Вы находитесь на странице: 1из 16

www.annuurpapers.co.

tz

Facebook:annuurpapers@yahoo.com

Sauti ya Waislamu

ISSN 0856 - 3861 Na. 1115 JAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA , MACHI 7-13, 2014 BEI TShs 500/=, Kshs 50/=

Kesi ya Uamsho:

Tujifunze kutoka Uganda Uk. 2

Isije kuwa SMZ ndio mchochezi


Madai ya ugaidi ni hatari, usaliti Wanasiasa wetu watizame Nigeria

ASKARI wa kundi la Anti Balaka akimuua Muislamu mbele ya askari wenzake na baadhi ya raia Bangui katika machafuko yanayoendelea Jamhuri ya Afrika ya Kati.

Waislamu wazingirwa hawana pa kukimbilia


Waliokimbilia kanisani kulipuliwa
Uk. 4

Umoja wa Mataifa waijia juu Vatican


Ripoti kali ya UN imeitaka Vatican kuchukua hatua mara moja dhidi ya vitendo vya ngono dhidi ya watoto (child sexual abuse). Uk. 13

SHEIKH Farid Hadd.

SHEIKH Azzan Hamdan.

2
www.annuurpapers.co.tz

Tahariri/Habari
Cel: 0784 370 208, 0713 110 148, 0755 260 087 , DSM. E-mail: annuurpapers@yahoo.co.uk Ofisi zetu zipo: Manzese Tip Top Usangi House (Jengo dogo), barabara ya Morogoro, D'Salaam

JAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA MACHI 7-13, 2014 isije kuwa sababu ya kuridhia mashinikizo kama haya ya kukubali mambo machafu yakutuangamiza kama haya ya ushoga na usagaji. Tunalazimika kutoa tahadhari hii kwa kuwa tumezoea kuona sheria mbovu zikiridhiwa kwa shinikozo la Mataifa haya makubwa hata kama hazina tija nasi. Kwa mfano sheria ya ugaidi ya Marekani (Patriotic Act) ambayo t u m e n g a n g a n i wa k u i r i d h i a na kuisaini bila hata kuhoji wanaoinganganiza wana agenda gani. Tujifunze kutoka Uganda, misaada isije kuwa sababu ya kupoteza utu wetu kwa maslahi ya wengine.

AN-NUUR

AN-NUUR S.L.P. 55105, Simu: +022 2400786

HIVI karibuni tumeshuhudia jirani zetu Uganda, Rais wao Bw. Yoweri Kaguta Museven, akiweka saini kuanza kutumika kwa sheria dhidi ya vitendo vya ushoga nchini humo. Katika Sheria hiyo, adhabu kali zitatolewa kwa wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja ikiwemo kifungo cha maisha jela. Aidha sharia hiyo imewabana wanawake ambao huvaa kihasara na kukiuka maadili na ustaarabu wenye heshima. Tangu Rais Museven asaini sheria hiyo, kelele zimesikika dunia nzima, hususan kwa mataifa ya Magharibi na Marekani wakipinga sheria hiyo, kwa madai kwamba inakiuka demokrasia, haki uhuru wa binadamu. Baadhi ya mataifa haya ambayo kwa nchi nyingi za Kiafrika tumezoea kuyaita nchi wahisani, wametangaza kuondoa uhisani wao kwa serikali ya Uganda kwa kukerwa na kuidhinishwa sheria hiyo ya kupambana na vitendo vha kishoga. Uholanzi wao wameshasema kwamba misaada yao ya kifedha waliyokuwa wakiitoa kusaidia bajeti ya serikali ya Uganda kwa ajili ya shughuli za Maendeleo, sasa msaada huo wataupeleka katika taasisi zinazoendesha kampeni za haki za binadamu, hususan zile zinazotetea maslahi ya mapenzi ya jinsia moja. Kwa makusudio hayo, ni wazi kwamba sasa fedha zitamwagwa Uganda ili kuhamasisha harakati za kutetea ushoga. Turudi hapa nchini kwetu ambapo kumesikika wanaharakati wakipambana na mawazo ya jamii kuhusiana uhalali na uharamu wa mapenzi ya jinsia moja. Tunajiuliza, hivi ni nini mantiki ya mataifa yenye nguvu kiuchumi kuyalazimisha mataifa yanayoendelea, hasa ya Afrika kufuata maadili yao na kuwa sheria katika nchi hizo? Hivi maisha ya mashoga na wasagaji yapo hatarini kwa kiasi gani mpaka kulazimishana kutungwa sheria za kuwalinda? Kwa mtazamo wetu, mahusiano ya kingono kati ya jinsia mbili, mke na mume ni mwanzo wa kuendeleza kizazi na familia. Kwa kifupi mapenzi ya mwanamke na mwanaume, pamoja na mambo mengine muhimu lakini lengo kuu ni kupata uzao. Hatuoni sababu nyingine yeyote, iwe ya kibaolojia au ya kimantiki mwanadamu kuingia kwenye uchafu wa ndoa za jinsia moja, zaidi ya hila za kuhitimisha mwendelezo wa kizazi. Inafahamika kwamba katika mahusiano ya ndoa (mume na mke) ni lazima wenza wawe na uwezo wa kutoa viini ambavyo hurutubishwa kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu kitika viungo vya uzazi wa mwenza mwingine ili kutunga mimba hatimaye kizazi kuendelea kwa kupata mtoto ama watoto. Vile vile kwa mtindo huo huo wa jinsia mbili tofauti, mume na mke hupata tulizo la starehe kwa mujibu wa Maumbile yao. Lakini uchafu huu wa ushoga au usagaji,

Tujifunze kutoka Uganda

ni matokeo ya tamaa za kishetani zisizokuwa za msingi, ambazo ni laana na chukizo kubwa kwa Muumba, na hakuna tija yeyote inayopatikana kwayo. Tunalazimishwa kuhalalisha uchafu huu ili kukidhi haja za waliochafuka, na sisi kuishia kuangamia. Tunafahamu kwamba utamaduni wetu sisi Watanzania na sehemu kubwa ya jamii ya bara la Afrika tangu enzi za mabau zetu, hatuna utamaduni huu wa kaumu Lutwi. Lakini kwa jinsi upepo unavyovuma, tutoe tu angalizo kwa serikali yetu kwamba, hofu ya kunyimwa misaada ya kiuchumi kutoka mataifa makubwa, kamwe

Na Bakari Mwakangwale

Masheikh wa Uamsho hawakudhurika jela


hali kile walichokifanya kimeleta faida kama unafuatilia mambo. Alisema Kiongozi huyo, akisherehesha maongezi yake na Viongozi hao. Alisema, kufuatia tukio hilo, Masheikh hao wamemueleza kwamba kuna mambo mengi ya kujifunza, lakini kubwa zaidi wamebaini kuwapo wabomoaji wachache a m b a o k a z i ya o n i kuwagawa Waislamu na huchukia umoja na mshikamano baina ya Waislamu. Aidha, alisema kufuatia kuwepo kwa kauli au amri ya shikamaneni katika kamba ya Mwenyezi Mungu, Masheikh walisema walitegemea wanachuoni, Maimam na viongiozi wa Taasisi za Kiislamu wangekuwa ni mahiri wa kusimamia kauli hiyo katika kuwaongoza Waislamu. Kiongozi huyo alisema, Viongozi hao wameonyesha kusikitishwa na baadhi ya Taasisi au Masheikh, ambao wanajua wazi k w a m b a Wa i s l a m u wamedhulumiwa lakini wanazuka na kupinga kwa ajili ya maslahi ya wanasiasa. Kwa hiyo, alisema Masheikh wa aina hiyo na Taasisi zao hawapo kwa ajili ya Dini. K wa m a a n a h i y o , a k a s e m a Wa i s l a m u wanapaswa waelewe kwamba kuna Masheikh pamoja na kuwa wana elimu za Dini lakini matakwa yao sio kwa a j i l i ya k u i m a r i s h a Dini ya Mungu, bali wanachitizama ni masilahi binafsi. M a s h e i k h wa m e f a r i j i k a k wa n i Wa i s l a m u wa m e t o a misaada yao ya hali na mali na kuonyesha mshikamano mkubwa baina ya Bara na Visiwani lakini pia walishikamana katika ibada za Itiqaf kwa kumlilia na kumshtakia Mwenyezi Mungu, yote hiyo imeonyesha kuwa tupo pamoja kiasi gani. Alisema. Alisema, viongozi hao wameonyesha kuhitaji zaidi kuendeleza umoja baina ya Waislamu kama walivyoonyesha wakati wao wakiwa gerezani na kuweka pembeni tofauti zao kwani umma wowote hauwezi kufanikiwa bila ya kuwa na umoja madhubuti. Alisema, ipo haja ya kuwa na uongozi maalum i l i Wa i s l a m u wa we wa n a k we n d a k a t i k a dira inayofahamika moja kwa moja, kutokana na kwamba Uislamu ni mfumo mzima wa maisha ambao unahitaji usimamizi makini katika nyanja zote.

VIONGOZI wa Wa i s l a m u k u p i t i a Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu wamesema, hawajadhurika pamoja na yote waliyokumbana nayo wakiwa gerezani zaidi ya kuwaletea faida katika harakati zao. Hayo yamebainishwa na viongozi hao kupitia kwa viongozi wenzao waandamizi wa Jumuiya hizo kufuatia wao kubanwa na masharti ya dhamana zao. An nuur, ililazimika k u p a t a m a e l e z o ya Masheikh hao kupitia I d a r a ya H a b a r i ya Uamsho, ambapo msemaji alitoa maelezo kwa niaba yao kufutia maelezo waliyoyapata baada ya kuongea nao kwa ujumla baada ya kutoka gerezani. Hata hivyo msemaji h u y o a l i o n g e a k wa masharti ya kutotajwa jina lake gazetini, alisema kwa ujumla viongozi hao wamesema h awajadh urika kwa muda wote waliokaa jela. Mashekh wamesema hawajadhurika wala hawajaathirika pamoja na yote waliyokumbana n a y o t o k a walivyokamatwa mwezi Oktoba mwaka juzi, na kutiwa jela allaakuli

Habari

JAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA MACHI 7-13, 2014

AN-NUUR

Kesi ya Uamsho:
Na Mwandishi Wetu BAADA ya kulegeza mashariti ya dhamana jambo lililowawezesha Masheikh wa Uamsho kuwa nje wakisubiri kesi zao kuzungumzwa, bado yapo maswali m e n g i ya n a y o h i t a j i majibu. Na kwa upande mwingine, b a d o S E R I K A L I ya Mapinduzi Zanzibar inacho kibarua kigumu cha kuthibitisha kuwa kweli ilikuwa na sababu za kuwakamata Masheikh hao, kuwaweka ndani muda wote huo kwa kuzuiya dhamana zao. Tunasema ikizuiya dhamana kwa sababu mshitaki hapa ni Serikali na ni upande wa mashitaka uliozuiya dhamana. Kesi tunayozungumzia hapa ni ile inayowahusu masheikh 11 ambao walisota gerezani kwa zaidi ya mwaka wakikabiliwa na tuhuma za kuhatarisha usalama na kuharibu mali. Masheikh hao wakiongozwa na Amir wao Sheikh Farid Ahmed Hadi, mkazi wa Mbuyuni mjini Zanzibar mwenye umri wa miaka 41, wana kesi mbili mahkamani wa k i d a i wa k u v u n j a Sheria ya Usalama wa Taifa ya Mwaka 1968 inayosimamiwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kesi nyingine ipo mbele ya hakimu wa wilaya kwenye Mahkama ya Mwanakwerekwe, mjini Zanzibar ambayo watuhumiwa walifanikiwa kupata dhamana lakini wakazuiwa kutoka r u m a n d e k wa a m r i y a M k u r u g e n z i wa Mashitaka wa Zanzibar (DPP), Ibrahim Mzee. Masheikh wengine waliokuwa ndani ni Mselem bin Ali Mselem (52) wa Kwamtipura,

Isije kuwa SMZ ndio mchochezi

BAADHI ya viongozi wa Uamsho waliopewa dhamana na mahakama hivi karibuni. Mussa Juma Mussa (47) wa Makadara, Azzan Khalid Hamdan (48) wa Mfenesini, Suleiman Juma Suleiman (66) wa Makadara, Khamis Ali Suleiman (59) wa Mwanakwerekwe, Hassan Bakar Suleiman (39) wa Tomondo, Ghalib Ahmada Juma (39) wa Mwanakwerekwe, Abdalla Said Ali (48) wa Misuni na Majaliwa Fikirini Majaliwa wa Magomeni Hawa wanakabiliwa na mashitaka matatu kwa pamoja ya kuharibu mali, kufanya uchochezi k wa k u s h a w i s h i n a kuhamasisha fujo, na kula njama ya kutenda kosa. Sh eikh Azzan ana shitaka moja zaidi la peke yake la kutoa maneno ya matusi kwa Kamishna wa Polisi Zanzibar yanayoweza kusababisha uvunjifu wa amani. Makosa hayo ambayo wote w a m e y a k a n a , wanadaiwa kuyatenda katika maeneo tafauti ndani ya Manispaa ya Mji wa Zanzibar, kati ya Oktoba 17, 18 na 19 mwaka jana. Walikaa gerezani kwa zaidi ya mwaka kutokana na kuzuiwa kwa dhamana yao kwa kibali cha DPP Mzee. Masheikh wa Uamsho walikamatwa katikati ya mwezi Oktoba mwaka juzi 2012 mara tu Sheikh Farid alipoibuka baada ya kutoonekana kwa siku tatu mfululizo.Kuibuka kwake kulizusha mjadala mkali huku viongozi wenzake wa Kiislamu wakishinikiza Jeshi la Polisi litoe taarifa kwa kuwa hicho ndicho chombo mahsusi cha nchi chenye jukumu la kusimamia na kuwahakikishia raia ulinzi na usalama wao na wa mali zao. Hata hivyo, badala yake Polisi , walimtaka Sheikh Farid ake kituoni na kueleza alikokuwa. Viongozi wakuu wa P o l i s i wa l i k a n u s h a tuhuma kwamba Sheikh Farid alitekwa na wana-usalama na kuchwa kusikojulikana. Isipokuwa walidai alijicha makusudi ili kuisingizia uovu serikali. Sheikh Farid aliitika wito wa Kamishna wa P o l i s i Z a n z i b a r (ZCP), Mussa Ali Mussa kuripoti Makao Makuu ya Polisi yaliyo Mwembemadema, ambako alihojiwa. Hakupewa dhamana, badala yake waliendelea kumshikilia hadi walipompeleka mahakamani kwa tuhuma za kutoa taarifa Inaendelea Uk. 4

