Академический Документы
Профессиональный Документы
Культура Документы
tz
Sauti ya Waislamu
ISSN 0856 - 3861 Na. 1110 RABIUL AWWAL 1435, IJUMAA , JANUARI 31 - FEB. 6, 2014 BEI TShs 500/=, Kshs 50/=
WAISLAMU tunataka kusikia majina ya Masheikh na wasomi wa Kiislamu wakijitosa katika chaguzi mbalimbali zijazo-Udiwani, Bunge n.k. Soma Uk. 6
Alghaithiyyah, Zanzibar MAJAJI na Mahakimu wametakiwa kujifunza kutoka mafundisho ya Quran ambapo masilahi ya kifamilia na kijamii huzingatiwa zaidi hasa katika migogoro ya kifamilia. U k a t o l e wa m f a n o wa migogoro ya ndoa a m b a p o , b a d a l a ya kungangania kutafuta nani mshindi kati ya mume na mke, mtizamo na mkazo huwa katika kuleta sulhu na
Unakumbuka mauwaji Njia mpya kuelekea Iran Ijumaa Jan. 26, 2001?
Jaji Mkuu wa Zanzibar Omar Othman Makungu. Inaendelea Uk. 3
Prof. Lipumba alisema tusamehe lakini Baada ya u-IGP, muhimu sasa kutubia Uk. 2
2
S.L.P. 55105, Simu: +022 2400786 Cel: 0784 370 208, 0713 110 148, 0755 260 087 , DSM. www.annuurpapers.co.tz E-mail: annuurpapers@yahoo.co.uk Ofisi zetu zipo: Manzese Tip Top Usangi House (Jengo dogo), barabara ya Morogoro, D'Salaam
Tahariri/Maoni
AN-NUUR
AN-NUUR
Unakumbuka mauwaji Waislamu wakizinduka na Ijumaa Jan. 26, 2001? kuifanyia kazi zaka watafaulu N
NI ukweli usiopingika k wa m b a z a k a k a t i k a U i s l a m u , n i m o j a ya vyanzo muhimu sana vya mapato katika jamii. Mapato ambayo msingi wake ni walio na uwezo waliojaaliwa na Mwenyezi Mungu, wanalazimika kutoa sehemu ya mali zao kwa ajili ya kuwasaidia wale wasiokuwa na uwezo. Kutoa zaka ni faradhi n a n g u z o ya t a t u ya Uislamu. Amri ya kutoa zaka imebainishwa wazi k a t i k a Q u r a n 1 4 : 3 1 , pale Mwenyezi Mungu aliposema, Waambieni waja wangu walioamini, wasimamishe swala n a wa t o e k a t i k a v i l e tulivyowaruzuku, kwa siri na kwa dhahiri kabla haijafika siku isiyokuwa na (msaada unaopatikana kwa) kujikomboa wala urafiki. Waislamu tunapaswa kufahamu kwamba neno zakat ni la Kiarabu likiwa na maana ya utakaso. Katika sheria Kiislamu, zaka ni sehemu ya mali ya mwenye uwezo, kwa maana ya asilimia 2.5 ambayo anaitoa mhusika kutekeleza amri ya Allah (sw) na kuwapa wale wanaostahiki (wasio na uwezo) baada ya kwisha mwaka au baada ya mavuno au mapato iwapo mali hiyo imefikia kiwango au faida. Licha ya kuwa kutoa zaka ni ibada na nguzo katika Uislamu, laiti kama Waislamu wangezinduka, wakawa kitu kimoja na kuazimia kuitendea haki kanuni ya zaka na kuitekeleza ipasavyo, leo umma wa Kiislamu ungekuwa katika neema kubwa. Tunamaanisha kwamba zaka ni moja ya vyanzo bora na vizuri vya jamii kuwezeshana, hususan katika huduma za kijamii na kiuchumi. Baadhi tunafahamu kwamba angalao taasisi wanataamula wa K i i s l a m u ( TA M P R O ) walianzisha utaratibu huu wa kukusanya zaka na kuipeleka panapohusika, lakini bado hawajapata ushirikiano unaostahili kutoka jamii ya Kiislamu au labda tuseme, hawajaifanyia kazi vizuri. Inaonekana kama walijaribu au hawajaipa umuhimu unaostahiki. La kuwakumbusha ni kuwa kuna kazi kubwa ya elimu inatakiwa kufanyika. Pili, hii ni taasisi inayohitaji watendaji makini. Ni zaidi ya taasisi za kiserikali za kodi kama TRA. Kwa hiyo si jambo la kufanya kama part time au mradi liende. Tunachukua fursa hii kuwasihi viongozi wetu wa taasisi za Kiislamu nchini, kukutana na kujadili namna ya kuunganisha nguvu zao katika kutekeleza nguzo hii muhimu katika Uislamu. Mfuko huo unaweza kuanzishwa kwa kuwatumia wanataalama wa Kiislamu, kuweka taratibu wa kukutana na matajiri wa Kiislamu na Waislamu wenye uwezo kwa ujumla, ili kukubalina na mna ya kuuendesha na kuusimamia mfuko huo. Wenzetu katika baadhi ya majimbo nchini Nigeria, wamefanikiwa na kila mwaka hutathmini pato la zaka na kuhudimia jamii ya Kiislamu. Aidha katika ngazi za misikiti, utaratibu huo utakaoanzishwa unaweza kupelekwa misikitini, a m b a p o v i o n g o z i wa Misikiti nao watakuwa na chombo maalum cha k u k u s a n ya z a k a k i l a mwaka na kuhudumia jamii ya Kiislamu katika eneo husika. Ni mtazamo wetu kwamba, iwapo Waislamu watazinduka, wakaacha ujinga unaotokana na kuabudu hitilafu zao zisozokuwa za msingi katika dini, wakaweka U i s l a m u wa o m b e l e , watapata mafanikio makubwa kabisa ya kimaendeleo. Hatuwezi kusonga mbele kwa kutaraji sadaka za Ijumaa miskitini. Zaka inaweza kuwa suluhu ya matatizo yaliyopo, la msingi na muhimu ni busara na uadilifu katika kukusanya na kusimamia matumizi ya Zakka kwa mujibu wa sharia na kwa uadilifu.
I miaka 13 imepita toka kuuliwa kwa Imam wa Msikiti wa Mwembetanga. Inawezekana Bwana Omar Mahita, hata hakumbuki kuwa kulikuwa na kiumbe kama huyo duniani. Lakini mjane wa Sheikh Juma Khamis Mohammed anakumbuka. Ya t i m a w a l i o a c h w a , wazazi, ndugu na waumini waliokuwa wanaswalishwa na Imam Juma Khamis, hawawezi kusahau. Ndio maana kila mara wa n a m w o m b e a D u a n a k wa u p a n d e m w i n g i n e , wanamlilia Mola wao juu ya kadhia hii. Kwamba Yeye tu pekee, aliye Hakimu wa mahakimu, Maliki yaumid diin, ndiye atakayetoa hukumu ya haki juu ya waliofanya Jinai ya kumpiga risasi na kumuuwa Imam Juma Khamis. Baada ya serikali kupiga marufuku maandamano ya CUF, Polisi hawakusubiri Jumamosi ifike. Wao walianza kazi Ijumaa, wakifanyia kazi agizo la Makamo wa Rais Omar Ali Juma (Marehemu) kwamba watu wakimaliza tu swala, hakuna cha uradi, dhikri wala mawaidha. Watawanyike, la sivyo! Marehemu Ali Nabwa a l i wa h i k u t o a k a u l i ya kumtetea Makamo wa Rais Omar Ali Juma kwamba ilikuwa kauli na agizo la kuwatahadharisha Wazanzibari kwa sababu alijua kwamba kuna shari ilikuwa imeandaliwa juu yao na hakuwa na namna ya kuwatahadharisha kwa lugha nyingine. Kwa sababu ni jambo la kiserikali naye ni mtumishi wa serikali, lazima alisimamie. Ila kwa huruma ya watu wake ndio akatoa kauli hiyo kama watamwelewa, wajifungie majumbani mwao. Allah ndiye mjuzi nini kilipangwa na nini nafasi ya kiumbe huyo wa Allah, Omar Ali Juma, ambaye sasa hivi yupo Barzakh. Lakini mtekelezaji mkuu, kwa maana kuwa wakati huo alikuwa ndiye Mkuu wa Polisi (IGP), Inspekta Generali wa Polisi, Bwana Omari Mahita, bado yu hai. Na bila shaka Fadhakkir kwake bado inafanya kazi. Ndiyo inayofanyika hapa. Kama alivyosema Profesa Lipumba, ili jinai hii isisahaulike, tukajisahau tukaifanya tena, IGP Mstaafu Omar Mahita akumbuke kuwa mara baada ya swala ya Ijumaa mnamo tarehe 26 Januari, 2001, Polisi walifika Masjid Mwembetanga wakiwa na silaha za moto. Ilikuwa ni majira ya saa saba na nusu mchana siku hiyo, ndio kwanza Waislamu wanamaliza sala zao misikitini. Misikiti mingine ilikuwa imeshamaliza kusali na watu wako milangoni wakitakiana kheri na kuagana. Bila shaka wengine wa l i k u wa n j i a n i t a ya r i wakielekea majumbani kwani misikiti mingine hutangulia kusali kidogo. Kwa Msikiti wa Mwembetanga, ndio kwanza watu walikuwa wanatoka wakiwa wamechanganyika changanyika kwa kusalimiana na kutakiana kheri ya Ijumaa na kuagana. Mara Polisi waliokuwa na silaha walifika ghafla kama waliotumwa kupambana na wahalifu. Baadhi ya mashuhuda wanasema kuwa kikosi kile kilikuwa kinaongozwa na Ofisa wa Polisi, maarufu sana hapa Unguja.
