma wazitoazo katika hospitali mbalimbali nchini. Ustadhi Tate, alisema kutokana na mchango wao kutambulika, Serikali kupitia Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, imewatunuku Cheti cha ushiriki wa utoaji wa huduma hiyo. Hii ni kuthibitisha kuwa Jumuiya ya Akhlaaqul Islam ni mdau mzuri wa mpango wa Taifa wa Damu Salama. Kimesema Cheti hicho kilichosainiwa na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Hussein Mwinyi. U s t a d h i Ta t e , alivitaja vituo vilivyoshiriki utoaji wa damu mwishoni mwa wiki iliyopita kuwa kwa Jijini Dar es Salaam, ni Hospitali za Mwanayamala, Amana pamoja na Temeke. Kwa Mkoa wa Pwani zoezi hilo litafanyika katika Hospitali za Tumbi, Kisarawe, Mafia na Bagamoyo. Ama mkoani Morogoro, zoezi hilo litafanyika jirani na Hospitali kuu katika ofisi za damu salamu, pamoja na Hospitali ya Wilaya ya Kilosa. Kwa mkoa wa Tanga, zoezi hilo litaendeshwa katika vituo vya Hospitali za Bombo, na katiika Hospitali za Wilaya za Korogwe, Muheza pamoja na Pangani, ambapo katika Mkoa wa Kilimanjaro, zoezi hilo litafanyika katika Hospitali ya Mawenzi. Mkoani Iringa, huduma hiyo itatolewa katika Hospitali ya Mkoa huo, kama ilivyo kwa Mkoani Dodoma, huku Mkoani Tabora, huduma hiyo itatolewa katika Hospitali ya Kitete, ambapo huduma kama hizo pia zitatolewa Sumbawanga Mjini. Kwa upande wake Amirat Aisha Fumita, alisema kuna wanawake wapatao 70, katika jumiya yao katika utoaji wa damu ila namba hiyo huwa hupanda na kushuka kutokana na masharti ya utoaji wa damu kwani kila anayetoa inamlazimu kukaa miezi minne kabla ya kutoa tena.

Watahiniwa wapewa semina


Na Azza Ally Ahmed
za kuwakatisha tamaa na kumsahau muumba wao. Hivyo amewataka wanafunzi hao kujitahidi kumjua Mola wao na kuweka hofu ya kumuogopa Mwenyezi Mungu huku wakitambua kwamba, kusoma ni amri iliyotoka kwa Mola wao. Aidha Ust. S h a b a n a m e wa t a k a wanafunzi hao kuzijua changamoto mbalimbali zinazowakabili Waislamu na wanafunzi wa Kiislamu, ili kuweza kukabiliana nazo bila kukata tamaa pindi watakapokutana nazo. Alizitaja baadhi ya changamoto hizo kuwa ni kunyimwa haki ya kufanya ibada wawapo katika shule mbalimbali pamoja na kutothaminiwa kama walivyo wanafunzi wengine, wanafunzi wa kike kudhalilishwa na baadhi ya walimu wasiokuwa na maadili na kuvuliwa hijab zao. H i v y o aliwatahadharisha wanafunzi hao kujiandaa na changamoto zozote wa t a k a z o k a b i l i a n a nazo katika maeneo yao watakapokuwa na kutokubali kushindwa na changamoto hizo. Msikubali kutoka nje ya maamrisho ya Allah (S.w.) kwani kufanya hivyo ni chukizo kubwa kwa Allah. Nami napenda kuwausia mubaki na msimamo huu kama a m b a v y o n a wa o n a mbele yangu, kwani hata mtakapo kuwa vyuoni mtaweza kuipa heshima dini yetu tukufu.Alisisitiza. Naye Bw. Msafiri Mpendu, mtaalam wa

Mbali ya utoaji wa damu katika kitengo hicho cha ustawi wa jamii, Amirat huyo alisema pia hujihusisha na shughuli za mazishi k wa Wa i s l a m u , hususani kwa wale wanaokosa ndugu. Alisema, shughuli hizo ni za kujitolea zaidi kwa nguvu na mali za wanakikundi na hakuna muwezeshaji, zaidi ya kujitolea huku akitoa wito kwa Waislamu kwa ujumla kujitokeza kushiriki katika zoezi hilo endelevu.