Isije kuwa SMZ ndio mchochezi


Inatoka Uk. 3 za uongo kwa nia ya kuzusha tafrani kati ya wananchi na serikali yao. Kutoka hapo, Polisi wakawa wanamwita Sheikh mmoja baada ya mwengine na waliwaita hata watumishi wa osi ya Uamsho. Tena hapo ikawa ni kamatakamata baada ya kuzuka vurugu lililosababisha kuharibiwa baadhi ya mali za raia na serikali. Na hapo ndio Masheikh wa Uamsho kuwekwa ndani wakidaiwa kuhusika na vurugu hizo halikadhalika kudaiwa kuwa wao ndio walioharibu mali. Jambo ambalo watu wengi wanajiuliza ni hili: Kama polisi, kama s e r i k a l i i l i k u wa n a sababu za msingi na ilikuwa na ushahidi wenye kujitosheleza kuwa Masheikh hao wana hatia kwa mujibu wa sheria iliyopelekea kufunguo kesi hizo, kitu gani tena kinasababisha kesi zisizungumzwe kwa zaidi ya mwaka? Tunachofahamu ni kuwa polisi hawawezi kumkamata mtu mpaka wawe na sababu za kutosha kuamini au japo kudhani kuwa mtu huyo ni muhalifu na wanakuwa na vigezo au vielelezo vya kuwasilisha mahakamani. Sasa haiwezi kuwa una vielelezo vyako mkononi halafu tena uwe na kigugumizi kwa zaidi ya mwaka mzima unafanya uchunguzi au unasita kuviwasilisha mahakamani. Uzoefu unatuambia kuwa kezi za namna hiyo huwa tu zile za kisiasa au za kukomoa watu kwa u b a b e wa m w e n y e mamlaka. Sasa tusingependa dhana hii ijengeke katika mioyo ya watu kuwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa na Maridhiano inaweza kutunga kesi za kisiasa kuwakomoa Masheikh au mtu yeyote kwa sababu kufanya hivyo ni dhulma. Pengine tugusie jambo moja hapa ambalo ni la hatari sana. Wakati alipotoweka Sheikh Farid na zikaibuka fujo kutokana na mihadhara, mawaidha na makongamano yaliyokuwa yakifanyika, vyombo vya dola, baadhi ya watendaji wa serikali na wanasiasa walio kazini na hata wa s t a a f u , wa l i p i g a sana debe na porojo za ugaidi-wakiwapachika UAMSHO Ugaidi wa Ki-Al Shabab, Al-Qaida na Boko Haram. Hakuna mwanasiasa aliye razini japo kwa kiwango cha kawaida tu, na hakuna mtumishi y e y o t e wa c h o m b o cha dola anayejua analofanya, ambaye mpaka sasa hajajua kuwa hii inayoitwa vita ya ugaidi ni njama za kupanga False Flag Operations (Destabilization Plots) za Beberu Mkuu na washirika wake la kupata sababu ya kuzivuruga nchi na kusambaza utando wake wa kikachero na kijeshi kwa manufaa yake ya kiuchumi na mambo mengine muhimu kutosheleza malengo yake ya kibeberu. Lakini pia kama sababu ya kuupiga vita Uislamu. Hivi sasa Nigeria hakukali. Juzi hapa wameuliwa takribani watu 100 wasio na hatia. Kwa mujibu wa taarifa za vyombo mbalimbali vya habari, mabomu mawili yaliyotengwa katika gari, yalilipuka na kuuwa watu 51, huku wengine 39 wakiuliwa kwa kupigwa risasi na wadunguaji katika mji wa jirani. Mi l i p u k o h iyo n a upigaji risasi, ulitokea Jumamosi iliyopita usiku katika kijiji kimoja katika mji wa Maiduguri, Kaskazini mwa Nigeri. Kutokana na uzito wa mabomu hayo, majengo yaliyokuwa jirani yaliporomoka na kufukia watu. Miongoni mwa watu waliouliwa, ni watoto wa d o g o wa l i o k u wa wakisherehekea harusi na watu wengine waliokuwa wakitizama mechi za mpira katika banda la kuoneshea sinema. Kiasi maili 30 k u t o k a ya l i p o t o k e a mashambulizi hayo, watu kadhaa waliokuwa wamevalia sare za kijeshi wakiwa na bunduki aina ya Kalashnikovs (AK-47 rifles) waliwashambulia watu waliokuwa wakijiandaa kwa swala Msikitini. Katika shambulio hilo, waliuliwa watu 39. Upo ushahidi mwingi wa k u t o s h a n a wa k u j i t o s h e l e z a k u wa watu hawa wanaofanya mashambulizi haya, hawana tofauti na wale wanaotumiwa katika Proxy War nyingine za mabeberu duniani. Sasa wanachotakiwa kufahamu makamanda w e t u wa p o l i s i n a

Makala

JAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA MACHI 7-13, 2014

AN-NUUR

wa n a s i a s a n i k u wa wimbo mbaya wanaomwimbia mwana, hatimaye ni kutufikisha h a p a i l i p o f i k i s h wa Nigeri. Sasa labda tuwaulize wanasiasa na makamanda wetu wa polisi, wao katika hali hii watakuwa wanafaidi au kunufaika vipi? Kama wakitufikisha hapo, wao na UAMSHO, nani watakuwa wachochezi, wasaliti na wahaini wa dola na wananchi?

BANGUI

Waislamuwazingirwahawanapakukimbilia
kumleta madarakani Michel Djotodia, ambaye alilazimika kuondoka madarakani Januari 10 mwaka huu kutokana na mashinikizo ya kimataifa. Ta n g u w a k a t i h u o magenge ya Wakristo wenye misimamo mikali kutoka kundi la AntiBalaka, wamewaua maelfu ya Waislamu katika nchi hiyo huku maelfu wakilazimika kukimbilia katika nchi jirani. Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limesema kuna mauaji yanayoendela nchini humo ni njama za makusudi za kuwaangamiza Waislamu Jamhuri ya Afrika ya Kati. Misikiti imebomolewa na nyumba na maduka ya Waislamu kuporwa na magaidi wa Anti Balaka. Kuna askari 1,600 wa Ufaransa na maelfu ya askari wengine wa kulinda amani kutoka nchi za Kiafrika huko Jamhuri ya Afrika ya Kati, lakini hadi sasa wameshindwa kuzuia m a u a j i ya Wa i s l a m u yanayofanywa na magaidi wa kundi la anti-Balaka. Mwishoni mwa mwezi F e b r u a r i , Wa i s l a m u wasiopungua 70 waliuliwa na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya la Anti Balaka kushambulia kijiji kimoja kilichopo kusini magharibi mwa Jamhuri ya Afrika ya Kati. Ta a r i f a z i n a s e m a k u wa , k u n d i h i l o l a Kikristo la Anti Balaka lilivamia kijiji cha Guen na kuwalazimisha watu wote kulala chini, kisha kuanza kuwafyatulia risasi na baadhi yao kuwakatakata kwa mapanga na mundu. Mchungaji Rigobert Dolongo, aliviambia vyombo vya habari kwamba mauaji hayo yalikuwa ya kikatili mno. Mashuhuda wa tukio hilo wameeleza kuwa m a m i a ya Wa i s l a m u wakazi wa kijiji hicho, wameamua kukimbilia kanisani kwa hofu ya kushambuliwa na hata kuuawa na wanamgambo hao wa Anti Balaka. Karibu Waislamu 800 walikimbilia ndani ya Kanisa Katoliki kwenye mji wa Carnot wa kusinimaghairbi mwa nchi hiyo kujaribu kunusuru maisha yao. Kufuatia hali hiyo magaidi hao waliwataka Waislamu waliojisitiri katika kanisa hilo kuondoka nchini humo au wauawe. Waliwataka Waislamu hao waondoke la sivyo Kanisa hilo litateketezwa kwa moto na wao wakiwa ndani. Hivi karibuni gazeti la Daily Telegraph la nchini Uingereza liliandika kuwa, maelfu ya Waislamu wameshauawa nchini humo, huku maelfu ya wengine wakimbilia nchi jirani. U m o j a wa M a t a i f a u l i s h a w a t a k a wanamgambo wa Anti Balaka kuweka silaha zao chini, lakini viongozi wa kundi hilo wamekataa kutii amri hiyo na kusisitiza kwamba wataendeleza mauaji dhidi ya Waislamu nchini humo. Pamoja na kukudhiri mauaji hayo, mpaka sasa bado hakuna hatua zozote zilizochukuliwa dhidi ya wauaji huko CAR.

Ripoti zinaeleza kuwa Wa i s l a m u k a t i k a Jamhuri ya Afrika ya Kati wamezingirwa huku vikosi vya Ufaransa na vinginevyo vikishindwa k u ya p o k o n ya s i l a h a magenge ya Wakristo. Mhariri wa Pan-African News Wire, Abayomi Azikiwe, alisema katika mahojiano na waandishi habari kuwa, jamii y a Wa i s l a m u k a t i k a Jamhuri ya Afrika ya Kati inazingirwa huku watu wanaojaribu kuondoka nchini humo wakizuiwa. Jumamosi iliyopita, magaidi wa Kikristo wa anti-Balaka waliokuwa na bunduki, waliwapiga risasi na kuwauwa Waislamu watatu waliokuwa ndani ya gari huko Bangui, mji mkuu wa Jamhuri ya Afrika ya Kati. Katika tukio hilo la J u m a m o s i , Wa i s l a m u waliokuwa ndani ya taxi walifyatuliwa risasi na kuuawa na magaidi hao wa anti-Balaka. Dereva wa taxi aliyekuwa amewabeba Waislamu hao ambaye alinusurika, alisema alikuwa amewabeba Waislamu hao kutoka kambi moja ya wakimbizi na walikuwa wakielekea katika mtaa wa Waislamu kabla ya kupigwa risasi na kuuawa. M a c h a f u k o ya s a s a Jamhuri ya Afrika ya Kati yalianza Desemba 2 0 1 2 b a a d a ya wa a s i wa Seleka kumpindua Rais Francois Bozize na

Rais Museven asisitiza Uganda sio jaa la taka


KAMPALA Rais Yoweri Kaguta Museveni amesisitiza kuwa Uganda sio jaa la taka akiweka mkazo kuwa ni lazima kuwe na sharia ya kulinda maadili ya Waganda. Ameyasema hayo b a a d a ya n c h i z a Ulaya kukata misaada ya k e z i k i o n ye s h a kukasirishwa kwao kutokana na hatua ya Uganda kuweka sheria ya kuwatia adabu mashoga. Siku chache baada y a R a i s Yo w e r i Museveni wa Uganda kusaini muswada wa sheria ya kupinga l i wa t i n a u s a g a j i katika nchi yake, nchi kadhaa za Magharibi zimetangaza kuikatia misaada serikali ya Kampala kufuatia hatua hiyo. Alhamisi wiki iliyopita, Serikali ya Uholanzi imetangaza kwamba itaondoa m i s a a d a ya k e ya takriban dola milioni nane kwa serikali ya Uganda na kwamba misaada hiyo sasa watapewa makundi ya kiraia. Norway na Denmark pia zimetangaza kwamba zitapunguza misaada yake kwa Uganda baada ya Rais Museveni kuidhinisha sheria inayopiga marufuku liwati na usagaji. Katika radiamali yake kwa hatua hiyo, serikali ya Kampala imesisitiza kwamba, haitalegeza kamba katika kulinda utamaduni wa wananchi wake na ule wa bara la Afrika

Habari za Kimataifa

JAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA MACHI 7-13, 2014

AN-NUUR

RAIS Barack Obama. kwa ujumla. Msemaji wa serikali ya Uganda, Ofwono Opondo, amesema nchi za magharibi zinaweza kuondoa misaada yao, lakini Kampala haitabadili msimamo wala kufuta sheria hiyo.

RAIS Yoweri Museven. Rais Museveni kwa upande wake, amelaani hatua ya Wa m a g h a r i b i y a kuikatia misaada nchi
yake, lakini akasisitiza kwamba Uganda sio jaa la takataka la kuhifadhi uchafu wote wa wakoloni mamboleo.

Madaktari sasa wazuiwa kutibu Waislamu Myanmar


PHNON PENN Serikali ya Myanmar imelizuia shirika la madaktari wasio na mipaka (MSF), kutembelea jimbo la R o k h i n e wa n a l o i s h i Waislamu wengi nchini h u m o i l i k u wa p a t i a m a t i b a b u , k wa k i l e ilichodai kuwa ni kukasirishwa na ripoti iliyotolewa na madaktari hao mwezi Januari, kuhusiana na ukatili unaofanywa na Mabudha wa kuuwa kwa halaiki Waislamu nchini humo. Taarifa iliyotolewa na madaktari hao imeeleza kuwa, hali ya kimaisha inayowakabili Waislamu katika jimbo hilo ni ya kutisha na kusikitisha na kwamba, watu hao wanahitaji misaada ya kibinadamu haraka iwezekanavyo. Hivi karibuni, Mashirika ya kutetea haki za binadamu yaliripoti kukidhiri vitendo vya kinyama vinavyofanywa na askari usalama wa Myanmar vya kuwateka nyara wanawake na mabanati wa Kiislamu wa kabila la Rohingya,

Boko Haram wadaiwa kuuwa watu 90


Nigeria YA M E FA N Y I K A m a u wa j i ya k u t i s h a ambapo watu 90 walilipuliwa kwa bomu katika kijiji kimoja nchini Nigeria. Kwa mujibu wa taarifa za vyombo mbalimbali v ya h a b a r i , m a b o m u mawili yaliyotengwa katika gari, yalilipuka na kuuwa watu 51, huku wengine 39 wakiuliwa kwa kupigwa risasi na wadunguaji katika mji wa jirani. Milipuko hiyo na upigaji risasi, ulitokea Jumamosi iliyopita usiku katika kijiji kimoja katika mji wa Maiduguri, Kaskazini mwa Nigeri. Kutokana na uzito wa mabomu hayo, majengo yaliyokuwa jirani yaliporomoka na kufukia watu. Miongoni mwa watu waliouliwa, ni watoto wadogo waliokuwa wakisherehekea harusi na watu wengine waliokuwa wakitizama mechi za mpira katika banda la kuoneshea sinema. Mashuhuda wa tukio hilo wanasema kuwa, waliona mtu mmoja akiruka kutoka katika gari lililolipuka akijaribu kuchukua pikipiki na kukimbia nayo.

kuwapiga, kuwalazimisha kutumia dawa za kulevya na kisha kuwanajisi katika kambi za kijeshi. Ta n g u m wa k a 2 0 1 2 Waislamu wa Myanmar

wamekuwa wakivamiwa na kushambuliwa, kuuawa n a k u c h o m e wa m o t o nyumba zao, huku serikali ya nchi hiyo ikipiga kimya kuchukua hatua zozote.

H a t a h i v y o , wakamkamata na kumpiga sana na amelazwa katika hospitali ya Umaru Shehu (Umaru Shehu General Hospital.) Kiasi maili 30 kutoka yalipotokea mashambulizi hayo, watu kadhaa waliokuwa wamevalia sare za kijeshi wakiwa na bunduki aina ya Kalashnikovs (AK-47 rifles) waliwashambulia watu waliokuwa wakijiandaa kwa swala. Katika shambulio hilo, waliuliwa watu 39. Taarifa za awali zinadai kuwa wahusika na mauwaji hayo ni magaidi wa Boko Haram.