3
Inatoka Uk. 1
maelewano baina yao. Kwamba ukienda kwa mtindo wa kutafuta mshindi, kwanza mashauri huchukua muda mrefu, lakini pia huondoa maelewano na kuharibu maslaha ya familia. Akiongea katika semina ya Majaji na Mahakimu iliyofanyika Zanzibar, Kadhi wa Kenya Mshali Khamis Mshali amesema kutatua m i g o g o r o k wa n j i a za usuluhishi ni bora zaidi kuliko kwenda mahakamani kwa kuwa k e s i z i n a z o a m u l i wa mahakamani huchukua muda mrefu. Mkutano huo wa Majaji na Mahakimu kutoka nchi tano za Afrika Mashariki ulikuwa wa kutafuta njia mbadala za usuluhishi badala ya kutegemea njia ya Mahakamani. Katika mkutano huo uliofanyika Hoteli ya Ocean View Mjini hapa, Mshali alisema kutatua migogoro kwa njia ya usuluhishi ni jambo zuri ambalo wamekuwa wanalitumia muda wote kutokana na kuwa wamekuwa wakisuluhisha migogoro mbali mbali ya kifamilia, ikiwemo ile ya kijamii, urithi, ndoa, talaka na mambo yanayohusiana na hayo. Sisi Makadhi tumeshazowea kutatua migogoro ya kifamilia kwa kutumia njia za kukaa pamoja na kutafuta ufumbuzi hasa kwa kutumia Quran Tukufu na Hadithi za Bwana Mtume (s.a.w) hivyo mafunzo kama haya yatatusaidia sana katika kuendeleza utatuzi wetu tuliouzowea, alisema Kadhi huyo. Alisema, Uislamu umefundisha wazi unapohukumu kesi na hivyo jambo la kwanza ni kusikiliza kwa makini kati ya pande mbili, mdai na mdaiwa. Mantiki ya kusikiliza pande zote mbili za mgogoro kwa makini ni kuwa katika kuhukumu basi, hukumu itolewe kwa haki. Hata hivyo, katika
Habari
RABIUL AWWAL 1435, IJUMAA JANUARI 31-FEB. 6, 2014 ilianza kutumika mwaka 1994 na imekuwa ikitumika sana lakini bado haijaingia miongoni mwa wanasheria. U s u l u h i s h i unatumika katika mashauri yote ya k a z i n a a j i r a h u wa inashughulikiwa katika suluhu mpaka ishindikane ndio inakwenda mahakamani alisema. Alisema utatuzi wa migogoro sio jambo geni katika nchi za Afrika na kutoa mfano kuwa kuna baadhi ya mabaraza ya wazee yanafanya kazi za mahakama katika jamii kwa kusuluhisha migogoro mbali mbali. Aidha alishauri mfumo huo wa utatuzi mbadala wa migogoro uanze kufundishwa vyuoni ili kuanza kujua mbinu za kutatua migogoro kwa njia mpya ya usuluhishi. Kwa upande wake Mwanasheria wa Jumuiya ya Afrika Mshariki Bi Rehema Kirefu ambaye ndio Mratibu wa semina hiyo amesema mafunzo hayo n i m u e n d e l e z o k wa Majaji na Mahakimu ambapo lengo ni kuwajengea uwezo na kuwapa mafunzo ya kutatua migogoro ikiwa ni njia ya kuisaidia mahakama katika kutatua kesi. Katika nchi zetu kuna mrindikano mkubwa na ucheleweshaji mkubwa wa kesi kwa hivyo dunia imeona kama kuna njia nyengine ya kutatua migogoro kwa hivyo wa m e o n a wa h u s i k a wa kesi wakenda nje ya mahakama itasaidia kupunguza 0kesi zilizopo mahakamani, alisema Kirefu. Mkutano huo unafanyika wakati wananchi wengi wanalalamika kuhusu utendaji wa mahakama ambapo ucheleweshaji wa kesi unahusishwa pia na kuwepo kwa rushwa na kutowajibika kwa watendaji wa Mahakamani wakiwemo Majaji na Mahakimu.
AN-NUUR
MAJAJI na Mahakimu nchi za Afrika Mashariki wakiwa katika semina Zanzibar hivi karibuni. m a s h a u r i ya n d o a , ni bora kuyarejesha kwa wanafamilia na kuwahusisha wazazi wa pande zote mbili ili kutafuta ufumbuzi utakaodumisha mahusiano mazuri na kudumisha ndoa. Urudishe utata ule kwa familia na wazazi ndio watakuwa watatuzi wa migogoro ya ndoa, na hayo ndio mafunzo ya dini yetu. Alisema. Akitoa ufafanuzi alitoa mafunzo yanayopatikana kutoka Surat Nisaa aya ya 35 ambayo inasisitiza juu ya sulhu. Aya hiyo inasema: Na kama mkiona kuwa kuna ugomvi baina ya mke na mume, basi pelekeni mwamuzi mmoja katika jamaa za mwanamume na mmoja katika jamaa za mwanamke. Kama wa k i t a k a m a p a t a n o Mwenyezi Mungu atawawezesha. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa habari za siri na habari za dhahiri. (4:35) Mkutano huo wa siku tatu umewashirikisha Majaji na Mahakimu kutoka nchi za Kenya, Rwanda, Burundi, Uganda, na wenyeji Tanzania na Zanzibar ikiwa ni njia moja ya juhudi za kutafuta njia mbadala za kutatua migogoro hiyo inayozidi kujitokeza katika jamii. Akifungua mkutano huo wa mafunzo, Jaji M k u u wa Z a n z i b a r Omar Othman Makungu alisema kumekuwepo na malalamiko ya mashitaka (kesi) kuchelewa, kwa hivyo hivi sasa majaji na mahakimu wanatafuta njia bora za kupunguza changamoto za wingi wa kesi katika mahakama zao. Alisema, ingawa Mahakimu wengi hawapendi njia ya usuluhishi na wanapendelea njia ya kuamuliwa mahakamani jambo ambalo kunakuwa na mshindi na mshindwa katika kesi, lakini mfumo h u o wa u s u l u h i s h i utasaidia sana katika jamii hasa kwa kuzingatia kesi nyingi huzorota mahakamani. Makungu alisema mafunzo hayo yatawaelimisha majaji na mahakimu katika kupunguza kesi za mahakamani pamoja na kuwafanya wafurahie suala la mahakama. S u a l a linalopendekezwa ni kutafuta njia mbadala ya usuluhishi sisi kama mahakama tunaipendelea ingawa mahakimu wengi hawaupendi utaratibu huu ambao umekuwa u k i t u m i wa n a n c h i nyingi duniani hivi sasa, tunaamini utarapunguza kesi mahakamani na pia utarahisisha upatikanaji wa haki kati ya mdai na mdaiwa, alisema Jaji Makungu. Akizungumza kando ya mkutano huo Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Robert Vincent alisema jambo la utatuzi wa migogoro sio geni kwa Tanzania umekuwa ukitumika zamani kabla ya kuja kwa ukoloni ulikuwa ukitumiwa ndani ya familia. Alisema utatuzi kwa njia mbadala uliondoka baada ya kutungwa kwa sheria za nchi lakini bado unaweza kutumika na kuondosha migogoro kwa kuwa jamii inaweza kutumia mfumo huo wa zamani kurejeshwa na kufuata utaratibu wa zamani wa kutatua migogoro ambapo sheria yake ilirekebishwa na
4
