Академический Документы
Профессиональный Документы
Культура Документы
30 Januari , 2018
Katika Mkutano huo ambao Waziri Mkuu alimuwakilisha Rais Dkt. John Magufuli,
alisema nchi za Afrika zimejipanga kuzalisha umeme wa kutosha mijini na vijijini.
Waziri Mkuu alisema nchi hizo zimeazimia kuzalisha umeme mwingi kwa lengo
la kuinua kiwango cha maisha ya wananchi wake na kuharakisha maendeleo ya
kiuchumi.
“Tanzania iko vizuri kwa sababu ina vyanzo vingi vya kuzalisha umene na sasa
inamikakati ya kuzalisha umeme wa kutosha kuendesha viwanda vikubwa na
kukaribisha wawekezaji kwenye maeneo mbalimbali.”
1
“Tume nyingine ilihusika na mapitio ya namna kuhamasisha nchi za Afrika kufikia
kwenye maendeleo na nyingine ilikuwa inahamasisha mahusiano ya nchi kupitia
kwenye Jumuia zilizopo ndani ya Bara la Afrika kama SADC.”
Alisema Tanzania ilihusika kutoa mchango juu suala la amani na usalama katika
nchi za Afrika. ambapo kila nchi inawajibika kujilinda yenyewe na kulinda nchi
jirani pamoja na Jumuia zake.
(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU
JUMANNE, JANUARI 30, 2018.