Makala

JAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA MACHI 7-13, 2014

AN-NUUR

Hekima ni njia ya kufaulu


Mwenyezi Mungu lazima aambatanisha hekima atafaulu katika ulinganiaji wake kwa dalili ya aya ya Qur ani Tukufu amesema Mwenyezi Mungu (Na ni nani anenaye kauli bora zaidi kuliko aitae viumbe kwa Mwenyezi Mungu na Mwenyewe akafanya vitendo vizuri na husema kwa maneno yake vitendo vyake hakika mimi ni miongoni mwa Waislamu kwa hiyo nipo pamoja nao kwa kila jambo) fusilat aya ya (33) na hafanyi haya isipokuwa baada ya kupewa hekima na Mwenyezi Mungu na akamjulisha njia ya waliofaulina kufanikiwa na kumjulisha kuwa naye ni miongoni mwa watu wa kheri kwa mujibu wa Q u r - a n i t u k u f u amesema Mwenyezi Mungu (na wawepo katika (Uislamu) na wanaoamrisha mema na wakakataza mabaya na maovu na hao nao watakao tengenekewa ) Aal-imrani (104) hekima katika lugha ya kiarabu ni kulipatia jambo kwa njia yake kwa kulijua kwa haki. Ama kwa makubaliano ya wanachuoni ni kulipatia jambo kwa njia ya ulinganiaji kwa mwenyezi Mungu M t u k u f u k wa ya l e yanayoshikamana na D i n i k wa n j i a z a k e kwa wakati wake nayo inamaanisha kumuiga nabii Muhammad. (SAW) na isalimike na makosa na iepukane na upotevu na kupoteza watu. Na kwa namna hii itakuwa ni wito u t a k a o s i k i l i z wa n a watu watakufuata kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu. Hapana budi kwa anayetaka kufaulu aijadili akili na awe mpole kwa anaowalingania na kuwaliwaza na kushikamana nao nakuwaombea dua na kuwa mpole Kwa mjinga na kumuelimisha na kumfafanulia na ujitenge na kumuudhi

Na Sheikh Salah Sayed. Shukrani zote anastahiki Mwenyezi Mungu Mola wa ulimwengu, na Rehema na Amani zimfikie mbora wa mitume. Ama baada ya utangulizi huu mfupi:Hakika ya Hekima katika kulingania na njia ya kufaulu, na wengi hunyimwa Neema hii ya Kufaulu, na mtu akizitazama aya za Qur ani tukufu ataiba kwa macho yake namna gani Mwenyezi Mungu alivyo ambatanisha hekima pale aliposema (Humpa hekima amtakae na yeyote mwenye kupewa hekima kwa hakika amepewa hekima kwa hakika amepewa heri nyingi) Surat baqarat aya ya (1189) imeunganyishwa utoaji wa Mwenyezi Mungu na hekima na kufauli kwa kila jambo hutegemea na hekima hivyo amesema Mwenyezi Mungu. Kwa yeyote anayetaka kufaulu katika kulingania kwake lazima atumie hekima kwani Mwenyezi Mungu a m e s e m a ( i t a wa t u katika Dini kwa hekima na mawaidha mazuri na jadiliana nao kwa lile lililo zuri zaidi) Annahli (125) na amesema tena Mwenyezi Mungu (sema hii ndiyo njia ya n g u n i n a i t a k wa Mwenyezi Mungu kwa ujuzi wa kweli mimi na kila wanaonifuata, na Mwenyezi Mungu ametakasika na kila upungufu wala mimi s i m o m i o n g n i m wa wanaomshirikisha Mwenyezi Mungu) Y u s u f ( 1 0 8 ) ameambatanisha kufaulu na hekima katika aya hii kwa kila a n a y e l i n g a n i a k wa

kwa maneno au vitendo na kuwasifia walinganiwaji, na sifa hizi ziambatanishwe na maelekezo kwa njia ya kulingania na asishikilie sana yale yaliyobora na awahimize yaliyo ya suna na anapotaka kumnasihi mlinganiwa basi atumie ishara ni bora kuliko njia ya uwazi na huu ndio u l i k u wa m u o n g o z o wa M t u m e ( S . A . W ) alikuwa akisema (kuna baadhi ya watu lakini hasemi kwa uwazi na kumshambulia mtu na kwa wale wanaotaka njia ya kufaulu katika kulingania kwake kwanza ajisafishe upendo wake na yule anayemlingania. Kwanza aanze k u wa l i n g a n i a wanafamilia yake wa karibu na afulilize ulingano wake kwao, na awe mwepesi wa kutoa zawadi kama litawezekana hilo kwani kitu kinachoacha athari kubwa na nzuri katika nafsi, na awalinganie marafiki kwani rafiki ni kuafikiana kama wasemavyo. Na awafungulie mlango walinganiwa kwa kuwasifu ikiwa ni watu wa haki au wa kheri na kuwahimiza juu

ya utoaji wa sadaka na kufunga na mengineyo. A n a t a k i w a mlinganiaji ajihimize kuwalingania wazazi wawili kwani wao ndio sababu ya kuja kwako na hiyo ndio njia ya kwanza katika kufaulu katika kulingania k wa k o n a a c h a g u e mada inayonasibiana na hali yao ili asiwaambie maneno wasioyafahamu au yaliyo juu ya ufahamu wao wa kiakili na apange mipaka ya malengo yake katika ulingania kwako na achague mada inayosibiana na hali yao ili asiwaambie maneno wasio yafahamu au yaliyo juu ya lifahamu wao wa kiakili. Na apange mipaka ya malengo yake katika ulinganiaji wake na aweke kwa mpango wa kidogo kidogo ili watu wasichoke kwani ilikuwa muongozi wa M t u m e ( S . A . W ) alikuwa anawabashiria watu katika kulingania kwake na wala alikuwa h a f u k u z i wa t u . N a alikuwa akiwepesisha na wala hatii ugumu. Hivyo amesema Mtume (S.A.W) (wepesisheni na wala msifukuze watu wabashirieni amesema t e n a ( wa b a s h i r i e n i

wala msiwafukuzishe na wepesisheni na wala msitie ugumu) na anasema (kwa yakini mumeletwa ni wenye wepesi) na tumeamrishwa tuwe watu wa haki na tuzunguke na haki popote utakapokuwa. Na uangalie uhai wa watu na uhai wa wengine ni kwa ajili hiyo ndio maana umepewa Elimu na hekima na uwezo mwenye kuongeza Elimu kama alivyosema Mwenyezi Mungu (na hamkupenda Elimu isipokuwa kidogo) na awe yeye Mwenyewe Mwenye kuielezewa hekima kuwa ni kitu kilichompotea muumini popote atakapoikuta hukokota. Na kwa nini isiwe hivyo na hii ni njia ya kufaulu na kufanikiwa Duniani na akhera. Na juu yako ujue kwamba hekima kama alivyosema Ibnu L-qayimi kufanya yanayotakiwa kwa namna inayotakiwa na kutokana na hili utajipangia wewe m w e n y e w e n j i a ya kufaulu. Ninamuomba mwenyezi Mungu atufanye miongoni mwa wanaosikiliza maneno na kuyafuata kwa vizuri.

AWALI ya yote ni wajibu wetu kumshukuru sana ALLAH (s.w.t.), aliyetuwezesha kufika hapa tulipo katika suala zima la mchakato wa katiba yetu mpya. Hali kadhalika tunapaswa kuipa kongole awamu hii ya n n e ya u t a wa l a wa nchi yetu, awamu ambayo hatamu zake zimeshikwa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete. Kongole ni zake kwa kubuni mfumo huu wa aina yake wa Bunge maalumu la katiba. Katika historia ya nchi yetu, hili ndilo litakuwa Bunge la kwanza la aina hiyo nchini. Ni muhimu sisi Watanzania kuwa na kuuendeleza utamaduni huu mzuri wa kumpongeza na kumshukuru kiongozi anapofanya jambo zuri, bila ya kujali chama chake, kabila lake, dini au itikadi yake. Bunge maalumu la katiba lilianza vizuri siku ya Jumanne ya Februari 18, ingawa lilikuwa na baadhi ya kasoro ambazo kwa siku ya mwanzo zinaonekana ni kasoro kubwa. Lakini kadiri siku zinavyosonga mbele, kasoro katika Bunge hili zinazidi kukua badala ya kupungua. Hoja za kupoteza muda na kuvurugana badala ya kujadiliana, zimekuwa zikimlazimu Mwenyekiti wa muda wa Bunge hili maalum, M h e . Pa n d u A m e i r Kificho, kuahirisha vikao mara kwa mara na kuendelea baadae, ikiwa ni kama njia ya kuwapa muda wajumbe kutuliza wahaka, angalau kuweza kuendelea na mjadala. Ikumbukwe kwamba ndio kwanza wajumbe hao wapop katika kujadilki kanuni tu, za kuliendesha Bunge

Uhuru uwe ndio uti wa mgongo wa Katiba yetu


lenyewe. Wakati hayo yakifanyika, hoja za msingi zinaendela kuwepo mezani bila kujadiliwa huku muda nao ukizidi kunyonyoma na wajumbe wakiendelea kumungunya posho zao licha ya kutokuwepo tija katika mjadala unaoendelea. Uchaguzi wa kwanza wa kumpata Mwenyekiti wa m u d a h a u k u wa katika nidhamu/ utaratibu mzuri wa kufurahisha kwa sababu zifuatazo: Baadhi ya wabunge walikuwa huru sana kama kwamba hawako B u n g e n i , wa l i k u wa kama kwamba wako kijiweni, jambo ambalo l i l i k u wa l i k i a s h i r i a kujiamini sana kwa sababu ya uzoefu wao wa kuwapo bungeni kwa kipindi kirefu. Au huenda ikawa wapo wengine hiyo ndio mara yao ya kwanza kuwa bungeni na ndio sababu ikawa hawajui heshima/kanuni/ taratibu za Bunge. Aidha vicheko vilikuwa vingi sana hasa kwa upande wa wabunge wanawake, kama kwamba wako katika sherehe zao za harusi au mfano wake. Mzozo wa kutaka nyongeza ya posho, pia ulichafua taswira nzuri ya Bunge hili maalumu la katiba. Baadhi ya wabunge wetu walitaka nyo nge za ya posh o katika kipindi cha mwanzo tu cha Bunge hili, wakati ambapo hata sisi wawakilishwa wao hatujauona umuhimu na namna wanavyo yawakilisha matakwa yetu katika Bunge hilo. Pamoja na kasoro hizo zilizojitokeza, s i s i wana n c h i b ado hatujakata tamaa na tunataraji Bunge letu hilo

Makala

JAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA MACHI 7-13, 2014

AN-NUUR

litakuwa na tija, ufanisi na matokeo mazuri yanayo kusudiwa, Inshallah. Kwa upande wetu sisi watu wa Taasisi za Dini, tunampongeza sana ndugu yetu Mhe. Sheikh Musa Kundecha kwa mchango aliouonyesha wa kutetea haki zetu za kiimani. Aliyoyasema Kundecha katika Bunge hili la katiba, ndio hayo ambayo yanasemwa mara kwa mara na watu wenye itikadi sahihi katika dini ya Kiislamu. K a d h i a ya K a t i b a kutambua uwepo wa Mungu, ni kadhia isiyohitaji mjadala mbele ya viongozi wa dini zote kuu hapa nchini. Kwa sababu lengo la Katiba hii ni kutumiwa na watu katika siasa zao, maamuzi yao na mambo yao yote, na walengwa wenyewe ni hawa Watanzania ambao asilimia kubwa ni Waislamu au Wakristo na wote hao wanaamini kuwa Mungu yupo. Jingine ambalo Mhe. Kundecha alilitilia mkazo, ni uhuru wa kuabudu. Waislamu wawe huru katika

AMIR wa Shura ya Maimamu, Sheikh Mussa Kundecha.


kutekeleza ibada zao na hali kadhalika Wakristo nao wawe huru kutekeleza ibada zao kwa mujibu wa imani yao, bila ya masharti wala kubughudhiwa. Hivi ni kusema k wa m b a k a d h i a ya uhuru katika Katiba yetu; uhuru wa kuabudu, uhuru wa kutoa maoni na kujieleza, vyote hivi vinakaa nafasi ya u t i wa m g o n g o katika kiwiliwili cha mwanadamu. Hakuna Demokrasia bila ya uhuru, wala hakuna uhuru unaomzuia mtu kufanya ibada au kutoa maoni na kujieleza. Bunge letu linapaswa kuwa mfano na kiigizo c h e m a k w e t u , k wa kuvitumia vifungu vyote vilivyomo ndani ya rasimu ya Katiba na kuvifanyia kazi kabla mjadala haujakamilika na Bunge kukamilisha kazi yake tuliyolipa. Mfano mzuri ni kuanza kukifanyia kazi kifungu cha uhuru wa kuabudu kwa maana ya kwamba, vikao vyote vya Bunge visimamishwe kila siku ya Ijumaa ili kutoa fursa kwa wabunge Waislamu

kuhudhuria swala ya Ijumaa Misikitini, bila ya kuwa na wahaka wa kupitwa na mijadala inayoendelea. Kama ilivyo hivyo hivyo pia kwa kila siku ya Jumapili, wabunge Wakristo nao wanapata fursa ya kuhudhuria ibada Makanisani. Kadhia nyingine ambayo ni sehemu katika uhuru wa kutoa maoni, ni ule mjadala wa kura ya wabunge kupigwa kwa siri au kwa dhahiri. Kwa maana hii pana, haja gani kura iwe dhahiri wakati kupiga kura ni amana baina ya mja na Mola wake, katika kuiwakilisha nafsi yake na nafsi za anaowawakilisha? Sio jambo jema watu kutoaminiana kiasi cha kufikia wanapowasilisha maoni wenyewe, iwe lazima yaonwe au kusikiwa na wengine. Madai yanayotolewa na baadhi yetu kwamba kiongozi wa awamu ya pili ya Dola ya Kiislamu, aliyeshika hatamu za uongozi baada ya kufariki kwa Bwana Mtume Muhammad Inaendelea Uk. 13

