Вы находитесь на странице: 1из 20

Wizara

Wizarayaya
Maliasili
Maliasili
nana
Utalii
Utalii
CHUMBA CHA HABARI
Wahariri:
Hamza Temba
Dorina G. Makaya
Lusungu Helela
Yaliyomo Uk
Sera ya Uhariri:
Madhumuni ya jarida hili la MALIASILI 1. Mapato ya Utalii yaongezeka kwa asilimia 5.6 ....................... Uk.4
ni:
2. Tanzania yatajwa nchi bora kwa Safari za Utalii
(i) Kuhabarisha na kuelimisha umma barani Afrika ........................................................................... Uk.5
kuhusu sekta ya Maliasili, Malikale
na Maendeleo ya Utalii. 3 . Kigwangalla aagiza msako mkali kwa walioua
Simba tisa Serengeti .............................................................. Uk.6
(ii) Kuwa jukwaa la mawasiliano la
watumishi.
4. Madhimisho ya Kimondo cha Mbozi kufanyika
Juni, 2018 ............................................................................. Uk. 7
(iii) Kufafanua na kuelezea sera za
Wizara ya Maliasili na Utalii.
5. Olduvai; Chimbuko la binadamu ............................................ Uk.8
Isipokuwa pale ambapo itakatazwa,
makala za MALIASILI zinaweza 6. Tanzania yasisitiza ujenzi mradi wa Stiegler’s Gorge .............. Uk.9
kunukuliwa kwa kutambua jarida
hili kama chanzo cha habari husika 7. Mapori Matano ya Akiba Kupandishwa hadhi ya kuwa
(Source). Hifadhi za Taifa .................................................................... Uk.10

Hutolewa na: 8. Mhispania aweka rekodi ya kupanda Mlima Kilimanjaro


Kitengo cha Mawasiliano Serikalini kwa kutumia baiskeli ............................................................ Uk.11
Wizara ya Maliasili na Utalii
Barabara ya Askari, Mtaa wa Kilimani 9. Serikali kuboresha eneo la barabara ya lami ambalo
S.L.P. 1351, 40472 - Dodoma, Tanzania.
ni kivutio cha utalii nchini .................................................... Uk.12

Simu: +255 26 2 321 566


10. Dondoo muhimu kuhusu nyara za serikali ........................... Uk.13
Nukushi: +255 26 - 2321514
Barua-pepe: ps@mnrt.go.tz
Tovuti: www.mnrt.go.tz 11. Ujangili nchini wapungua kwa zaidi ya asilimia 50................ Uk.14
Blog: www.wizarayamaliasilinautalii. blogspot.
com 12. Wadau waaswa kutumia fursa ya ufugaji nyuki
Facebook: Wizara ya Maliasili na Utalii - Tanzania kujikwamua kwenye umaskini .............................................. Uk.15

13. Utaratibu wa kufuga wanyamapori kwenye mashamba,


ranchi na bustani .................................................................. Uk.16

14. Jengo la NCAA kuwa kivutio cha utoaji wa huduma za


Utalii Jijini Arusha ................................................................ Uk.18

15. Faru mwenye umri mkubwa kuliko wote Duniani ................ Uk.19

2 Jarida la MALIASILI
Tahariri Wizara ya Maliasili na Utalii

REGROW:
ikawe chachu
ya kufungua
Utalii Kanda
ya Kusini
Wizara ya Maliasili na Utalii ina dhamana ya kusimamia sekta Mwezi Novemba mwaka jana (2017) Serikali ilisaini mkopo
ya Maliasili na Malikale na Kuendeleza Utalii hapa nchini. wa masharti nafuu wa Dola za Kimarekani milioni 150, sawa
Inaelezwa kuwa katika kufanikisha utekelezaji wa jukumu hilo, na takriban Bilioni 340 za Tanzania kutoka Benki ya Dunia
Wizara kwa kushirikiana na Benki ya Dunia imeandaa mradi
kwa ajili ya kuendeleza mradi huo.
wa kusimamia maliasili na kuendeleza utalii wa kanda ya
kusini ujulikanao kama REGROW (Resilient Natural Resource
for Tourism and Growth). Tunafahamu kuwa mradi huu ni moja ya mkakati wa Serikali
kupanua wigo wa vivutio vya utalii nchini kwa kuongeza
Lengo la mradi huo ni kuongeza mchango wa sekta ya mazao mbalimbali ya utalii na kusisimua kanda zingine za
maliasili na utalii katika uchumi wa Taifa kwa kuboresha vivutio utalii ziweze kutumika ipasavyo kuleta tija katika sekta hii
vya utalii, miundombinu, usimamizi wa vivutio na kuongeza na kuongeza pato la Taifa tofauti na ilivyo hivi sasa ambapo
faida za kiuchumi kwa jamii zinazoishi jirani na maeneo ya vivutio vingi vinavyotumika ni vile vya ukanda wa Kaskazini.
hifadhi katika ukanda huo wa kusini.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dkt. Hamisi Kigwangalla
Mradi huu ambao maandalizi yake yalianza mwezi Novemba anaeleza kuwa kwa sasa vivutio vya utalii vya kaskazini
2014 ulizinduliwa rasmi na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya vimeanza kuelemewa kwa kuwa watalii wengi hutembelea
Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan tarehe
vivutio hivyo kutokana na uwepo wa mazingira bora ya
12 Februari, 2018 katika viwanja vya Kihesa Kilolo Mjini Iringa
miundo mbinu, uwekezaji katika huduma za utalii na utangazaji
na Kauli Mbiu ya uzinduzi huo ikiwa “Utalii kwa Maendeleo
Endelevu- Karibu Kusini”. tofauti na ilivyo kwa maeneo mengine yenye vivutio ambayo
yanakabiliwa na changamoto mbalimbali.
Akizindua mradi huo, Makamu wa Rais alisema utasaidia
kupambana na athari zitokanazo na mabadiliko ya tabia nchi Tunaamini kuwa REGROW itakuwa chachu ya kurekebisha
na kuchochea ukuaji wa sekta hiyo katika Nyanda za Juu changamoto zilizopo katika ukanda wa kusini ili nao uweze
Kusini kwakuwa vivutio vyake havijapewa kipaumbele cha kutembelewa na watalii wengi kama ilivyo kwa kanda ya
kutosha kama vile vya maeneo ya kaskazini mwa nchi. Kaskazini.

Taasisi zinazohusika na utekelezaji wa mradi huo ni Wizara Tunatoa rai kwa kila mdau anayehusika na utekelezaji wa
ya Maliasili na Utalii, Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania, mradi huu kutimiza wajibu wake kwa kufanya kazi kwa bidii
Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania, Tume ya na ubunifu wa hali ya juu ili matunda yaliyokusudiwa ya
Taifa ya Umwagiliaji, Ofisi ya Bonde la Mto Rufiji, Bodi ya mradi huu yaweze kupatikana kwa faida ya kizazi cha sasa
Utalii Tanzania, Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania na na kijacho.
Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania kwa kushirikiana
na Halmashauri za Wilaya mbalimbali nchini. Sambamba na mradi huu tunatoa wito kwa wadau wengine
wa sekta ya umma na binafsi kutumia fursa ya mradi huo
Mradi huo utaanza utekelezaji katika maeneo ya kipaumbele kuwekeza katika ujenzi wa miundombinu ikiwemo ya hoteli za
ambayo ni Hifad hi ya Taifa ya Ruaha, Mikumi, Udzungwa kitalii na utoaji wa huduma nyingine mbalimbali za utalii.
na Pori la Akiba la Selous hususan Kanda ya Kaskazini
unakofanyika utalii wa picha. Mhariri.

