Вы находитесь на странице: 1из 19

SALA YA EKARISTI I

Sala ya Ekaristi ya Kwanza, yaani Kanuni ya Kirumi, inaweza kutumiwa


Sikuzote. Lakini inafaa zaidi itumike siku ambapo inasemwa Tunashirikiana
Ya pekee, au katika Misa inaposemwa Kwa hiyo ya pekee.

Sala ya Ekaristi I yafaa isemwe pia katika sikukuu za Mitume na Watakatifu


Wanaotajwa katika sala hii, na katika Misa za Jumapili, isipokuwa
Kama inafaa isemwe sala nyingine yaa Ekaristi kwa sababu fulani za kichungaji.

Sehemu fulani za sala hii zinaweza kuimbwa; nazo ni kuanizia Ewe Mungu
Tunakuomba mpaka tujazwe kila baraka na neema ya mbinguni.
Doksolojia ya mwisho inaweza kuimbwa pia.

Sehemu za sala ya Ekaristi zinazosemwa na wakonselebranti wote pamoja


Zisemwe jinsi sauti ya kiongozi wao isikilike zaidi kuliko sauti za wenzake.
Kwa hiyo wat wataweza kusikia vizuri zaidi maneno yasemwayo.

Anafumbua mikono CP
Ee Baba mwema, Wakoselebranti
Wanafumba
tunakusihi kwa unyenyekevu, Mikono.
na kukuomba kwa njia ya Yesu Kristu Mwanao, Bwana wetu,
uzipokee na kuzibariki dhabihu hizi takatifu,

tunazokutolea kwa ajili ya Kanisa lako takatifu katoliki;


ukubali kuliletea amani na umoja,
kulilinda na kuliongoza po pote duniani;

tunakotolea pia
kwa ajili ya mtumishi wako Baba Mtakatifu wetu F.
na Askofu wetu F.
Nao wote wenye kushika imani katoliki ya Mitume.

Ee Bwana, uwakumbuke watumishi wako F. Na F. C1


Anafumba mikono anasubiri kidogo- anafumbua mikono:

na wote waliopo hapa;


wewe wajua imani na ibada yao.
Kwa ajili yao tunakutolea sadaka hii ya kukusifu;
nao wenyewe wanakutolea sadaka hiyo
kwa ajili yao na jamaa zao,
ili waokoke
na tumaini lao la kupata uzima na usalama litimie.

Ndivyo wanavyokuomba wewe,


Mungu wa kweli, Mungu wa milele.

TUNASHIRIKIANA ZA PEKEE
Noeli na oktava yake:

Tunashirikiana kuadhimisha ile siku takatifu,


(ule isiku mtakatifu)
Maria mweye heri daima Bikira
alipoizalia dunia hii Mkombozi.
Tena tunamheshimu kwanza huyo Maria mtukufu
daima Bikira,
Mama wa huyo Yesu Kristu Mungu Bwana wetu.-

Epifania:
Tunashirikiana kuadhimisha ile siku takatifu,
Mwanao wa pekee aliopotokea na kuonekana mtu
kama sisi.
Ndiye Mwanao aliye milele pamoja nawe katika
utukufo wako.
Tena tunamheshimu kwanza Maria mtukufu
daima Bikira,
Mama wa huyo Yesu Kristu Mungu Bwana wetu.-

Vijilia ya Paska, Paska na Oktava yake:


Tunashirikiana kuadhimisha ile siku takatifu ya
(ule isiku mtakatifu wa)
kufufuka kwake Bwana wetu Yesu Kristu.
Tena tunamheshimu kwanza Maria mtukufu
daima Bikira, Mama wa huyo Yesu Kristu Mungu Bwana wetu.-
Kupaa Bwana:
Tunashirikiana kuadhimisha ile siku takatifu,
Mwanao wa pekee Bwana wetu alipopaa mbinguni,
akakaa kuume kwako, akautukuza abinadamu wetu.
Tena tunamheshimu kwanza Maria mtukufu
daima Bikira
Mama wa huyo Yesu Kristu Mungu Bwana wetu.-