Makala

JAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA MACHI 7-13, 2014

AN-NUUR

Majeshi ya Marekani na bunduki za Yesu-2


Na Philip Giraldi, Mtandao wa kupashana habari KWANINI yote hii iwe muhimu; kama kila mtu anajiamulia mwenyewe anachotaka kuamini? Ni muhimu kwa sababu k a d h a a . Wa u m i n i ambao hawajengi u k u t a wa m o t o wa kile wanachoamini na majukumu yao ya kikazi, ambako kwa askari inahitaji kujumuisha Wamarekani wote na siyo tu wale ambao wanafikiri kama yeye mwenyewe, kwa hakika atawapendelea wanadini wenzake, hasa kama inazungumzwa kuwa ushupavu wa dini ni kifanikishi muhimu cha kuwa askari. Wakereketwa wengi wa Kikristo inaeleweka kuwa wanaamini kuwa wajibu wao wa kwanza ni kwa Mungu, na siyo lazima kwa nchi yao au kwa wananchi wenzao, lakini wanashindwa kuona jinsi uelekeo huo unavyoweza kuwa haukubaliki kwa mtu am baye am echagua kuitumikia serikali. Ni kwa jinsi gani dhana ya Mungu kabla ya nchi inafanya kazi katika medani ya jeshi inaweza kuyakinishwa na kilichotokea katika harakati ya Chuo cha Jeshi la Anga kuhusu ushuhudiaji chuoni. Makundi ya wanafunzi yalikuwa yakikusanyika k a t i k a v y u m b a v ya pamoja kwenye mabweni na maktaba kuwa na vipindi vya kusoma Biblia. Uelewa k u wa e n e o l a wa t u kutumia katika chuo hicho nia yake ilikuwa ni kutumiwa na watu wote, na kuamua kutumia eneo hilo kwa shughuli maalum ya kushtukiza ya kundi moja ingezuia wengine kutumia au kupoteza hamu ya kutumia eneo hilo ilibaki mwelekeo unaofahamika hadi Naibu Mkuu wa chuo, mkereketwa wa Kikristo aitwaye Johnny Weida ambaye mapema aliwashauri wanafunzi k u wa u n a wa j i b i k a kwanza kwa Mungu wako, alisema bila wasiwasi kuwa hali hiyo itaendelea. Unataka kuwa na somo la Biblia katika chumba cha TV cha wanafunzi? Hakuna tatizo. Kuongezeka kwa uanadini unaojionyesha kwa uwazi miongoni mwa askari wa Marekani pia kumekuwa na matokeo si haba ya hali halisi, kwa kuwa chombo cha propaganda kwa makundi kama Al Qaeda na kuimarisha imani iliyoenea kote kuwa Marekani inaendesha vita mpya ya dini dhidi ya tawala za Kiislamu. Juhudi za kuwataka askari wasambaze Biblia katika lugha za Afghanistan, zilizosisitizwa na wasimamizi ibada katika jeshi, zimetajwa na wachunguzi wa ndani na wa kimataifa kuwa ni hulka inayopingana na kanuni za jeshi pamoja na amri za jeshi kuhusiana na eneo la kivita la Afghanistan. Halafu kuna zile habari za kushangaza za Pat Tillman, mchezaji wa raga wa ligi ya taifa ambaye alipigwa risasi na kuuawa na askari wenzake wakiwa katika doria nchini Afghanistan mwezi Aprili 2004, na kusababisha juhudi kubwa za jeshi kuficha kilichotokea hadi kufikia kifo chake Tillman anaelekea alikuwa mtu asiyeamini, na akijieleza hivyo wakati wote, na kuna ushahidi kuwa alikuwa ameanza kupinga vita vya Irak na vya Afghanistan. Uvumi uliohusishwa na familia ya Tillman na pia jenerali mstaafu Wesley Clark unasema

Kituo cha Kiislamu cha Kimisri kimefanya kongamano la kidini siku ya Jumamosi iliyopita kwa kushirikiana na Msikiti wa Kichangani Magomeni lenye anuani ya ( ULINGANIAJI WA ATHARI ZAKE KATIKA KUPIGA VITA UBABE NA UGAIDI. aliuawa kwa makusudi,
na mapango ya mbweha ambacho kina ukweli kwa kiwango kile kile cha vibwagizo vingine. Ni kuwa jeshi la Marekani l i n a o n e k a n a k u wa l a wapiganaji wa kupenda kazi hiyo ambalo halina uhusiano wa karibu na wananchi wa kawaida, hali ambayo kwa hilo tu inaleta wasiwasi. Na kuwa inawezekana pia wa kidini aliyekuwa, ninavyokumbuka, Kanali na Mkatoliki kutoka Ireland alikuja katika kambi yetu akibwabwaja moto na mateso ya kiama. Alitoa picha nzuri ya Pat OBrien akicheza nafasi ya Padri Francis Duffy wa kikosi cha 69 cha wapiganaji kabla hajapotea katika wingu la moshi wa sigara nene, akikoroma jambo fulani kuhusu kuua wa k o m uni s t i . Vi j a na wawili kutoka Chicago walimfuata nyuma wakiita Fatha, Fatha, bila shaka wakiwa na haja ya msaada wa kiroho wa aina moja au nyingine, lakini alishahitimisha ziara yake ya kiroho kambini. Kazi ilikuwa imemalizika. (Philip Giraldi, ofisa wa zamani wa CIA, ni Mkurugenzi Mtendaji wa kitengo huria cha ushauri wa masuala ya sera za kiusalama nchini Marekani, Council for the National Interest.)

mashimo matatu ya risasi utosini yakionyesha kuwa alipigwa risasi kwa silaha ya M - 1 6 k wa k a r i b u . Askari wenzake katika hatua isiyo ya kawaida walizichoma moto nguo zake na deraya zake za mwili baada ya kufa, na kitabu chake cha kuandika kumbukumbu zake za siku hadi siku kilikuwa hakionekani. Uchunguzi wa jinai uliombwa lakini ukakataliwa na utawala wa jeshi. Wakati familia ilipolalamika, ofisa wa uchunguzi mwandamizi Luteni Kanali Ralph Kauzlarich alisema kuwa wanadai hilo kwani familia ya Tillman wote hawaamini. Kama wewe unakana kuwa Mungu yupo na huamini katika chochote, kama unakufa, ni wapi unapokwenda? Hakuna chochote. Unakuwa sehemu tu ya minyoo ardhini. Kuna kibwagizo kuhusu askari, kutoamini

inajijenga kuwa tabaka la wapiganaji ambalo pia lina ushawishi wa kina wa kidini kama hitaji muhimu inasaidia tu kuongeza umbali wa kihisia kati ya askari n a wa n a n c h i wa l i o wengi, nje ya masuala ya kikatiba inayozuia. Uzoefu wangu na vita vitakatifu kwa msaada wa Jeshi la Marekani umekuwa tofauti kidogo, lakini ulikuwa ni wa askari wa mujibu wa sheria, zamani sa na. Katika mafunzo
ya awali wakati wa vita ya Vi e t n a m m s h a u r i

Makala

JAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA MACHI 7-13, 2014

AN-NUUR

Filamu Siri za Vatican' yafunua mikwamo ya kimaadili inayomkabili Papa mpya


Na Frontline/Yahoo News, Februari 25, 2014

KANISA Katoliki linafurahia kiwango cha juu cha kupendeza katika vyombo vya habari kuliko ilivyokuwa kwa miongo kadhaa sasa, na mamia ya maelfu ya Wakatoliki waliokuwa wamekata tamaa wanarudi, kwa upande mmoja kutokana na u o n g o z i m p ya n a kwa njia fulani wa k i m a p i n d u z i , wa Papa Francis I. Lakini, kama inavyosema makala ya kina ya kituo cha utangazaji cha PBS 'Frontline' chenye kichwa cha habari S i r i z a Va t i c a n , mikasa ya kimaadili ambayo ilikaribia kuteketeza imani ya wengi katika kanisa, iliyoanza baada ya kifo cha Papa Yohana Paulo II mwaka 2005, bado haijatokomea. Isitoshe, kufaulu kwa Upapa wa Francis I kutategemea anavyoitatua mikasa hiyo kwa haraka na kwa kina. Siri za Vatican iliyoonyeshwa Washington Februari 25 katika vituo vya wazi vya televisheni, inaangalia bila kubakiza kitu, hali ya kanisa Papa Francis aliyoirithi kutoka kwa mtangulizi wake, Papa Benedict XVI ambaye alimfuatia Papa Yohana Paulo II, na mkuu wa kwanza wa kanisa kujiuzulu katika kipindi cha miaka 600. 2012 ulikuwa

mwaka wa machukizo kwa (Benedict)," anasema Antony Thomas, mtengenezaji wa kipindi/makala hiyo, mwandishi na mkurugenzi wa filamu hiyo kwa ajili ya Frontline, aliiambia Yahoo News katika mahojiano. Kila kitu kilikuwa kinaporomoka. Alikuwa anataka kuisafisha benki ya Va t i c a n . A l i k u w a katika hali ngumu sana muda wote." Mwaka wa mikasa katika maeneo mengi, siyo tu kuhusiana na ubadhirifu wa fedha katika benki ya Vatican, ila pamoja na matukio ya uingiliaji (kunajisi) wa watoto wadogo na mapadre kuenea zaidi ya nchi 20, na hivyo kuzidi kudhihirika kwa unafiki wa kanisa kuhusu ushoga. Mabadiliko mawili muhimu yaliyoletwa na Benedict yalikuwa yamebadilisha kwa uwazi katekismo ya Kikatoliki - yaani, kanuni za kutumika kwake - kuainisha ushoga kama uharibifu wa kimsingi, kuweka mazingira ya, pamoja na mambo mengine, kuwaondoa mapadri shoga. Wakati huo huo, taarifa zilianza kusikika Roma kuhusu uwepo wa mafia ya kishoga' ndani ya kanisa ambayo ilikuwa inajumuisha baadhi ya maofisa wake wakuu, ambao hawakuwa na simile katika kutumia nguvu zao za kisiasa na pia kuendelea kuishi maisha ya wazi kabisa na ya ushiriki

PAPA Francis (katikati) akiongea na Rais Barack Obama (kushoto) pamoja na mkewe. mwingi katika ushoga. N a a m i n i a n a t a k a ambaye pia alifaulu Kuliwa na mengi tuwahudumie watu kuzaa watoto kadhaa yaliyojitokeza, ikiwa ni w a k e , n a h i v y o na wanawake takriban pamoja na mtu mmoja, chapisho linaposema wawili. Makosa ya Maciel ambaye anasemekana huwezi', hilo ni janga a l i k u w a a n a t o a kubwa. Ni maumivu.. ya l i f i c h u l i wa k wa wavulana wa kwaya n a t u m a i n i k u w a , njia isiyopingika na kama wa kupanga," siku moja, Mapadri uchunguzi wa Vatican T h o m a s a l i s e m a . w a n a w e z a k u w a ulitolewa mwaka T u l i c h o j a r i b u huru katika uhusiano mmoja baada ya kifo kufanya katika filamu na wawe Mapadri c h a Pa p a Yo h a n a hii, ni kutokufanya wazuri. Kuwa useja P a u l o I I . H u k u j a m b o h i l o l i w e katika Kanisa utakuwa akiwa anatazamiwa wa kujiamulia." kutangazwa mtakatifu rahisi. Wako watu Siri za Vatican" h a p o A p r i l 2 7 , wengi katika Vatican p i a i n a a n g a l i a Papa huyo alikuwa ambao ni mashoga mwingiliano kati ya m u u n g a j i m k o n o na wanaishi maisha hitaji la Kanisa kuwa mkubwa wa Maciel ya useja, na hii ni M a p a d r i wa b a k i e na wana-Mgambo wa ngumu kwao. Na kuna katika useja na idadi Kristo, ambayo ilijenga wengine wanashiriki kubwa ya uingiliaji sifa ya ukusanyaji k i k a wa i d a k a t i k a watoto katika ngazi raslimali kwa nguvu, ushoga." zake tofauti. Si mengi kuwashawishi vijana K a t i k a f i l a m u yalikuwa mabaya kama k u wa wa t a wa , n a h i y o , Pa d r i s h o g a lile la Padri Marcial k u s i m a m a w i m a a n a y e f a n y a k a z i Maciel Degollado, d h i d i ya u l i b e r a l i Vatican anaeleza athari mwanzilishi wa umoja (uhuru wa mtu binafsi za mafundisho ya w a k i - K a n i s a w a kupindukia). kanisa kuwa ni kama Legionaires of Christ Ikiwa imekaribia kisu moyoni mwako, (wana-Mgambo wa kufilisika kutokana kwani naamini katika Kristo), mwingiliaji n a k u f i c h u l i w a wito, Naamini katika w a t o t o a m b a y e k w a m a t e n d o y a k u i t i k i a k u f a n y a vitendo vyake Kanisa mwanzilishi wake, k a z i ya M u n g u . lilivipuuzia kwa Namwamini Yesu. miongo kadhaa - na Inaendelea Uk. 11

10
Na Said Mihiko KUIBUKA na kuanguka kwa mataifa, mara zote kumefuata mpangilio wa kanuni na taratibu, ambazo zimefafanuliwa vyema ndani ya Qur'an kwa njia mbalimbali. Hakuna sababu ya kuamini kwamba kanuni hizi zitabadilika katika karne ya 21, eti kwa sababu tu kuna mataifa yameweza kuunda vyombo vya kwenda angani na makombora ya 'cruise'! Utambuzi wa kweli wa hali ya Umma wa Wa i s l a m u , u n a w e z a kutoka ndani ya Qur'an tu, kwa sababu vigezo vingine vyote, ama ni nusu ukweli au mawazo matupu, ambayo hayana uhusiano wowote na uhalisia. Kigezo kimoja muhimu cha Qur'an, katika kufahamu hali ya jamii, ni kuchunguza hali ya watu binafsi, wanawake n a wa n a u m e , a m b a o ndiyo wanaounda jamii. Msisitizo huu wa mtu mmoja mmoja, pia ndiyo njia ya Qur'an ya kujenga jamii zenye haki. Kwa hiyo, ili kuleta mabadiliko yoyote katika j a m i i z a Wa i s l a m u , mabadiliko lazima yatokee katika hali za kimaadili, kiroho na kimali (material) za mtu mmoja mmoja, ambao ndiyo wanaounda jamii hizo. Kwa hiyo, inapodaiwa kuwa ulimwengu wa Waislamu uko katika hali mbaya, maana yake ni kwamba hali za wanaume na wanawake, wa n a o j i i t a Wa i s l a m u ndiyo mbaya. Na hili ni matokeo ya moja kwa moja ya Waislamu kutupa vyanzo vyao viwili vya Uislamu, ambavyo ndivyo vinavyowapa mfumo wao wa maisha. Mfumo ambao u n a wa we z e s h a k u wa Makhalifa wa Mwenyezi Mungu hapa duniani. Kimsingi, Muislamu wa kweli hawezi kuwa katika hali mbaya kama ilivyo sasa. Ni ukweli uliothibitika wazi kihistoria kwamba, wakati Waislamu walipoufuata Uislamu kwa ukweli, waliweza kuunda jamii bora zenye ustawi na waliweza kutawala dunia. Kwa hiyo, kuuacha Uislamu, ndiyo sababu ya Waislamu kuwa katika hali mbaya duniani leo! B a a d a ya k u u t u p a Uislamu kama mfumo kamili wa maisha,