Jarida la MALIASILI 3
Wizara ya Maliasili na Utalii

Mapato ya Utalii yaongezeka kwa


asilimia 5.6

Mapato yatokanayo na utalii nchini na kudhibiti matukio ya ujangili na “Mfumo huo utaunganishwa na
yameongezeka kutoka Dola za matumizi yasiyo endelevu ya maliasili mfumo wa Serikali wa malipo ya
Marekani milioni 2,131.57 kwa mwaka na malikale. kielektroniki na kuhuishwa na mifumo
2016 hadi kufikia Dola za Marekani
mingine ya Serikali kama vile Uhamiaji,
milioni 2,250.3 kwa mwaka 2017 ikiwa Aliongeza kuwa, katika juhudi
ni sawa na ongezeko la asilimia 5.6. za kutangaza utalii, Wizara yake NIDA, TIRA, BRELA, TRA na NBS.
imeendelea kutekeleza mikakati Mfumo huo utaiwezesha Wizara
Hayo yalielezwa Bungeni Jijini Dodoma mabalimbali ikiwemo kuandaa kufuatilia watalii wa nje na wa ndani,
na Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. utambulisho wa Tanzania Kimataifa kukusanya na kuchambua takwimu
Dkt. Hamisi Kigwangalla alipokuwa (Destination Branding). Lengo ikiwa za sekta ya maliasili na utalii kwa
akiwasilisha makadirio ya mapato na ni kuitambulisha Tanzania kama kituo
wakati, kuimarishsa utoaji wa huduma
matumizi ya wizara yake kwa mwaka mahsusi cha utalii Duniani.
wa Fedha 2018/2019. kwa wateja na kufanikisha ukusanyaji
Alisema wizara yake inashirikiana na udhibiti wa mapato,” alisema Dkt.
“Idadi ya watalii walioingia nchini Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa Kigwangalla.
imeongezeka kutoka watalii 1,284,279 na Michezo kuanzisha chaneli maalum
kwa mwaka 2016 hadi kufikia watalii katika Televisheni ya Taifa (TBC 1) kwa Mfumo huo ambao utatumiwa na
ajili ya kutangaza utalii ambapo kwa Wizara, Taasisi na wadau mbalimbali
1,327,143 kwa mwaka 2017, ikiwa
sasa Wizara kupitia TTB inaendelea unatarajia kuanza kutumika rasmi
ni ongezeko la asilimia 3.3. Watalii
na maandalizi ya kuanzisha studio mwaka ujao wa fedha.
kutoka Marekani wameongoza katika
maalum ya kutangaza utalii kwa njia ya
kuitembelea Tanzania wakifuatiwa na Kwa upande wake Mwenyekiti wa
teknolojia ya habari na mawasiliano.
nchi za Uingereza, India, Uholanzi na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi,
Uswisi,” alisema Dkt. Kigwangalla. Aidha, alisema, Wizara yake imeanza Maliasili na Utalii, Mhe. Nape Nnauye
kutengeneza mfumo mmoja funganishi aliipongeza Serikali kwa kuboresha
Alisema, mafanikio hayo yanatokana na wa TEHAMA unaoitwa “MNRT Portal” miundombinu ya utalii hususan
ujenzi wa miundombinu ya barabara, kwa kutoa leseni na vibali, ukusanyaji barabara, huduma za maji na umeme
kuongezeka kwa kasi ya kuboresha na wa takwimu na mapato kutoka vyanzo ambavyo vimeendelea kuvutia watalii
kutangaza vivutio vya utalii, kuimarishwa mbalimbali vya sekta ya Maliasili na wengi kutembelea vivutio vya utalii na
kwa mifumo ya ukusanyaji maduhuli Utalii. kuongeza idadi ya watalii hapa nchini.

4 Jarida la MALIASILI
Wizara ya Maliasili na Utalii

Tanzania yatajwa nchi bora kwa


Safari za Utalii barani Afrika
Tanzania imetajwa kuwa nchi bora
ya kufanya safari za utalii barani
Afrika, kwa mujibu wa mtandao
wa SafariBookings.com, mtandao
mkubwa wa masoko kwa utalii Afrika.

Tovuti hiyo iliendesha utafiti wake


kupitia wataalam zaidi ya 2,500 sanjari
na kuzungumza na wafanya safari hizo
na kutangaza kuwa Tanzania ni sehemu
nzuri kwa utalii kwa mwaka 2017.

“Uchambuzi wetu ulihusisha


wataalamu zaidi ya 2,500 na tathimini
za watalii. Tathmini hiyo ililenga
kuangalia kinachopendwa kwa jumla
na kuamua mshindi wa mwaka 2017,”
ilisema sehemu ya ripoti hiyo katika
Wote hao walifanikiwa kutembela Mbali na miaka hiyo, mlima huo ulitwaa
mtandao huo.
sehemu za kitalii ikiwemo Hifadhi ya Taifa tuzo hiyo mwaka 2013, lakini mwaka
ya Serengeti na Mlima Kilimanjaro. 2014, Table Mountain, ya Afrika Kusini
Tathmini hiyo iliandikwa na watalii
iliibuka mshindi.
ambao walitembelea mbuga tofauti
Sekta ya utalii inaongoza kwa kuliingizia
barani Afrika na baadhi ya wataalam
taifa mapato ya kigeni kwa asilimia 25 Ushindi huo ulitangazwa katika hafla
wa kampuni zinazoongoza katika
huku mchango wake kwenye pato la ya Tuzo ya Maeneo yanayotembelewa
kusafirisha watalii Afrika.
taifa ukiwa asilimia 17.5. zaidi duniani (World Travel Awards-
WTA) zilizofanyika katika jiji la Kigali
“Katika uchambuzi wetu halisi wa
Katika hatua nyingine Mtandao wa nchini Rwanda, mwishoni mwa mwaka
mwaka 2013, Tanzania pia iliyaondoa
kimataifa wa National Geographic jana.
mataifa mengine ya kusini mwa bara
uliitaja Hifadhi ya Taifa ya Ruaha iliyopo
la Afrika kutokana na changamoto
Iringa, Tanzania kuwa miongoni mwa Tanzania pia ilipata tuzo nyingine
zilizokuwepo. Hii ni mara ya Pili kwa
maeneo bora zaidi yanayopaswa ikiwemo ya kisiwa bora kwa utalii cha
nchi hii kupokea tuzo ya ushindi wa
kutembelewa mwaka huu, 2018. Thanda na nyumba bora ya kulala
jumla kwa Afrika katika biashara ya
wageni ya Four Seasons iliyopo katika
safari.”
Maeneo mengine yaliyotajwa kwenye Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
mtandao huo ni mji wa kihistoria wa
Tovuti hiyo imeongeza kuwa, uchambuzi
Harar nchini Ethiopia, Jujuy Province
huo pia uliweka wazi kuwa Tanzania ni
(Argentina), Tbilisi (Georgia), Sydney
maarufu kwa kuwa na aina nyingi za
(Australia), Oaxaca (Mexico), Vienna
wanyamapori na kubeba ushindi wa
(Austria), North Shore- Oahu (Hawaii)
jumla kwa kuwa na wanyamapori wengi
na Phnom Penh (Cambodia).
ambapo uliitaja hifadhi ya Serengeti na
Ngorongoro kama chachu ya ubora
Katika tovuti ya mtandao huo ya www.
huo.
nationalgeographic.com, hifadhi hiyo
kubwa nchini imetajwa kwa kigezo cha
Watu maarufu kadhaa katika miezi ya
kuwalinda na kuhifadhi simba wenye
hivi karibuni wamekuwa wakimiminika
asili ya Afrika walio hatarini kutoweka.
kutembelea vivutio mbalimbali nchini
Tanzania.
Kwa mujibu wa mtandao huo, simba
hao wenye asili ya Africa ‘African
Miongoni mwao ni pamoja na
Mwanamuziki wa Marekani Usher Lion’ wapo hatarini kutoweka na
Raymond, mchezaji wa zamani wa wamepungua kwa asilimia 90.
soka, Manchester United na Real
Madrid player David Beckham, Wakati huo huo, Mlima Kilimanjaro
mchezaji wa zamani wa klabu ya ulishinda tuzo ya Kivutio Bora cha Utalii
Liverpool Mamadou Sakho, mchezaji barani Afrika kwa mwaka 2017 ikiwa ni
wa Everton Morgan Schneiderlin na ya tatu mfululizo kwa Mlima huo ambao
wachezaji nyota wa filamu wa Marekani ulishinda tena mwaka 2015, 2016.
Will Smith na Harrison Ford.

Jarida la MALIASILI 5
Wizara ya Maliasili na Utalii

Dr. Kigwangalla aagiza msako mkali


walioua Simba tisa Serengeti

Askari wa wanyamapori wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti wakikusanya miili ya simba tisa waliouwawa kikatili kwa kulishwa sumu, mmoja
kukatwa na kuchomolewa baadhi ya viungo vyake na wananchi katika kijiji cha Nyichoka, wilaya ya Serengeti mkoani Mara hivi karibuni kwa
ajili ya kuwafanyia uchunguzi kubaini chanzo cha vifo vyao.

WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Mhe. Walipouawa simba wa Ruaha hivi kwanza kutokea hapa nchini ambapo
Dkt. Hamisi Kigwangalla ameagiza karibuni walikufa fisi zaidi ya 70 na mwishoni mwa mwaka jana simba
Kikosi Kazi Dhidi ya Ujangili cha ndege mbeshi zaidi ya 100, achilia wengine watano waliuawa pembezoni
Taifa kushirikiana na Kamati ya Ulinzi mbali wadudu,” amesema Dkt. mwa Hifadhi ya Taifa ya Ruaha.
na Usalama ya wilaya ya Serengeti Kigwangalla kwa masikitiko makubwa.
kuwasaka watu waliohusika na mauaji “Mwaka huo huo mwanzoni simba
ya simba tisa katika kijiji cha Nyichoka, Amesema pamoja na faida kubwa za watatu nao walipigwa risasi kikatili
wilaya ya Serengeti mkoani Mara na simba kwa Taifa kiuchumi, Kijiji cha wilayani Serengeti huku mwaka 2015
kuwafikisha kwenye vyombo vya Nyichoka pekee walikouwawa simba simba 7 wakauwawa tena kwa sumu,
sheria. hao ni katika sehemu iliyofaidika sana huko huko Serengeti”.
na miradi ya ujirani mwema kutoka
Dkt. Kigwangalla ametoa agizo hilo Hifadhi ya Taifa ya Serengeti. Akizungumzia sababu za ujangili huo
ofisini kwake Jijini Dodoma baada ya amesema mara nyingi ni kwa ajili ya
kupokea taarifa rasmi ya mauaji hayo “Wanyama hawa jamii ya paka kulipiza kisasi baada ya ng’ombe wa
ya kikatili yaliyoripotiwa hivi karibuni wakubwa ni muhimu sana kwa kuweka wananchi kuliwa na simba, changamoto
kwa simba hao kulishwa sumu kali mizania ya ikolojia sawa, maana ambayo husababishwa na wananchi
katika kijiji hicho huku mmoja akikatwa wanadhibiti idadi ya wanyama wala wenyewe kusogelea na kuweka makazi
miguu, mkia, ngozi ya juu ya mgongo nyasi kwa kuwala, bila hivyo hifadhi karibu kabisa na mipaka ya hifadhi za
na kuchukuliwa baadhi ya viungo zote zinaweza kugeuka kuwa jangwa. wanyamapori kwa lengo la kulisha
vyake ambapo amesema mauaji hayo mifugo pembezoni na wakati mwingine
hayavumiliki kwa kuwa yana athari “Hakuna mtalii atakayekuja hifadhini ndani ya hifadhi hizo kinyemela.
kubwa kiikolojia, kiutalii na uchumi wa asitamani kumuangalia simba, mfalme
Taifa kwa ujumla. wa pori. Wanapouawa maana yake Simba ambao wanakadiriwa kuwa zaidi
tunashusha hadhi ya hifadhi zetu kidogo ya 22,000, pamoja na wanyama
“Bahati mbaya sana ni kuwa kiutalii na hivyo kutishia kupoteza wengine jamii ya paka wamepungua
anapouawa simba kwa sumu hafi mapato yanayotokana na utalii” sana miaka ya hivi karibuni kiasi cha
peke yake, inakufa familia nzima ya amesisitiza Dkt. Kigwangalla. kuwekewa tishio la kutoweka hapa
simba, na mara nyingi wanakufa pia duniani. Duma nao wanakadiriwa
wanyamapori wengine wanaodowea Amesema tukio hilo la kuuwawa kwa kubaki 1,200 pekee.
nyama na wanaokula mizoga. Simba wa Ikolojia ya Serengeti sio la

6 Jarida la MALIASILI
Wizara ya Maliasili na Utalii

Maadhimisho ya Kimondo cha


Mbozi kufanyika Juni, 2018

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga na viongozi wengine wa mkoa wa Songwe, wakiangalia Kimondo cha Mbozi.

Mkoa wa Songwe kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili riadha (Kimondo Marathon), mashindano ya netiboli na mpira
na Utalii na wadau wengine wa uhifadhi na maendeleo wa miguu (Kimondo Ligi).
utafanya maadhimisho ya siku ya Kimondo cha Mbozi kwa
mara ya kwanza katika historia kwenye Kijiji cha Ndolezi Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.
Kata ya Mlangali, wilayani Mbozi kuanzia Juni 28 hadi 30 Japhet Hasunga amesema Serikali kupitia Wizara yake
mwaka huu . itashiriki kikamilifu katika maadhimisho hayo kwa kushirikiana
na mkoa wa Songwe na wadau wengine ili kuhakikisha
Maadhimisho hayo yataenda sambamba na maadhimisho kivutio hicho cha Kimondo kinajulikana zaidi ndani na nje ya
ya siku ya Vimondo duniani ambayo yaliazimiwa kufanyika nchi na hatimaye kiongeze idadi ya watalii na mapato.
Juni 30 kila mwaka na kikao cha Umoja wa Mataifa cha
tarehe 6 Desemba, 2016. Amesema wizara yake ina mkakati maalum wa kuimarisha
kituo hicho cha utalii ambapo hivi sasa imeshajenga kituo
Pamoja na mambo mengine, kikao hicho pia kiliazimia maalum cha taarifa ambacho kimegharimu zaidi ya Shilingi
tarehe hiyo kuwa siku ya kuelimisha umma kuhusu elimu ya milioni 400 za Kitanzania.
anga na mafanikio ya tafiti mbalimbali yaliyopatikana kuhusu
elimu hiyo, kutambua juhudi zilizofanyika, kuweka sheria Aidha, amesema kupitia mkakati mpya wa wizara wa
za kimataifa na kutoa tahadhari juu ya athari zinazoweza kuimarisha na kuvijengea uwezo vituo vya malikale nchini
kutokea endapo dunia itafanya uharibifu juu ya anga. kwa kuzishirikisha taasisi za uhifadhi wa wanyamapori na
misitu, Shirika la Hifadhi za Taifa Tanapa litashirikiana na kituo
Akizungumza wakati akiwasilisha taarifa ya maandalizi ya hicho kwa kuimarisha miundombinu pamoja na utangazaji.
maadhimisho hayo kwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,
Mhe. Japhet Hasunga Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Kimondo cha Mbozi kinakadiriwa kilianguka mwaka 1840
Songwe, Herman Tesha amesema lengo la maadhimisho kutoka kwenye obiti yake huko angani huku kikikadiriwa
hayo ni kutangaza Kimondo hicho kama kivutio muhimu cha kuwa na tani 12 na mchanganyiko wa madini ya Chuma
utalii mkoani Songwe pamoja na vivutio vingine vya mkoa 90%, Nickel 8.69%, Copper 0.66%, Sulphur 0.01% na
huo kwa ujumla ili kutoa fursa ya uwekezaji kwenye sekta ya Phosphorus 0.11. Kimomdo hicho ni cha pili kwa ukubwa
utalii mkoani humo. barani Afrika na cha nane duniani kati ya vimondo 600
vilivyodondoka maeneo mbalimbali ulimwenguni, sifa yake
Amesema maadhimisho hayo yataenda sambamba na kubwa ni kuwa na ubaridi wakati wote hata mchana wa jua
kongamano la uwekezaji na sayansi ya vimondo, maonesho kali.
ya malikale, maonesho ya kiutamaduni, mashindano ya

Jarida la MALIASILI 7
Wizara ya Maliasili na Utalii

Olduvai; Chimbuko la binadamu

Serikali ya Tanzania kupitia Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la zamadamu wanaoitwa Zinjanthropus au Paranthropus boisei
Ngorongoro kwa kushirikiana na Umoja wa Ulaya imejenga na Homo habilis, zana za mawe za mwanzo zilizotumika
Makumbusho mapya ya Olduvai ambayo inaonesha (Oldowan) katika kujipatia chakula na ushahidi wa kale wa
Chimbuko la Binadamu (The Cradle of Humankind) katika ulaji wa nyama katika historia ya mabadiliko ya binadamu,
Bara la Afrika. takribani miaka million 2 iliyopita.

