Академический Документы
Профессиональный Документы
Культура Документы
Mahakama ya Kadhi
Sauti ya Waislamu
ISSN 0856 - 3861 Na. 1163 RABIUL THANI 1436, IJUMAA , FEBRUARI 6 - 12, 2015 BEI TShs 500/=, Kshs 50/=
Uk.16
Kura ya Maoni.
Hatari tupu
kwa Zanzibar
Vereje wa-Bara wapige kura!
Ya nini hadaa na janja yote hii
Kuinyima Zanzibari sauti ya kuamua?
Soma Uk. 13
Tahariri
AN-NUUR
MALALAMIKO
kuhusu utendaji
usioridhisha wa jeshi
letu la polisi yamekuwa
mengi. Raia wa kawaida
ndio ambao wamekuwa
wakilalamika zaidi,
lakini kwa bahati
mbaya, sauti zao hazina
msikilizaji.
Viongozi wa vyama
vya upinzani na asasi
za wanaharakati nao
wamekuwa wakipaza
sauti zao, kilio kikiwa ni
kile kile cha utendaji ulio
jaa dhulma na ukiukwaji
wa haki za binadamu wa
jeshi hilo. Nao hakuna
aliyewasikiliza.
Lakini kwa upande
mwingine, jeshi hilo
hilo la polisi limekuwa
na utekelezaji mzuri
wa amri kutoka kwa
wanasiasa walioshikilia
dola na hata wenye
fedha na ukwasi wa
mali. Vyombo vya habari
mara kadhaa vimekuwa
vikiripoti madhila kadha
wa kadha yanayofanywa
na jeshi hilo dhidi ya raia
na wanyonge, wakiwa na
matumaini labda serikali
inaweza kuguswa na
kuamua kulisafisha jeshi
hilo, ili liweze kufanya
kazi zake kiadilifu na
kwa weledi kwa mujibu
wa sheria bila kuwaonea
watu.
Pamoja na kelele za
viongozi wa vyama vya
siasa na wanaharakati
pamoja na raia ambao
kwa namna moja au
nyingine wameumizwa
na jeshi hilo, bado hakuna
hatua zozote madhubuti
zilizochukuliwa
kuliboresha jeshi letu
likawa la kistaarabu na
linalofuata sheria na haki
za binadamu.
Takwimu za taasisi
mbalimbali zimeonyesha
kuwa jeshi hilo ndio
kinara wa rusha nchini.
Pamoja na kutolewa
taarifa hizo za kitafiti,
bado serikali imepiga
kimya.
B a a d h i
y a
polisi wamekuwa
l i k i l a l a m i k i wa k wa
kubambikia watu
kesi, hakuna hatua
zilizodhihirika za
kukomesha unyama huo.
B a a d h i
y a
askari wamekuwa
wakituhumiwa
kuhusika katika baadhi
ya vitendo vya kihalifu
kama ujambazi, bado
hatusikii wala kuona
usafi ukifanyika ndani
ya jeshi hilo.
W a n a s i a s a
wamelalamika kuwa
jeshi linatumiwa kisiasa
kudhibiti wanasiasa hasa
wa upinzani, hususana
katika kutumia haki
yao ya msingi ya
kufanya mikutano
au kuandamana kwa
amani, njia mbazo
ndizo zilizozoeleka
kwa wanasiasa
kuwafikia watu wao.
Tumeshuhudia mikutano
ya k i s i a s a i k i p i g wa
marufuku kwasababu
zinazoitwa za kiusalama,
lakini kimantiki lengo
likiwa ni kuzuia nguvu
ya upinzani. Hapa ndipo
tulipolifikisha jeshi letu.
Limegeuka kuwa kama
chombo cha kulinda
maslahi ya watu kisiasa,
kugeuza vituo vyake
kuwa ofisi za kuchuma
fedha chafu kwa njia ya
rushwa, kugeuka pepo
ya wenye fedha kununua
haki za wanyonge nk.
Siku hizi kwa
upande wa walala hoi,
wakifikishana polisi
kutatuliwa mashauri yao,
kila upande utalazimika
kutoa chochote
ukitegemea kupata
haki. Muhimu si nani
kamkosea mwenzake. Ni
mfuko wako.
Kuna tetesi kwamba
hata faini za vyombo
vya moto barabarani
(Notification) nazo zipo
halisi na za kughushi.
Lakini hakuna wa
kuchunguza licha ya
tetesi hizo kusambaa kila
kona.
Watu wamejeruhiwa
kwa vipigo bila hatia.
Wa p o w a l i o p o t e z a
maisha yao, wapo
walioharibiwa mali zao,
yote hayo ni matokeo ya
kinachodaiwa kuwa ni
uozo ndani ya jeshi hilo.
Tunakumbuka mwaka
2006 kulikuwa na
mpango wa kuboresha
Jeshi letu la Polisi uliotwa
Programu ya Maboresho
ya Jeshi la Polisi.
Ilikuwa ni Programu
ya serikali ya kuboresha
utendaji wa Jeshi la
P o l i s i c h i n i Wi z a r a
ya Mambo ya Ndani
ya N c h i , i l i y o k u wa
imegawanywa kwa
awamu mbili. Awamu ya
kwanza ilielezwa kuanza
2010/2011 hadi 2014/2015
na awamu ya pili
iliahidiwa kutekelezwa
kati ya mwaka 2015/2016
hadi 2019/2020.
Programu hiyo ilianza
baada ya Jeshi la Polisi
kupokea ripoti ya timu
iliyohusisha watalaamu
wa ndani na nje ya Jeshi
la Polisi iliyofanya utafiti
na kutoa mapendekezo
yao kwa uongozi wa
Jeshi la Polisi na Wizara
ya Usalama wa Raia.
Timu hiyo iliweza
kukusanya maoni toka
kwa viongozi wa juu wa
nchi wakiwemo Marais
waliokuwa madaraakni
na wastaafu, Rais,
Mawaziri, wanachuoni,
viongozi wa vyama vya
siasa na dini, wananchi
wa kawaida na wadau
wengine.
Moja ya Mapendekezo
ilikuwa ni kuanzishwa
kwa Programu ya
Maboresho ya Jeshi la
Polisi ili kuzifanyia kazi
changamoto mbalimbali
zilizokuwa zinalikabili
Jeshi la Polisi.
Mwaka
2007
iliteuliwa timu ya
kuratibu na kusimamia
maboresho iliyohusisha
AN-NUUR
polisi wakaendeleza
kipigo kwake. Matukio
ya namna hii yamekuwa
mengi na hakuna
anayewajibika.
Wananchi wanataka
ifike tamati ya mazoea
yaliyojengeka kwa
miongo kadhaa ya
watu kudhulumu kwa
kutumia Crown.
Watanzania wanahitaji
jeshi safi lenye maadili,
linalofuata sheria
na haki za binadamu
katika ukekelezaji wa
majukumu yake.
Si jambo lenye tija wala
la kujivunia kuendelea
kuwa na jeshi la polisi
lisiloaminika mbele ya
raia wake.
Habari/Tangazo
AN-NUUR
WAISLAMU waliduwaa
kwa muda baada ya
juzi Jumanne wiki hii
kumuona Mkurugenzi
wa Fedha na Utawala
wa TAMPRO, Ustadhi
Haruna Mussa Lugeye,
pamoja na mkewe
wakipandishwa
kizimbani katika kesi
nyingine ya ugaidi.
Ustadh Lugeye
pamoja na mkewe Bi.
M w a j u m b e We n d u
Bakari, walipandishwa
kizimbani katika
Mahakama ya Kisutu
jijini Dar es Salaam,
mbele ya Hakimu Janet
Kaluyenda.
Hata hivyo Hakimu
Kaluyenda aliahirisha
kesi hiyo hadi Februari
16 mwaka huu kwa kuwa
Hakimu anayeisikiliza
kesi yao Mh. Moshi
hakuwepo mahakamani.
Juhudi za kumtoa
mkewe kwa dhamana
nazo zilikwama pia.
Hii ni kutokana na
H a k i m u K a l u ye n d a
kusisitiza kuwa yeye
hatoweza kutoa
dhamana kwa sababu
shauri halipo kwake.
Na hivyo kushauri
Wa k i l i w a u t e t e z i
amsubiri Hakimu
mwenye shauri hilo.
Kuhusu kesi hiyo,
wakili Salim alisema Bw.
Haruna Mussa Lugeye na
mkewe wanatuhumiwa
kwa mashitaka ya ugaidi
na Kesi yao ilianza tarehe
10/12/2014.
Alisema hiyo ni kama
mara ya tatu au ya nne
kutajwa Mahakamani
hapo.
Wakati huo huo, kesi ya
Watuhumiwa wa ugaidi
inayowakabili Waislamu
2 3 a k i we m o S h e i k h
Mselem Ali Mselem
na Waislamu wengine,
wameilalamikia
mahakama kuwa
gari linalowabeba
wakati wakipelekwa
mahakamani hapo
halifai.