Maradhi ya umma-2

Makala

JAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA MACHI 7-13, 2014

AN-NUUR

MWANAMKE wa Kiislamu (kulia) akitoa da'awah kwa asiyekuwa Muislamu. mfumo wa Kimagharibi ukapandikizwa kwenye jamii za Waislamu kama mbadala. Kuhama huku, kutoka kwenye mfumo wa Kiislamu na kuingia k we n ye U m a g h a r i b i , kumeleta madhara makubwa kwa Waislamu. Kumesababisha maadili ya Waislamu yabadilike na hata vigezo vya kuyaangalia mambo. Hali hii imetia ukungu maono ya wazi yaliyoletwa na Uislamu, katika kiwango ambacho mapambo bandia ya Kimagharibi, yamewachanganya kabisa Wa i s l a m u ! Wa n a t a k a kuiga kila kitu - mtindo wa maisha, maadili, fikra na mifumo mbalimbali ya Kimagharibi. Wanalazimisha mfumo huu wa maisha kwa jamii zao. Waislamu wengi zaidi wakifuata mfumo huo, basi maradhi ndiyo yanazidi kusambaa kwenye jamii nzima ya Waislamu. Changamoto kubwa inayowakabili wasomi Waislamu duniani leo, ni kutafuta njia za kukabili wimbi zito linalotaka kuzibadili jamii zao na kuwa za Kimagharibi. Wanahitaji kubainisha mapungufu ya mfumo wa Kimagharibi na kuonyesha, vipi maisha yanayozingatia misingi ya Kiislamu, ndiyo suluhisho pekee la matatizo yote ya n a y o z i k a b i l i j a m i i za Waislamu duniani. Baada ya kuelewa hilo, sasa mkazo unakuwa kwa Muislamu mmoja mmoja, katika mchakato wa kuijenga upya jamii ya Waislamu. Lazima tutambue vishawishi ambavyo vinajenga na kuunda maisha ya mtu mmoja mmoja kwenye jamii. Kwa maneno mengine, tunahitaji kuelewa kitu gani hasa k i n a m f a n ya m t u a we Muislamu madhubuti. Vishawishi muhimu zaidi vinavyojenga maisha ya mtoto vinatoka 'nyumbani' na shule. Miaka ya awali ya elimu, siyo tu inazalisha stadi za mtoto, bali pia inajenga mtazamo wake kuhusu ulimwengu na tabia zake za kudumu. Hiyo ndiyo sababu Qur'an huwa Kitabu cha mwanzo kabisa kusomwa na kila mtoto kwenye ulimwengu wa Waislamu. Hisia za mwanzo za Qur'an ndizo zilizokuwa zikifinyanga maisha ya Waislamu. Watoto pia walikuwa wakijifunza taaluma na stadi nyingine za msingi kimaisha kupitia falsafa ya Qur'an. Katika zama za sasa, idadi kubwa ya Waislamu hawaifahamu vizuri Qur'an. Wanashindwa kutambua kwamba kusoma Qur'an siyo tu ni ibada ya kupata thawabu, bali pia ni njia inayoweza kubadili maisha yote ya Muislamu anayesoma Aya hizo za Kitabu cha Mwenyezi Mungu. Ni mchakato hai wa ndani, ambao unambadilisha na kumjenga Muislamu, j i n s i ya k u ya a n g a l i a mambo yote yaliyopo na yanayotokea duniani. Muingiliano huu na Kitabu cha Mwenyezi Mungu pia ulikuwa ni mchakato wa kujifunza wa maisha yote ya Muislamu. Ilikuwa ni Kitabu hiki ndicho kilichozalisha uongozi madhubuti katika jamii za Waislamu - uongozi ambao, awali uliweza kufahamu matatizo makubwa ya ulimwengu huu na kuyapatia ufumbuzi, ikiwa ni pamoja na kugundua njia sahihi ya kuelekea ulimwengu ujao. Hali haiko hivyo tena leo. Mtazamo kuhusu dunia walionao Waislamu wengi haukujengwa juu ya msingi wa Qur'an, bali umejengwa na elimu za kisekula, huku Uislamu ukifundishwa kwa kudonoa, tena katika mtindo wa nusu nusu. Huu ndiyo mzizi wa majanga yote yanayowakumba Waislamu duniani leo. Wakoloni waliowatawala Waislamu walifahamu vyema kwamba ili kuudhoofisha ulimwengu wa Waislamu, lazima wakate kabisa mizizi ya Mfumo wa Elimu wa Waislamu. Walihujumu vipawa na karama za Wa i s l a m u . Wa l i p o r a mali na kuvuruga taasisi za Elimu za Waislamu, ambazo ndizo zilizokuwa zikizalisha Wasomi wa Kiislamu, sina maana ya Wasomi

Waislamu, na badala yake wakapandikiza mifumo na taasisi zao za kielimu. Baada ya muda, mifumo hii mipya ya elimu kutoka ulimwengu wa Magharibi, ikabadili mfumo mzima wa elimu katika ulimwengu wa Waislamu, na kuzalisha aina mpya ya Wasomi, ambao wameng'olewa kutoka kwenye shamba lao la kiitikadi na kitaaluma. Matokeo yake, Waislamu wengi leo duniani, wana ufahamu mdogo sana kuhusu dini yao na mila yake ya kisomi. Leo hii, mafundisho ya Uislamu na utamaduni wa k e m a d h u b u t i wa kitaaluma, vimepuuzwa k a b i s a n a Wa i s l a m u walio wengi. Elimu ya Kisekula inazalisha Waislamu Masekula tu, isipokuwa wachache mno, wale wenye ufahamu wa kutosha kuhusu dini yao. Waislamu wenye mtazamo wa Kisekula, ni wale wanaouweka Uislamu upande mmoja, na dunia upande mwingine. Kwao wao, Uislamu ni kwa ajili ya Akhirah tu, ingawa hawasemi hivyo wazi. Unapozungumzia masuala ya Uislamu kutawala na kuendesha mambo, wanaona haiwezekani. Elimu walizopitia zimewaandaa hivyo. Ndugu zangu katika imani, maradhi hayo yameutafuna sana umma wa Kiislamu, kiasi kwamba si rahisi siku hizi, kukuta "Waislamu Walioelimika" wanajua chochote kuhusu kazi za wanazuoni wakubwa kama Fakhr al - Din al - Razi, Abu Hamid al - Ghazali, Ibn Qayyim al - Jawziah, Abul ala Maududi, Sayyid Qutb, Ibn Khaldun na mamia ya wanazuoni wengine wa Kiislamu. Waislamu wengi "Wasomi" wanaziona kazi za kitaaluma za wanazuoni hawa kuwa hazifai, z i m e p i t wa n a wa k a t i na zinastahili kutupwa jalalani. Na mbaya zaidi, wamezitupa kazi hizo, bila ya kufungua hata kurasa moja na kuona ubaya wake, kama adabu za kisomi zinavyotaka. Wanataaluma hawa bobezi wa Kiislamu, wameacha hazina kubwa ya utaalamu, ambayo imeangalia na kuchambua masuala m u h i m u ya n a y o g u s a maisha ya kila siku ya Waislamu. Wasomi wetu Waislamu katika zama hizi hawajui hilo. Rejea kuu Inaendelea Uk. 12

11

Makala

JAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA MACHI 7-13, 2014

AN-NUUR

Filamu Siri za Vatican' yafunua mikwamo ya kimaadili inayomkabili Papa mpya


Inatoka Uk. 9

wa n a - M g a m b o walimlaani Maciel mwezi Februari na kuwaomba radhi waliowaumiza, licha ya kuwa kundi hilo lilimchagua mmoja wa wasaidizi wake wa karibu kuwa kiongozi wao. S i r i z a Va t i c a n " i n a m h o j i m m o j a wa wanae Maciel, ambaye anaelezea ubaya aliokuwa akifanyiwa na baba yake. Thomas alisema kubainisha katika filamu kwa aina ya unyanyasaji wa kingono ulikuwa lazima - kwa sababu bado ni jambo linaloleta wasiwasi mkubwa na kwa sababu ya umuhimu

Uhuru uwe ndio uti wa mgongo wa Katiba yetu


Inatoka Uk. 7 (s.a.w.), alichaguliwa na maswahaba kwa kura ya wazi ni madai yasiyooana na kadhia hii. Tofauti baina ya kadhia mbili hizi ni kubwa kama tofauti ya mbingu na ardhi, kwa hoja zifuatazo: Sayyidna Abubakar S i d d i q ; K h a l i f a wa kwanza katika Dola ya Kiislamu, hakutawazwa kushika uongozi baada ya Bwana Mtume (s.a.w.) na kura za umma. Abubakar Siddiq aliungwa mkono na Maswahaba kushika hatamu za uongozi baada ya Bwana Mtume (s.a.w.) kuashiria kwa ishara nyingi kwamba, yeye Abubakar ndiye anayestahiki kuuongoza u m m a b a a d a ya k e , na wala hakuwa na mpinzani. Hayo yanajitokeza hata katika hotuba yake ya kwanza yeye mwenyewe baada ya kushika madaraka. Siddiq Abubakar aliwahutubia watu na akasema: ...kwa hakika, mimi nimetawalishwa juu yenu wala mimi si mbora kuliko nyinyi.... Hakusema kwamba watu hao hao n d i o wa l i o m u we k a madarakani kupitia kura zao. Watu hao wa wakati huo ni tofauti na sisi wa wa k a t i wa l e o . Wa l e w a l i k u w a n i Maswahaba, hawajui rushwa wala takrima na kila mmoja alikuwa na uwezo wa kujiwakilisha m w e n y e w e b i l a ya kuhitaji kampeni wala propaganda, si vibaraka wa l a m a d h a i f u wa kuburuzwa na maoni ya watu wengine. Allah (swt) awape hidaya wawakilishi wetu kutengeneza Katiba ya nchi yetu, Katiba

wake inawezekana bado haujazingatiwa kiasi cha kutosha katika hisia za watu. Ni kwa kiasi gani ni vibaya zaidi kufanyiwa vitendo viovu na Mchungaji wako - na jinsi waingiliaji watoto wanavyowafanya watoto wajisikie hatiani pale wanapoambiwa ni wewe utakayekwenda motoni kama utasema lolote juu ya jambo hili' (kwa maana kuwa walitishwa n a Wa c h u n g a j i walio wanajisi kuwa watakwenda Jahanamu iwapo watasema kuwa wamefanyiwa mchezo huo mbaya). Unachukua mawazo ya ndani kabisa ya mtoto na

kuyakanyagakanyaga." Na bado, Thomas alisema, licha ya k u wa h o j i m a k u n d i kadhaa ya watu katika utengenezaji wa filamu hiyo uliochukua karibu mwaka mmoja, aligundua kitu kilichokuwa karibu ya mwujiza. Ni mtu mmoja t u a l i ye s e m a k u wa makosa makubwa ya Kanisa katika kipindi cha muongo mmoja kinapunguza imani. Watu wote ambao ni wakinzani wakubwa wa kile kinachotokea, wote ni waumini wakubwa wa Ukatoliki, na nadhani hiyo ni adhimu sana," Thomas alisema. Zaidi, licha ya kuwa Papa

Francis bado hajaangalia kwa karibu masuala magumu kama utoaji mimba na uzuiaji mimba, ameinua mioyo na matumaini ya makundi makubwa ya Wakatoliki waliokuwa wamekata tamaa. Ameelezea msimamo bayana kuhusu kuongezeka k wa p e n g o k a t i ya watu tajiri na maskini duniani. Mtazamo ambao anaendana na Rais Barack Obama wa Marekani, ambaye anapanga kutembelea Makao Makuu ya Papa hapo Machi 27.

Kama Francis ataweza kufunga mafundo yaliyoachwa yananing'inia ya Benedict kwa kuifanyia mageuzi Benki ya Vatican na Curia (Sekretarieti) ambayo inasimamia mfumo wake wa u ta wa l a , ni ha d i thi ambayo hitimisho lake bado. Lakini Papa mpya kwa hali yoyote ile anakabiliana na hali hii. Thomas alisema. Ni mchangamfu, mshiriki kwa hisia na wa kawaida. Tayari amefanikiwa kufanya mengi na hajakaa madarakani kwa mwaka mmoja bado."

itakayokidhi mahitaji na matakwa ya makundi jamii yote yanayounda hiki kinachoitwa leo Jamhuri ya Muungano ya Tanzania. Wabillah taufiq Sheikh Abdallah Ahmad Bawazir 0767 215 898

MWENYEKITI wa muda Bunge Maalum la Katiba, Pandu Ameir Kificho, akitoka bungeni baada ya kuahirisha kikao cha Bunge hilo hivi karibuni.

12

Mashairi/Makala

JAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA MACHI 7-13, 2014

AN-NUUR

Bunge la Katiba (CHONDECHONDE WAJUMBE!)


Leo inanilazimu, kutoa yangu indhari, Kwa wa Bunge Maalumu, wajumbe watafakari, Kuhusu jambo adhimu, la 'Amiri' kukhitari, Mkichagua fisadi, Bunge atalifisidi ! Chondechonde kwa nidhamu, nakupeni tahadhari, Katu msijidhulumu, kwa fisadi kukhitari, Kadhalika na kaumu, kwa hilo kuihatiri, Mkichagua fisadi, Bunge atalifisidi ! Fisadi tangu kadimu, yake i mui dhamiri, kwa wenza binaadamu, kadhalika kwa Qahari, Toka zama za Adamu, mpaka za Mukhtari, Mkichagua fisadi, Bunge atalifisidi ! Fisadi kutakadamu, mbele jambo la hatari, Tajiriba na elimu, visije vikawaghuri, Mkamfanya 'Imamu', wa ya rasimu safari, Mkichagua fisadi, Bunge atalifisidi ! Yu awe na darahimu, kadhalika itibari, Si mtu wa kuadhimu, wa kutosa aisari, Msifanye urahimu, kurani mumdamiri, Mkichagua fisadi, Bunge atalifisidi ! Kwa hili nyote mkimu, kikoa muwe ngangari, Mjenge mastakimu, na Bunge lenye urari, Si lile la kukasimu, watu kwa zao nadhari, Mkichagua fisadi, Bunge atalifisidi ! Msijuzishe dhalimu, Bunge lenu kuamiri, Si chombo cha kidhalimu, fisidifu cha fujuri, Falau cha kidhalimu, hewala! Mumkhitari !, Mkichagua fisadi Bunge atalifisidi ! Kwa wa kwangu ufahamu, thakili kwa abrari, Kumchagua dhalimu, fisadi au fujari, Katu silo jambo gumu, sahali kwa mafujari, Mkichagua fisadi, Bunge atalifisidi ! Kushika huyu hatamu, ni kuridhia ghururi, Kwalo Bunge Maalumu, rasimu linohawiri, Msichague dhalimu, chondechonde, nakariri, Mkichagua fisadi, Bunge atalifisidi ! Risala tama tamamu, kwa wajumbe ya indhari, Walo Bunge Maalumu, ya 'Amiri' kukhitari, Si wa muda wa kudumu, wa Bunge hadi akhiri, Kaditamati indhari, naweka chini kalamu. ABUU NYAMKOMOGI MWANZA.