Makumbusho hayo mapya na Onesho la Chimbuko la Sehemu ya tatu inahusu maisha ya jamii ya Homo erectus.
Binadamu, yalifunguliwa rasmi na Makamu wa Rais wa Jamii hii ilikuwa inafanana zaidi na binadamu wa sasa kuliko
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu jamii zilizotangulia. Aidha yapo pia masalia ya zamadamu
Hassan mwishoni mwa mwaka jana katika eneo la Olduvai, Homo erectus, zana za mawe (Acheulian) na ushahidi wa
ndani ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro. ulaji wa wanyama wakubwa kama vile Nyati na tembo katika
historia ya mabadiliko ya binadamu, takribani miaka million
Onesho hilo ni matokeo ya utafiti wa muda mrefu uliofanyika 1.7 iliyopita.
katika Bonde la Olduvai na Laetoli katika Wilaya ya
Ngorongoro mkoani Arusha. Sehemu ya nne inaonesha kipindi cha mwanzo cha
binadamu wa sasa (Homo sapiens) walioanza kutokea hapa
Idadi kubwa ya vioneshwa katika Makumbusho hii, vilipatikana Afrika miaka laki 2 iliyopita. Sehemu hii pia inaonesha mila na
katika bonde la Olduvai na Laetoli nchini Tanzania kupitia utamaduni wa makabila mbalimbali kama vile Wahadzabe,
utafiti wa kisayansi wa muda mrefu na vilikuwa vimehifadhiwa wamasai na Datoga. Yapo pia mavazi ya asili ya jamii hizo,
katika Makumbusho ya Taifa, Jijini Dar es Salaam. zana za kuwinda na vifaa mbalimbali wanavyovitumia katika
maisha yao ya kila siku.
Vioneshwa hivi ni pamoja na masalia ya zamadamu, zana
za mawe na masalia ya wanyama walioishi takribani miaka
milioni 4 iliyopita.

Makumbusho hii inaonesha sehemu kuu nne zinazowiana.

Sehemu ya kwanza inahusu ushahidi wa nyayo za zamadamu


zilizongunduliwa huko Laetoli mwaka 1978 na mtafiti Dr. Mary
D. Leakey. Nyayo hizi ziliachwa na zamadamu anayeiitwa
Australopithecus afarensis na ndio ushaidi usiopingika wa
zamadamu kutembea wima kwa miguu miwili takribani
miaka milioni 3.6 iliyopita.

Sehemu ya pili inahusu hadithi ya kusisimua ya kuwa


binadamu (Genus Homo); ambapo yapo na masalia ya

8 Jarida la MALIASILI
Wizara ya Maliasili na Utalii

Tanzania yasisitiza ujenzi wa mradi


wa Stiegler’s Gorge kuendelea...
Tanzania imesisitiza uamuzi wake wa kuendelea na mpango
wa kujenga mradi mkubwa wa kuzalisha umeme katika
maporomoko ya mto Rufiji (Stiegler’s Gorge Hydro Power
Project) yaliyopo ndani ya Pori la Akiba la Selous mbele
ya wajumbe wa Kamati ya Urithi wa Dunia kutokana na
umuhimu wake kwa maendeleo ya Watanzania.

Akizungumza katika mkutano wa 41 wa wajumbe wa Kamati


ya Urithi wa Dunia ulioendeshwa na Shirika la Elimu, Sayansi
na Utamaduni la Umoja wa Mataifa (UNESCO) na kufanyika
katika Jiji la Krakov nchini Poland, Kiongozi wa msafara wa
Tanzania ambaye ni Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii,
Meja Jenerali Gaudence Milanzi aliwaeleza wajumbe wa
mkutano huo kuwa mpango huo ulikuwepo katika ajenda
ya Serikali ya Tanzania tangu miaka ya 1960’s na kwamba
ukubwa wa eneo litakalotumika kutekeleza mradi huo ni
asilimia tatu tu ya eneo lote la pori hilo ambalo lina ukubwa
wa kilometa za mraba 50,000.
Bodi za Ushauri ya kituo hicho na kuwasilisha kwa maandishi
“Itakumbukwa kuwa mnamo mwaka 1982 wakati pori hili msimamo wa Tanzania kuhusu ujenzi wa mradi huo.
(Selous) limewekwa katika orodha ya maeneo ya urithi wa
dunia, Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhifadhi wa Asili (IUCN) “Tanzania ilipinga vikali rasimu ya azimio No. 41 COM 7 A.17
liliutambua mradi huo wa Stiegler’s Gorge kutokuwa na aya ya 7 ambalo liliitaka kusitisha kabisa (to permanently
madhara makubwa katika uharibifu wa mazingira ukizingatia abandon) ujenzi wa mradi wa kuzalisha umeme katika
ukubwa wa pori hilo na eneo litakalotumika kujenga mradi maporomoko ya mto Rufiji (Stiegler’s Gorge Hydro Power
huo” alisema Maj. Gen. Milanzi. Project). Baada ya tamko la Tanzania kupinga azimio hilo
kipengele hicho kilifanyiwa marekebisho ipasavyo na neno
Aidha, aliwaeleza wajumbe hao kuwa, Serikali ya Tanzania “to permanently abandon” (kusitisha kabisa) liliondolewa
inatekeleza sera ya kujenga uchumi wa viwanda hali katika azimio hilo kupisha majadiliano zaidi” alisema.
inayopelekea kuwa na mahitaji makubwa ya nishati ya
umeme hivyo kwa kuzingatia vyanzo vilivyopo imekuwa ni Tanzania ni miongoni mwa nchi wanachama zilizosaini
muhimu sasa kufikiria tena ujenzi wa mradi huo kama chanzo mkataba wa urithi wa Dunia wa mwaka 1972 huku ikiwa na
kingine muhimu cha nishati kuwezesha kufikia azma hiyo. maeneo sita yaliyorodheshwa katika urithi huo ikiwepo Pori la
Alisema mradi huo utaongeza uzalishaji wa umeme nchini Akiba la Selous, Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro, Hifadhi ya Taifa
kufikia asilimia 144.8 hivyo kuondoa upungufu wa nishati ya Serengeti, Mji Mkongwe (Zanzibar), Hifadhi ya Ngorongoro
uliopo kwa sasa na pindi utakapokamilika utawanufaisha na Michoro ya kondoa, Kilwa Kisiwani na Songo Mnara.
watanzania wengi wanaoishi bila umeme ikiwa ni pamoja na Aidha, ni mwanachama wa Kamati ya Urithi wa Dunia kwa
kukidhi mahitaji yake ya kuendesha viwanda. kipindi cha miaka minne hadi mwaka 2019. Tokea ijiunge na
kamati hiyo mwaka 2015, Tanzania imekua na msimamo wa
Meja Jenerali Milanzi alilazimika kutoa maelezo hayo kwa kuwa na maendeleo endelevu katika ajenda za mikutano yake
kamati hiyo ili kuweka bayana dhamira ya dhati Serikali ya pamoja na miongozo yake ili kuruhusu kuendeleza maeneo
Tanzania ya kuendelea na ujenzi wa mradi huo kwa ajili ya ya urithi wa dunia kuweza kufikia maendeleo ya kijamii na
maendeleo endelevu huku akitoa rai kwao kuwa Serikali bado kiuchumi bila kuwepo kwa athari kubwa katika mazingira.
ipo tayari kwa mazungumzo ya namna bora ya kutekeleza
mradi huo kwa faida ya jamii, uchumi na mustakbali bora wa Mkutano huo wa 41 wa wajumbe wa Kamati ya Urithi wa
mazingira ya hifadhi ya Selous na taifa kwa ujumla. Dunia uliofanyika mwezi Julai mwaka jana katika jiji la Krakov
nchini Poland ulihudhuriwa na nchi wanachama 193 ambao
“Kwa kutumia teknolojia bora zilizopo, mipango imara na walijadili mambo mbalimbali muhimu kuhusu uhifadhi na ulinzi
usimamizi thabiti, mradi huu utakua na faida kubwa kwa maeneo ya urithi wa dunia pamoja na kutangaza maeneo
taifa ikiwa na pamoja na kuboresha maisha ya watu maskini mengine mapya ya urithi wa dunia yaliyowasilishwa na nchi
na jamii kwa ujumla bila kuathiri mazingira yanayotoa faida nyingine wanachama katika mkutano huo.
hizo”, alisema Milanzi.
Ujumbe wa Tanzania katika mkutano huo ulijumuisha pia
Hapo awali, kabla ya mkutano huo, ujumbe wa Tanzania Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa ambaye pia ni mjumbe
ukiongozwa na Katibu Mkuu huyo ulifanya mazungumzo wa kudumu wa UNESCO, Samwel W. Shulukindo na Maafisa
na Maafisa Waandamizi wa Kituo cha Urithi wa Dunia na Waandamizi kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii

Jarida la MALIASILI 9
Wizara ya Maliasili na Utalii

Mapori Matano ya Akiba Kupandishwa


hadhi ya kuwa Hifadhi za Taifa

Baadhi ya Twiga katika mwambao wa ziwa Burigi kwenye Pori la Akiba Burigi ambalo litapandishwa hadhi kuwa Hifadhi ya Taifa.