Na Mtume alikuwa akisema: Ee Mola wangu m l e z i ! H a k i k a wa t u wangu wameifanya hii Qur'ani ni kihame. (Al Furqan 25:30). Kila sifa njema zinamstahiki Mwenyezi Mungu, Swala na Amani zimfikiye Mtume Muhammad (s.a.w) na jamaa zake. Lengo la kushushwa Q u r a n n a v i t a b u vingine vyote vya Allah (Sw) ni kumuongoza mwanadamu katika njia iliyooka. Amesema Allah (Sw), Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa h u m o Q u r ' a n i k u wa ni uwongofu kwa wat u , na ho ja zilizo wazi za uwongofu na upambanuzi... ( Al Baqara 2:185). Katika kuonyesha uwezo wake wa k u m u o n g o z a mwanaadamu Quran i m e i t wa k wa m a j i n a mengi na moja kati ya majina hayo ni Al-Quran. Maana yake ni Chenye kuunganishwa pamoja au Chenye kusomwa. Yaani Quran ni kitabu kilichofumwa na herufi, silabi, maneno aya na s u r a , k i n a c h o s o m wa mara kwa mara. Kitabu hiki kimeitwa kwa jina Al-Quran kwasababu ni mkusanyiko wa mafunzo ya msingi ya maisha ambayo mtu h a n a b u d i k u ya r e j e a mara kwa mara. Quran ndio Muongozo pekee wa maisha ya mwadamu hivi sasa. Aya nyingi za Quran zinatufahamisha kuwa Q u ra n h u wa o n g o z a waumini katika njia iliyonyooka, huwanyanyua na kuwafanya watawala katika jamii, huwatatulia matatizo yao na kuwaondolea mashaka yote yanayoikabili jamii ya mwadamu kwa ujumla. Huwatoa katika maishagiza nakuwaingiza katika nuru. Amesema Allah (Sw) Hiki ni Kitabu kisichokuwa na shaka ndani yake; ni uwongofu kwa wachamungu, (Al Baqara 2:2). Hakika hii Qur'ani inaongoa kwenye ya yaliyo nyooka kabisa, na inawabashiria Waumini ambao wanatenda mema ya kwamba watapata malipo makubwa. (Al Israai or Bani Israil: 17:9) Tukiwa na yakini kuwa
Makala
AN-NUUR
BINT wa Kiislamu akitoa Da'awah kwa asiye Muislamu. Quran ni kitabu cha Allah (Subhaanahu wa Taala) kisicho na shaka ndani yake (Al Baqara 2:2), na kila tumalizapo kusoma Quran tunabwagiza kwa: Swadaqallahul-adhiim yaani, Kasema Kweli Allah Aliyemtukufu, iweje leo hii Waisamu takribani ulimwenguni kote wawe ni dhalili na wenye mashaka kinyume na aya tulizo rejea? Tatizo liko wapi? Ukichunguza kidogo utagundua kuwa tatizo liko kwenye kuiendea Quran. Ukirejea historia ya kushuka Quran amri ya: ...Na Soma Quran vilivyo (tartila) ni amri yatatu aliyopewa Mtume (Swalla Allaahu alayhi wa sallam) na Mola wake baada ya amri ya kusoma (96:1-5) na ile ya kusimama usiku kwa swala (73:2-3). Kusoma Quran vilivyo (tartila) ni kusoma kwa mazingatio katika utekelezaji hatua kwa hatua, je, amri hii ya Mola wetu tunaitekeza katika kuisoma kwetu? Ni katika msisitizo w a k u i s o m a Q u r a n kwa mazingatio, Allaah (Subhaanahu wa Taala) anatuhimiza kila isomwapo tuisikilize na tuwe kimya ili tustahili rehma zake. Amesema Allah (Sw), Na isomwapo Qur'ani isikilizeni na mnyamaze ili mpate kurehemewa. (Al-A'raaf 7:204) Tareikh inatuonyesha kuwa pale jamii ya Waislamu ilipoiendea Quran kwa mazingatio, iliweza kuja juu na kuendesha mambo yake yote ya kibinafsi na kijamii kwa mujibu wa Quran na Sunnah ya Mtume (Saw) na haikuweza kutawaliwa na matwaaghuut kirahisi. Kwa mfano historia inatuonyesha kuwa Wa i n g e r e z a wa l i p a t a ugumu sana kutawala makoloni yao yaliyokuwa akikaliwa na Waislamu. Wa l i o n y e s h a u g u m u huo katika kuitawala Misri, Uturuki na Afrika Mashariki. Mwaka 1882, Waziri Mkuu wa Uingereza, Bw. Gladstone, akiwa ameinua juu kitabu c h a Q u r a n , a l i s e m a k u wa a m b i a wa b u n g e wa Uingereza (House of Commons): So long as the Egyptions have got this book with them, we will never be able to enjoy quit of peace in that land. (Muhammed Qutb 1972: xi) Tafsiri: M a d h a l i Wa m i s r i wa n a c h o k i t a b u h i k i hatuwezi kamwe kufurahia utulivu au amani katika nchi ile. Katika miaka 1900, kauli kama hiyo ilitolewa na Waziri wa Makoloni ya Uingereza huko Uturuki pale aliposema: Muda wa kuwa Waislamu wanayo Quran, basi watakuwa kikwazo kwetu. Kwahiyo ni lazima tuiondowe kutoka maishani mwao. Mwaka 1900 Kamishina wa Makoloni huko Uganda, Sir Henry Johnson, alimwandikia D.C. wa Wilaya ya Busoga, kumfahamisha sera ya serikali ya kikoloni juu ya Uislamu pale aliposema: Haitakuwa kwa maslahi ya Serikali ya Uingereza iwapo Uislamu utapata wafuasi wengi k wa n i k wa a s i l i ya o Waislamu ni wagumu kuwatawala na katika nyoyo zao wanapinga utawala wa dola ya Kikirsto/Kitwaaghuut. Marekani kwa kupitia a l i ye k u wa Wa z i r i wa Mambo ya Nchi za Nje wa zamani Bw. Collin P o w e l l , n a Wa z i r i wa Ulinzi bw. Dolnad Rumfeld, wamesema kuwa umadhubuti wa Waislamu unatokana na wao kusoma, kufundisha, kuiamini na kuifuta Quran. Hivyo ufumbuzi wa kudumu ni kuwatoa Waislamu katika Uislamu wao kwa kuingilia mafundisho ya Quran. Na njia nzuri ni kuanzia kwenye Madrasa zao. Kampeni hiyo iwe ya dunia nzima. Hapa tutangalia tu wanayafanya Tanzania na mafnikio yao ukilinganisha na yetu sisi Waislamu (wanaharakati). Njia ya kwanza waliona ni kutoa misaada kwenye Madrasa ili iwe ni mwanya na hatimaye kubadilisha
Habari mchanganyiko
AN-NUUR
kiholela. Kuna askari 1,600 wa Ufaransa na maelfu ya askari wengine wa kulinda amani kutoka nchi za Kiafrika huko Jamhuri ya Afrika ya Kati, lakini wameshindwa kuzuia m a u a j i ya Wa i s l a m u yanayofanywa na magenge ya Wakristo. Mashirika ya kutetea haki za binadamu yameonya kuwa kuna uwezekano wa kutokea mauaji ya kimbari dhidi ya Waislamu katika nchi hiyo ya katikati mwa Afrika. Waziri Mkuu mpya wa n c h i h i y o A n d r e Nzapayek e, ameunda Baraza la Mawaziri 20 wa k i w e m o w a u n g a j i mkono wa Seleka na anti-balaka ili kujaribu kurejesha utulivu nchini humo. Mapigano ya ndani katika Jamhuri ya Afrika ya Kati yalianza mwezi Machi mwaka jana, baada ya kung'olewa madarakani serikali ya aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Francois Bozize.
Ikrima, katika mji wa Barawe lakini operesheni hiyo haikufanikiwa. Uchunguzi uliofanywa na Bureau of Investigative Journalism (TBIJ) yenye makao yake nchini Uingereza, unaonyesha kuwa ndege zisizo na rubani za Marekani zimeuwa kiasi cha watu 2,400 duniani katika kipindi cha miaka mitano tangu Rais Barack Obama achukue madaraka nchini humo.