WA N A F U N Z I wa kidato cha pili na wale wa kidato cha nne, wamehimizwa kujiandaa vyema na mitihani inayowakabili hivi sasa, ili waweze kufanya vizuri katika mitihani hiyo. Wito huo umetolewa na Mratibu wa Elimu ya Dini ya Kiislamu Wilaya ya Temeke, Ustadh Abubakar Shaaban, katika Msikiti wa Muuminina- Buza nje kidogo ya Jijini la Dar es salaam mwishoni mwa wiki iliyopita, kwa ajili ya wanafunzi wa Kiislamu wa kidato cha pili wanaofanya mitihani yao hivi sasa n a wa l e wa k i d a t o cha nne wanaotarajia kufanya mtihani wa Ta i f a N o v e m b a 4 mwaka huu. Nawasisitizia kuyafanyia kazi yale yote mliyofundishwa na walimu wenu kwa vitendo kwani kusoma ni ibada kama zilivyo ibada nyingine. Alitilia mkazo Ust. Shaaban. Alisema kuwa wanafunzi wa sasa ndio viongozi wa baade n a k wa m b a , k a m a hawatajengewa misingi i m a r a ya d i n i k wa wakati huu, isitarajiwe kupatikana viongozi wa baadae watakaomjua Allah (s.w) na watetezi wa dini yetu katika dunia hii na kwamba kitarajiwe kizazi kibovu katika jamii. Aidha wanafunzi hao wameaswa kuwa makini na mbinu mbalimbali za maadui wa Uislamu na Waislamu katika yanja mbalimbali, kwani mbinu hizo ni

m a m b o ya u s h a u r i alitoa nasaha zake kwa wanafunzi kwa kuwataka wasome sana kabla ya mtihani, lakini siku ya mtihani hawatakiwi kusoma kwa kukesha usiku mzima ikiwa siku inayofuata wana mitihani. Alisema hali hiyo inaweza kumsababishia m w a n a f u n z i kushindwa kwa sababu ya akili kuchoka sana na kutokukumbuka yale aliyosoma siku za nyuma. A m e w a t a k a watahiniwa hao kuswali rakaa mbili usiku wa kuamkia siku ya mtihani kumuomba Mwenyezi Mungu kuwafanyia wepesi katika mitihani yao. A i d h a a l i wa t a k a wanafunzi hao kuwa makini wanapopewa karatasi ya maswali kwa kuzisoma kwa umakini kila kipengele, kwani wa k i k o s e a k u s o m a maelezo (Instructions) kwa makini ndio m wa n z o wa k u f e l i mtihani. Mtaalamu huyo amewataka wanafunzi kutokujadili mtihani uliopita kwa kukaa vikundi vikundi na kupoteza muda badala yake wametakiwa kujiandaa na somo linalofuata. Kwa upande wake, Sheikh Mikidadi K h a l f a n a l i ye k u wa amewakilisha Baraza la Wazee wa Kiislamu Msikitini hapo, amewataka wanafunzi hao kuzifanyia kazi nasaha walizopewa na yote waliofundishwa na walimu wao ili kufanya vizuri katika mitihani ya o n a k u f a n i k i wa katika maisha yao ya baadae.

11
BARAZA LA VIJANA WA KIISLAMU
MKOA WA DAR ES SALAAM
KAMATI YA MAANDALIZI YA MKUTANO WA SEKRETARIETI (KAMATI NDOGO YA KITAIFA) TUNATOA SHUKRANI ZA DHATI KWA WALE WOTE WALIOSAIDIA KUFANYIKA KWA MKUTANO WA PILI TAREHE 26-29/09/2013 KWA MAFANIKIO MAKUBWA SANA. AIDHA TUNAWAPONGEZA WAJUMBE WOTE KUTOKA MIKOA YOTE YA TANZANIA KWA KUSHIRIKI VIZURI. IKUMBUKWE VIJANA WA KIISLAM HATUJAWAHI KUKUTANA KITAIFA MARA YA MWISHO ILIKUWA MIAKA 14 ILIYOPITA. TUNAWAKUMBUSHA WAPENDA MAENDELEO YA UISLAMU NA HARAKATI ZA VIJANA MKUTANO MKUBWA WA KITAIFA UTAKAOSHIRIKISHA VIJANA WOTE TOKA NCHI ZOTE ZA AFRIKA MASHARIKI UTAKAOFANYIKA MWANZA HAPO DISEMBAINSHAALLAH WAJUMBE KUTOKA KILA JUMUIYA ZA VIJANA KUTOKA KILA JIMBO, WILAYA NA MIKOA YA TANZANIA WAJIANDAE KWA MKUTANO HUO. TUNAWATAKIA MAANDALIZI MEMA YA MKUTANO HUO WA KIHISTORIA. WA S H I R I K I WA N AW E Z A K U P I G A N A M B A ZIFUATAZO: 0715/0756/0784/0772/822332 AU 0759 362888 AU 0713 495992 AHSANTENI SANA AMIR-KAMATI YA MAANDALIZI