Wa t u h u m i wa h a o
walidai gari walilokuwa
wamepanda lilikuwa
l i k i f u n g wa v i o o n a
kusababisha kuvuta
hewa kwa taabu.
Akizungumza
mahakamani hapo,
wakili wa upande wa
utetezi Abubakari
Salim, alisema kuwa
ameshangazwa na
kitendo hicho kwani
sio cha kiuungwana
na kuitaka Mahakama
itambue kuwa,
watuhumiwa hao ni
binadamu wanaohitaji
hewa.
Akithibitisha kutokea
kwa tukio hilo, dereva
wa gari linalowabeba
watuhumiwa hao
(jina la dereva huyo
halikufahamika mara
moja) alisema kuwa vioo
vilifungwa kwa sababu
za kiusalama kufuatia
vurugu zilizotaka
kujitokeza katika eneo
l a m a g e r e z a wa k a t i
wanajiandaa kuanza
safari ya kuelekea
mahakani.
Niliamua kufunga
vioo baada ya kuona
dalili ya vurugu,
lakini kabla sijaamua
kufunga niliwatangazia
watuhumiwa kuwa
nafunga kwasababu ya
usalama wao na wangu.
Kwa bahati mbaya
nilisahau kufungua,
lakini sikuwa na nia
yoyote mbaya", alisema
dereva huyo.
Kwa upande wake
hakimu anayesikiliza
kesi hiyo Mh. Janet
Kaluyenda, alimtaka
dereva huyo kutorudia
tena kitendo hicho na
endapo kitajirudia, basi
t a a r i f a i t o l e we k wa
mkuu wa magereza ili
atoe maamuzi, kwani
mahakama haihusiki na
masuala ya magereza.
Hakimu Kaluyenda
aliahirisha kesi hiyo hadi
Februari 16 mwaka huu.
Naye Wakili waupande
wa utetezi Abubakari
Salim, alisema kesi zote
mbili zilipangwa kwa
ajili ya kutajwa.
"Ile Kesi ya Masheikh
na Waislamu wengine
na chamgamoto kadhaa
ulimwenguni hasa
mashuleni, vyuoni,
makazini na hata kwenye
sehemu za umma.
Muhadhara wa mwezi
Rabiul Thani 1436/2015
4
SI panya mnyama aishie na
watu, wala si changudoa
samaki kitoweo kizuri na
chenye bei nzuri. Hawa ni
watoto wetu, ama ni ndugu
zetu kwa nasaba au kwa
majirani. Inashtusha na
kushangaza. Dar es Salaam
ilikumbwa na taharuki
ya Dar es PANYA ROAD
(Mbwa Mwitu).
Mengi yamesemwa na
watu mbalimbali wakiwemo
watu wazito katika jamii,
l a k i n i w e n g i wa l i o o n a
kwa karibu tukio husika
wakihadithia unahisi kama
wanahadithia filamu ya
Anorld SChwatzneeger au
Sylvester Stallone.
Hofu, vicheko na mzaha
vilikuwa ndio gumzo kubwa
la kwanza la mwaka 2015
hapa Jijini Dar es Salaam.
Imesababisha mpaka wengine
kushukuru wapendwa wao
kurudi nyumbani mapema
na wengine kuhuzunika
wapenzi wao kuchelewa
kurudi nyumbani, kisa
Sekeseke la Panya Road
maeneo kadhaa ya jiji la Dar
es Salaam.
Wengi waliangukia katika
kuinyooshea vidole serikali,
hasa Jeshi la Polisi kwa
kuzembea kupata habari za
Ki-intelijensia kuthibiti hali
hilo na wengine wamehoji,
wapi zile mbwembwe za
polisi jamii katika kupambana
na uhalifu.
Nilikaa na kuangalia
nini hasa kimetokea na
wapi tunaenda. Nini nafasi
ya k i l a c h o m b o h u s i k a
katika taharuki kama hizi.
Familia, jirani, Misikiti,
Kanisa, Serikali Polisi na
walimwengu kwa ujumla.
Nakubaliana na maoni ya
watu mbalimbali juu ya Polisi
na vyombo vya usalama
kukosa taarifa za msingi juu
ya kuthibiti kilichotokea.
Lakini kwa sehemu kubwa
vyombo habari vya kijamii,
yaani social media (Whats
U p , F a c e b o o k , Tw i t e r ,
Blogs, Instagram etc) nazo
zimekuwa mtihani sana kwa
kukuza mambo kuliko hali
halisi.
Pamoja na kwamba kuna
faida, lakini hii moja ya
madhara ya vyombo hivi
katika jamii. Upokeaji wa
habari kwa vyombo hivi
u n a h i t a ji u ma k i n i sa n a
kwani nusu ya taarifa huwa
zinatengenezwa na watu
b i n a f s i we n ye m a l e n g o
tofauti.
Nadhani kuna umuhimu
wa kuongeza mtazamo wa
ziada juu ya hili, nalo ni mkao
wa jamii yetu ya Kitanzania
kwa ujumla.
Panyaroad, changudoa,
mbwa mwitu, kiboko msheli,
American etc ni vikundi
ZAO la kuporomoka kwa
maadili ya Jamii. Hawa vijana
wanatoka katika jamii zetu.
Tunaishi nao kama watoto
wetu, wadogo zetu, majirani
zetu, waumini wenzetu etc.
Nini kumetokea mpaka
tumefika hapa na nini
matumaini ya baadae kama
tutaendelea na visingizio
vya kutushughulisha na
mambo mepesi na kuacha
kushughulikia matatizo ya
msingi, ambayo sehemu
kubwa ni kuporomoka kwa
mfumo wa familia na maadili
katika Jamii zetu na kukosa
upendo kwa watu wa imani
na dini mbalimbali.
Familia ni taasisi kongwe
na kubwa, ambayo ndio ya
Makala
AN-NUUR
Pa n ya r o a d wa p o a k i n a
Abdallah na John au Fatuma
na Ester. Pia katika harakati
zao za vurugu mbalimbali
tumewaona akina Ephraim
na akina Hassan wakipata
kibano.
Laiti jamii hizi za dini
zingekuwa na mtazamo
mpana wa kushirikiana
katika mambo ya msingi bila
hila, ambayo kwayo ndio
maamrisho ya vitabu vyao,
basi matatizo kama haya ya
Panyaroad yangekuwa ni
kwa nadra sana kwa kuwa
sehemu kubwa ya jamii
ingekuwa tiifu na yenye
upendo.
Kwa ujumla bado sehemu
kubwa ya jamii inainyoosha
kidole serikali, hasa jeshi
la polisi pasi na kuangalia
ukubwa wa tatizo husika.
Ukiangalia kwa makini
muelekeo wa Watanzania
wengi kwa sasa, utaona
tunashughulishwa sana na
vitu ambavyo si matatizo
ya msingi katika jamii yetu,
tunaacha kuhangaika na
matatizo halisi ambayo
yanaendelea kututafuna
tunashabikia mambo ya
kijinga.
EPA ESCROW na ujambazi
mwingine, yote hayo ni
matokeo ya kuporomoka
malezi ndani ya jamii yetu.
Tumekuwa tukiamini katika
maendeleo ya ubinafsi na
kusahau kuwa tunatengeneza
bomu zito.
Nadhani kama nchi,
tukiweza kuchunguza na
kutambua upungufu wetu,
kwa kutafakari kwa kina,
tunaweza kupata njia nzuri
ya kuondokana na ongezeko
la maovu ndani ya jamii na
kujenga jamii bora yenye
amani na utulivu wa kweli.
N a a m i n i p a n ya r o a d
na Machangudoa ni tatizo
la kijamii zaidi, kuliko
kuwaonyesha vidole vyote
Jeshi la Polisi na Serikali.
Japo nalo limekuwa jeshi la
operesheni zenye maslahi
zaidi kwao kuliko kulinda
mali na usalama wa watu kwa
ujumla kama inavyotakikana.
Kwa zile jamii zenye
madai maalum na serikali
kuyazima madai hayo kwa
nguvu au hila, basi hapa
tusishangae anguko la
kijamii likiongezeka, hasa la
kutotii mamlaka zilizopo na
kuongezeka zaidi hao panya
road.
Jamii ya Kitanzania
ikishirikiana inaweza
kuondoa mashaka mengi
ya kijamii na kiuchumi
na kuleta maendeleo ya
pamoja kama jamii moja.
Hili linawezekana, lakini
linahitaji uongozi thabiti
unaoona umuhimu wa jamii
yanye maadili kuanzia ngazi
ya familia, koo, ujirani hadi
serikalini kwa Ujumla.
Vi o n g o z i wa s e r i k a l i
wana dhima ya kulisimamia
hili na kulisema kadri
iwezekanavyo. Wao wawe
mfano wa uadilifu katika
nyadhifa zao.
Mungu ibariki Tanzania,
Mungu ibariki Afrika.
Maasalaam...
Makala
AN-NUUR
Makala
AN-NUUR
na hivyo kuboresha
ufyonzwaji wa virutubisho
na uondoshaji wa uchafu
mwilini kwa njia ya haja.