Maradhi ya umma-2
wanazotegemea kuhusu ulimwengu na mambo yake, ni wanazuoni na wachambuzi wa Kimagharibi. Hawa ndiyo "Wasomi" wetu Waislamu. Lakini wale ambao hawakupitia taasisi za kisekula za elimu, nao wanaugua maradhi mengine sugu. Wanasoma elimu za madrasa a m b a z o m a u d h u i ya kidini (religious content) ya mitaala wanayopitia, inaishia kwenye vitabu vichache tu, na shehena k u b wa ya k i t a a l u m a inayozungumzia ulimwengu wa kisasa haiguswi kabisa. Masomo kama Sayansi ya Tiba, H i s a b a t i , S a ya n s i z a Kijamii (Social Sciences) na Sayansi Asilia (Natural Sciences), hayafundishwi kabisa katika shule hizi za "mafunzo ya kidini". Kwa hiyo shule hizi hazina u we z o wa k u z a l i s h a Wa i s l a m u a m b a o wa n a we z a k u k a m a t a nafasi za uongozi katika jamii. Kwa hiyo jukumu zito la uongozi na utawala katika jamii, linaachwa mikononi mwa Waislamu waliopitia taasisi za kisekula za elimu, ambazo zimejengwa kwa miundo na falsafa za Kimagharibi, zinazopinga vikali Uislamu. Hali hii imeweka ufa mkubwa katika jamii n y i n g i z a Wa i s l a m u d u n i a n i , Ta n z a n i a i k i w e m o . Wa i s l a m u wengi wanapewa elimu ya kisekula na wachache wanapata elimu ya "kidini". Makundi haya mawili mara kwa mara yanakuwa katika msuguano na kusababisha hali tete katika jamii, kutokana na tofauti zao kimtazamo kuhusu ulimwengu. Bila shaka, kuna Waislamu ambao kupitia jitihada zao wenyewe, wa m e we z a k u j i p a t i a elimu kutoka pande zote mbili za ulimwengu, lakini hawa ni wachache mno. Ili kuweka msingi wa harakati endelevu za kusimamisha Uislamu, mabadiliko makubwa yanahitajika katika jamii za Waislamu, tena kwenye ngazi zote, hususan sekta ya elimu. Wakati Waislamu wengi wanafahamu hitajio hilo,

Inatoka Uk. 10

Nimeishika kalamu,mkono wa kuumeni Niandike ya kaumu,yanayojiri nchini Yahitajika nidhamu,uadilifu moyoni Japo vuta nikuvute,hatutafuti mshindi Yupo atakae moja, siyo kwamba majinuni Anazo zakwake hoja,bora nafasi mpeni Mawazoye kuyachuja,hilo ni jambo auni Japo vuta nikuvute,hatutafuti mshindi Anayezitaka mbili,pia msikilizeni Mzitulize akili,mjadili kwa makini Huru mkalijadili,pasi vitisho sirini Japo vuta nikuvute,hatutafuti mshindi Wanao zitaka tatu,siyo kwamba jambo geni Wamevivaa viatu,vilivyo achwa zamani Wame ukabili mwitu,sasa mambo hadharani Japo vuta nikuvute,hatutafuti mshindi Kweli vuta nikuvute,basi kwa haki vuteni Masilahi muyalete,ni yataifa mbeleni Makundi msiyatute,kuyaingiza bungeni Japo vuta nikuvute,hatutafuti mshindi Hatutafuti mshindi,limeshinda kundi gani Japo nimejitahidi,utamuwe si uoni Nimefika kwenye tindi,kalamu naweka chini Japo vuta nikuvute,hatutafuti mshindi Isihaka Hemed Mzuzuri(Sauti ya Mkutubi) MUM-Morogoro

VUTA NIKUVUTE

kuna taasisi chache mno zilizodhamiria kwa dhati kuendeleza rasilimali mpya za kielimu, ambazo zimejengwa juu ya mtazamo wa Qur'an kuhusu ulimwengu (Qur'anic Worldview). Yaani taasisi za kielimu za Kiislamu ambazo zina uwezo wa kujenga stadi, kulea vipaji, na kutoa mafunzo muhimu yanayohitajika, ili kuuelewa ulimwengu wa kisasa. Ukosefu wa mtaala kama huo, utawafanya watoto wetu waendelee kutumikia taasisi za kisekula, hatua ambayo inazifanya jamii za Waislamu duniani ziendelee kuwa mbali na mtazamo wa Qur'an kuhusu ulimwengu. Ndugu zangu katika imani, hali hiyo ndiyo inayotufanya Waislamu t u we wa n y o n g e k wa ulimwengu wa Magharibi kila siku, kwa sababu hicho ndicho mfumo wa elimu unachopanda kwenye vichwa vya watoto wetu. Bila shaka kuleta mabadiliko ni mchakato utakaochukua muda mrefu sana, na wala hakuna njia ya mkato katika kutibu maradhi haya mazito ya umma wa Kiislamu. Ukiangalia kuibuka na kuporomoka kwa mataifa mbalimbali kupitia macho ya Qur'an, pengine njia ya haraka zaidi kuanza mchakato

h u u wa m a g e u z i n i kujenga rasilimali mpya za kielimu, na taasisi za mafunzo kufundisha mtaala huu mpya. Njia hii itatuletea Waislamu wenye kuyaona mambo K i i s l a m u . Wa i s l a m u waliozama kwenye maono ya Kiislamu, wenye uwezo wa kutafakari, kuchambua na kukabiliana na changamoto zinazowakabili Waislamu duniani leo. Baadhi ya wachambuzi waliozama zaidi kwenye elimu ya kisekula, wanadhani Marekani kupitia shirika lake la k i j a s u s i ( C I A) , i n a mipango mizito sana ya kuwamaliza Waislamu, b i l a y a Wa i s l a m u we n ye we k u t a m b u a . Lakini wachambuzi waliozama zaidi kwenye Qur'an, wanaziona mbinu hizo ni dhaifu tu, kama alivyobainisha Mwenyezi Mungu mwenyewe, ndani ya kitabu chake: " Wa l e w a l i o a m i n i wanapigana katika njia ya Mwenyezi Mungu, lakini waliokufuru wanapigana katika njia ya Shetani. Basi piganeni na marafiki wa Shetani. Hakika hila za Shetani ni dhaifu" Qur(4:76) Tuupe nafasi umma wetu kuwajua mashujaa wake, jinsi walivyoishi hapa duniani na pia jinsi walivyorejea kwa Mola wao.

DVD

DVD

DVD

DVD, inayozungumzia umuhimu wa Elimu ya kumjua ALLAH (SWT), sasa zinapatikana. Mwasilishaji wa mada hiyo ni Sheikh Fahad Ibrahim kutoka Shule ya Alfurqaan, Buguruni-Malapa. Kwa mahitaji na mawasiliano zaidi piga Simu No:- 0773 032 328, 0712 232 328, 0768 816 040.

Umoja wa Mataifa waijia juu Vatican


Updated Thu 6 Feb 2014, 1:00pm AEDT UMOJA wa Mataifa umeitaka Vatican kuwaondoa mara moja makasisi wote ambao wanafahamika au wanatuhumiwa kufanya m a p e n z i n a wa t o t o n a kuwakabidhi kwa mamlaka. Katika ripoti hiyo maalum, Kamati ya Haki za Watoto ilisema maofisa wa Kanisa Katoliki waliweka kanuni ya kunyamazia vitendo hivyo vya makasisi kuwalinda katika kuwaripoti polisi kwa vitendo hivyo, huku watuhumiwa wakihamishwa kutoka kigango kimoja k we n d a k i n g i n e k a t i k a jitihada za kuficha makosa yao. Ilielezwa kuwa Holy See lazime iwakabidhi mafanikio yake juu ya wakosaji wanaohusishwa na vitendo ngono kwa maelfu ya watoto pamoja na wale waliofichwa dhidi ya makosa hayo na kwamba hatua hiyo itasaidia uwajibikaji. Vatican walijibu mara moja juu ya madai hayo wakisema Kanisa linawajibika kutunza na kulinda haki za watoto na kuahidi kuipatia UN ripoti. Hata hivyo, Kanisa liliongeza katika majibu yake kuwa UN inaingilia mafundisho ya maadili ya Kanisa kwasababu ripoti yake inakosoa hata nafasi ya Kanisa katika masuala ya mapenzi ya jinsia moja na utoaji mimba. Uchunguzi huo maalum wa UN dhidi ya utawala wa Kanisa Katoliki umekuja kufuatia jamii kuwatuhumu maofisa wa Vatican mwezi uliopita. Kamati ilitilia mkazo zaidi kwamba The Holy See haikutaka kutambua na kuweka wazi makosa yaliyofanywa, wala haikuchukua hatua muhimu kukataza vitendo vya ubakaji kwa watoto na wakati huo huo ikafuata sera zilizosaidia wakosaji kuendeleza zaidi ubakaji watoto., ripoti hiyo imeeleza. Kwa msingi huo Vatican ilitakiwa kuwaondoa mara moja wale wote wanaofahamika au kushutumiwa kujihusisha na ubakaji watoto katika majukumu na kupeleka suala hilo mbele ya mamlaka za kisheria kwa ajili ya uchunguzi na zile za kutoa adhabu. Katika mkutano na waandishi wa habari kufuatia kutolewa ripoti hiyo, mjumbe wa kamati hiyo Kirsten Sandberg, alisema kimfumo Vatican iliweka heshima yake katika kuwalinda watoto. Hadi sasa wanakiuka mkataba kuhusu haki za mtoto kwasababu hawakutekeleza mambo yote waliyopaswa kutekeleza, aliwaeleza waandishi wa habari. Rais wa shirika la Survivors Network of Those Abused by Priests, lenye makao yake nchini Marekani, Barbara Blaine, alisema amesikitishwa sana na yaliyomo katika ripoti hiyo ya UN. Hiki ndicho kile ambacho sisi waathirika tumekuwa tukikieleza kwa miongo kadhaa alisema. Wajanja walionusurika nchini Australia, ambao walizungumza, hii inaonyesha kile walichokuwa wakikizungumza na wanaithibitishia Tume huru yale yanayofanyika. Tumekuwa tukijaribu kwa kila njia tuliyoweza kuwafikia maofisa wa Kanisa n a k u wa o m b a k u f a n ya mambo sahihi na kile tulichojifunza wakati wa kufanya kazi hiyo ni kwamba walichukua hatua rahisi sana, tena kwasababu ya kusakamwa na changamoto za nje. Mwito wa UN kufichuliwa vitendo hivyo vya maofisa wa Kanisa dhidi ya watoto, ulisaidiwa na Mkuu wa Baraza la Catholic Churchs Truth Justice and Healing Council nchini Australia, Francis Sullivan. C h a n g a m o t o k u b wa kwa Vatican sio kujilinda, lakini ni kujipambanua na kudhihirisha kile wanachokwenda kukifanya ili kurejesha imani, si kwa jamii ya kikatoliki pekee, lakini kwa jamii yote kwa ujumla, alisema. Katika taarifa yake, Vatican ilisema: The Holy See imechukua wazo la kuhitimisha uchambuzi wa ripoti zake, ambazo zitawasilishwa kwa ajili ya kuchunguzwa n a k u t a t h m i n i wa z a i d i kwa mujibu wa sheria ya kimataifa. Au s t r a l i a : M a p a d r i , Wasaidi, wameshitakiwa kwa makosa zaidi ya 100 ya ngono dhidi ya watoto kuanzia miaka ya 1970s katika shule ya St. Stanislaus school, Bathurst. Shirika la Royal inaweza kuruhusiwa . Pia ripoti hiyo ililitaka Kanisa kutumia barabara mamlaka zake za kimaadili kulaani manyanyaso ya aina zote, ubaguzi au utumiaji nguvu dhidi ya watoto kwa k u t i z a m wa k i m a p e n z i , ikiwa ni jitihada za kusaidia kuachana na mapenzi ya jinsia moja kimataifa. Vatican ilisema inasikitika kuona baadhi ya nukta za kuhitimisha uchunguzi katika ripoti hiyo zimelenga kuingilia mafundisho ya K a n i s a K a t o l i k i j u u ya heshma ya mtu na kutekeleza uhuru wa kidini . Iliongeza kuwa ripoti hiyo inarudia majukumu ya Kanisa ya kulinda na kutetea haki za mtoto kwa mujibu wa maadili desturi za dini zinazotolewa na kanuni za Katoliki. UN ilisema Kanisa Katoliki bado halijachukua hatua kuzuia kurudiarudia kesi za kashfa kama zile za Irelands Magdalene laundries, ambako mabinti walilazimishwa kufanya kazi zozote zile katika mazingira ya kufanyishwa kazi kwa nguvu. Ripoti ilitaka kufanyika uchunguzi wa ndani katika maeneo hayo na katika asasi zinazofanana na hapo, ili yule ambaye amehusika na jinai hiyo achukuliwe na fidia kamili kulipwa kwa waathirika na familia zao. Pia ilisema Mapadri waliokuwa wakiwalea watoto lazima wawajibishwe i l i k u wa f a n ya wa w e z e kuwatunza vyema watoto. Tume iliyoundwa na Papa Francis mwezi Desemba lazima ichunguze kesi zote za kubakwa watoto pamoja na utendaji wa utawala wa Katoliki katika kuwatunza watoto hao, ilieleza ripoti hiyo. Tu n a t a r a j i a H o l y See (na Papa) kuzingatia mapendekezo hayakulinda waathirika na kuwalipa fidia, alisema Ms Sandberg mjini Geneva. Katika mkutano wa hadhara mwezi uliopita, kamati ya UN iliutaka ujumbe wa Va t i c a n k u b a i n i s h a ukubwa wa tatizo la miongo mingi la ubakaji watoto kunakofanywa na Mapadri wa Kanisa Katoliki, kitendo ambacho Papa Francis hukiita Aibu ya Kanisa . Ujumbe wa Holy See wakati ukijibu swali kutoka Jukwaa la Kimataifa la Haki kwa mara ya kwanza tangu kufichuka kwa kashfa hizi zaidi ya miongo miwili iliyopita, ulikataa madai ya Vatican kuficha jinai hizo na kusema ilishaweka wazi miongozo kulinda watoto dhidi ya Mapadri wabakaji.

