Вы находитесь на странице: 1из 1

1

STATE HOUSE ZANZIBAR


OFFICE OF THE PRESS SECRETARY

PRESS RELEASE
Zanzibar 12. 08 .201 7

RAIS wa Zanzibar na Mwenye kiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed


Shein , a metoa pongezi kwa Bodi y a Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) , Wizara
ya Fedha na Mipango pamoja na uongozi wa B enki hiyo kwa mafanikio iliyoyapata
na kuitaka kujiendesha kibiashara ili ipate kuimarika zaidi .

Dk. Shein aliyasema hay o, alipokutana na U ongozi wa Wizara ya Fedha na Mi pango,


Bodi ya Wakurugenzi ya Bodi ya Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ), pamoja na
uongozi wa Bodi ya PBZ katika vikao vinavyoendelea Ikulu mjini Zanzibar.

Katika vikao vya leo, Dk. Shein kwa nyakati tofauti alikutana na Uongo zi wa Wizara
ya Fedha na Mipang o, Bodi ya Wakurugenzi ya PBZ na uongozi wake pamoja na Bodi
ya Wakurugenzi ya Shirika la Bima na uongozi wake .

Aidha, Dk. Shein alieleza kuwa licha ya changamoto zilizojitokeza lakini Benki hiyo
imeweza kupata mafanikio makubwa na kusisitiza haja ya kuw epo kwa mashirikiano
ya pamoja hatua ambayo itasaidia kuiendeleza Benki hiyo.

A kitoa maelezo yake Dk. Shein alisema kuwa wafanyakazi Benki hiyo ni lazima
wafuate maadili, sheria na taratibu za kazi na kuutaka uongozi kuwapongeza kwa
wale wana ofanya vizuri .

Waziri wa Wizara ya Fedha na Mipango Dk. Khalid Mohamed alitoa pongezi k wa Rais
Dk. Shein kwa miongozo anayoitoa kwa Wizara hiyo na kupongeza hatua zilizofikiwa
na PBZ kwa kumiliki asilimia 41 ya mikopo kwa Soko la Mabenki hapa Zanzibar kwa
mwaka 2016 ha tua ina yoonesha jinsi Benki hiyo inavyoaminiwa.

Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi Dk. Abdulhamid Yahya Mzee
kwa u pande wake ali toa pongezi kwa hatua kubwa iliyofikiwa na Benki hiyo sambamba
na ku sisitiza haja kwa Benki hiyo kuwa Serika li ina matumaini makubwa n a chombo
hicho kwani ni chanzo kimojawapo cha kuiongezea mapato yake.

Вам также может понравиться