TINDIKALI ZA AMINO AU
VIJENZI VYA PROTINI: VIJENZI
VYA PROTINI NI NINI?
Vi j e n z i v ya p r o t i n i
( tindikali za amino/
amino acids) ni molekuli
(molecule) ndogondogo
zinazotumika kama tofali
za kuundia protini. Protini
ni molekuli (molecule)
kubwa za kibaiolojia zenye
majukumu kadhaa wa
kadhaa ndani ya mwili.
Idadi kubwa ya shughuli
mbali mbali katika seli za
mwili hufanywa na protini.
Aidha protini zinahitajika
katika uratibu na utendaji
kazi wa tishu na viungo
vya mwili, ikiwa ni pamoja
na kuunda maumbo ya
tishu na viungo husika.
P r o t i n i h u u n d wa n a
m a m i a a u m a e l f u ya
molekuli za tindikali
za amino zilizoungana
katika umbile la nyororo.
Kuna tindikali za amino
20 zinazoweza kuungana
katika michanganyiko
mbalimbali (combination)
kutengeneza molekuli za
protini. Kwa kawaida
huwa tunatakiwa tupate
vijenzi vyote vya protini
tunavyohitaji kupitia
katika lishe. Hata hivyo
kutokana na mapungufu
mbalimbali yaliyoko katika
lishe zetu inatokea tukawa
na upungufu wa baadhi
ya hivi vijenzi vya protini
na hivyo kukumbwa na
magonjwa yanayohusiana
na huo upungufu.
V I J E N Z I M U H I M U V YA
PROTINI VILIVYOKO KATIKA
HAIIBA TIMAMU TEA
Baadhi ya vijenzi
m u h i m u v ya p r o t i n i
v i l i v y o k o k wa w i n g i
katika chai hii ni
Arginine, Histidine,
Isoleicine, Leucine,
Lysine, Methionine,
Phenylalanine, Threonine,
Tryptophan, na valine.
Arginine: Faida
za argininei ni nyingi.
Miongoni mwa faida hizi
ni pamoja na: Huongeza
kasi na ufanisi wa kupona
majeraha. Huongeza
ufanisi wa figo katika
kuondosha uchafu
mwilini. Huboresha kinga
za mwili na utendaji kazi
wa homoni. Huboresha
mzunguko wa damu na
hivyo huusaidia moyo
kufanya kazi kwa ufanisi
kupunguza uwezekano
wa kupata magonjwa
yanayohusiswa na
mkakamo wa mishipa ya
damu kama shinikizo la
damu, kupoteza nguvu
za kiume, shambulizi
la moyo na maumvu ya
kifua yanayosababishwa
na mzunguko dhaifu wa
damu (angina).
Histidine: Faida
za Shaba ni nyingi.
Miongoni mwa faida hizi
ni pamoja na: Huhusika na
kuimarika kwa tishu zote
ndani ya mwili, hususan
zile zinazounda utando
unaozunguka mishipa yote
ya fahamu (myelin sheath).
Hupunguza uwezekano
wa kupata ugonjwa wa
ukungu katika lenzi
za macho (carrtaracts).
Hupunguza uwezekano
wa k u p a t a b a r i d i ya
yabisi (rheumatoid
arthritis) na hupunguza
athari na maumivu
yanayoambatana na
ugonjwa huo.
Isoleucine: Faida za
Isoleucine ni nyingi.
Miongoni mwa faida hizi
ni pamoja na: Kutengeneza
chembechembe nyekundu
za damu (Hemoglobin).
Inachochea ukarabati wa
tishu baada ya upasuaji au
ajali. Inaleta unafuu kwa
magonjwa mbalimbali
ya akili kama msongo
endelevu, mfadhaiko,
kukosa usingizi,
nakadhalika. Inazuia
misuli isiharibike wakati
wa kufanya mazoezi.
Inaongeza nguvu mwilini;
na inajenga uwezo wa
mwili kuhimili kazi
ngumu.
Leucine: Hii ni miongoni
mwa tindikali za amino
ambazo hazizalishwi ndani
ya miili yetu na kwa hivyo
ni lazima kuipata kupitia
lishe. Faida za Leucine ni
nyingi. Miongoni mwa
faida hizi ni pamoja
na: Inachagiza ujenzi
wa protini zinazounda
misuli mbalimbali ya
mwili. Humsaidia mtu
anayepunguza kula ili
kupunguza uzito aunguze
mafuta yaliyolundikana
mwilini, bila kuathiri
misuli; na inachagiza
kemikali moja inayokaa
kwenye misuli inayoitwa
m-TOR (mammalian target
of rapamycin) ambayo
hufanya kazi kama swichi
ya kuwezesha uzalishaji
wa protini zinazohitajika
katika kujenga misuli
kufanya kazi kikamilifu.
Lysine: Hii ni miongoni
mwa tindikali za amino
ambazo hazizalishwi
ndani ya miili yetu na kwa
hivyo ni lazima kuipata
kupitia lishe. Faida za
Lysine ni nyingi. Miongoni
mwa faida hizi ni pamoja
na: Husaidia kuratibu
k i wa n g o c h a l e h e m u
(cholesterol) mwilini.
Ni muhimu sana katika
kulinda afya ya mifupa.
Inasaidia mwili kupokea
na kutumia madini ya
kalisi (calsium) kwa weledi
zaidi na pia husaidia
kupunguza upoteaji
wa kalisi kutoka katika
7
Na Shaban Rajab
MWENYEZI Mungu
amemuumba mwanadamu
na kumtengenezea
mazingira ya kuishi
duniani, na akampa uwezo
wa kumudu kuishi
katika mazingira hayo na
kumwabudu hadi siku yake
ya mwisho ya uhai wake.
Binadamu aliwekewa kila
alilolihitaji katika kumudu
maisha ya duniani. Baadhi
ya vitu muhimu kabisa
vya kimaisha ambavyo
binadamu tunategemea
kuendelea kuhifadhi
mfumo wa uhai wake ni
chakula, mavazi na malazi.
Haya ni mahitaji ya asili
ambavyo binadamu hapaswi
kuyakosa.
Zaidi ya hapo binadamu
amejaaliwa kuwa na maarifa,
fikra na ujuzi, nyenzo ambazo
huzitumia katika kufanya
mambo yake mbalimbali ya
kimaisha hapa duniani, ili
kupata ufanisi na tija.
Lakini pia kuna sehemu
nyingine ya mahitaji ambayo
tunaweza kusema kuwa ni
yale yasiyokuwa ya lazima.
Katika zama hizi mahitaji
haya yasiyo ya lazima,
ndio yamegeuzwa kuwa
ya msingi katika maisha ya
mwanadamu kiasi cha kuwa
chanzo cha kuibuka fikra za
ubinafsi, chuki, tamaa na
kibri.
Mahitaji kama haya hayana
kikomo katika kuhitajika
kwake, kwani ni mengi na
wala mtu hawezi kuyapata
au kukidhi yote, ila katika
ndoto na mawazo tu. Kiu
ya kutafuta mali za ziada
ili kukidhi matumizi yake
ya kitamaa imetawala nafsi
za wengi. Na kwa hakika
udhaifu huu, ndio chanzo
cha na kumfanya binadamu
awe mpumbavu, alewe kiasi
cha kushindwa kutumia akili
yake aliyopewa na Mwenyezi
Mungu vizuri.
Kwa kuwa kudumu
na kustawi katika maisha
ya mahitaji ya tamaa
kunategemea mali zaidi,
watu siku hizi hulazimika
kudhulumu, kufisidi,
k u f a n ya u b a d h i r i f u n a
kuhakikisha kuwa anakuwa
na ubinafsi wa hali ya juu.
Kufuatana na muundo
wa kimaumbile, kwa
namna moja au nyingine
kila mtu anahitajia msaada
wa mwenzake kwa ajili ya
kustawisha, kukamilisha na
kuzalisha matunda ya vipawa
vyake. Anahitajika kuwa
na moyo wa kushirikiana
na kusaidiana kama msingi
muhimu katika kuleta
maendeleo na mafanikio.
M u u n d o wa u u m b a j i
wa binadamu umeundwa
k wa a j i l i ya m a i s h a ya
kijamii, hivyo kimaumbile
binadamu anastahili
kushirikiana na wenzake
katika kutatua matatizo yake
ya kimaisha. Kwa upande
mwingine, utajiri mwingi
mara nyingi huambatana
na kiburi, majivuno na tabia
chafuchafu. Mtu anapokuwa
Makala
AN-NUUR
Threonine: Hii ni
miongoni mwa tindikali
za amino ambazo
hazizalishwi ndani ya
miili yetu na kwa hivyo
ni lazima kuipata kupitia
lishe. Faida za Lysine ni
nyingi. Miongoni mwa
faida hizi ni pamoja na:
H u r a t i b u u w i a n o wa
protini ndani ya mwili
ili kudhibiti upungufu.
Inachagiza tindikali
nyingine za amino kujenga
protini mbalimbali
zinazohitajika kwa ajili ya
tishu mbalimbali xa mwili.