13

Makala

JAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA MACHI 7-13, 2014

AN-NUUR

Papa Francis Commission into Institutional Responses to Child Sexual Abuse, lilizinduliwa April 2013. Linatarajiwa kuhoji waathirika wa vitendo hivyo vya ngono kuanzia 5,000. Canada: Kituo cha Mount Cashel Orphanage, Newfoundland, kilifungwa mwaka 1990 baada ya wafanyakazi wake kuwafanyia ngono watoto kwa miongo kadhaa. Mwaka 2002, muungano wa waliojitangaza kuwa ni waathirika zaidi ya 10,000 wa vitendo vya ngono, waliunganisha nguvu kudai malipo ya fidia. Nchini Marekani: U c h u n g u z i wa m a k o s a ya jinai wa mwaka 2004 uliwanasa Mapadri 4,400 na makosa ya kufanya ngono na watoto kati ya mwaka 1950 na 2002; ubakaji huo uliathiri watoto wapatao 11,000. Askofu Mkuu wa zamani wa Boston Bernard Law alilazimishwa kujiuzulu mwaka 2002 kwa kuwalinda Makasisi wabakaji. Askofu Mkuu wa zamani wa Los Angeles, Roger Mahony, alikubali kulipa dola za kimarekani milioni 660 kwa waathirika 500wa vitendo vya ngono. Nchini Ireland: Padri mmoja alikiri kubaka zaidi ya watoto 100, mwingine alisema mara kadha alikuwa akifanya ngono na watoto k wa z i d i ya m i a k a 2 5 . Jumla ya watoto wa Irish 14,500 wameripotiwa kuwa waathirika wa vitendo vya ngono walivyofanyiwa na Makasisi. Nchini Ujerumani: Mapema mwaka 2010, mamia ya kesi za kubakwa watoto katika taasisi za makanisa zilijitokeza. Katika chuo cha Jesuit college Canisius jijini Berlin kiasi cha kesi 20 kiliripotiwa. Mwishoni mwa mwaka 2012, ripoti ilisema kwa uchache maofisa 66 wa Kanisa walituhumiwa kujihusisha na vitendo vya ngono dhidi ya watoto. Nchini Uholanzi: Mwishoni mwa mwaka 2011, ripoti ilisema,maelfu ya watoto walibakwa ndani ya taasisi za Kanisa kati ya mwaka 1945 na 2010, na kiasi cha washukiwa wapatao 800 walitambuliwa. L a k i n i Va t i c a n p i a lilikasirishwa na kile ilichokiita kuingiliwa m a f u n d i s h o ya K a n i s a baada ya UN kuitaka Vatican irekebishe misimamo yake. Askofu Mkuu Silvano Tomasi, Mkuu wa Ujumbe wa Holy See kwenye Umoja wa Mataifa mjini Geneva, alitetea rekodi ya kanisa ya kupambana na ubakaji watoto. Nafikiri ni vigumu sana kupata taasisi nyingine au hata dola ambayo imefanya vya kutosha hasusan katika kuwalinda watoto, alisema. Ripoti iliitaka Vatican kutizama upya nafasi yake juu ya utoaji mimba ambao ni wazi kwamba ni jambo la hatari katika maisha na afya za wasichana na kutoa mwito wa kulegea kidogo katika kutambua hali ambayo uwezekano wa kuwepo huduma ya kutoa mimba

14

TANGAZO

JAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA MACHI 7-13, 2014

AN-NUUR

NAFASI ZA KIDATO CHA TANO JULAI, 2014


Waislamu kote nchini mnatangaziwa nafasi za kidato cha tano kwa shule zifuatazo: KIRINJIKO ISLAMIC SECONDARY SCHOOL NYASAKA ISLAMIC SECONDARY SCHOOL UBUNGO ISLAMIC HIGH SCHOOL SAME KILIMANJARO MWANZA DAR ES SALAAM

ISLAMIC PROPAGATION CENTRE

1. Shule hizi ni za Kiislamu zenye lengo la kuwapa wanafunzi taaluma ya hali ya juu na malezi bora ya Kiislamu. 2. Shule hizi ni za bweni za mchanganyiko wa wavulana na wasichana . 3. ZipoCombinationszaSAYANSI, ARTSnaBIASHARA.Piawanafunzi wote wanafundishwa Islamic Knowledge,Introduction to Arabic na Compyuta. 4. Muombaji awe na Crediti tatu na Pass mbili au zaidi katika mtihani wa kidato cha nne. 5. Fomu za Maombi zinapatikana kwa gharama ya shilingi 10,000/= katika vituo vilivyoorodheshwa hapa chini.
Arusha - - - Ofisi ya Islamic Education Panel Jambo Plastic Ghorofa ya 2 mkabala na msikiti Mkuu Bondeni - 0763 282 371/ 0784 406 610 Moshi: Msikiti wa Riadha 0654 723 418 Same: Kirinjiko Islamic Secondry School: 0784 296424/0655 697 075 Uongofu Bookshop: - 0784 982525/ Mandia Shop - Lushoto: 0782257533 Nyasaka Islamic Secondary School 0717 417685/0786 417685 Ofisi ya Islamic Education Panel - Mwanza - Mtaa wa Rufiji mkabala na Msikiti Al-Amin 0785 086 770 Duka la Kansolele -Stendi ya zamani sokoni - 0714587193 Bukoba: Alhuda Caf Kwa mzee Kinobe karibu na ofisi za TRA. - 0688 479 667 Msiikiti wa Majengo-0718866869 Kahama ofisi ya AN NUUR Karibu na msikiti wa Ibadhi: 0753 993930 Ubungo Islamic High School 0754 260 241/0712033556 Ofisi ya Islamic Ed. Panel Temeke -Msikiti wa Nurul Yakin 0655144474 Wasiliana na Ramadhani Chale :0715704380 Hijra Islamic Primary School : 0716 544757/0712 325086 Ofisis ya Islamic Ed. Panel karibu Nuru snack Hotel 0714285465 Babati: Shule ya Msingi Hangoni: 0784 667575 Msikiti wa mwanga Kigoma: 0753 355224 Kibondo Islamic Nursery School: 0784 442860 Kasulu: Murubona Isl.SS. 0714710802. Wapemba Store: 0784 974041/0786 959663 Amana Islamic S.S 0786 729 973 Kilimanjaro

Tanga - - Mwanza Musoma Kagera - - - -

Shinyanga - - . Dar es Salaam - - Morogoro Dodoma Singida Manyara - - - -

Kigoma - - - Lindi - -

Mtwara Songea Mbeya

- Kwa Kawanga Karibu na Msikiti wa NURU 0715 681701/0716791113 - Mkuzo Islamic High School. 0716 791113 - Duka la vifaa vya Kiislamu nje ya Msikiti wa Uyole 0713 200209 Rexona Video mkabala na Mbeya RETICO: 0713 200209 Sumbawanga: Masjid TAQWA 0717082 073 Kituo cha Kiislamu Isevya: 0784 944566 Madrastun Najah: 0714 522 122 Wete: Wete Islamic Education Center: 0777 432331

- Rukwa Tabora Iringa Pemba Unguja Mafia - - - -

- Madrasatul Fallah: 0777125074- - Ofisi ya ust. Yusufu Ally jirani na msikiti mkuu 0653705627

6. Pia Fomu zinapatikana kwenye Tovuti: www.ipctz.org. Ikumbukwe kuwa watakaopata fomu kupitia tovuti (download) watatakiwa kuzilipia wakati wa kuzirejesha. USIKOSE NAFASI HII ADHIMU WAHI KUCHUKUA FOMU SASA! Wabillah Tawfiiq MKURUGENZI

Waislamu tuwe makini na vinywaji vyenye alkoholi (alcohol) 0% alc


Inatoka Uk. 16
harufu, ladha, rangi, gesi, n.k. bali kipimo cha kisheria cha kuweza kutoa hukumu kama bidhaa iliyotengenezwa kwa alkoholi (kilevi) ni haramu au ni halali ni viwango vya kilevi vilivyomo kwenye bidhaa hiyo (0.5 % alc). Mathalani, kuna baadhi ya watu (madaiyah) wanatoa Fatwa kwamba ni haramu kutumia vinywaji au vyakula vilivyotengenezwa kwa kutumia nafaka ya Malt, bila ya kuwafahamisha kwamba Malt ni kitu gani. Malt ni nafaka ambayo hutumiwa kufanya bia, whisky, kutengeneza shakes, malt siki, vinywaji vya ladha kama vile Horlicks, Ovaltine na Milo, na baadhi ya bidhaa za kuokwa, kama vile malt ya mkate, bagels na biskuti nk. Na Ladha ya malt ni sawa ya Beer (bia), kwani katika process ya kutengeneza bia miongoni mwa vitu vinavyotumika ni Malt. Hivyo baadhi Madaiyah wanapotoa fatwa juu ya jambo, n i l a z i m a wa we n a hakika (facts) ya kisheria kwa mujibu taarifa za wataalamu wa jambo husika ili kupata ithibati j u u ya j a m b o h i l o . Kigegezi cha harufu au ladha nk. ya Malt kuwa sawa na bia isiweni dalili ya kuweza kuitolea fatwa ya uharamu. Dk. Joseph Wells, D a k t a r i B i n g wa wa Hospitali ya Maryvale, Phoenix, Marekani, pamoja na Dk. Edward Jackobs, bingwa wa magonjwa ya watoto, wa m e o n ya k wa m b a hizo zinazoitwa alkoholi (vilevya) vilivyo na athari ya kusisimua kujenga tabia ya kupenda kunywa zaidi na zaidi kila mara, kuzoea harufu, na ladha ya alkoholi. Kama wataalamu wa afya wana shauri kuwa ni bora kuepuka kabisa vinywaji vyote ambavyo vina ladha au harufu ya alkoholi, kwani mwenye kunywa vinywaji hivi yuko katika mazingira ya hatari zaidi kuingia kwenye unywaji wa alkoholi, yaani kuwa ni Aroto. Ni wajibu kwa kila Muislamu kuhakikisha anajiepusha na vitu vyenye mushkeli na utata ili asije kutumbukia kwenye kunywa na kula vya haramu. Au ajitahidi kutafuta uhakika wa kinywaji au chakula chenyewe kabla ya kukila au kukinywa. kwa mujibu wa kauli ya Mtume wetu (s.a.w) kama ilivopokelewa na Nuuman bin Basheer kwamba Mtume (Saw) amesema: Halali iko wazi na haramu iko wazi, baina yao ni vitu vyenye shaka ambavyo watu wengi hawajui. Kwa hivyo, yule anayeepuka vyenye shaka anajisafisha nafsi yake kwenye dini yake na heshima yake, lakini yule anayetumbukia katika mambo yenye shaka, huanguka katika haramu, kama mchunga anayechunga pembezoni mwa mpaka, mara huingia ndani (ya shamba la mtu). Hakika kila mfalme ana mipaka yake, na mipaka ya Allah (SWT) ni makatazo Yake. Na hakika katika kiwiliwili kuna kipande cha nyama kikitengenea, kiwiliwili chote kitakua kizima, kikiharibika kiwiliwili chote huharibika. Basi jua (kipande hicho cha nyama) ni moyo. (Imesimuliwa na Bukhari na Muslim) Wabilah Tawfiq. (Makala hii imeandikwa na Abu saumu, Kombo Hassani kidumbu. Tanga, Ta n z a n i a . E - m a i l : hassanikombo@yahoo. com Mob: 0714720965)

15

Makala/Tangazo

JAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA MACHI 7-13, 2014

AN-NUUR

NAFASI ZA DIPLOMA YA UALIMU WA KIARABU JULAI,2014


Waislamu kote nchini mnatangaziwa nafasi za Diploma ya Ualimu wa Lugha ya Kiarabu katika chuo cha Ualimu Kirinjikokilichopo Same mkoani Kilimanjaro Lengo la kozi hii ni kuwandaa walimu mahiri wa kufundisha somo la lugha ya Kiarabu katika shule za sekondari na shule za msingi. Muda wa kozi hii ya aina yake ni miaka miwili na itaanza Julai ,2014. Muombaji anatakiwa awe na sifa zifuatazo: (a) Awe amehitimu katika chuo cha mafunzo ya Dini na Kiarabukwa angalau kiwango cha IIdad au zaidi (b) Awe amemaliza kidato cha nne na kupata crediti katika somo la Lugha ya Kiarabu au (c) Awe anayeweza kusoma ,kuandika ,kusikiliza na kuzungumza lugha ya Kiarabu kwa ufasaha hata kama hana sifa (a) na (b). Waombaji wote watafanyiwa usaili tarehe 10-11,Mei 2014 katika chuo cha Ualimu Ubungo Islamic-Dar Es Salaam . Fomu za Maombi zinapatikana kwa gharama ya shilingi ELFU TANO katika vituo vilivyoorodheshwa katika Tangazo la kujiunga na Kidato cha Tano lililopo katika ukurasa wa 14 wa gazeti hili. Pia Fomu zinapatikana kwenye Tovuti: www.ipctz.org. Ikumbukwe kuwa watakaopata fomu kupitia tovuti (download) watatakiwa kuzilipia wakati wa kuzirejesha. USIKOSE NAFASI HII ADHIMU WAHI KUCHUKUA FOMU SASA! Wabillah Tawfiiq MKURUGENZI

ISLAMIC PROPAGATION CENTRE

16

AN-NUUR
MAKALA

JAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA MACHI 7-13, 2014

16

JAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA MACHI 7-13, 2014

Soma AN-NUUR kila Ijumaa

AN-NUUR

Waislamu tuwe makini na vinywaji vyenye alkoholi (alcohol) 0% alc


KILA sifa njema zinamstahiki M we n ye z i M u n g u , swala na amani zimfikiye Mtume Muhammad (Saw) na jamaa zake. Pombe ni kinywaji cha aina yoyote ambacho kinalewesha. Kwa mujibu wa kauli ya Mtume (s.a.w) pale aliposema: Kila kinacholewesha ni Pombe, na kila Pombe ni haramu. (Muslim). Ni haramu kunywa pombe (kilevi) kidogo au kingi kwa mujibu wa kauli ya Allah (Swt). Enyi mlio amini! Bila ya shaka ulevi, na kamari, na kuabudu masanamu, na kupiga ramli, ni uchafu katika kazi ya shetani. Basi jiepusheni navyo, ili mpate kufanikiwa. (Al Maida 5:90) H a k i k a s h e t a n i anataka kutia kati yenu uadui na chuki kwa ulevi na kamari, na akuzuieni k u m k u m b u k a Mwenyezi Mungu na kusali. Basi je, mmeacha? (Al Maida 5:91). Kwa mujibu wa k i t a b u c h a S a ya n s i Darasa la Saba (7), Kitabu cha Mwanafunzi kilichotolewa na Taasisi ya E l i m u Ta n z a n i a Toleo la 1,998 Uk. 18 imeelezwa kwamba: Pombe ni kinywaji ambacho kina Alkoholi (Alcohol), Alkoholi ni aina ya dawa ambayo ina nguvu ya kudhoofisha/ kulegeza mwili na akili kwa muda mfupi. Alkoholi licha ya k wa m b a i n a t u m i k a katika kutengeneza pombe (kilevi), lakini pia inatumika katika kutengeneza bidhaa mbalimbali za viwandani na majumbani. Mathalani hutumika katika k u t e n g e n e z a d a wa za aina mbalimbali, mikate, manukato (perfumes), juisi, bia, whisky n.k. A l k o h o l i inatengenezwa na vitu ambavyo asili yake ni halali kwa mtizamo wa kisheria katika Uislamu. Kwa mfano viazi mbatata (Irish patotoes), ndizi, miwa, malt, ngano, mahindi, tende n.k. Amesema Allah (Swt): Na kutokana na matunda ya mitende na mizabibu mnatengeneza ulevi na riziki nzuri. Hakika katika hayo ipo Ishara kwa wanao tumia akili. (An Nahl 16:67) Kuna dhana inayotolewa baadhi ya walinganizi ( M a d a i y a h ) , k u h a r a m i s h a kinywaji ambacho kimechanganywa na Alkoholi katika utengenezaji wake. Na hivyo kutumia dhana na maneno ya mitaani bila kufanya utafiti (research) ili kuweza kupata hakika (facts) ya kisheria. Viwanda vingi vinavyomilikiwa na Waislamu na wasiokuwa Waislamu, vinazalisha bidhaa ambazo zimetengenezwa na kuachanganywa pamoja na Alkoholi. Ukizungumzia kiwango cha alkoholi kilichomo kwenye kinywaji chochote katika viwango vya kimataifa vilivyotolewa