Pentekoste:
Tunashirikiana kuadhimisha ile siku takatifu ya
Pentekoste,
Roho Mtakatifu alipowatokea Mitume katika ndimi
za moto.
Tena tunamheshimu kwanza Maria mtukufu
daima Bikira
Mama wa huyo Yesu Kristu Mungu Bwana wetu.-

Tunashirikiana kumheshimu kwanza C2

Maria mtakatifu
daima Bikira,
Mama wa Yesu Kristu Mungu Bwana wetu.
Halafu tunamheshimu Yosefu mwenye heri,
mume wake huyo Bikira,
na Mitume na Mashahidi wako wenye heri Petro na Paulo, Andrea,
( Yakobo, Yohane, Toma, Yakobo, Filipo, Bartolomeo,
Mateo, Simoni na Tadeo, Lini, Kleti, Klementi, Sisti,
Korneli, Sipriano, Laurenti, Krisogoni,
Yohane na Paulo, Kosma na Damiano)
na Watakatifu wako wote.

Utujalie ulinzi wako


kwa mastahili na maombezi yao,
ili tuwe salama katika mambo yote.
(Tunaomba hayo kwa njia ya Kristu Bwana wetu. Amina. )
CP
Kwa hiyo, ee Bwana,
tunakuomba upokee kwa wema sadaka hii
tunayokutolea sisi watumishi wako na jamaa yako yote.

Tangu Misa ya vigilia ya Paska mpaka jumapili ya pili ya Paska:


tunayokutolea pia kwa ajili ya hao
uliopenda wazaliwe upya kwa maji na
Roho Mtakatifu,
na kuwaondolea dhambi zao zote.

Utujalie amani yako maishani mwetu,


utuepushe na laana ya milele,
utuweke miongoni mwa wateule wako.
(Tunaomba hayo kwa njia ya Kristu Bwana wetu. Amina. )

Anatandaza mikono juu ya mkake na divai : * CC

Ewe Mungu, tunakuomba,


uibariki sadaka hii,
ikupendeze, uipokee,
ili iwe kwetu Mwili na Damu ya Mwanao Bwana wetu Yesu Kristu.

Siku iliyotangulia kuteswa kwake, CC


Anainua kidogo hostia: Wanafumba
mikono.
Yeye alitwaa mkate katika mikono yake mitukufu,
Anatazama juu:
akainua macho mbinguni
kwako wewe Baba yake mwenyezi,
akakushukuru na kukutukuza,
akaumega, akawapa wafuasi wake akisema:
Anainama kidogo. Wananyosha
Twaeni, mle wote: Mikono ya kulia
Kuonyesha hostia.
huu ndio mwili wangu,
utakaotolewa kwa ajili yenu.
Anawaonyesha watu hostia, anaiweka juu ya patena na kupiga goti. Wanatazama
Hostia;
Kisha wanainama
sana.
Vivyo hivyo baada ya kula,
Anashika na kuinua kidogo kikombe.

akatwaa kikombe
katika mikono yake mitukufu,
akakushukuru na kukutukuza,
akawapa wafuasi wake akisema:
Anainama kidogo. Wananyosha
Mikono ya kulia
Twaeni, mnywe wote: Kuonyesha kikombe.

hiki ni kikombe cha damu yangu,


damu ya agano jipya la milele,
itakayomwagika kwa ajili yenu
na kwa ajili ya wengi
kwa maondoleo ya dhambi.
Fanyeni hivi kwa kunikumbuka mimi.
Anawaonyesha watu kikombe, anakiweka juu ya korporale, Wanatazama
na kupiga goti.
kikombe;
Kisha wanainama
sana.
CP
Hili ni fumbo la imani:

Wote: Ee Bwana, tunatangaza kifo chako


na kutukuza ufufuko wako mpaka utakapokuja.
Au :
1. Ee Bwana, kila tunapokula mkate huu
na kunywa kikombe hiki,
tunatangaza kifo chako mpaka utakapokuja.

2. Ee Mwokozi wa dunia, utuokoe,


wewe uliyetukomboa kwa msalaba na ufufuko wako.
Anafumbua mikono: *
CC

Kwa hiyo, ee Bwana,


sisi watumishi wako na taifa lako takatifu
tunakumbuka mateso matakatifu
ya huyo Kristu Mwanao Bwana wetu.