Inatengeneza tindikali za
amino za glycine na serine
2 ambazo ni muhimu sana
katika uundaji wa protini
aina za collagen na elastin
ambazo ni vitu muhimu
sana kwa siha ya ngozi,
tishu zinazounganisha
misuli na mishipa ya damu.
Inatengeneza tabaka
jembamba linalozunguka
jino kwa nje (tooth
enamel). Inashirikiana na
methionine na tindikali
aina ya aspartic (aspartic
acid) kuliwezesha ini
kuondokana na mafuta.
Inafanya sukari ya damu
isiongezeke au kupungua
kiholea. Inaboresha
mfumo wa kinga za mwili.
Ina umuhimu wa kipekee
katika ukuaji wa tezi ya
thymus katika ubongo.
Ni ya lazima kwa ajili
ya siha bora ya mfumo
wa mishipa ya fahamu.
Inasaidia kupambana na
msongo na mfadhaiko.
Inawezesha mchakato
wa kikemia unaohitajika
kuzalisha nishati katika seli
(krebs cycle) kufanya kazi
kwa ufanisi unaotakiwa.
Husaidia ujenzi wa mifupa
imara; na huongeza kasi ya
kupona kwa majeraha.
Siku zote kinga ni bora
Makala
AN-NUUR
Makala
AN-NUUR
MAKAMU wa kwanza
wa Rais wa Zanzibar, Seif
Sharif Hamad.
usalama kwa waendeshaji
wa magari.
Utajiuliza kwanini leo
watoto wanaokwenda
skuli kuwa humo njiani
wanamopita ni kelele
tupu na kusema maneno
yasiostahiki. Basi tena
usadifu kupanda daladala
n a o h a p o u t a ya s i k i a
usioyapata kuyasikia.
Wa l i m u h u k o n y u m a
ndio waliokuwa kioo kwa
wanafunzi na jamii kwa
jumla. Leo aghlabia ya
walimu mienendo yao
sio yenye maadili. Siku
h i z i k u s i k i a wa l i m u
wa madrasa baada ya
k u e l e k e z a k u t e n d wa
mwenendo mwema wao
ndio sasa wanaowaharibu
watoto, inasikitisha kusikia
humo kwenye madrasa
watoto ndio wanaharibiwa.
Hivi sasa unasikia fukuto
lilokuwa sio la chini kwa
chini lakini lishatoa moto
wala sio moshi kusikia
mapenzi yanayofanywa
na watu wa jinsia mmoja,
halafu kumsikia mtu
analizungumzia kama ni
jambo la kawaida katika
jamii. Anatamka mtu
yule mpenzi wake, huyo
anayoambiwa ni mpenzi
wake ni wote wawili
ni watu wa jinsia moja.
Hapa ndipo unapojiuliza,
hao wanaopiga zumari
kuhalalishwa matendo
hayo machafu sio
watapata mwanya
kusema yahalalisheni
kuliko kuwachia
kuwa hayatendeki na
kuwakosesha mashetani
hao uhondo?
Leo madanguro yapo na
MAKAMU wa pili wa
Rais wa Zanzibar, Balozi
Seif Idd.
unapouliza unaambiwa laa
hio ni gesti tu. Inafahamika
fika kuwa nyumba hizo
zinaruhusiwa na wamiliki
wake watu kwenda
kujifanyia watakavyo. La
kujiuliza, kweli na huo
UKIMWI utatoweka?
Siku hizi kuna maeneo
ukipita nyakati za usiku
utakutana na wale
wanaouza miili yao na
soko hilo huambiwa ni la
watalii, lakini na wenyeji
nao sio kalili.
Zamani ilikuwa mtu
akiwa na haja ya nazi
huwenda kwa mmiliki wa
shamba na kumuomba
nazi. Hapo mmiliki ama
atamgea kama zipo au
atamwambia kama
unaweza kuukwea
mnazi, basi kajichukulie
zitazokidhi haja zako.
Huko nyuma utaikuta
ndizi imekaa kwenye
mgomba kila ukipita
imekutumbulia macho.
Leo wizi wa mazao
umeshika kasi na kupamba
m o t o . M we n ye n d i z i
anaikata ingali changa
kwa kuhofia isije kuibiwa.
Leo la kusikitisha nikuona
mifugo inavyoangamizwa.
Mtu anamchinja
ngombe aliomuiba kisha
akachukua paja moja tu
na kumwacha ngombe
na sehemu zake zilizobaki
kama mzoga. Wakulima
na wafugaji kila mmoja
anafanya amali hizo kwa
kuwa ni mazoea tu, lakini
sio wenye matumaini na
kupata kipato kutokana na
kazi hizo.
Mvuvi amekuwa
mfano wa yule anawekea
10
Na Omar Msangi
WASWAHILI wana msemo
wao, siku njema huonekana
asubuhi. Lakini kwa mantiki
hiyo hiyo, hata mbaya pia.
Zipo sababu za kuwa na
wasiwasi kuwa huenda hali
ikawa mbaya katika mwaka
huu wa uchaguzi mkuu,
na hasa Zanzibar. Kama
huko nyuma kulikuwa
na melody, basi huenda
melody ya mwaka huu
ikawa mbaya zaidi. Hii ni
kutokana na yaliyojitokeza
katika mkutano na
maandamano ya Chama cha
Wanachi, CUF, yaliyokuwa
yafanyike Jan. 27, 2015 na
kuzuiwa na Polisi.
Yapo mambo matatu ya
kuongoza mjadala huu.
Moja ni ile kauli ya Waziri
w a M a m b o ya N d a n i ,
Mheshimiwa Mathias
Chikawe, pale alipoliambia
Bunge kuwa, ilibidi polisi
wazuiye maandamano kwa
sababu kuna ugaidi na
kwamba, panapokuwepo
ugaidi, basi magaidi huwa
wanatumia mikusanyiko ya
watu wengi kufanya ugaidi
wao.
Pili, ni kile kilichoonekana
watu kupigwa mpaka
kupitiliza. Taarifa ndani ya
bunge ikasema kuwa baadhi
ya polisi walitumia spana
za magari (chuma/nondo)
kupiga watu vichwani.
Ta t u , n i i l e k a u l i
iliyoripotiwa pia Bungeni
k u wa b a a d h i ya p o l i s i
walipoulizwa kwa nini
walifanya vile, walidai kuwa
ni amri kutoka juu.
Katika mauwaji ya
Vietnam, Cambodia na Laos,
ambapo mamilioni ya raia
wasio na hatia waliuliwa
na wanajeshi wa Marekani
kati ya mwaka 1969 na 1973,
Henry Kissinger, wakati
h u o a k i w a Wa z i r i w a
Mambo ya Nje, anadaiwa
kuwa msimamizi mkuu
wa m a u wa j i h a y o p a l e
alipopeleka ujumbe kwa
askari akiwaambia kuwa
anachotaka kusikia Rais
Nixon ni kuuwa, kupiga
mabomu bila kikomo na bila
huruma. Kila kinachotembea
au kutambaa, kila kilicho hai
kisiachwe. Kipigwe tu.
[Nixon] wants a massive
bombing campaign in
Cambodia. He doesn't want to
hear anything about it. It's an
order, to be done. Anything that
flies or anything that moves.
Na kweli, kutokana
na amri hii kutoka juu,
mamilioni ya watu wasio
na hatia waliuliwa. Na kwa
vile amri ilisema, chochote
kinachotembea, kipigwe
tu. Hapakuwa na msalie
kwa raia.
Kila yakitokea matukio
yanayotafsiriwa kuwa
ni ugaidi, viongozi wetu
wanatuambia kuwa
wameagiza FBI kutusaidia
kwa sababu wana uzoefu
katika mambo haya. Na hivi
sasa tumekuwa ni washirika
wao wazuri katika mambo
Makala
AN-NUUR
Inaendelea Uk. 12
11
HALI ya mambo siku
chache kabla ya upigaji
kura kwenye Bunge
Maalum la Katiba ilikuwa
ngumu sana kwa watu
saba walioamua kuikataa
katiba iliyolazimishwa na
Chama Cha Mapinduzi
(CCM). Mwandishi Salma
Said ameandika alichoita
Simulizi za Ushuhuda
wa hali waliyokuwa nayo
kwa sababu tu waliazimia
na hatimaye kupiga kura
ya HAPANA. Fuatilia
si m ul i zi zake katika
makala yake.
Ningependa niandike
simulizi za siku chache
kabla ya upigaji kura namna
ambavyo hali ngumu
ilivyotukabili sisi watu
saba tulioamua kupiga
kura ya HAPANA, tena ya
wazi, kwani Wazanzibari
wenzetu walituchukulia
kwa mtazamo tofauti
kutoka nyumbani
Zanzibar. Baadhi ya vijana
walichapisha vipeperushi
na kuvisambaza kwenye
m i t a n d a o ya k i j a m i i
wakitutaka turudi
nyumbani na kutuita
wasaliti, huku Wazanzibari
wenzetu Dodoma nao
wakitupa vitisho vya
kila namna tu maana
haikuwa kutushawishi
tu, bali mambo yalizidi na
kupindukia mipaka hadi
wengine wakitwambia
tukipiga kura ya hapana
tutakiona cha moto.
