Академический Документы
Профессиональный Документы
Культура Документы
21 Januari , 2018
Waziri Mkuu alitoa agizo hilo jana (Januari 20, 2018) wakati akizungumza na
watumishi na madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Bitiama katika ukumbi wa
chuo Kikuu cha Kilimo cha Mwalimu Nyerere cha Mara.
Waziri Mkuu alisema fedha zingine ni pamoja na sh. milioni 70 za elimu maalumu,
sh. milioni 288 za mradi wa maji Butiama ambazo zote hazijulikani zimetumikaje.
“Hatuwezi kuvumilia vitendo hivi fanyeni uchunguzi na naomba taarifa yake mara
mtakapokamilisha.
1
Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) mkoani Mara, Mhandisi Peter Salim baada
ya kushindwa kutekeleza ujenzi wa mradi wa ofisi za Halmashauri ya wilaya ya
Butiama.
Waziri Mkuu alisema kuwa Serikali ilitoa sh milioni 600 Aprili, 2017 kwa ajili ya
kuanza kwa ujenzi wa ofisi za Halmashauri ya wilaya hiyo lakini hadi sasa wakala
huo haujafanya kazi yoyote.
Katika maelezo yake Mhandisi Salim alisema ujenzi wa ofisi hiyo hadi kukamilika
utagharimu sh. bilioni tatu, kati ya sh. milioni 600 zilizotolewa na Serikali sh milioni
400 zimetumika kujengea msingi, kauli ambayo ilipingwa na Mkuu wa wilaya hiyo
Bibi Anna-Rose Nyamubi.
“Mheshimiwa Waziri Mkuu siyo kweli kwamba kuna kazi inayoendelea bali
kilichopo pale ni mashimo ambayo hayajulikani ni ya nini. Pia kuna jengo moja
lilijengwa kwa mabati kama stoo na hakuna mafundi wanaoendelea na kazi"
Waziri Mkuu alisema kuwa Serikali iko katika mchakato wa kuboresha mazingira
ya wafanyakazi ikiwa ni pamoja na ujenzi wa ofisi za watumishi na kwamba
haitamvumilia mtu yeyote atayekwamisha juhudi hizo.
(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU
JUMAPILI, JANUARI 21, 2018.
2
3