Tunakumbuka pia kufufuka kwake katika wafu


na kupaa kwake mbinguni kwa utukufu.

Ewe Mwenyezi,
kati ya zawadi ulizotujalia
tunakutolea sadaka safi na takatifu,
yaani mkate mtakatifu wa uzima wa milele
na kikombe cha wokovu wa milele.

Uwe radhi kuitazama sadaka hii kwa uso wa rehema;


uipokee
kama ulivyokubali kupolea sadaka ya Abel
mtumishi wako mwaminifu,
na sadaka ya babu yetu Ibrahimu,
na ile sadaka takatifu isiyo na doa
aliyokutolea Melkisedek, kuhani wako mkuu.

Anainama sana, anafumba mikono: *

Ee Mungu Mwenyezi,
tunakuomba kwa unyenyekevu,
umtume malaika wako mtakatifu,
aichukue sadaka hii
na kuipeleka kwenye altare yako mbinguni,
mbele ya uso wako mtukufu.
Nasi tutakaopokea
Mwili na Damu takatifu ya Mwanao
katika altare hii,
Anainuka, anafanya ishara ya msalaba: *
C3
tujazwe kila baraka na neema ya mbinguni. Wanafumba
mikono.
(Tunaomba hayo kwa njia ya Kristu Bwana wetu. Amina. )

Anafumbua mikono:

Ee Bwana,
uwakumbuke pia watumishi wako marehemu F. na F. ,
waliotutangulia wakiwa na ishara ya imani,
wamepumzika usingizi wa amani.
Anafumba mikono anasali kimya kwa muda mfupi anafumbua mikono:

Tunakuomba, ee Bwana,
uwapatie mahali pa faraja, mwanga na amani,
hao na wote wanaopumzika katika Kristu.
(Tunaomba hayo kwa njia ya Kristu Bwana wetu. Amina. )

Anajipiga kifua: *
C4
Nasi pia watumishi wako wakosefu,
tunaotumainia wingi wa rehema zako,
utujalie nafasi
tukae pamoja na Mitume na Mashahidi wako watakatifu:
Yohane, Stefano, Matia, Barnaba,
( Inyasi, Aleksanda, Marselino, Petro, Felisita, Perpetua, Agata,
Lusia, Anyesi, Sesilia, Anastasia)
na Watakatifu wako wote.
Tunakuomba utupokee kwa huruma miongoni mwao
ingawa hatustahili.
Anafumba mikono: CP

Ee Bwana, kwa njia ya Kristu


unaumba daima mema yote,
na kuyatakasa, kuyatia uzima,
kuyabariki na kutujalia sisi.
Anainua hostia na kikombe pamoja, akisema kwa sauti :
PC
Kwa njia yake, pamoja naye, na ndani yake,
Wewe Mungu Baba Mwenyenzi
Katika umoja wa Roho Mtakatifu
Unapata heshima na utukufu wote,
Daima na milele.

Wote: Amina.
SALA YA EKARISTI II

Sala ya Ekaristi ya pili yafaa itumike katika Misa za juma au katika mazingira
ya aina fulani kwa ajili ya maneno yake ya pekee.

Ingawaje sala hii ina utangulizi wake, inaweza kutumika pamoja na


utangulizi mwingine unaoeleza vema fumbo la wokovu, k.m. mmojawapo
ya tangulizi za Jumapili za mwaka au tangulizi za kawaida.

Sehemu fulani za sala hii zinaweza kuimbwa; nazo ni kuanzia Yeye alipojitoa
mpaka ...kusimama mbele yako na kukutumikia. Doksolojia ya mwisho
inaweza kuimbwa pia.

Rubrika zimefupishwa kadiri iwezekanavyo, na zinawahusu mapadre


wanaoadhimisha Misa peke peke na wakonselebranti pia. Mambo ya kuangalia
yameelezwa mwanzo wa Sala ya Ekaristi I.

Anafumbua mikono:
Bwana awe nanyi
Awe pia nawe
Anainua mikono juu:
Inueni mioyo
Tumeiinua kwa Bwana.
Anafumbua mikono:
Tumshukuru Bwana Mungu wetu
Ni vema na haki.
UTANGULIZI

Kweli ni vema na haki CP


tukushukuru daima na popote, ee Bwana, Baba mwema, Wakonselebranti
kwa njia ya Mwanao mpenzi Yesu Kristu. Wanafumba
Mikono.