Matangazo

DHUL-HIJJA 1434, IJUMAA

OKTOBA 11-17, 2013

AN-NUUR

Chalinze Islamic Seminary Pre-Form One


Inatangaza nafasi za Masomo kwa wanafunzi wote wanaohitaji kujiunga na Pre- Form One Boarding and Day. Masomo yameanza Tarehe 30/09/2013, Shule ipo Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani-km 7 kutoka njia Panda ya Chalinze Tanga, Kuelekea Morogoro. Nafasi za Kidato cha Kwanza mwaka 2014 Pia tuna nafasi za kuhamia kwa Kidato cha 2 na 3. Usaili Kidato cha Kwanza utafanyika Tarehe 16/11/2013, kwa awamu ya kwanza. Awamu ya pili usaili utafanyika Tarehe 30/11/2013 na awamu ya Tatu Tarehe 20/12/2013. Kwa maelezo zaidi piga simu hizi:0762-270 378/ 0659 303 203/ 0784- 323 203. Au E-mail: chalinzecentre@ yahoo.com MKUU WA SHULE

CHUO CHA UALIMU UNUNIO


S.L.P 32654, DAR ES SALAAM, SIMU: 0713673405, 0715822332, 0715455137/0654083940 E-mail: ununiot@yahoo.com Blog: www.ununio.blogspot.com

NAFASI ZA MASOMO YA UALIMU OFA MAALUMU


(2013/2014)
STASHAHADA (DIPLOMA)- ADA LAKI TANO TU KWA HUDUMA ZOTE KWA MWAKA GRADE 3A (CHETI) SIFA ISIZIDI DIVISION 4.27-ADA LAKI SABA TU KWA HUDUMA ZOTE WASIOTIMIZA POINTI 27 WATAPEWA MAANDALIZI MAALUMU WAKIWA CHUONI. CHUO NI CHA BWENI KWA JINSIA ZOTE NA HUDUMA ZETU MALAZI NA CHAKULA NI BURE NA NI ZA KIWANGO CHA JUU. WANANDOA WANARUHUSIWA KUSOMA. USAJIRI MWISHO NI TAR: 28-OKTOBA 2013 Msajili: 0715 822332 /0756 822332/0784 822332 Mkuu wa Chuo: 0713 673405 WABILLAH TAWFIQ

12

AN-NUUR
MAKALA

12

DHUL-HIJJA 1434, IJUMAA

OKTOBA 11-17, 2013

Tunawatakia Waislamu wote Eid el-Hajj! Eid Mubarak!


DHUL-HIJJA 1434, IJUMAA

OKTOBA 11-17, 2013

AN-NUUR

Uingereza kusaidia uchimbaji mafuta Zanibar


UINGEREZA imeahidi kuwa itashirikiana na Zanzibar katika kuwajengea uwezo wananchi katika sekta ya mafuta na gesi asilia. Balozi wa Uingereza nchini Tanzania bibi Dianna Melrose, ameeleza hayo wakati akizungumza na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, nyumbani kwake Mbweni, nje kidogo ya mji wa Zanzibar. Balozi Melrose amesema anaamini kuwa Zanzibar ina utajiri mkubwa wa maliasili ikiwemo gesi asilia, na kwamba ili wananchi waweze kunufaika nayo, ni lazima wawe weledi na wataalamu wazalendo katika fani hiyo. Naye Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, amemuhakikishi balozi huyo kuwa Zanzibar itashirikiana na Uingereza, na kwamba itafarijika kupata msaada huo wa kitaaluma. Amesema Zanzibar inahitaji sana wananchi wake kupatiwa taaluma na kujengewa uwezo katika sekta ya mafuta na gesi asilia, haa wakati huu ambapo suala hilo linatarajiwa kutolewa katika orodha ya mambo ya Muungano. Mazungumzo hayo pia yalimuhusisha Mkuu wa I d a r a ya A f r i k a Mashariki na Magharibi, Ofisi ya Mambo ya Nje na Jumuiya ya Madola wa Uingereza bibi Harriet Mathews. Wakati huo Maalim Seif amekutana na Balozi wa Norway nchini Tanzania bibi Ingunn Klepsvik na kujadiliana juu ya mambo kadhaa yakiwemo Serikali ya Umoja wa Kitaifa na mchakato wa mabadiliko ya Katiba. Amesema viongozi wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa wanaendelea kushirikiana vizuri