Wizara ya Maliasili na Utalii imetangaza kuanza mchakato kwa ajili ya kuidhinishwa kuwa Sheria kamili ya kupandisha
wa kuyapandisha hadhi Mapori ya Akiba ya Burigi, Kimisi, hadhi mapori hayo.
Biharamulo, Ibanda na Rumanyika kuwa Hifadhi za Taifa.
Akizungumzia mikakati mingine mipya ya kuboresha sekta ya
Mchakato huo tayari umeungwa mkono na Rais wa Jamhuri maliasili na utalii itakayotekelezwa, Dkt. Kigwangalla alisema
ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph ni pamoja na kuanzisha mamlaka ya usimamizi na uendelezaji
Magufuli. wa utalii wa fukwe nchini, kuhuisha maeneo ya vivutio vya
Mambo ya Kale na kuviunganisha katika ‘package’ moja ya
Hayo yameelezwa bungeni Jijini Dodoma na Waziri wa Maliasili utalii na vivutio vya wanyamapori.
na Utalii, Mhe. Dkt. Hamisi Kigwangalla wakati akihitimisha
mjadala wa bajeti wa makadirio ya mapato na matumizi ya Mikakati mingine ni kuunda mfumo mmoja funganishi
wizara yake kwa mwaka wa fedha 2018/2019. wa TEHAMA uitwao “MNRT Portal” kwa ajili ya kutoa
leseni na vibali, ukusanyaji wa takwimu na mapato kutoka
“Mheshimiwa Spika, ninaomba kulitaarifu Bunge lako tukufu vyanzo mbalimbali vya sekta ya maliasili na utalii, ambapo
kuwa Mhe. Rais ameridhia ombi letu la kupandisha hadhi utaunganishwa na mifumo mingine ya Serikali iliwemo GePG,
Mapori ya Akiba ya Burigi, Kimisi, Biharamulo, Ibanda na NIDA, TIRA, BRELA, TRA na NBS.
Chief Rumanyika kuwa Hifadhi za Taifa, kipekee namshukuru
sana Mhe. Rais kwa kuridhia ombi letu hilo” alisema Dkt. Alisema mikakati mingine ni kuanzisha Jeshi Usu, Utambulisho
Kigwangalla. wa Utalii wa Tanzania Kimataifa ujulikanao kama “Tanzania,
Unforgettable”, kufungua utalii wa kanda ya kusini, kuanzisha
Alisema kufuatia hatua hiyo, wizara yake inaanzisha mchakato mwezi wa maadhimisho ya Urithi wa Mtanzania “Urithi
rasmi wa kukamilisha taratibu za kupandisha hadhi mapori Festival” (Septemba), kuhuisha sheria za TANAPA, TAWA na
hayo ili kupanua wigo wa vivutio vya utalii katika kanda TFS, pamoja na kuunda kanuni mpya za kusimamia vizuri
ya Kaskazini Magharibi na hivyo kufikia azma ya Serikali sekta hizo.
kuongeza idadi ya watalii kufikia milioni 8 na mapato ya dola
za kimarekani bilioni 16 katika kipindi cha miaka 7 ijayo. Pori la Akiba Burigi lina ukubwa wa kilomita za mraba 2,941
katika wilaya za Karagwe, Muleba na Ngara mkoani Kagera,
Inaelezwa kuwa mchakato huo utapitia hatua mbalimbali wakati Pori la Kimisi likiwa na ukubwa wa kilomita za mraba
ikiwemo kuwashirikisha wadau husika kupata maoni yao, 1,030 katika wilaya za Ngara na Karagwe mkoani humo.
mapendekezo kuwasilishwa baraza la mawaziri kabla ya
kujadiliwa bungeni na hatimaye kuwasilishwa kwa Mhe. Rais (Inaendelea Uk. 11)

10 Jarida la MALIASILI
Wizara ya Maliasili na Utalii

Mhispania aweka rekodi ya (Inatoka Uk. 10)

kupanda Mlima Kilimanjaro


Pori la Akiba Biharamulo lina ukubwa
wa kilomita za mraba 731 katika wilaya
ya Muleba mkoani Kagera na wilaya ya

kwa kutumia baiskeli Chato mkoani Geita, huku Pori la Akiba


Ibanda likiwa na ukubwa wa kilomita za
mraba 200 na Pori la Akiba Rumanyika
kilomita za mraba 800 katika wilaya ya
Kyerwa mkoani Kagera.

Mapori haya yapo katika ukanda


muhimu wa kuunganisha watalii kutoka
ikolojia za Magharibi na Mashariki
ambapo uwanja wa ndege wa
Chato utakuwa muhimu katika kutoa
mawasiliano.

Mapori hayo ya Akiba yanapokea


wanyamapori wanaohama kutoka
mapori ya Akiba ya Moyowosi na
kufanya Ikolojia ya Magharibi kuwa
kivutio kikubwa cha utalii ambapo
inatengeneza muunganiko mzuri kati
ya ikolojia ya Serengeti na Hifadhi ya
Taifa ya Rubondo.

Pamoja na sifa hizo, shughuli za utalii


zinazoweza kufanyika katika maeneo
hayo ni pamoja na utalii wa picha,
uendeshaji wa boti na mitumbwi,
MPANDA milima mashuhuri Duniani Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa) upandaji milima, uvuvi mahiri, utalii wa
kwa kutumia Baiskeli, Juanito limekuwa mstari wa mbele katika usiku na matembezi.
Oiarzabal ameweka rekodi ya kuwa kubuni aina mpya ya bidhaa za utalii
Mhispania wa kwanza kupanda Mlima ili kushindana na nchi nyingine duniani Mapori hayo pia yana maeneo mazuri
Kilimanjaro huku akitumia saa 31 katika uuzaji wa safari kwa watalii. kwa uwekezaji kama Nkonje, Ziwa
akiendesha baiskeli katika siku tano Ngoma na Msengapaya.
hadi kufika kilele cha Uhuru. Kwa upande wake Juanito Oiarzabal
ambaye amepata ulemavu wa kukatika Hatua hii ni mafaniko kwa Wizara ya
Juanito na wenzake wawili, Eduardo vidole kutokana na barafu katika Milima Maliasili na Utalii kwa kuweza kutunza
Pascuaz na Ramon Abecia waliianza mbalimbali aliyopanda amesema maeneo hayo hadi kufikia hadhi ya
safari ya kupanda Mlima Kilimanjaro changamoto aliyokutana nayo wakati kupandishwa kuwa Hifadhi za Taifa
kwa kutumia Baiskeli ,wakianza safari wa kupanda mlima ni kuzoea hali ya ambapo uwindaji wa wanyamapori
yao kupitia lango la Kilema, aina hii ya hewa ya mlima ambayo imekuwa hauruhusiwi na badala yake hutumika
utalii ikiwa ni bidhaa mpya katika Mlima ikibadilika kila mara. kwa ajili ya utalii wa picha pekee.
huo mrefu kuliko yote barani Afrika.
Mkurugenzi wa kampuni ya Safari Mapori hayo ambayo yanasimamiwa
Aina hii mpya ya utalii ambayo kwa sasa Bike Africa iliyoratibu changamoto ya na Mamlaka ya Usimamizi wa
imeanza kushika kasi katika Hifadhi za kupanda Mlima Kilimanjaro kwa kutumia Wanyamapori Tanzania - TAWA sasa
Taifa za Mlima Kilimanjaro, Arusha na Baiskeli kwa wageni hao, Mario Martos yatakuwa chini ya Shirika la Hifadhi za
Saadan inatokana na Shirika la Hifadhi alisema kampuni yake imekusudia Taifa Tanzania - TANAPA punde baada
za Taifa (TANAPA) kuendelea kupanua kuleta mabadiliko katika sekta ya utalii ya mchakato wa kuyapandisha hadhi
wigo wa vivutio katika Hifadhi zake 16. kwa kufanikisha safari za watalii wa kukamilika.
kutumia baiskeli.
Meneja Mawasiliano na Mahusiano Bunge limeidhinisha Sh. bilioni 115.794
wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Shirika la Hifdhi za Taifa (TANAPA) kwa ajili ya makadirio ya mapato na
Pascal Shelutete anaeleza hatua ya limejipanga kuhakikisha usalama wa matumizi ya Wizara ya Maliasili na
Juanito na wenzake kufika katika kilele hali ya juu kwa wageni watakaofanya Utalii kwa mwaka wa fedha 2018/2019
cha Uhuru inaashiria kuanza kufunguka aina hii mpya ya utalii katika Hifadhi zake ambapo Sh. bilioni 85.816 ni kwa
kwa aina hii mpya ya utalii katika Hifadhi kwa kuwa na taahadhari sambamba na ajili ya Matumizi ya Kawaida na Sh.
za Taifa. waongoza wageni waliobobea katika bilioni 29,978 ni kwa ajili ya miradi ya
kazi ya Utalii. maendeleo.
Shelutete anaeleza namna ambavyo

Jarida la MALIASILI 11
Wizara ya Maliasili na Utalii

Serikali kuboresha eneo la barabara ya


lami ambalo ni kivutio cha utalii nchini

Eneo katika shamba la Miti Kawetire mkoani Mbeya, ilipopita Barabara ya lami ambayo ipo juu zaidi ya nyingine nchini ikiwa na urefu (Altitude)
wa mita 2961 kutoka usawa wa bahari. Serikali itaboresha mazingira ya eneo hilo ili yatumike kama kivutio cha utalii nchini.