Makala
AN-NUUR
AMIR wa Shura ya Maimamu, Sheikh Mussa Kundecha (kulia) lakini hakuna jibu sahihi lililotoka, zaidi ya lile la Mzee Benjamin Mkapa. Mzee Mkapa, akiwa Rais wa awamu ya Tatu, akijibu malalamiko na madai ya Waislamu aliyopewa ili kuyatafutia ufumbuzi, alikuja na majibu kuwa matatizo ya Waislamu nchini ni ya kihistoria! K wa s a s a s i h a b a , Jumuiya na taasisi mbalimbali za Kiislamu zimejikita katika kuanzisha na kuendesha Shule za Kiislamu bila shaka walijiratibu na kujipanga, na kwa sasa kupitia Shule hizo vijana wengi wanapata fursa ya kusoma tofauti na pale awali ambapo malalamiko ya l i k u wa wa t o t o wa Kiislamu wananyimwa elimu. Bila shaka, kupitia Shule hizo kuna vijana wengi wenye elimu ya kutosha kushika nafasi mbalimbali za kisiasa kuanzia ngazi ya mtaa mpaka Taifa, cha msingi kilichopo ni kwa viongozi (Masheikh) kuitumia rasilimali vijana hawa, kuratibu nakufanya nao kazi kwa lengo la kuwaingiza kunako maamuzi na kupigania haki za Waislamu kwa hoja. Ukiangalia hivi sasa katika idara na Taasisi za umma, kumejaa watu au watendaji wa imani ya dini moja (Wakristo) jambo ambalo linatia mashaka katika maamuzi yanayohusu Waislamu, kwani inawezekana kabisa kuwa maamuzi yao huzingatia utashi wa kiimani. Muasisi wa Chadema, Mzee Edwin Mtei, aliwahi kuilalamikia hali hiyo pale Rais Jakaya Kikwete, a l i p o t e u wa Tu m e ya kuratibu Katiba mpya baada ya majina mengi kujitokeza kuwa ni ya Waislamu. Nikihesabu Waislamu k a t i k a h i i Tu m e k wa kuzingatia majina, naona zaidi ya theluthi mbili ni wao (Waislamu). Wengine (theluthi moja) ni Wakristo au watu wasio kuwa na dini. Alisema Mtei. Muasisi huyo wa Chadema, aliongeza kwa kusema licha ya kwamba Tanzania siyo nchi inayozingatia dini katika maamuzi yake ya kisiasa, ni lazima ikubalike kuwa madhehebu ya Dini yana Influence (ushawishi) katika mchakato na hatima ya maamuzi. Ndiyo maana hata aliyekuwa Rais wa kwanza Tanzania, Mwalim Juliaus K . N y e r e r e , a l i k u wa a k i t e u w a Wa k r i s t o kwa malengo yake, hii ilibainika mwaka 1970, pale alipokuwa akieleza mikakati ya kulisaidia Kanisa Katoliki (Wakristo) nchini, kwamba ni pamoja na kuteuwa watu wenye imani thabiti ya Kikristo na kuwapa uongozi katika Chama (CCM) na Serikali. Hayo yalikuwa ni maongezi baina ya Mwalimu Nyerere (1970), alipo wakaribisha Ikulu, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu ( Ta n z a n i a E p i s c o p a l Conference-TEC) Fr. Robert Rweyemamu na mwakilishi wa Pope nchini, Mgr. Giovano Cerrano. Mikakati na mipango hiyo ya Mwalimu Nyerere, ndiyo inayowaumiza hadi leo Waislamu, kwani ni wazi alifanikiwa kuweka watu wenye Imani thabiti ya Ukristo , ambao na wa o wa m e j i e l e wa n a kuindeleza hali hiyo, a m b a c h o Wa i s l a m u wamekipa jina Mfumo Kristo. Unaweza ukajiuliza kwa nini madai ya Wa i s l a m u ya n a k u wa hayashughulikiwi ipasavyo mbali ya kuyazungumzia majukwaani lakini pia ya n a wa s i l i s h wa k wa maandishi katika mamlaka husika. Hapa ndio ukirejea kauli ya Mzee Mtei, ambaye naye alifanya kazi kwa karibu na Mwalimu Nyerere (awamu ya kwanza) na kauli ya
Nyerere, mwenyewe kwa viongozi wake wa Kanisa, unapata jibu kwa nini Waislamu mambo yao mengi yanapofika S e r i k a l i n i h u k wa m a . Lakini ya upande wa pili yanapatiwa! Kwa mtazamo huo, Waislamu hawana budi kujipanga wenyewe kuanzia ngazi ya chini kwa kujiratibu na kuangalia wanaweza vipi kuingia kwa wingi katika ngazi za maamuzi, ili japo uwiano wa viongozi uwe sawa na katika maamuzi washindane kwa hoja. Kama hushiriki au haumo katika maamuzi ya kiuongozi aidha Mtaa wako, Kata yako, Jimbo lako la uchaguzi na hatimaye Serikali yako, basi uelewe kuwa wale ambao watashiriki ndio watakaokupangia wewe uwe katika hali gani na p e n g i n e k u k wa m i s h a mambo yenu. Kwa kifupi mchakato wa kuwaondoa Waislamu katika hali waliyonayo hivi sasa kama sehemu ya jamii unaanzia katika kukamata nafasi za kisiasa, kwa lengo la kushiriki katika maamuzi kuanzia ngazi ya chini. Masheikh, pamoja na viongozi wa Kiislamu waelewe moja ya jambo ambalo wanapaswa kulishughulikia na kulisimamia wakati huu tukielekea katika chaguzi kuanzia ngazi ya Mtaa (2014). Madiwani, Wabunge na hatimaye Rais (2015) ni hili, je, Waislamu wanaingia na wanashiriki vipi katika hatua hizo. Ni vyema, viongozi wa Kiislamu wakafikiria kuwa na viongozi wa Kisiasa, ambao wana malengo ya kutetea usawa katika jamii na kuondoa dhulma, na waende huko si kwa kudai upendeleo kwa jamii ya Waislamu bali kusimamia haki kwa wote na kutahadharisha ubaya wa kukandamiza kundi moja katika jamii na kulipa nafasi kundi lingine. Ta t i z o M a s h e i k h wanashindwa kubaini kwa muda mrefu kwamba wingi wa Waislamu nchini Inaendelea Uk. 7
Makala
AN-NUUR
SHEIKH Illunga Hassan Kapungu akiwa katika moja ya makongamano ya Waislamu yaliyofanyika Diamond Jubilee miaka ya hivi karibuni. (Picha kutoka Maktaba yetu)
Makala
AN-NUUR
Na Omar Msangi
IJANA mmoja mwanaharakati, kwa uchungu kabisa huku akigugumia kwa kwikwi na kushindwa kuongea, alisimama muda mfupi mara baada ya kumalizika kisimamo cha usiku na kabla ya adhana ya swalat subhi, kueleza masikitiko yake, kwa nini vita inayoendelea Somali na Syria, inaitwa Civil War (Vita ya wenyewe kwa wenyewe) badala ya kuitwa Jihad. S i s i t u n a n ya n y u a mikono tunaomba, A l l a h u m a n s u r l-mujahidina Fi Somali, Syria, mtu anapigwa risasi ya kifua kwa ajili ya dini ya Allah, halafu mtu anasema ile ni Civil War!!... Kufika hapo kijana aliishiwa nguvu kabisa akashindwa kuongea. Wa t u wa l i o k u wa wamekaa mstari wa mbele wakamsaidia kukaa. Hiyo ilikuwa katika semina moja iliyofanyika hivi karibuni mkoani Kilimanjaro ambapo pamoja na mada nyingine, ilitolewa mada juu ya tahadhari. Ilikuwa ni katika mada hiyo, ilisisitizwa kuwa watu wawe makini na wachukue tahadhari wasije wakajiangamiza kwa mikono yao wenyewe. Civil War, ni neno la Kiingereza ambalo kwa Kiswahili maana yake ni vita ya wenyewe kwa weyewe. Syria wanapigana wanajeshi wa serikali, ambao ni Wasyria wakipambana na waasi ambao ni Wasyria pia. Somalia, pamoja na k u w e p o wa l e a s k a r i wa AMISOM ambao wanawasaidia askari wa serikali, lakini kimsingi wanaopigana ni askari wa Somalia, ambao ni Wasomali na Al Shabab, ambao ni Wasomali pia. Kwa upande mwingine, Al Shabab wanapambana na Hizbul Islami na Ahlu Sunna Wal Jamaa ambao ni Wasomali pia. Hata hivyo, hilo halikuwa ndio suala la msingi. Hoja ilikuwa juu ya tahadhari katika kufanya Dawah na Jihad.