Uliumba vitu vyote kwa kwa njia ya Neno wako.


Tena ukamtuma kwetu kama Mwokozi na Mkombozi,
akajifanya mtu kwa uwezo wa Roho Mtakatifu,
akazaliwa na Bikira.
Kwa kuwa alitaka kutimiza mapenzi yako
na kukupatia taifa takatifu,
alisulibiwa msalabani
akashinda mauti na kudhihirisha ufufuko.
Kwa sababu hiyo, sisi pamoja na Malaika na Watakatifu wote,
Tunatangaza utukufu wako, tukisema kwa sauti moja:

Anafumba mikono:

Wote: Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu, Bwana Mungu wa majeshi.


Mbingu na dunia zimejaa utukufu wako.
Hosana juu mbinguni
Mbarikiwa anayekuja kwa jina la Bwana.
Hosana juu mbinguni.

Anafumbua mikono:
Ee Bwana, kweli u mtakatifu na chemchemi ya utakatifu wote.
Anafumba mikono, kisha anafumbua na kuitandaza juu ya mkate na divai: *
Tunakusihi uzutakase kwa nguvu ya Roho wako dhabihu hizi,
Anafumba mikono, anabariki mkate na kikombe:
ili ziwe kwetu Mwili na Damu ya Bwana wetu Yesu Kristu.

Anafumba mikono: Wanafumba


Yeye alipojitoa kwa hiari yake ateswe, Mikono.
Anainua kidogo hostia:
Alitwaa mkate akashukuru, akaumega,
Akawapa wafuasi wake, akisema:

Wananyosha
Anainama kidogo: mikono ya kulia
Twaeni, mle wote: kuonyesha hostia.

huu ndio mwili wangu,


utakaotolewa kwa ajili yenu. Wanatazama
hostia;
kisha wanainama
Anawaonyesha watu hostia, aniweka juu ya patena na kupiga goti. sana.
Anafunua kikombe:
Vivyo hivyo baada ya kula,
Anashika na kuinua kidogo kikombe:
akatwaa kikombe,
akashukuru tena, akawapa wafuasi wake, akisema:

Anainama kidogo. Wanaonyesha


mikono ya kulia
Twaeni, mnywe wote: kuonyesha kikombe
hiki ni kikombe cha damu yangu,
damu ya agano jipya la milele,
itakayomwagika kwa ajili yenu
na kwa ajili ya wengi
kwa maondoleo ya dhambi.
Fanyani hivi kwa kunikumbuka mimi. Wanatazama
Anawaonyesha watu kikombe, anakiweka juu ya korporale, kokombe;
na kupiga goti. kisha wanainama
sana.

Hili ni fumbo la imani:


CP

Wote: Ee Bwana, tunatangaza kifo chako


na kutukuza ufufuko wako mpaka utakapokuja.

Au : 1. Ee Bwana, kila tunapokula mkate huu


na kunywa kikombe hiki,
tunatangaza kifo chako mpaka utakapokuja.

2. Ee Mwokozi wa dunia, utuokoe,wewe uliyetukomboa


kwa msalaba na ufufukowako.
Anafumbua mikono: *
Kwa hiyo, ee Bwana, CC
tunapokumbuka kufa na kufufuka kwake Mwanao,
tunakutolea mkate wa uzima na kikombe cha wokovu.
Tunakushukuru kwa kuwa umetujalia
tusimame mbele yako na kukutumikia.
Tunaomba kwa unyenyekevu
Roho Mtakatifu atufanye tuwe jamaa moja
sisi tunaoshiriki Mwili na Damu ya Kristu.
C1
Ee Bwana, ulikumbuke Kanisa lako po pote duniani,
utukamilishe katika upendo,
sisi pamoja na Baba Mtakatifu wetu F. na Askofu wetu F.
Na watumishi wako wote.


Katika Misa ya wafu, anaweza kuongeza:

Umkumbuke ntumishi wako F. uliyemwita kwako (leo)


kutoka dunia hii.
Kwa kuwa alishiriki kifo cha Kristu kwa Ubatizo,
umjalie ashiriki pia ufufuko wake.