Serikali imesema itaboresha mazingira ambayo ni lazima tuiboreshe tuweke ya kale yaliyotumiwa na wakoloni
ya kivutio cha utalii cha barabara kibao kizuri tuweke mazingira mazuri katika shamba hilo na badala yake
ya lami ambayo ipo juu zaidi kutoka pamoja na kukitangaza ili watanzania yatumike kwenye utalii wa mambo ya
usawa wa bahari kuliko barabara zote na watalii kutoka nje waweze kale sambamba na utalii wa misitu ya
nchini ili kupanua wigo wa vivutio vya kutembelea hapa,” alisema Hasunga. kupandwa inayopatikana pia katika
utalii na kuongeza idadi ya watalii na shamba hilo.
mapato. Alisema ili kufikia lengo liliwekwa na
Serikali la kuongeza idadi ya watalii Hata hivyo alisema kupitia mradi wa
Hayo yalielezwa na Naibu Waziri wa kufikia milioni mbili mwaka 2020 na REGROW wa kuendeleza utalii kanda
Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga milioni 8 mwaka 2025 vivutio vyote vya ya kusini Serikali imepokea mkopo wa
baada ya kutembelea shamba la miti la utalii vilivyopo nchini vitatambuliwa, masharti nafuu wa dola za Kimarekani
Kawetire wilayani Mbeya na kujionea kuimarishwa na kuviwekea milioni 150 sawa za zaidi ya bilioni
sehemu ya barabara ya lami inayopita miundombinu itakayowavutia watalii 340 za kitanzania kutoka benki ya
katikati ya shamba hilo katika mlima kuvitembelea. dunia kwa ajili ya kusaidia kuboresha
Kawetire kwenye safu za milima ya miundombinu ya vivutio vya ukanda
Mbeya. Aidha aliuagiza uongozi wa shamba huo.
hilo kushirikiana na wakala wa
Eneo hilo la barabara hiyo ambayo huduma za barabara –Tanroads katika Kwa upande wake Meneja wa shamba
hupitisha magari kutoka Jijini Mbeya kuboresha mazingira yanayozunguka hilo, Arnorld Shoo alisema eneo hilo
kwenda katika Wilaya ya Chunya na eneo hilo ikiwa ni pamoja na kuweka la barabara limekuwa ni kivutio cha
Mikoa ya Singida na Tabora lina urefu bango la kisasa la kutambulisha eneo kipekee cha utalii katika shamba hilo
(Altitude) wa mita 2961 kutoka usawa hilo, kujenga bustani na maeneo rafiki ambapo pia hupata mapato kupitia
wa bahari katika Latitude 08’ 35 S na ya kupumzikia kwa ajili ya kuwavutia watu na vikundi mbalimbali ikiwemo
Longitude 33’ 25 E. watalii kutembelea eneo hilo na kupiga wanakwaya na wanafunzi ambao
picha. hufika eneo hilo kwa ajili ya kupiga
“Hatutaki ule utalii wa kutegemea picha za kumbukumbu.
wanyamapori pekee, hii sasa ni Mbali na kivutio hicho aliuagiza uongozi
sehemu ya aina nyingine ya utalii wa shamba hilo kutobomoa majengo

12 Jarida la MALIASILI
Wizara ya Maliasili na Utalii

Watumishi wa Umma kukopeshwa


mitungi ya gesi na vifaa vyake

Mtendaji Mkuu wa TFS, Prof. Dos Santos Silayo (kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa Mihan Gas, Hamisi Ramadhan (kulia) wakisaini
mkataba wa makubaliano wa kukopesha mitungi ya gesi na vifaa vyake kwa watumishi wa Umma Jijini Dodoma hivi karibuni. Katikati
anayeshuhudia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Maj. Gen. Gaudence Milanzi.

Serikali imesaini mkataba na Kampuni Pamoja na kusaini mkataba huo, TFS upatikanaji wa huduma hiyo ni
ya Gesi ya Mihan Gas kwa aijili ya na Kampuni ya Mihan Gas zilizindua jitihada za kuhakikisha matumizi ya
kukopesha mitungi ya gesi na vifaa kampeni ya kukopesha mitungi mkaa yanapungua.
vyake kwa watumishi wa umma. ya gesi na vifaa vya vyake kwa
Watumishi wa Umma. Alisema nishati mbadala ndiyo njia
pekee itakayosaidia jamii kuachana
Hatua hiyo imekuja ikiwa ni juhudi
Awali, Katibu Mkuu Wizara ya na matumizi ya mkaa na kuni.
za Serikali za kutaka kupunguza
Maliasili na Utalii, Maj. Gen. Milanzi
matumizi ya mkaa pamoja na kuni akizungumza katika hafla hiyo, Kwa upande wake, Mkurugenzi
kwa lengo la kuimarisha uhifadhi wa alitoa wito kwa watumishi wa umma Mtendaji wa Kampuni ya Mihan
misitu ambayo imekuwa ikitumika kuchangamkia fursa hiyo ambayo Gas, Hamisi Ramadhani aliishukuru
kama nishati kuu. itasaidia kupunguza uharibifu ya Serikali kwa kuikubalia kampuni hiyo
misitu nchini. kusambaza gesi kwa watumishi wa
Mkataba huo ulisainiwa hivi karibuni umma.
Jijini Dodoma na Mtendaji Mkuu “Hili ni tukio kubwa hasa kwa wale
wa Wakala wa Huduma za Misitu ambao ni watunzaji wa mazingira Akizungumzia namna watumishi
Tanzania (TFS), Profesa Dos Santos katika kuiwezesha jamii kuanza watakavyonufaika na mpango huo,
Silayo na Mkurugenzi Mtendaji wa matumizi ya nishati mbadala,” Mkurugenzi huyo alisema kampuni
kampuni ya Mihan Gas, Hamisi alisema. hiyo imetenga fungu la kutosha kwa
ajili ya kuwezesha ukopeshaji wa
Ramadhan huku Katibu Mkuu wa
Naye, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa vifaa hivyo na kwamba kila Mtumishi
Wizara ya Maliasili na Utalii, Mej.
Misitu zaTanzania (TFS), Profesa Dos atapewa nafasi ya kukopa na kulipa
Gen. Gaudence Milanzi akishuhudia Santos Silayo akizungumza baada mwezi mmoja mara baada ya kuanza
tukio hilo. ya kusaini mkataba huo alisema, matumizi ya gesi hiyo.

Jarida la MALIASILI 13
Wizara ya Maliasili na Utalii

Ujangili nchini wapungua kwa zaidi ya


asilimia 50

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na balozi wa Uingereza hapa nchini, Mhe. Sarah Cooke.