Mwaka 1971 vijana waliokuwa wamevalia k a m a Wa p a l e s t i n a , kimavazi na lugha ya Kiarabu ulikuwa huna n a m n a ya k u wa k i s i a kuwa sio Wapalestina, walijitambulisha kwa m p i g a n a j i m m o j a wa Kipalestina katika Gaza wakijitambulisha kuwa wao ni wapiganaji wa Kipalestina wa kundi la Popular Front for the Liberation of Palestine (PFLP) kutoka tawi la Kambi ya Wakimbizi wa Kipalestina Lebanon. Wakiwa na vitambulisho vya kughushi, walidai kuwa wametumwa na Kamanda Abu Seif waje Gaza kukutana na makamanda wa PFLP katika Kambi ya Beth Lahia (Kusini mwa Ukanda wa Gaza). Asubuhi iliyofuata wageni hawa kutoka Lebanon walikutana na kikosi cha watu kadhaa kutoka Beth Lahia katika nyumba moja ya siri. B a a d a ya wa t u w o t e waliokusudiwa kufika na kuchukua nafasi zao katika viti, mgeni mmoja kutoka Lebanon alinyanyua mkono na kutizama saa yake ya mkononi. Ghafla risasi zikarindima, wapiganaji wote wa Beth Lahia, wakauliwa. Ta r a t i b u n a k w a tahadhari kubwa, wageni wale wakatoka katika nyumba ile wakaingia katika vichochoro vya mitaa ya Gaza wakapita njia za panya na kuingia Israel. Jioni ile Kapteni Meir Dagan, aliyekuwa Kamanda wa kikosi maalum cha siri (secret Rimon Commando Unit) katika jeshi la Israel (IDF) akaripoti kwa Generali Ariel (Arik) Sharon kuwa Operation Chamelion (Operesheni Kinyonga), imefanikiwa. Viongozi wote wa Popular Front katika Beth Lahia, wameuliwa. Huu ni mfano tu wa m a t u k i o a m b a y o yanaonyesha nafasi ya tahadhari, na hasa katika kupigania haki na kupigania dini ya Allah a m b a y o i n a a n d a m wa na maadui wengi katika
KIJANA wa Kiislamu (mwenye kofia) akitoa Da'awah nje ya Msikiti nchini Ufaransa. Manasara na Mayahudi, inavyotokea baina ya Al ya mwaka 2009 iliyopewa tunaowajua na tusio wajua. Shabab na Hizbu Islamia, jina, "Which Path to Persia?" Labda kabla ya kwenda S o m a l i a a u b a i n a ya Ukisoma, Which Path m b e l e n i t o e n u k u u makundi ya Jihad katika to Persia: Options for a ifuatayo: Syria). new American Strategy In my opinion, there is a Wakati ule Nasrallah Toward Iran (Analysis huge campaign through the a k i t o k a m a o n i ya k e , Paper Number 20, June 2009) media throughout the world ndio zilikuwa zikipamba inaelezwa kuwa: to put each side up against the moto zile harakati za Kinachotafutwa katika other (to deliberately instigate kulipuliwa misikiti Iraq. vurugu na kelele zote juu fitna). I believe that all this is Leo unalipuliwa wa Shia, ya Syria na Iran, ni Western being run by American and wanakufa makumi ya hegemony across the Middle Israeli intelligence. watu wasio na hatia. Kesho East, with Saudi Arabia Maneno haya yalisemwa unalipuliwa wa Sunni, and Israel the principle dual na kiongozi wa Hezbullah wa n a k u f a Wa i s l a m u . benefactors. Hassan Nasrallah, mwaka Bila kutafakari kwa nini, Kwamba Marekani na 2007 wakati akifanya Waislamu wakajengeana Ulaya ziendelee kuzidhibiti mahojiano na mwandishi chuki na visasi. Leo kila nchi za Mashariki ya Seymour Hersh. uchao ni mauwaji Iraq. Kati huku Israel nayo U n a p o z u n g u m z i a Shia wanauwana na Sunni, ikinufaika. Saudi Arabia f i t n a m a a n a y a k e jambo ambalo halikuwepo n a y o i m e t a j wa k u wa kwa Kiingereza kama kabisa wakati wa Saddam i t a n u f a i k a ! ! ! ! K i v i p i ? alivyoiweka mwandishi Hussein. Labda kwa kuhakikisha Hersh katika makala yake Labda niseme kuwa kuwa ufalme unadumu na ni: kwa jinsi alivyokuwa hakuna wa kuutikisa! i n s u r r e c t i o n a n d na uchungu kijana yule Seymour Hersh akieleza fragmentation within Islam. k u t o k a Ta n g a k a t i k a kinachoendelea Syria hivi U f u p i w a m a n e n o semina ile ya Wilayani sasa, kilipotokea mwaka n i u p i n z a n i w a Same, ni wazi kuwa ule 2007 na malengo yake, k u u v u n j a v u n j a n a mpango wa George W anasema, ili kuidhoofisha kuuangamzia Uislamu Bush, umefanikiwa kwa Iran, serikali ya Bush k u t o k e a n d a n i . K wa kiwango kikubwa sana na iliamua kushirikiana na maana ya kutumia mikono unaendelea kuwanufaisha Suni wa Saudi Arabia ya Waislamu kujiangamiza maadui wa Uislamu na k u a n d a a m i p a n g o ya wenyewe. kwa upande mwingine h u j u m a ( c l a n d e s t i n e N a s r a l l a h k a m a kuwaangamiza Waislamu operations) iliyokusudiwa alivyofafanua, alituhumu na nchi za Waislamu. kuidhoofisha Hizbullah, uongozi wa Rais Bush inayoungwa mkono na k wa m b a wa k a t i h u o Kinachotafutwa Syria sio Iran. ulikuwa ukiandaa mpango Khilafah wala demokrasia Akasema kuwa katika wa fitna ambao lau K w a w a n a o p e n d a clandestine operations hizo, utafanikiwa utaleta balaa kujua ukweli wa mambo, ikawekwa mikakati ya kubwa kwa ummah wa watizame makala ya Hersh kuwatumia Mujahidina Kiislamu: katika gazeti la New Yorker wa Kisuni waliojazwa Kwanza utawafanya (2007) ikisema: f i k r a n a k u c h o c h e wa Waislamu kupambana "The Redirection: Is the kuwa hakuna namna ya wenyewe kwa wenyewe Administration's new policy kufanya mashauriano baina ya Shia na Sunni na benefiting our enemies in the na Ulaya/Marekani, ila pili hata Sunni kwa Sunni war on terrorism?" Jihad. Na kwa upande watakuwa wakipambana Watizame pia ile ripoti mwingine, mujahidina na kuuwana pia (kama ya taasisi ya Brookings Inaendelea Uk. 10
Makala
AN-NUUR
uyu ni Skip Estes mwanamuziki wa kwaya za Kanisa na mhubiri kutoka Texas. Yeye anasema, kiukweli kabisa alikuwa Mkristo mchamungu "dedicated Christian" and a good 'ole boy from Texas. Kama walivyo watu kama yeye katika Marekani, Skip anasema, alichukia kila kilichonasibishwa na Uislamu. Aliaminishwa na akaamini kuwa Waislamu hawaamini Mungu, wanaabudu Jiwe Jeusi huko jangwani, Makkah, ni magaidi wauwaji, ila tu wanabusu ardhi mara tano kwa siku kabla ya kulipua watu katika harakati zao za kufanya ugaidi na kuteka nyara watoto na wanawake. Ni kama ada kwamba ukiwa Mkristo Muamerika, n i l a z i m a u wa c h u k i e Wa i s l a m u n a u a m i n i kuwa ni magaidi, ndivyo alivyojieleza Skip. Akiwa na miaka 70 sasa, Skip Estes alioa na kutaliki, kisha akaoa tena na ana watoto 5. Kutokana na shughuli zake za mahubiri na biashara, amesafiri sana takriban majimbo yote ya Marekani na nje hapo. Nchi alizotembelea ni pamoja na Monaco, the Grand Bahamas, Canada, Mexico, France, Germany, England, Italy, Sweden, Denmark, Holland, Ireland, Germany, na Austria. Akijieleza mwenyewe alivyosilimu, Skip anasema mara nyingi watu wanamuuliza inakuwaje mhubiri na mchungaji wa K i k r i s t o k u b a d i l i dini na kuwa Muislamu, hasa ikizingatiwa jinsi Uislamu na Waislamu wanavyopakwa matope n a k u c h u k i wa k a t i k a ulimwengu wa Ulaya na Marekani unaochukuliwa kuwa ndio ulimwengu wa Wastaarabu? Skip, kwa sasa Yusuf Estes alizaliwa katika familia ya Kikristo Midwest. Kutoka enzi za mababu zake na kutokana na imani yao thabiti katika Ukristo, wamejenga makanisa na shule za Kikristo katika maeneo mbalimbali katika Jimbo lao. Akiwa katika umri wa kuanza shule ya msingi, walihamia Houston, Te x a s ( 1 9 4 9 ) a m b a p o aliendelea na masomo ya dini (Sunday school) na kubatizwa akiwa na umri wa miaka 12. Katika ujana wake, Skip anasema alijawa na kiu ya