Anafumbua mikono:
C2
Uwakumbuke pia ndugu zetu,
waliofariki dunia wakiwa na tumaini la ufufuko.
Uwakumbuke na marehemu wote,
uwapokee kwenye nuru ya uso wako.
Tunakuomba utuhurumie sisi sote, C3
ili tustahili kushiriki uzima wa milele
na kukusifu na kukutukuza
pamoja na Maria Bikira mwenye heri Mama wa Mungu,
Mitume wenye heri na Watakatifu wote
waliokupendeza tangu kale.

Anafumba mikono:
Tunakuomba hayo kwa njia ya Mwanao Yesu Kristu.

Anainua hostia na kikombe pamoja, akisema kwa sauti :

CP
Kwa njia yake, pamoja naye, na ndani yake,
wewe Mungu Baba Mwenyenzi
katika umoja wa Roho Mtakatifu
unapata heshima na utukufu wote,
daima na milele.

Wote: Amina.
SALA YA EKARISTI III
Sala ya Ekaristi ya tatu inawezwa kusemwa na utangulizi wo wote. Inafaa
itumike hasa katika Misa za Jumapili na za sikuku, kama vile Sala ya
Ekaristi ya kwanza (kanuni ya Kirumi) inavyotumika.

Sehemu Fulani za sala hii zinaweza kuimbwa; nazo ni kuanzia Usiku ule
alipotolewa mpaka Sadaka hii yenye uzima utakatifu. Doksolojia ya
mwisho anaweza kuimbwa pia.

Rubrika zimefupishwa kadiri iwezekanavyo, na zinawahusu mapadre


wanaodhimisha Misa peke peke na wakonselebranti pia. Mambo ya
kuangalia yameelezwa mwanzo wa Sala ya Ekaristi I.

Anafumbua mkono:

CP
Ee Bwana, kweli u Mtakatifu,
na kila kiumbe kilichoumbwa nawe kinakusifu kwa haki. Wakonselebranti
Wanafumba
Maana, kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristu Mwanao, Mikono.
na kwa uwezo wa Roho Mtakatifu,
unatia uzima na kutakasa vitu vyote,
Wala huachi kuwakusanya watu kwako,
ili toka maawio ya jua hata machweo yake
Wakutolee sadaka safi.
Anafumba mikono nakuitandaza juu ya mkate na divai: CC
Basi, tunakusihi, ee Bwana, .
Uzibariki dhabihu hizi tunazokutolea,
Upende kuzitakasa kwa Roho wako,

Anafumba mikono, anabariki mkate na kikombe:

ili zigeuke kuwa Mwili na Damu


ya Mwanao Bwana wetu Yesu Kristo,

Anafumba mikono:

Aliyetuamuru tuadhimishe mafumbo haya.


Wanafumba
Usiku ule alipotolewa, mikono
.

Anainua kidogo hostia:


Yeye mwenyewe alitwaa mkate,
akakushukuru, akakutukuza,
akaumega, akawapa wanafuasi wake, akisema:

wanaonyesha
Anainama kidogo. mikono ya kulia
kuonyesha hostia.
Twaeni, mle wote:
Huu ndio mwili wangu,
utakaotolewa kwa ajili yenu.
Anawaonyesha watu hostia, aniweka juu ya patena na kupiga goti. Wanatazama hostia;
kisha wanainama
Anafunua kikombe: sana.

Vivyo hivyo baada ya kula,


Anashika na kuinua kidogo kikombe:
Akatwaa kikombe,
akakushukuru, akakutukuza,
akawapa wafuasi wake akisema:

Anainama kidogo.
Wananyosha
mikono ya kulia
Twaeni, mnywe wote: kuonyesha kikombe.