Serikali imefanikiwa kudhibiti vitendo vitendo hivyo kwa kuimarisha ulinzi wa Fukwe nchini ili kuimarisha utalii wa
vya ujangili hapa nchini kwa zaidi ya katika maeneo ya hifadhi nchini ikiwa ni fukwe pamoja na kutambua barabara
asilimia 50. pamoja na kuanzisha jeshi maalum la iliyokuwa ikitumika katika biashara ya
usimamizi wa Misitu na Wanyamapori, utumwa wakati wa ukoloni ili iweze
Hayo yalielezwa na Waziri wa Maliasili Sheria ya wanyamapori na za taasisi kutumika kiutalii.
na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla za uhifadhi zimeanza kufanyiwa
wakati akizungumza na Balozi wa marekebisho kuwezesha mabadiliko Akizungumzia migogoro ya mipaka
Uingereza hapa nchini, Sarah Cooke hayo. iliyopo baina ya wananchi na maeneo
ofisini kwake jijini Dodoma. ya hifadhi, Dk. Kigwangalla alisema
Katika hatua nyingine Dk. Kigwangalla Serikali itatatua migogoro hiyo kwa
Mazungumzo hayo yalilenga kujadili alimueleza balozi Cooke kuwa, Serikali kushirikisha wananchi sambamba na
mambo mbalimbali ikiwemo kuimarisha kupitia Wizara yake inaendelea kuwasaidia kutatua changamoto za
ushirikiano baina ya nchi hizo mbili kuimarisha vivutio vya utalii hapa nchini msingi ambazo ni kuimarisha maeneo
katika sekta ya uhifadhi na maendeleo kwa kupanua jeografia ya maeneo ya ya malisho ya mifugo, upatikanaji wa
ya utalii. utalii sambamba na kuongeza vivutio ili maji kwa ajili ya wananchi na mifugo,
kuongeza idadi ya watalii na mapato. mpango bora wa matumizi ya ardhi na
Dk. Kigwangalla alisema katika kipindi uendelezaji wa kilimo na ufugaji.
cha miezi sita iliyopita hakuna mauaji Alisema Serikali itajenga makumbusho
mapya ya wanyamapori yaliyoripotiwa ya Marais Wastaafu wa Tanzania Kwa upande wake balozi Cooke
na kwamba nyara zinazokamatwa hivi mjini Dodoma pamoja kuanzisha alisema nchi yake itaendelea
sasa ikiwemo meno ya tembo na ngozi makumbusho ya meno ya tembo kuimarisha ushirikiano inaoutoa kwa
za wanyamapori ni masalia ya zamani. katika miji ya Dar es Salaam, Arusha, Serikali ya Tanzania katika kudhibiti
Iringa na Dodoma. mtandao wa uhalifu wa madawa ya
Alisema mafanikio hayo yametokana kulevya, rushwa na ujangili.
na juhudi mbalimbali zinazofanywa na Sambamba na hayo alisema Serikali
Serikali kudhibiti vitendo vya ujangili itaanzisha mwezi maalum wa Alisema kwa sasa watalii zaidi ya
ikiwemo doria za mara kwa mara maadhimisho ya urithi wa Mtanzania 75,000 wa Uingereza hutembelea
za kiitelijensia ambazo zimekuwa ambao utafanyika mwezi Septemba Tanzania kila mwaka na wengine
zikishirikisha vyombo mbalimbali kila mwaka pamoja na kuendeleza wamewekeza katika sekta utalii
vya ulinzi na usalama pamoja na raia utalii wa mikutano. hapa nchini, hivyo akaiomba Serikali
wema. kurekebisha baadhi ya changamoto
Alisema Serikali pia itaanzisha chache zilizopo katika sekta hiyo
Alisema Serikali itaendelea kudhibiti Mamlaka ya Usimamizi na Uendelezaji kwenye mtiririko wa kodi.

14 Jarida la MALIASILI
Wizara ya Maliasili na Utalii

Wadau waaswa kutumia fursa ya ufugaji


nyuki kujikwamua kwenye umaskini

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kushoto) akizungumza na wadau wa sekta ya ufugaji nyuki nchini katika kikao
alichokiitisha kujadili maendeleo ya sekta hiyo ikiwemo marekebisho ya kanuni za ufugaji nyuki za mwaka 2017 Jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Alisema mbali na kuongeza uzalishaji, 54 ya ukubwa ardhi yote ya Tanzania
Mhe. Japhet Hasunga ametoa wito mazao hayo pia yanatakiwa ambayo ikitumiwa ipasavyo na
kwa wananchi kutumia fursa kubwa kuongezewa thamani na kuwekewa wananchi itawawawezesha kujiajiri na
iliyopo hapa nchini ya ufugaji nyuki ngazi za ubora ili yaweze kuhimili kuongeza uzalisahaji wa mazao ya
na uwepo wa masoko ya ndani na nje masoko ya ndani na nje ya nchi. nyuki na mapato.
ya nchi kwa kuongeza uzalishaji wa
mazao yake na kuyaongezea thamani Aliongeza kuwa, ili kuimarisha sekta Alisema ili kulinda mazalia ya nyuki
ili kuinua uchumi wao na taifa kwa hiyo Serikali itashirikiana na wadau na kuongeza uzalishaji wa mazao ya
ujumla. kutatua changamoto zilizopo ikiwemo nyuki nchini, Serikali kupitia Wakala
kutafuta masoko, kuimarisha uwekezaji wa Huduma za Misitu Tanzania TFS,
Alitoa wito huo mbele ya wadau wa na kuanzisha viwanda vidogo vya imeanzisha hifadhi za nyuki 11 huku
sekta ya ufugaji nyuki kutoka mikoa kuchakata mazao ya nyuki ikiwemo Serikali za vijiji zikianzisha hifadhi za
yote nchini katika mkutano aliouitisha asali na nta ambayo ina soko kubwa nyuki 14.
kujadili maendeleo ya sekta hiyo nje ya nchi.
ikiwemo marekebisho ya kanuni za Wadau walioshiriki mkutano huo
ufugaji nyuki za mwaka 2017 katika Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi ambao ni wazalishaji, wachakataji na
ukumbi wa Hazina Jijini Dodoma. wa Idara ya Misitu na Nyuki wa wizara wasafirishaji waliishukuru Serikali kwa
hiyo, Deosdedit Bwoyo alisema kuandaa mkutano huo na kuiomba
Alisema kwa sasa mchango wa sekta Tanzania ni moja kati ya nchi 50 duniani kusaidia katika tafiti, elimu kwa
ya nyuki katika pato la taifa bado ni zenye utajiri mkubwa wa rasilimali za wananachi wanaojihusisha na ufugaji
mdogo ukilinganisha na fursa zilizopo misitu ambazo zinatoa fursa pana ya nyuki hususan maeneo ya vijijini na
za ufugaji nyuki hapa nchini ambazo ufugaji nyuki nchini. utafutaji wa masoko ya uhakika.
zikitumiwa ipasavyo zitasaidia kuinua
pato la wananchi na taifa kwa ujumla. Alisema eneo la misitu ni takriban
hekta milioni 48.1 ambalo ni asilimia

Jarida la MALIASILI 15
Wizara ya Maliasili na Utalii

Utaratibu wa kufuga wanyamapori kwenye


mashamba, ranchi na bustani
1. Utangulizi
Sera ya Wanyamapori ya mwaka 2007 na Sheria ya Kuhifadhi Wanyamapori Sura 283 zinahimiza
ushiriki wa wananchi katika matumizi endelevu ya rasilimali ya Wanyamapori. Matumizi ya
wanyamapori yamegawanyika katika sehemu mbili ambazo ni:

a) Matumizi yasiyo ya uvunaji


Aina hii ya matumizi hufanyika bila kuwaondoa wanyamapori katika maeneo yao ya asili, mfano
kuangalia wanyamapori.

b) Matumizi ya uvunaji
Aina hii ya matumizi hufanyika kwa kuwaondoa wanyamapori katika maeneo yao ya asili, mfano
uwindaji wa kitalii, uwindaji wa kitoweo, ukamataji wa wanyamapori kwa ajili ya ufugaji na biashara
ya wanyamapori hai.

• Ufugaji wa wanyamapori nchini,


Ufugaji wa wanyamapori ni kitendo cha kuhifadhi au kutunza wanyamapori nje ya mazingira
yao ya asili huku wakihudumiwa na kupewa mahitaji yao muhimu.

• Sheria, Kanuni, Mikataba ya Kimataifa inayosimamia shughuli hii,


Sera ya Wanyamapori ya mwaka 2007 na Sheria ya Kuhifadhi Wanyamapor Sura 283
zimetoa fursa ya ufugaji kwa yeyote anayehitaji. Utaratibu wa kufuga wanyamapori na
matumizi yao umeainishwa katika kanuni zifuatazo:
1. Kanuni za Biashara ya Nyara Na. 230 za mwaka 2010,
2. Kanuni za Ufugaji Wanyamapori Na. 379 za mwaka 2013,
3. Kanuni za Ukamataji wa Wanyamapori za mwaka 2010,
4. Kanuni zinazosimamia Utekelezaji wa Mkataba wa Biashara ya Kimataifa ya Wanya-
mapori na Mimea iliyo Hatarini Kutoweka za mwaka 2005.

2. Wanufaika wa shughuli hii


Ufugaji wa wanyamapori nchini ni fursa kwa watanzania na wageni kujipatia kipato kwa njia ya
utalii, kitoweo, kuzalisha kwa ajili ya biashara. Ufugaji wa wanyamapori hupunguza utegemezi na
shinikizo la uvunaji wa wanyamapori katika maeneo ya asili. Ufugaji hufanyika katika maeneo yaliyo
nje ya maeneo yaliyohifadhiwa kisheria (Protected Areas).