na Kamati ya Vyakula na Kilimo Ulimwenguni ( FA O C o m m i t e e ) inayoitwa CODEX A L M E N TA R I U S , iliyotaja kwamba kinywaji chochote ambacho kina kiwango cha Alkoholi chini ya asilimia 0.5% kinahesabika kwamba hakina Alkoholi (yaani kimeepukana na kilevi). Kwa mujibu viwango vya kitaalamu, vinywaji vilivyoepukana na kilevi Chini 0.5% alc (Alcohol) vimegawanyika katika makundi matatu nayo: Alcohol free beer/ wine/ lager. De-alcoholized. Non-alcohol. K u n d i l a k wa n z a na pili pamoja na kwamba vinywaji vyake vinahesabika kwamba vimeeepukana na kilevi, yaani alkoholi chini ya 0.5% alc (alcohol). Lakini kimaabara vina alkoholi ambayo ina kiwango kinachopimika (measurable). Kwa mujibu wa mtizamo wa Kiislamu, kila kinacholewesha kidogo au sana kunywa

ni haramu kama tulivyoyoona hapo juu kwa mujibu wa Quran na Hadithi. Kundi la kwanza na pili kwa mujibu wa viwango vya FAO, vinahesabika kwamba havina (kilevi) alkoholi chini ya 0.5% alc (Alcohol), lakini vina kilevi ambacho kinaweza kulewesha, kwa hivyo, ni haramu kwa Muislamu kunywa vinywaji vilivyotengezwa kulingana na makundi hayo mawili kati ya ALCOHOL FREE BEER/ WINE/ LAGER na DEALCOHOLIZED. Kundi la tatu ambalo ni Non-Alcohol ni vinywaji vyote ambavyo vimeepukana kabisa na kilevi (Alkoholi), k wa v i n y wa j i h i v i kwenye utengenezaji wake vimengenywa ( e n z y m e s ) havikurutubishwa. Na mtengenezaji pombe pia hutumia ngano kwa kuchanganya na vimengenyo (hamira) katika mchakato (process) wa utengenezaji wake,

lakini huvirutubisha vimengenyo (enzymes) ili kuweza kupata alkoholi (kilevi). Hivyo hukumu ya uhalali na uharamu wa alkoholi (kilevi) itatolewa kulingana n a k i wa n g o c h a k e kilichomo kwenye b i d h a a ya c h a k u l a (kinywaji), ( % alc). Muislamu ni wajibu wake kabla ya kutumia bidhaa za viwandani ambazo vina alkoholi kwa ajili ya matumizi ya chakula au vinywaji kwa mujibu wa viwango vya FAO ( 0.5 % alc) ni wajibu wake kujua viko kwenye kundi gani la viwango vya alkoholi nilivyovitaja hapo juu na ni lazima asome tangazo (lebel) ili kuweza kuangalia viambata (Ingredients or constituents) vilivyomo kwenye bidhaa. Vyakula au vinywaji ambavyo vimeepukana na kilevi huwezi kuvitolea hukumu kisheria katika dini (Uislamu) kwamba ni kilevi kwa dhana ya Inaendelea Uk. 15

Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na POA Printing Works LTD, S.L.P. 4605, Dar es Salaam.

Вам также может понравиться

  • Dini ya Fedha
    Dini ya Fedha
    От Everand
    Dini ya Fedha
    Оценок пока нет
  • Annuur 114
    Annuur 114
    Документ12 страниц
    Annuur 114
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Hofu
    Hofu
    От Everand
    Hofu
    Рейтинг: 5 из 5 звезд
    5/5 (1)
  • Annur:Toleo La Ijumaa Tarehe 13-01-2012
    Annur:Toleo La Ijumaa Tarehe 13-01-2012
    Документ16 страниц
    Annur:Toleo La Ijumaa Tarehe 13-01-2012
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Mwongozo wa Tumbo Lisiloshiba na Hadithi Nyinginge
    Mwongozo wa Tumbo Lisiloshiba na Hadithi Nyinginge
    От Everand
    Mwongozo wa Tumbo Lisiloshiba na Hadithi Nyinginge
    Рейтинг: 4.5 из 5 звезд
    4.5/5 (3)
  • Annuur 1153 PDF
    Annuur 1153 PDF
    Документ16 страниц
    Annuur 1153 PDF
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Tishio la Ukombozi: Ubeberu na Mapinduzi Zanzibar
    Tishio la Ukombozi: Ubeberu na Mapinduzi Zanzibar
    От Everand
    Tishio la Ukombozi: Ubeberu na Mapinduzi Zanzibar
    Оценок пока нет
  • Annuur 1114
    Annuur 1114
    Документ16 страниц
    Annuur 1114
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Afisa Usalama Wa Taifa Ni Mtu Wa Aina Gani? Na Anafanya Nini?
    Afisa Usalama Wa Taifa Ni Mtu Wa Aina Gani? Na Anafanya Nini?
    От Everand
    Afisa Usalama Wa Taifa Ni Mtu Wa Aina Gani? Na Anafanya Nini?
    Рейтинг: 4 из 5 звезд
    4/5 (24)
  • An-Nuur 1071
    An-Nuur 1071
    Документ12 страниц
    An-Nuur 1071
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Laikos: Watenda Kazi wa Kawaida na Huduma
    Laikos: Watenda Kazi wa Kawaida na Huduma
    От Everand
    Laikos: Watenda Kazi wa Kawaida na Huduma
    Оценок пока нет
  • Annuur 1062
    Annuur 1062
    Документ16 страниц
    Annuur 1062
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • HAYAAN, The Long Journey of the Nomad Boy
    HAYAAN, The Long Journey of the Nomad Boy
    От Everand
    HAYAAN, The Long Journey of the Nomad Boy
    Рейтинг: 5 из 5 звезд
    5/5 (2)
  • ANNUUR1004
    ANNUUR1004
    Документ16 страниц
    ANNUUR1004
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Simulizi Ya Dunia Kwa Kugeza Tanzania
    Simulizi Ya Dunia Kwa Kugeza Tanzania
    От Everand
    Simulizi Ya Dunia Kwa Kugeza Tanzania
    Оценок пока нет
  • Annuur 1157 PDF
    Annuur 1157 PDF
    Документ16 страниц
    Annuur 1157 PDF
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Bwana Okoa Ndoa Yangu
    Bwana Okoa Ndoa Yangu
    От Everand
    Bwana Okoa Ndoa Yangu
    Оценок пока нет
  • Gazeti La Annur
    Gazeti La Annur
    Документ12 страниц
    Gazeti La Annur
    Hassan Mussa Khamis
    Оценок пока нет
  • Mguso Mzuri Wa Upako
    Mguso Mzuri Wa Upako
    От Everand
    Mguso Mzuri Wa Upako
    Оценок пока нет
  • Annuur 1143
    Annuur 1143
    Документ16 страниц
    Annuur 1143
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Miaka Miwili Ya Urais Wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Au Nyota Iliyofifia?
    Miaka Miwili Ya Urais Wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Au Nyota Iliyofifia?
    От Everand
    Miaka Miwili Ya Urais Wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Au Nyota Iliyofifia?
    Рейтинг: 1 из 5 звезд
    1/5 (1)
  • Annuur 1151
    Annuur 1151
    Документ16 страниц
    Annuur 1151
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Imani Ya Mtu Wingine
    Imani Ya Mtu Wingine
    От Everand
    Imani Ya Mtu Wingine
    Оценок пока нет
  • Annuur 1064
    Annuur 1064
    Документ12 страниц
    Annuur 1064
    annurtanzania
    Оценок пока нет
  • Mti Na Huduma Yako
    Mti Na Huduma Yako
    От Everand
    Mti Na Huduma Yako
    Рейтинг: 2.5 из 5 звезд
    2.5/5 (2)
  • Annur Toleo La Ijumaa
    Annur Toleo La Ijumaa
    Документ16 страниц
    Annur Toleo La Ijumaa
    annurtanzania
    Оценок пока нет
  • Sanaa ya Kufuata
    Sanaa ya Kufuata
    От Everand
    Sanaa ya Kufuata
    Оценок пока нет
  • ANNUUR 1175b PDF
    ANNUUR 1175b PDF
    Документ20 страниц
    ANNUUR 1175b PDF
    annurtanzania
    Оценок пока нет
  • Annuur 1055 PDF
    Annuur 1055 PDF
    Документ16 страниц
    Annuur 1055 PDF
    annurtanzania
    Оценок пока нет
  • Annuur 115
    Annuur 115
    Документ16 страниц
    Annuur 115
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Annuur 1046
    Annuur 1046
    Документ12 страниц
    Annuur 1046
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Annuur 1028
    Annuur 1028
    Документ16 страниц
    Annuur 1028
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • ANNUUR 1169a PDF
    ANNUUR 1169a PDF
    Документ20 страниц
    ANNUUR 1169a PDF
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1065
    Annuur 1065
    Документ12 страниц
    Annuur 1065
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Annuur 1060
    Annuur 1060
    Документ16 страниц
    Annuur 1060
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Annuur 1158
    Annuur 1158
    Документ16 страниц
    Annuur 1158
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1122
    Annuur 1122
    Документ16 страниц
    Annuur 1122
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1027
    Annuur 1027
    Документ16 страниц
    Annuur 1027
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Imaan Newspaper Issue 1
    Imaan Newspaper Issue 1
    Документ19 страниц
    Imaan Newspaper Issue 1
    Imaan Newspaper
    100% (1)
  • Annuur 1119
    Annuur 1119
    Документ16 страниц
    Annuur 1119
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1183 PDF
    Annuur 1183 PDF
    Документ20 страниц
    Annuur 1183 PDF
    annurtanzania
    100% (2)
  • Annuur 1082
    Annuur 1082
    Документ16 страниц
    Annuur 1082
    MZALENDO.NET
    100% (1)
  • Annuur 1214
    Annuur 1214
    Документ20 страниц
    Annuur 1214
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1111
    Annuur 1111
    Документ16 страниц
    Annuur 1111
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1005
    Annuur 1005
    Документ16 страниц
    Annuur 1005
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Annuur 1109
    Annuur 1109
    Документ16 страниц
    Annuur 1109
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Rushwa Ya Ngono PDF
    Rushwa Ya Ngono PDF
    Документ19 страниц
    Rushwa Ya Ngono PDF
    Joselin Josephat
    Оценок пока нет
  • Annuur 1140
    Annuur 1140
    Документ16 страниц
    Annuur 1140
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1148
    Annuur 1148
    Документ16 страниц
    Annuur 1148
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1179 PDF
    Annuur 1179 PDF
    Документ20 страниц
    Annuur 1179 PDF
    annurtanzania
    100% (1)
  • Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari
    Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari
    Документ2 страницы
    Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari
    Hassan Mussa Khamis
    Оценок пока нет
  • Annuur 1078
    Annuur 1078
    Документ12 страниц
    Annuur 1078
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Annuur 1077
    Annuur 1077
    Документ12 страниц
    Annuur 1077
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Annur:Toleo La Ijumaa Februari 3 - 9, 2012
    Annur:Toleo La Ijumaa Februari 3 - 9, 2012
    Документ16 страниц
    Annur:Toleo La Ijumaa Februari 3 - 9, 2012
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • ANNUUR 1176b PDF
    ANNUUR 1176b PDF
    Документ20 страниц
    ANNUUR 1176b PDF
    annurtanzania
    Оценок пока нет
  • Annuur 1088 PDF
    Annuur 1088 PDF
    Документ12 страниц
    Annuur 1088 PDF
    annurtanzania
    Оценок пока нет
  • Zanzibar Daima Online, Toleo La Tano
    Zanzibar Daima Online, Toleo La Tano
    Документ24 страницы
    Zanzibar Daima Online, Toleo La Tano
    Hassan Mussa Khamis
    Оценок пока нет
  • Annuur 1049
    Annuur 1049
    Документ12 страниц
    Annuur 1049
    MZALENDO.NET
    Оценок пока нет
  • Annuur 1056 PDF
    Annuur 1056 PDF
    Документ16 страниц
    Annuur 1056 PDF
    annurtanzania
    Оценок пока нет
  • Imaan Newspaper Issue 4
    Imaan Newspaper Issue 4
    Документ15 страниц
    Imaan Newspaper Issue 4
    Imaan Newspaper
    Оценок пока нет
  • Annuur 1262
    Annuur 1262
    Документ20 страниц
    Annuur 1262
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1231 PDF
    Annuur 1231 PDF
    Документ20 страниц
    Annuur 1231 PDF
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1264
    Annuur 1264
    Документ20 страниц
    Annuur 1264
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1229 PDF
    Annuur 1229 PDF
    Документ20 страниц
    Annuur 1229 PDF
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1232 PDF
    Annuur 1232 PDF
    Документ20 страниц
    Annuur 1232 PDF
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1227 PDF
    Annuur 1227 PDF
    Документ20 страниц
    Annuur 1227 PDF
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • ANNUUR 1228d
    ANNUUR 1228d
    Документ20 страниц
    ANNUUR 1228d
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1224
    Annuur 1224
    Документ20 страниц
    Annuur 1224
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1226 PDF
    Annuur 1226 PDF
    Документ20 страниц
    Annuur 1226 PDF
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1230 PDF
    Annuur 1230 PDF
    Документ20 страниц
    Annuur 1230 PDF
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • ANNUUR 1228d
    ANNUUR 1228d
    Документ20 страниц
    ANNUUR 1228d
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1225
    Annuur 1225
    Документ20 страниц
    Annuur 1225
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1207...
    Annuur 1207...
    Документ20 страниц
    Annuur 1207...
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1214
    Annuur 1214
    Документ20 страниц
    Annuur 1214
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1220
    Annuur 1220
    Документ20 страниц
    Annuur 1220
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1223
    Annuur 1223
    Документ20 страниц
    Annuur 1223
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1219
    Annuur 1219
    Документ20 страниц
    Annuur 1219
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1217
    Annuur 1217
    Документ20 страниц
    Annuur 1217
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1218 PDF
    Annuur 1218 PDF
    Документ20 страниц
    Annuur 1218 PDF
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • ANNUUR 1216d
    ANNUUR 1216d
    Документ20 страниц
    ANNUUR 1216d
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1213 PDF
    Annuur 1213 PDF
    Документ20 страниц
    Annuur 1213 PDF
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1210a
    Annuur 1210a
    Документ20 страниц
    Annuur 1210a
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • ANNUUR 1209aaa
    ANNUUR 1209aaa
    Документ20 страниц
    ANNUUR 1209aaa
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1208
    Annuur 1208
    Документ20 страниц
    Annuur 1208
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1202
    Annuur 1202
    Документ20 страниц
    Annuur 1202
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1204
    Annuur 1204
    Документ20 страниц
    Annuur 1204
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1195
    Annuur 1195
    Документ20 страниц
    Annuur 1195
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1200
    Annuur 1200
    Документ20 страниц
    Annuur 1200
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет
  • Annuur 1201
    Annuur 1201
    Документ20 страниц
    Annuur 1201
    Anonymous x8QGwFF
    Оценок пока нет