katika kutekeleza majukumu ya serikali, ingawaje bado zipo changamoto katika ngazi za chini za uongozi. Amesema baadhi ya viongozi wa ngazi za chini wakiwemo masheha, bado wanahitaji taaluma zaidi katika kuufahamu muundo huo mpya wa serikali, ili kufikia malengo yaliyowekwa na serikali hiyo, ikiwa ni pamoja na kuwanganisha wananchi. Kuhusu mchakato wa mabadiliko ya Katiba, Maalim Seif amesema kwa sasa wananchi wa n a s u b i r i b u s a r a

za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Rais Jakaya Kikwete ambaye ndiye aliyeasisi mchakato huo. Kwa upande wake balozi Ingunn ameelezea matumaini yake kuwa mchakato wa katiba mpya utamalizika salama na Tanzania itasonga mbele kimaendeleo. Hata hivyo amesema ipo haja kwa Tanzania kusimamia vyema zoezi hilo, ili kuhakikisha kuwa inapata Katiba itakayokidhi haja, kulingana na mabadiliko ya hali ya kiuchumi, kisiasa na kijamii.

MUSLIM UNIVERSITY OF MOROGORO


P.O. BOX 1031 Morogoro, Tanzania. Tel: +255 23 2600256; Fax: +255 23 2600286 Website: www.mum.ac.tz, E-mail address: mum@mum.ac.tz

SIXTH GRADUATION CEREMONY FOR UNDERGRADUATE DEGREES CONFERMENT 2013


The sixth graduation ceremony will be held at the campus of the Muslim University of Morogoro o n S AT U R D AY, 9 t h November, 2013. The ceremony is expected to start at 2.00 pm and end at 5.30 pm. Students eligible to attend the ceremony are undergraduates who successfully completed their studies in 2013. Parents, relatives and guests of the students as well as interested members of the general public are welcome to attend the graduation ceremony in the arena. Guests are expected to dress modestly and decently. Lady guests attending the ceremony are advised to wear the hijab or any dress that does not expose the body other than the face, hands and feet. All eligible students are requested to attend the occasion, regardless of whether or not they bring guests. However, they must inform the office of DVC (Academic) of their intention to participate in the ceremony NOT L AT E R T H A N 1 s t N o v e m b e r, 2 0 1 3 . Preferably call or sms Mobile No: 0712 - 277598 Academic costumes (gowns, hoods and caps) are available for hire by the graduands starting from 1st to 8th November 2013 .The University cashier s office must receive from each of the participating students a total of Ts h . 3 5 , 0 0 0 ( Ts . 20,000 for hiring the costumes, Ts. 10,000 deposit security which is refundable, and Ts. 5,000 convocation fee). Graduands, who do not have costumes on, will not be allowed to participate in the Ceremony. Strictly , we shall not issue Academic costumes on the Graduation day, each and every Graduand shall have to have hired his/her gowns between 1st - 8th November, 2013. Graduands are required to bear in mind that the hired gowns shall have to be returned after the ceremony. A heavy fine will be imposed in case the costumes are damaged, or not returned and/or in time. A hi r i ng C ontr ac t Form will be provided for completion by those intending to hire the costumes. For the safety of all participants and their guests, close-up picture taking and video recording is restricted. morning (9th November, 2013 at 8.30 ) at the graduation site. Failure to attend all rehearsals by students will result in immediate cancellation of their eligibility to participate in the graduation ceremony.