Skip Estes kusoma na kujua zaidi juu ya Mungu na Kanisa kwa hiyo alisoma maandiko na kuhudhuria mahubiri ya makanisa mbalimbali yakiwemo Baptists, Methodists, Episcopalians, Charismatic movements, Nazarene, Church of Christ, Church of God, Church of God in Christ, Full Gospel, Agape, Catholic, Presbyterian n.k Lakini pia alisoma na kupata ufahamu juu ya Hinduism, Judaism, Buddhism, Metaphysics na imani za Waamerika wa asili (native American beliefs). Hata hivyo anasema, pamoja na kiu hiyo ya kumjua Mungu na Neno la Mungu, lakini hakusoma juu ya Uislamu. Alipenda muziki na hivyo kuwa muhubiri na kiongozi wa kwaya na muziki wa kanisa. Katika miaka ya 1960s alikuwa akifundisha upigaji k inanda na h atimaye kuanzisha studio yake ya muziki aliyoipa jina Estes Music Studios kule Laurel, Maryland. Kwa zaidi ya miaka 30 Skip Estes alikuwa a k i f a n ya b i a s h a r a n a baba yake katika eneo la burudani, na hasa muziki pamoja na studio wakiwa na maduka ya kuuza vifaa vya muziki na kuandaa program mbalimbali za starehe kutoka Texas na Oklahoma hadi Florida. I made millions of dollars in those years, but could not find the peace of mind that can only come through knowing the truth and finding the real plan of salvation. I'm sure you have asked yourself the question; "Why did God create me?" or "What is it that God wants me to do?" or "Exactly who is God, anyway?" "Why do we believe in 'original sin?" and "Why would the sons of Adam be forced to accept his 'sins' and then as a result be punished forever. But if you asked anyone these questions, they would probably tell you that you have to believe without asking, or that it is a 'mystery' and you shouldn't ask. Anasema Skip Estes kwamba kutokana na biashara hizo, alipata faida ya mamilioni ya dola, lakini kamwe hakuwa na furaha ya maisha. Hii ni kwa sababu alikuwa akijiuliza maswali ya msingi ambayo hakuwa akipata majibu sahihi. Maswali yenyewe ni kama, nani Mungu, kwa nini nimeumbwa. Kilichomtatiza zaidi anasema ni dhambi ya asili. Kwanini dhambi ya asili. Kwa nini mtu aadhibiwe kwa dhambi ya asili? Ukiuliza sana unaambiwa hilo ni fumbo takatifu unachotakiwa ni kuwa na imani! And then there is the concept of the 'Trinity.' If I would ask preachers or ministers to give me some sort of an idea how 'one' could figure out to become 'three' or how God Himself, Who can do anything He Wills to do, cannot just forgive people's sins, but rather and had to become a man, come down on earth, be a human, and then take on the sins of all people. Keeping in mind that all along He is still God of the whole universe and does as He Wills to do, both in and outside of the universe as we know it. Hiyo tisa, kubwa yake anasema ni ile imani ya Utatu Mtakatifu. Anasema kadiri alivyouliza maaskofu, mapadiri na wachungaji, huyu Mungu mmoja, anakuwaje watatu na hawa watatu wanakuwaje mmoja, walikwama kumpa jibu la kutoshekeza akili yake. L a k i n i p i a a l i k u wa akihoji, huyu Mungu muweza wa kila kitu, Muumba wa vitu v y o t e , a n a s h i n d wa j e kuwasamehe watu wake waliomkosea mpaka alazimike kujishusha ajivike mwili wa kibinadamu (na wakati huo huo ni Mungu) ili ateswe apate uchungu wa kibinadamu, kwa dhambi ambayo haukuitenda Yeye, ili iwe ndio kafara ya watu waovu!!!
10
Inatoka Uk. 8 hao hao watumike kuwapiga Mashia huku Mashia nao wakitumika kuwapiga Sunni. Lakini wakati huo huo, Marekani wanawatangaza hawa mujadina kuwa ni magaidi na kupinga mpango wao wa kuweka serikali ya Kiislamu. Sasa Muislamu leo akisikia kila anayepigwa vita na Marekani na kuitwa gaidi, yeye anaona huyo ndiye Mujahidina, kumbe ni wakala wa proxy war. Kwa namna hiyo, Waislamu Sunni wataona makundi haya kama alNusra Front, ni Mujahidina wanaopigana Syria kuwangoa Shia-Alawites ili kusimamisha Khilafah, hivyo watawashabikia na kuwaunga mkono. (The Redirection, Seymour Hersh) Katika kutimiza lengo hilo Hersh anasema, ilikubaliwa Saudi Arabia (na Qatar ) watumiwe kuandaa wapiganaji (Mujahidina) ambao watapambanishwa na majeshi ya Rais Bashar Assad. Lakini ukifanya hivyo, utakuwa pia umewaingiza Hizbullah katika vita, kwa sababu Hizbullah (Lebanon) na Shia, Iran, wataingia vitani kuwatetea Shia, Syria dhidi ya wapiganaji Sunni wanaoandaliwa na kufadhiliwa na Saudi Arabia. Katika vita kama hii, kadiri itakavyoachwa kuchukua muda mrefu, itaidhoofisha Syria kijeshi na kidiplomasia ya kimataifa, kwa hiyo, haitakuwa tena na uwezo wa kukabiliana na Israel katika medani ya kisiasa au kijeshi. Na kweli, hivi sasa inaripotiwa kuwa Israel imeingia Syria na kutoa v i b a l i v ya u c h i m b a j i mafuta katika milima ya Golan, eneo ambalo ni la Syria. Israel imetoa vibali hivyo kwa makampuni ya Murdoch na Rothschild. "Israel has granted oil exploration rights inside Syria, in the occupied Golan Heights, to Genie Energy. Major shareholders of Genie Energy which also has interests in shale gas in the United States and shale oil in Israel include Rupert Murdoch and Lord Jacob Rothschild.
Makala
AN-NUUR
MMOJA ya vikosi vya Kiislamu vinavyopigana Somalia. hivyo miaka 20 iliyopita, lakini serikali madhubuti ya Syria ik a pin g a na ikapata kuungwa mkono na jumuiya ya kimataifa ikashinda. Hata Marekani wakati ule haikuweza kuihami Israel katika dhamira yake ya uporaji. Lakini kwa fursa hii ambayo imepata baada ya Mujahidina kutumiwa kupigana Proxy War ya mabeberu na kudhoofisha serikali Syria, Israel inaona s a s a k u wa n i wa k a t i muafaka na fursa nzuri kwenda mbio kuanza kuvuna mafuta katika milima ya Golan. Sisi huku tunasubiri na tunatamaa kuwa akingoka tu Bashar Assad, Khilafah inasimama Syria! Katika hali ya kusikitisha Seymour Hersh anasema kuwa wakati baadhi ya nchi za Kiarabu zikijifanya zinaichukia Israel na nchi za kibeberu, kwa mlango wa nyuma nchi hizo hizo zinatumika kwa masilahi ya I s r a e l n a n c h i z a Magharibi. Anasema zinatumika kwa namna mbaya kwa sababu zinaunda vikundi vya Kijihad, zinapandikiza hisia za kupigana na jeshi la Syria kama vilivyotumika kupigana Libya. Ni hali ya kusikitisha k wa s a b a b u a n a s e m a inaleta maafa makubwa kwa Waislamu na watu wengine wasio na hatia kama ambavyo raia wa Syria hivi sasa wanateseka na vita ambayo haitanufaisha Syria bali kuiangamiza. Katika makala yake, 2007 New Yorker Article Exposed US-Israeli-Saudi Conspiracy to Overthrow Assad, mwandishi na mchambuzi Tony Cartalucci, anasema kuwa japo ni mbinu ya tangu zama iliyotumiwa na watawala kuwa ukitaka kuwashinda na kuwatawala watu, uwagawe, lakini baadhi ya nchi za Kiarabu zinatumiwa vibaya mno. K wa m b a s i a s a k a l i wanaodaiwa kuwa virusi hatari kwa ustaarbu wa Magharibi, hali iliyozaa vita dhidi ya ugaidi, waliandaliwa na wanapepewa kuendelea kuwepo kwa mpango maalum. Na kwamba baadhi ya nchi za Kiarabu m a k a c h e r o wa S a u d i Arabia akiihakikishia Marekani kuwa wasiwe na wasiwasi na hawa siasa kali na wana-Jihad. Unajua kwa nini? Anasema: Kwa sababu wameyaunda makundi hayo yanayopigana Syria na yaliyokuwa Libya na ni wao wanaoyapa fedha na silaha, hawatashindwa kuyadhibiti. Na kwamba hata kama watafanya v i t e n d o v i n g i n e v ya kigaidi wasivyotumwa na wafadhili wao, lakini ilimuradi hawa Mujahidina wanarusha mabomu kuwapiga Mashia, Hezbollah, Moqtada al-Sadr, Iran, na kwa Syria, kama itaendelea kushirikiana na Hezbollah na Iran, sio tatizo. (-The Redirection, Seymour Hersh.) Hivi sasa nchi za Magharibi, na hasa Marekani, pamoja na Umoja wa Mataifa, wanakuja juu kuishutumu serikali ya Syria kuwa inafanya mauwaji kwa raiya. Jumuiya za kimataifa nazo zinatahadharisha juu ya maafa na janga linaloadamana na mauwaji ya halaiki na maangamizi
11