Hiki ni kikombe cha damu yangu,


Damu ya agano jipya la milele,
Itakayomwagika kwa ajili yenu
Na kwa ajili ya wengi
Kwa maondoleo ya dhambi.
Fanyani hivi kwa kunikumbuka mimi.
Wanatanzama
Anawaonyesha watu kikombe, anakiweka juu ya korporale, na kupiga goti. kikombe
kisha wanainama
sana
Hili ni fumbo la imani ; CP
wanainama sana.
Wote:
Ee Bwana,tunatanganza kifo chako
Na kutukuza ufufuko wako mpaka utakapokuja.
Au: 1. Ee Bwana, kila tunapokula mkate huu
Na kunywa kikombe hiki,
Tunatangaza kifochako mpaka utakapokuja.
2. Ee Mwokozi wa dunia, utuokoe,
Wewe uliyetukomboa kwa msalaba na ufufuko wako.
Anafumbua mikono : *
CC
Kwa hiyo, ee Bwana, tunapokumbuka mateso
ya huyo Mwanao,
Na kufufuka na kupaa kwake mbinguni;
Tunapongojea na kuja kwake mara ya pili,
Tunakutolea kwa shukrani
Sadaka hii yenye uzima na utakatifu.

Tunakuomba uiangalie na kuikubali hii sadaka ya kanisa lako


Uliyotaka kutulizwa nayo.
Utujalie sisi tunaolihwa mwili na Damu ya Mwanao
Tujazwe na Roho wake Mtakatifu,
Ili tuwe mwili mmoja na roho moja katika Kristu.
C1
Yeye atufanye sisi tuwe kwako sadaka ya milele,
Ili tuweze kupata urithi pamoja na wateule wako:
Bikira Maria mwenye heri, mama wa Mungu,
Na Mitume na Mashahidi wako wenye heri
(na Mtakatifu F. Mt. wa siku au Msimamizi)
Na watakatifu wote,
Ambao daima wanatuombea kwako.
C2
Tunakuomba, ee Bwana, sadaka hii ya kutupatanisha nawe
Ilete amani na wokovu duniani kote.
Uliimarishie Kanisa lako imani na mapendo hapa duniani,
Yaani mtumishi wako Baba Mtakatifu wetu F. na Askofu
wetu F.
Maaskofu na watumishi wako wote,
Pamoja na taifa lako lote.

C3
Usikilize kwa wema
Sala za jamaa hii iliyo hapa mbele yako.
Ee Baba mwema, kwa huruma yako uwakusanye kwako
Wanao wote waliotawanyika po pote duniani.

Katika Misa ya wafu husema sala za pekee mpaka mwisho:


tazama ukarasa ufuatao.

Uwapokee katika ufalme wako ndugu zetu marehemu


Na wote walioga dunia katika hali ya neema.
Nasi tunatumaini kujawa na utukufu milele
Katika ufalme wako.

Anafumba mikono :
Utujalie hayo kwa njia ya Kristu Bwana wetu
Aliye asili ya mema yote.
Anainua hostia na kikombe pamoja, akisema kwa sauti :

CP
Kwa njia yake, pamoja naye, na ndani yake,
Wewe Mungu Baba Mwenyenzi
Katika umoja wa Roho Mtakatifu
Unapata heshima na utukufu wote,
Daima na milele.
Wote: Amina.

Katika Misa ya wafu:

Ukumbuke mtumishi wako F.


uliyemwita kwako (leo) kutoka dunia hii.
Kwa kuwa alishiriki kifo cha Kristu kwa ubatizo,
umjalie ashiriki pia ufufuko wake.
siku ya ufufuko
Kristu ataifananisha miili yetu na mwuili wake mtukufu.

Pia uwapokee katika ufalme wako ndugu zetu marehemu


na wote walioaga dunia katika hali ya neema.
Nasi tunatumaini kujawa na utukufu milele
katika ufalme wako.
Ndipo utakapofuta machozi yetu yote,
maana kwa kukuona wewe Mungu wetu kama ulivyo,
tutafanana nawe milele yote,
na kukusifu bila mwisho.

Anafumba mikono:
utujalie hayo kwa njia ya Kristu Bwana wetu,
aliye asili ya mema yote.

Anainua hostia kikombe pamoja, akisema:


Kwa njia yake, pamoja naye, na ndani yake
Wewe Mungu Baba Mwenyenzi
Katika umoja wa Roho Mtakatifu
Unapata heshima na utukufu wote,
Daima na milele.

Wote: Amina.

Вам также может понравиться