Baada ya kuonekana
wapo watakaopiga
kura za hapana, lugha
iliyokuwa ikitumika
miongoni mwa wenzetu
wa CCM wakisema
k u n a wa t u wa n a t a k a
kuharibu mchakato wa
katiba inayopendekezwa
katika dakika za mwisho
lakini waliapa kwenda na
sisi iwapo hatutaregeza
misimamo yetu ya
kuikataa rasimu hiyo.
Sio kazi rahisi kama
we n g i wa n a v y o d h a n i
kama ambavyo haikuwa
we p e s i wa l i o t o k a n j e
ya b u n g e , U m o j a wa
K a t i b a y a Wa n a n c h i
( U K AWA) k u r u d i
ndani, halikadhalika
ugumu ulikuwepo kwa
waliokuwepo ndani kutoka
nje, wengine tuliamini hata
maamuzi ya watu kutoka
bungeni wangetoka basi
naamini wangetoka watu
wachache kama watu
wa t a t u t u a u wa n n e
ambao wana msimamo
madhubuti na wengine
wangebaki na kurahisisha
mafanikio ya kupatikana
2/3 kirahisi, kutokana na
khofu miongoni mwetu.
Baadhi ya wajumbe
kutoka Zanzibar hasa wale
wanaotokana na kundi la
Makala
AN-NUUR
wakati Mwenyekiti wa
Bunge Maalum la Katiba
akitangaza timu yake ya
kamati hiyo wajumbe
w o t e s a b a wa l i o p i g a
HAPANA wapo njiani
kurejea Zanzibar; jee
wajumbe wangapi hao
waliotajwa kukutana na
Kamati ya Maridhiano
wakati hawakuwepo tena
Dodoma?
Wajumbe saba waliamua
kuondoka Dodoma
kutokana na dharau,
matusi ya nguoni, vitisho
walivyokuwa wakivipata
kutoka kwa wajumbe
walio wengi ambao ni wa
CCM, hawakujifanya tu
kuwa wao ndio wengi, bali
walijifanya wao ni wenye
nguvu, wenye maamuzi ya
wenzao kwa kisingizio cha
kuwa na dola eti wao ni
wenye uwezo wa kufanya
chochote katika katiba
hii kutokana na kauli
walizokuwa wakituambia.
Lakini pia ningependa
niandike namna
g a n i Wa z a n z i b a r i
walivyotumika kufanyiana
u a d u i we n y e we k wa
wenyewe; kuoneshana
ubabe, dharau, matusi ya
nguoni, kebehi na vijembe
kutokana na kuwa na
mitazamo tofauti wakati
wenziwao wa Tanzania
Bara wakikaa pamoja.
Hii Katiba itapita
mtake msitake, hii katiba
nyinyi hata mkipiga
hapana nyote mliopo
ndani ya ukumbi huu mjue
tu kwamba tutaipitisha
mnacheza na wana CCM
nyie, hii ndio chama dume,
hiki ndio chama chenye
uwezo, hiki ndio chama
tawala ..., ni maneno ya
kiongozi CCM Zanzibar.
Kauli kama hizo
zik itolewa na b aadhi
ya viongozi wa Chama
Cha Mapinduzi (CCM)
na wanachama wengine
waliondoka katika nafasi
zao bungeni na kuja
pale tulipokaa sisi na
kuunga kauli za Shaka
na wenzake kama wanne
kuanza kuongea maneno
k a m a ha y o k uo ne s ha
sisi ni watu wajinga,
watu tunaotumiwa kwa
kuongozwa na kuburuzwa.
Hamtaki hata haki ya
kuishi hata mtu kuishi
hataki basi kila kitu hapana
tu, alisema mmoja wao
(jina nalihifadhi).
Wa j i n g a wa n a m j i
wao tutawaonesha hawa
wanaosema hapana ni
watu wenye kutumiwa
na wakoloni wanatumiwa
na Waarabu na wengine
hapa wala sio kwao, kwao
ni Oman lakini hii katiba
itapita mtake msitake hizo
Inaendelea Uk. 14
12
MAKALA/SHAIRI
Inatoka Uk. 10
AN-NUUR
Na A.S Chachika
SHEIKH Mohammed
Idd, maarufu kama
Abuu Idd, amefungulia
m wa n g wi ili sa u ti
ambayo ilikwisha
toka kwa kupitia
vinywa anuai kuhusu
BAKWATA, kuwa ni
kikwazo kikubwa kwa
maendeleo ya Uislamu na
Waislamu. Aliyoyasema
Sheikh ni yale yale
yaliyokuwa yanasemwa
na Waislamu wote wenye
kuguswa na vikwazo
vinavyofanywa na
Taasisi inayojinasibisha
na uongozi na
uendelezaji wa Uislamu
na Waislamu nchini
Tanzania.
Amenukuliwa na
An-nuur, No. 1156
ya Desemba 2014,
akidhihirisha yale
yanayomkera, aliyataja
machache ambayo ni
Bakwata Kuhodhi mali
za waqfu na kuzitumia
kinyume na malengo
yake. Jingine alilosema ni
kuwa, Bakwata kukosa
mipango ya maendeleo,
hali inayofanya
Waislamu, wakose dira
na kuvunja umoja wa
Kiislamu kwani yule
aliyejivika ukinara wa
kuongoza, hana mpango
wa mambo ya maendeleo.
Zaidi Abuu Idd, alisema
Bakwata huwasiliana na
na Serikali siku za Idd au
kama wameletewa mbuzi
au Tende kutoka Makka.
Labda tuchukue
fursa hii kumkumbusha
Abuu Idd, kuwa hayo
aliyoyasema ni machache
miongoni mwa mengi
na mazito yaliyokuwa
yamefanywa na Waislamu
wa kada mbalimbali
na kwa nyakati tofauti
z a wa t u ( Wa i s l a m u )
walipofunuliwa na
k u e l e wa u k i r i t i m b a
wa Bwakata dhidi ya
Uislamu na Waislamu.
Hivyo haya aliyoyataja ni
mwangwi (Echo).
Moja ni ile ya Mufti
wa B a k wa t a , S h e i k h
Simba, aliyoitoa Jijini,
Tanga, mnamo Juni 30,
2007, katika sherehe
ya kutimiza miaka 50
ya Taasisi ya TAMTA.
13
SIKU moja baada ya
kupiga kura ya hapana kila
mmoja wetu alikabiliwa
na vitisho na matusi
mbalimbali, lakini kila
mmoja alisimama imara
hadi dakika za mwisho.
Hakuna aliyetetereka na
kubadilisha msimamo
wake, zaidi ya watu 14
walikuwa na msimamo
wa kuikataa rasimu yote
lakini kutokana na khofu
wakaanza kupungua na
kuamua kupiga kura za
siri.
Kulikuwa na vikundi
vidogo vidogo vikitujadili
tuliokubali kupiga kura ya
HAPANA kwa njia ya wazi
kuwa eti si wazalendo
na nikitangazwa mimi
kuwa ndio Public Enemy
Number One, lakini hilo
katu halikunitia khofu
wala kunivunja moyo
kwa kuwa nilijua mambo
kama hayo yatanikuta na
nilijitayarisha kuyapokea
na kuyakabili kwa hali
yoyote.
Ingawa wajumbe
wengi waliotoka Zanzibar
walikuwa wana msimamo
kama wetu wa kupiga
kura ya hapana kuanzia
sura ya kwanza hadi
sura ya 19 na ibara zake
zote, lakini hawakuwa na
uwezo wa kutetea uamuzi
wao huo kwa kupiga
kura ya wazi kutokana
na ushawishi, vitisho
na khofu za kuogopa
kupoteza kazi zao, nafasi
z a o n a wa p o a m b a o
walikuwa wakiona muhali
kupiga kura ya wazi kwa
sababu tu wamekuwa na
maelewano ya karibu na
baadhi yao katika kipindi
chote cha bunge na baadhi
ya wale watu ambao wana
mitazamo tofauti.
Mimi nipo pamoja na
nyie lakini kwa kweli nikiri
kwamba siwezi kupiga
kura ya wazi kwa sababu
tumeshakaa na hawa watu
na wananiamini sana
kwamba mimi ni mwenzao
sasa nikipiga kura ya wazi
nitawavunja moyo sana
lakini niaminini kwamba
mimi sijapokea pesa na
hata kama nimepokea,
nitapiga kura ya hapana,
alisema mmoja wa
wajumbe walopiga kura
ya siri.
Kilichotokea ambacho
wengi hawakijui, wajumbe
wengi, viongozi wengi
wa l i h a d a i k a n a wa l e
wachache waliomo
katika kamati zetu 12
kukubaliana na maoni ya
wengi na hivyo kuona
idadi ya wanaopingana
na rasimu hii ni wachache,
lakini walisahau kwamba
n d a n i ya k wa m f a n o
kulikuwa na wajumbe
Makala
AN-NUUR
ya kuombwa awakutanishe
alishindwa kabisa kuwaita
Wazanzibari na kukaa nao
pamoja ingawa baadhi
yao walipenda iwe hivyo
akiwemo aliyekuwa
Mwanasheria Mkuu wa
Zanzibar, Othman Masoud
Othman na baadhi ya
wajumbe wa CCM.