ASJID Sahaba, katika jiji la Paris, Ufaransa umekuwa maarufu kwa k u p o k e a Wa i s l a m u wapya, kiasi kwamba sasa unaitwa Msikiti wa Waliosilimu (the mosque of the converts). K i l a m wa k a k a t i k a msikiti huo ulio katika eneo la Crteil, Paris, kumekuwa kukifanyika tafrija zaidi 150 za kupokea Waislamu wapya waliosilimu kutoka Ukristo. Msikiti huo uliojengwa mwaka 2008 ukiwa na mnara (minaret) wenye futi 81, ni moja ya alama kuwa Uislamu unakuwa kwa kasi Ufaransa. Inaelezwa kuwa katika mamia ya watu wanaofurika hapo siku ya Ijumaa kwa swala, ni vijana ambao awali walikuwa Wakatoliki wakasilimu. Kwa sasa wanaonekana wakiwa wamevaa kanzu na kofia. Wachambuzi wa siasa za Ufaransa wanasema kuwa hali hii ya kusilimu raia wa nchi hiyo, japo haiwezi kusemwa ni kubwa sana ikilinganishwa na idadi ya Wakristo wa nchi hiyo, lakini inatoa changamoto kubwa kutoka kwa serikali na jamii ya Ufaransa k wa u j u m l a a m b a y o imeonyesha chuki kubwa kwa Uislamu. Ni kutokana na hali hiyo, makachero wa Ufaransa walio katika kikosi cha kupambana na ugaidi, wanajaribu kutoa kitisho juu ya hali hiyo kama njia ya kuichochea serikali kuchukua hatua kali ili kuepukana na ugaidi unaodaiwa kuwa utaletwa na kuongezeka kwa idadi ya Waislamu raia. Wanajenga hoja kuwa kupambana na magaidi wa nje ni jambo jepesi kwa sababu unaweza kuwazuiya wasiingie, lakini hawa wanaozidi kusilimu watakuwa ni raia wenye hati za kusafiria za Ufaransa. M wa k a j a n a p o l i s i waliendesha operesheni waliyo dai ya kusaka magaidi walikamatwa watu 12 wakiwemo raia wawili wa Ufaransa waliosilimu siku za karibuni. Kwa upande mwingine inadaiwa kuwa magereza ya nchi hiyo yamekuwa kama shule za kusilimishia watu kutokana na rekodi ya kusilimu watu wengi wakitokea gerezani. Inadaiwa kuwa pamoja na uchache wao katika n c h i h i y o , Wa i s l a m u
Makala/Tangazo
AN-NUUR
Masjid Sahaba, katika jiji la Paris, Ufaransa ndio waliojazana katika magereza ikiwa ni zaidi ya theluthi ya wafungwa wote na kwamba wakiwa huko ndani hugeuza jela kuwa uwanja wa kusilimisha na kupandikiza siasa kali za Kiislamu. Hivi sasa inakadiriwa kuwa idadi ya Waislamu Ufaransa ni kiasi milioni 6 (kati ya watu milioni 65) ambapo kiasi laki moja (100,000) wanadaiwa ni wa kusilimu. Hii ikiwa ni takwimu rasmi ya kiserikali, taasisi za Kiislamu zinasema kuwa waliosilimu ni zaidi ya 200,000. Huko nyuma, watu wengi walisimu kupitia n d o a . K wa m b a k a m a ni msichana alipata mchumba Muislamu na akakubali kusilimu na kinyume chake, lakini hivi sasa wengi wanasilimu kwa kuangalia maadili na hali za maisha ya Waislamu. Anatajwa kijana CharlieLoup, wa shule ya kanisa, St.-Maur-des-Fosss, aliye na miaka 21 sasa, ambaye alisilimu akiwa na umri wa miaka 19 baada ya kugombana na mama yake. Huyu alilelewa katika Ukatoliki, lakini akiwa na marafiki wengi Waislamu akiwa shuleni. Katika maeneo mengi yenye Waislamu wengi inaelezwa kuwa vijana wenye marafiki Waislamu hufikia nao kufunga mwezi wa Rmadhani, japo si Waislamu katika kile kinachoitwa athari ya makundi (the group effect). Kwa wengi wanaMagharibi, Uislamu ndio mfumo wanaoona utawarejesha katika maadili ya kifamilia na kijamii ambapo haki za wa n a wa k e n a wa t o t o z i t a z i n g a t i wa , l a k i n i ikizingatiwa pia tofauti ya m k e n a m u m e n a majukumu yao katika familia. Katika mji wa Marseille, idadi ya wanaosilimu
MASJID Kadiria Mwasiti uliopo Kijiji cha Kibuta Wilayani Kisarawe Mkoani Pwani wanaomba msaada wa k u c h i m b i wa k i s i m a katika Msikiti huo pamoja na Jenereta kwa ajili ya kusukuma maji kwa matumizi ya Msikitini. Gharama za uchimbaji wa k i s i m a h i c h o n i Shilingi milioni tatu. Dada Mwasiti amejitahidi kuchangisha pesa kwa ajili ya kuchimba kisima hicho na mpaka sasa a m e f a n i k i wa k u p a t a milioni moja tu. Shime Waislamu kutoa n i m o y o , u n a o m b wa kuchangia chochote ulichojaaliwa na Muumba wako kwa ajili ya kuweka akiba ya Akhera yako. Kwa mawasiliano zaidi wasiliana na Dada Mwasiti kupitia namba:0656 092 436. Wabillah Tawfiq
DADA Mwasiti (kulia) akiwa na wanafunzi wa Madrasa katika Masjid Kadiria Mwasiti Kibuta Kisarawe.
12
Mashairi/Makala
AN-NUUR
13
Makala
AN-NUUR
Na Mwandishi Wetu
AARIFA zilizokuwa zimezagaa katika vyombo vya habari Ijumaa iliyopita, ziliarifu kuwa zaidi ya Waislamu 16 waliuliwa na wengine zaidi ya 100 kutekwa ambapo wanawake walibakwa. Mauwaji na utesaji huo ulifanywa na Polisi wa Burma usiku wa Januari 14 walipovamia kijiji cha Du Char Yar Tan, usiku wa tarehe 14 Januari, 2014. Mauwaji hayo yanakuja siku chache baada ya kugundulika mauwaji ya Waislamu wengi wa Rohingya waliofukiwa katika kaburi moja. Kwa mujibu wa taarifa mbalimbali za makundi ya haki za binadamu, wasichana wa Kiislamu wamekuwa wahanga wakubwa wa visa na ukatili wa jeshi na polisi kwani kila wanapovamia miji na vijiji vya Waislamu, hufanya ubakaji. Haya ndiyo yanayowakuta Waislamu wa Rohingya ndani ya nchi ya Burma ambao kilio na machozi yao hayafiki kokote. Si Umoja wa Mataifa wa l a n c h i z a K i i s l a m u zinazopeleka Jihad huko. Katika Burma, watu wa kabila la Rohingya ndiyo walio Waislamu na wengi wao wanaishi katika Jimbo la Rakhine (Rakhine state), ambapo imekuwa kana kwamba serikali ya Kibudha imeweka sera ya kuwahilikisha. Ukiacha mauwaji yanayofanywa na Polisi na wanajeshi, kumekuwa pia na makundi ya watu (Mabudha) wanaovamia vijiji vya Waislamu wakafanya mauwaji, ubakaji, uporaji na kisha kuteketeza nyumba kwa moto. Ilichoweza kufanya Umoja wa Mataifa mpaka sasa ni kusema tu kuwa Waislamu wa Rohingya, ndio watu wanaonyanyaswa na kuteswa kuliko watu wengine duniani kote. Kwa kule kuwa Waislamu, kwa sheria ya Burma ya mwaka 1982, Waislamu hao sio raiya. Wanaonekana kama wahamiaji haramu ndani ya nchi yao (illegal immigrants in their own home.) Haya si madhila yaliyoanza jana au juzi, bali ndiyo maisha ya Waislamu wa Burma miaka nenda mika rudi. Hata hivyo, kwa mujibu wa taarifa za Shirika la Amnesty International na Human Rights Watch, wimbi la sasa hivi lililoanza kiasi miezi 12 iliyopita, imekuwa kama mkakati wa kuhakikisha kuwa Waislamu wanamalizwa kabisa (ethnic cleansing) katika Jimbo la Rakhine. Takwimu za Umoja wa Mataifa zinaonyesha kuwa z a i d i ya wa t u 1 4 0 , 0 0 0 wamekimbia mateso hayo, na hiyo ikiwa ni moja ya njama za serikali ya Burma,
14
Habari
AN-NUUR
M O J A w a Wa n a z u o n i w a Kiislamu Tanzania (HAY-ATUL- ULAMAA) umepokea kwa huzuni kubwa taarifa ya kifo cha mwanachuoni mkubwa wa Kiislamu ulimwenguni Sheikh Dkt. Abdukarim Zaidan, kilichotokea asubuhi ya Jumatatu Januari 27,2014 katika mji mkuu wa Sanaa nchini Yemen. A k i t o a t a a r i f a k wa M a s h e i k h , Ta a s i s i , vyombo vya habari na watu mbalimbali nchini, Katibu mtendaji wa Hay-atu- Ulamaa Sheikh Dkt. Ibrahim Hamad, amesema kuwa Umoja wa Wanazuoni wa Kiislamu Tanzania tayari umepeleka salamu za rambirambi kwa wahusika pamoja na uongozi wa juu wa Chuo Kikuu cha Al-imaan (ALEMAN UNIVERSITY) cha nchini Yemen, ambacho Sheikh Dkt. Abdukarim Zaidan amekuwa akikitumikia kwa muda mrefu mpaka kufariki kwake. Sheikh Dkt. Abdukarim
AL-MARHUUM Sheikh Dkt. Abdukarim Zaidan. nchini Tanzania ni: Sheikh. Ibrahim Ally Hamad, Sheikh. Ramadhan Khamis Kwangaya, Sheikh. Omar Khamis Shaame, Sheikh. Rajab Kassim Mgeo, Sheikh. Yussuf Mwilima na Sheikh. Akhfash Harun Mbwana. Tunamuomba Allah (S.W) amueke Almarhum Sheikh Dkt. Abdukarim Zaidan mahali pema Peponi Aamiyn.