3. Utaratibu wa kuanzisha Mashamba, Bustani na Ranchi za Wanyamapori


Kabla ya kuanzisha mradi wa ufugaji wa wanyamapori katika mashamba, bustani na ranchi za
wanyamapori mwombaji anapaswa kufanya yafuatayo:-
1. Kuwa na eneo la mradi,
2. Kuandaa andiko la mradi,
3. Kupata ushauri wa wataalamu kuhusu mradi unao pendekezwa,
4. Kusajili mradi wako kwa Mamlaka ya Usajili (BRELA –Jina la Biashara au Kampuni
5. Kuhakikisha eneo la mradi linaendana na Mpango wa Matumizi ya Ardhi,
6. Kufanya tathmini ya athari katika mazingira kwa mradi pendekezwa,

4. Masharti ya kupata lesseni,


Baada ya kukamilisha utaratibu wa kuanzisha shamba/bustani/ranchi, mwombaji atatakiwa
kuwasilisha maombi ya leseni kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori

16 Jarida la MALIASILI
Wizara ya Maliasili na Utalii

Tanzania – TAWA kwa kujaza fomu ya maombi. Mwombaji aambatishe nyaraka zifuatazo kwenye
fomu ya maombi:-
i. Uthibitisho wa malipo ya ada ya maombi ya leseni yaani Stakabadhi ya Serikali (ERV),
ii. Nakala ya Hati ya Usajili wa aina la biashara /kampuni pamoja na nakala ya katiba na
mwongozo wa kampuni (Memorandum and Articles of Association),
iii. Andiko la mradi likijumuisha Mpango wa Biashara (Project Proposal and Business Plan),
iv. Uthibitisho wa umiliki wa eneo la mradi,
v. Cheti cha Tathmini ya Athari ya Mazingira (EIA Certificate),
vi. Nakala ya utambulisho wa mlipa kodi (Taxpayer Identification Number - TIN)
Muda wa kuwasilisha maombi ya leseni ni kuanzia tarehe 1 Oktoba hadi tarehe 15 Novemba katika
mwaka husika.

5. Lesseni zinazotolewa,
Ufugaji wa wanyamapori uko katika daraja tatu zifuatazo:-
i. Daraja 17: Bustani ya wanyamapori
ii. Daraja 18: Mashamba ya ufugaji wa wanyamapori
iii. Daraja 20: Ranchi za wanyamapori

6. Usajili wa Mashamba, Bustani na Ranchi za Wanyamapori


Baada ya kupewa leseni, mradi wa ufugaji wa wanyamapori utatakiwa kusajiliwa. Uhai wa usajili ni
miaka 15.

7. Ada zinazotozwa
Ada kwa maombi ya leseni ya ufugaji wa wanyamapori ni kama ifuatavyo:-
i. Bustani ya wanyamapori
Dola za kimarekani 150 kwa mradi unaomilikiwa na mzawa peke yake. Dola za kimarekani
250 kwa mradi unaomilikiwa kwa ubia kati ya mzawa na mgeni.
ii. Mashamba ya ufugaji wanyamapori
Dola za kimarekani 200 kwa mradi unaomilikiwa na mzawa peke yake. Dola za kimarekani
500 kwa mradi unaomilikiwa kwa ubia kati ya mzawa na mgeni.
iii. Ranchi za wanyamapori
Dola za kimarekani 500 kwa mradi unaomilikiwa na mzawa peke yake. Dola za kimarekani
1000 kwa mradi unaomilikiwa kwa ubia kati ya mzawa na mgeni.

8. Usimamizi wa wanyamapori katika mashamba/bustani/ranchi


8.1 Namna ya kupata wanyamapori mbegu,
Baada ya kusajili mradi wa ufugaji, mwombaji atatakiwa kuomba wanyamapori wa mbegu
(parent stock) kwa ajili ya uendelezaji wa mradi. Wanyamapori hao wanaweza kukamatwa
kutoka kwenya maeneo ya wazi au kutoka katika Mashamba, Bustani na Ranchi
Wanyamapori.

Sheria imetoa fursa ya kuingiza wanyamapori nchini kwa kuomba kibali cha kuingiza
wanyamapori (Import Permit).
8.2 Matumizi ya wanyamapori wanaofungwa
Matumizi ya wanyamapori wanaofugwa pia yako katika makundi mawili:-
i. Matumizi ya uvunaji na
ii. Matumizi yasiyo ya uvunaji

Matumizi hayo hufanyika kwa ajili ya utalii wa ndani na nje, kuzalisha na kusafirisha nje ya nchi,
kitoweo na kujipatia kipato.

Jarida la MALIASILI 17
Wizara ya Maliasili na Utalii

Jengo la NCAA kuwa kivutio cha utoaji


wa huduma za utalii Jijini Arusha

JENGO la kitega uchumi la Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo huko porini watakuwa wanaonekana “LIVE” (Mubashara)
la Ngorongoro jijini Arusha (pichani) ambalo ujenzi wake kwenye jengo hili kupitia LED Screen ambazo zitakuwa
unatarajiwa kukamilika mwezi juni mwaka huu litakuwa zimezunguka jengo hili” alisema Dk. Kigwangalla.
kivutio cha kihistoria cha utoaji wa huduma za utalii hapa
nchini. Alisema huduma nyingine zitakazotolewa katika Jengo
hilo ni pamoja na zile za kuangalia jiji la Arusha kupitia
Hayo yameelezwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dk. darubini, huduma za burudani ikiwemo kumbi za starehe
Hamisi Kigwangalla muda mfupi baada ya kukagua jengo na migahawa.
hilo ambalo linasemekana kuwa refu kuliko majengo yote
jijini Arusha likiwa na jumla ya ghorofa 18. Kwa upande wake Meneja wa Idara ya Urithi wa Utamaduni
wa Mamlaka hiyo, Mhandisi Joshua Mwankundwa alisema
Alisema jengo hilo ambalo linatizamana na Round About ya ujenzi wa jengo hilo ambalo ulianza mwezi Novemba, 2013
AICC katikati ya jiji hilo, limekusudiwa kuwa Kituo Kimoja unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi juni mwaka
(One Stop Centre) cha shughuli zote za utoaji wa huduma za huu.
utalii jijini humo kuanzia uwekezaji, utangazaji na menejimenti
kwa ujumla. Alisema jengo hilo ambalo lina uwezo wa kupaki magari
67 kwa wakati mmoja katika ghorofa za chini linagharimu
Alisema jengo hilo litatoa fursa kwa wadau mbalimbali shilingi za Kitanzania bilioni 45.
wanaotoa huduma za utalii kuweka ofisi zao ikiwemo
mabenki, watoa huduma za usafiri, mashirika ya ndege, Katika ziara hiyo ya siku moja ya ukaguzi wa jengo hilo, Dk.
mawakala wa safari za utalii na huduma, maduka ya bidhaa Kigwangalla aliongozwa na Mhifadhi Mkuu wa Mamlaka
za utalii na mahoteli. ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro, Dk. Fredy Manongi na
Naibu Mhifadhi wa Huduma za Uendeshaji wa Mamlaka
“Tutapamba pia jengo hili na” live screen” (Mabango ya Video hiyo, Asangye Bangu.
Mubashara) za vivutio, hivyo wanyama wakiwa wanapita

18 Jarida la MALIASILI
Wizara ya Maliasili na Utalii

Huyu ndiye Faru mwenye umri mkubwa


kuliko wote Duniani kwa sasa!

HISTORIA FUPI YA FARU FAUSTA;


Tafiti zinaonyesha kuwa ndiye Faru mwenye umri mkubwa kuliko wote Duniani kwa sasa.

Faru huyu anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 55 anapatikana katika Hifadhi ya Ngorongoro na
alianza kuonekana mwaka 1963 akiwa angali mdogo.

Faru huyu amekuwepo tangu enzi za Faru John. Faru John alikuwa mnyama mwenye umbo kubwa,
machachari na mwenye nguvu kuliko faru wengine.

Faru John alijimilikisha karibu faru jike wote katika Kreta ya Ngorongoro na hakutoa nafasi kwa faru
dume wengine kujihusisha na faru jike yeyote.

Robo tatu ya faru weusi waliopo katika Hifadhi ya Ngorongoro kwa hivi sasa wametokana na uzao wa
Faru John.

Pamoja na wasifu wake huo mzuri, Faru John alishindwa kumzalisha Faru Fausta ambae waliishi nae
kwa muda mrefu.

Katika umri wake huo faru Fausta hakubahatika kupata mtoto mpaka leo.

Aidha, faru huyo anatumia jicho moja tu kutokana na jicho jingine kuwa bovu (Chongo).

Jarida la MALIASILI 19

Вам также может понравиться