Na hilo la kukaa kama
Wazanzibari lilianzia
ndani ya kikao cha Baraza
la Wawakilishi ambapo
Mwakilishi wa Jimbo la
Mji Mkongwe, Ismail Jussa
Ladhu alitaka kujua iwapo
Wazanzibari wanakwenda
kwenye bunge la katiba
wanakwenda kama nani,
Wa z i r i wa S h e r i a n a
Katiba, Abubakar Khamis
Bakary alisema yeye kama
Abubakar angependa
kuona wanakwenda
kama Wazanzibari na
sio kama CCM au CUF.
Lakini kwa bahati mbaya
sana aliposimama kuja
kufunga kikao hicho,
Balozi Seif alisema serikali
haina msimamo, na kauli
hiyo ndio iliyokwenda
kuharibu na kuathiri
m a m b o n a u m o j a wa
Wazanzibari kule bungeni.
K a b l a y a U K AWA
kutoka nje ya bunge,
juhudi za kuwakutanisha
Wa z a n z i b a r i p a m o j a
zilifanyika kupitia
wajumbe kutoka CCM na
CUF kumuendelea Balozi
Seif na kutaka wakae
pamoja kuzungumzia
maslahi ya Zanzibar,
lakini bahati mbaya zilifeli
katika hatua za mwanzo
kwa kuwa hakukuwa
na dhamira ya dhati ya
kuitetea Zanzibar ndani ya
katiba hii.
Hatimae Wazanzibari
wakawa wanakwenda
katika vikao vya kamati
hawana kitu mkononi
kama walivyojipanga
wenziwao; na matokeo yake
wakawa wanaandikiwa
baadhi ya mapendekezo
wakipewa wayasome na
wao wanayasoma lakini
wakiambiwa wayatetee
au kuyatolea ufafanuzi
h a wa we z i k wa k u wa
hawajaandika wao.
Kwa hakika ilikuwa
ni mambo ya aibu na
kujifedhehesha kama
Wazanzibari. Yalitamkwa
mengi na wenzetu wa
Bara, lakini tukistahiki
matusi hayo.
Wapo watu wengine
wa l i k u wa wa k i d h a n i
pesa ndio iliyowahadaa
Wazanzibari na kukubali
kupitisha mambo kirahisi.
Ukweli ni kwamba sio
pesa peke yake, kulikuwa
na hila na mbinu chafu na
hadaa ikifuatiwa na chuki
ndani yake ambayo kwa
kiasi kikubwa imechangia
ukubwa na ubabe wa
mkubwa dhidi ya mdogo
na hata wale waliokuwa
wana msimamo wa
kuitetea Zanzibar
walifunikwa katika
kichaka cha chama na
matokeo yake wakajiona
wanafuata mkumbo wa
kuhofia kuwajibishwa
na hivyo hisia zao za
uzalendo zikafichika ndani
ya kichaka hicho.
Sisi tulitakiwa tukae
kama Wazanzibari na
sio kama CCM na CUF
kwa sababu tushaingia
katika vikao hivyo
lakini hivyo vikao ni vya
chama bara na Zanzibar
lakini tunapotoa hoja ya
Zanzibar tu tunaonekana
kama wasaliti kama
ilivyojitokeza kwenye
Kamati ya Uongozi,
ukiongea kitu ukanukuu
Katiba ya Zanzibar unapata
upinzani mkali kutoka kwa
wenzetu, lakini ukichukua
nukuu hiyo hiyo ukaisema
itachukuliwa kama
hujaitaja Zanzibar,
alisema mmoja wa
wajumbe wa CCM ambaye
ni mjumbe wa kamati ya
uongozi.
Pia ningependa
kugusia kidogo namna
Mwanasheria Mkuu,
Othman Masoud
alivyokaangwa kuanzia
ndani ya kamati yetu na
baadae kikao cha pamoja na
mawaziri na watani wake
walivyoshiriki kummaliza,
ujasiri na msimamo
wake madhubuti juu ya
Zanzibar na hatimae kura
yake HAPANA.
Othman alianza
kupingwa ndani ya
kamati yake namba 11
ambapo Mwenyekiti
wake ni Anna Kilango
na Makamo Mwenyekiti
wake ni Hamad Masauni,
wakati Othman akitoa
mapendekezo yake,
baadhi ya wabunge kutoka
Bara walisema kimsingi
wanaona mapendekezo
yaliyotolewa na Othman
yana mantiki na baadhi
yake wanakubaliana nayo
na pia yanabeba msimamo
wa serikali, lakini mjumbe
mmoja kutoka Zanzibar,
Mbunge wa viti Maalum
CCM, alipingana na
wajumbe wenzake wa
CCM.
Othman ni mjumbe
kama wajumbe wengine
na mawazo yake
yasichukuliwe kama yeye
anaiwakilisha serikali
k wa h i v y o n a i k i wa
yeye ni mwanasheria wa
serikali, basi yeye Othman
anaunga mkono serikali
ya shirikisho haya basi
tumfateni eeeeh si mnataka
kuchukua maneno yake,
alisema Mjumbe huyo kwa
kebehi.
Ningeandika maneno
machache sana kabla ya
kumalizia yanayomkhusu
rafiki yangu wa karibu
sana asiye mwanasiasa,
ni mtu mwenye misingi,
mtu mwenye uchungu
na nchi yake, mwenye na
msimamo mzuri sana na
mwenye uadilifu wa hali ya
juu sijawahi kusikia kama
amewahi kuburuzwa au
kumfuata mtu kwa kile
asichokiamini lakini kwa
hili aaaah sikutarajia hata
siku moja kama ataweza
kwenda kinyume na
u a d i l i f u wa k e k a t i k a
utendaji wake wa kazi.
Aaaaaaah siamini sikubali
na sitaki kusikia kama
yeye ndio aliofanikisha la
kupatikana 2/3? No siamini
kama ni madaraka siamini
kama ni fedha na siamini
kama nguvu zilizomfanya
atende asichokiani. Ipo
siku nitamsuta japo sio
Inaendelea Uk. 14
14
Makala
AN-NUUR
Inatoka Uk. 11
kura zenu za hapana ni
bure tu, alisikikia akisema
m w i n g i n e a m b a ye n i
Mbunge (CCM) akihama
kutoka alipokuwa na kuja
tulipokaa sisi.
M h e s h i m i wa Ya h ya
Kassim Issa, Mbunge
wa Chwaka na wenzake
walioniomba nipige
kura ya NDIO ambapo
Dk. Mwinyihaji Makame
Mwadini aliuliza iwapo
kama hatujaona jambo zuri
hata moja katika rasimu
iliyopendekezwa hata
tupige kura ya HAPANA
lakini jibu letu lilikuwa
wa k e n a n d i o m a a n a
alithubutu kunikabili
n a k u n i e l e z a wa k a t i
wenzake wakiniona kama
n i a d u i wa o , i n g a wa
baadhi wanamlaumu kwa
nini na yeye asichukue
uamuzi mgumu? Wengi
hawajamfahamu lakini
mimi nimemfahamu sana
kutokana na uamuzi wake
huo.
Natamani nivute
kumbumbuku pale dakika
chache kabla ya kura ya
HAPANA siku ya kwanza
ambayo alianza kupiga
Adil Mohammed Ali
akifuatiwa na Dk. Alley
Soud, akaja Ali Omar,
Fatma Mohammed na Bi
Jamila Abeid na baadae
mimi na hatimae kura
ya mwisho ambaye
ikitarajiwa kupigwa na
Mwanaidi Othman lakini
muda mfupi aliondoka
na kwenda chooni
akitujulisha kwa simu
ya m k o n o n i k wa m b a
Siwezi kupiga kura ya
wazi nitapiga kura ya siri
na kisha aliondoka katika
sehemu ambayo alikuwa
amekaa na kwenda kukaa
kwenye kiti akiwekwa
kati kati upande mmoja
akiwa ameketi Mwana na
upande mwengine akiwa
ameketi Mahmoud Thabit
Kombo.
Lakini mwisho alipiga
kura ya wazi na kusema
HAPANA na baada ya
kura 7 za hapana hapana
zilivyoanza kujipanga
kura ya mwisho namna
ilivyopatikana katika
tundu ya shindano kwa
mikiki, vitisho, dharau,
khofu, kulazimishwa na
kutekwa nyara na matusi
ya nguoni lakini pamoja
na yote hayo kura saba
zilipiga HAPANA na
ndio mwisho wa mchezo.
(Salma Said)
15
Makala
AN-NUUR
Na Ally Saleh
N I M E WA H I k u s e m a
kuwa kuna haja kubwa
ya kutumika busara ili
Kura ya Maoni isifanyike
kabisa mwaka huu na
niliungana na wale
waliokuwa na fikra kama
hiyo, hadi pale wenzangu
walipobadilika.