Certificates and transcripts of the graduands will not be given at the ceremony. These can be received at another convenient day from the Office of REHEARSAL the DVC (Academic) Since the rehearsal upon signing register is an integral part books and presenting of the ceremony , all an ID card. graduands who wish to attend the graduation ceremony MUST attend DEPUTY VICE the rehearsal which is CHANCELLOR scheduled on Saturday (ACADEMIC)

Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na Business Printers Limited, S.L.P. 78495 Dar es Salaam.

13

DHUL-HIJJA 1434, IJUMAA

OKTOBA 11-17, 2013

AN-NUUR

14

DHUL-HIJJA 1434, IJUMAA

OKTOBA 11-17, 2013

AN-NUUR

15

DHUL-HIJJA 1434, IJUMAA

OKTOBA 11-17, 2013

AN-NUUR

16

DHUL-HIJJA 1434, IJUMAA

OKTOBA 11-17, 2013

AN-NUUR

Вам также может понравиться

  • Rasimu Ya Katiba (Toleo La Pili)
    Rasimu Ya Katiba (Toleo La Pili)
    Документ0 страниц
    Rasimu Ya Katiba (Toleo La Pili)
    Muhidin Issa Michuzi
    0% (1)
  • Annuur 1183 PDF
    Annuur 1183 PDF
    Документ20 страниц
    Annuur 1183 PDF
    annurtanzania
    100% (2)
  • Annuur 1180 PDF
    Annuur 1180 PDF
    Документ20 страниц
    Annuur 1180 PDF
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1190
    Annuur 1190
    Документ20 страниц
    Annuur 1190
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1193
    Annuur 1193
    Документ20 страниц
    Annuur 1193
    annurtanzania
    Оценок пока нет
  • Annuur 1185
    Annuur 1185
    Документ20 страниц
    Annuur 1185
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1182
    Annuur 1182
    Документ20 страниц
    Annuur 1182
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1179 PDF
    Annuur 1179 PDF
    Документ20 страниц
    Annuur 1179 PDF
    annurtanzania
    100% (1)
  • Annuur 1178
    Annuur 1178
    Документ20 страниц
    Annuur 1178
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1181 PDF
    Annuur 1181 PDF
    Документ20 страниц
    Annuur 1181 PDF
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • ANNUUR 1175b PDF
    ANNUUR 1175b PDF
    Документ20 страниц
    ANNUUR 1175b PDF
    annurtanzania
    Оценок пока нет
  • Annuur 1173 PDF
    Annuur 1173 PDF
    Документ20 страниц
    Annuur 1173 PDF
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1102
    Annuur 1102
    Документ12 страниц
    Annuur 1102
    annurtanzania
    Оценок пока нет
  • Annuur 1112
    Annuur 1112
    Документ16 страниц
    Annuur 1112
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • ANNUUR 1110cc
    ANNUUR 1110cc
    Документ16 страниц
    ANNUUR 1110cc
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • ANNUUR 1176b PDF
    ANNUUR 1176b PDF
    Документ20 страниц
    ANNUUR 1176b PDF
    annurtanzania
    Оценок пока нет
  • Annuur 1107
    Annuur 1107
    Документ16 страниц
    Annuur 1107
    annurtanzania
    Оценок пока нет
  • Annuur 1096
    Annuur 1096
    Документ12 страниц
    Annuur 1096
    annurtanzania
    Оценок пока нет
  • Annuur 1105
    Annuur 1105
    Документ12 страниц
    Annuur 1105
    annurtanzania
    Оценок пока нет
  • Annuur 1091
    Annuur 1091
    Документ16 страниц
    Annuur 1091
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Annuur 1093
    Annuur 1093
    Документ16 страниц
    Annuur 1093
    annurtanzania
    Оценок пока нет
  • Annuur 1094
    Annuur 1094
    Документ16 страниц
    Annuur 1094
    annurtanzania
    100% (1)
  • Annuur 1090
    Annuur 1090
    Документ12 страниц
    Annuur 1090
    annurtanzania
    Оценок пока нет
  • Annuur 1090
    Annuur 1090
    Документ12 страниц
    Annuur 1090
    annurtanzania
    Оценок пока нет
  • Annuur 1089
    Annuur 1089
    Документ12 страниц
    Annuur 1089
    Hassan Mussa Khamis
    Оценок пока нет
  • Annuur 1088 PDF
    Annuur 1088 PDF
    Документ12 страниц
    Annuur 1088 PDF
    annurtanzania
    Оценок пока нет