Inatoka Uk. 16 tutakuwa tumemalizana. Yeye aende panapostahili, i we B a r a z a l o l o t e l a Wa i s l a m u a u Ta a s i s i inayokubalika na msikiti husika tunaweza kuwasaidiana nao katika kutatua taizo husika. Alifafanua Kamanda Kiondo. Alisema kuwa tayari Polisi temeke wana Kamati zao za kushughulikia masuala ya dini kwa kila upande. Yaani Kamati ya kushughulikia masuala ya Waislamu kuna polisi Waislamu wakiongozwa na Bw. Zuberi Mombeki ambaye ni Mweyekiti wa Kamati, kadhalika na kamati ya kushughulikia masuala ya Wakristo ina wajumbe Wakristo. Aidha Kamanda Kiondo alisema kufuatia
wale wanaopendezwa na mizozo misikitini watafikia tamati. Hata hivyo alisema matendo ndio yawe yenye kufuatwa zaidi kuliko maneno katika makubaliano yaliyofikiwa. Imamu huyo amewataka Waislamu kuendelea kushikamana katika kitabu chao ili waweze kufanikiwa k a t i k a m a m b o ya o yanayowakabili. Naye Imamu wa Ve t e n a r i S h e i k h Nurdin Kishki, alisema makubaliano waliyofikiwa yanaweza kuondoa migogoro ya misikiti au kuipunguza. Alisema ni jambo la aibu kwa Waislamu kugombana na kupeleka migogoro yao polisi, kwani kwa mujibu wa Kamanda Kiondo hata
Wa k r i s t o wa m e k u wa wakigombana lakini ugomvi wao huutatua wenyewe. Wa k i j a p o l i s i , warejeshwe kwenye Mabaraza ambayo misikiti yao inayafuata ili kujadili na kupata suluhu. Kamanda
kawakumbusha wajibu wao. Alisema Sheikh Kishki. Sheikh Kishki alisema kuwa tatizo linalowasumbua Misikiti mingi pale panapotokea mizozo, ni dharau za wao kwa wao katika usuluhishi. M k u t a n o h u o wa Polisi na viongozi wa dini ya Kiislamu Temeke, umekuja kufuatia kuibuka migogoro mingi misikitini jambo linalowafanya polisi kupokea kesi ambazo kwa mujibu wa kanuni zao hawapaswi kuingilia mambo hayo ya kiibada.
15
Na Salma Said
Makala
AN-NUUR
I mwenye furaha usoni mwake, huwezi kuamini kama ni mgonjwa. Huwezi kukubali kama ana machungu ndani ya moyo wake kwa kuwa sura yake ni ya kutabasamu wakati wote na kuonesha matumaini ya kuishi kwa amani. Lakini utagundua tu, pale utakapomsikiliza kwa makini sana katika maelezo yake na ukimtulizia jicho, ndipo utakapobaini kweli kijana Mansoor Hamad Saleh (21) ana majonzi na maumivu makali anayoyapata katika kiwiliwili chake. Ni miaka mitatu sasa tangu Mansoor alipoanza kulala kitandani kutokana na matatizo ya kupooza miguu yake yote miwili, chanzo chake khasa cha ulemavu huo kilikuwa ni kuanguka juu ya mnazi huko Maangwe, Wete Pemba alipokuwa amepanda kwa ajili ya kuangua nazi kwa ajili ya matumizi ya nyumbani kwao. Mansoor ni mwanafunzi wa kidato cha pili ambaye alikuwa akijitayarisha na kufanya mitihani, lakini kwa bahati mbaya sana kabla ya kuanza tarehe za mitihani alipata mtihani mkubwa wa kuanguka kutoka juu ya mnazi hadi chini na kusababisha matatizo m a k u b wa ya l i y o m l a z a kitandani hadi leo hii, akiwa hana matumaini tena katika maisha yake. Hata hivyo Mansoor anajipa moyo kwamba iwapo atatibiwa na akafanikiwa kupata fedha za kumfikisha nchini India, ataweza kurejea katika hali yake ya kawaida. Amekuwa akiomba apate matibabu hayo ili aweze kurejea shuleni kuendelea na masomo yake kama kawaida. Awali Mansoor alipoanguka kutoka juu ya mnazi miaka mitatu iliyopita, alikimbizwa katika hospitali ya Chake Chake Kisiwani Pemba na alilazwa hapo kwa muda wa mwaka mmoja chini ya uangalizi wa Daktari Shaaban wa hospitali hiyo, kabla ya kusafirishwa na k u l e t wa U n g u j a k a t i k a Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja kwa matibabu zaidi. Lakini licha ya matibabu hayo ya mwaka mzima, hakuweza kupata nafuu na bado yupo kitandani. K wa k u wa n i k i j a n a mdogo, hapendi kulala muda wote na amekuwa akipenda sana kujishughulisha ingawa hawezi, lakini anajilazimisha kukaa japokuwa ni vigumu kwake kukaa katika kiti muda mrefu, hata hivyo amekuwa akijaribu kukaa na kulala mara kwa mara. Napenda niendelee kusoma lakini siwezi kwenda skuli na hiki kigari changu kwa sababu kila wakati naumia sana mgongo wangu, kwa hivyo inanibidi kila wakati
16
AN-NUUR
MAKALA
16
Tupo Mwananyamala Islamic Club Kona ya Makumbusho Dar es salaam. Tunaendelea Kusajili wanafunzi wa Q.T, Reseaters O-Level, waliofeli Kidato cha Pili na Kidato cha nne. Kwa mawasiliano zaidi tutembelee Shuleni au piga simu 0767 307 607, 0783- 723 312 au 0652 010 136. Pata elimu Bora kwa Gharama Nafuu.
AN-NUUR
KAMANDA wa Polisi mkoa wa kipolisi Temeke RPC Engelbert Kiondo (wa tatu kushoto waliokaa) katika picha ya pamoja na Masheikh na Maimamu wilayani Temeke.
tofauti wilayani Kilosa, wamekosa makazi baada ya kaya zao kusombwa na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa zilizonyesha milimani. Mafuriko hayo mbali na kuharibu makazi ya watu, pia yamesababisha uharibifu wa vyakula vya akiba majumbani sambamba n a m a z a o ya l i y o k u wa mashambani kwa kusombwa na maji. Islamic Foundation ni taasisi ya Dini ya Kiislamu ambayo inasimamia mambo mbalimbali ikiwemo kujenga Misikiti, kuchimba visima. Hadi sasa taasisi hiyo imeshajenga takribani Misikiti 600 na kuchimba visima zaidi ya 500 katika sehemu mbalimbali nchini. Kazi nyingine za Islamic Foundation ni kusaidia kutoa mahitaji kulingana na aina ya athari pindi panapotokea maafa, kupitia kitengo maalum kinachoitwa Kitengo cha Maafa.
Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na POA Printing Works LTD, S.L.P. 4605, Dar es Salaam.