Walibadilika kwa sababu
walikuwa na lengo la
kisiasa. Walichukulia
fursa ya kufanyika Kura
ya Maoni na ushindi
utaopatikana kama ikipita
ni sawa na kukifyagilia
njia Chama cha
Mapinduzi kwa ushindi
wa Uchaguzi Mkuu kote
Bara na Zanzibar.
Hoja yangu wakati huo
ilikuwa ni kuwa Kura ya
Maoni kwa hadhi zote ni
sawa na Uchaguzi Mkuu
maana huwa na kipindi
cha elimu ya mpiga kura,
kisha huwepo na kampeni
na kuwepo pande
zinazopingana katika
hicho kinachopigiwa kura
na kwa hili la katiba, ni
dhahiri kutakuwa na kazi
kubwa. Kazi kubwa maana
yake pande zinazotaka
katiba ipite na isipite zote
zimeshanowa visu kwa
ushindani mkali na bila ya
shaka kutapelekea kuwepo
mvutano, uhasama na
pengine hata magomvi
ambayo huambatana na
uchaguzi katika mazingira
yetu ya Kiafrika zaidi.
Wasiwasi wangu ni
kuwa kunaweza kukawa
na chaguzi nne katika nchi
kwa mwaka mmoja kwa
maana ya Kura ya Maoni
ya April 30 na iwapo
itarudiwa kwa kupigwa
H A PA N A m a r a y a
kwanza. Kisha kufuatiwa
na Kura ya Maoni ya
Wazanzibari kupitisha
hiyo Katiba Pendekezwa
na mabadiliko yake kwa
Katiba ya Zanzibar ya 1984
na kisha Uchaguzi Mkuu
wa 2015 mwezi Oktoba.
Naionea huruma sana
Zanzibar yangu ambayo
itakuwa na chaguzi zote
lolote linalofanyika
la kuutia umma imani
kuwa kweli kuna mambo
yanayotoka au pengine ni
kwa sababu ya usiri? Jee
umma unaweza kuwekwa
nje ya kujua jambo hili kwa
kiasi chote hiki?
Kwa sababu hizo basi,
ndio kukaanza kuzuka
kundi jengine kabisa, na
khasa Umoja wa Katiba ya
Wananchi UKAWA ambao
umekuja na mpya kuwa
wao wanasusia kabisa
mchakato kupita Kura ya
Maoni kwa sasa sababu
k u wa h a k i t a p a t i k a n a
kilichokusudiwa. Wao
wanaona, hasa kwa vile
waliukimbia mchakato
huo katika Bunge Maalum
la Katiba, kuwa hapana
liwalo na Kura ya Maoni
haina tija kwa aina ya
k a t i b a i n a y o p e l e k wa
k wa wa n a n c h i ya a n i
i l e i n a y o i t wa K a t i b a
Pendekezwa ambayo ni
shikilia la Rais Kikwete
na Chama cha Mapinduzi.
Pili, wanaona ni haramu
kitu ambacho walikikataa
katika utengejezaji wake
kisha warudi wakipigie
kura kukihalalisha.
Wanasema hiyo abadan
na tayari wamewataka
wanachama wao na
wanachi wasusie kura
hiyo. Taasisi nyengine
pia kama Kituo cha Haki
za Binadamu (HRLC)
wa m e t o k a wa z i wa z i
wakisema katiba hiyo
haifai kupigiwa kura ya
kuungwa mkono ingawa
wao wanataka wananchi
wakapige kura na waikatae
Katiba Pendekezwa.
Mimi kama Mzanzibari
nataka nijihusishe zaidi
na ubaya wa Sheria ya
Kura ya Maoni ambayo
ndio inayoongoza taratibu
nzima za kura hiyo na
a mb a y o i n a madh a r a
makubwa kwa Zanzibar.
Kwa mujibu wa Kifungu
cha 34 cha Sheria hiyo, kura
za upande wa Zanzbar,
ambapo kila upande ili
kura zipige itahesabiwa
kwa zaidi ya asilimia
16
Makala
AN-NUUR
Inaendelea Uk. 17
17
Makala
AN-NUUR
Na Mohammed Ghassani
I J U M A A ya l e o , R a i s
Joachim Gauck wa
Ujerumani na ujumbe
wake wanaondoka kurejea
kwao baada ya kuwepo
ndani ya ardhi ya Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania
tangu usiku wa Jumatatu,
tarehe 2 Februari.
Pale uwanja wa ndege wa
kimataifa wa Mwalimu Julius
Nyerere, Dar es Salaam,
ujumbe huo ulipokelewa
kwa matarumbeta na ngoma
nyengine za kienyeji. Siku
ya pili yake alipokelewa
rasmi na mwenyeji wake,
Rais Jakaya Kikwete kwenye
Ikulu ya Magogoni, ambako
mbali ya matarumbeta ya
bendi ya jeshi, gwaride na
mizinga 21 kwa heshima
ya kiongozi wa nchi,
uwanja mzima wa Ikulu
hiyo ulitanda matarumbeta
mengine.
Wa k a t i m k e w e R a i s
Gauck, Bi Daniela Gauck,
alipotembelea kituo cha tiba
cha CCBRT kilicho kando
kidogo ya kitovu cha jiji la
Dar es Salaam, wagonjwa
wa fistula wanaotibiwa
huko walikuwa na muda
pia wa kumuimbia nyimbo
mwanamke mwenzao huyo,
wakisema Sisi ni tegemeo la
akinababa, sisi ni tegemeo la
watoto. Sisi ni tegemeo.
Usiku wa tarehe 3
Februari, Rais Kikwete na
mkewe, Bi Salma Kikwete,
waliwakaribisha tena
wageni wao Ikulu kwenye
chakula cha jioni. Ndani ya
ukumbi muliporomoshwa
muziki mkali wa bendi ya
polisi. Wakati wageni hao
wanaondoka kurudi hotelini
kwao saa 4:00 usiku, nje
kulikuwa na vikundi vya
ngoma za kienyeji kuwaaga.
Wa k a t i wa n a o n d o k a
siku ya Jumatano kuelekea
Zanzibar kwa boti ya Azam
Marine, bandarini palikuwa
n a b e n d i n ye n g i n e ya
matarumbeta ikitumbuiza
kwa zogo na shangwe.
Wi m b o K i t o r o r o wa
msanii nyota wa Tanzania,
Naseeb Abdul, maarufu
kama Diamond Platinumz.
Zanzibar na Arusha
nako hali haikuwa tafauti.
Kulikuwa na ngoma wakati
wa kuwasili na ngoma
wakati wa kuondoka. Kwa
makisio tu, hadi Rais Gauck
n a w e n z a k e wa n a r u d i
Ujerumani, baada ya kuwepo
Tanzania kwa siku zisizozidi
tano, tayari walishapigiwa
ngoma zaidi ya mara saba.
Wa l a u j u m b e wa
Rais Gauck si pekee
unaokumbana na ukarimu
huu wa kukatikiwa mauno.
Ni utamaduni mkongwe
ambao sasa unahitaji
kuhojiwa kwa sababu sio tu
unaudhi, bali pia unabeba
maana kadhaa zisizosema
uhalisia ulivyo.
Rais Joachim Gauck wa Ujerumani na ujumbe wake wakiondoka kurejea kwao baada
ya kuwepo nchini. Hapa wakiwa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu
Julius Nyerere, Dar es Salaam ambapo ujumbe huo ulipokelewa kwa matarumbeta
na ngoma nyengine za kienyeji.
Kitamaduni na kijamii,
nafahamu kwamba
kwetu Waafrika ngoma
si kielelezo cha mikatiko
na minyumbuliko ya miili
yetu tu, bali pia njia ya
mawasiliano. Hata hivyo,
ninaamini kuwa nyuma ya
ngoma zinazotayarishwa,
kulipiwa na kushajiishwa
na dola kuchezwa mbele ya
wageni kutoka nje, ujumbe
unaotumwa una maana
mbaya sana.
Chukulia mfano huu
halisi. Dhamira ya ziara ya
Rais Gauck nchini Tanzania
ilikuwa na dhamira mbili
kuu: moja ya kisiasa na
nyengine ya kiuchumi.
Sikiliza hotuba yake, angalia
maeneo waliyoyatembelea,
u t a j u a k u wa wa l i k u wa
wamekuja kwa lengo
maalum na lenye uzito wa
aina yake. Mikutano ya
wafanyabiashara wa pande
mbili iliyoangalia fursa za
uwekezaji, mazungumzo na
asasi za kijamii, waandishi
wa habari, wanasiasa na
wanasheria. Ujumbe huu
una ujumbe ndani yake.
Ongeza ukweli mmoja
mchungu sana pia.
Ujerumani ilikuwa mkoloni
wa Ta n g a n y i k a n a i n a
historia refu inayorudi
nyuma kwenye majilio ya
wakoloni kwenye ardhi hii
yenye wingi wa rasilimali
tangu mwishoni mwa
karne ya 19 kupitia wale
waitwao wavumbuzi na
wamishionari. Miongoni
mwa upotoshaji uliomo
kwenye historia ya
kimapokezi ni kwamba
wahenga wa Kitanganyika
waliweza kudanganywa
na wavumbuzi akina
Karl Peters wa Ujerumani
wakawapa ardhi na
rasilimali zao kwa shanga
n a s i g a r a , wa k a t i wa o
wakicheza ngoma na
kufanya matambiko.
Si lazima upotoshaji huu
uwe na ukweli wa asilimia
Inatoka Uk. 16
kikuu kinachowakilisha
chombo kinachowakilisha
Waislamu wote. Hili ni
kosa kubwa kwa kuwa
BAKWATA siyo chombo
cha Waislamu wote nchini.
8. K u n a m a t a m k o
yametolewa na taasisi
na watu binafsi ambao
wa n a t u m i a m u s wa d a
huu wa Mahakama
ya K a d h i k u l e t a h o j a
zinazokusudia kuleta
faraka za kimadhehebu
kwa propaganda ambazo
hazina msingi au ukweli
wowote katika dini ya
Kiislamu hasa suala la
kupinga Mufti kuwa ndiye
mteuzi wa makadhi na
utengenezaji wa kanuni
za Mahakama ya Kadhi.
Tunaotoa udhaifu wa
kumpa madaraka hayo
Mufti tumezingatia
hoja za kisheria, kidini
na kimantiki. Hivyo si
kweli kuwa tunapinga
Mufti kupewa madaraka
hayo kutokana na tofauti
za madhehebu ndani ya
Uislamu. .
9. Kadhalika, wapo
viongozi wa dini ambao
s i Wa i s l a m u ( m f a n o
maaskofu) wametoa
m a t a m k o ya k u p i n g a
M a h a k a m a ya K a d h i
kwa hoja kuwa italeta
hukumu za kukata
mikono, kuhukumu wasio
kuwa Waislamu, kubagua
wasio kuwa Waislamu
nk. Hoja hizo zote siyo
za kweli na watoaji wa
hoja hizo wanajua ukweli
k u wa M a h a k a m a ya
Kadhi inayokusudiwa ni
mahakama itakayotumia
sheria za Kiislamu ambazo
zinatumika kwenye
mahakama za kawaida
toka enzi za ukoloni
mpaka leo. Inajulikana
wazi kuwa Mahakama
ya Kadhi itas hughulika
na mambo binafsi ya watu
kwa mujibu wa sheria za
Kiislamu ambazo ni sehemu
ya sheria halali zinazotumika
hapa nchini, mfano mambo
kama ndoa, talaka, mirathi,
wakfu na malezi ya watoto.
Kinachofanywa na viongozi
hao wa dini wasiokuwa
Waislamu ni kuivunjia
heshima jamii ya Kiislamu
na kupotosha ukweli ambao
uko wazi.
Sheikh Abdallah A.
Bawazir
Makamu Mwenyekiti
wa Hay Atul -Ulamaa
03/02/2015
18
Na Shaban Rajab
HIVI karibuni vyombo
mbalimbali vya habari
duniani vilitangaza tukio
la kukamatwa kamanda
wa kikundi cha waasi cha
Uganda cha Lord Resistance
Army (LRA), Bw. Dominic
Ongwen. Hata hivyo
taarifa zimesema kuwa
hivi karibuni Bw. Ongwen,
alijisalimisha mwenyewe
kwa vikosi maalum vya
majeshi ya Umoja wa Afrika
vinavyosimamia amani
Jamhuri ya Afrika ya Kati
Januari 17 na Jumamosi,
alikabidhiwa kwa
Mahakama ya Kimataifa
ya Jinai za Kivita The
Hague, kwa ajili ya kusubiri
mashitaka dhidi yake.
Dominic Ongwen,
ameelezwa kuwa alikuwa
msaidizi wa Bw. Joseph
Kony, Kamanda Mkuu wa
kundi la waasi la Kikristo
linaopigania serikali
inayosimamia amri kumi za
Biblia (LRA) nchini Uganda.
Imefahamika kuwa baada
ya kujisalimisha, Bw. Ongwen
alidai aliamua kufanya hivyo
baada ya bosi wake Bw.
Kony, kubaini kuwa alikuwa
na nia ya kujisalimisha kwa
serikali ya Uganda, ambayo
awali ilitangaza msamaha
kwa wanachama wa LRA
watakaojisalimisha kwa
hiari.
Vyombo vya habari vilidai
kuwa alifanya hivyo baada ya
wapiganaji watiifu wa Kony,
kumweka chini ya ulinzi
huku wakimtesa ili abadili
nia yake ya kujisalimisha na
kwamba, iwapo angeendelea
na msimamo wake huo basi
angeuliwa.
Aidha alinukuliwa
akisema kuwa hata yeye
aliingia katika himaya ya
Kony baada ya kutekwa
akiwa mtoto ndogo.
O
n
g
w e
n
a m e s h a k a b i d h i wa T h e
Hague akisubiri kukabiliwa
na tuhuma za kutenda jinai
za kivita, mauaji ya halaiki
kwa raia, utumwa na jinai
dhidi ya binadamu. Tayari
imeripotiwa kuwa mawakili
zaidi ya 30 wamejitokeza
kutaka kumtetea katika kesi
itakayomkabili.
Mwaka 2005, ICC ilitoa hati
ya kukamatwa makamanda
watano wa kundi la LRA,
akiwemo Dominic Ongwen.
Bado operesheni za kumsaka
Joseph Kony, ambaye
anadiwa kujificha huko
Jamhuri ya Afrika ya Kati
zinaendelea.
Waasi wa Kikristo wa
Lord's Resistance Army huko
Kaskazini mwa Uganda,
ambao wamekithiri kutenda
jinai dhidi ya raia wasio na
hatia hasa watoto, awali
walianza uasi dhidi ya
serikali ya Kampala mwaka
1980.
Pamoja na kutenda jinai
za kutisha kwa muda mrefu
dhidi ya watu wasio na
hatia hasa katika maeneo
ya Kaskazini mwa Uganda,
kufanya mauaji ya halaiki kwa
AN-NUUR
Makala
19
Makala
AN-NUUR
AN-NUUR
20
MAKALA
20
Na Bakari Mwakangwale
AMALI
njema
kwa mwanadamu
alizochuma kabla ya
kufikiwa na umauti,
ndizo zitakazo mfaa
katika maisha yake ya
kaburini.
Hayo yamesemwa
na Ustadhi Saidi
Juma, akiwahutubia
Waislamu katika hotuba
ya swala ya Ijumaa ya
wiki iliyopita katika
Msikiti wa Taqadir,
Mwendapole, Wilayani
Kibaha.
Ust. Juma, alisema
mwanadamu anatakiwa
kutengeneza akhera
kwa kuwa ni ya kudumu
kuliko kutengeneza
maisha ya dunia,
ambayo ataiacha muda
wowote.
U s t .
J u m a
akisherehesha hadithi ya
Anas Ibn Malik, alisema
Mtume (s a w) ameeleza
kuwa atakapofariki
mwanaadamu,
atasindikizwa na
mambo matatu kwanza
ndugu zake, mali zake,
kisha amali zake.
Lakini, akasema kwa
mujibu wa hadithi hiyo,
katika hivyo vitatu,
viwili vitarudi baada ya
mwanaadamu kuzikwa
kwani havina uwezo wa
kuingia alipoingizwa
mwanaadamu huyo.
Akasema hadithi hiyo
inabainisha kuwa amali
njema alizozichuma
mtu huyo akiwa hai
ndizo atakazo baki nazo
akitiwa kaburini na
ndizo zitakazo msaidia
kwa muda wote mpaka
pale Allah (s w) atakapo
simamisha kiama.
Ndugu zetu, wake
zetu, watoto wetu hata
wakilia na kujigaragaza,
l a k i n i h a wa t a k u wa
na uwezo wa kuingia
kaburini kukusaidia,
kwani wataishia katika
kizingiti cha kaburi.
Huenda ndugu
akawa na uwezo wa
kumnufaisha ndugu
yake katika ardhi
Soma
gazeti la
AN-NUUR
kila Ijumaa
(maisha yake ya
dunia) na kusahau
(kuiandaa) akhera
yake ili hali Mwenyezi
Mungu, amemuasa
M w a n a d a m u
awe makini na
kutodanganyika na
maisha ya dunia kwani
maisha ya akhera ni
yenye kudumu.
Ewe Mwanaadamu
kuwa mwepesi katika
AN-NUUR
k u ya e n d e a m a m b o
mazuri na kuwa pamoja
na wale waendao mbio
miongoni mwa wale
wanaoipigania akhera
zaidi kwani mali na
ndugu hivyo ni amana
tu na ipo siku amana
hiyo itarudi kwa
mwenyewe. Alisema.
Ust. Juma, akawataka
Waislamu kuitumia
fursa ya uhai wao wa
Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na POA Printing Works LTD, S.L.P. 4605, Dar es Salaam.